Category Archives: Uncategorized

21-1121 Kiu

UJUMBE: 65-0919 Kiu

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Mpendwa Bibi Mteule,

Muungano mkuu wa mwisho unafanyika kwa ajili ya Unyakuo. Roho Mtakatifu anamleta Bibi-arusi Wake pamoja kutoka katika mataifa yote; kutoka Pwani ya Magharibi hadi Pwani ya Mashariki, kutoka Kaskazini hadi Kusini, kutoka pembe nne za dunia.

Anatukusanya pamoja katika makanisa yetu na katika nyumba zetu kupitia Mawimbi Bora sana. Ni bora hata zaidi kuliko njia ya kurusha matangazo. Ni mawasiliano ya simu. Tunaweka vipokezi au maikrofoni, ama chochote kile, katika chumba, na ni sawa sawa tu na kusimama katika chumba pamoja na nabii Wake. Ni njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku hii kumuunganisha na kumleta Bibi-arusi Wake pamoja na, “Bwana Asema Hivi”.

Miaka hamsini na sita iliyopita, Mungu alianza mpango wake wa kuwakusanya Bibi-arusi Wake pamoja ili waweze kumsikia akinena kupitia malaika Wake mwenye nguvu kwa wakati mmoja. Hata aliifanya huduma tano yake kusitisha kuhudumu na kuwakusanya watu wao pamoja, nao Wakajiunganisha Kwa Radio katika makanisa yao, kwani alitaka Bibi-arusi Wake aisikie Sauti Yake wote kwa wakati mmoja. Mpango wake mkuu ulikuwa umeanza. Haijawahi kamwe kuwezekana katika historia ya ulimwengu. Nabii wake alijua jambo Hilo na alifurahishwa sana. Sasa Mungu angeweza kusema moja kwa moja na Bibi-arusi Wake wote kwa wakati mmoja. Wote wangeweza kusikia wenyewe, Mungu akizungumza nao moja kwa moja, na haingehitaji fasiri yoyote.

Leo, ulimwengu uko katika mshangao. Kwa nini watu kutoka duniani kote, wakiwa na majira tofauti ya maeneo Yao ; 6:00 sita mchana., 8:00 Nane mchana., 2:00 mbili usiku., usiku wa manane, wanakusanyika pamoja wote kwa wakati mmoja ili kusikia Ujumbe ambao wanaweza kusikiliza wakati wowote. Nini kinachovutia?

Imefunuliwa kwao kwamba huu ni mpango wa Mungu, njia iliyotolewa na Mungu ya kuwaunganisha kiroho. Ni Mungu akitayarisha kuzungumza na Bibi-arusi Wake wote kwa wakati mmoja.

HAKUNA kingine ila Sauti ya Mungu, Neno Lake, Ujumbe Huu, ulionenwa na nabii Wake ungeweza kufanya hivyo. Hakuna mtu, wala kitu kingine chochote, ambacho Bibi-arusi wote wanaweza kukubaliana kwacho.

Mtu fulani anaweza kusema, “Mimi humsikiliza mchungaji wangu anaponukuu na kuhubiri Neno kama tu vile Ndugu Branham alivyosema afanye.” Bwana asifiwe. Hilo ni zuri na umebarikiwa sana kuwa na mchungaji anayedumu na Neno. Ameitwa kuweka kundi pamoja na kukupa na kukuelekeza kwenye Neno, Lakini hilo silo ninalozungumzia. Huna budi kuwa na Yakini, Neno la mwisho. Maneno Ambayo SOTE TUNAWEZA KUKUBALIANA KWAYO. Kadiri alivyoitwa na kupakwa mafuta jinsi mtu ye yote awezavyo kuwa, hakuna neno la mtu yeyote ambalo ni kamilifu, na hakuna huduma ya mtu yeyote inayoweza kumuunganisha Bibi-arusi.

