Category Archives: Uncategorized

22-0414  Kutoka kwa Tatu na Kutawadhana Miguu

Ujume: 63-0630m Kutoka kwa tatu

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Mpendwa BIBI-ARUSI ALIYEUNGANA Ambaye Anayenena NENO,

Huu ni wakati mzuri zaidi wa maisha yangu marafiki zangu! Tunaona Neno likitimizwa mbele ya macho yetu kuliko wakati mwingine wowote. Inasisimua jinsi gani kutambua Yeye ni Nani, mjumbe Aliyemtuma ni nani, na kisha KUJUA SISI NI NANI! Asante Baba. Hatukufikiri kamwe matukio haya yangetukia namna hii, lakini haya hapa yanatukia papa hapa mbele ya macho yetu, jinsi kabisa nabii Wako alivyosema kwenye kanda.

Niko chini ya matarajio makubwa kuona Roho wake Mtakatifu akituleta karibu Naye kuliko hapo awali kabla ya wikendi hii ya Pasaka. Ningependa kuwaalika kila mmoja wenu kushiriki nasi kwenye Ujumbe huu, pamoja na Bibi-arusi Wake ulimwenguni kote.

” Basi wakati jambo lo lote ndogo linapozuka, mbona unatenda kama mtoto? Inakupasa kuwa mtu mzima. Nena na watu! Amina. “Kisha mwendelee mbele.” Amina. Ndivyo hivyo “Usilie, nena!” Amina. Jamani, napenda hilo. “Mbona unanililia? Nena tu na watu, kisha songeni mbele kwa shabaha yenu.” Cho chote kile, kama ni magonjwa, cho chote kile, kama ni kufufua wafu ama cho chote kile, nena! Nilithibitisha hayo. Nena na watu! ”

Ni fursa iliyoje tuliyo nayo ya kuchangamsha imani yetu, hivyo sisi pia tunaweza Kunena NENO. Njoo ukusanyike pamoja na Bibi-arusi katika wikendi ya Pasaka, tunapojitayarisha kwa ajili ya Kutoka kwa mwisho. Maisha yetu lazima yaistahili Injili, kwa maana kizazi hiki kiko chini ya Shtaka. LAKINI SASA hakuna sababu ya Bibi-arusi wake kulialia, BALI KUNENA! Songeni mbele kwa shabaha yenu. Jina la Bwana lihimidiwe!

Kama kawaida yetu tufanyavyo kwa wikendi ya Pasaka, Hebu tujifungie mbali na ulimwengu kadri tuwezavyo kwa kuzima simu zetu isipokuwa kupiga picha, kusikia Nukuu ya Siku, na kucheza kanda kwenye programu ya Lifeline au kutoka kwenye anuani ya kupakua. Hebu na tumtolee Bwana wikendi hii takatifu kikamilifu, na tusiifanye Pasaka hii kuwa jambo la kijamii, bali kujiweka wakfu kwenye Neno, katika nyumba zetu. Ningependa sisi sote tuungane pamoja wikendi hii kwa ratiba ifuatayo, kwa Saa za kutwa za Mashariki (EDT) isipokuwa kama ifahamike vinginevyo.

ALHAMISI

Ilikuwa ni Alhamisi usiku ambapo Bwana Yesu alikula Karamu ya Mwisho na wanafunzi wake katika ukumbusho wa Pasaka kabla ya kutoka kwa wana wa Israeli. Ni fursa iliyoje ya kufanya ushirika na Bwana katika nyumba zetu, kabla ya wikendi yetu takatifu, na kumwomba atubariki sisi na familia zetu, na kutupa sisi sote kile tunachohitaji katika safari yetu.

Baba wa Mbinguni, tunashukuru kwa ajili ya jambo hili, wakati mwingine wa kukusanyika pamoja, upande huu wa Umilele. Na tunatarajia asubuhi ya leo kuhuishwa upya kwa nguvu kuja kutoka Kwako, zipate kututia moyo kwa ajili ya safari iliyoko mbele. Tumekusanyika kama wana wa Kiebrania walivyofanya asubuhi na mapema, kuokota mana iliyokuwa imetolewa kwa ajili yao usiku kucha, kuwapa nguvu kwa ajili ya siku ijayo. Tunakusanyika kwa ajili ya Mana ya kiroho, asubuhi ya leo, ipate kutupa nguvu kwa ajili ya safari.

Hebu na tuanze wote saa 12:00 kumi na mbili JIONI . kwa masaa ya nchi zetu, na tumsikie Yeye akituambia kwamba tuko katika Kutoka kwa mwisho, tunapokusanyika kukizunguka Kiti Chake cha Enzi ili kusikia Ujumbe: Kutoka kwa Tatu 63-0630M .

Sambamba Tunaposikiliza Ujumbe, tutakusanyika na familia zetu katika nyumba zetu na kushiriki Meza ya Bwana.

Hivi punde tutakuwa na Anuani ya kupakua kanda na ibada ya Ushirika, au, itapatikana kwa muda ulioratibiwa wa ibada kwenye Voice Radio, kwenye app ya Lifeline.

IJUMAA
Hebu na twende kwenye maombi na familia zetu saa 3 :00 Tatu ASUBUHI ( Ni saa 10:00 Kumi jioni ya Tanzania) ., na kisha tena saa 6:00 Sita MCHANA, ( Ni Saa 1:00 Moja Jioni ya Tanzania) Kumualika Bwana awe pamoja nasi na Bibi-arusi wake kutoka ulimwenguni kote katika wikendi hii ya kipekee sana; na ajaze nyumba zetu kwa Roho wake Mtakatifu tunapojitolea kumwabudu.

Hebu Fahamu zetu na zirudi nyuma hadi siku ile pale Kalvari, zaidi ya miaka 2000 iliyopita, na kumwona Mwokozi wetu akining’inia msalabani, kisha tujitoe vivyo hivyo kufanya daima yale yanayompendeza Baba.

Sasa angalieni. Wakati alipokuja ulimwenguni, wakati kulikuwapo na zaidi, kutokuamini kwingi duniani wakati huo kadiri kulivyowahi kuwa, hata hakukumpunguzia mwendo. Aliendelea moja kwa moja kuhubiri vivyo hivyo, na kuponya vivyo hivyo. Hakukumsumbua. Kulikuwako na wakosoaji. Mtu huyo alikosolewa tangu alipokuwa mtoto mchanga mpaka alipokufa msalabani. Je! hilo lilimzuia? La, bwana. Lengo Lake lilikuwa ni nini? “Kufanya sikuzote yale Baba ameandika. Kufanya daima yale yanayompendeza .”
.

