Category Archives: Uncategorized

23-0917 Kusimama Katika Pengo

UJUME: 63-0623M Kusimama Katika Pengo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wateule,

Bwana wetu Yesu anatupenda sana, hata ikampendeza Yeye kututumia nabii katika siku yetu. Mmoja yule ambaye alimwamini asilimia mia moja. Mmoja yule Yeye angeweza kuja na kuishi ndani yake, ili aweze kujifunua Mwenyewe kupitia ule mwili wa mwanadamu kumwita Bibi-arusi Wake.

Nabii wake alitupenda sana hata akatuahidi, sisi, na Mungu, ya kwamba Ujumbe wo wote mpya ungetoka kwenye maskani yake ndogo. Angeurekodi, kuuhifadhi, ili Bibi-arusi wa Mungu apate Chakula cha Kiroho cha kufanyia karamu, hata alipokuwa ameondoka.

Mungu alimpenda malaika-nabii Wake sana Yeye alimsaidia nabii Wake kulitimiza neno lake kwetu.

Baada ya Mungu kunena kupitia malaika Wake mwenye nguvu na kuifunua kikamilifu na kutufasiria sisi Biblia nzima, ndipo akakifungua kilele cha Mwamba ulio kama piramidi, ambao hata haukuandikwa, na kulifunua hilo kwa malaika Wake, ili aweze kutupa sisi siri Zake zote zilizofichwa, Bibi-arusi Wake.

Mungu hata alitoa ono kwa Ndugu Roberson, ambapo aliona Nguzo ya Moto ikimtwaa nabii Wake na kumpeleka Magharibi, kisha ikamrudisha na kumweka mbele ya Meza ambapo alikuwa amekwisha badilishwa.

Ndipo Roho Mtakatifu akanena na kumwambia,
“Huyu ni mtumishi Wangu. Nami nimemwita kuwa nabii kwa wakati huu, kuwaongoza watu kama tu Musa alivyofanya. Naye amepewa mamlaka, angeweza kunena kitu kiwepo.”

Wito wa Musa ulikuwa ni upi? Yeye alipaswa kufanya kitu gani? Mungu alikuwa amemwagiza Musa kuwaongoza watu hadi nchi ya ahadi. Lakini waliinuka watu waliokuwa wameamua kwamba wangeingilia agizo ambalo Mungu alimpa Musa, wakisema, “Umejitwalia madaraka mengi mno wewe. Wewe, ukijaribu kujifanya mtu wa pekee katika kundi hili ambaye ana mamlaka yote.”

Tendo hili lilimuudhi Mungu sana mpaka akamwambia Musa, “Jitenge ukaondoke miongoni mwao. Nitaliua tu kundi hilo lote, na kuanza kizazi kipya kwako.” Naye Musa akaanguka mbele za Mungu na kusema yeye itambidi kuja juu yake.

Kama Mungu angeamua kuwaangamiza watu katika siku yetu, ni nani angesimama kama Musa kwa ajili ya watu? Tungempata wapi mtu ambaye angesimama, au angeweza kusimama, ambaye Mungu angemkubali kama Yeye alivyomkubali Musa? Kuna maisha ya mtu mmoja tu duniani yaliyo muhimu sana kwa Mungu kuizuia hasira yake, malaika wake wa saba mwenye nguvu.

Mungu daima amekuwa na mpango. Bibi-arusi Wake atautambua mpango huo naye atadumu nao Neno kwa Neno. Wao wanajua inawabidi wadumu na Sauti hiyo ambayo Mungu ameichagua kuwaongoza kufika kwenye Nchi ya Ahadi.

Mungu alinena kupitia nabii wake naye akatoa nafasi ya kutosha ya kwenda mwelekeo tofauti upendao, kama vile Nuhu alivyowafanyia yule njiwa na kunguru ndani ya safina. Lakini kama tu vile njiwa ambaye daima alirudi ndani ya Safina, Bibi-arusi daima atarudi kwenye Ujumbe, Sauti hiyo, KANDA.

Nabii wa Siku yetu alikuwa nani? Kumekuwa na manabii wenye nguvu hapo awali ambao Mungu alikuwa amewaita na kuwatuma kuongoza watu wake kote katika nyakati: Ibrahimu, Musa, Eliya, Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyekuwa kama huyu nabii mwenye nguvu wa siku yetu. Yeye Aliitwa kuwepo kwenye huduma ya juu zaidi kuliko hao wote. Yeye ndiye ambaye Mungu alimchagua kufunua siri zake zote. Yeye ndiye ambaye Mungu alimchagua kunena kitu fulani kiwepo pasipo na kitu. Yeye ndiye aliyechaguliwa kufunua Mvuto wa Tatu. Yeye ndiye ambaye Mungu alimchagua kumwongoza Bibi-arusi Wake.

Sisi ni watu waliobarikiwa jinsi gani, Bibi-arusi mteule wa Mungu. Tunawezaje kushushwa chini? Tunawezaje kuwa na huzuni? Shetani anajaribu kutukatisha tamaa, lakini tunao ushindi, tuko ndani tumetiwa muhuri, salama ndani ya Safina. Milango imefungwa. Hakuna kinachoweza kutudhuru. Sisi ni Adamu Wake aliyerejeshwa.

Anakuja kwa ajili yetu, Bibi-arusi Wake mteule. Kutakuwa na baadhi yetu ambao haitawalazimu kuonja kifo, lakini watabadilishwa mara moja, kufumba na kufumbua. UTUKUFU!!

Kama vile kila mmoja wenu, nimechangamshwa sana, wakati kila siku, Neno Lake, Ufunuo wangu aliyonipa, unazidi kuwa mkuu zaidi na zaidi. Niko chini ya matarajio makubwa. Ikiwa Yeye hatakuja leo, huenda kesho, lakini najua Yeye yuaja hivi karibuni sana na Anakuja KWA AJILI YANGU NA KWA AJILI YAKO.

Njoo uungane nasi Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ), tunaposikia Chakula ambacho kimehifadhiwa mahali pamoja padogo tunapotazama na kusikia: Kusimama Katika Pengo 63-0623M. Tutauanza Ujumbe huu kwenye namba ndogo ya 27.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma Kabla ya Kusikiliza Ujumbe:

Hesabu 16:3-4

23-0910 Muhuri Wa Saba

UJUME: 63-0324E Muhuri Wa Saba

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Kanda,

Ni siku ya namna gani tunayoishi! Ni wakati mkuu jinsi gani! Zile siri, mafumbo, yote yanayofunuliwa kwetu kila siku. Hatuoni tu yale ambayo tumeyapita, tunajua ile saa hasa tunayoishi na yale hasa yaliyo mbele.

Tunaambiwa mstari kwa mstari kile kitakachotokea. Yeye anatuambia waziwazi sisi ni nani, ni akina nani watakaokuwapo kule, na hata kile tutakachofanya. Wale Wayahudi 144,000, lile kanisa lililotakaswa kwa Dhiki, watenda kazi katika mashamba ya mizabibu ambao watakaoleta heshima na utukufu wao katika mji ule.

