22-1127 Ndoa Na Talaka

Ujume: 65-0221M Ndoa Na Talaka

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 14MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Mpendwa kundi la Nabii,

Kumbuka, ninasema jambo hili kwa kundi langu tu. Na huko nje hewani, ninasema hili kwa wafuasi wangu mwenyewe. Ujumbe huu ni kwa ajili yao tu, na yale nitakayosema hapa.

Mhudumu ye yote, yeye, hao ni wake, ndiyo, yeye ni mchungaji wa kundi, acha atende cho chote anachotaka. Hilo ni juu yake na Mungu. Kasisi ye yote, mhubiri ye yote, hiyo ni juu yako, ndugu yangu.

Ninazungumza tu hapa Jeffersonville, mahali pekee ambapo ningezungumzia jambo hili , ni kwa sababu ni kundi langu mwenyewe . Ndilo kundi ambalo Roho Mtakatifu amenipa kulifahamu na kuwa msimamizi wake , ataniwajibisha kwa ajili yake . Na watu hawa wangu wamekuwa waongofu hapa kutoka nchini kote, ambao nimewaongoza kwa Kristo .

Ni jiwe la kifuniko kwa wikendi ya Shukrani jinsi gani . Ninashukuru sana kuwa sehemu ya kundi hilo dogo ambalo bado analisimamia pamoja na kila mmoja wenu. Hakuna mahali pengine ambapo tunaweza kwenda.

Baba ametutumia tai mkuu arukaye ili kumwongoza Bibi-arusi Wake. Kuna sauti nyingi zinazowatia moyo watu na kunena Maneno ambayo yaliyonenwa na nabii wake, lakini kuna SAUTI MOJA tu iliyotumwa kumuongoza na kumuunganisha Bibi-arusi Wake.

Maneno ambayo nabii wa Mungu aliyonena kwenye Kanda ni Yakini yetu. Tunaeleweka vibaya kwa sababu tunasema tunaamini KILA NENO, lakini tuliamriwa na nabii wa Mungu kufanya hivyo hasa.

Nasema vivyo hivyo katika Jina la Yesu Kristo. Usiongeze kitu. Usiondoe—kuliwekea mawazo yako. Wewe sema tu yaliyosemwa katika kanda hizo. Tenda sawasawa kabisa na vile Bwana Mungu amekuamuru kutenda. Usiongezee Kwake.!

Amka ulimwengu. Muda umekaribia. Maneno aliyosema nabii wa Mungu, MUNGU AMETUAMURU ; Kuamini, kusema na kutenda, HASA yale aliyosema kwenye kanda. Si kile ninachosema, si kile kuhani ama wahubiri wenu wanayosema, bali yale nabii wa Mungu aliyosema KWENYE KANDA .

Hakuna kitu muhimu zaidi kuliko kusikia Sauti Hiyo kwenye kanda, HAKUNA. Tutaenda kuhukumiwa kwa yale yaliyonenwa KWENYE KANDA . Sio kwa niliyosema, bali yale ALIYOSEMA YEYE .

Nakutakia YALIYO BORA SANA. Maneno yangu machache ni ya kuwatia moyo, kama vile mchungaji yeyote apaswavyo, kuamini kila Neno. Siwafundishi : kutilia shaka jambo lolote mnalosikia kwenye kanda, kuna makosa kwenye kanda, hamna budi kunisikia mimi kadiri mpaswavyo kumsikia nabii. Nawaandikia maneno machache ya kuwatia moyo DUMUNI NA NENO LA ASILI, BONYEZA PLAY. Ninawataka muwe Bibi-arusi Neno safi, asiyeghoshiwa.

Mungu aliruhusu Maneno Yake yarekodiwe katika siku hii ili kila kiumbe hai kiweze kusikia Sauti Yake. Katika siku za Paulo, walikuwa na waandishi wa kuandika yale aliyokuwa akihubiri, ambayo ni Biblia. Lakini LEO, Mungu alitaka iwe KUU zaidi. Tunaweza Kubonyeza Play na kumsikia kwa masikio yetu wenyewe Yesu Kristo aliyefufuka akizungumza nasi, mdomo kwa sikio.

Ni siku ya jinsi gani tunayoishi. Huku ulimwengu wa kawaida ukiporomoka karibu nasi, tuna mahali palipoandaliwa ambapo tunaweza kwenda na kupumzika tu. Tunapapata kwenye KANDA. Tumeziweka katika vyumba vyetu baridi na kufanyia karamu Chakula Kilichohifadhiwa ambacho kimehifadhiwa katika ghala. Nabii wetu anaweza kuwa ameondoka muda mrefu, lakini bado tunangali tunakumbuka mambo haya ni kweli, na tunafanya kama vile Mungu alivyotuamuru kufanya, DUMUNI NA HIZO KANDA.

Njoo uwe na karamu iliyo bora ya Shukrani ambayo hujawahi kamwe kula Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, ( Ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya tanzania) Wakati Sauti ya Mungu inapozungumza nasi Ujumbe: Ndoa Na Talaka 65-0221M .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma Kabla ya Kusikiliza Ujumbe :

Mathayo Mtakatifu 5: 31-32 / 16: 18 / 19: 1-8 / 28:19
Matendo 2:38
Warumi 9:14-23
1Timotheo 2:9-15
1Wakorintho 7:10-15 / 14:34
Waebrania 11:4
Ufunuo 10:7
Mwanzo sura ya 3 yote
Mambo ya Walawi 21:7
Ayubu 14:1-2
Isaya 53 yote
Ezekieli 44:22