Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu tukutane pamoja Jumapili saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) kusikiliza 65-0801E Matukio Yakidhihirishwa na Unabii.
Mpendwa Kundi dogo, Bibi-arusi Neno Bikira wa Kristo:
Jinsi gani mioyo yetu ilivyofurahi tulipomsikia malaika Wake mwenye nguvu akitangaza kwamba sisi ndio Uzao wa Mungu uliochaguliwa tangu asili ambao hauwezi kutenda kitu kingine chochote ila kuifuata Sauti Yake. Ni zaidi ya maisha kwetu sisi. Unaweza kuyatwaa maisha yetu, lakini huwezi kuichukua Sauti Yake. Sisi ni Mmoja na Neno Lake. Sisi ni Mmoja na Sauti Yake. Sisi ni Mmoja na Yeye.
Inaonekana la kushangaza kwetu sisi kwamba tunaeleweka vibaya na kudhihakiwa kwa sababu tunasema tunaamini katika kuzicheza kanda; kwamba ni Sauti ya Mungu ikinena na Bibi-arusi Wake. Shetani amewafanya watu kudanganywa sana hivi kwamba wanadhani kwa sisi kutangaza kwamba sisi ni kanisa la kanda, ati ni jambo fulani lililo kinyume na Neno, jambo fulani la makosa, na ati tunapotoshwa, huku wakati wote Ndio njia kamilifu ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake.
Inawezaje kuwa njia nyingineyo? Ukilifasiri vibaya Neno moja lililonenwa, umepotea. Wao wanaweza kuwa na nia na lengo sahihi, bali wawe wamekosea. Mtu anaweza kuwa ametiwa mafuta na Roho Mtakatifu na bado awe amekosea.
Kama Mungu hangekuwa ameiandaa njia ambayo Bibi-arusi Wake wangeweza kusikia wao wenyewe kila Neno, basi kungekuwa na haja ya njia nyingine. Bali Yeye ameiandaa njia kwa kila mwanadamu duniani kupata fursa ya kulisikia Neno likizungumza nao moja kwa moja bila kuhitaji fasiri, maelezo, au ufafanuzi. Yote ni Bwana Asema Hivi…MWISHO WA MANENO!
Sote tunakubaliana kwamba ni lazima tudumu na Neno ili tuweze kuwa Bibi-arusi Wake.
Ninaamini ya kwamba kila kitu tunachohitaji kimeandikwa papa Hapa, kinahitaji tu kufasiriwa na Roho Mtakatifu. Siamini ya kwamba mtu ye yote duniani ana haki ya kuweka fasiri yake kwenye Neno. Mungu hahitaji mtu ye yote kulifasiri Neno Lake. Yeye ndiye anayejifasiria. Alisema angefanya jambo hilo, Naye hulifanya.
Waziwazi, Bwana amenena na kumfunulia Bibi-arusi Wake kwamba hakuna njia nyingine ya kuwa Bibi-arusi Wake mteule ila kudumu na Neno Lake. Mungu Mwenyewe hulifasiri Neno Lake Mwenyewe, na hakuna mtu aliye na haki ya kuongeza fasiri yake Kwake.
Neno pia linasema kwamba NABII Wake ndiye mfasiri wa Neno Lake. Yeye ni Sauti ya Mungu kwa watu. Kile yeye asemacho ndilo Neno la siku yetu.
Kwa kuisikiliza Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda, sisi ni unabii unaotimizwa.
Hakuna kilicho na nguvu zaidi, kitakatifu zaidi, hakuna kinachotimiza zaidi, hakuna kilicho kikamilifu zaidi kuliko kuisikiliza Sauti ya Mungu iliyothibitishwa ikizungumza nawe.
Wakati wengine wanaweza kusema jambo hilo halina lolote, tai wanakusanyika na kushangilia kwa furaha kubwa mno, wakiwa na uhakika kwamba wanalishika Neno la Mungu. Alituambia kama una kinasasauti, likusanye kundi la watu pamoja, na ukaicheze, na msikilize kwa makini. Kwa neema na rehema Zake, hicho ndicho hasa tunachofanya.
Mungu ametuita kutoka katika wakati huu mwovu kwa ajili ya Jina Lake. Tunapitia mitihani na majaribu mengi ambayo hayajawahi kutokea. Shetani yuko katika mashambulizi kwani anajua wakati wake umekwisha. Unaweza kujiuliza, nawezaje kupitia mambo haya yote, na huku mimi ni Bibi-arusi Wake?
Unadhihirishwa, unajaribiwa, na kumthibitishia Shetani, SISI NI BIBI-ARUSI WAKE YEYE. Sisi ni Neno lililo katika mwili. Tunaweza kunena Neno nalo litatimia. Ni BWANA ASEMA HIVI.
Tuna Sauti ya Mungu ikizungumza moja kwa moja na Shetani na kumwambia:
Shetani, umeshindwa. Wewe u muongo. Na, kama mtumishi wa Mungu, na kama watumishi, tunakuamuru ya kwamba katika Jina la Yesu Kristo, ya kwamba utii Neno la Mungu na utoke ndani ya watu, kwa maana imeandikwa, “Katika Jina Langu watatoa pepo.”
Lolote…LOLOTE tunalohitaji, tunahitaji tu kuomba, kuamini na kukaa papo hapo. Linaweza kudhihirika mara moja; yaweza kuwa wiki, mwezi, mwaka. Haijalishi kile tunachokiona au kuhisi, LIILITUKIA PAPO HAPO.
Kila ibada tunayokusanyika pamoja inazidi kuwa Kuu zaidi na zaidi kwa Tai wa Mungu. Tumekusanyika katika nia Moja na kwa Umoja, tukiketi pamoja katika ulimwengu wa roho, tukiisikiliza Sauti ikizungumza nasi na kutukamilisha kwa Neno Lake.
