Category Archives: Uncategorized

26-0419 Kuchagua Bibi-Arusi

UJUMBE: 65-0429E Kuchagua Bibi-Arusi

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliyechaguliwa,

Wakati tunapousikiliza Ujumbe huu, Kuchagua Bibi-arusi, wengine wanafikiri kwamba nabii anazungumza tu na kutufundisha kuhusu tabia na kimo ambacho mwanamume anapaswa kuangalia wakati anapomchagua mwanamke anayemtaka awe mke wake. Hiyo ni kweli, anafanya hivyo, lakini hapo kuna barua ya mahaba halisi iliyofichwa katika Maneno Yake. Kile Yeye anachomfunulia Bibi-arusi Wake ni cha kina zaidi. Mungu anazungumza na Yeye(Bibi-arusi) moja kwa moja, akimwambia kile Yeye alichokuwa akikitafuta ndani Yake, na kwa nini Yeye alimchagua tangu mwanzo. Yeye alimtaka Yeye(Bibi-arusi) ajue kwamba Yeye amemchagua awe BIBI-ARUSI WAKE KIPENZI WA KUPENDEZA, ambaye Yeye alitaka ashiriki naye Umilele Wake.

Hapo mwanzo, Mungu alikuwa akimtafuta Bibi-arusi ambaye angekuwa na Tabia ile ile ya Kwake. Roho Wake yule yule angedhihirishwa ndani Yake(Bibi-arusi). Yeye alimtaka Bibi-arusi ambaye alikuwa amejitolea kabisa-kabisa Kwake, na Neno Lake lililoahidiwa, mpaka Nia ile ile iliyokuwamo ndani Yake iwe ndani yake Yeye(Bibi-arusi). Lazima afinyangwe kama Yeye alivyo.

Yeye alimtaka awe mwili Wake ule ule, mifupa ile ile, Roho yule yule, kila kitu kile kile, kama tu Yeye hasa. Wawili hao wangekuwa MMOJA.

Yeye hangekuwa na namna fulani ya macho jeuri. Yeye hangebembana huko na sauti nyingine yoyote. Yeye angekuwa mwaminifu na mkweli Kwake, haijalishi mtu yeyote angesema nini. Yeye angemkubali kwa Neno Lake. Chochote Yeye alichosema, YEYE ANGEAMINI KILA NENO, haijalishi ingechukua muda gani hilo kutimia, yeye angeliamini. Yeye angedumu na Neno Lake.

Yeye(Bibi-arusi) angempenda Yeye, na Yeye peke yake. Haikumlazimu Yeye kumpa utajiri mwingi, yeye alikuwa na Lulu ya thamani kuu, ule Ufunuo wa kweli wa Yeye( Bwana-Arusi). Yeye(Bibi-arusi) angejua, wao walikuwa MMOJA na kitu kimoja. Roho Wake angekaa ndani Yake. Chochote Yeye (Bibi-arusi) alichokihitaji, Yeye angempa; kitu tu Yeye(Bibi-arusi) alichopaswa kufanya ni kuomba na kuamini, na Yeye angekifanya.

Yeye(Bibi-arusi) alijua Yeye(Bwana-Arusi) angeondoka kwa muda mrefu kwenda kumjengea Yeye nyumba ambayo ingekuwa na kila kitu jinsi tu vile Yeye apendavyo kiwe na atakavyo. Yeye alikuwa akiijenga jinsi ambavyo Yeye (Bibi-arusi) angeipenda. Yeye (Bibi-arusi) alijua siku moja Yeye (Bwana-Arusi) angerudi kumchukua Yeye, kama Yeye alivyoahidi, kisha wangekuwa na Karamu Kuu ya Harusi kwa miaka elfu. Ndipo, wao wangeenda pamoja kwenye Makao hayo mazuri Yeye aliyomjengea waishi milele.

Hakuna kitu kingine ambacho kingekuwa muhimu kwake Yeye. Yeye asingetaka kitu kingine chochote. Yeye angeridhika mno na kutosheka na Ufunuo kujua Yeye (Bwana-Arusi) ni nani, na Yeye (Bibi-arusi) ni nani. Yeye (Bibi-arusi) angejua kwamba Yeye(Bwana-Arusi) angelitimiza Neno Lake. YEYE ANGETIMIZWA, AKIJUA YEYE NDIYE YULE AMBAYE YEYE ALIYEMCHAGUA KUWA BIBI-ARUSI WAKE.

Ndugu na dada zangu, Mungu mwenye nguvu wa Mbingu na nchi alitazama kote katika Umilele na AKAWACHAGUA NYINYI… NYINYI KUWA BIBI-ARUSI WAKE KIPENZI ALIYOWACHAGUA.

Ninawaalika mje muungane nami na sehemu ya Bibi-arusi Wake Jumapili hii, wakati Yeye anapozungumza kupitia malaika Wake Mwenye nguvu na kutuambia sisi ndio Bibi-arusi Wake Aliyowachagua.

