Category Archives: Uncategorized

24-0324 Kutambua Siku Yako Na Ujumbe Wake

UJUMBE: 64-0726M Kutambua Siku Yako Na Ujumbe Wake

PDF

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapenzi Watu Wathamani na Wapendwa,

Inapendeza sana jinsi gani kujua sisi ndio Bibi-arusi Wake mpendwa na Wathamani. Tumefanyizwa kutoka ulimwenguni kote, tukikusanyika pamoja kulizunguka Neno Lake, tukisikiliza Sauti ya Mungu ikizilisha nafsi zetu.

Tumelikubali katika ukamilifu wake, na katika nguvu ya kuthibitishwa kwake na ufunuo wake. Tumekuwa sehemu Yake. Ni kitu ambacho kiko ndani yetu. Ni zaidi ya uhai kwetu.

Tumetambua: Malaika-Mjumbe Wake wa Saba.
Tumetambua: Ujumbe wa Nuru ya Jioni.
Tumetambua: Sisi ni Nani.

Mungu amechukua Neno la nabii Wake na kutubangua. Ametukata kwa Malaki 4, kama alivyoahidi angefanya. Tunaamini kila Neno kwa mioyo yetu yote.

Kuna uamsho mkubwa unaoendelea miongoni mwa watu. Wao pia wanatambua umuhimu wa kuisikia Sauti hiyo. Wanataka kurudi na kuzicheza kanda katika makanisa yao.

Wamejulishwa na Roho Mtakatifu, kwamba hii ndiyo Njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku hii. Wanatambua kuwa hii ndio Sauti wanayohitaji kuisikia. Ndicho Chakula cha Mungu kilichohifadhiwa kwa ajili ya kumkamilisha Bibi-arusi Wake.

Neno liliahidi jambo Hilo. Kanda zinalitangaza. Wao wanaliamini.

Ilifanyaje? Iliwasumbua makuhani, kuona hao watu wakiondoka makanisani na kwenda zao. Akasema, “Kama yeyote wenu akihudhuria mikutano Yake, mtatengwa na ushirika. Tutawafukuza moja kwa moja kutoka katika dhehebu.”

Haliaminiki, lakini hilo limekuwa ni jambo lile lile leo hii. Watakufukuza katika makanisa yao ukisema, “Tafadhali, chezeni kanda.” Je! Hivi tumewahi kamwe kuwazia huenda hiki ndicho kinachowatenganisha watu? Kuicheza Sauti ya Mungu katika makanisa yetu?

Kanisa limesahau manabii wao. Wao “hawawahitaji tena,” ndivyo wanavyodai. Bali Mungu anajua hana budi kuwa nao; Yeye huwakata watu Wake kwa Neno Lake. Lakini kwao Hilo limepitwa na wakati sana katika siku hii.

Tutakaa na nabii wetu. Tunaamini kuwa ndio Sauti inayomwita Bibi-arusi Wake. Kwetu sisi, hakuna kitu chochote kilicho muhimu zaidi ya KUBONYEZA PLAY.

Loo, enyi kondoo za Mungu, sikilizeni Sauti ya Mungu! “Kondoo Wangu huisikia Sauti Yangu.”

Njoo uisikie na uitambue Sauti hiyo pamoja nasi, Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) tunaposikia,  Kutambua Siku Yako na Ujumbe Wake 64-0726M.

Ndugu. Joseph Branham

24-0317 Kuenda Nje Ya Kambi

UJUMBE: 64-0719E Kuenda Nje Ya Kambi

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Askari Wakristo,

Wazieni jambo hilo! Ni mwisho wa wakati, Haleluya! Tumewasili. Ile Siku kuu ya Kuja kwa Bwana kumchukua Bibi-arusi Wake imekaribia. Tunakusanyika wenyewe pamoja kutoka ulimwenguni kote, tukikamilishwa kwa kusikiliza Sauti ya Mungu. Tunatazamia na kungojea wapendwa wetu watokee… ni siku yoyote sasa.

Kitu pekee ambacho tumeagizwa kufanya ni “Dumuni na Neno”. Yote tuyaonayo ni Yesu, na Yeye ni Neno lililofanyika mwili. Huo ndio Ufunuo wa siku yetu. Hiyo ndio Kambi ya Mungu kwa ajili ya Bibi-arusi Wake.

Ujumbe huu, Sauti hii, kanda hizi, ndicho kila kitu tunachohitaji kwa ajili ya Unyakuo. Hatuhitaji kitu kingine chochote. Tumeitwa tutoke, tumetengwa na kila kitu kingine isipokuwa ile Sauti. Tumeshawishika kuwa Sauti hiyo ndiyo Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii.

Wazieni jambo hilo, Yeye ametupatia nabii mkuu wa nyakati zote. Yule ambaye Nguzo ya Moto Mwenyewe alipiga picha naye ili aweze kuuambia ulimwengu, “Huyu ni malaika wangu mwenye nguvu. Yeye ni Sauti Yangu kwenu. Yale Anenayo duniani Mimi nitarudisha mwangwi mbinguni. Hakuna aliye kama yeye”.

“Nimemkabidhi yeye, na yeye peke yake, siri Zangu zote nilizozificha tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu. Yeye ndiye niliyemchagua tangu awali kuwaita NINYI mtoke katika ulimwengu huu mje Kwangu. Yeye ndiye niliyemchagua kuwatangulia, kuwaongoza, na kuwaelekeza. Nawatangazieni, msikieni Yeye, kwa maana si yeye anenaye, NI MIMI, YULE MIMI NIKO ALIYE MKUU.

Nimewaweka wakfu watu wakuu na kuwaita kuutangazia ulimwengu na kuuambia , “Leo maandiko ya Malaki 4, Ufunuo 10:7 na Luka 17:30 yametimia mbele ya macho yenu. Yule Malaika wake mwenye nguvu amewasili, kama jinsi Maandiko yalivyotangaza. Mungu yuko hapa miongoni mwetu, akijifunua Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu kama alivyosema angefanya.”

Ni Yesu Kristo yeye yule jana, leo na hata milele. Tumeitwa kuwaelekeza ninyi kwake yeye, malaika wa Mungu. Yeye ndiye ambaye Roho Mtakatifu alimchagua kuongoza na kumwita Bibi-arusi Wake atoke. Msihojiane, msibishane, msigombane na kushindana ni nani atakayekuwa kuhani mkuu; nani anayetakiwa kuwa hili, lile, ama linginelo. DUMUNI NA SAUTI HIYO. Kwa maana kuna SAUTI YA MUNGU moja tu iliyothibitishwa na jina lake ni William Marrion Branham.