Kisha saa 6:30 Sita na Nusu MCHANA . (Ni saa 1:30 Moja na Nusu jioni ya Tanzania) hebu na tufikirie kwa dhati juu ya swali muhimu sana katika maisha yetu, tunapokusanyika kukizunguka Kiti Chake cha Enzi ili kusikia Ujumbe: Je, Maisha Yako Yanaistahili Injili? 63-0630E .

Kisha Hebu na tuungane pamoja Tena katika maombi saa 9:00 Tisa ALASIRI (Ni saa 4:00 Nne Usiku ya Tanzania) . katika ukumbusho wa kusulubiwa kwa Bwana wetu.

JUMAMOSI

Hebu na Tuungane pamoja kwa mara nyingine tena katika maombi saa 3:00 Tatu ASUBUHI ( Ni Saa 10:00 Kumi jioni ya Tanzania) ., na saa 6:00 Sita MCHANA .,( Ni Saa 1:00 Moja Jioni ya Tanzania) na tuitayarishe mioyo yetu kwa ajili ya mambo makuu atakayotutendea kati yetu,

“ Baada ya kulileta shtaka hili dhidi ya marafiki wa—wangu wahubiri huko, na yanibidi niseme mambo haya magumu; lakini Bwana, niliyatenda kwa punzi Yako. Najisikia kuwa Wewe uliniambia nitende hili. Sasa, haumo mabegani mwangu, Bwana. Ni—ninafuraha umeniondokea. Na wao watende nao lo lote wapendalo, Baba. Naomba kuwa wataupokea. Naomba kuwa Wewe utamwokoa kila mmoja, Bwana. Na humo kutokee ufufuo wa wenye haki na Uweza mkuu uje kati ya Kanisa kabla tu ya kuondoka Kwake. Si vigumu kuomba hayo, kwa maana Wewe uliyaahidi. Nasi twatazamia, Bwana, huo mvuto wa tatu tunaojua kuwa utatenda mambo kati yetu .”

Kisha saa 6:30 Sita na Nusu MCHANA.( Ni Saa 10:30 Kumi na Nusu jioni ya Tanzania). sote tutakusanyika pamoja ili kusikia NENO: Lile shtaka 63-0707M . Hii itakuwa SIKU ILIYO KUU jinsi gani kwa Bibi-arusi Wake ulimwenguni kote.

Kisha Hebu na tuungane pamoja tena katika maombi saa 9:00 Tisa ALASIRI. ( Ni Saa 4:00 Nne Usiku ya Tanzania) katika ukumbusho wa kusulubiwa kwa Bwana wetu.

JUMAPILI

Ni siku nzuri jinsi gani ya kutolialia tena, Bali KUNENA! Ni asubuhi iliyoje ya ufufuo! Hebu na tuamke mapema kama vile Ndugu Branham alivyofanya asubuhi ile wakati rafiki yake mdogo, robin, alipomwamsha Saa 11:00 Kumi na moja ALFAJIRI ( ni Saa 6:00 Sita Mchana ya Tanzania) .. Hebu na tumshukuru tu Bwana kwa kumfufua Yesu kutoka kwa wafu:

“ Saa kumi na moja asubuhi ya leo, rafiki yangu mdogo mwenye kifua chekundu aliruka dirishani akaniamsha. Ilionekana kana kwamba moyo wake mdogo ungepasuka, akisema, “Amefufuka.”

Saa 3:00 Tatu ASUBUHI Saa za Jeffersonville ( ni Saa 10:00 Kumi jioni ya Tanzania) Hebu na tuungane kwa dhati kwa mara nyingine tena katika Maombi yetu ya mnyororo , kuombeana mmoja kwa mwingine na tukijitayarisha wenyewe kuisikia Sauti ya Mungu.

Saa 6:30 Sita na Nusu MCHANA saa za Jeffersonville ( Ni saa 1:30 Moja na Nusu Jioni ya Tanzania) tutakusanyika pamoja ili kusikia Ujumbe wetu wa Pasaka: Mbona unalialia? Nena! 63-0714M .

Baada ya Ibada hii, Hebu na tuungane tena katika maombi, Kumshukuru kwa WIKENDI YA AJABU ALIOTUPATIA PAMOJA NAYE NA PAMOJA NA BIBI-ARUSI WAKE ULIMWENGUNI KOTE.

Kwa ndugu na dada zangu walio nchi za ng’ambo, ningependa kuwaalika kuungana nasi kwa matukio haya kwa masaa ya Jeffersonville, kwa masaa yote ya maombi kwenye ratiba hii na kwa kanda itakayochezwa Jumapili asubuhi. Ninatambua, hata hivyo, kwamba kucheza Kanda hizi za Alhamisi, Ijumaa, na Jumamosi alasiri kwa masaa ya Jeffersonville ingekuwa vigumu sana kwa wengi wenu, kwa hivyo tafadhali jisikie huru kucheza Jumbe hizo wakati wowote wa siku husika unaokufaa. Ningependa, hata hivyo, sote tuungane pamoja Jumapili saa 6:30 Sita na Nusu MCHANA za Jeffersonville, ( Ni Saa 1:30 Moja na Nusu Jioni ya Tanzania) ili kusikia Ujumbe wetu wa Jumapili kwa pamoja.

Ningependa pia kukualika wewe na watoto wako kuwa sehemu ya karatasi za creations, mafunzo , na maswali ya YF, ambayo familia yako yote inaweza kufurahia pamoja. Tunafikiri mtayapenda kwa kuwa yote yanahusu NENO ambalo tutakalosikia wikendi hii.

Kwa ratiba ya wikendi, Taarifa kuhusu kujiandaa kwa ajili ya ibada ya Ushirika, nyenzo zitakazohitajika kwa ajili ya kazi za creations , Maswali ya Pasaka, na taarifa nyinginezo, tazama anuani zilizo hapa chini.

Ni heshima kubwa kwangu kukualika wewe na familia yako kuungana pamoja na Bibi-arusi duniani kote kwa wikendi iliyojaa KUABUDU , SIFA NA UPONYAJI. Ninaamini kweli ni wikendi ambayo itabadilisha maisha yako milele.

