All posts by admin5

26-0208 Maswali na Majibu #3

UJUMBE: 64-0830M Maswali na Majibu #3

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Aliomzalia Kristo,

Mtu anawezaje kuuweka katika maneno matupu ya kibinadamu upendo na furaha iliyo mioyoni mwetu kuujua Ufunuo wa kweli wa Neno Lake kwa ajili ya siku yetu? Kuwazia, hatukuwa na uhusiano wowote nalo, lakini YEYE, Yule MIMI NIKO aliye Mkuu, kwa uchaguzi Wake Mwenyewe, Yeye alituchagua SISI kimbele kuwa na kitu kikubwa zaidi ambacho angeweza kutupa, UFUNUO WA NENO LAKE KWA AJILI YA WAKATI WETU.

Yeye alingoja, hadi utimilifu wa wakati ulipotimia, atupulizie pumzi ya uhai ndani yetu, ili tuweze kumsikia Yeye akizungumza nasi na kusema:

Sasa, nimejaribu kadiri niwezavyo ku—ku—kuwaarifu ninyi watu na kuwaongoza kama baba angewaongoza watoto wake. Ninyi mu watoto wangu; nimewazaa katika Kristo kwa Injili hii ninayohubiri. Ona? Nami—ni—ni—ninawatakeni mkuze watoto waliokomaa vilivyo, au—au watoto. Nami nataka kuwakabidhini Kristo siku hiyo, kama vile Paulo alivyosema, “Bikira safi.” Hakuna kitu katika Neno ila lile moyo wako utaitikia kwa “amina.”

Mungu, akinena kupitia malaika Wake mwenye nguvu, anatuelekeza na kutuongoza, Bibi-arusi wa Yesu Kristo. Sisi ndio bikira Wake safi, watoto waliyokomaa. Na kwa neema Yake ya ajabu, tunaliitikia kila Neno tunalosikia kwa AMINA! Ndio fasiri kamilifu ya Neno lenye thibitisho la Kiungu!

• Ikiwa Sauti tunayoisikia kwenye kanda ndio: fasiri kamilifu ya Neno, ni kitu gani kingine ambacho Bibi-arusi wa Yesu Kristo anachohitaji?… HAKUNA!

Yeye ametuchagua SISI, kundi Lake dogo alilolichagua kwa mkono Wake, ili tuwe na Ufunuo wa kweli wa Neno Lake la wakati wetu. Sisi ndio aliowachagua kuwapo duniani, katika miili ya nyama, wakati wa ile miaka elfu moja ya Utawala wa Miaka Elfu.

Enyi marafiki, hebu tulizungumzie hilo kwa dakika moja.

Tutakuwa na mwili uliotukuzwa papa hapa duniani. Tutakuwa tukila, tukinywa, tukijenga majumba, tukiishi kama tunavyoishi sasa kwa miaka elfu moja. Itakuwa ni fungate yetu ambapo Bibi-arusi (SISI) na Bwana harusi (Bwana Yesu Kristo) wamefanyika MMOJA.

Tunakesha na kungoja wakati huu mtukufu kila dakika ya kila siku. Uko karibu sana kiasi kwamba inaonekana kama tunaweza kuugusa. Ninaamini, kwa moyo wangu wote, hili ndilo linalotendeka kwetu sisi leo:

Loo, huo muungano wa kiroho wa Kristo na Kanisa Lake sasa, wakati mwili unapofanyika Neno, nalo Neno linafanyika mwili, linadhihirishwa, linathibitishwa. Vile vile hasa Biblia ilivyosema ingetendeka katika siku hii, inatendeka, siku baada ya siku. Mbona, inalundikana upesi sana huko nje, katika yale majangwa, na mambo yanayotendeka, hata nisingeweza kufuatilia jambo hilo. Tuko karibu na kule Kuja kwa Yesu, kuunganishwa na Kanisa Lake, ambapo Neno linafanyika Neno.

Kwa kila Ujumbe tunaosikia, ndivyo Yeye anavyozidi kutupata Ufunuo zaidi. Unalundikana upesi sana hivi kwamba hata hatuwezi kufuatilia jambo hilo. Tunaliona Neno likifanyika Neno zaidi ya wakati wowote. Hakuna shaka moja hata chembe; kwa Ufunuo, tunajua sisi ni nani haswa.

Yeye anamuunganisha Bibi-arusi Wake kama vile tu alivyosema angefanya, nasi tu sehemu ya hilo. Tunaliona likitendeka kwa macho yetu wenyewe. Wengine huenda wasilione ama kulielewa. Hilo si kwa ajili yao, NI KWA AJILI YETU SISI, WATOTO WAKE ALIOWAZAA.

Bibi-arusi walikuwa na maswali ya kumuuliza nabii.

Je, inatosha kusikiliza Sauti ya Mungu PEKE YAKE kwenye kanda? Mungu alijibu na kusema: NDIYO!!

Je, watoto wetu pia wanaweza kupata kila kitu wanachokihitaji ili kuwa Bibi-arusi wa Kristo kwa kusikiliza kanda tu: NDIYO!!

Kwa hivyo, Kila kitu Bibi-arusi anachokihitaji kipo KWENYE KANDA.

Pia tunajua Mungu ameziandaa njia zingine nyingi kwa ajili ya watoto Wake.

“Kwa kupigwa Kwake wewe uliponywa.” Sasa, kwanza Neno linasema hivyo, hilo linapaswa kutosha, lakini ikiwa huliamini katika Neno, basi kuna karama Kanisani, kama vile wanaume waliovuviwa kujua jinsi ya kufundisha hilo, hilo litafanya liwe wazi kwako, ndilo, na imani ya kuamini.

Tunashukuru mno Mungu amewaandaa wanaume waliovuviwa kujua jinsi ya kufundisha uponyaji na Neno Lake ili kulifanya wazi kwa wengine, lakini Bibi-arusi Wake anataka NJIA YAKE KAMILIFU ILIYOANDALIWA ITOSHELEZAYO. Ndiyo tu TUNAYOHITAJI.

Ningependa kuwaalika muungane na Maskani ya Branham Jumapili hii saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 2:00 USIKU ya Afrika Mashariki) tunaposikia: Maswali na Majibu #3 64-0830M.

Ni jambo la kupendeza vipi kuwa na Ufunuo wa Neno Lake na kujua kwamba sisi ni Neno lililofanyika mwili.

Ndugu Joseph Branham

26-0201 Maswali na Majibu #2

UJUMBE: 64-0823E Maswali na Majibu #2

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wana Tai,

Palipo na Mzoga, hapo ndipo Bibi-arusi watakapokusanyika. Na kwetu sisi, kuna mahali pamoja tu pa kamilifu tunapoweza kuipata hiyo nyama mbichi ya Mana: kwa kubonyeza play na kuisikia Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.

Nena kuhusu Mana MPYA, Je, hivi tunaweza hata kuanza kuwazia kile tulicho nacho katika ncha ya vidole vyetu? Sauti halisi ya Mungu ikizungumza na Bibi-arusi Wake mpendwa kwenye kanda, ambapo hakuna kubahatisha, hakuna kushangaa, hakuna kuhoji wala kutilia shaka kile tunachokisikia ni Mungu, akitumia sauti ya mwanadamu, kunena Bwana Asema Hivi kwa Bibi-arusi Wake.

Kwa ufunuo, tunaamini ndipo mahali PEKEE tunapoweza kwenda na kuzipumzisha nafsi zetu kwamba Maneno tunayoyasikia si neno la mwanadamu, wala fasiri yake au wazo lake halijaongezwa Kwake, bali ni Neno safi la Mungu likizungumza nasi wana tai, akilifunua Neno Lake.

