All posts by admin5

24-0310 Sikukuu Ya Baragumu

UJUMBE: 64-0719M Sikukuu Ya Baragumu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Watoto wa Nuru,

Tunayo shukurani jinsi gani kuwa tunatembea katika Nuru Yake. Kuwa sehemu ya Nuru hiyo, kutambulishwa na Nuru Yake. Kuitwa na kuchaguliwa Na Yeye. Sisi ni Bibi-arusi wa Kristo, tumetambulishwa pamoja Naye. Hao wawili sasa ni Mmoja.

Nisingeweza kuliandika mara nyingi sana. Hatuwezi kulisema vya kutosha. Ujumbe huu unamaanisha KILA KITU kwetu. Kujua kuwa tunao Ufunuo wa kweli wa Neno Lake ni zaidi ya chochote tungeweza kuweka kwa maneno.

Kuishi katika siku hii na kuwa sehemu ya kile kinachotendeka, ndio heshima iliyo kuu ambayo Mungu angeweza kutupa. Jinsi lilivyokuwa jambo kuu kuketi katika mikutano katika Maskani ya Branham, kuona na kumsikia malaika wa Mungu akizileta Jumbe hizi, ni KUU hata na zaidi kule kuishi katika siku hii, na wakati huu, na kuwa ule utimilifu wa Neno hilo.

Mungu, katika Mpango Wake mkuu, ameandaa Njia ambayo tungeweza kukusanyika kutoka ulimwenguni kote, kuisikiliza Sauti ya Mungu sote kwa wakati mmoja, ili kukamilishwa na Neno Lake. Kusubiri kusikia katika sekunde yoyote malaika-mjumbe wetu wa saba aseme;

“Tazama Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!”

Hakujawahi kuwa na kitu chochote kama Hicho tangu mwanzo wa wakati. Kule Kumalizika kwa Mpango mkuu wa Mungu kunatukia, SASA HIVI, na sisi tu sehemu Yake. Ile Siku kuu ya Bwana imekaribia.

Siri zote zimefunuliwa kwa Bibi-arusi na malaika-mjumbe wa Mungu. Ile Mihuri, zile Nyakati, Ngurumo, Imani ya Kunyakuliwa, Mvuto wa Tatu…KILA KITU kimekwishanenwa na kiko kwenye kanda ili Bibi-arusi aweze kuzisikia tena na tena, nayo INATUKAMILISHA.

Roho Mtakatifu amerudi Kanisani tena; Kristo, Mwenyewe, akifunuliwa katika mwili wakibinadamu, wakati wa jioni kama alivyoahidi.

Sikiliza kwa makini sasa ewe Bibi-arusi, likamate.

Tumeitwa na Neno; Kristo mwenyewe ametuita. Amejiweka mwenyewe dhahiri kwetu; Waebrania 13:8, Luka 17:30, Malaki 4, Waebrania 4:12, Maandiko haya yote aliyoahidi.

Ni Yesu, Mwana wa Mungu, ambaye amejifunua kwetu kwa Maandiko haya ambayo yaliyochaguliwa tangu zamani kwa ajili ya siku hii, YAISHI TENA.

Na, kuamini Hilo, ndio dhihirisho la Roho Mtakatifu.

Mungu alimtuma nabii Wake kumwita Bibi-arusi Wake atoke. Neno linatuambia nabii ni Neno lililo hai la Mungu, lililodhihirishwa. Ndio ishara ya mwisho ambayo ulimwengu utakayopata; Yehova akinena katika umbo la mwanadamu.

Mtu katika mwili wa kibinadamu, kama nabii, hata hivyo ilikuwa ni Elohimu akilitambua wazo lililokuwa katika moyo wa Sara, nyuma Yake. Naye Yesu alisema, “Kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, ndivyo itakavyokuwa katika ukamilifu wa dahari, wakati Mwana wa Adamu,” si Mwana wa Mungu, “wakati Mwana wa Adamu atakapokuwa akifunua.”

Bibi-arusi anajua isipokuwa uwe daima katika Neno, hutajua Yeye ni nani. Wao wanajua umuhimu wa kuiweka Sauti hiyo mbele zao kila siku kwa Kubonyeza Play.

Sasa Bibi-arusi hana budi kuondoka jukwaani, na kwenda juu, ili wale manabii wawili wa Mungu katika Ufunuo waweze kutokea jukwaani ili kupiga Baragumu ya Saba. Kuwajulisha Kristo.

Njoo uwe sehemu ya unabii uliotimia Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) wakati nabii wa Mungu anapoleta Ujumbe, Sikukuu ya Baragumu 64-0719M, na kuzungumza na Baba na kusema,

Yawezekana kuwe na baadhi huko nje katika mataifa, ulimwenguni kote, ambao hata kanda hii ingewakuta manyumbani mwao au makanisani mwao. Tungeomba, Bwana, kwamba wakati ibada inaendelea, pale—pale…au kanda inachezwa, au nafasi yo yote tunayoweza kuwamo, au—au hali, yule Mungu mkuu wa Mbinguni na aheshimu huu unyofu wa mioyo yetu asubuhi hii, na kuponya wahitaji.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Walawi 16 yote
Walawi 23:23-27
Isaya 18:1-3
Isaya 27:12-13
Ufunuo 10:1-7
Ufunuo 9:13-14
Ufunuo 17:8

24-0303 Kile Kipeo

UJUMBE: 64-0705 Kile Kipeo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Familia Iliyo Kipeo,

Jinsi gani Jumbe hizi za mwisho zimekuwa Kamilifu kabisa kwa Bibi-arusi wa Kristo. Mungu, akijifunua Mwenyewe mbele zetu, akijifunua Mwenyewe waziwazi. Ulimwengu hauwezi kuliona Hilo, lakini kwetu sisi, Bibi-arusi Wake, Hilo ndilo tuonalo.

Tumelipenya pazia na kumwona Yeye waziwazi kabisa. Mungu, nyuma ya ngozi ya mwanadamu. Neno limefanyika mwili, kama vile hasa Yeye alivyoahidi katika Luka 17 na Malaki 4. Amejificha Mwenyewe katika pazia la mwanadamu, katika nabii Wake na katika Kanisa Lake.

Sisi ndio watu wenye furaha kuliko wote ulimwenguni wakati tunapomsikia Mungu akinena kupitia malaika-mjumbe Wake na kutuambia,

Ninashukuru sana kwa ajili yenu. Nina furaha sana kushirikiana pamoja nanyi. Nina furaha sana kuwa mmoja wenu. Mungu awe nanyi.Atakuwa nanyi. Yeye hatawaacha kamwe. Hatawapungukia. Yeye hatawaacha. Tayari mmekwisha pita katika ile pazia.

Tumekuwa watu wa kipekee kwa kila mtu, hata katika nyadhifa zetu wenyewe, lakini tunajivunia, na kushukuru sana, kwa Ufunuo Ambao Yeye ametupa wa Neno Lake wa siku hii. Kuwa wapumbavu kwa ajili ya Kristo na Neno Lake lililodhihirishwa.

Tumeweka imani yetu pamoja na imani ya nabii Wake, nasi tumeungana pamoja, tukifanya UMOJA mkuu wa Mungu. Yeye Hawezi kitu bila sisi; sisi hatuwezi kufanya lolote bila nabii huyo; wala hatuwezi kufanya lolote bila Mungu. kwa hiyo sote pamoja, TUNAFANYA KITU KIMOJA, Ule Muungano; Mungu, nabii Wake, Bibi-arusi Wake. Tumekuwa Kipeo Chake.

