Category Archives: Uncategorized

22-0626 Yeye Aliye Ndani Yenu

UJUMBE: 63-1110E Yeye Aliye Ndani Yenu

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi mwenye Imani kuu sana,

Ninajua hii ni barua rahisi tu yenye sarufi isiyofaa, lakini nataka ulimwengu ujue ya kwamba tunaamini kila neno ambalo nabii wetu alisema na kulikubali kuwa ni Bwana Asema Hivi . Tunapomsikia yeye akisema jambo fulani kwenye kanda, tunaliamini, tunalikubali, na kisha tunalipokea kibinafsi kuwa ni Mungu Mwenyewe akizungumza nasi moja kwa moja.

Imehubiriwa, na kuthibitishwa kwelikweli kwa Neno la Mungu, ya kwamba isingekuwa ni mwanadamu, haina budi kuwa ni Mungu.

Tunaamini ishara zilezile za kuonekana dhahiri kimwili zimetukia duniani leo ambazo zilitukia wakati Yesu alipokuwa hapa. Nguzo ile ile ya Moto ambayo Mtakatifu Paulo aliiona ikiwa na Tabia ile ile, ikifanya jambo lile lile, imekuja katika wakati wetu. Ni Mungu anazungumza nasi moja kwa moja:

Ishara zile zile za kiroho ambazo alijitambulisha Mwenyewe kama Masihi, zimemtambulisha leo. Yeye yungali ni Masihi !

Unaweza tu kupokea baraka hizi kuu IWAPO unaamini kila Neno kwa kubonyeza Play ni Bwana Asema Hivi. Ikiwa wewe ni mtu ambaye huamini hivyo, na yakubidi uamue kiakili au kwa kupitia mtu fulani anayekuambia: “Hili ni Neno la Bwana, na hili ni Ndugu Branham tu anayezungumza,” basi hili si kwa ajili yako.

Katika wakati ule Musa alipowaongoza wana wa Israeli, alikuwepo mmoja, huyo alikuwa Musa. Wengine wao walifuata tu Ujumbe. Unaona?

Lakini leo hii, kwetu sisi TUNAOAMINI JAMBO HILO JINSI HIYO, mioyo yetu imejaa furaha na kububujika, ni vigumu sana kujizuia.

Ninajisikia kwamba Yeye ametukomboa. Ninajisikia ya kwamba majina yetu yamo kwenye Kitabu Chake. Ninaamini ya kwamba tumekombolewa kwa Damu ya Mwana-Kondoo .

Kwa sababu tunaamini kuwa Ujumbe huu ni Sauti ya Mungu inayozungumza nasi moja kwa moja, tunakubali hili kuwa ni Mungu Mwenyewe akizungumza nasi mdomo kwa sikio. HAKUNA SHAKA majina yetu yako kwenye Kitabu chake.

Naomba niliweke namna hii, huduma ya Yesu Kristo ikifanyika mwili katika Kanisa Lake katika siku hizi za mwisho. Hivyo ndivyo wengi wetu wanavyoamini. Ninaamini pamoja nanyi.

Hivyo ndivyo hasa sisi tunavyoamini jambo hilo , Yesu Kristo akifanyika mwili , akizungumza na Bibi-arusi Wake kwenye kanda.

Kila mara tunapobonyeza play imani yetu hufikia viwango vipya. Huyu sio tu mhubiri mwingine anayezungumza, huyu ni Mungu Mwenyewe anayezungumza nasi. Tunataka Neno safi peke yake 100% .

Hebu ni kuulize Jambo fulani . Je, William Marrion Branham ndiye mchungaji wako? Je, yeye ndiye Malaika-mjumbe wa saba aliyethibitishwa na Mungu? Je, unaamini alichomwomba Mungu afanye, Mungu alifanya ? Je! unaamini yeye alikuwa ni Sauti ya Mungu kwa wakati huu? Unaamini kila neno alilosema? Basi Jumapili utabarikiwa mara tena isivyoelezeka .

Hakuna njia nyingine unayoweza kupokea baraka hii isipokuwa unasikiliza kanda na kuamini kile unachosikia kuwa ni Bwana Asema Hivi. Huna budi kuamini Kile anachosema ni Mungu ananena nawe moja kwa moja.

Nami, kama mchungaji wenu, ndugu yenu, kwa imani niliyo nayo, nimemwomba Mungu aiweke hiyo juu yenu. Ninaamini kwamba nitapokea kile nilichoomba. Sasa ikiwa mtaamini pamoja nami; kwa imani ile niliyo nayo, ninawapa hiyo sasa hivi .

Kwetu sisi yeye ni mchungaji wetu. Hakuna mtu ulimwenguni aliye na Imani zaidi, au kuu kuliko MCHUNGAJI WETU, nabii wa Mungu. Sasa nabii wa Mungu amemwomba Mungu atupe IMANI YAKE KUU. IKIWA unaamini hilo kwa moyo wako wote, ni IMANI YAKO Hivi sasa….UTUKUFU, TUNAAMINI !!! Imani yetu inaweza kuwa dhaifu, lakini sivyo tena, kwa maana sasa tunayo IMANI yake.

