All posts by admin5

25-0921 Lile Shtaka

UJUMBE: 63-0707M Lile Shtaka

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Walioachiwa Huru,  

Sasa, Hapo “wao,” sio wenye dhambi, “Wao,” hao ni, kanisa la siku hiyo, walimwonea makosa yule Mtu aliyekuwa ndiye lile Neno. Sivyo? Walimwonea makosa yule Mtu aliyekuwa lile Neno. Sasa wao hulionea makosa lile Neno likitenda kazi kupitia kwa mtu.

Tangu mwanzo ulimwengu umemtupilia Yeye mbali, umemkataa, umekataa kudumu na Neno Lake kwa kuyashika mapokeo yao, kanuni zao za imani, mawazo yao.  Daima wao wameukosa mpango wa Mungu; Mungu, kama Mtu, ambaye alikuwa Neno, na sasa Neno likifanya kazi kupitia huyo mtu.

Lakini katika siku yetu Yeye alisema, “Nitakuwa na kundi dogo, wateule wachache. Wao walikuwa ndani Yangu tangu mwanzo. Watanipokea Mimi na kuliamini Neno Langu na yule mtu Niliyemchagua kulifunua Neno Langu.  Yeye atakuwa Sauti Yangu kwao.” 

“Wao hawataonea haya kuitangaza Sauti Yangu. Hawataonea haya kuuambia ulimwengu kwamba Mimi nimekuja tena na Nimejidhihirisha Mwenyewe kupitia mwili wa mwanadamu kama nilivyosema Ningefanya. Wakati huu wao hawatamwabudu huyo mtu, lakini wataniabudu Mimi, Neno, litakalonena kupitia mtu huyo. Wao watanipenda Mimi na kunitangaza Mimi kwa kila mshipa wa utu wao.”

“Kwa hivyo, Nimewapa yote wanayohitaji kufanyika Bibi-arusi Wangu. Nimewaimarisha kwa Neno Langu; kwa maana wao NI NENO LANGU lililofanyika mwili. Ikiwa wanahitaji uponyaji, wao hulinena Neno Langu. Ikiwa wana kizuizi chochote kinachowazuia, wao hulinena Neno Langu. Ikiwa wanaye mtoto ambaye amekengeuka, wao hulinena Neno Langu. Chochote kile wanachohitaji, wao hulinena Neno Langu, kwa kuwa wao ni Neno Langu lililofanyika mwili ndani yao.”

“Wanajijua wao ni nani, kwa kuwa Mimi nimejifunua Mwenyewe kwao. Wamedumu wa kweli na waaminifu kwa Neno Langu nao wanaungana pamoja kwenye Sauti Yangu. Kwa maana wanaijua Sauti Yangu, Neno Langu, Roho Wangu Mtakatifu. Wanajua, pale Neno lilipo ndipo Tai watakapokusanyika.”

Wakati nabii Wake alinenapo Neno Lake na kukishtaki kizazi hiki kwa kumsulubisha Yesu Kristo mara ya pili na kuwatangaza kuwa wameangamia, Bibi-arusi atakuwa akifurahi.  Kwa maana tunajua SISI NDIYE Bibi-arusi Wake ambaye amelikubali na kulipokea Neno Lake. Tunapaza sauti kutoka ndani ya mioyo yetu na kusema: 

Mimi ni Wako, Bwana. Najilaza mwenyewe kwenye madhabahu haya, kwa kujitakasa kama tu nijuavyo kujitendea mwenyewe. Ondosha ulimwengu ndani yangu, Bwana. Yaondoe mambo yaharibikayo kwangu; nipe mambo yasiyoharibika: Neno la Mungu. Na niweze kuishi karibu sana na hilo Neno, hata lile Neno liwe ndani yangu na mimi ndani yake. Nijalie, Bwana. Nisiondoke kwalo kamwe.

Kuna uzima, na kuna mauti. Kuna njia sahihi, na kuna njia mbaya. Kuna ukweli, na kuna uongo. Ujumbe huu, Sauti hii, ndio njia kamilifu iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku hii. Njoo uuungane na sehemu ya Bibi-arusi mkuu wa Mungu tunapokusanyika kulizunguka Neno Lake lililofunuliwa na kuusikia Ujumbe:  Lile Shtaka 63-0707M.

Ndugu. Joseph Branham

25-0914 Je, Maisha Yako Yanaistahili Injili?

UJUMBE: 63-0630E Je! Maisha Yako Yanaistahili Injili?

PDF

BranhamTabernacle.org

Ndugu na Dada Wapendwa,

Ninampenda Bwana, Neno la Mungu, Ujumbe huu, Sauti Yake, nabii Wake, Bibi-arusi Wake, zaidi ya uhai wenyewe. Wote ni KITU KIMOJA KWANGU MIMI. Sitaki kamwe kupatana kwenye yodi moja, nukta moja ndogo, ama NENO MOJA ambalo Mungu aliloandika katika Neno Lake ama alilolinena kupitia nabii Wake. Kwangu mimi, Yote ni Bwana Asema Hivi.

Mungu aliliwaza, kisha akalinena kwa manabii Wake, nao wakaliandika Neno Lake. Ndipo akamtuma malaika Wake mwenye nguvu, William Marrion Branham, duniani katika siku yetu ili Yeye aweze kujifunua Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu kwa mara nyingine tena, kama alivyofanya kwa Ibrahimu. Kisha Yeye akanena kupitia nabii Wake awe Sauti ya Mungu kwa ulimwengu, kufunua na kuzifasiri siri zote ambazo zimefichwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu kwa Bibi-arusi Wake aliyechaguliwa tangu zamani.

Sasa, Bibi-arusi Wake, NINYI, mnakuwa Neno lililofanyika mwili; Mmoja na Yeye, Bibi-arusi Neno Wake aliyerejeshwa kikamilifu.

Najua ninaeleweka vibaya kwa kile ninachosema na ninachoandika. Naomba niseme kwa unyenyekevu kama nabii wetu alivyosema, mimi sina elimu nami najua siwezi kuandika ama kuzungumza kwa usahihi kile ninachojisikia moyoni mwangu. Ninakubali inaonekana kama ninaandika kwa ukali sana wakati mwingine. Ninapofanya hivyo, sio kuonyesha kutoheshimu, au kuwa na mtazamo mbaya ama kumhukumu mtu fulani, bali kinyume chake. Ninafanya hivyo kwa upendo ulio moyoni mwangu kwa Neno la Mungu.

Ninataka kila mtu aukubali na kuuamini Ujumbe huu Mungu alioutuma kumwita Bibi-arusi Wake atoke. Sijawahi kamwe kuhisi moyoni mwangu au akilini kwamba wahudumu hawapaswi kuhubiri tena; ingekuwa ni kwenda kinyume na Neno la Mungu. Mimi nina bidii tu kwa ajili ya Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. Ninaamini ndiyo Sauti muhimu sana WAHUDUMU WOTE wanayopaswa kuiweka Kuwa ya KWANZA mbele ya watu. Hii haimaanishi kuwa hawawezi kuhubiri, nataka tu kuwatia moyo kuzicheza kanda katika makanisa yao wakati watu wamekusanyika chini ya upako huo.