Ilimchukua Yeye miaka elfu nne kutengeneza Kipeo Chake cha kwanza. Sasa, imemchukua Yeye miaka elfu mbili kutengeneza Kipeo Chake kingine, SISI, Bibi-arusi Wake, familia Yake kuu iliyo Kipeo, Adamu wa Pili na Hawa wa Pili. Sasa tuko tayari kwa ajili ya ile bustani, ule Utawala wa Miaka Elfu. Ametufinyanga tena na sasa tuko tayari.

Sisi ndiye Bibi-arusi Wake Neno Kamilifu, sehemu ya ule Uumbaji Wake ASILI. Ubua, kishada, na ganda, sasa vinakusanyika katika ile Mbegu, tayari kwa ufufuo, na tayari kwa mavuno. Alfa imekuwa Omega. Ile Mbegu iliyoingia ndani, imepitia hatua fulani na imekuwa Mbegu tena.

Ile mbegu iliyoanguka katika bustani ya Edeni kisha ikafa kule, ilirudi. kutoka kwa ile mbegu isiyo kamilifu iliyokufia kule, ikarudi ikawa Mbegu kamilifu, Adamu wa Pili.

Sisi sasa tumekuwa Adamu wa Pili, Bibi-arusi wa kweli, ile Mbegu, amerudi na Neno la asili tena. Na lazima tuwe na Neno lote kusudi tupate kuwa ile Mbegu. Hatupaswi kuwa na nusu ya Mbegu; hatuwezi kukua, lazima tuwe Mbegu nzima.

Kuna jambo moja tu lililosalia, mavuno yamefika. Tumeiva kabisa. Tuko tayari kwa kule Kuja. Ni wakati wa mavuno. Ile Mbegu imeirudia hali yake ya asili. Ile Familia ilio Kipeo imekuja tena, Kristo na Bibi-arusi Wake.

Ili kumtia moyo nabii Wake na Bibi-arusi Wake, Bwana alimpa malaika wake ono kuu. Alimpa kuonekana kimbele kwetu SISI, Bibi-arusi Wake. Tulipopita karibu naye, alisema, tulikuwa wanawake wadogo walio wazuri mno. Alisema sote tulikuwa tukimtazama, tulipokuwa tukipita.

Mwishoni, wengine walikuwa wametoka kwenye mstari, nao walikuwa wakijaribu wawezavyo kurudi mstarini. Kisha aliona kitu fulani muhimu sana, walikuwa wakiangalia mahali pengine, Hawakuwa wakimtazama Yeye. Walikuwa wakiliangalia hilo kanisa lililoingia katika machafuko. Jinsi gani ninavyojivunia na ninavyoshukuru kusema, sio SISI, Hao waliokuwa mbele, sisi hatukutoka nje ya hatua ama kuyaondoa macho yetu Kwake Yeye.

Kwa hiyo kile Kipeo na Mwana wa Mungu—Kipeo na Bibi-arusi, Naye ni sehemu Yake, ambayo ni lazima iwe kutimizwa kwa Neno. Neno limekwishatimizwa, nasi tuko tayari kwa kule Kuja kwa Bwana.

Tunayoshukrani jinsi gani kujua, sisi ndio ile Familia iliyo Vipeo Vyake, Bibi-arusi Wake wa kweli. Neno limekwishatimizwa, nasi tuko tayari kwa kule Kuja kwa Bwana.

Ninawaalika mje muungane nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) ili kusikia Neno pamoja nasi, na kuwa sehemu ya ile Familia iliyo Kipeo cha Mungu, tunapomsikia nabii akituletea Ujumbe: Kile Kipeo 64-0705.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Isaya 53:1-12
Malaki 3:6
Mathayo 24:24
Marko 9:7
Yohana Mtakatifu 12:24 / 14:19

24-0225 Wa Kipekee

UJUMBE: 64-0614E Wa Kipekee

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Marafiki Wapendwa,

Ni saa 6:00 SITA MCHANA huko Jeffersonville, saa 1:00 MOJA JIONI huko Afrika, saa 4:00 NNE ASUBUHI huko Arizona; Bibi-arusi wamekusanyika pamoja kutoka ulimwenguni kote. Tumesubiri wiki nzima kuufikia wakati huu. Tuko chini ya matarajio makubwa, tukimngojea Mungu aseme nasi kupitia midomo ya mwanadamu kwa njia ya malaika-mjumbe Wake wa saba mwenye nguvu. Tunaomba, “Bwana nitayarishe, unitie mafuta, na unipe Ufunuo zaidi wa Neno Lako.”

Tumeridhika, kwa maana tunajua hakika, ya kwamba nabii, na nabii peke yake, ndiye aliye na Maneno ya Uzima ya saa hii. Huenda tusiweze Kulieleza lote, lakini tunajua tunaamini kila Neno na tunalitegemea Hilo.

Tunajua, kama vile Bwana alivyofanya na Musa, Mungu Anajiandaa kumtukuza nabii wake mbele zetu. Wakati huo, Yeye aliitikisa tu milima. Wakati huu, Yeye Anazitikisa mbingu na nchi.

Ule wakati umefika. Mioyo yetu inaenda mbio ndani yetu. Tunausikia wimbo wetu wa Taifa umeanza kucheza. Kwa moyo mmoja, Bibi-arusi kutoka ulimwenguni kote wainuka kwa miguu yao na kuanza kuimba, AMINI TU , yote yawezekana, Amini Tu. Mungu anajiandaa kuzungumza nasi.

Tunasikia: “Habari za asubuhi marafiki.”

Mioyo yetu inafurahi kusikia tu maneno haya 3 rahisi. Nabii ametoka kuniita mimi rafiki yake. Kisha anatuambia,

Ninawakosa ninyi nyote. Si—sijali ninapokwenda, ni—ni…si, si ninyi. Nina marafiki, kila mahali ulimwenguni, bali si—si ninyi nyote. Kuna kitu fulani kuhusu kundi hili dogo ambalo lina ninino tu…Sijui. Mimi huwafikiria…Sina ku—kundi fulani ulimwenguni, nilijualo, linaloshikamana nami kama kundi hili. Mungu na—na ajalie tuwe wasioweza kutengana sana, hata, katika Ufalme ujao, naomba kwamba tuwe huko pamoja; ombi langu.

Ni Ufunuo mkuu jinsi gani ambao Mungu atatufunulia leo? Tunaenda kusikia kitu gani? Labda tumelisikia mara nyingi, nyingi sana hapo kabla, lakini leo itakuwa tofauti, ni kama vile haijawahi siku yoyote hapo kabla.

Ni kitu gani? Chakula cha Mwaminio. Mkate wa Wonyesho kutoka Mbinguni tutakaousheherekea. Mkate wa Wonyesho ulio kwa ajili yetu tu, Bibi-arusi Wake. Ni Utukufu wa Shekina juu ya Mkate huo wa Wonyesho unaotufanya tusiharibike.

Hao walio nje hututazama na kuuliza, “Ninyi watu mnafanya nini? Mnasikiliza tu kanda? Ninyi ni Wa Kipekee kweli kweli.”

Utukufu!! Tunayo furaha sana, na tunamshukuru sana Bwana sisi kuwa Wa Kipekee; wapumbavu kwa ajili Yake na Neno Lake lililothibitishwa. Tunafurahi kuuambia ulimwengu, “NDIYO, NINAAMINI HUDUMA YA KANDA. NINAAMINI KUBONYEZA PLAY. NINAAMINI NDIO SAUTI ILIYO MUHIMU SANA UNAYOPASWA KUISIKIA. NDIYO, NINAAMINI KUZIRUDISHA KANDA MIBARANI.”

