All posts by admin5

25-0907 Kutoka Kwa Tatu

UJUME: 63-0630M Kutoka Kwa Tatu

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Kutoka Kwa Tatu,

Ikiwa huna jicho la kiroho, hulipati. Lakini jicho la kiroho linaweza kuona Nguvu za Mungu zikitenda kazi maana hilo liko kwenye Neno kikamilifu. Ni Neno, nalo Neno la Mungu halibadiliki kamwe. Kile Yeye alichokifanya hapo mwanzo, anafanya vivyo hivyo sasa nalo jicho la kiroho linaliona, linaliamini, na KULISIKIA.

Ulimwengu unaweza kutokukubaliana nami katika kile ninachoamini kuwa ndiyo njia ya Mungu iliyoandaliwa Kwa ajili ya wakati huu: Sauti iliyo muhimu sana unayopaswa kuisikia ni Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. Ni lazima mzicheze kanda makanisani mwenu, lakini KAMA kweli mnauamini Ujumbe huu, basi hamwezi kupingana na kile nabii wa Mungu anachosema.

Jumapili hii tutakusanyika kama wale wana wa Kiebrania walivyofanya ili kuipata mana ile iliyokuwa imeandaliwa kwa ajili yao usiku kucha, ambayo ingewahifadhi siku inayofuata. Sisi tutakusanyika kwa ajili ya Mana yetu ya Kiroho itakayotutia nguvu kwa ajili ya kule Kutoka kwetu kukuu kunakokuja hivi karibuni.

Hakuna njia bora zaidi kuliko kumruhusu Sauti ya Mungu yeye aliseme hilo Mwenyewe, kumhusu yeye Mwenyewe, nao Ujumbe huu tunaoenda kuusikia UMESHEHENI!

Mungu alimpeleka mtu mmoja nyikani, akamfunza. Kisha akamrudisha, na kukipeleka kitu hicho huko, kisha akawatoa hao watu. Mnaona ninalomaanisha? Yeye hawezi kubadilisha mpango Wake. Yeye ni Mungu.

Kwa hivyo hapa Yeye anatuambia waziwazi Yeye kamwe habadilishi mpango Wake. Kile Yeye alichokifanya tangu mwanzo, atakifanya tena mwishoni, Yeye aliahidi. Kwa hiyo sasa ni lazima tujue Mpango Wake ulikuwa nini wakati ule kwani utakuwa ni Mpango ule ule hivi sasa.

Kamwe hatashughulika na kundi. Kamwe hajafanya hivyo. Yeye hushughulika na mtu mmoja; na alifanya hivyo, na atafanya hivyo. Na aliahidi, hata katika Malaki 4, angefanya hivyo.

Yeye kamwe hashughuliki na kundi. Kwa hivyo, Yeye aliahidi katika wakati wetu kwamba angemtuma mtu Mmoja, Malaki 4, akiwa na Bwana Asema Hivi.

Hiyo ni kweli. Kwa hiyo kuna ahadi Yake, kwamba Yeye alikuwa ni nani; ahadi ya kile alichosema Yeye angekifanya, na basi tumewasili. Tunapaswa kuwa ni watu wenye furaha jinsi gani; akiwapa ishara, kwa ishara ya Neno Lake lililoahidiwa, Neno lililoahidiwa. Aliahidi angefanya hivyo.

Mungu alichagua kumwongoza Bibi-arusi Wake namna gani wakati ule?

Mungu alichagua, katika siku za kule kutoka, Yeye aliliita kundi moja litoke. Na kutoka kwenye kundi hilo, ninawataka muone jambo fulani, Yeye alipata tu wawili walioingia kwenye nchi ya ahadi. Yeye alichagua kuwatoa kwa kutumia nini?

Hili hapa. Hili ni muhimu sana kwa wenye nia ya kiroho kuweza kulishika. Mungu alichagua kumwongoza na kumpeleka Bibi-arusi kwenye Nchi ya Ahadi namna gani?

Siasa? dhehebu? Yeye alichagua nabii, akiwa na ishara ya kimbinguni ya Nguzo ya Moto, watu wasije wakakosea. Yale nabii aliyosema yalikuwa ni Kweli. Na Mungu alishuka, Nguzo ya Moto, na kujithibitisha Mwenyewe, akaonyesha Neno Lake. Hiyo ni kweli? Hiyo ndiyo aliyoileta, kutoka Kwake kwa kwanza. Kutoka Kwake kwa pili…

Kwa hiyo, ili kuhakikisha kwamba watu hawangekosea, Yeye aliwatumia nabii akiwa na ishara ya kimbinguni ya Nguzo ya Moto kwa ajili ya kule kutoka kwao kukuu.

Yeye alifanya nini, kule kutoka kwa kwanza? Alimtuma nabii, aliyetiwa mafuta kwa Nguzo ya Moto, naye akawaita watu wakatoka. Huko kulikuwa ni kutoka Kwake kwa kwanza…

Kutoka kwa pili, Yeye alimleta Nabii, aliyetiwa mafuta, ambaye alikuwa ni Mwanawe, Mungu-Nabii. Musa alisema Yeye angekuwa ni Nabii; Naye alikuwa na Nguzo ya Moto, na akafanya ishara na maajabu…

Na hapa Yeye aliahidi jambo lile lile katika kule kutoka katika siku za mwisho, wala hawezi kulibadili…

Wengi watakubali kwa kusema, naam, Yeye alimtuma nabii kumwita Bibi-arusi atoke, lakini sasa hivi Roho Mtakatifu Yeye atamwongoza Bibi-arusi kupitia wahudumu; lakini Yeye hakusema hivyo…hebu na tuendelee kusoma.

Angalieni ile Nguzo ya Moto iliyowaita watoke, ikawaongoza kwenye nchi ya ahadi, chini ya upako wa nabii. Nguzo ya Moto ambayo wangeweza kuiangalia, iliwaongoza kwenye nchi ya ahadi, chini ya nabii aliyetiwa mafuta. Nao daima walimkataa. Hiyo ni kweli? Hakika.

Nguzo ii hii ya Moto inawaongoza watu tena kwenye Nchi ya ahadi, ule Utawala wa Miaka Elfu.

Ile Nguzo ya Moto, chini ya uongozi wa Mungu…Mungu alikuwa ni ule Moto, na ile Nguzo ya Moto ilimtia mafuta tu yule nabii. Ile Nguzo ya Moto ilikuwa isimame kama ushahidi wa Mbinguni kwamba Musa alikuwa ameitwa atoke.

Sasa, kumbukeni, Musa hakuwa hiyo Nguzo ya Moto. Yeye alikuwa ni kiongozi aliyetiwa mafuta, chini ya hiyo Nguzo ya Moto, na hiyo Nguzo ya Moto iliuthibitisha tu Ujumbe wake kwa ishara na maajabu.

Hakuna kosa, enyi marafiki. Si yale ninayosema mimi; mimi ni ndugu yenu tu. Lakini, ni yale Mungu anayowathibitishia, ndiyo yanayolifanya Kweli. Nguzo ile ile ya Moto aliyoitumia kwenye kule kwingine kuwili, Yeye ameileta miongoni mwenu leo, na kuithibitisha kisayansi.

Mungu kamwe habadilishi mpango Wake. Mungu anayo njia iliyoandaliwa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake leo: ile Nguzo ya Moto, chini ya uongozi wa Mungu… Mungu alikuwa ni ule Moto, na ile Nguzo ya Moto ilimtia mafuta tu nabii.

