Category Archives: Uncategorized

25-0601 Kimo Cha Mtu Mkamilifu

UJUMBE: 62-1014M Kimo Cha Mtu Mkamilifu

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa, Minara Ya Ukumbusho Iliyo Hai,

Sauti tunayoisikia kwenye kanda ndio Urimu na Thumimu ya Mungu kwa Bibi-arusi Wake. Hiyo sasa imemuunganisha sawasawa pamoja Bibi-arusi Wake katika moyo mmoja na nia moja kuwa kanisa halisi lililojazwa na Roho, lililojaa nguvu za Mungu, linaloketi pamoja katika katika mahali pa kimbinguni, likitoa dhabihu za kiroho, sifa za Mungu, huku Roho Mtakatifu akitembea kati yetu.

Kristo alitutumia sisi Roho Wake Mtakatifu anene kupitia malaika Wake wa saba ili atujenge sisi kama watu binafsi tufikie kiwango cha Yesu Kristo, kusudi tupate kuwa kituo cha nguvu na makao ya Roho Mtakatifu, kwa Neno Lake.

Sisi ni warithi wa kila kitu. Ni mali yetu binafsi, hiyo ni MALI YETU sisi. Ni zawadi ya Mungu kwetu, na hakuna mtu anayeweza kuichukua kutoka kwetu. NI YETU.

“Lolote mtakalomwomba Baba katika Jina Langu, hilo nitalifanya.” Nani awezaye kukana lolote hapo? “Amin, amin, nakuambia, ukiuambia mlima huu, Ng’oka, wala usitie shaka moyoni mwako, bali waamini kwamba hayo uliyosema yatatukia, lolote ulilosema litakuwa lako.” Ni ahadi zilizoje! Haziishii tu kwenye uponyaji, lakini kwa lo lote.

Utukufu kwa Mungu…LOLOTE TUOMBALO!

Tangu mwanzo wa wakati, viumbe vyote vya Mungu vimekuwa vikiugua na kuingojea siku ambayo wana wakamilifu wa Mungu watakapodhihirishwa. Siku hiyo imefika. Hii ndiyo siku hiyo. Huu ndio huo wakati. Sisi ndio hao wana na binti za Mungu waliodhihirishwa.

Sisi ni chombo kilicho hai cha Mungu anachotembelea, anachoona nacho, anachotumia kuzungumza, anachofanyia kazi. Ni Mungu akitembea kwa miguu miwili NDANI YETU.

Sisi tu nyaraka Zake zilizoandikwa zinazosomwa na watu wote. Wana na binti Zake wenye mamlaka waliochaguliwa, waliochaguliwa tangu zamani, anaowafanya kuwa mtu aliye hai, sanamu hai, kimo cha mtu mkamilifu.

Tunaanguka kifudifudi mbele ya Mungu aliye hai, nguvu zilizo hai, maarifa hai, saburi hai, utauwa hai, Nguvu hai zitokazo kwa Mungu aliye hai, zinamfanya mtu aliye hai kuwa sanamu hai katika kimo cha Mungu.

Ni Kristo, katika utu wa Roho Mtakatifu juu yetu, pamoja na ubatizo wa kweli wa Roho Wake Mtakatifu, na Wema Wake wote ukiwa umetiwa muhuri ndani yetu. Mungu, akiishi ndani yetu katika Maskani iitwayo Jengo. Maskani iliyo hai, ya mahali pa kukaa Mungu aliye hai; Kanisa kamilifu, kwa ajili ya Jiwe Kamilifu la Kifuniko la kutufunika.

Mungu alimtuma nabii kumwita Bibi-arusi Wake atoke na kumwongoza. Ilikuwa ni Adamu Wake wa kwanza aliyerejeshwa kikamilifu, kimo cha mtu mkamilifu katika siku yetu, kulifunua Neno Lake kwa Bibi-arusi Wake.
Siwezi kuondoshwa kwenye hilo. Hakuna kinachoweza kuniondosha. Sijali mtu ye yote anasema nini; halinisogezi hata kidogo. Nitashikilia papo hapo.

Nitangoja, nitangoja, nitangoja. Haileti tofauti yo yote. Inashikilia pale pale. Kisha, siku moja, nitapiga kelele pamoja na watakatifu wengine wote kwa moyo mmoja: “Tunapumzika kwa uhakika juu ya kila Neno!

Ninaahidi, asubuhi ya leo, Kwake, kwa moyo wangu wote, ya kwamba, kwa masaada Wake na kwa neema Yake, ninaomba ya kwamba nitaomba kila siku, bila kukoma, mpaka nitakaposikia kila moja ya mahitaji haya yakitiririka katika maskini mwili wangu huu, mpaka niweze kuwa dhihirisho la Kristo aliye hai.

KWANGU MIMI, kuisikiliza Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda ndio mpango wa Mungu kwa ajili ya siku hii. Ndilo Neno lililo hai la Yesu Kristo. Ndio Yakini yangu kulingana na Neno la Mungu. Ndio njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii.

Hivyo, ningependa kuwaalika kuungana nami Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) ninapomsikiliza William Marrion Branham, ambaye ninaamini kuwa ndiye Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku yetu, akimfundisha Bibi-arusi wa Kristo jinsi ya kuwa: Kimo Cha Mtu Mkamilifu 62-1014M.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Ujumbe:

Mathayo 5:48
Luka Mtakatifu 6:19
Yohana Mtakatifu 1:1 / 3:3 / 3:16 / 5:14 / 14:12
Matendo 2:38 / 7:44–49 / Sura ya 10 / 19:11 / 28:19
Waefeso 4:11-13
Wakolosai Sura ya 3
Waebrania 10:5 / 11:1 / 11:32-40
Yakobo 5:14
2 Petro 1-7
Isaya 28:19

25-0525 Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #4

UJUMBE: 60-0522E Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #4

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Waongofu,

Kwa Kubonyeza Play, tunalisikiliza Neno la Mungu lisilokosea. Ni kila Neno Kweli, kila kifungu Chake. Tumeitwa na kuhifadhiwa, tumejazwa na kutengwa; tumejazwa na Roho Mtakatifu, na sasa tayari tuko katika Nchi ya Kanaani. Hatuogopi cho chote…LO LOTE LILE, tunajua sisi ni nani.

Kwa sababu tumedumu na Neno Lake, kama alivyotuamuru kufanya, Anaenda kutuambia kwamba alituachia sisi urithi. Ulilifanya jambo hilo lini, Baba? Nilipowachagua ninyi na kuyaweka majina yenu kwenye Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Wakati utimilifu wa wakati ulipowadia, nilimtuma Yesu Mwana-Kondoo, Aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili muupate urithi wenu wa kuwa wana na binti Zangu, miungu wadogo.

