22-0814 Kile Kipeo

UJUMBE: 64-0705 Kile Kipeo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Kipeo,

Nawezaje kuwaandikia leo bila kuwakumbusha kile ambacho mchungaji wetu alichosema kuhusu kila mmoja wetu Jumapili iliyopita?

Bali kujua ya kwamba mahali po pote niwezapo kwenda…sina ku—kundi fulani ulimwenguni , nilijualo, linaloshikamana nami kama kundi hili. Mungu na—na ajalie tuwe wasioweza kutengana sana, hata, katika Ufalme ujao, naomba kwamba tuwe huko pamoja; ombi langu.

Hakuna kundi duniani linaloshikamana na nabii wa Mungu, na Ujumbe ambao Mungu alionena kwenye kanda, kama sisi. Na kwa sababu tunafanya hivyo, tutakuwa tusioweza kutengana katika Ufalme ule mpya pamoja naye na Bwana wetu Yesu Kristo. Haiwi bora zaidi ya hapo!

Hizi ni siku kuu sana za maisha yetu. Tumeridhika kabisa kuwa mpumbavu wa Kristo na Ujumbe Wake wa wakati wa mwisho. Kuitwa nati kwa sababu tunaamini kila Neno kwenye kanda hizo na kusema, BONYEZA PLAY.

Sisi ni Washiriki wa Lile Kanisa Moja la Pekee. Hatukujiunga Nalo, tulizaliwa ndani Yake. Kila wiki tunakusanyika pamoja kutoka ulimwenguni kote na kuendeleza mapenzi na Kristo na kusema, “Loo, jinsi ninavyokupenda ‘Jesu!’”

Tunaweza kuwa nati kwa ulimwengu, lakini Baba ametupa Ufunuo Wa yeye Mwenyewe katika wakati wetu, Mungu mwenye ngozi, na imetuvuta, Bibi-arusi Wake, Kwake.

Tunapenda tu jinsi lilivyo rahisi, lakini wakati huo huo, jinsi tu lilivyo la Kilindi. Lakini yakupasa uwe na Ufunuo upate kuliona, Nasi TUNAO.

Alijificha Mwenyewe katika utaji wa binadamu, katika Kanisa Lake, akijifunua Mwenyewe kwa imani yako na imani yangu, pamoja, kutuunganisha pamoja, tukifanya umoja wa Mungu. Mimi siwezi kufanya kitu bila ninyi; ninyi hamwezi kufanya kitu bila mimi; hakuna anayeweza kufanya kitu bila Mungu. Kwa hiyo, sote pamoja linafanya kitu kimoja, ule muungano. Mungu alinituma kwa kusudi hilo; mnaamini jambo hilo; na hapa linatendeka. Ndilo hilo hasa, mnaona, limehakikishwa kikamilifu.

Sisi ni Kama wale watu wakitembea barabarani kutoka Emau siku ile. Tunamsikiliza Yeye akizungumza nasi sote wakati wa mchana. Kisha tunamwalika ndani ya nyumba zetu ili tuweze kujifungia pamoja Naye peke yake. Ndipo anafanya jambo fulani awezalo yeye tu kulifanya, kuumega Mkate wa Uzima wa Milele. Tunamtambua papo hapo. Kisha tunasema, je mioyo yetu haikuwaka ndani yetu alipokuwa akisema nasi njiani.

Kila Wiki tunakusanyika kwa matarajio makubwa, tukijiuliza, “Atatuambia na kutufunulia nini wiki hii”. Tutatumiana nukuu mmoja kwa mwingine na kuzungumzia hilo wiki nzima. “Je, ulimsikia aliposema”:

“Ilinichukua miaka elfu nne kukitengeneza Kipeo Changu; lakini sasa imenichukua karibu miaka elfu mbili kutengeneza Kipeo kingine, Wewe, Bibi-arusi Wangu. Ninakitengeneza kwa njia Yake isiyobadilika , namna ile ile nilivyokitengeneza Kipeo Changu cha kwanza, Neno Langu. Hivyo ndivyo ninavyojitengenezea Vipeo Vyangu , kwa kuwa unaweza tu kuwa Kipeo kikamilifu wakati linapokuwa ni Neno kamilifu.”

Ndugu yangu, usione hili kuwa baya, lakini waza kwa dakika moja. Kama Yeye alitoa Kwake, kile kiumbe cha asili, ili amtengenezee Bibi-arusi, Yeye hakuumba kiumbe kingine; Yeye alichukua sehemu ya ule uumbaji asili. Basi kama Yeye alikuwa Neno, Bibi-arusi anapaswa kuwa nini? Hana budi kuwa Neno la asili, Mungu Aliye Hai katika Neno.

Nena kuhusu yubile ya mlo bora. Sisi ni sehemu ya uumbaji wa asili. Sisi ni sehemu ya Neno la asili. Mungu anaishi ndani yetu. Sisi ni Kipeo Chake. Sisi ndio kundi lile linaloshikamana na nabii Wake. Sisi ni wasioweza kutengana na nabii Wake na Bwana Yesu Kristo. Sisi ni MMOJA Na Yeye.

Kama nawe pia ungependa moyo wako uwake ndani yako kama unavyowaka ndani yetu, njoo uungane nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville,( ni Saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania), Wakati sehemu ya Bibi-arusi inapokusanyika Pamoja na kumwalika Yeye Majumbani mwetu, na katika makanisa yetu, tunapomsikia Mungu akisema Nasi na kutufunulia Maneno ya Uzima wa Milele, anapotuletea Ujumbe: Kile Kipeo 64-0705 .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Isaya 53:1-12
Malaki 3:6
Mathayo Mt 24:24
Marko Mt 9:7
Yohana Mt 12:24 / 14:19