22-0821 Sikukuu Ya Baragumu

UJUMBE: 64-0719M Sikukuu Ya Baragumu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Kubonyeza Play,

Kila Jumapili tunakusanyika na kusikiliza Huduma kuu iliyo hai katika historia ya ulimwengu. Tunapata wakati mtukufu zaidi tunapokutana pamoja ili kusikia Sauti ya Mungu! Ni Yesu, Mwana wa Mungu, akijifunua Mwenyewe kwa Maandiko, akilifanya andiko hilo ambalo limechaguliwa tangu zamani kwa ajili ya Siku siku hii, kama ilivyokuwa katika siku Yake, na siku Zingine zote, LIISHI. Na Kuamini Hilo, ndio Dhihirisho la kuwa una Roho Mtakatifu .

Dhihirisho la kweli la kuwa na Roho Mtakatifu sio ati kwenda kanisani kila Jumapili; Ni kwamba unaamini ya kwamba “Mimi Ndiye ,” Neno la Siku yako. Neno la Siku hii ni nini? Nabii wa Mungu ndiye Neno la Siku hii naye anapaswa kuwarudisha watu kwenye Neno, ili kwamba Bibi-arusi amjue Mumewe, amjue Mwenziwe, Neno lililofunuliwa.

Maisha yake mwenyewe, kazi zake mwenyewe, hufunua na kulithibitisha Neno la Siku hii.

Ni Roho Mtakatifu aliyerudi tena Kanisani; Kristo, Mwenyewe, aliyefunuliwa katika mwili wa mwanadamu, wakati wa jioni, kama tu alivyoahidi angefanya. Ninajua kwa namna fulani hilo linawakaba wao kidogo, lakini lazima usome katikati ya mistari na kuona, hiyo inafanya ile picha ije.

Sisi ni Uzao wa Kifalme wa Ibrahimu, Bibi-arusi. Ishara ya mwisho ambayo Ibrahimu aliwahi kuona kabla ya mwana aliyeahidiwa kuja ilikuwa ni nani? Mungu, katika umbo la mwanadamu, ambaye aliweza kuyatambua mawazo ya watu. Mtu mmoja, sio dazani, mtu mmoja.

Najua watu wengi hawakubaliani na jambo hilo, bali najua ndilo hili. Najua jambo hilo. Si kwa sababu ninasema mnalisema; kwa sababu, sikulitoa kwangu mimi. Ma—mawazo yangu si yangu mwenyewe . Cho chote kile kilichoniambia jambo hilo, kama kimekosea, basi kimekosea. Bali sisemi jambo hili kwa nafsi yangu, ninasema yale Mtu mwingine amesema. Mtu huyo mwingine ni Mungu aliyenena nasi na kufanya mambo haya yote ambayo amefanya, na akajitokeza, mnaona, kwa hiyo mimi najua ya kwamba ni kweli.

Tunasikiliza wazo lenyewe la Mungu; si mawazo ya mwanadamu, bali ya Mungu. Nabii wetu ndiye mfunuzi wa Neno lililoandikwa.

Tunaelewa kwamba kuzicheza kanda majumbani mwenu ama makanisani mwenu si kwa kila mtu, bali ni kwa ajili Yetu , Ndiyo NJIA PEKEE. Tunapenda kusikia Sauti ya Mungu ikizungumza nasi moja kwa moja. Hatuhitaji fasiri au ufafanuzi wowote; ni Mungu akisema Nasi mdomo kwa sikio .

Jumapili hii tutakuwa tukimsikia Mungu akisema na kutuambia jinsi alivyomwonyesha nabii wake sisi katika onyesho la awali ng’ambo ya pili. Jinsi Bibi-arusi huyo alivyokuwa akimtazama yeye moja kwa moja, akizungumza naye, nasi tulikuwa tumesimama pamoja naye. Tulikuwa tukitembea kikamilifu mbele za Bwana.

Kisha Mungu anazungumza kupitia nabii wake na kutabiri kwa mara nyingine tena na kusema:

Yawezekana kuwe na baadhi huko nje katika mataifa, ulimwenguni kote, ambao hata kanda hii ingewakuta manyumbani mwao au makanisani mwao. Tungeomba, Bwana, kwamba wakati ibada inaendelea, pale—pale…au kanda inachezwa, au nafasi yo yote tunayoweza kuwamo, au—au hali, yule Mungu mkuu wa Mbinguni na aheshimu huu unyofu wa mioyo yetu asubuhi hii, na kuponya wahitaji, kuwapa wao yale wanayohitaji.

Kama unazisikiliza hizo Kanda, na kuamini kwamba ndizo
Sauti ya Mungu kwa ajili ya wakati wetu, basi chochote unachoweza kuwa unakihitaji, Mungu atakuwa akizungumza kupitia mjumbe Wake na kusema, “ Wape chochote tunachohitaji .

Hilo linaweza kutukia tu kwa KUBONYEZA PLAY rafiki yangu.
Ikiwa ungependa kumsikia Mungu akinema na kufasiri Neno Lake Mwenyewe, akijifunua Mwenyewe kupitia mwili wa mwanadamu, na upokee chochote unachohitaji, njoo uungane nasi Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA , saa Jeffersonville,( Ni Saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania) tunapomsikia Mungu akisema nasi tunaposikia: Sikukuu ya Baragumu 64-0719M .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Mambo ya Walawi Sura ya16 yote

Mambo ya Walawi 23:23-27

Isaya 18:1-3

Isaya 27:12-13

Ufunuo 10:1-7

Ufunuo 9:13-14

Ufunuo 17:8