Lakini basi anatuambia huyo hatakuwa wewe…loo la, wewe ni Bibi-arusi Wangu, uko pamoja Nami katika Mji ule. Wewe hutakuwa huko nje ukifanya kazi katika mashamba ya mizabibu, wewe ni kipenzi changu. Wewe u Malkia Wangu pamoja Nami, Mfalme wako. Ninyi ndio wale moja ya mia ya hao moja kwa tano niliyowachagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Nimepatengeneza Mahali hapa KWA AJILI YENU TU…NA JINSI TU MNAVYOLIPENDA.

Kuwazia tu, tunakusanyika kuizunguka Meza yake anapozungumza nasi wiki baada ya wiki, siku baada ya siku, saa baada ya saa, akitufunulia Neno Lake lote la ajabu. Yeye anatuambia tena na tena sisi ni nani; jinsi gani Yeye anavyotupenda; kile kilichokuwa, kile kilicho sasa, na kile kitakachotukia.

Hakuna maneno ya kuelezea jinsi inavyomaanisha kwetu, ama jinsi tunavyojisikia wakati tunapomsikia Yeye akituambia mambo haya. Wakati Tunapobonyeza Play na kuisikia Sauti hiyo, tunaondoka katika ulimwengu huu na mara moja tunaketi katika ulimwengu wa Roho pamoja Naye. Nafsi zetu zinafarijiwa. Tunajisikia Roho Mtakatifu akijaza utu wetu wote kwa Roho Wake. Ni furaha isiyoweza kuelezeka. Mungu anazungumza NASI. Kila Neno lililonenwa kwenye kanda hizo, Yeye alinena kwa ajili yetu. Yeye anajua hasa kile ambacho tungehitaji kusikia na wakati ambao tuliyohitaji kulisikia… na mara nyingi tunahitaji kulisikia tena na tena…. na kila wakati HUFURIKA NAFSI ZETU.

Sisi hatuchoki kumsikia yeye akituambia kuhusu Maono, Ndoto, Bwana Asema Hivi, ng’ambo ya pazia, akituona sisi tumevaa nguo ndefu nyeupe, Mvuto wa Tatu, kuwaumba kindi, Ule Upanga wa Mungu uliyoenea mkononi mwake barabara, chakula kilichohifadhiwa, tukiwa tumewekwa kwa Mkuu wa Meza, Ngurumo, Malaika wenye nguvu wakija na kumtwaa juu, yule malaika wa saba wakipekee aliyemaanisha kitu cha zaidi kwake, ishara ya milele ya vilele saba vya milima vinavyoendeleza herufi BRANHAM, semeni tu hasa yale yaliyo kwenye kanda hizo, ninayo Maneno ya kutoweza kukosea, Yeye ameitiwa wito wa juu zaidi, nitawaambia UFUNUO WANGU, Mimi ni Sauti ya Mungu kwenu, shikilieni kabisa hayo mafundisho ya kanda, nitawaita BIBI-ARUSI, aiko, iyo, dafuta… sisi tunayapenda YOTE.

Hili ndilo ono langu. Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda ndio Mapenzi makamilifu ya Mungu, MWISHO WA MANENO. Kuzicheza kanda ndio Mapenzi makamilifu ya Mungu, MWISHO WA MANENO. Wewe unaweza kuwasikia wahubiri, waalimu, mitume, manabii, wachungaji, LAKINI kanda ndizo, na zinatakiwa kuwa, Sauti iliyo muhimu sana unayotakiwa kuisikia, MWISHO WA MANENO. Sauti iliyo kwenye kanda ndio Sauti pekee ambayo Mungu Mwenyewe aliyosema, MSIKIENI YEYE, MWISHO WA MANENO.

Ndugu na dada zangu, simpingi mtu ye yote, Mimi niko kwa ajili ya Sauti hiyo tu. Inatupasa, na mimi, nawapenda wote wanaotangaza kwamba wanapenda na kuamini Ujumbe huu. Hata kama mnajisikia kwamba ninawaambia watu vibaya kuwaambia kubonyeza play, Ninawapenda na ninaamini mnanipenda. Sote tunataka kuwa katika Mapenzi yake Makamilifu. Tafadhali endelea kufanya yale Mungu aliyokuitia kufanya; hubiri, fundisha, kuwa mchungaji, wewe liambie tu kundi lako ni Sauti gani iliyo muhimu sana wanayotakiwa kuisikia.

Ni Sauti hiyo tu iliyo kwenye kanda isemayo jambo lile lile KILA WAKATI. Haibadiliki kamwe. Bibi-arusi anaweza TU KUSEMA AMINA kwa kila Neno lililo kwenye kanda, lakini Bibi-arusi hawezi kusema AMINA kwa kila neno ambalo mwanadamu ye yote asemalo, MWISHO WA MANENO.

Kama huamini jambo hilo, wewe si Bibi-arusi. Ikiwa unaamini jambo hilo, basi hutakuwa na shida kuwaambia kundi lako kwamba kuzisikiliza kanda ndiyo Sauti iliyo muhimu zaidi wanayotakiwa kuisikia.

Kwa Mimi kutoa kauli hizi nimesikia kutoka kwa wahudumu wengi tofauti ambao wanasema kwamba ninawaambia watu wasiwasikilize wachungaji wao na kuyaacha makanisa yao, HIYO SI KWELI. Siwezi kusema jambo hilo na siamini jambo hilo.

Ni kweli wengi wanasema mambo ambayo sijawahi kamwe kusema, wala kuamini. Siwezi kuwajibishwa kwa ajili yao, lakini tu kwa yale niliyosema na yale ninayoamini. Nimezungumza waziwazi na kuyaweka katika mfumo wa barua yale ninayoamini. Wao / ninyi mnapindisha kwa manufaa yenu yale ninayosema /na ninayomaanisha.

Bibi-arusi wote watakuwa wakisema jambo lile lile. Hakuna watu wawili wasemao jambo lile lile. Sauti Moja. Nabii mmoja. Bibi-arusi Mmoja.

Mimi Siamini kwamba yakubidi kuusikia Ujumbe kwa wakati mmoja kabisa, kama wanavyofanya waamini wengi ulimwenguni kote, ili uwe Bibi-arusi Wake, lakini Naamini unapaswa kuisikia Sauti ya malaika-mjumbe wa saba Jumapili asubuhi…ipe hiyo sauti nafasi ya KWANZA.

Unaalikwa kusikiliza pamoja nasi: Muhuri wa Saba 63-0324E, Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) Wakati sehemu ya Bibi-arusi kutoka kote ulimwenguni watakaposikia Sauti hiyo kwa wakati mmoja kabisa.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Kusikiliza Ujumbe:

Kumbukumbu la Torati 29:16-19
1 Wafalme 12:25-30
Ezekieli 48:1-7, 23-29
Mathayo 24:31-32
Ufunuo 7 yote
Ufunuo 8:1
Ufunuo 10:1-7
Ufunuo 14 yote

23-0903 Maswali Na Majibu Juu Ya Mihuri

UJUME: 63-0324M Maswali Na Majibu Juu Ya Mihuri

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Ndugu Branham,

Ninaamini kwa moyo wangu wote wewe ndiye malaika-mjumbe wa Saba wa Mungu aliyetumwa kumwita Bibi-arusi Wake atoke. Wewe ni Sauti ya Mungu uliye na Bwana Asema Hivi kwa ulimwengu. Ninaamini wewe ndiye yule aliyemchagua kumfunulia siri zote za Biblia. Ninaamini kila Neno unalosema kwenye hizo kanda.

