21-0829 Kuonea Haya

UJUMBE: 65-0711 Kuonea Haya

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Wapendwa Maskani ya Branham,

Tunashukuru sana alituteua Sisi Tangu Asili kuchagua kanisa linalofaa kuziingiza familia zetu.

kama nilikuwa ninachagua kanisa, ningalichagua kanisa la kweli, lenye mafundisho ya kimsingi, linaloamini Injili Yote, kanisa la Biblia, kama ningelikuwa nachagua moja kuwaingiza familia yangu.

Tunashukuru sana tunauambia ulimwengu mchungaji wetu ni Nani, na kwamba tunatenda tu kama yeye.

kama utachunguza tabia ya hilo kanisa, hebu mwangalie tu mchungaji kwa muda mfupi, na mara nyingi utaona ya kwamba kanisa hutenda kama mchungaji wake .

Tunashukuru sana haijalishi tuko wapi ulimwenguni, Yeye hukutana nasi .

Aliahidi kukutana nao popote wawili watatu wamekusanyika pamoja. Hakika. Hapo ndipo mwaminio wa kweli huweka matumaini yake, ni katika hilo Neno la Mungu linalodhihirishwa katika Kweli.

Tunashukuru sana tunamwamini Nabii Wake, na kila Neno lililonenwa.

Kama unaniamini mimi kuwa nabii wa Mungu, sikiliza yale niliyokwambia.

Je! Nabii wake alikuwa ahubiri nini?

Ujumbe mkamilifu , kurudi kwenye Neno ,

Alitumwa kwa kusudi gani?

“ Nenda ukamlete Bibi-arusi huyo!” Ndilo jukumu. Hiyo ndiyo sababu ya mimi kuwapo hapa. Hilo ndilo ninalojaribu kufanya , ni kumwita Bibi-arusi atoke .

Je! Vipi Ikiwa tutatoka nje ya Mstari?

Na hivyo ndivyo nilivyopaswa kufanya , kumweka Bibi-arusi huyo kwenye mstari, nimtafute mtu huyo.

Sasa Baba amemwekea Akiba nini Bibiarusi wake?

Ninarudi nyumbani, nifanye upya nadhiri zangu tena, na kuanza upya.” Kwa hiyo hilo ndilo tunalopanga kufanya, hiyo ndiyo sababu nipo hapa.

Bwana asifiwe, tunaanza lini ibada zetu za kufanya upya?

Halafu basi, Bwana akipenda, Jumapili ijayo asubuhi tutaanza ibada. Nanyi nyote mnisaidie, nasi tutaomba, kwa maana lilikuwa moyoni mwangu kujaribu…Wao walisema, “Vema, tungeenda Louisville ama tungeshuka twende huko New Albany.” Lakini mkutano huo ulipaswa kuwa ni wa Jeffersonville. Nitaenda Louisville na New Albany, katika nyakati tofauti, lakini huu unapaswa kuwa hapa Jeffersonville.

Tuko tayari Baba. Tai wako watakusanyika na kusikiliza. Ni kitu Gani kitakachotukia wakati huu?

“… Ninafikia mahali, ninahitaji imani zaidi.” Hiyo ndiyo sababu niko nyumbani sasa ni kupata ujazo m—mpya wa imani.

Bwana asifiwe, hilo ndilo tunalohitaji pia Baba, Ujazo Mpya wa IMANI.
Tunajua imani huja kwa kusikia, kusikia Neno lako, na Neno lako Linamjia Nabii.

Ujumbe huu, Nguvu za Mwenyezi Mungu , Zimeenea kote ulimwenguni , lakini wakati wa Kutengana unatukia sasa. Mungu anamwita Bibi-arusi, naye shetani analiita kanisa. Sisi ni sehemu ya Ujumbe huu, Neno Lake, Bibi-arusi Wake!

Tuna hakikisho na tunajua tunalozungumzia. Hatuonei haya kwamba tunaamini Ujumbe huu na Mjumbe Wake, kwa kuwa wao ni kitu kimoja. Hatu haya kusema: “Tunaamini kila Neno”. Hatuonei haya kusema: “Tunacheza kanda kanisani mwetu”. Hatuonei haya kusema: “Sisi ni Watu wa Kanda”.

Ni ngumu kwetu kuelewa kwamba mwamini yeyote, au mhudumu wa huduma tano, anayedai kuamini Ujumbe huu, na kusema Ndugu Branham ni Nabii na Mjumbe wa Mungu, Kisha Angeamini na kuwaambia watu kuwa ni makosa na sio kulingana na Neno kucheza hasa Sauti ya Mungu iliyothibitishwa katika kanisa Lao.

Na tuwe tayari, wakati ufaao na wakati usiofaa; karipia, kemea na … kwa uvumilivu wote na mafundisho. Kwa sababu utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima ;

ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia pamoja waalimu makundi makundi ; kwa kuwa wana masikio ya utafiti ;

Nao watageuzwa … _
wasisikie yaliyo kweli ,…
watazigeukia hadithi za uongo .

Inapofikia Neno la Mungu Halisi, lisiloghoshiwa, lililothibitishwa na Mungu, Sauti ya Mungu iliyothibitishwa, Inaonekana kulitahayarisha hata kundi hilo lingine. Wana tahayari kwa jambo hilo nao wanaamini Kwamba kuwa Kanisa la Kanda ni kuwa kinyume cha Neno.

Bali kwetu sisi, Ni Halisi. Hatuonei haya. Wakati tulipopokea Ufunuo huo, kulikuwa na kitu ambacho kilitulia ndani yetu, na sasa hakuna kinachoweza kupachukua Mahali pake. Tunajivunia kuitwa Mmoja wao, Kanisa la Kanda, Kundi la Kanda, Watu wa Kanda.

Tunakualika uje kusikiliza pamoja na Maskani ya Branham kwenye huduma ya Kanda ya Mungu, Jumapili saa 8:00 Nane Mchana, saa za Jeffersonville,( Ni Saa 3:00 Usiku ya Tanzania) tunapokusanyika kwa matarajio makubwa; kuzifanya upya nadhiri zetu tena, na kuanza upya, kwa kusikia: Kuonea Haya 65-0711 .

Ndugu. Joseph Branham

Marko Mtakatifu 8: 34-38