Category Archives: Uncategorized

24-1201 Wale Wanawali Kumi, Na Wayahudi Mia Na Arobaini Na Nne Elfu

UJUMBE: 60-1211M Wale Wanawali Kumi, Na Wayahudi Mia Na Arobaini Na Nne Elfu

PDF

BranhamTabernacle.org

Habari Za Asubuhi Marafiki,

Haijawahi kutokea katika historia ya ulimwengu kuwepo na wakati ambapo Bibi-arusi wa Kristo kutoka ulimwenguni kote angeweza kuungana pamoja katika nia moja, wakati sauti kutoka Mbinguni, ile Sauti halisi ya Mungu, ingeweza kuja ikienda kasi.

Maandiko yanatimia. Ni ishara ya Mbegu ya wakati wa kuungana. Ule muungano usioonekana wa Bibi-arusi wa Kristo unafanyika tukiketi katika uwepo wa Mwana, tukiivishwa, tukijiweka wenyewe tayari kwa kuisikia Sauti ya Mungu halisi.

Sisi tunakamilishwa na huduma tano Yake.

Ni wangapi wanaoamini kwamba karama na miito havina majuto? Biblia ilisema kuna karama tano katika kanisa. Mungu ameweka katika kanisa Mitume, au wamishenari, mitume, manabii, waalimu, wainjilisti, wachungaji.

  • . Mhubiri: Ningeenda barabarani. Mtu fulani angesema, “Je, wewe ni mhubiri?” Ningesema, “Ndiyo bwana. Loo, Ndiyo, mimi ni mhubiri.”
  • . Mwalimu: Na sasa sababu sikuchukua kuhubiri asubuhi ya leo, ilikuwa ni kwamba, nilifikiri, katika kufundisha, tungelielewa vizuri zaidi kuliko kuchukua somo na kulipitia juu juu. Tungelifundisha tu.
  • . Mtume: Neno “mmishenari” linamaanisha “mtu aliyetumwa.” “Mtume” maana yake ni “mtu aliyetumwa.” Mmishenari ni mtume. Mimi—mimi, mimi ni mmishenari, kama mjuavyo, ninafanya uinjilisti, kazi ya kimishenari, karibu mara saba nchi za ng’ambo, kote ulimwenguni.
  • . Nabii: Je, unaniamini mimi kuwa nabii wa Mungu? Basi nenda ukafanye kile ninachokuambia.
  • . Mchungaji: Je, mumeelewa na hayo niliyowatendea? Ninyi mumeniita “mchungaji wenu”; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo.

Nami nikawaona hao mamilioni wamesimama pale, nikasema, “Hivi hawa wote ni wa Branham?” Kasema, “La.” Kasema, “Hao ni waongofu wako.” Ndipo nikasema, ni—nikasema, “Ninataka kumwona Yesu.” Akasema, “Bado. Itachukua muda kabla Yeye hajaja. Ila atakuja kwako kwanza nawe utahukumiwa kwa Neno ambalo ulihubiri,

Ndipo sisi sote tutainua mikono yetu na kusema, “Tunatumainia hilo!”

Jambo fulani liko karibu kutukia. Nini kinatendeka? Waliokufa katika Kristo wameanza kufufuka pande zote kunizunguka. Ninahisi badiliko likija mwilini mwangu. Nywele zangu za mvi, zimeondoka. Angalia uso wangu… makunyanzi yangu yote yametoweka. Kuugua kwangu na maumivu…. YAMEKWISHA. Kuhisi kwangu huzuni kumetoweka mara moja. Nimebadilishwa kwa dakika moja, katika kufumba na kufumbua jicho.

Kisha tutaanza kutazama kando yetu na kuwaona wapendwa wetu. Loo, yule pale Mama na Baba…Utukufu, mwanangu…binti yangu. Babu, Bibi, loo, nimewakumbuka sana nyote wawili. Halo …yule pale rafiki yangu wa zamani. LOO, TAZAMA, ni Ndugu Branham, nabii wetu, Haleluya!! yuko hapa. Linatukia!

Kisha pamoja, wote kwa pamoja, tutanyakuliwa huko juu mahali fulani hewani ng’ambo ya nchi. Tutamlaki Bwana wakati akishuka. Tutasimama huko pamoja Naye juu ya mizingo ya dunia hii na kuziimba nyimbo za ukombozi. Tutaimba na kumsifu Yeye kwa ajili ya neema Yake ya ukombozi ambayo ametupa.

Ni mangapi yote yanayomngojea Bibi-arusi Wake. Tutakuwa na wakati ulioje katika umilele sisi kwa sisi, na pamoja na Bwana wetu Yesu. Maneno ya kibinadamu hayawezi kueleza, Bwana, jinsi tunavyojisikia mioyoni mwetu.

Kama ungependa kumsikia Yeye akikuita Bibi-arusi Wake, na kukuambia jinsi gani itakavyokuwa pamoja Naye, njoo uungane nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki), nawe utabarikiwa kupita kipimo.

Ndugu. Joseph Branham

60-1211M Wale Wanawali Kumi, Na Wayahudi Mia Na Arobaini na Nne Elfu

24-1124 Wakati Wa Kanisa La Filadelfia

UJUMBE: 60-1210 Wakati Wa Kanisa La Filadelfia

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bi Yesu Kristo,

Je! Jumapili hii itashikilia kitu gani kwa ajili ya Bibi-arusi wa Yesu Kristo? Ni yapi yote Roho Mtakatifu atakayotufunulia? Utimilifu Mkamilifu. Sasa tutafahamu kikamilifu kwa Ufunuo, kitu chenyewe ukilinganisha na mfano wake na kitu chenyewe na kivuli chake. Yesu ndiye mkate wa kweli wa Uzima. Yeye ndiye wote wa Hilo. Yeye ni Mungu Mmoja. Yeye ni Waebrania 13:8. Yeye ndiye MIMI NIKO.

Kristo, akiisha kutokea katika mwili na kumwaga Damu Yake mwenyewe, ameziondoa dhambi zetu mara moja na kwa yote kwa toleo la nafsi Yake; kwa hiyo sasa ametufanya sisi kuwa WAKAMILIFU. Uhai Wake mwenyewe umo ndani yetu. Damu Yake imetusafisha. Roho Wake hutujaza. Mapigo Yake TAYARI yametuponya. Neno Lake liko ndani ya mioyo na mdomo wetu. Ni Kristo katika maisha yetu na si kitu kingine chochote, kwani kila kitu maishani mwetu hufifia na kuwa duni, isipokuwa Yeye na Neno Lake.

Mioyo yetu itajawa na furaha anapotuambia kwamba kwa uamuzi wa kiungu, Yeye alijua ni nani hasa angalikuwa Bibi-arusi Wake. Jinsi alivyotuchagua. Yeye alituita. Alitufia sisi. Alitununua na sisi ni mali Yake, na ni Wake peke Yake. Yeye hunena, nasi tunatii, kwa maana hiyo ndiyo furaha yetu. Sisi ni mali Yake peke Yake Naye hana mwingine ila SISI. Yeye ni Mfalme wetu wa Wafalme nasi ni ufalme Wake. Sisi ni mali Yake ya milele.

Yeye atatutia nguvu na kutuangazia kwa Neno la Sauti Yake. Ataeleza waziwazi na kufunua kuwa Yeye ndiye Mlango wa kondoo. Yeye ni Alfa na Omega. Yeye ni Baba, Yeye ni Mwana, na Yeye ni Roho Mtakatifu. Yeye ni Mmoja, nasi tu Mmoja na Naye na ndani Yake.