Ndiyo, ningependa kuufanya ulimwengu mzima usikilize Ujumbe ule ule kwa wakati mmoja ulimwenguni kote. Si kwa sababu “Mimi” nilisema hivyo, au kwa sababu “Mimi” niliichagua kanda ya kusikiliza, bali ninahisi hakika Bibi-arusi angeona Jinsi gani Mungu ameifanya njia kwa jambo hili kutendeka katika siku yetu.

Kama tungekuwa na rekodi za Yesu akinena leo kwenye kanda, si maandishi ya Mathayo, Marko, Luka au ya Yohana ya yale Yesu aliyosema (kwa maana wote walilisema tofauti kidogo), bali tungeweza kuisikia Sauti ya Yesu, utu Wake, aiko, pepa, na dafuta Zake kwa masikio yetu wenyewe, je! wahudumu leo wangeliambia kanisa lao, “Hatutaicheza rekodi ya Yesu kanisani mwetu. Mimi nimeitwa na nimepakwa mafuta kuihubiri na kuinukuu. Ninyi isikilizeni mwendapo nyumbani.” Je! watu wangelisimamia hilo? Inasikitisha kusema hivyo, lakini hivyo ndivyo wao wanavyofanya leo hii. HAKUNA TOFAUTI, haijalishi jinsi gani wanavyolipaka chokaa.

Kwangu mimi, Ndugu Branham alitupa kielelezo. Alipenda wakati makanisa yote, majumba, au popote pale walipokuwa, walipokuwa kwenye muunganisho wa simu ili waweze kuusikia Ujumbe wote kwa wakati mmoja. Yeye alijua wangeweza, na wangezipata, kanda na kuisikiliza baadaye, lakini yeye aliwataka waungane na kuusikia Ujumbe wote kwa wakati mmoja….KWANGU MIMI HUYO ALIKUWA NI MUNGU AKIMUONYESHA BIBI-ARUSI WAKE NINI KITATOKEA KATIKA SIKU YETU NA KIPI CHA KUFANYA.

Kila mhudumu mwaminio wa kweli wa Ujumbe atakubali hakuna kitu kilicho kikuu zaidi ya kukaa chini ya upako wa Sauti ya Mungu, ambayo imerekodiwa na kuwekwa kwenye kanda. Bibi-arusi ataamini, na kuwa na Ufunuo, ya kwamba Ujumbe huu ndilo Neno la Mungu la wakati huu. Ninaweza tu kuhukumu kwa Neno, lakini mtu ye yote ambaye hangesema Ujumbe huu ndiyo Yakini yao, hana Ufunuo wa Neno la wakati huu, kwa hivyo, wangewezaje kuwa Bibi-arusi Wake?

Siyo tu kulinukuu, kulihubiri au kulifundisha, bali kulisikia kwenye kanda ndipo MAHALI PEKEE ambapo Bibi-arusi anaweza kusema ninaliamini kila Neno. Ujumbe huu ni Bwana Asema Hivi. Kile ninachohubiri au ninachofundisha si Bwana Asema Hivi, bali yale Sauti ya Mungu isemayo kwenye kanda NDIYO…hiyo ndiyo Sauti PEKEE iliyothibitishwa na Nguzo ya Moto.

Ninajua kuna ndugu na dada wanaosema, na kuhisi, ati “Kama hamsikilizi Ujumbe ambao Maskani ya Branham inaoutuma, hamzisomi barua za Tai Wanakusanyika, na kusikiliza majumbani mwenu wakati ule ule wewe si Bibi-arusi,” ama, “Ni makosa kwenda kanisani, inakubidi ukae nyumbani kwako.” HILO NI KOSA SANA. Sijawahi KAMWE kuwaza hivyo, kusema hivyo, ama kuamini hivyo. Hilo limesababisha utengano hata na zaidi, fikra ngumu, na kuondoa ushirika miongoni mwa Bibi-arusi naye adui anatumia jambo hilo kuwatenganisha watu.

Sitaki kamwe kumtenganisha Bibi-arusi, nataka kumuunganisha Bibi-arusi kama vile Neno lilivyosema LAZIMA TUUNGANE TUWE KITU KIMOJA. Hatupaswi kubishana sisi kwa sisi, lakini hakuna kabisa kitu kingine chochote kile kinachoweza kutuunganisha ila Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.

Hatupaswi kuzozana na kuwaambia watu WANAPASWA WAFANYE nini la sivyo wao sio Bibi-arusi, ninyi fanyeni jinsi BWANA ANAVYOWAONGOZA. Wao bado ni ndugu na dada zetu. Tunahitaji kupendana na kuheshimiana mmoja kwa mwingine.

Sasa, usibishane. Unaona? Hasira huzaa hasira. Muda si muda wajua, unamhuzunisha Roho Mtakatifu anakuacha, utarudisha ubishi tena. Ndipo Roho Mtakatifu anaruka anaenda zake. Hasira huzaa hasira.

Kwa kile nabii alichosema hapa, sitaki kamwe kumhuzunisha Roho Mtakatifu. Sitaki kubishana kamwe. Tunaweza kusemezana kwa upendo, lakini si kubishana. Ikiwa nimesema jambo lolote ambalo limemuudhi yeyote katika yale niliyoyaandika ama kusema, tafadhali nisamehe, haikuwa kusudi langu.

Kama nilivyoeleza hapo awali, ninauhisi wito maishani mwangu kutoka kwa Bwana kuwaelekeza watu kwenye Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku hii. Wahudumu wengine wana miito mingine na pengine wanaona mambo tofauti, Bwana asifiwe, wanafanya kile WAO wanachojisikia wanaongozwa na Roho Mtakatifu. Huduma yangu ni kumwambia tu Bibi-arusi, “BONYEZA PLAY” na “Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda ndiyo Sauti iliyo muhimu zaidi mnayoweza kuisikia.” “Ninaamini kwamba wahudumu wanapaswa kuicheza Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda katika makanisa yao.”

Barua ninazoziandika kila wiki ni za sehemu ya Bibi-arusi wale wanaojisikia kuwa ni sehemu ya Maskani ya Branham. Najua wengine wengi huzisoma, Lakini mimi ninawajibika tu kufanya vile ninavyojisikia kuongozwa kwa ajili ya kanisa letu. Kila kanisa linajitawala lenyewe; hawanabudi kufanya vile wanavyojisikia wanaongozwa na Bwana kufanya, hilo ni Neno 100%. Mimi siwapingi wao, tunatofautiana tu. Mimi na Maskani ya Branham, tunataka tu kuisikia Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.

