Category Archives: Uncategorized

24-0721 Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake

UJUMBE: 65-0718M Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu tukusanyike pamoja Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA saa za Jeffersonville,(Ni Saa 1 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki), kusikia
65-0718M – Kujaribu Kumtendea Mungu Kazi Bila ya Kuwa Mapenzi ya Mungu.

Ndugu. Joseph Branham

24-0714 Kuonea Haya

UJUMBE: 65-0711 Kuonea Haya

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Asiyeonea Haya, 

Hakujawahi kuwa na wakati au watu kama leo hii. Sisi tumo ndani yake, warithi wa yote aliyotununulia. Anashiriki utakatifu wake pamoja nasi, mpaka ndani yake, tumekuwa haki halisi ya Mungu. 

Yeye alitujua tangu zamani kwa amri ya Kiungu, ya kwamba tungekuwa Bibi-arusi Wake. Alituchagua sisi, hatukumchagua Yeye kamwe. Hatukuja wenyewe, ilikuwa ni chaguo Lake. Sasa ameweka ndani ya mioyo yetu na nafsi zetu Ufunuo mkamilifu wa Neno Lake.

Siku baada ya siku, Yeye anatufunulia Neno Lake, akimimina Roho Wake juu yetu, akiyadhihirisha maisha Yake mwenyewe ndani yetu. Kamwe Bibi-arusi Wake hakuwahi kutia nanga zaidi mioyoni mwao wakijua wako katika mapenzi Yake makamilifu, na katika mpango Wake, kwa kukaa na Neno Lake, kuisikia Sauti Yake.

Upendo wa Mungu na Ujumbe huu umejaa mioyoni mwetu mpaka unabubujika tu. Hakuna kitu kingine sisi tunachotaka kusikia, kuzungumzia, kufanyia ushirika, au kushiriki tu nukuu ambayo tumesikia na kumsifu Bwana.

Sisi ni kama vile Musa upande wa nyuma ya jangwa. Tumetembea uso kwa uso na Mwenyezi Mungu, nasi tunaiona hiyo Sauti ikisema nasi; imeambatana kabisa na Neno na ahadi ya wakati huu. Imetufanyia kitu fulani. Hatuionei haya. Tunapenda kuitangaza kwa ulimwengu. Tunaamini Bwana Yesu ndiye Ujumbe wa saa hii na sisi NDIO BIBI-ARUSI WAKE.

Ametuimarisha kwa Neno Lake. Hakuna shaka hata kidogo, hii ndiyo njia iliyoandaliwa na Mungu. Mungu kamwe habadilishi nia Yake kuhusu Neno Lake. Yeye alimchagua malaika Wake wa saba kumwita Bibi-arusi Wake atoke, na kisha kumweka Yeye kwenye mstari sawa na Neno Lake.

Hakuna kitu katika maisha haya ila Yeye na Neno Lake. Hatuwezi kupata ya kutosha ya jambo hilo. Ni zaidi ya uhai kwetu sisi. Injili na Nguvu za Mwenyezi Mungu zimeenea ulimwenguni kote kuliko hapo awali. Neno sasa liko mikononi na masikioni mwa Bibi-arusi. Wakati wa kutengana unatukia sasa, wakati Mungu anamwita Bibi-arusi, naye shetani analiita kanisa.

Tunakupenda Wewe na Neno Lako, Bwana. Hatuwezi kupata ya kutosha. Tumeketi katika uwepo wa Neno lako kila siku, tukiivishwa, tukijitayarisha kwa ajili ya Kuja Kwako hivi karibuni. Baba, litakuwa limekaribia sana. Tunaweza kulihisi, Bwana. Tunasubiri kwa hamu kubwa. 

Baba, jalia tuwe waaminifu vya kutosha na tuzifanye upya nadhiri zetu tena. Tunajua Imani yetu katika Neno lako inawaka mioyoni mwetu. Umeondoa mashaka yote. Hakuna kitu hapo ila Neno Lako. Tuna hakika, nasi hatuoni haya kuuambia ulimwengu, sisi ni Bibi-arusi Wako wa Kanda.  

Ninataka kuualika ulimwengu kuja kusikiliza pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia Ujumbe:  Kuonea Haya 65-0711.

Ndugu. Joseph Branham 

Maandiko ya kusoma kabla ya Kusikiliza Kanda:

Marko 8:34-38

24-0707 Je! Mungu Habadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake?

UJUMBE: 65-0418E Je! Mungu Habadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake?

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Mapenzi Makamilifu,

Siku imeenda sana na Kuja kwa Bwana kumekaribia. Mlango unajifunga na wakati unaisha, ikiwa bado haujaisha. Muda umeenda sana kushangaa-shangaa; wa kuwa kama unyasi unaotikiswa na upepo; wa kuwa na masikio ya utafiti. Ni wakati wa kufanya maamuzi dhahiri. Yanilazimu nifanye nini ili kuwa Bibi-arusi Wake?

Je! Mungu hubadilisha Nia Yake kuhusu Neno Lake? KAMWE. Basi tunapaswa kujitahidi kila siku, kwa moyo na roho zetu zote kuwa katika MAPENZI YAKE MAKAMILIFU. Inatupasa kujikabidhi wenyewe kwenye mapenzi Yake na Neno Lake. Usilihoji kamwe, liamini tu na ulikubali. Usijaribu kutafuta njia ya kuliepa. Lichukue tu jinsi lilivyo.

Nabii anatuambia katika Ujumbe huu ya kwamba kusudi lake lote ni kutuonyesha ya kwamba Mungu hana budi kutimiza Neno Lake kusudi adumu kuwa Mungu, lakini watu wengi wanataka kuliepa, na kupitia njia nyingine. Wanapofanya jambo hilo, wanajikuta wakipiga hatua, na Mungu akiwabariki, bali wanafanya kazi katika mapenzi Yake ya kuruhusia na wala si katika mapenzi Yake makamilifu, ya Kiungu.

Nabii anaturudisha kwenye Neno na kutupa mifano ya kutazama, kujifunza, na kutukumbusha, Mungu HABADILISHI Nia Yake wala njia Yake, Yeye ni Mungu wala HABADILIKI.