Ndugu Joseph Branham

22-0410 Kiongozi

Ujume: 62-1014e Kiongozi

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wana-Kondoo Wanaoongozwa,

Vita vya mwisho vimekaribia. Tunaenda mahali ambapo hatujawahi kufika hapo awali. Tunapita katika nyika, nasi tumo njiani kuelekea mahali fulani, nasi hatuwezi kuendelea bila Kiongozi. Msiwe na wasiwasi enyi kundi dogo, Mungu ametoa Kiongozi wa kutuongoza.

Kiongozi huyu atatufunulia mambo, naye atatuambia mambo aliyosikia; Anaweza kurudia maneno yetu moja kwa moja na kusema tuliyosema. Hatuna budi kumfuata Kiongozi huyu, kwa maana Yeye ndiye peke Yake ajuaye njia.

Wakati Yesu alipokuwa duniani, aliwaambia wanafunzi wake kwamba alikuwa na mambo mengi zaidi ya kusema na kutufunulia, hivyo angetutumia huyo Roho wa kweli, naye atatuongoza atutie kwenye kweli hizi zote. Yeye Alisema Bibi-arusi Wake angemtambua kwa kuwa angejifunua na kujithibitisha Mwenyewe kama tu alivyofanya alipokuja katika mwili mara ya kwanza.

Atajua kila wazo lililo moyoni mwetu. Atatujua sisi ni nani na tumefanya nini. Atajua kila kitu kutuhusu sisi. Yeye ni Kiongozi wa Mungu, Roho Mtakatifu akiishi na kujidhihirisha Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu.

Kama vile Yesu Mwenyewe alivyosema, “ Si Mimi nizifanyaye zile kazi; ni Baba Yangu anayekaa ndani Yangu. Amini nawaambieni, Mwana hawezi kufanya neno kwa nafsi Yake Mwenyewe; bali lile analomwona Baba akifanya, ndilo analofanya Mwana vile vile. Baba anafanya kazi, Nami ninafanya kazi vile vile .”

Vivyo hivyo malaika wake hatanena kwa shauri lake mwenyewe, Lakini yote atakayoyasikia atayanena. Atatwaa haya yote kutoka kwa Baba, na ndipo atatupasha Habari . Atafunua siri zote zilizofichwa katika Neno.

Baba alituambia ya kwamba angekuwa na MTU ambaye angemwakilisha yeye hapa duniani, Kiongozi, na kwamba Bibi-arusi Wake atamtambua waziwazi na kumfuata .

Yeye atamtukuza Mungu tu. Yeye atasema waziwazi, Si yeye, yule malaika wa saba, ni kudhihirishwa kwa Mwana wa Adamu. Ni siri ya Mungu iliyofunuliwa. Si mwanadamu, ni Mungu. Yeye si Mwana wa Adamu; yeye ni mjumbe kutoka kwa Mwana wa Adamu. Mwana wa Adamu ni Kristo, Yeye Ndiye tunayejilisha.

Wengi watasema wao ndio waliotiwa mafuta ili kumwongoza Bibi-arusi, lakini Mungu hataki utegemee Akili zako mwenyewe ama mawazo yako mwenyewe , wala mawazo yoyote yaliyotungwa na mwanadamu. Mungu hutuma Kiongozi, naye Mungu anataka mkumbuke ya kwamba huyo ni Kiongozi Wake aliyemchagua.

Kiongozi wetu hatampeleka mmoja huku na mwingine kule na kusema: yakubidi umsikilize mhubiri huyu, kisha yakubidi umsikilize mhubiri yule;
Wao hata hawakubaliani wao kwa wao. Hilo linawezaje kukukamilisha?

Kuna NENO MOJA Tu LILILOKAMILIFU litakalotukusanya na kutuweka pamoja, NENO LA SAUTI YAKE ILIYOTHIBITISHWA KIKAMILIFU KWENYE KANDA .

Wao Wanasema leo hii Roho Mtakatifu anamuongoza kila mmoja wetu kama mtu binafsi, ambalo ni kweli. Basi kwa nini uwe na mhubiri ikiwa Roho Mtakatifu anakuongoza? Jisikilize mwenyewe: Ni afadhali niwe na mhubiri aniongoze na anifundishe badala ya nabii aliyethibitishwa wa Mungu? Afadhali nipate fasiri yake ya Neno kuliko kulisikia moja kwa moja kutoka kwa Sauti ya Mungu Mwenyewe jinsi yeye anavyoweza kulifafanua vizuri zaidi?

Mimi Sijaribu kushutumu hizo huduma, au kusema ni za uwongo, au kwamba hupaswi kuzisikiliza hizo huduma. Tafadhali nisamehe ikiwa silitamki ipasavyo . Ninasema tu haziwezi kuwa Mkataa wako, neno la mwisho, Kiongozi wako. Watu hawawezi kukubaliana kamwe. Kila mtu ana wazo tofauti, uongozi tofauti. Hilo linawezaje kumkamilisha Bibi-arusi? Ikiwa unawasikiliza wote, na kujua wote hawawezi kukubaliana na kile wao wanachosema kuwa ni Neno kamilifu la Mungu, hilo linawezaje kumkamilisha Bibi-arusi? Je, hilo Linawezaje kuwa kiongozi wako?

Na kama tutamwacha tu Roho Mtakatifu atuweke pamoja na Neno Lake, ni kwamba Wote tutakuwa na moyo mmoja, nia moja, na katika umoja, kwa Roho mmoja; Roho Mtakatifu, Kiongozi wa Mungu atakayetuongoza atutie kwenye Kweli yote. Lakini hunabudi kumfuata Kiongozi wako.

Usishindane kamwe na Neno la Kiongozi wako. Mfuate Yeye. Kama humfuati, utapotea. Pia, kumbuka, unapomwacha, uko peke yako, kwa hiyo tunataka kuwa karibu na yule Kiongozi.

Roho Mtakatifu anatuongoza kumfuata Kiongozi wake, ambaye ni Roho Mtakatifu anayenena kupitia Malaika-Mjumbe wake wa saba . Si Neno la mwanadamu, Ni Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi Wake na NDILO JAMBO PEKEE LINALOWEZA KUMKAMILISHA BIBI-ARUSI .

Njoo tuwe pamoja Jumapili saa 6:00 Sita MCHANA , saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 Jioni ya Tanzania), tunapoianza wiki yetu ya Pasaka kumsikiliza Kiongozi wetu. Anaenda kutuongoza mahali ambapo hatujawahi kamwe kufika hapo awali.

