22-1106 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi

Ujume: 65-0218 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 9MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi-Neno Bikira ,

Tuko hapa. Tumefika. Muda umekaribia. Kapi limejitenga na Mbegu. Tumekuwa tukikaa katika Uwepo wa Mwana, tukiiva. Tutakaa katika Uwepo huo mpaka kundi letu dogo litakapoiva sana kwa Kristo, mpaka tuwe mkate kwenye meza Yake. Bwana Ashukuriwe!

Ujumbe huu umethibitisha Malaki 4, umethibitisha Luka 17:30, umethibitisha Waebrania 13:8, umethibitisha Yohana Mtakatifu 14:12, umethibitisha Ufunuo sura ya 10, kufunguliwa kwa ile Mihuri Saba, siri za Mungu, uzao wa nyoka, ndoa na talaka. na siri hizi nyingine zote ambazo zilikuwa zimefichwa chini ya nguzo kwa miaka hii yote.

Sisi ni mabikira kwa Neno. Hatuwezi na hatutagusa kitu kingine chochote. Kwa kila Ujumbe tunaosikia, ni msafi na mpya; Mana mpya ambayo ndio kwanza imeshuka kutoka Mbinguni.

Lakini alituonya kwamba katika wakati wa mwisho kutakuwa na roho mbili ambazo zingefanana sana, zingewapoteza walio wateule , kama Yamkini. Hivyo, ni lazima tuwe macho kwa roho hiyo kwani itaonekana kuwa kama Bibi-arusi mwenyewe.

Tazama, ona zinavyofanana. Mathayo ilisema—Mathayo Mt. 24:24, ilisema kwamba hizo roho mbili katika siku za mwisho , roho ya kanisa ya watu wa kanisa na Roho ya watu wa Bibi-Arusi , zitafanana sana hata ingewapoteza, kama yamkini, walio Wateule. Hivyo ndivyo jinsi zinavyofanana.

Alisema ROHO ya watu wa kanisa na ROHO ya watu wa Bibi-arusi zitafanana sana moja kwa nyingine . Hiyo ingemaanisha kwamba roho ya watu wa kanisa ingepaswa kusema wanaamini Ujumbe wa wakati huu ili KUFANANA JINSI HIYO.

Hiyo haingekuwa methodisti, Baptisti, presbiteri, au hata wapentekoste; Wao wako mbali sana na Neno na hata wanaukataa Ujumbe. Hakuna hata mmoja wao aliye na roho inayofanana na Bibi-arusi.

Shetani amejaribu, na amefanikiwa sana, kuwa mdanganyifu sana. Hata tangu hapo mwanzo, alisema tu, “Hakika,” hivyo akimwambia Hawa atumie hoja yake naye amsikilize yeye na si Neno tu. Kuna jambo moja tu aliloamriwa kufanya: kukaa na Neno.

Ukweli:

Ikiwa una swali, lazima kuwe na jibu. Hivyo ndivyo nabii alivyotuambia. Jibu lazima litoke katika Neno. Neno huja kwa nabii peke yake. Nabii ndiye mfasiri pekee wa Neno. Ikiwa mwanamume au mwanamke yeyote atakupatia jibu, lazima liwe vile nabii alivyokwishasema . Haiwezi kuwa fasiri yao , wazo au ufahamu wao. Hawana budi waliunganishe kwa Neno lililonenwa na nabii wa Mungu aliyethibitishwa. Wala Sio neno la nabii pamoja na, ni kile tu nabii alichosema.

Kuna itikadi mbili sasa hivi .

1 : Ni lazima uamini kila Neno kwenye hizo kanda kwani ndizo Jumbe muhimu sana unazopaswa kusikia.

2 : Wala Huhitaji kuamini kila Neno kwenye hizo kanda, na wahudumu sasa wao wanazo jumbe muhimu sana unazopaswa kusikia.