Yatupasa kuwa waangalifu sana kudumu na hiyo Sauti, kwa kuwa kuna wengi wanaotaka kuwaongoza kwingineko. Mapokeo yao yanaiweka Sauti hiyo ya kweli mbali na watu. Yeye amekuwa mgeni kwa wengi wao. Sauti yao imepachukua mahali pa Sauti hiyo, hata wakati Mungu, kwa njia ya kanda, anapowazuru, Yeye ni mgeni.

Ule uwepo mkuu wa Agosti u pamoja nasi. Mtu yeyote mwepesi wa kuhisi Roho anaweza kujua Sauti hiyo ni Sauti ya Mungu. Ndio ile Kambi ya Mungu kwa ajili ya siku hii.

Kila mtu anayedai kuwa Bibi-arusi wa Kristo lazima aamue ni Kambi gani aliyomo. Ni lazima wajiulize swali hili rahisi: Hivi ni Sauti gani ambayo Bibi-arusi wote wanaweza kusema “AMINA” kwayo?

Kama kweli wewe ni Bibi-arusi wa Kristo, mwenye Ufunuo wa kweli wa Neno la siku hii, kuna jibu moja tu: Sauti ya Mungu iliyo kwenye Kanda. Bila shaka Shetani anajaribu kuliendesha hilo kwa njia nyingi tofauti, lakini hakuna jibu lingine kwa Bibi-arusi. Ni rahisi jinsi hiyo.

Sote tunajua kwamba Shetani anatumia jibu hilo ili kutugawanya. Lakini Neno linatuambia Bibi-arusi hana budi KUUNGANA… TUMEUNGANA, kwa SAUTI PEKEE INAYOTUUNGANISHA.

Njoo uungane nasi, kwa maana ile saa imechelewa sana.

“Nataka kwenda nje ya kambi. Haidhuru itanigharimu nini, nitautwaa msalaba wangu na kuubeba kila siku. Nitatoka nje ya kambi. Hata watu waseme nini juu yangu, nataka kumfuata nje ya kambi. Niko tayari kwenda.”

Ikiwa unataka kuwa katika ile Kambi ya Mungu ya siku hii, LAZIMA UAMINI Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda ndio Sauti iliyo muhimu sana unayopaswa kuisikia.

Njoo uungane na sehemu ya Bibi-arusi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) tunapoisikia ile Sauti ambayo Mungu aliyoichagua kumwongoza Bibi-arusi Wake, anapotuletea Ujumbe, Kuenda Nje ya Kambi 64-0719E.

Sio “kambi fulani”; ni “ILE KAMBI”.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Ibada :

Waebrania 13:10-14
Mathayo 17:4-8

24-0310 Sikukuu Ya Baragumu

UJUMBE: 64-0719M Sikukuu Ya Baragumu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Watoto wa Nuru,

Tunayo shukurani jinsi gani kuwa tunatembea katika Nuru Yake. Kuwa sehemu ya Nuru hiyo, kutambulishwa na Nuru Yake. Kuitwa na kuchaguliwa Na Yeye. Sisi ni Bibi-arusi wa Kristo, tumetambulishwa pamoja Naye. Hao wawili sasa ni Mmoja.

Nisingeweza kuliandika mara nyingi sana. Hatuwezi kulisema vya kutosha. Ujumbe huu unamaanisha KILA KITU kwetu. Kujua kuwa tunao Ufunuo wa kweli wa Neno Lake ni zaidi ya chochote tungeweza kuweka kwa maneno.

Kuishi katika siku hii na kuwa sehemu ya kile kinachotendeka, ndio heshima iliyo kuu ambayo Mungu angeweza kutupa. Jinsi lilivyokuwa jambo kuu kuketi katika mikutano katika Maskani ya Branham, kuona na kumsikia malaika wa Mungu akizileta Jumbe hizi, ni KUU hata na zaidi kule kuishi katika siku hii, na wakati huu, na kuwa ule utimilifu wa Neno hilo.

Mungu, katika Mpango Wake mkuu, ameandaa Njia ambayo tungeweza kukusanyika kutoka ulimwenguni kote, kuisikiliza Sauti ya Mungu sote kwa wakati mmoja, ili kukamilishwa na Neno Lake. Kusubiri kusikia katika sekunde yoyote malaika-mjumbe wetu wa saba aseme;

“Tazama Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!”

Hakujawahi kuwa na kitu chochote kama Hicho tangu mwanzo wa wakati. Kule Kumalizika kwa Mpango mkuu wa Mungu kunatukia, SASA HIVI, na sisi tu sehemu Yake. Ile Siku kuu ya Bwana imekaribia.

Siri zote zimefunuliwa kwa Bibi-arusi na malaika-mjumbe wa Mungu. Ile Mihuri, zile Nyakati, Ngurumo, Imani ya Kunyakuliwa, Mvuto wa Tatu…KILA KITU kimekwishanenwa na kiko kwenye kanda ili Bibi-arusi aweze kuzisikia tena na tena, nayo INATUKAMILISHA.

Roho Mtakatifu amerudi Kanisani tena; Kristo, Mwenyewe, akifunuliwa katika mwili wakibinadamu, wakati wa jioni kama alivyoahidi.

Sikiliza kwa makini sasa ewe Bibi-arusi, likamate.

Tumeitwa na Neno; Kristo mwenyewe ametuita. Amejiweka mwenyewe dhahiri kwetu; Waebrania 13:8, Luka 17:30, Malaki 4, Waebrania 4:12, Maandiko haya yote aliyoahidi.

Ni Yesu, Mwana wa Mungu, ambaye amejifunua kwetu kwa Maandiko haya ambayo yaliyochaguliwa tangu zamani kwa ajili ya siku hii, YAISHI TENA.

Na, kuamini Hilo, ndio dhihirisho la Roho Mtakatifu.

Mungu alimtuma nabii Wake kumwita Bibi-arusi Wake atoke. Neno linatuambia nabii ni Neno lililo hai la Mungu, lililodhihirishwa. Ndio ishara ya mwisho ambayo ulimwengu utakayopata; Yehova akinena katika umbo la mwanadamu.

