Category Archives: Uncategorized

25-1012 Kukata Tamaa

UJUMBE: 63-0901E Kukata Tamaa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Kanda,

Sasa, ninyi watu kwenye kanda.

Bwana, tunawezaje kuanza kueleza kile maneno haya madogo sita yanachomaanisha kwetu sisi, Bibi-arusi wa Yesu Kristo? Ndio Ufunuo wa Ujumbe wa saa hii kwetu sisi. Ni Mungu akizungumza kupitia malaika-mjumbe Wake akimwambia Bibi-arusi Wake, “Ninajua mtadumu na Sauti Yangu. Ninajua Neno Langu lililo kwenye kanda hizi vile litakavyomaanisha kwenu. Ninajua mtakuwa na Ufunuo ya kwamba Jumbe hizi nilizozinena kwenye kanda ndio Ishara Yangu ya wakati huu.”

“Nimeiweka Sauti Yangu kwenye kanda hizi za sumaku; kwa maana Jumbe hizi hazina budi kulimalizia Neno lote. Kutakuwako na maelfu mara maelfu ambao wataisikia Sauti Yangu kwenye kanda nao watakuwa na Ufunuo ya kwamba hii ndiyo huduma Yangu. Ndio Roho Mtakatifu wa wakati huu. Ndio Ujumbe Wangu ulio Ishara”

“Nimewatuma wahudumu wengi waaminifu ulimwenguni kote kuitangaza huduma Yangu. Waliporudi, waliniambia, ‘Tumeyatii maagizo Yako kwa kuzicheza kanda Zako. Tumewapata watu walioamini kila Neno. Wamezifanya nyumba zao wenyewe kuwa kanisa kuupokea Ujumbe Wako. Tuliwaambia, wote ambao wangekuja chini ya Ishara Yako, Ujumbe wa saa hii, wangeokolewa.’”

Ni wakati ambapo kila mtu lazima ajichunguze na kujiuliza, Ni ipi njia kamilifu ya Mungu ya siku hii? Neno la nabii halijashindwa hata wakati mmoja. Limethibitishwa kuwa ndiyo Kweli PEKEE, ndicho kitu PEKEE kitakachomuunganisha Bibi-arusi Wake.

Chochote yeye alichokisema kimetukia jinsi vile hasa alivyokisema. Nguzo ya Moto ingali hapa pamoja nasi. Sauti ya Mungu ingali inazungumza nasi kwenye kanda. Nabii amemaliza kutuambia ya kwamba Mungu angepita juu wakati tu atakapoiona ile Ishara. Ni wakati wa kudhikika kwa wote kuingia chini ya Ujumbe huo ulio Ishara.

Tumeuona Mkono mkuu wa Mungu katika wakati huu wa mwisho. Ametupa Ufunuo wa kweli wa Neno Lake nao umekuja chini ya ushahidi wa ile Ishara. Sasa, wakati tuwapo chini ya ushahidi wa ile Ishara, hebu na tukusanyike pamoja na kuula Ushirika kwa kudhikika; kwa maana tunajua kwamba Mungu yuko tayari kutoa hukumu.

Ningependa kuwaalika kila mmoja wenu kusikia na kuwa na Ibada ya Ushirika na Kutawadhana Miguu Miguu Jumapili hii, tunapousikia Ujumbe: Kukata Tamaa 63-0901E.

Ujumbe na Ibada ya Ushirika itakuwa kwenye Redio ya Sauti kuanzia saa 11:00 JIONI. Saa za Jeffersonville. Tafadhali jisikieni huru kuifanya ibada yenu saa 11:00 JIONI. Kwa masaa ya maeneo yenu mkipenda, kama nijuavyo itakuwa vigumu kwa waamini wetu wengi wa nchi za ng’ambo kuianza ibada yenu kwa wakati huo wa huku. Kutakuwa na anuani ya faili la kupakuliwa la ibada.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Kutoka 12:11
Yeremia 29:10-14
Luka 16:16
Yohana 14:23
Wagalatia 5:6
Yakobo 5:16

25-1005 Ile Ishara

UJUMBE: 63-0901M Ile Ishara

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Ile Ishara,

Tunapokutana pamoja, hatuzungumzi tu juu ya Ujumbe, tunakutana pamoja kuipaka ile Damu, kuiweka ile Ishara; nayo ile Ishara ni Ujumbe wa wakati huu! Huo ndio Ujumbe wa majira haya! Huo ndio Ujumbe wa wakati huu.

Tumeiweka hiyo Ishara kwetu sisi wenyewe, kwa nyumba zetu, na kwa familia zetu. Hatuonei haya. Hatujali nani anayeijua. Tunataka kila mtu aijue, kila mpita njia aione na ajue: Sisi ni Watu wa Kanda. Sisi ni Nyumba ya Kanda. Sisi ni Bibi-arusi wa Kanda wa Mungu.

Roho Mtakatifu = Ile Ishara = Ujumbe. Yote ni mamoja. Huwezi kuyatenganisha. Baba, Mwana, Roho Mtakatifu = Bwana Yesu Kristo. Huwezi kuwatenganisha.

Ujumbe = Mjumbe. Haidhuru wakosoaji wanasema nini, NABII ALISEMA, huwezi kuwatenganisha.

Mungu ndiye furaha yako. Mungu ndiye nguvu zako. Kuujua Ujumbe huu, Kujua ndio Kweli pekee, tukijua ndio ile Ishara, huo ndio utoshelevu wetu. Wengine waweza kusema, “Ninauamini, ninauamini, ninauamini kuwa ni Kweli. Ninaukubali kama Kweli.” Hayo yote ni mazuri, lakini hata hivyo haina budi kuwekwa.

Nabii alisema Ujumbe huu ndiyo ile Ishara ya wakati huu. Ujumbe huu ni Roho Mtakatifu. Kama unao Ufunuo wowote wa Ujumbe huu unaweza kuona waziwazi saa tunayoishi. Wengi sana wanasema, “Ninauamini. Mungu alimtuma nabii. Ni Ujumbe wa wakati huu,” lakini wao wanajigamba kwa kusema hawaichezi, na hawataicheza, Sauti yenyewe ya ile Ishara katika makanisa yao.

Mungu hakunena kupitia malaika Wake mwenye nguvu na kusema tu jambo fulani isipokuwa lilikuwa na maana. Alituambia yeye alitufundisha kwa mifano na vivuli. Katika Ujumbe huu, nabii anaeleza kwa kina sana kutuambia kile Rahabu na familia yake walichofanya ili WAOKOLEWE, kuwa Bibi-arusi. Alikuwa wazi juu ya kile yeye alichofanya.

Wakati wavulana wa kanda walipocheza “KANDA”…Hebu kidogo, mjumbe huyo alifanya nini? Alicheza Kanda. Kisha Rahabu akafanya nini? Aliifanya nyumba yake kuwa KANISA LA KANDA. Hakuonea haya kusema, “Mnaiona ile kamba nyekundu, hiyo inamaanisha kwamba mimi ni KANISA LA KANDA”.

