23-0108 Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake

UJUMBE: 65-0718e Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Watafuta Madini ,

Kuna kisima kinachofoka maji cha Ufunuo ambacho kinabubujika ndani yetu zaidi ya hapo awali. Tumesikia Ujumbe huu maisha yetu yote, na daima tumeamini kila Neno, lakini SASA imedhihirishwa ndani yetu zaidi kabisa ya hapo awali.

Sasa huu ndio wakati wake , sasa ni majira yake tunakula mambo ya siri ya Mungu ambayo ulimwengu umefichwa. Kitu kile watu wanachokicheka, ndicho kitu tunachokiomba. Kile kitu ambacho watu wanaita “wenda wazimu,” tunakiita “Kikuu!”
Mungu ametufunulia kuna njia moja tu iliyoandaliwa ya kuwa Bibi-arusi Wake, KUBONYEZA PLAY.

Lakini Mungu ashukuriwe, tuna Chakula kilichofichwa, Chakula cha kiroho, hata tunaishi kwa fadhili na rehema za ufunuo wa Yesu Kristo katika siku hizi za mwisho, akijithibitisha Mwenyewe miongoni mwa watu Wake.

Kwa kila Ujumbe anaousikia Bibi-arusi, Yeye hututhibitishia hayo ni Mapenzi yake makamilifu. Sio kile TUNACHODHANI Anasema, wala si kile TUNACHODHANI Inamaanisha , NI HASA KABISA Yale yeye Asemayo na bado wengine hata hawawezi kuliona; wamepofushwa. Mungu amelificha. Wanalitazama moja kwa moja, lakini hawalioni. Kwetu sisi, NDIYO YOTE TUYAONAYO.

Tunapokusanyika kila wiki, ni vigumu kungoja kusikia kile Atakachoenda kutuambia na kutufunulia. Jumapili hii, yeye hatatupa vijisehemu fulani vidogo vya vito vya thamani vilivyofichwa, Yeye atatupa jiwe kubwa la madini na KULlLIPUA tena na tena ili kuhakikisha tunalipata.

. Huyo nabii alikuwa amekaa kwa muda mrefu sana katika Uwepo wa Mungu, Manabii wa Agano la Kale, ama wa wakati wo wote, walipoishi katika Uwepo wa Mungu mpaka wakawa Neno, Ujumbe wao ni Neno Lenyewe . Pia, kumbukeni, yeye alisema, “BWANA ASEMA HIVI.”

. Tunaona ya kwamba mtu anapokuja, ametumwa kutoka kwa Mungu, amechaguliwa na Mungu, akiwa na BWANA ASEMA HIVI ya kweli, ujumbe huo na mjumbe huyo ni mmoja na kitu kimoja.

. Basi wakati mtu anapokuja na BWANA ASEMA HIVI , yeye na Ujumbe huo ni mmoja .

. Mbingu zinatangaza jambo hilo, Biblia inalitangaza, Ujumbe unalitangaza. Yote ni jambo lile lile.

. Nabii, Neno, Ujumbe; mjumbe, Ujumbe, na Ujumbe, walikuwa mmoja.

. Mtu ye yote na ujumbe wake ni mmoja .

Nena kuhusu Mgodi wa Dhahabu.

Ikiwa una hata chembe ya Ufunuo , nadhani yeye analiweka wazi kweli hilo; Ujumbe na mjumbe ni MMOJA . Je, unasikia alichosema… MMOJA !! Basi Enyi Wahudumu, hamwezi kumtenganisha mjumbe na Ujumbe.

Unatakiwa kumweka MJUMBE kanisani mwako pamoja na UJUMBE aliouleta vinginevyo wewe haukubali UJUMBE WOTE. WEWE SI BIBI-ARUSI.

Loo! Tena, jambo hilo linaufanya Ujumbe na mjumbe kuwa ni kitu kimoja. Chakula cha kiroho kiko tayari, na kiko katika wakati wake sasa.

Kwetu sisi, tunaoamini saa ya Mungu tunayoishi, mjumbe Aliyemtuma, kila Neno alilonena; mambo haya ni Chakula kilichofichwa.

Jinsi tunavyoupenda Ujumbe huu, na unapowazia tu, “Kunawezaje kuwa mengine zaidi?” Yeye Anaweka jiwe la kifuniko juu Yake kwa kutuambia sisi ni nani sasa.

Hivi hamwoni mamlaka ya Mungu aliye hai katika Kanisa lililo hai, Bibi-arusi ? Wagonjwa wanaponywa, wafu wanafufuliwa, viwete wanatembea, vipofu wanaona, Injili inatangazwa katika nguvu Zake, kwa maana Ujumbe na mjumbe ni kitu kimoja. Neno liko ndani ya Kanisa, katika mtu.

Neno Hilo NDANI YETU . Sisi ni Ujumbe. Tunayo mamlaka. Ujumbe huu na sisi NI MMOJA!! Nena kuhusu kububujika tena na tena na tena.

Bibi-arusi ni sehemu ya Mume, Kanisa ni sawa na Kristo. “Kazi nizifanyazo Mimi ninyi nanyi mtazifanya.”

Sisi ni sehemu ya Mume!!

SISI NI SAWA NA KRISTO!!

Unafikiri inasikika sasa vizuri , na kuubariki moyo wako kwa kusoma tu nukuu hizi, subiri tu mpaka uisikie Sauti ya Mungu ikikuelezea hizo mdomo kwa sikio Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville,( ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya tanzania na Kenya pia) tunaposikia: 65-0718E. Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake.

Umealikwa kuja kuungana nasi. Kama huwezi, BONYEZA PLAY wakati wowote, Ujumbe wowote, mahali popote, na umsikie mjumbe wa Mungu akikuletea Ujumbe wa Mungu.

Ndugu. Joseph Branham.

Ndivyo ilivyo leo, ya kwamba Chakula cha Uzima ambacho watoto wanakula, kinafuata Ujumbe wa Mungu, kuwahifadhi katika wakati wa ukame.

Maandiko ya kusoma kabla ya Kusikiliza Ujumbe :

1 Wafalme 17:1-7
Amosi 3:7
Yoeli 2:28
Malaki 4:4
Luka 17:30
Yohana 14:12