Ndugu Joseph Branham

Ujumbe: 65-0429E / Kuchagua Bibi-arusi
Muda: saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki)

Maandiko Matakatifu:
Mwanzo 24:12-14
Isaya 53:2
Ufunuo 21:9

26-0412 Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake?

UJUMBE: 65-0418E Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake?

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Waliohuishwa,

Jinsi gani mioyo yetu ilivyoinuka kama Tai wikendi hii ya Pasaka. Siku baada ya siku, upako Wake ulizidi kuwa mkubwa. Ushirika, Kuzikwa, Ukamilifu, kisha kile kilele kikuu Alichotujengea: Ni Kuchomoza kwa Jua…UTUKUFU, AMEFUFUKA na Yuko hai ndani ya kila mmoja wetu. Yeye alikuwa akilifunua Neno Lake kwa kila mmoja wetu jinsi tusivyowahi kusikia hapo awali. Ule upako uliifurika mioyo yetu, uwepo Wake uliitanda hewa; ilionekana kana kwamba Unyakuo ulikuwa umekaribia.

Yeye alituambia yale yaliyotukia miaka 2000 iliyopita, na kisha yale yaliyokuwa yakitukia sasa mwaka wa 2026. Yesu alikuwa Chembe ya kwanza ya Ngano ya Mungu iliyofufuka kutoka kwa wafu. Yeye alikuwa amefufuliwa na Nguvu za Mungu za kuhuisha. Mungu alikuwa ameyahuisha maisha Yake, akamfufua kutoka kwa wafu, Naye alikuwa malimbuko ya kwanza ya wale waliolala. Yeye alikuwa wa kwanza kukomaa, Mganda wa Mungu uliotikiswa kama ukumbusho wa kutoa shukrani kwa Mungu, akiamini kwamba sisi wengine tungekuja. Ilikuwa ishara.

KISHA YEYE AKATUFUNULIA KILE KILICHOTUKIA LEO. Kama vile Yeye alivyotikiswa siku ya Pentekoste wakati sauti kutoka Mbinguni iliposikika kama upepo wa nguvu ukienda kasi ukitikiswa juu ya watu. Ulikuwa ukitikiswa tena mbele ya watu kama alivyoahidi katika Luka 17:30 na Malaki 4, wakati Mwana wa Adamu atakapofunuliwa na kutikiswa tena juu ya watu.

Sasa, Mwana wa Adamu ni Nani? “Hapo mwanzo alikuwako Neno, naye Neno alikuwa kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Naye Neno akafanyika mwili, akakaa kwetu.” Na iwapo mafundisho yote tuliyo nayo, na thibitisho la Neno la Mungu; kwa Neno la Mungu, kwa ishara, kwa maajabu, tunaona leo, ya kwamba katika Kitabu cha—cha Luka hapa, ya kwamba kama tulivyonukuu hicho hivi punde, ama Lu—Luka mlango wa 17 na kifungu cha 30; na Malaki 4, na Maandiko mbalimbali ambayo tunayajua, ya kwamba hilo Neno tena linatikiswa juu ya watu, ya kwamba mapokeo yaliyokufa ya mwanadamu yamekufa, na Mwana wa Mungu yu hai tena na ubatizo wa Roho Mtakatifu moja kwa moja miongoni mwetu, naye anatupa Uzima.

Roho Mtakatifu aliendelea kutikisa na kutikisa juu yetu, akifunua na kufunua Neno Lake… Nguvu za utendaji, mitambo, Nguvu za kuhuisha…

Ndipo, ilipoonekana kana kwamba Haiwezi kuwa kuu zaidi, Yeye alituambia:

Naye akaniruhusu niangalie ng’ambo ya pazia, nami nikawaona ninyi nyote kule ng’ambo… Wote uliowahi kupenda, na wote waliowahi kukupenda, umepewa wewe.” Mnaona? Niliwaona hao kila mahali pale namna hiyo. Ilikuwa nini? Nguvu za kuhuisha.

YEYE ALITUONA SISI KULE!! Ng’ambo ya pazia la wakati….tulikuwa KULE pamoja naye; wapendwa wetu wote waliotutangulia…akina baba, mama, watoto. Tulikuwa kule pamoja nao na wale wote ambao hatujawahi kukutana nao: Musa, Eliya, Petro, Paulo….tulikuwa sote kule pamoja.

Kisha, kama vile Roho Mtakatifu alivyo mzuri, Yeye hakutaka kutusahau sisi tulio wagonjwa, wenye huzuni na waliopigwa, kwa hivyo Yeye alijitikisa Mwenyewe juu yetu tena ili kila mtu aponywe chochote kile tulichokuwa na haja nacho.