Nina swali moyoni mwangu ambalo ningependa kukuuliza. Kuna watu wengi sana, sauti nyingi sana, zinazosema mambo mengi tofauti kuhusu kile tunachopaswa kufanya ili kuwa Bibi-arusi wa Kristo. Ninataka kuwa katika Mapenzi yake makamilifu. Nataka kuwa na Imani kamilifu. Simpingi mtu yeyote, lakini nataka kusikia wewe unasemaje.

Ni kitu gani kitakachomkusanya Bibi-arusi pamoja na kutupa Imani ya kunyakuliwa tunayohitaji?

Nami naamini ya kwamba, kupitia Ngurumo hizo Saba, zitafunuliwa katika siku za mwisho ili kumkusanya Bibi-arusi pamoja kwa ajili ya kupata imani ya kunyakuliwa.

Ndugu Branham, Je, zile Ngurumo Saba ambazo ni sawa na siri saba zimekwisha kufunuliwa? Je, zilifunuliwa katika zile Muhuri Saba, ila bado hazijajulikana kwetu kama zile Ngurumo?

La, zilifunuliwa katika zile Muhuri Saba; hivyo ndivyo zile ngurumo zilivyokuwa. Ilibidi zifunue…Zile Ngurumo Saba zilizotoa sauti zao na hakuna ye yote angetambua ilikuwa nini…Yohana alijua zilikuwa nini, lakini yeye alikatazwa kuandika habari zake. Yeye alisema, “Bali yule malaika wa saba, katika siku za kupiga baragumu yake, zile siri saba za zile Ngurumo Saba zitafunuliwa.” Na yule malaika wa saba ndiye mjumbe wa ule Wakati wa Saba wa Kanisa.

Utukufu kwa Mungu. Hilo hapo jibu langu. Siri ya zile Ngurumo Saba imefunuliwa. Ni Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda na sasa inamuunganisha Bibi-arusi pamoja na kutupa ile IMANI YA KUNYAKULIWA, tunayohitaji.

Asante, Ndugu Branham, kwa kujibu swali langu. Nilijua kuwa jibu la swali nililokuwa nalo moyoni mwangu lingekuwa kwenye kanda.

Hayo ndiyo yote ninayohitaji kujua. Nitaendelea Kubonyeza Play kila siku na kupokea IMANI YA KUNYAKULIWA zaidi.

Njoo upokee Imani ya Kunyakuliwa pamoja nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) tunaposikia: Maswali na Majibu Juu ya Mihuri. 63-0324M.

Ndugu. Joseph Branham

23-0827 Muhuri Wa Sita

UJUME: 63-0323 Muhuri Wa Sita

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

Wapendwa Watu wa Nabii Wa Mungu,

Sikilizeni, nina jambo fulani tu la kuwaambia. Ni zuri sana, linanichoma tu ndani kabisa moyoni mwangu. Ninatumaini hamjalisahau, mnaona. Hebu niseme jambo hili, mbele Zake. Kwa neema Yake, Yeye aliniruhusu pia kuwaona WATU WANGU, si muda mrefu uliopita, wakiwa katika mavazi meupe.

Kutoka Pwani ya Mashariki hadi ya Magharibi, kote nchini, tunakusanyika pamoja. Tuko umbali wa saa mengi, Bali tuko pamoja kama watu wa Nabii wa Mungu. Sisi ni JAMII MOJA.

Wakati nabii wa Mungu alipokuwa hapa duniani, mahali pekee palipo pakuu sana, na mahali ambapo Bibi-arusi alitaka kuwa, ilikuwa ni kuungana pamoja kwenye mawasiliano ya simu, wakingojea kusikia sauti hiyo ikisema, “Habari za Asubuhi Marafiki.”

Jinsi gani wangependa kukaa katika umati huo kwenye kona ya barabara ya Nane na Penn. Wangefurahia kutumia usiku kucha kwenye maegesho ili tu kupata kiti, ama kuweza kusimama na kuegemea ukutani kwa masaa. Wangeuza vyote walivyokuwa navyo, wangepoteza kazi zao, kama ingebidi ili tu kuwa katika ibada hiyo moja.

Maisha yao yote yalikuwa yakitegemea kila Neno ambalo nabii alilonena. Hawakutaka kukosa kitu. Ingawa walijua ya kwamba siku moja wangeweza kupata kanda hiyo, walitaka kuungana na Bibi-arusi wakati ule ule Mungu alipokuwa akinena kupitia midomo ya mwanadamu.

Haya ndiyo yalikuwa maisha yao. Hili ndilo walilongojea kila wiki. Hakuna kilichokuwa cha maana zaidi kwao ila kusikia Ujumbe unaofuata. Jinsi gani walivyojaa furaha kwa kujua, SASA, walikuwa na nafasi ya kusikia wao wenyewe, wote kwa wakati mmoja, Neno kwa Neno, yale ambayo nabii malaika-mjumbe wa Mungu aliyosema.

Mungu alikuwa ameandaa njia. Alitaka Bibi-arusi Wake aungane pamoja kwenye Sauti Yake. Alitaka Bibi-arusi Wake aisikie Sauti Yake wote kwa wakati mmoja. Alijua Sauti Yake iliyonenwa kupitia malaika-mjumbe Wake ndiyo Sauti pekee ambayo ingemuunganisha Bibi-arusi Wake.

Mpango wake mkuu ulikuwa ukitendeka.

Wachungaji kutoka kote Marekani walihakikisha kwamba makanisa yao yameunganishwa kwa njia ya simu. Walikuwa wamelipata lile ono ya kwamba HAKUNA KITU kilicho muhimu zaidi kuliko kusikia Sauti Hiyo.

Hivyo ndivyo walivyokuwa wamefundisha makusanyiko yao. “Mungu amemtuma nabii akiwa na Bwana Asema Hivi. Amethibitishwa na Nguzo ya Moto. Hii ni Sauti ya Mungu kwenu. Hii ni Malaki 4, na Ufunuo 10:7. Yeye ndiye mtu aliyeitwa na Mungu kumwongoza Bibi-arusi Wake. Huyu ndiye nabii yule niliyewaambia habari zake zote. Sasa hatuna budi sote kumsikiliza. Kama vile Yohana wa kale, sina budi kupungua na yeye ataongezeka.

Mpango wa Mungu ungali bado unatimizwa. Bibi-arusi angali bado anaungana kwenye Sauti Yake. Lakini sasa tunaungana KUTOKA ULIMWENGUNI KOTE. Kila Jumapili, sehemu ya Bibi-arusi Wake wanangojea kwa matarajio makubwa kusikia kila Neno, wote kwa wakati mmoja.

Labda tumeusikia Ujumbe mara mia moja hapo kabla, lakini wakati huu unajisikia kana kwamba ni MARA YA KWANZA. Tunajua tutapata Ufunuo MKUBWA kuliko hapo awali.

Hakuna mahali pengine tunapotaka kuwa. Hakuna kitu kingine kilicho muhimu zaidi. Kwetu sisi, Hili ​​ndilo Lile. Huu ni mpango wa Mungu KWETU. Sauti hii inaita, inaunganisha na kumkamilisha Bibi-arusi Wake…NA SISI NDIO HUYO BIBI-ARUSI.