Mtu katika mwili wa kibinadamu, kama nabii, hata hivyo ilikuwa ni Elohimu akilitambua wazo lililokuwa katika moyo wa Sara, nyuma Yake. Naye Yesu alisema, “Kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, ndivyo itakavyokuwa katika ukamilifu wa dahari, wakati Mwana wa Adamu,” si Mwana wa Mungu, “wakati Mwana wa Adamu atakapokuwa akifunua.”

Bibi-arusi anajua isipokuwa uwe daima katika Neno, hutajua Yeye ni nani. Wao wanajua umuhimu wa kuiweka Sauti hiyo mbele zao kila siku kwa Kubonyeza Play.

Sasa Bibi-arusi hana budi kuondoka jukwaani, na kwenda juu, ili wale manabii wawili wa Mungu katika Ufunuo waweze kutokea jukwaani ili kupiga Baragumu ya Saba. Kuwajulisha Kristo.

Njoo uwe sehemu ya unabii uliotimia Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) wakati nabii wa Mungu anapoleta Ujumbe, Sikukuu ya Baragumu 64-0719M, na kuzungumza na Baba na kusema,

Yawezekana kuwe na baadhi huko nje katika mataifa, ulimwenguni kote, ambao hata kanda hii ingewakuta manyumbani mwao au makanisani mwao. Tungeomba, Bwana, kwamba wakati ibada inaendelea, pale—pale…au kanda inachezwa, au nafasi yo yote tunayoweza kuwamo, au—au hali, yule Mungu mkuu wa Mbinguni na aheshimu huu unyofu wa mioyo yetu asubuhi hii, na kuponya wahitaji.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Walawi 16 yote
Walawi 23:23-27
Isaya 18:1-3
Isaya 27:12-13
Ufunuo 10:1-7
Ufunuo 9:13-14
Ufunuo 17:8

24-0303 Kile Kipeo

UJUMBE: 64-0705 Kile Kipeo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Familia Iliyo Kipeo,

Jinsi gani Jumbe hizi za mwisho zimekuwa Kamilifu kabisa kwa Bibi-arusi wa Kristo. Mungu, akijifunua Mwenyewe mbele zetu, akijifunua Mwenyewe waziwazi. Ulimwengu hauwezi kuliona Hilo, lakini kwetu sisi, Bibi-arusi Wake, Hilo ndilo tuonalo.

Tumelipenya pazia na kumwona Yeye waziwazi kabisa. Mungu, nyuma ya ngozi ya mwanadamu. Neno limefanyika mwili, kama vile hasa Yeye alivyoahidi katika Luka 17 na Malaki 4. Amejificha Mwenyewe katika pazia la mwanadamu, katika nabii Wake na katika Kanisa Lake.

Sisi ndio watu wenye furaha kuliko wote ulimwenguni wakati tunapomsikia Mungu akinena kupitia malaika-mjumbe Wake na kutuambia,

Ninashukuru sana kwa ajili yenu. Nina furaha sana kushirikiana pamoja nanyi. Nina furaha sana kuwa mmoja wenu. Mungu awe nanyi.Atakuwa nanyi. Yeye hatawaacha kamwe. Hatawapungukia. Yeye hatawaacha. Tayari mmekwisha pita katika ile pazia.

Tumekuwa watu wa kipekee kwa kila mtu, hata katika nyadhifa zetu wenyewe, lakini tunajivunia, na kushukuru sana, kwa Ufunuo Ambao Yeye ametupa wa Neno Lake wa siku hii. Kuwa wapumbavu kwa ajili ya Kristo na Neno Lake lililodhihirishwa.

Tumeweka imani yetu pamoja na imani ya nabii Wake, nasi tumeungana pamoja, tukifanya UMOJA mkuu wa Mungu. Yeye Hawezi kitu bila sisi; sisi hatuwezi kufanya lolote bila nabii huyo; wala hatuwezi kufanya lolote bila Mungu. kwa hiyo sote pamoja, TUNAFANYA KITU KIMOJA, Ule Muungano; Mungu, nabii Wake, Bibi-arusi Wake. Tumekuwa Kipeo Chake.

Ilimchukua Yeye miaka elfu nne kutengeneza Kipeo Chake cha kwanza. Sasa, imemchukua Yeye miaka elfu mbili kutengeneza Kipeo Chake kingine, SISI, Bibi-arusi Wake, familia Yake kuu iliyo Kipeo, Adamu wa Pili na Hawa wa Pili. Sasa tuko tayari kwa ajili ya ile bustani, ule Utawala wa Miaka Elfu. Ametufinyanga tena na sasa tuko tayari.

Sisi ndiye Bibi-arusi Wake Neno Kamilifu, sehemu ya ule Uumbaji Wake ASILI. Ubua, kishada, na ganda, sasa vinakusanyika katika ile Mbegu, tayari kwa ufufuo, na tayari kwa mavuno. Alfa imekuwa Omega. Ile Mbegu iliyoingia ndani, imepitia hatua fulani na imekuwa Mbegu tena.

Ile mbegu iliyoanguka katika bustani ya Edeni kisha ikafa kule, ilirudi. kutoka kwa ile mbegu isiyo kamilifu iliyokufia kule, ikarudi ikawa Mbegu kamilifu, Adamu wa Pili.

Sisi sasa tumekuwa Adamu wa Pili, Bibi-arusi wa kweli, ile Mbegu, amerudi na Neno la asili tena. Na lazima tuwe na Neno lote kusudi tupate kuwa ile Mbegu. Hatupaswi kuwa na nusu ya Mbegu; hatuwezi kukua, lazima tuwe Mbegu nzima.

Kuna jambo moja tu lililosalia, mavuno yamefika. Tumeiva kabisa. Tuko tayari kwa kule Kuja. Ni wakati wa mavuno. Ile Mbegu imeirudia hali yake ya asili. Ile Familia ilio Kipeo imekuja tena, Kristo na Bibi-arusi Wake.

Ili kumtia moyo nabii Wake na Bibi-arusi Wake, Bwana alimpa malaika wake ono kuu. Alimpa kuonekana kimbele kwetu SISI, Bibi-arusi Wake. Tulipopita karibu naye, alisema, tulikuwa wanawake wadogo walio wazuri mno. Alisema sote tulikuwa tukimtazama, tulipokuwa tukipita.