Watu hawa, ambao ni raia wenza wa Ufalme, mmiliki wa Nguvu za kuhuisha, lihuishe kwao, Bwana, sasa hivi. Pia naomba Roho aende kutoka tai hadi tai, kutoka kwenye Neno hadi Neno, mpaka utimilifu wa Yesu Kristo udhihirishwe katika kila mmoja wa hiyo miili, kwa ajili ya haja za kimwili, za kiroho, ama haja zozote walizo nazo, tunapowekeana mikono sisi kwa sisi. Katika Jina la Yesu Kristo.

Neno Hilo. Sauti Hiyo. KILA KITU tunachokihitaji kiko kwenye kanda, Ewe, Bibi-arusi. Mungu habadilishi nia Yake kuhusu Neno Lake. Hakuna nukta moja au yodi moja inayoweza kubadilishwa, kwa hivyo Yeye alitengeneza njia ambayo Bibi-arusi Wake angeweza kusikia kwa masikio yao wenyewe kile hasa Yeye alichotaka kuwaambia.

Mungu amenena na Bibi-arusi Wake na kufunua KILA KITU. Kimerekodiwa. Bibi-arusi lazima aje kwa Bwana Arusi; hiyo ndio Njia Yake kamilifu iliyoandaliwa ambayo imetengenezwa kwa ajili ya siku hii. Ni BWANA ASEMA HIVI.

Je! Mungu hubadilisha Nia Yake kuhusu Neno Lake? HAPANA. Yeye anayo MAPENZI MAKAMILIFU NA MAPENZI YAKURUHUSIA.  Bibi-arusi yambidi awe katika MAPENZI YAKE MAKAMILIFU. Hakuna Mapenzi yaliyo makamilifu zaidi, au mahali pakamilifu, kuliko kuisikia Sauti ya Mungu moja kwa moja kutoka kwa Mungu Mwenyewe.

Mwaliko wangu kwa kila mmoja wenu ni muungane nasi Jumapili saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville(ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki), kuisikia Sauti ya Mungu ikituletea Neno Safi. Hakuna haja ya kubahatisha, wewe keti tu na useme AMINA KWA KILA NENO….hakuna mahali pengine hilo linaweza kufanywa, ila kwa KUBONYEZA PLAY.

Ndugu Joseph Branham.

Ujumbe: 65-0418E — Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake?

Tutaanzia kwenye aya ya 61.

Maandiko ya kusoma kabla ya kuusikia Ujumbe:

Kutoka sura ya 19

Hesabu 22:31

Mathayo Mt. 28:19

Luka 17:30

Ufunuo sura ya 17

PASAKA 2026 – Ibada Maalum ya Ushirika na Kutawadhana MIGUU

Wapendwa Raia Wenza Wa Ufalme,

Pasaka hii inaahidi kuwa Pasaka iliyo kuu kuliko ambayo Bibi-arusi amewahi kuwa nayo. Tumekuwa tukiketi katika Uwepo wa Mwana, tukiivishwa, tukijitambua sisi ni nani. Ule utimilifu wa Yesu Kristo unadhihirishwa ndani ya kila mmoja wetu huku Neno Lake, Sauti Yake, ikipiga kelele, Tai kwa tai, ikituita kutoka kwenda kwenye Karamu yetu ya Arusi.

Kila mwaka wakati huu Bibi-arusi anaisubiri kwa hamu kubwa wikendi ijayo ya Pasaka. Wakati ambapo Yeye atatuunganisha kutoka kote ulimwenguni kwa siku nne mfululizo, tukimwabudu Yeye, tukimshukuru Yeye, tukimsifu Yeye; kwa maana Yeye amefufuka na anaishi ndani ya kila mmoja wetu. Bwana Arusi na Bibi-arusi wanakuwa MMOJA.

Yeye anatupa sisi wakati huu maalum wa kufungia nje vitu vyote vya kilimwengu vinavyotuzunguka na kuutumia tu muda pamoja Naye. Hakuna vizubaishi vya kilimwengu huu, huku tunapouumba ulimwengu wetu wenyewe pamoja Naye. Tufunge milango yetu, tuvizime vifaa vyetu vyote vya kielektroniki na chochote kinachotukengeusha kutoka Kwake.

Haja iliyo kuu ambayo kila mmoja wetu aliyonayo ni kuwa karibu Naye. Tunataka kuishi maisha yaliyowekwa wakfu zaidi kwa ajili Yake; kuwa daima katika mapenzi Yake makamilifu. Kuwa tayari kwa ajili ya Kuja Kwake. Hakuna chochote katika ulimwengu huu, au katika maisha yetu, kilicho muhimu zaidi kuliko hili.

Yeye ametupa sisi fursa hii maalum ya kuutumia tu muda pamoja Naye, kuzungumza na kumtafakari Yeye. Kuingia katika uwepo Wake na kuifungua mioyo yetu Kwake. ITAKUWA IBADILISHAYO MAISHA KWA BIBI-ARUSI WAKE!