Wakati utaji wa mapokeo umeondolewa, unaweza kuona ya kwamba Mungu angali ni Mungu wa Neno Lake. Yeye angali anadumisha Neno Lake. Yeye ni ninii—Yeye ndiye Mungu, Mwandishi wa Neno Lake.

Haijalishi yale mtu yeyote afanyayo, ama asemayo, tunaliamini Hilo, na kisha tunalitendea Hilo kazi. Kama wewe hulifanyi Hilo, basi huliamini. Hauko nyuma ya pazia. Pazia hilo ni la mtu mmoja. Ujumbe huo ni mmoja.

Nami ninatumaini na kuamini ya kwamba—ya kwamba mmekuwa na ufahamu wa kiroho juu ya yale Mungu amekuwa akijaribu kuliambia Kanisa bila ya kulisema moja kwa moja. Unaona? Ni jambo, wakati mwingine, inatubidi kusema mambo kwa njia fulani kwamba iweze kupunguza, iweze kuwafanya wengine kutoka nje, wengine kuondoka, na wengine ku—ku—kutafakari. Lakini hilo linafanywa makusudi. Lazima lifanywe hivyo.

Neno lilifunuliwa kwa nabii wa Mungu. Hakuna cha kundi, Mafarisayo, ama Masadukayo, ama dhehebu fulani ama ukoo. Ni NABII! Mungu alimpata mtu mmoja. Hakupata mawazo mawili au matatu tofauti. Yeye alimchukua mtu mmoja. Ndiye aliye na Neno, na yeye peke yake.

Ndipo huenda ikawa kwamba wengine wangesema, “Unamaanisha Mungu angefanya jambo kama hilo makusudi?” Hakika alifanya. Angali anafanya.

Kama vile walivyosema mamia ya miaka iliyopita, tunasikia jambo lile lile leo hii: “Lakini kuna watu wengine hapa ambao Mungu amewaita.” Hiyo ni kweli. Na maadamu tu wanafuata na kwenda pamoja, ni Amina, bali wakati mtu anapojaribu kupiga hatua na kuchukua nafasi ya Mungu ambayo Mungu aliyompa nabii wetu, ambayo Yeye alichaguliwa tangu zamani na kuwekwa kwa ajili ya kazi hiyo, inatubidi kukaa na Neno lililothibitishwa, ile Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku yetu.

Angalia, kifo, kukaa mbali Nalo sasa. Huna budi kuingia ndani Yake kupitia kwenye pazia hili, la sivyo hutaingia. Jinsi ambavyo Mungu angeweza kuwarehemu, bali kumbukeni vile ilivyokuwa, ya kwamba Mungu anadhihirisha kile kilichokuwa nyuma ya lile pazia. Angalieni kile kilichokuwa nyuma ya pazia, hilo Neno! Lilifunika nini? Neno! Ilikuwa ni kitu gani? Liko kwenye sanduku. Lilikuwa ni lile Neno ambalo lile pazia lililificha. Mnaona? Naye Yesu alikuwa ndiye Neno hilo, Naye Ndiye hilo Neno, nalo pazia la mwili Wake lililificha.

Kwetu sisi, ni udhihirisho! Sio neno tena, ni uhalisia! Amina!

Tunajua kwa wengine sisi ni Wa Kipekee, na linaweza likasikika kama nati kwa ulimwengu, lakini linawavuta watu wote Kwake.

Njoo uingizwe kwenye Neno pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) tunapomsikia nabii akiuambia ulimwengu jinsi sisi tulivyo Wa Kipekee 64-0614E. Tunajivunia na tunashukuru sana kusema ndivyo sisi tulivyo.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

I Wakorintho 1:18-25
2 Wakorintho 12:11

24-0218 Kufunuliwa Kwa Mungu

UJUMBE: 64-0614M Kufunuliwa Kwa Mungu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliye Nyuma ya Pazia,

Kwa nini ninaendelea kuwaambia tena na tena, “KUBONYEZA PLAY ndilo jambo lililo muhimu zaidi mnalopaswa kufanya”? Kwa nini ninaendelea kuwaambia wachungaji, “Mrudisheni Ndugu Branham kwenye mimbara zenu”?

Ni rahisi tu namna hii. Kule kuisikiliza Sauti ya malaika-mjumbe wa saba kwenye kanda, ni kusikiliza NENO LILILO HAI.

Mbele za watu, Mungu alijitia utaji tena na kumthibitisha Musa, kwa utaji, kwa kujitia utaji kwa Moto ule ule, Nguzo ile ile ya Moto ilishuka. Tangu—tangu wakati huo…Kutoka kwao, kwa hiyo wangeweza tu kusikia Neno la Mungu. Mnalipata? Neno pekee, waliisikia Sauti Yake. Kwa kuwa, Musa alikuwa, kwao, Neno lililo hai.

Nena kuhusu Mhudumu aliye Hai! Sauti tunayoisikiliza kwenye kanda ndio Sauti ya Neno lililo Hai la siku yetu. Hakuna nyingine iliyo kuu kuliko Hiyo.

Katika siku za Musa, ni wana wa Israeli tu waliokuwa kambini ndio wangeweza kuisikia Sauti Yake. Lakini leo, Mungu alitaka ULIMWENGU uisikie Sauti Yake, KWA HIYO AKAIREKODI KWENYE KANDA, ili Bibi-arusi Wake aweze kuisikia Sauti ya Neno lililo Hai.

Mungu alikuwa amejificha nyuma ya pazia la nabii Wake, apate kuwaambia Neno Lake. Hilo ndilo alilokuwa amefanya. Musa alikuwa ndiye hilo Neno lililo hai kwa watu, lililotiwa utaji kwa Nguzo ya Moto.

Kama huna Ufunuo wa jambo hilo kwa ajili ya siku yetu, huwezi kuwa Bibi-arusi wa Yesu Kristo. Kama unao, basi wewe NI Bibi-arusi wa Yesu Kristo na itakubidi kusema, “hakuna jambo lililo muhimu zaidi kuliko kuzisikiliza kanda, kwa maana ni Sauti ya Mungu ikinena nawe mdomo kwa sikio.”

Wengi wanajaribu kuwatisha watu na kusema tunamsifu sana nabii; tunamuabudu. Enyi marafiki, Yeye ndiye aliyesema mambo haya, si mimi. Mimi nina nukuu tu Neno.

Kama ilivyofanyika katika kila wakati, Uungu ukitiwa utaji katika mwili wa binadamu. Angalieni, Yeye alifanya hivyo. Manabii walikuwa ni Uungu, umetiwa utaji. Walikuwa ni Neno la Mungu (hiyo ni kweli?) lililotiwa utaji katika mwili wa binadamu. Kwa hiyo wala hawakumwona Musa wetu, mnaona, Yesu.

Hatumwabudu mwanadamu, bali Mungu, Ambaye ametiwa utaji na anayejifunua Mwenyewe kupitia nabii. Ili kuelewa na kuamini hilo, yakubidi ufanye hivi.

Hamko nyuma ya pazia hilo tena, enyi Watoto wadogo. Mungu anaonekana wazi kabisa kwenu.

Hatuko nyuma ya pazia hilo tena, tunaweza kuona Ni Mungu anayejifunua Mwenyewe waziwazi. Imefunuliwa ya kwamba kusikiliza Sauti hiyo kwenye kanda ni Mungu akizungumza na Bibi-arusi Wake. Tunaamini ndiyo Njia Yake iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii.

