All posts by admin5

22-0807 Wa Kipekee

UJUMBE: 64-0614E Wa Kipekee

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Utukufu wa Shekina,

Jinsi gani mioyo na nafsi zetu zilivyoinuliwa hadi kufikia viwango vipya tulipokuwa tumekusanyika pamoja kutoka duniani kote, tukisikiliza Sauti ya Mungu ikizungumza kupitia mjumbe Wake na kutuhakikishia kwa mara nyingine tena, sisi ni nani.

Naye Anajifunika leo, katika vyombo vya udongo, pamoja na Shekina. Nje wanaonekana kana kwamba ni kundi la watakatifu wanaojifingirisha, ngozi za kale za pomboo, lakini ndani yake zinaficha Utukufu wa Shekina.

Utukufu kwa Mungu! Ndani yetu unajificha Utukufu wa Shekina. Tumeenda nyuma ya pazia nasi tunaweza kumwona Kristo waziwazi.

Leo hii, Mungu hatendi kazi akiwa ndani ya mwanadamu, Anatenda kazi kupitia mwanadamu. Yeye Alikuwa akitenda kazi akiwa katika mwanadamu wakati huo, Yesu. Sasa, Yeye anatenda Kazi kupitia mwanadamu ambaye yeye amemchagua kwa kusudi hili. Mungu, katika umbo la mwanadamu; Yeye Alijibadilisha kutoka katika umbo la Mungu, akawa katika umbo la mwanadamu.

Mungu Mwenyewe alijitokeza katika umbo la mwanadamu , kwa uzao wa kawaida wa Ibrahimu, kabla ya yale maangamizi, na Yesu alisema litakuwa ni jambo lile lile kwa Uzao huu wa kifalme kabla ya kurudi kwa Mwana aliyeahidiwa.

Mungu amejitokeza kwa mara nyingine tena katika umbo la mwanadamu, kama alivyoahidi angefanya. Ni Mungu aliyefichwa nyuma ya pazia la mwili uitwao William Marrion Branham. Isipokuwa uende nyuma ya pazia hilo na kuona Mungu, na si mwanadamu, umeukosa mpango wote wa Mungu.

Baadhi ya watu husema, “Ninyi watu mnamfanya Ndugu Branham kuwa mungu”. Vema, jambo hilo liko sawa kwa Namna fulani . Tunajua wanajaribu tu kutulaumu. Tunajua sisi hatukufanya hivyo. Bali pia tunajua hawalifahamu hilo, kwa maana wao wako upande wa pili wa ngozi, hawajaja nyuma ya pazia.

Tunaweza kusema waziwazi, “Vema, jambo hilo haliko mbali sana na Neno la Mungu sivyo? Tunawataka tu wajue kwamba hatujapotea. Tunajua tunaposimama. Tunajua tumetweka matanga ya namna gani, Na ni upepo wa namna gani unaoyavumia. Tunajua Hesi zetu zilivyo, na Nati yetu ni ipi . Nasi tunajua jinsi tunavyosimama.

Mungu alipodhihirishwa ulimwenguni, Yeye alikuwa amejificha nyuma ya pazia, nyuma ya ngozi ya Mtu aliyeitwa Yesu. Yeye alikuwa ametiwa utaji na kujificha nyuma ya ngozi ya mtu aliyeitwa Musa, nao walikuwa miungu, si Mungu ; bali walikuwa Mungu, yule Mungu mmoja, akibadilisha kinyago Chake tu, akifanya jambo lile lile kila wakati, akileta Neno hili.

Tumeingizwa kwenye Neno, Ujumbe na nabii wa wakati huu, na unatuvuta na kutupeleka kwenye Makao yetu ya Mbinguni. Sisi ni Wa Kipekee kwa ulimwengu, lakini Mungu ametutumia Nati ambayo inamtoa Bibi-arusi Wake atoke katika mchafuko huu, imwingize katika Uwepo wa Mungu. Sisi ni nati tuliyotiwa hesi kwa Neno.

Mungu, aliye na ngozi! Linaweza likasikika kama nati, kwa ulimwengu, bali linawavuta watu wote Kwake.

Ujumbe huu ni Mana itokayo Mbinguni, Chakula cha waamini ambacho ni kwa ajili yetu tu, nacho Kinamvuta Bibi-arusi Wake Kwake. Utukufu wa Shekina, juu ya Mkate wa Wonyesho, uliufanya usiharibike.

Mungu ameandaa Njia kwa ajili ya siku hii, Ujumbe huu na mjumbe wake; Mungu aliyefunikwa Aliye na ngozi . Sasa ni Mungu akijificha Mwenyewe ndani yetu, Bibi-arusi Wake, anayeweza tu kujilisha Sauti safi ya Mungu iliyothibitishwa na Nguzo ya Moto.

Sisi Hatupingani na huduma tano, Mungu apishe mbali, Mungu amewaita kuhudumu. Wanafuata na kufanya jinsi Roho Mtakatifu anavyowaongoza. Na sisi Tunafanya tu jinsi Roho Mtakatifu anavyotuongoza kufanya naye anatuongoza na kutuelekeza kushikilia hizo kanda peke yake.