Yeye anajua yaweza kuwa vigumu kwa baadhi yenu wenye watoto, familia, na majukumu mengine tuliyo nayo, lakini tukiitumia kila sekunde huru tuliyonayo kuzungumza Naye, kumkaribia Yeye, kumfungulia Yeye mioyo yetu, kutakuwako na badiliko kubwa katika kutembea kwetu pamoja Naye, hata hatutakuwa vile tulivyokuwa.

Kama vile Yeye alivyofanya katika ile siku ya Musa alipowaleta watoto Wake majumbani mwao, damu ilikuwa imepakwa nao walikuwa wakijiandaa kwa ajili ya kule Kutoka kwao; itakuwa vivyo hivyo na wikendi hii maalum ya Pasaka ambayo Yeye ameiandaa kwa kila mmoja wetu.

ALHAMISI

Ilikuwa ni Alhamisi usiku ambapo Bwana Yesu aliila Karamu ya Mwisho pamoja na wanafunzi Wake, katika ukumbusho wa Pasaka kabla ya kule kutoka kwa wana wa Israeli. Tunayo fursa iliyoje ya kufanya ushirika na Bwana majumbani mwetu, kabla ya wikendi yetu takatifu, na kumwomba Yeye atusamehe dhambi zetu, na atupe yote tunayohitaji katika safari yetu.

Baba wa Mbinguni, tunashukuru kwa ajili ya jambo hili, wakati mwingine wa kukusanyika pamoja, upande huu wa Umilele. Na tunatarajia asubuhi ya leo kuhuishwa upya kwa nguvu kuja kutoka Kwako, zipate kututia moyo kwa ajili ya safari iliyoko mbele. Tumekusanyika kama wana wa Kiebrania walivyofanya asubuhi na mapema, kuokota mana iliyokuwa imetolewa kwa ajili yao usiku kucha, kuwapa nguvu kwa ajili ya siku ijayo. Tunakusanyika kwa ajili ya Mana ya kiroho, asubuhi ya leo, ipate kutupa nguvu kwa ajili ya safari.

Hebu sote tuanze saa 12:00 KUMI NA MBILI JIONI. masaa ya eneo unaloishi ili kusikiliza Ushirika 62-0204, na kisha nabii atatupeleka kwenye ibada yetu maalum ya Ushirika na Kutawadhana Miguu baada ya kanda kukamilika, ambayo itachezwa kwenye app ya Lifeline (kwa Kiingereza), au unaweza kuipakua ibada hiyo kwa Kiingereza au lugha zingine kwa kubofya anuani iliyo hapa chini.

IJUMAA

Hebu na twende katika maombi pamoja na familia zetu saa 3:00 TATU ASUBUHI,(Ni saa 10:00 KUMI JIONI ya Afrika Mashariki) na kisha tena saa 06:00 SITA MCHANA,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki), tukimwalika Bwana awe pamoja nasi na kuzijaza nyumba zetu kwa Roho Mtakatifu tunapojiweka wakfu Kwake.

Hebu akili zetu na zirudi huko nyuma hadi kwenye siku ile pale Kalvari, yapata miaka 2000 iliyopita, na kumwona Mwokozi wetu akining’inia msalabani. Na tukumbuke ile gharama kuu Yeye aliyoilipa kwa ajili yetu. Yeye alikuwa Mwana wa Mungu asiye na dhambi, lakini ilibidi ateseke kuliko mtu mwingine angeweza kuteseka, kwa sababu dhambi zetu sisi ziliwekwa juu Yake.

Ilibidi amtume Yeye kuzimu akiwa amehukumiwa (Unaona?), kwa sababu Yeye alizichukua dhambi zetu. Naye Kristo alikufa, si mwenye haki; Kristo alikufa mwenye dhambi. Unaona? Kristo mwenyewe hakutenda dhambi, bali alizichukua dhambi zetu juu Yake.

Kisha saa 06:30 SITA NA NUSU MCHANA,(Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) na tuungane pamoja majumbani mwetu kusikia: 57-0419 Ukamilifu.

Kisha na tuungane tena katika maombi mara tu baada ya ibada, katika ukumbusho wa kusulubiwa kwa Bwana wetu.

JUMAMOSI

Hebu na tuungane tena sote katika maombi saa 3:00 ASUBUHI (Ni saa KUMI JIONI ya Afrika Mashariki) na saa 06:00 SITA MCHANA,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) na tuiandae mioyo yetu kwa ajili ya mambo makuu Yeye atakayotutendea sisi miongoni mwetu.

Ninaweza kumsikia akisema, “Shetani, njoo hapa!” Yeye ni Bosi sasa. Ananyosha mkono, anaunyakua ule ufunguo wa mauti na kuzimu kutoka ubavuni mwake, akauning’iniza ubavuni Mwake Mwenyewe. “Ninataka kukupa notisi. Umekuwa laghai muda mrefu kutosha. Mimi ni Mwana wa Mungu aliye hai niliyezaliwa na bikira. Damu Yangu ingali imelowa msalabani, na deni kamili limelipwa! Huna haki tena. Umenyang’anywa zote. Nipe funguo hizo!”