Ilinibidi niwakague mitikisiko na sehemu zilizolegea kabla sijawaweka mahali penu.

● “Je! Unaamini kuicheza Sauti Yangu iliyo kwenye kanda kanisani ni makosa?”

● “Ndiyo, hupaswi kuzicheza kanda kanisani.”

● “Analikataa. Unatikisika.”

● “Je! Unaamini Neno Langu lililo kwenye kanda linahitaji kufasiriwa?”

● “Ndiyo, Linahitaji mtu fulani kulifafanua.”

● “Unatikisika. Lipige teke nje. Bado hauko tayari.”

Ukiwa tayari, utasema, “Amina” kwa kila Neno.

● “Je! Mnaamini kwamba Mimi ni yeye yule jana, leo na hata milele?”

● “Amina.”

● “Je! Mnaamini kuwa Sauti Yangu iliyo kwenye kanda ndio SAUTI ILIYO MUHIMU KULIKO ZOTE mnayopaswa kuisikia?”

● “Amina.”

● “Je! Mnaamini Sauti Yangu iliyo kwenye kanda ndio itakayomuunganisha Bibi-arusi?”

● “Amina.”

● “Je! Mnaamini kwamba malaika Wangu mwenye nguvu ndiye atakayewatambulisha ninyi Kwangu Mimi?”

● “Amina.”

Mmeanza kukazika sasa. Nimewakagua mtikisiko na maeneo yaliyolegea. Niko tayari kuufunga mlango. Nitauweka Muhuri Wangu juu yenu. Mmefuzu ukaguzi Wangu.

Sasa hebu niwaambieni jambo fulani, Enyi Watu Wangu wapendwa na wa thamani mlio katika nchi za kanda; huko nchi za ng’ambo na popote mlipo, msiogope. Kila kitu ni sawa. Niliwajua ninyi kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Nilijua mambo yote yatakayotukia.

Ninakuja kuwachukua ninyi hivi karibuni na kuwapeleka Mahali ambapo Hakuna mauti, hakuna huzuni, hakuna wivu, hakuna kitu cho chote; Ni ukamilifu tu, upendo mkamilifu.

Hadi wakati huo, msisahau kamwe, Ninawapa Neno Langu, NINYI NI NENO LANGU lililofanyika mwili. Kama mnahitaji JAMBO LOLOTE, Linene, kisha Liaminini; Ni urithi wenu.

Nitawatumia ninyi Sauti Yangu tena Jumapili hii na kuwafafanulia jambo Hilo Lote. Nitawaambia kwa mara nyingine tena ninyi ni nani, wapi mnakoelekea, na jinsi gani kulivyo kule ng’ambo, sasa hivi.

Njooni muungane na Bibi-arusi Wangu ninapowafanya wao waketi pamoja katika mahali pa Mbinguni Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) na mnisikie Mimi nikiwaweka ninyi mahali penu kwa Neno Langu. 60-0522E Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #4

Ndugu. Joseph Branham

25-0518 Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #3

UJUMBE: 60-0522M Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #3

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bikira Safi, 

Tunapobonyeza Play, ni asali mwambani, ni furaha isiyotamkika, ni dhamana iliyobarikiwa, ni nanga ya nafsi zetu, ndio tumaini na tegemeo letu, ni Mwamba wenye Imara, ni kila kitu kilicho chema, ndio Njia ya Mungu iliyoandaliwa ya siku hii. 

Kwa sababu Tunabonyeza Play, Sauti ya Mungu imetuposea; imetuposa kwa Kristo, kama Bikira Safi kwa Neno Lake. Tunaye ila Mwalimu Mmoja tu, Sauti Moja, Nabii Mmoja, anayetuongoza kwa Roho Mtakatifu. 

Bali hili ni kanisa, ninawafundisha. Haya yananaswa kwenye kanda. Nawataka watu wanaosikiliza kanda, wakumbuke, hili ni kwa ajili ya kanisa langu.

Ni thibitisho lililoje kwetu sisi ya kwamba tuko katika Mapenzi Yake makamilifu. Kanda hizo ni kwa ajili ya kanisa Lake. Yeye anatufundisha. Anatuambia, sikilizeni kanda.

Yeye aliuanza mfululizo huu wa Kufanywa Wana Wenye Mamlaka kwa kutueleza kile kilichotokea siku chache zilizopita. Ndipo, kwenye kila Ujumbe, yeye hunena habari za wakati alipokuwa amebadilishwa. Jinsi gani Hilo litakuwa ni muhimu kwa Bibi-arusi kusikia kile kilichotukia na kile Bibi-arusi alichomwambia yeye.  

Nabii wetu atahukumiwa kwa Neno alilohubiri na kuliacha kwenye kanda. Wale Bibi-arusi kule ng’ambo ya pili walimwambia atakubaliwa na Bwana wetu. Kisha yeye atatukabidhi Kwake kama tunu za huduma yake, kisha tutarudi duniani tena tukaishi milele.

Kila Neno tunalolisikia ni kito cha thamani. Tunaendelea tu kuliweka wazi na kuliweka wazi Yeye anapozidi kufunua zaidi tunaposoma katikati ya mistari. 

Jinsi gani tupendavyo kulishiriki Hilo na ndugu na dada zetu, “Je, umelisikia hili?” 

“Yeye alituchagua katika Yeye kabla ulimwengu hata haujakuweko”? Huo ndio urithi wetu. Mungu alituchagua, kisha akamwacha Yesu aje alipe ile deni. Hiyo ni nini? Kumwaga Kwake kwa Damu Yake, kusudi tusihesabiwe dhambi. Hufanyi lo lote.

Kisha, mara tu baada ya hilo, Je, umelipata hili?

“Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, kwa Bwana.” Umeelekeza macho yako Kalvari, na hakuna kitu kitachokuzuia! Mwenendo wa maisha yako, unatembea katika Barabara Kuu ya Mfalme, umepakwa na Mafuta ya thamani, ukielekea kwenye Patakatifu pa patakatifu. Whiu! Amina.

Sisi tulikuwa kama ile fimbo ya Haruni, fimbo ya kale iliyokauka ambayo alikuwa ameibeba kwa miaka arobaini kule jangwani.  Lakini sasa, kwa sababu tumewekwa katika Mahali pale Patakatifu kwa kuisikia Sauti ya Mungu ikinena nasi kwenye kanda, tumechipuka na kuchanua, tukiwa tumejaa Roho Wake Mtakatifu, nasi Bibi-arusi Wake tukipaza sauti kwa mapafu yetu yote.

⚪ Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, kwa Bwana, kanda ndizo nafasi ya kwanza mioyoni mwetu.  

⚪ Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu kwa Bwana, Yeye alituchagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.