Kuna Sauti moja tu, nabii mmoja, aliye na Bwana Asema Hivi, William Marrion Branham. Yeye si ile Nguzo ya Moto, bali yeye ni kiongozi aliyetiwa mafuta chini ya hiyo Nguzo ya Moto.

Sote tunataka kuwa katika Mapenzi MAKAMILIFU ya Mungu. Neno Lake NDIYO mapenzi Yake Makamilifu. Neno lililothibitishwa la wakati wetu ni Ujumbe huu. Nabii Wake ndiye aliyechaguliwa kumwongoza Bibi-arusi Wake. Kama huliamini hilo, huwezi kuwa Bibi-arusi Wake.

Njooni mjiandae kwa ajili ya kule Kutoka kwetu kuu kwa kulisikia Neno Kamilifu la Mungu pamoja nasi Jumapili saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia: Kutoka Kwa Tatu 63-0630M.

Ndugu. Joseph Branham

25-0831 Mbona Unalialia? Nena!

UJUMBE: 63-0714M Mbona Unalialia? Nena!

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Kanisa la Mungu,

Mungu alinena na kusema, ““Mimi sitendi kazi duniani ila kupitia tu kwa mwanadamu. Mimi-Mimi- Mimi ndimi Mzabibu; nanyi ni matawi, na Mimi nitajijulisha Mweyewe tu ninapoweza kumpata mtu MMOJA, na Mimi nimemchagua yeye, William Marrion Branham. Mimi nimemtuma aje akamtoe Bibi-arusi Wangu. Nitaliweka Neno Langu kinywani mwake. Neno Langu litakuwa Neno Lake. Yeye atalinena tu Neno Langu na kusema tu yale Mimi nisemayo.”

Sauti ya Maandiko ilinena kupitia Nguzo ya Moto na kumwambia yeye, “Nimekuchagua wewe, William Branham. Wewe ndiye mtu huyo. Nilikuinua wewe kwa kusudi hili. Nitakuthibitisha kwa ishara na maajabu. Unashuka chini kule kulifunua Neno Langu na kumwongoza Bibi-arusi Wangu. Neno Langu halina budi kutimizwa na WEWE.”

Nabii wetu alikuwa anajua yeye alikuwa ametumwa kwa kusudi hilo hasa la kuzifunua siri zote za Biblia na kumwongoza Bibi-arusi wa Mungu kwenda Nchi ya Ahadi. Yeye alijua kile alichosema, Mungu angekiheshimu na kukitimiza. Nawatakeni msilisahau kamwe Neno hilo. Kile alichokisema nabii wetu, Mungu atakiheshimu, kwa maana Neno la Mungu lilikuwa ndani ya William Marrion Branham. Yeye ni Sauti ya Mungu kwa ulimwengu.

Yeye alijua alikuwa ndiye malaika-mjumbe wa saba wa Mungu aliyetiwa mafuta. Yeye alijua moyoni mwake mambo yote ambayo Mungu aliyokuwa ameyasema kumhusu yeye katika Neno Lake. Kile kilichokuwa kinawaka moyoni mwake kikawa halisi. Yeye alikuwa ametiwa mafuta na alijua alikuwa na BWANA ASEMA HIVI. Hakukuwa na kitu kingalimzuia yeye kutokwenda kulinena Neno la Mungu.

Mungu alimwambia yeye, “Neno Langu, na wewe, mjumbe Wangu, ni kitu kimoja.” Alijua yeye ndiye aliyechaguliwa kulinena Neno lisilokosea. Hilo ndilo tu yeye alilohitaji. Angeweza KUNENA, NAYE MUNGU ANGELITIMIZA.

Ufunuo wa Ujumbe huu NA mjumbe wa Mungu vimeitia mafuta imani yetu zaidi ya hapo awali. Imetupeleka katika miduara mikubwa. Hilo limetutenga na kila kitu isipokuwa Ujumbe Wake, Neno Lake, Sauti Yake, Kanda Zake.

Haijalishi sisi ni wachache jinsi gani, jinsi gani tunavyochekwa, jinsi tunavyodhihakiwa, haileti tofauti hata kidogo. SISI TUNALIONA. SISI TUNALIAMINI. Kuna kitu fulani ndani yetu. Tulichaguliwa tangu awali kuliona HILO na hakuna kitu kitakachotuzuia sisi tusiliamini HILO.

Tunakumbuka kile lile ono lilichosema, “rudi ukakihifadhi Chakula”. Hilo ghala lilikuwa wapi? Maskani ya Branham. Ni mahali gani nchini, ama ulimwenguni mahali popote, pangelinganishwa na Jumbe tulizo nazo? NDIYO Sauti pekee iliyothibitishwa na Mungu Mwenyewe kuwa Bwana Asema Hivi. SAUTI PEKEE!

Ni wapi pengine tungeweza, au tungetaka kwenda, wakati yeye alisema;

Hapa ndipo chakula kimehifadhiwa…

Umehifadhiwa hapa. Uko kwenye kanda; utaenda ulimwengu mzima katika kanda ambapo watu manyumbani mwao. Hizo kanda zitaangukia mikononi mwa wale waliochaguliwa tangu awali wa Mungu. Yeye anaweza kuliongoza Neno; yeye ataelekeza kila kitu kuelekea njia yake hasa. Hiyo ndiyo sababu Yeye alinituma nirudi nikafanye hivi. “Kihifadhi chakula hapa.”

Sisi ni Bibi-arusi Neno Wake Mkamilifu ambaye amedumu na Chakula Chake Kilichohifadhiwa. Hakuna haja ya kulialia tena, tunanena tu Neno na kusonga mbele, kwa kuwa sisi NI Neno.

Hakuna kitu cha kuhofia. Hakuna haja ya mikutano ya maombi ya usiku kucha kufunua sisi ni nani, Neno limekwishafunuliwa kwetu. Tunajijua sisi ni nani, kama vile yeye nabii wa Mungu, naye tayari amekwishatuambia ni nani ambaye angekwenda.

Kila mmoja wetu! Hata kama wewe ni mke wa nyumbani, ama u yaya mdogo, ama hata kama wewe ni mama kizee, ama kijana mwanamume, ama cho chote kile, tutaenda kwa vyo vyote. Hamna hata mmoja wetu atakayeachwa nyuma.” Amina. “Kila mmoja wetu ataenda. Hatutazuiwa na kingine chochote.”

Nena kuhusu kutupa IMANI ya Kunyakuliwa!!!

Njooni muungane na sehemu ya Bibi-arusi wa Mungu tunapokusanyika pamoja kwenye Sauti ya Mungu iliyothibitishwa, anaponena na kutuambia: Kipenzi Changu, Mteule Wangu, Bibi-arusi Wangu, Mbona Unalialia, Nena, na usonge mbele.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: 63-0714M Mbona Unalialia? Nena!

Saa: 06:00 MCHANA, Saa za Jeffersonville (ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki)

Mahali:

Bali kuna Kanisa moja tu halisi, hujiungi nalo; unazaliwa ndani yake. Waona? Na iwapo umezaliwa ukiwa ndani yake, Mungu Aliye Hai hutenda kazi kwako, akijifanya Mwenyewe ajulikane. Waona? Humo ndimo Mungu anamoishi, Kanisani Mwake. Mungu huenda Kanisani kila siku__huishi Kanisani, Yeye huishi ndani yako. Wewe ni Kanisa Lake. Wewe ni Kanisa Lake. Wewe ni hekalu anamoishi Mungu. Wewe binafsi ni Kanisa la Mungu Aliye Hai.