Kisha saa 06:30 SITA NA NUSU MCHANA,(Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) sote tutakusanyika pamoja kulisikiliza NENO: 57-0420 Kuzikwa.

Hii itakuwa SIKU ILIYO MAALUM vipi kwa Bibi-arusi Wake kote ulimwenguni.

Kisha hebu na tuungane tena pamoja katika maombi mara tu baada ya ibada.

JUMAPILI

Hebu kwanza na tuamke mapema kama vile Ndugu Branham alivyofanya asubuhi ile wakati rafiki yake mdogo, robini, alipomwamsha saa 11:00 Alfajiri. Natumshukuru tu Bwana kwa kumfufua Yesu kutoka kwa wafu:

Saa kumi na moja asubuhi ya leo, maskini rafiki yangu mwenye kifua chekundu aliruka dirishani akaniamsha. Ilionekana kana kwamba moyo wake mdogo ungepasuka, akisema, “Amefufuka.”

Saa 3:00 TATU ASUBUHI, (Ni saa KUMI JIONI ya Afrika Mashariki) tuungane tena katika mnyororo wetu wa maombi, tukiombeana na kujiandaa kuisikia Sauti ya Mungu.

Saa 3:30 TATU NA NUSU ASUBUHI, (Ni saa KUMI NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) tutakusanyika pamoja kuusikiliza Ujumbe wetu wa Pasaka: 65-0418M Ni Kuchomoza kwa Jua.

Saa 06:00 SITA MCHANA. (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tutaziinua sauti zetu Kwake tukimshukuru kwa ajili ya Nguvu za Kuhuisha.

Saa 9:00 TISA ALASIRI.(Ni saa 4:00 NNE USIKU ya Afrika Mashariki), Hebu na tuungane tena katika maombi, tukimshukuru Yeye kwa ajili ya WIKENDI YA KUPENDEZA ALIYOTUPA SISI PAMOJA NAYE NA BIBI-ARUSI WAKE KOTE ULIMWENGUNI.

Kwa ndugu na dada zangu walio nchi za ng’ambo, kama vile mwaka jana, ningependa kuwaalika muungane nasi katika masaa ya Jeffersonville, kwa masaa yote ya maombi katika ratiba hii. Hata hivyo, ninatambua kwamba kuzicheza Kanda Alhamisi, Ijumaa, na Jumamosi alasiri kwa masaa ya Jeffersonville itakuwa vigumu sana kwa wengi wenu, kwa hivyo tafadhali jisikieni huru kuzicheza Jumbe hizo kwa masaa yafaayo kwenu. Hata hivyo, ningependa sote tuungane pamoja Jumapili saa 3:30 TATU NA NUSU ASUBUHI masaa ya Jeffersonville (Ni saa 10:30 KUMI NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki), kuusikia Ujumbe wetu wa Jumapili pamoja.

Pia ningependa kukualika wewe na watoto wako kuwa sehemu ya vipindi vya Creations, Journaling na mapishi, ambayo familia yako yote inaweza kufurahia pamoja. Tunafikiri mtayapenda kwani yote yanalenga NENO tutakalolisikia wikendi hii.

Kwa ajili ya ratiba ya wikendi, taarifa kuhusu jinsi ya kujiandaa kwa ajili ya ibada ya Ushirika, nyenzo zitakazohitajika Kwa ajili ya vipindi vya Creations, na taarifa nyinginezo, tazama anuani zilizo hapa chini.

Hebu tuzifunge simu zetu kwa ajili ya wikendi ya Pasaka isipokuwa kupiga picha, kusikiliza Nukuu ya Siku, na kucheza kanda kutoka kwenye app ya The Table, app ya Lifeline, au kwenye anuani ya kupakulia.

Ni heshima kubwa kwangu kukualika wewe na familia yako kuja pamoja na Bibi-arusi ulimwenguni kote katika wikendi iliyojaa KUABUDU, KUSIFU NA UPONYAJI. Ninaamini kweli hii ni wikendi ambayo itayabadilisha maisha yako milele.

Ndugu Joseph Branham

26-0329 Huyu Melkizedeki Ni Nani?

UJUMBE: 65-0221E Huyu Melkizedeki Ni Nani?

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Uzima Wa Milele,

Sauti hiyo ni nani inayozungumza nasi kwenye kanda?