⚪ Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, kwa Bwana, sisi ni Bibi-arusi wa Yesu Kristo.

⚪ Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, kwa Bwana, haileti tofauti yo yote yale mtu ye yote asemayo, hatuzirudishi kanda, tunazicheza nyingi zaidi. 

⚪ Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, kwa Bwana, tumeyaelekeza macho yetu Kalvari, na hakuna kitu kitakachotuzuia. 

Nina furaha sana kuungana moyoni na watu wengi hapa ambao wanajua kwamba Hili ni Neno la Mungu lisilokosea. Basi Hilo, Hilo ni Kweli kwa kila Neno, kila Neno Lake, kila fungu Lake. Na kwa neema ya Mungu, kama nilivyotunukiwa kuiangalia ile Nchi ambayo siku moja tutaizuru.

Njoo uungane nasi Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika) Nabii anapolichukua kila Neno na kulifafanua tu kindani. Atalipeleka hadi Mwanzo na kulifafanua kindani, na atalipeleka hadi Kutoka na kulifafanua tena, na hata hadi Ufunuo; na Ni Yesu kwa kila kipengee!

Ndugu. Joseph Branham 

Ujumbe: 

Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #3 60-0522M

Maandiko:

Mathayo 28:19

Yohana 17:7-19

Matendo 9:1-6, Sura ya 18 na 19

Warumi 8:14-19

1 Wakorintho 12:12-13

Wagalatia 1:8-18

Waefeso Sura ya 1

Waebrania 6:4-6, 9:11-12

25-0511 Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #2

UJUMBE: 60-0518 Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #2

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Ukuhani Wa Kifalme,

Kila mtu na aume kidole chake, finya nafsi yako, na ufanye moyo wako thabiti. Leo, Bibi-arusi wa Yesu Kristo anapaza sauti:

Leo, unabii huu umetimia mbele ya macho yetu.

Ninaamini, moja ya siku hizi tukufu, wakati muungano huu wa umoja wa kanisa utakapoungana, kisha papa mpya atoke Marekani na kuwekwa huko juu kulingana na unabii, ndipo basi watafanya sanamu kama ya yule mnyama.

Sauti ya nabii wa Mungu ililinena hilo Tarehe 19 mwezi Desemba, 1954, na miezi 9 baadaye, Robert Prevost, ambaye sasa anajulikana kama Papa Leo XIV, alizaliwa. Yeye sasa ndiye papa mpya wa Rumi. “Bwana Asema Hivi” imetimia.

Tarehe 7 mwezi Mei, 1946, MUNGU alimweka nabii Wake kule Green’s Mill, Indiana, kumpa agizo lake na kuutangazia ulimwengu, huyu ndiye malaika-mjumbe Wangu wa saba mwenye nguvu, Sauti Yangu kwa ulimwengu. Msikieni Yeye.

Wakati Malaika wa Bwana alipokutana nami kule Green’s Mill, Indiana, miaka minane iliyopita; baada ya kuwa tangu utotoni, akinifuata, akionyesha maono. Nilipomwendea, alisema, “Kama utakuwa mwaminifu, wafanye watu wakuamini, hakuna kitakachosimama mbele ya maombi.”

William Marrion Branham ndiye Sauti teule ya Mungu kwa ulimwengu. Nabii hodari ambaye Neno la Mungu humjia. Kulingana na Neno, yeye ndiye mfasiri PEKEE wa Kiungu wa Neno la Mungu.

Yeye alithibitishwa na Mungu Mwenyewe, kwa Nguzo ya Moto.

Tarehe 7 mwezi Mei, 2025, SHETANI aliliweka Baraza lake la Makardinali katika Kanisa la Sistine huko Rumi ili kumchagua Halifa wao wa Kristo, ili kuitimiza Bwana Asema Hivi.

Yeye alithibitishwa na mtu mwenye PAFU LA MOSHI MWEUPE.

Bibi-arusi wa Kristo ulimwenguni kote anafurahi, anapiga kelele, anapiga vifijo na kumsifu Bwana tunaposikia, na kuona kwa macho yetu wenyewe, unabii wa nabii ukitimia.

Ni kana kwamba tunaiona Bahari ya shamu ikifunguka mbele ya macho yetu. Mana mpya ikianguka kutoka angani. Mamilioni ya kware wakimshibisha Bibi-arusi. Maji yakitoka kwenye Mwamba. Moto ukishuka na kuiteketeza dhabihu tukiwa na Eliya.

Unabii unatimizwa kila siku. Neno la Mungu lililoahidiwa linadhihirishwa katika maisha yetu. Mambo yanatukia pande zote. Bibi-arusi amejiweka mwenyewe tayari kwa kulisikia na kuliamini Neno. Sisi ni Neno lililofanyika mwili.

Hakika, tumewasili. Muda umewadia. Bibi-arusi anafurahi na kuungana pamoja ulimwenguni kote kuliko hapo awali. Nabii anamhakikishia upya Bibi-arusi kwa kutuambia sisi ni ukuhani wa kifalme wa Mungu, taifa takatifu, watu wa kipekee walioitwa watoke, wateule, waliochaguliwa na wakatengwa.

Sisi SASA TU Wana na Binti za Mungu, Tukiongozwa na Roho wa Mungu; si na mwanadamu, bali na Roho. Tunajua, pasipo na shaka hata chembe, SISI NI BIBI-ARUSI WAKE. IMANI yetu inafikia viwango vipya kila siku. Hakuna wa kutuzuia au kutupunguza mwendo, Mungu ametufunulia hilo na kulitia nanga katika mioyo na nafsi zetu.

Bibi-arusi tumetambua kikamilifu sisi ni nani. Tuko katika Nchi yetu ya ahadi ya kiroho, tumemiliki kabisa kila kitu. Tuna amani ya Kimbinguni, baraka za Kimbinguni, Roho wa Kimbinguni. KILA KITU NI CHETU. Tunajiweka tayari tu kwa ajili ya yale yajayo ambayo Yeye ametutayarishia.

Parapanda ya Bwana italia, nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Miili hii ya mbinguni itashuka ije ivae ya duniani, miili ya utukufu nasi tutabadilishwa kwa dakika moja, kufumba na kufumbua. Tutanyakuliwa pamoja nao, kumlaki Bwana hewani.

Ni siku ilioje. Ni wakati wa jinsi gani. Hakuna njia ya mimi kusema kwa maneno ya kibinadamu kile sisi sote tunachokihisi katika nafsi zetu. Mioyo yetu inaenda mbio. Hatulifanyi hilo, Roho Mtakatifu ni kama kisima kinachofoka maji kikibubujika ndani yetu. Bibi-arusi amekuwa akiungojea wakati huu tangu siku za Adamu…NA SASA SISI TUMEWASILI.

