22-1113 Leo Maandiko Haya Yametimia

Ujume: 65-0219 Leo Maandiko Haya Yametimia

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 8MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Uzao wa Kifalme wa kiroho wa Ibrahimu,

Ni kanisa gani unaloweza kwenda na kujua, bila shaka yo yote, ya kwamba kila Neno unalosikia ni Bwana Asema Hivi? Hakuna mahali popote, isipokuwa tu usikilize Sauti ya Mungu ikisema nawe kwenye kanda.

Sisi ni tai wa Mungu na hatutapatana hata kwa Neno moja. Tunataka tu Mana mpya kila ibada na Haiji tena mpya kuliko kuisikia moja kwa moja kutoka kwa Mungu Mwenyewe. Tunaruka juu zaidi na zaidi tunaposikia kila Ujumbe. Kadiri tunavyoenda juu zaidi , ndivyo tunavyoweza kuona zaidi . Kama hakuna Mana katika kanisa hili, tai wa Mungu wanapaa juu kidogo mpaka waipate.

Jinsi gani mioyo yetu inavyoruka kwa furaha tunapomsikia Mungu akizungumza nasi na kutuambia ya kwamba sisi ndio Kanisa Lake halisi, Kanisa la Mungu, lililozaliwa mara ya pili, ambalo linaloamini kila Neno la Mungu mbele ya kitu chochote kile, bila kujali ni kitu gani, kwa sababu sisi ni Bibi-arusi-Neno Bikira Wake Asiyeghoshiwa.

Kuna msukosuko mwingi miongoni mwa watu leo. Kama ilivyokuwa katika siku za Yesu, wale waliojiita waamini walikuwa wakichukua mafafanuzi ya yale makuhani walikuwa Wamesema kuhusu Maandiko. Walikuwa wakiamini mafafanuzi ya Neno ya Watu. Hiyo ndiyo ilisababisha wakose kuiona ile Kweli ya Mungu, kwa sababu kulikuwa na mafafanuzi mengi sana yaliyotengenezwa na Wanadamu ya Neno la Mungu. Mungu hahitaji mtu yeyote afafanue Neno Lake. Yeye ni Mfafanuzi Wake Mwenyewe.

Je, unaamini kama ungeishi wakati wa Yesu, ungeamini kila Neno alilosema, bila kujali kuhani wako alisema nini? Je, ungemwambia kuhani wako kwamba kumsikiliza Yesu ndilo jambo muhimu zaidi unaloweza kufanya? Je, ungemwambia Maneno ya Yesu hayahitaji kufasiriwa? Kama wangekuwa na kanda za Mahubiri ya Yesu, je! ungalimwambia kuhani wako unataka abonyeze play ili uweze kusikia yale hasa Yesu aliyosema na jinsi alivyoyasema?

Vema, hilo halikuwa kwa ajili ya wakati wako; huu ni wakati wako, huu ndio wakati wako. Biblia yasema, ni Yeye yule jana, leo, na hata milele. Kile Unachofanya na kusema hivi sasa ndivyo hasa ungefanya wakati huo.

Tunaamini kwamba M-w-a-n-a wa Mungu yule yule aliyetokea mashariki na kujithibitisha Mwenyewe kama Mungu aliyefanyika mwili, ndiye M-w-a-n-a yule yule wa Mungu Aliyeko katika kizio cha magharibi cha dunia ambaye anajitambulisha Mwenyewe miongoni mwetu. Tunaamini Leo Maandiko haya yametimia mbele yetu.

Hakika ninaamini huu ndio mwaka uliokubaliwa, mwaka wa yubile. (ama mwaka wa Sikukuu). Ikiwa Unatamani kubaki mtumwa na kutoamini Ujumbe huu kuwa ni Bwana Asema Hivi ; Ikiwa Ujumbe huu sio Yakini yako; ikiwa unaamini inahitaji mtu kuufafanua Ujumbe huu; Ikiwa unaamini ni makosa kuzicheza kanda kanisani mwako; Basi itakubidi upelekwe na shimo litatobolewa masikioni mwako kwa msharasi, Na ndipo itakupasa kumtumikia huyo mwenye watumwa siku zako zote.

Lakini Kanisa la kweli la Bibi-arusi linaamini Neno lote la Mungu katika utimilifu Wake na katika nguvu Zake. Sisi ndio lile Kanisa Teule ambalo linajiondoa na kuwekwa kando kutoka kwenye mambo hayo, nalo dhihirisho la Mungu limeuvutia usikivu wetu. Sisi ndio ule Uzao wa Kifalme wa kiroho wa Ibrahimu.

Kwa hivyo tuna shukrani kwenu kuwa hapa mkafurahie ushirika huu pamoja nasi, ambao tunatarajia Mungu atatupa katika mkutano huu.

Kwa hivyo tunakualika uungane nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, ( Ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya tanzania) tunaposikia 65-0219 Leo Maandiko Haya Yametimia . Tunatarajia Kile Mungu anachofanya wakati wa mikutano hii. Ile Nuru ya jioni ya Mwana imekuja.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma :

Yohana Mtakatifu Sura ya 16 yote
Isaya 61:1-2
Luka Mtakatifu 4:16