Kwa hiyo, sasa , sikiliza kila Neno . Likamate. Na—na iwapo mnaunasa Huo kwenye kanda, ama cho chote kile , basi shikilieni kabisa Mafundisho hayo ya kanda . Msiseme kitu ila kile kanda hiyo inachosema. Semeni tu yale hasa kanda inayosema .

Kwetu sisi, NJIA PEKEE YA KUSIKIA: “KILA NENO,” “ SI KINGINECHO BALI YALE KANDA ZINACHOSEMA,” “ YALE HASA KANDA ZINACHOSEMA,” NI KUBONYEZA PLAY NA KUZISIKILIZA KANDA.

Kwa hiyo tunakualika uje kusikiliza yale hasa kanda zinachosema Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, ( Ni saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania) na uwe Wa Kipekee pamoja nasi tunaposikia Ujumbe: Wa Kipekee 64-0614E .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe :

I Wakorintho 1:18-25
2 Wakorintho 12:11

22-0731 Kufunuliwa Kwa Mungu

UJUMBE: 64-0614M Kufunuliwa Kwa Mungu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Neno lililoandikwa,

Kila wiki inakua kuu zaidi na zaidi. Jumapili, tulipata fursa ya kutazama, na kuamua, TULIONA NINI? Je, tuliona mhudumu , HAPANA! Je, tuliona mchungaji wetu, HAPANA! Tulipotazama nyuma ya pazia la mwili wa mwanadamu tulimwona Yesu Kristo akijifunua Mwenyewe na kujidhihirisha Mwenyewe.

Wakati tumekuwa tukizisikiliza hizo kanda kama zijavyo, Imekuwa dhahiri zaidi na zaidi, kama unayo masikio ya kusikia na macho ya kuona. Sasa tunamwona Mungu waziwazi. Pazia limepasuka, nasi tunamwona Mungu akisimama waziwazi mbele zetu, Yule Nguzo ya Moto Akijidhihirisha Mwenyewe waziwazi.

Imewapofusha wengine, Lakini kwetu sisi, Imefunua ile Kweli. Mungu amemtukuza mjumbe wake mbele zetu, kama alivyomtukuza Musa.

Hamko nyuma ya pazia hilo tena, enyi Watoto wadogo. Mungu anaonekana wazi kabisa kwenu.

Ni kitu gani? Uungu uliofunikwa katika mwili wa mwanadamu. Mungu, katika umbo la mwanadamu, akijificha Mwenyewe wasimwone. Wanaweza tu kumwona mwanadamu na kusema Nabii wa Mungu anakosea, hata alisema hivyo yeye mwenyewe, akijaribu kuwafundisha watu ya kwamba kuna makosa kwenye hizi kanda . Lakini kwetu sisi, Bibi-arusi Wake Aliyechaguliwa tangu Awali, tunamwona Mungu na kumsikia na hakuna makosa.

Mmoja aliona mwanadamu, huyo mwingine alimwona Mungu. Unaona? Na ilikuwa ni Mungu nyuma ya pazia la mwanadamu, ikiwafanya wote wawili kuwa sahihi, lakini imani yako katika yale usiyoyaona.

Kwetu sisi, tutaamini na kufuata makosa ya nabii wa Mungu aliyethibitishwa, kama kungekuwepo na yoyote , kabla hatujachukua na kuamini Bwana Asema hivi yao.

Musa hakupaswa kuupiga Mwamba mara ya pili. Roho yuleyule angalisema katika siku hiyo, “Ona, Musa anakosea.” Lakini maji yalitoka hata hivyo, na ikiwa hukunywa kutoka kwenye kile kinachoitwa kosa la musa, ulikufa. Ndivyo ilivyo leo hii. Mashtaka mengi sana.

Musa alikuwa na Neno. Sasa kumbukeni, baada ya Neno kudhihirishwa, Musa alikuwa ni Musa tena. Mnaona? Lakini wakati Neno hilo lilipokuwa ndani Yake lipate kutolewa, yeye alikuwa ni Mungu; vema, yeye hakuwa ni Musa tena.

Ndugu Branham alikuwa na Neno. Baada ya Neno kudhihirishwa, Ndugu Branham alikuwa Ndugu Branham tena, Lakini wakati Neno hilo lilipokuwa ndani yake lipate kutolewa kwa watu kwenye kanda, yeye alikuwa ni Mungu; hakuwa Ndugu Branham. Hivyo tunajifunza, yaliyo kwenye hizi kanda ni Maneno ya Mungu, na hakuna makosa katika Maneno ya Mungu.

Sisi sio tu kwamba tunaliamini, bali tunaliishi. Wakati hao wengine wote wanaliondokea, sisi tunadumu Nalo! Tunaliamini! Haijalishi kile mtu ye yote anachofanya ama anachosema , sisi tunaliamini na kisha tunalitendea kazi. Kama wewe hufanyi hivyo, basi huliamini.

Nasema vivyo hivyo katika Jina la Yesu Kristo. Usiongeze kitu. Usiondoe—kuliwekea mawazo yako. Wewe sema tu yaliyosemwa katika kanda hizo. Tenda sawasawa kabisa na vile Bwana Mungu amekuamuru kutenda. Usiongezee Kwake!

Bonyeza play na uamini KILA NENO kama vile Mungu alivyotuamuru kutenda. Ni Mungu akinena mdomo kwa sikio na Bibi-arusi Wake.