Unadhani kama angalisema, “Ndiyo, ninamwamini mjumbe na Ujumbe, lakini sisi hatuzichezi Kanda tena kanisani mwetu. Ninaye mchungaji anayesema HAPANA, yeye anapaswa tu kuhubiri na kuyanukuu yale Kanda zinachosema.” Hivi unafikiri angeokolewa…???

Akaweka ile ishara, nayo nyumba yake ikaokolewa, ama angaliangamia kule chini alikokuwa.

Umewasikia wahudumu wengi wakitoa visingizio kuhusu kuzicheza kanda, lakini wengi wao husema: “Nabii hakusema kamwe kuzicheza kanda kanisani.”

Nabii alisema Rahabu aliifanya nyumba yake kuwa kanisa, nalo kanisa lake lilizicheza Kanda. Na kwa sababu alizicheza Kanda kanisani mwake, yeye, na Kanisa lake lote la KANDA, walikuwa chini ya ile Ishara na wakaokolewa. Kila kanisa lingine liliangamia.

Ndugu na dada, tafadhali, sisemi mchungaji hawezi kuuhubiri Ujumbe huu, au ni makosa kama anahubiri. Kwa njia yangu mwenyewe, ninahubiri sasa hivi kupitia barua hii, lakini ufungue moyo wako na usikilize kile nabii asemacho na kukuonya. Kama mchungaji wako hachezi, au hatazicheza, kanda kanisani mwenu kwa kutoa udhuru fulani; chochote kile, kulingana na Neno, haidhuru anasema vipi, ninauamini Ujumbe wa wakati huu, kulingana na kile ninachoamini Neno lisemavyo, ile Ishara, Ujumbe wa saa hii, haijawekwa.

Jumapili hii, ninawaalika mje msikilize pamoja na Maskani ya Branham saa 06:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) Ujumbe: Ile Ishara 63-0901M. Ikiwa hamwezi kuungana nasi, chezeni Ujumbe wowote wa Ile Ishara, na muiweke.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Mwanzo 4:10
Kutoka sura ya 12
Yoshua sura ya 12
Matendo 16:31 / 19:1-7
Warumi 8:1
1 Wakorintho 12:13
Waefeso 2:12 / 4:30
Waebrania 6:4 / 9:11-14 / 10:26-29 / 11:37 / 12:24 / 13:8, 10-20
Yohana 14:12

25-0928 Wakati Wa Kuungana Na Ishara Yake

UJUMBE: 63-0818 Wakati Wa Kuungana Na Ishara Yake

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliyeungana,

Nimechangamshwa sana, na niko chini ya matarajio makubwa ya aina yake, kuwa sehemu ya yote Mungu anayofanya katika siku yetu.  Mawazo ya Mungu ya huko mwanzo sasa yanatimizwa mbele ya macho yetu, na sisi tu sehemu ya hilo.

Kote katika Biblia, manabii walitabiri na kunena yale ambayo yangetukia.  Wakati fulani unabii huo haukutimia kwa mamia ya miaka baadaye, lakini wakati utimilifu wa wakati ulipowadia, ulitimia;  kwa maana mawazo ya Mungu yaliyonenwa kwa kinywa cha nabii Wake LAZIMA yatimie.

Nabii Isaya alisema, “Bikira atachukua mimba”.  Kila familia ya Kiebrania ilimtayarisha binti yao mdogo kumpata mtoto huyu.  Walinunua viatu na vibuti, na nguo ndogo za kichanga, nao wakajitayarisha kwa ajili ya mtoto huyo kuwasili.  Vizazi vilipita, lakini hatimaye Neno la Mungu lilitimia.

Nilipokuwa mvulana mdogo nilishangaa daima, Bwana, naona katika Neno Lako kwamba Wewe daima umewaunganisha watu Wako pamoja ili kulitimiza Neno Lako.  Uliwaunganisha watoto Wako wa Kiebrania kupitia mtu mmoja, Musa, ambaye aliwaongoza kwa Nguzo ya Moto kwenda Nchi ya Ahadi.

Ulipofanyika mwili na kukaa hapa duniani, Wewe uliwaunganisha wanafunzi Wako.  Uliwatenga na kila kitu na kila mtu ili uwafunulie Neno Lako.  Siku ya Pentekoste, kwa mara nyingine tena ulilikusanya Kanisa Lako mahali pamoja, kwa nia moja kwa umoja kabla hujaja na kuwapa Roho Wako Mtakatifu.

Nikawaza, hilo litawezekanaje leo Bwana?  Bibi-arusi Wako ametawanyika kote ulimwenguni.  Je! Bibi-arusi wote watakuja Jeffersonville?  Sijaona hilo likitendeka Bwana.  Lakini BWANA, Wewe kamwe haubadilishi mpango Wako.  Ni Sheria Yako, hakuna njia ya kulizuia hilo.  Utalifanyaje?

UTUKUFU…LEO, tunaweza kuona kwa macho yetu wenyewe, na muhimu zaidi, KUWA SEHEMU YAKE: Neno la Milele la Mungu likitimizwa.  HATUKO KIMWILI mahali pamoja, tumetawanyika ulimwenguni kote, lakini Roho Mtakatifu SASA AMEMUUNGANISHA BIBI-ARUSI WAKE KWA SAUTI YA MUNGU.  NENO LAKE LILILONENWA NA KUREKODIWA KWENYE KANDA, Yakini ya Mungu ya siku hii, inamkusanya na KUMUUNGANISHA BIBI-ARUSI WAKE… NA HAKUNA LOLOTE LINALOWEZA KULIZUIA HILO.

Mungu anamuunganisha Bibi-arusi Wake. Anakusanyika pamoja, kutoka Mashariki na Magharibi, na Kaskazini na Kusini. Kuna wakati wa kuungana, na huo unaendelea sasa hivi. Anaungana kwa sababu gani? Unyakuo. Amina!

Wakati wa kuungana unafanyika SASA HIVI!!!   Ni kitu gani kinachotuunganisha?  Roho Mtakatifu kwa Neno Lake, Sauti Yake.  Tunaungana kwa sababu gani?  UNYAKUO!!!  Nasi tunakwenda sote na hatuachi hata MMOJA nyuma.

Mungu anamtayarisha. Naam bwana, kuungana! Anaungana na kitu gani? Na Neno!

Neno la siku yetu ni lipi?  UJUMBE Huu, SAUTI YAKE, Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi Wake.  Sio mtu.  Sio watu.   Sio kundi. Ni SAUTI ya Mungu iliyo kwenye kanda Iliyothibitishwa, kwa Nguzo ya Moto.

“Kwa maana mbingu zote na nchi zitapita, bali Neno Langu halitapita kamwe.” Anajiunganisha Mwenyewe na BWANA ASEMA HIVI haidhuru madhehebu yoyote ama mtu yeyote mwingine anasema nini.

