UJUMBE: 65-0718E Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake
- 26-0503 Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake
- 24-0728 Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake
- 23-0108 Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake
- 21-0912 Chakula cha Kiroho kwa Wakati Wake
- NUKUU YA LEO KWA KISWAHILI
- 20-0329 Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake
- 18-1014 Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake – Preliminari
- 16-1221 Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake
Bibi-arusi Kipenzi,
Sauti tunayopenda sote kuisikia itazungumza Jumapili hii, na kutuletea Ujumbe Maalum wa Barua ya Mahaba, kwa ajili ya Bibi-arusi wa Yesu Kristo tu.
Sauti hiyo imetoka kuuambia ulimwengu na kuwaonya, “Msijaribu kunitendea Mimi kazi bila ya kuwa mapenzi Yangu. Ninayo njia kamilifu niliyoiandaa kwa ajili yenu, Bibi-arusi Wangu. Kumbukeni Maneno Yangu, semeni tu yale niliyosema kwenye kanda Zangu, kwa maana mnaingia hukumuni. Rehema imekataliwa. Lakini furahini, na mshukuru, kwa kuwa nimewaandalia na kuwapa Chakula Kilichofichwa, Chakula cha Kiroho, ili mpate kuishi kwa fadhili na rehema za Ufunuo wa Yesu Kristo.
Sasa hivi kuna ukame nchini kwa ajili ya kuisikiliza Sauti Yangu. Wao hawawaelewi ninyi kwa sababu mnasema ninyi ni watu wa Kanda, na mnataka tu kuisikia Sauti Yangu iliyo kwenye Kanda; lakini nimewaita ninyi na kuwafunulia njia Yangu kamilifu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii.
Ninyi hamjashirikiana na wasioamini katika wakati wa ukame. Nimewapeni ninyi Sauti Yangu ipate kuwalisha. Kwa kuicheza Sauti Yangu, pipa lenu halitapunguka, wala chupa yenu haitaisha kamwe, hata siku ile nitakapokuja na kuwachukueni kama Bibi-arusi Wangu.
Hiyo ndio sababu hasa niliirekodi Sauti Yangu, Ili mwezekuwa na mahali pa kamilifu pa kwenda, ambapo hamna kosa, hamna haja ya fasiri, ni Sauti Safi ya Mungu tu. Mahali ambapo mnaweza kwenda ili mweze kusikia kile haswa nilichosema: Bwana Asema Hivi.
Nitazungumza nanyi waziwazi Jumapili. Nawatakeni msisahau kamwe kile nitakachowaambia. Kanda hizi ndicho Chakula chenu cha Kiroho cha wakati huu. Ni kinono mno kwa baadhi ya hao; hawawezi tu kukipokea. Hakijafunuliwa kwao, bali Mimi nimewachagua NINYI, na kuwapa Ufunuo wa njia Yangu kamilifu iliyoandaliwa.
Kwenu ninyi, Ni Chakula Kilichofichwa, hata mnaishi kwa fadhili na rehema za Neno Lililo Hai.
Wakati nilipokuwa nikiishi katika mwili ndani ya Mwanangu, wao hawakuweza kabisa kukubali Mimi nilikuwa nani: Mungu na mwanadamu. Kisha niliahidi kwamba ningerudi tena katika siku za mwisho na kuishi katika mwili wa mwanadamu kwa mara nyingine tena kama nilivyofanya mbele ya Ibrahimu, na ningeshuka na kujifanya Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu kama nilivyofanya wakati huo.
Hiki ndicho wao walichokosa, wakati huo na sasa hivi, lakini Mimi sitaki kamwe ninyi msahau. Chakula hiki kilichohifadhiwa ninachowalisha ninyi, hicho na mjumbe Wangu, ni kitu kimoja. Huwezi kuwatenganisha. Ujumbe na mjumbe ni kitu kimoja. Niliwaambieni katika Neno Langu kile Mimi ningefanya katika siku hii. Ndiyo maana ni mapenzi Yangu kuiweka Sauti Yangu katika makanisa yenu, majumbani mwenu, kila mahali muendapo; kwa maana ndio Sauti iliyo muhimu zaidi mnayopaswa ninyi kuisikia. Ndio Sauti PEKEE iliyothibitishwa inenayo Bwana Asema Hivi.
Rehema imekataliwa. Sasa ninyi mnaishi kwa Neno Langu. Nimewapa Ufunuo wa Mimi Ni nani na NINYI NI nani. Hakupaswi kuwa na shaka hata chembe mioyoni na akilini mwenu. Ninyi ndio Bibi-arusi Wangu Niliyemchagua, Mteule, Aliyekusudiwa Kimbele. Ninyi ndio Neno Langu Lililonenwa lile lililokuwa ndani Yangu hapo mwanzo.
Ninyi mna ruhusa ya kukikaribia Chakula, Chakula cha Kiroho, ambacho ulimwengu haujui chochote kukihusu.
Mna ruhusa ya kuufikia uponyaji wa miili yetu wakati madaktari wameshindwa; Ni kimoja cha Vyakula Mimi nilichoahidi na nilichowapa ninyi katika siku za mwisho.
Niliahidi kuzifunua siri za mioyo yenu na kuyafanya mambo haya. Mimi niko ndani yenu. Ninyi ni sehemu Yangu, Nami ni sehemu yenu. Ishara hizi zitafuatana na hao waaminio.
Jumapili hii nitakuwa nikimuunganisha Bibi-arusi Wangu kutoka kote ulimwenguni kwa Sauti Yangu. Nitawaambia mwekeane mikono juu ya mmoja kwa mwingine. Msijiombee, mwombee yule mliyemwekea mikono, kwa sababu wao wanawaombea. Tutaomba pamoja, na hakutakuwa na mtu mnyonge popote kote ulimwenguni ikiwa mtaamini.
Kama unaamini, na huna shaka moyoni mwako, nitatangaza:
Shetani, umeshindwa! Yesu Kristo alikushinda! Yeye alifufuka katika wafu na anasimama miongoni mwetu usiku wa leo, akithibitisha Ujumbe huu wa siku za mwisho. Toka katika watu hawa! Waache, katika Jina la Yesu Kristo! “Katika Jina Langu watatoa pepo,” nawe umetolewa nje. Katika Jina la Yesu Kristo, liache kusanyiko hili!
Kutakuwako na uponyaji ukifanyika kote ulimwenguni kuliko hapo awali.
Kwa nini tungojee tena zaidi, ndugu yangu mpendwa, dada, Huyu hapa, Roho Mtakatifu, Mungu, papa hapa, jambo lenyewe hasa tulilozungumzia.”
Ninauwalika ulimwengu mzima uje uungane nasi Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) na tuusikie Ujumbe na mjumbe Wake atuletee Chakula cha Kiroho kwa Wakati Wake, Chakula Kilichofichwa kwa ajili ya Bibi-arusi.
Ndugu Joseph Branham
Ujumbe: Chakula cha Kiroho kwa Wakati Wake 65-0718E
Mjumbe: Kasisi William Marrion Branham
Maandiko:1 Wafalme 17:1-7 / Amosi 3:7 / Yoeli 2:28
Malaki 4:4 / Luka 17:30 / Yohana Mt. 14:12