Tunaweza tu kusema AMINA kwa Sauti hiyo, si kingine. Sauti hiyo itahubiri, itafundisha na kutufunulia kila kitu tunachohitaji kujua. Sauti hiyo itatutambulisha sisi kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Sauti hiyo ndiyo yote tunayotaka na tunayohitaji.

Tunashukuru kwa huduma 5 ambayo Mungu anayoitumia kuwaelekeza watu kwenye Sauti hiyo; kwa ajili ya wachungaji ambao wamelipata lile ono na walio na ufunuo kwamba kuzicheza kanda katika makanisa yao ndilo jambo kubwa sana wanaloweza kufanya kwa ajili ya watu wao.

Tunawaalika mje msikilize pamoja nasi ile Sauti yenye nguvu ya Neno lililo Hai Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) tunapoisikia ikifunua:  Kufunuliwa Kwa Mungu 64-0614M.

Ndugu. Joseph Branham

24-0211 Tazama Aliko Yesu

UJUMBE: 63-1229E Tazama Aliko Yesu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Mbegu Iliyorutubishwa,

Je! mwaweza kuwazia jinsi gani ingekuwa ni jambo la kupendeza kuketi na kumsikia malaika-mjumbe wa saba wa Mungu akiwaambia jinsi ambavyo hakujiepusha na kuwahubiria habari ya Kusudi lote la Mungu? Akiingia kwa undani sana kuhusu Mvuto wa Tatu, na kuwahakikishia jinsi ambavyo sasa ulivyothibitishwa?

Jinsi Mungu alivyonena na kindi wakatokea; kama vile tu alivyomnena kondoo dume kwa ajili ya Ibrahimu. Jinsi ambavyo Sauti ile ile ilivyomwambia amweleze maskini dada mnyenyekevu aitwaye Hattie, ambaye aliyesema neno sahihi, na kumwambia ya kwamba Sauti ile ile ambayo ilinena kuhusu wale kindi wakawepo ilisema ampe kile alichotaka na aone kama hakitatokea mara moja.

Jinsi ambavyo siku moja wakati alipokuwa akiwinda nyikani pamoja na rafiki zake, dhoruba kali ilitokea ambayo ingemlazimu kuondoka. Lakini jinsi Mungu alivyozungumza naye, mdomo kwa sikio, na kusema, “Niliumba mbingu na nchi. Nilituliza zile pepo zenye nguvu juu ya bahari.”

Jinsi alivyoruka juu na kuvua kofia yake wakati ile Sauti ilipomwambia, “Iambie tu dhoruba, nayo itakoma. Lo lote utakalosema, hivyo ndivyo itakavyokuwa.”

Yeye kamwe hakuihoji hiyo Sauti, bali alinena na kusema, “Dhoruba, koma. Nawe, jua, waka kama kawaida kwa siku nne, hadi tutakapokuwa tumetoka hapa.”

Kabla hajamaliza kusema hayo, ile mvua ya theluji, theluji na kila kitu kilisimama. Jinsi ambavyo katika dakika moja jua kali lilikuwa linawaka mgongoni mwake. pepo zilibadilika na mawingu, kama kitu cha siri, yakiinuka juu angani, na jua lilikuwa linawaka katika dakika chache.

Kisha angewaambia ambavyo miaka 16 kabla hata haujadhihirika, Mungu alimwonyesha kulikuwa na uvimbe kwenye kifuko cha kushoto cha mayai cha Dada Branham, na kwa nini huo ulikuwepo pale. Jinsi walivyoomba na kuomba Mungu auondoe. Ndipo, akatambua kuwa ni Mungu tu anayeijaribu imani yao.

Ndipo tu kabla haujaondolewa kwa upasuaji, alikuwa akizungumza na Mungu na Kumwambia jinsi gani amekuwa mke mzuri sana kwake. Jinsi ambavyo hakuwahi kulalamika kuhusu yeye kutokuwepo nyumbani. Jinsi ambavyo daima alivyotayarisha kila kitu kwa ajili yake wakati alipotaka kwenda kuwinda, kupumzika na kuzungumza na Bwana.

Kisha akasikia kitu fulani chumbani. Alipoinua macho, ile Sauti ikasema, “Simama,” na kumwambia, “Basi lolote utakalosema, hivyo ndivyo itakavyokuwa.”

Alisubiri kwa dakika moja tu, kisha akasema, “Kabla mkono wa daktari haujamgusa, Mkono wa Mungu utaondoa ule uvimbe, na hata hautaonekana.”

Sekunde moja kabla ya mkono wa daktari haujaweza kumgusa, aliponywa. Jinsi daktari alivyomwambia, “Ninataka kukuhakikishia, Bibi Branham, ya kwamba huo uvimbe haupo. Huna uvimbe wowote.”

Jinsi lilivyo Kamilifu Neno la Bwana!

Kumsikia Yeye akiwaambia hakuna shaka tena niani mwake, anajua ule Mvuto wa Tatu ni nini, na anajua unayotenda. Kwa maoni yake, utakuwa kile kitu ambacho kitaanzisha ile imani ya Kunyakuliwa, kwa ajili ya kuondoka.

Kwetu sisi ni kuwa na kicho, na kukaa kimya tu, kwa kuwa ile saa itawadia hivi karibuni ambapo Mungu atatutendea mambo fulani makuu. wakati huo ujapo, wakati kule kufinywa kutakaposhuka, ndipo mtaona, yale mmeona kwa kitambo, yakidhihirishwa katika ule utimilifu wa nguvu zake.

Tutakuwa na baraka hiyo kuu Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA., saa za Jeffersonville. ( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) Ningependa kuwaalika kuungana pamoja nasi tunaposikia: Tazama Aliko Yesu 63-1229E.

Hatutakusanyika pamoja ili kumsikiliza mwanadamu; kuna watu wengi sana barabarani, na wote wanafanana. Hatutakuwa tunatazama na kusikia mhudumu tu, ama mchungaji, tutakuwa tukimtazama na kumsikiliza Yesu. Tutaungana pamoja kutoka ulimwenguni kote kumsikia Yule Mtu, Yule Mtu wa Mungu, Yule Yesu wa Nazareti wa mwili, akiwa Mungu, akinena na Bibi-arusi Wake.

Yakubidi ujiulize mwenyewe, unatazama nini leo? Unaona nini unapotazama? Unaweza tu kumwona Yeye unapomtazama Yeye kupitia kwenye Neno.

Alichokuwa wakati alipotembea Galilaya, ni jambo lile lile alilo huku Jeffersonville, jambo lili alilo kwenye Maskani ya Branham. Unaangalia uone nini, mwanzilishi, mtu wa kimadhehebu? Hutaona jambo hilo katika Yesu. Unatazama umwone mtu mkuu wa kikasisi? Hutaona jambo hilo katika Yesu. La. Unamwonaje Yesu? Kwenye Neno la Mungu likidhihirishwa, kwa maana Yeye alikuwa Neno la Mungu lililodhihirishwa. Alivyokuwa wakati huo, ndivyo alivyo usiku wa leo, na atakuwa hivyo milele.

Mtazame Yesu hivi sasa upate kuishi;
Kwa maana imeandikwa katika Neno Lake, haleluya!
Ni kwamba tu “tunatazama na kuishi.”