Tungependa muungane nasi Jumapili hii saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapoisikia Sauti ya Mungu ikizungumza nasi kwa mara nyingine tena na kutuletea fasiri ya Neno Lake Mwenyewe.
Ndugu. Joseph Branham
Ujumbe: Mungu Wa Wakati Huu Mwovu 65-0801M
Maandiko ya kusoma kabla ya Kuusikiliza Ujumbe: Mathayo Mt. sura ya 24 / 27:15-23 Luka Mtakatifu 17:30 Yohana Mt. 1:1 / 14:12 Matendo 10:47-48 1 Wakorintho 4:1-5 / sura ya 14 2 Wakorintho 4:1-6 Wagalatia 1:1-4 Waefeso 2:1-2 / 4:30 2 Wathesalonike 2:2-4 / 2:11 Waebrania sura ya 7 1 Yohana sura ya 1 / 3:10 / 4:4-5 Ufunuo 3:14 / 13:4 / sura ya 6-8 na 11-12 / 18:1-5 Mithali 3:5 Isaya 14:12-14
Huu mvuto mkubwa ni wa nini unaotendeka kote ulimwenguni? Watu kutoka kote ulimwenguni wanakusanyika saa 6:00 MCHANA masaa ya Jeffersonville, wakiketi majumbani mwao na makanisani mwao kwa matarajio makubwa, wakingojea kuisikia Sauti ya Mungu izungumze nao.
Ni jambo la ajabu mno na lisilo na mantiki kwa ulimwengu kuzisikiliza Kanda tu. Wao wanasema sisi tunaweza kuzisikia kanda wakati wowote. Hakuna lolote kusikiliza kwa wakati mmoja. Lazima uisikilize huduma iliyo mubashara, mhubiri, Si ati kanda tu. Wao wamekwama katika mapokeo yao.
Hakuna kitu kama hiki kimewahi kutokea katika historia ya ulimwengu. Ni nini kimewavutia watu hawa kuungana wote kwa wakati mmoja kuisikia Sauti hiyo ikimwita Bibi-arusi Wake atoke? Ni Mungu akitimiza Luka 17:30. Ni Mungu akitimiza Ufunuo 10:7. Ni Mungu akifunua Waebrania 13:8, Melkizedeki katika mwili wa mwanadamu, kama vile alivyofanya kwa Ibrahimu.
Wanasubiri na kujiuliza, Hivi Yeye atasema nini? Nini kitatokea wakati Yeye atakapoanza kunena? Wao wanataka kuwa pale kwenye mawasiliano ya simu ili kupata chochote kile Yeye asemacho. Wanakitaka. Wanataka kukisikia wote kwa wakati mmoja pamoja na Bibi-arusi kote ulimwenguni. Kwa maana wanaamini yeye ndiye sauti ambayo Mungu aliichagua kuwa Sauti Yake kumwita atoke na kumwongoza Bibi-arusi Wake.
Ingawa wako umbali wa masaa mengi, bali wao wote wako pamoja kama JAMII MOJA, wameunganishwa, wakiisikiliza Sauti hiyo ikizungumza nao kutokea Kanisa lao la Nyumbani. Wamekaa katika uwepo wa Mwana, wakiivishwa na kungojea Kuja kwa Masihi.
Mioyo yao inaenda mbio. Roho Mtakatifu anawafunulia wao kile kinachotendeka. Mungu amesubiri kufikia leo hii kulidhihirisha Neno Lake na kumkusanya Bibi-arusi Wake. Linatendeka, nao ni sehemu ya hilo. Uhalisia wa kile kinachotendeka unaingia mioyoni mwao. Wamesoma kulihusu hilo katika Maandiko kwa karne nyingi, bali sasa hivi ni uhalisia. Ufunuo wa Neno unadhihirishwa kupitia wao. Unabii wa nabii unatimizwa.
Wakati wanapoketi chini ya upako huo mkuu wa Sauti Yake yenye nguvu, Yeye anawatangazia wajiandae; Kwa maana usiku wa leo atawaombea kila mmoja wao. Yeye anatuambia wakati anapoanza kuomba, wawekeeni mikono walio wagonjwa, kwa maana uwepo wa Mungu aliye kila mahali uko kila mahali pamoja nao, haijalishi wako wapi: Texas, kule juu California, juu kule Arizona, Amerika Kusini, hata kwenye vibanda vilivyopo msituni ule upande mwingine wa dunia. Mahali popote pale wanaposikiliza hewani kwa simu, wawekeane mikono tunapoanza kuomba na Mungu atamponya kila mmoja wao, ikiwa wanaamini, kwa maana Ni Bwana Asema Hivi.
Wao sasa wanaelewa kwamba kupitia kila kizazi na kila nabii ambaye alikuwako au ambaye angekuwako, kutakuweko na kiasi fulani cha watu ambao wamechaguliwa tangu asili kuusikia Ujumbe huo, nao wataufuata. Hao hawatajali umati wa watu. Wao hawajali ukosoaji wa asiyeamini anayesema ati ni makosa au sio njia ya Mungu iliyoandaliwa. Wao hawabishani nao. Wana Wajibu mmoja WANAOPASWA KUFANYA, huo ni kuamini na kupata kila sehemu Yake wawezayo, waiingize ndani kama Mariamu aliyeketi Miguuni pa Yesu. Wao hawaonei haya, wanajivunia kusema wao ni kijana wa kanda au binti wa kanda anayebonyeza play.
Sauti hiyo tayari imekwisha kuwaonya wao kwamba kutakuwako na watiwa mafuta katika wakati wa mwisho ambao watakuwa na upako mkubwa, Roho Mtakatifu. Watamnukuu nabii na Ujumbe wa saa hii; wanadai kuwa waaminio, bali ni watiwa mafuta wa uongo.