Ninawaalika kuungana nasi Jumapili hii, saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) tunapoungana KUSIKIA Sauti ya Mungu Anapotufunulia:   Muhuri wa Sita 63-0323.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikia Ujumbe:

Kutoka 10:21-23
Isaya 13:6-11
Danieli 12:1-3
Mathayo 24:1-30
Mathayo 27:45
Yohana 10:27
Ufunuo 6 yote
Ufunuo 11:3-6

23-0820 Muhuri Wa Tano

UJUME: 63-0322 Muhuri Wa Tano

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Neno Mkamilifu,

Mungu ametuma nguvu yake ya mwisho. Amemleta tai Wake mkuu ili aturudishe kwenye ile Imani ya asili ya baba zetu. Huu ni wakati wa tai. Hakuna Wanyama wengine tena. Hakuna wajumbe wengine tena. Hakuna kundi lingine la watu tena. Wamekwisha. Tuko mwisho. Sauti ya Ufunuo 10:7 imewasili Naye amemtumia nabii-tai wake mkuu kumwita Bibi-arusi Wake atoke.

Kama ungalimsikiliza mchungaji wetu Jumapili, yule tai mkuu wa Mungu, ungemsikia akikuambia kama alivyotuambia sisi:

“ Ninyi ndilo kundi lile ambalo litakalozichukua hizo Ngurumo Saba; Neno la Mungu mwenyewe, na kukata vipande-vipande na kukata na hata kuzifunga mbingu. Mnaweza kufunga hiki, ama kufanya vile, lo lote mnalotaka kufanya. Adui anauawa kwa Neno litokalo katika kinywa chenu, kwa maana ni kali kuliko upanga wenye makali kuwili. Mnaweza kuagiza tani bilioni mia moja za inzi kama mkitaka. Lo lote mtakalosema, litatukia, kwa maana ni Neno la Mungu likitoka katika kinywa cha Mungu. Ni Neno Lake, lakini daima Yeye hutumia mwanadamu kulifanyiza kazi.”

Ninawezaje kusisitiza vya kutosha umuhimu wa Kubonyeza Play; kumsikia yule tai aliyetumwa na Mungu? Ujumbe huu ni muhimu sana, mkamilifu sana…MKAMILIFU SANA, hivi kwamba hata hangeweza kuuweka mikononi mwa Malaika. Hapakuwa na mtu mwingine, hapakuwa na kundi lingine la watu, HAKUNA MTU YE YOTE Yeye angaliweza kumpa Hilo, ILA NABII-TAI WAKE MKUU.

Tunaweza kuzungumza kulihusu, kulifundisha, na hata kulihubiri, lakini kuna SAUTI MOJA PEKEE iliyo na “Bwana Asema Hivi,” nawe huna budi kuamini kila Neno. Kuna Sauti moja tu unayoweza kuweka kikomo chako cha milele kwake. Kuna SAUTI MOJA tu ambayo Mungu aliyoichagua kumwongoza Bibi-arusi Wake, na NI BIBI-ARUSI WAKE PEKE YAKE NDIYE ATAKAYEKUWA NA UFUNUO HUO.

Kulikuwa na nabii-tai mmoja tu aliyemchagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu kumfunulia NENO LAKE LOTE …WILLIAM MARRION BRANHAM, na yeye, na yeye peke yake, ndiye tai-mjumbe wa Mungu kwa ajili ya siku hii. Yeye, na yeye peke yake, ndiye aliyetumwa kumwongoza Bibi-arusi wa Mungu.

Wito wangu Mimi, ama wito wa wahudumu wo wote, ni jambo moja tu: KUWAONGOZENI NINYI KWAKE YEYE, YULE TAI MKUU WA MUNGU. Yule aliyemchagua. Yule aliyemthibitisha kwa Nguzo Yake ya Moto. Yule aliyemchagua wakati alipokifungua kile Kitabu, na kuivunja ile Mihuri, na kukituma duniani, ili akifunue kwetu sisi, Watu Wake.

Maneno hayo aliyosema kwenye kanda si maneno yake yeye, ni Mawazo hasa ya Mungu mwenyewe yaliyonenwa na kurekodiwa kwenye kanda ili Bibi-arusi Wake asikie; na ni WEWE tu, Bibi-arusi WAKE uliye na Ufunuo wa kweli wa jambo hilo.

Bibi-arusi, hebu fikiria jambo hilo! Tumewasili. Hakuna cha zaidi. Utafiti wa kisayansi umethibitisha jambo Hilo. Thibitisho la Neno limehakikisha jambo Hilo. Nasi tumewasili! Na Ufunuo huu unatoka kwa Mungu, nao ni Kweli. Na kwa sababu mnalitambua jambo Hilo, SISI NI wana na binti zake waliorejeshwa kikamilifu.

Hakuna kushangaa tena. Hakuna kujiuliza-uliza tena. SISI NI BIBI-ARUSI NENO WAKE MKAMILIFU. Tunajitambua sisi ni nani. Sisi ndio wale, kwa Neema ya Mungu, aliyomruhusu tai Wake kuwaona wote wakiwa wamevaa nguo ndefu nyeupe.

Jipe moyo Bibi-arusi. Tumekaribia. Tunaweza kuliihisi hilo. Ni halisi zaidi kwetu sasa kuliko hapo awali. Adui anatuchukia, LAKINI MUNGU ANATUPENDA. Si kwamba yeye yuko nasi tu, YUKO NDANI YETU. SISI NI NENO LAKE LILILOFANYIKA MWILI.

Yeye anamthibitishia Shetani, SISI HATUWEZI, NA HATUTASHINDWA. Kuna IMANI na shaka tu. Sisi tuna IMANI TU. Si katika sisi wenyewe, KATIKA NENO LAKE, NALO haliwezi kushindwa. Kwa nini? SISI NI NENO. Mungu alisema hivyo!!

Wewe hukumchagua Yeye, ALIKUCHAGUA WEWE. Shetani anawezaje kukufanyia lo lote, MUNGU ALIKUCHAGUA. Yeye alikuchagua wewe kwa sababu ALIJUA hungeshindwa kuamini Neno Lake. Shetani anakuambia, “lakini unashindwa, unashindwa, unashindwa”… uko sahihi, nashindwa katika mwili wangu, lakini NIMEHESABIWA HAKI, nami sitashindwa kuamini KILA NENO.

Tunapata kujaribiwa na kupitia mitihani kwa ajili ya MUNGU, ili apate KUMTHIBITISHIA, ADUI YAKE NA ADUI YETU… SISI NI BIBI-ARUSI NENO WAKE MKAMILIFU.

Roho Mtakatifu Mkuu na ajaze nyumba zenu, makanisa yenu, ama popote mlipo Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunapomsikia tai mkuu wa Mungu akileta Ufunuo kwa:  Muhuri wa Tano 63-0322.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Kusikiliza Ujumbe:

Danieli 9:20-27
Matendo 15:13-14
Warumi 11:25-26
Ufunuo 6:9-11 / 11:7-8 / 22:8-9

23-0813 Muhuri Wa Nne

UJUME: 63-0321 Muhuri Wa Nne

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wana Tai,

Sauti ya Mungu inatupaisha kwenye kilele ambacho hatujawahi kufika hapo awali, na kufunua Neno Lake. Tumeichimbia midomo yetu midogo ndani ya Mbawa Zake kuu anapotupeleka juu angani. Tunapaa juu zaidi ya anga zote zenye mawingu. Tunaweza kuona mbali sana katika umilele. Ni Ufunuo mpya kabisa kwetu. Kadiri anavyotupeleka juu zaidi, ndivyo inavyokuwa wazi zaidi. Tunapiga kelele: NALIONA…NALIONA.

