UJUMBE: 65-0218 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi
- 26-0301 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi
- 24-0602 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi
- 22-1106 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi
- 19-1027 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi – Preliminari
- 17-0104 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi
Mpendwa Bibi-arusi Neno Bikira,
Nimeketi hapa asubuhi ya leo nikiuhisi upako Wa aina yake ninapousikiliza, kuusoma na kujifunza Ujumbe huu ambao Bibi-arusi atakaousikia Jumapili. Utu wangu wote umejaa upako. Moyo wangu unabubujika kwa furaha kubwa nikijua, SOTE TUTAKUSANYIKA PAMOJA KUTOKA KOTE ULIMWENGUNI KWA UPAKO HUU ULE ULE. Tutakuwa tukifurahi, tukimsifu Bwana, sote kwa wakati mmoja, Yeye anapozungumza na kila mmoja wetu na kulifunua Neno Lake.
Upako utakuwa mkubwa sana hivi kwamba kutakuwa na kupiga makelele na kupaza sauti, “haleluya, amina, Jina la Bwana lisifiwe” kote ulimwenguni kwa wakati mmoja, tunapovumisha Mbingu kwa sifa na kuabudu kwetu.
Kitu gani kitakachotukia? Mungu atakuwa akimuunganisha na kuzungumza na Bibi-arusi Wake. Tutakuwa Jamii Moja, katika nia moja kwa umoja anapojifunua na kujidhihirisha Mwenyewe kwetu.
Hakuna mahali pakuu zaidi unapoweza kwenda, hakuna Sauti kuu zaidi unayoweza kuisikia; hakuna upako mkuu zaidi kuliko Sauti ya Mungu ikizungumza nawe moja kwa moja kwenye kanda.
Mungu amelilinda Neno Lake tangu mwanzo na ameandaa mahali ambapo watoto Wake wote wanaweza kwenda na kumsikia Yeye akinena na kulifasiri Neno Lake Mwenyewe. Mahali ambapo hakuna kubahatisha, hakuna kutumai, hakuna kushangaa-shangaa; Ndio mahali palipoandaliwa na Mungu pa kuisikia BWANA ASEMA HIVI.
Wakati hilo linapofunuliwa kwako, ni kama nuru kubwa ambayo imewashwa moyoni na nafsini mwako…unapaza sauti, “hili ndilo. Naliona. Mimi ni MMOJA NA NENO. MIMI NI NENO. MIMI NDIYE BIBI-ARUSI. NIMEWASILI.”
Linatendeka, nao hawajui. Hiyo ni kweli. Mwaona? Naam, bwana! “Kwa kuwa po pote ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai,” halisi tu kama ulimwengu. Unaona? Hivyo ndivyo ilivyosema. Je, mzoga ni nini? Neno. Yeye ni Neno, mzoga, Kristo! “Kristo ndani yako” yeye yule jana leo, na hata milele. Jinsi ilivyo kweli!
Tunapokusanyika kulisikiliza Neno, wasiwasi wetu wote, msongo wetu wote wa mawazo, matatizo yetu yote, hutoweka tu. Tunafurahi tunapogundua kuwa hatuna cha kuwa na wasiwasi nacho; sisi ni Bibi-arusi Wake. Yeye Hayuko tu pamoja nasi, BALI YU NDANI YETU. SISI NI ILE MBEGU BIBI-ARUSI NENO. Kila kitu ni kikamilifu. Wakati Wake ni mkamilifu. Sisi ni wakamilifu.
Tumeridhika mno na kushukuru sana kusema sisi ni Neno Lake lililodhihirishwa tuliyozaliwa kibikira; Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele, akiishi na kukaa ndani yetu. Haleluya!
Hatuwezi kupatana hata kwenye NENO MOJA. Lazima tuisikie Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.
Je, umepata kuona tai akipatana? La, bwana! Yeye hapatani kamwe. Wala Mkristo halisi pia. Yeye si mtu mdhaifu. Yeye atawinda hata atakapoipata. Amina! Naam, bwana! atapata nyama yake. Yeye anataka mana mpya. Atafika kule na kuchimbua mpaka aipate. Ataruka juu zaidi na zaidi. Iwapo haimo kwenye bonde hili, ataruka juu zaidi. Kadiri urukavyo juu, ndivyo unavyoweza kuona mbali zaidi. Kwa hivyo ni wakati wa tai wa siku hizi kuruka juu zaidi, wakachimbue kwenye ahadi za Mungu, si kuishi kwa chakula cha mwewe kilichouawa miaka mingi iliyopita. Tokeni kwake.
Kaa tayari ewe Bibi-arusi, tutaila Mana hiyo mpya, tukiketi chini ya ule upako mkuu zaidi uliopo, Jumapili hii saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 2:00 USIKU ya Afrika Mashariki) tunaposikia: 65-0218 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja na Kapi.
Tunawaalika Bibi-arusi kutoka kote ulimwenguni kuungana nasi kula kwenye Njia kamilifu ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii. Mahali pekee ambapo BIBI-ARUSI Anaweza kusema amina kwa kila Neno. Ambapo upako mkuu wa Roho Mtakatifu unaponena na kumkamilisha Bibi-arusi Wake kwa Kubonyeza Play na kusikia na kulipokea Neno Lake.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko:
Mathayo 24:24
Luka 17:30
Yohana 5:24 / 14:12
Warumi 8:1
Wagalatia 4: 27-31
Waebrania 13:8
1 Yohana 5:7
Ufunuo 10
Malaki 4