Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukutanike pamoja Jumapili saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1 JIONI ya Afrika Mashariki) kusikiliza 60-1210 Wakati Wa Kanisa La Filadelfia.
Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukutanike pamoja Jumapili saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) kusikiliza 60-1209 Wakati Wa Kanisa la Sardi.
Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukutanike pamoja Jumapili saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(ni saa 1 JIONI ya Afrika Mashariki) kusikiliza 60-1207 Wakati wa Kanisa la Pergamo.
Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukutanike Jumapili saa 06:00 MCHANA masaa ya Jeffersonville, (ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) Kusikia 60-1205 Wakati Wa Kanisa La Smirna.
Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukutanike Jumapili saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) kusikiliza 60-1205 Wakati wa Kanisa la Efeso.
Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukusanyike pamoja Jumapili saa 06 MCHANA masaa ya Jeffersonville, (ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) kusikia 60-1204E Ono La Patimo.
Jinsi gani tunavyopenda neno, UFUNUO! Umuhimu wa Ufunuo WOTE wa Kweli kupitia Roho Mtakatifu kwa mwamini wa kweli hauwezi kamwe kutiliwa mkazo sana. Ufunuo ni zaidi ya maisha kwa Bibi-arusi; kwani juu ya MWAMBA HUU, UFUNUO, nitalijenga Kanisa langu, na kwa neema na rehema za Mungu, sisi ndilo Kanisa Lake lenye Ufunuo Wake wa Kweli.
Kitabu cha Ufunuo hakikukusudiwa kwa kila mtu. Hakuna mtu anayeweza kukielewa. Ni Kitabu cha kinabii kilichoandikwa kwa ajili ya, na kinaweza tu kueleweka na, tabaka la watu wa kinabii: SISI, Bibi-arusi wa Yesu Kristo.
Ndicho Kitabu pekee ambacho Kristo alikiandika Mwenyewe katika Biblia nzima, bali alikituma na kukionyesha kupitia malaika Wake kwa mtumishi Wake Yohana. Wanafunzi hawakuzijua kweli hizi zilizorekodiwa. Haikuwa imefunuliwa kwao hapo awali. Hata Yesu hakuweza kuwaambia kuhusu nafasi Yake Yeye ndani ya Hilo; kwani Baba alikuwa hajamfunulia Yeye hilo.
Lakini sasa, baada ya mauti na kufufuka Kwake, na katika wakati huu maalum, Yeye anaweza kumweleza Yohana Ufunuo huu wa Yeye Mwenyewe, kile utukufu Wake na uwepo katika kanisa ungemaanisha na kutenda.
Lakini hata sasa, baada ya miaka elfu mbili, ulimwengu umetafakari, wanatheolojia wamesoma na kuwazua, bali hakuna mtu aliye na fasiri sahihi na Ufunuo wa siri hizi zilizoandikwa katika Kitabu cha Ufunuo hadi leo hii, hadi wakati huu, ambapo Mungu alimtuma malaika yuyo huyo duniani ili kuyafunua yote Hayo kwetu sisi, Bibi-arusi Wake aliyemchagua.
Kujaribu kuelewa ukubwa wa kwamba Mungu alinichagua mimi, na Alikuchagua wewe; kuwa na Ufunuo wa Kweli wa Neno Lake yapita maelezo ya kibinadamu. Ingawa kuna wengi wanaodai wanaufuata Ujumbe na kusema wanaamini Mungu alimtuma nabii, wao hawana Ufunuo kamili kwa kujua matokeo ya kutoifanya Sauti Yake kuwa ndio sauti iliyo muhimu zaidi ambayo HAWANA BUDI KUISIKIA. Kuwa na Ufunuo huu wa Sauti Yake katika siku hii kweli ndio ile Lulu ya thamani kuu.
Mungu ametuchagua sisi kutufunulia huo UFUNUO WA KWELI. Hivyo basi, sisi ndilo KANISA Lake LA KWELI, jeshi Lake lisiloweza kushindwa ambalo Shetani hana nguvu mbele yalo, na kwa dhahiri atashindwa. Tukiwa na Ufunuo Wake wa Kweli maishani mwetu, malango ya kuzimu hayawezi kutushinda, bali tutayashinda. HAKUNA KITU kinachoweza kusimama mbele zetu.
Ufunuo wa Kweli na mkamilifu wa siku hii ni kutambua umuhimu wa Sauti ya Mungu ya siku yetu. Ikiwa kwenda kanisani, kuwa mshirika wa kanisa, kutoa dhabihu, kuomba, na kumwabudu Mungu ndio yote ambayo Mungu anayohitaji, basi Mungu angekuwa asiye haki kumhukumu Kaini kwa yeye kufanya kile alichosema afanye.
Hiki ndicho Sauti iliyo kwenye kanda inachomaanisha kwetu sisi:
Ufunuo wa kitu hicho chote umewekwa hapa nyuma pamoja na baraka kwa yeye alisomaye na kulisikia, pamoja na laana kwa hao watakaoongeza ama kutoa. Ni kitabu rasmi kikamilifu, loo, ile yakini. Hakuna kitu kinachoweza kuongezewa Kwake. Ndipo mtu anapojaribu kutoa chochote kutoka Kwake, au kuongeza chochote Kwake, Mungu alisema ataondoa sehemu iyo hiyo kutoka kwenye Kitabu cha Uzima. Mnaona? Angeondoa sehemu yake kutoka kwenye Kitabu, ikiwa angeongeza Kwake.
