22-1023 Maswali na Majibu #4

Ujume: 64-0830E Maswali na Majibu #4

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 11MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Ndugu Joseph,

 1. Nimekusikia ukisema kwamba unaamini KILA NENO la Ujumbe huu ni BWANA ASEMA HIVI.

 Kutoka kilindi cha moyo wangu na kila mshipa katika mwili wangu NINAAMINI HILO.  Ni Sauti yenyewe hasa ya Mungu ikinena mdomo kwa sikio kwa Bibi-arusi Wake.

 Mungu alinena kupitia nabii wake na kusema:

  Nasema vivyo hivyo katika Jina la Yesu Kristo. Usiongeze kitu. Usiondoe—kuliwekea mawazo yako. Wewe sema tu yaliyosemwa katika kanda hizo. Tenda sawasawa kabisa na vile Bwana Mungu amekuamuru kutenda. Usiongezee Kwake .

 Ikiwa unadai unaamini Ujumbe huu wa wakati wa mwisho, wewe pia lazima uamini KILA NENO ili uwe Bibi-arusi Wake.  Shetani anajaribu kulipiga msasa Kupitia Wahudumu na kusema, “Ndugu Branham alipokuwa akisimulia hadithi za kuwinda au kusema ‘mnaye mpishi bora zaidi nchini’, au ‘Sina Maandiko kwa jambo hilo, lakini nitakuambia kile ninachofikiri;’ Haikupasi  kuamini sehemu hiyo.  Roho Mtakatifu yuko hapa kutuongoza kuelewa kile ambacho ni Neno na kisichokuwa Neno .”  HUYO NI IBILISI YULE YULE ALIYEONGEA NA HAWA NA KUSEMA, HAKIKA…. HAKUMAANISHA KILA NENO.  Je, linasikika kama unalifahamu?

 Wanafanya yale ALIYOWAAGIZA wasifanye.  Alisema SEMA YANAYOSEMWA kwenye kanda hizo, usiliwekee mawazo yako au uelewa wako.  Hakusema, “Kila kitu ISIPOKUWA sehemu hii na ile, na mchungaji wako atakuambia ni wakati gani alipokuwa Roho Mtakatifu  akizungumza na wakati gani alikuwa ni mimi tu.”  Mimi ni moja ya changarawe ndogo tu pwani kati ya mawe haya makubwa.

  2. Je, unafikiri Ndugu Branham na/au kanda zake ndizo Yakini?

 Ndugu Branham si Yakini Yangu bali Ujumbe alionena kwenye kanda ndiyo Yakini yangu Kabisa.

 Watu wengi husema hiyo si sahihi, Biblia ndiyo Yakini.  Rafiki yangu, Biblia na Ujumbe uliyo kwenye kanda ni kitu kimoja.  Hicho ndicho kiini hasa cha Ujumbe.  Ujumbe uliyo kwenye kanda ndiyo fasiri ya Biblia.  Hivyo ni kitu kimoja na jambo lile lile .

 Ukweli rahisi ni kwamba,  1: Biblia ni Neno.  2: Neno humjia nabii.  3: Nabii ndiye Mfasiri PEKEE wa Kiungu wa Neno.   4: Nabii wetu, William Marrion Branham, ndiye Neno lililodhihirishwa la siku yetu na alitumwa kulifasiri Neno.  5: Neno la Mungu halihitaji kufasiriwa.  Anachosema kupitia nabii wake kwenye kanda  NDIYO FASIRI YA NENO LAKE.

 Biblia inatuambia kwamba alikuwa anakuja tena na kuishi katika mwili kama alivyofanya na Ibrahimu na Yesu Kristo.  Alisema alikuwa na mambo mengi ya kutuambia.  Alisema angefunua siri hizi zote kuu ambazo zimefichwa katika Neno Lake.  Alisema hazihitaji fasiri yoyote.  Hakusema kamwe angetuma kundi kuongoza na kuwaunganisha watu Wake, YEYE MWENYEWE ANGEWAONGOZA WATU KUTUMIA NABII WAKE KAMA ALIVYOFANYA DAIMA.  NENO LAKE HALIWEZI KUBADILIKA.