Mbele za watu, Mungu alijitia utaji tena na kumthibitisha Musa, kwa utaji, kwa kujitia utaji kwa Moto ule ule, Nguzo ile ile ya Moto ilishuka. Tangu—tangu wakati huo…Kutoka kwao, kwa hiyo wangeweza tu kusikia Neno la Mungu. Mnalipata? Neno pekee, waliisikia Sauti Yake. Kwa kuwa, Musa alikuwa, kwao, Neno lililo hai .

Mungu habadilishi, na hawezi kubadilisha mpango Wake. Yeye Ni Yesu Kristo yeye yule jana, leo na hata milele. Kwa hiyo, kwetu sisi, nabii Wake aliyethibitishwa, William Marrion Branham ndiye Sauti yetu ya Mungu, na Neno lililo Hai la wakati wetu.

Sasa si Neno tu lililoandikwa kwetu, ni kitu halisi. Tuko ndani Yake. Sasa tunafurahia. Sasa tunamwona Yeye. Sasa tunamwona, lile Neno, akijidhihirisha Mwenyewe. Limefichwa, huko nje, kwa sababu (kwa nini?) Limetiwa utaji katika mwili wa binadamu. Mnaona?

Haidhuru nini, wao hawalioni. Kwa nini? Haikutumwa kwao .

Kwa sababu unaliona, je, uko tayari kumsikia yeye akikuambia kwa mara nyingine tena WEWE NI NANI? Anapotazama chini kutoka kwenye ngome za Utukufu na kukuona, Yeye Anamwona nani?

* Ninaona Neno likidhihirishwa. Yale aliyosema angeyafanya katika siku hizi za mwisho, ninaliona likikua. Ninaona watoto wakila huo Mkate wa Shekina unaotoka kwenye kule kuiva kwa hilo Neno, ambao wanaliamini. Amina!

* Basi, sisi, ndipo tunakuwa sehemu Yake, kwa kuwa wewe ni utaji unaomficha Yeye. Wewe ni sehemu Yake, mradi Kristo yumo ndani yako, kama vile Kristo alivyokuwa wa Mungu. Kwa kuwa Mungu alikuwa ndani Yake, ilimfanya Mungu. Na kwa kuwa Kristo yumo ndani yako, tumaini la Utukufu, unakuwa sehemu ya Kristo.

* “Ninyi,” Hilo lilisema, “ninyi ni nyaraka zilizoandikwa,” ama, “ninyi ni Neno, ambalo limeandikwa, lililodhihirishwa,” hakuna kitu kinachoweza kuongezewa Kwake. Huwezi kusema, “Mimi ni waraka ulioandikwa,” na kuishi namna nyingine mbali na vile Hii imeandika tayari, kwa maana hakuna kitu kinachoweza kuongezwa wala kuondolewa .

Jina la Bwana Yesu Kristo litukuzwe. YEYE ANATUONA SISI. SISI TUNAMWONA YEYE. Sisi ni Neno Lake lililodhihirishwa leo hii.

Njoo uungane nasi Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania), Mungu akisimama mbele zetu; ile Nguzo ya Moto ikiwa imefichwa katika mwili wa mwanadamu, nayo inazungumza nasi Neno tunalopaswa kuishi kwalo katika siku hii. Ni Utukufu wa Shekina unaotuivisha. Mkate wa Wonyesho kwa mwamini.

Kufunuliwa Kwa Mungu 64-0614M

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikia Ujumbe:

Mathayo 24:24
Luka Mtakatifu 17:28-29
Yohana Mtakatifu 14:14
1 Wakorintho 12:13
2 Wakorintho 3:6 – 2 Wakorintho 4:3
Wafilipi 2:1-8
1 Timotheo 3:16
Waebrania 13:8
Ufunuo 10:7 & 19:13
Kutoka sura ya 19 yote & sura ya 20 yote
Yoeli 2:28
Malaki 4:5

22-0724 Tazama Aliko Yesu

UJUMBE: 63-1229E Tazama Aliko Yesu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Nuru Zilizodhihirishwa,

Hebu sote na tukusanyike pamoja na kusikiliza Ujumbe 63-1229E Tazama Aliko Yesu Jumapili hii saa 6:00 SITA Mchana , saa za Jeffersonville.( Ni saa 1:00 MOJA jioni ya Tanzania).

Ndugu Joseph Branham

Maandiko ya kusoma ili kujitayarisha kusikia ujumbe :

Hesabu 21:5-19

Isaya 45:22

Zekaria 12:10

Yohana Mtakatifu 14:12

22-0717 Yupo Mtu Hapa Anayeweza Kuiwasha Taa

UJUMBE: 63-1229M Yupo Mtu Hapa Anayeweza Kuiwasha Taa

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Sura ya Yesu Kristo,

Kama yule mvulana mdogo aliyejitazama kwenye kioo na asitambue kwamba alikuwa akijiangalia mwenyewe, sasa tunatazama katika Kioo cha Mungu, Neno Lake, na tunatambua, BABA, HUYO NI MIMI, Mimi ni Sura ya Neno Lako. Mimi ni Neno Lako lililodhihirishwa. Mimi ni mwamini, mimi ndiye Bibi-arusi Wako!