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma ili kujitayarisha kusikiliza Ujumbe:

Hesabu 21:5-19
Isaya 45:22
Zekaria 12:10
Yohana 14:12

24-0204 Yupo Mtu Hapa Anayeweza Kuiwasha Taa

UJUMBE: 63-1229M Yupo Mtu Hapa Anayeweza Kuiwasha Taa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Sura ya Yesu Kristo,

Watu wanafikiri sisi ni wendawazimu, tunavyoketi katika nyumba zetu na makanisa, kuzisikiliza kanda. Wanafikiri tunakufa kwa njaa. Hawatambui kuwa tumeketi katika uwepo wa Nuru ya Mwana ya Agosti , tukiivishwa, na kulishwa Chakula Kilichohifadhiwa kama ndama zizini.

Sisi ndio ile Ngano iliyoendelea zaidi, tuko tayari kulipokea. Ikiwa wanataka kuishi katika mapokeo yao, na waendelee. Sio SISI, sisi tunaishi katika Nuru ya siku yetu.

Nuru ya siku yetu ni nini? Mungu alimtuma ulimwenguni malaika wake wa saba mwenye nguvu kumwongoza Bibi-arusi wake. Yeye alikuwa nani? Alikuwa nabii. Yale aliyosema yalitimia. Yeye alikuwa Neno la Mungu lililodhihirishwa. Yeye alikuwa dhihirisho la Nuru ya Neno la Mungu. Yeye alikuwa Nuru ya Mungu kwa ajili ya siku hii.

Musa aliendelea tu hata hivyo, kwa sababu alikuwa ile Nuru. Alikuwa Nuru ya saa ile. Kile alichokuwa nacho, kilikuwa nini? Mungu akidhihirisha Neno Lake lililoahidiwa kupitia kwa Musa, na Musa alikuwa Nuru.

Eliya alikuwa Nuru…Alikuwa nini? Ile Nuru. Haleluya! Alikuwa Nuru, ile Nuru; alikuwa Neno la Mungu lililodhihirishwa.

Yohana, alipokuja duniani… Basi alipojitokeza Yesu alisema alikuwa Taa angavu inayong’ara. Haleluya! Kwa nini? Alikuwa Neno lililodhihirishwa.

Basi kulingana na Neno, Nuru ya siku yetu ni nabii wa Mungu, William Marrion Branham. Yeye yule aliaye katika nyika ya Babeli “Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake.”

Yeye alikuwa kutimizwa kwa Malaki 4:5, na Ufunuo 10:7. Yeye alinena tu na kusema, “itakuwa pale,” nayo ilikuwa pale, bila kitu chochote ndani yake. Hakuwa kamwe amempata kindi; hapakuwa na yeyote hapo. Yeye alisema tu, “Na iwe,” na ikawa.

Neno la Mungu halikosei, nalo halina budi kutimia. Tumeiona Nuru; Neno Lake aliloahidi kwa ajili ya siku hii. Limethibitishwa na kuhakikishwa ya kwamba ni Kweli. Ni Nuru ya saa hii.

Hakuna kibadala katika kujua kile tunachosikiliza ni Neno lililodhihirishwa kwa ajili ya siku hii. HALINA WAFURUKUTA MIKIA NDANI YAKE… HATA CHEMBE. Ikiwa wengine watosheka na kitu kingine, na waendelee, lakini sio sisi.

Haimaanishi kuwa huwezi kumsikiliza mchungaji wako, ama kwamba mhudumu hawezi kuhubiri; sivyo hata kidogo, lakini LAZIMA uchuje kila neno unalosikia kupitia chujio kuu la Mungu, UJUMBE HUU KWENYE Kanda.

Wanaposema siku za Ujumbe wa mtu mmoja zimepita, hao ni WAFURUKUTA MKIA. Wanaposema Ujumbe huu sio Yakini yao, hao ni WAFURUKUTA MKIA. Wanaposema kusikiliza kanda haitoshi, hao ni WAFURUKUTA MKIA.

Hakuna kitu kikubwa zaidi ya Kubonyeza Play tu, kujua unaweza kusema AMINA kwa kila neno. Hakuna mahali pengine unapoweza kufanya hivyo isipokuwa kusikiliza Ujumbe wa saa hii.

Sasa sisi ni sura ya Yesu Kristo kwa ajili ya siku hii. Sisi ni Neno Lake lililodhihirishwa. Sisi ndio wale aliowachagua kupokea Ufunuo Wake mkuu wa wakati wa mwisho. Sisi ndio BIBI-ARUSI WAKE.

Ni Bibi-arusi Wake peke yake ndiye atakayekuwa na Ufunuo wa kweli wa Nuru ya siku hii. Watajua, Nuru hii itawakamilisha. Nuru hii ni Roho Mtakatifu akinena kupitia malaika-mjumbe Wake.

Je! ungependa kuketi katika uwepo wa Nuru ya Mungu ya saa hii? Basi ninakualika uje uungane nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA saa za Jeffersonville,( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) tunaposikia  Yupo Mtu Hapa Anayeweza Kuiwasha Taa 63-1229M.

Ndugu. Joseph Branham.

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Mwanzo 1:3, Sura ya 2
Zaburi 22
Yoeli 2:28
Isaya 7:14, 9:6, 28:10, 42:1-7
Mathayo 4:12-17, Sura ya 24 na ya 28
Marko Sura ya 16
Ufunuo Sura ya 3

24-0128 Aina Tatu Za Waamini

UJUMBE: 63-1124E Aina Tatu Za Waamini

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Mwamini,

Jinsi inavyopendeza kusema, MIMI NI MWAMINI. Si wa kanuni za imani; Neno! Si wa madhehebu; Neno! Si wa kile anachosema mtu mwingine; bali kile lisemacho Neno!

Sisi hatuulizi kitu, tunaliamini tu. Haidhuru Linasikika namna gani ama lolote mtu ye yote asemalo juu yake, sisi ni waamini halisi. Tuna ufunuo wa kiroho wa Neno.

Tunaiona ile saa tunayoishi. Tunauona ule Ujumbe wa saa hii. Tunamwona yule mjumbe wa saa hii. Tunamwona Mungu akijifunua Mwenyewe katika Neno Lake. Tunaona hakuna kitu kingine ila Ujumbe Huu, Mjumbe Huyu, Neno Hili.

Mwamini halisi hasikii kitu ila Neno. Hakuna zaidi. Yeye huliangalia Neno. Hatafuti mianya. Yeye hatafuti viinimacho. Anamwamini Mungu, na hilo latosha, naye anaendelea tu. Mnaona? Huyo hapo mwamini.

Sisi hatuwezi kusikia kitu kingine ila Neno; Neno linalomjia nabii peke yake. Si mianya, si fasiri ya mtu fulani, Neno Safi lililonenwa na kuwekwa kwenye kanda kwa ajili ya Bibi-arusi.

Roho amelihuisha Neno hilo ndani yetu nalo limekuwa hai. Kwa imani, tunaliona na kuliamini. Itakuja sauti kutoka Mbinguni ambayo italeta ubatizo mkubwa sana wa Roho Mtakatifu katika Bibi-arusi, ambao utatuondoa duniani, katika Neema ya Kunyakuliwa. Mungu aliahidi jambo hilo.

Tunawekwa majaribuni kila wakati, kila siku. Shetani anajaribu kutuambia majaribu na mitihani yetu ni Mungu anatuadhibu. Lakini MUNGU ASIFIWE, sivyo ilivyo, ni Shetani anayefanya jambo hilo naye Mungu analiruhusu.

Mungu anatujaribu, na kutufinyanga ili aone kile tutakachofanya. Jaribio huja kututikisa, kutuweka kule chini kabisa, kuona mahali tutakaposimama. Lakini tunashinda kila vita, kwa kuwa sisi ni mifano iliyo hai; Neno la Mungu linaishi ndani yetu na kupitia kwetu.