Mwishoni, wengine walikuwa wametoka kwenye mstari, nao walikuwa wakijaribu wawezavyo kurudi mstarini. Kisha aliona kitu fulani muhimu sana, walikuwa wakiangalia mahali pengine, Hawakuwa wakimtazama Yeye. Walikuwa wakiliangalia hilo kanisa lililoingia katika machafuko. Jinsi gani ninavyojivunia na ninavyoshukuru kusema, sio SISI, Hao waliokuwa mbele, sisi hatukutoka nje ya hatua ama kuyaondoa macho yetu Kwake Yeye.

Kwa hiyo kile Kipeo na Mwana wa Mungu—Kipeo na Bibi-arusi, Naye ni sehemu Yake, ambayo ni lazima iwe kutimizwa kwa Neno. Neno limekwishatimizwa, nasi tuko tayari kwa kule Kuja kwa Bwana.

Tunayoshukrani jinsi gani kujua, sisi ndio ile Familia iliyo Vipeo Vyake, Bibi-arusi Wake wa kweli. Neno limekwishatimizwa, nasi tuko tayari kwa kule Kuja kwa Bwana.

Ninawaalika mje muungane nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) ili kusikia Neno pamoja nasi, na kuwa sehemu ya ile Familia iliyo Kipeo cha Mungu, tunapomsikia nabii akituletea Ujumbe: Kile Kipeo 64-0705.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Isaya 53:1-12
Malaki 3:6
Mathayo 24:24
Marko 9:7
Yohana Mtakatifu 12:24 / 14:19

24-0225 Wa Kipekee

UJUMBE: 64-0614E Wa Kipekee

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Marafiki Wapendwa,

Ni saa 6:00 SITA MCHANA huko Jeffersonville, saa 1:00 MOJA JIONI huko Afrika, saa 4:00 NNE ASUBUHI huko Arizona; Bibi-arusi wamekusanyika pamoja kutoka ulimwenguni kote. Tumesubiri wiki nzima kuufikia wakati huu. Tuko chini ya matarajio makubwa, tukimngojea Mungu aseme nasi kupitia midomo ya mwanadamu kwa njia ya malaika-mjumbe Wake wa saba mwenye nguvu. Tunaomba, “Bwana nitayarishe, unitie mafuta, na unipe Ufunuo zaidi wa Neno Lako.”

Tumeridhika, kwa maana tunajua hakika, ya kwamba nabii, na nabii peke yake, ndiye aliye na Maneno ya Uzima ya saa hii. Huenda tusiweze Kulieleza lote, lakini tunajua tunaamini kila Neno na tunalitegemea Hilo.

Tunajua, kama vile Bwana alivyofanya na Musa, Mungu Anajiandaa kumtukuza nabii wake mbele zetu. Wakati huo, Yeye aliitikisa tu milima. Wakati huu, Yeye Anazitikisa mbingu na nchi.

Ule wakati umefika. Mioyo yetu inaenda mbio ndani yetu. Tunausikia wimbo wetu wa Taifa umeanza kucheza. Kwa moyo mmoja, Bibi-arusi kutoka ulimwenguni kote wainuka kwa miguu yao na kuanza kuimba, AMINI TU , yote yawezekana, Amini Tu. Mungu anajiandaa kuzungumza nasi.

Tunasikia: “Habari za asubuhi marafiki.”

Mioyo yetu inafurahi kusikia tu maneno haya 3 rahisi. Nabii ametoka kuniita mimi rafiki yake. Kisha anatuambia,

Ninawakosa ninyi nyote. Si—sijali ninapokwenda, ni—ni…si, si ninyi. Nina marafiki, kila mahali ulimwenguni, bali si—si ninyi nyote. Kuna kitu fulani kuhusu kundi hili dogo ambalo lina ninino tu…Sijui. Mimi huwafikiria…Sina ku—kundi fulani ulimwenguni, nilijualo, linaloshikamana nami kama kundi hili. Mungu na—na ajalie tuwe wasioweza kutengana sana, hata, katika Ufalme ujao, naomba kwamba tuwe huko pamoja; ombi langu.

Ni Ufunuo mkuu jinsi gani ambao Mungu atatufunulia leo? Tunaenda kusikia kitu gani? Labda tumelisikia mara nyingi, nyingi sana hapo kabla, lakini leo itakuwa tofauti, ni kama vile haijawahi siku yoyote hapo kabla.

Ni kitu gani? Chakula cha Mwaminio. Mkate wa Wonyesho kutoka Mbinguni tutakaousheherekea. Mkate wa Wonyesho ulio kwa ajili yetu tu, Bibi-arusi Wake. Ni Utukufu wa Shekina juu ya Mkate huo wa Wonyesho unaotufanya tusiharibike.

Hao walio nje hututazama na kuuliza, “Ninyi watu mnafanya nini? Mnasikiliza tu kanda? Ninyi ni Wa Kipekee kweli kweli.”

Utukufu!! Tunayo furaha sana, na tunamshukuru sana Bwana sisi kuwa Wa Kipekee; wapumbavu kwa ajili Yake na Neno Lake lililothibitishwa. Tunafurahi kuuambia ulimwengu, “NDIYO, NINAAMINI HUDUMA YA KANDA. NINAAMINI KUBONYEZA PLAY. NINAAMINI NDIO SAUTI ILIYO MUHIMU SANA UNAYOPASWA KUISIKIA. NDIYO, NINAAMINI KUZIRUDISHA KANDA MIBARANI.”

Wakati utaji wa mapokeo umeondolewa, unaweza kuona ya kwamba Mungu angali ni Mungu wa Neno Lake. Yeye angali anadumisha Neno Lake. Yeye ni ninii—Yeye ndiye Mungu, Mwandishi wa Neno Lake.

Haijalishi yale mtu yeyote afanyayo, ama asemayo, tunaliamini Hilo, na kisha tunalitendea Hilo kazi. Kama wewe hulifanyi Hilo, basi huliamini. Hauko nyuma ya pazia. Pazia hilo ni la mtu mmoja. Ujumbe huo ni mmoja.

Nami ninatumaini na kuamini ya kwamba—ya kwamba mmekuwa na ufahamu wa kiroho juu ya yale Mungu amekuwa akijaribu kuliambia Kanisa bila ya kulisema moja kwa moja. Unaona? Ni jambo, wakati mwingine, inatubidi kusema mambo kwa njia fulani kwamba iweze kupunguza, iweze kuwafanya wengine kutoka nje, wengine kuondoka, na wengine ku—ku—kutafakari. Lakini hilo linafanywa makusudi. Lazima lifanywe hivyo.

