23-1231 Kukata Tamaa

UJUMBE: 63-0901E Kukata Tamaa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Baba mpendwa,

Tumecheza muda mrefu vya kutosha. Tumehudhuria kanisa muda mrefu vya kutosha. Tangu kuusikia Ujumbe, ile Ishara, imemtupa Bibi-arusi Wako katika hali ya kudhikika.

Tunajua jambo fulani linakaribia kutukia. Wakati umekaribia. Tunataka Uje ututoe katika ulimwengu huu. Tunataka kuwa pamoja na Wewe. Tunahisi hali ya kudhikika ndani kabisa ya nafsi zetu.

Je! hivi tutalizungumzia tu? Je! tumedhikika vya kutosha? Je! tunakulilia Wewe mchana na usiku kama tunavyopaswa?

Loo, Kanisa, amka na ujitikise! Finya dhamira yako, amka katika saa hii! Hatuna budi kukata tamaa ama tutaangamia! Kuna jambo linalokuja kutoka kwa Bwana! Ninajua jambo hilo kwamba ni BWANA ASEMA HIVI. Kuna jambo linalokuja, na ni afadhali tukate tamaa. Ni kati ya uzima na mauti. Litapita katikati yetu wala hatutaliona.

Tunajua inahitaji hali ya kudhikika kukuleta Wewe jukwaani. Hatuna budi Tulipate sasa hivi ama tuangamie. Bwana, tujalie tudhikike kuliko hapo awali, ndipo utajitokeza jukwaani na kuja kumchukua Bibi-arusi Wako anayengoja.

Tusaidie Baba kujiingiza kwa nguvu. Si kutembea tu na kuingia ndani Yake kwa urahisi, bali kujiingiza ndani yake kwa nguvu. Sio tu kulizungumzia na kuendelea na maisha yetu ya kila siku. Tunataka kukutafuta kwa mioyo yetu yote, kwa roho zetu zote na kwa akili zetu zote. Bwana, tusaidie.

Tunajua tumekukosa mara nyingi, Bwana, lakini ulituambia kama tukishindwa, hilo halina uhusiano wo wote na jambo hilo; sisi ni wenye kushindwa kwanza, lakini tuna Wewe umesimama hapo na mkono wenye nguvu na unaweza kutushika chini na kutuinua juu ya maji.

Nabii alitutangazia ya kwamba Wewe ungepita juu yetu wakati tu unapoona ile Ishara ikiwa imewekwa. Bwana, tumefuata maagizo Yako na tumeiweka ile Ishara na kufanya nyumba zetu kuwa Kanisa la Kanda, tukisikiliza na kuamini kila Neno.

Yeye hutambua tu I—Ishara. Huo ndio Ujumbe wa wakati huu! Huo ndio Ujumbe wa siku hizi! Huo ndio Ujumbe wa wakati huu! Katika Jina la Yesu Kristo, upokeeni!

Sisi tuna Hakika kabisa, na tunaamini na kuweka kila kitu kulingana na yale nabii aliyotuambia.

Tunaamini kila kitu kinafanyika na hutokea kwa wakati Wako mkamilifu. Hakuna kitu kilicho nje ya mahali. Tumeiona miujiza Yako yote, nasi tumesikia na kuja chini ya ushahidi wa ile Ishara.

Sasa wakati tukiwa chini ya ushahidi wa ile Ishara, tutaula Ushirika Jumapili hii katika hali ya kudhikika. Kwa maana tunajua Wewe uko tayari kutoa hukumu.

Jalia tuule kama mfano wa Pasaka, wakati ilipoliwa kwa dharura, katika wakati wa kudhikika. Tupo katika kudhikika tena leo Baba.

Tunashukuru, Bwana, kwamba tunaweza kutazama nyuma kwenye mwaka huu na kuona yote ambayo umetufanyia. Umelifunua Neno Lako na kutupa Ufunuo juu ya Ufunuo kuliko hapo awali.

Sasa tunajua sisi ni wana na binti Zako. Sisi ndiye Bibi-arusi-Neno kamilifu Wako ambaye Umemngojea kwa muda mrefu sana. Ni Wewe, unayeishi na kukaa ndani yetu. Ulituchagua, ukatujua sisi tangu zamani na sasa unakuja kutuchukua.

Bwana, jalia tukutafute mchana na usiku. Na tuwe wenye kudhikika sana kukulilia Wewe. Jalia tujiingize kwa nguvu zaidi ya tulivyowahi kufanya hapo awali. Huu ukawe ndio mwaka wewe utakaokuja kutuchukua. Tunakupenda Baba, na tunataka kuwa katika Mapenzi yako makamilifu. Njoo uwe nasi tunapoungana saa 11:00 KUMI NA MOJA JIONI, saa za Jeffersonville, kuizunguka Sauti Yako na kukusikia Wewe ukituambia jinsi ya kuingia katika : Kudhikika (Kukata Tamaa) 63-0901E. Kisha uwe pamoja nasi tunaposhiriki katika kudhikika, Meza ya Bwana.

Hizi ndizo siku kuu za maisha yetu Baba. Kwa maana tunajua Unakuja upesi kutupeleka kwenye Makao yetu ya Baadaye pamoja nawe. Tunatazamia kila siku kwa hamu kubwa wale watakatifu ambao wametutangulia. Tunajua pindi tuwaonapo, ule wakati wa kuja kwako umefika….UTUKUFU!!!

Tuko katika hali ya Kudhikika kwa ajili ya siku hiyo, Baba.

Ndugu. Joseph Branham.

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Kutoka 12:11
Yeremia 29:10-14
Luka 16:16
Yohana 14:23
Wagalatia 5:6
Yakobo 5:16