Haidhuru MTU YEYOTE anasema nini, sisi tunajiunganisha na Sauti ya Bwana Asema Hivi iliyohakikishwa, iliyothibitishwa ya siku yetu.  Sio fasiri ya mtu fulani;  kwa nini tufanye hivyo?  Hiyo hubadilika kwa kila mtu, lakini Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda HAIBADILIKI KAMWE nayo Imetangazwa na Nguzo ya Moto Yenyewe kuwa Neno la Mungu na Sauti ya Mungu.

Shida yake ni kwamba, kwa binadamu, yeye hamjui kiongozi wake. Naam, bwana. Watakusanyika chini ya dhehebu fulani, watakusanyika chini ya askofu ama mtu fulani, bali hawatakusanyika chini ya yule Kiongozi, Roho Mtakatifu katika Neno. Unaona? Wao wanasema, “Loo, vema, nahofu nitakuwa kidogo mshupavu wa dini; ninahofu nitaelekea kubaya.” Loooo, haya basi!

Hapa ndipo wakosoaji wanapoelekezea makutano yao na kusema, “Ona, wanamwinua mtu, Ndugu Branham. Wao ni waabudu mungu-mtu nao wanakusanyika chini yake, mtu huyo, si Roho Mtakatifu.”

Upuuzi, sisi tunaungana chini ya SAUTI YA MUNGU ILIYOTHIBITISHWA ILIYONENWA KUPITIA MTU HUYO.  Kumbukeni, huyo ndiye mtu ambaye Mungu alimchagua kuwa Sauti Yake kumwita atoke na kumwongoza Bibi-arusi Wake katika siku hii.  Hiyo ndiyo Sauti PEKEE iliyothibitishwa na Mungu Mwenyewe.  Lakini kinyume chake, WAO wanaungana chini ya WANADAMU.  HAWATA icheza Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda katika makanisa yao.  Unaweza kuliwazia hilo???  Mhudumu anayedai kuuamini Ujumbe huu kuwa ndio Ujumbe wa wakati huu, Bwana Asema hivi, lakini anatafuta aina fulani ya kisingizio cha KUTO icheza Sauti hiyo makanisani mwao, bali kuwahudumia watu LAZIMA wawasikilize wao na wahudumu wengine wakihubiri Neno… kisha wao wanasema ati sisi tunamfuata mtu!!!

Tumetoka kusikia jumapili iliyopita kile Mungu alichowafanya watu hao!!

Tunajiandaa kufanya Harusi.  Tunafanyika Mmoja na Yeye.  Neno linakuwa wewe, na wewe unakuwa Neno.  Yesu alisema, “Katika siku ile mtaijua. Yote aliyo Baba, ndivyo nilivyo Mimi; na yote niliyo Mimi, ndivyo mlivyo ninyi; na yote mliyo ninyi, ndivyo nilivyo Mimi. Katika siku hiyo mtajua ya kwamba Mimi niko ndani ya Baba Yangu, Baba ndani Yangu, Mimi ndani yenu, nanyi ndani Yangu.”

Asante Bwana kwa Ufunuo wa Wewe Mwenyewe, na wa sisi wenyewe, katika siku yetu.  Bibi-arusi Wako anajiweka mwenyewe tayari kwa Neno Lako Lililonenwa.  Tunajua tuko katika Mapenzi Yako makamilifu kwa sisi kukaa na Neno Lako lililorekodiwa.

Ninaualika ulimwengu kuisikiliza Sauti pekee ya Mungu iliyothibitishwa ya siku yetu Jumapili hii.  Mnakaribishwa muungane nasi Jumapili saa 06:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia: 63-0818, Wakati Wa Kuungana Na Ishara Yake. Ikiwa hamuwezi kujiunganisha kwa simu na kusikiliza pamoja nasi, chagueni kanda, KANDA YOYOTE;  zote ni Bwana Asema Hivi, na msikilize Neno la Mungu liwakamilishe na kuwafanya tayari kwa ajili ya ujio Wake uliyokaribu.

 Ndugu.  Joseph Branham

 Zaburi 86:1-11
 Mathayo 16:1-3

Anajiunganisha Mwenyewe. Anajitayarisha. Kwa nini? Yeye ni Bibi-arusi. Hiyo ni kweli. Naye amejiunganisha pamoja na Bwana Arusi Wake, unaona, na Bwana Arusi ni Neno. “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Naye Neno alifanyika mwili akakaa kwetu.”

25-0921 Lile Shtaka

UJUMBE: 63-0707M Lile Shtaka

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Walioachiwa Huru,  

Sasa, Hapo “wao,” sio wenye dhambi, “Wao,” hao ni, kanisa la siku hiyo, walimwonea makosa yule Mtu aliyekuwa ndiye lile Neno. Sivyo? Walimwonea makosa yule Mtu aliyekuwa lile Neno. Sasa wao hulionea makosa lile Neno likitenda kazi kupitia kwa mtu.

Tangu mwanzo ulimwengu umemtupilia Yeye mbali, umemkataa, umekataa kudumu na Neno Lake kwa kuyashika mapokeo yao, kanuni zao za imani, mawazo yao.  Daima wao wameukosa mpango wa Mungu; Mungu, kama Mtu, ambaye alikuwa Neno, na sasa Neno likifanya kazi kupitia huyo mtu.

Lakini katika siku yetu Yeye alisema, “Nitakuwa na kundi dogo, wateule wachache. Wao walikuwa ndani Yangu tangu mwanzo. Watanipokea Mimi na kuliamini Neno Langu na yule mtu Niliyemchagua kulifunua Neno Langu.  Yeye atakuwa Sauti Yangu kwao.” 

“Wao hawataonea haya kuitangaza Sauti Yangu. Hawataonea haya kuuambia ulimwengu kwamba Mimi nimekuja tena na Nimejidhihirisha Mwenyewe kupitia mwili wa mwanadamu kama nilivyosema Ningefanya. Wakati huu wao hawatamwabudu huyo mtu, lakini wataniabudu Mimi, Neno, litakalonena kupitia mtu huyo. Wao watanipenda Mimi na kunitangaza Mimi kwa kila mshipa wa utu wao.”

“Kwa hivyo, Nimewapa yote wanayohitaji kufanyika Bibi-arusi Wangu. Nimewaimarisha kwa Neno Langu; kwa maana wao NI NENO LANGU lililofanyika mwili. Ikiwa wanahitaji uponyaji, wao hulinena Neno Langu. Ikiwa wana kizuizi chochote kinachowazuia, wao hulinena Neno Langu. Ikiwa wanaye mtoto ambaye amekengeuka, wao hulinena Neno Langu. Chochote kile wanachohitaji, wao hulinena Neno Langu, kwa kuwa wao ni Neno Langu lililofanyika mwili ndani yao.”

“Wanajijua wao ni nani, kwa kuwa Mimi nimejifunua Mwenyewe kwao. Wamedumu wa kweli na waaminifu kwa Neno Langu nao wanaungana pamoja kwenye Sauti Yangu. Kwa maana wanaijua Sauti Yangu, Neno Langu, Roho Wangu Mtakatifu. Wanajua, pale Neno lilipo ndipo Tai watakapokusanyika.”