“Hilo ni wazo lako tu na maoni yako. Thibitisha hilo kwa Neno, Ndugu Joseph”.

Kwa sababu ukiwa na watu wawili, una maoni mawili . Yapasa kuwe na yakini Moja ya mwisho , na yakini yangu ni Neno, Biblia . kama mchungaji hapa wa kanisa, Yakini yangu ni Neno, nami ninataka … ninajua ninyi, ndugu zetu, kwa namna fulani
mnanichukua mimi kama Yakini yenu kwa yale…mradi ninamfuata Mungu kama Paulo alivyosema katika Maandiko, “Mnifuate mimi kama ninavyomfuata Kristo .”

Hivyo basi, wakati nabii anaponena, ni Yakini kwa Bibi-arusi. Ujumbe Wake si neno lake yeye, wala si fasiri yake yeye ya Neno. Ni Mungu akifasiri Neno Lake Mwenyewe kwa njia Yake pekee aliyoiandaa ya kufanya hivyo: kwa nabii Wake.

Ikiwa unasema unaamini Ujumbe Huu.
Ikiwa unasema unaamini nukuu hii.
Ikiwa unasema na kuamini kuwa wewe ni Bibi-arusi wa Kristo, Basi kile kilichonenwa kwenye kanda lazima kiwe Yakini Yako.

Hivi, ni nini kingine kinachoweza kumleta Bibi-arusi wa Kristo wote pamoja isipokuwa Yakini yetu? HAKUNA KINGINE. Hizo Kanda ni Sauti Yake, Neno Lake, Yakini Yetu. Nabii alituambia kwamba nabii Kwa ajili ya wakati huu ni Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu huchagua mtu MMOJA, Sauti MOJA kufunulia Neno Lake na Sauti hiyo inamuunganisha Bibi-arusi Wake kwa njia Yake aliyoiandaa kwa ajili ya siku hii, KWA KUBONYEZA PLAY .

Ninajaribu sana niwezavyo kudumu kwa unyofu na Neno , kwa ajili ya hawa ambao wamewekwa mikononi mwangu kwa ajili ya Mungu , maana kondoo huhitaji chakula cha kondoo, bila shaka. “Kondoo wangu huisikia Sauti Yangu.” Na hilo ndilo tunaloishi kwalo, kila Neno litokalo…Si yote…Si Neno moja mara hii na mara nyingine; bali kila Neno litokalo kinywani mwa Mungu, hilo ndilo ambalo watakatifu wanapaswa kuishi kwalo.

Tunapaswa kuishi kwa kila Neno litokalo katika kinywa cha Mungu. Je, kinywa cha Mungu kilichothibitishwa kwa ajili ya wakati huu ni kipi? Mimi? Mimi si Malaika- Mjumbe wa 7 wa Mungu aliyethibitishwa , wala kinywa Cha Mungu si mchungaji wako wala mtu ye yote yule; Ni Mungu akitumia sauti ya WILLIAM MARRION BRANHAM.

Tutahukumiwa kwa Ujumbe ALIONENA kwenye kanda. Si kwa Fasiri ya mtu mwingine ye yote ama kuhubiri kile alichonena, Bali kwa Neno KWENYE KANDA. Kama wapakwa mafuta na Roho Mtakatifu jinsi tuwezavyo kuwa, tunaweza kukosea. Sisemi muhudumu yeyote ni wa uwongo au amekosea; tumeitwa kuhubiri, na kufundisha, na kukaa na Neno, Lakini wito wetu ni kuwaelekeza ninyi KWENYE NENO, na NENO PEKEE LILILOTHIBITISHWA KIKAMILIFU liko kwenye Kanda.