Sasa amechukua Mabawa Yake yenye nguvu, akayatikisa sana na kutuambia, “RUKENI ENYI WANANGU, RUKENI. Mwanzoni tuliogopa sana. Yule adui alikuwa akizijaza akili zetu mashaka mengi sana. Siwezi, Siwezi kabisa. Kisha tukamsikia Yeye akitupazia sauti na kurudia kunguruma, “MNAWEZA, NYINYI NI WANA TAI WANGU, ANZENI TU KUYAPIGA MABAWA YENU!!”

Kisha, yote kwa pamoja mabawa yetu madogo kwa kawaida huanza kupiga-piga. Kadiri tunavyosikiliza Neno Lake hutuhakikishia sisi ni nani, na nini cha kufanya, na ndivyo mabawa yetu yanavyozidi kuwa na nguvu. Piga, piga, piga….Bonyeza Play, Bonyeza Play, Bonyeza Play …kisha ghafla, tunaruka. Sisi ni Tai.

Wakati Hofu kidogo inapojaribu kuingia niani mwetu, tuliangalia tu huku na kule na kuanza kusikiliza Sauti Yake. Huyo hapo, akiruka karibu nasi ili kutukamata ikiwa tutaanza kuanguka. Tunatambua hatuna cha kuogopa, Baba Tai yuko papo hapo pamoja nasi. Yeye anaangalia kila hatua tunayofanya. Hataruhusu chochote kitupate.

Uhuru na hakikisho jinsi hii ambao kiasi kwamba hatujawahi kuuhisi hapo awali. Yeye anaendelea kutuambia, Ninyi ni wana tai Wangu. Mnatii na kufanya kile hasa Nilichowaambia mfanye kwa kukaa na Sauti Yangu Niliyowaachia.

Yeye anajua anapotuambia jambo lo lote kwenye kanda, tutaenda kulifanya, kwa maana tunajua ni Neno Lake. Yeye atasimama moja kwa moja nyuma ya Jambo hilo. Hata kama halikuandikwa katika Biblia, Yeye ataliunga mkono, hata hivyo.

Tunajua, kama liko nje ya jambo hilo, Yeye atalifunua kwa nabii Wake. Tunatambua ya kwamba siri zote za Mungu zinajulishwa kwa nabii Wake, na yeye peke yake, kwa hiyo lo lote tunalohitaji kujua, Liko kwenye kanda.

Nena kuhusu nguvu za Ufunuo unaoleta changamko. Tunataka kupiga makelele kwa sauti zetu zote. Tunataka ulimwengu ujue, Mimi ni tai wa Kanda!

Mawazo ya Mungu yakawa uumbaji wakati yaliponenwa, kwa Neno. Hapo ndipo wakati anapoyaleta kwa—kwako kama wazo, wazo Lake, nalo linafunuliwa kwako. Halafu, lingali ni wazo mpaka wewe utakapolinena.

Imefunuliwa kwetu. Utukufu. Sasa tunataka kulinena. Sisi ni Bibi-arusi wa Yesu Kristo. Alinijua mimi, alinichagua tangu zamani kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Mimi ni Neno Lake lililo hai lililofanyika mwili. Aliniambia OMBA nawe utapokea. Bisha, utafunguliwa. Chochote tunachokihitaji, TUNAKINENA.

Huu ni Wakati wa Tai na sisi ndio Wana Tai Wake. Hatujawahi kuwa na furaha ama kuridhika zaidi katika maisha yetu. Bila hofu. Bila wasiwasi.

Ninakualika uje uruke umbali wa upeo mpya pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ), Wakati tai mwenye nguvu wa Mungu anapopaza sauti na kufunua Muhuri wa Nne 63-0321.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma ili kujitayarisha kusikia ujumbe wa Muhuri wa Nne 63-0321:

Mathayo Mt. sura ya 4 yote
Luka Mt. 24:49
Yohana Mt. 6:63
Matendo 2:38
Ufunuo 2:18-23, 6:7-8, 10:1-7, 12:13, 13:1-14, 16:12-16, 19:15-17
Mwanzo 1:1
Zaburi 16:8-11
2 Samweli 6:14
Yeremia sura 32 yote
Yoeli 2:28
Amosi 3:7
Malaki sura ya 4 yote

23-0806 Muhuri Wa Tatu

UJUMBE:63-0320 Muhuri Wa Tatu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi mwenye Changamko,

Jitayarisheni, Jumapili hii mtapata Changamko kwa Ufunuo zaidi kuliko ambavyo mmewahi kupata maishani mwenu. Mtakuwa mkilewa tu kwenye Neno. Itakuwa nzuri sana, na kusikika vizuri…na hata dhahiri zaidi kuliko wakati Alipoizungumza. Na kuna njia moja tu ya kulipata, yakubidi Ubonyeze Play!

Chukueni kanda, zisikilizeni kwa makini sana. Kwa sababu,
utalipata kwenye kanda, kwa sababu wamekuwa wakizicheza kanda hizo, na ni nzuri zinasikika vizuri. Kwa hiyo, mtalisikia vizuri zaidi humo.

Malaika-mjumbe wa saba wa Mungu ametoka kusema nini? Yule ambaye Mungu alimchagua kumfunulia siri zote za Biblia; yule aliyemchagua kutoa Ufunuo wa ile Mihuri Saba, zile Ngurumo, na Neno Lake lote. Malaika yule aliyemchagua kumwita Bibi-arusi Wake atoke. Yule aliyemchagua kuwa Sauti Yake katika siku za mwisho.

Hebu tusome tu nukuu hiyo kwa mara nyingine tena ili kuhakikisha kwamba tunaelewa kile alichotoka kusema kwamba tufanye.

“Utalipata kwenye”, WAPI?
“Utalisikia vizuri zaidi”, WAPI?

Nena kuhusu jinsi ilivyo muhimu Kubonyeza Play na kuzisikiliza Kanda. UTUKUFU!! Hili si neno langu, hili ni NENO la MUNGU akimwambia Bibi-arusi Wake, LIPATE HUMO…KWENYE KANDA. Enyi Wahubiri, ondokeni mgongoni kwangu.

Mtu ye yote anayedai kuwa anaamini Ujumbe huu anawezaje kusema kwamba kuzicheza kanda si jambo lililo KUU ZAIDI ambalo Bibi-arusi analotakiwa kufanya? mchungaji anawezaje kuweka huduma yake kuwa juu ya ile ya nabii? Sio tu kuinukuu….Ninafanya hivyo sasa hivi pia, bali kuicheza Sauti hiyo kwa kundi lake ili waweze “KULISIKIA VIZURI ZAIDI HUMO”.

Huduma iliyo kuu zaidi ulimwenguni ni Huduma ya Kanda. Hakuna kitu kilicho kikubwa zaidi kuliko Kubonyeza Play. Kuna Sauti moja tu ambayo imeamriwa na Mungu kuwa Bwana Asema Hivi kwa Bibi-arusi Wake, ni Sauti iliyo kwenye kanda.

