23-1105 Yeye Hujali. Je! Wewe Unajali?

UJUMBE: 63-0721 Yeye Hujali. Je! Wewe Unajali?

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Watoto wa Injili,

Sisi ni watu waliobarikiwa zaidi ambao wamewahi kutembea juu ya uso wa dunia. Je! Hivi tunaweza kuwazia malaika-mjumbe wa saba aliyechaguliwa na Mungu kutuambia maneno haya:

Ninawapenda. Loo, ninawapenda kana kwamba mlikuwa ni watoto wangu binafsi, nanyi ni watoto wangu katika Injili. Nimewazaa kwa Kristo, kwa njia ya Injili.

Mungu anatujali sana hata Yeye alitutumia nabii Wake aliyethibitishwa akiwa na ishara ya Nguzo ya Moto kutufanya tujue ya kwamba haikuwa tu ni mtu huyu aliyekuwa akitembea pamoja nasi, bali ilikuwa ni Mungu papo hapo juu yake. Yeye ndiye anayeongoza njia.

Kwa sababu anatujali, kabla ya hukumu iliyo kuu haijaja, ameiandaa njia ambayo tutakuwa huru na hukumu zote zinazokuja. Njia hiyo ya kuepukia ni kwa ajili yetu sisi tu, Wateule. Sisi ndio tumeikubali seli zazi hii ya Uhai. Sisi ndio tuliokusudiwa tangu awali kuliona. Sisi ndio tulio na Ufunuo wa huduma hii kuu ya kanda.

Yeye aliifia huduma hii. Alikufa kusudi Roho Mtakatifu aweze kuwa hapa siku hizi kuonyesha mambo haya. Yeye alikujali. Alijali kuuleta hapa. Alijali kutoa tamshi. Alijali kwa kuwa alikupenda. Alijali vya kutosha kufanya jambo hilo, kumtuma Roho Mtakatifu kwenye hili, kuifanya huduma hii leo.

Kama umechaguliwa tangu zamani kwa Uzima wa Milele, utalisikiliza na utalifurahia. Ni Faraja yako. Ndicho kitu ambacho umekitamani maishani mwako mwote. Ni ile Lulu ya thamani kuu. Tunaachana na kila kitu kwa ajili ya Ujumbe huu, Sauti hii. Ni Bwana wetu Yesu Kristo akizungumza nasi.

Hakuna mtu anayepaswa kutubembeleza-bembeleza, SISI NI WAAMINIO, hakuna kitu kinachoweza kuliondoa kwetu. Hatujali yale mtu ye yote asemayo, tunaamini kila Neno.

Yeye anatujali sana; ikiwa tunahitaji uponyaji, tunaamini tu Neno Lake kutoka ndani kabisa ya kilindi cha moyo wetu. Basi haijalishi mshauri yeyote, mfariji ye yote, daktari ye yote, hospitali yo yote, ubaini wowote ungesema nini, tunaamini tu Neno Lake. Tunajua tu hilo! Hakuna haja ya kusema jambo lingine lolote kulihusu; tunajua hilo.

Yeye alitujali sana hata akamfanya nabii Wake akihifadhi Chakula kwa ajili ya Bibi-arusi Wake. Aliagiza hata kila mchungaji, mhudumu, na kundi la watu ulimwenguni kote kufuata maagizo yake na kuzicheza kanda hizi katika MAKUSANYIKO ama makundi yao.

Kama ninyi watu mtafanya hivyo asubuhi ya leo, mtakaoombewa Na ninyi watu mnaoisikia kanda hii, kote ulimwenguni, na baada ya kanda hii kuchezwa na mhudumu ama mtu anayeicheza katika makundi ya kusanyiko huko misituni ama popote mlipo, mnaoicheza, kwanza mtafanya toba yenu dhahiri, kisha mje bila chochote moyoni mwenu, ila imani, na kuombewa, hapo ndipo Dawa itakapofanya kazi.

Nilidhani wakosoaji wetu wanasema kuwa nabii HAKUSEMA kucheza kanda kanisani? Si tu kwamba Yeye alisema katika makanisa yao, bali katika misitu ama POPOTE mlipo…CHEZENI KANDA.

Kama utatii na kufanya yale hasa Mungu aliyonena kupitia malaika-mjumbe Wake wa saba aliyethibitishwa, basi wewe pia unaweza kuwa na IMANI kuu kuliko zote unayoweza kuwa nayo.

Kwanza, na kulikaribia hili, wasikilizaji hawana budi kutiwa mafuta kwa imani. Wewe, kama huna imani, basi hakuna—hakuna hata haja ya kuja kuombewa, kwa maana itahitaji imani yako na imani yangu pamoja; imani yangu kumwamini Yeye,imani yako kumwamini Yeye.

Sisi hatudhanii, ama kukisia, ama kutumainia ni hivyo. Kanda ndiyo Njia ya Mungu iliyoandaliwa ya siku hii. Si maneno ya mtu anayeitwa William Marrion Branham, Ni Maneno yaliyofunuliwa ya Bwana wetu Yesu Kristo. Kabisa ni, “Amina!” Ndio mkataa wetu. Ni Kweli na si kitu ila Kweli tupu.

Na unapoupata Mkataa wa Mungu, Neno Lake, ahadi juu ya jambo fulani, inakubidi kujua kwanza ya kwamba ni Neno la Mungu, ya kwamba jambo unaloliona likitekelezwa ni Mungu. Ha—hakuna—hakuna “huenda ikawa ndivyo, ingewezekana, inaonekana kana kwamba huenda ikawa.” “Ni Mungu!” Ndipo unapofikia mahali hapo, basi hiyo ndiyo ile Lulu ya thamani kubwa, huna budi kuachana na chochote mtu yeyote anachokwambia kinyume Chake. Haikupasi kuangalia kile mwanadamu ametimiza.

Tunakwenda kuwa na KARAMU KUBWA MNO YA UPENDO Jumapili hii. Tutafanya kile ambacho malalika-mjumbe wa saba wa Mungu aliyethibitishwa aliyotuambia tufanye: Bonyeza Play na kutii.

LOLOTE tunalohitaji, tutalipokea. Tutalipokea kwa sababu tutaiweka imani yetu pamoja na IMANI YAKE kumwamini Yeye. Kisha sote tutasema:

Tangu sasa na kuendelea, kuna kitu moyoni mwangu kinachoniambia ya kwamba shida zangu zimekwisha. Mimi ni—mimi ni mzima, nitapona”? Mnaamini hilo? Inueni mikono yenu, “Ninaamini Hilo!” Mungu awabariki.

Kwa sababu Mungu anajali, ninakualika uje kuungana nasi; ama umtie moyo mchungaji wako, kiongozi wako, kufuata maagizo ya nabii, na kumsikia malaika wa saba wa Mungu akinena Neno la Mungu na upokee lolote unalohitaji, Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville ( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) tunaposikia: 63-0721 Yeye Hujali. Je! Wewe Unajali?

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Yohana Mt 5:24 / 15:26
1 Petro 5:1-7
Waebrania 4:1-4