Tunawakaribisheni. Tunawaalika. Tunawasihi. Njooni muungane nasi kwa ajili ya wakati mkuu sana ambao ulimwengu umepata kuujua, tunapoisikia Sauti ya Mungu ikilifunua Neno Lake kwetu Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia: 60-0518 Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #2.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Ujumbe:

Mwanzo 1:26
Waefeso Sura ya 1
Warumi 8:19
Wagalatia 1:6-9
Waebrania Sura ya Sita
Yohana 1:17

25-0504 Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #1

UJUMBE: 60-0515E Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #1

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Waliofanywa Wana Wenye Mamlaka,

Sasa hivi tunakula vile vitu vigumu vya Mungu na kuwa na ufahamu pevu wa Neno Lake. Mungu ametupa Ufunuo wa kweli wa Neno Lake. Ufahamu wetu wa kiroho haujavurugika.

Sisi TUNAJUA Yeye ni Nani hasa. TUNAJUA hasa kile Yeye alicho. TUNAJUA hasa wapi tunakoelekea. TUNAJUA hasa sisi ni nani. TUNAMJUA Yeye tunayemwamini na kusadiki kuwa Yeye aweza kukilinda kile tulichoweka amana kwake hata siku ile.

Yeye amenena na kutufunulia sisi siri zote zilizokuwa zimefichwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu. Alituambia jinsi ambavyo wengine daima wao wameikataa njia Yake iliyoandaliwa na kutamani uongozi tofauti, lakini Yeye angekuwa na kundi dogo ambalo litadumu waaminifu kwa Neno Lake.

Kote ulimwenguni, hawatakusanyika mahali pamoja na kuwa na vitu shirika. Lakini makundi madogo yatakuwa yametawanyika kote duniani.

Utukufu, tumetawanyika duniani kote, lakini Tumeungana kama Mmoja kwa Kubonyeza Play na kuisikiliza Sauti ya Mungu ikizungumza nasi.

Hebu na tuchunguze na tutangulie kuonja yale Yeye atakayokuwa akitueleza kupitia malaika Wake mwenye nguvu siku ya Jumapili.

Wapendwa Wangu waliochaguliwa, sasa mmeketi pamoja katika Mahali pa Mbinguni. Si popote pale, bali katika mahali pa “Mbinguni”; ndipo mahali pako kama mwaminio. Mmeomba vya kutosha nanyi mko tayari kwa Ujumbe. Mmekusanyika pamoja kama watakatifu, mliobatizwa na Roho Mtakatifu, mliojazwa na baraka za Mungu. Mmeitwa, mmeteuliwa, nazo roho zenu zimewaleta katika hali ya Kimbinguni.

Nini kingetokea. Roho Wangu Mtakatifu atakuwa akitembea katika kila moyo. Mmezaliwa upya na mmekuwa kiumbe kipya katika Kristo Yesu. Dhambi zenu zote ziko chini ya Damu. Mko katika ibada kamilifu, huku mikono na mioyo yenu imeinuliwa Kwangu Mimi, mkiniabudu MIMI pamoja katika mahali pa Mbinguni.

Ninyi mlichaguliwa kimbele, Mkateuliwa, katika kutangulia Kwangu Kujua. Mkachaguliwa, Mkatakaswa, mkahesabiwa Haki kwa Kukusudiwa Kimbele. Haiwezekani kwenu ninyi kudanganywa. Nimewakusudia kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Ninyi ni mungu mdogo, mliotiwa muhuri kwa Roho Mtakatifu wa ahadi; sio tu waliozaliwa katika familia, Wana na Binti Zangu wenye mamlaka.

Nitawabariki kwa uponyaji wa kiungu, kutangulia kujua, ufunuo, maono, nguvu, lugha, fasiri, hekima, maarifa, na baraka zote za Kimbinguni, kwa furaha isiyoneneka na iliyojawa na Utukufu.

Kila moyo utajazwa na Roho Wangu. Mtakuwa mkitembea pamoja, mkiketi pamoja, katika mahali pa mbinguni. Hakuna wazo moja baya kati yenu, hakuna hata sigara moja inayovutwa, hakuna nguo moja fupi, hakuna jambo hili, lile au lingine, hakuna wazo moja baya, hakuna aliye na neno dhidi ya mwingine, kila mtu akinena kwa upendo na upatanifu, kila mmoja katika moyo mmoja na mahali pamoja.

Ndipo kutakuja ghafla toka Mbinguni sauti kama upepo wa nguvu ukienda kasi Nami nitawabariki kwa baraka zote za rohoni. Ndipo mtakuwa kama vile Daudi, mkicheza mbele ya Sanduku, mkiuambia ulimwengu hamuonei haya, NINYI NI BIBI-ARUSI WANGU WA KANDA! Mnabonyeza play na mnaamini KILA NENO ninalosema. Ninyi hamta, na hamwezi kuondoshwa!

Wengine wanaweza kulikataa, au wasilielewe, lakini kwenu ninyi, Ni Beji yenu ya Heshima. Kama vile Daudi alivyomwambia mkewe; “Hivi Mnadhani hili lilikuwa ni kitu, ngojeni tu hadi kesho, tutakuwa tukisikiliza kanda hata na zaidi, tukimsifu Bwana, tukiwa tumejazwa na Roho Wake; kwa maana tunaishi Kanaani, tukielekea nchi ya ahadi.”

Kisha nitaangalia chini kutoka Mbinguni na kukuambia:

“Wewe ni Bibi-arusi aupendezaye moyo Wangu.”

Baraka hizi zinaweza kuwa zako pia. Njoo, uungane nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) na ujionee uwepo wa Bwana zaidi ya hapo awali tunapoisikiliza Sauti ya Mungu ya siku hii ikinena nasi na kutuletea Ujumbe: Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #1 60-0515E.

Kumbukeni, hili ni kwa ajili ya kanisa, si kwa mtu aliyeko nje. Kwake ni siri katika mafumbo kwake, hawezi kulielewa kamwe, linamshinda akili, hajui kitu hata kidogo juu yake. Bali, kwa kanisa, ni asali mwambani, ni furaha isiyotamkika, ni dhamana iliyobarikiwa, ni nanga ya nafsini, ni tumaini na tegemeo letu, ni Mwamba wenye Imara, loo, ni kila kilicho chema. Kwa kuwa mbingu na nchi zitapita, bali Neno la Mungu halitapita kamwe.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Ujumbe:

Yoeli 2:28
Waefeso 1:1-5
I Wakorintho 12:13
1 Petro 1:20
Ufunuo 17:8
Ufunuo 13

25-0427 Mfalme Aliyekataliwa

UJUMBE: 60-0515M Mfalme Aliyekataliwa

PDF

BranhamTabernacle.org

Rafiki Zangu Wapendwa,

Rafiki zangu wapendwa, wapendwa wangu, wapenzi wangu wa Injili, watoto wangu niliomzalia Mungu.