Na sasa, katika Jina la Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, kataeni mateso yenu, magonjwa yenu, na mseme “Huna budi kuondoka,” sababu mnayo imani yenu , na imani yangu, pamoja na nguvu za Yesu Kristo , Ambaye uwepo Wake wa kila mahali upo hapa kudhihirisha jambo hilo na kuthibitisha kwamba Yuko hapa, atawapa afya sasa.

Ninaweza kusema nini kitakachokufanya uje kuungana nasi na kupokea baraka hii kuu? Wazia jambo hilo, chochote unachohitaji, unaweza kukipata kama utakuja kusikiliza na kuliamini kwa urahisi.

Njoo usikilize pamoja na Bibi-arusi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville. ( Ni saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania) Tutakusanyika na kusikiliza kutoka Mashariki, Magharibi, Kaskazini na Kusini, wote kwa wakati mmoja, wakati Bwana Asema hivi ikituzungumzia na kutuambia yote kuhusu: Yeye Aliye Ndani Yenu 63-1110E .

Ikiwa huwezi kusikiliza pamoja nasi kwa wakati mmoja Jumapili, haijalishi, bonyeza play tu wakati wowote na usikilize na uamini kile unachosikia kuwa ni Sauti ya Mungu inayozungumza nawe.

Ndugu. Joseph Branham

22-0619 Nafsi Zilizo Kifungoni Sasa

UJUMBE: 63-1110M Nafsi Zilizo Kifungoni Sasa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Baba Mpendwa, ninaweza kuandika nini leo ili upate kunitumia, kwa njia fulani ndogo, kumtia moyo Bibi-arusi Wako wa thamani?

Mungu amekuja katika wakati wetu na kuishi katika mwili wa mwanadamu, ndani ya mtu aitwaye William Marrion Branham, ili aweze kufunua na kutimiza Neno Lake. Huo ndio Ufunuo wa Yesu Kristo katika wakati wetu.

Kuisikiliza Sauti hiyo na kuamini kila Neno ndiyo njia pekee iliyoandaliwa na Mungu kwa siku ya leo. Alituma ulimwenguni watu wengi waliotiwa mafuta na Roho wake Mtakatifu, Lakini Yeye hutuma na kunena kupitia mtu mmoja tu kufunua Neno Lake na kumwongoza Bibi-arusi Wake.

Yeye kamwe habadilishi Mpango Wake au Njia Yake ya kufanya mambo. Jinsi alivyofanya jambo hilo mara ya kwanza, Yeye hulifanya hilo kila wakati. Yeye huwaongoza watu Wake Mwenyewe, kwa Nguzo ya Moto.

Wewe ni Bibi-arusi mteule wa Mungu na hakuna kitu shetani anachoweza kufanya au kusema ambacho kinaweza kulitoa jambo hilo kwako, HAKUNA! Alikuchagua tangu asili kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Alikujua wakati huo, nawe ulikuwa pamoja Naye wakati huo. Alijua jina lako. Alijua kila kitu kukuhusu. Alijua mema na mabaya yako. Alijua kushindwa kwako, makosa yako, na bado alikupenda, kwa kuwa ulikuwa sehemu yake.

Nafsi yako inaweza tu kujilisha Neno Lake. Hakuna kinachoweza kukutosheleza ila Neno Lake. Unapenda kusoma Neno Lake na kumtafakari Yeye, kuomba kutoka ndani kabisa ya moyo wako, lakini unaposikia Sauti Yake ikizungumza nawe moja kwa moja, inakuinua juu ng’ambo ya pazia la wakati. Kwa maana unajua umeketi naye katika ulimwengu wa roho huku akinena nawe mdomo kwa sikio, akifunua Neno lake, akikukumbusha, WEWE NI BIBI-ARUSI WANGU.

Shetani anaweza kukupiga tena na tena. Unaweza kushushwa moyo sana wakati mwingine na kuhisi wewe ni uliyeshindwa kabisa; Kujisikia kana kwamba umemkosea zaidi ya mtu yeyote yule. Wewe ni mbaya zaidi kuliko waovu wote , lakini mahali fulani, ndani kabisa katika nafsi yako, unasikia ile Sauti Ndogo tulivu ikikuambia: “Hakuna kitu kinachoweza kukutenganisha na Neno Langu, WEWE NI NENO LANGU. Nililiweka jina lako kwenye Kitabu changu cha Uzima cha Mwana-Kondoo, Mimi Mwenyewe.”

Niseme nini ili kukutia moyo leo hii? Bonyeza Play tu kila siku na usikie Sauti ya Mungu ikinena na kukuambia: Bwana Asema hivi.

Umealikwa kuungana na Bibi-arusi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA ., Saa za Jeffersonville,( Ni Saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania ) tunapokusanyika kusikiliza ile sauti ndogo tulivu: 63-1110m Nafsi Zilizo Kifungoni Sasa.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada :

Mwanzo 15:16
Mathayo Mtakatifu 23:27-34
Yohana Mtakatifu 4:23-24 / 6:49 / 14:12
1 Petro 3:18-22
2 Petro 2:4-5
Yuda 1:5-6

22-0612 Kukata Tamaa

UJUMBE: 63-0901E Kukata Tamaa

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa wa Mungu waliofungwa kwa Damu, waliofungwa kwa Ile Ishara, watu wa Agano.