62-1014E Kiongozi

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Marko Mtakatifu 16:15-18

Yohana Mtakatifu 1:1 / 16:7-15

Matendo 2:38

Waefeso 4:11-13 / 4:30

Waebrania 4:12

2 Petro 1:21

Kutoka 13:21

22-0403 Kimulimuli Chekundu Cha Dalili Ya Kuja Kwake

Ujume: 63-0623E Kimulimuli Chekundu Cha Dalili Ya Kuja Kwake

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Sisi Wote ndani,

Utukufu kwa Mungu, ni siku ilioje tunayoishi. Tunasikiliza Ujumbe ambao umethibitishwa, kwa kila tendo, kuwa ni Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele. Umefanya mambo yale yale aliyofanya alipokuwa hapa duniani; aliponya wagonjwa, alijua mawazo ya nia, akaonyesha mambo ambayo yangetukia, Aliwafufua wafu, na kila wakati, imekuwa kamilifu.

Maji yameosha udongo wote kutoka juu ya kilele kwenye mlima. Hakukuwa na kitu kilichobaki isipokuwa Mwamba. Kulikuwa na Maandishi ya Ajabu juu ya Mwamba, kwa hiyo Mungu akatutumia nabii wake mwenye nguvu ili kufasiri hayo Maandishi kwa Bibi-arusi Wake. Sasa Biblia imefasiriwa kikamilifu kabisa.

Akampeleka malaika wake mwenye nguvu juu ya mlima na akaweka UPANGA WA BWANA MKONONI MWAKE. Kisha malaika wake akakata kilele cha mlima ule na kukiinua juu. Ndani yake kulikuwa na mwamba mweupe, kitu kama namna ya jiwe gumu jeupe ambalo hata halikuwa limeandikwa.

Yeye Alituambia tuangalie Huu wakati alipokwenda Magharibi. Kisha alitwaliwa katikati ya Malaika Saba na akarudi na kutufunulia YOTE YALE HATA HAYAKUWA YAMEANDIKWA NDANI YA MWAMBA.

“ Huyu ni mtumishi Wangu. Nami nimemwita kuwa nabii kwa wakati huu, kuwaongoza watu kama tu Musa alivyofanya. Naye amepewa mamlaka, angeweza kunena kitu kiwepo.” Au kitu kama hicho, kama Musa alivyofanya, kama kunena watokee inzi. Nasi tunajua kuhusu wale kindi, na kadhalika, na mambo ambayo tayari yamekwisha kutukia. Maskini Hattie Wright nyuma kule, nadhani mnajua lililotukia kule nyumbani .

W-I-L-L-I-A-M M-A-R-R-I-O-N B-R-A-N-H-A-M ndiye mtu ambaye Mungu Amemchagua kumwongoza Bibi-arusi Wake leo hii. Yeye ni mwili aliouchagua kuzungumza nasi kama alivyofanya alipokuja katika mwili miaka 2000 iliyopita. Kila Andiko linathibitisha Hilo. Roho Mtakatifu amelifunua jambo hilo . Sasa kuna uhakikisho wa kwamba tunao UFUNUO WA KWELI wa Yeye ALIKUWA Nani, YEYE NI NANI na sisi NI NANI: Bibi-arusi wake Kipenzi Aliyechaguliwa .

Tunajua tuko katika Mapenzi yake makamilifu kwa kudumu na Neno Lake. Inaleta Furaha na shangwe kweli. Haiwezekani kuelezea kwa maneno tu kile inachomaanisha kwetu.

Daima tumejua ndani ya mioyo na Nafsi zetu kwamba kulikuwa na kitu tofauti hapo. Tulijua, hata bado tulipokuwa katika dhambi, kulikuwa na kitu pale ambacho hatukuweza kuelezea, lakini kilikuwa pale tu. Sasa TUNAJUA. Hatujawahi kuhisi hivi hapo awali, hakuna mashaka tena, hakuna kushangaa tena, hakuna kuuliza tena, Imechongwa na kuandikwa katika nafsi zetu. UTUKUFU KWA MUNGU!!

Sisi ndio kizazi kile ambacho hakitapita hadi mambo haya yote yatimie. Sisi ndio kizazi kile kinachoona ule ukengeufu ukifanyika mbele ya macho yetu. Wakati umekaribia. Kile Kimulimuli Chekundu cha Kuja Kwake kiko hapa. Onyo lake la mwisho linafanyika.

Mauti na Maangamizi vimetuzunguka pande zote. Tunaishi katika Sodoma na Gomora. Uchafu, dhambi, moyo wa mwanadamu unakufa kwa hofu, mabomu ya atomiki, dhiki kati ya mataifa, na wakati wote tunaungana na kuketi pamoja katika Ulimwengu wa Roho wakati Mungu mwenyewe akituambia, MSIOGOPE, NINYI NDIYO KIPENZI CHANGU. Hakuna kinachoweza kuwapata ninyi . Hebu tu mioyo yenu iwake ndani yenu ninapozungumza nanyi njiani na kuwaambia, NINYI NI BIBI-ARUSI WANGU.

Njoo uungane nasi Jumapili hii saa 6:00 Sita Mchana , saa za Jeffersonville, ( Ni Saa 1:00 Moja Jioni ya Tanzania), Wakati kuna makelele yanayosikika. Selo imeshuka. Kimulimuli Chekundu kimeanza kumemetesha . Iwapo unatarajia kuondoka pamoja nasi, afadhali utupe chini kifurushi hicho cha njugu karanga , uache kupiga domo , uchukue makasha yako, ukajitayarishe la sivyo utaachwa,  sababu litasimama hapo kwa muda mfupi tu. Limekuja kusema: Kimulimuli Chekundu Cha Dalili ya Kuja Kwake 63-0623E.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Ujumbe:

Mathayo Mtakatifu 5:28 / 22:20 / Sura ya 24 yote

2 Timotheo Sura ya 4 yote

Yuda 1:7

Mwanzo Sura ya 6 yote

22-0327 Kusimama Katika Pengo

Ujume: 63-0623M Kusimama Katika Pengo

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Walio Waaminifu,

Wiki hizi zilizopita zimekuwa wakati wa utukufu zaidi katika maisha yetu yote.
Imekuwa mojawapo ya mambo makuu zaidi kuungana na Bibi-arusi Wake ulimwenguni kote, kumsikiliza Mungu akifunua ile Mihuri Saba.

Je, sisi sote tuliungana pamoja kusikiliza kitu gani pia?

“Kule ndani ya hiyo piramidi, kulikuwako na Jiwe jeupe ambalo halikuwa limeandikwa.” Hiyo ndiyo sababu ilinibidi kwenda magharibi, kuungana na Ujumbe wa Malaika hawa, kurudi hapa na kuufunulia kanisa .