25-0824 Ushirika

UJUMBE: 65-1212 Ushirika

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Neno Lililothibitishwa Peke Yake,

Jinsi gani tunavyomshukuru Roho Mtakatifu kwa Ufunuo wa kweli wa Neno Lake lililothibitishwa la wakati huu. Wengi wanakiri kwamba wanaamini Ndugu Branham ndiye nabii wa Mungu anayetimiza Maandiko yaliyoahidiwa kumhusu yeye, lakini Ufunuo wa kweli wa Neno na mpango wa Mungu umefichwa kwao.

Kwa kila Ujumbe wa Barua ya mahaba ambao Bibi-arusi anaousikia, Mungu anatuthibitishia kwamba tuko katika Mapenzi Yake makamilifu kwa kuisikiliza Njia Yake iliyoandaliwa kwa ajili ya wakati huu, Sauti ya Mungu iliyo kwenye Kanda.

Nasi hatuna budi kumfuata, ndiyo njia pekee ya kupata Uzima wa Milele. Kwa hivyo uongozi wa Mungu ni: fuata Neno lililothibitishwa la wakati huu na Roho Mtakatifu.

NJIA PEKEE ya uzima wa Milele ni: Roho Mtakatifu kukuongoza kulifuata Neno lililothibitishwa. Ni nani aliye na Neno lililothibitishwa la wakati huu? Mungu alimchagua nani kulifasiri Neno Lake? Ni nani ambaye Mungu alimsema ndiye Sauti Yake ya wakati huu? Ni nani ambaye Mungu Mwenyewe alimsema alikuwa ndiye kiongozi aliyethibitishwa kumwongoza Bibi-arusi Wake leo? Je, Ni wahudumu?

Kama tu nilivyosema, maskini yule tai mdogo aliposikia Sauti ya Bwana Arusi, alienda Kwake, Neno la Mungu lililotiwa mafuta, lililothibitishwa kwa ajili ya siku hizi za mwisho.

Nuhu alikuwa ndiye Neno lililothibitishwa la wakati wake.

Musa alikuwa ndiye Neno lililothibitishwa la wakati wake.

Yohana alikuwa ni Neno lililothibitishwa

Wanaweza kulipindisha au kuliwekea fasiri yoyote Kwake watakayo, Bali:

WILLIAM MARRION BRANHAM NDIYE NENO LA MUNGU LILILOTHIBITISHWA LA WAKATI HUU!!

Kwa hivyo uongozi wa Mungu ni: fuata Neno lililothibitishwa la wakati huu na Roho Mtakatifu.

Na Je, kuicheza Sauti ya Mungu iliyothibitishwa katika kanisa lako silo jambo lililo muhimu kuliko ambalo Bibi-arusi analopaswa kufanya? Je, ni muhimu zaidi kuisikiliza sauti tofauti?

Je! ni kundi la watu na huduma yao ndiyo itakayomuunganisha na kumwongoza Bibi-arusi? Je, Bibi-arusi ataunganishwa na yale wasemayo wahudumu? Wote wanasema mambo tofauti, kwa hivyo tumfuate nani?

Je! Ni fasiri yao ya Ujumbe huu ndiyo tutakayohukumiwa kwayo? Je! wao wanayo Nguzo ya Moto inayoithibitisha huduma yao? Je! fasiri yao ya Neno ndiyo Yakini yako?

Nabii alisema Bibi-arusi ANGEUNGANA. Jiulize mwenyewe, ni kitu gani kitakachoufanya unabii huu utimie ili Bwana aje na kumnyakua Bibi-arusi Wake?

Ndiposa, watu wa Mungu waanzapo kukusanyika pamoja, kuna umoja, kuna nguvu. Ona? Na wakati wo wote watu wa Mungu watakapoungana pamoja kabisa, naamini ufufuo utatokea wakati huo. Kutakuwako na wakati wa kunyakuliwa Roho Mtakatifu aanzapo kuwakusanya. Wao—itakuwa katika uchache, bila shaka, lakini kutakuwepo na kukutanika kukuu.

Je! Kutakuwepo na kukutanika kukuu kwenye huduma ya mtu fulani, mbali na nabii wa Mungu aliyethibitishwa? Je! litakuwa ni KUNDI la wahudumu kwa sababu baadhi ya wahudumu wa huduma tano wanasema Hupaswi KAMWE kuicheza Sauti ya Mungu kanisani mwako, ni makosa. Je! wao watamwongoza Bibi-arusi basi?

TAFADHALI NISAIDIE! NI MHUDUMU GANI NINAYEPASWA KUMFUATA, KWANI NATAKA KUUNGANA KATIKA KULE KUKUTANIKA KUKUU.

Wengine husema ati wahudumu wa huduma tano wa Ngurumo Saba ndiyo watakaomkamilisha Bibi-arusi. Baadhi ya wahudumu wa huduma tano wanasema siku za huduma ya Mtu Mmoja zimekwisha. Baadhi ya wahudumu wa huduma tano wanasema yatubidi turudi kwenye Pentekoste. Wengine husema Ujumbe SIO Yakini. Wengine wanasema ukizicheza kanda wewe ni mwamini mungu-mtu. Wote wanasema kitu fulani tofauti, na WOTE wana fasiri tofauti, mawazo tofauti, lakini kila mmoja anasema WAO wanaongozwa na Roho Mtakatifu.

NI MHUDUMU GANI WA HUDUMA TANO NIMFUATE? Maadamu ninamfuata mchungaji “WANGU” wa huduma tano, nitakuwa Bibi-arusi? Kuna “Vikundi” vingi tofauti vya wahudumu wa huduma tano. Hawa wahudumu 20 wanakusanyika na kufanya mikutano yao, lakini wao hawakubaliani kabisa na wahudumu hao wengine 20 walio na mikutano tofauti…niende kwenye mikutano gani ili nikamilishwe na kuungana…baadhi ya hiyo…yote?

Nao watu wanaamini ati MCHAFUKO HUU UTAMUUNGANISHA NA KUMKAMILISHA BIBI-ARUSI? Wote wanasema wao ni WATUMISHI WA KWELI WA HUDUMA TANO ALIYEITWA NA MUNGU. Lakini wao hawawaongozi ninyi kwenye UONGOZI WA KWELI WA ROHO MTAKATIFU, WAO WANAWAONGOZA NINYI KWAO WENYEWE NA KWENYE HUDUMA YAO.

Kwangu mimi, hata huhitaji ufunuo kujua kwamba hilo haliwezi kamwe KUMUUNGANISHA au KUMUONGOZA Bibi-arusi wote. Ni NENO PEKE YAKE litakalomuunganisha Bibi-arusi, kwa SAUTI YA MUNGU MWENYEWE ILIYO KWENYE KANDA.

Ndugu na dada, afadhali muamke ikiwa mnamfuata mchungaji ambaye anahubiri tu na kunukuu Neno, ambalo ni zuri na NDILO HASA analopaswa kuwa akifanya, lakini yeye hawaambii, na muhimu zaidi, HAFANYI HIVYO, kuicheza SAUTI YA MUNGU ILIYO KWENYE KANDA KANISANI MWENU.