Kumbuka tu, sisi si Hawa, sisi si mmoja wa hawa wenye mashaka wanaopatana na Shetani. Tuna imani isiyotikisika katika Neno hili! Tunashikilia kila Neno la Mungu aliloandika na kunena kwenye kanda. Imetupa IMANI KAMILIFU .

Hatutafuti imani fulani kubwa inayotulazimu kuwa nayo ndani yetu wenyewe . Hatujaribu kuwa wema vya kutosha; hatutawahi kamwe kuwa wema vya kutosha, tutashindwa kila wakati. Hilo silo alilotuambia tuwe na imani nalo. Alisema iweni na imani na kuamini KILA NENO alilosema kuwa ni Bwana Asema Hivi. TUNAAMINI HIVYO na Imetupa IMANI KAMILIFU KATIKA NENO LAKE.

Hebu tusikilize kile ambacho Roho Mtakatifu amekuwa akiripoti na kumwambia Baba kutuhusu sisi.

“Nimetii amri zako. Nilitafuta na nimepata baadhi ya vikundi vidogo vya watu waliotawanyika kote ulimwenguni. Nilituma vijana wa kanda Majumbani kwao na kucheza kanda chache. Waliposikia kanda hizo, waliamini kila Neno. Sasa wamezifanya nyumba zao kuwa kanisa wapate kuupokea Ujumbe huu. Wao ni Tai Wako waliochaguliwa tangu asili wanaokusanyika Pamoja kusikia Neno Lako.

Niliwaambia ya kwamba wote ambao wangekuja chini ya ile Ishara, Ujumbe wa wakati huu, wangeokolewa. Niliwaambia wawe Mmoja na Wewe na Neno Lako. Kama ilitenda kazi kwao, basi waiweke kwa watoto wao Ishara hiyo. Waiweke kwa wapendwa wao na kuwaleta chini ya hiyo Ishara na wao pia wataokolewa.

Niliwaambia waliokuwa Wakisikiliza kanda: Ninawadai kwa Mungu. Waliliamini nilipolisema jambo hilo, kwa mioyo yao yote na nafsi zao zote. Wao ni watu wangu, ndio niwapendao wanaosikiliza kanda hizi.

Niliwaambia angalieni kile Kilichokuja baada ya ile Mihuri Saba: ule muungano wa watu, ishara zilizounganika, kimulimuli chekukundu katika siku za mwisho, Zimetiwa kifuniko katika kitu hiki kimoja, ile Ishara.”

Loo, Kanisa, amka na ujitikise! Finya dhamira yako, amka katika saa hii! Hatuna budi kukata tamaa ama tutaangamia! Kuna jambo linalokuja kutoka kwa Bwana! Ninajua jambo hilo kwamba ni BWANA ASEMA HIVI. Kuna jambo linalokuja, na ni afadhali tukate tamaa. Ni kati ya uzima na mauti. Litapita katikati yetu wala hatutaliona.

Nasi tunajua jambo fulani liko karibu kutukia. Kule Kuja kwa Bwana kutakuwa ni kuondoka kwa ghafla, na kwa siri. Tumekata tamaa. Wakati umekaribia. Tumeitambua ile Ishara kwa ajili ya siku yetu nayo imewekwa.

Tunachukua Mifano ya Pasaka Jumapili hii ambayo ililiwa kwa dharura, katika Nyakati za kukata tamaa. Tunakusanyika ulimwenguni kote, kulizunguka Neno Lake.

Njoo uwe sehemu ya tukio hili kuu Jumapili hii saa 10:00 KUMI JIONI , saa za Jeffersonville,( Ni Saa 5:00 TANO USIKU ya Tanzania?) tunapokusanyika ili kusikia Neno: 63-0901E _ KUKATA TAMAA .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada :

Kutoka 12:11
Yeremia 29:10-14
Luka Mtakatifu 16:16
Yohana Mtakatifu 14:23
Wagalatia 5:6
Yakobo 5:16

22-0529 Imani Kamilifu

UJUMBE: 63-0825E Imani Kamilifu

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi mwenye Imani Kamilifu,

Kwa mara nyingine tena, naona haiwezekani kuweka kwa maneno kile ambacho Ujumbe huu, barua za Upendo wa Mungu wa kibinafsi, zilizoandikwa kwa Damu Yake, zilizonenwa kwa Sauti Yake, zinamaanisha kwetu. Kila kitu kingine hakimaanishi chochote. Tunampenda kutoka ndani kabisa ya mioyo yetu na Ametupa Upendo Mkamilifu Kwa ajili yake . Hakuna kinachoweza kutuondoa kwenye Neno hilo. Hakuna uradhi mwingine katika maisha yetu zaidi ya kumsikia yeye akiwasiliana nasi kama Rafiki kwa rafiki.

Hata sio sisi, ni Yeye anayeishi ndani yetu, akijiita Mwenyewe. Ni kilindi kikiita kilindi. Furaha kamili ya Kubonyeza play na kumsikia Mungu akitumia sauti ya mwanadamu kutuambia, sisi ni wateule wake. Kutuambia alitupenda kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu; kwa maana alijua tungempenda kwa yote yaliyokuwa ndani yetu, na tungedumu kuwa waaminifu Kwake na Neno Lake.

Yote tunayohitaji, Ametupa. Hakuna kinachokosekana. Neno Lake aliliandika kwa namna ya barua na kulihifadhi kwa maelfu ya miaka ili aweze kutuambia Upendo wote uliokuwa moyoni Mwake kwa ajili yetu.

