24-0225 Wa Kipekee

UJUMBE: 64-0614E Wa Kipekee

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Marafiki Wapendwa,

Ni saa 6:00 SITA MCHANA huko Jeffersonville, saa 1:00 MOJA JIONI huko Afrika, saa 4:00 NNE ASUBUHI huko Arizona; Bibi-arusi wamekusanyika pamoja kutoka ulimwenguni kote. Tumesubiri wiki nzima kuufikia wakati huu. Tuko chini ya matarajio makubwa, tukimngojea Mungu aseme nasi kupitia midomo ya mwanadamu kwa njia ya malaika-mjumbe Wake wa saba mwenye nguvu. Tunaomba, “Bwana nitayarishe, unitie mafuta, na unipe Ufunuo zaidi wa Neno Lako.”

Tumeridhika, kwa maana tunajua hakika, ya kwamba nabii, na nabii peke yake, ndiye aliye na Maneno ya Uzima ya saa hii. Huenda tusiweze Kulieleza lote, lakini tunajua tunaamini kila Neno na tunalitegemea Hilo.

Tunajua, kama vile Bwana alivyofanya na Musa, Mungu Anajiandaa kumtukuza nabii wake mbele zetu. Wakati huo, Yeye aliitikisa tu milima. Wakati huu, Yeye Anazitikisa mbingu na nchi.

Ule wakati umefika. Mioyo yetu inaenda mbio ndani yetu. Tunausikia wimbo wetu wa Taifa umeanza kucheza. Kwa moyo mmoja, Bibi-arusi kutoka ulimwenguni kote wainuka kwa miguu yao na kuanza kuimba, AMINI TU , yote yawezekana, Amini Tu. Mungu anajiandaa kuzungumza nasi.

Tunasikia: “Habari za asubuhi marafiki.”

Mioyo yetu inafurahi kusikia tu maneno haya 3 rahisi. Nabii ametoka kuniita mimi rafiki yake. Kisha anatuambia,

Ninawakosa ninyi nyote. Si—sijali ninapokwenda, ni—ni…si, si ninyi. Nina marafiki, kila mahali ulimwenguni, bali si—si ninyi nyote. Kuna kitu fulani kuhusu kundi hili dogo ambalo lina ninino tu…Sijui. Mimi huwafikiria…Sina ku—kundi fulani ulimwenguni, nilijualo, linaloshikamana nami kama kundi hili. Mungu na—na ajalie tuwe wasioweza kutengana sana, hata, katika Ufalme ujao, naomba kwamba tuwe huko pamoja; ombi langu.

Ni Ufunuo mkuu jinsi gani ambao Mungu atatufunulia leo? Tunaenda kusikia kitu gani? Labda tumelisikia mara nyingi, nyingi sana hapo kabla, lakini leo itakuwa tofauti, ni kama vile haijawahi siku yoyote hapo kabla.

Ni kitu gani? Chakula cha Mwaminio. Mkate wa Wonyesho kutoka Mbinguni tutakaousheherekea. Mkate wa Wonyesho ulio kwa ajili yetu tu, Bibi-arusi Wake. Ni Utukufu wa Shekina juu ya Mkate huo wa Wonyesho unaotufanya tusiharibike.

Hao walio nje hututazama na kuuliza, “Ninyi watu mnafanya nini? Mnasikiliza tu kanda? Ninyi ni Wa Kipekee kweli kweli.”

Utukufu!! Tunayo furaha sana, na tunamshukuru sana Bwana sisi kuwa Wa Kipekee; wapumbavu kwa ajili Yake na Neno Lake lililothibitishwa. Tunafurahi kuuambia ulimwengu, “NDIYO, NINAAMINI HUDUMA YA KANDA. NINAAMINI KUBONYEZA PLAY. NINAAMINI NDIO SAUTI ILIYO MUHIMU SANA UNAYOPASWA KUISIKIA. NDIYO, NINAAMINI KUZIRUDISHA KANDA MIBARANI.”

Wakati utaji wa mapokeo umeondolewa, unaweza kuona ya kwamba Mungu angali ni Mungu wa Neno Lake. Yeye angali anadumisha Neno Lake. Yeye ni ninii—Yeye ndiye Mungu, Mwandishi wa Neno Lake.

Haijalishi yale mtu yeyote afanyayo, ama asemayo, tunaliamini Hilo, na kisha tunalitendea Hilo kazi. Kama wewe hulifanyi Hilo, basi huliamini. Hauko nyuma ya pazia. Pazia hilo ni la mtu mmoja. Ujumbe huo ni mmoja.

Nami ninatumaini na kuamini ya kwamba—ya kwamba mmekuwa na ufahamu wa kiroho juu ya yale Mungu amekuwa akijaribu kuliambia Kanisa bila ya kulisema moja kwa moja. Unaona? Ni jambo, wakati mwingine, inatubidi kusema mambo kwa njia fulani kwamba iweze kupunguza, iweze kuwafanya wengine kutoka nje, wengine kuondoka, na wengine ku—ku—kutafakari. Lakini hilo linafanywa makusudi. Lazima lifanywe hivyo.

Neno lilifunuliwa kwa nabii wa Mungu. Hakuna cha kundi, Mafarisayo, ama Masadukayo, ama dhehebu fulani ama ukoo. Ni NABII! Mungu alimpata mtu mmoja. Hakupata mawazo mawili au matatu tofauti. Yeye alimchukua mtu mmoja. Ndiye aliye na Neno, na yeye peke yake.

Ndipo huenda ikawa kwamba wengine wangesema, “Unamaanisha Mungu angefanya jambo kama hilo makusudi?” Hakika alifanya. Angali anafanya.

Kama vile walivyosema mamia ya miaka iliyopita, tunasikia jambo lile lile leo hii: “Lakini kuna watu wengine hapa ambao Mungu amewaita.” Hiyo ni kweli. Na maadamu tu wanafuata na kwenda pamoja, ni Amina, bali wakati mtu anapojaribu kupiga hatua na kuchukua nafasi ya Mungu ambayo Mungu aliyompa nabii wetu, ambayo Yeye alichaguliwa tangu zamani na kuwekwa kwa ajili ya kazi hiyo, inatubidi kukaa na Neno lililothibitishwa, ile Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku yetu.

Angalia, kifo, kukaa mbali Nalo sasa. Huna budi kuingia ndani Yake kupitia kwenye pazia hili, la sivyo hutaingia. Jinsi ambavyo Mungu angeweza kuwarehemu, bali kumbukeni vile ilivyokuwa, ya kwamba Mungu anadhihirisha kile kilichokuwa nyuma ya lile pazia. Angalieni kile kilichokuwa nyuma ya pazia, hilo Neno! Lilifunika nini? Neno! Ilikuwa ni kitu gani? Liko kwenye sanduku. Lilikuwa ni lile Neno ambalo lile pazia lililificha. Mnaona? Naye Yesu alikuwa ndiye Neno hilo, Naye Ndiye hilo Neno, nalo pazia la mwili Wake lililificha.

Kwetu sisi, ni udhihirisho! Sio neno tena, ni uhalisia! Amina!

Tunajua kwa wengine sisi ni Wa Kipekee, na linaweza likasikika kama nati kwa ulimwengu, lakini linawavuta watu wote Kwake.

Njoo uingizwe kwenye Neno pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) tunapomsikia nabii akiuambia ulimwengu jinsi sisi tulivyo Wa Kipekee 64-0614E. Tunajivunia na tunashukuru sana kusema ndivyo sisi tulivyo.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

I Wakorintho 1:18-25
2 Wakorintho 12:11