Neno lilifunuliwa kwa nabii wa Mungu. Hakuna cha kundi, Mafarisayo, ama Masadukayo, ama dhehebu fulani ama ukoo. Ni NABII! Mungu alimpata mtu mmoja. Hakupata mawazo mawili au matatu tofauti. Yeye alimchukua mtu mmoja. Ndiye aliye na Neno, na yeye peke yake.

Ndipo huenda ikawa kwamba wengine wangesema, “Unamaanisha Mungu angefanya jambo kama hilo makusudi?” Hakika alifanya. Angali anafanya.

Kama vile walivyosema mamia ya miaka iliyopita, tunasikia jambo lile lile leo hii: “Lakini kuna watu wengine hapa ambao Mungu amewaita.” Hiyo ni kweli. Na maadamu tu wanafuata na kwenda pamoja, ni Amina, bali wakati mtu anapojaribu kupiga hatua na kuchukua nafasi ya Mungu ambayo Mungu aliyompa nabii wetu, ambayo Yeye alichaguliwa tangu zamani na kuwekwa kwa ajili ya kazi hiyo, inatubidi kukaa na Neno lililothibitishwa, ile Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku yetu.

Angalia, kifo, kukaa mbali Nalo sasa. Huna budi kuingia ndani Yake kupitia kwenye pazia hili, la sivyo hutaingia. Jinsi ambavyo Mungu angeweza kuwarehemu, bali kumbukeni vile ilivyokuwa, ya kwamba Mungu anadhihirisha kile kilichokuwa nyuma ya lile pazia. Angalieni kile kilichokuwa nyuma ya pazia, hilo Neno! Lilifunika nini? Neno! Ilikuwa ni kitu gani? Liko kwenye sanduku. Lilikuwa ni lile Neno ambalo lile pazia lililificha. Mnaona? Naye Yesu alikuwa ndiye Neno hilo, Naye Ndiye hilo Neno, nalo pazia la mwili Wake lililificha.

Kwetu sisi, ni udhihirisho! Sio neno tena, ni uhalisia! Amina!

Tunajua kwa wengine sisi ni Wa Kipekee, na linaweza likasikika kama nati kwa ulimwengu, lakini linawavuta watu wote Kwake.

Njoo uingizwe kwenye Neno pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) tunapomsikia nabii akiuambia ulimwengu jinsi sisi tulivyo Wa Kipekee 64-0614E. Tunajivunia na tunashukuru sana kusema ndivyo sisi tulivyo.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

I Wakorintho 1:18-25
2 Wakorintho 12:11

24-0218 Kufunuliwa Kwa Mungu

UJUMBE: 64-0614M Kufunuliwa Kwa Mungu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliye Nyuma ya Pazia,

Kwa nini ninaendelea kuwaambia tena na tena, “KUBONYEZA PLAY ndilo jambo lililo muhimu zaidi mnalopaswa kufanya”? Kwa nini ninaendelea kuwaambia wachungaji, “Mrudisheni Ndugu Branham kwenye mimbara zenu”?

Ni rahisi tu namna hii. Kule kuisikiliza Sauti ya malaika-mjumbe wa saba kwenye kanda, ni kusikiliza NENO LILILO HAI.

Mbele za watu, Mungu alijitia utaji tena na kumthibitisha Musa, kwa utaji, kwa kujitia utaji kwa Moto ule ule, Nguzo ile ile ya Moto ilishuka. Tangu—tangu wakati huo…Kutoka kwao, kwa hiyo wangeweza tu kusikia Neno la Mungu. Mnalipata? Neno pekee, waliisikia Sauti Yake. Kwa kuwa, Musa alikuwa, kwao, Neno lililo hai.

Nena kuhusu Mhudumu aliye Hai! Sauti tunayoisikiliza kwenye kanda ndio Sauti ya Neno lililo Hai la siku yetu. Hakuna nyingine iliyo kuu kuliko Hiyo.

Katika siku za Musa, ni wana wa Israeli tu waliokuwa kambini ndio wangeweza kuisikia Sauti Yake. Lakini leo, Mungu alitaka ULIMWENGU uisikie Sauti Yake, KWA HIYO AKAIREKODI KWENYE KANDA, ili Bibi-arusi Wake aweze kuisikia Sauti ya Neno lililo Hai.

Mungu alikuwa amejificha nyuma ya pazia la nabii Wake, apate kuwaambia Neno Lake. Hilo ndilo alilokuwa amefanya. Musa alikuwa ndiye hilo Neno lililo hai kwa watu, lililotiwa utaji kwa Nguzo ya Moto.

Kama huna Ufunuo wa jambo hilo kwa ajili ya siku yetu, huwezi kuwa Bibi-arusi wa Yesu Kristo. Kama unao, basi wewe NI Bibi-arusi wa Yesu Kristo na itakubidi kusema, “hakuna jambo lililo muhimu zaidi kuliko kuzisikiliza kanda, kwa maana ni Sauti ya Mungu ikinena nawe mdomo kwa sikio.”

Wengi wanajaribu kuwatisha watu na kusema tunamsifu sana nabii; tunamuabudu. Enyi marafiki, Yeye ndiye aliyesema mambo haya, si mimi. Mimi nina nukuu tu Neno.

Kama ilivyofanyika katika kila wakati, Uungu ukitiwa utaji katika mwili wa binadamu. Angalieni, Yeye alifanya hivyo. Manabii walikuwa ni Uungu, umetiwa utaji. Walikuwa ni Neno la Mungu (hiyo ni kweli?) lililotiwa utaji katika mwili wa binadamu. Kwa hiyo wala hawakumwona Musa wetu, mnaona, Yesu.

Hatumwabudu mwanadamu, bali Mungu, Ambaye ametiwa utaji na anayejifunua Mwenyewe kupitia nabii. Ili kuelewa na kuamini hilo, yakubidi ufanye hivi.

Hamko nyuma ya pazia hilo tena, enyi Watoto wadogo. Mungu anaonekana wazi kabisa kwenu.

Hatuko nyuma ya pazia hilo tena, tunaweza kuona Ni Mungu anayejifunua Mwenyewe waziwazi. Imefunuliwa ya kwamba kusikiliza Sauti hiyo kwenye kanda ni Mungu akizungumza na Bibi-arusi Wake. Tunaamini ndiyo Njia Yake iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii.