Sisi tuna umuhimu jinsi gani machoni pake?

Hakuna mtu anayeweza kupachukua mahali pako, haidhuru ni padogo namna gani. Unasema, “Mimi ni mke wa nyumbani tu.” Hakuna mtu anayeweza kupachukua mahali pako. Mungu, katika uchumi Wake mkuu, ameweka jambo hilo hivyo, Mwili wa Kristo, katika utaratibu, hata hapana mtu anayeweza kupachukua mahali pako.

Hilo ni lakupendeza jinsi gani? Kila mmoja wetu ana mahali. Kila mmoja wetu alikuwa hapa wakati Mungu aliponena ulimwengu ukawa. Aliweka mwili wetu hapa wakati huo huo. Mungu alituweka sisi duniani katika wakati huu ili kulitimiza Neno lake na kutupa Uzima wa Milele.

Kila mmoja anapaswa kufanya uamuzi. Unasimama wapi kuhusu Neno hili, Ujumbe huu, mjumbe huyu? Ni muhimu jinsi gani kulisikia Neno linalonenwa kwenye kanda?

Kwenye sehemu mbalimbali ulimwenguni, kanda hizi zinakopita, huduma za kanda.

Ni huduma ya kanda iliyotumwa kwa Bibi-arusi Wake ulimwenguni kote kutoka kwa Mungu. Inakuambia mahali ulipo hasa, wewe ni nani, na iwapo wewe ni mwamini katika Neno.

Wewe umo katika moja ya tabaka hizi. Katika hali yako ya sasa hivi, hali yako ya sasa ya akili, kwamba, ninyi mlio hapa katika mkutano huu unaoonekana, nanyi mtakaokuwa katika mikutano isiyoonekana ya kanda hii, hali yako ya sasa ya akili baada ya kuisikiliza kanda hii, inakuthibitishia uko katika tabaka gani.

Baada ya wewe kusikiliza kanda hii, inathibitisha uko katika tabaka la watu gani. Baadhi wanaamini unahitaji zaidi ya Neno safi tu lililonenwa kwenye kanda. Wengine wanaamini kwamba siku za Ujumbe wa mtu mmoja zimepita; ni lazima umsikilize mchungaji wako vinginevyo umepotea.

Mgawanyiko mkuu sana katika Ujumbe siku hizi ni umuhimu uliowekwa katika kuzisikiliza kanda. Baadhi wanafundisha kuwa ni makosa kuzicheza kanda kanisani; ni mchungaji pekee yake ndiye anayepaswa kuhudumu. Wengine wanasema kuna ulingalifu, lakini kamwe hawazichezi kanda kanisani, na kama wakizicheza ni mara chache sana.

Kulivyo na mitazamo mingi, mawazo mengi, fasiri nyingi za Neno, ni nani aliye sahihi? Ni yupi utakaye mwamini? Hilo ndilo swali ambalo kila mmoja wetu anapaswa kujiuliza.

Nabii alituambia tulichunguze kwa NENO, sio yale mtu yeyote asemayo. unalifanyaje jambo hilo? KUNA NJIA MOJA TU PEKEE ya kufanya jambo hilo, BONYEZA PLAY.

Lazima kuwe na jibu sahihi, njia sahihi. Kila mtu lazima aamue mwenyewe. Jumapili hii itaamua wakati ujao wa wote wanaosikia Ujumbe huu.

Jambo unalopaswa wewe mwenyewe kujiuliza: Ni nani pekee aliye na Bwana Asema Hivi? Nguzo ya Moto ilimthibitisha nani? Ni nani atakaye tutambulisha kwa Yesu? Ni nani aliyenena Neno la kutokukosea? Ni maneno ya nani yaliyonenwa duniani yalikuwa muhimu sana, yakarudisha mwangwi mbinguni?

Iwapo ungependa kupata majibu sahihi, ningependa kukualika uje kusikiliza Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) kusikiliza Ujumbe:   63-1124E —Aina Tatu za Waamini.

Ndugu. Joseph Branham

Yohana Mtakatifu 6:60-71

24-0121 Nimtendeje Yesu Aitwaye Kristo?

UJUMBE: 63-1124M Nimtendeje Yesu Aitwaye Kristo?

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wapenda Kanda,

Tunaupenda Ujumbe huu kwa moyo wetu wote. Ni utamu wa miwa ya Mungu. Ni Neno la Mungu ambalo limethibitishwa kinaganaga, na kuhakikishwa, tena na tena. Ujumbe huu ni jibu la Neno la Mungu. Ni Kristo yeye yule aliyetiwa mafuta, lile Neno lililotiwa mafuta la siku yetu.

Tuna Neno la Mungu lililothibitishwa hapa, likithibitisha, kuhakikishwa na Roho, ya kwamba Yeye ametupokea na kutupa Ubatizo wa Roho Mtakatifu. Tumebatizwa katika Jina la Yesu Kristo. Injili ile ile, ishara zile zile, maajabu yale yale, huduma ile ile, hata Nguzo ya Moto ile ile ikionekana mbele zetu, ikionyesha ishara na maajabu. Hakuna udhuru, mahali po pote.

Ni wakati wa kuungana kwa Mungu na Bibi-arusi Wake. Bibi-arusi wa Kristo amekwishaitwa. Tumetiwa muhuri katika Ufalme wa Mungu. Mitambo iko hapa tunangojea tu Nguvu za Utendaji zitakazotuondoa kwenye dunia hii kuingia Utukufuni, katika Kunyakuliwa.

Hizo Nguvu za utendaji ni kujazwa tena kwa Roho Mtakatifu. Jiwe la Kufunika litashuka na kuungana na ule Mwili. Ndipo, wakati Kichwa hicho na Mwili huo vinapoungana pamoja, zile nguvu kamili za Roho Mtakatifu zitatuinua SISI juu na waliokufa katika Kristo watafufuka katika uzuri wa utakatifu Wake, na kuruka kwenda hewani.

Saa hiyo inawadia haraka sana. Wakati umefika mwisho. Maamuzi ya mwisho hayana budi kufanywa. Utafanya nini na Neno lililotiwa mafuta la siku hii? Msimamo wako ni upi juu ya Ujumbe wa saa hii?

Je, hivi utasema tu: “Ninaamini Ujumbe. Ninaamini Mungu alimtuma nabii.”

Usifikie tu umbali huu, ukasema, “Naamini Ujumbe.” Tii mjumbe.

Iwapo huna budi KUMTII mjumbe: ANGALIA, alisema tii mjumbe. Basi ni muhimu jinsi gani kuamini na kusikia kila Neno ambalo mjumbe huyo alilosema?

Unasema, “ Vema, Naamini kila neno lililosemwa, Ndugu Branham.” Hilo ni sawa, bali hiyo ni—hiyo ni uwezo tu wa kusoma.

Kwa nini watu wasiridhike na kanda? Kila mtu hawezi kuwa nabii. Kuna nabii mmoja tu, na Neno huja kwa nabii huyo.

Kanisa lilifanya vizuri mpaka walipoanza kulihoji hilo; ama walitaka sauti zingine kuwaambia, na kuwafasiria, yale ambayo nabii huyo aliyosema. Walitaka Kora na Dathani wa sasa.

Mnaona, ilianza na upotoshaji mdogo tu wa Neno, na, jambo lile lile, inaishia vile vile.