Yeye atatufundisha subira, kama alivyomfundisha Ibrahimu, kwa kueleza jinsi tunavyopaswa kungojea kwa subira na kuvumilia ikiwa tunataka kupata ahadi yoyote.

Yeye atatuonyesha waziwazi siku hasa tunayoishi. Jinsi zile pilikapilika za ekumeni zitakavyopata nguvu kisiasa, na kuishurutisha serikali kuwafanya wote waungane nao aidha moja kwa moja ama kwa kufuata kanuni zilizofanywa sheria hivi kwamba hakuna watu watakaotambuliwa kama makanisa isipokuwa chini ya uongozi wa moja kwa moja ama usio wa moja kwa moja wa halmashauri yao.

Yeye atafunua jinsi gani wengi sana watakubaliana nao, wakidhani wanamtumikia Mungu katika utaratibu uliowekwa wa shirika. Bali Yeye anatuambia sisi, “Msiogope, kwa maana Bibi-arusi hatadanganywa, sisi tutadumu na Neno Lake, Sauti Yake.”

Litakuwa jambo lakutia moyo jinsi gani kumsikia Yeye akituambia: “Shika sana, vumilia. Usife moyo, bali vaa silaha zote za Mungu, kila silaha, kila karama niliyokupa iko mikononi mwetu. Usivunjike moyo kamwe kipenzi, endelea tu kuangalia mbele kwa furaha kwa sababu utatiwa taji na Mimi, Mfalme wako wa Wafalme na Bwana wa Mabwana, Mumeo.”

Ninyi ndio kanisa Langu la kweli; hekalu halisi la Mungu kwa Roho Wangu Mtakatifu aishiye ndani yenu. Mtakuwa nguzo katika hilo hekalu jipya; ule msingi utakaoshikilia sehemu ya juu. Nitawaweka kama washindi pamoja na mitume na manabii, kwa maana Nimewapa Ufunuo wa Neno Langu, wa Mimi Mwenyewe.

Yeye atatufunulia waziwazi kwamba majina yetu yaliandikwa katika Kitabu Chake cha Uzima cha Mwana-Kondoo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Kwa hiyo tutakuwa mbele ya kiti Chake cha enzi usiku na mchana kumtumikia hekaluni Mwake. Sisi tuko chini ya ulinzi maalum wa Bwana; sisi ni Bibi-arusi Wake.

Tutakuwa na jina jipya kwa kulichukua jina Lake. Litakuwa ndilo jina tulilopewa sisi wakati anapotuchukua Kwake. Tutakuwa Bi Yesu Kristo Wake.

Yerusalemu mpya ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, Bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa Mumewe. Mauti haitakuwapo tena, huzuni, wala kilio. Wala maumivu hayatakuwapo tena kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita. Ahadi zote nzuri za Mungu zitatimizwa. Badiliko litakamilika. Mwana-Kondoo na Bibi-arusi Wake watakaa milele katika ukamilifu wote wa Mungu.

Mpendwa Bi Yesu Kristo, OTA JUU YAKE. Itakuwa nzuri zaidi kuliko vile unavyoweza kuwazia.

Ninamwalika kila mtu aje kuungana nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) wakati Mume wetu, Yesu Kristo, anenapo kupitia malaika-mjumbe Wake wa saba mwenye nguvu na kutuambia mambo haya yote.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: Wakati Wa Kanisa la Filadelfia 60-1210

24-1117 Wakati Wa Kanisa La Sardi

UJUMBE: 60-1209 Wakati Wa Kanisa La Sardi

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Watu Wa Kanda,

Tunajivunia jinsi gani kuitwa “Watu wa Kanda”. Mioyo yetu inaenda mbio kwa changamko kila wiki tukijua tutaungana pamoja ulimwenguni kote kwa kuisikia Sauti ya Mungu ikisema nasi.

Tunajua, bila chembe ya shaka hata moja, tuko katika Mapenzi makamilifu ya Mungu kwa sisi kukaa na Neno Lake; kuisikiliza Sauti Yake kwa njia ya malaika-mjumbe Wake wa saba mwenye nguvu.

Mjumbe Aliyemchagua kwa ajili ya siku yetu ni William Marrion Branham. Yeye ndiye taa ya Mungu kwa ulimwengu, inayoakisi nuru ya Mungu. Yeye anamwita Bibi-arusi Neno Safi Wake aliyechaguliwa atoke kupitia malaika Wake.

Kwa kujifunza kwa makini Neno Lake, Ametufunulia sisi kwa Roho Wake Mtakatifu kwamba William Marrion Branham ndiye malaika ambaye Yeye aliyemchagua kumpa Ufunuo Wake na Huduma Yake kwa ajili ya siku yetu. Tunamwona malaika Wake, NYOTA YETU, katika mkono Wake wa kuume huku akimpa nguvu Zake za kufunua Neno Lake na kumwita Bibi-arusi Wake atoke.

Yeye ametupa Ufunuo mzima wa Yeye Mwenyewe. Roho Mtakatifu akijitambulisha kwetu kupitia maisha ya malaika-mjumbe Wake wa saba; malaika aliyemchagua kuwa macho Yake kwa ajili ya siku yetu.

Jinsi gani mioyo yetu inavyowaka ndani yetu wakati anapotuambia kwa kila Ujumbe kwamba ni kusudi Lake kutuleta Kwake; ya kwamba sisi ni Bibi-arusi Neno Wake.

Yeye anapenda kutuambia mara kwa mara jinsi alivyotuchagua sisi kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu NDANI YAKE. Jinsi tulivyojulikana kimbele na kupendwa Naye.

Jinsi tunavyopenda kumsikia Yeye akinena na kutuambia tulikombolewa kwa Damu Yake na HATUWEZI kamwe kuja hukumuni. Hatuwezi kamwe kuwa katika hukumu, kwa sababu dhambi haiwezi kuhesabiwa kwetu sisi.

Jinsi tutakavyoketi pamoja Na Yeye wakati akichukua kiti chake cha enzi cha duniani cha Daudi, na kutawala pamoja Naye; kama tu Yeye alivyofanya mbinguni, pamoja na uwezo na mamlaka juu ya dunia nzima. Majaribu na majaribio ya maisha haya yataonekana kuwa si kitu wakati huo.

Lakini pia Yeye ametuonya jinsi gani tunavyopaswa kuwa waangalifu. Kwamba katika nyakati zote ile mizabibu miwili ilikua pamoja. Jinsi ambavyo adui daima amekuwa akifanana sana; mdanganyifu sana. Hata Yuda alichaguliwa na Mungu, na kufundishwa katika kweli. Alishiriki maarifa ya zile siri. Alikuwa na huduma ya nguvu aliyopewa naye akawaponya wagonjwa na kutoa pepo katika Jina la Yesu. Lakini yeye hakuweza kwenda hadi mwisho.

Huwezi kuendelea na sehemu tu ya Neno, huna budi kuchukua Neno LOTE. Kuna watu wanaoonekana wanahusika na mambo ya Mungu karibu asilimia mia moja, lakini sio.

Yeye alisema wala haitoshi kwamba Yeye amejihusisha na kanisa zima, ama hata na huduma tano ya Waefeso nne. Yeye alituonya kwamba katika kila wakati kanisa hupotoka, na wala si wafuasi tu bali na kundi la makasisi – wachungaji wako makosani na kondoo pia.

Kwa hiyo kwa shauri lililokusudiwa la mapenzi Yake Mwenyewe, Yeye amejitokeza Mwenyewe katika wakati wetu kama Mchungaji Mkuu katika huduma ya malaika-mjumbe Wake wa saba kuwaongoza watu Wake wairudie ile kweli na zile nguvu nyingi za kweli hiyo.

