24-0419
24-0418
24-0417
24-0416
24-0415
24-0414
24-0413
24-0412
24-0411
24-0410
24-0409
24-0408
24-0407
24-0406
24-0405
24-0404
24-0403
24-0402
24-0401
24-0330
61-0205M – Tarajio
Sasa, huwezi kuudanganyia; huna budi kuwa nao. Hu—huwezi kuudanganyia. Hautadanganya. Shetani si…yeye—yeye anajua kama unadanganya ama la. Lakini wakati hudanganyi, yeye anajua pia. Wakati kitu fulani kinapotia nanga moyoni mwako ambapo unajua ya kwamba ndivyo ilivyo, basi jambo fulani litatukia.
Ibrahimu aliamini hilo. Yeye alimwamini Mungu. Aliliamini Neno la Mungu na chini ya matarajio; alingojea miaka ishirini na mitano huku tarajio hilo likizidi kuwa kubwa zaidi na zaidi. Ndipo hatimaye huyo mtoto akazaliwa, kwa sababu alikuwa akilitarajia.
Akajitenga. Na kama utaangalia kile alichongojea, Mungu alimwambia ajitenge na jamaa zake wote, wala Mungu kamwe hakumbariki tena mpaka alipomtii kikamilifu. Maadamu—maadamu baba yake aliendelea kuandamana naye, mbona, huyo jamaa mzee alisababisha matatizo. Kisha akaandamana na Lutu, halafu Lutu akasababisha matatizo. Na—na yote hata alipojitenga mwenyewe, na kuondokea, kutokuamini kote kukaondolewa kwake, ndipo Mungu alishuka na kuzungumza naye, ndipo jambo fulani likatukia.
Basi tunapoondolea mbali kutoka kwetu maskini roho zote za kutokuamini, na kuliamini tu Neno la Mungu, na, “Sijali yale Fulani-wa-fulani aliyosema, ama Fulani-wa-fulani aliyosema, Mungu alitoa ahadi, ninasimama papo hapo.” Ndipo Mungu ataanza kujibu.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha. 2 Wakorintho 6:17
24-0329
24-0328
24-0327
24-0326
24-0325
24-0324
24-0323
24-0322
24-0321
24-0320
24-0319
24-0318
24-0317
24-0316
24-0315
24-0314
24-0313
24-0312
24-0311
24-0310
24-0309
24-0308
24-0307
24-0306
65-0219 – Leo Maandiko Haya Yametimia
Basi, ingewezekanaje wale watu wasiweze kuona Yeye alikuwa nani? walilikosaje? Ingewezekanaje wakati ilikuwa imejulikana dhahiri na kuonyeshwa? Wangekosaje kuona wakati Yeye…ni Neno jinsi gani! Wazia hilo! “Leo Maandiko haya yametimia machoni penu!”
Nani alisema hayo?—Mungu Mwenyewe, aliye mfafanusi wa Neno Lake Mwenyewe. “Leo Maandiko haya yametimia.” Yule Masihi Mwenyewe, akisimama mbele ya makutano na akisoma neno toka kwa Biblia linalomhusu Yeye Mwenyewe, na ndipo akasema, “Leo Maandiko haya yametimia,” nao bado walishindwa kulifahamu.
MKATE WA KILA SIKU
Akaanza kuwaambia, Leo maandiko haya yametimia masikioni mwenu. Luka 4:21
24-0305
24-0303
57-0825M – Waebrania, Mlango Wa Pili #1
Mungu daima hushuhudu. Maisha yako yatashuhudu. Sijui ushuhuda wako ukoje, bali maisha yako yananena kwa sauti kubwa sana, sauti yako haiwezi kusikika. Lakini, mwe—mwenendo wako, maisha yako ya kila siku yatashuhudia kwamba wewe u nani. Mungu hushuhudia. Naam. Roho Mtakatifu ni muhuri, na muhuri huchukua pande zote mbili za karatasi. Wanakuona umesimama hapa na wanakuona ukiondoka. Si kanisani tu bali katika kazi ya kila siku. Umetiwa muhuri pande zote mbili, ndani na nje. Kwa furaha uliyo nayo, na kwa maisha unayoishi, umetiwa muhuri, ndani na nje, kwamba unajua umeokoka na ulimwengu unajua umeokoka, kwa maisha unayoishi, kwa maana Mungu anashuhudia. Jina Lake Takatifu litukuzwe!
MKATE WA KILA SIKU
Na Bwana vivyo hivyo ameamuru kwamba wale waihubirio Injili wapate riziki kwa hiyo Injili. 1 Wakorintho 9:14
24-0302
53-0831 – Mungu Alinena na Musa
Sasa, hili…Makanisa leo hii, mengi yao, yanatafuta wachanganyishaji. Mtu fulani anayeweza kuchanganyisha na labda kufanya kidogo hili na lile, na tafrija ndogo, na kucheza gofu, na labda karamu chache na kadhalika.
Sasa, ulimwengu unatafuta wachanganyishaji wazuri, lakini Mungu anatafuta watenganyishaji, wale watakaojitenga wenyewe. “Tokeni kati yao, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zao.” Jitenge…
Huko Misri, wakati mwana-kondoo alipotolewa, Mungu aliweka utofauti. Aliwatenga—Waisraeli kutoka kwa—kutoka kwa Mataifa, na kufanya tofauti kati yao. Na watu wa Mungu ni watu waliotengwa, taifa takatifu, watu wateule, wa kipekee, wenye kutenda kiajabu.
Kwa hivyo ulimwengu hautawaelewa kamwe. Kwa hiyo msiwazie juu ya ulimwengu; wazieni juu ya Mungu. Hilo ndilo jambo kuu.
MKATE WA KILA SIKU
Basi Lutu akajichagulia Bonde lote la Yordani; Lutu akasafiri kwenda upande wa mashariki; wakatengana wao kwa wao. Mwanzo 13:11