Hebu niseme wazi kwa mara nyingine tena. Mimi SIPINGANI na mhudumu yeyote anayehubiri, wala sihisi mhudumu hawezi kuhubiri ama kufundisha. Lakini kwangu mimi na huduma yangu, nimeitwa kuuambia ulimwengu mzima kusikiliza Neno lililofanyika mwili, ambalo limerekodiwa na kuhifadhiwa kwenye kanda ya sumaku. Ninaamini ni Sauti ya Mungu, na ni HILO, na HILO peke yake, linalojibu maswali yako yote. Litakupa kila kitu unachohitaji, ikijumuisha na Imani ya Kunyakuliwa, kwa maana ni BWANA ASEMA HIVI.

Bibi-arusi hahitaji neno langu, ninanukuu tu Neno kama wahudumu wengine wote. Ninyi mnanukuu na kusema jinsi ilivyo muhimu kusikia huduma yenu na wito wenu, Bwana asifiwe. Mimi Ninawaambia watu huduma ILIYO MUHIMU ZAIDI ni Sauti ya Mungu iliyo kwenye Kanda. Hakuna kilicho kikuu zaidi yake. Wao Hawapaswi kuwa na kitu kingine chochote.

Sisemi mambo haya ili watu wawe na roho mbaya au mtazamo mbaya kwa mhudumu yeyote ama huduma yoyote, Mungu apishe mbali. Ninawapenda. Wao ni ndugu zangu. Mungu ameweka wito katika maisha yao. Je! nithubutu kunena dhidi ya watiwa mafuta wa Mungu, LAKINI nalazimika kunena na kusema kwamba wengi wameweka mkazo sana kwenye huduma YAO na hawakuiweka Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda kuwa ndiyo SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI ambayo Bibi-arusi anayotakiwa kuisikia.

Nilisema kwa urahisi, “Mrudisheni Ndugu Branham kwenye mimbara zenu,” na wengi wa wahudumu wamevalia njuga kuwaambia watu wao ati Ndugu Branham hakusema jambo hilo kwenye kanda, na HAO wameitwa kulichukua Neno na kuwapa watu; wanatoa visingizio vya KUTOCHEZA KANDA MAKANISANI MWAO.

Wanasema ni MAKOSA ikiwa mchungaji anacheza kanda kanisani mwao, wanawakosoa watu wanasema, ikiwa wanasikiliza tu kanda katika makanisa yao, na sio wahudumu, wao si Bibi-arusi.

Nimesikia visingizio vingi sana wanavyotumia na kuwaambia watu. Kamwe hawatawaambia watu wao, “KANDA NDILO JAMBO LILILO MUHIMU SANA MNALOPASWA NINYI KUSIKILIZA”. Kama wangefanya hivyo, basi hao watu wangeuliza… “basi kwa nini hatuzichezi kanda kanisani mwetu kama ndio muhimu ZAIDI?”

Huyu ndiye tutakayemsikiliza Jumapili:

Mungu alijidhihirisha katika Mwanadamu, na akatambua ni nani aliyekuwa nyuma Yake; na yale Sara aliyotenda, akicheka hemani. Na Maandiko haya yote, ya Malaki, na kadhalika, yaliyobashiriwa katika siku za mwisho. Waebrania 4 ilisema, wakati “Neno” litakaporudi. Malaki 4 ilisema Hilo lingerudi kwa njia ya mtu.

Neno hilo limerudi kwa njia ya mtu nasi tuna Sauti Yake imerekodiwa kwenye Kanda na Tutaisikia KILA JUMAPILI.

Ninayo furaha kutangaza kwamba kwa mara nyingine tena, Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) tutasikiliza Neno lililofanyika mwili na kurekodiwa kwenye kanda ya sumaku. Linatupa Ufunuo juu ya: Muhuri wa Tatu 63-0320.

Ni wakati uliyoje tutakaokuwa nao, Bibi-arusi. Ni furaha iliyoje itakayojaza mioyo yetu. Ni amani iliyoje itakayofariji nafsi zetu, tunaposikia yale ambayo Mungu Mwenyewe aliyomwambia Shetani: “Waache. Kama ukimshika mmoja wao, Wa Kondoo zangu waliojazwa na Mafuta Yangu na Divai ya Neno lililo safi, usiwalazimishe kusema ‘Salamu Maria’ yo yote, ama baadhi ya kanuni zako za imani. Usiwaguse. Wanajua wanakoenda, kwa maana wametiwa Mafuta Yangu na wana divai ya furaha, maana wanajua Neno Langu la ahadi. ‘Nitawafufua tena.’ Usidhuru Hao! Usiende ukajaribu kuwachafua…Usiwakaribie tu hata kidogo.”

Hatuna cha kuogopa. Tuna Neno. SISI NI NENO. Hatusimami kwa lolote. Sisi ni Wana na Binti za Mungu. Shetani, pisha njia, KILA kitu ni mali yetu. Mungu Alisema Hivyo. Imeandikwa!

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma kabla ya Kusikiliza Ujumbe:

Mathayo Mt 25:3-4
Yohana Mt 1:1, 1:14, 14:12, 17:17
Matendo Sura ya 2 yote
I Timotheo 3:16
Waebrania 4:12, 13:8
1 Yohana 5:7
Mambo ya Walawi 8:12
Yeremia Sura ya 32 yote
Yoeli 2:28
Zekaria 4:12

23-0730 Muhuri Wa Pili

UJUMBE: 63-0319 Muhuri Wa Pili

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa, Bibi-arusi

Bibi-arusi hashangai kuhusu Ujumbe huu wala mjumbe Wake tangu mwaka 1933, wakati Nguzo ya Moto ilipotokea kwenye Mto Ohio siku hiyo. Tumejua ya kwamba William Marrion Branham ndiye malaika-mjumbe wa 7 mwenye nguvu wa Mungu aliyemtuma duniani kumwita Bibi-arusi Wake atoke.

Tangu siku hiyo, Mungu amekuwa akimkusanya Bibi-arusi Wake pamoja kwa ajili ya Kuja Kwake. Tuko chini ya matarajio hayo makubwa; maana tunajua itakuwa tu siku yo yote sasa.

Yeye amekuwa akiijenga Imani yetu kuliko hapo awali, akituambia, akituhakikishia, sisi ni Bibi-arusi Wake mwaminifu. Tunajua kwa sisi kukaa na Chakula Chake Kilichohifadhiwa ghalani, cho chote tunachohitaji kipo HAPO, KWENYE KANDA.

Tunajuaje jambo hilo kwa uhakika? Neno linasema MUNGU hatafanya NENO LO LOTE mpaka atakapolifunua kwa watumishi wake manabii. Kwa hiyo tunajua ikiwa Mungu atatufunulia jambo lo lote, ama kufanya jambo lo lote, kutupa Imani ya kunyakuliwa, Yeye atalinguruma kupitia nabii wetu, na nabii Wake peke yake.

Siku za kujiuliza-uliza zimekwisha. Bibi-arusi amechukua msimamo. Hakuna jambo lililo muhimu zaidi kuliko kumsikia Mungu akinena na Bibi-arusi Wake kwenye Kanda. Ndiyo Maneno pekee yaliyothibitishwa na Mungu Mwenyewe kuwa Bwana Asema Hivi.