Wao wangefanana sana na upako halisi kiasi kwamba ingewadanganya kama yamkini walio wateule, bali wao wanajua hawawezi kudanganywa, kwa maana wao NI NENO. Wao ndio Bibi-arusi wa kweli aliyedumu na Sauti ya Mungu. Sauti hiyo inawatangazia kwamba katika siku hii haitakuwa limau, au balungi. Hiyo ingekuwa rahisi kutofautisha. Lakini itakuwa tangelo, nusu limau, nusu chungwa, uzao uliochanganyikana. Itaonekana kabisa kama chungwa, lakini haitakuwa, kwa maana tawi hilo jipya litakuwa asilimia 100% kama lile la asili. Wao WATADUMU na Neno hilo la asili la Sauti. Hawatabahatisha. Wao watadumu na yule, ambaye Mungu Mwenyewe alimtangaza kuwa ndiye SAUTI YAKE, NENO LAKE, aliyethibitishwa kwa Nguzo ya Moto.
Ni nini kinachotendeka?
Uzao wa Mungu uliochaguliwa tangu asili hauwezi kutenda chochote bali kuifuata na kuisikiliza Sauti hiyo, kwa maana ni zaidi ya maisha kwao. Unaweza kuyatwaa maisha yao, bali huwezi kuichukua Sauti hiyo.
Je, ni mvuto gani?
Mungu, kama kawaida, akitimiza Neno Lake.
Njoo uungane nasi na uwe sehemu ya unabii wa nabii unaotimizwa Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapoyasikia Maandiko yakidhihirishwa.
Kichwa pekee cha Ujumbe wa wiki hii kinafunua kule kumhisi Roho Mtakatifu kwa Bibiarusi. Kuwazia kutakuwa na wanaume watiwa mafuta wa kweli watakaoinuka katika siku hii, wakiwa na upako wa kweli wa Roho Mtakatifu yule yule aliyekuwa juu ya nabii wetu, bali wawe wa uongo.
Neno linatuambia watafanya ishara na maajabu, wanapokea mvua ile ile, baraka zile zile kama nabii wa kweli. Watu wangegeukia mbali kutoka kwenye Neno la kweli lililothibitishwa la siku hii na kuzifuata nia zao wenyewe, wakijipatia waalimu makundi makundi, wenye masikio ya utafiti. Hilo litafanana sana na Neno la kweli hata karibu litawadanganya Walioteuliwa.
Hivi upako huo utafanana sana kiasi gani? Je, itakuwa rahisi kupambanua kilicho kweli na cha uongo? Nabii alituambia kwamba Mfalme Daudi, mtu anayeupendeza moyo wa Mungu, akiwa na upako juu yake, alipata ufunuo wa kweli; bali ilikuwa makosani.
ATI NINI!! Hebu hilo lizame ndani kwa muda. Mfalme aliyechaguliwa na Mungu alikuwa na upako wa kweli na ufunuo wa kweli, bali alikuwa makosani! Kondoo wa Mungu watatakiwa kuwa macho sana ili kujua kile wanachokisikia ni upako wa kweli au wa uongo; kwani kikomo chao cha milele kinategemea maamuzi haya.
Tunajua Mungu ameweka wahudumu wengi wa kweli waliotiwa mafuta ili kusaidia kuongoza na kumweka Bibi-arusi Wake katika Neno. Neno Lake linasema hivyo, nasi tunamshukuru sana Bwana kwa ajili ya kila mmoja wao. Wameitwa kuwa wachungaji kuyaangalia makundi yao. Wapo kwa ajili ya kuwaweka wao katika Neno. Kwa kufanya hivyo, hawapaswi kushindwa kuicheza Sauti PEKEE ya Mungu iliyothibitishwa kwa makundi yao.
Kama tulivyotoka kusikia jinsi ambavyo kila mtu anavyoweza kukosea, hata pamoja na upako wa kweli na ufunuo wa kweli. Bali Bibi-arusi wanaweza kuwa na uhakika, kwa sababu Mungu ameiandaa njia kamilifu ambayo daima wanaweza kuusikia UPAKO WA KWELI, UFUNUO WA KWELI, BWANA ASEMA HIVI YA KWELI; BONYEZA PLAY TU.
“Palipo na Mzoga,” palipo na Mana, palipo na Neno, “ndipo watakapokusanyika tai.”
Palipo na Mzoga, hapo ndipo sisi Tai tutakapokusanyika. Mahali palipo na Nyama mbichi, Neno la wakati huu, Ujumbe wa saa hii. Na hakuna mahali pazuri pa kuila Mana hiyo kuliko kuisikia Sauti ya Mungu akinena Yeye Mwenyewe.
Hilo ni Neno Lake. “Mtu hataishi kwa mkate tu, bali kwa kila Neno.” Mnaona? Waliochaguliwa tangu awali wanajua jambo hili. “Neno geni, ama sauti ngeni, hawataifuata.”
Sababu ya sisi kutofanya hivyo, na hatuwezi kudanganywa, ni kwa sababu sisi ni Neno wenye Ufunuo huu. Hatuwezi kuwa kitu kingine. Hatuwezi kusikia kitu kingine. Hatujui kitu kingine.
“MIMI NIKO!” Si “Nilikuwa, wala Nitakuwa.” “MIMI NIKO,” wakati uliopo, Neno sasa hivi. Si Neno lililokuwa, wala Neno litakalokuja; Neno lililopo sasa. Mnaona? Mnalifahamu? “MIMI NIKO!” “MIMI NIKO” ni Neno. “Hapo mwanzo alikuwapo Neno, Naye Neno alikuwako pamoja na Mungu.” Hiyo ni kweli? “MIMI NIKO.” “Mungu alinituma kama nabii Wake, kuthibitisha jambo hili kuwa ni kweli. Mimi ndiye jibu la Neno hili, kwa hiyo, wakati Yeye anaposhuka huku na kufanya jambo hili.”
