NUKUU YA LEO KWA KISWAHILI

23-1209

23-1208

23-1207

23-1206

23-1205

23-1204

53-0506 – Yesu Kristo Yeye Yule Jana, Leo, Na hata Milele

Katika miaka ishirini ya utafiti wa Biblia, na kuzungumza na Malaika wa Bwana, na mambo mengi, naona hapa kuna mambo mawili: hayo ni upendo na imani. Kama unampenda Mungu, upendo tu halisi usioghoshiwa, huna budi kuwa na imani katika Yeye, itaambatana na imani kila wakati. Na wakati upendo na imani zinapooana, omba utakalo, nawe utapata.

Hiyo ni…Unapojua kwamba Baba yako wa Mbinguni hawezi kukuambia uwongo wowote, Yeye ni Mungu. Hawezi kusema uongo. Na kisha unapomwamini Yeye kwa moyo wako wote, na unaamini kwamba unachoomba, hauombi kwa nia yo yote ya ubinafsi, bali nia yako sahihi nyuma yake ni kuomba hilo kwa ajili ya utukufu wa Mungu, na kuamini bila shaka hata kidogo, ya kwamba Baba Yako hawezi kukuambia uwongo, jambo fulani litatukia, utakapoyaondoa magugu yote njiani, na utazame moja kwa moja pale Kalvari, na uamini jambo hilo kwa moyo wako wote.

MKATE WA KILA SIKU

Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. 1 Wakorintho 13:2

23-1203

62-0607 – Kuvaa Silaha Zote za Mungu

Sasa, walimpata mtu anayezunguka angani. Wote wanalipigia kelele hilo mwajua, “Tunaye mtu angani.” Mbona, hilo si lolote, sisi Wakristo tumekuwa na mmoja angani kwa miaka elfu mbili, mwajua. Hiyo ni kweli. Hiyo ni kweli. Wanapiga kelele kuhusu hilo, hilo si jambo jipya, hilo ni la kale kwetu sisi, tulijua hilo wakati wote. Kwa hiyo, unaona? Unaona, hivyo ndivyo tulivyo mbele, ni kwamba tu hawatambui.

Ndiyo, kujenga barabara kuu kubwa na vitu vya ajabu kama hivyo na kujaribu kuifanya dunia kuwa mahali pazuri na kadhalika, hawatambui ya kwamba wapole watairithi, haya basi. Kwa hiyo tu—ni nii tu…Unaona, Mungu alikwisha tupangia yote. Ndilo, jambo pekee tunalopaswa kufanya, ni kushikilia tu Kwake na kuendelea tu mbele. Unaona? Ndilo, kuamini tu, hilo ndilo tu alilotuomba tufanye, Yeye atatuvusha moja kwa moja.

MKATE WA KILA SIKU

Hawa wanataja magari na hawa farasi, Bali sisi tutalitaja jina la BWANA, Mungu wetu. Zaburi 20:7

23-1202

55-0604 – Yairo, Mwamini wa Siri

Na maji yaliposonga mbele, baada ya muda mfupi Yesu akanena na kusema, “Msiogope. Ni Mimi.”

Petro akasema, kama ni Wewe, Bwana, nijaribu kidogo tu.

Na ombeni nanyi mtapata. Kwa hiyo alimpa jaribio, na alipojaribu kufanya jambo hilo yeye mwenyewe, alishindwa, na kila mtu mwingine atashindwa. Aliondoa macho yake kwa Yesu na kuanza kutazama jinsi mawimbi yalivyokuwa makubwa. Alipoona mawimbi yako dhidi yake, alianza kuzama. Na kila mtu atakaye tazama matatizo yake baada ya kuombewa hakika atazama.

Usiangalie shida yako. Wewe weka macho yako kwa Mpaji wa ahadi, Bwana Yesu Kristo. Weka macho yako kwenye Neno Lake. Yeye Ndiye Aliyeahidi. Yeye huiangalia ili aitimize. Yeye huiweka katika vitanga vya mkono Wake, na katika vilindi vya moyo wake imelazwa. Maneno Yake hayana budi kuwa Kweli.

Yaondoe mawazo yako kwenye ugonjwa wako, yaondoe kwenye shida zako. Kaza macho yako kwa Yesu.

MKATE WA KILA SIKU

Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake. 2 Petro 3:9

23-1201

23-1130

23-1129

23-1128

23-1127

23-1126

56-0218E – Mwenye Dhambi Kuliko Wote Katika mji

Natamani ningesimama pale aliposimama. Nilitamani ningesimama mahali pale alipokuwa amesimama. Unajua ningefanya nini? Loo, nisingevutiwa na mambo lukuki ya kanisa; Ningepomoka kifudifudi na kusema, “Mpendwa Bwana Yesu, Bwana wa Uzima, nipe neema Yako ya msamaha,” kama ningekuwa na nafasi ya kusimama mbele Zake.

Naamini hivyo ndivyo kila mtu hapa usiku wa leo anavyojisikia. Tungefanya jambo lile lile. Mimi…Lakini leo ni kama tu ilivyokuwa wakati huo. Tumechukuliwa sana na mambo mengi sana kanisani ya sisi kufanya, mambo mengi sana kanisa linatutaka tufanye, na sehemu nyingi sana za kwenda, mpaka kweli, tunashindwa mara nyingi kuipokea ile fursa. Na labda, usiku fulani ilitubidi kwenda kufanya mazoezi kwa ajili ya ibada ya nyimbo. Ilitubidi kufanya jambo lingine.

Jambo fulani, huenda, asili ya kidini, lakini wakati Roho Mtakatifu anazungumza moyoni mwako, jambo bora unaloweza kufanya ni kujibu kila wakati, haijalishi ni kitu gani, ni wakati gani wa usiku, ama ni aina gani ya kazi unayofanya; kwa sababu huenda asiongee tena kwa muda mrefu, na labda hatawahi kamwe.

MKATE WA KILA SIKU

Acheni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu… Zaburi 46:10

23-1125

23-1124

23-1123

23-1122

65-0801E – Matukio Yakidhihirishwa Na Unabii

Biblia hii inatabiri, kwa unabii, ni siku gani tunayoishi, na wakati gani tunaoishi, na ni matukio ya namna gani yanayopaswa kutukia. Inatabiri jambo hilo kikamilifu kabisa, wala haijakosea hata kizazi kimoja, wakati wote. Hakuna hata wakati mmoja ambapo imekosea, wala haitakosea, kwa kuwa waliochaguliwa tangu zamani kuliona wataliona.

Yesu alisema, “Hakuna mtu awezaye kuja Kwangu asipovutwa na Baba Yangu, na wote alionipa Baba Yangu watakuja.” Ni Neno likiungana na Neno. Haliwezi kutenda vinginevyo. Tunajua jambo hilo, siku tunayoishi.

Lakini kama vile ilivyokuwa katika kila wakati, watu wanamwachilia mtu aweke tafsiri yao kwenye Neno hili, na inawafanya watu wasione matukio yaliyotukia. Jambo lile lile limefanyika kwa Mafarisayo na Masadukayo.

MKATE WA KILA SIKU

Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho. Yohana 6:44

23-1121

61-0122 – Kama Vile Tai Ataharikishavyo Kiota Chake

Tai huwa hajengi kiota chake ardhini.  Tai hujenga kiota chake huko mbali juu awezavyo kufika kwenye kilele cha juu zaidi.

 Hiyo ndiyo sababu Mungu alimfananisha na kanisa lake.  Wewe ni mshumaa uliowekwa juu ya kilima.  Hiyo ni kweli.  Matazamio makuu, matarajio makuu, tunatarajia mambo makubwa.  Sisi si…Kusema, “Vema, mimi ni Mpentekoste.  Hilo linatosha.”  Hilo halitoshi kwangu mimi.  Natarajia mambo makubwa zaidi.

 “Mimi ni Mbaptisti.  Mimi ni Mmethodisti.  Mimi ni Waumoja, Uwili, Utatu,” ama chochote ulicho.  Hilo haliniridhishi Mimi.  Nina shauku ya kuendelea hadi nikutane Naye: juu-juu, juu-juu.

“Nilimpokea Roho Mtakatifu.  Hilo latosha.”  Halijanitosha.  Bado nalitwaa, na kusonga juu zaidi na zaidi (hiyo ni kweli.), kusonga mbele tu: matazamio makubwa, matarajio makubwa, matarajio.

