UJUMBE: 59-0510M Siku Kuu Ya Mama
Bibi-arusi Kipenzi,
Sasa, nafikiri hakuna heshima ya kutosha ambayo tungeweza kumpa mama.
Mama yetu ndiye wa kwanza wa kuwa na sisi, na amepewa jukumu kubwa la kile tutakachokuwa na njia tunayopaswa kuifuata. Amepewa jukumu kutoka kwa Mungu la kutuweka kwenye njia sahihi. Ndiyo sababu akina mama wana mguso mdogo maalum, waliopewa kutoka kwa Mungu.
Ni baraka ya kipekee iliyoje tuliyowekewa Jumapili hii, tunapowapa heshima wa Mama wote, wakati tunapomsikia malaika wa saba wa Mungu akielezea upendo na heshima ambayo mama zetu waliyonayo mioyoni mwetu.
Tunajua kila siku ni Siku kuu ya Mama, lakini Jumapili hii tutatoa heshima maalum kwa wa Mama wote tunapomsikia nabii wetu akiwapa heshima kama alivyonena miaka 67 iliyopita siku iyo hiyo hasa, tarehe 10, Mei, 1959.
Ndugu. Joseph Branham
Ujumbe: Siku Kuu Ya Mama 59-0510M
Saa: 6:00 MCHANA. Masaa ya Jeffersonville(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki)
Maandiko: Wakorintho wa Kwanza 15:1-4