NUKUU YA LEO KWA KISWAHILI

24-0419

24-0418

24-0417

24-0416

24-0415

24-0414

24-0413

24-0412

24-0411

24-0410

24-0409

24-0408

24-0407

24-0406

24-0405

24-0404

24-0403

24-0402

24-0401

24-0330

61-0205M –  Tarajio

Sasa, huwezi kuudanganyia; huna budi kuwa nao. Hu—huwezi kuudanganyia. Hautadanganya. Shetani si…yeye—yeye anajua kama unadanganya ama la. Lakini wakati hudanganyi, yeye anajua pia. Wakati kitu fulani kinapotia nanga moyoni mwako ambapo unajua ya kwamba ndivyo ilivyo, basi jambo fulani litatukia.

Ibrahimu aliamini hilo. Yeye alimwamini Mungu. Aliliamini Neno la Mungu na chini ya matarajio; alingojea miaka ishirini na mitano huku tarajio hilo likizidi kuwa kubwa zaidi na zaidi. Ndipo hatimaye huyo mtoto akazaliwa, kwa sababu alikuwa akilitarajia.

Akajitenga. Na kama utaangalia kile alichongojea, Mungu alimwambia ajitenge na jamaa zake wote, wala Mungu kamwe hakumbariki tena mpaka alipomtii kikamilifu. Maadamu—maadamu baba yake aliendelea kuandamana naye, mbona, huyo jamaa mzee alisababisha matatizo. Kisha akaandamana na Lutu, halafu Lutu akasababisha matatizo. Na—na yote hata alipojitenga mwenyewe, na kuondokea, kutokuamini kote kukaondolewa kwake, ndipo Mungu alishuka na kuzungumza naye, ndipo jambo fulani likatukia.

Basi tunapoondolea mbali kutoka kwetu maskini roho zote za kutokuamini, na kuliamini tu Neno la Mungu, na, “Sijali yale Fulani-wa-fulani aliyosema, ama Fulani-wa-fulani aliyosema, Mungu alitoa ahadi, ninasimama papo hapo.” Ndipo Mungu ataanza kujibu.

MKATE WA KILA SIKU

Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.       2 Wakorintho 6:17

24-0329

24-0328

24-0327

24-0326

24-0325

24-0324

24-0323

24-0322

24-0321

24-0320

24-0319

24-0318

24-0317

24-0316

24-0315

24-0314

24-0313

24-0312

24-0311

24-0310

24-0309

24-0308

24-0307

24-0306

65-0219 –  Leo Maandiko Haya Yametimia

Basi, ingewezekanaje wale watu wasiweze kuona Yeye alikuwa nani? walilikosaje? Ingewezekanaje wakati ilikuwa imejulikana dhahiri na kuonyeshwa? Wangekosaje kuona wakati Yeye…ni Neno jinsi gani! Wazia hilo! “Leo Maandiko haya yametimia machoni penu!”

Nani alisema hayo?—Mungu Mwenyewe, aliye mfafanusi wa Neno Lake Mwenyewe. “Leo Maandiko haya yametimia.” Yule Masihi Mwenyewe, akisimama mbele ya makutano na akisoma neno toka kwa Biblia linalomhusu Yeye Mwenyewe, na ndipo akasema, “Leo Maandiko haya yametimia,” nao bado walishindwa kulifahamu.

MKATE WA KILA SIKU

Akaanza kuwaambia, Leo maandiko haya yametimia masikioni mwenu.  Luka 4:21

24-0305

24-0303

57-0825M –  Waebrania, Mlango Wa Pili #1

Mungu daima hushuhudu. Maisha yako yatashuhudu. Sijui ushuhuda wako ukoje, bali maisha yako yananena kwa sauti kubwa sana, sauti yako haiwezi kusikika. Lakini, mwe—mwenendo wako, maisha yako ya kila siku yatashuhudia kwamba wewe u nani. Mungu hushuhudia. Naam. Roho Mtakatifu ni muhuri, na muhuri huchukua pande zote mbili za karatasi. Wanakuona umesimama hapa na wanakuona ukiondoka. Si kanisani tu bali katika kazi ya kila siku. Umetiwa muhuri pande zote mbili, ndani na nje. Kwa furaha uliyo nayo, na kwa maisha unayoishi, umetiwa muhuri, ndani na nje, kwamba unajua umeokoka na ulimwengu unajua umeokoka, kwa maisha unayoishi, kwa maana Mungu anashuhudia. Jina Lake Takatifu litukuzwe!

MKATE WA KILA SIKU

Na Bwana vivyo hivyo ameamuru kwamba wale waihubirio Injili wapate riziki kwa hiyo Injili.       1 Wakorintho 9:14

24-0302

53-0831 – Mungu Alinena na Musa

Sasa, hili…Makanisa leo hii, mengi yao, yanatafuta wachanganyishaji. Mtu fulani anayeweza kuchanganyisha na labda kufanya kidogo hili na lile, na tafrija ndogo, na kucheza gofu, na labda karamu chache na kadhalika.

Sasa, ulimwengu unatafuta wachanganyishaji wazuri, lakini Mungu anatafuta watenganyishaji, wale watakaojitenga wenyewe. “Tokeni kati yao, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zao.” Jitenge…

Huko Misri, wakati mwana-kondoo alipotolewa, Mungu aliweka utofauti. Aliwatenga—Waisraeli kutoka kwa—kutoka kwa Mataifa, na kufanya tofauti kati yao. Na watu wa Mungu ni watu waliotengwa, taifa takatifu, watu wateule, wa kipekee, wenye kutenda kiajabu.

Kwa hivyo ulimwengu hautawaelewa kamwe. Kwa hiyo msiwazie juu ya ulimwengu; wazieni juu ya Mungu. Hilo ndilo jambo kuu.

MKATE WA KILA SIKU

Basi Lutu akajichagulia Bonde lote la Yordani; Lutu akasafiri kwenda upande wa mashariki; wakatengana wao kwa wao. Mwanzo 13:11

24-0301

An Independent Church of the WORD,