Na alipofanya jambo hilo, Farao akasema, “Vema, tuna vijana wengi sana katika kundi letu wanaoweza kufanya jambo hilo, pia,” waigaji.
Yesu alisema, “Naam, hiyo itajirudia tena katika siku za mwisho,” mnaona, wakidai jambo lile lile.
Bwana asifiwe. Nena kuhusu hakikisho kwa Bibi-arusi. Kama unao Ufunuo huu, basi utajua wewe ndiye Bibi-arusi Wake kipenzi mteule, aliyechaguliwa tangu zamani.
Kwa kuisikiliza Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda, tunamsikiliza Mwana wa Adamu, ambaye ni Kristo. Yeye ndiye tunayejilisha. Hatujilishi mwanadamu; mwanadamu, maneno yake yatashindwa. Bali tunakula Mwili-Neno lisiloshindwa la Mwana wa Adamu.
Ikiwa unataka kuwa na uhakika wa asilimia 100 kwamba unasikiliza Bwana Asema Hivi, njoo uungane na sehemu ya Bibi-arusi Jumapili hii saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapoisikia Sauti ya Mungu ikitufunulia yote kuhusu watiwa mafuta katika wakati wa mwisho.
Ndugu Joseph Branham
Ujumbe: Watiwa Mafuta Katika Wakati Wa Mwisho 65-0725M
Maandiko: Mathayo Mt. 5:44-45 / 7:21 / 24:15-28 Luka Mt. 17:30 / 18:1-8 Yohana Mt. 14:12 Waefeso 1:5 II Timotheo 3:1-8 Waebrania 6:1-8 / 11:4 Ufunuo 10:1-7 / 16:13-14 Malaki 4:5 I Wafalme 22:1-28 Yeremia: Sura ya 27 na 28
Sasa, nafikiri hakuna heshima ya kutosha ambayo tungeweza kumpa mama.
Mama yetu ndiye wa kwanza wa kuwa na sisi, na amepewa jukumu kubwa la kile tutakachokuwa na njia tunayopaswa kuifuata. Amepewa jukumu kutoka kwa Mungu la kutuweka kwenye njia sahihi. Ndiyo sababu akina mama wana mguso mdogo maalum, waliopewa kutoka kwa Mungu.
Ni baraka ya kipekee iliyoje tuliyowekewa Jumapili hii, tunapowapa heshima wa Mama wote, wakati tunapomsikia malaika wa saba wa Mungu akielezea upendo na heshima ambayo mama zetu waliyonayo mioyoni mwetu.
Tunajua kila siku ni Siku kuu ya Mama, lakini Jumapili hii tutatoa heshima maalum kwa wa Mama wote tunapomsikia nabii wetu akiwapa heshima kama alivyonena miaka 67 iliyopita siku iyo hiyo hasa, tarehe 10, Mei, 1959.
Ndugu. Joseph Branham
Ujumbe: Siku Kuu Ya Mama 59-0510M
Saa: 6:00 MCHANA. Masaa ya Jeffersonville(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki)
Sauti tunayopenda sote kuisikia itazungumza Jumapili hii, na kutuletea Ujumbe Maalum wa Barua ya Mahaba, kwa ajili ya Bibi-arusi wa Yesu Kristo tu.
Sauti hiyo imetoka kuuambia ulimwengu na kuwaonya, “Msijaribu kunitendea Mimi kazi bila ya kuwa mapenzi Yangu. Ninayo njia kamilifu niliyoiandaa kwa ajili yenu, Bibi-arusi Wangu. Kumbukeni Maneno Yangu, semeni tu yale niliyosema kwenye kanda Zangu, kwa maana mnaingia hukumuni. Rehema imekataliwa. Lakini furahini, na mshukuru, kwa kuwa nimewaandalia na kuwapa Chakula Kilichofichwa, Chakula cha Kiroho, ili mpate kuishi kwa fadhili na rehema za Ufunuo wa Yesu Kristo.
Sasa hivi kuna ukame nchini kwa ajili ya kuisikiliza Sauti Yangu. Wao hawawaelewi ninyi kwa sababu mnasema ninyi ni watu wa Kanda, na mnataka tu kuisikia Sauti Yangu iliyo kwenye Kanda; lakini nimewaita ninyi na kuwafunulia njia Yangu kamilifu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii.
Ninyi hamjashirikiana na wasioamini katika wakati wa ukame. Nimewapeni ninyi Sauti Yangu ipate kuwalisha. Kwa kuicheza Sauti Yangu, pipa lenu halitapunguka, wala chupa yenu haitaisha kamwe, hata siku ile nitakapokuja na kuwachukueni kama Bibi-arusi Wangu.
Hiyo ndio sababu hasa niliirekodi Sauti Yangu, Ili mwezekuwa na mahali pa kamilifu pa kwenda, ambapo hamna kosa, hamna haja ya fasiri, ni Sauti Safi ya Mungu tu. Mahali ambapo mnaweza kwenda ili mweze kusikia kile haswa nilichosema: Bwana Asema Hivi.
Nitazungumza nanyi waziwazi Jumapili. Nawatakeni msisahau kamwe kile nitakachowaambia. Kanda hizi ndicho Chakula chenu cha Kiroho cha wakati huu. Ni kinono mno kwa baadhi ya hao; hawawezi tu kukipokea. Hakijafunuliwa kwao, bali Mimi nimewachagua NINYI, na kuwapa Ufunuo wa njia Yangu kamilifu iliyoandaliwa.
Kwenu ninyi, Ni Chakula Kilichofichwa, hata mnaishi kwa fadhili na rehema za Neno Lililo Hai.