Wakati nabii Wake alinenapo Neno Lake na kukishtaki kizazi hiki kwa kumsulubisha Yesu Kristo mara ya pili na kuwatangaza kuwa wameangamia, Bibi-arusi atakuwa akifurahi.  Kwa maana tunajua SISI NDIYE Bibi-arusi Wake ambaye amelikubali na kulipokea Neno Lake. Tunapaza sauti kutoka ndani ya mioyo yetu na kusema: 

Mimi ni Wako, Bwana. Najilaza mwenyewe kwenye madhabahu haya, kwa kujitakasa kama tu nijuavyo kujitendea mwenyewe. Ondosha ulimwengu ndani yangu, Bwana. Yaondoe mambo yaharibikayo kwangu; nipe mambo yasiyoharibika: Neno la Mungu. Na niweze kuishi karibu sana na hilo Neno, hata lile Neno liwe ndani yangu na mimi ndani yake. Nijalie, Bwana. Nisiondoke kwalo kamwe.

Kuna uzima, na kuna mauti. Kuna njia sahihi, na kuna njia mbaya. Kuna ukweli, na kuna uongo. Ujumbe huu, Sauti hii, ndio njia kamilifu iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku hii. Njoo uuungane na sehemu ya Bibi-arusi mkuu wa Mungu tunapokusanyika kulizunguka Neno Lake lililofunuliwa na kuusikia Ujumbe:  Lile Shtaka 63-0707M.

Ndugu. Joseph Branham

25-0914 Je, Maisha Yako Yanaistahili Injili?

UJUMBE: 63-0630E Je! Maisha Yako Yanaistahili Injili?

PDF

BranhamTabernacle.org

Ndugu na Dada Wapendwa,

Ninampenda Bwana, Neno la Mungu, Ujumbe huu, Sauti Yake, nabii Wake, Bibi-arusi Wake, zaidi ya uhai wenyewe. Wote ni KITU KIMOJA KWANGU MIMI. Sitaki kamwe kupatana kwenye yodi moja, nukta moja ndogo, ama NENO MOJA ambalo Mungu aliloandika katika Neno Lake ama alilolinena kupitia nabii Wake. Kwangu mimi, Yote ni Bwana Asema Hivi.

Mungu aliliwaza, kisha akalinena kwa manabii Wake, nao wakaliandika Neno Lake. Ndipo akamtuma malaika Wake mwenye nguvu, William Marrion Branham, duniani katika siku yetu ili Yeye aweze kujifunua Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu kwa mara nyingine tena, kama alivyofanya kwa Ibrahimu. Kisha Yeye akanena kupitia nabii Wake awe Sauti ya Mungu kwa ulimwengu, kufunua na kuzifasiri siri zote ambazo zimefichwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu kwa Bibi-arusi Wake aliyechaguliwa tangu zamani.

Sasa, Bibi-arusi Wake, NINYI, mnakuwa Neno lililofanyika mwili; Mmoja na Yeye, Bibi-arusi Neno Wake aliyerejeshwa kikamilifu.

Najua ninaeleweka vibaya kwa kile ninachosema na ninachoandika. Naomba niseme kwa unyenyekevu kama nabii wetu alivyosema, mimi sina elimu nami najua siwezi kuandika ama kuzungumza kwa usahihi kile ninachojisikia moyoni mwangu. Ninakubali inaonekana kama ninaandika kwa ukali sana wakati mwingine. Ninapofanya hivyo, sio kuonyesha kutoheshimu, au kuwa na mtazamo mbaya ama kumhukumu mtu fulani, bali kinyume chake. Ninafanya hivyo kwa upendo ulio moyoni mwangu kwa Neno la Mungu.

Ninataka kila mtu aukubali na kuuamini Ujumbe huu Mungu alioutuma kumwita Bibi-arusi Wake atoke. Sijawahi kamwe kuhisi moyoni mwangu au akilini kwamba wahudumu hawapaswi kuhubiri tena; ingekuwa ni kwenda kinyume na Neno la Mungu. Mimi nina bidii tu kwa ajili ya Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. Ninaamini ndiyo Sauti muhimu sana WAHUDUMU WOTE wanayopaswa kuiweka Kuwa ya KWANZA mbele ya watu. Hii haimaanishi kuwa hawawezi kuhubiri, nataka tu kuwatia moyo kuzicheza kanda katika makanisa yao wakati watu wamekusanyika chini ya upako huo.

Ndiyo, ningependa kuufanya ulimwengu mzima usikilize Ujumbe ule ule kwa wakati mmoja ulimwenguni kote. Si kwa sababu “Mimi” nilisema hivyo, au kwa sababu “Mimi” niliichagua kanda ya kusikiliza, bali ninahisi hakika Bibi-arusi angeona Jinsi gani Mungu ameifanya njia kwa jambo hili kutendeka katika siku yetu.

Kama tungekuwa na rekodi za Yesu akinena leo kwenye kanda, si maandishi ya Mathayo, Marko, Luka au ya Yohana ya yale Yesu aliyosema (kwa maana wote walilisema tofauti kidogo), bali tungeweza kuisikia Sauti ya Yesu, utu Wake, aiko, pepa, na dafuta Zake kwa masikio yetu wenyewe, je! wahudumu leo wangeliambia kanisa lao, “Hatutaicheza rekodi ya Yesu kanisani mwetu. Mimi nimeitwa na nimepakwa mafuta kuihubiri na kuinukuu. Ninyi isikilizeni mwendapo nyumbani.” Je! watu wangelisimamia hilo? Inasikitisha kusema hivyo, lakini hivyo ndivyo wao wanavyofanya leo hii. HAKUNA TOFAUTI, haijalishi jinsi gani wanavyolipaka chokaa.

Kwangu mimi, Ndugu Branham alitupa kielelezo. Alipenda wakati makanisa yote, majumba, au popote pale walipokuwa, walipokuwa kwenye muunganisho wa simu ili waweze kuusikia Ujumbe wote kwa wakati mmoja. Yeye alijua wangeweza, na wangezipata, kanda na kuisikiliza baadaye, lakini yeye aliwataka waungane na kuusikia Ujumbe wote kwa wakati mmoja….KWANGU MIMI HUYO ALIKUWA NI MUNGU AKIMUONYESHA BIBI-ARUSI WAKE NINI KITATOKEA KATIKA SIKU YETU NA KIPI CHA KUFANYA.

Kila mhudumu mwaminio wa kweli wa Ujumbe atakubali hakuna kitu kilicho kikuu zaidi ya kukaa chini ya upako wa Sauti ya Mungu, ambayo imerekodiwa na kuwekwa kwenye kanda. Bibi-arusi ataamini, na kuwa na Ufunuo, ya kwamba Ujumbe huu ndilo Neno la Mungu la wakati huu. Ninaweza tu kuhukumu kwa Neno, lakini mtu ye yote ambaye hangesema Ujumbe huu ndiyo Yakini yao, hana Ufunuo wa Neno la wakati huu, kwa hivyo, wangewezaje kuwa Bibi-arusi Wake?