Tunaweza tu kujua jibu la swali hilo kwa Ufunuo kutoka kwa Mungu. Ni Bibi-arusi Wake aliyechaguliwa tangu zamani peke yake ndiye atakayekuwa na Ufunuo huo. Kwa hivyo, lazima tutafute Neno Lake ili kuelewa alisema Yeye alikuwa ni nani: Mfasiri pekee wa Neno Lake. Ni nani angeivunja na kuifunua ile Mihuri Saba? Ni nani angezifunua siri zote zilizofichwa za Biblia? Ni nani atakayemwita atoke na kumwongoza Bibi-arusi Wake? Ni nani atakayekuwa na ile Sauti ya kutokukosea?

Kulingana na Neno, si mwingine ila Melkizedeki, Yeye Mwenyewe. Mtu asiye na baba wala mama, Ambaye hakuwa na mwanzo wala mwisho wa siku Zake. Mungu, Ambaye alifanyika mwili na akala nyama na mkate wa mahindi, akanywa maziwa ya siagi, na akanena na Ibrahimu. Yeye alikuwa Mtu mwenye utu, akiishi katika mwili wa mwanadamu.

Neno lilo hilo lililosema kwamba Melkizedeki, Mtu huyo, utu huo, angeishi na kujifunua Mwenyewe tena katika mwili wa mwanadamu kama vile alivyofanya kwa Ibrahimu, kisha tena katika Yesu Kristo; bali leo, katika malaika-mjumbe Wake wa saba wa Ufunuo 10:7.

Roho Wake angeiteketeza hiyo maskani ya duniani ili Yeye aweze kuzungumza na kujifunua Mwenyewe kwa Bibi-arusi Wake. Mungu Mwenyewe akiishi na kuzungumza katika mwili wa mwanadamu. Mbegu Yake ya kwanza iliyorejeshwa kikamilifu ilikuwa imefikia kukomaa kabisa. Ule mpango kamili wa Mungu ulikuwa umewasili; Mungu na mwanadamu walikuwa Mmoja. Mungu alikuwa akizungumza mdomo kwa mdomo na Bibi-arusi Wake kama alivyofanya kwa Ibrahimu.

Akaingia na kuishi katika huo, katika Utu wa Melkizedeki. Ndipo baadaye hatukusikia tena habari za Melkizedeki, kwa sababu Yeye alifanyika Yesu Kristo. Melkizedeki alikuwa yule Kuhani, bali akafanyika Yesu Kristo, Basi, wewe uliruka hilo, kwa kuwa katika umbo hilo Yeye alijua yote, Nawe haujapata kujua hayo bado.

BADO…!! Basi sisi ni nani?

Macho yetu, kimo chetu, chochote kile tulichokuwa, tulikuwa katika mawazo Yake hapo mwanzo. Kabla hajakuwepo Malaika, nyota, Kerubi, au chochote kile. Yeye aliliwazia, Akalinena, nasi hawa hapa.

Hiyo ni isiyo kikomo. Hatuwezi kuelewa kwa akili zetu. Bali huyo ni Mungu. Mungu, asiye kikomo.

Kwa kuwa tulikuwa ndani Yake hapo mwanzo, nini kinachotokea kwetu sisi baada ya maisha haya yapatikanayo na mauti hapa duniani kwisha?

Joho hili la mwili linapobwagwa chini, kunao mwili wa kawaida, mwili wa kiungu, mwili ambao haukujengwa kwa mikono, wala kuzaliwa na mwanamke, ambamo tunaingia. Ndipo huo mwili unarudi huku na kuchukua mwili uliotukuzwa.

Ni mambo ya kupendeza vipi aliyowekewa Bibi-arusi Wake. Angalia yale yanayoendelea sasa hivi wakati Yeye akitufunulia Neno Lake zaidi ya wakati wowote ule. Nena kuhusu barua ya mahaba kwa Bibi-arusi Wake! Ni siku iliyoje tunayoishi.

Tuna Ufunuo na tunajua ni Melkizedeki, Sauti ya Mungu, anayezungumza nasi kwenye kanda. Tuna Ufunuo ndio mapenzi ya Mungu yaliyoandaliwa na makamilifu kwa ajili ya siku hii. Hivyo, tunamjua YEYE NI NANI NASI NDIYE BIBI-ARUSI WAKE.

Ufunuo huo unazidi kuwa mkubwa zaidi na zaidi kila siku. Kila siku ipitayo hutuletea furaha zaidi, Ufunuo zaidi. Bibi-arusi anajiweka mwenyewe tayari kwa kuketi katika uwepo wa Sauti Yake, Yeye anapotuambia Sisi ni nani, jinsi gani Yeye anavyotupenda Sisi, jinsi ambavyo Yeye anavyosubiri kwa hamu kuwa pamoja Nasi!!!

Njooni, mjiweke tayari saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) kwa ajili ya kile kinachokaribia kutukia, tunapoisikiliza Sauti ya Melkizedeki.

Ndugu Joseph Branham

Ujumbe: 65-0221E “Huyu Melkizedeki Ni Nani?”