Sasa, tunaona ya kwamba wote hawa wawili walikuwa watu wa kiroho, wote wawili walikuwa manabii, wote wawili walikuwa wameitwa. Naye Musa, akiwa moja kwa moja kazini, akiwa na Nguzo ya Moto mpya mbele yake kila siku, Roho wa Mungu akiwa juu yake, akiwa kazini. Huyu hapa mtumishi mwingine wa Mungu anakuja, aliyeitwa na Mungu, aliyechaguliwa na Mungu, nabii ambaye anajiliwa na Neno la Mungu. Hapa ndipo penye hatari. Hakuna mtu angaliweza kukataa mtu huyo kuwa ni wa Mungu—wa Mungu, kwa maana Biblia ilisema Roho wa Mungu alinena naye, naye alikuwa nabii.

Bwana, jinsi gani hilo linavyofanana sana? Ninawezaje kujua, wakati WOTE wawili walikuwa manabii? Wote wawili ni watu waliojazwa na Roho walioitwa na Mungu, waliochaguliwa na Mungu; manabii wa Mungu ambao Neno la Mungu huwajia. Wote wawili wakisema Roho Mtakatifu anawaongoza.

Hebu tusome na tujifunze nukuu chache kwa makini sana kuhusu kile ambacho malaika-mjumbe wa saba wa Mungu asemacho. Tunataka kile yeye anachosema; si kile kanisa linachosema, kile ambacho Daktari Jones asemacho, ama kile mtu mwingine yeyote asemacho. Sisi Tunataka kile BWANA ASEMA HIVI asemacho kupitia nabii Wake.

Musa, akiwa nabii aliyechaguliwa na Neno la Bwana, alithibitishwa ya kwamba alikuwa amechaguliwa kuwa kiongozi wao kwa ajili ya majira hayo, na ya kwamba Ibrahimu alikuwa ameahidi mambo haya yote,…

Hakuna mtu angaliweza kupachukua mahali pa Musa. Haidhuru ni Kora wangapi walioinuka, na ni Dathani wangapi; ilikuwa ni Musa, Mungu alikuwa amemwita, kwa vyo vyote.

Musa ndiye ambaye Mungu alikuwa amemchagua kuwaongoza watu. Wanaume wengine waliinuka na kusema wamepakwa mafuta, watu waliojazwa na Roho Mtakatifu pia. Mungu alikuwa amewaita waongoze pia. Lakini Musa alikuwa ndiye kiongozi wa Mapenzi Makamilifu ya ya Mungu ya asili wa kuwaongoza.

Lakini, na iwapo watu hawatatembea katika mapenzi Yake makamilifu, Yeye ana mapenzi ya kuruhusia atakayokufanya uende kwayo. Angalia, Yeye hurusu jambo hilo, kweli, bali atalifanya litende kazi kwa utukufu Wake, katika mapenzi Yake makamilifu. Sasa kama mngetaka…

Hakuna anayetaka kuwa katika mapenzi ya Mungu yakuruhusia. Bibi-arusi wa kweli anataka kuwa katika mapenzi Yake makamilifu, wakati wote, haijalishi gharama.

Kuna kutokubaliana kwingi, mawazo mengi, mkanganyiko mwingi, maoni mengi, juu ya umuhimu wa kucheza kanda.

Sote tunajua hili ndilo suala lenyewe ambalo limewatenganisha waaminio wa Ujumbe leo. Tunajua Bibi-arusi LAZIMA, NA ATA-ungana pamoja; hilo ni Neno.

Kuna watu waliojazwa na Roho, walioitwa na Mungu katika Kanisa leo. Wao ni watu waliotiwa mafuta na Mungu walioitwa kuhubiri Ujumbe huu. Lakini hakuna hata mmoja wao ambaye tunaweza sote kukubaliana kwake.

Wanawezaje wao kuwa ndio wa kumuunganisha Bibi-arusi? Je, twaweza kuungana kwenye huduma yao? Kwa kweli wao wameitwa kuliongoza kundi lao, lakini kuwarudisha hao kwenye MPANGO WA ASILI wa Mungu. kwa KIONGOZI WAKE. Kwa NABII WAKE. Sio kwenye huduma yao.

Kama wao hawakufundishi kwamba ile Sauti iliyo kwenye kanda hiyo ndio UNAPASWA uifuate, na lazima uamini kuwa ndiyo Sauti iliyo muhimu zaidi unayopaswa kuisikia, wako tu katika mapenzi Yake ya kuruhusia.

Iwapo wanakuambia kuwa Ndio Sauti iliyo muhimu zaidi, nao wanaamini kweli hivyo, basi inakuwaje hawabonyezi play kila wakati mnapokutana?

Ikiwa unataka kuwa na hakika, NA HAKIKA, kwamba uko katika mapenzi Yake makamilifu, kuna NJIA moja tu ya HAKIKA. Ni kusikia Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kwenye kanda.

Muda si muda, kanda inaangukia nyumbani mwao. Imelenga penyewe, basi. Kama yeye ni kondoo, anakuja moja kwa moja Nalo. Kama yeye ni mbuzi, anapiga hiyo kanda teke.

Lazima niwe na HAKIKA. Siwezi, na sita-bahatisha hata kidogo kwa kikomo changu cha Milele. NAJUA Sauti iliyo kwenye kanda ni Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi. NAJUA Hiyo haikosei. NAJUA Ilithibitishwa na Nguzo ya Moto. NAJUA Ndiye ambaye Mungu alimchagua kumwongoza Bibi-arusi Wake. NAJUA ya kwamba Sauti hiyo ndiyo Sauti pekee inayoweza na itakayo muunganisha Bibi-arusi. NAJUA itakuwa ni Sauti hiyo nitakayoisikia ikisema “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu”.

LAZIMA NIBONYEZE PLAY niisikie hiyo Sauti. Unaalikwa kuja kuungana nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia: 65-0418E Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake?

Ndugu. Joseph Branham

Tutauanza Ujumbe huu kwenye aya ya 61.

Maandiko ya kusoma kabla ya Kusikiliza Ujumbe:

Kutoka sura ya 19
Hesabu 22:31
Mathayo Mt. 28:19
Luka 17:30
Ufunuo sura ya 17

24-0630 Huyu Melkizedeki Ni Nani?