Tunayo mengi sana, kama Bibi-arusi wa Kristo, ya kushukuru.

je kama tungaliijaza bahari kwa wino, Na kama mbingu zote zimetengenezwa kwa karatasi; Kama kila shina duniani lingekuwa ni kalamu, Na kila mtu awe kazi yake ni mwandishi; Kuuandika upendo wa Mungu aliye juu Kungeikausha bahari yote; Ama kama gombo hilo lingechukua nafasi yote, Hata kama limetandazwa kutoka mbingu hadi mbingu.

Tunakaribia kuwa na juma kuu la Shukrani la maishani mwetu.
Sikukuu ya Chakula cha Kiroho cha kujaza Nafsi. Sikukuu ambapo Bibi-arusi ataungana na kuketi pamoja katika Uwepo wa Jua kuivishwa.

Mungu atanena kupitia mjumbe wake na kutuambia:

. Sisi ni Bibi Mteule wake.

. Majina yetu yako kwenye Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo.

. Hatuna dhambi.

. Tulihesabiwa haki kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.

. Sisi ndio walioitwa watoke na wateule.

. Sisi ndio ambao mpango mzima wa Mungu umekuwa ukingojea.

. Sisi ni Bibi-arusi safi, mwema, asiye na dhambi wa Mwana wa Mungu aliye hai.

. Sisi ni wakamilifu mbele zake.

Hakuna mwisho wa kuyaandika yale yote ambayo Roho Mtakatifu anakwenda kutufunulia na kututendea.

Nena kuhusu Shukrani !!!

Nimehisi kushinikizwa katika Roho yangu kutoka kwa Bwana ili tuweke wakfu juma zima, kuanzia Jumapili hii, kwa ajili ya Shukrani kwa Bwana.

Iliyoambatishwa hapa ni kalenda yenye siku, masaa na Jumbe tutakazosikia.

Kama unavyoweza kuona, Jumapili sote tutaungana pamoja katika muda wetu wa kawaida wa saa 8:00 Nane mchana, saa za Jeffersonville, ( ni saa 4:00 nne usiku ya Tanzania) , ili kusikia Ujumbe: Kiu 65-0919.

Jumatatu Hadi Jumatano , ningependa tusikie Jumbe 3 zinazofuata ambazo Ndugu Branham alizileta katika mfuatano, mwaka wa 1965. Tutakuwa tukizituma kwenye Voice Radio (Radio ya Sauti, iliyopo kwenye app ya Lifeline ya vgr ) saa 3:00 tatu Asubuhi saa za Jeffersonville,( ni saa 11:00 kumi na Moja jioni ya Tanzania) na tena saa 1:00 Moja jioni, saa za Jeffersonville,( ni saa 9:00 Tisa usiku ya Tanzania).

Najua itakuwa vigumu kwa wengi kusikiliza kwa wakati uliowekwa kutokana na ratiba zao za kazi au majukumu mengine, lakini tunatumai mnaweza kusikiliza wakati mmojawapo Kwa pamoja na familia zenu.

Kisha Alhamisi , mwezi wa 11, tarehe 25, ningependa tuungane pamoja saa 8:00 Nane mchana, saa za Jeffersonville, ( ni saa 4:00 nne usiku ya Tanzania ) kuanza wikendi yetu nzuri ya Kutoa Shukrani tunapounganishwa tena ili kusikia Sauti ya Mungu ikituletea Ujumbe wa kwanza wa wikendi yetu: Muungano Usioonekana wa Bibi-arusi wa Kristo 65-1125.

Ilikuwa ni baraka ya pekee kwangu kutambua itakuwa miaka 56 iliyopita, hadi siku ya leo, ambapo Mungu alinena kupitia nabii Wake kutuletea mfululizo huu wa Jumbe. Ilikuwa pia miaka 56 tangu kuzaliwa kwa Ndugu Branham mwaka wa 1909, hadi mwaka wa 1965, ambapo alizinena Jumbe hizi.