Wakati nilipokuwa nikiishi katika mwili ndani ya Mwanangu, wao hawakuweza kabisa kukubali Mimi nilikuwa nani: Mungu na mwanadamu. Kisha niliahidi kwamba ningerudi tena katika siku za mwisho na kuishi katika mwili wa mwanadamu kwa mara nyingine tena kama nilivyofanya mbele ya Ibrahimu, na ningeshuka na kujifanya Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu kama nilivyofanya wakati huo.
Hiki ndicho wao walichokosa, wakati huo na sasa hivi, lakini Mimi sitaki kamwe ninyi msahau. Chakula hiki kilichohifadhiwa ninachowalisha ninyi, hicho na mjumbe Wangu, ni kitu kimoja. Huwezi kuwatenganisha. Ujumbe na mjumbe ni kitu kimoja. Niliwaambieni katika Neno Langu kile Mimi ningefanya katika siku hii. Ndiyo maana ni mapenzi Yangu kuiweka Sauti Yangu katika makanisa yenu, majumbani mwenu, kila mahali muendapo; kwa maana ndio Sauti iliyo muhimu zaidi mnayopaswa ninyi kuisikia. Ndio Sauti PEKEE iliyothibitishwa inenayo Bwana Asema Hivi.
Rehema imekataliwa. Sasa ninyi mnaishi kwa Neno Langu. Nimewapa Ufunuo wa Mimi Ni nani na NINYI NI nani. Hakupaswi kuwa na shaka hata chembe mioyoni na akilini mwenu. Ninyi ndio Bibi-arusi Wangu Niliyemchagua, Mteule, Aliyekusudiwa Kimbele. Ninyi ndio Neno Langu Lililonenwa lile lililokuwa ndani Yangu hapo mwanzo.
Ninyi mna ruhusa ya kukikaribia Chakula, Chakula cha Kiroho, ambacho ulimwengu haujui chochote kukihusu.
Mna ruhusa ya kuufikia uponyaji wa miili yetu wakati madaktari wameshindwa; Ni kimoja cha Vyakula Mimi nilichoahidi na nilichowapa ninyi katika siku za mwisho.
Niliahidi kuzifunua siri za mioyo yenu na kuyafanya mambo haya. Mimi niko ndani yenu. Ninyi ni sehemu Yangu, Nami ni sehemu yenu. Ishara hizi zitafuatana na hao waaminio.
Jumapili hii nitakuwa nikimuunganisha Bibi-arusi Wangu kutoka kote ulimwenguni kwa Sauti Yangu. Nitawaambia mwekeane mikono juu ya mmoja kwa mwingine. Msijiombee, mwombee yule mliyemwekea mikono, kwa sababu wao wanawaombea. Tutaomba pamoja, na hakutakuwa na mtu mnyonge popote kote ulimwenguni ikiwa mtaamini.
Kama unaamini, na huna shaka moyoni mwako, nitatangaza:
Shetani, umeshindwa! Yesu Kristo alikushinda! Yeye alifufuka katika wafu na anasimama miongoni mwetu usiku wa leo, akithibitisha Ujumbe huu wa siku za mwisho. Toka katika watu hawa! Waache, katika Jina la Yesu Kristo! “Katika Jina Langu watatoa pepo,” nawe umetolewa nje. Katika Jina la Yesu Kristo, liache kusanyiko hili!
Kutakuwako na uponyaji ukifanyika kote ulimwenguni kuliko hapo awali.
Kwa nini tungojee tena zaidi, ndugu yangu mpendwa, dada, Huyu hapa, Roho Mtakatifu, Mungu, papa hapa, jambo lenyewe hasa tulilozungumzia.”
Ninauwalika ulimwengu mzima uje uungane nasi Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) na tuusikie Ujumbe na mjumbe Wake atuletee Chakula cha Kiroho kwa Wakati Wake, Chakula Kilichofichwa kwa ajili ya Bibi-arusi.
Ndugu Joseph Branham
Ujumbe: Chakula cha Kiroho kwa Wakati Wake 65-0718E
Saa imeenda sana. Wakati umekaribia. Maamuzi hayana budi kufanywa. Mungu anawaonya watoto Wake. Bwana Mungu wetu ametutangazia na kututhibitishia Kweli Yake ni ipi kwa Neno Lake, na kwa Roho Wake. Si kwa nguvu, si kwa uweza, bali kwa Roho Wangu, na Neno Lako ni Kweli.
Yeye amemthibitishia Bibi-arusi kikamilifu leo kwamba Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo, na hata milele. Yeye ametuonyesha na kutufunulia Ujumbe na mjumbe wa saa hii ni kitu kimoja. Yeye ametufunulia siri Zake zote zilizokuwa zimefichwa katika Neno. Ametuthibitishia hilo kwa Roho Wake Mtakatifu. Hakuna swali akilini mwetu, mioyoni mwetu au rohoni mwetu. Sauti Yake iliyo kwenye kanda ni BWANA ASEMA HIVI KWA BIBI-ARUSI WAKE.
Mungu daima ameruhusu njia nyingi kumjia Yeye. Anayafanya mapenzi Yake ya kuruhusia katika mapenzi Yake Makamilifu. Yeye pia daima ameandaa MAPENZI MAKAMILIFU NA NJIA KAMILIFU KWA AJILI YA WATOTO WAKE. Wengi hujaribu kuja kwa njia tofauti kwa kumtendea Mungu kazi bila ya kuwa mapenzi Yake Makamilifu. Huenda yakaonekana na kusikika kama mapenzi Yake makamilifu, lakini sio kulingana na Neno Lake.
Hata mtu mkuu, aliyepakwa mafuta hivi karibuni, akitoka Uweponi mwa Mungu, akiwa na ufunuo wa kumfanyia Mungu jambo fulani, naye alitaka kulifanya hilo kwa ajili ya Mungu; lakini ufunuo aliokuwa nao ulikuwa si sahihi.