UJUMBE: 65-0221E Huyu Melkizedeki Ni Nani?

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Kristo,
Hebu sote tukusanyike pamoja Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA saa za Jeffersonville (ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) kusikia 65-0221E – “Huyu Melkizedeki Ni Nani?”

Ndugu Joseph Branham

24-0623 Ndoa Na Talaka

UJUMBE: 65-0221M Ndoa Na Talaka

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Safi Asiyeghoshiwa wa Neno,

Sisi ndio Bibi Wake mdogo anayependeza; asiyeghoshiwa, asiyeguswa na dhehebu la mtu ye yote, nadharia yo yote iliyobuniwa na mwanadamu. Sisi ni Bibi-arusi wa Neno asiyeghoshiwa kabisa! Sisi ndio yule binti wa Mungu aliyetiwa mimba.

Sisi ni watoto wa Neno Lake lililonenwa, ambalo ni Neno Lake la asili! Hakuna dhambi katika Mungu, kwa hivyo hakuna dhambi ndani yetu, kwa vile tulivyo mfano Wake Mwenyewe. Twawezaje kuanguka? Hilo Haliwezekani….HAIWEZEKANI! Sisi ni sehemu Yake, NENO Lake LA ASILI.

Tunawezaje kujua hili bila shaka yoyote? UFUNUO. Biblia nzima, Ujumbe huu, Neno la Mungu, yote ni Ufunuo. Hivyo ndivyo tunavyojua ukweli kati ya Sauti hii na sauti zingine zote, kwa sababu ni Ufunuo. Na Ufunuo wetu unaambatana kabisa na Neno, sio kinyume cha Neno.

Na juu ya mwamba huu” (ufunuo wa kiroho wa Neno ni nini) “Nitajenga Kanisa Langu; wala milango ya kuzimu haitaliangamiza.” Mke Wake hatashawishiwa na mwanamume mwingine. “Nitalijenga Kanisa Langu, na milango ya kuzimu haiwezi kulitikisa kamwe.”

Tutakuwa wakweli na waaminifu kwa Neno Lake na Sauti Yake, peke yake. Kamwe hatutatiwa unajisi na mwanamume mwingine na kufanya uzinzi. Tutabaki kuwa Bibi-arusi Neno Bikira Wake. Hatutaangalia, kusikiliza au kuvutiwa na neno lingine lolote.

Liko ndani ya mioyo yetu. Hatungaliweza kamwe kuwa na mume mwingine, ila MUME wetu MMOJA, Yesu Kristo, Mtu mmoja, Mungu, Imanueli. Mkewe atakuwa maelfu mara maelfu ya maelfu. Hilo linaonyesha ya kwamba Bibi-arusi hana budi kutoka katika Neno. “Bwana Yesu Mmoja, na Bibi-arusi Wake wengi, umoja.”

Lazima tukumbuke na kuelewa hili si la kila mtu, ni kundi la nabii PEKE YAKE. Wafuasi wake mwenyewe. Ujumbe huu ni kwa ajili yao tu, lile kundi dogo ambalo Roho Mtakatifu alimpa kulisimamia.

Mungu atamwajibisha yeye kwa yale anayotuambia, na Mungu atatuwajibisha sisi, waongofu wake kutoka nchini kote, wale ambao amewaongoza kwa Kristo, kuamini kila Neno Lake na kutokupatana kamwe.

Ni jambo lakupendeza sana jinsi gani kwetu kuketi na kumsikiliza Yeye akitueleza jinsi sisi tulivyo wateule wake. Jinsi Bibi-arusi Wake wa kwanza, na Bibi-arusi wa pili, walivyomwangusha; Bali sisi, Bibi-arusi Wake mkuu wa wakati wa mwisho HATUTAMWANGUSHA. Tutabaki kuwa Bibi-arusi Neno Bikira Wake wa kweli, na mwaminifu hadi mwisho.

Imani yetu katika Neno lake inakua zaidi kila siku. Tunajiweka wenyewe tayari kwa kusikiliza na kutii kila Neno Lake, kuisikia Sauti yake ikinena nasi, kuzisoma Biblia zetu, kuomba na kumwabudu Yeye siku nzima.

Tunajua Yeye anakuja upesi sana. Dakika yoyote sasa. Kama vile Nuhu, tulikuwa tukitumaini Yeye alikuwa yuaja jana; labda kesho asubuhi, adhuhuri, jioni, lakini tunajua Yeye anakuja. Nabii wa Mungu na Neno Lake hawakosei, ANAKUJA. Tunahisi ni siku ya 7, nasi tunaweza kuona mawingu yakijikusanya na matone makubwa ya mvua yakianguka; wakati umefika.

Tuko salama salimini ndani ya Safina, tukingojea kwa hamu kubwa. Njoo uungane nasi wakati tunaposikia Sauti ya Mungu ikitufariji Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, tunaposikia: Ndoa Na Talaka 65-0221M.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Mathayo Mt 5:31-32 / 16:18 / 19:1-8 / 28:19
Matendo 2:38
Warumi 9:14-23
Timotheo wa Kwanza 2:9-15
Wakorintho wa Kwanza 7:10-15 / 14:34
Waebrania 11:4
Ufunuo 10:7
Mwanzo sura ya 3
Mambo ya Walawi 21:7
Ayubu 14:1-2
Isaya 53
Ezekieli 44:22

24-0616 Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia

UJUMBE: 65-0220 Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bi Yesu Kristo,

Kama tungeuliza swali kuhusu cho chote maishani mwetu, yapaswa kuwe na jibu la kweli. Kwaweza kuwe na lililo la karibu nalo, lakini kunapaswa kuwa na jibu la kweli, la moja kwa moja kwa kila swali. Kwa hiyo, basi kila swali linalozuka maishani mwetu, yabidi kuwe na jibu la kweli na sahihi.

Kama tuna swali la Biblia, lazima kuwe na jibu la Biblia. Hatutaki lije kutoka kwenye kundi la watu, kutoka kwenye ushirika wo wote ule, au kutoka kwa mwalimu fulani, au kutoka kwa madhehebu fulani. Tunataka litoke moja kwa moja katika Maandiko. Ni lazima tujue: ni mahali gani pa kweli na sahihi pa Mungu pa kumwabudia?

