23-0924 Kimulimuli Chekundu Cha Dalili Ya Kuja Kwake

UJUME: 63-0623E Kimulimuli Chekundu Cha Dalili Ya Kuja Kwake

PDF

pakua – mp3 (VGR dynamic audio)

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Asiye na Hofu,

ONYO!! ONYO!! Taa nyekundu inamemetesha. Kule kushushwa kwa pazia kumefika. Yatubidi tuweke kila kitu kando, KILA KITU, na tuwe tayari. Tumefika mwisho. Ule wakati ambao tulikuwa tukiungojea tangu mwanzo umefika. Unabii sasa unatimizwa.

Mungu alimwinua mjumbe-tai Wake mwenye nguvu juu sana katika mbingu kutazama miaka sitini ng’ambo ya mwaka 1963 hadi leo, Septemba mwaka 2023, kuyaona yote ambayo yangetendeka katika siku yetu… hali ambayo ulimwengu ungekuwemo, ukosefu wa uadilifu wa wanawake, kanisa na hali yake, wazimu wa watu; mwovu, kipofu, uchi, kahaba mkuu katika matawi yote ya serikali, ufisadi katika siasa, naye ametuonya ni yapi yangetukia.

Sasa tunaliona hilo likidhihirishwa mbele ya macho yetu vile hasa alivyotuambia ingekuwa. Sisi ndio wale walioyaona mambo haya yote yakitimia. Kila kitu kiko mahali pake. Limekuwa chungu kubwa mno la uchafu.

Ulimwengu wote uko katika hali ya hofu. Wanajua hakuna tumaini lililobakia. Inazidi kuwa mbaya kila siku. Hofu imetanda uso wa Dunia. Uchumi umekwisha, mauaji ya bila sababu, wanawake wanataka kuwa wanaume, wanaume wanataka kuwa mwanamke. Cho chote na kila kitu kinakubaliwa. kitu gani kinaweza kutokea wakati wo wote? Wanajua ni kama volkeno; Kitalipuka sekunde yo yote. Unaliona jambo hilo kwenye nyuso zao, katika matendo yao, HAKUNA TUMAINI, HOFU.

Hata makanisa yanayojiita ya Kikristo yanakumbatia watu waliobadili jinsia kuwa wachungaji, viongozi wa kiroho wa watu. Imekuwa mbaya zaidi kuliko Sodoma na Gomora. Shetani na ufalme wake wanaungana na kuwa kitu kimoja. Yeye amelifikia lengo lake.

LAKINI UTUKUFU KWA MUNGU, katikati ya mchafuko huo wote na hofu, Baba ametuhifadhi, SISI, kundi lake la watu teule, Bibi-arusi kipenzi Wake, salama Mikononi Mwake nasi tuna muungano wa Kiroho pamoja Naye zaidi ya wakati wo wote ule. Huu ni wakati mkuu zaidi wa maisha yetu. Ni ajabu. Ni tukufu. Ni la kimbinguni. Ni zaidi ya maneno ambayo tungeweza kueleza.

Miili yetu inafanyika Neno, nalo Neno linafanyika mwili; linadhihirishwa, linathibitishwa. Vile vile hasa Biblia ilivyosema ingetendeka katika siku hii, inatendeka, siku baada ya siku.

Mambo yanatukia na kutendeka upesi sana hivi kwamba hatuwezi hata kufuatilia jambo hilo. Tuko karibu sana na kule Kuja kwa Bwana wetu Yesu; kuunganishwa Naye, ambapo Neno linafanyika Neno.

Pamoja na mambo haya yote yanayotukia kutuzunguka pande zote, HATUJAWAHI KAMWE KUWA NA FURAHA, kuridhika zaidi ama kutosheka zaidi hivi. Mioyo na nafsi zetu zinabubujika kwa furaha isiyotamkika na iliyojaa utukufu. Ni kitendawili.

Tunapata faraja kuliko wakati mwingine wo wote ule, tukijua kwamba tangu mwanzo kabisa, tulichaguliwa tangu zamani kuwa mwana na binti wa Mungu.

SISI ni Bibi-arusi mwadilifu wa Kristo, aliyeoshwa kwa Damu ya Kristo. Mwana wa Mungu wa thamani, mwadilifu, asiye na dhambi akiwa amesimama na Bibi-arusi Neno asiye na doa, asiyeghoshiwa, aliyemwosha kwa Maji ya Damu Yake Mwenyewe. Sisi tulichaguliwa tangu zamani katika kifua cha Baba kabla ya mwanzo wa wakati; kama vile alivyokuwa Yeye ….UTUKUFU!! HALELUYA!

Sisi si hivyo tu tulivyo, lakini hivi karibuni tunaenda kwenye arusi huko mbinguni, tukiwa tumevaa utepe wa arusi ya waliochaguliwa tangu zamani. Alitujua SISI…Hebu tafakari tu juu ya hilo, ALITUJUA kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, kwa hiyo akatuvisha utepe wa arusi PALE na akaliandika JINA LETU KWENYE KITABU CHAKE CHA UZIMA CHA MWANA-KONDOO, si tu kusamehewa, bali KUHESABIWA HAKI.

Kuna njia moja tu ya kuwa na haya yote, yakubidi uje kwa Njia pekee iliyoandaliwa na Mungu. Neno la asili, BONYEZA PLAY.

Tunashukuru sana tunao Ufunuo huu. Ni wazi sana kwetu. Mwili na damu havikutufunulia jambo Hilo, lakini Baba yetu wa Mbinguni na hakuna maneno katika msamiati wetu wa kumwelezea jinsi tunavyompenda Yeye kwa ajili ya Jambo hilo….NEEMA YA AJABU.

Hakuna cha kulinganishwa na kuisikia Sauti ya Mungu ikikuzungumzia mdomo kwa sikio. Furaha inayofurika mioyo yetu. Hakuna kushangaa, hakuna kubahatisha, hakuna, hata si kutumaini, TUNAJUA, NI BWANA ASEMA HIVI. Huwezi kuwa na uhakika huo wa 100% mahali pengine popote isipokuwa kwenye kanda.

Ningependa kukualika uje uungane pamoja nasi tunapoisikia Sauti ya Mungu ikituambia yote kuhusu siku tunayoishi, wakati yeye anaponena kupitia nabii-tai Wake mwenye nguvu na kutuletea Ujumbe: Kimulimuli Chekundu cha Dalili ya Kuja Kwake 63-0623E.

Tutakusanyika kutoka kote ulimwenguni saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville ( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki). Kama huwezi kuungana nasi pamoja, popote pale ulipo, lo lote lile ufanyalo, Bonyeza Play na uyasikie Maneno ya Uzima wa Milele.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Mathayo 5:28 / 22:20 / Sura ya 24 yote
2 Timotheo Sura ya 4 yote
Yuda 1:7
Mwanzo Sura ya 6 yote