 3. Je, unaamini kwamba wachungaji wanapaswa kucheza kanda katika makanisa yao?

 Kila mchungaji yampasa afanye kama anavyojisikia kuongozwa na  Bwana kufanya, kwa kuwa kila kanisa linajitawala lenyewe .  Ninaamini, na nimesema mara nyingi mimbarani, ya kwamba wachungaji wanapaswa kumrudisha Ndugu Branham kwenye mimbara zao kwa kuzicheza kanda.  Sijawahi kusema yawapasa waache kuhubiri, wacheze tu kanda.  Lakini wanatumia kila kisingizio cha kutocheza Sauti ya Mungu katika makanisa yao.

 Nitamwacha nabii aseme jinsi ninavyohisi kuhusu wachungaji ambao hawataicheza Sauti hiyo katika makanisa yao.

  Sasa, Ndugu Junior Jackson alikuwa na haki ya kutokukubaliana na hayo. Yeye ataka kanisa lake…Watu wote wanataka kunena kwa lugha na mengineyo mkutanoni. Hizo ni taabu za Ndugu Junior; hiyo ni—hiyo ni juu yake. Lakini Junior Jackson anaamini Ujumbe huu sawasawa kama wengine wetu wote wafanyavyo. Yeye ni mmoja wetu.

 4. Je, unaamini kwamba wahudumu wanapaswa kuacha kuhubiri?

 Hapana, sijawahi kusema hivyo wala siamini hivyo.  Neno linatuambia, na Ndugu Branham amekuwa wazi kabisa kwenye Jumbe hizi za Maswali na Majibu, kwa wahudumu kuendelea.

 Najisikia tu kuongozwa, kwa kanisa langu, kufanya utangulizi wa haraka;  ama kwa barua kwa sasa, kisha Kubonyeza Play na kusikia Sauti PEKEE ya Mungu  iliyothibitishwa kwa siku hii.  Nimesema mara nyingi kwamba nina huduma kuu zaidi ulimwenguni, napata kutambulisha Sauti ya Mungu kanisani kwangu kila Jumapili.

5. Watu wanasema unahisi  Usipojiunganisha na ibada za Maskani ya Branham wewe si Bibi-arusi?

 Sijawahi KAMWE kusema hivyo au hata kufikiria hivyo, ndugu na dada zangu.  Yeyote anayeweza kusema kitu kama hicho ni makosa . Nikiwa Kama mchungaji wa Maskani ya Branham, najisikia nikiongozwa kucheza kanda za Ndugu Branham.  Ninaamini hiyo Sauti ndiyo kitu pekee kitakachomuunganisha Bibi-arusi.

 Kama nilivyosema awali, ninaamini kila kitu kwenye kanda hizi ni Bwana Asema hivi na hakihitaji fasiri yoyote.  Ninaweza kusema amina kwa kila Neno ninalosikia.  Ninaamini William Marrion Branham alitumwa kumwita Bibi-arusi atoke .  Nafasi yangu katika huduma tano ni kuwaelekeza watu kwa mjumbe huyo na kisha Kubonyeza Play . Hakuna kitu kikubwa zaidi ya kuisikia Sauti hiyo.  Upako mkuu zaidi uko kwenye kanda, kwa hiyo kwa nini nitake kulipatia kanisa langu kitu kingine?

 Kila Jumapili ninaualika ulimwengu kusikiliza Ujumbe ambao Bwana ameweka moyoni mwangu ili kuucheza kwa kanisa langu.  Kila mtu anakaribishwa kusikiliza kwa wakati mmoja.

 Ninatumia kama kiongozi wangu kile Ndugu Branham alichosema kwenye kanda hizi .

Nasi tuna mfumo huu wa simu sasa, ambao ni mzuri sana, sana. Watu wanaweza kuketi moja kwa moja nyumbani mwao ama nini hii mwao…wakusanyike makwao, makanisani mwao, na kadhalika, na kusikiliza ibada. Nafurahia jambo hilo.