Mungu alichagua kukutana na binadamu; siyo kanisani, siyo katika madhehebu, siyo katika kanuni ya imani, lakini katika Kristo. Hapo ndipo mahali pekee ambapo Mungu atakutana na mtu, na anapoweza kumwabudia Mungu, ni katika Kristo. Ni mahali hapo pekee. Haidhuru kama wewe ni Mmethodisti, Mbatisti, Mkatoliki, Mprotestanti, hata uwe nani, kuna mahali pamoja tu ambapo unaweza kwa usahihi kumwabudu Mungu, hapo ni katika Kristo.

Mahali pekee sahihi, na alipopachagua Mungu pa kumwabudia Yeye ni katika Yesu Kristo; hiyo ni Njia Yake pekee iliyoandaliwa.

Biblia ilituahidi Tai katika Malaki 4; Nguzo ya Nuru tunayopaswa kuifuata. Atalionyesha kanisa lililokosea Yeye ni Waebrania 13:8, Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele. Pia tumeahidiwa katika Luka 17:30 kwamba Mwana wa Adamu (Tai) atakuwa akijifunua Mwenyewe kwa Bibi-arusi Wake.

Katika Ufunuo 4:7, inatuambia kwamba kulikuwa na Wenye Uhai wanne, na wa kwanza akiwa simba. Mwenye Uhai aliyefuata alikuwa ndama. Kisha, aliyefuata alikuwa ni mwanadamu; Na mwanadamu huyo alikuwa wale watengenezaji, elimu ya mwanadamu, theolojia, na kadhalika.

Lakini Biblia ilisema, wakati wa jioni, yule Mwenye Uhai wa mwisho ambaye alikuwa aje alikuwa Tai arukaye. Mungu angempa Bibi-arusi Wake wa wakati wa mwisho Tai; Mwana wa Adamu Mwenyewe, akijifunua Mwenyewe katika mwili kumwongoza Bibi-arusi Wake.

Biblia pia inasema mambo yote ya kale, katika Agano la Kale, yalikuwa ni vivuli vya mambo yajayo. Kivuli hicho kinapokaribia, negativu humezwa na picha yenyewe. Kile Kilichotokea wakati huo ni kivuli cha kile ambacho kingetokea leo.

Katika I Samweli 8, Agano la Kale linatuambia Mungu alikuwa amemtoa Samweli nabii kuwaongoza watu. Watu walimwendea na kumwambia wanataka mfalme. Samweli alifadhaika sana hata moyo wake nusura ukome.

Mungu alikuwa anawaongoza watu Wake kupitia kwa nabii huyu aliyewekwa wakfu, aliyethibitishwa kwa Maandiko naye akaona kwamba alikuwa amekataliwa. Akawakusanya watu akawasihi wasimwache Mungu Ambaye alikuwa amewabeba kama watoto, na kuwafanikisha na kuwabariki. Lakini wao wakakaidi.

Wakamwambia Samweli. “Hujakosea katika uongozi wako. Hujakuwa mdanganyifu katika mambo yako ya fedha. Umejaribu uwezavyo kutuweka sawa na Neno la Bwana. Tunaifurahia miujiza, hekima, chakula na ulinzi wa Mungu.Tunauamini. Tunaupenda. Na isitoshe hatutaki kuukosa. Ni kwamba tu tanataka mfalme wa kutuongoza vitani.

Sasa bila shaka tunapotoka kwenda vitani yangali ni makusudio yetu kuacha makuhani watutangulie huku Yuda wakifuata, nasi tutapiga matarubeta na kupiga makelele na kuimba. Hatutarajii kuacha yo yote ya mambo hayo. LAKINI TUNATAKA MFALME AMBAYE NI MMOJA WETU APATE KUTUONGOZA.”
    
Hawa hawakuwa watu wa kimadhehebu wa siku hizo. Kwa kweli hawa walikuwa ni watu waliodai kwamba YEYE ALIKUWA nabii wa Mungu ambaye alichaguliwa na Mungu kuwaongoza.

“Ndiyo, wewe ni nabii. Tunaamini Ujumbe. Mungu anakufunulia wewe Neno Lake, nasi tunalipenda, na isitoshe hatutaki kuukosa, lakini sisi tunamtaka mtu mwingine zaidi YAKO atuongoze; mmoja wetu sisi. Bado tunakusudia kusema tunauamini Ujumbe uliotuletea. Ni Neno. Wewe ni nabii, lakini si wewe tu pekee ama Sauti iliyo muhimu zaidi.”

Wapo watu wazuri ulimwenguni siku hizi, makanisa mazuri. Lakini kuna Bi Yesu Kristo mmoja, na Huyo ni sisi, ndio Wale Yeye anakuja kuwachukua; Bibi-arusi Neno Wake aliye safi ambaye atakayekaa na SAUTI PEKEE YA MUNGU ILIYOTHIBITISHWA NA KUHAKIKISHWA KUWA BWANA ASEMA HIVI.

Ikiwa ungependa kuungana nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)
bado tutakuwa kwenye mawasiliano ya simu ulimwenguni kote tukisikiliza. Hiki ndicho kitakachotendeka.

Njoo juu ya ndugu zangu, dada, rafiki zangu, hapa katika sehemu hii usiku wa leo na huko nje kwenye simu. Majimbo mengi mbalimbali yanasikiliza, mahali pote tokea Pwani ya Mashariki hadi ya Magharibi. Naomba, Mungu Mpenzi, huko chini kuvuka majangwa kule Tucson, huko mbali California, juu huko Nevada na Idaho, kwenda hadi Mashariki na kila mahali, chini huko Texas; wakati mwaliko huu unatolewa, watu wameketi katika—katika makanisa madogo, vituo vya mafuta, majumbani, wakisikiliza. Ee Mungu, jalia mwanamume yule aliyepotea au mwanamke, mvulana au msichana, saa hii, aje Kwako. Lijalie hilo sasa hivi. Tunaomba katika Jina la Yesu, kwamba wataona mahali hapa pa usalama wakati muda ungalipo.