Siyo tu kulinukuu, kulihubiri au kulifundisha, bali kulisikia kwenye kanda ndipo MAHALI PEKEE ambapo Bibi-arusi anaweza kusema ninaliamini kila Neno. Ujumbe huu ni Bwana Asema Hivi. Kile ninachohubiri au ninachofundisha si Bwana Asema Hivi, bali yale Sauti ya Mungu isemayo kwenye kanda NDIYO…hiyo ndiyo Sauti PEKEE iliyothibitishwa na Nguzo ya Moto.

Ninajua kuna ndugu na dada wanaosema, na kuhisi, ati “Kama hamsikilizi Ujumbe ambao Maskani ya Branham inaoutuma, hamzisomi barua za Tai Wanakusanyika, na kusikiliza majumbani mwenu wakati ule ule wewe si Bibi-arusi,” ama, “Ni makosa kwenda kanisani, inakubidi ukae nyumbani kwako.” HILO NI KOSA SANA. Sijawahi KAMWE kuwaza hivyo, kusema hivyo, ama kuamini hivyo. Hilo limesababisha utengano hata na zaidi, fikra ngumu, na kuondoa ushirika miongoni mwa Bibi-arusi naye adui anatumia jambo hilo kuwatenganisha watu.

Sitaki kamwe kumtenganisha Bibi-arusi, nataka kumuunganisha Bibi-arusi kama vile Neno lilivyosema LAZIMA TUUNGANE TUWE KITU KIMOJA. Hatupaswi kubishana sisi kwa sisi, lakini hakuna kabisa kitu kingine chochote kile kinachoweza kutuunganisha ila Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.

Hatupaswi kuzozana na kuwaambia watu WANAPASWA WAFANYE nini la sivyo wao sio Bibi-arusi, ninyi fanyeni jinsi BWANA ANAVYOWAONGOZA. Wao bado ni ndugu na dada zetu. Tunahitaji kupendana na kuheshimiana mmoja kwa mwingine.

Sasa, usibishane. Unaona? Hasira huzaa hasira. Muda si muda wajua, unamhuzunisha Roho Mtakatifu anakuacha, utarudisha ubishi tena. Ndipo Roho Mtakatifu anaruka anaenda zake. Hasira huzaa hasira.

Kwa kile nabii alichosema hapa, sitaki kamwe kumhuzunisha Roho Mtakatifu. Sitaki kubishana kamwe. Tunaweza kusemezana kwa upendo, lakini si kubishana. Ikiwa nimesema jambo lolote ambalo limemuudhi yeyote katika yale niliyoyaandika ama kusema, tafadhali nisamehe, haikuwa kusudi langu.

Kama nilivyoeleza hapo awali, ninauhisi wito maishani mwangu kutoka kwa Bwana kuwaelekeza watu kwenye Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku hii. Wahudumu wengine wana miito mingine na pengine wanaona mambo tofauti, Bwana asifiwe, wanafanya kile WAO wanachojisikia wanaongozwa na Roho Mtakatifu. Huduma yangu ni kumwambia tu Bibi-arusi, “BONYEZA PLAY” na “Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda ndiyo Sauti iliyo muhimu zaidi mnayoweza kuisikia.” “Ninaamini kwamba wahudumu wanapaswa kuicheza Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda katika makanisa yao.”

Barua ninazoziandika kila wiki ni za sehemu ya Bibi-arusi wale wanaojisikia kuwa ni sehemu ya Maskani ya Branham. Najua wengine wengi huzisoma, Lakini mimi ninawajibika tu kufanya vile ninavyojisikia kuongozwa kwa ajili ya kanisa letu. Kila kanisa linajitawala lenyewe; hawanabudi kufanya vile wanavyojisikia wanaongozwa na Bwana kufanya, hilo ni Neno 100%. Mimi siwapingi wao, tunatofautiana tu. Mimi na Maskani ya Branham, tunataka tu kuisikia Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.

Ninaualika ulimwengu kuungana nasi kila wiki. Ninawatia moyo ikiwa hawawezi kuungana nasi, wachague kanda, kanda yoyote, na kubonyeza play. Watatiwa mafuta kuliko hapo kabla. Hivyo, ninawaalika wiki hii muungane nasi Jumapili saa 06:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapoungana pamoja na kusikia, 63-0630E Je! Maisha Yako Yanaistahili Injili?

Ndugu Joseph Branham

25-0907 Kutoka Kwa Tatu

UJUME: 63-0630M Kutoka Kwa Tatu

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Kutoka Kwa Tatu,

Ikiwa huna jicho la kiroho, hulipati. Lakini jicho la kiroho linaweza kuona Nguvu za Mungu zikitenda kazi maana hilo liko kwenye Neno kikamilifu. Ni Neno, nalo Neno la Mungu halibadiliki kamwe. Kile Yeye alichokifanya hapo mwanzo, anafanya vivyo hivyo sasa nalo jicho la kiroho linaliona, linaliamini, na KULISIKIA.

Ulimwengu unaweza kutokukubaliana nami katika kile ninachoamini kuwa ndiyo njia ya Mungu iliyoandaliwa Kwa ajili ya wakati huu: Sauti iliyo muhimu sana unayopaswa kuisikia ni Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. Ni lazima mzicheze kanda makanisani mwenu, lakini KAMA kweli mnauamini Ujumbe huu, basi hamwezi kupingana na kile nabii wa Mungu anachosema.

Jumapili hii tutakusanyika kama wale wana wa Kiebrania walivyofanya ili kuipata mana ile iliyokuwa imeandaliwa kwa ajili yao usiku kucha, ambayo ingewahifadhi siku inayofuata. Sisi tutakusanyika kwa ajili ya Mana yetu ya Kiroho itakayotutia nguvu kwa ajili ya kule Kutoka kwetu kukuu kunakokuja hivi karibuni.

Hakuna njia bora zaidi kuliko kumruhusu Sauti ya Mungu yeye aliseme hilo Mwenyewe, kumhusu yeye Mwenyewe, nao Ujumbe huu tunaoenda kuusikia UMESHEHENI!

Mungu alimpeleka mtu mmoja nyikani, akamfunza. Kisha akamrudisha, na kukipeleka kitu hicho huko, kisha akawatoa hao watu. Mnaona ninalomaanisha? Yeye hawezi kubadilisha mpango Wake. Yeye ni Mungu.

Kwa hivyo hapa Yeye anatuambia waziwazi Yeye kamwe habadilishi mpango Wake. Kile Yeye alichokifanya tangu mwanzo, atakifanya tena mwishoni, Yeye aliahidi. Kwa hiyo sasa ni lazima tujue Mpango Wake ulikuwa nini wakati ule kwani utakuwa ni Mpango ule ule hivi sasa.