Kuliko hapo awali, Mungu ameiandaa NJIA KAMILIFU ya kutoongeza ama kutopunguza kutoka kwenye Neno Lake. Yeye ametupa fursa ya kuisikia Sauti Yake anaponena na kutufunulia sisi Neno Lake. Hakuwezi kabisa kuwa na kitu chochote kikuu zaidi ya hilo.
Huu ndio UFUNUO WA KWELI wa siku hii.
Nimesisimkwa mno na niko chini ya matarajio makubwa kwa yale yote Bwana aliyotuandalia tunaposikiliza, kusoma, na kujifunza Nyakati Saba za Kanisa. Mungu alikiandika, akamtuma malaika Wake kwa Yohana kumwonyesha Hicho, kisha akatusubiri sisi tuweze kuwa hapa duniani wakati huu hasa ili Yeye aweze kumtuma malaika yuyo huyo kwetu sisi kukifunua!
Hakujawahi kuwa na wakati mtukufu zaidi katika historia ya ulimwengu kuliko leo hii. Hakujawahi kuwa na heshima kubwa zaidi aliyowahi kupewa mwanadamu kuliko kupata fursa ya kuisikia Sauti ya Mungu wao wenyewe. Hakujawahi kuwa na wakati ambapo Bibi-arusi Wake angeweza kuungana pamoja kwa Sauti Yake wote kwa wakati mmoja.
Iweni tayari, Mungu anaenda kutupa Ufunuo zaidi kumhusu Yeye Mwenyewe na sisi ni nani: Jeshi Lake lisiloweza kushindwa, Bibi mteule, aliyechaguliwa, Kipenzi Chake ambaye amemngojea tangu mwanzo wa wakati.
Hakuna kinachoweza kutuondolea hilo. Limetia nanga katika mioyo na roho zetu zaidi ya hapo awali. Sasa limekuwa jambo halisi kwamba linatupa Imani Ya kunyakuliwa.
Tutaianza safari yetu kuu Jumapili hii saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapousikiliza Ujumbe wa kwanza: 60-1204M Ufunuo wa Yesu Kristo.
Nataka kukuhimiza ukitwae kitabu chako cha nyakati Saba za Kanisa, ukisome katika ukimya chumbani mwako na ujifunze, sura kwa sura, kila wiki. Tutaungana pamoja kuisikiliza Sauti Yake, kisha tujifunze Neno Lake.
Lakini kuuona udanganyifu wa adui, kamwe hatujawahi kuwa na wakati kama huu tunaoishi sasa, ni wakati wa ujanja sana, udanganyifu kuliko wakati wo wote. Na ninapoona hilo, huniletea hili kwamba Mkristo anapaswa kuwa mwangalifu zaidi siku ya leo, kuliko alivyowahi kuwa katika wakati mwingine wo wote.
Ndugu Branham alimwambia Bibi-arusi maneno haya karibu miaka 61 iliyopita hadi sasa. Udanganyifu wa yule adui miaka 61 iliyopita ulikuwaje ikilinganishwa na sasa? Ili kuliweka hilo katika mtazamo tofauti, teknolojia ya dunia miaka 61 iliyopita ilikuwaje ikilinganishwa na vile ilivyo leo?
Mwaka wa 1961 ulikuwa ndio mwanzo wa Mbio za Anga, kompyuta zilikuwa zenye fremu kuu kubwa zenye ukubwa wa chumba zikifanya kazi kupitia mirija ya utupu na kadi za panchi ambazo zilihitaji wanasayansi maalum kuzipanga. Simu zilifungwa ukutani na zilitegemea waya wa shaba wenye waya na analogia, fremu kuu za Transistor, taipureta za mitambo, mifumo ya kuhifadhi karatasi na vikokotoo vya mwanzoni vya kimitambo.
Lakini leo tuna Intaneti, mifumo ya Akili Mnemba ambayo ina uwezo wa kuunda sanaa, uandishi, na kusaidia kazi kwa wakati halisi. Roketi za kibinafsi zinazokwenda Mars. Simu janja zakuenea mfukoni, saa janja, na vifaa vya kibinafsi vinavyoendeshwa na mitandao ya kimataifa isiyotumia waya ambayo huunganisha mabilioni ya watu mara moja kupitia sauti, maandishi, na video. Wasaidizi wa kiroboti.
Ujanja na udanganyifu wa yule adui ni zaidi ya hapo awali. Uzao mwovu wa Shetani uko katika kukomaa kukamilifu nao umeunda Edeni ya Shetani. Bali wakati huo huo, Mungu anaye Bibi-arusi ambaye yuko katika kukomaa kukamilifu, Uzao Wake wa Kifalme ambao umejiweka wenyewe tayari kwa kukaa katika uwepo wa Mwanawe, Neno Lake, Sauti Yake.