Kila Ujumbe tunaosikia huinua Imani yetu hadi viwango vipya. Alituambia lazima tujitokeze katika mojawapo ya makundi matatu: Waamini, waamini wakujifanya au wasioamini. Tulipotazama kwenye kioo Chake tulipaza sauti, “Naona, bila kivuli cha shaka, sisi ndio Waamini. Hakika Mwamini ndiye atakayeamini kila nukta na kila yodi; BABA, HUYO NI MIMI.”

Hakuna kitu kinachoweza kuturidhisha na kutupa Uzima ila Neno la Mungu lililonenwa kwenye kanda. Ndiyo njia pekee Uzima unapoweza kuja, kupitia Neno Lake lililonenwa, Sauti ya Mungu kwa ajili ya wakati wetu.

Jitayarishe, kuna mengi zaidi yajayo Jumapili hii, Julai 17, 2022. Kuna mtu hapa ambaye atakaye iwasha Taa, na atakapofanya hivyo, sote tutakuwa na maumivu ya koo kwa kupiga kelele na kupaza sauti, Amina, Haleluya, Jina la Bwana lisifiwe, Utukufu kwa Mungu, kwa sababu Mungu Mwenyewe atakuwa akizungumza nasi moja kwa moja na kulifunua zaidi Neno Lake.

Kama vile lile jua linaloangaza leo litaivisha nafaka kwa ajili ya mavuno mwezi wa Julai. Mwaona ninayomaanisha? Bali Nuru ya leo haitafaa lolote kule nyuma Julai . Ina nguvu zaidi ; ngano imeendelea zaidi. Iko tayari kulipokea. Amina! Hakika iko hivyo .

Mavuno yameiva! Tumeendelea zaidi na tayari zaidi kulipokea. Yesu ana meza iliyotandazwa, ambapo watakatifu wa Mungu wanalishwa kwa Chakula kilichoiva cha siku hii. Nuru ya Injili ikithibitisha na kuhakikisha kwamba Yeye yuko hapa leo pamoja nasi. Watakatifu wanakula Chakula cha kiroho ambacho kimehifadhiwa, wakijiandaa kwa ajili ya Unyakuo.

Wakati Mchungaji wetu, Roho Mtakatifu anapozungumza kupitia kwa nabii Wake aliyethibitishwa, anabonyeza swichi hiyo na kuwasha nuru ya Ufunuo, Yeye atatuambia Yeye ni nani hasa katika wakati wetu. Atapaza sauti na kutuonya,
Natumaini hamjalala.

Nuhu alikuwa Nuru katika siku yake. Musa alikuwa ni Nuru ya saa yake, sasa Nimewatumia nabii mwenye Nguvu katika Wakati wenu, nami ninalidhihirisha Neno Langu lililoahidiwa kupitia kwake. Yeye ni Neno la Mungu lililodhihirishwa katika siku yenu. Yeye ndiye Nuru ya Wakati huu.

Nilipokuwa hapa duniani katika mwili mara ya mwisho, nilichukua ile mikate mitano ya shayiri na kuanza kuimega ile mikate. Kutoka ile ya asili, nilitengeneza mikate na kuwalisha elfu tano.

Kisha nikapata samaki, na kutoka kwa samaki huyo, nikafanya samaki mwingine na samaki mwingine, nikawalisha elfu tano.

Lakini Katika wakati wako, sikuwa na kitu. Nilinena tu na kusema , “Sema itakuwepo,” na ilikuwa pale, bila kuwa na kitu. Yeye alinena tu na kusema, “Sema itakuwapo!” na ilikuwa pale bila kuwa na kitu. Sikuwa na kindi; hapakuwa na mmoja pale. Yeye alisema tu, “Wawepo!” wakawa! Neno Langu haliwezi kukosea na Lazima litimie.
.

Kama wana wa Israeli, walipokuwa safarini, walikuwa wakila mana mpya kila siku. Walikuwa wakitembea katika Nuru ya Nguzo ya Moto. Hiyo Nguzo ya Moto ilikuwa ni Yesu Kristo.

Leo yuko pamoja nasi kwa mara nyingine tena, Nguzo ile ile ya Moto, akifanya mambo yale yale ambayo Yeye alifanya alipokuwa hapa duniani akilitimiza Neno Lake.

Tunakualika uungane nasi Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Tanzania) wakati mchungaji wetu, Roho Mtakatifu, ile Nguzo ya Moto, anapowasha Nuru Yake ya Ufunuo, tunaposikia : 63-1229M “Yupo Mtu hapa Anayeweza Kuiwasha Taa “.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada ni:

Mwanzo 1:3, Sura ya 2 yote

Zaburi 22 yote
Yoeli 2:28
Isaya 7:14, 9:6, 28:10, 42:1-7

Mathayo 4:12-17, Sura ya 24 yote na Sura ya 28 yote

Marko Mtakatifu Sura ya 16 yote.

Ufunuo Sura ya 3 yote

22-0710 Aina Tatu Za Waamini

UJUMBE: 63-1124E Aina Tatu Za Waamini

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa mwamini,

Hebu wazia jambo hilo, Mungu, ambaye aliumba vitu vyote na kuviweka katika mpangilio, alishuka na kufanyika mwili miongoni mwetu, apate kutukomboa. Na ndipo angetuheshimu sana kwa Uwepo Wake mtukufu, hata angesimama hapa kwenye dunia hii yenye dhambi katika siku za mwisho , na kuthibitisha Neno Lake kuwa hivyo, kwa sababu Yeye ana wajibu kwa Neno hilo.