Tungefanya nini kama tungejua Ndugu Branham atakuwepo Shreveport, LA wikendi hii ili kutuletea Jumbe hizi? Hakuna ….Namaanisha HAKUNA kitu kingaliweza kutuzuia kwenda. Mungu ana mpango kwa ajili ya Bibi-arusi Wake leo, na HAKUNA kitakachotuzuia.

Naamini kila mmoja wenu Yuko chini ya matarajio makubwa kwa juma hili zuri tutakalokuwa pamoja na Bwana; kumshukuru, kumsifu na kumwabudu kwa ajili ya yote aliyoyafanya, na yote anayokwenda kufanya kwa ajili ya kila mmoja wetu, BIBI MTEULE WAKE.

Ndugu. Joseph Branham

21-1114 Nguvu Za Mungu Za Kugeuza

UJUMBE: 65-0911 Nguvu Za Mungu Za Kugeuza

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai Wapendwa , hebu sote tukusanyike pamoja na kusikia Ujumbe  65-0911 Nguvu za Mungu za Kugeuza Jumapili hii saa 8:00 nane Mchana, saa za Jeffersonville.( Ni saa 4:00 nne usiku ya Tanzania).

Ndugu Joseph Branham

Maandiko ya kusoma:

Mwanzo Sura ya 4 yote

Isaya 9:6 / 14:12-14

Mathayo 5:6 / 24:24

Yohana Mtakatifu 1:1

Warumi 12:1-2

2 Wathesalonike 2:3-4

Waebrania 10:26-27

Ufunuo Sura ya 3 yote

21-1107 Edeni ya Shetani

UJUMBE: 65-0829 Edeni ya Shetani

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliyeangazwa,

Kama Siku ile iliyokwisha kupita, tulikuwa tumeunganishwa na Yeye akaja katika nyumba zetu na akawa pamoja nasi. Kote katika mataifa, sehemu ya Mwili wa Kristo, Ambayo nabii Wake amepewa haki ya kuilisha, waliketi pamoja katika ulimwengu wa roho Alipokuwa YEYE akisema nasi kupitia malaika Wake mkuu ambaye amemtuma; kuuangaza ulimwengu kwa Roho Wake Mtakatifu kupitia yeye, kumwita Bibi-arusi Wake atoke.

Mungu alituma, katika mlango huu wa 18, malaika mwenye nguvu, baada ya siri hiyo kujulikana, malaika mwenye nguvu, ama, mjumbe….

Mungu alimtuma malaika, mjumbe (kufanya nini?) kuwaita watoke. “Tokeni!” Ujumbe wa Wakati huu!…

Tokeni kwake! Mungu alituma wengi…malaika mkuu, ama, mjumbe. Na Nuru yake haikuwa kwenye maficho, iliangaza duniani kote… Kuiangaza nchi, na kuwaita watu Wake watoke kwake.

Sasa, mnajua jambo hilo ni Kweli. Mjumbe fulani alitumwa kutoka Mbinguni, kuwaita watu wa Mungu watoke Babeli. Na Nuru Yake ikaangaza nchi, Roho Mtakatifu aliye mkuu .

Wiki iliyopita mhudumu fulani aliliambia kusanyiko lake kwamba Mimi nilitaka watu waamini kwamba Ndugu Branham alikuwa ndiye malaika wa Ufunuo 18, lakini akadai kuwa huyo alikuwa ni malaika kutoka Mbinguni, na asingeweza kuwa Ndugu Branham. Kama huyo ndugu angalifanya tu kile nabii ALILOMWAMBIA afanye, kulichunguza jambo hilo kwa Neno, na SI kwa ufahamu wake, ANGESIKIA, KWAMBA KWA KWELI, ALIKUWA NI NDUGU BRANHAM ALIYESEMA YEYE ALIKUWA NDIYE MALAIKA HUYO .

…Angalia, huyu ni malaika wa Nuru, kumbukeni, malaika wa mwisho, ni malaika katika wakati wa kanisa wa Laodikia. Ni mjumbe wa Laodikia, huyo, ni wa mwisho, kwa kuwa mlango unaofuata tu ni mlango wa 19, ambao ni kuja kwa Bibi-Arusi .