Kila mmoja wetu lazima aipate njia Yake kamilifu iliyoandaliwa. Tutajuaje kwamba tuko katika mapenzi Yake makamilifu Je, ni ikiwa mtu ambaye amepakwa mafuta kweli, yakitoka mapya kutoka uweponi mwa Mungu, akiwa na ufunuo, hayuko katika mapenzi makamilifu ya Mungu?
Kuna NJIA MOJA PEKE YAKE YA KUJUA HAKIKA, naye Mungu ameiandaa njia hiyo kwa Bibi-arusi Wake.
Sauti ya Mungu Mwenyewe imeliambia kanisa hili, na ninyi watu wote mlio kwenye kanda, na watu waliounganishwa kwa redio katika sehemu zingine za dunia, wakati huo na SASA. Alituambia tumsikilize kile yeye alichokuwa akisema kwa makini sana, na ILI TUSIKOSE.
Nasema vivyo hivyo katika Jina la Yesu Kristo: Usiongeze kitu. Usiondoe, kuliwekea mawazo yako. Wewe sema tu yaliyosemwa katika kanda hizo. Tenda sawasawa kabisa na vile Bwana Mungu amekuamuru kutenda; Usiongezee Kwake.
Yeye hakusema, na haimaanishi, kwamba wahubiri hawawezi kulihubiri Neno, waalimu hawawezi kulifundisha Neno, au wachungaji au manabii wafanye kile ambacho tumeitiwa kufanya; yawapasa, Yanipasa. Tumeitiwa na kuteuliwa kufanya hivyo. Yatupasa tuwaelekeze na kuunukuu Ujumbe huu na mjumbe kwa watu, kwa maana Ndilo Neno la siku yetu.
Lakini Yeye anatuambia waziwazi kwamba sote tunaweza kupakwa mafuta, kwa upako wa kweli, tujazwe na Roho Wake Mtakatifu, kuwa na ufunuo mpya, na tuwe nje ya mapenzi Yake. Katika siku yetu, Yeye ameiandaa NJIA KAMILIFU ya kujua hakika unaisikia Sauti ya Mungu, kutoka kwa Mungu Mwenyewe. Ndiyo njia PEKEE kamilifu.
Wahudumu hawapaswi tu kuunukuu na kuuhubiri Ujumbe huu, inatubidi tuwachezee watu Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. Hakuna UPAKO MKUU kuliko kuisikia Sauti ya Mungu. Hakuna njia nyingine ya kujua bila shaka kwamba kile tunachokisikia ndicho HASA kile Mungu alichosema.
Katika siku hii, tofauti na siku nyingine yoyote ile katika historia ya ulimwengu, Mungu ameiandaa njia ambayo inalifanya kuwa vigumu kulikosa, ikiwa wewe ni Bibi-arusi Wake Aliyechaguliwa Kimbele. Limethibitishwa na kufunuliwa na Nguzo ya Moto Mwenyewe kuwa Sauti ya Mungu Yeye Mwenyewe akizungumza moja kwa moja na Kanisa Lake.
Kote kote katika tawala elfu za miaka, watoto wa Mungu wamekuwa wakitamani na kuonea njaa kuisikia Sauti ya Mungu wao wenyewe. Jinsi gani wao walivyotamani wangekuwa pale siku ile Yesu alipowahubiria maelfu kule mlimani. Kusikia jinsi Yeye alivyolinena Neno Lake kwa upendo na huruma. Kusikia jinsi Yeye alivyoliwekea msisitizo kila Neno. Jinsi ambavyo lingezungumza na kuitia moyo mioyo yao.
Tuko hai sasa na katika Uwepo wa Mungu tukiisikia Sauti ya Mungu.
Siku moja hivi karibuni hatutarudi katika maisha kama haya tena. Tutarudi kama kiumbe kisichokufa. Dhambi itaondolewa. Shetani atafungwa kwa miaka elfu moja nasi tutaishi katika nchi hii ambayo Bwana Mungu wetu ametupa.
Tumekamilika asilimia 100%. Hatujawahi kuwa wenye furaha zaidi hivi au kutokuwa na shaka zaidi hivi katika maisha yetu. Sisi ni Mmoja Naye na Neno Lake. Sisi tu Neno Lake. TUKO KATIKA MAPENZI YAKE MAKAMILIFU KWA SISI KUDUMU NA SAUTI YAKE, NENO LAKE. Atarudi siku yoyote sasa kutuchukua twende pamoja Naye.
Asante Bwana Yesu!
Bwana Mungu wako amekutangazia yaliyo Kweli. Bwana Mungu Wako amethibitisha Kweli ni nini kwa Neno Lake na kwa Roho Wake. “Si kwa uweza, wala si kwa nguvu, bali ni kwa Roho Yangu.” Na Roho, “Mungu anawatafuta wale ambao wanamwabudu katika Roho na Kweli.” “Neno Lake ni Kweli.” Na amethibitisha vizuri kabisa kwamba Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo, na hata milele. Amewaonyesha ninyi Mbegu za jioni. Ameifunua kwenu katika Neno. Amethibitisha hilo kwenu kwa Roho Wake.