Yeye yuko ndani ya mjumbe Wake na yeye ambaye angekuwa na utimilifu wa Mungu angemfuata huyo mjumbe kama vile huyo mjumbe alivyo mfuasi wa Bwana kwa Neno Lake.

Ninataka kuwa na utimilifu wa Mungu na kumfuata mjumbe Wake. Hivyo, kwetu sisi, Maskani ya Branham, njia pekee ya kumfuata mjumbe kama vile yeye anavyomfuata Bwana kwa Neno Lake, ni KUBONYEZA PLAY na kuisikia Sauti ya Mungu Safi ikisema nasi maneno ya kutoweza kukosea.

Haitubidi kukisia au kukagua kile tunachosikia, inatubidi tu Kubonyeza Play na kuamini kila Neno tunalosikia.

Nilimsikia Ndugu Branham akisema maneno yafuatayo mapema asubuhi moja kwenye redio ya Sauti. Nilipolisikia Hilo, ikanijia moyoni mwangu kwamba hivi ndivyo Mimi / sisi tunavyojisikia kuhusu kusema:

TUNABONYEZA PLAY TU NA KUZISIKILIZA KANDA.

Ilisikika kama tamshi la Imani yetu kwangu mimi.

Hiyo ndiyo sababu ninaamini katika uponyaji wa Kiungu. Hiyo ndiyo sababu ninaamini katika maono. Hiyo ndiyo sababu ninaamini katika Malaika. Hiyo ndiyo sababu ninaamini Ujumbe huu, ni kwa sababu unatoka kwenye Neno la Mungu. Na chochote nje ya Neno la Mungu, sikiamini. Inaweza kuwa hivyo, lakini hata hivyo nitadumu tu na yale Mungu aliyosema, ndipo niwe na hakika kwamba niko sahihi. Sasa, Mungu anaweza kufanya atakalo. Yeye ni Mungu. Lakini maadamu ninadumu na Neno Lake, basi ninajua hilo ni sawa. Ninaamini hilo.

Utukufu, yeye alilisema KAMILIFU kweli. Huduma zingine zote zinaweza kuwa, kwa sababu Mungu anaweza kufanya atakalo, na yule Yeye anayemtaka kulifanya, Yeye ni Mungu. Lakini maadamu ninadumu na Neno Lake, Sauti Yake, Kanda, basi ninajua hilo ni sawa. Ninaamini hilo.

Ninajua wengi huzisoma barua zangu na kutoelewa kile Mimi ninachosema na kile ninachoamini kuwa ni Mapenzi ya Bwana kwa kanisa letu. Nami niseme tena kwa unyenyekevu kama vile nabii alivyosema: “Barua hizi zimekusudiwa kwa ajili ya kanisa langu peke yake. Wale wanaotamani kuiita Maskani ya Branham kanisa lao. Wale WANAOTAKA KUTAMBULISHWA NA KUITWA WATU WA KANDA”.

Ikiwa hukubaliani na yale ninayosema na ninayoamini, hiyo ni sawa asilimia 100% ndugu zangu na dada zangu. Barua zangu si kwa ajili yenu au dhidi yenu au kwa makanisa yenu. Kanisa lako linajitawala lenyewe nawe ni lazima ufanye kama vile unavyohisi kuongozwa kufanya, bali kulingana na Neno, ndivyo lilivyo na letu, na hiki ndicho sisi tunachoamini kuwa ndio njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili yetu.

Wote mnakaribishwa kuungana nasi kila Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville.( Ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) Wiki hii, Nyota ya Mungu ya wakati wetu, William Marrion Branham, atakuwa akituletea Ujumbe, 60-1209 Wakati wa Kanisa la Sardi.

Ndugu. Joseph Branham

24-1110 Wakati Wa Kanisa La Thiatira

UJUMBE: 60-1208 Wakati Wa Kanisa La Thiatira

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliyeangaziwa,

Jinsi ambavyo Bwana anavyotufunulia kwamba katika nyakati zote kumekuwa na kundi dogo sana ambalo lilidumu na Neno Lake. Wao hawakuanguka katika mtego wa udanganyifu wa adui, bali walibaki wa kweli na waaminifu kwa Neno la siku yao.

Lakini hakujawahi kuwa na wakati, au kundi la watu, ambalo Bwana amekuwa akijivunia, au kuwa na imani zaidi nalo, kuliko sisi. Sisi ndio Bibi-arusi Bibi Mteule Wake ambaye hatadanganywa, na hata muhimu zaidi HATUWEZI, kudanganywa; kwa maana sisi tunaisikia Sauti ya Mchungaji na kumfuata.

Yeye anatuonyesha kwamba katika nyakati zote kumekuwa na makundi mawili ya watu, yote yakidai ufunuo wao kutoka kwa Mungu na uhusiano wao na Mungu. Lakini alituambia, Bwana awajua walio Wake. Anafuatilia mawazo yetu. Yeye anajua kilicho mioyoni mwetu. Yeye anaziona kazi zetu kwa kudumu na nabii na Neno Lake, ambayo ni madhihirisho dhahiri ya yale yaliyo ndani yetu. Madhumuni yetu, makusudi yetu yanajulikana Kwake kwa kuwa Yeye hulichunguza kila tendo letu.

Yeye anatuambia kwamba ahadi zote alizozitoa kwa kila wakati, ni ZETU. Anatuona sisi tunaoendelea kutenda kazi Zake kwa uaminifu hata mwisho. Yeye AMETUPA SISI mamlaka juu ya mataifa. Anatuambia sisi ni viongozi wenye nguvu, hodari, shupavu ambao wanaweza kukabiliana vizuri sana na hali yo yote. Hata adui aliye mbaya sana atavunjwa kama kukiweko na haja. Dhihirisho letu la kutawala kwa mamlaka Yake litakuwa kama lile lile la Mwanawe. UTUKUFU!!

Tumepata ujuzi wa kina cha Mungu katika maisha yetu. Ni tukio la kibinafsi la Roho wa Mungu akiishi ndani yetu. Nia zetu zinaangazwa na hekima na maarifa ya Mungu kwa kupitia Neno Lake.

Sisi tunaenda po pote Bwana-arusi alipo. Hatutaachwa Naye kamwe. Hatutaondoka ubavuni Mwake. Tutashiriki kiti cha enzi pamoja Naye. Tutatiwa taji kwa utukufu na sifa Zake.

Yeye ametufunulia jinsi gani ambavyo adui amekuwa mdanganyifu katika kila wakati na jinsi ilivyo muhimu KUDUMU NA NENO LAKE LA ASILI. Hakuna Neno moja linaloweza kubadilishwa. Kila wakati waliongeza kwake na kuondoa kutoka kwake, wakiweka fasiri yao wenyewe kwenye Neno la asili; nao wanapotea milele kwa kufanya hivyo.

Katika Wakati wa Kanisa la Thiatira, hiyo roho ya udanganyifu ilinena kupitia papa wa Rumi na kulibadilisha Neno Lake. Alilifanya kuwa “mpatanishi mmoja kati ya Mungu na mwanadamu (si wanadamu).” Kwa hiyo sasa yeye anapatanisha kati ya mpatanishi na wanadamu. Hivyo, mpango wote wa Mungu ulibadilishwa; si kwa kubadili neno, bali kwa kubadili HERUFI MOJA. Shetani alikuwa amebadilisha “E” kuwa “A”.

Kila Neno litahukumiwa kwa Neno Lake la Asili lililonenwa kwenye kanda. Kwa hiyo, Bibi-arusi Wake LAZIMA adumu na kanda. Wakati adui anajaribu kuwakatisha tamaa watu kwa kuwapa mpango tofauti, wazo tofauti, herufi tofauti, Bibi-arusi ATADUMU NA NENO LA ASILI.

