23-1029 Mfungwa

UJUMBE: 63-0717 Mfungwa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Jumamosi.

Wapendwa Wafungwa,

Maisha yako unayoishi sasa yataakisi maisha ambayo ungeishi ikiwa ungeishi katika siku za Nuhu, ama Musa, kwa sababu una roho yule yule. roho yeye yule aliye ndani yako sasa alikuwa ndani ya watu wakati huo.

Kama ungaliishi katika siku za Nuhu, ungechukua upande wa nani wakati huo? Je, ungeingia kwenye mashua pamoja na Nuhu ukiamini kwamba yeye ndiye ambaye Mungu alimchagua kujenga safina na kuwaongoza watu, au ungesema, “Mimi naweza kujenga safina pia. Mimi ni mzuri tu kama nahodha na mjenga mashua”?

Vipi kama ungaliishi katika siku za Musa? Je, ungekaa na Musa na kuamini kwamba yeye ndiye ambaye Mungu alimchagua kuwaongoza watu, ama ungeenda pamoja na Dathani na Kora waliposema “Sisi pia ni watakatifu, tunalo jambo la kusema. Mungu alituchagua sisi pia.”?

Kila mmoja wetu anapaswa kuchagua, leo hii, kati ya mauti na uzima. Sijali wewe unasema uko upande gani. Yale unayofanya, kila siku, yanathibitisha kile ulicho. Tunabonyeza Play KILA SIKU.

Je, uko katika Neno kila siku? Je, unaomba, ukitafuta Mapenzi makamilifu ya Bwana katika kila jambo unalofanya? Je, unabonyeza play na kuisikia Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kila siku? Je, unaamini ni muhimu kabisa Kubonyeza Play? Je! unaamini hiyo Sauti iliyo kwenye kanda ni Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku hii?

Kwetu sisi, jibu ni NDIYO. Tunauambia ulimwengu kwamba sisi ni Wafungwa wa Neno la Mungu, Ujumbe Wake, Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kwa ajili ya siku yetu. Ndiyo, tunaamini Kubonyeza Play kwa moyo wetu wote. Ndiyo, tunaamini mjumbe wa wakati wa 7 wa kanisa ndiye aliyeitiwa kumwongoza Bibi-arusi. Ndiyo, hiyo Sauti iliyo kwenye kanda ndiyo Sauti muhimu zaidi yakusikia.

Upendo wa Mungu, Sauti Yake, Ujumbe huu, ni mkuu sana, Ufunuo kama huu kwetu sisi, kwamba hatuwezi kamwe kuuacha. Tumekuwa Mfungwa Kwa jambo hilo.

Tumeuza kila kitu kingine. Haidhuru mtu mwingine yeyote anasema nini, tumefungiwa hatamu Kwake. Kuna jambo fulani kulihusu hili ambalo kamwe hatuwezi kuliacha. Ndio furaha ya maisha yetu. Hatuwezi kuishi bila hilo.

Tuna furaha sana, tunashukuru sana, tunajivunia kuwa Mfungwa kwa ajili ya Bwana na Ujumbe Wake; maana ni mamoja. Ni zaidi ya uhai kwetu. Kila siku inakuwa wazi na halisi zaidi kwamba sisi ni Bibi-arusi Wake. Tuko katika Mapenzi yake makamilifu. Tunaweza kunena Neno, kwa maana sisi ni Neno lililofanyika mwili.

Hatujaunganishwa na chochote ila Kristo na Ujumbe Wake wa saa; hata baba zetu, mama zetu, Ndugu zetu, dada zetu, waume zetu, wake zetu, yeyote yule. Tumeunganishwa tu na Kristo, na Yeye pekee. Tumeunganishwa na kufungwa nira kwa Ujumbe huu, Sauti hii, kwa maana ndiyo Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii, WALA HAKUNA NJIA NYINGINE.

Sisi si wafungwa tena wa utu wetu wenye ubinafsi, wa lengo letu. Tumejitolea kabisa na kufungwa nira Kwake. Haidhuru ulimwengu wote unawaza nini, vile hao wengine ulimwenguni wanavyofanya, tumefungwa kwa vifungo vya upendo Kwake na Sauti Yake.

Tunashukuru sana sisi kuwa Wafungwa. Nieleze, Baba, nini cha kufanya kila sekunde ya kila dakika ya kila siku. Hebu na Sauti Yako itufundishe katika kila jambo tunalofanya, tunalosema, na jinsi tunavyotenda. Hatutaki kujua kingine ila Wewe.

Njoo ufungwe hatamu pamoja nasi kwa Neno la Mungu na Sauti Yake Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia jinsi ya kuwa: Mfungwa 63-0717.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Kusikiliza Ujumbe:

Filemoni 1:1

Maelezo ya ziada:
Ndugu Branham, TUNAPENDA jinsi unavyotamka Filemoni, ni KAMILIFU kwa Bibi-arusi.