Ndipo upendo wake unakuwa mkuu zaidi kwetu alivyotuambia: “Nitakuja katika mwili mara nyingine tena na kunena nanyi mdomo kwa sikio ili kusiwe na kutokuelewa, kusiwe na Mkanganyiko , kusiwe na haja ya fasiri. Nitachukua muda Wangu na kuwaeleza Upendo Wangu kwenu , nanyi mtaweza kuusikia tena na tena na tena. Nataka mjue, Baba yu ndani Yangu, Mimi niko ndani yenu, ninyi mko ndani Yangu, sisi ni MMOJA. Mwili wenu ni Mwili wangu, mfupa wenu ni Mfupa wangu, roho yenu ni Roho yangu.

Nitawaambieni yote yaliyo ndani ya Moyo Wangu kwa undani sana. Nitaliweka wazi hivi kwamba mtajua bila shaka, Maneno niliyoandika na kunena ni kwa ajili yenu, na hayatashindwa kamwe.

Nitawapa Imani Kamilifu, na Itakuwa ni Mtawala wa kila hali. Haidhuru adui anasema nini, italitawala mkiwa na Imani Kamilifu katika kile Neno Langu linasema mlicho. Haidhuru adui anajaribu kuwaambia nini, hata Msimsikilize. Masikio yenu ni bubu kwa kitu kingine chochote isipokuwa kile ambacho Roho Wangu amekwisha waambieni. Kimetia nanga mioyoni mwenu, na hakuna kitu kitakachowafanya mtoke Kwake.”

Imani hiyo Kamilifu tuliyo nayo katika kuujua Ujumbe huu kuwa ni Bwana Asema hivi, tunaitumia IMANI hiyohiyo KAMILIFU kwa kila ahadi aliyotuambia ni yetu katika Neno Lake. Ikiwa sisi ni wagonjwa na tunahitaji uponyaji, ni wetu. Ikiwa tunahitaji chochote, tunaweza kukipata, kwa kuwa tumetiwa mafuta na Roho Wake. Sisi ni masihi Wake watiwa mafuta wa siku za mwisho, tukionyesha ufufuo wa Yesu Kristo.

Ni tendo la Mapenzi anapojimwaga Yeye mwenyewe ndani yetu. Tunakuwa mmoja Naye kwa ajili ya Karamu hiyo kuu ya Arusi. Roho wake yuko hapa pamoja nasi na ndani yetu. Tuna jambo moja tu la kufanya, nalo ni kuliamini, kulikubali.

Sisi sio Malaika-Mjumbe wa 7 wa Mungu, lakini sisi ni wana na binti zake. Mikono yetu ni Mikono yake. Tunaamini kile kinachonenwa kwenye kanda kuwa ni Bwana Asema hivi. Ni Neno lililo hai.

Nabii wake ndiye mchungaji wetu. Tunaposikiliza Neno lililorekodiwa, tunaamini ni Mungu anayezungumza nasi moja kwa moja. Tuna Imani Kamilifu tukiamini hivyo.

Tunapokusanyika pamoja ulimwenguni kote kumsikiliza Mungu akizungumza nasi kwa njia ya nabii Wake, imani yetu inainuliwa juu zaidi na zaidi Mungu anapomkusanya Bibi-arusi Wake pamoja kwenye Neno Lake lililothibitishwa.

Kesho haitakuwa kama siku nyingine. Tutachukua Imani yetu Kamilifu Aliyotupa na tutaitumia kwa chochote tunachohitaji, nasi tutakipokea wakati Nguzo ya Moto inaponena kupitia mjumbe Wake mteule na kutuambia:

Je, mumeelewa na hayo niliyowatendea? Ninyi mumeniita “mchungaji wenu”; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo. Ikiwa mimi, niliye mchungaji wenu, nimekwisha tambulishwa na Yesu Kristo, ya kwamba mimi ninatenda kazi Yake, basi aminini Neno langu. Kwa kutenda hili tendo la imani, kwa kuweka mikono yangu juu yenu , nimekwisha kuhukumu magonjwa na mateso yanayowasumbua. Aminini hayo, ndipo mtatimiziwa haja zenu, hata ziwe ni nini, kwa maana mambo yote yanawezekana kwa hao waaminio . Na mnapoomba, aminini ya kwamba mmepokea mlichoomba . Nami naamini kabisa ya kwamba napokea, na moyoni mwangu napokea uponyaji wa kila mmoja wenu, naupokea, ya kwamba umetendeka. Naamini, naamini hayo kwa yote yaliyo ndani yangu .

Tunaamini kwa yote yaliyo ndani yetu, Ujumbe huu kuwa ni Sauti ya Mungu, iliyonenwa, iliyorekodiwa, iliyothibitishwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya siku hii. Tunaamini lo lote tuombalo, tutapokea, kwa kuwa ni BWANA ASEMA HIVI NI LETU.

Njoo uungane nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania),ili kupokea chochote unachohitaji tunapomsikiliza nabii wa Mungu akituambia jinsi ya kupokea: Imani Kamilifu 63-0825E .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma Kabla Ya Ibada :

Marko Mtakatifu 11:22-26 / 16:15-18
Yohana Mtakatifu 14:12 / 15:7
Waebrania 11:1 / 4:14
Yakobo 5:14
1 Yohana 3:21

22-0522 Ninawezaje Kushinda?

UJUMBE: 63-0825M Ninawezaje Kushinda?

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Waliyoungana,

Wakati na Umilele vitaungana pamoja wakati Mungu na watu Wake watakapoungana pamoja .

Ninakualika uje uungane pamoja na Bibi-arusi wa Mungu na kusikia Ujumbe 63-0825M Ninawezaje Kushinda? Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville.( Ni saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania).

Ndugu Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Ufunuo 3:21-22

22-0515 Wakati Wa Kuungana Na Ishara Yake

UJUMBE: 63-0818 Wakati Wa Kuungana Na Ishara Yake

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Mwili wa Mwili Wake, Neno la Neno Lake, Uhai wa Uhai Wake, Roho wa Roho Wake,

Mpendwa Bibi-arusi Mtangulizi ,

Tulipoketi pamoja katika ulimwengu wa roho kutoka duniani kote Jumapili iliyopita , tulikuwa tukisikiliza Sauti pekee ya Mungu iliyothibitishwa ikizungumza nasi. Kama kawaida, tulikuwa chini ya matarajio makubwa kusikia kile alichokuwa anaenda kutuambia. Roho Mtakatifu anaenda kutufunulia nini leo?

Huenda tumesikia maneno yake mara nyingi hapo kabla, lakini tulijua siku hiyo ingekuwa tofauti. Tungesikia jambo fulani ambalo hatukuwahi kusikia hapo kabla. Tungepokea Ufunuo zaidi hata ya tunavyoweza kufikiria. Angefungua mioyo yetu, akili zetu na nafsi zetu, na kufunua jambo ambalo lilikuwa SASA HIVI, katika Majira yake Halisi, kufunuliwa.

Kisha linatokea. Maneno makuu sana bwana arusi awezayo kusema na kufunua kwa Bibi-arusi wake, “Wewe ni utimilifu kamili wa Uungu kwa jinsi ya mwili, mtangulizi. Yote niliyokuwa, niliyamimina katika Kristo; yote Kristo aliyokuwa, niliyamimina ndani YAKO . WEWE NI Bibi-arusi-Neno wangu Mkamilifu niliyemchagua . “

Utu wetu wote uliruka kwa furaha. Baba ndo kwanza atuambie, sisi ni Bibi-arusi wake. Sisi ndio wale awapendao. Sisi tumetiwa mimba na Neno lake, na Neno lake PEKE YAKE . Tumbo letu limefungwa kwa kitu kingine chochote. Yeye amekuwa akitungojea sisi, na kutamani kutupata Sisi … SISI !!

Na wajua nini ? Yeye kamwe hakumtuma mtu mwingine kutuambia Maneno haya, Yeye amekuja na kuishi katika mwili wa kibinadamu kwa mara nyingine tena, ili apate kuzungumza moja kwa moja, mdomo kwa sikio, na KUTUAMBIA : “Nakupenda, Bibi-arusi wangu kipenzi .”

Tunapenda kuimba, tunapenda ushirika, tunapenda kukusanyika pamoja na waaminio, Lakini tunachopenda zaidi ya yote ni kusikia Sauti ya Mungu; Hivi asema Bwana, ikinena Nasi moja kwa moja . Kila ujumbe ni Kitu kikuu cha binafsi KWETU . Yeye aliweka kila neno Alilotaka kutuambia kwenye kanda ya sumaku hivi kwamba tuyasikie sisi wenyewe.

Ni kitu gani Yeye atatuambia na kutufunulia Jumapili hii tutakapokusanyika? ni majira gani?

Isaya alinena na kusema, “Bikira atachukua mimba na kuzaa mtoto”, lakini ilikuwa ni miaka 700 kabla ya majira yake ya kutimia. Mfalme Daudi alisema, “Walizua mikono yangu na miguu yangu.” Alizungumza kana kwamba ilikuwa mikono yake na miguu yake, lakini Hayakuwa majira yake yakutimia bado miaka 1,000.

Mungu alinena kupitia nabii wetu katika wakati wetu na kusema mambo mengi yasingewezekana kutimia mpaka leo hii. Tunaona mataifa na ulimwengu wakiungana zaidi ya wakati mwingine wowote. Tulidhani Ukomunisti ulikuwa kitu cha zamani na ulikuwa umesambaratishwa, lakini sasa tunaona ni hai sana na ni chombo mikononi mwa Mungu, kama vile alivyotabiri na kutuambia ulikuwa hivyo.

Ulimwengu ulidhani vita baridi vilikwisha, na hakuna tena tishio la vita ya nyuklia. Lakini leo, tishio la vita ya nyuklia limekuwa ni Halisi. Kila kitu kimewekwa mahali pake kama tu vile alivyotuambia kwamba itakuwa. Haya ndio majira yenyewe .

Jumapili Hii, Yeye kwa mara nyingine tena ATANENA NASI MOJA KWA MOJA , mdomo kwa sikio, nasi tutasikia Jambo kuu lingine ambalo lilinenwa na kuhifadhiwa kwa ajili yetu tu tusikie. Ni kitu gani yeye Atasema na kutufunulia? ni majira gani? Ni Kitu gani kinachotendeka ?