Katika kila wakati Yesu anajitambulisha Mwenyewe na mjumbe wa wakati huo. Wao wanapokea kutoka Kwake ufunuo juu ya Neno kwa ajili ya wakati wao. Ufunuo huu wa Neno huwaleta wateule wa Mungu kutoka katika ulimwengu na waingie katika muungano mkamilifu na Yesu Kristo.

Yeye amewaita na kuwaweka wakfu watu wengi ili wawe baraka kwa kanisa, lakini Yeye ana ila MJUMBE MMOJA TU ambaye Yeye alimuita ili KULIONGOZA kanisa Lake kwa Roho Wake Mtakatifu. Kuna SAUTI MOJA yenye Bwana Asema Hivi. Kuna SAUTI MOJA ambayo Yeye alisema atatuhukumu kwayo. Kuna SAUTI MOJA ambayo Bibi-arusi Wake wameweka kikomo chao cha Milele. SAUTI HIYO NI SAUTI YA MUNGU ILIYO KWENYE KANDA.

Bibi-arusi, Mapenzi ya Mungu kwetu ni Ukamilifu, na mbele zake, sisi NI WAKAMILIFU. Na huo ukamilifu ni subira, kumngojea Mungu… na kumngoja Mungu. Anatuambia ni njia ya kuumba tabia zetu. Tunaweza kuwa na mitihani, majaribu na dhiki nyingi, lakini uaminifu wako kwa Neno Lake unafanya subira ndani yetu ili tuwe wakamilifu na watimilifu, bila kupungukiwa na neno.

Hatutasahau kamwe IMANI huja kwa kusikia, kusikia Neno, nalo Neno huja kwa nabii.

Njoo ujionee furaha kuu ya maisha yako unapoketi pamoja nasi katika Mahali pa Mbinguni tunapoisikia Sauti ya Mungu ikituletea Neno juu ya: Wakati wa Kanisa la Thiatira 60-1208, saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville.(Ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki)

Ndugu. Joseph Branham

24-1103 Wakati Wa Kanisa La Pergamo

UJUMBE: 60-1207 Wakati Wa Kanisa La Pergamo

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Bikira Safi,

Je! Mmekuwa mkifurahia Nyakati Saba za Kanisa? Mungu anampa Bibi-arusi Wake ufufuo kuliko hapo awali. Yeye anatupa Ufunuo zaidi, Imani zaidi, na hakikisho zaidi kujua sisi ni nani, na kile tunachofanya kwa kukaa na Neno, Njia Yake aliyoiandaa kwa ajili ya siku hii.

Sasa Yeye anatuambia: “Kuanzia ibada ya Jumapili na kuendelea, vaeni mawazo yenu ya kiroho. Acha Roho Mtakatifu alizamishe Hilo ndani na myashike matumizi ya kiroho katika yote nitakayofanya. Ni Neno Langu lililohuishwa na Roho lililonenwa na nabii Wangu wa Malaki 4.”

Hebu na tusome na tuyapate machache ya Maneno Yake nasi tutumie mawazo yetu ya kiroho kuyahusu.

Mungu alimweka kiongozi Wake aliyejazwa Roho kwa ajili ya kundi Lake lililojazwa na Roho; malaika Wake; Naye akatia juu yake muhuri wa jina, bali haimpasi kulifunua. Hapaswi kumwambia mtu, mnaona. “Hakuna mtu ajuaye ila yeye mwenyewe.”

Kwa hiyo Mungu alimpa Bibi-arusi Wake kiongozi aliyejazwa na Roho kwa ajili ya kundi Lake lililojazwa na Roho. KIONGOZI, SIO VIONGOZI kwa ajili ya kundi Lake lililojazwa na Roho.

Anayekuja ulimwenguni hivi karibuni, yule malaika mkuu wa Nuru atakayetujia, atakayetuongoza tutoke, Roho Mtakatifu mkuu, akija mamlakani, naye atatuongoza kwa Bwana Yesu Kristo.

Malaika mkuu wa Nuru. Malaika mkuu wa Nuru ni nani kwa wakati huu wa mwisho? William Marrion Branham. Yeye hazungumzi juu ya Roho Mtakatifu. Yeye tayari amekwishakuja naye anasema atakayekuja.

Atakaye TUONGOZA TUTOKE. Kwa kweli tunajua na kuamini kwamba ni Roho Mtakatifu anayetuongoza, lakini Yeye ameweka wazi malaika Wake na Roho Mtakatifu pamoja na kusema Yeye (Roho Mtakatifu Wake) atakuwa akituongoza (KUPITIA) malaika Wake mkuu wa Nuru.

Yeye anaendelea kuwaunganisha pamoja kwa kusema:

Labda hatajua hilo,

Yeye hasemi Roho Mtakatifu hatamjua ni nani, bali malaika-mjumbe Wake wa duniani yule ambaye Yeye amemchagua KUTUONGOZA TUTOKE.

Bali atakuwa hapa moja ya siku hizi. Atafanya… Mungu atamtambulisha. Haitambidi kujitambulisha mwenyewe, Mungu atamtambulisha. Mungu atamthibitisha aliye Wake.

Tena, Yeye hasemi Roho Mtakatifu atakuwa hapa MOJA YA SIKU HIZI, bali malaika Wake mkuu wa Nuru ili kumwongoza Bibi-arusi Wake. Haitambidi kujitambulisha mwenyewe, Mungu atamtambulisha kiongozi Wake mkuu kwa Bibi-arusi Wake Mwenyewe kwa UFUNUO.

Je, umeyashika matumizi ya kiroho? Je! unaona malaika wa Nuru ni nani ambaye Mungu alimchagua kumwongoza Bibi-arusi Wake? Je! Inasema hapa ati kijiti kimepokezwa viongozi wengine?

Kamwe hutaweza kuishi juu zaidi ya mchungaji wako. Kumbuka hilo tu, unaona.

Ingawa wengine wanaweza wasituelewe na kutudhihaki, jinsi sisi tunavyofurahi na tunavyoshukuru kweli kwa Ufunuo kusema, WILLIAM MARRION BRANHAM NDIYE MCHUNGAJI WETU.

Sasa kwa kuwa kila moja ya jumbe hizi umeelekezwa kwa ‘malaika’—(mjumbe wa kibinadamu) wajibu mkubwa sana na pia majaliwa makuu sana ni fungu lake.

Ujumbe ulielekezwa kwa malaika Wake, kisha malaika Wake anampa huo Bibi-arusi; si wahudumu tu, bali kwa BIBI-ARUSI WAKE WOTE Nao upo kwenye kanda kwa wote kuusikia. Hauwezi kuongezwa kwake au kuondolewa kitu kwake, Nao HAUHITAJI FASIRI YO YOTE.

“Hivi karibuni Yeye atakuja. Na atakapokuja, Yeye atakuja kwako kwanza. Nawe utahukumiwa kulingana na Injili uliyohubiri, nasi tutakuwa raia wako.” Nikasema, “Wataka kusema ninawajibika kwa hawa wote?” Akasema, “Sisi sote. Wewe ulizaliwa kiongozi.”

Wakati siku ile kuu ya hukumu itakapokuja, Yeye anakuja kwanza kwa malaika Wake wa Nuru naye atamhukumu yeye kwanza kulingana na injili aliyohubiri. Sisi ni RAIA WAKE. Yeye anawajibika kwa kila mmoja wetu kwa kuwa yeye alikuwa KIONGOZI aliyechaguliwa na Mungu.

