22-0904 Kutambua Siku Yako Na Ujumbe Wake

UJUMBE: 64-0726M Kutambua Siku Yako Na Ujumbe Wake

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Waliokatwa Watoke,

Nataka kila mtu ajue kwanini tunafuraha sana jinsi hii!!

Tumelikubali Neno la Bwana. Neno lililofunuliwa lililonenwa, na nabii wa Mungu wa Malaki 4. Sisi ni Bibi-arusi wa Yesu Kristo. Sisi Ndio ambao tumedumu waaminifu kwa Sauti Yake iliyothibitishwa. Sisi ndio ambao Aliyowapa Lulu ya thamani kuu, Ufunuo wa kweli wa Ujumbe Wake na mjumbe Wake.

Mungu amechukua Neno la nabii Wake na kumbangua Bibi-arusi anayeamini kila nukta na kila yodi. Ametukata, kama alivyoahidi atafanya. Sisi ni kondoo wa Mungu, na tunaisikia tu Sauti ya Mungu! “Kondoo Wangu huisikia Sauti Yangu,” tunapobonyeza Play.

Tuna Washiriki kutoka kote nchini; kutoka New York, kutoka Massachusetts, hadi Boston, Maine, Tennessee, Georgia, Alabama, na kote nchini. Kutoka Afrika hadi Mexico, Ulaya hadi Australia, tunakusanyika pamoja, chini ya Ujumbe Mmoja, Sauti Moja, nayo inamuunganisha Bibi-arusi kwa ajili ya Kunyakuliwa.

Nabii wetu, mjumbe wa Mungu, Mwana wa Adamu akijifunua Mwenyewe katika mwili, anapaza sauti, “Shetani, ondoka njiani, nina Ujumbe wa Mfalme. Mimi ni Mjumbe wa Mfalme. Nina Neno lililothibitishwa la siku hii. Nimekusudiwa kumwita Bibi-arusi Wake atoke na Kumwongoza.”

“Ninajaribu kuwavuta watu fulani, kuwakata niwaondoe kwenye mambo haya. kuwavuta watoke; kuwaonyesha, kwa Maandiko, ya kwamba Mungu amesimama hapa; pamoja na thibitisho la Nguzo ya Moto”

Mungu ametambua ya kwamba kuna watu fulani ulimwenguni ambao aliwakusudia Uzima. Alitambua ulikuwa ni wakati wa kumtuma mjumbe Wake kumwita Bibi-arusi Wake atoke, Hivyo Yeye Akamtuma . Sisi Ndio wale Waliotambua jambo hilo. Sisi ndio wale Aliojua tungeamini kila Neno.

Ibrahimu alitambua ya kwamba Mungu alikuwa akisema naye katika mwili wa Kibinadamu. Alitambua ishara Yake na kumwita B-W-A-N-A, Elohim, na akabarikiwa na Bwana. Tumetambua ya kwamba kama ilivyokuwa katika siku hiyo, ndivyo itakavyokuwa wakati Mwana wa Adamu atakapodhihirishwa, Elohim, akinena katika mwili wa kibinadamu.

Sisi ni sehemu yake, na Mwanawe, na tutadumu naye milele. Si kwa wito wetu au uchaguzi wetu, bali kwa uchaguzi wake. Hatukuwa na uhusiano wowote nalo. Yeye ndiye aliyetuchagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Haidhuru utahubiri namna gani, hata ufanye nini, haliwezi kuivishwa, haliwezi kudhihirishwa, haliwezi kuthibitishwa; ila tu na Yeye aliyesema, “Mimi Ndimi Nuru ya ulimwengu,” lile Neno. Kwa hiyo hakuna budi kutokee Nguvu fu—fu—fulani, Roho Mtakatifu Mwenyewe, kuivisha, ama kuthibitisha, ama kuhakikisha, ama kudhihirisha ya kwamba yale ambayo Yeye amebashiri yangetukia katika siku hii. Nuru ya jioni inaleta hilo. Ni wakati wa jinsi gani!

Alituona katika lile ono tulipokuwa tukipita mbele yake. Tulipitia mahali pale pale alipopitia Bibi-arusi wakati alipopitia hapo mwanzo, Alfa na Omega. Alikuwa akiangalia wengine wakitoka mstarini, na alikuwa akijaribu kumvuta , lakini sisi ndio Wale tuliopaza Sauti, “Tunategemea jambo Hilo.”

Angalia, “Kama vile Yane na Yambre pia walivyompinga Musa,” yeye atakuja moja kwa moja, baadhi yao . Si , sasa, yeye hazungumzi kuhusu Mmethodisti, Mbaptisti, hapa; wao wako nje ya picha . Unaona? “Lakini kama vile Yane na Yambre walivyoshindana na Musa na Haruni, vivyo hivyo hao nao; watu walioharibikiwa na akili zao kuhusu ile Kweli.” wamepotoka wakaingia katika mafundisho ya sharti na mafundisho ya kanisa, badala ya Biblia.

Jinsi inavyotupasa kuwa waangalifu sana kudumu na Neno la kweli, lililothibitishwa la siku yetu. Ni lazima kila wakati tukumbuke na kutambua Neno humjia nani. Ni nani aliye mfasiri pekee wa kiungu wa Neno? Ni nani Aliye Neno la siku yetu ?

Roho wa Mungu, ambaye ni Neno la Mungu, “Neno Langu ni Roho na Uzima,” litamweka Bibi-arusi mahali Pake. Kwa maana, Yeye Atatambua nafasi yake katika Neno, ndipo anakuwa ndani ya Kristo, litamweka kwenye nafasi yake .

Umealikwa kuja kusikiliza Sauti pekee ya Mungu iliyothibitishwa ya siku yetu, na kutambua nafasi yako katika Neno na kuwekwa mahali pako tunapomsikia Elohim akisema kupitia nabii Wake na kutuletea Ujumbe: Kutambua Siku Yako na Ujumbe Wake 64-0726M , saa 06:00 MCHANA , saa za Jeffersonville (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania.)

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikia Ujumbe:

Hosea: Sura ya 6 yote

Ezekieli: Sura ya 37 yote

Malaki: 3:1 / 4:5-6

2 Timotheo: 3:1-9

Ufunuo: Sura ya 11 yote

Mungu, umba ufufuo ndani yangu! Jalia niwe huo ufufuo. Jalia kila mmoja wetu awe huo ufufuo, ufufuo ndani yangu. Nifanye mimi, Bwana, nipate njaa, nifanye nione kiu. Umba ndani yangu, Bwana, kile ambacho kinahitajika ndani yangu. Nijalie, tangu saa hii na kuendelea, niwe wako; mtumishi aliyewekwa wakfu zaidi, mtumishi bora, aliyebarikiwa zaidi na Wewe; mwenye uwezo zaidi, mnyenyekevu zaidi, mwema zaidi, mwenye kupenda kufanya kazi zaidi; mwenye kuangalia zaidi mambo ambayo ni ya kweli, na kusahau mambo yaliyo nyuma, na mambo yasiyo ya kujenga. Jalia nikaze mwendo kuelekea kwenye mede ya wito mkuu wa Kristo. Amina.

Rev. William Marrion Branham