 Sio, “Vema, tuna kanisa dogo zuri sana.  Tutaketi tu.  Mimi na umati huu mdogo, hatutaki yeyote wenu katika kundi letu.”  Si mimi.  Ninataka kunyoosha mkono kwa kila ndugu aliyeanguka kwa kanuni ya imani, hata iweje; nimlete ndani. Matazamio, fanya kitu fulani.  Matarajio kwa mwanamume ambaye amewahi kutembea katika kweli ili kuona kweli…Huwezi kamwe kumleta ndani kwa njia hiyo ya kumshusha chini.

Inabidi umzungushie mkono wako, na umpende, na umfanye ajue kuwa wewe ni ndugu.  Kisha jambo fulani litatokea.  Ikiwa wewe ni jamaa ya Yehova utafanya hivyo.  Una Roho Wake.  Yeye alikuja kwa wale waliomchukia, waliomfedhei, na kumtemea mate usoni Mwake.  Bado aliomba waokolewe.  Hakika.  Huyo ndiye Roho wa Mungu ndani ya mtu.

MKATE WA KILA SIKU

Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. Mathayo 5:14

23-1120

55-0807A – Kiburi

Katika watu wa Marekani kupitia televisheni, na kwa njia ya maonyesho ya picha, wameona mengi sana ya maigizo, hadi wakawa maigizo wao wenyewe: vibaya sana. Nasi tunayakuta kanisani, waigizaji. Hmmm. Mungu hawataki. Na iwe mbali nasi kuwa waigizaji. Kuwa kile ulicho; Mungu anakutaka hivyo. Nachukia kuona mtu akijaribu kufanya jambo asiloweza kufanya.

Ni aibu iliyoje, nimeliona mara nyingi, na sauti nzuri ambazo Mungu amewapa watu, karama, na kisha wanaipindua. Nachukia kusikia sauti iliyozoezwa kupita kiasi, wanaposimama kuimba, na kuchukua aina fulani ya nota mpaka wanaishikilia kwa muda mrefu mpaka wanakuwa wa bluu usoni, ili tu kuwaonyesha kusanyiko ni muda gani wanaweza kuishikilia kwa maisha pendwa. Nao wanaporudi, hao watu hawamsifu Mungu; akili zao ziko kwenye nota zao.

MKATE WA KILA SIKU

Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana.

Wagalatia 5:26

23-1119

57-0303A – Kwa Nini Wakristo Wengi Hupata Ugumu Sana Kuishi Maisha Ya Kikristo?

Angalia, sasa, “Nami Nitawapa roho mpya, nami nitatia Roho Yangu…” Angalia, moyo mpya unawekwa moja kwa moja katikati yako. Na roho mpya inawekwa katikati ya moyo wako mpya. Na Roho wake anawekwa katikati kabisa ya hiyo roho mpya.

Ni kama springi kuu katika saa maarufu. Wakati hiyo…Wakati hiyo springi kuu inapowekwa katikati ya saa, inadhibiti kila mwendo wa saa hiyo. Na hilo ndilo jambo lenyewe, enyi marafiki. Sasa, natumai mnaona jambo hili. Nami sisemi hili ku-jaribu kupindisha ama kuwa tofauti; Ninasema jambo hilo tu kwa sababu najua kwamba siku moja nitasimama kwenye hukumu pamoja nanyi.

MKATE WA KILA SIKU

Unaona, ikiwa Roho Mtakatifu yuko katikati ya roho yako…Na hiyo springi ya saa hufanya mienendo mingine yote ielekee kabisa mahali pake, kudumisha wakati mkamilifu. Roho Mtakatifu anapokuwa katikati ya roho yako, hufanya kila tendo la Roho Mtakatifu ndani yako litimie sawasawa kabisa na Saa ya Mungu, Biblia. Kweli.

Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama. Nami nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda. Ezekieli 36:26

23-1118

59-0525 – Sura Za Kristo

JNimeambiwa, na mabingwa, kwamba…kabla hawajakuwa na siku za kiyeyushi, kutoa ma—takataka katika dhahabu, kutoa chuma na kimbwi. Kimbwi inafanana sana, na dhahabu halisi, hata inaitwa “dhahabu ya mjinga.” Lakini jinsi walivyotoa hayo yote, waliipiga kwa nyundo. Wahindi walikuwa wakifanya hivyo. Na wafua dhahabu wa kale walikuwa wakifanya hivyo, kuipiga kwa nyundo, na kuigeuza tena na tena, na kuipiga mpaka takataka yote ikatoka ndani yake.

Na njia pekee waliyojua ya kwamba ilikuwa imebaki tu dhahabu, ilikuwa ni wakati mpigaji aliweza kuona uakisi wake ndani yake. Yule ambaye alikuwa akipiga angeweza kuendelea kutazama, hadi karibu aweze kujinyoa, kwa uakisi wake katika dhahabu aliyokuwa akipiga.

Basi Roho Mtakatifu wa Mungu anapoanza kutupiga, kwa nyundo ya Injili, mpaka mambo yote ya ulimwengu yametolewa, nasi tunaweza kuakisi sura ya Bwana Mungu, ndipo ninaamini tunakuwa Wakristo. Maana, neno Mkristo linamaanisha “kama Kristo, na kumwakisi Yeye.”

MKATE WA KILA SIKU

Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha kati ya moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwavyo, nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo; wataliitia jina langu, nami nitawasikia; mimi nitasema, Watu hawa ndio wangu; nao watasema, Bwana ndiye Mungu wangu. Zekaria 13:9

23-1117

23-1116

23-1114

23-1113

23-1112

23-1111

23-1110

23-1109

 61-0213 – Na Uzao Wako Utamiliki Malango ya Adui Zake

Mungu anapenda kufanya hivyo.  Mungu anapenda kuonyesha mkono wake wenye nguvu.  Ndiyo, anafanya hivyo.  Anapenda kuonyesha nguvu zake.  Anangojea usiku wa leo kukuonyesha jambo hilo, kumchukua huyo mwenye dhambi na kumgeuza, kumchukua mwanamke huyo mwenye sifa mbaya na kumbadilisha awe mcha Mungu, mwanamke mtakatifu, kumchukua msichana huyo ambaye ameshika njia mbaya, mvulana huyo katika njia mbaya, kuwarudisha mahali, na kuwafanya wana na binti za Mungu kutoka kwao.

 Yuko tayari kumchukua mtu huyo anayekufa kwa kansa, ambaye aliye na shida ya moyo, ambaye ni kipofu, yule anayeteseka, kama ataweka tu imani yake mle ndani ya kumgeuza kutoka mautini kuingia uzimani, amwanzishe na ushuhuda.

 Anangoja kufanya jambo hilo, anakuweka moja kwa moja kwenye mtego ili kuona unachofanya.  Aliwaweka moja kwa moja kwenye mtego ule pale, ilionekana kana kwamba maumbile yenyewe yalikuwa yameficha uso wake.  Ndiyo.

Mwandishi mmoja alisema wakati mmoja, ya kwamba walipofika mahali pale, jiulize Musa angefanya nini. Walikuwa na amri moja, “Songa mbele.”

Ikiwa uko katika jukumu, haijalishi ni kitu gani kisimamacho njiani, uzoefu mkubwa zaidi ambao nimewahi kupata ni kulikabili jambo ambalo nisingeweza kulivuka, ama kupita chini yake, nasimama tu hapo na kutazama Mungu akifanya njia ya kulivuka. Hiyo ndiyo njia ya kulifanya, wewe songa mbele tu, endelea kusonga, sukuma pua yako kulikabili.  Endelea kusonga tu, endelea tu kusonga mbele, Mungu atafanya njia.

MKATE WA KILA SIKU

Mungu wangu amemtuma malaika wake, naye ameyafumba makanwa ya simba, Danieli 6:22

23-1108

23-1107

23-1106

23-1105

23-1104

23-1103

23-1102

23-1101

23-1031

23-1030

23-1029

23-1028

23-1027

23-1026

23-1025

23-1024

23-1023

23-1022

23-1021

23-1020

23-1019

23-1018

23-1017

23-1016

23-1015

23-1014

23-1013

23-1012

56-0723 – Kuongozwa Na Roho Wa Mungu

Je, Unataka—unataka Mungu atume nguvu juu yako, nenda ukaombe na kuamini. Roho Mtakatifu atakuletea hilo, uponyaji, wokovu, cho chote unachokihitaji kwa Mungu atakuletea.

Naweza kuona kundi la watu waliokuwa waoga, mia moja na ishirini. Loo, maskini watu, wakale, waoga na hao walikuwa hapo. Walipanda hatua ndogo ya kale wakati mmoja, kwa maana Mungu alisema, “Sasa, msihubiri tena; msiimbe tena; msishuhudie tena mpaka mmejazwa na Roho Mtakatifu. Kisha Yeye atawaongoza ninyi kwa mataifa yote mkaihubiri Injili hii.”

