UJUMBE: 65-0221E Huyu Melkizedeki Ni Nani?
- 26-0329 Huyu Melkizedeki Ni Nani?
- 24-0630 Huyu Melkizedeki Ni Nani?
- 22-1204 Huyu Melkizedeki Ni Nani?
- 19-0707 Huyu Melkizedeki Ni Nani? + Preliminari
- 17-1105 Huyu Melkizedeki Ni Nani? +Preliminari
Mpendwa Bibi-arusi Wa Uzima Wa Milele,
Sauti hiyo ni nani inayozungumza nasi kwenye kanda?
Tunaweza tu kujua jibu la swali hilo kwa Ufunuo kutoka kwa Mungu. Ni Bibi-arusi Wake aliyechaguliwa tangu zamani peke yake ndiye atakayekuwa na Ufunuo huo. Kwa hivyo, lazima tutafute Neno Lake ili kuelewa alisema Yeye alikuwa ni nani: Mfasiri pekee wa Neno Lake. Ni nani angeivunja na kuifunua ile Mihuri Saba? Ni nani angezifunua siri zote zilizofichwa za Biblia? Ni nani atakayemwita atoke na kumwongoza Bibi-arusi Wake? Ni nani atakayekuwa na ile Sauti ya kutokukosea?
Kulingana na Neno, si mwingine ila Melkizedeki, Yeye Mwenyewe. Mtu asiye na baba wala mama, Ambaye hakuwa na mwanzo wala mwisho wa siku Zake. Mungu, Ambaye alifanyika mwili na akala nyama na mkate wa mahindi, akanywa maziwa ya siagi, na akanena na Ibrahimu. Yeye alikuwa Mtu mwenye utu, akiishi katika mwili wa mwanadamu.
Neno lilo hilo lililosema kwamba Melkizedeki, Mtu huyo, utu huo, angeishi na kujifunua Mwenyewe tena katika mwili wa mwanadamu kama vile alivyofanya kwa Ibrahimu, kisha tena katika Yesu Kristo; bali leo, katika malaika-mjumbe Wake wa saba wa Ufunuo 10:7.
Roho Wake angeiteketeza hiyo maskani ya duniani ili Yeye aweze kuzungumza na kujifunua Mwenyewe kwa Bibi-arusi Wake. Mungu Mwenyewe akiishi na kuzungumza katika mwili wa mwanadamu. Mbegu Yake ya kwanza iliyorejeshwa kikamilifu ilikuwa imefikia kukomaa kabisa. Ule mpango kamili wa Mungu ulikuwa umewasili; Mungu na mwanadamu walikuwa Mmoja. Mungu alikuwa akizungumza mdomo kwa mdomo na Bibi-arusi Wake kama alivyofanya kwa Ibrahimu.
Akaingia na kuishi katika huo, katika Utu wa Melkizedeki. Ndipo baadaye hatukusikia tena habari za Melkizedeki, kwa sababu Yeye alifanyika Yesu Kristo. Melkizedeki alikuwa yule Kuhani, bali akafanyika Yesu Kristo, Basi, wewe uliruka hilo, kwa kuwa katika umbo hilo Yeye alijua yote, Nawe haujapata kujua hayo bado.
BADO…!! Basi sisi ni nani?
Macho yetu, kimo chetu, chochote kile tulichokuwa, tulikuwa katika mawazo Yake hapo mwanzo. Kabla hajakuwepo Malaika, nyota, Kerubi, au chochote kile. Yeye aliliwazia, Akalinena, nasi hawa hapa.
Hiyo ni isiyo kikomo. Hatuwezi kuelewa kwa akili zetu. Bali huyo ni Mungu. Mungu, asiye kikomo.
Kwa kuwa tulikuwa ndani Yake hapo mwanzo, nini kinachotokea kwetu sisi baada ya maisha haya yapatikanayo na mauti hapa duniani kwisha?
Joho hili la mwili linapobwagwa chini, kunao mwili wa kawaida, mwili wa kiungu, mwili ambao haukujengwa kwa mikono, wala kuzaliwa na mwanamke, ambamo tunaingia. Ndipo huo mwili unarudi huku na kuchukua mwili uliotukuzwa.
Ni mambo ya kupendeza vipi aliyowekewa Bibi-arusi Wake. Angalia yale yanayoendelea sasa hivi wakati Yeye akitufunulia Neno Lake zaidi ya wakati wowote ule. Nena kuhusu barua ya mahaba kwa Bibi-arusi Wake! Ni siku iliyoje tunayoishi.
Tuna Ufunuo na tunajua ni Melkizedeki, Sauti ya Mungu, anayezungumza nasi kwenye kanda. Tuna Ufunuo ndio mapenzi ya Mungu yaliyoandaliwa na makamilifu kwa ajili ya siku hii. Hivyo, tunamjua YEYE NI NANI NASI NDIYE BIBI-ARUSI WAKE.
Ufunuo huo unazidi kuwa mkubwa zaidi na zaidi kila siku. Kila siku ipitayo hutuletea furaha zaidi, Ufunuo zaidi. Bibi-arusi anajiweka mwenyewe tayari kwa kuketi katika uwepo wa Sauti Yake, Yeye anapotuambia Sisi ni nani, jinsi gani Yeye anavyotupenda Sisi, jinsi ambavyo Yeye anavyosubiri kwa hamu kuwa pamoja Nasi!!!
Njooni, mjiweke tayari saa 06:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) kwa ajili ya kile kinachokaribia kutukia, tunapoisikiliza Sauti ya Melkizedeki.
Ndugu Joseph Branham
Ujumbe: 65-0221E “Huyu Melkizedeki Ni Nani?”
Maandiko ya kusoma:
Mwanzo Sura ya 18
Kutoka 33:12-23
Yohana Mt. 1:1
Warumi 8:1
2 Wakorintho 5:1
1 Wathesalonike 4:13-18
Timotheo wa Kwanza 3:16 / 6:15
Waebrania 7:1-3 /13:8
Ufunuo 10:1-7 / 21:16