Kunazo tofauti nyingi, nyingi kwa hiyo itikadi ya pili: Roho Mtakatifu ataniongoza mimi au mchungaji wangu kutuambia kile ambacho ni Neno na kisichokuwa Neno. Tunahitaji zaidi ya yale tu aliyosema Ndugu Branham kwenye kanda. Huna budi kuwa na wahudumu wa kufafanua au kulivunja-vunja Neno. Bila ya wahudumu huwezi kuwa Bibi-arusi.

Kuna Mbegu za Hitilafu nyingi zaidi, lakini haiwezekani kuziorodhesha zote. Lakini hakuna tofauti ama mbegu za hitilafu kwa Ile namba ya kwanza. Ni AMINI KILA NENO, hivyo tu.

Mkiwa Kama waamini wa Ujumbe huu wa wakati wa mwisho, lazima mjiulize maswali haya:

1 : Je, unaamini kile nabii alichosema kwenye kanda ndio Yakini yako, au unaamini ni Roho Mtakatifu kupitia wewe au mchungaji wako?

2 : Je, unaamini kwamba huduma tano ina jumbe muhimu zaidi ambazo Bibi-arusi anazohitaji kusikia, au ni Ujumbe uliyo kwenye kanda?

Iwapo mchungaji wako, mhubiri, mwalimu, mwinjilisti au nabii hakuambii kwamba kuzisikiliza kanda ndizo JUMBE MUHIMU SANA unazopaswa kusikia, yeye ni wa UWONGO, NA ILE ROHO AMBAYO NABII ALITUONYA INGEKUJA.

Ikiwa anasema HIZO NDIZO Jumbe muhimu sana mnazoweza kusikia, lakini bado anakataa kuzicheza kanda katika kanisa lake, HAPO KUNA KASORO FULANI. Ikiwa anaamini kweli kwamba kuzisikiliza kanda ndilo jambo muhimu zaidi mnaloweza kufanya, basi angezicheza kanda KWANZA, kisha ahubiri ikiwa anahisi kuongozwa.

Mfano rahisi:

Kama ningekuambia, kunywa maji safi ndilo jambo moja muhimu zaidi uwezalo kufanya kwa ajili ya afya yako, na kuna maji MAMOJA tu ya kunywa yaliyothibitishwa na kuhakikishwa…lakini ujapo nyumbani kwangu kula chakula cha jioni, Nami sikuhudumii hayo maji yaliyothibitishwa. Ninakuambia, “unaweza kunywa maji hayo huko nyumbani kwako lakini nyumbani kwangu, lazima unywe kile Mimi ninachokupa .”

Ikiwa maji hayo ndio KITU BORA ninachoweza kukupa kwa ajili ya afya yako, ambayo yatakupa uhai, basi jambo la kwanza nitakalokupa unapoingia nyumbani Mwangu ni maji hayo safi ya kunywa.

Je, nimekosea kwa kusema, “CHEZENI KANDA KATIKA MAKANISA YENU, ndilo jambo bora sana muwezalo kufanya kwa watu wenu. Ni Bwana Asema Hivi.”

Au, wanakosea kwa kusema, “Ni makosa kucheza kanda kanisani, Ndugu Branham hakusema kamwe kucheza kanda kanisani mwenu. Tunawaambia watu wacheze kanda majumbani mwao, kwenye magari yenu, kila wakati, LAKINI kanisani lazima wanisikie MIMI.”

Ni Roho gani anayekuongoza? Je, Unasema, “kinachosemwa kwenye kanda ni Yakini yangu na ndilo jambo muhimu zaidi niwezalo kusikia”? Au, Unasema, “Kanda hizo hazitoshi. Sio Yakini yangu na sio jambo lililo muhimu zaidi kusikia, je ni Wahudumu ”?

Sasa, ni wakati wa mbegu au wakati wa Bibi-Arusi. Makapi yamekufa, yale makapi tayari yamekwisha kukauka. Ni wakati wa Neno bikira, lisilogoshiwa. Ni bikira, Kumbuka, wakati wa Neno bikira.

Njoo usikie Manna mpya ambayo ndio kwanza imeshuka kutoka Mbinguni Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, ( Ni saa 2:00 MBILI USIKU Ya Tanzania),Tunaposikia :  
65-0218 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja na Kapi.

Ndugu. Joseph Branham