Ndugu Branham alituambia:

Naam, tuna tu maagizo matatu ya Kiungu tuliyoachiwa: mojawapo ni—ni ushirika; kutawadhana miguu; ubatizo wa maji. Hayo ndiyo tu mambo matatu. Huo ndio ukamilifu, wa utatu, mnaona.

Ningependa tuwe na Ibada ya Ushirika na Kutawadhana Miguu Jumapili hii, Bwana akipenda. Kama tulivyofanya wakati uliopita, ningewahimiza muanze saa 11:00 JIONI. kwa masaa ya eneo mnaloishi. Ingawa Ndugu Branham alisema mitume walikuwa na Ushirika kila wakati walipokutana pamoja, alipendelea kuufanya wakati wa jioni, naye akautaja kama Meza ya Bwana.

Ujumbe na Ibada ya Ushirika utakuwa kwenye Redio ya Sauti, na pia kutakuwa na anuani ya faili lakupakuliwa, kwa wale ambao hawawezi kuifanikisha Redio ya Sauti Jumapili jioni.

Ndugu Joseph Branham

25-0810 Matukio Ya Sasa Yanadhihirishwa Na Unabii

UJUMBE: 65-1206 Matukio Ya Sasa Yanadhihirishwa Na Unabii

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Kweli na Aliye Hai,

Wakati Yesu, Neno Mwenyewe, alipokuja duniani miaka 2000 iliyopita, Yeye alikuja kama vile alivyosema angekuja, kama Nabii. Neno Lake linatangaza, ya kwamba kabla Yeye hajaja tena, kule kudhihirishwa kukamilifu kwa Utu wa Yesu Kristo kutadhihirishwa tena katika mwili, katika nabii. Nabii huyo amekuja, jina lake ni William Marrion Branham.

Mtu yeyote anawezaje kutotambua kwamba kuisikiliza Sauti ya Mungu ikizungumza nao moja kwa moja kwenye kanda ndiyo Mapenzi makamilifu ya Mungu? Tunajua Neno daima humjia nabii Wake; Haliwezi kuja kwa njia nyingine yoyote. Halina budi kuja kupitia njia ya Mungu ambayo Yeye alitutabiria. Hiyo ndiyo njia pekee litakavyopata kuja. Mungu anasonga mbele moja kwa moja jinsi Yeye alivyoahidi angefanya. Yeye kamwe hakosi kufanya kwa njia ile ile Yeye aliyofanya daima.

Kila mmoja wao alikula kitu kile kile, wote walicheza katika Roho, wote walikuwa na kila kitu shirika; bali ilipofikia wakati wa utengano, Neno lilitenganisha. Ndivyo ilivyo siku hizi! Neno lilitenganisha! Wakati utakapowadia…

Tunauona wakati huo unatukia sasa hivi, Neno linatenganisha. Bibi-arusi anashutumiwa kwa kumwinua sana nabii wakati wao wanaposema, “Kuna wengine walioitwa na Mungu, watu waliojazwa na Roho Mtakatifu wa kumwongoza Bibi-arusi leo. Mnahitaji zaidi ya hizo kanda tu. Mungu amewaweka watu leo kuliongoza kanisa.”

“Unajaribu kuwazia wewe ndiwe uliye peke yako kwenye kundi lile. Kusanyiko lote ni takatifu!” Mungu kamwe hajawahi kushughulika jinsi hiyo. Alipaswa kuwa amejua vyema kuliko hivyo. Naye akasema, “Vema, kusanyiko lote ni takatifu. Unajaribu kujifanya…” Kama tungalilisema siku hizi, maneno ya mtaani, “Changarawe pekee ufukoni.”

Naye Musa alijua ya kwamba Mungu alikuwa amemtuma huko chini kwa ajili ya jambo hilo.

Mungu anao watu waliojazwa na Roho Mtakatifu wa kumwongoza Bibi-arusi Wake; kuwaongoza KWENYE BWANA ASEMA HIVI, NABII-MJUMBE. Kwani Ujumbe na mjumbe ni kitu kimoja. Hiyo ndiyo njia ya Mungu isiyobadilika kamwe kwa ajili ya siku hii, na daima.

Kwa sababu walisikiliza kosa fulani. Wakati Musa, aliyethibitishwa na Mungu, na kiongozi wa kuwaonyesha njia ya kwenda kwenye nchi ya ahadi, nao walikuwa wamekuja umbali huo vema, lakini basi wasingeendelea pamoja naye… Sasa, waaminio wanaweza kuona jambo hilo, bali wasioamini hawawezi kuliona Hilo limethibitishwa.

Sio tu kwamba wewe ulichaguliwa kuupokea Ufunuo huu mkuu wa wakati wa mwisho wa siku hii, bali Mungu, kwa njia ya Chakula Chake kilichohifadhiwa cha kanda, hunena katikati ya mistari na Bibi-arusi Wake kipenzi.

Ndipo endapo wewe ni mwana wa Mungu ama binti ya Mungu, ulikuwa ndani ya Mungu wakati wote. Lakini Yeye alijua utapandwa kwenye tuta gani na katika wakati gani. Kwa hiyo sasa umefanywa kiumbe, mwana wa Mungu, mwana ama binti ya Mungu aliyedhihirishwa upate kukabiliana na changamoto ya wakati huu kumthibitisha Mungu wa kweli na aliye hai wa wakati huu, Ujumbe unaotokea katika wakati huu. Hiyo ni kweli! Ulikuwapo pale kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Ni barua ya mahaba ilioje ya katikati ya mistari kwa Bibi-arusi Wake, UTUKUFU!!! Sio tu kwamba Yeye alitujua na kutuchagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, bali hapa Yeye anatuambia kwamba alituchagua sisi tuwe wana na binti zake waliodhihirishwa wa SIKU HII. Alituweka hapa duniani leo, juu ya watakatifu wengine wote tangu mwanzo, kwa maana Alijua sisi tungekabiliana na changamoto ya wakati huu kumthibitisha Mungu wa kweli na aliye hai wa wakati huu, Ujumbe unaotokea katika wakati huu.

Sisi tulikuwa ndani ya Mungu, jeni, neno, sifa tangu mwanzo, lakini SASA tunaketi PAMOJA katika ulimwengu wa roho katika Kristo Yesu, tukishiriki pamoja Naye kwa Neno Lake, kupitia Neno Lake; kwa kuwa sisi ni NENO LAKE, nalo linazilisha nafsi zetu.

Hatuwezi, na hatutaingiza Kitu chochote maishani mwetu ila Neno la Mungu lisiloghoshiwa. Tunatambua na kuamini kuwa Ndio njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku hii.