Mungu Yeye alijua ilitakiwa aandae njia ya kumdumisha Bibi-arusi Wake katika wakati huu wa udanganyifu na mwovu. Njia kamilifu ambayo hawangehitaji kushangaa, kukisia, au kuchukua neno la mtu yeyote kwa Neno la kweli lisiloghoshiwa. Yeye alijua wangehitaji kuisikia wao wenyewe Sauti ya Mungu, kwa sababu Yeye alituonya kwamba itafanana sana kiasi kwamba ingewadanganya walio Wateule kama yamkini.
Watu wangeweza kupakwa mafuta, wajazwe na Roho Mtakatifu, na wawe wa uongo. Ilibidi aandae njia. Kwa hivyo, akatengeneza NJIA KAMILIFU kwa ajili ya Bibi-arusi Wake, ambayo ingeonekana haiwezekani wakati Yeye alipoanza kuirekodi Sauti Yake mwaka wa 1947; kwamba kwa ncha ya kidole chao, ulimwengu ungeweza kusikia wao wenyewe kila Neno Yeye alilosema, hata katika lugha yao wenyewe. Hakungekuwa na MASWALI, KUSHANGAA. WAO WANGEWEZA KUISIKIA BWANA ASEMA HIVI WAO WENYEWE.
Yeye hata ametengeneza njia ambayo angeweza kumuunganisha Bibi-arusi Wake kote ulimwenguni ili kuisikia Sauti Yake, wote kwa wakati mmoja, ili waweze kuwa katika nia moja, kwa umoja, wakimsikia Yeye akinena.
Ilimbidi Yeye amchukue mjumbe Wake, bali Yeye aliiacha Sauti Yake, Neno Lake kamilifu kwa ajili ya Bibi-arusi Wake Mkamilifu. Kwa kuisikia na kudumu na Sauti Yake, angejua wao hawawezi kudanganywa.
Na ndilo hili hapa: Hivyo ndivyo ambavyo Mungu huliimarisha Kanisa Lake. Kila Neno kwa jinsi yake. “Mtu hataishi kwa mkate tu, bali kwa kila Neno linalotoka kinywani mwa Mungu.”
Tunajua huku ni kuamini kila Neno ambalo Roho Mtakatifu asemalo, bali kwangu mimi, ninayo heshima kubwa zaidi ambayo mwanadamu amewahi kupewa. Ninaweza kusikia, kwa masikio yangu, SAUTI halisi IKINENA kila Neno linalotoka kinywani mwa Mungu.
Hakuna njia nyingine kwangu mimi. Mungu ametoa njia nyingi za kuwaokoa watoto Wake, bali kwangu mimi, Mungu ameiandaa NJIA KAMILIFU YA KUMKAMILISHA BIBI-ARUSI WAKE.
Leo, Shetani anafasiri vibaya sehemu ya Andiko linalohusu siku hii. Yeye atakuacha ujue yote yale Yesu aliyotenda yalikuwa sawa kabisa. Atakuacha ujue yote yale Ndugu Branham aliyotenda yalikuwa sawa kabisa, na alikuwa nabii wa Mungu. Bali linapokuja suala la kuicheza Sauti halisi Ya Mungu iliyothibitishwa katika kanisa lao, wao watasema hilo halitumiki leo hii, ni wahudumu.
Hilo ndilo tu lote linalompasa kufanya, unaona, ni kuwafanya watu kuamini hilo namna hiyo, na ni hilo tu. Kwani huwezi kuondoa neno moja Kwalo, au kuongeza neno moja Kwalo, lakini hilo ndilo afanyalo.
Kiongozi wako wa kiroho anawekea mkazo nini kanisani mwako? Ni Sauti gani iliyo muhimu zaidi ambayo Bibi-arusi hana budi kuisikia leo? Unaweza tu kuwa na 1 Kikuu.
A: Sauti ya wahudumu? B: Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda?
“Kila mbegu lazima izae kwa jinsi yake! Hivyo ndivyo ambavyo Mungu aliimarisha Edeni Yake.
Mimi sipingi wahudumu kuhudumu. Najua, na ninaamini, Mungu amewaita. Lakini kwangu mimi, huduma ya kweli itawaambia kusanyiko lake kwamba Sauti iliyo kwenye kanda ndiyo Sauti iliyo muhimu zaidi ambayo HAWANA BUDI kuisikia, kwa hivyo yawabidi wazicheze kanda kanisani mwao, kwani ndio SAUTI KUU.
Mimi na nyumba yangu, na Maskani ya Branham, tutadumu na NJIA KAMILIFU YA Mungu ILIYOANDALIWA. Tuta BONYEZA PLAY na kuisikia Sauti ya Mungu.
Ningependa kuualika ulimwengu mzima uje kuungana nasi kuisikia Sauti hiyo Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(ni saa 1 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapoungana kwa mara nyingine tena kwenye njia Yake iliyoandaliwa aliyoichagua kwa ajili ya siku hii.
Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukusanyike pamoja Jumapili saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,( ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki ) kusikiliza 65-0822E Chujio La Mtu Mwenye Busara.