Tunaweza tu kusema AMINA kwa Sauti hiyo, si kingine. Sauti hiyo itahubiri, itafundisha na kutufunulia kila kitu tunachohitaji kujua. Sauti hiyo itatutambulisha sisi kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Sauti hiyo ndiyo yote tunayotaka na tunayohitaji.

Tunashukuru kwa huduma 5 ambayo Mungu anayoitumia kuwaelekeza watu kwenye Sauti hiyo; kwa ajili ya wachungaji ambao wamelipata lile ono na walio na ufunuo kwamba kuzicheza kanda katika makanisa yao ndilo jambo kubwa sana wanaloweza kufanya kwa ajili ya watu wao.

Tunawaalika mje msikilize pamoja nasi ile Sauti yenye nguvu ya Neno lililo Hai Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) tunapoisikia ikifunua:  Kufunuliwa Kwa Mungu 64-0614M.

Ndugu. Joseph Branham

24-0211 Tazama Aliko Yesu

UJUMBE: 63-1229E Tazama Aliko Yesu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Mbegu Iliyorutubishwa,

Je! mwaweza kuwazia jinsi gani ingekuwa ni jambo la kupendeza kuketi na kumsikia malaika-mjumbe wa saba wa Mungu akiwaambia jinsi ambavyo hakujiepusha na kuwahubiria habari ya Kusudi lote la Mungu? Akiingia kwa undani sana kuhusu Mvuto wa Tatu, na kuwahakikishia jinsi ambavyo sasa ulivyothibitishwa?

Jinsi Mungu alivyonena na kindi wakatokea; kama vile tu alivyomnena kondoo dume kwa ajili ya Ibrahimu. Jinsi ambavyo Sauti ile ile ilivyomwambia amweleze maskini dada mnyenyekevu aitwaye Hattie, ambaye aliyesema neno sahihi, na kumwambia ya kwamba Sauti ile ile ambayo ilinena kuhusu wale kindi wakawepo ilisema ampe kile alichotaka na aone kama hakitatokea mara moja.

Jinsi ambavyo siku moja wakati alipokuwa akiwinda nyikani pamoja na rafiki zake, dhoruba kali ilitokea ambayo ingemlazimu kuondoka. Lakini jinsi Mungu alivyozungumza naye, mdomo kwa sikio, na kusema, “Niliumba mbingu na nchi. Nilituliza zile pepo zenye nguvu juu ya bahari.”

Jinsi alivyoruka juu na kuvua kofia yake wakati ile Sauti ilipomwambia, “Iambie tu dhoruba, nayo itakoma. Lo lote utakalosema, hivyo ndivyo itakavyokuwa.”

Yeye kamwe hakuihoji hiyo Sauti, bali alinena na kusema, “Dhoruba, koma. Nawe, jua, waka kama kawaida kwa siku nne, hadi tutakapokuwa tumetoka hapa.”

Kabla hajamaliza kusema hayo, ile mvua ya theluji, theluji na kila kitu kilisimama. Jinsi ambavyo katika dakika moja jua kali lilikuwa linawaka mgongoni mwake. pepo zilibadilika na mawingu, kama kitu cha siri, yakiinuka juu angani, na jua lilikuwa linawaka katika dakika chache.

Kisha angewaambia ambavyo miaka 16 kabla hata haujadhihirika, Mungu alimwonyesha kulikuwa na uvimbe kwenye kifuko cha kushoto cha mayai cha Dada Branham, na kwa nini huo ulikuwepo pale. Jinsi walivyoomba na kuomba Mungu auondoe. Ndipo, akatambua kuwa ni Mungu tu anayeijaribu imani yao.

Ndipo tu kabla haujaondolewa kwa upasuaji, alikuwa akizungumza na Mungu na Kumwambia jinsi gani amekuwa mke mzuri sana kwake. Jinsi ambavyo hakuwahi kulalamika kuhusu yeye kutokuwepo nyumbani. Jinsi ambavyo daima alivyotayarisha kila kitu kwa ajili yake wakati alipotaka kwenda kuwinda, kupumzika na kuzungumza na Bwana.

Kisha akasikia kitu fulani chumbani. Alipoinua macho, ile Sauti ikasema, “Simama,” na kumwambia, “Basi lolote utakalosema, hivyo ndivyo itakavyokuwa.”

Alisubiri kwa dakika moja tu, kisha akasema, “Kabla mkono wa daktari haujamgusa, Mkono wa Mungu utaondoa ule uvimbe, na hata hautaonekana.”

Sekunde moja kabla ya mkono wa daktari haujaweza kumgusa, aliponywa. Jinsi daktari alivyomwambia, “Ninataka kukuhakikishia, Bibi Branham, ya kwamba huo uvimbe haupo. Huna uvimbe wowote.”

Jinsi lilivyo Kamilifu Neno la Bwana!

Kumsikia Yeye akiwaambia hakuna shaka tena niani mwake, anajua ule Mvuto wa Tatu ni nini, na anajua unayotenda. Kwa maoni yake, utakuwa kile kitu ambacho kitaanzisha ile imani ya Kunyakuliwa, kwa ajili ya kuondoka.

Kwetu sisi ni kuwa na kicho, na kukaa kimya tu, kwa kuwa ile saa itawadia hivi karibuni ambapo Mungu atatutendea mambo fulani makuu. wakati huo ujapo, wakati kule kufinywa kutakaposhuka, ndipo mtaona, yale mmeona kwa kitambo, yakidhihirishwa katika ule utimilifu wa nguvu zake.

Tutakuwa na baraka hiyo kuu Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA., saa za Jeffersonville. ( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) Ningependa kuwaalika kuungana pamoja nasi tunaposikia: Tazama Aliko Yesu 63-1229E.

Hatutakusanyika pamoja ili kumsikiliza mwanadamu; kuna watu wengi sana barabarani, na wote wanafanana. Hatutakuwa tunatazama na kusikia mhudumu tu, ama mchungaji, tutakuwa tukimtazama na kumsikiliza Yesu. Tutaungana pamoja kutoka ulimwenguni kote kumsikia Yule Mtu, Yule Mtu wa Mungu, Yule Yesu wa Nazareti wa mwili, akiwa Mungu, akinena na Bibi-arusi Wake.

Yakubidi ujiulize mwenyewe, unatazama nini leo? Unaona nini unapotazama? Unaweza tu kumwona Yeye unapomtazama Yeye kupitia kwenye Neno.

