22-1002 Maswali na Majibu #1

Ujume: 64-0823M Maswali na Majibu #1

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 18MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Maskani ya Branham,

Kama hamwezi kuja hapa maskanini, tafuteni kanisa fulani mahali fulani; enendeni kwalo. Ikiwa huwezi kuzisikiliza kanda pamoja nasi, Zisikiliza kanda mahali fulani. Kucheza na kuzisikiliza Kanda ndilo jambo muhimu zaidi ambalo mhubiri, mwalimu, mtume, nabii, mwinjilisti au wewe unaloweza kufanya.

Hiki ndicho kituo changu cha nyumbani; haya ndiyo makao yangu makuu; hapa ndipo tumeimarika. Sasa, shikilia hilo mawazoni haijalishi itakuwaje. Sasa, kama mna busara, mtashika jambo fulani. Haijalishi itakuwaje, haya ndiyo makao yetu makuu, papa hapa! Na wekeni hilo mawazoni na mrejee kwenye kanda hii siku fulani, ambamo mlinisikia nikifanya unabii. Vema, kumbukeni hayo.

Nabii alikuwa akifanya nini? Akihifadhi Chakula. Akihifadhi Chakula ili kwamba tupate Kitu cha kula, ili kwamba tupate Kitu cha kufanyia karamu. Tumekiweka hicho kwenye kanda zetu tumeziweka katika chumba chetu chenye Baridi.

Alisema kulikuwa na ghala moja tu ndogo katika nchi hii yote , ghala moja ndogo. Aliweka tu Akiba nyingi ; Ile Ishara, Yakini, Mihuri, Nyakati Saba za Kanisa, Makao ya Baadaye ,kuthibitisha Neno Lake, yote kwa ajili yetu, kwa hiyo tungekaa hapa tu na kusikiliza Atakapokuwa ameondoka.

Yaonekana yuko mbali sana, lakini bado tunakumbuka, mambo haya ni kweli. Haya ni maisha ambayo yatubidi kutembea peke yetu.

Ghala ZIMEJAA . Hakuna Chakula kingine ambacho kimethibitishwa na Mungu mwenyewe kuwa ni NENO SAFI ambalo halijavunda.

Ikiwa ungependa kufanya karamu pamoja nasi, tunakukaribisha uungane nasi, Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA . Saa za Jeffersonville (Ni saa 1:00 jioni ya Tanzania) tunapokuja Mezani na kula kama wageni Wake.

Maswali na Majibu 64-0823M

Ndugu. Joseph Branham