Kwa moyo wangu wote ninawaalika kila mmoja wenu aje aungane na sehemu ya Bibi-arusi Wake tunapoungana kutoka kote ulimwenguni saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) kuisikia Sauti Yake ikinena kupitia malaika-mjumbe Wake wa saba na kutuletea Ujumbe: Kujaribu Kumtendea Mungu Kazi Bila Ya Kuwa Mapenzi Ya Mungu 65-0718M.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko ya kusoma kabla ya kuusikiliza Ujumbe: Kumbukumbu la Torati 4:1-4 / 4:25-26 1 Nyakati 13 1 Nyakati 15:15 Zaburi 22 Marko Mt. 7:7 Yoeli 2:28 Amosi 3:7 Malaki 3 Mathayo Mt.11:1-15 1 Wakorintho 13:1
Wakati tunapousikiliza Ujumbe huu, Kuchagua Bibi-arusi, wengine wanafikiri kwamba nabii anazungumza tu na kutufundisha kuhusu tabia na kimo ambacho mwanamume anapaswa kuangalia wakati anapomchagua mwanamke anayemtaka awe mke wake. Hiyo ni kweli, anafanya hivyo, lakini hapo kuna barua ya mahaba halisi iliyofichwa katika Maneno Yake. Kile Yeye anachomfunulia Bibi-arusi Wake ni cha kina zaidi. Mungu anazungumza na Yeye(Bibi-arusi) moja kwa moja, akimwambia kile Yeye alichokuwa akikitafuta ndani Yake, na kwa nini Yeye alimchagua tangu mwanzo. Yeye alimtaka Yeye(Bibi-arusi) ajue kwamba Yeye amemchagua awe BIBI-ARUSI WAKE KIPENZI WA KUPENDEZA, ambaye Yeye alitaka ashiriki naye Umilele Wake.
Hapo mwanzo, Mungu alikuwa akimtafuta Bibi-arusi ambaye angekuwa na Tabia ile ile ya Kwake. Roho Wake yule yule angedhihirishwa ndani Yake(Bibi-arusi). Yeye alimtaka Bibi-arusi ambaye alikuwa amejitolea kabisa-kabisa Kwake, na Neno Lake lililoahidiwa, mpaka Nia ile ile iliyokuwamo ndani Yake iwe ndani yake Yeye(Bibi-arusi). Lazima afinyangwe kama Yeye alivyo.
Yeye alimtaka awe mwili Wake ule ule, mifupa ile ile, Roho yule yule, kila kitu kile kile, kama tu Yeye hasa. Wawili hao wangekuwa MMOJA.
Yeye hangekuwa na namna fulani ya macho jeuri. Yeye hangebembana huko na sauti nyingine yoyote. Yeye angekuwa mwaminifu na mkweli Kwake, haijalishi mtu yeyote angesema nini. Yeye angemkubali kwa Neno Lake. Chochote Yeye alichosema, YEYE ANGEAMINI KILA NENO, haijalishi ingechukua muda gani hilo kutimia, yeye angeliamini. Yeye angedumu na Neno Lake.
Yeye(Bibi-arusi) angempenda Yeye, na Yeye peke yake. Haikumlazimu Yeye kumpa utajiri mwingi, yeye alikuwa na Lulu ya thamani kuu, ule Ufunuo wa kweli wa Yeye( Bwana-Arusi). Yeye(Bibi-arusi) angejua, wao walikuwa MMOJA na kitu kimoja. Roho Wake angekaa ndani Yake. Chochote Yeye (Bibi-arusi) alichokihitaji, Yeye angempa; kitu tu Yeye(Bibi-arusi) alichopaswa kufanya ni kuomba na kuamini, na Yeye angekifanya.
Yeye(Bibi-arusi) alijua Yeye(Bwana-Arusi) angeondoka kwa muda mrefu kwenda kumjengea Yeye nyumba ambayo ingekuwa na kila kitu jinsi tu vile Yeye apendavyo kiwe na atakavyo. Yeye alikuwa akiijenga jinsi ambavyo Yeye (Bibi-arusi) angeipenda. Yeye (Bibi-arusi) alijua siku moja Yeye (Bwana-Arusi) angerudi kumchukua Yeye, kama Yeye alivyoahidi, kisha wangekuwa na Karamu Kuu ya Harusi kwa miaka elfu. Ndipo, wao wangeenda pamoja kwenye Makao hayo mazuri Yeye aliyomjengea waishi milele.
Hakuna kitu kingine ambacho kingekuwa muhimu kwake Yeye. Yeye asingetaka kitu kingine chochote. Yeye angeridhika mno na kutosheka na Ufunuo kujua Yeye (Bwana-Arusi) ni nani, na Yeye (Bibi-arusi) ni nani. Yeye (Bibi-arusi) angejua kwamba Yeye(Bwana-Arusi) angelitimiza Neno Lake. YEYE ANGETIMIZWA, AKIJUA YEYE NDIYE YULE AMBAYE YEYE ALIYEMCHAGUA KUWA BIBI-ARUSI WAKE.
Ndugu na dada zangu, Mungu mwenye nguvu wa Mbingu na nchi alitazama kote katika Umilele na AKAWACHAGUA NYINYI… NYINYI KUWA BIBI-ARUSI WAKE KIPENZI ALIYOWACHAGUA.
Ninawaalika mje muungane nami na sehemu ya Bibi-arusi Wake Jumapili hii, wakati Yeye anapozungumza kupitia malaika Wake Mwenye nguvu na kutuambia sisi ndio Bibi-arusi Wake Aliyowachagua.
Ndugu Joseph Branham
Ujumbe: 65-0429E / Kuchagua Bibi-arusi Muda: saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki)
Jinsi gani mioyo yetu ilivyoinuka kama Tai wikendi hii ya Pasaka. Siku baada ya siku, upako Wake ulizidi kuwa mkubwa. Ushirika, Kuzikwa, Ukamilifu, kisha kile kilele kikuu Alichotujengea: Ni Kuchomoza kwa Jua…UTUKUFU, AMEFUFUKA na Yuko hai ndani ya kila mmoja wetu. Yeye alikuwa akilifunua Neno Lake kwa kila mmoja wetu jinsi tusivyowahi kusikia hapo awali. Ule upako uliifurika mioyo yetu, uwepo Wake uliitanda hewa; ilionekana kana kwamba Unyakuo ulikuwa umekaribia.