Ni wikendi ya ajabu vipi tuliokuwa nayo pamoja na Bwana wetu. Haikuwa kama kitu kingine chochote, kutumia tu wakati pamoja Naye, kuzungumza Naye, kuisikia Sauti Yake, kumwabudu Yeye, kumshukuru, na kumwambia jinsi gani tunavyompenda.

Ni heshima iliyoje kuishi katika siku hii na kuwa sehemu ya Maandiko yanayotimia. Maneno ya kibinadamu yanawezaje kueleza yote yaliyo moyoni mwetu? Kama vile nabii alivyosema, Si mimi, kuna Kitu Fulani ndani kilindini, kikisukuma na kububujika ndani yangu; kisima kinachofoka maji ya Roho Mtakatifu. Ni Bibi-arusi akijifanya Mwenyewe tayari kwa ajili ya Bwana-arusi.

Jinsi gani bibi-arusi huchangamka kabla ya harusi yake. Moyo wake huanza kudunda kwa kasi sana wakati sekunde chache za mwisho zinapopita….anajua kuwa hatimaye wakati umefika. “Nimejiweka tayari. Anakuja kunichukua. Sasa tutakuwa MMOJA.”

Kwa kweli tunaishi katika nyakati za mwisho za kumalizia za wakati. Bibi-arusi hivi karibuni atanyakuliwa na kuitwa kwenye Karamu yetu ya fungate. Yeye anatupeleka kwenye viwango vipya. Hakuna swali tena; hakuna tena kushangaa; SISI NDIO BIBI-ARUSI.

Na bado Yeye hajamaliza. Bado Yeye anataka kumbariki na kumtia moyo Bibi-arusi Wake kipenzi aliyechaguliwa. Jinsi gani Yeye anavyopenda kumtia moyo na kumwambia jinsi gani Yeye anavyompenda. Jinsi anavyojivunia Yeye.

Yeye bado anao Ufunuo mwingine wa kipekee sana wa kumpa Bibi-arusi. Wakati kuna sauti nyingi sana ulimwenguni zinazokataa kucheza kanda, Yeye anataka tena kumhakikishia Bibi-arusi kwamba wako katika Mapenzi Yake makamilifu na Njia Yake iliyoandaliwa.

Mpango Wake daima umekataliwa. Bibi-arusi Wake daima ameteswa. Watu daima wanataka njia yao wenyewe, mawazo yao. Wanataka kiongozi tofauti awaongoze. Lakini Mungu alimtuma kiongozi MMOJA kumwongoza Bibi-arusi Wake, Yeye Mwenyewe, Roho Mtakatifu, na Roho Mtakatifu wa siku hii, kama ilivyo katika SIKU ZINGINE ZOTE, NI NABII WA MUNGU.

Siku zote wao wametaka watu wawaongoze. Katika siku za Samweli, Mungu alisema walikuwa wakimkataa Yeye kwa kutotaka Samweli awaongoze. Ilionekana kuwa jambo la ajabu kwa vile Samweli yeye pia alikuwa mtu, lakini tofauti ilikuwa Samweli alikuwa ndiye mtu ambaye Mungu alimchagua kuwaongoza. Haikuwa Samweli, Ilikuwa ni Mungu akimtumia Samweli. Yeye alikuwa ndiye SAUTI na MTU ambaye Mungu alimchagua KUWAONGOZA, lakini wao walitaka sauti zingine.

Sauli alijua watu walimcha Samweli, hivyo ilimbidi atangaze, “Sauli NA Samweli”. Ilibidi awaogopeshe watu ili wamfuate yeye. Kweli, alikuwa ameitwa. Kweli, alikuwa ametiwa mafuta na Samweli kuwa mfalme wao, lakini Mungu ANGALI alikuwa anayo Njia iliyoandaliwa, na nabii aliyemchagua Yeye kuwaongoza, hata kumwongoza na Sauli. Mungu alinena na nabii Wake na kumwambia Sauli la kufanya. Wakati Sauli alipoamua kuwa amepakwa mafuta yeye pia, na hakutaka kumsikia nabii tu, Mungu aliuondoa ufalme wake.

Kwa hiyo basi walipofanya jambo hilo, wakati kule kushindwa kukuu kulipokuja, ndipo Sauli alichinja maksai wawili wakubwa na kuwapeleka kwa watu wote. Na laiti mngaliona hapa. Wakati Sauli alipopeleka vipande vya yule maksai kwa Israeli wote na kusema, “Na iwe kwamba mtu ye yote ambaye hatamfuata Samweli na Sauli, na awe (huyu maksai) kama huyu.” Mnaona jinsi alivyojaribu kujiwakilisha kwa hila pamoja na mtu wa Mungu? Jinsi lilivyokuwa si la Kikristo. Uchaji wa watu ulikuwa kwa ajili ya Samweli. Bali Sauli akawafanya wote wamfuate kwa maana watu walimcha Samweli. “Na wamfuate Samweli na Sauli.”

Siku moja Sauli alifadhaika sana. Hakuweza kupata jibu kutoka kwa Mungu. Hakuweza kupata faraja. Alitaka majibu. Alijua ni wapi alipaswa kwenda ili kupata jibu alilotaka; palikuwa na mahali pa moja tu, NABII WA MUNGU, SAMWELI. Alikuwa amekwisha vuka ng’ambo, lakini bado yeye alikuwa angali ni SAUTI YA MUNGU, HATA KATIKA PARADISO.

Baba alitaka Bibi-arusi Wake ajue Yeye Alimchagua nani kumwongoza Bibi-arusi Wake katika siku hii ya mwisho, kwa hivyo Yeye Akamchukua malaika Wake mwenye nguvu kule ng’ambo ya pazia la wakati ili kwa mara nyingine tena atuambie, atufariji, na kututia moyo kwamba tuko katika Mapenzi Yake makamilifu na yaliyoandaliwa.

Yasikilize kwa makini sana YOTE anayosema nabii.

Sasa, nisingewataka ninyi mrudie jambo hili. Hili ni mbele ya kanisa langu, ama kondoo wangu ninaowachunga.

Kabla yeye hajatuambia lo lote, kwanza anatutaka tujue hili ni kwa ajili YETU PEKE YAKE, KANISA LAKE, KONDOO WAKE, WALE ANAOWACHUNGA. Kwa hivyo, kama huwezi kusema, “Ndugu Branham ni mchungaji WANGU,” nimesema jambo hilo hapo awali, lakini hakuna tu haja ya kulisoma zaidi, hili si kwa ajili yako, pamoja na kwamba yeye hakututaka hata tulirudie kwa ye yote yule ila kwa wale wanaoamini na kusema, “Ndugu Branham ni mchungaji wangu”.