Mungu anamuunganisha Bibi-arusi Wake. Anakusanyika pamoja, kutoka Mashariki na Magharibi, na Kaskazini na Kusini. Kuna wakati wa kuungana, na huo unaendelea sasa hivi. Anaungana kwa sababu gani? Unyakuo.

Basi Ujumbe huu unatenda nini wakati tunaposikiliza Sauti ya Mungu kutoka kote ulimwenguni ? Kumuunganisha Bibi-arusi na Neno. Neno ni Mungu. Bwana arusi ni Neno. Bibi-arusi ni msikiaji wa hilo Neno, nasi Tunakuja pamoja katika muungano. Tunajiandaa kufanya arusi ambapo tunakuwa mmoja na Neno.

Yote aliyo Baba, ndivyo nilivyo Mimi; na yote niliyo Mimi, ndivyo mlivyo ninyi; na yote mliyo ninyi, ndivyo nilivyo Mimi. Katika siku hiyo mtajua ya kwamba Mimi niko ndani ya Baba Yangu, Baba ndani Yangu, Mimi ndani yenu, nanyi ndani Yangu.” Unaona? Katika “siku hiyo.” Siku gani ? Leo hii ! Tunaona zile siri kuu zilizofichwa za Mungu zikifunuliwa. Loo, jinsi ninavyopenda jambo hilo!

Huu ndio wakati wenyewe Hasa . Haya ndio majira yake hivi sasa . Bibi-arusi yuko tayari kwa ajili ya Bwana arusi. Tunasikiliza Tunaposikia kile kilio cha Usiku wa manane “Tazama, Bwana Arusi yuaja!” Tuko kabisa kwenye wakati wa mwisho.

Njoo uungane nasi Tunapoungana kwenye Neno, Jumapili Saa 6:00 SITA MCHANA ya Jeffersonville , ( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Tanzania) Tunaposikia sauti ya Mungu ikituambia ni : Wakati Wa Kuungana na Ishara Yake 63-0818 .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma Kabla ya ibada :

Zaburi 86: 1-11

Mathayo Mtakatifu 16: 1-3

22-0508 Kristo Ni Siri ya Mungu iliyofunuliwa

UJUMBE: 63-0728 Kristo Ni Siri Ya Mungu Iliyofunuliwa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Wapenzi wa Moyo Wake,

Ninayo heshima kubwa zaidi duniani. Bwana ameniruhusu nimtambulishe yeye mwenyewe kwenu, ili aweze kusema nanyi moja kwa moja kupitia chombo alichochagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu ili kunena na kuwafunulia Neno lake lote.

Si mtu wa Mungu tu, Ni Mungu Mwenyewe, Nguzo ya Moto, Roho Mtakatifu akizungumza nawe moja kwa moja, mdomo kwa sikio, nasi tunayo heshima na majaliwa kumwita nabii Wake mteule, MCHUNGAJI WETU.

Kamwe hatujiulizi kama kile tunachosikiliza ni mwanadamu, fikira zake, wazo lake, au fasiri yake ya Neno. Ni Mungu Mwenyewe Akinena nasi BWANA ASEMA HIVI.

Ninajua watu wanakariri tu jambo hilo, lakini sisi tunakunywa ndani . Kwa maana ndicho kitu pekee ambacho hukata kiu yetu na kutosheleza nafsi zetu. Ni Maneno ya Uzima wa Milele. Kwetu sisi, Ni Sauti ya Mungu. Ni Ujumbe wa wakati huu. Kwa hiyo, ni Neno, Sauti, Kanda, SIO KINGINECHO!

Tumeungana pamoja chini ya Kiongozi mmoja kama Israeli wa kale. Mungu Mmoja, aliyethibitishwa kwa Nguzo ya Moto, na kujifunua Mwenyewe kupitia nabii Wake kuwa Neno. Mungu yeye yule, Nguzo ile ile ya Moto, vivyo hivyo leo. Mungu hawezi kamwe kubadilisha asili yake. Mpango Wake hauwezi kamwe kubadilika kutoka kwa kile Alichoanza nacho, kwa sababu Yeye hana kikomo na mpango Wake na mawazo Yake yote ni kamilifu.

Ndiyo maana tuna matazamio makubwa kusikia kile ambacho anaenda kutufunulia siku ya Jumapili. Alisema ya kwamba Yeye amepiga pande zote za ncha zake, ndani na nje yake, na hata alionyesha kwa Maandiko na mpangilio wake wa matukio, mpaka tunajua ya kwamba Ujumbe huu ni Kweli kabisa. Hakuna makosa .

Lakini Jumapili, Roho Mtakatifu ataushika Ujumbe na kuuweka mahali ulipo sasa. Yeye ataujenga tangu pale ulipoanzia, na kuujenga moja kwa moja hadi wakati huu wa sasa.
Hebu tunywe machache tu ya yale Mungu atakayotuambia na kutufunulia kupitia mchungaji wetu siku ya Jumapili:

Ninyi ni mboni ya moyo wangu, wale ambao mmezaliwa kwa Bwana kwa Roho na kwa Neno la Kweli. Ninaomba tu na kumwomba Bwana awabariki na kuwaweka nyinyi kuunganishwa pamoja kwa vifungo vya upendo wa Kristo.

