23-1008 Je, Maisha Yako Yanaistahili Injili?

UJUME: Je, Maisha Yako Yanaistahili Injili? 63-0630E

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa kundi la Nabii wa Mungu,

Tuombe.

Baba wa Mbinguni, jinsi tunavyoshukuru kwa ajili ya wakati mwingine wa kukusanyika pamoja kutoka kote ulimwenguni upande huu wa Umilele. Kuwa katika nia moja na umoja pamoja Nawe; tukiiskia Sauti yako ikituzungumzia. Tunatarajia kwa mara nyingine tena kuhuishwa upya kwa nguvu kuja kutoka Kwako, zipate kututia moyo na nguvu kwa ajili ya safari iliyoko mbele.

Tunakusanyika pamoja ili kuipokea Mana iliyotolewa kwa ajili yetu. Ile Mana ya kiroho uliyoihifadhi ili itupe nguvu kwa ajili ya safari. Ndilo jambo PEKEE linaloweza kutuhifadhi katika siku zijazo.

Ulituambia, kabla hujaliweka Kanisa Lako katika utaratibu, itabidi utukusanye pamoja, mahali pamoja, na kwa nia moja. Ndipo ungemtuma Roho wako Mtakatifu kwetu kwa ajili ya uongozi; si baraza fulani la ekumeni, si kundi fulani la watu, bali Roho Wako Mtakatifu atuzungumzie mdomo kwa sikio.

Wewe ulinena kupitia malaika wako na kutuambia:

“Ninawatakeni mkae na mchungaji wenu na mdumu na Mafundisho ambayo yamefundishwa hapa. Dumuni na Neno hili, msiliache! Dumuni moja kwa moja na Neno hata iweje, dumuni na Neno hilo!”

Baba, tunalitii Neno Lako nasi tunakaa na mchungaji wetu. Ni Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku hii tu ndiye anenaye Neno Lako lililo safi ambalo limethibitishwa na kudhihirishwa kwa ajili ya siku yetu.

Ulituambia kama ilivyokuwa katika siku za Sodoma, ndivyo itakavyokuwa katika Kuja kwake Mwana wa Adamu; kwamba tungekuwa na mambo mawili ya kutuongoza, na ulimwengu wote uliyosalia ungekuwa na mambo mawili. Mambo yao mawili walikuwa wahubiri wawili.

Lakini kwa ajili ya Kanisa Lako la kiroho, Bibi-arusi Wako mteule, aliyechaguliwa tangu zamani, mambo yetu mawili yangekuwa ni Wewe, kudhihirishwa katika mwili wa kibinadamu, kutuongoza kwa Nguzo ya Moto.

Acha upepo uvume vikali. Acha tufani itikise. Tuko salama, milele. Tunapumzika papo hapo kwenye Neno Lako. Wakati umefika. Kule kutoka kwa kiroho kumewasili. Tunatembea na kuzungumza nawe kila siku, tukisikia Sauti Yako. Tuko katika ushirika wa daima na Wewe.

Tunataka kuwa Mikono Yako, Macho Yako, Ulimi Wako. Wewe ni mzabibu, sisi ni matawi Yako. Tutie nguvu, Baba, ili tuzae matunda yako. Nia yetu pekee ni kuwa na maisha yanayoistahili Injili Yako.

Jihakisi Mwenyewe kupitia sisi, Baba, ili kuendeleza kazi Yako na kutimiza Neno Lako lililoahidiwa. Nia yetu ni kuwa wajumbe Wako wa siku hii, ili kuitimiza haki yote.

Tunataka kukusikia Wewe ukituambia:

Ombi langu ni kwamba, kwa wale walioko kwenye redio ama kwenye…kwenye maeneo ya kanda, na wale waliopo hapa. Mungu wa neema yote, wa Mbinguni, na atuangazie sisi sote Roho Wake Mtakatifu, kusudi sisi, tangu usiku huu, kuendelea, tunaweza kuishi maisha ambayo Mungu angesema, “Nimependezwa. Ingieni katika furaha za Milele ambazo zimewekwa tayari kwa ajili yenu tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu.” Mungu wa Mbinguni na atume baraka Zake juu yenu nyote.

UTUKUFU…hao ni sisi Baba, Bibi-arusi Wako katika maeneo ya kanda. Hakika Wewe unatutumia baraka zako na kutufunulia Neno lako, ukituambia kwa kila Ujumbe tunaousikia, Wewe umependezwa, SISI NI BIBI-ARUSI WAKO.

Ikiwa ungependa kumsikia mchungaji wetu, mchungaji wa Mungu kwa ulimwengu mzima ambaye Yeye alimtuma kumwita atoke na kumwongoza Bibi-arusi Wake, njoo uungane nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) kumsikia Yeye akinena Maneno ya Uzima wa Milele, anapotuletea Ujumbe kutoka kwa Mungu: Je, Maisha Yako Yanaistahili Injili? 63-0630E.

Ndugu. Joseph Branham

Tangazo Maalum: Bwana akipenda, Jumapili ijayo usiku, tarehe 15 Oktoba. tutakuwa na Ibada ya Ushirika ya nyumbani na Kutawadhana Miguu.