Tungependa muungane nasi Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapoisikia SAUTI PEKEE, Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda, unayoweza kusema AMINA kwayo, kwa kila Neno unalosikia.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: Matukio Ya Sasa Yanadhihirishwa Na Unabii 65-1206

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Mwanzo 22
Kumbukumbu la Torati 18:15
Zaburi 16:10 / 22:1 / 22:18 / 22:7-8 / 35:11
Isaya 7:14 / 9:6 / 35:7 / 50:6 / 53:9 / 53:12 / 40:3
Amosi 3:7
Zekaria 11:12 / 13:7 / 14:7
Malaki 3:1 / 4:5-6
Mathayo 4:4 / 24:24 / 11:1-19
Luka 17:22-30 / 24:13–27
Waebrania 13:8 / 1:1
Yohana 1:1
Ufunuo 3:14-21 / 10:7

25-0803 Mambo Yatakayokuwapo

UJUMBE: 65-1205 Mambo Yatakayokuwapo

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Sifa za Mungu,

Kila Neno lililonenwa katika Ujumbe huu ni barua ya mahaba kwa Bibi-arusi Wake. Kuwazia kwamba Baba yetu wa Mbinguni Yeye anatupenda sana, si tu kwamba Yeye alitaka tulisome Neno Lake, bali Alitaka tuisikie Sauti Yake ikizungumza na mioyo yetu ili aweze kutuambia: “Wewe ndiye usia Wangu ulio hai, sifa Yangu iliyo hai, ambayo ninaweza kuionyesha kwa ulimwengu.”

Kisha kuwazia kwamba baada ya dhabihu zake zote alizotoa hapa duniani, maisha aliyoishi, njia aliyofuata. Aliomba jambo moja:

“Ili nilipo Mimi, nao wawepo.” Yeye aliomba ushirika wetu. Hicho ndicho kitu pekee alichomwomba Baba katika maombi, ushirika wenu milele.

Nilipo Mimi, “Neno Lake,” hatuna budi kuwapo pia, kupokea ushirika Wake, ushirika Wake, milele. Kwa hiyo, ni lazima tuishi kwa kila Neno Yeye alilonena nasi kwenye kanda ili tuwe Bibi-arusi Neno Bikira Wake, ambalo linatufanya kuwa sehemu ya Bwana-arusi.

Huo ndio UFUNUO wa Yesu Kristo katika wakati huu. Si vile Yeye alivyokuwa katika wakati mwingine, Yeye ni nani SASA HIVI. Neno la siku hii. Mungu yuko wapi leo. Huo ndio Ufunuo wa siku hii. Sasa unakua katika Bibi-arusi, ukitufanya kufikia kimo kikamilifu cha wana na binti.

Tunajiona wenyewe katika Neno Lake. Tunajua sisi ni nani. Tunajua tuko katika mpango Wake. Hii ndiyo Njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku hii. Tunajua Unyakuo umekaribia. Hivi karibuni wapendwa wetu wataonekana. Kisha tutajua: Tumewasili. Sote tunaenda Mbinguni…ndiyo, Mbinguni, mahali halisi tu kama hapa.

Tunaenda mahali halisi ambapo tutafanya mambo, ambapo tutaenda kuishi. Tutafanya kazi. Tutapafurahia. Tutaishi. Tunaenda kwenye Maisha, kwenye Maisha halisi ya Milele. Tunaenda Mbinguni, paradiso. Kama tu vile Adamu na Hawa walivyoshughulika, na kuishi, na kula, na kufurahia, katika bustani ya Edeni kabla dhambi haijaingia, tuko njiani tukirudi moja kwa moja kule tena, moja kwa moja, kurudi moja kwa moja. Adamu wa kwanza, kwa njia ya dhambi, alitutoa. Adamu wa Pili, kwa njia ya haki, anaturudisha kutuingiza ndani tena; anatuhesabia haki na kuturudisha ndani.

Mtu yeyote anawezaje kuliweka katika maneno Kile jambo hili linachomaanisha kwetu sisi? Uhalisia kwamba tunakwenda kwenye paradiso ambapo tunaishi katika umilele wote pamoja. Hakuna huzuni tena, maumivu au kilio, ni ukamilifu tu juu ya ukamilifu.

Mioyo yetu inafurahi, roho zetu zinawaka moto ndani yetu. Shetani anazidi kutupa presha kila siku, lakini bado tunafurahi. Kwa nini:

• TUNAJUA, SISI NI NANI.
• TUNAJUA, HATUJA, NA HATUTA, MWANGUSHA YEYE.
• TUNAJUA, TUKO KATIKA MAPENZI YAKE MAKAMILIFU.
• TUNAJUA, YEYE AMETUPA UFUNUO WA KWELI WA NENO LAKE.

Ndugu Joseph, unaandika jambo lile lile kila wiki. UTUKUFU, nitaliandika kila wiki kwa sababu Yeye anakutaka ujue jinsi gani anavyokupenda. Wewe ni nani. Ni wapi unakokwenda. Hasi inakuwa chanya. Wewe ni Neno ukifanyika Neno.

Mpendwa ulimwengu, njooni muungane nasi Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville, (ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) kwenye mawasiliano ya simu, si kwa sababu “Mimi” ninawaalika, bali kwa sababu “YEYE” anawaalika. Si kwa sababu “Mimi” niliichagua kanda, bali kulisikia Neno pamoja na sehemu ya Bibi-arusi ulimwenguni kote kwa wakati mmoja.

Je! tunaweza kutambua kwamba inawezekana kwa Bibi-arusi kuisikia Sauti ya Mungu ulimwenguni kote, wote kwa wakati ule ule hasa? Huyo hana budi kuwa ni Mungu. Mungu alimfanya nabii afanye hivyo wakati ule malaika Wake alipokuwa hapa duniani. Yeye alimuhimiza Bibi-arusi kuungana katika maombi, WOTE KWA WAKATI ULE ULE WA JEFFERSONVILLE, saa 3:00, 6;00, 9:00; hilo ni kuu jinsi gani sasa hivi, kwamba Bibi-arusi anaweza kuungana kama KITU KIMOJA kuisikia Sauti ya Mungu ikinena nao wote kwa wakati mmoja?

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: Mambo Yatakayokuwapo 65-1205

Maandiko:

Mathayo 22:1-14
Yohana 14:1-7
Waebrania 7:1-10

25-0727 Unyakuo

UJUMBE: 65-1204 Unyakuo

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Bila Masharti,

Bwana alitupa wakati mzuri sana kambini wiki iliyopita alipotufunulia Neno Lake. Alithibitisha, kwa Neno Lake, ya kwamba Yakini yetu ni: Neno Lake, Ujumbe Huu, Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda; wote ni mmoja, Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. 

Tulisikia jinsi ambavyo shetani anavyojaribu kuutenganisha Ujumbe kutoka kwa mjumbe, lakini Bwana Yesu asifiwe, Mungu Mwenyewe alinena kupitia malaika Wake Mwenye nguvu na kutuambia:

Tunaona ya kwamba mtu anapokuja, ametumwa kutoka kwa Mungu, amechaguliwa na Mungu, akiwa na BWANA ASEMA HIVI ya kweli, ujumbe huo na mjumbe huyo ni mmoja na kitu kimoja. Kwa sababu yeye ametumwa kuwakilisha BWANA ASEMA HIVI, Neno kwa Neno, kwa hiyo yeye pamoja na ujumbe wake ni mmoja.

Huwezi kuutenganisha Ujumbe na mjumbe, wao ni kitu kimoja, BWANA ASEMA HIVI. Haijalishi kile mpakwa mafuta yeyote wa uongo anachosema, Mungu alisema wao ni mmoja na hawawezi kutenganishwa.

Kisha akatuambia hatuhitaji tambara la chujio ili kuwashika wadudu wowote wakati tunapozisikiliza kanda, kwa maana hakuna wadudu ama utomvu wa mdudu katika Ujumbe Huu. Ni kisima Chake kinachofoka maji ambacho daima kinatiririka kisafi na cheupe. Hububujika daima, hakikauki kamwe, kinaendelea tu kusukuma na kusukuma, kikitupa Ufunuo zaidi na zaidi wa Neno Lake.