Tunashiriki kwenye Neno. Tunalisoma Neno Lake katika Biblia zetu.  Hata tunawasikia watu waliyowekwa wakfu na kuitwa waliojazwa na Roho Wake Mtakatifu, wakilinukuu na kulihubiri Neno la Mungu, bali katika wakati wetu, Mungu ameandaa mahali ambapo sisi tunaweza kulisikia NENO Lake KAMILIFU LIKINENWA, kwa kubonyeza Play.

Baba hata Yeye anampa Bibi-arusi Wake fursa ya kuuliza maswali yaliyokuwa mioyoni mwetu ili tupate jibu lililo kamilifu:

  • Je, Shetani anaweza kutumia karama za lugha au ya unabii katika mtu aliye na Roho Mtakatifu?
  • Yesu alimaanisha nini katika Mathayo 12, mstari wa 32?
  • Tafadhali fafanua Wakorintho wa Kwanza 13:8-12.
  • Je, wanawake wanaruhusiwa kufanya kazi katika mahali pa umma hali wakiwa na waume wenye afya na watoto?
  • Je, ni kosa kwa mwanamke kusokota nywele zake?

Mungu ameandaa njia nyingi sana za kumbariki na kumtia nguvu Bibi-arusi Wake, lakini kuna mahali pamoja tu Yeye alipopaandaa ambapo Bibi-arusi Wake wanaweza kuwa na ujasiri 100% kuwa kile wanachokisikia ni NENO LAKE KAMILIFU. Chemchemi Moja ya Maji ya Uzima ambapo Wana tai wanapoweza kunywa ambapo hakuna uwezekano wa vimelea vyovyote. BONYEZA PLAY.

Ninakualika uje kunywa kutoka kwenye Chemchemi hiyo Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 2:00 USIKU ya Afrika Mashariki) ambapo tutasikia 64-0823E “Maswali na Majibu #2.”

Ndugu Joseph Branham

26-0125 Maswali na Majibu #1

UJUMBE: 64-0823M Maswali na Majibu #1

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Maskani Ya Branham,

Salamu kwa Bibi-arusi wa Yesu Kristo waliopo kote ulimwenguni, wanaoamini Maskani ya Branham, Sauti ya Mungu, ndio kanisa lao la nyumbani ambapo wanalishwa kiroho kwa Mana iliyofichwa ambayo imehifadhiwa na kutunzwa kwa ajili ya Bibi-arusi wa Kristo.

Hiki ndicho kituo changu cha nyumbani; haya ndiyo makao yangu makuu; hapa ndipo tumeimarika. Sasa, shikilia hilo mawazoni haijalishi itakuwaje. Sasa, kama mna busara, mtashika jambo fulani. Haijalishi itakuwaje, haya ndiyo makao yetu makuu, papa hapa!

Waamini wengi wamekuwa wakielewa vibaya au kuweka wazo lao wenyewe au fasiri yao wenyewe kwenye kile nabii alichosema hapa, bali yeye anamwambia Bibi-arusi moja kwa moja, “kama mna busara, mtashika jambo fulani, haya ndiyo makao yetu makuu, papa hapa!”

Alimaanisha nini kwa jambo hilo?

Ndugu Branham alipokuwa hapa, wengi hawakumwelewa nao walidhani Bibi-arusi alipaswa kwenda Arizona na kumfuata yeye huko, ili waweze Kunyakuliwa. Ndugu Branham aliwajibu waziwazi: KAENI HAPA, HAPA NDIPO MAHALI PENYEWE.

Kundi kubwa mno lao waliondoka hivyo, nao walitaka kuenda hivi na kufanya yale baada ya mimi kuwaambia wakae pale. Kaeni pale, kaeni papa hapa; hapa ndipo mahali panapofaa.

Watu waliondoka kutoka kila mahali kote Marekani kwenda Arizona, lakini yeye aliwaambia waziwazi: Kaeni papa hapa, hapa ndipo mahali penyewe!

Kaeni Jeffersonville? Hivyo ndivyo yeye alivyosema!

Ufunuo wangu ni kwamba, ilikuwa ni Mungu, akizungumza kupitia nabii Wake na kuwaambia watu, “KAENI NA KANDA.” Hapo ndipo MAHALI PENYEWE!

Alikasirika mno na akasema ilibidi afanye jambo fulani kuhusu watu hao wote. Yamlazimu afanye nini? Angewapeleka kwenye kanisa gani? Wao wanapaswa waende wapi? Ndugu Branham alisema inamlazimu afanye nini?

Kwa hivyo sasa, yanipasa kuwarudisha hao watoto hapa wapate kula. Wako chini kule jangwani wakiumia kwa njaa.

Yeye hakusema ati wangehitaji kwenda kwenye kanisa la mahali na kupata vipande vidogo ambavyo wangeweza kula. Yeye alisema lazima AWARUDISHE HAPA wapate kula, la sivyo WANGEKUFA KWA NJAA.

UFUNUO WANGU, Enyi MARAFIKI.

Sasa, msimwelewe vibaya kwa mara nyingine tena, au kusema kitu fulani ambacho hakusema, kwa kusema, “Ndugu Branham alitaka kila mwamini ahamie Jeffersonville ili kuwa Bibi-arusi.” Ndugu Branham aliwajua watu hao wote, na KILA mwamini kutoka kote ulimwenguni, hawangeweza kuhamia na kuishi Jeffersonville. Hilo lisingewezekana. Kwa hivyo yeye alimaanisha nini? Yeye alikuwa ANAMUUNGANISHA Bibi-arusi wa Kristo kwenye KANDA ambazo zilikuwa zimerekodiwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya Bibi-arusi kuzila.

Ujumbe huu, Sauti Hii, ndilo Neno la Mungu Lililonenwa kwa ajili ya siku hii nalo Litamuunganisha na kumkamilisha Bibi-arusi wa Yesu Kristo.

Mzoga ni kile anachokula tai. Sasa, tai huhesabiwa katika Biblia, nabii. Nabii ni tai. Mungu—Mungu hujiita Mwenyewe Tai, nasi tu “wana tai” basi, wa—waamini. Mwaona? Na mzoga waulao ni nini? Ni Neno. Po pote lilipo Neno, tabia halisi ya ndege itajidhihirisha yenyewe.

Liko wapi Neno la Bwana lililo safi, lililothibitishwa, lisilo na mkanganyiko, Bwana Asema Hivi kwa ajili ya siku hii? Kuna mahali pamoja tu, kwenye Kanda.

Ningeweza kuendelea na kuendelea, nukuu kwa nukuu, lakini Ujumbe huu na kile Ndugu Branham alichosema kinahitaji Ufunuo kutoka kwa Mungu. Yatupasa kusoma katikati ya mistari kwa ufunuo, bali tuseme kile yeye alichosema. Kwa maana ni NENO SAFI.

Maswali na Majibu ya leo na kile MIMI NINACHOAMINI.

Leo, wahudumu wengi wanawaambia watu kwamba kwa sisi kuwa na Kanisa La Kanda La Nyumbani tumetoka nje ya Neno na kile Ndugu Branham alichosema tufanye. Wao wanahisi ni lazima tuende kwenye kile wanachokiita na kukichukulia kanisa.

Kuna nukuu nyingi, nyingi sana kiukweli ambapo Ndugu Branham analisema hili waziwazi.

Sasa, ninyi endeni kwa kanisa fulani nzuri la Injili Nzima mpate kanisa la nyumbani.

