UJUMBE: 64-0617 Kristo Aliyetambulishwa Katika Nyakati Zote
- 25-1116 Kristo Aliyetambulishwa Katika Nyakati Zote
- MAJARIBIO YA KANDA YA KILA MWEZI YA YF
- 20-0809 Kristo Aliyetambulishwa Katika Nyakati Zote
- 17-0208 Kristo Aliyetambulishwa Katika Nyakati Zote
Mpendwa Neno La Mungu Lililo Hai,
Miaka hii yote nimelificha moyoni mwangu, nikimficha Kristo, Nguzo ile ile ya Moto ikilifasiri Neno, kama ilivyoahidiwa.
Najua hili litasikika kama la kipuuzi kwa watu wengi, lakini ikiwa tu utamvumilia malaika-mjumbe wa Mungu kwa dakika chache, na kumwomba Mungu Ufunuo zaidi, naamini kwamba yeye, kwa msaada wa Mungu na kwa Neno Lake, na kulingana na Neno Lake, atamleta Yeye hapa mbele yako. Mungu, akijifunua na kujidhihirisha Mwenyewe, akilifasiri na kulifunua Neno Lake.
Ni uamsho ulioje ambao umekuwa ukitendeka mwezi huu uliopita ndani ya Bibi-arusi wa Yesu Kristo. Mungu, akijifunua Mwenyewe zaidi ya wakati wowote ule, akizungumza na Kipenzi Chake, akifanya mapenzi Naye, akimhakikishia, Sisi ni Mmoja na Yeye.
Hakuna kusitasita, hakuna kutokuwa na uhakika, hakuna kushuku, hakuna shaka hata chembe; Mungu ametufunulia: Sauti ya Mungu inayozungumza kwenye kanda ndio NJIA YA MUNGU ILIYOANDALIWA NA ILIYOKAMILIFU KWA BIBI-ARUSI WAKE LEO.
Aliiandaa njia hii ili Tusije kamwe tukalazimika hilo kuwekewa chujio, kufafanuliwa, kuelezewa, wala kushikwa-shikwa na mikono ya watu kwa njia yoyote; kuisikiliza tu Sauti Safi ya Mungu ikizungumza mdomo kwa sikio na kila mmoja wetu.
Yeye alijua siku hii ilikuwa inakuja. Alijua Bibi-arusi Wake angeweza kula tu hiyo Mana iliyofichwa, Chakula Chake cha Kondoo. Hatungetaka kusikia chochote ila Sauti ya Mungu kutoka kwa Mungu Mwenyewe.
Tumevunja tukapitia kwenye pazia hilo nasi tumeingia katika Utukufu wa Shekina. Ulimwengu hauwezi kuliona. Nabii wetu huenda asiyatamke maneno yake ipasavyo. Huenda asivalie ipasavyo. Huenda asivikwe mavazi ya kikasisi. Lakini nyuma ya ngozi hiyo ya kibinadamu, mle ndani mna ule Utukufu wa Shekina. Mle ndani mna nguvu. Mle ndani mna Neno. Mle ndani mna Mkate wa Wonyesho. Mle ndani mna Utukufu wa Shekina, ambao ndiyo Nuru inayomwivisha Bibi-arusi.
Na mpaka utakapokuja nyuma ya hiyo ngozi ya pomboo, mpaka utakapotoka nyuma ya ngozi yako ya kale, mawazo yako ya kale, kanuni zako za imani za kale, na uingie katika Uwepo wa Mungu; ndipo Neno linakuwa hali halisi iliyo hai kwako, ndipo umeinuka katika Utukufu wa Shekina, ndipo Biblia inakuwa ni Kitabu Kipya, ndipo Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo, na hata milele. Unaishi katika Uwepo Wake, ukila mkate wa wonyesho ambao unatolewa tu siku hiyo kwa waaminio, makuhani pekee. “Na sisi ni makuhani, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa kipekee, tukimtolea Mungu dhabihu za kiroho.” Lakini huna budi kuingia, huko nyuma ya pazia, upate kumwona Mungu aliyefunuliwa. Na Mungu anafunuliwa, hilo ni Neno Lake lililodhihirishwa.
Sisi ni wa kipekee kwa ulimwengu, lakini tumeridhika kujua Skrubu yetu ni nani na tunajivunia sisi kuwa nati Zake za kanda, tuliyotiwa hesi kwa Neno Lake, kwani linatuvuta Kwake.
Kama hujaingizwa kwenye kanda, wewe si kitu ila lundo la vitu shaghalabaghala!!!
Sasa, angalieni sasa, Mungu! Yesu alisema ya kwamba, “Wale waliojiliwa na Neno, waliitwa ‘miungu,’” hao walikuwa ni manabii. Sasa, si kwamba mtu huyo mwenyewe alikuwa ni Mungu, si zaidi ya vile mwili wa Yesu Kristo ulivyokuwa ni Mungu. Yeye alikuwa ni mwanadamu, Naye Mungu alikuwa amefunikwa nyuma yake.
Mungu, siku moja alifunikwa nyuma ya ngozi za pomboo. Mungu, siku moja alifunikwa katika mwili wa mwanadamu aitwaye Melkizedeki. Mungu, alifunikwa katika mwili wa mwanadamu aitwaye Yesu. Mungu, alifunikwa katika mwili wa mwanadamu aitwaye William Marrion Branham. Mungu, amefunikwa katika mwili wa mwanadamu aitwaye BIBI-ARUSI WAKE.
Ni muhimu sana kukumbuka, lakini walio wengi wanashindwa na wanatafuta kitu kingine. Jambo la mwisho ambalo Ibrahimu aliona, jambo la mwisho kutukia kabla ya moto kushuka na kuuhukumu ulimwengu wa Mataifa, kabla ya yule mwana aliyeahidiwa kutokea, jambo la mwisho ambalo kanisa la Kikristo litaliona mpaka kule kuonekana kwa Yesu Kristo ni Melkizedeki, Mungu aliyedhihirishwa katika mwili, akilifunua Neno Lake kwa Bibi-arusi Wake.
Hakuna kitu kingine kitakachokuja. Hakuna kitu kingine kilichoahidiwa katika Neno Lake. Hakuna mtu, wala kundi la watu watakaokuja kumkamilisha Bibi-arusi.
La! Wanataka kuja humu kanisani kwa ajili ya kukamilishwa. Ona? Ili sisi—sisi tupate ushirika sisi kwa sisi hapa kanisani, lakini kukamilishwa huja kati yetu na Mungu. Damu ya Kristo ndiyo inayotukamilisha katika Roho Mtakatifu.
Ujumbe huu, Sauti Hii, Neno la Mungu lililothibitishwa, linamkamilisha Bibi-arusi wa Yesu Kristo.
Ninawaalika kila mmoja wenu mje muisikilize pamoja nasi Sauti ya Mungu inapomkamilisha Bibi-arusi Wake Jumapili hii saa 06:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(ni saa 2 USIKU ya Afrika Mashariki) tunaposikia: 64-0617 “Kristo Aliyetambulishwa Katika Nyakati Zote”.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko ya kusoma kabla ya Ujumbe:
Kumbukumbu la Torati 18:15
Zekaria 14:6
Malaki 3: 1-6
Luka Mtakatifu 17: 28-30
Yohana Mtakatifu 1:1 / 4:1-30 / 8: 57-58 / 10:32-39
Waebrania 1:1 / 4:12 / 13:8
Ufunuo 22:19