Nao wakapanda juu orofani na kukaa huko, kwa woga, mlango ulikuwa umefungwa, madirisha yamefungwa, wakijiombea kwa sauti ya chini sana, na wakijificha Wayahudi wasiwaone mpaka Roho Mtakatifu alipowashukia.

“Kukatokea sauti kutoka mbinguni kama upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. Ndimi zilizogawanyika ziliwaka juu yao kama moto, na kutokea milangoni na madirishani wote wakatoka kwenda mitaani wakiongozwa na Roho Mtakatifu. Na ule Moto uliowashwa katika siku ya Pentekoste ungali umeigusa mioyo yetu tangu siku hiyo hata leo hii. Watu wanaotaka kuongozwa na Roho Mtakatifu…

MKATE WA KILA SIKU

…lakini watu wamjuao Mungu wao watakuwa hodari, na kutenda mambo makuu Danieli 11:32

23-1011

64-0816 – Kuthibitisha Neno Lake

Mungu hujifasiria Mwenyewe.

Alipoahidi, alisema, “Iwe nuru,” ikawa nuru. Akasema, “Bikira atachukua mimba,” akafanya hivyo. Mnaona, lo lote asemalo Mungu, Mungu hulithibitisha.

Haidhuru utajaribu vipi kuwazia kuwa ufufuo wa mwili haungewezekana, na watu hao wako kule nyuma, wakiwa mavumbi ya ardhi, na tayari wamepita mavumbi sasa, wamekuwa madawa na gesi ambayo miili yao ilifanyiwa. Nafsi zao zingali hai. Mungu alisema, “Nitaifufua.”

Ayubu alisema, “Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi na mabuu ya ngozini, lakini katika mwili wangu nitamwona Mungu.” Mnaona, haidhuru, kila Neno halina budi kutiiwa, na mtu ataishi kwa Neno hilo.

MKATE WA KILA SIKU

Akaniambia, Mwanadamu, je! Mifupa hii yaweza kuishi? Nami nikajibu, Ee Bwana MUNGU, wajua wewe. Ezekieli 37:3

23-1010

60-0109 – Mabwana, Tunataka kumwona Yesu

Njia pekee ya kumwona Mungu ni kumweka Yeye ndani yako, ili aweze kutumia macho yako. Utamuona Yeye. Lakini kama unajaribu kumwona katika dhana ya kiakili ya Neno Lake, ama kazi ya hisi fulani, haitafaa chochote; Anapaswa Yeye awe ndani yako.

Kisha utalia wakati wa machweo na mawio ya jua. Utatazama ukuu wa mwaka ujao. Kabla hata baridi au upepo wa baridi haujawahi kugonga dunia, utomvu utaiacha miti na kwenda chini kwenye mizizi, kujificha. Kwa sababu ukikaa huko, majira ya baridi kali yataua mti huo.

Kisha ninauliza swali hili, “Ni akili gani inayoendesha huo utomvu kutoka kwenye mti huo hadi kwenye mizizi ili kujificha kwa ajili ya majira ya baridi?” Loo, kafiri hana sababu. Lakini atakapoingia, utamwona katika kila kitu.

MKATE WA KILA SIKU

Ameiumba dunia kwa uweza wake, Ameuthibitisha ulimwengu kwa hekima yake, Yeremia 51:15

23-1009

54-0515 – Maswali na Majibu

Na hapa Biblia yanena kuwa Marekani (tuliyapata katika unabii) ilianza kama mwana-kondoo, “uhuru wa dini,” na moja kwa moja wakaunganisha mambo hayo pamoja, naye akanena kama joka na kutumia uwezo wote wa mnyama yule wa kwanza mbele yake, hiyo ni Marekani! Naam.

Mhudumu fulani aliniambia si muda mrefu uliopita, rafiki yangu, alisema, “Ndugu Branham, Mungu hataachilia kamwe Marekani ianguke, kwa sababu ya msingi wa waanzilishi wake wa kale, msingi wake ni dini.”

Nilisema, “Yeye aliwaachilia Wayahudi; wakaangukabili shaka, nao walikuwa na msimamo bora kuliko tuliokuwa nao.” Na hiyo ni kweli. Mungu hapendelei vizazi fulani vilivyopita; wewe utembee mstarini, la sivyo, haumo katika Ufalme, hivyo tu. Hakika! Hilo ni kali mno, lakini hilo ni zuri kwenu.

MKATE WA KILA SIKU

Lakini, jihadhari nafsi yako, ukailinde roho yako kwa bidii, usije ukayasahau mambo yale uliyoyaona kwa macho yako, yakaondoka moyoni mwako siku zote za maisha yako; bali uwajulishe watoto wako na watoto wa watoto wako; Kumbukumbu la Torati 4:9

23-1008

61-0219 – Malkia wa Sheba

Daima kumbukeni, enyi kanisa, Neno la Mungu ni kweli. Ninaamini mtazamo sahihi wa kiakili kwa ahadi yo yote ya Kiungu ya Mungu utaitimiza, ikiwa unaweza kuiangalia kwa njia ifaayo.

Lakini kumbuka, hiki kimekuwa ndicho ki—kipimo changu maishani, nimejaribu kufanya hivi: Jambo la kwanza, ninataka kujua kama ni mapenzi ya Mungu au la, hilo… ndipo ninajua ni mapenzi ya Mungu.
jambo linalofuata, ni lengo langu kuhusu jambo hilo, na nia yangu ya kulifanya; basi kama ni mapenzi ya Mungu, na lengo langu ni sahihi, na nia yangu ni sahihi, nina imani ya kwamba hilo litatendeka.

Kwa sababu, kwanza, ni mapenzi ya Mungu, nami nina— na lengo langu ni kumtukuza Yeye, na nia yangu ni kumpa Yeye utukufu wote. Unaona? Kwa hivyo hakuna nia za ubinafsi kuhusu jambo hilo, ikiwa una nia ya ubinafsi halitafanya kazi. Ikiwa lengo lako ni kujitengenezea pesa, ama kitu kingine, mbona, hutafanikiwa kamwe. Na kisha ujaribu kufanya jambo fulani nje ya mapenzi ya Bwana, basi halitafanya kazi tangiapo.

MKATE WA KILA SIKU

Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu:

     Wafilipi 2:5

23-1007

51-0729A – Kufufuliwa kwa Lazaro

Angalia. Uungu…Mimi ni sehemu ya Charles Branham, kwa sababu nilizaliwa kutoka kwa Charlie Branham, baba yangu. Mimi ni sehemu yake. Nina paji la uso kama yeye. Nywele zangu zilikuwa kama yeye. Mimi ni mtu mdogo kama yeye. Mimi niko katika asili kama yeye, kwa sababu yeye ni baba yangu.

Na tukifanyika katika roho wana wa Mungu, Uungu hukaa ndani ya mwanadamu. Haleluya! Basi Nena kuhusu macho ya vipofu kufunguliwa .

Walisema Hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu . Mungu Alisema Hakuna neno lisilowezekana kwako, kama utaamini, si kwa Mungu, bali wewe. Uungu uko ndani ya mwanadamu.

Mungu yeye yule aliyesimama kule nyuma kwenye jukwaa la umilele alilobuni, na kuziondoa dunia kutoka mikononi Mwake, na kuumba vitu hivi anakupa majaliwa ya kuwa mwanawe, nawe ni sehemu Yake. Na Mungu anakaa ndani ya wanadamu, na mwanadamu mwenyewe ni mungu. Haleluya!

Haya Basi. Laweza kukukaba, lakini jifunze juu ya hilo kwa muda kidogo Unaona?

MKATE WA KILA SIKU

Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu: Warumi 8:16

23-1006

58-0202 – Epukia Hapa, Njoo Upesi

Loo, ndugu, ni siku ilioje tunayoishi. Biblia ilisema katika siku hii ya kwamba (katika Timotheo wa Pili) “Roho anena waziwazi katika siku za mwisho watu watajitenga na imani, nao watakuwa wakaidi, na wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu.”

Nilikuja kanisani hivi majuzi; ilikuwa kuna theluji sana na kubaya kuja hapa. Lakini walikuwa na mchezo wa mpira wa kikapu, na iliwabidi wawafukuze mamia. Ni gani? Mungu wao ni mpira wa kikapu. Na ni yupi Mungu wenu basi? Kipande kikubwa cha hewa kilichopuzwa.

Ninayo furaha kwamba Mungu wetu ni Bwana Yesu Kristo katika Utu wa kufufuka Kwake, Muumba halisi aliye hai Aliyeziumba mbingu na dunia. Lakini wao wanataka kuliona jambo hilo. roho aliye ndani yao anavuta kwenye jambo hilo. Roho aliye ndani ya Mkristo humvuta kwa Kristo. “Mtu awezaje kuja Kwangu asipovutwa na Baba Yangu.”