Hilo papo hapo jibu letu kwa swali tunalopata shutuma nyingi sana kwa sisi kusema: “Ndugu Bramham ndiye mchungaji wetu.” (Hao ni wale watu wa kanda.) Wako sahihi, yeye yuko hivyo, nasi tuko hivyo.

Tafadhali msinikasirikie, mimi sisemi mambo haya ili kumkasirisha mtu ye yote, hilo lingekuwa kosa, bali ni yale Yeye anayomwambia Bibi-arusi. Mimi siweki fasiri yangu kwake, Yeye analisema wazi…Neno la Mungu halihitaji fasiri yo yote.

Ama ilikuwa kwamba nilikuwa katika mwili ama nje yake, ama ilikuwa kuhamishwa, Haikuwa kama ono lo lote nililopata kuona.

Sasa yeye anatuambia hili halikuwa kama ono lo lote alilopata kuona. Alikwenda mahali ambapo hajawahi kufika. Lilikuwa KUBWA kuliko ono lolote alilowahi kuona. Hakuwa akiota, aliuona mwili wake kitandani; ALIKUWEPO KULE.

Bibi-arusi wa Yesu Kristo, hebu hilo na lizame vizuri sana. Walikuwa ni Bibi-arusi wa Yesu Kristo kule ng’ambo ya pili, wa wakati uliopo, waliyokuja wakimkimbilia, wakipiga kelele na kumshika, wakimkumbatia na kusema, “Loo, ndugu yetu wathamani!”

Yeye alikuwa kule; aliweza kulihisi; aliweza kuwasikia. Walikuwa wakizungumza naye. Alisimama, na kutazama, alikuwa kijana. Akaangalia nyuma kwenye mwili wake mzee uliokuwa umelala pale mikono yake ikiwa nyuma ya kichwa chake.

Sasa tumethibitisha YEYE ALIKUWEPO KULE, na Ilikuwa ni Bibi-arusi wa Yesu Kristo aliyekuwa akimwona. Sasa hebu na tusikie kile ile sauti kutoka juu ilichokuwa ikimwambia.

Ndipo sauti hiyo iliyokuwa ikinena nami kutoka juu yangu, ikasema, “Unajua imeandikwa katika Biblia ya kwamba manabii walikusanywa pamoja na watu wao.”

Mungu hakuwa tu akimwonyesha na kumtia moyo nabii Wake, bali kulikuwa na mengi zaidi Kwenye jambo Hilo. Yeye angerudi na kutuambia sio tu wapi tunakoelekea na jinsi gani kungekuwa, bali kutuambia sisi tuko katika Mapenzi Yake makamilifu kwa Kubonyeza Play na hivyo ndivyo unavyofika mahali alipo Bibi-arusi.

Ndugu Branham alisema yeye alitaka kumwona Yesu vibaya sana. Lakini wakamwambia:

“Naam, Yuko juu kidogo tu, moja kwa moja upande ule.” Kasema, “Siku moja Yeye atakuja kwako.”

Wakaendelea kumwambia yeye ALIKUWA NANI.

“Wewe ulitumwa kuwa kiongozi na Mungu atakuja, na atakapokuja, Yeye atakuhukumu kulingana na yale uliyowafundisha, kwanza; kama wataingia ama hawataingia. Tutaingia kulingana na mafundisho yako.”

Ni nani aliyetumwa kama kiongozi? Tunaenda kuhukumiwa kulingana na yale nani aliyotufundisha? Tutaingia Mbinguni kulingana na mafundisho ya nani?

Mtu mmoja anaweza kusema, ninawafundisha watu wangu yale tu Ndugu Branham aliyosema…amina, unapaswa nami naamini baadhi wanafanya hivyo, lakini usilifanye “Ndugu Branham na Mimi”

Hebu tuendelee kusoma kwani Yeye anataka KUHAKIKISHA kwamba tunaelewa kwa uwazi zaidi.

Ndipo hao watu wakapiga kelele wakasema, “Tunajua jambo hilo, nasi tunajua tunarudi pamoja nawe siku moja duniani.” Kasema, “Yesu atakuja, nawe utahukumiwa kulingana na Neno ulilotuhubiria sisi.

Tutahukumiwa kwa Neno YEYE alilotuhubiria. Hivyo, hukumu inakuja kutokana na kile Sauti ya Mungu ilichosema kwenye kanda. Mtu yeyote anawezaje kusema ati hiyo Sauti iliyo kwenye kanda sio SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI mnayopaswa kuisikia?

“Halafu, kama ukikubalika wakati huo, ambapo utakubalika”

Je! Mko tayari. Hili litapigilia msumari kuhusu Mapenzi makamilifu ya Bwana ni yapi kwa Bibi-arusi wa Yesu Kristo. Bibi-arusi anamwambia nabii kile YEYE ATAKACHOFANYA. Si mtu mwingine. Sio kundi. Si mchungaji mwingine, nabii wa Mungu, WILLIAM MARRION BRANHAM.

“basi wewe utatukabidhi Kwake kama tunu yako ya huduma yako.”

Je! Ni nani atakayetukabidhi kwa Bwana Yesu?
Je! Siku za kumsikiliza tu nabii zimekwisha?
Je! Ndugu Branham hakuwahi kamwe kusema tucheze kanda?

Bibi-arusi anapiga kelele na kusema kama unataka kuwa Bibi-arusi ni bora Ubonyeze Play.

Bado haujashawishika? Vema, kuna hata na zaidi.

Kasema, “Utatuongoza Kwake na sote pamoja tutarudi duniani tukaishi milele.”

Ni nani wa kutuongoza Kwake? Ni nani anayemwongoza Bibi-arusi? Bibi-arusi anamwambia yeye kwamba YEYE ATAWAONGOZA BIBI-ARUSI KWAKE, kisha tutarudi duniani tukaishi milele.

Ikiwa kuna Ufunuo WOWOTE ndani yako hata kidogo. Ikiwa unadai unauamini Ujumbe Huu, ninaomba ya kwamba Mungu akufunulie ya kwamba ni LAZIMA uiweke Sauti Yake, kanda, kuwa ya KWANZA.
Enyi Wachungaji, mrudisheni nabii kwenye mimbara zenu. Kanda ndio Sauti iliyo muhimu sana mnayopaswa kuisikia kwani mtaenda kuhukumiwa kwa SAUTI HIYO.

Kulingana na Neno, tuko katika Mapenzi Yake makamilifu na yaliyoandaliwa kwa ajili ya siku yetu kwa kusikiliza Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.