Ilimbidi aende magharibi ili kuungana na wale Malaika 7, ili arudi kutufunulia yale ambayo hata hayakuwa yameandikwa; lakini sasa, kwa Ufunuo, yamefunuliwa kwetu na yanatupa Imani ya Kunyakuliwa.

Tumezisikia Jumbe hizi maishani mwetu mwote, lakini sasa zimefunuliwa kuliko hapo awali; hii ndiyo siku yenyewe , huu ndio wakati wenyewe. Tunaona na kusikia yale aliyotuambia yangetukia, ulimwenguni na katika Ujumbe huu, na sasa yanadhihirishwa mbele ya macho yetu kabisa.

Je, Malaika_Mjumbe wetu wa 7 alikuwa ni nabii tu kama manabii wa kale? Hapana, Yeye aliitwa kwenye huduma ya juu zaidi kuliko manabii wote waliomtangulia. Kwa maana ilikuwa ni Mwana wa Adamu akijifunua Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu kama tu alivyofanya miaka 2000 iliyopita. Nabii wetu aliitwa KUONGOZA BIBI-ARUSI mpaka kwenye Makao yetu mapya, kisha atatukabidhi kwa Bwana.

Yeye Alituambia huduma yake ilifananisha maisha ya Musa kikamilifu. Musa alipokuwa katika safari yake akiifuata Nguzo ya Moto, watu waliinuka na kumkabili. Watu hawa walikuwa wameitwa na walikuwa njiani kuelekea kwenye nchi ya ahadi. Walimpinga Musa kwa kusema alijitwalia madaraka mno; hakuwa mtakatifu pekee yake aliyeitwa, wao pia walikuwa watakatifu na walihitaji kuhubiri kitu fulani pia.

Alisema walikuwa watu watakatifu, na ya kwamba kweli walikuwa na jambo Fulani la kufanya, Lakini Mungu alikuwa amemwita YEYE, MUSA, MTU MMOJA, kuwaongoza watu.

Wao Walikuwa na nafasi yao. Walitiwa mafuta. Walikuwa wakifanya kile walichoitiwa na kuagizwa kufanya kwa kuwaambia watu, “msikilizeni Musa”, Lakini walitaka kusema KITU FULANI ZAIDI, AU KUFAFANUA KILE MUSA ALICHOKUWA ANASEMA . Hawakuridhika kuwaelekeza tu watu wamsikilize Musa. Walitaka wao wawaongoze watu. Walitaka kufanya jambo fulani zaidi, au tofauti, kuliko lile waliloagizwa kufanya.

Ukiwahi kutilia shaka Niani mwako kile nabii wetu alicho, au aliitiwa kufanya Nini, ninakualika uende magharibi kutazama safu ya milima ambayo Mungu Mwenyewe aliifanya kama ishara ya milele duniani, kwa kuweka jina la nabii wetu, B-R-A-N-H-A-M. , kwenye mlima huo.

Wewe ni Bibi-arusi wa Yesu Kristo. Alikuchagua na kukuteua tangu awali. Neno lake linaishi na kukaa ndani yako. Wewe ni Neno lililo hai lililofanyika mwili. Alikupa Ufunuo wa Neno Lake. Shetani hana nguvu juu yako. Ile Imani ya Kunyakuliwa inaishi na kukaa ndani yako.

Roho Mtakatifu anamwongoza Bibi-arusi Wake kwa njia Yake pekee aliyoiandaa kwa ajili ya wakati huu, Neno Lake lililonenwa na nabii Wake malaika wa Saba. Nabii huyo ndiye Mchungaji wetu.

Mchungaji wetu alituahidi kwamba ujumbe wowote mpya wa kanda ungetoka kwanza kwenye Ghala, mpaka Bwana alibadili . Kwa maana hapo ndipo kanda zilizowekwa kwenye ghala zingenasiwa.

Yeye Pia alimwelekeza mchungaji msaidizi wake Ndugu Neville, na wakati huu kwa Neema Yake, mimi mwenyewe, kile tunachopaswa kufanya kanisani.

Ninaomba ya kwamba utamsaidia mchungaji wetu mpendwa, Ndugu Neville. Mfanye, Bwana, kujaa neema na kujaa nguvu, na pamoja na ufahamu, apate kuchukua Chakula hiki Kilichowekwa kwenye ghala na kuwalisha kondoo wa Mungu.

Kanda hizi ni za wale ambao nabii aliitiwa kuwachunga. Ikiwa unataka kusikia BWANA ASEMA HIVI, njoo usikilize pamoja nasi Jumapili saa 12:00 Sita Mchana , saa za Jeffersonville, ( Ni saa 1:00 Moja jioni ya Tanzania), ili: Kusimama Katika Pengo 63-0623M , tunaposikia Chakula kilichowekwa kwenye ghala ambacho kimeandaliwa kwa ajili ya Bibi-arusi.

Tutauanza Ujumbe huu kuanzia kwenye namba ndogo (paragraph) ya 27.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe :

Hesabu 16: 3-4

22-0320 Muhuri Wa Saba

Ujume: 63-0324e Muhuri Wa Saba

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Mwaminifu,

Hata alipoifungua muhuri ya saba, kukawa kimya mbinguni kama muda wa nusu saa .

  • Lakini hapa kuna Ngurumo Saba mfululizo, moja baada ya nyingine: moja, mbili, tatu, nne, tano, sita, saba, hiyo namba kamilifu. Ngurumo Saba mfululizo, zilitoa sauti, si… zikifanya tu—tu moja, mbili, tatu, nne, tano, sita, saba, mfululizo. Ndipo, Mbingu hazingeweza kuandika jambo Hilo. Mbingu haziwezi kujua juu ya jambo Hilo, hakuna jambo lingine lo lote, maana hakuna jambo linaloendelea. Ilikuwa ni wakati wa kupumzika. Ilikuwa ni kuu sana, mpaka, ikafichwa Malaika.
  • Hata ngurumo saba zilipotoa sauti zao, nalikuwa tayari kuandika:…
    Kulikuwa kumenenwa kitu. Haikuwa ni kelele tu. Kitu fulani kilinenwa. Alikuwa tayari kuandika .
    Nami nilisikia sauti kutoka mbinguni ikisema,
    Angalia mahali zile sauti zilikokuwa katika zile Ngurumo. si Mbinguni, Nchini! Zile Ngurumo hazikutoa sauti kamwe toka mbinguni , zilitoa sauti toka Nchini.
  • Saba, nambari ya Mungu iliyo kamilifu. Saba moja kwa moja tu mfululizo . Ngurumo Saba zililia mfululizo pamoja , kana kwamba zilikuwa zikiendeleza herufi za kitu fulani .