Maandiko ya kusoma:
Mwanzo Sura ya 18
Kutoka 33:12-23
Yohana Mt. 1:1
Warumi 8:1
2 Wakorintho 5:1
1 Wathesalonike 4:13-18
Timotheo wa Kwanza 3:16 / 6:15
Waebrania 7:1-3 /13:8
Ufunuo 10:1-7 / 21:16

26-0322 Ndoa Na Talaka

UJUMBE: 65-0221M Ndoa Na Talaka

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliyechaguliwa, Mteule, na Aliyekusudiwa Kimbele:

Nakumbuka nilipokuwa kijana mdogo nikikua, nikijaribu kuchagua kanda ya kusikiliza. Nilipokuwa nikisoma majina ya jumbe daima Niliwaza, sitasikiliza Ndoa na Talaka, kwani huo hauna uhusiano wowote nami; ni kwa watu waliooa tu.

Kisha siku moja, nilipokuwa nikisikiliza Ndoa na Talaka, Baba akanipa Ufunuo wa Ujumbe huo. Upako Wake ulikuja moyoni mwangu. Yeye anazungumza nami. Ujumbe huu NI kwa ajili yangu. ANANIAMBIA Alinichagua mimi kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Huu ndio sherehe yangu ya arusi. Simtaki mtu mwingine ila Yeye. Mimi ni mkweli na mwaminifu Kwake, na kwa Neno Lake, na kwa Sauti Yake, PEKE YAKE. Sisi ni MMOJA.

Kwa kweli Ujumbe huu ulikuwa kwa ajili ya ndugu na dada wengi waliokuwa wameoana na sasa wamepeana talaka, na Yeye akiwaambia kile wanachopaswa kufanya; Lakini hapo kulikuwa na maana KAMILI NA KUBWA zaidi, iliyo kuu zaidi, yenye nguvu zaidi.

Kulikuwa na Mume mmoja, na Yeye alikuwa akiwaita na kuzungumza na Bibi-arusi Wake wengi, waliochaguliwa.  SAUTI YA MUNGU ILIKUWA IKIMWITA ATOKE BIBI-ARUSI MSAFI, NENO BIKIRA WAKE, ASIYEGHOSHIWA. Yule ambaye hajaguswa au kuchafuliwa na mwanamume. Yule ambaye ni mkweli na mwaminifu Kwake na kwa Neno Lake peke yake. Yule ambaye aliyeridhika kabisa Naye na Sauti Yake.

Kwa Neema na Rehema Zake, leo tunaweza kusema, bila shaka yoyote, SISI NDIYE BIBI-ARUSI NENO BIKIRA WAKE. UTUKUFU!!

Yeye alitaka kuhakikisha kuwa hakutakuwa na mambo yaliyoachwa linapokuja suala la kumwita Bibi-arusi Wake, kwa hivyo Yeye alikuja Mwenyewe na kuishi katika mwili wa mwanadamu ili kulifunua Neno Lake na kumwita Bibi-arusi Wake Kwake. Yeye alikuwa ndiye Eliezeri ambaye angemchagua Bibi-arusi Wake mwenyewe.

Ili kuhakikisha kuwa hakukuwa na njia ambayo tungechanganyikiwa ni nani aliyekuwa akituchumbia, Yeye Mwenyewe alikithibitisha chombo Chake kiteule kwa kuzungumza naye kutoka katika kisulisuli kilichokuwa kikining’inia kwenye mti. Kisha akazungumza naye waziwazi kule chini kwenye Mto Ohio mbele ya maelfu.

Yeye hata alipigwa picha pamoja naye ili kuuonyesha na kuuambia ulimwengu, NILIWAAMBIA NITARUDI TENA NA KUISHI KATIKA MWILI.  YEYE NDIYE NILIYEMCHAGUA KUISHI NDANI YAKE, KUWAITA NINYI MTOKE ILI MUWE BIBI-ARUSI WANGU. SI YEYE; NI MIMI NINAYENENA KUPITIA YEYE. NINAITUMIA SAUTI YAKE TU KUWA SAUTI YANGU KWENU. MIMI NDIYE NILIYEWAITA NA KUWAKAMILISHA ILI MUWE BIBI-ARUSI WANGU MKAMILIFU.

Ufunuo wa Ujumbe Huu, Neno Lake, Sauti Yake, na sasa SISI ni NANI yapita maneno ya mwanadamu kujaribu kueleza. Najua mnajua hasa kile ninachosema. Imani ya kunyakuliwa inatendeka. Bibi-arusi anajiweka Mwenyewe tayari kwa kuketi katika uwepo wa Mungu Mwenyewe, akikamilishwa.

Ni fursa iliyoje dunia iliyonayo kuisikia Sauti ya Mungu ikizungumza nao; kuketi na kulisikiliza Neno kwa Neno anaponena na kulifunua Neno Lake na kutuambia sisi ni nani. Hakuna cha kufananisha na kuketi katika uwepo Wake, kwa hivyo njooni muungane nasi Jumapili saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapomsikia Yeye akizungumza na Bibi-arusi Wake, Ujumbe, “Ndoa Na Talaka” 65-0221M.