Ikiwa Mungu ameyafungua macho yako kwenye Ufunuo wa kweli wa Neno Lake, ninakualika uungane nasi Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tusikiapo 60-0515M Mfalme Aliyekataliwa.

Ndugu. Joseph Branham

Pasaka 2025 – Ibada Maalum ya Ushirika na Kutawadhana Miguu

UJUMBE: 62-0204 Ushirika

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Kristo,

Ni wakati mzuri sana jinsi gani ambao Bibi-arusi atakaokuwa nao Wikendi hii ya Pasaka. Naamini itakuwa moja ya mambo muhimu katika maisha yetu; wakati ambao hatutausahau kamwe. Wikendi kuu maalum.

Kila Pasaka imekuwa wakati ulio maalum kwa Bibi-arusi, tunapoufungia milango yetu ulimwengu wa nje kwa kuvizima vifaa vyetu vyote na vikengeusha-fikira vya kilimwengu, na kuyaweka tu wakfu upya maisha yetu Kwake. Ni wikendi nzima iliyowekwa wakfu kwa ajili Yake katika ibada, tunapozungumza Naye siku nzima kila siku, na kisha kulisikia Neno Lake.

Adui ameyafanya maisha yetu kukengeuka sana na kujaa shughuli za mambo mengi sana ya maisha hadi imekuwa vigumu sana kuufungia ulimwengu nje na kuongea Naye. Hata vifaa vile vile tunavyovitumia kusikia Neno, Shetani hutumia kuhatarisha wakati wetu.

Lakini wikendi hii itakuwa tofauti, na si kama wikendi nyingine ya Pasaka ambayo tumewahi kuwa nayo.

Wakati Bwana alipoweka moyoni mwangu kusikiliza ile Mihuri, sikujua jinsi gani tarehe zingeangukia. Lakini kama kawaida, wakati Wake ni mkamilifu. Jumapili mbili zilizopita, tulikuwa na majaliwa ya kuusikia Muhuri wa 4, Wakati wa Tai, tarehe 6 Aprili, siku ya kuzaliwa ya nabii; jinsi inavyofaa.

Lakini sasa, Bwana anayo hata na zaidi mengi aliyotuwekea sisi. Kama nilivyosema, nilipojisikia Bwana ameweka moyoni mwangu kuicheza Mihuri, nilijua ingechukua wiki kadhaa kumaliza kuicheza kwani kuna Jumbe 10 katika mfululizo huo.

Nilipoitazama kalenda, niliona kwamba Pasaka iliiangia kabla hatujamaliza kuusikia huu mfululizo mzima. Nikawaza mwenyewe, nadhani inatubidi tuache kuisikiliza ile Mihuri na Yeye atanipa Jumbe kwa ajili ya Pasaka.

Mara moja niliona… itakuwa KAMILIFU. Tunaweza kuendelea kuicheza Mihuri huku Muhuri wa Saba ukichezwa Asubuhi ya Jumapili ya Pasaka. Sikuweza kuamini, hilo liliendana kabisa na ratiba. Nilijua papo hapo, HUYU NI WEWE, BWANA.

Nimekuwa nimechangamshwa na nikiwa chini ya matarajio makubwa kwa ajili ya wakati wetu wa Pasaka pamoja na kila mmoja wetu, na pamoja Naye. Nilijua Yeye ametutengenezea ratiba.

Hivyo, ikiwa Bwana akipenda, tutaendelea kuisikiliza Mihuri katika kipindi chote cha Wikendi yetu ya kipekee ya Pasaka.

ALHAMISI

Ilikuwa ni Alhamisi usiku ambapo Bwana Yesu alishiriki Karamu ya Mwisho na wanafunzi Wake, katika ukumbusho wa Pasaka kabla ya kule kutoka kwa wana wa Israeli. Ni fursa iliyoje tuliyo nayo ya kufanya ushirika na Bwana majumbani mwetu, kabla ya wikendi yetu takatifu, na kumwomba atusamehe dhambi zetu, na atupe sisi sote kile tunachohitaji katika safari yetu.

Lijalie, Bwana. Waponye walio wagonjwa. Wafariji walio wachovu. Wape furaha wanaodhulumiwa. Wape amani walio wachovu, Chakula kwa wenye njaa, Maji kwa wenye kiu, furaha kwa wenye huzuni, uwezo kwa kanisa. Bwana, mlete Yesu miongoni mwetu usiku wa leo, tukiwa tunajitayarisha kushiriki ushirika unaowakilisha mwili Wake uliovunjwa-vunjwa. Tunaomba, Bwana, kwamba Yeye atatuzuru kwa njia ya ajabu sana…

Wabariki wengine, Bwana, kila mahali ulimwenguni, ambao wanangojea kwa furaha kuja kwa Bwana, taa zimetengenezwa, na dohani zimesuguliwa kabisa, na Nuru ya Injili ikiangaza katika sehemu zenye giza.

Hebu na tuanze sote saa 12:00 KUMI NA MBILI JIONI. kwa masaa ya nchi unayoishi ili kusikia Ushirika 62-0204, na kisha nabii atatupeleka katika ibada yetu maalum ya Ushirika na Kutawadhana Miguu, ambayo itakuwa ikicheza kwenye app ya Lifeline (kwa Kiingereza), au unaweza kuipakua ibada hiyo kwa Kiingereza au lugha nyinginezo kwa kubofya anuani iliyo hapa chini.

Tukiufuata Ujumbe, tutakusanyika pamoja na familia zetu majumbani mwetu na kuishiriki Meza ya Bwana.

IJUMAA

Hebu na twende kwenye maombi na familia zetu saa 3:00 TATU ASUBUHI(Ni saa 10:00 KUMI JIONI ya Afrika Mashariki)., na kisha tena saa 06:00 SITA MCHANA, (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tukimkaribisha Bwana awe pamoja nasi na azijaze nyumba zetu kwa Roho Mtakatifu tunapojiweka wakfu Kwake.

Mawazo yetu na yarudi huko nyuma hadi kwenye siku ile pale Kalvari, yapata miaka 2000 iliyopita, na kumwona Mwokozi wetu akining’inia msalabani, na kisha tujitoe vivyo hivyo kufanya daima yale yanayompendeza Baba:

Iwapo siku hii ni muhimu sana, moja ya siku zilizo kuu sana, hebu na tuangalie mambo matatu ambayo siku hiyo ilimaanisha kwetu. Tungechukua mamia. Bali asubuhi ya leo nimechagua tu mambo matatu tofauti yaliyo muhimu sana ambayo tunataka kuyachunguza katika muda mfupi ujao; ambayo Kalvari ilimaanisha kwetu. Nami naomba ya kwamba itamhukumu kila mwenye dhambi aliyeko, ya kwamba itamfanya kila mtakatifu kupiga magoti yake, ya kwamba itamfanya kila mgonjwa ainue imani yake kwa Mungu na aondoke ameponywa, kila mwenye dhambi aokolewe, kila aliyerudi nyuma arudi na ajionee aibu, na kila mtakatifu afurahi na apate tumaini jipya na tumaini jipya.