Ndugu na dada zangu, NINACHUKIA kusema mambo haya na kuyabainisha. Kama vile Ndugu Branham asemavyo, “Naeleweka vibaya sana ”. Mimi Simaanishi kuwa ni wahudumu wote wanaosema mambo haya, wala siamini wahudumu wote ni wauongo, au hawapaswi kuhudumu. HAPANA, lakini walio wengi sana wanawadanganya watu kwa kuweka umuhimu zaidi katika huduma yao kwa kuhubiri Neno, badala ya kubonyeza play na watu wao na kusikia HASA kile nabii alichosema.

kama umechaguliwa tangu awali, unaliona. Hakuna njia ya kulificha toka kwako. Utaangalia na kusema, “ ni dhahiri sana mbele ya uso wangu! Ninaliangalia moja kwa moja. Ninaliona. Hili hapa, lile Neno; kila Neno, Neno kwa Neno. limedhihirishwa mbele yangu na nafsi yangu yote imefungamanishwa ndani yake.”

Hebu niwape nukuu hii ndugu zangu wahudumu, ambayo inaeleza yale tu mimi, na kanisa ambalo Bwana amenipa kuwa mchungaji, tunaamini kuhusu kucheza kanda kanisani.

Na sasa kumbukeni, kama hili linanaswa…Sijui. Siwezi kumwona ye yote. Naam, naweza, naweza kumwona Ndugu Terry kule kwenye—kwenye chumba cha kurekodia. Na kama hili linanaswa; kwa ajili ya wahudumu wo wote mahali po pote, wakati wo wote, hili halielekezwi kwa madhumuni ya kudharau mafundisho yenu, hili hata halielekezwi kwa kondoo wenu. Ujumbe huu, na Jumbe zote zingine ambazo ninazungumzia, zinaelekezwa kwenye kusanyiko langu. Si kwa ajili ya kusanyiko lako isipokuwa wawe wanataka kulipokea. Bali limeelekezwa kwa watu hawa hapa.

Watu hununua kanda hizi. Watu kila mahali ulimwenguni huzinunua na kuzicheza. Mara nyingi wananiandikia. Na sikuzote mimi huwarejesha, kama wao ni washiriki wa kanisa fulani, “ Mwoneni mchungaji wenu.”

Wananitazama Mimi kama mchungaji wao Wa mahali hapa , ndiomana ninawaambia, “NINAAMINI KUZIPOKEA KANDA NA KUBONYEZA PLAY . Ndugu Branham ndiye mchungaji wetu. Sisi ni sehemu ya Kusanyiko lake ”.

Sasa, ewe mchungaji , nataka ujue jambo hilo, ya kwamba, ninazungumza haya kwa ajili ya kusanyiko langu peke yake. Nami nina haki ya kutenda jambo hilo, kwa maana nimewekwa na Roho Mtakatifu kuwachunga kondoo hawa. Na ole wangu kama siwaambii ninayofikiria ni Kweli, na jinsi ninavyofikiri linakuja. Bali si kwa ajili ya ulimwengu wala kwa makanisa mengine. Ninyi fanyeni lo lote ambalo Mungu anawaambia mtende. Siwezi kuwajibieni, wala ninyi hamwezi kunijibia .
Lakini kila mmoja wetu hana budi kujibu mbele za Mungu, kwa ajili ya huduma yetu

Sina budi kujibu kwa Mungu kwa ajili ya huduma aliyonipa. Kwa kila hali ya utu wangu naamini ni lazima ucheze Sauti ya Mungu katika kanisa lako kwa njia ya Jumbe zilizorekodiwa . Ni njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku hii kuivisha Bibi-arusi Wake. Ndiyo njia PEKEE kwa Bibi-arusi kuunganishwa na kukamilishwa.