Nami naliamini hilo kwa moyo wangu wote, kwa sababu yeye alisema hivyo. Lakini naamini sisi tunafanya hivyo kwa KUWA NA KANISA LA KANDA LA NYUMBANI. Mahali petu si ndipo palipo muhimu kwa Bwana. Hilo ni jengo tu. Lakini wajibu wetu kwa Bwana ni kukaa na Neno Lake, SIO MAHALI AU JENGO. Mahali hapo hapamwokoi na kumkamilisha Bibi-arusi, NENO NDILO.

Kama nikienda kwenye jengo la kanisa, lakini wao wamesahau JAMBO LILILO KUU: kuisikia Sauti ya Mungu kwa Kubonyeza Play, nao wameibadilisha hiyo kwa kuwasikia wahudumu TU wakiuhubiri Ujumbe, Je, hilo litairidhisha na kuilisha nafsi yako kabisa? Huenda hilo likairidhisha nafsi yako, ndugu na dada yangu, bali hilo halitamridhisha Bibi-arusi.

Hebu niingilie kati hapa na niseme kuna maelfu ya watu ambao hawana jengo la kanisa la kwenda. Je, wamepotea? Ikiwa hawana mchungaji au kanisa, Je, hiyo ina maana kwamba hawawezi kuwa Bibi-arusi? Ikiwa unaishi ndani ya maili 100 kutoka kwenye jengo la kanisa, Je, ni lazima uende kwenye kanisa hilo? Lakini ikiwa ninaishi mbali zaidi, si lazima? Nalazimika kumsikiliza Mhubiri hewani, lakini siwezi kusikiliza kanda hewani? Je, jengo la kawaida ndilo ambalo nabii anasema ndilo jambo lililo muhimu zaidi tunalopaswa kwenda?

Nabii alitaka kumleta Bibi-arusi wapi?

Kama hamwezi kuja hapa maskanini, tafuteni kanisa fulani mahali fulani; enendeni kwalo.

Kwa mara nyingine tena, liko wapi chaguo lake la kwanza la kuwapeleka watu? Kwenye Maskani ya Branham, Neno, kanda. Hilo ndilo Mungu amempa Bibi-arusi Wake kufanya katika wakati huu wa mwisho, nasi tunafanya hivyo kila siku NA kila Jumapili.

Msinielewe vibaya. MIMI SISEMI lazima usikilize kanda hewani pamoja na Maskani ya Branham ili uwe Bibi-arusi. SISEMI hupaswi kwenda kanisani. SISEMI huwezi kuwasikiliza wahudumu. Ikiwa unaamini hivyo, uko nje ya Neno. Ninasema kuisikia Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda ndio Sauti iliyo muhimu zaidi UNAYOPASWA KUISIKIA, na ninaamini kwamba kila mchungaji anapaswa kuicheza Sauti hiyo, Kanda, katika makanisa yao. Lakini wao wametoa kila namna ya udhuru uliopo ILI KUTOZICHEZA KANDA. Ikiwa hilo ndilo kanisa lako, wewe huli Neno.

Hili ni wazi jambo ambalo yeye hakutaka litokee na ndicho ambacho watu walichokuwa wakifanya.

Nanyi nendeni kanisani; msiketi nyumbani, kuenda kuvua samaki, na kuwinda, na mambo kama hayo mnamo Jumapili.

Sisi hatufanyi hivyo. Sisi tunaungana kwenye kitu pekee kitakachomuunganisha Bibi-arusi, Ujumbe huu, Sauti hii.

Kwa mara nyingine tena, Mimi ninaamini katika kwenda kanisani. Kuna makanisa mengi ulimwenguni kote ambayo yanaziweka kanda nafasi ya kwanza kwenye mimbara zao, Bwana asifiwe. Je, ninaamini lazima ukae nyumbani la sivyo wewe si Bibi-arusi? LA, LA, LA….Sijawahi kuliwazia, sijawahi kuliamini. Nataka tu UBONYEZE PLAY bila kujali uko wapi au unaenda kwenye kanisa gani.

Kama huna Ufunuo wa kile anachosema, basi unaweza kusema waziwazi, “Sihitaji kumsikiliza Ndugu Branham au hata kulazimika KUKUBALIANA na yote asemayo. Hata hivyo alisema, kuna watu wengine wengi walioitwa na Mungu.”

Endelea. Twaona hapa lasema, “Yatupasa kuhuduria kanisa lingine lisilokubaliana nawe?” Hakika, si…Mimi siye changarawe pekee pwani, mwajua. Kuna—kuna watu wengine wacha Mungu kila mahali; natumai mimi ni mmojawao.

Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda ndio JIWE LA UFUKWENI LANGU, MWAMBA WANGU. Ndio Sauti ninayotaka Mimi kuisikia na ndio Sauti ninayotaka Maskani ya Branham waisikie.

Kama mngependa kuungana nasi, mnakaribishwa mno, ndugu na dada zangu. ungeneni nasi Jumapili saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(ni saa 2:00 USIKU ya Afrika Mashariki) tunapoisikia Sauti ya Mungu ikinena na kuyajibu maswali mengi unayoweza kuwa nayo moyoni mwako. Na usikie mwenyewe ikiwa mambo niliyoyasema katika barua hii hayako sawa na Neno na nimeelewa vibaya kile Mungu anachomwambia Bibi-arusi Wake.

Kile yeye anachosema kwenye kanda ni Bwana Asema Hivi. Si kile mimi Ninachosema anasema, au kile Ninachoamini anasema, na Mungu PEKE YAKE ndiye anayeweza kukupa Ufunuo wa kweli.

Ndugu Joseph Branham

26-0118 Kuthibitisha Neno Lake

UJUMBE: 64-0816 Kuthibitisha Neno Lake

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukusanyike pamoja Jumapili saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(ni saa 2:00 USIKU ya Afrika Mashariki) kusikiliza 64-0816 – Kuthibitisha Neno Lake.

Ndugu Joseph Branham

26-0111 Makao Ya Baadaye Ya Bwana Arusi Wa Mbinguni Na Bibi-Arusi Wa Duniani

UJUMBE: 64-0802 Makao Ya Baadaye Ya Bwana Arusi Wa Mbinguni Na Bibi-Arusi Wa Duniani

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Kipenzi Cha Moyo Wangu,

Nakupenda sana. Wewe ni mwili wa mwili Wangu, na mfupa wa mfupa Wangu. Hata kabla sijaziumba nyota, mwezi, ulimwengu Wangu wote, nilikuona nami nilikupenda wakati huo. Nilijua wewe ulikuwa sehemu Yangu, Kipenzi Changu cha pekee. Wewe na Mimi tulikuwa MMOJA.

Ile siku ambayo nimeitamani na kuisubiri tangu nilipowaona hatimaye imefika. Sasa ninawaita na kuwaunganisha kutoka mashariki na magharibi, kaskazini na kusini, kwa Sauti Yangu. Ninyi ni mawazo Yangu, Neno Langu, Bibi-arusi Wangu, aliyedhihirishwa.

Nimetamani sana kuwaambia kila kitu kilicho moyoni Mwangu, kwa hivyo Nililiandika kupitia manabii Wangu na nimelilinda kwa maelfu ya miaka. Wengi wamelisoma, na kuliamini kwa karne nyingi, lakini nimeyaweka mambo mengi kuwa siri hadi NINYI MLIPOFIKA. Ninyi ndio WATU PEKEE nitakaowaambia.