Sasa, Bwana, pambano hili limekwisha kabiliwa, kwamba Shetani, yule laghai mkuu, yeye hana haki ya kumshikilia mtoto wa Mungu. Yeye ni kiumbe kilichoshindwa. Yesu Kristo, mahali pekee pa kuabudia, Jina pekee la kweli, alilomshindia hapo Kalvari. Nasi tunadai Damu Yake sasa hivi, kwamba Yeye alishinda kila maradhi, kila ugonjwa.

Nami namwagiza Shetani kuwaacha wasikizi hawa. Katika Jina la Yesu Kristo, toka katika watu hawa, na wafanywe huru

Kila mtu ambaye anakubali kuponywa kwake juu ya msingi wa Neno lililoandikwa, toa ushuhuda wako kwa kusimama kwa miguu yako na kusema, “Ninakubali sasa kuponywa kwangu katika Jina la Yesu Kristo.” Simama kwa miguu yako.

Mungu asifiwe! Basi. Angalia huku, viwete na kadhalika wakiinuka. Mungu asifiwe. Naam. Aminini tu. Yeye yupo hapa.

Ndugu. Joseph Branham

Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia 65-0220

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Kumbukumbu la Torati 16:1-3
Kutoka 12:3-6
Malaki Sura ya 3 & 4
Luka 17:30
Warumi 8:1
Ufunuo 4:7

24-0609 Leo Maandiko Haya Yametimia

UJUMBE: 65-0219 Leo Maandiko Haya Yametimia

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Uzao Maalum wa Kiroho wa Kifalme,

Hakuna kusubiri tena, hakuna kushangaa tena, TUMEFIKA! Sisi NDIYE yule Bibi-arusi Uzao maalum wa Kiroho wa Kifalme. Uzao wa Kiroho kwa Mwana yule wa Kifalme aliyeahidiwa. Sio kundi fulani katika siku zijazo; si kizazi kijacho; tunaishi katika siku ya mwisho, sisi ndio kizazi kile kitakachomwona Yesu Kristo akirudi duniani.

Leo, Maandiko haya Yametimia!

Injili ile ile, Nguvu zile zile, Mwana wa Adamu YULE YULE aliyekuwako jana, yupo leo, na atakuwako milele.

Leo, Maandiko haya Yametimia!

Marafiki wapendwa huko Arizona, California, Texas, kote nchini Amerika Na ULIMWENGUNI KOTE mnaosikiliza kanda hii hewani kwenye muunganiko wa simu; M-w-a-n-a wa Mungu yule yule aliyetokea mashariki na kujithibitisha Mwenyewe kama Mungu aliyefanyika mwili, ndiye M-w-a-n-a yule yule wa Mungu katika kizio cha magharibi cha dunia hapa, ambaye anayejitambulisha Mwenyewe kati ya kanisa usiku huu, yeye yule jana, leo, na hata milele. Ile Nuru ya jioni ya Mwana imekuja.

Leo, Maandiko haya Yametimia!

Sauti ya Masihi, aliyekuwa akisimama na kunena jukwaani katika siku Yake, akijitambulisha Mwenyewe na Neno la ahadi la wakati huo, ndio Sauti ile ile ya Masihi, inayonena na Bibi-arusi Wake leo ulimwenguni kote kwenye kanda, ikituambia: Mimi ni yeye yule jana, leo na hata milele. MIMI NI Sauti ya Mungu Kwenu. WEWE NI BIBI-ARUSI WANGU UZAO WA KIROHO WA KIFALME ambaye amekaa na Neno Langu.

Leo, Maandiko haya Yametimia!

Kuna msukosuko mwingi kati ya watu siku hizi hata wanashindwa kuiona Kweli ya Mungu. Ni kwa sababu kuna mafafanuzi mengi sana ya Neno la Mungu yaliyotengenezwa na wanadamu. Mungu hahitaji mtu yeyote afafanue Neno Lake. Yeye Mwenyewe ndiye mfafanuzi. Alimtumia Bibi-arusi Wake nabii-malaika wa siku za Sauti wa Ufunuo 10:7 kulifafanua Neno Lake. Ni BWANA ASEMA HIVI.

Leo, Maandiko haya Yametimia!

Unasema, “kama ningalikuwa wakati ule Yesu alipokuwa duniani, ningalifanya hivi na hivi.” Vema, hicho hakikuwa kizazi chako. Lakini, hiki ndicho kizazi chako, huu ndio wakati wako. Ni Sauti gani unayosema ndio Sauti ya Mungu? Ni Sauti gani ndio iliyo muhimu sana kwako?

Leo, Maandiko haya Yametimia!

Ibilisi anaenda huku na huko kuliko hapo nyuma kumshambulia Bibi-arusi Wake. Anaweza kukufanya ufikiri kuwa una maradhi au aina fulani ya ugonjwa, au kuishambulia familia yako. Wakati mwingine Mungu huruhusu mambo kuwa meusi sana hata huwezi kuona juu, kando—kando, au penginepo pote, na ndipo Yeye huja kutengeneza njia kupitia kwayo, ili uweze kusema,
“Mimi si uzao wa Hajiri, mimi si uzao wa Sara, mimi hata si uzao wa Mariamu, mimi ni Uzao wa Kiroho wa Mungu wa Kifalme wa Ibrahimu. Ninalichukua Neno la Mungu lililoahidiwa kwa ajili yangu, Ni Bwana Asema hivi. sitatikiswa. Haidhuru inaonekanaje, shetani anasema nini. Chochote ninachohitaji, nitamchukua Mungu katika Neno Lake.

Leo, Maandiko haya Yametimia!

Sauti ya Mungu imesema. Nimekihifadhi Chakula chote cha Kiroho mnachohitaji. Semeni TU yale yaliyo kwenye kanda hizo. Mimi ni Sauti ya Mungu kwenu. Neno Langu halihitaji fasiri. Msibishane au kupigana, pendaneni, BALI kaeni na NENO LANGU.

Leo, Maandiko haya Yametimia!

Usijikunyate. Usiwe na huzuni. Usimruhusu Shetani akunyang’anye FURAHA yako. Kumbuka wewe NI NANI, kule uendako, itakuwaje kwenye Karamu hiyo kuu ya Arusi. Kuishi katika mji huo mzuri aliyokujengea wewe tu. Ambamo utakuwa Milele yote pamoja Naye na wale wote waliyotangulia.