Ninaualika ulimwengu kuungana nasi kila wiki. Ninawatia moyo ikiwa hawawezi kuungana nasi, wachague kanda, kanda yoyote, na kubonyeza play. Watatiwa mafuta kuliko hapo kabla. Hivyo, ninawaalika wiki hii muungane nasi Jumapili saa 06:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapoungana pamoja na kusikia, 63-0630E Je! Maisha Yako Yanaistahili Injili?

Ndugu Joseph Branham

25-0907 Kutoka Kwa Tatu

UJUME: 63-0630M Kutoka Kwa Tatu

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Kutoka Kwa Tatu,

Ikiwa huna jicho la kiroho, hulipati. Lakini jicho la kiroho linaweza kuona Nguvu za Mungu zikitenda kazi maana hilo liko kwenye Neno kikamilifu. Ni Neno, nalo Neno la Mungu halibadiliki kamwe. Kile Yeye alichokifanya hapo mwanzo, anafanya vivyo hivyo sasa nalo jicho la kiroho linaliona, linaliamini, na KULISIKIA.

Ulimwengu unaweza kutokukubaliana nami katika kile ninachoamini kuwa ndiyo njia ya Mungu iliyoandaliwa Kwa ajili ya wakati huu: Sauti iliyo muhimu sana unayopaswa kuisikia ni Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. Ni lazima mzicheze kanda makanisani mwenu, lakini KAMA kweli mnauamini Ujumbe huu, basi hamwezi kupingana na kile nabii wa Mungu anachosema.

Jumapili hii tutakusanyika kama wale wana wa Kiebrania walivyofanya ili kuipata mana ile iliyokuwa imeandaliwa kwa ajili yao usiku kucha, ambayo ingewahifadhi siku inayofuata. Sisi tutakusanyika kwa ajili ya Mana yetu ya Kiroho itakayotutia nguvu kwa ajili ya kule Kutoka kwetu kukuu kunakokuja hivi karibuni.

Hakuna njia bora zaidi kuliko kumruhusu Sauti ya Mungu yeye aliseme hilo Mwenyewe, kumhusu yeye Mwenyewe, nao Ujumbe huu tunaoenda kuusikia UMESHEHENI!

Mungu alimpeleka mtu mmoja nyikani, akamfunza. Kisha akamrudisha, na kukipeleka kitu hicho huko, kisha akawatoa hao watu. Mnaona ninalomaanisha? Yeye hawezi kubadilisha mpango Wake. Yeye ni Mungu.

Kwa hivyo hapa Yeye anatuambia waziwazi Yeye kamwe habadilishi mpango Wake. Kile Yeye alichokifanya tangu mwanzo, atakifanya tena mwishoni, Yeye aliahidi. Kwa hiyo sasa ni lazima tujue Mpango Wake ulikuwa nini wakati ule kwani utakuwa ni Mpango ule ule hivi sasa.

Kamwe hatashughulika na kundi. Kamwe hajafanya hivyo. Yeye hushughulika na mtu mmoja; na alifanya hivyo, na atafanya hivyo. Na aliahidi, hata katika Malaki 4, angefanya hivyo.

Yeye kamwe hashughuliki na kundi. Kwa hivyo, Yeye aliahidi katika wakati wetu kwamba angemtuma mtu Mmoja, Malaki 4, akiwa na Bwana Asema Hivi.

Hiyo ni kweli. Kwa hiyo kuna ahadi Yake, kwamba Yeye alikuwa ni nani; ahadi ya kile alichosema Yeye angekifanya, na basi tumewasili. Tunapaswa kuwa ni watu wenye furaha jinsi gani; akiwapa ishara, kwa ishara ya Neno Lake lililoahidiwa, Neno lililoahidiwa. Aliahidi angefanya hivyo.

Mungu alichagua kumwongoza Bibi-arusi Wake namna gani wakati ule?

Mungu alichagua, katika siku za kule kutoka, Yeye aliliita kundi moja litoke. Na kutoka kwenye kundi hilo, ninawataka muone jambo fulani, Yeye alipata tu wawili walioingia kwenye nchi ya ahadi. Yeye alichagua kuwatoa kwa kutumia nini?

Hili hapa. Hili ni muhimu sana kwa wenye nia ya kiroho kuweza kulishika. Mungu alichagua kumwongoza na kumpeleka Bibi-arusi kwenye Nchi ya Ahadi namna gani?

Siasa? dhehebu? Yeye alichagua nabii, akiwa na ishara ya kimbinguni ya Nguzo ya Moto, watu wasije wakakosea. Yale nabii aliyosema yalikuwa ni Kweli. Na Mungu alishuka, Nguzo ya Moto, na kujithibitisha Mwenyewe, akaonyesha Neno Lake. Hiyo ni kweli? Hiyo ndiyo aliyoileta, kutoka Kwake kwa kwanza. Kutoka Kwake kwa pili…

Kwa hiyo, ili kuhakikisha kwamba watu hawangekosea, Yeye aliwatumia nabii akiwa na ishara ya kimbinguni ya Nguzo ya Moto kwa ajili ya kule kutoka kwao kukuu.

Yeye alifanya nini, kule kutoka kwa kwanza? Alimtuma nabii, aliyetiwa mafuta kwa Nguzo ya Moto, naye akawaita watu wakatoka. Huko kulikuwa ni kutoka Kwake kwa kwanza…

Kutoka kwa pili, Yeye alimleta Nabii, aliyetiwa mafuta, ambaye alikuwa ni Mwanawe, Mungu-Nabii. Musa alisema Yeye angekuwa ni Nabii; Naye alikuwa na Nguzo ya Moto, na akafanya ishara na maajabu…

Na hapa Yeye aliahidi jambo lile lile katika kule kutoka katika siku za mwisho, wala hawezi kulibadili…

Wengi watakubali kwa kusema, naam, Yeye alimtuma nabii kumwita Bibi-arusi atoke, lakini sasa hivi Roho Mtakatifu Yeye atamwongoza Bibi-arusi kupitia wahudumu; lakini Yeye hakusema hivyo…hebu na tuendelee kusoma.

Angalieni ile Nguzo ya Moto iliyowaita watoke, ikawaongoza kwenye nchi ya ahadi, chini ya upako wa nabii. Nguzo ya Moto ambayo wangeweza kuiangalia, iliwaongoza kwenye nchi ya ahadi, chini ya nabii aliyetiwa mafuta. Nao daima walimkataa. Hiyo ni kweli? Hakika.

Nguzo ii hii ya Moto inawaongoza watu tena kwenye Nchi ya ahadi, ule Utawala wa Miaka Elfu.

Ile Nguzo ya Moto, chini ya uongozi wa Mungu…Mungu alikuwa ni ule Moto, na ile Nguzo ya Moto ilimtia mafuta tu yule nabii. Ile Nguzo ya Moto ilikuwa isimame kama ushahidi wa Mbinguni kwamba Musa alikuwa ameitwa atoke.