Wao walitamani kuyajua na kuyasikia mambo haya yote ya ajabu ambayo nimeyaficha, lakini kama vile nilivyokuahidi, nimesubiri na kuyaweka kuwa siri hadi hivi sasa, kwa ajili yako WEWE tu, WANGU MMOJA NA WA PEKEE.

Nilikuahidi Mimi ningekuja na kujifunua Mwenyewe tena katika mwili wa mwanadamu, ili niweze kukuambia, na kukufunulia mambo haya yote. Nilitaka uisikie SAUTI YANGU ikizungumza nawe moja kwa moja.

Nimewatia mafuta wengine wengi kwa Roho Wangu Mtakatifu kukuambia kuhusu upendo Wangu, lakini kama nilivyofanya siku zote, Nami kamwe siwezi kubadilika, nilimchagua mtu mmoja: Malaika Wangu, Nabii Wangu, awe Sauti Yangu ili niweze kunena Bwana Asema Hivi kwako.

Nilitaka kukuambia, wewe hukuokolewa siku yoyote Maalum. Daima ulikuwa umeokolewa. Nilikuja tu kukukomboa. Uliokolewa tangu mwanzo kwa maana ulikuwa na Uzima wa Milele, kwanza. Kwa hivyo, machoni Pangu, dhambi zako zote haziwezi hata kuonekana Nami, kitu pekee ninachosikia ni sauti yako. Ninauona tu uwakilisho wako.

Jinsi gani nimesubiri kwa hamu kukuambia mambo mengi. Moyo wangu unabubujika kwa shauku. Jinsi gani nimeisubiri kwa hamu Karamu yetu ya Harusi, Miaka elfu moja ya Utawala wetu Wa Miaka Elfu tukiwa pamoja. Nikikuambia kwa undani kuhusu Makao Yetu ya Baadaye pamoja; Jinsi nilivyokuandalia kila kitu, kila kitu jinsi tu unavyopenda hasa.

Kipenzi Changu, ikiwa unaona ni vizuri mno sasa hivi kuisikiliza Sauti yangu ikizungumza nawe, subiri tu, hiki ni kivuli tu cha jinsi itakavyokuwa wakati tutakapoishi Katika ule Mji pamoja. Nabii wako yeye hata ataishi karibu nawe; atakuwa jirani yako.

Tutatembea kwenye barabara hizo za dhahabu na kunywa kutoka kwenye chemchemi pamoja. Tutatembea katika paradiso za Mungu huku Malaika wakiizunguka dunia, wakiimba nyimbo za sifa….Itakuwa ni Siku ya namna gani!

Najua njia inaonekana inaparuza, na wakati mwingine inakuwa ngumu kwako, lakini itakuwa kitu kidogo sana, kidogo sana, Tutakapokuwa pamoja.

Kwa sasa, nitakukusanya Kwa mara nyingine tena na kuzungumza nawe Jumapili hii saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville, (ni saa 2:00 USIKU ya Afrika Mashariki) na kukuambia kila kitu kuhusu “Makao Ya Baadaye Ya Bwana Arusi wa Mbinguni na Bibi-arusi wa Duniani”. Nasubiri kwa hamu kuungana nawe wakati huo.

Kumbuka, na kamwe usisahau, nakupenda sana.

Kwa niaba Yake,

Ndugu Joseph Branham

Maandiko:
Mathayo Mt. 19:28
Yohana Mt. 14: 1-3
Waefeso 1:10
2 Petro 2:5-6 / Sura ya 3
Ufunuo 2:7 / 6:14 / 21:1-14
Walawi 23:36
Isaya Sura ya 4 / 28:10 / 65:17-25
Malaki 3:6

26-0104 Mabirika Yavujayo

UJUMBE: 64-0726E Mabirika Yavujayo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wanywaji Wa Kisima Kinachofoka Maji,

Ni Krismasi na Mwaka Mpya ulioje tuliokuwa nao. Tumezikubali na kuzifungua zawadi za Mungu alizomtumia Bibi-arusi Wake. Zawadi yetu ya kwanza ilikuwa ni Zawadi kuu kuliko zote ya Krismasi iliyowahi kufungwa. Mungu Mwenyewe alijifunga Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu na akakituma kifurushi hicho duniani. Ilikuwa ndio Zawadi Yake kubwa sana ya kwanza ya kumrejesha Bibi-arusi Wake.

Kisha Mungu akakituma kifurushi kingine kikubwa kwa Bibi-arusi Wake. Yeye alitupenda sana hivi kwamba alikuja na kujifunua Mwenyewe katika mwili tena ili aweze kuzungumza nasi mdomo kwa sikio. Alitaka Yeye na Bibi-arusi Wake wawe Mmoja.

Na sasa, enyi marafiki, msinielewe vibaya. Naomba niliseme hili kwa heshima moyoni mwangu, nikijua kwamba mimi ni mtu ninayeelekea kwenye Umilele ambaye nitasimama mbele ya Hukumu siku moja: Maelfu ya watu wanaikosa zawadi yao waliotumiwa. Unaona? Hawawezi kuielewa. Nao wanaangalia, na kusema, “Loo, yeye ni mtu tu.” hiyo ni kweli. Je, ilikuwa ni Mungu au Musa aliyewaokoa wale watu? Ilikuwa ni Mungu ndani ya Musa. Unaona? Wao walimlilia mkombozi. Na wakati Mungu alipowatumia huyo mkombozi, walishindwa kuliona, kwa sababu ilikuwa kupitia mtu, lakini haikuwa huyo mtu, ilikuwa ni Mungu ndani ya mtu huyo.

Leo, kwa mara nyingine tena, maelfu ya watu wanaikosa zawadi yao na kusema, “huna haja ya kusikiliza kanda, hivi sasa kuna watu wengine waliotiwa mafuta,” ambayo ni kweli, lakini wao wanashindwa kutambua kuwa hiyo ndio Sauti PEKEE iliyothibitishwa na Mungu, inenayo Bwana Asema Hivi kupitia mtu huyo. Sauti hiyo ndio Urimu na Thumimu ya Mungu, Yakini Yake ya wakati huu.

Tunapoisikiliza Sauti Yake iliyo kwenye kanda tunakunywa kweli kutoka kwenye Kisima cha Mungu kinachofoka maji, ambacho hakihitaji kuvuta kwa mashine, kuvuta, kujiunga, kuteka; sisi tunaamini tu na kutegemea kila Neno Linalonenwa.

Kwa sisi kuisikiliza Sauti hiyo iliyo kwenye kanda, kulingana na Yesu Mwenyewe, tunao ushahidi wa kweli wa Roho Mtakatifu katika siku yetu.

Kwa hiyo huo hapo ushahidi halisi wa Roho Mtakatifu! Yeye hajaniambia bado jambo lo lote ambalo si sahihi. Ya kwamba, “Ni ushahidi wa Roho Mtakatifu, ni yeye yule anayeweza kuliamini Neno.” kama unaweza kulipokea.

Mungu ametuandalia Chemchemi tunayoweza kuinywea kila dakika ya kila siku. Daima ni safi. Si kitu fulani kilichooza, Ni Chemchemi Yake isiyokauka, inayojitegemea; unatakiwa tu Ubonyeze Play.

Tukinena kuhusu ZAWADI kutoka kwa Mungu, Je, unaweza kuwazia kweli jinsi gani Zawadi hii ilivyo KUU? Kwa Kubonyeza play tu na kuisikiliza Sauti Yake iliyo kwenye kanda, ndiyo pekee… SAUTI PEKEE duniani ambayo huhitaji chujio, kichujio, au chochote kile. Unatakiwa tu kusikiliza, kuamini, na kusema amina kwa kila Neno.