MKATE WA KILA SIKU

Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi. Wakolosai 3:2

23-1005

63-1229M – Yupo Mtu Hapa Anayeweza Kuiwasha Taa

Kumbuka, katika kila wakati wa giza Mungu daima amekuwa na Neno Lake la kutenganisha Nuru na giza. Alikuwa nalo katika siku za Luther wakati kanisa Katoliki lilikuwa na kila kitu. Alimpeleka Luther kama Nuru iangazayo. Naye Luther akatenganisha Kweli na giza. Na wakati Waluteri walipotatanishwa, akamtayarisha John Wesley. Naye akatenganisha Nuru na giza.

Na katika siku za Pentekoste wakati Wamethodisti walipo—nao Wamethodisti walipojitatanisha, na Batisti, na Presbeteria, aliupeleka ujumbe wa Pentekoste kutenganisha Nuru na giza. Pentekoste ikarudi tena mpaka gizani vivyo hivyo tena katika dhehebu lao, ikachukua kanuni zao za imani na mengineyo.

Sasa, saa imewadia ambapo Neno hili litathibitishwa. Anapeleka Nuru, Neno lililodhihirishwa, kama alivyofanya mwanzoni, anapeleka Neno, na linajithibitisha Lenyewe.

MKATE WA KILA SIKU

Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na nzige, na parare, na madumadu, na tunutu… Yoeli 2:25

23-1004

61-0903 – Vivyo Hivyo Nuru Yenu na Iangaze Mbele ya Watu

Nafikiri tunamhitaji Kristo. Ndiyo, bwana. Njia pekee tunayomwona Kristo ni wakati ameakisi ndani ya sisi kwa sisi. Ninamwona Kristo ndani yako. Wewe unamwona ndani yangu. Hivyo ndivyo tunavyomwangalia Kristo. Ninakuja kwenye mkutano. Ninaanza kuhubiri. Ninawaangalia watu. Unaweza kuona kama wao wanavutiwa ama hawavutiwi, dakika chache tu. Unaangalia kwenye kusanyiko lako. Unaweza kujua kama unawachosha ama kama huwachoshi. Unaona?

Na muda si muda unajua, unawaona wameketi pale, wakishikilia kila Neno, chini ya matarajio. Unaona? Ninamwona Kristo ameakisiwa katika mtu yule, kwa maana anasikia njaa na kiu ya Mungu.

Halafu, mimi, nikihubiri Injili, yeye anamwona Kristo akiakisi ndani yangu. Ninamwona Kristo akiakisiwa ndani yake. Hiyo inamaanisha Kristo yuko miongoni mwetu basi. Amina. “Kuona njaa na kiu.” Ninawaangalia wasikilizaji, jinsi wanavyolichukua. Nasema kitu cho chote kile, ninaangalia lina matokeo ga—gani kwao. Ninaangalia nyuso zao zikichangamka, zimejaa furaha. Wako tayari wakati uo huo kupokea kitu fulani. Huyo ni Kristo. Ninamwona Kristo akiakisi katika mtu huyo kwa maana Injili, hii Injili rahisi ya Kristo, inashikilia kwenye moyo huo, kwa kuwa wanaona njaa na kiu.


MKATE WA KILA SIKU

Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu… Wakolosai 3:16

23-1003

54-0402 – Kipofu Bartimayo

Hapo, Yesu, akitazama juu ya barabara ile, barabara ambayo wewe na mimi usiku wa leo, sisi sote tuna hatia ya kumpeleka kwenye njia hiyo. Niani Mwake, alijua ya kwamba alikuwa anaenda Kalvari, kwenye njia hiyo. Katika njia hiyo alijua alikuwa anaenda Gethsemane.

Alikuwa akienda kwenye jumba la hukumu la Pilato. Alikuwa apigwe, adhihakiwe, na kisha vipawa vyake vikuu vya Mungu vilikuwa vijaribiwe. Wamfunge kitambaa kichwani Mwake na kumpiga kichwani na—na kusema, “Sasa, kama unajua yote yaliyo katika mioyo na akili za watu, niambie ni nani aliyekupiga.” Mambo hayo yote yalimkabili. Kifo cha kutetemeka, kichungu, hapo, ilimbidi akumbane nacho.

Naye alijua, likining’inia niani mwake, ya kuwa anakwea ili mikono yake akaangikwe mtini; Nguo Zake ziraruliwe kutoka Kwake, na viboko ambavyo vingechoma hadi kwenye mfupa, vilikuwa vikimzunguka. Na Damu Yake ingeosha mbavu Zake na taji la miiba katili lingewekwa juu ya kichwa Chake, Naye angesulubishwa msalabani na kuning’inia pale, akivuja damu, akilia, akifa, kama Dhabihu iliyojaa damu iliyowahi kutolewa ulimwenguni.


MKATE WA KILA SIKU

Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu;
Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona. Isaya 53:5

23-1002

23-1001

23-0930

23-0929

23-0928

23-0927

60-1125 – Kongamano

Hebu wazia tu. Ninaweza kumwona Gabrieli akishuka, upanga Wake mkuu ukiwa ubavuni Mwake. Ninaweza kumwona pakanga. Ninaweza kuwaona Malaika wengine wakuu wakiangaza juu ya mawe yaliyozunguka kando. Ilikuwa ni kitu gani? Meza ya kongamano ilikuwa imeandaliwa.

Kisha huyo Roho Mtakatifu wa Mungu, kama tuonavyo kwenye picha ya Gethsemane, ile Nuru, ambayo Mungu ni Nuru, El Elohim, Yeye Aishie Peke Yake, wakati aliposhuka katika Uwepo Wake. “Je! Unataka kupitia jambo hili, Mwanangu?” Kitu gani? Malaika wakisikiliza. “Ni nini Matokeo yake? Ulimwengu wote uko begani Mwako. Je! Unataka kulipia gharama, ama unataka kufanya nini? Waweza kuja sasa hivi moja kwa moja bila ya mauti. Hiyo hapo Kalvari iko mbele Yako. Ambapo watakutemea mate usoni Mwako, nao watakupeleka Kalvari, mambo haya yote. Utakufa kwa uchungu na taji ya miiba juu ya kichwa chako, na Damu yako itamwagika. Je, uko tayari?”

Hebu tuone hilo kongamano. Mwitikio wake utakuwaje? Malaika wote wamesimama huku wakishangaa kinachotukia sasa. Uamuzi umefanywa. Ni upi? “Si mapenzi Yangu bali Yako yatimizwe.” lo, Malaika wakazimwaga baraka zao na kuanza kumtumikia wakati huo, wakimtayarisha kwa ajili ya saa ile kuu. Kongamano lilifanywa. Uamuzi ukafanywa. Ninayo furaha kweli kwa uamuzi huo.

MKATE WA KILA SIKU

Akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke Luka 22:42

23-0926

60-0522E – Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #4

Hukuokolewa kwa Damu, unahifadhiwa mwongofu na ile Damu. Bali uliokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, ukiiamini Hiyo. Mungu alibisha moyoni mwako kwa kuwa alikuchagua tangu zamani. Uliinua macho yako ukaiamini, ukaikubali. Sasa Damu inafanya upatanisho kwa dhambi zako.

Kumbuka, nilisema, “Mungu hamhukumu mwenye dhambi kwa ajili ya kufanya dhambi.” Yeye kwanza ni mwenye dhambi. Yeye humhukumu Mkristo kwa kutenda dhambi. Na basi kwa sababu amemhukumu, Kristo alichukua hukumu yetu. Kwa hiyo hakuna hukumu ya dhambi kwa wale walio katika Kristo Yesu, wanaoenenda si kwa jinsi ya mwili, bali kwa jinsi ya Roho.

Na kama ukitenda jambo lo lote baya, si kwa maksudi. Hutendi dhambi maksudi. Mtu anayetenda dhambi makusudi, anaondoka na kutenda dhambi makusudi, hajaingia katika ule Mwili bado. Bali mara mtu anapoingia mle, amekufa, na uhai wake umefichwa katika Mungu, kwa njia ya Kristo, akatiwa muhuri na Roho Mtakatifu, wala Ibilisi hata hawezi kumpata, yuko kule nyuma kabisa. Itambidi kutoka mle kabla Ibilisi hajaweza kumpata, “Kwa kuwa umekufa!”