Sasa, kumbukeni, Musa hakuwa hiyo Nguzo ya Moto. Yeye alikuwa ni kiongozi aliyetiwa mafuta, chini ya hiyo Nguzo ya Moto, na hiyo Nguzo ya Moto iliuthibitisha tu Ujumbe wake kwa ishara na maajabu.

Hakuna kosa, enyi marafiki. Si yale ninayosema mimi; mimi ni ndugu yenu tu. Lakini, ni yale Mungu anayowathibitishia, ndiyo yanayolifanya Kweli. Nguzo ile ile ya Moto aliyoitumia kwenye kule kwingine kuwili, Yeye ameileta miongoni mwenu leo, na kuithibitisha kisayansi.

Mungu kamwe habadilishi mpango Wake. Mungu anayo njia iliyoandaliwa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake leo: ile Nguzo ya Moto, chini ya uongozi wa Mungu… Mungu alikuwa ni ule Moto, na ile Nguzo ya Moto ilimtia mafuta tu nabii.

Kuna Sauti moja tu, nabii mmoja, aliye na Bwana Asema Hivi, William Marrion Branham. Yeye si ile Nguzo ya Moto, bali yeye ni kiongozi aliyetiwa mafuta chini ya hiyo Nguzo ya Moto.

Sote tunataka kuwa katika Mapenzi MAKAMILIFU ya Mungu. Neno Lake NDIYO mapenzi Yake Makamilifu. Neno lililothibitishwa la wakati wetu ni Ujumbe huu. Nabii Wake ndiye aliyechaguliwa kumwongoza Bibi-arusi Wake. Kama huliamini hilo, huwezi kuwa Bibi-arusi Wake.

Njooni mjiandae kwa ajili ya kule Kutoka kwetu kuu kwa kulisikia Neno Kamilifu la Mungu pamoja nasi Jumapili saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia: Kutoka Kwa Tatu 63-0630M.

Ndugu. Joseph Branham

25-0831 Mbona Unalialia? Nena!

UJUMBE: 63-0714M Mbona Unalialia? Nena!

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Kanisa la Mungu,

Mungu alinena na kusema, ““Mimi sitendi kazi duniani ila kupitia tu kwa mwanadamu. Mimi-Mimi- Mimi ndimi Mzabibu; nanyi ni matawi, na Mimi nitajijulisha Mweyewe tu ninapoweza kumpata mtu MMOJA, na Mimi nimemchagua yeye, William Marrion Branham. Mimi nimemtuma aje akamtoe Bibi-arusi Wangu. Nitaliweka Neno Langu kinywani mwake. Neno Langu litakuwa Neno Lake. Yeye atalinena tu Neno Langu na kusema tu yale Mimi nisemayo.”

Sauti ya Maandiko ilinena kupitia Nguzo ya Moto na kumwambia yeye, “Nimekuchagua wewe, William Branham. Wewe ndiye mtu huyo. Nilikuinua wewe kwa kusudi hili. Nitakuthibitisha kwa ishara na maajabu. Unashuka chini kule kulifunua Neno Langu na kumwongoza Bibi-arusi Wangu. Neno Langu halina budi kutimizwa na WEWE.”

Nabii wetu alikuwa anajua yeye alikuwa ametumwa kwa kusudi hilo hasa la kuzifunua siri zote za Biblia na kumwongoza Bibi-arusi wa Mungu kwenda Nchi ya Ahadi. Yeye alijua kile alichosema, Mungu angekiheshimu na kukitimiza. Nawatakeni msilisahau kamwe Neno hilo. Kile alichokisema nabii wetu, Mungu atakiheshimu, kwa maana Neno la Mungu lilikuwa ndani ya William Marrion Branham. Yeye ni Sauti ya Mungu kwa ulimwengu.

Yeye alijua alikuwa ndiye malaika-mjumbe wa saba wa Mungu aliyetiwa mafuta. Yeye alijua moyoni mwake mambo yote ambayo Mungu aliyokuwa ameyasema kumhusu yeye katika Neno Lake. Kile kilichokuwa kinawaka moyoni mwake kikawa halisi. Yeye alikuwa ametiwa mafuta na alijua alikuwa na BWANA ASEMA HIVI. Hakukuwa na kitu kingalimzuia yeye kutokwenda kulinena Neno la Mungu.

Mungu alimwambia yeye, “Neno Langu, na wewe, mjumbe Wangu, ni kitu kimoja.” Alijua yeye ndiye aliyechaguliwa kulinena Neno lisilokosea. Hilo ndilo tu yeye alilohitaji. Angeweza KUNENA, NAYE MUNGU ANGELITIMIZA.

Ufunuo wa Ujumbe huu NA mjumbe wa Mungu vimeitia mafuta imani yetu zaidi ya hapo awali. Imetupeleka katika miduara mikubwa. Hilo limetutenga na kila kitu isipokuwa Ujumbe Wake, Neno Lake, Sauti Yake, Kanda Zake.

Haijalishi sisi ni wachache jinsi gani, jinsi gani tunavyochekwa, jinsi tunavyodhihakiwa, haileti tofauti hata kidogo. SISI TUNALIONA. SISI TUNALIAMINI. Kuna kitu fulani ndani yetu. Tulichaguliwa tangu awali kuliona HILO na hakuna kitu kitakachotuzuia sisi tusiliamini HILO.

Tunakumbuka kile lile ono lilichosema, “rudi ukakihifadhi Chakula”. Hilo ghala lilikuwa wapi? Maskani ya Branham. Ni mahali gani nchini, ama ulimwenguni mahali popote, pangelinganishwa na Jumbe tulizo nazo? NDIYO Sauti pekee iliyothibitishwa na Mungu Mwenyewe kuwa Bwana Asema Hivi. SAUTI PEKEE!

Ni wapi pengine tungeweza, au tungetaka kwenda, wakati yeye alisema;

Hapa ndipo chakula kimehifadhiwa…

Umehifadhiwa hapa. Uko kwenye kanda; utaenda ulimwengu mzima katika kanda ambapo watu manyumbani mwao. Hizo kanda zitaangukia mikononi mwa wale waliochaguliwa tangu awali wa Mungu. Yeye anaweza kuliongoza Neno; yeye ataelekeza kila kitu kuelekea njia yake hasa. Hiyo ndiyo sababu Yeye alinituma nirudi nikafanye hivi. “Kihifadhi chakula hapa.”

Sisi ni Bibi-arusi Neno Wake Mkamilifu ambaye amedumu na Chakula Chake Kilichohifadhiwa. Hakuna haja ya kulialia tena, tunanena tu Neno na kusonga mbele, kwa kuwa sisi NI Neno.

Hakuna kitu cha kuhofia. Hakuna haja ya mikutano ya maombi ya usiku kucha kufunua sisi ni nani, Neno limekwishafunuliwa kwetu. Tunajijua sisi ni nani, kama vile yeye nabii wa Mungu, naye tayari amekwishatuambia ni nani ambaye angekwenda.