Yeye alituambia yale yaliyotukia miaka 2000 iliyopita, na kisha yale yaliyokuwa yakitukia sasa mwaka wa 2026. Yesu alikuwa Chembe ya kwanza ya Ngano ya Mungu iliyofufuka kutoka kwa wafu. Yeye alikuwa amefufuliwa na Nguvu za Mungu za kuhuisha. Mungu alikuwa ameyahuisha maisha Yake, akamfufua kutoka kwa wafu, Naye alikuwa malimbuko ya kwanza ya wale waliolala. Yeye alikuwa wa kwanza kukomaa, Mganda wa Mungu uliotikiswa kama ukumbusho wa kutoa shukrani kwa Mungu, akiamini kwamba sisi wengine tungekuja. Ilikuwa ishara.
KISHA YEYE AKATUFUNULIA KILE KILICHOTUKIA LEO. Kama vile Yeye alivyotikiswa siku ya Pentekoste wakati sauti kutoka Mbinguni iliposikika kama upepo wa nguvu ukienda kasi ukitikiswa juu ya watu. Ulikuwa ukitikiswa tena mbele ya watu kama alivyoahidi katika Luka 17:30 na Malaki 4, wakati Mwana wa Adamu atakapofunuliwa na kutikiswa tena juu ya watu.
Sasa, Mwana wa Adamu ni Nani? “Hapo mwanzo alikuwako Neno, naye Neno alikuwa kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Naye Neno akafanyika mwili, akakaa kwetu.” Na iwapo mafundisho yote tuliyo nayo, na thibitisho la Neno la Mungu; kwa Neno la Mungu, kwa ishara, kwa maajabu, tunaona leo, ya kwamba katika Kitabu cha—cha Luka hapa, ya kwamba kama tulivyonukuu hicho hivi punde, ama Lu—Luka mlango wa 17 na kifungu cha 30; na Malaki 4, na Maandiko mbalimbali ambayo tunayajua, ya kwamba hilo Neno tena linatikiswa juu ya watu, ya kwamba mapokeo yaliyokufa ya mwanadamu yamekufa, na Mwana wa Mungu yu hai tena na ubatizo wa Roho Mtakatifu moja kwa moja miongoni mwetu, naye anatupa Uzima.
Roho Mtakatifu aliendelea kutikisa na kutikisa juu yetu, akifunua na kufunua Neno Lake… Nguvu za utendaji, mitambo, Nguvu za kuhuisha…
Ndipo, ilipoonekana kana kwamba Haiwezi kuwa kuu zaidi, Yeye alituambia:
Naye akaniruhusu niangalie ng’ambo ya pazia, nami nikawaona ninyi nyote kule ng’ambo… Wote uliowahi kupenda, na wote waliowahi kukupenda, umepewa wewe.” Mnaona? Niliwaona hao kila mahali pale namna hiyo. Ilikuwa nini? Nguvu za kuhuisha.
YEYE ALITUONA SISI KULE!! Ng’ambo ya pazia la wakati….tulikuwa KULE pamoja naye; wapendwa wetu wote waliotutangulia…akina baba, mama, watoto. Tulikuwa kule pamoja nao na wale wote ambao hatujawahi kukutana nao: Musa, Eliya, Petro, Paulo….tulikuwa sote kule pamoja.
Kisha, kama vile Roho Mtakatifu alivyo mzuri, Yeye hakutaka kutusahau sisi tulio wagonjwa, wenye huzuni na waliopigwa, kwa hivyo Yeye alijitikisa Mwenyewe juu yetu tena ili kila mtu aponywe chochote kile tulichokuwa na haja nacho.
Watu hawa, ambao ni raia wenza wa Ufalme, mmiliki wa Nguvu za kuhuisha, lihuishe kwao, Bwana, sasa hivi. Pia naomba Roho aende kutoka tai hadi tai, kutoka kwenye Neno hadi Neno, mpaka utimilifu wa Yesu Kristo udhihirishwe katika kila mmoja wa hiyo miili, kwa ajili ya haja za kimwili, za kiroho, ama haja zozote walizo nazo, tunapowekeana mikono sisi kwa sisi. Katika Jina la Yesu Kristo.
Neno Hilo. Sauti Hiyo. KILA KITU tunachokihitaji kiko kwenye kanda, Ewe, Bibi-arusi. Mungu habadilishi nia Yake kuhusu Neno Lake. Hakuna nukta moja au yodi moja inayoweza kubadilishwa, kwa hivyo Yeye alitengeneza njia ambayo Bibi-arusi Wake angeweza kusikia kwa masikio yao wenyewe kile hasa Yeye alichotaka kuwaambia.
Mungu amenena na Bibi-arusi Wake na kufunua KILA KITU. Kimerekodiwa. Bibi-arusi lazima aje kwa Bwana Arusi; hiyo ndio Njia Yake kamilifu iliyoandaliwa ambayo imetengenezwa kwa ajili ya siku hii. Ni BWANA ASEMA HIVI.
Je! Mungu hubadilisha Nia Yake kuhusu Neno Lake? HAPANA. Yeye anayo MAPENZI MAKAMILIFU NA MAPENZI YAKURUHUSIA. Bibi-arusi yambidi awe katika MAPENZI YAKE MAKAMILIFU. Hakuna Mapenzi yaliyo makamilifu zaidi, au mahali pakamilifu, kuliko kuisikia Sauti ya Mungu moja kwa moja kutoka kwa Mungu Mwenyewe.
Mwaliko wangu kwa kila mmoja wenu ni muungane nasi Jumapili saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville(ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki), kuisikia Sauti ya Mungu ikituletea Neno Safi. Hakuna haja ya kubahatisha, wewe keti tu na useme AMINA KWA KILA NENO….hakuna mahali pengine hilo linaweza kufanywa, ila kwa KUBONYEZA PLAY.
Ndugu Joseph Branham.
Ujumbe: 65-0418E — Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake?