UJUMBE: 65-0418M Ni Kuchomoza Kwa Jua
All posts by admin5
26-0404 Kuzikwa
26-0403 Ukamilifu
24-0402 Ushirika
PASAKA 2026 – Ibada Maalum ya Ushirika na Kutawadhana MIGUU
Wapendwa Raia Wenza Wa Ufalme,
Pasaka hii inaahidi kuwa Pasaka iliyo kuu kuliko ambayo Bibi-arusi amewahi kuwa nayo. Tumekuwa tukiketi katika Uwepo wa Mwana, tukiivishwa, tukijitambua sisi ni nani. Ule utimilifu wa Yesu Kristo unadhihirishwa ndani ya kila mmoja wetu huku Neno Lake, Sauti Yake, ikipiga kelele, Tai kwa tai, ikituita kutoka kwenda kwenye Karamu yetu ya Arusi.
Kila mwaka wakati huu Bibi-arusi anaisubiri kwa hamu kubwa wikendi ijayo ya Pasaka. Wakati ambapo Yeye atatuunganisha kutoka kote ulimwenguni kwa siku nne mfululizo, tukimwabudu Yeye, tukimshukuru Yeye, tukimsifu Yeye; kwa maana Yeye amefufuka na anaishi ndani ya kila mmoja wetu. Bwana Arusi na Bibi-arusi wanakuwa MMOJA.
Yeye anatupa sisi wakati huu maalum wa kufungia nje vitu vyote vya kilimwengu vinavyotuzunguka na kuutumia tu muda pamoja Naye. Hakuna vizubaishi vya kilimwengu huu, huku tunapouumba ulimwengu wetu wenyewe pamoja Naye. Tufunge milango yetu, tuvizime vifaa vyetu vyote vya kielektroniki na chochote kinachotukengeusha kutoka Kwake.
Haja iliyo kuu ambayo kila mmoja wetu aliyonayo ni kuwa karibu Naye. Tunataka kuishi maisha yaliyowekwa wakfu zaidi kwa ajili Yake; kuwa daima katika mapenzi Yake makamilifu. Kuwa tayari kwa ajili ya Kuja Kwake. Hakuna chochote katika ulimwengu huu, au katika maisha yetu, kilicho muhimu zaidi kuliko hili.
Yeye ametupa sisi fursa hii maalum ya kuutumia tu muda pamoja Naye, kuzungumza na kumtafakari Yeye. Kuingia katika uwepo Wake na kuifungua mioyo yetu Kwake. ITAKUWA IBADILISHAYO MAISHA KWA BIBI-ARUSI WAKE!
Yeye anajua yaweza kuwa vigumu kwa baadhi yenu wenye watoto, familia, na majukumu mengine tuliyo nayo, lakini tukiitumia kila sekunde huru tuliyonayo kuzungumza Naye, kumkaribia Yeye, kumfungulia Yeye mioyo yetu, kutakuwako na badiliko kubwa katika kutembea kwetu pamoja Naye, hata hatutakuwa vile tulivyokuwa.
Kama vile Yeye alivyofanya katika ile siku ya Musa alipowaleta watoto Wake majumbani mwao, damu ilikuwa imepakwa nao walikuwa wakijiandaa kwa ajili ya kule Kutoka kwao; itakuwa vivyo hivyo na wikendi hii maalum ya Pasaka ambayo Yeye ameiandaa kwa kila mmoja wetu.
ALHAMISI
Ilikuwa ni Alhamisi usiku ambapo Bwana Yesu aliila Karamu ya Mwisho pamoja na wanafunzi Wake, katika ukumbusho wa Pasaka kabla ya kule kutoka kwa wana wa Israeli. Tunayo fursa iliyoje ya kufanya ushirika na Bwana majumbani mwetu, kabla ya wikendi yetu takatifu, na kumwomba Yeye atusamehe dhambi zetu, na atupe yote tunayohitaji katika safari yetu.
Baba wa Mbinguni, tunashukuru kwa ajili ya jambo hili, wakati mwingine wa kukusanyika pamoja, upande huu wa Umilele. Na tunatarajia asubuhi ya leo kuhuishwa upya kwa nguvu kuja kutoka Kwako, zipate kututia moyo kwa ajili ya safari iliyoko mbele. Tumekusanyika kama wana wa Kiebrania walivyofanya asubuhi na mapema, kuokota mana iliyokuwa imetolewa kwa ajili yao usiku kucha, kuwapa nguvu kwa ajili ya siku ijayo. Tunakusanyika kwa ajili ya Mana ya kiroho, asubuhi ya leo, ipate kutupa nguvu kwa ajili ya safari.
Hebu sote tuanze saa 12:00 KUMI NA MBILI JIONI. masaa ya eneo unaloishi ili kusikiliza Ushirika 62-0204, na kisha nabii atatupeleka kwenye ibada yetu maalum ya Ushirika na Kutawadhana Miguu baada ya kanda kukamilika, ambayo itachezwa kwenye app ya Lifeline (kwa Kiingereza), au unaweza kuipakua ibada hiyo kwa Kiingereza au lugha zingine kwa kubofya anuani iliyo hapa chini.
IJUMAA
Hebu na twende katika maombi pamoja na familia zetu saa 3:00 TATU ASUBUHI,(Ni saa 10:00 KUMI JIONI ya Afrika Mashariki) na kisha tena saa 06:00 SITA MCHANA,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki), tukimwalika Bwana awe pamoja nasi na kuzijaza nyumba zetu kwa Roho Mtakatifu tunapojiweka wakfu Kwake.
Hebu akili zetu na zirudi huko nyuma hadi kwenye siku ile pale Kalvari, yapata miaka 2000 iliyopita, na kumwona Mwokozi wetu akining’inia msalabani. Na tukumbuke ile gharama kuu Yeye aliyoilipa kwa ajili yetu. Yeye alikuwa Mwana wa Mungu asiye na dhambi, lakini ilibidi ateseke kuliko mtu mwingine angeweza kuteseka, kwa sababu dhambi zetu sisi ziliwekwa juu Yake.
Ilibidi amtume Yeye kuzimu akiwa amehukumiwa (Unaona?), kwa sababu Yeye alizichukua dhambi zetu. Naye Kristo alikufa, si mwenye haki; Kristo alikufa mwenye dhambi. Unaona? Kristo mwenyewe hakutenda dhambi, bali alizichukua dhambi zetu juu Yake.
Kisha saa 06:30 SITA NA NUSU MCHANA,(Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) na tuungane pamoja majumbani mwetu kusikia: 57-0419 Ukamilifu.
Kisha na tuungane tena katika maombi mara tu baada ya ibada, katika ukumbusho wa kusulubiwa kwa Bwana wetu.
JUMAMOSI
Hebu na tuungane tena sote katika maombi saa 3:00 ASUBUHI (Ni saa KUMI JIONI ya Afrika Mashariki) na saa 06:00 SITA MCHANA,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) na tuiandae mioyo yetu kwa ajili ya mambo makuu Yeye atakayotutendea sisi miongoni mwetu.
Ninaweza kumsikia akisema, “Shetani, njoo hapa!” Yeye ni Bosi sasa. Ananyosha mkono, anaunyakua ule ufunguo wa mauti na kuzimu kutoka ubavuni mwake, akauning’iniza ubavuni Mwake Mwenyewe. “Ninataka kukupa notisi. Umekuwa laghai muda mrefu kutosha. Mimi ni Mwana wa Mungu aliye hai niliyezaliwa na bikira. Damu Yangu ingali imelowa msalabani, na deni kamili limelipwa! Huna haki tena. Umenyang’anywa zote. Nipe funguo hizo!”
Kisha saa 06:30 SITA NA NUSU MCHANA,(Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) sote tutakusanyika pamoja kulisikiliza NENO: 57-0420 Kuzikwa.
Hii itakuwa SIKU ILIYO MAALUM vipi kwa Bibi-arusi Wake kote ulimwenguni.
Kisha hebu na tuungane tena pamoja katika maombi mara tu baada ya ibada.
JUMAPILI
Hebu kwanza na tuamke mapema kama vile Ndugu Branham alivyofanya asubuhi ile wakati rafiki yake mdogo, robini, alipomwamsha saa 11:00 Alfajiri. Natumshukuru tu Bwana kwa kumfufua Yesu kutoka kwa wafu:
Saa kumi na moja asubuhi ya leo, maskini rafiki yangu mwenye kifua chekundu aliruka dirishani akaniamsha. Ilionekana kana kwamba moyo wake mdogo ungepasuka, akisema, “Amefufuka.”
Saa 3:00 TATU ASUBUHI, (Ni saa KUMI JIONI ya Afrika Mashariki) tuungane tena katika mnyororo wetu wa maombi, tukiombeana na kujiandaa kuisikia Sauti ya Mungu.
Saa 3:30 TATU NA NUSU ASUBUHI, (Ni saa KUMI NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) tutakusanyika pamoja kuusikiliza Ujumbe wetu wa Pasaka: 65-0418M Ni Kuchomoza kwa Jua.
Saa 06:00 SITA MCHANA. (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tutaziinua sauti zetu Kwake tukimshukuru kwa ajili ya Nguvu za Kuhuisha.
Saa 9:00 TISA ALASIRI.(Ni saa 4:00 NNE USIKU ya Afrika Mashariki), Hebu na tuungane tena katika maombi, tukimshukuru Yeye kwa ajili ya WIKENDI YA KUPENDEZA ALIYOTUPA SISI PAMOJA NAYE NA BIBI-ARUSI WAKE KOTE ULIMWENGUNI.
Kwa ndugu na dada zangu walio nchi za ng’ambo, kama vile mwaka jana, ningependa kuwaalika muungane nasi katika masaa ya Jeffersonville, kwa masaa yote ya maombi katika ratiba hii. Hata hivyo, ninatambua kwamba kuzicheza Kanda Alhamisi, Ijumaa, na Jumamosi alasiri kwa masaa ya Jeffersonville itakuwa vigumu sana kwa wengi wenu, kwa hivyo tafadhali jisikieni huru kuzicheza Jumbe hizo kwa masaa yafaayo kwenu. Hata hivyo, ningependa sote tuungane pamoja Jumapili saa 3:30 TATU NA NUSU ASUBUHI masaa ya Jeffersonville (Ni saa 10:30 KUMI NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki), kuusikia Ujumbe wetu wa Jumapili pamoja.
Pia ningependa kukualika wewe na watoto wako kuwa sehemu ya vipindi vya Creations, Journaling na mapishi, ambayo familia yako yote inaweza kufurahia pamoja. Tunafikiri mtayapenda kwani yote yanalenga NENO tutakalolisikia wikendi hii.
Kwa ajili ya ratiba ya wikendi, taarifa kuhusu jinsi ya kujiandaa kwa ajili ya ibada ya Ushirika, nyenzo zitakazohitajika Kwa ajili ya vipindi vya Creations, na taarifa nyinginezo, tazama anuani zilizo hapa chini.
Hebu tuzifunge simu zetu kwa ajili ya wikendi ya Pasaka isipokuwa kupiga picha, kusikiliza Nukuu ya Siku, na kucheza kanda kutoka kwenye app ya The Table, app ya Lifeline, au kwenye anuani ya kupakulia.
Ni heshima kubwa kwangu kukualika wewe na familia yako kuja pamoja na Bibi-arusi ulimwenguni kote katika wikendi iliyojaa KUABUDU, KUSIFU NA UPONYAJI. Ninaamini kweli hii ni wikendi ambayo itayabadilisha maisha yako milele.
Ndugu Joseph Branham
26-0329 Huyu Melkizedeki Ni Nani?
UJUMBE: 65-0221E Huyu Melkizedeki Ni Nani?
- 26-0329 Huyu Melkizedeki Ni Nani?
- 24-0630 Huyu Melkizedeki Ni Nani?
- 22-1204 Huyu Melkizedeki Ni Nani?
- 19-0707 Huyu Melkizedeki Ni Nani? + Preliminari
- 17-1105 Huyu Melkizedeki Ni Nani? +Preliminari
Mpendwa Bibi-arusi Wa Uzima Wa Milele,
Sauti hiyo ni nani inayozungumza nasi kwenye kanda?
Tunaweza tu kujua jibu la swali hilo kwa Ufunuo kutoka kwa Mungu. Ni Bibi-arusi Wake aliyechaguliwa tangu zamani peke yake ndiye atakayekuwa na Ufunuo huo. Kwa hivyo, lazima tutafute Neno Lake ili kuelewa alisema Yeye alikuwa ni nani: Mfasiri pekee wa Neno Lake. Ni nani angeivunja na kuifunua ile Mihuri Saba? Ni nani angezifunua siri zote zilizofichwa za Biblia? Ni nani atakayemwita atoke na kumwongoza Bibi-arusi Wake? Ni nani atakayekuwa na ile Sauti ya kutokukosea?
Kulingana na Neno, si mwingine ila Melkizedeki, Yeye Mwenyewe. Mtu asiye na baba wala mama, Ambaye hakuwa na mwanzo wala mwisho wa siku Zake. Mungu, Ambaye alifanyika mwili na akala nyama na mkate wa mahindi, akanywa maziwa ya siagi, na akanena na Ibrahimu. Yeye alikuwa Mtu mwenye utu, akiishi katika mwili wa mwanadamu.
Neno lilo hilo lililosema kwamba Melkizedeki, Mtu huyo, utu huo, angeishi na kujifunua Mwenyewe tena katika mwili wa mwanadamu kama vile alivyofanya kwa Ibrahimu, kisha tena katika Yesu Kristo; bali leo, katika malaika-mjumbe Wake wa saba wa Ufunuo 10:7.
Roho Wake angeiteketeza hiyo maskani ya duniani ili Yeye aweze kuzungumza na kujifunua Mwenyewe kwa Bibi-arusi Wake. Mungu Mwenyewe akiishi na kuzungumza katika mwili wa mwanadamu. Mbegu Yake ya kwanza iliyorejeshwa kikamilifu ilikuwa imefikia kukomaa kabisa. Ule mpango kamili wa Mungu ulikuwa umewasili; Mungu na mwanadamu walikuwa Mmoja. Mungu alikuwa akizungumza mdomo kwa mdomo na Bibi-arusi Wake kama alivyofanya kwa Ibrahimu.
Akaingia na kuishi katika huo, katika Utu wa Melkizedeki. Ndipo baadaye hatukusikia tena habari za Melkizedeki, kwa sababu Yeye alifanyika Yesu Kristo. Melkizedeki alikuwa yule Kuhani, bali akafanyika Yesu Kristo, Basi, wewe uliruka hilo, kwa kuwa katika umbo hilo Yeye alijua yote, Nawe haujapata kujua hayo bado.
BADO…!! Basi sisi ni nani?
Macho yetu, kimo chetu, chochote kile tulichokuwa, tulikuwa katika mawazo Yake hapo mwanzo. Kabla hajakuwepo Malaika, nyota, Kerubi, au chochote kile. Yeye aliliwazia, Akalinena, nasi hawa hapa.
Hiyo ni isiyo kikomo. Hatuwezi kuelewa kwa akili zetu. Bali huyo ni Mungu. Mungu, asiye kikomo.
Kwa kuwa tulikuwa ndani Yake hapo mwanzo, nini kinachotokea kwetu sisi baada ya maisha haya yapatikanayo na mauti hapa duniani kwisha?
Joho hili la mwili linapobwagwa chini, kunao mwili wa kawaida, mwili wa kiungu, mwili ambao haukujengwa kwa mikono, wala kuzaliwa na mwanamke, ambamo tunaingia. Ndipo huo mwili unarudi huku na kuchukua mwili uliotukuzwa.
Ni mambo ya kupendeza vipi aliyowekewa Bibi-arusi Wake. Angalia yale yanayoendelea sasa hivi wakati Yeye akitufunulia Neno Lake zaidi ya wakati wowote ule. Nena kuhusu barua ya mahaba kwa Bibi-arusi Wake! Ni siku iliyoje tunayoishi.
Tuna Ufunuo na tunajua ni Melkizedeki, Sauti ya Mungu, anayezungumza nasi kwenye kanda. Tuna Ufunuo ndio mapenzi ya Mungu yaliyoandaliwa na makamilifu kwa ajili ya siku hii. Hivyo, tunamjua YEYE NI NANI NASI NDIYE BIBI-ARUSI WAKE.
Ufunuo huo unazidi kuwa mkubwa zaidi na zaidi kila siku. Kila siku ipitayo hutuletea furaha zaidi, Ufunuo zaidi. Bibi-arusi anajiweka mwenyewe tayari kwa kuketi katika uwepo wa Sauti Yake, Yeye anapotuambia Sisi ni nani, jinsi gani Yeye anavyotupenda Sisi, jinsi ambavyo Yeye anavyosubiri kwa hamu kuwa pamoja Nasi!!!
Njooni, mjiweke tayari saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) kwa ajili ya kile kinachokaribia kutukia, tunapoisikiliza Sauti ya Melkizedeki.
Ndugu Joseph Branham
Ujumbe: 65-0221E “Huyu Melkizedeki Ni Nani?”
Maandiko ya kusoma:
Mwanzo Sura ya 18
Kutoka 33:12-23
Yohana Mt. 1:1
Warumi 8:1
2 Wakorintho 5:1
1 Wathesalonike 4:13-18
Timotheo wa Kwanza 3:16 / 6:15
Waebrania 7:1-3 /13:8
Ufunuo 10:1-7 / 21:16
26-0322 Ndoa Na Talaka
UJUMBE: 65-0221M Ndoa Na Talaka
Mpendwa Bibi-arusi Aliyechaguliwa, Mteule, na Aliyekusudiwa Kimbele:
Nakumbuka nilipokuwa kijana mdogo nikikua, nikijaribu kuchagua kanda ya kusikiliza. Nilipokuwa nikisoma majina ya jumbe daima Niliwaza, sitasikiliza Ndoa na Talaka, kwani huo hauna uhusiano wowote nami; ni kwa watu waliooa tu.
Kisha siku moja, nilipokuwa nikisikiliza Ndoa na Talaka, Baba akanipa Ufunuo wa Ujumbe huo. Upako Wake ulikuja moyoni mwangu. Yeye anazungumza nami. Ujumbe huu NI kwa ajili yangu. ANANIAMBIA Alinichagua mimi kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Huu ndio sherehe yangu ya arusi. Simtaki mtu mwingine ila Yeye. Mimi ni mkweli na mwaminifu Kwake, na kwa Neno Lake, na kwa Sauti Yake, PEKE YAKE. Sisi ni MMOJA.
Kwa kweli Ujumbe huu ulikuwa kwa ajili ya ndugu na dada wengi waliokuwa wameoana na sasa wamepeana talaka, na Yeye akiwaambia kile wanachopaswa kufanya; Lakini hapo kulikuwa na maana KAMILI NA KUBWA zaidi, iliyo kuu zaidi, yenye nguvu zaidi.
Kulikuwa na Mume mmoja, na Yeye alikuwa akiwaita na kuzungumza na Bibi-arusi Wake wengi, waliochaguliwa. SAUTI YA MUNGU ILIKUWA IKIMWITA ATOKE BIBI-ARUSI MSAFI, NENO BIKIRA WAKE, ASIYEGHOSHIWA. Yule ambaye hajaguswa au kuchafuliwa na mwanamume. Yule ambaye ni mkweli na mwaminifu Kwake na kwa Neno Lake peke yake. Yule ambaye aliyeridhika kabisa Naye na Sauti Yake.
Kwa Neema na Rehema Zake, leo tunaweza kusema, bila shaka yoyote, SISI NDIYE BIBI-ARUSI NENO BIKIRA WAKE. UTUKUFU!!
Yeye alitaka kuhakikisha kuwa hakutakuwa na mambo yaliyoachwa linapokuja suala la kumwita Bibi-arusi Wake, kwa hivyo Yeye alikuja Mwenyewe na kuishi katika mwili wa mwanadamu ili kulifunua Neno Lake na kumwita Bibi-arusi Wake Kwake. Yeye alikuwa ndiye Eliezeri ambaye angemchagua Bibi-arusi Wake mwenyewe.
Ili kuhakikisha kuwa hakukuwa na njia ambayo tungechanganyikiwa ni nani aliyekuwa akituchumbia, Yeye Mwenyewe alikithibitisha chombo Chake kiteule kwa kuzungumza naye kutoka katika kisulisuli kilichokuwa kikining’inia kwenye mti. Kisha akazungumza naye waziwazi kule chini kwenye Mto Ohio mbele ya maelfu.
Yeye hata alipigwa picha pamoja naye ili kuuonyesha na kuuambia ulimwengu, NILIWAAMBIA NITARUDI TENA NA KUISHI KATIKA MWILI. YEYE NDIYE NILIYEMCHAGUA KUISHI NDANI YAKE, KUWAITA NINYI MTOKE ILI MUWE BIBI-ARUSI WANGU. SI YEYE; NI MIMI NINAYENENA KUPITIA YEYE. NINAITUMIA SAUTI YAKE TU KUWA SAUTI YANGU KWENU. MIMI NDIYE NILIYEWAITA NA KUWAKAMILISHA ILI MUWE BIBI-ARUSI WANGU MKAMILIFU.
Ufunuo wa Ujumbe Huu, Neno Lake, Sauti Yake, na sasa SISI ni NANI yapita maneno ya mwanadamu kujaribu kueleza. Najua mnajua hasa kile ninachosema. Imani ya kunyakuliwa inatendeka. Bibi-arusi anajiweka Mwenyewe tayari kwa kuketi katika uwepo wa Mungu Mwenyewe, akikamilishwa.
Ni fursa iliyoje dunia iliyonayo kuisikia Sauti ya Mungu ikizungumza nao; kuketi na kulisikiliza Neno kwa Neno anaponena na kulifunua Neno Lake na kutuambia sisi ni nani. Hakuna cha kufananisha na kuketi katika uwepo Wake, kwa hivyo njooni muungane nasi Jumapili saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapomsikia Yeye akizungumza na Bibi-arusi Wake, Ujumbe, “Ndoa Na Talaka” 65-0221M.
Ndugu Joseph Branham
Maandiko ya kusoma kabla ya kuusikia Ujumbe:
Mathayo Mt 5:31-32 / 16:18 / 19:1-8 / 28:19
Matendo 2:38
Warumi 9:14-23
Timotheo wa Kwanza 2:9-15
Wakorintho wa Kwanza 7:10-15 / 14:34
Waebrania 11:4
Ufunuo 10:7
Mwanzo sura ya 3
Walawi 21:7
Ayubu 14:1-2
Isaya 53
Ezekieli 44:22
26-0315 Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia
UJUMBE: 65-0220 Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia
- 26-0315 Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia
- 24-0616 Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia
- 22-1120 Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia
Mpendwa Bi. Yesu Kristo,
Hii ndiyo siku yenyewe. Huu ndio wakati wenyewe. Mungu alimtuma tai Wake mwenye nguvu duniani kumwita Bi. Yesu Kristo Wake atoke, kunena na kumwambia, “Wewe NDIYE niliyemchagua. Wewe NDIYE ninayempenda. Wewe ndiye Bibi-arusi Neno bikira Wangu Mkamilifu. Sisi ni MMOJA.”
Kuyasikia maneno hayo tu, mioyo yetu inaruka kwa furaha. Kuwazia, katika ulimwengu wote, pamoja na mamilioni na mamilioni yake ya watu, kuna Bi. Yesu Kristo MMOJA tu, na WEWE ndiye Huyo, YULE anayemjia.
Kuna mahali PAMOJA tu palipochaguliwa pa kuabudia. Kuna Ujumbe MMOJA tu mkamilifu uliochaguliwa. Kuna BIBI-ARUSI MMOJA tu MKAMILIFU aliyechaguliwa…NASI NDIO!!
Baba ana mahali PAMOJA peke yake alipopachagua pa kuabudia, Bwana Yesu Kristo; Yeye ni Neno. Leo, kuna mahali PAMOJA peke yake ambapo mauti ya kiroho haiwezi kupiga: Neno. Mauti haiwezi kulipiga Neno, kwa sababu ni Neno la Mungu lililo Hai.
Ufunuo kamili wa Neno hilo lililo Hai umefunuliwa kwa Bi. Yesu Kristo peke yake. Kuna mahali PAMOJA tu palipochaguliwa ambapo Bi. Yesu Kristo anaweza kwenda na kulisikia NENO KAMILIFU LIKINENWA. Kuna nabii MMOJA tu aliyechaguliwa kuwa Sauti ya Mungu. Kuna mahali PAMOJA tu ambapo Bi. Yesu anapoweza kwenda na kuisikia, BWANA ASEMA HIVI: KUBONYEZA PLAY.
Kutakuweko Nuru mnamo wakati wa jioni, mahali pekee alipopachagua Mungu pa kuabudia. Loo, Ujumbe huu umefika wapi, Yeye atafanya nini? Na katika siku yake itakuweko Nuru wakati wa jioni, na (nini?) kuwakaribisha watoto Wake wanaporudi nyumbani kwenye Nchi ya kweli ya ahadi, kwa ishara ile ile ya Nguzo ya Moto ambayo iliwaongoza wana wa Israeli kupitia nyikani.
Jinsi gani Bibi-arusi Wake anavyopaswa kuwa mwangalifu kuifuata na kuisikia Sauti ya Mumewe ikizungumza Naye. Kuna mahali PAMOJA tu tunapoweza kwenda na kuwa na hakika 100%. Kuna Sauti MOJA tu tuliyoiwekea kikomo chetu cha Milele.
Bi. Yesu Kristo anaamini kwamba Maneno anayoyasikia kwenye kanda ni Maneno ya Mumewe. Yeye anaamini Neno Lake halihitaji fasiri yoyote. Kwa hivyo, Yeye anaamini kuna mahali PAMOJA tu palipoandaliwa ambapo Yeye anapoweza kwenda na kusema AMINA kwa kila Neno, Sauti ya Mumewe iliyo kwenye kanda.
Kwa mara nyingine tena, Bi. Yesu Kristo, kutoka kote ulimwenguni, anaweza kusema, “Leo, Neno hili lililonenwa, linatimizwa”.
Mungu Mpenzi, huko chini kuvuka majangwa kule Tucson, huko mbali California, juu huko Nevada na Idaho, kwenda hadi Mashariki na kila mahali, chini huko Texas; wakati mwaliko huu unatolewa, watu wamekiketi katika—katika makanisa madogo, vituo vya mafuta, majumbani, wakisikiliza.
Umealikwa kuja kusikiliza pamoja na Maskani ya Branham saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapomsikia Mungu akizungumza na Bibi-arusi Wake mteule, Ujumbe: “Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia” 65-0220.
Ndugu Joseph Branham
Maandiko: Kumbukumbu la Torati 16:1 hadi 3.
26-0308 Leo Maandiko Haya Yametimia
UJUMBE: 65-0219 Leo Maandiko Haya Yametimia
- 26-0308 Leo Maandiko Haya Yametimia
- 24-0609 Leo Maandiko Haya Yametimia
- 22-1113 Leo Maandiko Haya Yametimia
- 19-0616 Leo Maandiko Haya Yametimia – Preliminari
Mpendwa Uzao Mkuu Wa Kifalme,
Ule wakati ambao tumekuwa tukiusubiri kwa hamu na kuutamani umewadia. Tumewasili. Tunauona ukijifunua mbele ya macho yetu. Kila siku unabii unatimia, nasi tunaweza kusema: LEO MAANDIKO HAYA YAMETIMIA MBELE YA MACHO YETU.
Ni changamko la Ufunuo lililoje linalotukia kwa Bibi-arusi. Kwa kila Ujumbe tunaousikia, tunahisi ndani ya mioyo na roho zetu, ” Linawezaje kuwa kubwa zaidi ya hapa na la ajabu zaidi kuliko hivi, Bwana?” Ndipo Yeye anakuja miongoni mwetu kwa mara nyingine tena na kututia mafuta tunapoisikia Sauti Yake ikituita na kusema, “Wewe ni Kipenzi Changu. Nilikuchagua wewe uwe Bibi-arusi Wangu. Kama vile nilivyokuahidi, ninakuja kukuchukua. Niko njiani. Hivi karibuni Tutakuwa pamoja milele.”
Tunapaza sauti kutoka kote ulimwenguni, tukivumisha Mbingu kwa haleluya zetu, utukufu, sifa, na kuabudu kwetu Kwake. Shetani ameshindwa. Baba ameyaondolea mbali mashaka yetu yote, kutokuwa na uhakika kwetu kote, kudhania kote. Tunaweza kutangaza kwa mioyo na roho zetu zote, SISI NDIO ule Uzao Mkuu wa Kifalme wa Ibrahimu. Bibi-arusi wa Kifalme kwa Mwana yule wa Kifalme aliyeahidiwa.
Uwepo wa Bwana umekuwa wa ajabu mno kwa anavyotufunulia Neno Lake kuliko hapo awali. Yeye amemuunganisha Bibi-arusi Wake pamoja na Neno Lake, na kutuweka katika Nia moja kwa umoja kama jamii moja, tukiisikiliza Sauti ya Mungu ikinena na kutukamilisha kwa Neno Lake.
Kila Ujumbe tunaousikia ni kama vile kisima kinachofoka maji kinachofurika ndani ya nafsi zetu; kikitiririka, kikisukuma, na kububujika kutoka kwenye Kiti cha Enzi cha Mungu. Tunakunywa, kunywa na kunywa, yakiziburudisha nafsi zetu.
Ndugu na Dada zangu, sisi ndio utimilifu wa Maandiko yanayosema Yeye atakuwa na Bibi-arusi Neno bikira. Sisi ndio: Leo Maandiko haya yametimia.
Mungu Mwenyewe alinena kutoka Mbinguni na malaika Wake wa saba na kusema, “Kama vile Yohana Mbatizaji alivyotumwa kutangulia Kuja kwa kwanza kwa Kristo, Ujumbe wako utatangulia Kuja Kwake kwa pili, duniani kote.” Bibi-arusi anaweza kusema: Leo Maandiko haya yametimia.
Je, hivi tunaweza kuelewa kwamba Sauti ya Mungu halisi imenena katika siku yetu kupitia midomo ya mwanadamu, ikarekodiwa, ikahifadhiwa, na kutunzwa ili Yeye aweze kunena na kila mmoja wetu, Bwana Asema Hivi? Yeye ameliwezesha hilo ili tusichukue neno la mtu yeyote, mawazo ya mtu yeyote, fikra za mtu yeyote, ni sisi kuketi tu na kuisikiliza Sauti Yake ikinena nasi moja kwa moja Neno Lake Safi.
NI KITU GANI KINACHOTENDEKA LEO?
Na M-w-a-n-a yule yule wa Mungu aliyetokea mashariki na kujithibitisha Mwenyewe kama Mungu aliyefanyika mwili, ndiye M-w-a-n-a yule yule wa Mungu aliyeko katika kizio cha magharibi cha dunia, ambaye anajitambulisha Mwenyewe kati ya kanisa usiku huu, Yeye yule jana, leo, na hata milele. Ile Nuru ya jioni ya Mwana imekuja. Leo Maandiko haya yametimia mbele yetu.
JE! TUKO KATIKA MAPENZI MAKAMILIFU YA MUNGU KWA SISI KUSEMA NA KUAMINI KUWA: “KUZICHEZA KANDA NDIO NJIA ILIYOANDALIWA NA MUNGU KWA AJILI YA BIBI-ARUSI WAKE”?
JE! KUNA KITU KILICHO KIKUU ZAIDI YA KUZISIKILIZA KANDA?
Kila mara katika utatu kama nilivyosema usiku uliopita Mungu huwakilishwa. Pale kulikuwako Wasodoma. Walutu, na Waibrahimu. Ni hali ile ile usiku huu, ulimwengu ukikaa tu hivyo!
Tazama, Yule aliyekaa pamoja na Ibrahimu alikuwa Mungu Mwenyewe; na wale wengine wawili walikuwa Malaika wajumbe.
KWA HIVYO NI NANI ANAYEZUNGUMZA NASI KWENYE KANDA?
Hebu niwaulizeni kitu fulani. Tazama utaratibu huu sasa. Ibrahimu alimwita huyu aliyeongea naye, “Elohim.” Neno la Kiebrania Elohim maana yake ni “Yule aridhishaye kwa vyote. Yeye yule Aliye wa Milele,” Elohim, Mungu Mwenyewe!
NI MUHIMU JINSI GANI KUBONYEZA PLAY?
…“wakati mmoja Roho Mtakatifu atakuja na kufanya mambo yale yale, na kunena tu neno moja dhidi Yake hautasamehewa kamwe. Hiyo ni siku hizi, ambapo kila neno yapasa liunganike pamoja. Nena neno dhidi Yake, halitasamehewa katika dunia hii wala dunia ijayo.”
Haleluya zetu za wiki iliyopita na kumsifu Bwana zilikuwa ni maandalizi tu ya kutuandaa kwa ajili ya kile kitakachotendeka Jumapili hii, Kwani Bibi-arusi kwa mara nyingine tena anaungana na kumsikiliza MUNGU akitutia moyo na kutuhakikishia kwamba sisi ndiyo wateule Wake, Naye anakuja hivi karibuni kutupeleka kwenda kwenye Karamu yetu kuu ya Harusi, kisha Makao yetu ya Baadaye.
Siku hii ndiyo aliyoifanya BWANA; tutashangilia na kuifurahia.
Ndugu Joseph Branham
Ujumbe: 65-0219 – “Leo Maandiko Haya Yametimia”
Maandiko:
Yohana Sura ya 16
Isaya 61:1-2
Luka 4:16
26-0301 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi
UJUMBE: 65-0218 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi
- 26-0301 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi
- 24-0602 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi
- 22-1106 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi
- 19-1027 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi – Preliminari
- 17-0104 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi
Mpendwa Bibi-arusi Neno Bikira,
Nimeketi hapa asubuhi ya leo nikiuhisi upako Wa aina yake ninapousikiliza, kuusoma na kujifunza Ujumbe huu ambao Bibi-arusi atakaousikia Jumapili. Utu wangu wote umejaa upako. Moyo wangu unabubujika kwa furaha kubwa nikijua, SOTE TUTAKUSANYIKA PAMOJA KUTOKA KOTE ULIMWENGUNI KWA UPAKO HUU ULE ULE. Tutakuwa tukifurahi, tukimsifu Bwana, sote kwa wakati mmoja, Yeye anapozungumza na kila mmoja wetu na kulifunua Neno Lake.