Ujumbe tutakaosikia Jumapili ulinenwa na kurekodiwa kwa ajili ya LEO HII. Ni Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati wake. Hebu na tufungue mioyo yetu ili Roho Mtakatifu aweze kututia mafuta ili tusikie kile alichokuwa anatuonya tutazamie katika siku hizi za mwisho.

Alitueleza roho zote mbili zitadhihirishwa kikamilifu katika siku hii ya mwisho. Alitueleza ingefanana sana hata ingewadanganya wateule kama yamkini. Siku hiyo ndiyo hii.

Angalia, wakati Yesu alipokuja—unaona, Shetani alikuwemo katika kundi lile la waalimu wa Kiyaudi na marabi na makuhani, akijaribu kuwaambia washike Torati ya Musa, ambapo Neno lenyewe lilisema—kwamba katika siku hiyo, Mwana wa Adamu angefunuliwa. Unaona? Kwamba angejifunua Mwenyewe . Kwa hiyo walikuwa wakijaribu…kadiri ambavyo waliwaweka wa kidini, na katika Torati ya Musa…unaona alilotenda ? Alikuwa akijaribu kuwaambia, “Sehemu hiyo ya Neno ni sawa kabisa, lakini mtu huyu siye mtu yule.” Unaona jinsi alivyo mdanganyifu ? Hiyo ndiyo hiyo siku yenyewe hasa ya udanganyifu.

HATUWEZI kudanganywa, sisi ni Bibi-arusi. Sisi NI watoto wa Mungu. Sisi NI sehemu ya sifa ya Mungu iliyokuwa ndani Yake, tulifanyika mwili kama vile Yeye alivyofanyika mwili, ili tuweze kuwa na ushirika sisi kwa sisi kama familia ya Mungu duniani. Hatulikumbuki jambo hilo kwa sasa, lakini tulikuwa huko. Alijua jambo hilo. Na alitaka tuwe hivyo ili aweze kuwasiliana nasi, aseme nasi na kutupenda, na kupeana nasi mikono,
UTUKUFU!!!

Hakuna tena, “NADHANI MIMI ni Bibi-arusi Wake. NATUMAI MIMI ni Bibi-arusi Wake.” TUNAJUA SISI NI BIBI-ARUSI WAKE .

Roho Mtakatifu anatenda kazi ndani yetu . Ni Uzima. Si msisimko wa mwili; sio namna fulani ya uhakika wa matendo ya kimwili, bali ni Mtu, Yesu Kristo, Neno la Mungu lililowekwa katika mioyo yetu kuhuisha kila neno la wakati huu.

Unakaribishwa kuungana nasi kwa kuunganishwa Jumapili saa nane 8:00 mchana , saa Jeffersonville, ( ni saa nne 4:00 usiku ya Tanzania), Roho Mtakatifu anapotuangazia kwa Neno Lake lililonenwa kupitia malaika Wake, na kutuletea Ujumbe: Edeni ya Shetani 65-0829

Ndugu. Joseph Branham.

Maandiko ya kusoma

2 Timotheo 3:1-9

Ufunuo 3:14

2 Wathesalonike 2:1-4

Isaya 14:12-14

Mathayo 24:24

21-1031 Chujio La Mtu Mwenye Busara

Ujume: 65-0822e Chujio La Mtu Mwenye Busara

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Waamini wa Biblia,

Ni siku tukufu jinsi gani tunayoishi. Mioyo yetu inawaka ndani yetu anapozungumza nasi kila siku njiani. Kristo amefunuliwa kwetu kwa Neno Lake. Ni Ufunuo wa Yesu Kristo, Neno Mwenyewe aliyedhihirishwa katika mwili. Ni Sauti ya Mungu ikimwita Bibi-arusi Wake atoke.

