23-1112 Mungu Hamwiti Mtu Hukumuni Bila Ya Kumwonya Kwanza

UJUMBE: 63-0724 Mungu Hamwiti Mtu Hukumuni Bila Ya Kumwonya Kwanza

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Kamani, Springi kuu, Mkulima na Mke nyumbani,

Chochote kile ambacho Mungu alichokupa kufanya, una utumishi kwa jambo hilo. Huna budi kuwajibika kwa hilo kwa Mungu. Haijalishi adui aweza kukuambia kuwa wewe ni mdogo jinsi gani, wewe ni muhimu sana kwa Mungu hivi kwamba saa Yake kuu haiwezi kusonga bila wewe.

Alikuita, akakuchagua, alikukusudia tangu awali, na akakupa Ufunuo wa Ujumbe Wake mkuu wa wakati wa mwisho. Ana imani na wewe asilimia 100%. Wewe ndiwe yule Bibi-arusi mwenyewe wa Yesu Kristo, Kipenzi Chake, naye Anakupenda sana.

Daima amewaonya watu kote katika mataifa, “Tubuni, la sivyo mtaangamia,” “Rudini kwenye Neno,” “Jitayarisheni, kuna jambo linaenda kutukia.” Wakati huo hatimaye umefika. Mungu anakuja kumchukua Bibi-arusi Wake, kama vile tu alivyotuahidi Angefanya. Ameliita Gurudumu Lake kutoka kwenye gurudumu.

Wengi wameanguka kutoka kwenye Ujumbe mkuu wa Mungu wa wakati wa mwisho leo hii, wakisema, “yale aliyosema yangetukia, hayakufanyika. Mambo yote yako vile vile.” Ilikuwa ni vizazi vingi vilivyopita kabla ya unabii mwingi wa manabii wa Mungu kutimia. Lakini yalitendeka hata hivyo, kama tu walivyosema, Neno kwa Neno.

Biblia yake inatuambia hivi: “Kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika kuja Kwake Mwana wa Adamu.” Kabla Mungu hajatuma hukumu kuuangamiza ule ulimwengu uliotangulia gharika, Mungu alimtuma nabii ulimwenguni. Nabii huyo alifanya nini?

Akawatayarisha watu kwa ajili ya wakati huo. Nuhu aliwatayarisha watu, nao ulikuwa ni wito wa rehema kabla ya hukumu.

Nuhu aliwatayarisha watu kabla ya hukumu kuja aliowaonya kuihusu. Ilikuwa ndio Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hiyo.

Nabii wa Mungu alituambia kwamba Mungu kamwe habadilishi mpango Wake. Yale aliyoyafanya wakati huo, anayafanya vivyo hivyo leo hii. Sisi tutakaa tu na MPANGO WA MUNGU ULIYOANDALIWA KWA AJILI YA SIKU HII NA KUBONYEZA PLAY.

Kama ilivyokuwa wakati huo, watu husema tunaweka mkazo sana kwa nabii wa Mungu; Ni Roho Mtakatifu, si William Branham. Tunasema, AMINA, hatumsikilizi huyo mtu , tunasikiliza tu YALE ALIYOSEMA.

Roho Mtakatifu ndiye Nabii wa wakati huu; Yeye analihakikisha Neno Lake, akilithibitisha. Roho Mtakatifu alikuwa ndiye Nabii wa wakati wa Musa. Roho Mtakatifu alikuwa Nabii wa wakati wa Mikaya. Roho Mtakatifu, aliyeliandika Neno, anakuja na kulithibitisha Neno.

Lakini Ndugu Branham ndio kwanza awaambie juma lililopita;

Sasa, mnaona, daima nimewaomba mwe waangalifu kwa yale mnayosikiliza. Mnaona? Kuna mengi sana ambayo ni upande tu wa kibinadamu.

Sisemi ya kwamba Bwana aliniambia jambo hilo. “Mimi” naamini, unaona. Na naamini halipaswi kufanywa.

Kwangu mimi na nyumba yangu, nitachukua yale malaika-mjumbe wa saba wa Mungu ANAYOAMINI, ANAYOWAZIA AU HATA ANAYOJISIKIA kuliko ya mhudumu mwingine yeyote, askofu ama mtu.

Ni nani ambaye Mungu aliwahi kumtuma kuhukumu kile nabii Wake anachoamini, anachohisi ama hata anachofikiria ndicho ama halijavuviwa?…Hebu niwaambieni ni nani ninayefikiri.

Mwangalieni Kora, katika siku ambazo Mungu alimtuma Musa na ujumbe, naye Kora na Dathani wakawazia, wakamwendea Musa, na kusema, “Sasa, hebu kidogo, unajichukulia mengi kupita kiasi! Unafikiri wewe ndiwe changarawe ya pekee ufukoni; bata kidimbwini, ndiwe wa pekee. Nitakufahamisha wapo watu wengine walio watakatifu, pia!”

Onyo, hukumu iko karibu. Rudini kwenye NENO LA ASILI. Rudini kwenye Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kwa ajili ya siku yetu. Rudini kwa nabii wa Mungu. Ujumbe huu, Sauti Yake. Inapaswa kuwa ya KWANZA na kuwa jambo lililo muhimu zaidi kwenu.

Bila shaka wengine wana sauti, na wito, kuhubiri na kufundisha Ujumbe huu. Bali Kanda hizo, Sauti hiyo, haina budi kuwa ndio Sauti iliyo muhimu sana mnayopaswa kuisikia katika nyumba zenu, magari yenu, na muhimu zaidi, kanisani mwenu, kama mnataka kuwa Bibi-arusi wa Mungu.

Njooni msikie hiyo Sauti pamoja nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) Wakati nabii wa Mungu anapouonya ulimwengu kwamba Kuja kwa Bwana kumekaribia. Hii inaweza kuwa ndio mara ya mwisho.

Ndugu. Joseph Branham

Mungu Hamwiti Mtu Hukumuni Bila Ya Kumwonya Kwanza. 63-0724

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Isaya 38:1-5
Amosi Sura ya 1