23-1119 Kristo Ni Siri Ya Mungu Iliyofunuliwa

UJUMBE: 63-0728 Kristo Ni Siri Ya Mungu Iliyofunuliwa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Kitovu Cha Moyo Wa Nabii,

Wao ndio—ndio wamezaliwa Kwako, kwa Roho na kwa Neno la Kweli. Nami naomba ya kwamba utawabariki, Bwana, na kuwaweka wameunganishwa pamoja kwa karibu na vifungo vya upendo wa Kristo.

Jitayarisheni, tutakuwa na baraka, upako na Ufunuo kuliko awali. Twaweza kulihisi jambo hilo katika nafsi zetu, jambo fulani linakaribia kutukia. Wakati uko tayari. Tumechangamshwa sana kwa furaha na tuko chini ya matarajio makubwa ya aina yake. Bibi-arusi ulimwenguni kote anakusanyika pamoja ili kusikia kutoka kwenye kiti cha enzi cha Mungu Ujumbe ambao utatupeleka kwenye viwango vipya, na kutujaza, na kujaza, na kisha kutujaza upya na Roho Wake Mtakatifu.

Maandiko yanaenda kutimia. Onyo limefanyika. Hukumu iko karibu. Bwana anakuja kumwita Bibi-arusi Wake kwenda kwenye Karamu yetu ya Arusi. Ule wito wa mwisho umepita. Ujio wa Mungu umefika. ANAKUJA KUTUCHUKUA.

Sisi ndio ile mbegu iliyochaguliwa tangu zamani ambayo huliona na kulikubali. Dhambi zetu zimeangamizwa, zimekwisha. Zimetupwa kwenye wino wa Damu ya Yesu Kristo, wala hazitakumbukwa tena. MUNGU amezisahau ZOTE. Tunasimama kama mwana na binti wa Mungu, mbele za Mungu. Ndivyo tulivyo SASA…si tutakuwa; SASA sisi ni wana na binti za Mungu.

Tunatambua kitu kimoja, NENO. KANDA HIZI. UJUMBE HUU. Hayo ni mamoja.

Na mara moja, muda mfupi tu uliopita, ulipoonyesha lile ono, hii maskani ndogo hapa, karibu kuweka Chakula akiba, kwamba utakuja wakati ambapo haya yote yangehitajika … “Weka Chakula hiki akiba hapa kwa ajili ya huu wakati.”

Huu ndio wakati. Hiki ndicho Chakula. Sisi ndio watu hao. Sisi tunao Ufunuo.

Wengine wanaweza kuukosa umuhimu wa Huduma ya Kanda. Sisi sisi sivyo. Ni maisha yetu, ni kila kitu kwetu. Ni zaidi ya uhai kwetu. Tunapokuwa na swali kuhusu jambo fulani, hatuendi kumwomba mtu atufafanulie, ama atutafutie. Sisi tunafanya vile hasa malaika wa Mungu alivyotuagiza kufanya ikiwa tutashindwa kuelewa au tukiwa na swali.

Mnalipata? Mkishindwa, rudini kwenye kanda hii tena. Sijui nitakuwa nanyi kwa muda gani zaidi. Kumbukeni, hii ndiyo Kweli, ya BWANA ASEMA HIVI. Ndiyo Kweli. Ni Maandiko.

Mkishindwa, rudini kwenye kanda.

Msitukasirikie, hivyo ndivyo YEYE ALIVYOSEMA…PAMOJA NA, hii ndiyo KWELI YA BWANA ASEMA HIVI . Yeye hakusema kiasi chake, baadhi Yake, ama wakati mtu fulani anapofasiri kile kilicho na ambacho si Neno lililotiwa mafuta. KANDA HIZI NI BWANA ASEMA HIVI.

Huenda wewe usilipate, ama kulielewa, ama bado halijafunuliwa kwako . Lakini kwetu sisi, haya ndiyo YEYE anayotuambia kupitia nabii Wake.

Unajua jinsi unavyomwambia mke wako mambo, unajua, msichana mdogo utakayemwoa. Unampenda sana, unamwambia tu siri, na kumweka karibu nawe, na kukupenda wewe na kadhalika. Unajua jinsi ilivyo. Hivyo ndivyo Mungu, Kristo, analifanyia Kanisa. Mnaona? Anamjulisha siri, siri tu. Sio hawa wafanya utani; ninamaanisha Mke Wake.

Nasi tunayazingatia yote. Loo jinsi gani Bibi-arusi alivyo mwenye furaha na changamko la shangwe kabla tu ya arusi yake. Hatuwezi kabisa kusimama kimya. Tunazihesabu dakika …. sekunde. Yeye anaendelea kutuambia tena na tena jinsi gani anavyotupenda.

Shetani anaendelea kutushambulia kuliko awali, lakini kile hajajiandaa, ni kwamba sasa TUNAJIJUA sisi ni nani. Hakuna shaka tena, SISI NI NENO LILILONENWA. Tunaweza, na tuna, nena Neno. Tuna jibu la Shetani. Mungu amejithibitisha Mwenyewe. Mungu amejihakikisha Mwenyewe. Sisi ni Neno Lake lililo hai nasi tuna nena kwa mamlaka yote aliyotupa.

Naye huyu hapa leo, katika Neno Lake, akidhihirisha jambo lile lile alilofanya kule. Hawezi kutambua uongozi mwingine. La, bwana. Hakuna askofu, hakuna chochote. Anatambua Uongozi mmoja, huo ni Kristo, naye Kristo ni Neno. Loo, jamani! Whiu! Napenda hilo. Uh! Naam, bwana.

Sisi ni raia wa Ufalme, nao huo Ufalme ni Neno la Mungu lililofanyika Roho na Uzima katika maisha yetu wenyewe. Kwa hiyo, sisi ni Neno Lake lililo hai.

Hili Hakika lanena YOTE enyi marafiki, IKIWA UNA UFUNUO WA KWELI WA KULIPOKEA NA KULIAMINI.

Sasa angalieni. Angalieni sasa, wameunganishwa pamoja chini ya Uongozi mmoja, kwa namna ile ile, mfano wa Israeli wa kale. Sasa mnalipata? Kama Israeli wa kale; Mungu mmoja, aliyethibitishwa kwa Nguzo ya Moto, na kujifunua Mwenyewe kupitia nabii, kuwa Neno. Mungu yeye yule, Nguzo ile ile ya Moto, kwa njia ile ile; Hawezi kubadili njia Yake . Hilo ni… Kamili tu kama iwezavyo kuwa.

Nabii…Hebu hilo lizame ndani kilindini. Mungu Mmoja, aliyethibitishwa kwa Nguzo ya Moto, kupitia nabii, kuwa Neno la siku hiyo, Naye hawezi kubadilika.

Ningeweza kuendelea na kuendelea, na tungeweza kufurahia na kushiriki nukuu baada ya nukuu; nasi tutafanya hivyo, kutoka kote ulimwenguni Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) tunaposikia:  Kristo Ni Siri ya Mungu Iliyofunuliwa 63-0728.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Mathayo 16:15-17
Luka Sura ya 24
Yohana Mtakatifu 5:24 / 14:12
1 Wakorintho Sura ya 2
Waefeso Sura ya 1
Wakolosai Sura ya 1
Ufunuo 7:9-10