Kama ilianza hivyo, na itaishia hivyo, upotoshaji mdogo tu wa Neno, hakika mnatambua jinsi gani MNAVYOPASWA kukaa na kanda. Hakika mnaona kwa nini Mungu alihakikisha kuwa Ujumbe huu umerekodiwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya Bibi-arusi.

Sisemi mambo haya kuwashusha wachungaji wenu, au kusema msimsikilize mchungaji wenu, HAPANA, bali kuwaonyesha umuhimu wa kubonyeza play na kuusikia Ujumbe huu kwenye kanda.

Jinsi Kanisa linapaswa kuwa linahakikisha tena, na tena, na tena, na tena! Tunakungojea Kuja Kwake. Tunaamka, tunakungojea kule kuondoka. Inatubidi kulichunguza kwa Neno, si kile mtu fulani alichosema. Hakikisha unajua, wewe mwenyewe, kama tukio la kibinafsi pamoja na Kristo. Lichunguze tena, na tena, na tena.

AMESEMAJE? Inatubidi kulichunguza kwa Neno tena, na tena, na tena. Unalichunguzaje kwa Neno? Neno la siku hii ni lipi? Ni lile lile kama lilivyokuwa tangu mwanzo, Biblia.

Mungu anasema ni nani aliye mfasiri wa Neno Lake? ni Mimi? Ni Mchungaji wako? HAPANA, nabii wa Mungu aliyethibitishwa wa wakati huu ndiye mfasiri pekee wa Neno. Kwa hiyo, ni lazima ulichunguze kwa KANDA kila Neno analosema mtu yeyote tena, na tena, na tena!

Ikiwa tamshi hilo ni la kweli, na unaamini kwamba jambo lililo muhimu zaidi ambalo mtu yeyote, au mchungaji yeyote analoweza kufanya, ni KUBONYEZA PLAY, Basi kwa nini hilo ni gumu sana kwa yeyote anayedai kuamini Ujumbe kusema hivyo? Kwa sababu tu hawaliamini.

Uamuzi WAKO wa mwisho ni upi? Kwangu mimi na nyumba yangu, tutabaki na Ujumbe huu na mjumbe wa Mungu, Kanda hizi. Tunaamini hakuna kitu muhimu zaidi kuliko kusikiliza Sauti ya Mungu kwenye kanda.

  • Kuna Sauti MOJA tu ya Bwana Asema Hivi.
  • Kuna Sauti MOJA tu ambayo Nguzo ya Moto iliithibitisha.
  • Kuna malaika-mjumbe wa saba MMOJA tu.
  • Kuna Sauti MOJA tu ambayo Bibi-arusi wote wanayoweza kukubaliana kwake.
  • Kuna Sauti ya Mungu MOJA tu kwa ajili ya kizazi hiki.

Kama unao Ufunuo huo huo, njoo uungane nami na kundi dogo la waaminio ulimwenguni kote wanaoamini jinsi hiyo hiyo, Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) tunaposikia na kufanya uamuzi wetu wa mwisho: Nimtendeje Yesu Aitwaye Kristo? 63-1124M.

Ndugu. Joseph Branham

24-0114 Yeye Aliye Ndani Yenu

UJUMBE: 63-1110E Yeye Aliye Ndani Yenu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Waamini wenye Imani Kamilifu,

Kila siku mioyo yetu inaenda mbio kwa matarajio makubwa. Tunangojea ile saa ifike ya kule Kuja Kwake hivi karibuni. Hofu zote zimetoweka. Hakuna kujiuliza-uliza tena, “Je! sisi ni Bibi-arusi Wake”? Imetiwa nanga ndani ya mioyo yetu zaidi ya hapo nyuma, SISI NI BIBI-ARUSI WAKE.

Tumeshikwa katika hali ya Kimbinguni, tukisikiliza huduma ya Yesu Kristo, aliyefanyika mwili upya katika Kanisa Lake. Ujumbe huu umethibitishwa kotekote na Neno la Mungu, hivi kwamba hawezi kuwa ni mwanadamu, haina budi kuwa ni Mungu akinena mdomo kwa sikio na Bibi-arusi Wake.

Sisi tunaamini si mwanadamu anayenena nasi kwenye kanda hizi, ni Mungu.

Ninachojaribu kusema, “Usife moyo.” Usimruhusu Shetani akuambie ubaya kunihusu mimi; sababu ana mengi. Bali wewe shikilia matumaini hayo; sababu, usipoyashikilia, haitatendeka. Usiniangalie mimi, kama mwanadamu; mimi ni mwanadamu, nimejaa makosa. Bali tazama yale ambayo ninayosema kumhusu Yeye. Ni Yeye. Yeye Ndiye.

Yakubidi kuamini na kuwa na matumaini katika yale ANAYOSEMA, LA SIVYO HAITATENDEKA. Hatumwangalii nabii wa Mungu kama mwanadamu, kama wengi wanavyofikiri tunafanya hivyo. Tuko nyuma ya pazia la mwili wa mwanadamu, na yote tunayoyaona na kusikia ni Mungu akinena kupitia midomo ya mwanadamu, NA TUNAYO MATUMAINI NA KUAMINI KILA NENO.

Huo ndio Ufunuo wa Yesu Kristo kwa ajili ya siku hii. Kuamini kuwa ni Mungu, si mwanadamu, anayenena kwenye kanda. Ukilikosa jambo hilo, rafiki, umeukosa Ujumbe wa wakati huu na huwezi kuwa Bibi-arusi.

Shetani anaweka fasiri yake kwenye jambo hilo, na asilimia 99% ya wakati ananukuu Ujumbe kama tu vile alivyomfanyia Hawa, bali Hawa aliamriwa kukaa na Neno; yale Adamu aliyomwambia ndio Mungu aliyosema, si yale ambayo mtu mwingine aliyosema ati yalimaanisha. Hawa alipaswa kukaa na Sauti ya Mungu.

Hii ndio siku iliyo kuu ambayo ulimwengu umewahi kujua. Maisha ya Yesu Kristo, yale aliyoishi na kujifunua Mwenyewe katika maisha ya nabii Wake, sasa yanaishi katika mwili ndani YETU, Bibi-arusi Wake.

Tunafanya vile hasa Yeye alivyotuamuru kufanya: kukaa na Neno kwa kukaa na Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. Ndio huduma ya kanda ya Mungu na mpango wa Mungu wa siku hii.

Ikiwa kweli unaamini William Marrion Branham alikuwa ndiye malaika-mjumbe wa saba aliyechaguliwa na Mungu, yule ambaye Mungu alimchagua kunena na kufunua siri zote zilizofichwa katika Neno, aliye Sauti ya Mungu kwa kizazi hiki, mtu aliyekuwa na imani kuliko mtu mwingine yeyote yule, yule ambaye malaika wa Bwana alimwambia “ikiwa utawafanya watu WAKUAMINI, hakuna kitu kitakachosimama mbele ya maombi yako”, basi Jumapili hii itakuwa siku kuu kuliko.

HAKUNA KITU ambacho kinachoweza kamwe kuuondoa Ufunuo wa Ujumbe Huu kwetu sisi, HAKUNA. Hatuwezi KAMWE kuutilia shaka. Kama Yeye aliusema, sisi tunauamini. Huenda tusiuelewe Wote, lakini tunauamini hata hivyo.

Yesu mwenyewe alituambia: “Yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika ulimwengu.” hebu hilo na lizame mioyoni mwetu. Roho Wake anaishi ndani yetu. Je, twaweza kulishika hilo? Sasa hivi, unaposoma Barua hii, Roho Mtakatifu, Mungu Mwenyewe, Nguzo ya Moto, anaishi na kukaa ndani yetu? Tunajuaje kuwa hiyo ni kweli? MUNGU ALISEMA HIVYO!!