Hakuna ugonjwa tena. Hakuna huzuni tena. Hakuna kifo tena. Hakuna vita tena. Uzima wa Milele tu pamoja Naye. Ndipo tutasema:

Leo, Maandiko haya Yametimia!

Hebu tusiwe na huzuni na kusema, “Nimechoswa sana na mahali hapa, nataka kutoka hapa. Hebu na tuliseme namna hii: Anakuja dakika yoyote sasa, KWA AJILI YANGU…UTUKUFU! Siwezi kusubiri. Nitawaona wapendwa wangu wote. Watatokea mbele yangu, ndipo nitajua, IMEKWISHA, TUMEFIKA.

Kisha, chini ya dakika moja ya kufumba na kufumbua, sote tutakuwa pamoja ng’ambo ya pili.

Hebu tufurahi na tupige shangwe, kwa kuwa ile arusi ya Mwana-Kondoo i karibu, na Bibi-arusi Wake… Bibi-arusi Wake amejifanya tayari!

Kama ungependa kupiga shangwe, na kuwa kwenye Arusi ya Mwana-Kondoo pamoja nasi, njoo ujiweke tayari Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia:

Leo, Maandiko Haya Yametimia 65-0219

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma:

Yohana Mt Sura ya 16
Isaya 61:1-2
Luka Mt 4:16

24-0602 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi

UJUMBE: 65-0218 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Uzao Wa Kifalme Wa Ibrahimu,

Ninatuma salamu ulimwenguni kote, kwa wale waliokusanyika pamoja, wakisikiliza hewani kwa njia ya simu, wakizilisha nafsi zao kwa ile Mana mpya inayoanguka kutoka Mbinguni. Ninyi mmenunuliwa kwa Damu ya Yesu Kristo Mwenyewe.

Bwana Yesu, naomba ya kwamba Wewe utayapa upako maneno haya usiku huu yakasikiwe na kila sikio linaloongozwa na sauti ya Kiungu. Na ikiwa kuna mmoja hapa anayesikiza nchini kote.

Mungu anayapaka mafuta masikio ya kila mmoja wetu, tunaposikiza kutoka kote ulimwenguni na kuisikia sauti ya Kiungu ya Sauti ya Mungu ikisema nasi, Bwana Asema Hivi.

Sisi ndio Kanisa halisi la Mungu lililozaliwa mara ya pili ambalo huamini KILA Neno la Mungu dhidi ya cho chote kile, bila kujali ni kitu gani, kwa maana ni Sauti ya Mungu ya kweli isiyoghoshiwa inayonena.

Mungu anajidhihirisha Mwenyewe ndani yetu, Kanisa Bibi-arusi Wake. Sisi sio wabebaji wa ile Mbegu, SISI NI UZAO WA KIFALME. Uzima Wake wote uliokuwamo ndani Yake umejizaa tena ndani YETU, Kanisa Bibi-arusi halisi na wa kweli akizaa Neno zima la Mungu katika utimilifu Wake na katika nguvu Zake.

Hapawezi kuwepo nyakati zingine za kanisa baada ya huu. Tuko katika wakati wa mwisho, ndugu na dada. Tuko hapa; tumefika. Bwana ashukuriwe!

Tuko mwisho. Tumewasili. Bibi-arusi YEYE ametambua Sisi ni nani. Ni wakati wa Bibi-arusi Mbegu. Makapi yamekufa. Yale makapi tayari yamekwisha kukauka. Sisi ndio Neno la Mungu lililozaliwa kibikira lililodhihirishwa, Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele.

Hatutaguswa. Hakutakuwa na kuguswa-guswa na watu ndani YETU. Sisi NDIKO Kuzaliwa kibikira kwa Bibi-arusi. Tumeamriwa na Mungu kudumu waaminifu kwa Neno bikira. Mbegu haina budi kukaa katika Uwepo wa Mwana, Roho Mtakatifu, Sauti ya Mwana wa Adamu, ili Iweze kuivishwa. Na kwetu sisi, KUNA NJIA MOJA TU PEKEE: KUBONYEZA PLAY NA KUISIKIA SAUTI YA MWANA WA ADAMU MWENYEWE.

Na kama nisemavyo kuna Kanisa lililoteuliwa mahali fulani ulimwenguni lililotoka na kujiweka mbali na mambo hayo. Na madhihirisho ya Mungu yamelivutia macho. Tumo katika siku za mwisho.

Sisi ni Tai wa Mungu. Hakuna kupatana ndani yetu. Tunaweza tu kula Mana mpya. Sisi ni kama ndama zizini. Tunakula tu Chakula kilichohifadhiwa ambacho kimeandaliwa kwa ajili yetu.

Tunawaona Tai wa Mungu kote ulimwenguni wakitaka hiyo Mana mpya. Wataendelea kuitafuta mpaka waipate. Wataruka juu zaidi na zaidi. Iwapo haimo katika bonde hili, ataruka juu zaidi. Wanataka Neno la Mungu jipya kutoka kwenye Sauti ya Mungu. Kikomo chao cha Milele kimetulia juu Yake. Palipo na Mzoga, Tai wanakusanyika.

Roho wake amekuja juu yetu kufanya mambo yale aliyofanya. Ni kujizaa tena kwa ile Punje. Sisi ndio ule Uzao wa Kifalme wa Imani ya Ibrahimu ambao tunachukua lolote lilio kinyume cha Neno la Mungu na kukiita kana kwamba Sivyo kilivyo. Hatuwezi kutilia shaka ama kuliweka mahala pasipo pake Neno hata moja la Mungu, kwa maana tunaamini ni BWANA ASEMA HIVI. Yesu Kristo yeye yule jana, leo na hata milele.

Mungu mpendwa, hebu na tusiyape kisogo kwa ajili ya upuzi wa ulimwengu, bali hebu na tumpokee Yeye usiku wa leo kwa mioyo yetu yote._Nawe Bwana, kaumbe ndani yangu roho zuri, Roho ya Uzima, nipate kuamini maneno Yako yote na kumkubali Yesu, aliye Neno, yeye yule jana, leo, na hata milele, na nikaamini leo ile sehemu ambayo imekusudiwa kwa wakati huu. Tujalie, Bwana. Naomba katika Jina la Yesu.
   