Kisha saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA,(Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) Hebu na tuungane pamoja majumbani mwetu kusikia: 63-0323 Muhuri wa Sita.

Kisha tuungane pamoja katika maombi mara baada ya ibada, katika ukumbusho wa kusulubiwa kwa Bwana wetu.

JUMAMOSI

Tuungane tena sote katika maombi Saa 3:00 TATU ASUBUHI (Ni saa 10:00 KUMI JIONI ya Afrika Mashariki) na saa 6:00 Saa SITA MCHANA,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) na kuitayarisha mioyo yetu kwa ajili ya mambo makuu Yeye atakayotufanyia miongoni mwetu.

Ninaweza kumsikia akisema, “Shetani, njoo hapa!” Yeye ni Bosi sasa. Ananyosha mkono, anaunyakua ule ufunguo wa mauti na kuzimu kutoka ubavuni mwake, akauning’iniza ubavuni Mwake Mwenyewe. “Ninataka kukupa notisi. Umekuwa laghai muda mrefu kutosha. Mimi ni Mwana wa Mungu aliye hai niliyezaliwa na bikira. Damu Yangu ingali imelowa msalabani, na deni kamili limelipwa! Huna haki tena. Umenyang’anywa zote. Nipe funguo hizo!”

Kisha saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, sote tutakusanyika pamoja kulisikia NENO: 63-0324m Maswali na Majibu Juu ya Mihuri.

Hii itakuwa SIKU ILIYO MAALUM jinsi gani kwa Bibi-arusi Wake ulimwenguni kote.

Kisha tuungane pamoja katika maombi mara baada ya ibada.

JUMAPILI

Hebu kwanza na tuamke mapema kama vile Ndugu Branham alivyofanya asubuhi wakati rafiki yake mdogo, robin, alipomwamsha saa 11:00 ASUBUHI.. Hebu na tumshukuru tu Bwana kwa kumfufua Yesu kutoka kwa wafu:

Saa kumi na moja asubuhi ya leo, maskini rafiki yangu mwenye kifua chekundu aliruka dirishani akaniamsha. Ilionekana kana kwamba moyo wake mdogo ungepasuka, akisema, “Amefufuka.”

Saa 3:00 TATU ASUBUHI (Ni saa 10:00 KUMI JIONI ya Afrika Mashariki) na saa 6:00 Saa SITA MCHANA,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tuungane kwa mara nyingine tena katika mnyororo wetu wa maombi, tuombeane na kujitayarisha kuisikia Sauti ya Mungu.

Saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, (Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) tutakusanyika pamoja kuusikia Ujumbe wetu wa Pasaka: 63-0324e Muhuri wa Saba.

Saa 9:00 TISA ALASIRI, Hebu na tuungane tena katika maombi, tumshukuru Yeye kwa Ajili ya WIKENDI YA AJABU ALIOTUPATIA KUWA PAMOJA NAYE NA PAMOJA NA BIBI-ARUSI WAKE ULIMWENGUNI KOTE.

Kwa ndugu na dada zangu walio nchi za ng’ambo, kama vile mwaka jana, ningependa kuwaalika kuungana nasi kwa masaa ya Jeffersonville, katika nyakati zote za maombi kwenye ratiba hii. Ninatambua, hata hivyo, kwamba kuzicheza Kanda Alhamisi, Ijumaa, na Jumamosi alasiri kwa masaa ya Jeffersonville ingekuwa vigumu sana kwa wengi wenu, kwa hivyo tafadhali jisikieni huru kuzicheza Jumbe hizo katika masaa yanayowafaa. Ningependa, hata hivyo, tuungane pamoja sote Jumapili saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) ili kuusikia Ujumbe wetu wa Jumapili pamoja.

Ningependa pia kukualika wewe na watoto wako kushiriki vipindi vya Creations, Journaling, na maswali ya YF, ambayo familia yako yote inaweza kufurahia pamoja. Tunafikiri mtayapenda kwa kuwa yote yanalenga NENO tutakalosikiliza wikendi hii.

Kwa ratiba ya wikendi, taarifa ya kuhusu jinsi ya kujiandaa na ibada ya Ushirika, nyenzo zitakazohitajika kwa ajili ya vipindi vya Creations, Maswali ya Pasaka, na taarifa nyinginezo, tazama anuani zilizopo hapa chini.

Hebu na tuzifunge simu zetu kwa ajili ya wikendi ya Pasaka isipokuwa kupiga picha, kusikia Nukuu ya Siku, na kucheza kanda kwenye app ya the Table, app ya Lifeline, au anuani inayoweza kupakuliwa.

Ni heshima kubwa kwangu kukualika wewe na familia yako kukusanyika pamoja na Bibi-arusi kote ulimwenguni kwa ajili ya wikendi iliyosheheni IBADA, SIFA NA UPONYAJI. Ninaamini kweli ni wikendi ambayo itayabadilisha maisha yako milele.

Ndugu Joseph Branham

Unahitaji anuani za:

Vitu vya kupakuliwa

Ibada ya Ushirika na Kutawadhana

Kalenda ya ratiba

https://vgrwebsites.blob.core.windows.net/branhamtabernacle/48eec3f2-152c-4c94-8dd1-0a639108de49.pdf

https://vgrwebsites.blob.core.windows.net/branhamtabernacle/48eec3f2-152c-4c94-8dd1-0a639108de49.pdf

Taarifa juu ya jinsi ya kujiandaa na Ushirika

https://branhamtabernacle.org/en/articles/view/1212021_InstructionsForBakingBreadMakingWine

Nyenzo zinazohitajika kwa ajili vipindi vya Creations

https://youngfoundations.org/easter

Maswali ya Pasaka

https://youngfoundations.org/articles/TheRevelationOfTheSevenSeals

ALHAMISI– 6:00 PM (saa za ndani)

62-0204 Ushirika (Huduma Maalum ya Ushirika na Kuosha Miguu)

IJUMAA – saa 06:30 SITA NA NUSU MCHANA (saa za nchi mnayoishi)

63-0323
Muhuri wa Sita

JUMAMOSI– saa 06:30 SITA NA NUSU MCHANA (saa za nchi mnayoishi)

63-0324M
Maswali Na Majibu Juu Ya Mihuri

JUMAPILI– saa 06:30 SITA NA NUSU MCHANA (saa za Jeffersonville) (Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki)

63-0324E
Muhuri wa Saba