Shauku ya mioyo yetu ni kuwa mwana au binti wa kweli wa Mungu; kuwa tayari kwa Unyakuo Wake unaokuja hivi karibuni. Kwa hiyo ni lazima tumuulize Bwana: “Ni kitu gani kitakachompa Bibi-arusi Imani ya kunyakuliwa anayohitaji”?

  • Nami naamini ya kwamba, kupitia Ngurumo hizo Saba, zitafunuliwa katika siku za mwisho ili kumkusanya Bibi-arusi pamoja kwa ajili ya kupata imani ya kunyakuliwa .
  • Nazo Ngurumo Saba papa hapa katika ufunuo, hapa, wa Yesu Kristo, ni siri fulani. Biblia haisemi kwamba ” huu ni ufunuo wa Yesu Kristo” ? Vema, kuna siri fulani yake iliyofichwa. Ni nini? Zile Ngurumo Saba zina hiyo siri. Kwa maana Yohana alikuwa tayari kuandika, na sauti ilishuka kutoka Mbinguni ikasema, “Usiliandike. Bali litie muhuri; litie muhuri. Liweke kwenye upande wa nyuma wa kile Kitabu .” Lapaswa lifunuliwe. Ni zile siri .

Je! Roho Mtakatifu, atamfunulia Bibi-arusi Wake Ufunuo wa zile Ngurumo Saba utakaowapa imani ya Kunyakuliwa kupitia hizi huduma ?

  • Sasa mjumbe huyu wa Malaki 4 na Ufunuo 10:7 atafanya mambo mawili . Moja : Kulingana na Malaki 4 ataigeuza mioyo ya watoto iwaelekee baba zao . Pili : Atafunua siri za ngurumo saba katika Ufunuo 10 ambazo ni mafunuo yale yaliyo ndani ya zile muhuri saba.
  • Muhuri hizi ziko nyuma ya kile Kitabu, na wakati yule Malaika wa Saba atakapopiga baragumu, siri zote ambazo zimeandikwa katika Kitabu
    zimekamilishwa. Na mara tu, Kitabu ambacho kilikuwa kimefunguliwa na kuandikwa ndani, kinafungwa, “Siri za Mungu zimetimizwa.” Na hizi ndizo siri za Mungu: kunyakuliwa kwa Kanisa, na mambo haya yote mengine. “Siri zimekwisha.”
    Wakati yule malaika wa saba anapiga baragumu ya kila siri , imekwisha. Hata awe nani. Hata iwe nini. Neno la Mungu haliwezi kushindwa .

NI RAHISI HIVI:

Siri kupitia hizo Ngurumo Saba zitampa Bibi-arusi Imani ya Kunyakuliwa . Ni Mungu PEKE YAKE , kupitia malaika Wake wa Saba, atakayefunua zile NGURUMO SABA kwa Bibi-arusi.

Ukitaka zile Ngurumo Saba zifunuliwe kwako, kukupa Imani ya Kunyakuliwa , hakuna njia nyingine ya kuupokea Ufunuo huo ila kuupata kutoka kwenye Sauti pekee ya Mungu iliyothibitishwa kwa ajili ya siku yetu; si kutoka kwangu, si kutoka kwa mchungaji wako wa mahala, mwinjilisti, au mwalimu, Bali kutoka kwa mchungaji wa Mungu kwa ulimwengu wote, kwa KUBONYEZA PLAY.

Njoo usikie siri zote zikifunuliwa; kupokea Imani ya Kunyakuliwa na ujaze Taa yako Mafuta, Jumapili saa 6:00 Sita mchana, saa za Jeffersonville, (ni saa 1:00 Moja jioni ya Tanzania), tunapomsikia Mungu akizungumza na kujifunua Mwenyewe katika urahisi na kutuletea: Muhuri wa Saba 63-0324E .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Kumbukumbu la Torati 29:16-19

1 Wafalme 12:25-30

Ezekieli 48:1-7, na mstari wa 23-29

Mathayo 24:31-32

Ufunuo sura 7 yote

Ufunuo 8:1

Ufunuo 10:1-7

Ufunuo sura 14 yote

22-0313 Maswali Na Majibu Juu Ya Mihuri

Ujume: 63-0324M Maswali Na Majibu Juu Ya Mihuri

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi aliyepumzika,

Leo hii dunia inasoma vichwa vya habari kusikia yaliyojiri duniani jana: Hofu, wasiwasi, Makombora, Mabomu ya Nyuklia, maangamizi , Uongo, Udanganyifu, Siasa, Mauti.

Lakini Bibi-arusi wana Bonyeza Play, na kusikia Sauti ya Mungu ikinena nao na kusema: Nguo ndefu Nyeupe, Kuhesabiwa haki, Kuchaguliwa tangu awali, changamko, Ufunuo, Kweli, Kunyakuliwa, Uzima wa Milele.

Usiogope ewe kipenzi, Mimi niko pamoja nawe, kila sekunde ya kila siku. Huu ndio mpango Wangu mkuu wote ambao Nimewaambia yote kuuhusu. Sasa, utazameni wote ukiwekwa wazi mbele ya macho yenu.

Wao : Hizi ni siku mbaya zaidi za maisha yetu; kila kitu kinaweza kufikia mwisho kesho.

Sisi : Hizi ndizo siku kuu za maisha yetu; kila kitu kinaweza kufikia mwisho kesho.

Mungu ana njia iliyoandaliwa, NENO LAKE. Yeye Alimtuma malaika-nabii wake pamoja na Neno Lake kumwita Bibi-arusi Wake atoke na kuwaongoza kwenye Makao yao Mapya aliyowaandalia.

Ikiwa ungependa faraja , amani, na uhakikisho huu huu tulionao; kama ungependa kuja kuishi katika Makao hayo ambayo yeye amemwandalia Bibi-arusi Wake; njoo uungane nasi Jumapili saa 6:00 Sita Mchana, saa za Jeffersonville, ( ni saa 2:00 mbili Usiku ya Tanzania), kusikia Njia pekee ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii, na kusikiliza sauti Yake iliyothibitishwa ikinguruma kwetu : Maswali Na Majibu juu ya Mihuri 63-0324M.

Muhtasari mdogo wa vichwa vya habari utakavyosikia Jumapili.

