23-1022 Mbona Unalialia? Nena!

UJUMBE: 63-0714M Mbona Unalialia? Nena!

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa maskani za Mungu,

Mimi ni Kanisa Lake. Wewe ni Kanisa Lake. Sisi tu maskani ambamo Mungu anakaa ndani yake. Sisi ni Kanisa la Mungu aliye hai; Mungu aliye hai akiishi katika nafsi zetu. Matendo yetu ni matendo ya Mungu. Utukufu!!

Sote tunakusanyika pamoja, katika maeneo madogo kutoka kote ulimwenguni; sote tukikusanyika pamoja ilipo Sauti ya Mungu, Neno Lake la siku hii.

Ni ajabu sana. Hakuna kufungwa kwa kitu kingine, ila kwa Yesu Kristo na Neno Lake. Hilo Ndilo, mwisho wa maneno. Tumeketi pamoja katika ulimwengu wa Roho tukikamilishwa na Sauti ya Mungu mwenyewe.

Tunaenda kabisa. tunaenda sote kwenye Nchi ya Ahadi. Kila mmoja wetu! Hata kama wewe ni mke wa nyumbani, u yaya mdogo, mama kizee, babu ama kijana mwanamume, chochote ulicho, tutaenda sisi sote. Hakutakuwa hata na mmoja wetu atakayeachwa nyuma. Kila mmoja wetu ataenda, na “hatutazuiwa na kingine chochote.”

Tunaamini kwamba tunapaswa kuwa wote pamoja. Kundi moja kubwa lililoungana la Mwili wa Yesu Kristo, linalongojea kule Kuja kwenye utukufu. Hatungepaswa kutengana, lakini mwanadamu ametoka kwenye njia iliyowekwa ya mafundisho ya Injili.

Yabidi kuwe njia fulani ya kuonyesha kabisa ni ipi iliyo kweli na iliyo makosa. Na njia pekee utakayotenda, ni kutokuweka fasiri yo yote kwenye Neno, lisome tu jinsi lilivyo na uliamini hivyo. Kila mtu anaweka fasiri yake mwenyewe, na inalifanya linene jambo lingine tofauti. Kuna SAUTI YA MUNGU MOJA tu KWA BIBI-ARUSI. BONYEZA PLAY!

Nayasema kwa kanda hii na kwa wasikizaji hawa; nasema hili chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu, “Ni nani aliye upande wa Bwana? Na aje chini ya Neno hili.”

Neno la siku yetu lina Sauti. Nabii wetu ndiye Sauti hiyo. Sauti hiyo ndilo Neno lililo hai kwa ajili ya siku yetu. Tulichaguliwa tangu zamani kuisikia Sauti hiyo na kuona saa hii, na hakuna kitu kitakachotuzuia kuisikia Sauti hiyo.

Imani yetu inaiona hiyo na kuchagua kuisikia hiyo bila kujali mtu yeyote anasema nini. Sisi hatushushi darubini yetu kutazama upande mwingine. Tunaweka kipini chetu cha kulengea shabaha katikati ya Neno kabisa na masikio yetu yametuniwa kwenye Sauti hiyo.

Kwa kujiweka wakfu Kwako Bwana, kutoka mioyoni mwetu hadi Masikioni Mwako, haya ni maombi yetu ya dhati.

Kusudi maisha yetu yapate kubadilika tangu leo na kuendelea, tupate kuwa na mawazo mema. Tutajaribu kuishi vizuri sana na kuwa wanyenyekevu pia tukiamini yale tunayomwomba Mungu, Mungu atampa kila mmoja. Nasi hatutanena maovu sisi kwa sisi ama dhidi ya mtu ye yote. Tutawaombea adui zetu na kuwapenda; tuwafanyie mema wanaotufanyia mabaya. Mungu ndiye Hakimu wa asiye na makosa na aliye na makosa.

Ninawaalika mje kutia mafuta Imani yenu kwa kuisikia Sauti ya Mungu pamoja nasi Jumapili, saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) tunaposikia: Mbona Unalialia? Nena! 63-0714M.

Ndugu. Joseph Branham