MKATE WA KILA SIKU

Unilinde kama mboni ya jicho, Unifiche chini ya uvuli wa mbawa zako; Zaburi 17:8

23-0925

52-0713E – Mungu Akishuhudia Karama Zake

Unapochukua msimamo wako kwa ajili ya Yesu Kristo, kaa hapo na ulifie jambo hilo. Yale asemayo Mungu ni kweli, nawe usiogope kile…Shetani hana lo lote la kufanya juu ya jambo hilo. Wewe usihojiane naye; usibishane naye. Wewe mpuuze tu na uondoke zako. Endapo ukibishana naye, atakufanya ubishane mchana na usiku. Unaona? “Vema,” yeye atasema, “Unajua hujaponywa.”

Utasema, “Vema, sasa, tazama, Shetani, nataka kukuambia jambo fulani.” Usiliseme. Wewe Sema tu, “Ondoka, sitaki kusikia lo lote kukuhusu.” Na uendelee kwenda, na useme, “Asante, Bwana.” Endelea. Unaona? Usivutie usikivu wo wote kwa jambo hilo.

MKATE WA KILA SIKU

Nimemweka BWANA mbele yangu daima, Kwa kuwa yuko kuumeni kwangu, sitaondoshwa. Zaburi 16:8

23-0924

50-0227 – Mungu Katika Watu Wake

Wengi wao walimwelewa. Watu wa kawaida walikuwa wakimsikiliza kwa furaha. Na ni jambo kubwa jinsi hiyo leo hii. Lakini nimeona Watu; madhehebu yote karibu yanahudhuria mikutano. Tuna hata Waorthodoksi, Wayahudi, Wagiriki, Wakatoliki, na wa kila aina. Lakini Mungu kamwe haheshimu madhehebu yoyote tofauti; Anaheshimu tu imani iliyo ndani ya mtu binafsi. “Naweza, mkiamini,” Yeye alisema.

Kisha akasema, “Nenda na usitende dhambi tena, au lisije likakupata jambo lililo baya zaidi. Kwa hivyo basi, ili kuupokea uponyaji wako, itabidi uwe Mkristo baada ya wewe kuponywa. Nami naamini, ningesema hivi, nikizungumza juu ya upatanisho wenye sehemu mbili, unapoponywa, dhambi zako zimesamehewa. Sikusikia amina nyingi sana juu ya jambo hilo, lakini hiyo ni kweli. Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa.

“Nendeni zenu, wala msitende dhambi tena, lisije likawapata ninyi jambo lililo baya zaidi. Yesu alisema, “Ni lipi lililo jepesi? Kusema umesamehewa dhambi zako, ama ujitwike godoro lako, uende”? Yote yanafanana.

MKATE WA KILA SIKU

Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii. Yakobo 5:16

23-0923

51-0717 – Dhihirisho la Roho

Sasa, unawezaje kuokolewa? Hebu na tulichukue hili katika hali ya kitoto ambapo kila mwamini, haidhuru kama wewe ni—ni wa kanisa gani. Na mchungaji wako, kama yeye ni mtu sahihi, atakuambia ya kwamba—ya kwamba unaweza tu kuokolewa kupitia imani, si kwa matendo, kwa imani. Sasa, unaamini ya kwamba Yeye alikuokoa.

Sasa, jambo la kwanza, hilo linatoka moyoni. Unaliamini jambo hilo. Kisha unatembea na kulikiri. Sema, “Ninamkubali Yesu kama Mwokozi wangu binafsi. Ninaamini Yeye aliniokoa.” Hakuna kitu cha kimwili duniani ambacho unaweza kuthibitisha kwamba umeokolewa. Macho yako yana rangi ile ile, umevaa shati lile lile ulilokuwa umevaa. Nenda nje huko na lile kundi la kale linasema, “Hakuna lo lote katika jambo hilo.” Lakini wewe unaamini kwamba kuna jambo fulani katika jambo hilo, sivyo?

Sasa, vipi…Vipi ikiwa ukisema, “Vema, nitaona jinsi litakavyokuwa.” Halitafanikiwa hadi uendelee na ushuhuda wako.

Unaamini kuwa umeokolewa. Unatenda kama umeokolewa. Unatamka umeokolewa. Nawe unashirikiana na wale waliookolewa, na inaleta wokovu. Je, hiyo ni kweli? Na jambo lile lile litatendeka kwa uponyaji wa Kiungu. Unaamini umeponywa. Unatenda kama Yeye amekwishakuponya. Unatamka umepona. Naye ni Kuhani Mkuu wa maungamo yako ili kufanya lo lote lile unalokiri kwamba Yeye amekwishalifanya kabla—mbele za Baba. Hilo hapo.

MKATE WA KILA SIKU

Basi, iwapo tunaye kuhani mkuu aliyeingia katika mbingu, Yesu, Mwana wa Mungu, na tuyashike sana maungamo yetu. Waebrania 4:14

23-0922

55-0603 – Yesu Kristo ni Yeye Yule Jana, Leo, Na hata Milele

Sasa, kama mhubiri sidhani kama Yesu alikuwa mhubiri mkuu mwenye nguvu. Yohana mbatizaji alikuwa mhubiri, lakini hakufanya ishara hata kidogo. Hakufanya muujiza kamwe.

Lakini Yesu alikuja kwa kutohubiri kwa nguvu kama Yohana, bali kulikuwa na ishara na maajabu yaliyofuatana naye. Yeye alisema, “Kama hamwezi kuniamini Mimi aminini kazi nizifanyazo. Kama hamwezi kuniamini Mimi aminini thibitisho ambalo Baba alilotoa kunihusu Mimi, kwa kuwa kazi nizifanyazo mimi, ndizo zinazoshuhudia ya kwamba Baba amenituma.” Ni kauli ilioje.

Wazia jambo hilo. “Kazi nizifanyazo zashuhudia ya kuwa Baba amenituma.” Mwanadamu anaweza kutoa kauli ya aina yoyote, lakini Mungu asipounga mkono kauli hiyo, unayo haki ya kusema si sahihi. Lakini Mungu anapokuja na kuithibitisha kauli hiyo kuwa ni kweli basi ni dhambi kutokuiamini.

Kwa maana dhambi ni nini? Dhambi ni jambo moja: “kutokuamini.”

MKATE WA KILA SIKU

Basi sasa, isikilize sauti na maneno ya BWANA. 1 Samweli 15:1

23-0921

61-1119 – Uweza Mkamilifu Kwa Udhaifu Mkamilifu

Kamwe hakukuwako na wito wa madhabahuni uliopata kufanywa katika Biblia nzima. Hakuna kitu kama hicho katika Maandiko. Hamna mahali kote katika nyakati ulipotolewa mpaka kwenye wakati wa Methodisti, yapata miaka mia mbili iliyopita, mnaona?

Miito ya madhabahuni ni wakati watu wanapokuja huku na kujaribu kuwashawishi na kuwavuta watu, “Njoo huku, Yohana. Unajua, wao…Mama yako alikufa, akikuombea. Njoo huku, Yohana.” Hiyo si imani, marafiki. La. Wa—wa aina hiyo, ninaninii…ni kwa nadra sana unasikia mmoja anayeenda mbali sana.

Na, katika jambo hilo, unapata kila kitu. Hiyo ndiyo sababu kanisa limechanganyikiwa kabisa jinsi lilivyo leo hii, ni kwa sababu ya mambo kama hayo.

Imani, haikubidi kusema jambo moja, ndugu, Mungu yupo na tayari ametenda kazi. “Petro alipokuwa akisema Maneno haya Roho Mtakatifu akawashukia wale waliolisikia lile Neno.” Unaona? Unaona? Unaona? Hakuna wito wa madhabahni, unaona, hakuna kitu kama hicho.

MKATE WA KILA SIKU

Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi. Luka 18:13

23-0920

61-0521 – Utuonyeshe Baba

Nami nawapenda tai, kwa sababu Mungu huwafananisha watoto Wake, urithi Wake, na tai, na Mungu, Mwenyewe, anajiita Tai, Yeye ni Yehova Tai, Baba Tai, sisi ni wana tai Wake wadogo.

Tai anaweza kuruka juu zaidi kuliko ndege yeyote yule aliyepo. Kama mwewe angejaribu kumfuata, angesambaratika hewani, kwa hiyo unajaribu kuiga Ukristo, unajisambaratisha tu mwenyewe, hivyo tu, isikusaidie chochote. Kuwa tai, zaliwa mara ya pili, maumbile yabadilike, ndipo unaweza kupanda ngazi ya Yakobo, ndipo unaweza kupanda hadi mahali pa juu sana ambapo mambo yote yanawezekana kwa hao waaminio, bali huna budi kuwa tai, mwamini.