Kila mmoja wetu! Hata kama wewe ni mke wa nyumbani, ama u yaya mdogo, ama hata kama wewe ni mama kizee, ama kijana mwanamume, ama cho chote kile, tutaenda kwa vyo vyote. Hamna hata mmoja wetu atakayeachwa nyuma.” Amina. “Kila mmoja wetu ataenda. Hatutazuiwa na kingine chochote.”

Nena kuhusu kutupa IMANI ya Kunyakuliwa!!!

Njooni muungane na sehemu ya Bibi-arusi wa Mungu tunapokusanyika pamoja kwenye Sauti ya Mungu iliyothibitishwa, anaponena na kutuambia: Kipenzi Changu, Mteule Wangu, Bibi-arusi Wangu, Mbona Unalialia, Nena, na usonge mbele.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: 63-0714M Mbona Unalialia? Nena!

Saa: 06:00 MCHANA, Saa za Jeffersonville (ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki)

Mahali:

Bali kuna Kanisa moja tu halisi, hujiungi nalo; unazaliwa ndani yake. Waona? Na iwapo umezaliwa ukiwa ndani yake, Mungu Aliye Hai hutenda kazi kwako, akijifanya Mwenyewe ajulikane. Waona? Humo ndimo Mungu anamoishi, Kanisani Mwake. Mungu huenda Kanisani kila siku__huishi Kanisani, Yeye huishi ndani yako. Wewe ni Kanisa Lake. Wewe ni Kanisa Lake. Wewe ni hekalu anamoishi Mungu. Wewe binafsi ni Kanisa la Mungu Aliye Hai.

25-0824 Ushirika

UJUMBE: 65-1212 Ushirika

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Neno Lililothibitishwa Peke Yake,

Jinsi gani tunavyomshukuru Roho Mtakatifu kwa Ufunuo wa kweli wa Neno Lake lililothibitishwa la wakati huu. Wengi wanakiri kwamba wanaamini Ndugu Branham ndiye nabii wa Mungu anayetimiza Maandiko yaliyoahidiwa kumhusu yeye, lakini Ufunuo wa kweli wa Neno na mpango wa Mungu umefichwa kwao.

Kwa kila Ujumbe wa Barua ya mahaba ambao Bibi-arusi anaousikia, Mungu anatuthibitishia kwamba tuko katika Mapenzi Yake makamilifu kwa kuisikiliza Njia Yake iliyoandaliwa kwa ajili ya wakati huu, Sauti ya Mungu iliyo kwenye Kanda.

Nasi hatuna budi kumfuata, ndiyo njia pekee ya kupata Uzima wa Milele. Kwa hivyo uongozi wa Mungu ni: fuata Neno lililothibitishwa la wakati huu na Roho Mtakatifu.

NJIA PEKEE ya uzima wa Milele ni: Roho Mtakatifu kukuongoza kulifuata Neno lililothibitishwa. Ni nani aliye na Neno lililothibitishwa la wakati huu? Mungu alimchagua nani kulifasiri Neno Lake? Ni nani ambaye Mungu alimsema ndiye Sauti Yake ya wakati huu? Ni nani ambaye Mungu Mwenyewe alimsema alikuwa ndiye kiongozi aliyethibitishwa kumwongoza Bibi-arusi Wake leo? Je, Ni wahudumu?

Kama tu nilivyosema, maskini yule tai mdogo aliposikia Sauti ya Bwana Arusi, alienda Kwake, Neno la Mungu lililotiwa mafuta, lililothibitishwa kwa ajili ya siku hizi za mwisho.

Nuhu alikuwa ndiye Neno lililothibitishwa la wakati wake.

Musa alikuwa ndiye Neno lililothibitishwa la wakati wake.

Yohana alikuwa ni Neno lililothibitishwa

Wanaweza kulipindisha au kuliwekea fasiri yoyote Kwake watakayo, Bali:

WILLIAM MARRION BRANHAM NDIYE NENO LA MUNGU LILILOTHIBITISHWA LA WAKATI HUU!!

Kwa hivyo uongozi wa Mungu ni: fuata Neno lililothibitishwa la wakati huu na Roho Mtakatifu.

Na Je, kuicheza Sauti ya Mungu iliyothibitishwa katika kanisa lako silo jambo lililo muhimu kuliko ambalo Bibi-arusi analopaswa kufanya? Je, ni muhimu zaidi kuisikiliza sauti tofauti?

Je! ni kundi la watu na huduma yao ndiyo itakayomuunganisha na kumwongoza Bibi-arusi? Je, Bibi-arusi ataunganishwa na yale wasemayo wahudumu? Wote wanasema mambo tofauti, kwa hivyo tumfuate nani?

Je! Ni fasiri yao ya Ujumbe huu ndiyo tutakayohukumiwa kwayo? Je! wao wanayo Nguzo ya Moto inayoithibitisha huduma yao? Je! fasiri yao ya Neno ndiyo Yakini yako?

Nabii alisema Bibi-arusi ANGEUNGANA. Jiulize mwenyewe, ni kitu gani kitakachoufanya unabii huu utimie ili Bwana aje na kumnyakua Bibi-arusi Wake?

Ndiposa, watu wa Mungu waanzapo kukusanyika pamoja, kuna umoja, kuna nguvu. Ona? Na wakati wo wote watu wa Mungu watakapoungana pamoja kabisa, naamini ufufuo utatokea wakati huo. Kutakuwako na wakati wa kunyakuliwa Roho Mtakatifu aanzapo kuwakusanya. Wao—itakuwa katika uchache, bila shaka, lakini kutakuwepo na kukutanika kukuu.

Je! Kutakuwepo na kukutanika kukuu kwenye huduma ya mtu fulani, mbali na nabii wa Mungu aliyethibitishwa? Je! litakuwa ni KUNDI la wahudumu kwa sababu baadhi ya wahudumu wa huduma tano wanasema Hupaswi KAMWE kuicheza Sauti ya Mungu kanisani mwako, ni makosa. Je! wao watamwongoza Bibi-arusi basi?

TAFADHALI NISAIDIE! NI MHUDUMU GANI NINAYEPASWA KUMFUATA, KWANI NATAKA KUUNGANA KATIKA KULE KUKUTANIKA KUKUU.

Wengine husema ati wahudumu wa huduma tano wa Ngurumo Saba ndiyo watakaomkamilisha Bibi-arusi. Baadhi ya wahudumu wa huduma tano wanasema siku za huduma ya Mtu Mmoja zimekwisha. Baadhi ya wahudumu wa huduma tano wanasema yatubidi turudi kwenye Pentekoste. Wengine husema Ujumbe SIO Yakini. Wengine wanasema ukizicheza kanda wewe ni mwamini mungu-mtu. Wote wanasema kitu fulani tofauti, na WOTE wana fasiri tofauti, mawazo tofauti, lakini kila mmoja anasema WAO wanaongozwa na Roho Mtakatifu.