Tunao Mkataa, neno la mwisho, Yakini yetu; ni Neno Lake, Biblia. Sasa kama “Biblia” ndiyo Yakini yetu, hebu na tuone kile nabii alichosema Biblia ilichokuwa .

Yeye Alisema Mungu aliandika Biblia kwa kutumia manabii pekee yao. Hiyo ndiyo ilikuwa njia Yake ya kufanya jambo hilo. Hiyo ndiyo njia Aliyokuwa nayo ya kuleta Neno Lake kwa watu: kupitia midomo ya manabii Wake. Neno Lake lilimjia nabii peke yake .

Nabii alikuwa ameelekeza nia yake daima kwenye yale Mungu aliyosema; si vile mwanadamu alivyofikiri, vile huo wakati ulivyofikiri, vile kanisa lilivyofikiri, vile ufalme ulivyofikiri. Bali Vile Mungu alivyofikiri, yeye alitamka tu mawazo ya Mungu kwa Neno, wakati Mungu alipoyafunua mawazo Yake kwake, yeye aliyatamka kwa Neno lililoandikwa.

Kwa hiyo, Biblia nzima si maneno ya mwanadamu, wala haikuandikwa na mwanadamu, kuletwa na mwanadamu, ama wala haiwezi kufunuliwa na mwanadamu. Ni Neno la Mungu hufunuliwa na Mungu Mwenyewe, Hujifasiria Mwenyewe. Neno Lake.

Sasa manabii hawa walisema, “Si mimi. Sina uhusiano wowote nalo, bali ni BWANA ASEMA HIVI.” Kwa hivyo, Biblia ni BWANA ASEMA HIVI kupitia manabii. Manabii hawa hawakunena tu na kuandika Neno, lakini pia alikuwa Mfasiri wa Kiungu wa Neno hilo lililoandikwa.

Kwa hiyo, Biblia ni mawazo hasa ya Mungu yaliyoandikwa na manabii. Nabii ndiye mfasiri pekee wa kiungu wa Biblia. Ujumbe, Neno, Biblia na mjumbe ni kitu kimoja . Hivyo, tutahukumiwa kwa fasiri ya Biblia iliyonenwa na nabii.

” Wewe ulitumwa kuwa kiongozi na Mungu atakuja, na atakapokuja, Yeye atakuhukumu kulingana na yale uliyowafundisha, kwanza; kama wataingia ama hawataingia. Tutaingia kulingana na mafundisho yako .”

Je hivi yeye amesema NINI? Atahukumiwa kwanza kwa yale YEYE aliyotufundisha. Tunaweza TU kuingia kulingana na mafundisho YAKE. Kwa hiyo ni jinsi gani ilivyo muhimu kusema tu yale yaliyo kwenye kanda kwani tutahukumiwa kwa NENO LAKE KWENYE KANDA; ambayo ni fasiri ya Biblia.
Je, utaamini kikomo chako cha Milele juu ya kile mtu fulani anachosema? Sio Bibi arusi!! Sisi Tutafanya na kusema nini?

Ndipo hao wote wakapaza sauti kwa pamoja, “Tunajua hilo! Tunastarehe kwa uhakika.”

Kwa hiyo, Bibi-arusi anastarehe juu ya kila Neno ambalo nabii alilonena, ambayo ilikuwa ni fasiri ya mawazo ya Mungu yaliyoandikwa na manabii, na katika siku hizi za mwisho yamenenwa na Mungu Mwenyewe kupitia midomo ya nabii Wake.

“Wewe utatukabidhi Kwake, na ndipo tutarudi duniani tena, tukaishi milele.”

Ee wandugu na wadada, amkeni kabla hamjachelewa. Huu ni wito Wake wa mwisho. Fungua moyo wako na uone jinsi unavyopaswa kusikiliza Sauti ya Mungu kwenye kanda. Ikiwa tutahukumiwa kwa Ujumbe ambao Mungu alinena kupitia mjumbe Wake kwenye kanda, unawezaje kutokuona jinsi ilivyo muhimu, na njia pekee ya kuwa sahihi na kuwa mstari mmoja na Neno Lake, ni kwa kusikia Sauti ya Mungu kwenye kanda.