Roho Mtakatifu amelihuisha Neno hilo kwetu. Nalo Limekuwa hai. Kwa imani tunaliona. Tunajua ni hivyo kwa sababu Neno lilisema hivyo, naye Roho analihuisha Neno hilo kwetu. Sasa tunaunganishwa na Neno la Mungu lililodhihirishwa katika mwili, kama vile tu nabii alivyosema lingefanya.

Mwamini huliamini, anaamini (kitu gani?) Neno. Si kanuni za imani; Neno! Si madhehebu; Neno! Si kile anachosema mtu mwingine; kile lisemacho Neno! Naam, kumbukeni, huyo ni mwamini. Mwamini haulizi. Mwamini hasemi, “Inawezekanaje? Laiti ningaliweza kulielezea !” Huyo ni asiyeamini . A-ha. Ni mwamini, ambaye, haidhuru ni kitu gani, “Kama ni Neno, Ni Neno! Hilo ni kweli.” Huyo ndiye mwamini.

Huna budi kuamini kila nukta na kila yodi, na kila kitu kilichosemwa Humo ndani. Hakina budi kuwa ni kweli. kama Ukisema, “Siamini Jambo hilo. Baadhi ni Mungu, baadhi ni mwanadamu, baadhi ni hadithi za kuwinda tu.” Vema, basi wewe ni Asiyeamini. Mwamini haulizi. Mwamini huliamini Hilo, haidhuru linasikika namna gani ama lo lote mtu ye yote asemalo juu Yake, jinsi linavyoonekana lisilowezekana , SISI TUNALIAMINI!

Kila mtu aliyepo hapa, aliyeko, kila mtu anayesikiliza kanda hii; na hata ingawa siku moja sina budi kuondoka humu duniani, kanda hizi zingali zitaendelea. Hiyo ni kweli. Mnaona? Nanyi mmo katika moja ya tabaka hizi. Huna budi kuwa katika moja ya hizo.

Tunaishi katika siku za mwisho na yakubidi uangalie maisha yako na uone ni tabaka gani la watu ulilomo. Je! unasema, “Ninaamini Mungu alimtuma nabii ambaye amethibitishwa kwa Nguzo ya Moto?” yeye Alituambia tuamini kila Neno. Kusema HASA kile kilicho kwenye kanda na kutobadili hata Neno moja. Tutahukumiwa kwa yale YEYE ALIYOSEMA, si kwa yale ambayo mtu fulani aliyosema ati alisema, ama yale mtu fulani anasema alimaanisha, bali kwa yale kanda zisemavyo.

Au, utaambatana pamoja na Kora na Dathani, na wale wanaosema, “Yeye siye mtu pekee aliye mtakatifu. Kuna wengine wameitwa kufanya mambo haya aliyofanya. Unamtukuza sana nabii wa Mungu. Roho Mtakatifu ndiye anayetuongoza hivi sasa. Huu ni wakati tofauti.”

Wewe umo katika moja ya tabaka hizi. Katika hali yako ya sasa hivi, hali yako ya sasa ya akili, kwamba, ninyi mlio hapa katika mkutano huu unaoonekana, nanyi mtakaokuwa katika mikutano isiyoonekana ya kanda hii, hali yako ya sasa ya akili baada ya kuisikiliza kanda hii, inakuthibitishia uko katika tabaka gani. Inakwambia mahali ulipo hasa, iwapo wewe ni mwamini katika Neno na utadumu Nalo, kama ungeondoka uende zako, ama kufunga kanda hiyo.

Jina la Bwana lihimidiwe, sisi ndio WAAMINI Halisi, si mtu aliyeshawishiwa na mtu mwingine; si kwa jambo lingine, bali Roho Mtakatifu ametufunulia Neno Lenyewe. Tunaona Neno likiwekwa wazi, Likithibitishwa na kudhihirishwa.

Tunajaribiwa kwa hayo majaribu, zile barabara zenye mavumbi, joto la jua la mateso, lakini uaminifu wa mioyo yetu unavifua vitu hivyo vya Neno. Sasa tunakuwa tayari kufinyangwa. Sisi ni Watoto wa Mungu, tumetengenezwa barabara kwa Neno Lake. Sisi ni mifano iliyo hai, nalo Neno la Mungu likiishi kupitia kwetu. Jaribio huja kututikisa, kutuweka kule chini kabisa, kuona mahali tutakaposimama. Lakini hatutaondoshwa, Tunasimama kwenye Kila Neno.

Sikiliza anapokuambia wewe ni nani.

Kumbuka tu ya kwamba kila sehemu yako ilikuwa hapa, wakati Mungu aliponena ulimwengu ukawa. Yeye aliuweka mwili wako wakati uo huo. Wala hakuna kitu kinachoweza kuuondoa ila Mungu.

Hakuna kinachoweza kuliondoa hilo kutoka kwako. Hakuna mtu anayeweza kupachukua mahali pako, haidhuru ni padogo namna gani. Unasema, “Mimi ni mke wa nyumbani tu.” Hakuna mtu anayeweza kupachukua mahali pako. Mungu, katika uchumi Wake mkuu, ameweka jambo hilo hivyo, Mwili wa Kristo, katika utaratibu, hata hapana mtu anayeweza kupachukua mahali pako.