Weka matumizi yako ya kiroho kwenye jambo hilo. Tutahukumiwa kwa yale ambayo malaika wa Mungu aliyosema. Kwa hiyo, unataka kubahatisha kuhusu uzima wako wa milele kwa kile mtu fulani anachosema ALISEMA wakati wewe unaweza kusikia moja kwa moja kutoka KWAKE?

Anawezaje mtu yeyote kuamini kuwa kuna HUDUMA MUHIMU KULIKO ILE ILIYO KWENYE KANDA. Ikiwa unaamini hivyo, au umeshawishiwa hivyo kwa hoja, ni afadhali urudi kwenye NENO LA ASILI; kwa maana utahukumiwa kwa maneno yaliyo kwenye kanda. Dumu na Neno kama vile Lilivyonenwa.

Lakini huyu nabii atakuja, na kama vile yule mtangulizi wa kule kuja kwa kwanza alivyopaza sauti, “Tazama Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu,” vivyo hivyo bila shaka naye atapaza sauti, “Tazama Mwana-Kondoo wa Mungu anayekuja katika utukufu.” Atafanya jambo hili, kwa maana kama vile Yohana alivyokuwa mjumbe wa ile kweli kwa wateule, ndivyo alivyo na huyu mjumbe wa mwisho kwa wateule na kwa bibi-arusi aliyezaliwa kwa Neno.

Ni nani atakayetutambulisha kwa Bwana Yesu? Malaika Wake mkuu wa Nuru, William Marrion Branham.

Njoo uwe Bibi-arusi Bikira Safi pamoja nasi tunapomsikia malaika-mjumbe Wake mkuu akituletea Ufunuo zaidi, Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki) tunaposikia Ujumbe 60-1207 – “Wakati wa Kanisa la Pergamo.”

Ndugu. Joseph Branham

24-1027 Wakati Wa Kanisa La Smirna

UJUMBE: 60-1206 Wakati Wa Kanisa La Smirna

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliyejazwa Roho,

Kuna kundi moja tu la watu; kundi maalum sana la watu, ambao wanaweza kusikia yale Roho anayosema katika wakati huu wa mwisho. Ni kundi maalum ambalo limeupokea Ufunuo wa wakati huu. Kundi hilo ni la Mungu. Kundi lile ambalo haliwezi kusikia, si la Mungu.

Kundi ambalo linaweza, na linasikia yale Roho anayosema, linapokea Ufunuo wa Kweli. Sisi ndio hao walio na Roho wa Mungu. Sisi ndio hao waliozaliwa na Mungu na kubatizwa kwa Roho Mtakatifu. Sisi ndio Bibi-arusi Wake Aliyejazwa Roho ambaye ameupokea Ufunuo kwa ajili ya wakati wetu.

Inamaanisha nini kwetu sisi Kubonyeza Play? UFUNUO! Ni kusikia, kupokea na kukaa na Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii. Sauti ya Mungu mwenyewe ikinena mdomo kwa sikio na Bibi-arusi Wake. Ni Roho Mtakatifu akizungumza na mioyo na nafsi zetu.

Tunajua Mungu huwatumia watu waliotiwa mafuta na Roho wake kunena, lakini hakuna mahali pengine pa kuisikia Bwana Asema Hivi isipokuwa kwa Kubonyeza Play na kuisikia SAUTI ya malaika wake wa saba, William Marrion Branham. Ndiyo Sauti pekee iliyothibitishwa na Roho Mtakatifu Mwenyewe. Yeye ndiye Sauti ya Mungu, nabii wa Mungu, mchungaji wa Mungu, kwetu sisi, na kwa ulimwengu mzima.

Wakati Yeye anaponena, sisi tunasema AMINA kwa kila Neno; kwa maana ni Mungu mwenyewe anayesema nasi. Neno Lake ndilo Neno pekee lisilohitaji kufasiriwa. Ni Mungu akitumia sauti yake kuongea na Bibi-arusi Wake.

Ni Mungu mwenyewe anayetuambia, “Watoto wangu, si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi. Kabla hakujawa na chembe ya vumbi ya nyota; kabla hata sijajulikana kwako kuwa Mungu wako, Nilikujua. Ulikuwa Niani Mwangu, ukiwa katika Mawazo Yangu ya milele. Wewe ni Bibi-arusi Wangu halisi wa Uzao Wa Neno Lililonenwa.

Ingawa mlikuwa katika Mawazo Yangu ya milele, Sikuwadhihirisha hadi majira Yangu niliyoyakusudia na yaliyoamriwa. Kwa maana nilijua NINYI mngekuwa kundi langu maalum ambalo lingedumu na Neno Langu. Wengine wote wameshindwa, lakini Nilijua ninyi hamgeshindwa.

Ninajua ya kwamba unateswa na kudhihakiwa kwa sababu umedumu na nabii Wangu, lakini wewe ndiye Mzabibu Wangu wa Kweli ambao haujakengeuka kutoka kwenye Neno Langu, bali umedumu kuwa mkweli na mwaminifu kwa nabii Wangu ambaye hunena Maneno Yangu.

Kuna wengine wengi ambao wamefundishwa kwa uaminifu, lakini wao daima hawajifunzi jinsi ilivyo jambo muhimu kusema yale tu Mimi Niliyoyanena kupitia mjumbe Wangu.”

Jinsi tunavyopaswa kuwa waangalifu kusikia sauti MOJA, kwa kuwa Roho hana ila sauti moja ambayo ni sauti ya Mungu.

Loo! jinsi ilivyo muhimu kusikia sauti ya Mungu kwa njia ya wajumbe Wake, halafu kusema yale waliyopewa kuyaambia makanisa.

“Neno Langu daima limemjia nabii Wangu, lakini katika siku hii, Ilinibidi niirekodi Sauti Yangu ili KUSIWEKO NA MAKOSA kwa yale niliyomwambia Bibi-arusi. Kuna timazi moja tu, fimbo moja tu, na hiyo ni NENO nililolinena Mimi kupitia malaika Wangu. Kama ilivyo katika kila wakati, nabii Wangu ndiye Neno la siku hiyo.”

Kanda, Sauti Yake, ni barua ya mahaba kwetu sisi. Wakati adui anapotupiga mara kwa mara kupitia majaribio na dhiki na shida zetu, Yeye alimtuma malaika Wake mwenye nguvu kutuambia kwamba si chochote ila upendo wa kuchagua wa Mungu kwetu sisi, akituthibitishia kwamba ametuchagua sisi kwani hatutaondoshwa.

Kusudi Lake kuu ni kwamba baada ya sisi kuteseka kwa muda kidogo, angetufanya wakamilifu, atuimarishe na kututia nguvu. Alituambia kwamba hata Bwana wetu Yesu alikamilishwa kwa mateso Yake. Ni baraka iliyoje ambayo Yeye ametuachia. Kwa maana kwa mateso yetu, Yeye angetufikisha katika ukamilifu pia.

Anatujenga tabia kupitia majaribio na dhiki zetu. Maana tabia yetu haiumbiki bila mateso. Hivyo, mateso yetu ni USHINDI kwetu, na si karama.

Tunawezaje kuuthibitisha upendo wetu Kwake?

¶ Kwa kuamini yale aliyosema.

¶ Kukaa na Neno Lake.

¶ Kuenenda kwa furaha katikati ya majaribio na dhiki zetu, ambayo Yeye, katika hekima Yake kuu, anayaruhusu yatimie.

Jinsi anavyoinua roho zetu kwa kulisikia Neno Lake. Sauti Yake hufariji nafsi zetu. Tunapobonyeza Play na kumsikia Yeye akinena, mizigo yetu yote inainuliwa. Hatuwezi hata kuanza kufikiria ni hazina gani ambazo zimewekwa kwa ajili yetu kupitia dhiki zetu zote.