Mungu Mwenyewe ameiandaa njia hii, NJIA YAKE PEKEE, ya kupokea uzima wa milele, na muhimu zaidi, YA KUWA BIBI-ARUSI WAKE. Tunaweza tu kulala kifuani Mwake na kuzinyonya nguvu zetu kwa kuisikiliza Chemchemi Yake, Sauti Yake, El Shaddai akizungumza na Bibi-arusi Wake.

Hebu mwaka huu na uwe ndio mwaka atakaokuja kutuchukua, sisi Bibi-arusi Wake mpendwa. Tunatazamia na kungoja kwa matarajio makubwa. Siku yoyote hivi sasa tutawaona wale ambao tumetamani kuwaona wakitokea. Tutatambua, Katika kufumba na kufumbua jicho, tutakuwa tumetoka mahali hapa, tumeitwa kwenda kwenye Karamu yetu ya Harusi.

Bwana, tuonapo meza hiyo kubwa imetandazwa pale kwa ajili ya hiyo karamu, maelfu ya maili, tukitazamana, askari wa vita walio na majeraha, machozi ya furaha yakitiririka mashavuni mwetu… Mfalme akijitokeza katika uzuri Wake, utakatifu, ashuke mezani na kuchukua mikono Yake Mwenyewe na kuyafuta machozi kutoka machoni mwetu, akisema, “Msilie tena, yote yamekwisha. Ingieni katika raha za Bwana.” Taabu za safarini hazitaonekana kuwa kitu wakati huo, Baba, tutakapofika kwenye mwisho wa njia.

Njoo unywe, unywe, unywe, unywe pamoja nasi kutoka kwenye Chemchemi iliyoandaliwa na Mungu ya siku hii Jumapili hii saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville. (ni saa 2:00 USIKU ya Afrika Mashariki) Ndio mahali PEKEE ambapo unaweza kupumzika kabisa na kusema AMINA kwa kila Neno usikialo. Ndicho kisima Chake kinachofoka maji kilichoandaliwa ili Bibi-arusi Wake apate kukinywea.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: 64-0726E Mabirika Yavujayo

Maandiko ya kusoma kabla ya kuusikiliza Ujumbe:
Zaburi 36:9
Yeremia 2:12-13
Yohana 3:16
Ufunuo Sura ya 13

25-1228 Kutambua Siku Yako Na Ujumbe Wake

UJUMBE: 64-0726M Kutambua Siku Yako Na Ujumbe Wake

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliyekatwa Akatolewa,

Leo, kanisa limemsahau nabii wao. Hawamhitaji yeye tena ahubiri katika makanisa yao. Wanadai wana wachungaji wao wa kuwahubiria na kuwanukulia na kuwafasiria Neno. Kuhubiri ni muhimu zaidi kuliko kuisikiliza Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda katika makanisa yao.

Bali Mungu alijua Yeye hana budi kuwa na nabii Wake; hivyo ndivyo Yeye amekuwa akimwita atoke na kumwongoza Bibi-arusi Wake kila wakati. Yeye Alitukata akatutoa kutoka miongoni mwa mataifa mengine kwa Upanga Wake wenye makali kuwili, Roho Wake Mtakatifu, Sauti Yake iliyonenwa na nabii Wake.

Yeye ametukata kwa Sauti hiyo. Ndiyo maana aliirekodi na kuiweka kwenye kanda. Kwa Ufunuo tunaona jinsi Maandiko yalivyo makamilifu! Bibi-arusi hawezi kuivishwa isipokuwa Mwana aiivishe.

Haidhuru utahubiri namna gani, hata ufanye nini, haliwezi kuivishwa, haliwezi kudhihirishwa, haliwezi kuthibitishwa; ila tu na Yeye aliyesema, “Mimi Ndimi Nuru ya ulimwengu,” lile Neno.

Neno lilituambia Roho Mtakatifu Mwenyewe atatokea na kutuivisha, ili kuthibitisha, kuhakikisha na kujidhihirisha. Nuru ya jioni imekuja. Mungu akijidhihirisha Mwenyewe katika mwili ili kumwita Bibi-arusi Wake atoke.

Yeye Ndiye aliyekuita WEWE utoke kwa Roho Wake Mtakatifu, Neno Lake, Sauti Yake. Yeye Ndiye aliyekuchagua WEWE. Yeye Ndiye anayekufundisha WEWE. Yeye Ndiye anayekuongoza WEWE. Kwa kitu gani? Roho Wake Mtakatifu, Sauti Yake ikizungumza NA WEWE MOJA KWA MOJA.

Lakini kwao Hilo limepitwa na wakati sana katika siku hii. Wamepita muda wa kuzicheza kanda makanisani mwao. Wao hawalitambui. Hiyo ndiyo sababu wako katika hali waliyo nayo. Lakini kwako wewe, imefunuliwa Kuwa ndio njia ya Mungu Iliyoandaliwa, NI BWANA ASEMA HIVI KWAKO.

Kwa hiyo hakuna budi kutokee Nguvu fu—fu—fulani, Roho Mtakatifu Mwenyewe, kuivisha, ama kuthibitisha, ama kuhakikisha, ama kudhihirisha ya kwamba yale ambayo Yeye amebashiri yangetukia katika siku hii. Nuru ya jioni inaleta hilo. Ni wakati wa jinsi gani!

Sisi ndiye Bibi-arusi Neno mkamilifu ambaye nabii Wake alimwona katika ono. Sisi ndio wale ambao Yeye alimtuma nabii Wake kuwaita watoke kwa Neno Lake, na sasa tunao UAMSHO, kwa maana sasa tunajua sisi ni nani.

Kufufua, hapo, ni neno lile lile linalotumika mahali pengine popote, ndiyo kwanza nilichunguze, linamaanisha, “uamsho.” “Yeye atatufufua baada ya siku mbili.” Hiyo ingekuwa, “Katika siku ya tatu Yeye atatufufua tena, baada ya kututawanya, na kutupofusha, na kuturarua.”

Baba alimtuma nabii Wake kumwangalia Bibi-arusi Wake ili kwamba tusitoke mstarini. Kumbuka, hili lilikuwa ono!

Bibi-arusi alipitia mahali pale pale alipopitia wakati alipokuwa hapo mwanzo. Lakini nilikuwa nikimwangalia akitoka mstarini, na nikijaribu kumvuta arudi kwenye mstari.

Lakini “yeye” angewezaje kumvuta arudi mstarini leo? “Yeye”, mtu huyo, hayupo hapa duniani. KWA NENO! Neno PEKEE lililothibitishwa la wakati huu ni lipi? Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.

Wahudumu wameitiwa kulihubiri Neno kwa kunukuu kile hasa nabii alichosema. Kulingana na nabii mwenyewe, wao hawapaswi kusema chochote zaidi.

Kweli, wameitiwa kulifundisha na kulihubiri Neno hilo. Lakini kuna SAUTI MOJA PEKE YAKE ILIYOTHIBITISHWA NA MUNGU MWENYEWE KUWA BWANA ASEMA HIVI.

Nasema vivyo hivyo katika Jina la Yesu Kristo. Usiongeze kitu. Usiondoe—kuliwekea mawazo yako. Wewe sema tu yaliyosemwa katika kanda hizo. Tenda sawasawa kabisa na vile Bwana Mungu amekuamuru kutenda. Usiongezee Kwake!

Kama ukisema “amina” kwa kila neno ambalo mchungaji wako au mhudumu wako asemalo, umepotea. Lakini ukisema “AMINA” KWA KILA NENO AMBALO MUNGU ALILOLINENA KUPITIA NABII WAKE KWENYE KANDA, WEWE NDIYE BIBI-ARUSI NA UTAKUWA NA UZIMA WA MILELE.