Alichokuwa wakati alipotembea Galilaya, ni jambo lile lile alilo huku Jeffersonville, jambo lili alilo kwenye Maskani ya Branham. Unaangalia uone nini, mwanzilishi, mtu wa kimadhehebu? Hutaona jambo hilo katika Yesu. Unatazama umwone mtu mkuu wa kikasisi? Hutaona jambo hilo katika Yesu. La. Unamwonaje Yesu? Kwenye Neno la Mungu likidhihirishwa, kwa maana Yeye alikuwa Neno la Mungu lililodhihirishwa. Alivyokuwa wakati huo, ndivyo alivyo usiku wa leo, na atakuwa hivyo milele.

Mtazame Yesu hivi sasa upate kuishi;
Kwa maana imeandikwa katika Neno Lake, haleluya!
Ni kwamba tu “tunatazama na kuishi.”

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma ili kujitayarisha kusikiliza Ujumbe:

Hesabu 21:5-19
Isaya 45:22
Zekaria 12:10
Yohana 14:12

24-0204 Yupo Mtu Hapa Anayeweza Kuiwasha Taa

UJUMBE: 63-1229M Yupo Mtu Hapa Anayeweza Kuiwasha Taa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Sura ya Yesu Kristo,

Watu wanafikiri sisi ni wendawazimu, tunavyoketi katika nyumba zetu na makanisa, kuzisikiliza kanda. Wanafikiri tunakufa kwa njaa. Hawatambui kuwa tumeketi katika uwepo wa Nuru ya Mwana ya Agosti , tukiivishwa, na kulishwa Chakula Kilichohifadhiwa kama ndama zizini.

Sisi ndio ile Ngano iliyoendelea zaidi, tuko tayari kulipokea. Ikiwa wanataka kuishi katika mapokeo yao, na waendelee. Sio SISI, sisi tunaishi katika Nuru ya siku yetu.

Nuru ya siku yetu ni nini? Mungu alimtuma ulimwenguni malaika wake wa saba mwenye nguvu kumwongoza Bibi-arusi wake. Yeye alikuwa nani? Alikuwa nabii. Yale aliyosema yalitimia. Yeye alikuwa Neno la Mungu lililodhihirishwa. Yeye alikuwa dhihirisho la Nuru ya Neno la Mungu. Yeye alikuwa Nuru ya Mungu kwa ajili ya siku hii.

Musa aliendelea tu hata hivyo, kwa sababu alikuwa ile Nuru. Alikuwa Nuru ya saa ile. Kile alichokuwa nacho, kilikuwa nini? Mungu akidhihirisha Neno Lake lililoahidiwa kupitia kwa Musa, na Musa alikuwa Nuru.

Eliya alikuwa Nuru…Alikuwa nini? Ile Nuru. Haleluya! Alikuwa Nuru, ile Nuru; alikuwa Neno la Mungu lililodhihirishwa.

Yohana, alipokuja duniani… Basi alipojitokeza Yesu alisema alikuwa Taa angavu inayong’ara. Haleluya! Kwa nini? Alikuwa Neno lililodhihirishwa.

Basi kulingana na Neno, Nuru ya siku yetu ni nabii wa Mungu, William Marrion Branham. Yeye yule aliaye katika nyika ya Babeli “Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake.”

Yeye alikuwa kutimizwa kwa Malaki 4:5, na Ufunuo 10:7. Yeye alinena tu na kusema, “itakuwa pale,” nayo ilikuwa pale, bila kitu chochote ndani yake. Hakuwa kamwe amempata kindi; hapakuwa na yeyote hapo. Yeye alisema tu, “Na iwe,” na ikawa.

Neno la Mungu halikosei, nalo halina budi kutimia. Tumeiona Nuru; Neno Lake aliloahidi kwa ajili ya siku hii. Limethibitishwa na kuhakikishwa ya kwamba ni Kweli. Ni Nuru ya saa hii.

Hakuna kibadala katika kujua kile tunachosikiliza ni Neno lililodhihirishwa kwa ajili ya siku hii. HALINA WAFURUKUTA MIKIA NDANI YAKE… HATA CHEMBE. Ikiwa wengine watosheka na kitu kingine, na waendelee, lakini sio sisi.

Haimaanishi kuwa huwezi kumsikiliza mchungaji wako, ama kwamba mhudumu hawezi kuhubiri; sivyo hata kidogo, lakini LAZIMA uchuje kila neno unalosikia kupitia chujio kuu la Mungu, UJUMBE HUU KWENYE Kanda.

Wanaposema siku za Ujumbe wa mtu mmoja zimepita, hao ni WAFURUKUTA MKIA. Wanaposema Ujumbe huu sio Yakini yao, hao ni WAFURUKUTA MKIA. Wanaposema kusikiliza kanda haitoshi, hao ni WAFURUKUTA MKIA.

Hakuna kitu kikubwa zaidi ya Kubonyeza Play tu, kujua unaweza kusema AMINA kwa kila neno. Hakuna mahali pengine unapoweza kufanya hivyo isipokuwa kusikiliza Ujumbe wa saa hii.

Sasa sisi ni sura ya Yesu Kristo kwa ajili ya siku hii. Sisi ni Neno Lake lililodhihirishwa. Sisi ndio wale aliowachagua kupokea Ufunuo Wake mkuu wa wakati wa mwisho. Sisi ndio BIBI-ARUSI WAKE.

Ni Bibi-arusi Wake peke yake ndiye atakayekuwa na Ufunuo wa kweli wa Nuru ya siku hii. Watajua, Nuru hii itawakamilisha. Nuru hii ni Roho Mtakatifu akinena kupitia malaika-mjumbe Wake.

Je! ungependa kuketi katika uwepo wa Nuru ya Mungu ya saa hii? Basi ninakualika uje uungane nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA saa za Jeffersonville,( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) tunaposikia  Yupo Mtu Hapa Anayeweza Kuiwasha Taa 63-1229M.

Ndugu. Joseph Branham.

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Mwanzo 1:3, Sura ya 2
Zaburi 22
Yoeli 2:28
Isaya 7:14, 9:6, 28:10, 42:1-7
Mathayo 4:12-17, Sura ya 24 na ya 28
Marko Sura ya 16
Ufunuo Sura ya 3

24-0128 Aina Tatu Za Waamini

UJUMBE: 63-1124E Aina Tatu Za Waamini

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Mwamini,

Jinsi inavyopendeza kusema, MIMI NI MWAMINI. Si wa kanuni za imani; Neno! Si wa madhehebu; Neno! Si wa kile anachosema mtu mwingine; bali kile lisemacho Neno!

