22-1204 Huyu Melkizedeki Ni Nani?

Ujume: 65-0221E Huyu Melkizedeki Ni Nani?

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 10MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Mawazo ya Mungu,

Natumai uko tayari kwa Jumapili hii. Nena kuhusu jinsi mioyo yetu itakavyowaka ndani yetu anaponena nasi njiani katika nyumba zetu na makanisa yetu…SUBIRI TU!

Katika mwezi huu uliopita Ametuambia tuhakikishe tunaingia katika Merikebu sahihi…na tuko. Alituambia ya kwamba Uzao halisi wa Mungu hautarithi pamoja na kapi…ndipo akasema, SISI NDIYO UZAO HUO. Kisha, tukasikia kwa masikio yetu, Mungu akinena kupitia mwanadamu na kututangazia, Leo, Maandiko haya yametimia mbele ya yaya haya macho yetu.

Alituambia Jumapili iliyofuata kwamba tuko katika Mahali palipoandaliwa na Mungu pa Kuabudia, na kwa sababu tuko, HATUJAFANYA uzinzi na Neno Lake. Kwa hiyo, sisi ni Bibi-arusi Neno Bikira Safi wake.

Jumapili hii, Yeye atatuunganisha sisi sote kwa mara nyingine tena na kunena kupitia Malaika-Nabii Wake mkuu na kutuambia, MIMI NDIMI HUYU MELKIZEDEKI, nami ninajidhihirisha kwenu katika mwili wa kibinadamu, kama vile nilivyosema nitafanya katika Neno Langu.

UTUKUFU! Je, umefuraishwa? Je, umebarikiwa Kusikotamkika? Vema, KUNAYO MENGI ZAIDI YAJAYO. Anaenda kukamilisha hadithi hii kuu.

Wazia Hilo, TULIKUWA katika mawazo hasa ya Mungu tangu mwanzo. Miaka elfu nne kabla ya Yesu hajaja duniani, na miaka elfu kadhaa kabla hujaja duniani, Yesu, katika Mawazo ya Mungu, alikufa kwa ajili ya dhambi zetu. NA KISHA , MAJINA YETU yakawekwa kwenye Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo.

Je, hilo linazama niani mwako? Majina yetu yaliteuliwa na Mungu na kuwekwa kwenye Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo kabla kabisa ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Alijua macho yetu, kimo chetu, chochote tulicho. Tulikuwa katika mawazo Yake hapo mwanzo….katika mawazo ya Mungu! Basi, kitu pekee tulicho ni Neno la Mungu lililodhihirishwa. Baada ya Yeye kuliwaza, akalinena, nasi hawa hapa.

Ni vigumu kuelewa. Mungu akituambia mambo haya yote. Alitupenda sana hivi kwamba alitaka kuhakikisha kwamba tutalisikia moja kwa moja kutoka Kwake Mwenyewe , hivyo akafanya irekodiwe ili kwamba Jumapili, Desemba 4, 2022, Angeweza tena kumleta Bibi-arusi Wake pamoja na kutuambia: “Nilifanya haya yote kwa ajili yako wewe. Nilitaka ulisikie moja kwa moja kutoka Kwangu. NAKUPENDA. WEWE NI BIBI-ARUSI WANGU. NAKUJA KUKUCHUKUA HIVI KARIBUNI .”

Ndiyo maana tunajua tunapoingia katika Uwepo wa Mungu, kitu fulani ndani yetu kinatuambia ya kwamba tunatoka mahali fulani, nasi tunarudi tena kwa Nguvu hizo zinazotuvuta.

Mungu ameondoa kinyago kwenye kitu hicho chote na tunaweza kukiona. Mungu, en morphe, aliyetiwa kinyago katika Nguzo ya Moto. Mungu, en morphe, katika Mtu aliyeitwa Yesu. Mungu, en morphe, katika Kanisa Lake. Mungu juu yetu, Mungu pamoja nasi, Mungu ndani yetu; Mungu Anayejidhili.

Hatuna chochote cha kuogopa. Hakuna cha kuhofia, hata kifo. Tunapoondoka hapa, hata hatujafa. Nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii  ikiaribiwa, tuna nyingine TAYARI inayotungoja, En morphe.

Ni Vigumu Kwangu kungojea kumsikia akizungumza nasi na kufunua mambo haya yote Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville. (Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Tanzania) Njoo uungane nasi Katika mahali pekee unapoweza kusikia SAUTI YA MUNGU iliyothibitishwa ikikuambia mdomo kwa sikio Yeye NI NANI , sisi ni NANI na tunaelekea wapi. BONYEZA PLAY.

Huyu Melkizedeki Ni Nani? 65-0221E

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma Kabla ya Kusikiliza Ujumbe :

Mwanzo Sura ya 18 yote
Kutoka 33:12-23
Yohana Mtakatifu 1:1
Warumi 8:1
2 Wakorintho 5:1
2 Wathesalonike 4:13-18
1Timotheo 3:16 / 6:15
Waebrania 7:1-3 /13:8
Ufunuo 10:1-7 / 21:16