Kamwe hatashughulika na kundi. Kamwe hajafanya hivyo. Yeye hushughulika na mtu mmoja; na alifanya hivyo, na atafanya hivyo. Na aliahidi, hata katika Malaki 4, angefanya hivyo.

Yeye kamwe hashughuliki na kundi. Kwa hivyo, Yeye aliahidi katika wakati wetu kwamba angemtuma mtu Mmoja, Malaki 4, akiwa na Bwana Asema Hivi.

Hiyo ni kweli. Kwa hiyo kuna ahadi Yake, kwamba Yeye alikuwa ni nani; ahadi ya kile alichosema Yeye angekifanya, na basi tumewasili. Tunapaswa kuwa ni watu wenye furaha jinsi gani; akiwapa ishara, kwa ishara ya Neno Lake lililoahidiwa, Neno lililoahidiwa. Aliahidi angefanya hivyo.

Mungu alichagua kumwongoza Bibi-arusi Wake namna gani wakati ule?

Mungu alichagua, katika siku za kule kutoka, Yeye aliliita kundi moja litoke. Na kutoka kwenye kundi hilo, ninawataka muone jambo fulani, Yeye alipata tu wawili walioingia kwenye nchi ya ahadi. Yeye alichagua kuwatoa kwa kutumia nini?

Hili hapa. Hili ni muhimu sana kwa wenye nia ya kiroho kuweza kulishika. Mungu alichagua kumwongoza na kumpeleka Bibi-arusi kwenye Nchi ya Ahadi namna gani?

Siasa? dhehebu? Yeye alichagua nabii, akiwa na ishara ya kimbinguni ya Nguzo ya Moto, watu wasije wakakosea. Yale nabii aliyosema yalikuwa ni Kweli. Na Mungu alishuka, Nguzo ya Moto, na kujithibitisha Mwenyewe, akaonyesha Neno Lake. Hiyo ni kweli? Hiyo ndiyo aliyoileta, kutoka Kwake kwa kwanza. Kutoka Kwake kwa pili…

Kwa hiyo, ili kuhakikisha kwamba watu hawangekosea, Yeye aliwatumia nabii akiwa na ishara ya kimbinguni ya Nguzo ya Moto kwa ajili ya kule kutoka kwao kukuu.

Yeye alifanya nini, kule kutoka kwa kwanza? Alimtuma nabii, aliyetiwa mafuta kwa Nguzo ya Moto, naye akawaita watu wakatoka. Huko kulikuwa ni kutoka Kwake kwa kwanza…

Kutoka kwa pili, Yeye alimleta Nabii, aliyetiwa mafuta, ambaye alikuwa ni Mwanawe, Mungu-Nabii. Musa alisema Yeye angekuwa ni Nabii; Naye alikuwa na Nguzo ya Moto, na akafanya ishara na maajabu…

Na hapa Yeye aliahidi jambo lile lile katika kule kutoka katika siku za mwisho, wala hawezi kulibadili…

Wengi watakubali kwa kusema, naam, Yeye alimtuma nabii kumwita Bibi-arusi atoke, lakini sasa hivi Roho Mtakatifu Yeye atamwongoza Bibi-arusi kupitia wahudumu; lakini Yeye hakusema hivyo…hebu na tuendelee kusoma.

Angalieni ile Nguzo ya Moto iliyowaita watoke, ikawaongoza kwenye nchi ya ahadi, chini ya upako wa nabii. Nguzo ya Moto ambayo wangeweza kuiangalia, iliwaongoza kwenye nchi ya ahadi, chini ya nabii aliyetiwa mafuta. Nao daima walimkataa. Hiyo ni kweli? Hakika.

Nguzo ii hii ya Moto inawaongoza watu tena kwenye Nchi ya ahadi, ule Utawala wa Miaka Elfu.

Ile Nguzo ya Moto, chini ya uongozi wa Mungu…Mungu alikuwa ni ule Moto, na ile Nguzo ya Moto ilimtia mafuta tu yule nabii. Ile Nguzo ya Moto ilikuwa isimame kama ushahidi wa Mbinguni kwamba Musa alikuwa ameitwa atoke.

Sasa, kumbukeni, Musa hakuwa hiyo Nguzo ya Moto. Yeye alikuwa ni kiongozi aliyetiwa mafuta, chini ya hiyo Nguzo ya Moto, na hiyo Nguzo ya Moto iliuthibitisha tu Ujumbe wake kwa ishara na maajabu.

Hakuna kosa, enyi marafiki. Si yale ninayosema mimi; mimi ni ndugu yenu tu. Lakini, ni yale Mungu anayowathibitishia, ndiyo yanayolifanya Kweli. Nguzo ile ile ya Moto aliyoitumia kwenye kule kwingine kuwili, Yeye ameileta miongoni mwenu leo, na kuithibitisha kisayansi.

Mungu kamwe habadilishi mpango Wake. Mungu anayo njia iliyoandaliwa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake leo: ile Nguzo ya Moto, chini ya uongozi wa Mungu… Mungu alikuwa ni ule Moto, na ile Nguzo ya Moto ilimtia mafuta tu nabii.

Kuna Sauti moja tu, nabii mmoja, aliye na Bwana Asema Hivi, William Marrion Branham. Yeye si ile Nguzo ya Moto, bali yeye ni kiongozi aliyetiwa mafuta chini ya hiyo Nguzo ya Moto.

Sote tunataka kuwa katika Mapenzi MAKAMILIFU ya Mungu. Neno Lake NDIYO mapenzi Yake Makamilifu. Neno lililothibitishwa la wakati wetu ni Ujumbe huu. Nabii Wake ndiye aliyechaguliwa kumwongoza Bibi-arusi Wake. Kama huliamini hilo, huwezi kuwa Bibi-arusi Wake.

Njooni mjiandae kwa ajili ya kule Kutoka kwetu kuu kwa kulisikia Neno Kamilifu la Mungu pamoja nasi Jumapili saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia: Kutoka Kwa Tatu 63-0630M.

Ndugu. Joseph Branham

25-0831 Mbona Unalialia? Nena!

UJUMBE: 63-0714M Mbona Unalialia? Nena!

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Kanisa la Mungu,

Mungu alinena na kusema, ““Mimi sitendi kazi duniani ila kupitia tu kwa mwanadamu. Mimi-Mimi- Mimi ndimi Mzabibu; nanyi ni matawi, na Mimi nitajijulisha Mweyewe tu ninapoweza kumpata mtu MMOJA, na Mimi nimemchagua yeye, William Marrion Branham. Mimi nimemtuma aje akamtoe Bibi-arusi Wangu. Nitaliweka Neno Langu kinywani mwake. Neno Langu litakuwa Neno Lake. Yeye atalinena tu Neno Langu na kusema tu yale Mimi nisemayo.”