Sasa, ewe mchungaji, nataka ujue jambo hilo, ya kwamba, ninazungumza haya kwa ajili ya kusanyiko langu peke yake. Nami nina haki ya kutenda jambo hilo, kwa maana nimewekwa na Roho Mtakatifu kuwachunga kondoo hawa.

Ujumbe huu, na Jumbe zote zingine ambazo ninazungumzia, zinaelekezwa kwenye kusanyiko langu. Si kwa ajili ya kusanyiko lako isipokuwa wawe wanataka kulipokea. Bali limeelekezwa kwa watu hawa hapa.

Na hilo ni kote kote ulimwengu mzima. Na watu huamka usiku wa manane usiku, katika nchi za kale, hufanya mnyororo huo wa maombi kwa wakati mmoja.  Kwa hakika, makumi elfu na maelfu kwa maelfu wanaomba kwa wakati mmoja.  Mungu hana budi kusikia;  wewe ni—unaivumisha tu Mbingu kwa maombi, unaona, kwa hiyo hana budi kusikia.

 6. Je, ni kosa kwenda kanisani ?

 Sijawahi kusema hivyo wala kuamini hivyo.  Ikiwa niliamini hivyo kwa nini ningekuwa na kanisa?  Katika Maskani ya Branham tulikuwa na ibada 3 kwa wiki hadi ikawa vigumu sana kwangu kuwa na ibada nyingi jinsi hiyo kila wiki na kufanya kazi katika VGR.  Ndipo tukawa na ibada 2 kwa wiki katika Maskani hatimaye isingewezekana kutosha watu .  Kwa hiyo tulihamia kwenye jengo letu tulilotumia kwa ajili ya vijana wetu, ambalo lilikuwa jumba la mazoezi.

 Bwana alikuwa ameweka moyoni mwangu kutoa tamko Jumapili moja asubuhi.  Nilisema hata ikiwa siku moja wangefunga milango ya kanisa hili , hatutakosa hata mpigo kwani mchungaji wetu angeweza kuzungumza nasi popote tulipo.  Mwezi mmoja baadaye,  CORONA Ikaja ambayo ilifunga makanisa kote ulimwenguni.

 Nilijisikia kuongozwa kwamba wakati huo, tungekuwa na fursa nzuri ya kurekebisha ukumbi wa mazoezi, kwani tulihitaji mahali pakuabudia.  Kwa hivyo, tumekuwa na furaha katika nyumba zetu, kuungana na kumsikiliza nabii wa Mungu kwenye kanda pamoja na sehemu ya Bibi-arusi duniani kote, wakati kanisa linarekebishwa.

 Sasa hivi tunamalizia jengo, lakini kama vile tu wakati Ndugu Branham alipokuwa hapa kwenye Maskani ya Branham, tayari tumepita eneo la ziada la maegesho tulilojenga.  Itatubidi tu kuomba na kuona jinsi Bwana aongozavyo.

 Najua kuna maswali mengi, mengi zaidi kwenye mioyo ya watu.  Kuna mambo mengi niliyosema yameeleweka vibaya.  Ikiwa Ndugu Branham Walimwelewa vibaya, ni kiasi gani zaidi basi mimi nitakavyoeleweka vibaya?

 Ninaweza kuwa nimekosea katika kile nilichosema.  Ningeweza kuyasema vizuri zaidi au ningekuwa wazi zaidi kwa jinsi nilivyoyawasilisha.  Ila kuna jambo moja NAJUA ni sahihi, UJUMBE HUU NI MKAMILIFU .  Sio lazima unisikilize mimi au Kile nisemacho, lakini YAKUPASA UBONYEZE PLAY NA UAMINI KILA NENO.

 Kwa mara nyingine tena, ninakualika uungane na Maskani ya Branham Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania) tunaposikia: Maswali na Majibu #4 64-0830E .

 Ndugu.  Joseph Branham