Ningependa kuwaalika kuja kuisikia Sauti ya Mungu iliyothibitishwa ya wakati wa mwisho anapotupa Chakula cha Tai; ahadi ya Mungu. Inahitaji imani isiyoghoshiwa katika Neno hili la Mungu ili kuwa Bibi-arusi Wake.

Ndugu. Joseph Branham
    

Muda:

saa 6:00 SITA MCHANA Saa za Jeffersonville (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)

Ujumbe:

Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi 65-0218

Maandiko:

Mathayo 24:24
Luka Mt 17:30
Yohana Mt 5:24 / 14:12
Warumi 8:1
Wagalatia 4:27-31
Waebrania 13:8
1 Yohana 5:7
Ufunuo 10
Malaki 4

Bali unapofikia kusema, “Mimi na Baba Yangu ni Mmoja,” na mambo haya mengine, ndipo kapi linajiondoa kwake. Bali Kanisa Bibi-Arusi halisi atazaa Neno nzima la Mungu katika utimilifu Wake na nguvu Zake, kwa maana ni yeye yule jana, leo, na hata milele.

65-0218 -  Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi
Rev. William Marrion Branham 

Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele.
Roho yuaja juu ya Bibi-Arusi kufanya mambo yale aliyofanya. Mnaona, ni kujizaa tena kwa ile punje.

65-0218 – Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi
Rev. William Marrion Branham

24-0526 Mtu Anayejiepusha Na Uso Wa Bwana

UJUMBE: 65-0217 Mtu Anayejiepusha Na Uso Wa Bwana

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Abiria wa Ninawi,

Baba, palipo Mzoga Wako, ndipo Tai Wako wanakusanyika pamoja. Unatulisha kwa Mana Yako ya Kiungu. Zipe nafsi zetu kile tunachohitaji. Tunakuonea kiu, Ewe Baba. Tuko Mikononi Mwako.

Tumekaa katika uwepo Wako, tukiivishwa, kwa kuisikia Sauti Yako. Bibi-arusi hawana budi waamue niani mwao na kukabiliana nalo. Aidha ni Kweli au ni uongo. Je! kuisikia Sauti Yako iliyothibitishwa ndilo jambo lililo muhimu zaidi ambalo Bibi-arusi Wako analopaswa kufanya au la? Kama ni kweli, hebu na tulifanye. Usingojee zaidi, tafuta uone sasa ukweli ni upi na lililo sahihi, na udumu Nalo. Tunajua ni Kweli, tunajua Ndio Njia Yako iliyoandaliwa ya siku hii.

Ni lazima nipige kelele, “Simba amekwisha kunguruma, ni nani asiyeogopa? Mungu amenena, ni nani awezaye neno ila kutabiri?” Tunaliona katika Neno. Uliliahidi Hilo. Ni nani wawezao kunyamaza na kutulia?

Hatutaki wazo linalopendwa na watu wengi. Tunataka Ukweli. Nasi hatuninino, tuna(taka) hatutaki ku—hatutaki kukabili cho chote ila ambacho Mungu amesema ni Kweli.

Wakati umefika ambapo yakubidi uamue ni merikebu gani unayopanda. Je! unajilisha Neno lililonenwa moja kwa moja kutoka kwa Mwana wa Adamu, ama kitu kingine? Je! kuna mtu fulani anayekuambia kwamba yakubidi uzisikie sauti zingine ili uweze kuwa Bibi-arusi Wake? Kwamba kuzicheza kanda katika nyumba zenu au makanisani mwenu silo jambo lililo muhimu zaidi ambalo Bibi-arusi analotakiwa kufanya?

Unasikiliza sauti ya nani? Hiyo sauti inakuambia nini? Ni sauti gani unayoweka kikomo chako cha Milele, na cha familia yako kwake?

Si mimi, haikuwa yule malaika wa saba, loo, la; ilikuwa ni kudhihirishwa kwa Mwana wa Adamu. Haikuwa ni yule malaika, ujumbe wake; ilikuwa ni siri aliyoifunua Mungu. Si mwanadamu; ni Mungu. Yule malaika hakuwa Mwana wa Adamu; yeye alikuwa ni mjumbe kutoka kwa Mwana wa Adamu. Mwana wa Adamu ni Kristo; Yeye Ndiye mnayejilisha. Hamjilishi mwanadamu; mwanadamu, maneno yake yatashindwa. Bali mnakula Mwili-Neno lisiloshindwa la Mwana wa Adamu.

Msisikilize sauti yo yote ambayo haiweki Sauti hiyo, Mwili-Neno lisiloshindwa la Mwana wa Adamu, NAFASI YA KWANZA mbele zenu. Wao wanaweza kuhubiri, kufundisha, au kufanya yote ambayo Mungu amewaitia kufanya, lakini wao SIO ile sauti iliyo muhimu zaidi MNAYOPASWA KUISIKIA.

Kama wangeamini hivyo, basi wangeicheza Sauti hiyo mnapokuwa mmekusanyika pamoja na kuwaambia, “Sauti hii, iliyo kwenye kanda, ndio Sauti iliyo muhimu zaidi ya kusikiliza. Hiyo, na HIYO pekee ndio, BWANA ASEMA HIVI.”

Ni Sauti ipi unayoipenda? Kwa nini Yeye aliifanya Sauti Yake irekodiwe na kuhifadhiwa? Mungu alichagua Sauti ya nani kulinena Neno Lake kwa ajili ya siku yetu?

Kwa nabii Wake aliyemtoa, yule aliyemtuma kushuka kwenda kule na kuutangaza ujumbe huo. Naam, ilionekana kama kwamba Yeye angaliweza kumtuma nabii mwingine, bali Yeye alimchagua Yona; na hata Eliya asingalifaa; Yeremia asingalifaa; Musa asingalifaa. Yona ndiye ilikuwa aende Ninawi. Hakukuwa na lingine. Yeye alimwagiza na kumwambia aondoke aende. Na Yeye anaposema, “Nenda kule, Yona, nenda Ninawi,” hakuna mwingine anayeweza kwenda kufanya jambo hilo ila Yona.