Nabii wa Mungu alikuwa ndiye mtu ambaye Mungu alimchagua kuzungumza kupitia yeye. Ilikuwa ni CHAGUO LA MUNGU kumtumia yeye kulinena Neno Lake na kuliweka kwenye kanda ili kwamba Bibi-arusi angekuwa SIKU ZOTE NA BWANA ASEMA HIVI YA KUSIKIA.

Yeye hataki Bibi-arusi Wake ategemee kile watu wengine wasemacho, au fasiri yao ya Neno Lake. Yeye anataka Bibi-arusi Wake asikie kutoka kwenye midomo Yake hadi masikioni mwao. Yeye hataki Bibi-arusi Wake amtegemee mtu mwingine yeyote ila Yeye Mwenyewe.

Tunapoamka asubuhi, tunapenda Yeye atuambie, “Habari za asubuhi marafiki. Nitazungumza nanyi leo na kuwaambieni jinsi gani ninavyowapenda na jinsi ambavyo ninyi na Mimi tulivyo MMOJA. Ninao wengi ambao nitakaowapa uzima wa milele, bali ni WEWE peke yake ndiye Bibi-arusi niliyemchagua kwa mkono Wangu. WEWE peke yake ndiye niliyempa Ufunuo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Wengine wengi wanapenda kunisikia, lakini Mimi nimewachagua ninyi kuwa Bibi-arusi Wangu. Kwa maana mmenitambua Mimi nanyi mmedumu na Neno Langu. Hamjapatana, hamjabembana, bali mmedumu waaminifu na Neno Langu.

Muda umekaribia. Ninakuja kuwachukua hivi karibuni. Kwanza, mtawaona wale walio pamoja nami sasa. Loo, jinsi wao wanavyotamani kuwaona na kuwa pamoja nanyi. Msihofu enyi watoto, kila kitu kiko kikamilifu kwenye wakati unaofaa, endeleeni tu kusonga mbele.”

Kama mhudumu wa Injili, siwezi kuona jambo moja lililosalia ila kule kuondoka kwa Bibi-arusi.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: 64-0726M “Kutambua Siku Yako na Ujumbe Wake”

Muda: saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville(ni saa 2:00 USIKU ya Afrika Mashariki)

Maandiko ya kusoma kabla ya kuusikia Ujumbe:
Hosea: Sura ya 6
Ezekieli: Sura ya 37
Malaki: 3:1 / 4:5-6
Timotheo wa Pili: 3:1-9
Ufunuo: Sura ya 11

25-1221 Kuenda Nje Ya Kambi

UJUMBE: 64-0719E Kuenda Nje Ya Kambi

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Laazizi Mpendwa,

Mungu habadiliki. Neno Lake halibadiliki. Mpango Wake haubadiliki. Na Bibi-arusi Wake habadiliki, tutadumu na Neno. Ni zaidi ya uhai kwetu; Ni chemchemi ya Maji Yaliyo Hai.

Kitu pekee tulichoagizwa kufanya ni kulisikia Neno, ambalo ni Sauti ya Mungu iliyothibitishwa ambayo imerekodiwa na kuwekwa kwenye kanda. Kitu pekee tunachokiona si kanuni ya imani, si kundi la watu, hatuoni kitu kingine ila Yesu, Naye ni Neno lililofanyika mwili katika siku yetu.

Mungu yuko katika Kambi yetu nasi tuko njiani kuelekea Utukufuni tukiongozwa na Nguzo ya Moto, ambayo ni Mungu Mwenyewe akizungumza kupitia nabii Wake aliyethibitishwa wa Malaki 4. Tunakula ile Mana iliyofichwa, Maji Yaliyo Hai ambayo ni Bibi-arusi peke yake ndiye anayeweza kula.

Mungu habadilishi njia Zake, na wala shetani habadilishi zake. Kile alichofanya miaka 2000 iliyopita, yeye anafanya jambo lile lile leo, isipokuwa tu amekuwa mwerevu zaidi.

Sasa, baada ya miaka mia nne, Mungu alitembea moja kwa moja miongoni mwao siku moja. Kulingana na Maandiko, Yeye alikuwa afanyike mwili na akae miongoni mwao. “Jina Lake ataitwa Mshauri, Mfalme wa Amani, Mungu mwenye Nguvu, Baba wa Milele.” Na wakati alipokuja miongoni mwa watu, wao walisema, “Hatutaki Mtu huyu atutawale!….”

Kulingana na Maandiko, Mwana wa Adamu angekuja kwa mara nyingine tena na kuishi na kujifunua Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu, Naye alifanya hivyo, nao wanasema kitu kile kile. Hakika, wanaunukuu na kuuhubiri Ujumbe, lakini hawatataka mtu huyo awatawale.

Hiki ndicho hasa kinachotendeka:

Na kama ilivyokuwa wakati huo, ndivyo ilivyo leo! Biblia ilisema kanisa la Laodikia lingemtupa nje, Naye alikuwa anabisha, akijaribu kuingia. Kuna kasoro mahali fulani. Sasa, kwa nini? Walikuwa wamefanya kambi yao wenyewe.

Mtu anaweza kusema, “Ninajua na ninaamini Ndugu Branham alikuwa nabii. Alikuwa ndiye malaika wa saba. Alikuwa ndiye Eliya. Tunauamini Ujumbe huu. Kisha kutoa aina fulani ya udhuru, wowote ule uwao, wa kutoicheza Sauti PEKEE ya Mungu iliyothibitishwa kanisani mwao… Kuna kasoro mahali fulani. Sasa, kwa nini? Walikuwa wamefanya kambi yao wenyewe.

Ninayasema mambo haya si kulitenganisha kanisa, Neno la Mungu ndilo linalofanya jambo hilo. Mimi Nataka tuungane pamoja, tuwe KITU KIMOJA sisi kwa sisi na pamoja Naye, lakini kuna njia moja tu ya kufanya hivyo: kwenye Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. Hiyo ndio BWANA ASEMA HIVI PEKEE.

Mungu ametufunulia njia Yake kamilifu kwetu. Ni tukufu sana na hata hivyo ni rahisi sana. Kila Ujumbe tunaousikia akituambia, anatuhakikishia, anatutia moyo, kwamba SISI NDIO BIBI-ARUSI WAKE. Tuko katika mapenzi Yake makamilifu. Tumejiweka wenyewe tayari kwa KUMSIKIA YEYE.

Ujumbe huu ni wa hivi sasa kuliko gazeti la kesho. Sisi ni unabii unaotimizwa. Sisi ni Neno lililodhihirishwa. Mungu anatuthibitishia kwa kila Ujumbe tunaousikia kwamba leo, Maandiko haya yanatimizwa.

Yawezekana kuwe na baadhi huko nje katika mataifa, ulimwenguni kote, ambao hata kanda hii ingewakuta manyumbani mwao au makanisani mwao. Tungeomba, Bwana, kwamba wakati ibada inaendelea, pale—pale… au kanda inachezwa, au nafasi yo yote tunayoweza kuwamo, au—au hali, yule Mungu mkuu wa Mbinguni na aheshimu huu unyofu wa mioyo yetu asubuhi hii, na kuponya wahitaji, kuwapa wao yale wanayohitaji.

Hebu Subiri kidogo…. hivi Sauti ya Mungu kwa ulimwengu imetoka kutabiri nini na kusema nini?…. watu wangekuwa wakicheza kanda majumbani mwao au makanisani mwao.