Yeye alitukumbusha KAMWE TUSISAHAU kwamba agano Lake na sisi ni lisilopingika, halibadiliki, lakini zaidi ya yote, halina Masharti.

Iwe ni upendo, usaidizi au kujisalimisha, ikiwa jambo lisilo na masharti ni YAKINI nalo halijatii sheria na masharti yoyote maalum: litatendeka bila kujali ni nini kingine kitakachotokea.

Kisha akataka kuushindilia msumari, kwa hivyo akatuambia kwamba leo hii Maandiko Yake yanatimizwa mbele ya macho yetu.

J-u-a lile lile lipambazukalo mashariki ndilo j-u-a lile lile litualo magharibi. Na M-w-a-n-a yule yule wa Mungu aliyetokea mashariki na kujithibitisha Mwenyewe kama Mungu aliyefanyika mwili ndiye M-w-a-n-a yule yule wa Mungu aliyeko katika kizio cha magharibi cha dunia ambaye anajitambulisha Mwenyewe kati ya kanisa usiku huu, Yeye yule jana, leo, na hata milele. Ile Nuru ya jioni ya Mwana imekuja. Leo Maandiko haya yametimia mbele yetu.

Yule Mwana wa Adamu amekuja tena katika mwili wa mwanadamu katika siku yetu, kama vile tu Yeye alivyoahidi angefanya, kumwita Bibi-arusi atoke. Ni Yesu Kristo akizungumza nasi moja kwa moja, na haihitaji fasiri yoyote ya mwandamu. Kitu pekee tunachohitaji, kitu pekee tunachotaka, ni Sauti ya Mungu inayonena kwenye kanda kutoka kwa Mungu Mwenyewe.

Ni ufunuo wa dhihirisho la Neno likifanywa halisi. Nasi tunaishi katika siku hiyo; Mungu asifiwe; Ufunuo wa siri ya Yeye Mwenyewe.

Ni wakati mtukufu jinsi gani Bibi-arusi aliyonao, akiwa amekaa kwenye uwepo wa Mwana, akiivishwa. Ngano imeirudia ngano tena, na hakuna chachu miongoni mwetu. Ni Sauti ya Mungu safi tu ikinena nasi, ikitufinyanga na kutufanya kuwa sura ya Kristo, aliye Neno.

Sisi ni wana na binti za Mungu, sifa Yake ile aliyoichagua tangu zamani ije katika wakati huu, wakati ulio mkuu sana katika historia ya ulimwengu.  Yeye alijua sisi hatungeshindwa, hatungepatana, bali tungekuwa Bibi-arusi Neno Wake mkweli na mwaminifu, Uzao Wake Mkuu wa Kifalme wa Ibrahimu ulioahidiwa ambao ungekuja.

Unyakuo umekaribia. Wakati umefika mwisho. Yeye anakuja kumchukua Bibi-arusi Wake ambaye amejiweka mwenyewe tayari bali amekaa kwenye Uwepo wa Mwana, akiisikia Sauti Yake ikimvika Bibi-arusi Wake. Hivi karibuni tutaanza kuwaona wapendwa wetu walioko ng’ambo ya pazia la wakati, ambao wanatungojea na kutamani sana kuwa pamoja nasi.

Kanda ndiyo njia iliyoandaliwa na Mungu ya kumkamilisha Bibi-arusi Wake. Kanda hizi ndicho kitu pekee kitakachomuunganisha Bibi-arusi Wake. Kanda hizi ndiyo Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi Wake.

Ninawalika mje muungane nasi, sehemu ya Bibi-arusi Wake, Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia kila kitu kuhusu kile kinachokaribia kutukia hivi karibuni: Unyakuo 65-1204. 

 
Ndugu. Joseph Branham

25-0720 Juu Ya Mbawa Za Hua Mweupe Kama Theluji

UJUMBE: 65-1128E Juu Ya Mbawa Za Hua Mweupe Kama Theluji

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukusanyike pamoja Jumapili saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) ili kusikia  65-1128E Juu Ya Mbawa Za Hua Mweupe Kama Theluji.

Ndugu. Joseph Branham

25-0713 Mahali Pekee Palipowekwa Na Mungu Pa Kuabudia

UJUMBE: 65-1128M Mahali Pekee Palipowekwa Na Mungu Pa Kuabudia

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Familia ya Yesu Kristo,

Jambo fulani linatendeka zaidi ya hapo nyuma kwa Bibi-arusi wa Kristo kote ulimwenguni. Mambo ambayo tumeyasikia na kutamani kuyaona sasa yanadhihirika mbele ya macho yetu.

Roho Mtakatifu anamuunganisha Bibi-arusi Wake kama alivyosema angefanya, kwa njia Yake PEKEE aliyoiandaa kwa ajili ya siku hii, Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.

Yeye analifunua na kulithibitisha Neno Lake zaidi ya hapo awali. Kama Kisima kinachofoka maji, Ufunuo unabubujika ndani yetu.

Huo muungano wa kiroho wa Kristo na Kanisa Lake sasa, wakati mwili unapofanyika Neno, nalo Neno linafanyika mwili, linadhihirishwa, linathibitishwa. Vile vile hasa Biblia ilivyosema ingetendeka katika siku hii, inatendeka, siku baada ya siku. Mbona, inalundikana upesi sana huko nje, katika yale majangwa, na mambo yanayotendeka, hata nisingeweza kufuatilia jambo hilo.

Kila siku Ufunuo zaidi na zaidi unafunuliwa na kudhihirishwa kwetu. Kama vile nabii, mambo yanatokea na yanatendeka haraka sana, hatuwezi hata kuyafuatilia…UTUKUFU!!!

Wakati wetu umefika. Maandiko yanatimia. Mwili unafanyika Neno, nalo Neno linafanyika mwili. Vile vile nabii alivyosema yangetukia sasa yanatendeka.

Kwa nini sisi?

Hakuna chachu, hakuna sauti isiyojulikana, hakuna fasiri ya mwanadamu inayohitajika miongoni mwetu. Tunalisikiliza tu Neno Safi Kamilifu kutoka kwenye kinywa cha Mungu kwa anavyozungumza nasi mdomo kwa sikio.

Sasa tunaona Neno lile lile lililoahidiwa, la Luka, la Malaki, ahadi hizi nyingine zote za siku ya leo, zikifanyika mwili, zikikaa kati yetu, ambazo tulisikia kwa masikio yetu; sasa tunamwona Yeye (kwa macho yetu) akifasiri Neno Lake Mwenyewe, hatuhitaji fasiri yo yote ya mwanadamu.

Ewe Bibi-arusi, hilo haliwezi kuwa wazi zaidi ya hapo. Ni Mungu, akisimama mbele ya Bibi-arusi Wake katika mwili wa mwanadamu, ambaye tunaweza kumwona kwa macho yetu wenyewe, akizungumza na kulifasiri Neno Lake Mwenyewe, na kuliweka kwenye kanda. Neno Kamilifu lililonenwa na kurekodiwa na Mungu Mwenyewe, hivyo halihitaji fasiri yoyote ya mwanadamu.