NI MHUDUMU GANI WA HUDUMA TANO NIMFUATE? Maadamu ninamfuata mchungaji “WANGU” wa huduma tano, nitakuwa Bibi-arusi? Kuna “Vikundi” vingi tofauti vya wahudumu wa huduma tano. Hawa wahudumu 20 wanakusanyika na kufanya mikutano yao, lakini wao hawakubaliani kabisa na wahudumu hao wengine 20 walio na mikutano tofauti…niende kwenye mikutano gani ili nikamilishwe na kuungana…baadhi ya hiyo…yote?

Nao watu wanaamini ati MCHAFUKO HUU UTAMUUNGANISHA NA KUMKAMILISHA BIBI-ARUSI? Wote wanasema wao ni WATUMISHI WA KWELI WA HUDUMA TANO ALIYEITWA NA MUNGU. Lakini wao hawawaongozi ninyi kwenye UONGOZI WA KWELI WA ROHO MTAKATIFU, WAO WANAWAONGOZA NINYI KWAO WENYEWE NA KWENYE HUDUMA YAO.

Kwangu mimi, hata huhitaji ufunuo kujua kwamba hilo haliwezi kamwe KUMUUNGANISHA au KUMUONGOZA Bibi-arusi wote. Ni NENO PEKE YAKE litakalomuunganisha Bibi-arusi, kwa SAUTI YA MUNGU MWENYEWE ILIYO KWENYE KANDA.

Ndugu na dada, afadhali muamke ikiwa mnamfuata mchungaji ambaye anahubiri tu na kunukuu Neno, ambalo ni zuri na NDILO HASA analopaswa kuwa akifanya, lakini yeye hawaambii, na muhimu zaidi, HAFANYI HIVYO, kuicheza SAUTI YA MUNGU ILIYO KWENYE KANDA KANISANI MWENU.

Ndugu Branham alituambia:

Naam, tuna tu maagizo matatu ya Kiungu tuliyoachiwa: mojawapo ni—ni ushirika; kutawadhana miguu; ubatizo wa maji. Hayo ndiyo tu mambo matatu. Huo ndio ukamilifu, wa utatu, mnaona.

Ningependa tuwe na Ibada ya Ushirika na Kutawadhana Miguu Jumapili hii, Bwana akipenda. Kama tulivyofanya wakati uliopita, ningewahimiza muanze saa 11:00 JIONI. kwa masaa ya eneo mnaloishi. Ingawa Ndugu Branham alisema mitume walikuwa na Ushirika kila wakati walipokutana pamoja, alipendelea kuufanya wakati wa jioni, naye akautaja kama Meza ya Bwana.

Ujumbe na Ibada ya Ushirika utakuwa kwenye Redio ya Sauti, na pia kutakuwa na anuani ya faili lakupakuliwa, kwa wale ambao hawawezi kuifanikisha Redio ya Sauti Jumapili jioni.

Ndugu Joseph Branham

25-0810 Matukio Ya Sasa Yanadhihirishwa Na Unabii

UJUMBE: 65-1206 Matukio Ya Sasa Yanadhihirishwa Na Unabii

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Kweli na Aliye Hai,

Wakati Yesu, Neno Mwenyewe, alipokuja duniani miaka 2000 iliyopita, Yeye alikuja kama vile alivyosema angekuja, kama Nabii. Neno Lake linatangaza, ya kwamba kabla Yeye hajaja tena, kule kudhihirishwa kukamilifu kwa Utu wa Yesu Kristo kutadhihirishwa tena katika mwili, katika nabii. Nabii huyo amekuja, jina lake ni William Marrion Branham.

Mtu yeyote anawezaje kutotambua kwamba kuisikiliza Sauti ya Mungu ikizungumza nao moja kwa moja kwenye kanda ndiyo Mapenzi makamilifu ya Mungu? Tunajua Neno daima humjia nabii Wake; Haliwezi kuja kwa njia nyingine yoyote. Halina budi kuja kupitia njia ya Mungu ambayo Yeye alitutabiria. Hiyo ndiyo njia pekee litakavyopata kuja. Mungu anasonga mbele moja kwa moja jinsi Yeye alivyoahidi angefanya. Yeye kamwe hakosi kufanya kwa njia ile ile Yeye aliyofanya daima.

Kila mmoja wao alikula kitu kile kile, wote walicheza katika Roho, wote walikuwa na kila kitu shirika; bali ilipofikia wakati wa utengano, Neno lilitenganisha. Ndivyo ilivyo siku hizi! Neno lilitenganisha! Wakati utakapowadia…

Tunauona wakati huo unatukia sasa hivi, Neno linatenganisha. Bibi-arusi anashutumiwa kwa kumwinua sana nabii wakati wao wanaposema, “Kuna wengine walioitwa na Mungu, watu waliojazwa na Roho Mtakatifu wa kumwongoza Bibi-arusi leo. Mnahitaji zaidi ya hizo kanda tu. Mungu amewaweka watu leo kuliongoza kanisa.”

“Unajaribu kuwazia wewe ndiwe uliye peke yako kwenye kundi lile. Kusanyiko lote ni takatifu!” Mungu kamwe hajawahi kushughulika jinsi hiyo. Alipaswa kuwa amejua vyema kuliko hivyo. Naye akasema, “Vema, kusanyiko lote ni takatifu. Unajaribu kujifanya…” Kama tungalilisema siku hizi, maneno ya mtaani, “Changarawe pekee ufukoni.”

Naye Musa alijua ya kwamba Mungu alikuwa amemtuma huko chini kwa ajili ya jambo hilo.

Mungu anao watu waliojazwa na Roho Mtakatifu wa kumwongoza Bibi-arusi Wake; kuwaongoza KWENYE BWANA ASEMA HIVI, NABII-MJUMBE. Kwani Ujumbe na mjumbe ni kitu kimoja. Hiyo ndiyo njia ya Mungu isiyobadilika kamwe kwa ajili ya siku hii, na daima.

Kwa sababu walisikiliza kosa fulani. Wakati Musa, aliyethibitishwa na Mungu, na kiongozi wa kuwaonyesha njia ya kwenda kwenye nchi ya ahadi, nao walikuwa wamekuja umbali huo vema, lakini basi wasingeendelea pamoja naye… Sasa, waaminio wanaweza kuona jambo hilo, bali wasioamini hawawezi kuliona Hilo limethibitishwa.

Sio tu kwamba wewe ulichaguliwa kuupokea Ufunuo huu mkuu wa wakati wa mwisho wa siku hii, bali Mungu, kwa njia ya Chakula Chake kilichohifadhiwa cha kanda, hunena katikati ya mistari na Bibi-arusi Wake kipenzi.