Ni kitu gani kitakachomuunganisha Bibi-arusi: Neno .

Neno humjia nani: Nabii .

Nani Aliye mfasiri wa kiungu wa Neno hilo: Nabii .

Sauti ya Mungu kwako ni nani: Nabii .

Tutahukumiwa kwa Maneno ya nani: Neno la Mungu lililonenwa na: NABII .

Ndugu. Joseph Branham

22-0306 Muhuri Wa Sita

Ujume: 63-0323 Muhuri Wa Sita

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Kondoo wa Mungu,

Ni jambo gani kubwa zaidi liwezalo kuwa, tunaweza kuwa watu waliyotunukiwa zaidi vipi , kuliko kuwa na Mfalme wa wafalme , Bwana wa mabwana miongoni mwetu ?

Hebu fikiria jambo hilo. Uwepo wa Mfalme wa wafalme, Bwana wa mabwana uko pamoja nasi. Ametufunulia kuwa TUMEWASILI. Tumefika! Ufunuo aliotupa unatoka kwa Mungu. Ni kweli. Sisi ni Bibi-arusi Wake na Kondoo waliochaguliwa.

Tunasikia barua Zake za upendo kila wiki zikituambia: “Wana-Kondoo wangu wapendwa, nimefanya mwito Wangu wa kondoo. Mbuzi hawaujui, bali ninyi mmeutambua. Mmedumu waaminifu, kwa maana kondoo Wangu wananijua mimi na mgeni hawatamfuata. Haina budi kuwa ni ishara Yangu ya kiroho Sauti iliyothibitishwa PEKE YAKE .”

Hamkuchezeana kimahaba huko au hata kumtazama mwingine; mmedumu waaminifu kwa Sauti Yangu. Ninyi Ndio wale Nimekuwa nikingojea. Najua mmefanyiwa mzaha na kutoeleweka, lakini niliwaambia Mimi nitarudi kwa ajili yenu kama MTADUMU NA NENO LANGU, nanyi mmedumu nalo. SASA NAKUJA KWA AJILI YENU kama nilivyowahidi ningefanya. Neno ambalo mmekuwa mkilimwagilia maji linakuja kuwapeleka kwenye Makao Yetu Mapya.

Wengine wanaweza kutokuwa na ufunuo sisi tulio nao na kusema kuwa tunaonyesha heshima ya kibinadamu ; au kumwabudu mwanadamu na sio Bwana wetu. Wao ni vipofu jinsi gani . Ikiwa hiyo ni kweli, basi Bibi-arusi wa Kristo ng’ambo ya pazia la wakati pia walikuwa wamekosea.

Wakati Nabii alipomwona Bibi-arusi wakimkimbilia na kusema, “ndugu yetu mpendwa,” walimtwaa juu na kumketisha Mahali pa Juu . Nini…je BIBI-ARUSI wa Kristo alikuwa akionyesha heshima ya kibinadamu kwa nabii kwa kumweka Mahali pa Juu? Je Unasema hawakupaswa kufanya hivyo?

Kisha baada ya hayo, Bibi-arusi wote walikuwa wamesimama pale wakiwa wamevaa nguo zao ndefu nyeupe na kuanza kupaza Sauti, “Kama usingalijitokeza na Injili, tusingalikuwa hapa.” Kama yeye asingalijitokeza wasingalikuwa kule?

Ndipo Sauti kutoka juu ikasema tutahukumiwa kulingana na NENO alilotuhubiria, kisha atatukabidhi kwake.
Sauti haikusema kwamba tutahukumiwa kwa yale mtu fulani aliyosema au yale mtu fulani aliyofafanua kuwa alisema , bali yale Yeye aliyosema . Ndipo yeye atatukabidhi Kwake.

Naweza kuchukua nafasi hii kuzungumza kwa niaba ya sehemu ya Bibi-arusi walio na Ufunuo ule ule nilio nao, na niseme jinsi tunavyohisi. Kama tutahukumiwa kwa Neno hilo , na KIKOMO CHETU CHA MILELE kinategemea Neno ambalo Mungu alilonena kupitia nabii Wake, basi hatuna budi kulisikia PEKE YAKE Neno hilo kutoka kwenye Sauti ya Mungu kwa ajili ya wakati wetu. Hatuwezi, na hatutaweka kikomo chetu cha Milele juu ya yale mtu Fulani anafafanua, au kusema, bali yale ALIYOSEMA. TUNAWEZA KUSIKIA TU SAUTI YA MUNGU PEKE YAKE , na William Marrion Branham ndiye SAUTI PEKEE YA MUNGU…MUNGU ALISEMA HIVYO.

Niliwaudhi kwa kusema hivyo, samahani , lakini, nilihisi huenda nilakuchukiza, lakini, mimi ni Sauti ya Mungu kwenu .

Kwa hiyo tuna furaha na tunamshukuru Bwana kwamba tunafanya kama vile wale Bibi-arusi walivyokuwa wakifanya upande wa pili. Utukufu, Heshima na Sifa zote zinamwendea BWANA wetu MMOJA NA WA PEKEE YESU KRISTO. Kama vile nabii wa Ufunuo 22:9 alivyotuambia, mwabudu Mungu … TUNAFANYA HIVYO na kumpenda sana.

Muda umechelewa . Maandiko yanatimizwa haraka kuliko tunavyoweza kusoma yote yanayotendeka. Anakuja kwa ajili ya Bibi-arusi Wake upesi. Ulimwengu unaungana. Bibi-arusi anaungana. Jukwaa linaandaliwa kwa ajili ya Unyakuo.

Tunamsifu Bwana kwa ajili ya watu walioitwa na Mungu wanaohubiri Neno, Lakini wahudumu, wekeni Sauti hiyo nafasi ya Kwanza ambayo ninyi na watu wenu mtahukumiwa kwayo. Kusanyikeni katika makanisa yenu na msikie Sauti pekee ya Mungu iliyothibitishwa ikinena. Bonyeza Play.

Tunawaalika wote ambao wangetaka kuja ndani ya Safina na kuokolewa pamoja nasi tunapoungana na kusikia Sauti ya Mungu ikinena Maneno tutakayohukumiwa kwayo, saa 6:00 sita mchana , saa za Jeffersonville, ( ni saa 2:00 Mbili Usiku ya Tanzania) na kusikia Muhuri wa Sita 63-0323 .

Ni Chakula cha Kondoo kwa Kondoo wa Mungu. Hakuna kilichoongezwa, hakuna kilichoondolewa na hakuna kilichofafanuliwa, ni CHAKULA safi cha KONDOO kisichoghoshiwa.