Utukufu… Haleluya… Kusikiliza Chakula cha Mungu kilichowekwa ghalani kunazidi kuwa kukuu zaidi na ZAIDI . Kadiri tunavyomsikia Mungu akinena kupitia mjumbe wake mteule akituambia sisi ni nani, ndivyo Imani yetu inavyokuwa kubwa zaidi. Furaha kubwa ya kujua:

. Sisi ndio “WAAMINI HALISI”
. Sisi ndio “WAMOJA WAO”
. Sisi ndio “BIBI-ARUSI “

Ningependa KUKUALIKA KUBONYEZA PLAY pamoja nami, pamoja na Maskani ya Branham, pamoja na sehemu ya Bibi-arusi kutoka ulimwenguni kote saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, ( ni Saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania), Wakati tutakapokusanyika kutoka Mashariki, Magharibi, Kaskazini na Kusini Kusikia: Aina Tatu za Waamini 63-1124E . Hivi ndivyo Roho Mtakatifu anavyotuongoza kufanya. Kwetu sisi, huu ndio mpango wa Mungu.

. Bonyeza Play: Kanda yoyote ambayo Mungu anaweka moyoni mwako.

. Bonyeza Play : Sikiliza wakati wowote utakaochagua.

. BONYEZA PLAY : Ndiyo ujumbe wangu kwako.

Ndugu. Joseph Branham.

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada :

Yohana Mtakatifu 6:60 – 71

22-0626 Yeye Aliye Ndani Yenu

UJUMBE: 63-1110E Yeye Aliye Ndani Yenu

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi mwenye Imani kuu sana,

Ninajua hii ni barua rahisi tu yenye sarufi isiyofaa, lakini nataka ulimwengu ujue ya kwamba tunaamini kila neno ambalo nabii wetu alisema na kulikubali kuwa ni Bwana Asema Hivi . Tunapomsikia yeye akisema jambo fulani kwenye kanda, tunaliamini, tunalikubali, na kisha tunalipokea kibinafsi kuwa ni Mungu Mwenyewe akizungumza nasi moja kwa moja.

Imehubiriwa, na kuthibitishwa kwelikweli kwa Neno la Mungu, ya kwamba isingekuwa ni mwanadamu, haina budi kuwa ni Mungu.

Tunaamini ishara zilezile za kuonekana dhahiri kimwili zimetukia duniani leo ambazo zilitukia wakati Yesu alipokuwa hapa. Nguzo ile ile ya Moto ambayo Mtakatifu Paulo aliiona ikiwa na Tabia ile ile, ikifanya jambo lile lile, imekuja katika wakati wetu. Ni Mungu anazungumza nasi moja kwa moja:

Ishara zile zile za kiroho ambazo alijitambulisha Mwenyewe kama Masihi, zimemtambulisha leo. Yeye yungali ni Masihi !

Unaweza tu kupokea baraka hizi kuu IWAPO unaamini kila Neno kwa kubonyeza Play ni Bwana Asema Hivi. Ikiwa wewe ni mtu ambaye huamini hivyo, na yakubidi uamue kiakili au kwa kupitia mtu fulani anayekuambia: “Hili ni Neno la Bwana, na hili ni Ndugu Branham tu anayezungumza,” basi hili si kwa ajili yako.

Katika wakati ule Musa alipowaongoza wana wa Israeli, alikuwepo mmoja, huyo alikuwa Musa. Wengine wao walifuata tu Ujumbe. Unaona?

Lakini leo hii, kwetu sisi TUNAOAMINI JAMBO HILO JINSI HIYO, mioyo yetu imejaa furaha na kububujika, ni vigumu sana kujizuia.

Ninajisikia kwamba Yeye ametukomboa. Ninajisikia ya kwamba majina yetu yamo kwenye Kitabu Chake. Ninaamini ya kwamba tumekombolewa kwa Damu ya Mwana-Kondoo .

Kwa sababu tunaamini kuwa Ujumbe huu ni Sauti ya Mungu inayozungumza nasi moja kwa moja, tunakubali hili kuwa ni Mungu Mwenyewe akizungumza nasi mdomo kwa sikio. HAKUNA SHAKA majina yetu yako kwenye Kitabu chake.

Naomba niliweke namna hii, huduma ya Yesu Kristo ikifanyika mwili katika Kanisa Lake katika siku hizi za mwisho. Hivyo ndivyo wengi wetu wanavyoamini. Ninaamini pamoja nanyi.

Hivyo ndivyo hasa sisi tunavyoamini jambo hilo , Yesu Kristo akifanyika mwili , akizungumza na Bibi-arusi Wake kwenye kanda.

Kila mara tunapobonyeza play imani yetu hufikia viwango vipya. Huyu sio tu mhubiri mwingine anayezungumza, huyu ni Mungu Mwenyewe anayezungumza nasi. Tunataka Neno safi peke yake 100% .

Hebu ni kuulize Jambo fulani . Je, William Marrion Branham ndiye mchungaji wako? Je, yeye ndiye Malaika-mjumbe wa saba aliyethibitishwa na Mungu? Je, unaamini alichomwomba Mungu afanye, Mungu alifanya ? Je! unaamini yeye alikuwa ni Sauti ya Mungu kwa wakati huu? Unaamini kila neno alilosema? Basi Jumapili utabarikiwa mara tena isivyoelezeka .