Ndipo endapo wewe ni mwana wa Mungu ama binti ya Mungu, ulikuwa ndani ya Mungu wakati wote. Lakini Yeye alijua utapandwa kwenye tuta gani na katika wakati gani. Kwa hiyo sasa umefanywa kiumbe, mwana wa Mungu, mwana ama binti ya Mungu aliyedhihirishwa upate kukabiliana na changamoto ya wakati huu kumthibitisha Mungu wa kweli na aliye hai wa wakati huu, Ujumbe unaotokea katika wakati huu. Hiyo ni kweli! Ulikuwapo pale kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Ni barua ya mahaba ilioje ya katikati ya mistari kwa Bibi-arusi Wake, UTUKUFU!!! Sio tu kwamba Yeye alitujua na kutuchagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, bali hapa Yeye anatuambia kwamba alituchagua sisi tuwe wana na binti zake waliodhihirishwa wa SIKU HII. Alituweka hapa duniani leo, juu ya watakatifu wengine wote tangu mwanzo, kwa maana Alijua sisi tungekabiliana na changamoto ya wakati huu kumthibitisha Mungu wa kweli na aliye hai wa wakati huu, Ujumbe unaotokea katika wakati huu.

Sisi tulikuwa ndani ya Mungu, jeni, neno, sifa tangu mwanzo, lakini SASA tunaketi PAMOJA katika ulimwengu wa roho katika Kristo Yesu, tukishiriki pamoja Naye kwa Neno Lake, kupitia Neno Lake; kwa kuwa sisi ni NENO LAKE, nalo linazilisha nafsi zetu.

Hatuwezi, na hatutaingiza Kitu chochote maishani mwetu ila Neno la Mungu lisiloghoshiwa. Tunatambua na kuamini kuwa Ndio njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku hii.

Tungependa muungane nasi Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapoisikia SAUTI PEKEE, Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda, unayoweza kusema AMINA kwayo, kwa kila Neno unalosikia.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: Matukio Ya Sasa Yanadhihirishwa Na Unabii 65-1206

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Mwanzo 22
Kumbukumbu la Torati 18:15
Zaburi 16:10 / 22:1 / 22:18 / 22:7-8 / 35:11
Isaya 7:14 / 9:6 / 35:7 / 50:6 / 53:9 / 53:12 / 40:3
Amosi 3:7
Zekaria 11:12 / 13:7 / 14:7
Malaki 3:1 / 4:5-6
Mathayo 4:4 / 24:24 / 11:1-19
Luka 17:22-30 / 24:13–27
Waebrania 13:8 / 1:1
Yohana 1:1
Ufunuo 3:14-21 / 10:7

25-0803 Mambo Yatakayokuwapo

UJUMBE: 65-1205 Mambo Yatakayokuwapo

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Sifa za Mungu,

Kila Neno lililonenwa katika Ujumbe huu ni barua ya mahaba kwa Bibi-arusi Wake. Kuwazia kwamba Baba yetu wa Mbinguni Yeye anatupenda sana, si tu kwamba Yeye alitaka tulisome Neno Lake, bali Alitaka tuisikie Sauti Yake ikizungumza na mioyo yetu ili aweze kutuambia: “Wewe ndiye usia Wangu ulio hai, sifa Yangu iliyo hai, ambayo ninaweza kuionyesha kwa ulimwengu.”

Kisha kuwazia kwamba baada ya dhabihu zake zote alizotoa hapa duniani, maisha aliyoishi, njia aliyofuata. Aliomba jambo moja:

“Ili nilipo Mimi, nao wawepo.” Yeye aliomba ushirika wetu. Hicho ndicho kitu pekee alichomwomba Baba katika maombi, ushirika wenu milele.

Nilipo Mimi, “Neno Lake,” hatuna budi kuwapo pia, kupokea ushirika Wake, ushirika Wake, milele. Kwa hiyo, ni lazima tuishi kwa kila Neno Yeye alilonena nasi kwenye kanda ili tuwe Bibi-arusi Neno Bikira Wake, ambalo linatufanya kuwa sehemu ya Bwana-arusi.

Huo ndio UFUNUO wa Yesu Kristo katika wakati huu. Si vile Yeye alivyokuwa katika wakati mwingine, Yeye ni nani SASA HIVI. Neno la siku hii. Mungu yuko wapi leo. Huo ndio Ufunuo wa siku hii. Sasa unakua katika Bibi-arusi, ukitufanya kufikia kimo kikamilifu cha wana na binti.

Tunajiona wenyewe katika Neno Lake. Tunajua sisi ni nani. Tunajua tuko katika mpango Wake. Hii ndiyo Njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku hii. Tunajua Unyakuo umekaribia. Hivi karibuni wapendwa wetu wataonekana. Kisha tutajua: Tumewasili. Sote tunaenda Mbinguni…ndiyo, Mbinguni, mahali halisi tu kama hapa.

Tunaenda mahali halisi ambapo tutafanya mambo, ambapo tutaenda kuishi. Tutafanya kazi. Tutapafurahia. Tutaishi. Tunaenda kwenye Maisha, kwenye Maisha halisi ya Milele. Tunaenda Mbinguni, paradiso. Kama tu vile Adamu na Hawa walivyoshughulika, na kuishi, na kula, na kufurahia, katika bustani ya Edeni kabla dhambi haijaingia, tuko njiani tukirudi moja kwa moja kule tena, moja kwa moja, kurudi moja kwa moja. Adamu wa kwanza, kwa njia ya dhambi, alitutoa. Adamu wa Pili, kwa njia ya haki, anaturudisha kutuingiza ndani tena; anatuhesabia haki na kuturudisha ndani.

Mtu yeyote anawezaje kuliweka katika maneno Kile jambo hili linachomaanisha kwetu sisi? Uhalisia kwamba tunakwenda kwenye paradiso ambapo tunaishi katika umilele wote pamoja. Hakuna huzuni tena, maumivu au kilio, ni ukamilifu tu juu ya ukamilifu.

Mioyo yetu inafurahi, roho zetu zinawaka moto ndani yetu. Shetani anazidi kutupa presha kila siku, lakini bado tunafurahi. Kwa nini:

• TUNAJUA, SISI NI NANI.
• TUNAJUA, HATUJA, NA HATUTA, MWANGUSHA YEYE.
• TUNAJUA, TUKO KATIKA MAPENZI YAKE MAKAMILIFU.
• TUNAJUA, YEYE AMETUPA UFUNUO WA KWELI WA NENO LAKE.

Ndugu Joseph, unaandika jambo lile lile kila wiki. UTUKUFU, nitaliandika kila wiki kwa sababu Yeye anakutaka ujue jinsi gani anavyokupenda. Wewe ni nani. Ni wapi unakokwenda. Hasi inakuwa chanya. Wewe ni Neno ukifanyika Neno.

Mpendwa ulimwengu, njooni muungane nasi Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville, (ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) kwenye mawasiliano ya simu, si kwa sababu “Mimi” ninawaalika, bali kwa sababu “YEYE” anawaalika. Si kwa sababu “Mimi” niliichagua kanda, bali kulisikia Neno pamoja na sehemu ya Bibi-arusi ulimwenguni kote kwa wakati mmoja.