Loo, Bibi-arusi wa Yesu Kristo, ninayo furaha jinsi gani kuwa Mmoja Wao pamoja na kila mmoja wenu. Ni furaha iliyoje moyoni mwangu kujua Yeye ametupa Ufunuo wa Neno Lake. Wakati anapotuambia zitafanana sana ingewapoteza walio wateule kama yamkini, Yeye ametupa UFUNUO WA KWELI.

Njoo, uingie katika Roho pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 sita MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 moja JIONI ya Afrika Mashariki) tunapolisikia Neno kamilifu: 60-1206 – Wakati wa Kanisa la Smirna.

Ndugu. Joseph Branham

24-1020 Wakati Wa Kanisa La Efeso

UJUMBE: 60-1205 Wakati Wa Kanisa La Efeso

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Kweli,

Ni wakati mzuri sana jinsi gani tulio nao huku Uzima Wake ukitiririka na kudundadunda ndani na kupitia kwetu, ukitupa uzima. Bila ya Yeye, hakungekuwa na uzima wo wote. Neno Lake ndilo pumzi yetu.

Katika siku hii kuu ya giza, sisi ndio kundi Lake la mwisho ambalo limeinuka; Bibi-arusi Wake wa kweli wa siku ya mwisho ambaye atamsikiliza Roho peke yake, Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku yetu. 

Jinsi tunavyopenda kumsikia Yeye akituambia, “Kwangu Mimi, umefananishwa na dhahabu safi iliyofuliwa. Haki yako ni haki Yangu. Sifa zako ndio sifa Zangu zenye utukufu. Wewe ndiye Bibi-arusi Wangu wa Kweli wa kupendeza.”

Kama vile vita vyetu vinavyoonekana kuwa vigumu zaidi na zaidi kila wiki, sisi Tunabonyeza Play tu ili kumsikia Yeye akizungumza nasi kwa utamu sana na kutuambia, “Usijali, wewe unaistahili injili Yangu. Wewe ni kitu cha uzuri na furaha. Ninapenda kukutazama pindi unapomshinda adui kwa majaribu na majaribio ya maisha haya.”

Ninaiona taabu yako ya upendo; ni wito mkuu maishani mwako kunitumikia Mimi. Nilijua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu ya kwamba wewe ungemtambua malaika Wangu mwenye nguvu ambaye ningemtuma awe Sauti Yangu kwako; jinsi ambavyo usingedanganyika wakati ambapo wale mbwa-mwitu wakali wakija huku wakijaribu kudai ufunuo sawasawa. Wewe Hungetoka kwenye Neno Langu, hata kidogo, HATA KWA NUKTA MOJA. Wewe ungekaa na Neno Langu, Sauti Yangu.

Ungeona wakati ninapokufunulia Neno Langu jinsi gani ule Mzabibu wa Kweli na mzabibu wa uongo ile iliyoanza katika Bustani ya Edeni jinsi ingekua pamoja kote katika nyakati zote. 

Kile kilichoanza katika kanisa la kwanza kingeendelea katika kila wakati. Jinsi ambavyo katika wakati wa kwanza wa kanisa, ule mzabibu wa uongo wa Shetani ungeanza kujiingiza ndani, na kuwashinda washirika kwa roho yake ya unikolai. Lakini jinsi gani ninavyolipenda hili kwamba wewe tu, Bibi-arusi Wangu mteule, hutadanganywa. 

Wiki hii, Nitaliangazia Neno Langu ndani yenu kwa kuifichua ile siri kuu ya ule uzao wa nyoka. Nitawafunulia kwa undani yote yaliyotukia katika bustani ya Edeni; jinsi ambavyo Shetani alivyojichanganya katika jamii ya binadamu. 

Litakuwa wazo la kufurahisha sana wakati mtakapotambua kwamba Mimi, Ule Mti wa Uzima katika Bustani ya Edeni, ambao usingeweza kukaribiwa hadi sasa kwa sababu ya kuanguka kwa Adamu, sasa mmepewa ninyi, washindi Wangu. 

Hii ndiyo itakuwa thawabu yako. Nitakupa haki ya bustani ya Mungu; ushirika wa daima na Mimi. Kamwe hautatengana na Mimi. Po pote Niendapo, wewe, Bibi-arusi Wangu utakwenda. Kile kilicho Changu Mimi, Nitakishiriki na wewe, Mpendwa Wangu.

Jinsi gani mioyo yetu inavyoenda mbio ndani yetu wakati tunapoyasoma maneno haya. Tunajua ule utimilifu wa ahadi zake unakaribia upesi, na ni vigumu kwetu kusubiri. Na hebu tuharakishe kulitii Neno Lake na hapo tuthibitishe kustahili kwetu kushiriki utukufu Wake.

Ningependa kuwaalika mje kuungana nasi wakati tunapoendelea na somo letu kuu la Nyakati Saba za Kanisa, ambapo Mungu anapotufunulia Neno Lake kwa njia Yake aliyoiandaa, malaika-mjumbe Wake wa saba. 

Ndugu. Joseph Branham

Jumapili saa 6:00 sita MCHANA, saa za Jeffersonville. (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)
60-1205 Wakati Wa Kanisa La Efeso

24-1013 Ono La Patimo

UJUMBE: 60-1204E Ono La Patimo

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Neno Mkamilifu, 

Ni kitu gani kinachotukia ndani ya Bibi-arusi kote ulimwenguni? Tunaingia katika Roho, tukiinuka na kupaza sauti, “Utukufu! Haleluya! Bwana asifiwe!” Mungu anatusafirisha na kulifunua Neno Lake kwa Bibi-arusi Wake.

Mambo ambayo tumeyasoma na kuyasikia maisha yetu yote sasa yanadhihirika. Uhuishaji mkuu unatendeka. Tumeangaziwa na Neno kuliko wakati wowote. 

Tunalihisi ndani kabisa ya nafsi zetu. Kuna kitu fulani cha tofauti, kuna kitu kinatendeka. Tunamhisi Roho Mtakatifu akitutia mafuta, akiijaza mioyo na akili zetu kwa Neno Lake. 

Tunaweza kumsikia Yeye akisema nasi: Najua adui anapigana nanyi kuliko hapo awali, lakini msiogope enyi watoto wadogo, NINYI NI WANGU. Ninawapa upendo Wangu, ujasiri na uwezo. Mnene tu Neno, nami nitalitimiza. Mimi ni pamoja nanyi siku zote.

Katika somo letu kuu la Ufunuo wa Yesu Kristo, tuko chini ya matazamio makubwa kila wiki nini kifuatacho Atakachotufunulia. Neno lake ndilo kimbilio letu pekee, amani na faraja yetu. Tunasikiliza kwa makini tena na tena na tena. Kila aya ndogo tunayosoma, tunataka kupiga kelele na kupaza sauti wakati Neno linapofunuliwa mbele ya macho yetu. Imani ya Kunyakuliwa inakuja juu ya Bibi-arusi, ikizijaza nafsi zetu.

Hebu wazia, hakuna mahali pengine ulimwenguni unapoweza kwenda, ila papo hapo kwenye vidole vyako, kuisikia Sauti ya Mungu ikisema nawe na kulifunua Neno Lake. 

Jinsi ambavyo Mungu alivyoliondoa lile pazia, akalivuta, na kumruhusu Yohana atazame ndani na kuona kile ambacho kila wakati wa kanisa ungefanya, na kuyaandika katika Kitabu na kututumia sisi. Ndipo, wakati utimilifu wa wakati ulipotimia, Mungu alitutumia sisi malaika Wake wa saba mwenye nguvu kukinena, na kufunua yote Ilichomaanisha. 