Sisi hatuulizi kitu, tunaliamini tu. Haidhuru Linasikika namna gani ama lolote mtu ye yote asemalo juu yake, sisi ni waamini halisi. Tuna ufunuo wa kiroho wa Neno.

Tunaiona ile saa tunayoishi. Tunauona ule Ujumbe wa saa hii. Tunamwona yule mjumbe wa saa hii. Tunamwona Mungu akijifunua Mwenyewe katika Neno Lake. Tunaona hakuna kitu kingine ila Ujumbe Huu, Mjumbe Huyu, Neno Hili.

Mwamini halisi hasikii kitu ila Neno. Hakuna zaidi. Yeye huliangalia Neno. Hatafuti mianya. Yeye hatafuti viinimacho. Anamwamini Mungu, na hilo latosha, naye anaendelea tu. Mnaona? Huyo hapo mwamini.

Sisi hatuwezi kusikia kitu kingine ila Neno; Neno linalomjia nabii peke yake. Si mianya, si fasiri ya mtu fulani, Neno Safi lililonenwa na kuwekwa kwenye kanda kwa ajili ya Bibi-arusi.

Roho amelihuisha Neno hilo ndani yetu nalo limekuwa hai. Kwa imani, tunaliona na kuliamini. Itakuja sauti kutoka Mbinguni ambayo italeta ubatizo mkubwa sana wa Roho Mtakatifu katika Bibi-arusi, ambao utatuondoa duniani, katika Neema ya Kunyakuliwa. Mungu aliahidi jambo hilo.

Tunawekwa majaribuni kila wakati, kila siku. Shetani anajaribu kutuambia majaribu na mitihani yetu ni Mungu anatuadhibu. Lakini MUNGU ASIFIWE, sivyo ilivyo, ni Shetani anayefanya jambo hilo naye Mungu analiruhusu.

Mungu anatujaribu, na kutufinyanga ili aone kile tutakachofanya. Jaribio huja kututikisa, kutuweka kule chini kabisa, kuona mahali tutakaposimama. Lakini tunashinda kila vita, kwa kuwa sisi ni mifano iliyo hai; Neno la Mungu linaishi ndani yetu na kupitia kwetu.

Sisi tuna umuhimu jinsi gani machoni pake?

Hakuna mtu anayeweza kupachukua mahali pako, haidhuru ni padogo namna gani. Unasema, “Mimi ni mke wa nyumbani tu.” Hakuna mtu anayeweza kupachukua mahali pako. Mungu, katika uchumi Wake mkuu, ameweka jambo hilo hivyo, Mwili wa Kristo, katika utaratibu, hata hapana mtu anayeweza kupachukua mahali pako.

Hilo ni lakupendeza jinsi gani? Kila mmoja wetu ana mahali. Kila mmoja wetu alikuwa hapa wakati Mungu aliponena ulimwengu ukawa. Aliweka mwili wetu hapa wakati huo huo. Mungu alituweka sisi duniani katika wakati huu ili kulitimiza Neno lake na kutupa Uzima wa Milele.

Kila mmoja anapaswa kufanya uamuzi. Unasimama wapi kuhusu Neno hili, Ujumbe huu, mjumbe huyu? Ni muhimu jinsi gani kulisikia Neno linalonenwa kwenye kanda?

Kwenye sehemu mbalimbali ulimwenguni, kanda hizi zinakopita, huduma za kanda.

Ni huduma ya kanda iliyotumwa kwa Bibi-arusi Wake ulimwenguni kote kutoka kwa Mungu. Inakuambia mahali ulipo hasa, wewe ni nani, na iwapo wewe ni mwamini katika Neno.

Wewe umo katika moja ya tabaka hizi. Katika hali yako ya sasa hivi, hali yako ya sasa ya akili, kwamba, ninyi mlio hapa katika mkutano huu unaoonekana, nanyi mtakaokuwa katika mikutano isiyoonekana ya kanda hii, hali yako ya sasa ya akili baada ya kuisikiliza kanda hii, inakuthibitishia uko katika tabaka gani.

Baada ya wewe kusikiliza kanda hii, inathibitisha uko katika tabaka la watu gani. Baadhi wanaamini unahitaji zaidi ya Neno safi tu lililonenwa kwenye kanda. Wengine wanaamini kwamba siku za Ujumbe wa mtu mmoja zimepita; ni lazima umsikilize mchungaji wako vinginevyo umepotea.

Mgawanyiko mkuu sana katika Ujumbe siku hizi ni umuhimu uliowekwa katika kuzisikiliza kanda. Baadhi wanafundisha kuwa ni makosa kuzicheza kanda kanisani; ni mchungaji pekee yake ndiye anayepaswa kuhudumu. Wengine wanasema kuna ulingalifu, lakini kamwe hawazichezi kanda kanisani, na kama wakizicheza ni mara chache sana.

Kulivyo na mitazamo mingi, mawazo mengi, fasiri nyingi za Neno, ni nani aliye sahihi? Ni yupi utakaye mwamini? Hilo ndilo swali ambalo kila mmoja wetu anapaswa kujiuliza.

Nabii alituambia tulichunguze kwa NENO, sio yale mtu yeyote asemayo. unalifanyaje jambo hilo? KUNA NJIA MOJA TU PEKEE ya kufanya jambo hilo, BONYEZA PLAY.

Lazima kuwe na jibu sahihi, njia sahihi. Kila mtu lazima aamue mwenyewe. Jumapili hii itaamua wakati ujao wa wote wanaosikia Ujumbe huu.

Jambo unalopaswa wewe mwenyewe kujiuliza: Ni nani pekee aliye na Bwana Asema Hivi? Nguzo ya Moto ilimthibitisha nani? Ni nani atakaye tutambulisha kwa Yesu? Ni nani aliyenena Neno la kutokukosea? Ni maneno ya nani yaliyonenwa duniani yalikuwa muhimu sana, yakarudisha mwangwi mbinguni?

Iwapo ungependa kupata majibu sahihi, ningependa kukualika uje kusikiliza Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) kusikiliza Ujumbe:   63-1124E —Aina Tatu za Waamini.

Ndugu. Joseph Branham

Yohana Mtakatifu 6:60-71