Je! tunaweza kutambua kwamba inawezekana kwa Bibi-arusi kuisikia Sauti ya Mungu ulimwenguni kote, wote kwa wakati ule ule hasa? Huyo hana budi kuwa ni Mungu. Mungu alimfanya nabii afanye hivyo wakati ule malaika Wake alipokuwa hapa duniani. Yeye alimuhimiza Bibi-arusi kuungana katika maombi, WOTE KWA WAKATI ULE ULE WA JEFFERSONVILLE, saa 3:00, 6;00, 9:00; hilo ni kuu jinsi gani sasa hivi, kwamba Bibi-arusi anaweza kuungana kama KITU KIMOJA kuisikia Sauti ya Mungu ikinena nao wote kwa wakati mmoja?

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: Mambo Yatakayokuwapo 65-1205

Maandiko:

Mathayo 22:1-14
Yohana 14:1-7
Waebrania 7:1-10

25-0727 Unyakuo

UJUMBE: 65-1204 Unyakuo

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Bila Masharti,

Bwana alitupa wakati mzuri sana kambini wiki iliyopita alipotufunulia Neno Lake. Alithibitisha, kwa Neno Lake, ya kwamba Yakini yetu ni: Neno Lake, Ujumbe Huu, Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda; wote ni mmoja, Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. 

Tulisikia jinsi ambavyo shetani anavyojaribu kuutenganisha Ujumbe kutoka kwa mjumbe, lakini Bwana Yesu asifiwe, Mungu Mwenyewe alinena kupitia malaika Wake Mwenye nguvu na kutuambia:

Tunaona ya kwamba mtu anapokuja, ametumwa kutoka kwa Mungu, amechaguliwa na Mungu, akiwa na BWANA ASEMA HIVI ya kweli, ujumbe huo na mjumbe huyo ni mmoja na kitu kimoja. Kwa sababu yeye ametumwa kuwakilisha BWANA ASEMA HIVI, Neno kwa Neno, kwa hiyo yeye pamoja na ujumbe wake ni mmoja.

Huwezi kuutenganisha Ujumbe na mjumbe, wao ni kitu kimoja, BWANA ASEMA HIVI. Haijalishi kile mpakwa mafuta yeyote wa uongo anachosema, Mungu alisema wao ni mmoja na hawawezi kutenganishwa.

Kisha akatuambia hatuhitaji tambara la chujio ili kuwashika wadudu wowote wakati tunapozisikiliza kanda, kwa maana hakuna wadudu ama utomvu wa mdudu katika Ujumbe Huu. Ni kisima Chake kinachofoka maji ambacho daima kinatiririka kisafi na cheupe. Hububujika daima, hakikauki kamwe, kinaendelea tu kusukuma na kusukuma, kikitupa Ufunuo zaidi na zaidi wa Neno Lake.

Yeye alitukumbusha KAMWE TUSISAHAU kwamba agano Lake na sisi ni lisilopingika, halibadiliki, lakini zaidi ya yote, halina Masharti.

Iwe ni upendo, usaidizi au kujisalimisha, ikiwa jambo lisilo na masharti ni YAKINI nalo halijatii sheria na masharti yoyote maalum: litatendeka bila kujali ni nini kingine kitakachotokea.

Kisha akataka kuushindilia msumari, kwa hivyo akatuambia kwamba leo hii Maandiko Yake yanatimizwa mbele ya macho yetu.

J-u-a lile lile lipambazukalo mashariki ndilo j-u-a lile lile litualo magharibi. Na M-w-a-n-a yule yule wa Mungu aliyetokea mashariki na kujithibitisha Mwenyewe kama Mungu aliyefanyika mwili ndiye M-w-a-n-a yule yule wa Mungu aliyeko katika kizio cha magharibi cha dunia ambaye anajitambulisha Mwenyewe kati ya kanisa usiku huu, Yeye yule jana, leo, na hata milele. Ile Nuru ya jioni ya Mwana imekuja. Leo Maandiko haya yametimia mbele yetu.

Yule Mwana wa Adamu amekuja tena katika mwili wa mwanadamu katika siku yetu, kama vile tu Yeye alivyoahidi angefanya, kumwita Bibi-arusi atoke. Ni Yesu Kristo akizungumza nasi moja kwa moja, na haihitaji fasiri yoyote ya mwandamu. Kitu pekee tunachohitaji, kitu pekee tunachotaka, ni Sauti ya Mungu inayonena kwenye kanda kutoka kwa Mungu Mwenyewe.

Ni ufunuo wa dhihirisho la Neno likifanywa halisi. Nasi tunaishi katika siku hiyo; Mungu asifiwe; Ufunuo wa siri ya Yeye Mwenyewe.

Ni wakati mtukufu jinsi gani Bibi-arusi aliyonao, akiwa amekaa kwenye uwepo wa Mwana, akiivishwa. Ngano imeirudia ngano tena, na hakuna chachu miongoni mwetu. Ni Sauti ya Mungu safi tu ikinena nasi, ikitufinyanga na kutufanya kuwa sura ya Kristo, aliye Neno.

Sisi ni wana na binti za Mungu, sifa Yake ile aliyoichagua tangu zamani ije katika wakati huu, wakati ulio mkuu sana katika historia ya ulimwengu.  Yeye alijua sisi hatungeshindwa, hatungepatana, bali tungekuwa Bibi-arusi Neno Wake mkweli na mwaminifu, Uzao Wake Mkuu wa Kifalme wa Ibrahimu ulioahidiwa ambao ungekuja.

Unyakuo umekaribia. Wakati umefika mwisho. Yeye anakuja kumchukua Bibi-arusi Wake ambaye amejiweka mwenyewe tayari bali amekaa kwenye Uwepo wa Mwana, akiisikia Sauti Yake ikimvika Bibi-arusi Wake. Hivi karibuni tutaanza kuwaona wapendwa wetu walioko ng’ambo ya pazia la wakati, ambao wanatungojea na kutamani sana kuwa pamoja nasi.

Kanda ndiyo njia iliyoandaliwa na Mungu ya kumkamilisha Bibi-arusi Wake. Kanda hizi ndicho kitu pekee kitakachomuunganisha Bibi-arusi Wake. Kanda hizi ndiyo Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi Wake.

Ninawalika mje muungane nasi, sehemu ya Bibi-arusi Wake, Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia kila kitu kuhusu kile kinachokaribia kutukia hivi karibuni: Unyakuo 65-1204. 

 
Ndugu. Joseph Branham

25-0720 Juu Ya Mbawa Za Hua Mweupe Kama Theluji

UJUMBE: 65-1128E Juu Ya Mbawa Za Hua Mweupe Kama Theluji

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukusanyike pamoja Jumapili saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) ili kusikia  65-1128E Juu Ya Mbawa Za Hua Mweupe Kama Theluji.

Ndugu. Joseph Branham