Hakuna njia nyingine unayoweza kupokea baraka hii isipokuwa unasikiliza kanda na kuamini kile unachosikia kuwa ni Bwana Asema Hivi. Huna budi kuamini Kile anachosema ni Mungu ananena nawe moja kwa moja.

Nami, kama mchungaji wenu, ndugu yenu, kwa imani niliyo nayo, nimemwomba Mungu aiweke hiyo juu yenu. Ninaamini kwamba nitapokea kile nilichoomba. Sasa ikiwa mtaamini pamoja nami; kwa imani ile niliyo nayo, ninawapa hiyo sasa hivi .

Kwetu sisi yeye ni mchungaji wetu. Hakuna mtu ulimwenguni aliye na Imani zaidi, au kuu kuliko MCHUNGAJI WETU, nabii wa Mungu. Sasa nabii wa Mungu amemwomba Mungu atupe IMANI YAKE KUU. IKIWA unaamini hilo kwa moyo wako wote, ni IMANI YAKO Hivi sasa….UTUKUFU, TUNAAMINI !!! Imani yetu inaweza kuwa dhaifu, lakini sivyo tena, kwa maana sasa tunayo IMANI yake.

Na sasa, katika Jina la Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, kataeni mateso yenu, magonjwa yenu, na mseme “Huna budi kuondoka,” sababu mnayo imani yenu , na imani yangu, pamoja na nguvu za Yesu Kristo , Ambaye uwepo Wake wa kila mahali upo hapa kudhihirisha jambo hilo na kuthibitisha kwamba Yuko hapa, atawapa afya sasa.

Ninaweza kusema nini kitakachokufanya uje kuungana nasi na kupokea baraka hii kuu? Wazia jambo hilo, chochote unachohitaji, unaweza kukipata kama utakuja kusikiliza na kuliamini kwa urahisi.

Njoo usikilize pamoja na Bibi-arusi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville. ( Ni saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania) Tutakusanyika na kusikiliza kutoka Mashariki, Magharibi, Kaskazini na Kusini, wote kwa wakati mmoja, wakati Bwana Asema hivi ikituzungumzia na kutuambia yote kuhusu: Yeye Aliye Ndani Yenu 63-1110E .

Ikiwa huwezi kusikiliza pamoja nasi kwa wakati mmoja Jumapili, haijalishi, bonyeza play tu wakati wowote na usikilize na uamini kile unachosikia kuwa ni Sauti ya Mungu inayozungumza nawe.

Ndugu. Joseph Branham

22-0619 Nafsi Zilizo Kifungoni Sasa

UJUMBE: 63-1110M Nafsi Zilizo Kifungoni Sasa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Baba Mpendwa, ninaweza kuandika nini leo ili upate kunitumia, kwa njia fulani ndogo, kumtia moyo Bibi-arusi Wako wa thamani?

Mungu amekuja katika wakati wetu na kuishi katika mwili wa mwanadamu, ndani ya mtu aitwaye William Marrion Branham, ili aweze kufunua na kutimiza Neno Lake. Huo ndio Ufunuo wa Yesu Kristo katika wakati wetu.

Kuisikiliza Sauti hiyo na kuamini kila Neno ndiyo njia pekee iliyoandaliwa na Mungu kwa siku ya leo. Alituma ulimwenguni watu wengi waliotiwa mafuta na Roho wake Mtakatifu, Lakini Yeye hutuma na kunena kupitia mtu mmoja tu kufunua Neno Lake na kumwongoza Bibi-arusi Wake.

Yeye kamwe habadilishi Mpango Wake au Njia Yake ya kufanya mambo. Jinsi alivyofanya jambo hilo mara ya kwanza, Yeye hulifanya hilo kila wakati. Yeye huwaongoza watu Wake Mwenyewe, kwa Nguzo ya Moto.

Wewe ni Bibi-arusi mteule wa Mungu na hakuna kitu shetani anachoweza kufanya au kusema ambacho kinaweza kulitoa jambo hilo kwako, HAKUNA! Alikuchagua tangu asili kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Alikujua wakati huo, nawe ulikuwa pamoja Naye wakati huo. Alijua jina lako. Alijua kila kitu kukuhusu. Alijua mema na mabaya yako. Alijua kushindwa kwako, makosa yako, na bado alikupenda, kwa kuwa ulikuwa sehemu yake.

Nafsi yako inaweza tu kujilisha Neno Lake. Hakuna kinachoweza kukutosheleza ila Neno Lake. Unapenda kusoma Neno Lake na kumtafakari Yeye, kuomba kutoka ndani kabisa ya moyo wako, lakini unaposikia Sauti Yake ikizungumza nawe moja kwa moja, inakuinua juu ng’ambo ya pazia la wakati. Kwa maana unajua umeketi naye katika ulimwengu wa roho huku akinena nawe mdomo kwa sikio, akifunua Neno lake, akikukumbusha, WEWE NI BIBI-ARUSI WANGU.