Lakini tunakosolewa na kukemewa Kwa kusema ati HATUWEZI kuwa na Kanisa la Kanda la Nyumbani? Ati Ndugu Branham hakuwahi kusema chezeni kanda MAKANISANI mwenu?

UTUKUFU KWA MUNGU, LISIKIE, LISOME, NI BWANA ASEMA HIVI. Na si tu kwamba YEYE alilisema hilo, bali kwa kuzicheza kanda majumbani mwenu na makanisani MWENU, Yule Mungu mkuu wa Mbinguni ataheshimu unyofu wa mioyo yetu na kuwaponya wahitaji na kutupa YOYOTE YALE TUNAYOHITAJI!!

Hii nukuu moja INATHIBITISHA kwamba hawa watu wanawasikiliza wachungaji wao na HAWALISIKII NENO, la sivyo wangewapa changamoto na kuwathibitishia kwa NENO kwamba sisi tuko katika MAPENZI YAKE MAKAMILIFU, na kuko katika MAPENZI YAKE MAKAMILIFU KUZICHEZA KANDA KATIKA MAKANISA YAO.

Siliweki mahali pasipo pake au kulinukuu vibaya Neno kama wengi wasemavyo ati nafanya. Lisikie na ulisome wewe mwenyewe.

Ni rahisi sana na kamilifu sana, BONYEZA PLAY na uisikie Sauti ya Mungu ikizungumza nawe. Sema “Amina” kwa kila Neno usikialo. Hata huna haja ya kulielewa, wewe yakupasa tu kuliamini.

“Nataka kwenda nje ya kambi. Haidhuru itanigharimu nini, nitautwaa msalaba wangu na kuubeba kila siku. Nitatoka nje ya kambi. Hata watu waseme nini juu yangu, nataka kumfuata nje ya kambi. Niko tayari kwenda.”

Njoo upite kizuizi cha sauti uingie kwenye Neno la Mungu pamoja nasi Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville.(ni saa 2:00 USIKU ya Afrika Mashariki) Hayapimiki yale Mungu anayoweza na atakayofanya na mtu ambaye yuko tayari kwenda nje ya kambi ya mwanadamu.

Ndugu Joseph Branham

Ujumbe: 64-0719E Kuenda Nje Ya Kambi

Maandiko: Waebrania 13:10-14 / Mathayo 17:4-8

25-1214 Sikukuu Ya Baragumu

UJUMBE: 64-0719M Sikukuu Ya Baragumu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Mkamilifu,

Hili si jambo tu la kujibunia, enyi marafiki. Hii ni BWANA ASEMA HIVI, Maandiko.

Kila Mkristo anataka kuwa Bibi-arusi, lakini tunajua Bibi-arusi Wake watakuwa wachache tu waliochaguliwa. Tunajua Yeye anayo mapenzi ya kuruhusia, lakini Bibi-arusi Wake lazima awe katika mapenzi Yake makamilifu. Kwa hivyo, lazima tumtafute Mungu katika Neno Lake, na kisha kwa Ufunuo, tutajua mapenzi Yake makamilifu jinsi ya kuwa Bibi-arusi Wake.

Tunapaswa kuyachunguza Maandiko, kwa maana tunajua Mungu KAMWE Habadilishi mawazo Yake kuhusu Neno Lake. Mungu habadilishi mpango Wake. Yeye habadilishi CHOCHOTE. Jinsi alivyofanya mara ya kwanza ni kamilifu. Kile Yeye alichofanya jana atafanya vivyo hivyo leo.

Jinsi Yeye alivyomwokoa mwanadamu tangu mwanzo, itambidi amwokoe mtu leo kwa njia ile ile. Jinsi Yeye alivyomponya mtu wa kwanza, hana budi kufanya vivyo hivyo leo. Jinsi ambavyo Mungu alichagua kumwita na kumwongoza Bibi-arusi Wake, atafanya vivyo hivyo leo; kwa kuwa Yeye ni Mungu na hawezi kubadilika. Neno linatuambia kwamba Yesu Kristo ni YEYE YULE jana, leo na hata milele.

Kwa hivyo, wakati tunapolisoma Neno Lake, tunaweza kuona wazi kabisa Jinsi Yeye alivyochagua kumwita na kumwongoza Bibi-arusi Wake kwa kila kizazi. Yeye Alimchagua MTU MMOJA. Alisema wao walikuwa Neno la siku yao. Nabii alituambia Yeye KAMWE hakuwa na kundi la watu; wao wana njia tofauti, mawazo tofauti, na muhimu zaidi, alisema, NENO LA MUNGU HALIHITAJI KUFASIRIWA.

Kwa hivyo, kile kila nabii alichosema katika kila kizazi hakiwezi kuongezwa kwake au kuondolewa. Lazima iwe Neno kwa Neno kile ALICHONENA. Rahisi sana ukiniuliza mimi Njia ya Mungu iliyoandaliwa ni ipi….DUMU NA NABII.

Sasa, sio tu kwamba tunajua fika njia ya Mungu iliyoandaliwa tangu mwanzo vile imekuwa, bali Bwana Yeye hata atanena kupitia malaika Wake na kutuambia kile Yeye atakachofanya katika siku zijazo, ili tu kuthibitisha kwa mara nyingine tena, MUNGU HABADILISHI MPANGO WAKE.

Baada ya Bibi-arusi Wake (sisi) kuondoka hapa duniani na kuitwa kwenda kwenye Karamu ya Harusi, Mungu atawaitaje wale Wayahudi 144,000 waliochaguliwa? Kundi la watu?

Sasa, mara Kanisa hili (Bibi-arusi) limevutwa pamoja, linanyakuliwa; na ile siri ya Muhuri ya Saba, ama Muhuri ya Saba, ile siri ya kuondoka. Nao Wayahudi wanaitwa kwa siri ya Baragumu ya Saba, ambayo ni manabii wawili, Elia na Musa, nao wanarudi.

Kwa hivyo mara tu Bibi-arusi atakapovutwa pamoja, tutatwaliwa juu. Tunajua kuna kitu kimoja tu kinachoweza kumvuta Bibi-arusi pamoja, Roho Mtakatifu, Naye Roho Mtakatifu ni Neno Lake, nalo Neno Lake la siku hii ni Sauti ya Mungu, nayo Sauti ya Mungu ni…

Kama nimewaudhi kwa kusema hivyo, nisameheni, lakini, nilihisi hilo huenda lilichukiwa, bali, mimi ni Sauti ya Mungu kwenu. Mnaona? Nalisema hilo tena, wakati huo ilikuwa chini ya uvuvio, mnaona.

Naomba niingilie hapa na niseme, NUKUU hii MOJA tu kutoka kwa malaika-mjumbe wa Mungu aliyethibitishwa inapaswa kutosha kabisa kwa wote wanaojiita waaminio katika Ujumbe huu wa wakati wa mwisho wadai mchungaji wao ABONYEZE PLAY katika makanisa yao au ajiuzulu ili waweze kumpigia kura mchungaji mwenye UFUNUO WA KWELI KUTOKA KWA MUNGU.

Kwa hivyo, Baragumu ilipigwa nao manabii wawili wakatokea kwani Yeye hawezi kuwa na malaika Wake wa saba pamoja na Bibi-arusi Wake hapa duniani wakati ule ule wao wanapokuja. Kwa hivyo Yeye anawaitaje Wayahudi? Kwa njia ile ile aliyomwita Bibi-arusi Wake Mmataifa.

