22-0911 Mabirika Yavujayo

UJUMBE: 64-0726E Mabirika Yavujayo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wanywaji wa Maji ya Kisima Kinachofoka Maji.

Hatukupandikizwa, sisi ni sehemu ya uzao asili wa Neno. Roho Mtakatifu Mwenyewe, ameivisha, amethibitisha, na kujidhihirisha Mwenyewe kwetu. Tumelikubali kwa utimilifu Wake, kwa uwezo wa thibitisho lake na Ufunuo wa kile lilicho, nasi tumekuwa sehemu Yake. Ni zaidi ya uhai kwetu.

Roho Mtakatifu Mwenyewe alinena kupitia chombo kinyenyekevu, kisichostahili na kusema, “Hii hapa Fimbo Yangu ya kifalme , Neno Langu, lichukue, uende zako, na uupeleke Ujumbe.” Alichukua Neno Lake na kutubangua, kutufanya kuwa Bibi-arusi Wake.

Imewasumbua makasisi kuona watu wakitoka makanisani na kwenda kucheza kanda. Walisema, “Ikiwa yeyote wenu atahudhuria hiyo mikutano, utatupwa nje , tutakuweka nje ya shirika letu”.

Jibu lao ni: Mnaweza pia kutuachilia, tutaendelea hata hivyo! Tuko safarini pamoja na Bwana Yesu, Mwamba wetu uliopigwa, tukila Chakula cha malaika, mana iliyohifadhiwa ghalani kutoka juu, na kunywa kutoka kwenye Mwamba huo. Hatupaswi kamwe kuhangaikia kile tunachokunywa, Si chochote ila NENO SAFI.

Daima tumekuwa na uamsho unaoendelea. Chemchemi yetu daima inabubujika tena na tena, na tena na tena. Hakuna mwisho wake.
Tunapata kinywaji safi na baridi cha maji kila tunapobonyeza Play. Tunakitegemea na tunaishi kwacho. Jambo likupasalo kufanya tu ni kwenda kule na Unywe.

Tunaishi kwa chemchemi hiyo kila siku! Haitubidi kuvuta, kuchimba, kuvuta kwa mashine, au chochote kile; tunashiriki tu katika njia aliyoiandaa yeye , bure . Unaweza kuchukua taratibu zako zote zakujitengenezea unazotaka, visima vyako vyote vya kale vya maji yanayooza; kwetu sisi, tumekuja kwenye Chemchemi yake safi. Ni Furaha yetu. Ni Nuru na Nguvu zetu.

Yeye ndiye furaha yangu. Yeye ndiye Nuru yangu. Yeye ni—Yeye ni nguvu zangu. Yeye ni Maji yangu. Yeye ni Uzima wangu. Yeye ni Mponya wangu. Yeye ni Mwokozi wangu. Yeye ni Mfalme wangu. Kila ninachohitaji kinapatikana Kwake. Kwa nini niwe na hamu ya kukiendea kitu kingine?

Kwetu sisi hakuna mahali pengine pa kwenda ila moja kwa moja kwenye Chemchemi iliyotolewa na Mungu. Hatuna hofu kamwe tutakunywa nini. Haitulazimu kuweka kitambaa cha kale cha kuchujia ambacho kinaweza kutoa vitu vikubwa, lakini huacha juisi mbaya. TUNAPATA TU MAJI SAFI YA KISIMA KINACHOFOKA MAJI YENYE MADINI NA VIRUTUBISHO VYOTE TUNAVYOHITAJI.

Ametuhakikishia: Watoto wangu wachanga , msiwe na wasiwasi tena, mnao ushahidi wa kweli wa Roho Mtakatifu. Mmenithibitishia Mimi ya kwamba mnaamini kila Neno. Mmelipokea, NINYI NI WANGU. SISI NI KITU KIMOJA. MUME NA MKE.

Ninakuja kwa ajili yenu katika muda mfupi, katika kufumba na kufumbua jicho. Ninawaandalia Makao mapya. Mtapenda jinsi nilivyoyafanya.
Najua ni ngumu sana kwenu sasa, na mna mitihani mingi na majaribu na mizigo yenu ni mizito. Lakini msisahau, hamna chochote cha kuhofia , Nimewapa Neno Langu. Ninyi ni Neno Langu . Tayari nimefanya kila kitu kwa ajili yenu. Nena Neno na msiwe na shaka. Mnayo Imani yenu, pamoja na nabii Wangu aliwapa Imani yake.

Ningependa uungane nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, ( Ni saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania) kusikia 64-0726E Mabirika Yavujayo , na kunywa kutoka kwenye Chemchemi hii inayofoka maji inapobubujisha Neno Safi ambalo halihitaji chujio.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza ibada

Zaburi 36:9
Yeremia 2:12-13
Yohana Mtakatifu 3:16
Ufunuo Sura ya 13 yote.