Usijaribu…Waebrania walipovuka, kama tai, kuvuka Bahari ya Shamu, jaribu, likifuata, Wamisri wasiotahiriwa walijaribu kufanya jambo hilo nao wakapoteza maisha yao. Huwezi kuiga Ukristo, huna budi kuwa Mkristo. Hiyo ni kweli.

MKATE WA KILA SIKU

Maana yeye asiyekuwa na hayo ni kipofu, hawezi kuona vitu vilivyo mbali, amesahau kule kutakaswa dhambi zake za zamani. 2 Petro 1:9

23-0919

62-1013 – Ushawishi Wa Mwingine

Unapocheza mpira (kwa kuwa ni msimu wa kandanda), jambo tunalotaka kufanya, si kila mtu ajaribu kumnyang’anya mpira yule mtu aliye nao; ni kujaribu kumkinga huyo mtu. Mlindeni; mwache apite. Tunajaribu kuingiaza goli. Mwaona?

Bali ungaliwazia timu ambayo haijapata mazoezi sana hata kumpata mtu mmoja—mtu wao—akiwa na mpira amekimbia kuingiza goli, naye badala ya kujaribu kumwondolea adui, timu ya adui, kumwacha mtu wenu aliye na mpira kuukimbiza, kila mtu anajaribu kutoa mpira mikononi mwake. Naam, hapana shaka mtashindwa.

Na siku hizi, tuna jambo lile lile. Tunapomwona Mungu akijitokeza, na akibariki kitu fulani hebu na tuzuie adui kukifikia. Na tutumie ushawishi wetu kama wakinga, sio wakimbizaji, wakinga wanaomkinga anayekimbiza mpira, wamwache apite na mpira, maana hamna pingamizi, na yeyote ikupasayo kufanya ni kuendelea kukimbia. Nasi yatupasa kuwa wakinga.

MKATE WA KILA SIKU

Nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu. Wafilipi 3:14

23-0918

50-0115 – Je, Unasadiki Hayo?

Sasa, nataka uangalie tofauti kati ya Mariamu na Zakaria. Zakaria, yule mhudumu, mhudumu wa Injili, au mhubiri, kama ilivyokuwa katika siku hiyo, kuhani katika hekalu, Yeye alikuwa amejua kila namna ya mambo yaliyotukia hapo awali ya miujiza ya nguvu za Mungu, lakini yeye alimtilia shaka Malaika katika tukio lake. Ambapo Mariamu alisema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana. Hakuswali ingekuwaje ama kadhalika.

Na angalia ni kiasi gani Mariamu alipaswa kuamini zaidi ya kile zakaria alipaswa kuamini. Hana, alikuwa amepata mtoto hapo nyuma, alipokuwa amepita umri. Sara alipata mtoto kabla baada ya yeye kupita umri. Na hilo lilikuwa tayari limetokea mara nyingi. Lakini Mariamu alipaswa kuamini jambo ambalo halikuwahi kutokea. Hakuna mwanamke aliyewahi kuleta mtoto duniani namna hiyo bila kumjua mwanamume.

Lakini yeye alikuwa na mengi ya kuamini zaidi ya yale yaliompasa Zakaria. Hivyo basi, yeye hakumhoji Mungu; alimchukua tu Mungu kwenye Neno Lake. Amina. Nalipenda jambo hilo. Mchukue Mungu kwenye Neno Lake. Liamini hata hivyo. Haijalishi jinsi gani linavyoonekana kuwa haliwezekani, mwamini Mungu, Naye atalitimiza.

MKATE WA KILA SIKU

Akasema, Naamini, Bwana. Akamsujudia. Yohana 9:38

23-0917

55-0224 – Maji Kutoka Mwambani

Na Mungu anao mpango Wake, naye atakuweka na kukuweka mahali pako katika Kristo, mahali ambapo Yeye anafikiri utamfanyia kazi vyema zaidi, ikiwa utakaa tu katika wito wako.

Usijaribu kupata wito wa mtu mwingine. Kaa katika wito wako mwenyewe. Ikiwa wewe ni mama wa nyumbani, endelea kuwa mama wa nyumbani. Lo lote Mungu alilokuitia kufanya, baki papo hapo. Yeye Anajua mahali gani pa kuweka mkono wake juu yako na kukutumia.

Alikuwa na maskini mwanamke mdogo aliyeitwa Hana, wakati mmoja, mama mdogo wa nyumbani. Yeye alijua mahali pa kumweka, kile ambacho angetenda kazi naye. Alikuwa na mmoja aliyeitwa Mariamu, wakati mmoja. Loo, jamani, Yeye atakufanyia tu lo lote analotaka kufanya, ikiwa tu utamruhusu afanye jambo hilo. Uwe mnyenyekevu tu, jikabidhi kwake, na uendelee kusonga mbele.

MKATE WA KILA SIKU

Nami nafanya mambo yote kwa ajili ya Injili ili kuishiriki pamoja na wengine. 1 Wakorintho 9:23

23-0916

60-0522E – Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #4

Na wakati Mkristo amepakiwa Injili, amejazwa na wema wa Mungu, mambo yote mazuri ya Mungu yakikaa ndani Yake, kwa moyo mweupe, yuko tayari kufanya kazi, yuko tayari kuwekwa mahali pake, kufanya lo lote Roho Mtakatifu analomwambia afanye, amepita mautini akaingia Uzimani, ametakaswa na mambo yote ya ulimwengu, akitembea Nuruni jinsi Nuru inavyomjia, akisonga mbele, yeye yu tayari.

Ndipo Mungu anafunga mlango wa ulimwengu nyuma yake, na kuupiga pamoja hivyo, na kumtia muhuri kwa Roho wa ahadi aliye Mtakatifu. Haleluya!

Kwa muda gani? Hadi kwenye kikomo. Usimwondoe nje hapa kwenye mitambo ya reli na kumfungua uone kama kila kitu ni sawa tena. Ni sawa, mwache jinsi alivyo. Mkaguzi tayari amelikagua. Umetiwa muhuri kwa muda gani? Hata siku ya ukombozi wako. Huo ndio muda uliotiwa muhuri.

MKATE WA KILA SIKU

Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka. Mathayo 24:13

23-0915

62-0630B – Haikuwa Hivyo Tangu Mwanzo

Huenda usifikiri kuwa…watu wanakutazama, lakini wanatazama kila hatua unayofanya, wewe ni Biblia kwa watu wengi. Kwa hivyo, tunapaswa kuyaangalia yale tunayofanya, shughuli zetu za biashara na kila kitu tunachofanya katika mizunguko yetu yote.

Wewe jikabidhi tu kwa Roho, na Mungu atajidhihirisha Mwenyewe kupitia kwako, kama nilivyosema, kama vile mzabibu. Yesu alisema katika Yohana 15, “Mimi ni Mzabibu, ninyi ni matawi.” Vema, sasa kumbuka, mzabibu hauzai matunda, ni tawi ambalo huzaa matunda, lakini hupata uhai wake kutoka kwenye mzabibu.

MKATE WA KILA SIKU

Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda. Yohana 15:16

23-0914

54-0314 – Kwa Nini Ninawaombea Wagonjwa

Yeye kamwe Hakutuamuru sisi kujenga kanisa lolote. Yeye kamwe hakutuamuru kufanya hospitali, kufanya shule, au kuwa na seminari. Hakuwahi kutuagiza kufanya hivyo hata wakati mmoja. Mambo hayo yote ni mazuri, lakini hata hivyo alituagiza kuhubiri Injili kwa ulimwengu wote. Nasi tumejenga mashule, na maseminari, na kufundisha theolojia, na huku theluthi moja ya ulimwengu ndiyo yote ambayo bado imesikia kuhusu Yesu.

Lakini hata hivyo, kupitisha vijitabu si kuhubiri Injili. “Injili ilikuja si kwa neno tu,” alisema Paulo, “bali kwa nguvu na madhihirisho ya Roho Mtakatifu.” Unaona, unaenda…Si tu kufundisha Neno, bali kuhubiri, kulidhihirisha Neno. Neno halina budi kufanywa hai. Lingali ni andiko lililokufa hadi litakapodhihirishwa. Na ndipo linahuishwa, na linatimizwa, yale Mungu aliyosema kulihusu. Hiyo ndiyo Injili katika matendo, Ukristo wa Agano Jipya.