Sauti ya Maandiko ilinena kupitia Nguzo ya Moto na kumwambia yeye, “Nimekuchagua wewe, William Branham. Wewe ndiye mtu huyo. Nilikuinua wewe kwa kusudi hili. Nitakuthibitisha kwa ishara na maajabu. Unashuka chini kule kulifunua Neno Langu na kumwongoza Bibi-arusi Wangu. Neno Langu halina budi kutimizwa na WEWE.”

Nabii wetu alikuwa anajua yeye alikuwa ametumwa kwa kusudi hilo hasa la kuzifunua siri zote za Biblia na kumwongoza Bibi-arusi wa Mungu kwenda Nchi ya Ahadi. Yeye alijua kile alichosema, Mungu angekiheshimu na kukitimiza. Nawatakeni msilisahau kamwe Neno hilo. Kile alichokisema nabii wetu, Mungu atakiheshimu, kwa maana Neno la Mungu lilikuwa ndani ya William Marrion Branham. Yeye ni Sauti ya Mungu kwa ulimwengu.

Yeye alijua alikuwa ndiye malaika-mjumbe wa saba wa Mungu aliyetiwa mafuta. Yeye alijua moyoni mwake mambo yote ambayo Mungu aliyokuwa ameyasema kumhusu yeye katika Neno Lake. Kile kilichokuwa kinawaka moyoni mwake kikawa halisi. Yeye alikuwa ametiwa mafuta na alijua alikuwa na BWANA ASEMA HIVI. Hakukuwa na kitu kingalimzuia yeye kutokwenda kulinena Neno la Mungu.

Mungu alimwambia yeye, “Neno Langu, na wewe, mjumbe Wangu, ni kitu kimoja.” Alijua yeye ndiye aliyechaguliwa kulinena Neno lisilokosea. Hilo ndilo tu yeye alilohitaji. Angeweza KUNENA, NAYE MUNGU ANGELITIMIZA.

Ufunuo wa Ujumbe huu NA mjumbe wa Mungu vimeitia mafuta imani yetu zaidi ya hapo awali. Imetupeleka katika miduara mikubwa. Hilo limetutenga na kila kitu isipokuwa Ujumbe Wake, Neno Lake, Sauti Yake, Kanda Zake.

Haijalishi sisi ni wachache jinsi gani, jinsi gani tunavyochekwa, jinsi tunavyodhihakiwa, haileti tofauti hata kidogo. SISI TUNALIONA. SISI TUNALIAMINI. Kuna kitu fulani ndani yetu. Tulichaguliwa tangu awali kuliona HILO na hakuna kitu kitakachotuzuia sisi tusiliamini HILO.

Tunakumbuka kile lile ono lilichosema, “rudi ukakihifadhi Chakula”. Hilo ghala lilikuwa wapi? Maskani ya Branham. Ni mahali gani nchini, ama ulimwenguni mahali popote, pangelinganishwa na Jumbe tulizo nazo? NDIYO Sauti pekee iliyothibitishwa na Mungu Mwenyewe kuwa Bwana Asema Hivi. SAUTI PEKEE!

Ni wapi pengine tungeweza, au tungetaka kwenda, wakati yeye alisema;

Hapa ndipo chakula kimehifadhiwa…

Umehifadhiwa hapa. Uko kwenye kanda; utaenda ulimwengu mzima katika kanda ambapo watu manyumbani mwao. Hizo kanda zitaangukia mikononi mwa wale waliochaguliwa tangu awali wa Mungu. Yeye anaweza kuliongoza Neno; yeye ataelekeza kila kitu kuelekea njia yake hasa. Hiyo ndiyo sababu Yeye alinituma nirudi nikafanye hivi. “Kihifadhi chakula hapa.”

Sisi ni Bibi-arusi Neno Wake Mkamilifu ambaye amedumu na Chakula Chake Kilichohifadhiwa. Hakuna haja ya kulialia tena, tunanena tu Neno na kusonga mbele, kwa kuwa sisi NI Neno.

Hakuna kitu cha kuhofia. Hakuna haja ya mikutano ya maombi ya usiku kucha kufunua sisi ni nani, Neno limekwishafunuliwa kwetu. Tunajijua sisi ni nani, kama vile yeye nabii wa Mungu, naye tayari amekwishatuambia ni nani ambaye angekwenda.

Kila mmoja wetu! Hata kama wewe ni mke wa nyumbani, ama u yaya mdogo, ama hata kama wewe ni mama kizee, ama kijana mwanamume, ama cho chote kile, tutaenda kwa vyo vyote. Hamna hata mmoja wetu atakayeachwa nyuma.” Amina. “Kila mmoja wetu ataenda. Hatutazuiwa na kingine chochote.”

Nena kuhusu kutupa IMANI ya Kunyakuliwa!!!

Njooni muungane na sehemu ya Bibi-arusi wa Mungu tunapokusanyika pamoja kwenye Sauti ya Mungu iliyothibitishwa, anaponena na kutuambia: Kipenzi Changu, Mteule Wangu, Bibi-arusi Wangu, Mbona Unalialia, Nena, na usonge mbele.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: 63-0714M Mbona Unalialia? Nena!

Saa: 06:00 MCHANA, Saa za Jeffersonville (ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki)

Mahali:

Bali kuna Kanisa moja tu halisi, hujiungi nalo; unazaliwa ndani yake. Waona? Na iwapo umezaliwa ukiwa ndani yake, Mungu Aliye Hai hutenda kazi kwako, akijifanya Mwenyewe ajulikane. Waona? Humo ndimo Mungu anamoishi, Kanisani Mwake. Mungu huenda Kanisani kila siku__huishi Kanisani, Yeye huishi ndani yako. Wewe ni Kanisa Lake. Wewe ni Kanisa Lake. Wewe ni hekalu anamoishi Mungu. Wewe binafsi ni Kanisa la Mungu Aliye Hai.

25-0824 Ushirika

UJUMBE: 65-1212 Ushirika

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Neno Lililothibitishwa Peke Yake,

Jinsi gani tunavyomshukuru Roho Mtakatifu kwa Ufunuo wa kweli wa Neno Lake lililothibitishwa la wakati huu. Wengi wanakiri kwamba wanaamini Ndugu Branham ndiye nabii wa Mungu anayetimiza Maandiko yaliyoahidiwa kumhusu yeye, lakini Ufunuo wa kweli wa Neno na mpango wa Mungu umefichwa kwao.

Kwa kila Ujumbe wa Barua ya mahaba ambao Bibi-arusi anaousikia, Mungu anatuthibitishia kwamba tuko katika Mapenzi Yake makamilifu kwa kuisikiliza Njia Yake iliyoandaliwa kwa ajili ya wakati huu, Sauti ya Mungu iliyo kwenye Kanda.

Nasi hatuna budi kumfuata, ndiyo njia pekee ya kupata Uzima wa Milele. Kwa hivyo uongozi wa Mungu ni: fuata Neno lililothibitishwa la wakati huu na Roho Mtakatifu.