Nao Wayahudi wanaitwa kwa siri ya Baragumu ya Saba, ambayo ni manabii wawili…

Bibi-arusi hana budi kuondoka njiani, apate kwenda juu sasa; kusudi wale watumishi wawili, wale watumishi wawili wa Mungu, katika Ufunuo, wale manabii wawili, wapate kujitokeza, kusudi wawapigie ile Baragumu ya Saba, wawajulishe Kristo.

Ni wazi kabisa, Mungu habadilishi mpango Wake. Yeye aliwatuma manabii Wake. Kwa hivyo, Bibi-arusi Wake atadumu na njia Yake iliyoandaliwa, nabii-malaika Wake, Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.

Kisha ili kulifanya liwe wazi kabisa, Mungu kwa mara nyingine tena anazungumza na kumwambia Bibi-arusi Wake: Mmedumu waaminifu Kwangu na njia Yangu iliyoandaliwa, kwa hivyo njia Yangu iliyoandaliwa ya siku yenu itawaambieni:

Yule malaika wa saba, mjumbe, aseme, “Tazama Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!”

SAUTI HIYO ni muhimu sana; SAUTI YA MUNGU ikinena kupitia malaika Wake wa saba kwenye kanda. Mungu ataitumia SAUTI HIYO, SAUTI YA MALAIKA WAKE WA SABA. SIO KUNDI…SIO MIMI…SIO MCHUNGAJI WAKO…SAUTI YA MALAIKA-MJUMBE WAKE WA SABA kututambulisha sisi Kwake, Bwana wetu Yesu Kristo.

Kwa hivyo, tunafahamu:

  • SISI NDIO BIBI-ARUSI WAKE.
  • TUKO KATIKA MAPENZI YAKE MAKAMILIFU.
  • TUNAUFUATA MPANGO WAKE KWA AJILI YA SIKU HII KWA KUBONYEZA PLAY.

Sehemu ya Bibi-arusi Wake itakusanyika Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(ni saa 2:00 USIKU ya Afrika Mashariki) kumsikiliza mchungaji wetu, malaika- mjumbe wa Mungu, William Marrion Branham, Naye atakuwa akizungumza nasi na kutufunulia kwamba halipo kanisa lingine, hamna kundi lingine la watu tangu kuumbwa kwa ulimwengu, ambalo limewahi kupata fursa tuliyonayo ya kuungana pamoja kumsikiliza Mungu akizungumza nao moja kwa moja.

Sisi ni watu waliobarikiwa Jinsi gani. Tunayo furaha sana. Tunashukuru sana. Bibi-arusi anafanyika MMOJA na Bwana-Arusi

Ndugu Joseph Branham

Sikukuu Ya Baragumu 64-0719M.

Maandiko ya kusoma kabla ya Kusikiliza Ujumbe:
Mambo ya Malawi 16
Mambo ya Walawi 23:23-27
Isaya 18:1-3
Isaya 27:12-13
Ufunuo 10:1-7
Ufunuo 9:13-14
Ufunuo 17:8

25-1207 Ndipo Yesu Akaja Na Kuita

UJUMBE: 64-0213 Ndipo Yesu Akaja Na Kuita

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Neno,

Tunaishi katika saa zenye giza kuliko, lakini sisi HATUNA HOFU, Bwana amekuja. Amekuja kulitimiza Neno Lake katika siku ya mwisho. Jinsi Alivyokuwa wakati huo, ndivyo Alivyo leo. Jinsi udhihirisho na utambulisho Wake ulivyokuwa wakati huo, ndivyo ulivyo leo. Yeye angali ni Neno la Mungu, akijidhihirisha Mwenyewe katika mwili wa kibinadamu katika malaika Wake wa saba mwenye nguvu na ametufunulia, sisi ni Bibi-arusi Neno lililo Hai Wake.

Hatuna muda wa kujadiliana au kuzozana; tumepita wakati huo; tunasonga mbele, inatupasa kufika kule. Roho Mtakatifu amekuja miongoni mwetu. Bwana Yesu katika umbo la Roho amejifunua na kujidhihirisha Mwenyewe kupitia nabii Wake kwamba Yeye ni Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi Wake.

Yeye alisema angekuja. Alisema angefanya jambo hili. Alisema angejitokeza jukwaani katika siku za mwisho na kufanya mambo haya kama alivyofanya alipokuja katika mwili mara ya kwanza, Naye huyu hapa akilifanya jambo hilo. Mnaogopa nini? HAKUNA!!!

Tumo njiani kuelekea Utukufuni! Hakuna kitu kitakachotukomesha. Mungu atalithibitisha Neno Lake. Sijali ni kitu gani kitakachotukia. Wakati wa matendo umefika. Wakati wa kuamini ama kutokuamini umefika. Ule Mstari wa kutengana ambao huwajia kila mwanamume na mwanamke umewasili.

Wewe ulizaliwa kwa kusudi fulani. Wakati Nuru ilipokumulika, iliondoa giza lote ndani yako. Wakati ulipoisikia Sauti Yake ikizungumza nawe kwenye kanda, jambo fulani lilitendeka. Ilinena na nafsi yako. Ilisema, “Bwana amekuja na anakuita. Usifadhaike, usiogope, Ninakuita. Wewe ni Bibi-arusi Wangu”.

Enyi watu, iweni na hakika! Msibahatishe tu nusunusu kuhusu hilo. Mungu anao mpango: Neno Lake alilolirekodi kwenye kanda. Bwana amekuja na anawaita. Njooni kwenye njia ya Mungu iliyoandaliwa.

Bwana atamuunganisha kwa mara nyingine tena Bibi-arusi Wake kote ulimwenguni na Sauti Yake. Atatutia moyo, atatuhakikishia, atatuponya, atatuleta katika Uwepo Wake mkuu na kutuambia:

Bwana amekuja na anakuita. Loo, ewe mwenye dhambi, loo, ewe mgonjwa, hivi huoni Bwana aliyedhihirishwa katika mwanadamu, katikati ya waamini? Yeye amekuja kuwaita watoto Wake wanaoamini wapate afya. Amekuja kumwita mwenye dhambi apate kutubu. Ewe uliyerudi nyuma, mfuasi wa kanisa, Bwana amekuja na anakuita.

Ni kumwagwa kwa Roho Wake Mtakatifu kulikoje ambako Bibi-arusi atakuwanako Jumapili hii Mungu atakapowakusanya watoto Wake pamoja Kwa mara nyingine tena na kuingia katika nyumba zetu, makanisa yetu, mikusanyiko yetu, na kutuita na kusema, “Bwana amekuja na anawaita. Chochote mnachokihitaji, ni chenu.”

Hebu maneno hayo na yaingie ndani ya mioyo yenu, ndugu na dada. CHOCHOTE MNACHOKIHITAJI, BWANA AMEKUJA NA KUWAPENI JAMBO HILO.

Baba wa Mbinguni, Ee Bwana, jalia litukie tena. Mambo yote hayo ambayo nimesema, “Yesu amekuja na anakuita.” Yeye hufanya nini hapo anapokuja? Huita. Na jalia litendeke tena, Bwana. Jalia Roho Wako Mtakatifu aje miongoni mwa watu usiku wa leo, Bwana Yesu katika umbo la—la Roho. Jalia aje usiku wa leo na ajifunue Mwenyewe, halafu ajidhihirishe Mwenyewe.

Ndugu Joseph Branham

Ujumbe: 64-0213 Ndipo Yesu Akaja Na Kuita
Saa: 6:00 MCHANA masaa ya Jeffersonville(ni saa 2:00 USIKU ya Afrika Mashariki)

Maandiko:Yohana Mt. 11:18-28