Ndiyo, Mungu ameita huduma tano , lakini hawana budi kuweka umuhimu wa kuzisikiliza kanda zaidi ya huduma yao. Sisemi kwamba mchungaji wako hawezi kuhubiri au kufundisha. Sisemi kuacha kwenda kanisani; unapaswa kwenda kanisani, lakini wakati mchungaji wako haweki kanda, Sauti ya Mungu ambayo utahukumiwa kwayo, kuchukua nafasi ya kwanza na kuwapa hiyo kusikiliza, una chujio mbaya.

Hebu Jiulize, wakati mhudumu anapokuambia, unapaswa kucheza kanda tu nyumbani kwako na sio kanisani, je! Hilo linaingia akilini? Hakika, hujadanganganywa kiasi hicho . Sauti ile ile na Neno utakayohukumiwa kwayo inapaswa TU kusikilizwa majumbani mwenu na si kanisani? Ndugu Branham kamwe hakusema kucheza kanda kanisani, lakini unapaswa kunisikiliza mimi tu kama mchungaji wako unapokuja kanisani. hivi una hata chembe ya ufunuo kweli ?

Ni jambo gani linaloweza kuwa muhimu zaidi mnapokutanika pamoja katika kanisa lenu kumwabudu Bwana, kukua katika ufahamu wa Neno, kumkaribia Mungu zaidi, kuliko kuivishwa kwa kusikia sauti PEKEE…PEKEE iliyothibitishwa ya Mungu.

Je, ungeweza kuwazia Yoshua akiwaambia Israeli wote, najua tunayo maneno halisi ambayo Musa aliyonena, lakini Musa hakuwahi kusema tunapokutanika pamoja kwamba tunapaswa kusoma maandishi yake. Ninawaongoza sasa na mimi nitawaambia maneno ya Musa.

Kisha akasoma maneno yote ya torati, baraka na laana, sawasawa na yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati .

Wala Hapakuwa na neno lo lote katika yote aliyoamuru Musa, ambalo Yoshua hakulisoma mbele ya mkutano wote wa Israeli, pamoja na wanawake, na watoto, na wageni waliokaa kati yao .

Kwa maneno mengine, kama Yoshua angekuwa na kinasa sauti katika siku zake, alipowakusanya watu pamoja ange BONYEZA PLAY.

Malaki 4 amekuja na BWANA ASEMA HIVI, nawe utahukumiwa kwa kila neno lililonenwa kwenye hizo kanda . Ujumbe huu ni chujio lako. Sikiliza na uishi, kataa na ufe.

Je, tunawezaje kuchukua nafasi wakati kikomo chetu cha Milele kina uwalakini? Tunahitaji kuwa daima tunasikia Neno; katika nyumba zetu, katika magari yetu, wakati wakufua nguo, tunapofundisha watoto wetu, tunapoosha magari yetu, tunapokuwa matembezi, na muhimu zaidi, tunapokusanyika katika makanisa yetu.

Unakaribishwa kuungana na sehemu ya Bibi-arusi Wake, inayoamini KILA NENO kwenye kanda, tunaposikia Ujumbe: Chujio la Mtu Mwenye Busara 65-0822E , Jumapili saa 8:00 nane mchana , saa za Jeffersonville ( ni saa 3:00 tatu Usiku ya Tanzania) . Au mtie moyo mchungaji wako acheze kanda kanisani mwako ili wewe pia uweze kusikia Sauti ile ile itakayokutambulisha kwa Bwana wetu Yesu Kristo, na kisha tutarudi duniani tena ili kuishi milele. HAIWEZEKANI KUWA BORA ZAIDI YA HIYO.

Ndugu. Joseph Branham