Mungu alituchagua tangu zamani kwa ajili ya maisha haya. Sauti hii inatunenea Maneno ya Uzima wa Milele. Kwetu sisi, hii ndiyo Njia iliyoandaliwa na Mungu. Hii ndio Merikebu yetu. Kama umo kwenye merikebu inayoenda Tarshishi, Toka kabla haijachelewa sana.

Kama umekuwa ukishangaa, au una maswali yoyote moyoni mwako upitie njia gani ama ufanye nini, njoo uungane nasi. Ingia kwenye Merikebu pamoja nasi. Tunaenda Ninawi, kupiga kelele. Tunaiacha hiyo merikebu ya Tarshishi ishuke iende kama wakitaka. Tuna wajibu mbele za Mungu, huo ni Ujumbe ambao tunawajibika kwake.

Sisemi ikiwa unaenda kwenye kanisa lisilocheza kanda kuwa ni merikebu inayoelekea Tarshishi, lakini kama MTU YEYOTE haweki Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda kuwa ndio sauti iliyo muhimu sana ikupasayo kuisikia, afadhali uangalie kuona ni nani anayeiongoza merikebu yako na ni wapi merikebu yako inakoelekea.

Ninakualika uungane nasi Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) wakati Nahodha wa Merikebu yetu anapozungumza na kutuletea Ujumbe:   Mtu Anayejiepusha Na Uso Wa Bwana 65-0217.

Hebu na tuanze ufufuo huu vizuri. Hiyo ni kweli. Mnangojea nini? Tunaamini ya kwamba Kuja kwa Bwana kumekaribia, Naye atakuwa na Bibi-Arusi, na Yuko tayari. Nasi hatutaki merikebu zo zote zinazoelekea Tarshishi ye yote. Tunaenda Ninawi. Tunaenda Utukufuni. Amina. Hiyo ni kweli. Tunaelekea mahali ambapo Mungu atatubariki, na hivyo ndivyo tunavyotaka kufanya.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma:

Yona 1:1-3
Malaki 4
Yohana Mt 14:12
Luka 17:30

24-0519 Maswali na Majibu #4

UJUMBE: 64-0830E Maswali na Majibu #4

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Familia ya Kanda,

Nakusudia ninyi, familia yangu, na familia kule ulimwenguni ambako tume—ambapo kanda zetu huenda.

Hao ni sisi, Familia ya Kanda ya nabii; watoto wake waliotawanyika ulimwenguni kote, wale aliomzalia Kristo. Wale ambao Baba amewapa Ufunuo Wake Mwenyewe katika siku hizi za mwisho.

Nataka kuwakusanya wote pamoja mojawapo wa siku hizi (ona?)—Baba atafanya hivyo, kisha tuta—tutakuwa na Makao na hatutazurura tena.

NATAKA KUWAKUSANYA WOTE PAMOJA. Hilo linatendeka sasa hivi. Ujumbe huu, Neno Lake, Kanda hizi zinatenda jambo hilo hasa: zinakusanya Bibi-arusi wote pamoja, zinatuunganisha kama KITENGO KIMOJA kutoka ulimwenguni kote. Hakuna kingine ila Sauti Yake; Sauti ya Mungu kwenye kanda, ndiyo inayoweza kumkusanya Bibi-arusi Wake pamoja.

Nanyi, mnapojazwa na Roho Mtakatifu, hapa kuna mojawapo ya ishara bora nizijuazo: unapendana sana na Kristo na kuamini kila Neno ambalo Yeye asema kuwa ni Kweli. Ona? Hiyo ndiyo ishara kuwa umempokea Roho Mtakatifu. Na maisha yako yamejawa na furaha, na—na lo, kila kitu ni tofauti (ona?) kuliko vile ilivyokuwa. Huyo ni Roho Mtakatifu.

Mioyo yetu, akili na roho zetu zimejawa furaha, upendo na Ufunuo, hatuwezi kabisa kujizuia. Kila ujumbe tunaousikia huleta Ufunuo zaidi. Tunaona sisi ni nani na yale tufanyayo ili kuwa katika Mapenzi yake Makamilifu. Hakuna kitu kinachoweza kutuondoa kutoka kwenye yale Mungu aliyoweka ndani ya mioyo yetu. Kubonyeza Play ndiyo Njia Iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku ya leo. Hakuna kubahatisha, hakuna kutumai, hakuna kumuuliza Roho Mtakatifu, “Je! hili nililotoka kusikia ni Neno la kweli?” “Je! Ninahitaji kulichunguza kwa Neno?”

Sio sisi. Yale Tunayosikia kwenye kanda NI NENO. Neno hilo tunalosikia kwenye kanda ndilo NENO PEKEE ambalo limethibitishwa na Roho Mtakatifu Mwenyewe, ile Nguzo ya Moto, kuwa Bwana Asema Hivi kwa Bibi-arusi.

Endapo mtu fulani akituambia, “Kuna mengi sana yaliyosemwa kwenye kanda ambayo yalikuwa tu ni Ndugu Branham akinena, si Neno lililotiwa mafuta. Huyo alikuwa mtu tu. Roho Mtakatifu ametuongoza kwenye yale ambayo ni Neno na yale yaliyokuwa tu ni Ndugu Branham akizungumza.”

Sio kwetu sisi. Sisi tunaamini tu yale nabii aliyotuambia tusisahau kamwe.

Nawatakeni msisahau kamwe hilo Neno. Yale aliyosema Musa, Mungu aliyaheshimu, kwa maana Neno la Mungu lilikuwa ndani ya Musa.

Hatutasahau kamwe yale nabii aliyosema, nasi Tunayaamini; kwa maana yamechorwa kwa kalamu ya chuma juu ya mioyo yetu. Yale aliyosema kwenye kanda, Mungu aliyaheshimu, nasi tunayaamini.

Hakuna heshima iliyo kubwa kuliko kuketi kuisikia Sauti ya Mungu ikinena nasi. Atakuwa akizungumza na Bibi-arusi Wake Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) na kuyajibu maswali: 64-0830E Maswali Na Majibu #4. Ningependa kukualika kuungana nasi. Ni uamuzi ambao hautaujutia kamwe.

Ndugu. Joseph Branham