Bwana aliniweka Ni hifadhi Chakula ghalani kwa ajili yenu; mboga zenye afya nzuri, hapa katika maskani hii. Na leo hii, utapokea mzigo mzima wa Kanda . Itakufunulia Yesu Kristo katika saa tunayoishi. Ujumbe huu utawahifadhi na kuwatia nguvu. Utawapa nguvu za kiroho kwa kazi iliyo mbele yenu.

Hebu niwaambieni tena ninajua mnapenda kulisikia jambo hili: Ninyi ndiyo nambari iliyoteuliwa na iliyochaguliwa tangu zamani, ndio watu pekee watakaolisikiliza. Ninyi ndiye Bibi-arusi mteule ambaye hataanguka bali atashikilia Neno hilo bila kujali wengine wote ulimwenguni kote wanasema nini kuhusu hilo. Wewe ni Bibi-arusi Neno!

Mungu amekufunulia siri hii kuu, na huko ndiko Kuzaliwa upya. Sasa anakuleta pamoja ambapo ufunuo ulipo katika upatano mkamilifu. Mungu akilidhihirisha kupitia Neno Lake kwa matendo yale yale, mambo yale yale aliyofanya, akilidhihirisha Neno ndani yako.

Usisahau kamwe, Roho Mtakatifu, peke yake, ndiye Mfunuzi wa ufunuo wa Kiungu wa Kristo, na amekuwako katika nyakati zote. Kumbuka, Nyakati zote ! Neno la Bwana lilikuja kwa nani? Nabii, peke yake.

Ninatambua kuwa ninazungumza na maelfu kwenye kanda, tuna huduma ya kanda kote ulimwenguni. Na inaonekana kuwa tunaweza kutengeneza kanda kutoka hapa ambayo ni bora mara kumi kuliko mahali popote pengine . Ninatumai tu kila mwanamume anayesikia kanda hii, na kila mwanamke, ataelewa.

Sasa ni juu yao ikiwa wanataka kusikiliza kanda yoyote , lakini sitaki mlikose hili. Enyi watu wa kanda; huko msituni na popote mnapoisikia, sasa sikilizeni.

Tunazo kanda  kuhusu kile tunachoamini. Tunazo kanda zinazohusu nidhamu kanisani, jinsi tunavyoenenda sisi wenyewe katika kanisa la Mungu, jinsi tunavyopaswa kuja hapa pamoja na kuketi pamoja katika ulimwengu wa roho.

Natumai kila mtu kwenye kanda analipata jambo hilo. Ukishindwa, rudi kwenye kanda  hii tena . Sijui nitakuwa nanyi kwa muda gani zaidi. Kumbukeni, Hii ​​ndiyo Kweli, ya BWANA ASEMA HIVI. Ni kweli. Ni Maandiko .

Uongozi na Mwili umekuwa kitu kimoja. Ni Mungu akidhihirishwa ndani yenu , watu Wake. Hiyo ndiyo sababu mume na mke si wawili tena; wao ni mmoja. Mungu na Kanisa Lake ni mmoja, “Kristo ndani yenu,” ufunuo mkuu wa Mungu.

Sio wazo langu; ni Nguvu Zake, ni Neno Lake. Aliliahidi ; ndilo hili hapa. Alisema lingekuwa hapa, ndilo hili hapa. Ninyi ni wana wa Mungu. Si kwamba mtakuwa ; MKO SASA HIVI!

Jaza kikombe chetu Bwana, tunakiinua juu, Bwana, njoo ukate kiu ya roho zetu. Mkate wa Mbinguni, utulishe, hadi tusihitaji zaidi. Jaza kikombe chetu, kijaze mpaka pomoni na utufanye tuwe wazima.

Ni wakati wa jinsi gani wa uamsho tutakaokuwa nao ulimwenguni kote tutakapokusanyika Jumapili ili kusikia: Kristo Ni Siri ya Mungu iliyofunuliwa 63-0728 saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville.( ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Tanzania ).

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma kwa maandalizi ya kusikiliza Ujumbe :

Mathayo Mtakatifu 16:15-17

Luka Mtakatifu Sura ya 24 yote

Yohana Mtakatifu 5:24 / 14:12

1 Wakorintho Sura ya 2 yote

Waefeso Sura ya 1 yote

Wakolosai Sura ya 1 yote

Ufunuo 7:9-10

22-0501 Mungu Hamwiti Mtu Hukumuni Bila Ya Kumwonya Kwanza

UJUMBE: 63-0724 Mungu Hamwiti Mtu Hukumuni Bila Ya Kumwonya Kwanza

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa kamani ndogo , springi kuu, ama chochote ulicho :

Sote ni Mwili wa Kristo, katika mahali petu, katika upatano, tukijaribu kufanya kazi vizuri sana tuwezavyo kwa ajili Yake. Hakuna kitu kingine muhimu kwetu, ila Neno Lake, Ujumbe huu.

Tunapenda tu kusikia nabii wa Mungu akituambia : “Kuna jambo fulani juu yenu watu fulani. Ninyi ni watu maalum katika maisha yangu. Kuna kitu kingine ambacho napenda tu kukutana nanyi na kuzungumza tu nanyi ”.

“Naangalia huku kwenye huduma yangu ndogo nyenyekevu; Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele, nami naona kile inachofanya; inaita na kuunganisha kundi la Bibi-arusi pamoja. Nikutoa Gurudumu kutoka kwenye gurudumu.”

