21-0905 Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake

UJUMBE: 65-0718m Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Mpendwa Kanisa la Sauti Ya Mungu,

Sisi ni Kanisa lake la Sauti Ya Mungu, kipenzi chake Bibiarusi_Neno, na tunangoja kwa hamu kusikia kile Baba atakachonena na kutufunulia Jumapili hii.

Tunayo Sauti ya Mungu iliyo hai kiganjani mwetu. Kwa mguso mmoja wa kidole chetu tunaweza kumsikia Mungu akinena kupitia midomo ya mwanadamu, Maneno ya uzima wa Milele. Kwa kidole kimoja Anasema nasi na kutufunulia siri zote zilizokuwa zimefichwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Kwa kidole kimoja Anajibu swali lolote tulilo nalo mioyoni mwetu. Kwa kidole kimoja Anatuambia chochote tunachohitaji kujua. Kwa kidole kimoja tunaweza kusikia Sauti ya Mungu ikisema nasi na kutupa Imani ya Kunyakuliwa . Kwa kidole kimoja tunaweza kumsikia Mungu akinena na kutuambia, umeponywa.

Wakati adui anatuambia sisi sio Bibi-arusi wa Mungu, wewe ni uliyeshindwa tu, kwa kidole kimoja tunabonyeza Play na tunaweza kumsikia Baba akinena nasi na kutuhakikishia, “WEWE ni Bibi-arusi wangu mteule. Nilikuchagua kabla ya kuwekwa misingi ya Ulimwengu. ”

Tunaposhushwa Moyo na adui anatushambulia kutoka kila kona, kwa kidole chetu kimoja tunaweza kumsikia akisema nasi na kutamka tu, “Habari za asubuhi Marafiki,” na Amani ya Roho Mtakatifu inakijaza chumba.

Tunaposikia ADUI ANASEMA ninyi mnamfuata tu mtu na mnaweka mengi kumhusu , kwa kidole kimoja tu tunasikia Sauti ya Mungu ikituambia:

Yeye aliniambia ikiwa nitawafanya watu waniamini. Hilo linaonekana kuwa la ajabu mimi kusema hivi, “Unaniamini ?” Kasema, “Je! Haikubidi kumwamini Mungu ?” Unapaswa kuamini hilo. Yakubidi umwamini Mungu na umwamini Kristo, na umwamini Roho Mtakatifu. Halafu baada ya kuwaamini wote, Mungu anakutaka uniamini .

Wakati adui anajaribu kutuambia, “Si Maandiko na ni makosa kukusanyika kwa wakati fulani na kusikiliza tu kanda,” kwa kidole kimoja tu tunasikia Sauti ya Mungu ikituambia:

Na kwa kanisa hili, na kwenye kanda— watu wanaosikiza kanda , na watu katika sehemu zilizounganishwa kwa redio wanaosikiza nchini kote, nawatakeni msikilize hili kwa makini na msikose .

Wakati adui anaposema Ndugu Branham alisema kaa na Neno, sio kanda, kwa kidole kimoja tunasikia Sauti ya Mungu IKIPIGA KELELE kusema:

Nasema vivyo hivyo katika Jina la Yesu Kristo : Usiongeze kitu. Usiondoe—kuliwekea mawazo yako. Wewe sema tu yaliyosemwa katika kanda hizo. Tenda sawasawa kabisa na vile Bwana Mungu amekuamuru kutenda. Usiongezee Kwake!

Sauti hiyo hata hivyo inatueleza jinsi ya kulichunguza kwa Neno ili tusikosee.

Lazima zako tano ndizo hizo. Lazima iwe hivyo;

. Wakati Wake
. Majira Yake
. Mtu yule aliyemchagua
. Lazima ije kwa nabii
. Nabii yule lazima awe nabii aliyethibitishwa

Nabii wetu ni Yesu Kristo.

Neno lililothibitishwa la saa hii !
Neno lililothibitishwa la siku za Musa lilikuwa Yesu. Neno lililothibitishwa la siku za Isaya, Eliya, Yohana, wote, lilikuwa Yesu. Na Neno lililothibitishwa leo ni Yesu, yeye yule jana, leo na hata milele .

Kwa kidole kimoja tunaweza kubonyeza play na kumsikia Yesu Kristo mwenyewe akinena na kutufunulia:

. Huu ndiyo wakati ,
. Haya ndiyo Majira ,
. Huyu ndiye mtu niliyemchagua,
. Huyu ndiye nabii wangu,
. Nabii huyu amethibitishwa zaidi ya manabii Wangu wote wengine .

Leo, sio tu kwamba tuna yule Mungu wa Mbinguni anayetuzungumzia , lakini yeye yuko ndani yetu, anakaa, na anaishi Maisha yake kupitia sisi. Inapita ufahamu wetu.

Hebu na Tujiweke Tayari. Wakati umekaribia. Tunaona Maandiko yakitimizwa kila siku. Ujumbe unasomeka kama habari ya leo:

” Mshangao wa wakati huo, dhiki kati ya mataifa, matetemeko ya nchi mahali mahali, bahari ikivuma, na moyo wa mwanadamu ukikoma kwa hofu “

Hata maumbile yenyewe hutuambia leo, tunapoona mataifa yakivunjika, dunia ikididimia, maandiko kwenye ukuta.

Tunaona kanisa na hali lilimo. Twamuona Bibi-arusi na hali aliyomo. Nasi twajua kwa mambo ya asili kwamba Kanisa linajiweka tayari kuondoka.

UTUKUFU, tunajiandaa kuondoka. Kwa kidole kimoja tu unaweza kujifanya mwenyewe tayari. Ninakualika uungane nasi Jumapili saa 8:00 nane mchana , saa za Jeffersonville,(ni saa 3:00 tatu Usiku ya Tanzania) kusikia: Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake 65-0718M.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma Kabla ya ibada :

Kumbukumbu la Torati 4: 1-4 / 4: 25-26
1 Mambo ya Nyakati 13
1 Mambo ya Nyakati 15:15
Zaburi 22
Marko Mtakatifu 7: 7
Yoeli 2:28
Amosi 3: 7
Malaki 3
Mathayo Mtakatifu11: 1-15
1 Wakorintho 13: 1