Shetani anaendelea kutuambia kwamba sisi ni watu walioshindwa. Na yuko sahihi, ndivyo tulivyo. Anatukumbusha, hatupo mahali tunapotakiwa kuwa katika Neno. Sahihi tena, hatuko. Tunafanya mambo tunayojua vyema kuliko kuyafanya. Tusamehe Bwana, yuko sahihi.

Lakini hata pamoja na makosa yetu yote, madhaifu yetu yote, kushindwa kwetu kote, haibadilishi ukweli wa mambo, SISI NI BIBI-ARUSI. TUNAAMINI KILA NENO!

Hatujitazami sisi wenyewe ama chochote tunachoweza kufanya, sisi ni mchafuko. Sisi tunajua tu kwamba Yeye alituchagua na kutupa Ufunuo wa Neno Lake na hakuna kitu kinachoweza kuuondoa Ufunuo huo kwetu. Huo umewekwa ndani ya mioyo na roho zetu.

Yeye alituambia inatupasa kuwa na IMANI KAMILIFU. Tunayo Bwana, IMANI KAMILIFU katika Neno Lako. Tuna imani katika Yale Nabii Wako aliyosema kuwa ni Bwana Asema Hivi. Si neno lake, bali Neno lako kwetu sisi.

Nabii Wako alituambia chochote tunachohitaji, kama tu tutaamini, na kuwa na imani katika Neno Lako, tunaweza kupata chochote tunachohitaji. TUNAAMINI.

Bwana, ninalo hitaji. Ninakuja mbele Zako nikiwa na imani yote niliyo nayo katika Neno Lako, kwa maana haiwezi kushindwa. Lakini leo, Bwana, siji mbele Zako nikiwa tu na imani yangu, bali na imani uliyompa malaika-mjumbe wako wa saba mwenye nguvu.

Ee Bwana Mungu, nakuomba uturehemu. Na jalia kila mwanamume na mwanamke ambaye ameketi sasa, ambaye ana namna yo yote ya maradhi au mateso; na kama vile Musa alivyojitupa mwenyewe katika pengo, kwa ajili ya watu, usiku wa leo ninaweka moyo wangu mbele Zako, Bwana. Na kwa imani yote niliyo nayo, ambayo iko ndani Yako, ambayo Wewe umenipa, ninawapa.

Nami ninasema: nilicho nacho, nawapa wasikizi hawa! Kwa Jina la Yesu Kristo wa Nazareti, kataeni magonjwa yenu, kwa sababu Yeye aliye ndani yenu ni mkuu, kuliko huyo Ibilisi anayejaribu kuyatwaa maisha yenu. Ninyi ni wana wa Mungu. Mmekombolewa.

Imekwisha. Neno Lake haliwezi kushindwa. Chochote tunachohitaji, tunaweza kukipokea.

Njooni muungane nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki) kupokea baraka hii kuu na upako kutoka kwa Mungu pindi sehemu ya Bibi-arusi watakapokusanyika kutoka duniani kote kusikiliza Sauti ya Mungu akiweka IMANI yake pamoja na IMANI yetu.

Ndugu. Joseph Branham

63-1110E Yeye Aliye Ndani Yenu

24-0107 Nafsi Zilizo Kifungoni Sasa

UJUMBE: 63-1110M Nafsi Zilizo Kifungoni Sasa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Watu Waliotengwa,

Mungu amekuja katika wakati wetu na kujifunua katika mwili wa mwanadamu, katika mtu aitwaye William Marrion Branham, ili aweze kulitimiza Neno Lake. Huo ndio Ufunuo wa Yesu Kristo katika wakati wetu.

Kuisikiliza Sauti hiyo na kuamini kila Neno ndiyo Njia pekee iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku hii. Alituma ulimwenguni watu wengi waliopakwa mafuta na Roho wake Mtakatifu, lakini Yeye alituma na kunena kupitia mtu mmoja tu kufunua Neno Lake na kumwongoza Bibi-arusi Wake.

Yeye kamwe habadilishi Mpango Wake wala Njia Yake ya kufanya mambo. Jinsi alivyolifanya mara ya kwanza, Yeye hulifanya jinsi hiyo kila wakati. Yeye huwaongoza watu Wake Mwenyewe, kwa Nguzo ya Moto.

Usisahau kamwe, WEWE NI Bibi-arusi mteule wa Mungu na hakuna kitu shetani anachoweza kufanya au kusema ambacho kinaweza kuliondoa hilo kutoka kwako, HAKUNA! Alikuchagua wewe tangu asili kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Alikujua tangu wakati huo, nawe ulikuwa pamoja Naye. Alijua jina lako. Alijua kila kitu kukuhusu. Alijua heri na shari zako. Alijua kushindwa kwako, makosa yako, na bado alikupenda na kukuchagua wewe kwa kuwa ulikuwa sehemu yake.

Nafsi yako inaweza tu kujilisha kwenye Neno Lake. Hakuna kinachoweza kukutosheleza ila Neno Lake. Unapenda kusoma Neno Lake na kumtafakari Yeye, ukiomba kutoka katika kilindi cha moyo wako. Unaposikia Sauti Yake ikizungumza nawe moja kwa moja, inakuinua hadi ng’ambo ya pazia la wakati. Kwa maana unajua umeketi naye katika ulimwengu wa roho wakati anaponena nawe mdomo kwa sikio, akifunua Neno lake, akikukumbusha, WEWE NI BIBI-ARUSI WANGU.

Ibilisi aweza kukutwanga na kukutwanga. Waweza kushushwa moyo sana wakati mwingine na kuhisi wewe ni aliye shindwa kabisa; ujisikie kana kwamba umemkosa Yeye zaidi ya yeyote yule. Wewe ndiye mbaya zaidi kuliko wabaya wote, lakini mahali fulani, chini kabisa ndani ya nafsi yako, unasikia ile Sauti Ndogo Tulivu ikikuambia: “Hakuna kitu kinachoweza kukutenganisha na MIMI, WEWE NI NENO LANGU. Nililiweka jina lako kwenye Kitabu Changu Cha Uzima cha Mwana-Kondoo, Mimi Mwenyewe .”

Naweza kusema nini kuwatia moyo leo?

Kaeni tu katika Neno. BONYEZENI PLAY kila siku na mwisikie Sauti ya Mungu ikisema Bwana Asema hivi na kuwaambia; Ninawaunganisha katika Neno Langu. Mnaweza kushinda CHOCHOTE, kwa maana Neno Langu linaishi na kukaa ndani yenu. Nimewathibitishieni, mnayo IMANI KAMILIFU. Mmeiweka ile Ishara, nayo imewaweka katika Kudhikika. Nitasimama nyuma ya Neno Langu. Nitafanya kile nilichosema kuwa nitafanya.

Maneno Yake ni ya ajabu jinsi gani anayosema nasi kwenye Kanda. Tunajua si mtu fulani, mtu wa kimwili ambaye yuko miongoni mwetu. Ni Mungu wa Milele anayezungumza nasi, Bibi-arusi Wake.

Mnaalikwa kuungana na Bibi-arusi Jumapili hii saa 06:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) tunapokusanyika kusikiliza ile Sauti Ndogo Tulivu:  63-1110M Nafsi Zilizo Kifungoni Sasa.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Mwanzo 15:16
Mathayo 23:27-34
Yohana 4:23-24 / 6:49 / 14:12
1 Petro 3:18-22
2 Petro 2:4-5
Yuda 1:5-6