  • • Mungu anazungumza moja kwa moja na Bibi-arusi Wake, kwenye kanda.
  • • Mungu hulifasiri Neno Lake Mwenyewe, kwenye kanda.
  • • Mungu anajifunua Mwenyewe, kwenye kanda.
  • • Mungu akimwambia Bibi-arusi Wake, huhitaji fasiri yoyote ya mwanadamu, Neno Langu lililo kwenye kanda ndiyo yote BIBI-ARUSI WANGU ANALOHITAJI.

Kumbukeni, mtakapoondoka hapa, anzeni kutoka kwenye kapi sasa; mnaingia kwenye punje, bali kaeni katika Uwepo wa Mwana. Msiongeze, yale nimesema; msiondoe, yale nimesema. Kwa sababu, ninazungumza Ukweli kadiri niujuavyo, kama vile Baba alivyonipa. Mnaona?

Mungu ameitengeneza NJIA KAMILIFU PEKEE kwa Bibi-arusi kufanya vile hasa Yeye alivyotuamuru kufanya. Hilo halikuwezekana, hadi leo hii. Hakuna kubahatisha, hakuna kushangaa, hakuna swali ikiwa humo kuna kitu chochote kilichoongezwa, kuondolewa, au kufasiriwa. Bibi-arusi amepewa ule Ufunuo wa kweli: KUZICHEZA KANDA NDIYO NJIA KAMILIFU YA MUNGU.

Ikiwezekana, hebu niliseme hilo tena. Ufunuo wangu ni kwamba Bibi-arusi wa Yesu Kristo, si wengine, BIBI-ARUSI, hahitaji KITU KINGINE ila Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.

Lakini mara huyo Roho Mtakatifu kweli…Neno halisi linapoingia ndani yako (Neno, Yesu), basi, ndugu, Ujumbe si siri kwako basi; unaujua, ndugu, wote umeangaziwa mbele yako.

Ujumbe si siri kwangu. Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. Mbingu na nchi zote zinaitwa Yesu. Yesu ni Neno.

Nalo hilo Jina limo katika Neno kwa kuwa Yeye ni Neno. Amina! Yeye ni nini basi? Neno lililofasiriwa ni dhihirisho la Jina la Mungu.

Mungu anamuunganisha Bibi-arusi Wake na Sauti Yake, ambayo alikuwa ameirekodi na kuihifadhi kwa ajili ya siku hii, ili kwamba aweze kumkusanya Bibi-arusi Wake pamoja kama Jamii Moja. Bibi-arusi yeye ataliona na kulitambua Hilo kuwa NJIA PEKEE Yeye anayoweza kumkusanya Bibi-arusi Wake pamoja.

Yeye alilifanya hilo zaidi ya miaka 60 iliyopita ili kutuonyesha sisi jinsi gani ambavyo Yeye angelifanya hilo leo. Sisi ni “moja ya makanisa yake kwenye muunganisho wa simu”

Kama mimi siamini kwenda kanisani, basi kwa nini niwe na makanisa? Tulikuwa nayo kila mahali nchini, yameunganishwa hivi majuzi usiku, kila maili mia mbili mraba kulikuwapo na kanisa langu.

Wahudumu wengi huyaambia makanisa yao kuwa kwenye “muunganisho wa simu” au “kusikiliza hewani”, “kuusikiliza Ujumbe mmoja kwa wakati mmoja”, ati sio kwenda kanisani. YEYE AMETOKA KUSEMA HUKO NI KWENDA! Wao ni kwamba tu aidha hawalijui Neno ama hawawezi kuisoma barua ya mahaba kama vile Bibi-arusi awezavyo.

Kanisa ni nini? Hebu na tuone kile Ndugu Branham alichosema kanisa lilicho.

Makusanyiko mengi, mengi yamepata makao haya kama mlivyokuwa nayo hapa kutoka maskani. Pia imeunganishwa huko Phoenix, ya kwamba kila mahali ibada zilipo, inaingia moja kwa moja kwenye…Na wanakusanyika makanisani na majumbani, na mambo kama hayo, kupitia wimbi zuri sana.

Ndugu Branham anasema waziwazi kwamba watu wakiwa “majumbani” mwao na “mambo kama hayo” walikuwa ni moja ya makanisa yake kwenye muunganisho wa Simu. Kwa hivyo majumba, vituo vya mafuta, majengo, familia zilizokusanyika pamoja kwenye muunganisho wake wa simu hilo liliwafanya kuwa kanisa.

Hebu na tuisome kidogo zaidi BARUA YA MAHABA.

Tunayaombea makanisa yote na makusanyiko ambayo yamekusanyika kuzunguka vile—vile—vile vipaza sauti vidogo nchini kote, kutoka kwenye taifa, kote kote hata kwenye Pwani ya Magharibi, kule juu kwenye milima ya Arizona, chini kwenye mabonde ya Texas, mbali sana hata Pwani ya Mashariki, nchini kote, Bwana, ambako wao wamekutanika. Tuko umbali wa masaa mengi, bali, Bwana, sisi tuko pamoja usiku wa leo kama jamii moja, waamini, tukingojea kuja kwa Masihi.

Kwa hivyo wakiwa kwenye Muunganisho wa Simu, wakimsikiliza Ndugu Branham WOTE KWA WAKATI MMOJA; walikuwa pamoja kama jamii moja, waamini, wakingojea Kuja kwa Masihi.

Lakini ninyi mnasema ukifanya hivyo leo, huko sio kwenda kanisani, ati ni makosa, sio kukusanyika pamoja na zaidi sana tunapoona ile siku ikikaribia, huko sio kwenda kanisani?

Hebu niwaulizeni swali nanyi myajibu makusanyiko yenu. Kama Ndugu Branham angekuwa hapa leo, katika mwili, nanyi mngeweza kusikiliza hewani au kujiunganisha kwa simu ili kumsikiliza yeye kila Jumapili asubuhi, wote kwa wakati mmoja pamoja na Bibi-arusi kote ulimwenguni, enyi wachungaji, Je! mngeweza KUJIUNGANISHA KWA SIMU na kumsikia Ndugu Branham au mngehubiri?

Ndugu Branham anasema waziwazi wajibu wako ni kanisa lako. Kama ungekuwa hapa miaka 60 iliyopita naye Ndugu Branham alikuwa na ibada, lakini kanisa lako halingehudhuria bali lilikuwa na ibada yao wenyewe (jambo ambalo wahudumu wengi walilifanya wakati huo), Je, wewe ungeweza kwenda kwenye “kanisa lako”, au ungeenda kwenye “Maskani ya Branham” kumsikiliza Ndugu Branham?

Nitawapa jibu langu. Mimi ningekuwa nikisimama mlangoni kwenye mvua, theluji au tufani ya theluji ili niingie Maskanini kumsikiliza nabii wa Mungu. Kama NINGEKUWA nikienda kwenye lile kanisa lingine, ningeyabadilisha makanisa usiku huo.

Lakini mwanamke yule, hakujua kama nguvu zilikuwa katika ile fimbo ama la, bali yeye alijua Mungu alikuwa ndani ya Eliya. Hapo ndipo yule Mungu alipokuwa: ndani ya nabii Wake. Akasema, Kama Bwana aishivyo, na nafsi yako iishivyo, sitakuacha.

Ninawaalika kuungana nasi na kuwa moja ya makanisa ya Ndugu Branham kwenye muunganisho wa simu siku ya Jumapili saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapoisikia Sauti ya Mungu ikituletea Ujumbe: Mahali Pekee Palipowekwa Na Mungu Pa Kuabudia 65-1128M.