Muda umeenda sana nasi tunaweza kuhisi ule uzito wa pumzi chafu ya adui yetu kutuzunguka pande zote. Vita vimepamba moto naye Shetani anashambulia kila upande, lakini Mungu asifiwe tunacho Chakula cha Kiroho, nasi tunaketi kwenye Meza ya Bwana mchana na usiku, tukila hiyo Mana Iliyofichwa. Anaendelea kutufunulia zaidi na zaidi kila siku anapotuambia, “Yote yako sawa kipenzi. Nipo pamoja nawe. Nilikuambia sitakuacha kamwe wala sitakupungukia. Kazana. Wafukuze hao pepo. Ninakupa bomu Langu la atomiki, Neno Langu, litumie. Nililiwaza. Ndipo likaandikwa, na sasa, katika siku Yenu, Nimelinena ili upate kunisikia MIMI nikikuambia WEWE, Bwana Asema Hivi, Wewe ni Bibi-arusi Wangu. Wewe ni Neno lililofanyika mwili.”

Mungu amenena kupitia midomo ya mwanadamu na ametupa Neno lake; hatuna cha kuogopa. Si Neno letu, mawazo yetu, mitazamo yetu, Ni Neno la Mungu alilotupa SISI. IMANI yetu iko katika Neno lake nalo Neno lake haliwezi KUSHINDWA KAMWE!

Sasa, tunapoisikia Mihuri hii ikifunguliwa, Roho Mtakatifu anazungumza nasi kwa mara nyingine tena nasi tunaweza kuyaona majina yetu yameandikwa humo kwenye Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo. Hatuwezi kabisa kujizuia…NDIYO, ni jina langu lililoandikwa humo. Anazungumza kunihusu MIMI.

Njooni muungane nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( Ni saa 1 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) Na Kuusikia Muhuri wa Pili 63-0319, Wakati Sauti ya Mungu inapowaambia kuwa majina yenu yameandikwa katika Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Mathayo Mt 4:8 / 11:25-26 / 24:6
Marko 16:16
Yohana 14:12
2 Wathesalonike 2:3
Waebrania 4:12
Ufunuo 2:6 / 6:3-4 / Sura ya 17 / 19:11-16
Yoeli 2:25
Amosi 3:6-7

23-0723 Muhuri Wa Kwanza

UJUMBE: 63-0318 Muhuri Wa Kwanza

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa…Nitawaita Bibi-arusi,

Mungu, Muumba Mkuu, Alfa na Omega, Nyiroro ya mabondeni, Ua la Sharoni, Nyota yenye Kung’aa ya Asubuhi, Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu, Nguzo ya Moto, Mungu Mwenyewe, alikuja duniani na kunena nasi kupitia midomo ya mwanadamu, UTUKUFU!, Akaiweka kwenye kanda ya sumaku, ili Ninyi mweze kumsikia YEYE Akiwaita… “NINYI” BIBI-ARUSI WAKE.

Lioneni kwa picha dhairi jambo hili enyi marafiki. Bwana wetu Yesu Kristo, akiwatazama machoni na kuwaambia: “Ninyi ni Bibi-arusi Wangu. Nawapenda. Nimewangojea kwa muda mrefu sana. Kwangu Mimi, ninyi ni wakamilifu. Ninyi ni nyama ya nyama Yangu, mfupa wa mfupa Wangu. Niliwachagua ninyi kabla sijaumba Dunia au nyota. Nawapenda sana. Tutaishi Milele pamoja. Sasa, ninakuja kuwachukua.”

Hilo peke yake linapaswa kumpa kila mmoja wetu Imani ya Kunyakuliwa. Ni kitu gani ibilisi anaweza kuwarushia, kuwaambia, kukiweka juu yenu ambacho kinaweza kuwadhuru? HAKUNA CHOCHOTE, NINYI NI BIBI-ARUSI WA KRISTO! Ninyi ni Neno Lake lililofanyika mwili, ninyi ni Bibi-Yesu Kristo.

Anawezaje mtu yeyote, katika lugha yoyote, kuandika na kutuelezea nini maana yake? Huwezi kabisa.

Hakuna mahali popote duniani unapoweza kuwa na heshima na majaliwa hayo ya kusikia Maneno haya isipokuwa uwe na Ufunuo sahihi na UBONYEZE PLAY.

Yale matukio makuu zaidi ambayo ulimwengu umekuwa ukingojea tangu mwanzo wa wakati, yanatukia sasa hivi, nasi tu sehemu ya hilo. Yeye ameingojea siku hii, saa hii, watu hawa; NINYI, kuutimiza na kuutekeleza Mpango Wake Mkuu.

Ufunuo wa ile siri ya ile Mihuri Saba, zile Ngurumo zikifunuliwa, ukamilifu wetu, Adamu Wake aliyerejeshwa kikamilifu, Kuja Kwake, mambo haya yote yanadhihirishwa na yanatimia SASA HIVI, ndani YENU, BIBI-ARUSI WAKE!

Si katika siku za Musa. Si katika siku za Nuhu. Si katika siku za Yesu, Si hata katika siku za Yohana ama Paulo; Inatukia sasa, SASA HIVI, KWENU NINYI.

Hatutaki kulikosa. Tunataka kuwa tayari kwa ajili ya huku Kuja Kwake. Ili kufanya jambo hilo, tumeagizwa kwenda kwenye NENO kupata majibu yetu. Si wazo langu, ama wazo la mtu fulani ama mafikara yake, bali Yale Neno la Mungu lililothibitishwa linasemayo.

Tunajua Bibi-arusi yampasa kusema “amina” kwa kila Neno na kuungana pamoja kuwa Mmoja. Kwa hiyo ni lazima tuangalie katika Neno la Mungu ili tuone ni kitu gani kitakachomuunganisha Bibi-arusi pamoja.

Na ndipo kunakuja Ngurumo saba za siri ambazo hata hazijaandikwa kamwe. Hiyo ni kweli. Nami naamini ya kwamba, kupitia Ngurumo hizo Saba, zitafunuliwa katika siku za mwisho ili kumkusanya Bibi-arusi pamoja kwa ajili ya kupata imani ya kunyakuliwa.

Papo hapo liko katika Neno. Hizo Ngurumo Saba zitafunuliwa katika siku yetu ili kumkusanya Bibi-arusi pamoja kwa ajili ya kupata imani ya kunyakuliwa.

Kisha swali linalofuata tunalohitaji kujua ni: Je, hizo Ngurumo ni nini?

Wakati, ile “iliponguruma.” Kumbuka, sauti kuu ya kishindo cha Ngurumo ni Sauti ya Mungu. Hivyo ndivyo Biblia isemavyo, unaona, “kishindo cha Ngurumo.” Wao walidhani ilikuwa ni ngurumo, lakini ilikuwa ni Mungu. Yeye aliielewa, kwa maana ilifunuliwa Kwake. Unaona? Ilikuwa ni Ngurumo.

Kwa hiyo zile Ngurumo ni Sauti ya Mungu itakayomkusanya Bibi-arusi pamoja na kuwapa (SISI) imani ya Kunyakuliwa. Hilo hapo jibu letu.

Ni nani aliye Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi?
William Marrion Branham.

