23-1001 Kutoka Kwa Tatu

UJUME: 63-0630M Kutoka Kwa Tatu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Kutoka,

Mambo haya tunayoyaona yakitukia leo yasingeweza kutokea miaka ishirini iliyopita, ama miaka arobaini iliyopita; ni leo tu ndio yanafanyika. Hii ndio ile saa! Huu ndio wakati! Sasa ndio wakati wake wa kutimizwa. Mungu aliliahidi, NA NDILO HILI HAPA.

Sisi tuna ufahamu wa kiroho; uovu wa taifa hili umetimia. Ile saa imefika. Ni wakati wa kwenda kwenye ile Nchi ya ahadi. Sio nchi nyingine tu ya kuendea, bali Makao yetu ya Baadaye ambayo tumekuwa tukiyangojea.

Hebu Wazia jambo hilo, kile kinachotuongoza ni zaidi ya nabii. Ni Mungu aliyedhihirishwa katika mwili miongoni mwetu, pamoja na Neno Lake kuthibitisha jambo hilo. Nabii ambaye aliyefanya mara elfu zaidi ya nabii mwingine ye yote. Ni Nguzo ya Moto inayotuongoza kwenda kwenye ile Nchi ya ahadi, Utawala wa Miaka Elfu.

Yeye alimchagua nabii wetu na akampa ishara ya kimbinguni ya Nguzo ya Moto, ili asikosee. Yale nabii aliyosema ni Maneno hasa ya Mungu Mwenyewe. Alimchukua nabii wetu, akamfundisha, kisha akamrudisha kwetu pamoja na ile Nguzo ya Moto, ili ajithibitishe Mwenyewe kwetu, na kutupa Ufunuo mkamilifu wa Neno Lake lote.

Kama tunataka kwenda kwenye hiyo Nchi ya ahadi, hatupaswi kusahau kamwe, Mungu hawezi, na hatabadilisha mpango Wake. Yeye ni Mungu, Naye hawezi. Alituambia Yeye kamwe hatajishughulisha na Kundi. Hajawahi kamwe. Yeye hutushughulikia kama mtu mmoja-mmoja. Yeye alituahidi katika Neno Lake angetutumia Malaki 4 atuongoze kwenda kwenye Nchi hii, Naye ametutumia.

Lakini, unaona, Ahabu alikuwa na mfumo aliodhani ulikuwa ni wa Bwana. Akasema, “Nina mia nne wa hao, walioelimishwa na kufundishwa.” Nao wanadai kwamba ni manabii wa Kiebrania, kama vile makundi ya wahudumu yanavyodhani siku hizi.

Wengi hawataki kulikubali, lakini kama Eliya wa kale, Mjumbe-malaika wa saba wa Mungu, mchungaji wetu, ndiye mchungaji wa ulimwengu wote kumwongoza Bibi-arusi Wake.

Yeye ni Malaki 4:5, na Ufunuo 10:7. Yeye ndiye kutimizwa kwa Maandiko yote ambayo Biblia ilitabiri kumhusu. Ni Ujumbe huu, Sauti hii, ambayo ni Sauti ya Mungu inayomwita Bibi-arusi Wake. Ndiyo Ramani ya Mungu kwa ajili ya siku hii.

Ni Nguzo ile ile ya Moto, kwa mfumo ule ule uliotiwa mafuta. Mungu yeye yule akifanya mambo yale yale.

Sasa Neno limefanyika mwili na linaishi kati yetu katika miili yetu, Bibi-arusi Neno Wake.

Hebu na tumlilie na kumshukuru, tumsifu, tumwabudu, kwa yote aliyotenda: Kutuokoa, kutuchagua tangu zamani, kutuhesabia haki.

Yale Anayotufanyia sasa hivi; Yanatupa Ufunuo na Ufunuo, akituambia sisi ni nani. Na yote atakayotufanyia…Kuja kutuchukua kuwa Bibi-arusi Wake na kutupeleka kwenye Makao yetu ya Baadaye Aliyotuandalia, na kuwa pamoja Naye katika Milele yote.

Chochote tunachohitaji, mlilie Yeye. Hilo ndilo analotaka watoto Wake wafanye. Kumlilia Yeye mpaka tumeridhika na kupata kile tunachokihitaji.

Njoo ukaungane na sehemu ya Bibi-arusi Wake Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa Jeffersonville, ( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) na umsikie mchungaji wa Mungu kwa ulimwengu, William Marrion Branham, akituambia yote kuhusu: Kutoka kwa Tatu 63-0630M.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Ujumbe:

Kutoka 3:1-12
Mwanzo Sura ya 37 yote
Mwanzo Sura ya 43 yote