22-0612 Kukata Tamaa

UJUMBE: 63-0901E Kukata Tamaa

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa wa Mungu waliofungwa kwa Damu, waliofungwa kwa Ile Ishara, watu wa Agano.

Kumbuka tu, sisi si Hawa, sisi si mmoja wa hawa wenye mashaka wanaopatana na Shetani. Tuna imani isiyotikisika katika Neno hili! Tunashikilia kila Neno la Mungu aliloandika na kunena kwenye kanda. Imetupa IMANI KAMILIFU .

Hatutafuti imani fulani kubwa inayotulazimu kuwa nayo ndani yetu wenyewe . Hatujaribu kuwa wema vya kutosha; hatutawahi kamwe kuwa wema vya kutosha, tutashindwa kila wakati. Hilo silo alilotuambia tuwe na imani nalo. Alisema iweni na imani na kuamini KILA NENO alilosema kuwa ni Bwana Asema Hivi. TUNAAMINI HIVYO na Imetupa IMANI KAMILIFU KATIKA NENO LAKE.

Hebu tusikilize kile ambacho Roho Mtakatifu amekuwa akiripoti na kumwambia Baba kutuhusu sisi.

“Nimetii amri zako. Nilitafuta na nimepata baadhi ya vikundi vidogo vya watu waliotawanyika kote ulimwenguni. Nilituma vijana wa kanda Majumbani kwao na kucheza kanda chache. Waliposikia kanda hizo, waliamini kila Neno. Sasa wamezifanya nyumba zao kuwa kanisa wapate kuupokea Ujumbe huu. Wao ni Tai Wako waliochaguliwa tangu asili wanaokusanyika Pamoja kusikia Neno Lako.

Niliwaambia ya kwamba wote ambao wangekuja chini ya ile Ishara, Ujumbe wa wakati huu, wangeokolewa. Niliwaambia wawe Mmoja na Wewe na Neno Lako. Kama ilitenda kazi kwao, basi waiweke kwa watoto wao Ishara hiyo. Waiweke kwa wapendwa wao na kuwaleta chini ya hiyo Ishara na wao pia wataokolewa.

Niliwaambia waliokuwa Wakisikiliza kanda: Ninawadai kwa Mungu. Waliliamini nilipolisema jambo hilo, kwa mioyo yao yote na nafsi zao zote. Wao ni watu wangu, ndio niwapendao wanaosikiliza kanda hizi.

Niliwaambia angalieni kile Kilichokuja baada ya ile Mihuri Saba: ule muungano wa watu, ishara zilizounganika, kimulimuli chekukundu katika siku za mwisho, Zimetiwa kifuniko katika kitu hiki kimoja, ile Ishara.”

Loo, Kanisa, amka na ujitikise! Finya dhamira yako, amka katika saa hii! Hatuna budi kukata tamaa ama tutaangamia! Kuna jambo linalokuja kutoka kwa Bwana! Ninajua jambo hilo kwamba ni BWANA ASEMA HIVI. Kuna jambo linalokuja, na ni afadhali tukate tamaa. Ni kati ya uzima na mauti. Litapita katikati yetu wala hatutaliona.

Nasi tunajua jambo fulani liko karibu kutukia. Kule Kuja kwa Bwana kutakuwa ni kuondoka kwa ghafla, na kwa siri. Tumekata tamaa. Wakati umekaribia. Tumeitambua ile Ishara kwa ajili ya siku yetu nayo imewekwa.

Tunachukua Mifano ya Pasaka Jumapili hii ambayo ililiwa kwa dharura, katika Nyakati za kukata tamaa. Tunakusanyika ulimwenguni kote, kulizunguka Neno Lake.

Njoo uwe sehemu ya tukio hili kuu Jumapili hii saa 10:00 KUMI JIONI , saa za Jeffersonville,( Ni Saa 5:00 TANO USIKU ya Tanzania?) tunapokusanyika ili kusikia Neno: 63-0901E _ KUKATA TAMAA .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada :

Kutoka 12:11
Yeremia 29:10-14
Luka Mtakatifu 16:16
Yohana Mtakatifu 14:23
Wagalatia 5:6
Yakobo 5:16