Ndugu. Joseph Branham.

Kutoka 10:21-23
Isaya 13:6-11
Danieli 12:1-3
Mathayo 24:1-30
Mathayo 27:45
Yohana 10:27
Ufunuo sura ya 6 yote
Ufunuo 11:3-6

22-0227 Muhuri Wa Tano

Ujume: 63-0322 Muhuri Wa Tano

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Mwili Mmoja Mkuu wa Kristo,

Ni nini kinachotukia leo? Neno la Mungu linatimizwa. Siku ambazo Bibi-arusi alizongojea kwa muda mrefu sasa zinadhihirishwa mbele ya macho yetu. Siku ambazo nabii wa Mungu alituonya zinakuja, sasa zimefika.

Muhuri unafunguliwa. Ni kitu gani hicho? Siri inafunguliwa. Mnaona? Na wakati siri inapofunuliwa, basi baragumu inalia. Inatangaza vita. Pigo linashuka, na wakati wa kanisa ukaanza .

. Urusi
. Vita
. Ukomunisti
. Mafuta
. Mapigo

Wakati Urusi inapoenda huko kupata mafuta hayo, jihadhari .

Urusi, ukomunisti hauteki cho chote! Neno la Mungu haliwezi kushindwa. Urumi utauteka ulimwengu .

Malaika wa maangamizi anaushikilia mkono wa Urusi, ulioshika mabomu ya atomiki ; mpaka Kanisa la Mungu litakapoungana pamoja, na Mwili mmoja mkuu wa Kristo . “ Siwezi kufanya neno lo lote hadi utakapoingia huku.” Loo, kama hilo si dhamana iliyobarikiwa !

Kanisa, Bibi-arusi Wake, anaungana pamoja kutoka ulimwenguni kote kama Mwili Mmoja Mkuu wa Kristo, wakimsikiliza Mungu akinena na kufunua Neno Lake. Tunaona Neno likitimizwa katika ulimwengu unaotuzunguka, lakini pia tunaona Neno likitimizwa na kudhihirishwa ndani yetu.

Tunapokea changamko kwa Ufunuo kuliko hapo awali wakati nabii hizi zinapotimizwa.

Dunia iko katika hofu na wasiwasi . Wanangojea, wanatazama na kushangaa, nini kitatokea baadaye? Kesho ina kitu gani?
Je, haya yote yanamaanisha nini? Je, Urusi itateka? Vipi kuhusu uchumi?

Wakati huohuo, Bibi-arusi yuko kwenye AMANI. TUNAPUMZIKA, tukiwa tumejazwa na Roho wake Mtakatifu, tukimsikiliza akinena kupitia malaika wake mkuu mwenye nguvu akituambia: Msiogope kitu chochote Enyi kundi langu dogo, ninyi ni Kipenzi wangu Waliochaguliwa . Ninyi ni:

Waliochaguliwa kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Amina! Nao ni waaminifu kwa Neno. Amina! Whiu! Ninapenda jambo hilo. “Wanaitwa, waliochaguliwa, kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.” Na halafu, ni waaminifu kwa Neno, kwa uchaguzi wao, wote wamechangamshwa na divai mpya na Mafuta, wamepanda farasi tu moja kwa moja, wakishuka kuja kukabiliana na yeye. Wao wanajua zile Ngurumo zitatoa jambo hilo kwa ajili yetu, karibuni sana .

Anatambua kwamba sisi ni waaminifu kwa Neno lake. Tumefanya hivyo kwa uchaguzi wetu. Sasa tumepanda farasi tu moja kwa moja , tukijua zile Ngurumo zitatoa jambo hilo kwa ajili yetu karibuni sana, Naye atakuja na kutupeleka kwenye Makao yetu Mapya.

Kuna mengi zaidi anayotaka sisi tujue. Kitu fulani kinawaka tu moyoni mwake anataka kutuambia. Hawezi kusubiri zaidi kwani anajua itatupa Changamko. Kwa neema ya Mungu, alimruhusu nabii Wake atuone sisi, watu wake, kule ng’ambo ya pili pamoja naye. Akasema, “Nilipowaona ninyi nyote mlikuwa na NGUO NDEFU NYEUPE .”

Tulikuwa  tumekusanywa pamoja naye. Tulimchukua na kumketisha mahali pa juu kwenye kitu kikubwa na kirefu. Tulimwambia, “duniani, ulikuwa kiongozi wetu”.

Kulikuwa na mamilioni yetu sisi tukimkimbilia na kumkumbatia tukimwita “Ndugu”. Mara moja Sauti kutoka juu ilinena na kusema, “Watu hawa ni waongofu wako ambao umewaongoza. Utahukumiwa kwa yale uliyowaambia”.

Nabii alinena na kusema, “Kama kundi la Paulo likiingia, na langu pia , maana nimehubiri Neno lile lile kabisa.” Na sisi sote tukapaza Sauti WOTE MARA MOJA, KWA SAUTI MOJA:

” Tunategemea Jambo Hilo !”

Jina la Bwana lihimidiwe, tunategemea kila Neno alilonena kupitia nabii Wake. Tutahukumiwa kwa Neno hilo. Tulikuwa watu wa nabii. Alikuwa kiongozi wetu aliyetuongoza kwa Kristo. Sisi Sote tulikuwa na Nguo ndefu Nyeupe. Hatukutegemea kile mtu fulani alichosema ati Alisema , au kile mtu fulani alichosema inamaanisha , tulitegemea kila Neno Yeye alilosema.

Ni siku na wakati wa jinsi gani wa kuishi, Bibi-arusi. Ukisikia taarifa ya habari leo hii, utajua kilichotokea jana. Bonyeza Play, nawe utasikia kile kitakachotokea kesho, na siku inayofuata, na siku inayofuata, na siku inayofuata.

Njoo ukusanyike pamoja na Mwili Mmoja Mkuu Wa Kristo saa 6:00 Sita Mchana , saa za Jeffersonville, ( Ni saa 2:00 mbili Usiku ya Tanzania) Kusikia: Muhuri wa Tano 63-0322. Hakuna Kushangaa, hakuna kudhania , Bali ni KUJUA unasikia BWANA ASEMA HIVI kutoka kwenye Sauti ya Mungu kwa ajili ya wakati wetu.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Danieli 9:20-27

Matendo 15:13-14

Warumi 11:25-26

Ufunuo 6:9-11 / 11:7-8 / 22:8-9