UJUMBE: 65-0429E Kuchagua Bibi-Arusi
Mpendwa Bibi-arusi Aliyechaguliwa,
Wakati tunapousikiliza Ujumbe huu, Kuchagua Bibi-arusi, wengine wanafikiri kwamba nabii anazungumza tu na kutufundisha kuhusu tabia na kimo ambacho mwanamume anapaswa kuangalia wakati anapomchagua mwanamke anayemtaka awe mke wake. Hiyo ni kweli, anafanya hivyo, lakini hapo kuna barua ya mahaba halisi iliyofichwa katika Maneno Yake. Kile Yeye anachomfunulia Bibi-arusi Wake ni cha kina zaidi. Mungu anazungumza na Yeye(Bibi-arusi) moja kwa moja, akimwambia kile Yeye alichokuwa akikitafuta ndani Yake, na kwa nini Yeye alimchagua tangu mwanzo. Yeye alimtaka Yeye(Bibi-arusi) ajue kwamba Yeye amemchagua awe BIBI-ARUSI WAKE KIPENZI WA KUPENDEZA, ambaye Yeye alitaka ashiriki naye Umilele Wake.
Hapo mwanzo, Mungu alikuwa akimtafuta Bibi-arusi ambaye angekuwa na Tabia ile ile ya Kwake. Roho Wake yule yule angedhihirishwa ndani Yake(Bibi-arusi). Yeye alimtaka Bibi-arusi ambaye alikuwa amejitolea kabisa-kabisa Kwake, na Neno Lake lililoahidiwa, mpaka Nia ile ile iliyokuwamo ndani Yake iwe ndani yake Yeye(Bibi-arusi). Lazima afinyangwe kama Yeye alivyo.
Yeye alimtaka awe mwili Wake ule ule, mifupa ile ile, Roho yule yule, kila kitu kile kile, kama tu Yeye hasa. Wawili hao wangekuwa MMOJA.
Yeye hangekuwa na namna fulani ya macho jeuri. Yeye hangebembana huko na sauti nyingine yoyote. Yeye angekuwa mwaminifu na mkweli Kwake, haijalishi mtu yeyote angesema nini. Yeye angemkubali kwa Neno Lake. Chochote Yeye alichosema, YEYE ANGEAMINI KILA NENO, haijalishi ingechukua muda gani hilo kutimia, yeye angeliamini. Yeye angedumu na Neno Lake.
Yeye(Bibi-arusi) angempenda Yeye, na Yeye peke yake. Haikumlazimu Yeye kumpa utajiri mwingi, yeye alikuwa na Lulu ya thamani kuu, ule Ufunuo wa kweli wa Yeye( Bwana-Arusi). Yeye(Bibi-arusi) angejua, wao walikuwa MMOJA na kitu kimoja. Roho Wake angekaa ndani Yake. Chochote Yeye (Bibi-arusi) alichokihitaji, Yeye angempa; kitu tu Yeye(Bibi-arusi) alichopaswa kufanya ni kuomba na kuamini, na Yeye angekifanya.
Yeye(Bibi-arusi) alijua Yeye(Bwana-Arusi) angeondoka kwa muda mrefu kwenda kumjengea Yeye nyumba ambayo ingekuwa na kila kitu jinsi tu vile Yeye apendavyo kiwe na atakavyo. Yeye alikuwa akiijenga jinsi ambavyo Yeye (Bibi-arusi) angeipenda. Yeye (Bibi-arusi) alijua siku moja Yeye (Bwana-Arusi) angerudi kumchukua Yeye, kama Yeye alivyoahidi, kisha wangekuwa na Karamu Kuu ya Harusi kwa miaka elfu. Ndipo, wao wangeenda pamoja kwenye Makao hayo mazuri Yeye aliyomjengea waishi milele.
Hakuna kitu kingine ambacho kingekuwa muhimu kwake Yeye. Yeye asingetaka kitu kingine chochote. Yeye angeridhika mno na kutosheka na Ufunuo kujua Yeye (Bwana-Arusi) ni nani, na Yeye (Bibi-arusi) ni nani. Yeye (Bibi-arusi) angejua kwamba Yeye(Bwana-Arusi) angelitimiza Neno Lake. YEYE ANGETIMIZWA, AKIJUA YEYE NDIYE YULE AMBAYE YEYE ALIYEMCHAGUA KUWA BIBI-ARUSI WAKE.
Ndugu na dada zangu, Mungu mwenye nguvu wa Mbingu na nchi alitazama kote katika Umilele na AKAWACHAGUA NYINYI… NYINYI KUWA BIBI-ARUSI WAKE KIPENZI ALIYOWACHAGUA.
Ninawaalika mje muungane nami na sehemu ya Bibi-arusi Wake Jumapili hii, wakati Yeye anapozungumza kupitia malaika Wake Mwenye nguvu na kutuambia sisi ndio Bibi-arusi Wake Aliyowachagua.
Ndugu Joseph Branham
Ujumbe: 65-0429E / Kuchagua Bibi-arusi
Muda: saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki)
Maandiko Matakatifu:
Mwanzo 24:12-14
Isaya 53:2
Ufunuo 21:9