Ndugu Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kuusikia Ujumbe:

Mathayo Mt 5:31-32 / 16:18 / 19:1-8 / 28:19

Matendo 2:38

Warumi 9:14-23

Timotheo wa Kwanza 2:9-15

Wakorintho wa Kwanza 7:10-15 / 14:34

Waebrania 11:4

Ufunuo 10:7

Mwanzo sura ya 3

Walawi 21:7

Ayubu 14:1-2

Isaya 53

Ezekieli 44:22

26-0315 Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia

UJUMBE: 65-0220 Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bi. Yesu Kristo,

Hii ndiyo siku yenyewe. Huu ndio wakati wenyewe. Mungu alimtuma tai Wake mwenye nguvu duniani kumwita Bi. Yesu Kristo Wake atoke, kunena na kumwambia, “Wewe NDIYE niliyemchagua. Wewe NDIYE ninayempenda. Wewe ndiye Bibi-arusi Neno bikira Wangu Mkamilifu. Sisi ni MMOJA.”

Kuyasikia maneno hayo tu, mioyo yetu inaruka kwa furaha. Kuwazia, katika ulimwengu wote, pamoja na mamilioni na mamilioni yake ya watu, kuna Bi. Yesu Kristo MMOJA tu, na WEWE ndiye Huyo, YULE anayemjia.

Kuna mahali PAMOJA tu palipochaguliwa pa kuabudia. Kuna Ujumbe MMOJA tu mkamilifu uliochaguliwa. Kuna BIBI-ARUSI MMOJA tu MKAMILIFU aliyechaguliwa…NASI NDIO!!

Baba ana mahali PAMOJA peke yake alipopachagua pa kuabudia, Bwana Yesu Kristo; Yeye ni Neno. Leo, kuna mahali PAMOJA peke yake ambapo mauti ya kiroho haiwezi kupiga: Neno. Mauti haiwezi kulipiga Neno, kwa sababu ni Neno la Mungu lililo Hai.

Ufunuo kamili wa Neno hilo lililo Hai umefunuliwa kwa Bi. Yesu Kristo peke yake. Kuna mahali PAMOJA tu palipochaguliwa ambapo Bi. Yesu Kristo anaweza kwenda na kulisikia NENO KAMILIFU LIKINENWA. Kuna nabii MMOJA tu aliyechaguliwa kuwa Sauti ya Mungu. Kuna mahali PAMOJA tu ambapo Bi. Yesu anapoweza kwenda na kuisikia, BWANA ASEMA HIVI: KUBONYEZA PLAY.

Kutakuweko Nuru mnamo wakati wa jioni, mahali pekee alipopachagua Mungu pa kuabudia. Loo, Ujumbe huu umefika wapi, Yeye atafanya nini? Na katika siku yake itakuweko Nuru wakati wa jioni, na (nini?) kuwakaribisha watoto Wake wanaporudi nyumbani kwenye Nchi ya kweli ya ahadi, kwa ishara ile ile ya Nguzo ya Moto ambayo iliwaongoza wana wa Israeli kupitia nyikani.

Jinsi gani Bibi-arusi Wake anavyopaswa kuwa mwangalifu kuifuata na kuisikia Sauti ya Mumewe ikizungumza Naye. Kuna mahali PAMOJA tu tunapoweza kwenda na kuwa na hakika 100%. Kuna Sauti MOJA tu tuliyoiwekea kikomo chetu cha Milele.

Bi. Yesu Kristo anaamini kwamba Maneno anayoyasikia kwenye kanda ni Maneno ya Mumewe. Yeye anaamini Neno Lake halihitaji fasiri yoyote. Kwa hivyo, Yeye anaamini kuna mahali PAMOJA tu palipoandaliwa ambapo Yeye anapoweza kwenda na kusema AMINA kwa kila Neno, Sauti ya Mumewe iliyo kwenye kanda.

Kwa mara nyingine tena, Bi. Yesu Kristo, kutoka kote ulimwenguni, anaweza kusema, “Leo, Neno hili lililonenwa, linatimizwa”.

Mungu Mpenzi, huko chini kuvuka majangwa kule Tucson, huko mbali California, juu huko Nevada na Idaho, kwenda hadi Mashariki na kila mahali, chini huko Texas; wakati mwaliko huu unatolewa, watu wamekiketi katika—katika makanisa madogo, vituo vya mafuta, majumbani, wakisikiliza.

Umealikwa kuja kusikiliza pamoja na Maskani ya Branham saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapomsikia Mungu akizungumza na Bibi-arusi Wake mteule, Ujumbe: “Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia” 65-0220.

Ndugu Joseph Branham

Maandiko: Kumbukumbu la Torati 16:1 hadi 3.