Tunajua si mwanadamu, ni Neno la Mungu linalomkusanya Bibi-arusi Wake pamoja. Mambo ambayo tunaona yakitekelezwa si kitu mbali na Mungu. Hakuna tena huenda ikawa ndivyo, ingewezekana , inaonekana kana kwamba huenda ikawa, NI MUNGU!!

Tumefika mahali hapo kwamba Ndio Lulu ya thamani kubwa kwetu. Tumeachana na chochote mtu yeyote anachotuambia kinyume Chake. Hatuangalii kile mwanadamu ametimiza. Tunaangalia kile Mungu amesema na kile Yeye ameahidi angefanya katika Siku yetu, nasi tunamwona Yeye akikifanya.

Huo ndio Mkataa wetu. Kila kitu tulicho sisi, kila kitu tulichokuwa, kila kitu tunachotumaini kuwa, kimewekwa juu ya Ujumbe huu. Ni zaidi ya uhai kwetu.

Ni kama Haijawahi hapo kabla katika historia ya ulimwengu, tunamwona Mungu akitoa onyo, Jiandaeni kwa ajili ya hukumu. Bomu za atomiki ziko kwenye mabanda yake, kila kitu kiko tayari.

Wakati huu, si kwa kikundi kidogo tu cha watu, kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu, au katika siku za Ibrahimu; ni Mungu akiwaonya watu wa ulimwengu mzima, akinena kupitia nabii Wake, hili ndilo onyo lenu la mwisho.

Yeye Anatuambia, “Kabla sijaruhusu jambo hili litukie, ninatoa wito wa mwisho, kama tu nilivyofanya Sodoma, Tokeni kwake. Iweni tayari. Jambo fulani litatukia ”.

Ulimwengu unategemea ufanisi wao mkuu wa sayansi; uzalishaji wa kisayansi umeleta mauti kwa vizazi. Walio werevu na wenye elimu wanaingia upande wa kiakili : UMOJA WA MATAIFA , NATO, Shirikisho la Mataifa. Kila siku tunaona hukumu ikikaribia zaidi na zaidi. Kile nabii alichoona tokea mbali na kutuambia kingekuja kutokea, kinatendeka: Urusi, Vita, Mafuta, Vatikani, Wayahudi, Mabomu ya Nyuklia.

Hakuna tena kujiuliza nini kitatokea. Tunaliona likitendeka kila siku, na hofu duniani ni Hakika na inazidi kuwa kubwa zaidi na zaidi kila siku.

Lakini ni kama tu alivyofanya katika siku za Hezekia, wakati Mungu aliponena kupitia nabii wake na kuwaonya watu, “ Tengenezeni Mambo , kwa kuwa hukumu iko tayari kuanguka”. Nabii wake alikuwa akiwatayarisha watu kwa ajili ya wakati ule uliokuwa unakuja.

Nuhu aliwatayarisha watu kwa wakati wake. Ulikuwa ni wito wa rehema kabla ya hukumu. Mungu alikuwa na njia iliyoandaliwa, nabii wa kuwaongoza.

Aliwatumia Neno Lake. Naye daima hulituma Neno Lake kwa nabii Wake, kama alivyofanya katika wakati wa Nuhu. Alifanya jambo lile lile katika siku za Nuhu. Katika siku za Eli-…za Musa, tunaona Yeye alifanya jambo lile lile. Aliwatumia nabii Wake, nao wakajitenga na kutokuamini. Sasa, watu wa jinsi hiyo ndio waliotoka. Hao ndio walioliamini.

Tumejitenga na kutokuamini kote. Mungu anayo njia iliyoandaliwa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake leo. Alituahidi katika Neno Lake, “Kabla ya hukumu, nitawapelekea nabii kulikusanya Kundi langu dogo nyenyekevu, nami nitawaketisha upande mmoja, nao watakuwa na amani, wakiingojea hukumu ijayo na kuiepuka. ”.

Sisi ndio kundi lile dogo. Sisi ndio wale ambao Baba anaowapenda nasi tunangojea kwa hamu kubwa Ujio wake wa hivi karibuni . Ulimwengu unaporomoka pande zote kutuzunguka, lakini sisi tuko katika pumziko na amani.

Tunajua tuko katika mapenzi yake makamilifu. Haijalishi tuko wapi ulimwenguni, Mungu ana njia iliyoandaliwa kwamba sisi sote tunaweza kuungana pamoja kwenye Neno Lake, kwenye Sauti Yake. Ni njia iliyoandaliwa na Mungu.

Naye huyu nabii akawaongoza kwenye njia iliyoandaliwa na Mungu. Sasa, hiyo ndiyo njia ya Mungu ya kufanya mambo. Unaona?

Njoo uepuke hukumu ijayo pamoja nasi na usikilize:  63-0724 Mungu Hamwiti Mtu Hukumuni Bila ya Kumwonya Kwanza , Jumapili hii saa 6:00 Sita MCHANA , saa za Jeffersonville (Ni Saa 1:00 Moja JIONI ya Tanzania). Ni Sauti ya Mungu ikinena na kutuambia: Hii ndiyo njia Yangu iliyoandaliwa kwa ajili ya Siku hii.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kwa maandalizi ya kusikiliza Ujumbe :

Isaya 38:1-5

Amosi Sura ya 1 yote.