21-0919 Watiwa Mafuta Katika Wakati Wa Mwisho

UJUMBE: 65-0725m Watiwa Mafuta Katika Wakati Wa Mwisho

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliyeteuliwa,

Sababu ya Walioteuliwa, Yesu alisema, hawatadanganywa, ni kwa sababu wao ndio Neno hilo. Hawawezi kuwa kitu kingine. Hawawezi kusikia kitu kingine. Hawajui kitu kingine.

Hakuna kitu kikubwa maishani kuliko kujua kwamba Mungu alimchagua nabii Wake kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu kunena Maneno haya. Kisha, Aliruhusu Sauti Yake kurekodiwa, kwa hivyo sisi, Bibi-arusi Wake aliyechaguliwa kimbele , tunaweza kurejea nyuma na kusikia Sauti Yake ambayo iliyorekodiwa na kuhifadhiwa, kwa sababu alitaka tujue:

. Sisi ni Neno.
. Hatuwezi kudanganywa.
. Hatuwezi kuwa kitu kingine.
. Hatuwezi kusikia kitu kingine.
. Hatujui kitu kingine.

Yeye Alijua tungehitaji kutiwa moyo leo zaidi ya siku nyingine yoyote katika historia. Vita vingerindima zaidi ya hapo awali. Bibi-arusi wake angejaribiwa. Bali kama angeweza kumkumbusha Bibi-arusi wake wao ni akina nani, wangefurahi mioyoni mwao wakijua wao ndio Wapenzi Wake katika mapenzi Yake Makamilifu.

Chochote kile Shetani anachotutupia, lolote lile tunalopitia,
sasa tunajua, Yeye Anachagua Bibi-arusi, na sisi ndio Bibi-arusi huyo. Hatuonei haya Ufunuo wetu wa Neno. Hatutajaribu kamwe Kumtendea Mungu kazi Bila Mapenzi Yake. Kwetu sisi, ni Chakula cha Kiroho Kwa wakati Wake. Tunatambua kwamba kutakuwepo na Watiwa mafuta katika Wakati wa Mwisho, lakini sisi Tuta KAA NA NENO.

Ikiwa ungependa hakikisho lili hili, njoo uungane nasi Jumapili saa 8:00 nane mchana , saa za Jeffersonville, ( ni saa 3:00 tatu Usiku ya Tanzania) kusikia: 65-0725M Watiwa mafuta Katika Wakati wa Mwisho.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma :

Mathayo Mtakatifu 5: 44-45 / 7:21 / 24: 15-28

Luka Mtakatifu 17:30 / 18: 1-8

Yohana Mtakatifu 14:12

Waefeso 1: 5

2 Timotheo 3: 1-8

Waebrania 6: 1-8 / 11: 4

Ufunuo 10: 1-7 / 16: 13-14

Malaki 4: 5

I Wafalme 22: 1-28

Yeremia: Sura ya 27 yote na 28 yote