MKATE WA KILA SIKU

Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba. Mathayo 10:27

23-0913

61-0415B – Tangu Wakati Huo

Nguvu iliyo kuu kuliko zote duniani sio kunena kwa lugha, ama kufasiri lugha, ama kukirimiwa na Mungu kuwa mhudumu, ama kuwa mwinjilisti, ama kuwa nabii, silaha yenye nguvu kubwa zaidi ambayo nimewahi kupata maishani mwangu, ni upendo. Uta…Upendo wa phileo, ambao neno la Kiyunani linatokana na urafiki, kama vile ule ulionao kwa mke wako. Kuna tofauti. Itamfanya mama kwa mtoto huyo mchanga, apite kwenye moto mkali, maisha yake hayana maana yo yote, huo ni phileo. Agapao utafanya kitu gani? Unaona? Upendo wa kiungu.

Yatupasa kupendana, kupendana kiungu mmoja kwa mwingine, basi huoni kosa la ndugu yako. Kama akikosea, wewe kamwe, hutazama juu ya kosa hilo, nawe unampenda hata hivyo. Unaona? Hilo ndilo. Kuwapenda wale wanaowapenda ninyi, basi je, mwenye dhambi hafanyi vivyo hivyo?

Lakini wapende wale wasiokupenda, hilo ndilo linaloonyesha Roho wa Mungu yu ndani yako, kwa maana Yeye alikupenda ulipokuwa adui Yake, Naye alikupenda. Na kama huyo Roho yu ndani yako, atakufanya umpende adui yako, kama unavyompenda rafiki yako.

MKATE WA KILA SIKU

Tumikianeni kwa upendo. Wagalatia 5:13

23-0912

49-1225 – Uungu Wa Yesu Kristo

Basi angalieni basi, hiyo Damu ilishuka na ikawa…nayo ilikuwa ni Kristo Yesu. Naye Mungu Mwenyewe, akitoka katika Roho, aliingia ndani ya Kristo Yesu. Nayo Biblia ilisema, ya kwamba, “Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu kwa nafsi Yake.” Je, hiyo ni kweli? Mungu Mwenyewe, Yehova, aliishi ndani ya Kristo na akafanywa kuwa Jamaa yetu wa karibu, kwa sababu alizaliwa katika mwili wa mwanadamu kama sisi.

Je, hiyo ni kweli? Seli za Damu zilibuniwa na Mungu, na—nazo chembe za nyama zilikuzwa katika tumbo la uzazi la Mariamu, ambalo lilimzaa yule Mtoto. Basi Mungu akashuka na kuishi katika mwili wa mwanadamu, na akajaribiwa kwa kila njia kama tunavyojaribiwa. Je, mnaamini hilo? Vema.

Sasa, basi, alipofanya jambo hilo, Yeye alitoa Damu Yake bure. Haikumbidi kufanya hivyo. Alitoa dhabihu hiyo. Angeweza kwenda moja kwa moja Utukufuni. Angeweza kugeuzwa sura kama vile alivyogeuzwa kwenye Mlima wa Kugeuka sura, aende zake Mbinguni na kamwe asife kwa ajili yetu. Lakini akiwa tayari kutufia sisi, alitoa Damu Yake bure pale Kalvari. Hiyo ni kweli.

Naye akachagua…Alikuwa ni Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko, Naye akatoa ushuhuda hadharani.

MKATE WA KILA SIKU

Yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho. 2 Wakorintho 5:19

23-0911

53-0906A – Je, Unasadiki Hayo?

Na kama wanawake, kama tu mngetambua ni mamia ngapi ya mabilioni ya dola kila mwaka ambayo wanawake wanatumia Marekani kwa ajili ya vipodozi, kila unachoweka pajani—midomo mwako. Mimi Sijui vitu hivyo ni nini. Hata hivyo, ni mamilioni ngapi ya dola wanazotengeneza watu hawa kwa vitu hivyo wanavyojipaka usoni na kujipodoa namna hiyo…

Na wakati watoto wadogo maskini huko ng’ambo na wamishenari wanaoketi hapa wamelala kwa sababu hawawezi kwenda. Hawana pesa za kutosha kuendelea. Mungu atakuwajibisha juu ya jambo hilo siku ya hukumu. Hiyo ni kweli. Ni ukweli.

Ndio, Wakristo, mnajiita wenyewe Wakristo, huku mkija mkiwa mmejipamba na kujirembesha. Kulikuwa na mwanamke mmoja tu katika Biblia ambaye aliwahi kujipaka rangi usoni na huyo alikuwa Yezebeli. Unajua Mungu alimfanya nini? Alimlisha kwa mbwa. Hiyo ni kweli.

Na unapomwona mwanamke akitenda namna hiyo na kujiita mwenyewe Mkristo, wewe sema, “U hali gani, bibi nyama ya mbwa?” Hivyo ndivyo yeye alivyo: nyama ya mbwa. Mungu akamtoa kwa mbwa. Ndiyo, bwana.

Loo, tunachohitaji leo ni Roho Mtakatifu mwema wa mtindo wa kale akitembea kati ya watu kuwarudisha wanaume na wanawake kwa Mungu aliye hai tena.

MKATE WA KILA SIKU

Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani. Warumi 8:6

23-0910

62-1216 – Kuporomoka Kwa Ulimwengu

Mungu hana budi kuuhukumu ulimwengu kwa kitu fulani. Kama akiuhukumu kwa kanisa, atauhukumu kwa kanisa gani? Mbona, hakuna kitu cha kuuhukumia. Basi kuna Kitu kimoja tu kilichosalia, Neno Lake, Hilo ni la Milele, Hilo haliwezi kuongezewa wala kuondolewa.

Nimetia nanga nafsi yangu mle, kwa urahisi wa kuweka mikono yangu juu ya Dhabihu yangu, nikikiri ya kwamba mimi si mwema hata kidogo. Hakuna kitu ndani yangu, Ee Bwana Mungu. Mtume huyo Masihi juu yangu na ubadilishe utu wangu uwe vile nilivyokuwa, na unifanye katika sura Yako Mwenyewe, jinsi ungependa niwe.

Haijalishi ungaliuchoma mwili kiasi gani, jinsi gani ungalimwangamiza mtu, jinsi ungeongea dhidi yao, ama chochote anachosema, siku moja Yeye atatufufua tena. Na kuna Ufalme tunaoupokea ambao hauwezi kutikiswa. Loo, jamani!

MKATE WA KILA SIKU

Na mwenye haki akiokoka kwa shida, yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi ataonekana wapi? 1 Petro 4:18

23-0909

65-0424 – Mmoja Katika Milioni Moja

Yesu alisema, duniani, “Mtu hataishi kwa mkate tu, bali kwa kila Neno.” Kila Neno! Si tu mara kwa mara, Neno, bali kwa kila Neno.

Ilikuwa ni Neno moja lisiloaminiwa, na ninii ya Mungu…la amri za Mungu, lililosababisha mauti, huzuni, na kila maradhi na magonjwa ya moyo, kukosa Neno la Mungu, Neno moja! Kama aliipeleka jamii ya mwanadamu mautini, kwa kukosa, kutokuamini Neno moja, “hakika,” hakika. Bali Yeye alisema lingetukia. Shetani akasema, “Hakika halitatukia.” Lakini lilitukia.

Kwa hiyo, inatupasa kutimiza kila Neno la Mungu. Na kama mwanadamu na kuteseka huku kote na kadhalika kulikoingia kwenye jamii ya mwanadamu, kwa kuelewa vibaya, ama—ama kutokuamini Neno moja, tutarudi namna gani kwa kuacha Moja, kama liligharimu gharama hii yote, hata uhai wa Mwanawe?

MKATE WA KILA SIKU

Kwa maana ni amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni. Isaya 28:10

23-0908

59-1216 – Roho Mtakatifu Ni Nini?

Wakati Mkaguzi anapoingia ndani, kuyakagua maisha yako, kuona kana kwamba wewe si mlegevu kidogo kuhusu mambo, mlegevu kidogo juu ya maisha yako ya maombi, mlegevu kidogo juu ya hasira hiyo, mlegevu kidogo juu ya ulimi huo, kuzungumza juu ya wengine, Yeye kamwe hatalitia muhuri behewa hilo. Tabia fulani chafu, vitu fulani vichafu, nia fulani ya ushenzi, Yeye hawezi kulitia muhuri behewa hilo.

Bali wakati anapopata kila kitu mahali pake, yule Mkaguzi, basi analitia muhuri. Mtu ye yote asithubutu kufungua muhuri huo mpaka behewa hilo limefika kikomo chake ambacho limetiliwa muhuri! Hilo hapo.