NJIA PEKEE ya uzima wa Milele ni: Roho Mtakatifu kukuongoza kulifuata Neno lililothibitishwa. Ni nani aliye na Neno lililothibitishwa la wakati huu? Mungu alimchagua nani kulifasiri Neno Lake? Ni nani ambaye Mungu alimsema ndiye Sauti Yake ya wakati huu? Ni nani ambaye Mungu Mwenyewe alimsema alikuwa ndiye kiongozi aliyethibitishwa kumwongoza Bibi-arusi Wake leo? Je, Ni wahudumu?

Kama tu nilivyosema, maskini yule tai mdogo aliposikia Sauti ya Bwana Arusi, alienda Kwake, Neno la Mungu lililotiwa mafuta, lililothibitishwa kwa ajili ya siku hizi za mwisho.

Nuhu alikuwa ndiye Neno lililothibitishwa la wakati wake.

Musa alikuwa ndiye Neno lililothibitishwa la wakati wake.

Yohana alikuwa ni Neno lililothibitishwa

Wanaweza kulipindisha au kuliwekea fasiri yoyote Kwake watakayo, Bali:

WILLIAM MARRION BRANHAM NDIYE NENO LA MUNGU LILILOTHIBITISHWA LA WAKATI HUU!!

Kwa hivyo uongozi wa Mungu ni: fuata Neno lililothibitishwa la wakati huu na Roho Mtakatifu.

Na Je, kuicheza Sauti ya Mungu iliyothibitishwa katika kanisa lako silo jambo lililo muhimu kuliko ambalo Bibi-arusi analopaswa kufanya? Je, ni muhimu zaidi kuisikiliza sauti tofauti?

Je! ni kundi la watu na huduma yao ndiyo itakayomuunganisha na kumwongoza Bibi-arusi? Je, Bibi-arusi ataunganishwa na yale wasemayo wahudumu? Wote wanasema mambo tofauti, kwa hivyo tumfuate nani?

Je! Ni fasiri yao ya Ujumbe huu ndiyo tutakayohukumiwa kwayo? Je! wao wanayo Nguzo ya Moto inayoithibitisha huduma yao? Je! fasiri yao ya Neno ndiyo Yakini yako?

Nabii alisema Bibi-arusi ANGEUNGANA. Jiulize mwenyewe, ni kitu gani kitakachoufanya unabii huu utimie ili Bwana aje na kumnyakua Bibi-arusi Wake?

Ndiposa, watu wa Mungu waanzapo kukusanyika pamoja, kuna umoja, kuna nguvu. Ona? Na wakati wo wote watu wa Mungu watakapoungana pamoja kabisa, naamini ufufuo utatokea wakati huo. Kutakuwako na wakati wa kunyakuliwa Roho Mtakatifu aanzapo kuwakusanya. Wao—itakuwa katika uchache, bila shaka, lakini kutakuwepo na kukutanika kukuu.

Je! Kutakuwepo na kukutanika kukuu kwenye huduma ya mtu fulani, mbali na nabii wa Mungu aliyethibitishwa? Je! litakuwa ni KUNDI la wahudumu kwa sababu baadhi ya wahudumu wa huduma tano wanasema Hupaswi KAMWE kuicheza Sauti ya Mungu kanisani mwako, ni makosa. Je! wao watamwongoza Bibi-arusi basi?

TAFADHALI NISAIDIE! NI MHUDUMU GANI NINAYEPASWA KUMFUATA, KWANI NATAKA KUUNGANA KATIKA KULE KUKUTANIKA KUKUU.

Wengine husema ati wahudumu wa huduma tano wa Ngurumo Saba ndiyo watakaomkamilisha Bibi-arusi. Baadhi ya wahudumu wa huduma tano wanasema siku za huduma ya Mtu Mmoja zimekwisha. Baadhi ya wahudumu wa huduma tano wanasema yatubidi turudi kwenye Pentekoste. Wengine husema Ujumbe SIO Yakini. Wengine wanasema ukizicheza kanda wewe ni mwamini mungu-mtu. Wote wanasema kitu fulani tofauti, na WOTE wana fasiri tofauti, mawazo tofauti, lakini kila mmoja anasema WAO wanaongozwa na Roho Mtakatifu.

NI MHUDUMU GANI WA HUDUMA TANO NIMFUATE? Maadamu ninamfuata mchungaji “WANGU” wa huduma tano, nitakuwa Bibi-arusi? Kuna “Vikundi” vingi tofauti vya wahudumu wa huduma tano. Hawa wahudumu 20 wanakusanyika na kufanya mikutano yao, lakini wao hawakubaliani kabisa na wahudumu hao wengine 20 walio na mikutano tofauti…niende kwenye mikutano gani ili nikamilishwe na kuungana…baadhi ya hiyo…yote?

Nao watu wanaamini ati MCHAFUKO HUU UTAMUUNGANISHA NA KUMKAMILISHA BIBI-ARUSI? Wote wanasema wao ni WATUMISHI WA KWELI WA HUDUMA TANO ALIYEITWA NA MUNGU. Lakini wao hawawaongozi ninyi kwenye UONGOZI WA KWELI WA ROHO MTAKATIFU, WAO WANAWAONGOZA NINYI KWAO WENYEWE NA KWENYE HUDUMA YAO.

Kwangu mimi, hata huhitaji ufunuo kujua kwamba hilo haliwezi kamwe KUMUUNGANISHA au KUMUONGOZA Bibi-arusi wote. Ni NENO PEKE YAKE litakalomuunganisha Bibi-arusi, kwa SAUTI YA MUNGU MWENYEWE ILIYO KWENYE KANDA.

Ndugu na dada, afadhali muamke ikiwa mnamfuata mchungaji ambaye anahubiri tu na kunukuu Neno, ambalo ni zuri na NDILO HASA analopaswa kuwa akifanya, lakini yeye hawaambii, na muhimu zaidi, HAFANYI HIVYO, kuicheza SAUTI YA MUNGU ILIYO KWENYE KANDA KANISANI MWENU.

Ndugu Branham alituambia:

Naam, tuna tu maagizo matatu ya Kiungu tuliyoachiwa: mojawapo ni—ni ushirika; kutawadhana miguu; ubatizo wa maji. Hayo ndiyo tu mambo matatu. Huo ndio ukamilifu, wa utatu, mnaona.

Ningependa tuwe na Ibada ya Ushirika na Kutawadhana Miguu Jumapili hii, Bwana akipenda. Kama tulivyofanya wakati uliopita, ningewahimiza muanze saa 11:00 JIONI. kwa masaa ya eneo mnaloishi. Ingawa Ndugu Branham alisema mitume walikuwa na Ushirika kila wakati walipokutana pamoja, alipendelea kuufanya wakati wa jioni, naye akautaja kama Meza ya Bwana.

Ujumbe na Ibada ya Ushirika utakuwa kwenye Redio ya Sauti, na pia kutakuwa na anuani ya faili lakupakuliwa, kwa wale ambao hawawezi kuifanikisha Redio ya Sauti Jumapili jioni.

Ndugu Joseph Branham