UJUMBE: 64-0614M Kufunuliwa Kwa Mungu
- 25-1102 Kufunuliwa Kwa Mungu
- 24-0218 Kufunuliwa Kwa Mungu
- 22-0731 Kufunuliwa Kwa Mungu
- 21-0516 Kufunuliwa Kwa Mungu
- TAI WANAKUSANYIKA PAMOJA
- NUKUU YA LEO KWA KISWAHILI
- 19-0630 Kufunuliwa Kwa Mungu
- 19-0623 Kufunuliwa Kwa Mungu
- 16-1127 Kufunuliwa Kwa Mungu
Mpendwa Neno Lililodhihirishwa,
Je, tunaweza kuliwazia hilo! Nguzo ile ile ya Moto iliyowajia wale watu walioiandika Biblia ndio nguzo ile ile ya Moto tunayoisikia kila siku, ikitufasiria siri zote za Biblia: Neno la Mungu lililodhihirishwa!
Mungu alikuwa amejifunika katika manabii Wake ili aweze kuyanena maneno Yake, hilo ndilo Yeye alilolifanya wakati huo, lakini katika siku yetu, William Marrion Branham, Yeye alikuwa ndiye Neno lililo Hai kwa watu, lililofunikwa kwa Nguzo ya Moto.
Ule upako ni mtu. Neno Kristo maana yake ni aliyetiwa mafuta, mnaona, “aliyetiwa mafuta.” Basi, Musa alikuwa ni Kristo katika siku zake, alikuwa ndiye mtiwa mafuta. Yeremia alikuwa ni Kristo katika siku zake, akiwa na sehemu ya Neno kwa siku hizo.
Mungu hujifasiria Neno Lake Mwenyewe; Mungu alilifasiri, Yeye ndiye aliyekuwa na Neno, si kundi, bali William Marrion Branham!
Mungu alimchukua mtu MMOJA, Yeye hawezi kuwachukua watu wawili ama watatu wenye mawazo tofauti, Yeye humchukua mtu MMOJA, naye akawa Neno lililo Hai lililofunuliwa nyuma ya mwili wa mwanadamu.
Hatuko nyuma ya pazia hilo tena, enyi Watoto wadogo. Mungu anaonekana wazi kabisa kwetu. Ule utaji wa kale wa kimadhehebu na wa mapokeo umepasuliwa kutoka kwenye Neno la Mungu, kusudi lipate kudhihirishwa! Katika siku hii ya mwisho, ule utaji wa mapokeo umepasuliwa, na hii hapa imesimama Nguzo Ya Moto. Huyu hapa, akidhihirisha Neno kwa ajili ya siku hii. Pazia limepasuliwa.
Tazameni hizo kanda zinavyofuatana, tazameni kila moja, jinsi imekuja ikiwa dhahiri zaidi na zaidi; kama mna masikio ya kusikia, mnaona, macho ya kuona.
Hilo ndilo linalowapofusha watu leo, wao wanataka kusema kuwa nabii wa Mungu ndiye aliyelileta Neno, Lakini hivi sasa huo upako upo juu ya wengine ili kutuongoza, sio nabii.
Nabii alituambia kuwa Mungu hawezi kulivunja Neno Lake, katika siku za mwisho haina budi kuwa ni jambo lile lile tena, Mungu hawezi kuibadilisha Njia Yake, ama kulibadilisha Neno Lake, Yeye alisema habadiliki. Yeye aliwatuma manabii Wake sio tu kulileta Neno Lake bali kumwongoza Bibi-arusi Wake.
Kama ilivyofanyika katika kila wakati, Uungu ukitiwa utaji katika mwili wa binadamu. Angalieni, Yeye alifanya hivyo. Manabii walikuwa ni Uungu, umetiwa utaji. Walikuwa ni Neno la Mungu (hiyo ni kweli?) lililotiwa utaji katika mwili wa binadamu. Kwa hiyo wala hawakumwona Musa wetu, mnaona, Yesu.
Sasa si Neno tu lililoandikwa kwetu, ni kitu halisi. Tuko ndani Yake. Sasa tunafurahia. Sasa tunamwona Yeye. Sasa tunamwona, lile Neno, akijidhihirisha Mwenyewe.
Ndipo tunakuwa sehemu Yake, utaji unaomficha Yeye. Sisi ni sehemu Yake; mradi Kristo yumo ndani yetu, kama vile Kristo alivyokuwa wa Mungu, sisi tunamfunika Kristo katika hekalu letu la ngozi ya kibinadamu. Sisi ni nyaraka zilizoandikwa. Neno lililoandikwa. Sisi ni Neno lililoandikwa lililodhihirishwa.
Na mnapoliona Neno likidhihirishwa, mnamwona Baba, Mungu, kwa kuwa Neno ni Baba. Neno ni Mungu. Nalo Neno, likidhihirishwa, ni Mungu Mwenyewe akichukua Neno Lake Mwenyewe na kulidhihirisha miongoni mwa waaminio. Hakuna kitu kinachoweza kulifanya liishi ila waaminio, waaminio tu.
Mungu, amefunikwa katika mwili wa mwanadamu, akinena na kutufunulia Neno Lake siku baada ya siku. Mungu katika mwili wa mwanadamu akiishi ndani ya kila mmoja wetu.
Ndugu Joseph Branham
Ujumbe:
(64-0614m Kufunuliwa Kwa Mungu.)
Muda: saa 6:00 MCHANA saa za Jeffersonville( ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ).
Kumbukeni masaa ya kukomboa nyakati za mchana