Yohana aliandika kile alichokiona, lakini hakujua maana yake. Yesu hata hakulijua hilo wakati alipokuwa hapa duniani. Hakuna mtu katika nyakati zote aliyejua, mpaka siku hii, wakati huu, watu hawa, SISI, Bibi-arusi Wake.

Jinsi ambavyo ametufunulia kwamba hizo taa saba zilikuwa zikifyonza uhai na nuru kutoka kwenye hazina ya hilo bakuli kuu. Alitueleza jinsi ambavyo kila mmoja walivyokuwa wametumbikiza tambi zao mle. Kila mjumbe wa wakati wa kanisa alikuwa amewashwa moto na Roho Mtakatifu na utambi wake ukiwa umetumbukizwa ndani ya Kristo, akifyonza uzima halisi wa Kristo na kuitoa Nuru hiyo kwa kanisa. Na sasa, mjumbe wetu wa siku ya mwisho, aliye mkuu kuliko wajumbe wote, alikuwa na maisha yale yale na Nuru ile ile iliyodhihirishwa na maisha yaliyofichwa pamoja na Kristo katika Mungu.

Kisha malaika wetu mwenye nguvu anatuambia kuwa si tu kwamba kila mjumbe alionyeshwa hapo, BALI KILA MMOJA WETU NASI PIA, waamini wa kweli wa Mungu. Kila mmoja wetu pia anawakilishwa wazi wazi hapo. Kila mmoja wetu anafyonza kutoka kwenye chemchemi ile ile kama wale wajumbe. Sote tumetumbukizwa kwenye bakuli lile lile. Tumekufa kwa nafsi zetu na maisha YETU yamefichwa pamoja na, na ndani ya, Kristo Yesu Bwana wetu. 

Jinsi Yeye anavyotutia moyo kwa kusema hakuna mtu anayeweza kututoa sisi kutoka katika Mkono wa Mungu. Maisha yetu hayawezi kuchezewa. Maisha yetu yanayoonekana yanawaka moto na kuangaza, yakitoa nuru na madhihirisho ya Roho Mtakatifu. Maisha yetu ya ndani, yasiyoonekana yamefichwa ndani ya Mungu na kulishwa kwa Neno la Bwana. 

Vita ni vikali. Adui anashambulia kwa hasira kuliko hapo awali, akijaribu awezavyo kutuvunja moyo, kutupiga kabisa, lakini hawezi kulifanya hilo.  Mungu Mwenyewe ananena nasi kupitia midomo ya mwanadamu naye anatuambia, SISI NI BIBI-ARUSI WAKE, ALIYEMCHAGUA, na hilo linamshinda shetani KILA WAKATI. 

Bwana wetu Mkamilifu, akinena Neno Lake Kamilifu, akitoa Amani Kamilifu, kwa Bibi-arusi Wake Mkamilifu.

Kama kawaida, tunaualika ulimwengu mzima uje kuchovya utambi wao ndani ya BAKULI KUU, Ujumbe huu, ambao umehifadhiwa na kutunzwa kwa ajili ya Bibi-arusi. Tutakuwa tukipiga mayowe na kupaza sauti saa 6:00 Sita MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 Moja JIONI ya Afrika Mashariki) tunapoisikia Sauti ya Mungu ikinena na kufunua yaliyotukia katika: Ono la Patimo 60-1204E.

Ndugu. Joseph Branham 

24-1006 Ufunuo Wa Yesu Kristo

UJUMBE: 60-1204M Ufunuo Wa Yesu Kristo

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Jeshi la Mungu Lisiloweza Kushindwa,

Sisi ndio wale ambao Baba aliyowachagua na kuwapa UFUNUO WA KWELI wa Yeye Mwenyewe; KANISA Lake la KWELI na pekee. Wale aliowachagua watende KAZI Yake KUBWA ZAIDI. Kwa maana kwa Roho Wake, tunaweza kuitambua na kuipinga roho ya mpinga-Kristo ya Shetani. Yeye HANA NGUVU mbele ZETU, kwa sababu sisi ni Jeshi Lake Lisiloweza Kushindwa.

Shetani anachukia ufunuo wote. LAKINI SISI TUNAUPENDA. kwa maana sisi ni wapenzi wa Neno la Mungu lililofunuliwa. Tukiwa na ufunuo wa kweli maishani mwetu, milango ya kuzimu haiwezi kutushinda, tunamshinda adui. Kila pepo yuko chini ya miguu yetu. Sisi ni Mmoja na Yeye nasi tunaweza kunena Neno, kwa maana sisi ni Neno Lake.

Bwana ameliweka hilo moyoni mwangu kwamba tujifunze na kuzisikia Nyakati Saba za Kanisa. Zitakuwa Wiki kuu sana kwa kila mmoja wetu. Atakuwa akitufunulia Neno Lake kuliko hapo awali, kwa nguvu zake za ushindi.

Huu sasa ndio wakati. Haya ndio majira yake. Atakuwa akituhuisha, akitutia moyo, kwa kutupa Changamko kwa Ufunuo, nalo Litaiwasha moto mioyo yetu!!

Ufunuo wa Yesu Kristo ni Kitabu cha kinabii ambacho kinaweza tu kueleweka na tabaka fulani la watu walio na ono la kinabii, SISI, Bibi-arusi Wake. Inahitaji Ufunuo wa KWELI kujua kwamba unasoma na kuisikia Sauti ya Mungu inayotoka kwa malaika-mjumbe Wake aliyemchagua, akitupa mafundisho ya kimbinguni.

Ni Ufunuo wa Yesu Kristo aliopewa Yohana kwa ajili ya Wakristo wa nyakati zote. Ndicho kitabu pekee katika Biblia nzima ambacho kimeandikwa na Yesu Mwenyewe, kwa kumtokea mwandishi Yeye Mwenyewe.

Ufunuo 1:1-2, “Ufunuo wa Yesu Kristo, aliopewa na Mungu awaonyeshe watumwa wake mambo ambayo kwamba hayana budi kuwako upesi; naye akatuma kwa mkono wa malaika Wake na kumwonyesha mtumwa Wake Yohana: aliyelishuhudia Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu Kristo, yaani, mambo yote aliyoyaona.

Kitabu cha Ufunuo ni mawazo ya Mungu kabisa yaliyoandikwa na Mungu Mwenyewe. Lakini Yeye alituma na kumwonyesha mtumwa Wake Yohana kupitia malaika Wake. Yohana hakujua maana Yake; aliandika tu kile alichokiona na kusikia.

Lakini leo, Mungu alimtuma malaika Wake mwenye nguvu duniani kufunua Ufunuo huu Mkuu kwa Bibi-arusi Wake, ili tuweze kusoma na kusikia yale yaliyokuwa yametukia katika nyakati zote za kanisa. Tunaweza kuliona lile kundi Lake dogo lile lililodumu mwaminifu na wa kweli kwa Neno katika kila Wakati.

Mungu alinena kupitia malaika Wake na kusema ya kwamba katika siku hizi za mwisho, wakati Sauti ya mjumbe Wake wa wakati wa saba wa kanisa itakapoanza kupiga baragumu, Yeye atafunua siri za Mungu kama zilivyofunuliwa kwa Paulo. Wale wanaompokea nabii huyo katika jina lake mwenyewe watapokea matokeo mema ya huduma ya nabii huyo.

Utukufu, sisi ni Bibi-arusi wa Kubonyeza Play wa Mungu ambaye tumempokea nabii huyo katika jina lake mwenyewe, nasi tunapokea matokeo mema. Tunaamini ni Sauti ya Mungu inayonena na kumwongoza Bibi-arusi Wake.