Sasa, mimi ni ndugu yenu tu, kwa neema ya Mungu, lakini pindi huyo Malaika wa Bwana anaposhuka, inakuwa, basi, Sauti ya Mungu kwenu…Mimi siwezi kusema neno lolote mwenyewe, ila kile Yeye anachonionyesha, Mimi Nakisema. Ninyi aminini jambo hilo na mwone kinachotokea.

Liaminini jambo hilo na mwone kile kitendekacho na kutukia Jumapili hii, tutakapokusanyika pamoja, kupokea imani ya kunyakuliwa, kumsikia Yeye Akinguruma kwa Bibi-arusi Wake.

Nena “kuhusu kuketi sasa katika ulimwengu wa Roho”? Itakuwaje! Kama tunaweza kujisikia hivi, hali tumeketi hapa duniani, kabla ya kuja kwa Kunyakuliwa, katika hali hii tuliyo nayo sasa; nasi tunaweza kufurahi, na tukisimama kando-kando ya kuta, na kusimama kwenye mvua, ili tu kusikia jambo Hili; itakuwaje tutakapomwona Yeye ameketi pale! Loo! jamani! Loo! utakuwa ni wakati wa fahari kweli.

Usikose katika wakati huu mtukufu. Umealikwa kukusanyika pamoja nasi tunaposikia: Muhuri wa Kwanza 63-0318, saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville.( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma Kwa Maandilizi ya Kusikiliza Ujumbe:

Mtakatifu Mathayo 10:1 / 11:1-14 / 24:6 / 28:19
Yohana 12:23-28
Matendo 2:38
2 Wathesalonike 2:3-12
Waebrania 4:12
Ufunuo 6:1-2 / 10:1-7 / 12:7-9 / 13:16 / 19:11-16
Malaki Sura ya 3 na ya 4
Danieli 8:23-25 ​​/ 11:21 / 9:25-27

23-0716 Pengo Kati Ya Nyakati Saba Za Kanisa Na Ile Mihuri Saba

UJUMBE: 63-0317e Pengo Kati Ya Nyakati Saba Za Kanisa Na Ile Mihuri Saba

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Yungiyungi dogo za Kidimbwi,

Tumejipenyeza hadi juu ya maji yenye matope na kutandaza mbawa zetu. Petali zetu ndogo zimetokeza na sasa linaakisi ua la Uwandani . Tumeweka maisha yetu kikamilifu kwa Mungu na Neno lake.

Tuko katika wakati wa mwisho tukitoka Mashariki na Magharibi, Kaskazini na Kusini, tukijiweka tayari kwa ajili ya huo Unyakuo. Tukijishikilia imara kwa dakika chache mpaka kila mshipa umejazwa na Roho Mtakatifu. Tunajiweka tayari KUPAA JUU.

Siku yenyewe imefika. Anawaita watu Wake pamoja Kwake katika umoja wa kweli na Yeye Mwenyewe. Ni Yesu Kristo akiishi pamoja na Roho wake katika mwili wetu, akifanya mambo yale yale aliyoyafanya kama bendera kwa ulimwengu.

Jambo lililo tukufu zaidi katika Maandiko linatendeka katika wakati wetu. tendo, ambalo hata Malaika, hakuna kitu, kingaliweza kufanya jambo hilo, ila Mwana-Kondoo. Alikuja na kukitwaa kile Kitabu kutoka katika mkono wa kuume wa Yeye aliyeketi juu ya kile Kiti cha Enzi, akakifungua, akaichana ile Mihuri, na kukituma duniani, kwa malaika Wake wa saba, atufunulie SISI, Bibi-arusi Wake.

Mambo yanayotukia; Neno analotufunulia kila siku, hayaelezeki. Tunapaza sauti zetu, na kupiga vifijo na vigelegele, Haleluya! Upako, nguvu, utukufu, dhihirisho, Ufunuo huu wa Neno Lake ni mkuu kuliko ulivyopata kuwa tangu mwanzo wa wakati.

Pamoja na kila kiumbe kilichoko mbinguni, na juu ya nchi, na chini ya nchi, ndani ya bahari, na vyote vilivyomo ndani yake, tunapaza sauti: Baraka, heshima, utukufu, uweza, ni kwake Yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi, na Mwanakondoo milele, amina! Amina, na amina!

Kila kiumbe, kila mtu tangu mwanzo wa wakati walingojea siku hii ifike. Hata Mungu Mwenyewe alingojea mpaka malaika Wake mteule alipofika duniani kabla ya Yeye kujitokeza kukitwaa kile Kitabu, kukifungua na kuzifunua siri Zake zote kwa Bibi-arusi Wake mteule.

Sasa tunajua yale ambayo hakuna mwanadamu duniani, tangu mwanzo wa wakati, amewahi kujua. Kila kitu kilichopotezwa katika lile anguko. Kila kitu ambacho kimefichwa katika Neno Lake. Kila kitu ambacho Bibi-arusi anachohitaji kimerekodiwa na kimewekwa katika ghala moja dogo la Mungu.

Ametuonyesha Kule ng’ambo ya pili ya pazia la Wakati nasi tunajiona wenyewe tukiwa pamoja Naye kule upande wa Pili. Bibi-arusi amejifanya tayari kwa kusikia Neno.

Tumekuwa katika mafunzo. Tumevaa silaha zote za Mungu. Hakuna kinachoweza kutuondosha. Hakuna kinachoweza kututisha. Hakuna kinachoweza kutudhuru. Hakuna kinachoweza kutufanya kupatana hata kwenye Neno moja. SISI NI NENO.

Tunamngojea huku tukiwa na shada letu la maua mikononi mwetu. Muda umefika. Ile Saa ya kale inayoyoma. Tunasikia farasi wakienda shoti, mchanga ukivingirishwa chini ya gurudumu. Lile gari la Kale la farasi liko karibu kusimama.

Atakapokuja tutaruka kutoka katika ulimwengu huu wa kale nakuangukia Mikononi mwake. Atatunyakua na kusema, “Nilikuwa nimekwenda kuwaandalia mahali, lakini yote yamekwisha sasa, mpenzi”.

Kuja Kwake kumekaribia sana. Tuko chini ya matarajio zaidi ya hapo kabla. Tunayo furaha sana kwa anavyotaka tuisikie ile Mihuri Saba kwa mara nyingine tena. Tunajua tutapokea Ufunuo zaidi, kwa sababu kila Ujumbe tunaousikia ni kana kwamba kamwe hatujawahi kuusikia hapo awali.

Kuishi leo hii na kusikia Ujumbe huu ni hata kuu zaidi kuliko wakati uliporekodiwa. Yeye Anatufunulia hata na zaidi sasa hivi. Ni kitu gani kingeweza kutokea?

Njoo ukusanyike pamoja nasi saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki),na Kufurahia kusikiliza:  
63-0317E Pengo Kati ya Nyakati Saba za Kanisa na Ile Mihuri Saba. Ni Chakula Kilichohifadhiwa alichokiandaa Bwana kwa ajili ya Bibi-arusi kula.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kwa maandalizi ya kusikiliza Ujumbe:

Mambo ya Walawi 25:47-55
Yeremia 32:1-15
Zekaria 3:8-9 / 4:10
Warumi 8:22-23
Waefeso 1:13-14 / 4:30
Ufunuo 1:12-18 / Sura ya 5 yote/ 10:1-7 / 11:18