MKATE WA KILA SIKU

Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi. Waefeso 4:30

23-0907

54-1114 – Ukombozi Kwa Hukumu

Wao wanasema Biblia imechapishwa kimakosa, imefasiriwa vibaya, na kadhalika. Tazama. Usijali, kile watu wasemacho kuhusu Biblia hiyo kuchapishwa kimakosa. Kama hii imechapishwa kimakosa, kitu kingine wanasema, “Hii imechapishwa kimakosa,” imani yako imetulia wapi? Hili ni Neno la Mungu. Hivi ndivyo inavyoonekana papa hapa. Unaona? Nami naliamini tu…

Sasa, Neno la…Sasa, huu hapa ukweli. Yule bibi aliyenijia hapa, wakati fulani uliopita…Nami—yeye hakuamini ya kwamba Jina Lake lilikuwa ni Yesu. Alisema Jina Lake linapaswa kuwa Yehova, kadogoo. Hmm. Kwa hiyo nikasema, “Bibi…” Unaona, kile ilicho, marafiki, watu ambao wana akili hizo, vyombo vya—kwa ‘itikadi,’

Jambo la kwanza unajua, wanaipokea, roho ya upotevu, na kwenda zao na kuamini uongo. Na wako—wako tayari tu kwa kitu kama hicho. Nawe usifanye, usifanye jambo hilo. Kuwa imara. Biblia ilisema, “Iweni imara, msioyumbishwa, mnaona, mkizidi sana katika Kristo.”

MKATE WA KILA SIKU

Angalieni mtu asiwafanye mateka kwa elimu yake ya bure na madanganyo matupu… Wakolosai 2:8

23-0906

63-0126 – Uwekezaji

Waaminio hawapaswi kucheza kamari kamwe. “Loo, vema, hii ni sawa. Nitabahatisha kwa hii.” Usifanye hivyo.

Kuna kielelezo kilichowekwa, kitu halisi, na Hicho si cha kundi lolote lile la watu. Ni Neno la Mungu. Usibahatishe kwa Hilo. Sasa, usibahatishe.

Pia jambo lingine nilionalo miongoni mwa watu, wakati mwingine, hususan. Mtu anapata pesa kidogo, halafu atajaribu kuiwekeza katika namna fulani ya lala maskini-amka tajiri, biashara isiyotambulikana. Utapoteza shati kutoka mgongoni mwako, nawe unajua hilo. Unaona? Usijaribu hilo.

Naye mfanyabiashara mzuri, mwenye akili timamu hatafanya hivyo. Mtu asiye na uzoefu wa kazi ndiye atakayebahatisha hivyo. Kamwe haina faida.

MKATE WA KILA SIKU

Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu. Mithali 3:13

23-0905

55-0911 – Kristo Asiyekaribishwa

Sasa, ilifanyikaje? Inawezekanaje? Je! ni kwa jinsi gani huyo mwosha miguu alivyomwacha Yesu apite? Huyu hapa, ameketi kwenye karamu, kwenye chakula cha jioni, na miguu ambayo haijaoshwa. Ameketi kwenye kona. Oooh, natamani ningekuwa huyo mwosha miguu. Natamani ningechukua mahali pake. Huyu hapa Yesu, kwa namna fulani…

Loo, aliishika miguu ya Dk. Jones, bila shaka. Aliishika mingine yote. Aliwaosha na kuwapaka mafuta. Simoni akamkaribisha kwa busu. Na hao hapo, wamesimama pale, wameburudishwa kweli kweli. “Lo, Dk. Jones, unajua nini? Huko kwa fulani fulani, hivi majuzi, Mfarisayo Fulani-fulani…Je! mnamkumbuka Farisayo Fulani? Unakumbuka?” Loo, wanashughulika sana kuongea juu ya mambo, hata wakashindwa kumwona Yesu akiingia.

Nami nashangaa, leo, kama hatujihusishi sana kuwa sisi ni Wamethodisti, ama Wabaptisti, ama Wapresbiteri, tumeshindwa kumwona Yesu akiingia. Ee Mungu, turehemu!

MKATE WA KILA SIKU

Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika; Warumi 1:22

23-0904

61-0415E – Sauti Isiyojulikana

Musa alikuwa, labda, hakuwahi kuisikia Sauti ya Mungu, bali alijua kiakili, alijua kwa hisi ndani yake, ya kwamba yeye ndiye alikuwa mkombozi, bali alijaribu kufanya jambo hilo naye akashindwa, kwa hiyo akasema, huenda nilikosea.”

Huenda kukawa na wahubiri wanaoketi nje hapa kwa namna iyo hiyo, unayewazia ulikosea, ulipojikuta umeshindwa, hukungoja tu muda mrefu vya kutosha. Biblia ilisema, “Wale wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya, watapanda juu kwa mbawa kama tai.”

Musa alifikiri labda ameukosa wito wake, lakini siku moja wakati Mungu aliponena naye uso kwa uso, naye akasikia Neno la Mungu, Malaika wangu alinena naye, na inalingana na Neno, alipoiona hiyo Sauti iliyonena naye ilikuwa ni jambo lile lile ambalo Neno lilikuwa limeahidi, basi alikuwa na imani, naye alikuwa na hakika ya kwamba alikuwa yuaenda kule.

Alikuwa na hakika Israeli wangetoka utumwani, kwa sababu Mungu alitoa ahadi, ilikuwa ni ahadi ya Kimaandiko.

MKATE WA KILA SIKU

Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi; Na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini; Warumi 5:3-4

23-0903

55-0806 – Yesu Kristo Yeye Yule Jana, Leo, Na hata Milele

Ni wangapi wenu wanaoamini kwa moyo wote? Je, unaamini? Ikiwa unaamini, unaweza kupokea.

Wasiwasi si kitu kwa Mungu kutokuponya, bibi. Unaamini atakuponya hiyo shida ya neva. Kuna kundi zima la watu hawa wanaoteseka na kitu hicho hicho. Ni wangapi huko nje wanaosumbuliwa na shida ya neva, inua mkono wako. Mnaona ninalomaanisha?

Kunayo mengi sana ya kuita. Lakini hayo mapepo yanaitana, michirizi myeusi ikikimbia kila mahali. Shetani anajua ameshindwa. Yeye anajua kama anaweza tu kuwapata watu hao…Kama hao watu watamwamini Mungu tu, jambo hilo litawaacha sasa hivi, kila mmoja wao. Wote watapona.

mnaona, ni kweli. Sio jambo fulani la kujiuliza. Yeye yuko hapa. Amefufuka kutoka kwa wafu. Je, mnaweza kuamini jambo hilo? Kama mnaweza semeni, “Amina” Kwake yeye, “Amina” kwa moyo wenu wote. Mungu anaishi na anatawala. Ni dhambi kwenu kutokuamini. hamwamini Mungu. Si mimi; ni Yeye. Anajua yote kuwahusu.

MKATE WA KILA SIKU

Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea. Mathayo 21:22

23-0902

53-0405E – Mashahidi

Mnajua, nafikiri, siku hizi, tunawazika watu wengi kupita kiasi walio hai.

Mnazika watu wakiisha kufa. Hiyo ni kweli? Naaam, bwana. Sikiliza, ndugu, mtu aliyekufa hatabishana nawe. Unaweza kumwambia chochote unachotaka, umwite majina ya kila namna, hatasema neno. Kwa nini? Amekufa.

Na mtu ambaye amekufa katika Kristo, unaweza kumpa pombe, unaweza kumpa hiki, kile, ama kinginecho, lakini amekufa. Naye amefichwa ndani ya Kristo, kwa njia ya Mungu, ametiwa muhuri na Roho Mtakatifu. Amina. Ndiyo hiyo. Sasa, basi, hawezi kufanya mambo hayo, kwa sababu ha—hawezi tu kufanya hivyo. Ni kinyume na asili yake. Anakuwa kiumbe kipya.

Hebu mchukue nguruwe mzee na kumwosha, na kumsugua, na kuzipodoa kucha za vidole vyake vya miguu, na kumpa rangi ya mdomo, na kumvika, nailoni zote utakazo; mfungulie, ataenda moja kwa moja kwenye kugaagaa na kugaagaa. Kusugua hakufai kitu. Angali ana asili ya nguruwe.

Na kisha mchukue mwana-kondoo na kumtia kwenye shimo la matope, atapiga kelele mpaka umtoe nje. Kwa nini? Yeye ni asili ya mwana-kondoo.

Sasa, njia pekee ya kumzuia nguruwe asiingie kwenye matope ni kuibadilisha asili yake. Hiyo ni kweli.

Hiyo ndiyo njia pekee ya kumfanya Mkristo. Asili yake ibadilishwe, kutoka mwenye dhambi kuwa mtakatifu. Unaona? Na kuna dawa moja tu, hiyo ni Roho Mtakatifu. Ndipo wewe ni shahidi. Amina.

MKATE WA KILA SIKU

Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya. 2 Wakorintho 5:17

An Independent Church of the WORD