Lo, Kanisa, kile tutakachosoma na kukisikia katika wiki zijazo. Kwake Yeye, sisi tunafananishwa na dhahabu SAFI. Kile alicho Yeye, ndicho tulicho. Sisi ndio Mzabibu Wake wa Kweli. Tumeshinda. Tumefanywa wakamilifu, tumeimarishwa, tumetiwa nguvu. Tumechaguliwa kwa Upendo Wake wa Kuchagua. Hakuna cha kuogopa. Sisi ndio kundi lile lililomsikia mjumbe na Ujumbe wake na Kuutwaa na Kuuishi.

Kila wiki tutakuwa tunasema, “Je, mioyo yetu haiwaki ndani yetu wakati Yeye anaponena na kutufunulia Neno lake njiani”.

Ukitaka kuuhisi upako wa Roho Wake Mtakatifu, kupokea Ufunuo zaidi wa Neno la Mungu, na unataka kuketi katika uwepo wa Mwana kuivishwa, na kupokea Imani ya Kunyakuliwa, njoo uungane nasi Jumapili saa 6:00 Sita MCHANA, saa za Jeffersonville.(Ni saa 1:00 Moja JIONI ya Afrika Mashariki), tunapoanza somo letu kuu juu ya: Ufunuo Wa Yesu Kristo 60-1204M.

Ndugu. Joseph Branham

Ningependa kukuhimiza usikie, au kusoma, kila wiki Kitabu cha Maelezo ya nyakati za Kanisa, sura tuliyomaliza kusikiliza kila Jumapili.

24-0929 Ufunguo Wa Mlango

UJUMBE: 62-1007 Ufunguo Wa Mlango

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wenye Ufunguo wa Imani,

“Mimi ndiye Mlango wa zizi la kondoo. Mimi ndimi Njia, Njia pekee, Kweli, na Uzima, na mtu haji kwa Baba ila kwa njia ya Mimi. Mimi ndimi Mlango wa vitu vyote, na imani ndiyo ufunguo unaofungua mlango ili uweze kuingia.”

Kuna mkono mmoja tu unaoweza kuushikilia ufunguo huu, na huo ni mkono wa IMANI. IMANI ndiyo ufunguo pekee unaofungua ahadi zote za Mungu. IMANI katika kazi yake iliyokwisha kumalizika inaufungua kila mlango kwa kila hazina iliyo ndani ya Ufalme wa Mungu. IMANI ni Ufunguo malaya mkuu wa Mungu ambao unaufungua KILA MLANGO KWA BIBI-ARUSI WAKE nasi tunaushikilia huo Ufunguo katika MKONO wetu wa IMANI.

Ufunguo huo wa imani uko mioyoni mwetu, nasi tunasema, “Ni Neno la Mungu; Ni ahadi za Mungu kwa ajili yetu, nasi tunaushikilia ufunguo.” Na kisha, kwa kila sehemu ya imani tuliyo nayo, bila kutilia shaka hata chembe moja, tunaufungua kila mlango unaosimama kati yetu na baraka ambazo Mungu alizonazo kwa ajili yetu. Inazima jeuri ya moto. Inaufungua uponyaji kwa wagonjwa. Inaufungua wokovu wetu. Tumefika kwenye Mlango na lolote tunalofanya kwa neno au kwa tendo, tunayafanya yote katika Jina Lake, tukijua kwamba tunao ufunguo wa imani; nao ni ufunguo uliotengenezwa kwa Maandiko.

Sisi hatujali kile mtu yeyote anachowazia, kuna jambo moja la hakika: Mungu alituita SISI, alituchagua SISI tangu awali, alitufunulia SISI Neno Lake, alituambia sisi ni nani, nasi tumeyakinia kulifuata Neno Lake, kwa sababu Yeye ametuita sisi tuwe Bibi-arusi Wake.

Baba alizishikilia nyota Zake saba, wajumbe Wake saba, kwa zile nyakati saba mkononi Mwake. Amewashika mkononi Mwake, hivyo wanahusishwa na nguvu Zake. Hicho ndicho mkono unachomaanisha. Unamaanisha nguvu za Mungu! Na mamlaka ya Mungu.

Tumelishika Neno lake katika mikono yetu ya Imani, ikimaanisha uweza na mamlaka ya Mungu vipo MIKONONI MWETU naye ametupa UFUNGUO wa kuufungua kila mlango kwa kila jambo tunalohitaji. Ni Ufunguo Maalum ambao utaufungua KILA MLANGO.

Sasa ninajua kwa nini Mungu alitupa vidole 5 katika kila mkono; sio 4, sio 6, lakini 5, kwa hivyo kila wakati tunapoitazama mikono yetu tutakumbuka, tunayo ILE IMANI ya kuufungua kila mlango.

Ni ishara ya milele kwa jamii ya binadamu kwa hivyo sisi hatutasahau kamwe; daima tutakumbuka na kujipa moyo, kwamba tunaishikilia IMANI hiyo mikononi mwetu. Naye ataiinua imani yetu ya mbegu ya haradali na kutupa ILE IMANI YAKE KUU KATIKA NENO LAKE LISILOWEZA KUSHINDWA KAMWE, LA MILELE LISILOSHINDWA KAMWE!!!

Tunaweza kuinua mikono yetu Mbinguni, kuvinyoosha vidole vyetu 5 kwa kila mkono na kumwambia, “Baba, tunaamini na tunayo IMANI katika kila Neno ulilonena. Ni Ahadi Yako, Neno Lako, nawe Utatupatia Ile IMANI TUNAYOHITAJI ikiwa tu tutaamini….nasi TUNAAMINI.”

Kwa vile tutakuwa na ibada yetu ya Ushirika hadi ifikapo Jumapili jioni, ningependa kuwahimiza mchague Ujumbe wa kusikiliza pamoja na Kanisa lako, familia, au mtu binafsi, Jumapili asubuhi, kwa wakati unaofaa kwako. Hakika hakuna njia bora ya kuitathmini Imani yetu kuliko kusikia Neno; kwa maana IMANI huja kwa kusikia, kulisikia Neno, nalo Neno huja kwa nabii.

Hebu Basi tuungane wote kwa pamoja saa 11:00 kumi na moja JIONI. (kwa masaa ya nchi yako) ili kusikiliza Ujumbe, 62-1007 Ufunguo wa Mlango. Kama ilivyotangazwa, ningependa kuifanya hii kuwa Ibada Maalum ya Ushirika, ambayo itakuwa ikicheza kwenye Redio ya Sauti (Voice Radio) saa 11:00 kumi na moja JIONI. (Masaa ya Jeffersonville). Mnaweza kupakua na kucheza ibada kwa Kiingereza au lugha zingine kwa kubofya hapa: BOFYA HAPA.

Sawa na ibada zingine za Ushirika wa Nyumbani katika wakati uliyopita, mwishoni mwa kanda Ndugu Branham ataombea mkate na divai. Kutakuwa na muziki wa piano kwa dakika kadhaa ili mkamilishe sehemu ya ibada ya Ushirika. Kisha, Ndugu Branham atasoma Maandiko yanayohusu kutawadhana miguu, na Nyimbo za Injili zitafuata usomaji wake kwa dakika kadhaa, ili muweze kukamilisha sehemu ya ibada ya kutawadhana miguu.

Ni fursa iliyoje tuliyo nayo kumwalika Bwana wetu Yesu kula pamoja na kila mmoja wetu katika nyumba zetu, makanisani, au popote ulipo. Niombeeni wakati mnapozungumza Naye, kama ilivyo hakika nitakuwa nikiwaombea.

Mungu awabariki,

Ndugu Joseph Branham