Ndugu. Joseph Branham

25-0706 Nimesikia Bali Sasa Ninaona

UJUMBE: 65-1127E Nimesikia, Bali Sasa Ninaona

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi aliyeunganishwa kwa simu,

Leo, Maneno haya Mungu aliyoyanena kupitia Malaika-Mjumbe Wake wa Saba yangali yanatimia kupitia SISI, BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO. 

Kama mimi siamini kwenda kanisani, basi kwa nini niwe na makanisa? Tulikuwa nayo kila mahali nchini, yameunganishwa kwa simu hivi majuzi usiku, kila maili mia mbili mraba kulikuwapo na kanisa langu.

Walikuwa katika makanisa, majumbani, majengo madogo, na hata kituo cha mafuta; wakiwa wametawanyika kote Marekani, wakisikiliza, wote kwa wakati mmoja Neno lilikuwa likitoka. 

Na leo hii, sisi tungali ni MOJA YA MAKANISA YAKE.  Yeye ANGALI NI MCHUNGAJI WETU. Neno Lake LINGALI HALIHITAJI FASIRI YOYOTE, nasi TUNGALI tumekusanyika ulimwenguni kote, TUMEUNGANISHWA KWA SIMU, tukiisikiliza SAUTI ya Mungu ikimkamilisha Bibi-arusi wa Yesu Kristo.

Leo, Neno hili lingali linatimia.

Kwa nini wao walifanya hivyo wakati huo? Kwa nini wachungaji waliyafunga makanisa yao ili kuusikia Ujumbe moja kwa moja? Wao wangeweza kusubiri tu wazipate kanda, kisha wakahubiri Ujumbe wao wenyewe kwa watu wao baadaye; nami nina hakika wengi wasio na Ufunuo walifanya hivyo. 

Au labda wengine waliyaambia makusanyiko yao, “Sasa sikilizeni, sisi tunaamini Ndugu Branham ni nabii wa Mungu, lakini yeye hakusema tunatakiwa kumsikiliza yeye katika makanisa yetu. Mimi ninahubiri Jumapili hii, na kila Jumapili; ninyi zichukueni tu kanda na mzisikilize huko majumbani mwenu.”

Bibi-arusi wakati ule, ni kama tu Bibi-arusi sasa hivi, walikuwa na Ufunuo, nao walitaka kuisikia Sauti ya Mungu moja kwa moja wao wenyewe. Walitaka kuungana na Bibi-arusi kote nchini waisikie Sauti ya Mungu ilipokuwa ikitoka. Wao walitaka kutambulishwa kama moja ya makanisa yake, majumba, ama po pote walipokuwa, na Ujumbe, Sauti, na sasa, kanda. 

Leo, Neno hili lingali linatimia.

Kwa nini wao/sisi Tunaliona na wengine hawalioni? Kwa kujua tangu zamani, sisi tulichaguliwa kuliona Hili. Lakini ninyi ambao hamkuchaguliwa, kamwe hamtaliona. Ngano inaliona nayo imeanza kuondoka.

Haimaanishi kwamba unapaswa kuacha kwenda kwenye kanisa lako. Wala haimaanishi mchungaji wako aache kuhudumu.  Inamaanisha tu kwamba wahudumu wengi na wachungaji wengi wamesahau JAMBO KUU, nao hawawaambii watu wao SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI mnayopaswa kuisikia ni SAUTI ya Mungu iliyo kwenye kanda. 

Kwenda kanisani kila siku ya kila wiki hakukufanyi wewe kuwa Bibi-arusi; hayo si matakwa ya Mungu.  Mafarisayo na Masadukayo walikuwa na mafundisho hayo. Walijua kila herufi ya kila Neno, bali Neno lililo Hai lilikuwa limesimama PAPO HAPO katika mwili wa mwanadamu, lakini wao walifanya nini? Jambo lile lile wafanyalo wengi leo. 

Wao watasema, “hayo yalikuwa ni madhehebu aliyokuwa akizungumzia. Ambao hawangemruhusu Ndugu Branham kuhubiri makanisani mwao, bali sisi tunalihubiri Neno na tunasema vile tu yeye alivyosema.”

Hilo ni zuri. Bwana asifiwe. Hivyo ndivyo unavyopaswa kufanya. Lakini kisha useme, leo ni tofauti, ni makosa kuzicheza kanda za Ndugu Branham katika kanisa lako. Wewe hauna tofauti na Mafarisayo na Masadukayo, au madhehebu. 

Wewe ni mnafiki. 

Kama ilivyokuwa wakati huo, ni Yesu, akisimama mlangoni akibisha, akijaribu kuingia ndani anene moja kwa moja na Kanisa Lake, nao hawataifungua milango yao, nao hawatazicheza kanda katika makanisa yao. “Yeye haji katika kanisa letu ahubiri”.

Adui atageuza hilo na kulizungusha katika pande nyingi sana kwani ANACHUKIA kufichuliwa, lakini hata hivyo, linadhihirishwa mbele ya macho yetu na wengi wanajiondokea.  

“Hapo mwanzo kulikuwako” [kusanyiko linasema, “Neno!”—Mh.] “Naye Neno alikuwako kwa” [Kusanyiko linasema “Mungu!”—Mh.] “Naye Neno alikuwa” [Kusanyiko linasema “Mungu!”—Mh.]. “Naye Neno alifanyika mwili akakaa kwetu.” Hiyo ni kweli? Sasa tunaona Neno lile lile lililoahidiwa, la Luka, la Malaki, ahadi hizi nyingine zote za siku ya leo, zikifanyika mwili, zikikaa kati yetu, ambazo tulisikia kwa masikio yetu; sasa tunamwona Yeye (kwa macho yetu) akifasiri Neno Lake Mwenyewe, hatuhitaji fasiri yo yote ya mwanadamu. Ee kanisa la Mungu Aliye Hai! mlio hapa na kwenye simu! amkeni upesi, kabla hamjachelewa sana!

Ifungueni mioyo yenu na msikie yale ambayo Mungu ametoka kuwaambieni, makanisa yake yote. Sasa tunamwona YEYE, kwa macho yetu, AKILIFASIRI NENO LAKE MWENYEWE. Hatuhitaji fasiri yoyote ya mwanadamu!!  AMKENI KABLA HAMJACHELEWA!!

Tumeyasikia mambo haya maisha yetu yote yale yaliyokuwa yanaenda kutukia katika wakati wa mwisho. Sasa tunaliona kwa macho yetu hilo likitukia. 

Yeye Alituambia, KUNA NJIA MOJA PEKE YAKE, AMBAYO NDIYO NJIA YA MUNGU ILIYOANDALIWA ALIYOIFANYA KWA AJILI YA BIBI-ARUSI WAKE. LAZIMA UKAE NA SAUTI YA MUNGU ILIYO KWENYE KANDA.

Ninaualika ulimwengu mzima uje kuungana nasi Jumapili saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) na kuisikia Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii. Kisha wewe pia unaweza kusema, “Nimesikia habari Zako, bali sasa Ninakuona”.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: 65-1127E   Nimesikia Bali Sasa Ninaona

Maandiko

Mwanzo 17
Kutoka 14:13-16
Ayubu sura ya 14 na 42:1-5
Amosi 3:7
Marko 11:22-26 na 14:3-9
Luka 17:28-30