Upako utakuwa mkubwa sana hivi kwamba kutakuwa na kupiga makelele na kupaza sauti, “haleluya, amina, Jina la Bwana lisifiwe” kote ulimwenguni kwa wakati mmoja, tunapovumisha Mbingu kwa sifa na kuabudu kwetu.
Kitu gani kitakachotukia? Mungu atakuwa akimuunganisha na kuzungumza na Bibi-arusi Wake. Tutakuwa Jamii Moja, katika nia moja kwa umoja anapojifunua na kujidhihirisha Mwenyewe kwetu.
Hakuna mahali pakuu zaidi unapoweza kwenda, hakuna Sauti kuu zaidi unayoweza kuisikia; hakuna upako mkuu zaidi kuliko Sauti ya Mungu ikizungumza nawe moja kwa moja kwenye kanda.
Mungu amelilinda Neno Lake tangu mwanzo na ameandaa mahali ambapo watoto Wake wote wanaweza kwenda na kumsikia Yeye akinena na kulifasiri Neno Lake Mwenyewe. Mahali ambapo hakuna kubahatisha, hakuna kutumai, hakuna kushangaa-shangaa; Ndio mahali palipoandaliwa na Mungu pa kuisikia BWANA ASEMA HIVI.
Wakati hilo linapofunuliwa kwako, ni kama nuru kubwa ambayo imewashwa moyoni na nafsini mwako…unapaza sauti, “hili ndilo. Naliona. Mimi ni MMOJA NA NENO. MIMI NI NENO. MIMI NDIYE BIBI-ARUSI. NIMEWASILI.”
Linatendeka, nao hawajui. Hiyo ni kweli. Mwaona? Naam, bwana! “Kwa kuwa po pote ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai,” halisi tu kama ulimwengu. Unaona? Hivyo ndivyo ilivyosema. Je, mzoga ni nini? Neno. Yeye ni Neno, mzoga, Kristo! “Kristo ndani yako” yeye yule jana leo, na hata milele. Jinsi ilivyo kweli!
Tunapokusanyika kulisikiliza Neno, wasiwasi wetu wote, msongo wetu wote wa mawazo, matatizo yetu yote, hutoweka tu. Tunafurahi tunapogundua kuwa hatuna cha kuwa na wasiwasi nacho; sisi ni Bibi-arusi Wake. Yeye Hayuko tu pamoja nasi, BALI YU NDANI YETU. SISI NI ILE MBEGU BIBI-ARUSI NENO. Kila kitu ni kikamilifu. Wakati Wake ni mkamilifu. Sisi ni wakamilifu.
Tumeridhika mno na kushukuru sana kusema sisi ni Neno Lake lililodhihirishwa tuliyozaliwa kibikira; Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele, akiishi na kukaa ndani yetu. Haleluya!
Hatuwezi kupatana hata kwenye NENO MOJA. Lazima tuisikie Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.
Je, umepata kuona tai akipatana? La, bwana! Yeye hapatani kamwe. Wala Mkristo halisi pia. Yeye si mtu mdhaifu. Yeye atawinda hata atakapoipata. Amina! Naam, bwana! atapata nyama yake. Yeye anataka mana mpya. Atafika kule na kuchimbua mpaka aipate. Ataruka juu zaidi na zaidi. Iwapo haimo kwenye bonde hili, ataruka juu zaidi. Kadiri urukavyo juu, ndivyo unavyoweza kuona mbali zaidi. Kwa hivyo ni wakati wa tai wa siku hizi kuruka juu zaidi, wakachimbue kwenye ahadi za Mungu, si kuishi kwa chakula cha mwewe kilichouawa miaka mingi iliyopita. Tokeni kwake.
Kaa tayari ewe Bibi-arusi, tutaila Mana hiyo mpya, tukiketi chini ya ule upako mkuu zaidi uliopo, Jumapili hii saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 2:00 USIKU ya Afrika Mashariki) tunaposikia: 65-0218 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja na Kapi.
Tunawaalika Bibi-arusi kutoka kote ulimwenguni kuungana nasi kula kwenye Njia kamilifu ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii. Mahali pekee ambapo BIBI-ARUSI Anaweza kusema amina kwa kila Neno. Ambapo upako mkuu wa Roho Mtakatifu unaponena na kumkamilisha Bibi-arusi Wake kwa Kubonyeza Play na kusikia na kulipokea Neno Lake.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko:
Mathayo 24:24
Luka 17:30
Yohana 5:24 / 14:12
Warumi 8:1
Wagalatia 4: 27-31
Waebrania 13:8
1 Yohana 5:7
Ufunuo 10
Malaki 4