Shetani anaweza kukupiga tena na tena. Unaweza kushushwa moyo sana wakati mwingine na kuhisi wewe ni uliyeshindwa kabisa; Kujisikia kana kwamba umemkosea zaidi ya mtu yeyote yule. Wewe ni mbaya zaidi kuliko waovu wote , lakini mahali fulani, ndani kabisa katika nafsi yako, unasikia ile Sauti Ndogo tulivu ikikuambia: “Hakuna kitu kinachoweza kukutenganisha na Neno Langu, WEWE NI NENO LANGU. Nililiweka jina lako kwenye Kitabu changu cha Uzima cha Mwana-Kondoo, Mimi Mwenyewe.”

Niseme nini ili kukutia moyo leo hii? Bonyeza Play tu kila siku na usikie Sauti ya Mungu ikinena na kukuambia: Bwana Asema hivi.

Umealikwa kuungana na Bibi-arusi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA ., Saa za Jeffersonville,( Ni Saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania ) tunapokusanyika kusikiliza ile sauti ndogo tulivu: 63-1110m Nafsi Zilizo Kifungoni Sasa.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada :

Mwanzo 15:16
Mathayo Mtakatifu 23:27-34
Yohana Mtakatifu 4:23-24 / 6:49 / 14:12
1 Petro 3:18-22
2 Petro 2:4-5
Yuda 1:5-6

22-0612 Kukata Tamaa

UJUMBE: 63-0901E Kukata Tamaa

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa wa Mungu waliofungwa kwa Damu, waliofungwa kwa Ile Ishara, watu wa Agano.

Kumbuka tu, sisi si Hawa, sisi si mmoja wa hawa wenye mashaka wanaopatana na Shetani. Tuna imani isiyotikisika katika Neno hili! Tunashikilia kila Neno la Mungu aliloandika na kunena kwenye kanda. Imetupa IMANI KAMILIFU .

Hatutafuti imani fulani kubwa inayotulazimu kuwa nayo ndani yetu wenyewe . Hatujaribu kuwa wema vya kutosha; hatutawahi kamwe kuwa wema vya kutosha, tutashindwa kila wakati. Hilo silo alilotuambia tuwe na imani nalo. Alisema iweni na imani na kuamini KILA NENO alilosema kuwa ni Bwana Asema Hivi. TUNAAMINI HIVYO na Imetupa IMANI KAMILIFU KATIKA NENO LAKE.

Hebu tusikilize kile ambacho Roho Mtakatifu amekuwa akiripoti na kumwambia Baba kutuhusu sisi.

“Nimetii amri zako. Nilitafuta na nimepata baadhi ya vikundi vidogo vya watu waliotawanyika kote ulimwenguni. Nilituma vijana wa kanda Majumbani kwao na kucheza kanda chache. Waliposikia kanda hizo, waliamini kila Neno. Sasa wamezifanya nyumba zao kuwa kanisa wapate kuupokea Ujumbe huu. Wao ni Tai Wako waliochaguliwa tangu asili wanaokusanyika Pamoja kusikia Neno Lako.

Niliwaambia ya kwamba wote ambao wangekuja chini ya ile Ishara, Ujumbe wa wakati huu, wangeokolewa. Niliwaambia wawe Mmoja na Wewe na Neno Lako. Kama ilitenda kazi kwao, basi waiweke kwa watoto wao Ishara hiyo. Waiweke kwa wapendwa wao na kuwaleta chini ya hiyo Ishara na wao pia wataokolewa.

Niliwaambia waliokuwa Wakisikiliza kanda: Ninawadai kwa Mungu. Waliliamini nilipolisema jambo hilo, kwa mioyo yao yote na nafsi zao zote. Wao ni watu wangu, ndio niwapendao wanaosikiliza kanda hizi.

Niliwaambia angalieni kile Kilichokuja baada ya ile Mihuri Saba: ule muungano wa watu, ishara zilizounganika, kimulimuli chekukundu katika siku za mwisho, Zimetiwa kifuniko katika kitu hiki kimoja, ile Ishara.”

Loo, Kanisa, amka na ujitikise! Finya dhamira yako, amka katika saa hii! Hatuna budi kukata tamaa ama tutaangamia! Kuna jambo linalokuja kutoka kwa Bwana! Ninajua jambo hilo kwamba ni BWANA ASEMA HIVI. Kuna jambo linalokuja, na ni afadhali tukate tamaa. Ni kati ya uzima na mauti. Litapita katikati yetu wala hatutaliona.

Nasi tunajua jambo fulani liko karibu kutukia. Kule Kuja kwa Bwana kutakuwa ni kuondoka kwa ghafla, na kwa siri. Tumekata tamaa. Wakati umekaribia. Tumeitambua ile Ishara kwa ajili ya siku yetu nayo imewekwa.

Tunachukua Mifano ya Pasaka Jumapili hii ambayo ililiwa kwa dharura, katika Nyakati za kukata tamaa. Tunakusanyika ulimwenguni kote, kulizunguka Neno Lake.

Njoo uwe sehemu ya tukio hili kuu Jumapili hii saa 10:00 KUMI JIONI , saa za Jeffersonville,( Ni Saa 5:00 TANO USIKU ya Tanzania?) tunapokusanyika ili kusikia Neno: 63-0901E _ KUKATA TAMAA .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada :

Kutoka 12:11
Yeremia 29:10-14
Luka Mtakatifu 16:16
Yohana Mtakatifu 14:23
Wagalatia 5:6
Yakobo 5:16