22-0109 Hii Ndiyo Ishara Ya Mwisho, Bwana?

Ujume: 62-1230E Hii Ndiyo Ishara Ya Mwisho, Bwana?

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Hekalu la Mungu,

 Ujumbe huu hauna kikomo katika nguvu. Wenyewe Ni Mkamilifu ndani yake.  Ni Neno la mwisho juu ya mambo yote.  Hakuna kitu kingine kwa Bibi-arusi ila ile Sauti ambayo imerekodiwa kwenye kanda.  Ni Ujumbe wa Mungu uliothibitishwa wa wakati huu.  Ni Yakini yetu.

 Tuko safarini mwetu kuelekea Nchi ya Ahadi, tukiongozwa na Roho Mtakatifu, Nguzo ya Moto.  Chakula chetu cha Kiroho kimehifadhiwa ili kutuhifadhi  katika safari yetu.  Yote tunayohitaji yametolewa.

 Daudi alitayarisha kwa wingi kabla ya kifo chake vitu vyote vilivyohitajika ili kujenga nyumba ya Bwana .  Aliamuru kwamba lazima iwe ya ukuu kupindukia, ya umaarufu, na ya utukufu, katika nchi zote.

 Kisha akazungumza na Sulemani, na kumpa yote ambayo alikuwa ametayarisha kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu la Bwana.  Akampa mfano wa ukumbi, na nyumba zake, wa hazina, na vyumba vya juu, na vyumba vya ndani, na mahali pa kiti cha rehema.

 Akampa kielelezo cha vyote alivyokuwa navyo kwa roho, vya nyua za nyumba ya Bwana.  Vyumba vyote vilivyozunguka pande zote, hazina za nyumba ya Mungu, na hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.

 zamu za makuhani na Walawi, na kwa ajili ya kazi yote ya utumishi wa nyumba ya Bwana.  Pia akampa vyombo vyote vya utumishi katika nyumba ya Bwana .  Dhahabu na fedha kwa vyombo vyote vya huduma za kila namna.  Uzani wa dhahabu na fedha kwa kila kinara.  dhahabu na fedha kwa kila meza ya mikate ya wonyesho, ndoana, mabakuli, vikombe na mabakuli.

 kwa ajili ya madhabahu ya uvumba, dhahabu safi kwa uzani;  na dhahabu kwa mfano wa gari la makerubi, walionyosha mabawa yao, na kulifunika sanduku la agano la BWANA.

 Yote yalikuwa yametayarishwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya jengo hilo.  Hakukuwa na chochote kilichopungua.  Ni lazima afuate Ramani kwa usahihi  kulijenga Hekalu la Bwana.

 Lakini katika wakati wetu, Mungu anajenga Hekalu lingine, Bibi-arusi Wake.  Hekalu hili halitaharibiwa, bali litaishi Milele pamoja Naye.  Ametayarisha na kuhifadhi kwa wingi kwa kila kitu kinachohitajika ili kujenga Hekalu Lake jipya.

 Uungu, Uzao wa Nyoka, Majuma Sabini ya Danieli, Nyakati Saba za Kanisa, Mihuri Saba, Kutambua Siku Yako, Ndoa na Talaka, Kufunuliwa Kwa Mungu, Ile Ishara, Yakini, Watiwa-Mafuta, Chakula cha Kiroho, Kristo ni Siri, na mamia na mamia zaidi .  ambazo lazima zifuatwe kwa usahihi .

 Amehifadhi kila kitu tunachohitaji, lakini ni lazima tufuate Ramani kwa usahihi, bila kubadilisha yodi moja au nukta moja.

 Sasa, huku ni, jambo ninalonena asubuhi hii, ni kuhifadhi Chakula, kuhifadhi Chakula, ili kwamba mpate kitu cha kula, ili kwamba mpate kitu cha kufanyia karamu. Kiwekeni Hicho kwenye kanda zenu; mkaziweke katika chumba chenye baridi. Pengine wakati mrefu baada ya kuondoka kwangu, mngali mtakumbuka mambo haya ni kweli. Ketini chumbani mwenu mkazisikize. Mnaona? Na hiki ni Chakula, kihifadhini Hicho katika ghala.

 Alisema katika maskani huhisi kama nyumbani kwake kuliko mahali pengine popote.  Palikuwa ni Mahali ambapo Chakula kilihifadhiwa.

 Kule nje kwenye mikutano ninakoenda, hamnisikii nikihubiri Jumbe hizi. La, niliwaahidi, kuja kwenye Maskani hii. Papa hapa ndipo mimi huhubiria jumbe zangu. Nina tatu ama nne zaidi hapa, ambazo Bwana amenipa mimi, nina Maandiko juu yake, ambayo nisingethubutu kuhubiri mahali pengine po pote ila papa hapa. Hapa ndipo Neno la Mungu lilipoanzia. Na, hata Mungu atakapolibadili, ninakaa papa hapa na kuutoa papa hapa. Hiyo ni kweli.

 Nabii wa Bwana alinena na kusema kulikuwa na kundi la watu wanaomwamini, na walio na njaa na kushikilia kila neno alilosema. Ninyi ndilo kundi hilo la watu. Ninyi ndilo kusanyiko lake.  Ninyi ndilo hilo kundi lake dogo.

 Nimekuwa katika maombi na kuhisi Bwana anatuongoza kufuata Jumbe alizoziweka kwa wingi nabii Wake katika ghala Lake ili kumjenga Bibi-arusi Wake.

 Tutaendelea kumfuata nabii Wake tunaposikiliza:  Hii ​​Ndiyo Ishara ya Mwisho, Bwana?  62-1230E .  Ningependa kukualika uungane nasi Jumapili saa 4:00 nne Asubuhi ., saa za Jeffersonville,( ni saa 12:00 kumi na mbili jioni ya Tanzania), kusikia Chakula hiki kilichotayarishwa na kuhifadhiwa maalum ambacho kitakujenga ndani ya Hekalu la Bwana.

  “ Wakati umekwisha .” Kama ndivyo ilivyo, hebu na tujiandae, marafiki, kumlaki Mungu wetu. Kumekwisha wekwa chakula kingi sana sasa; hebu na tukitumie. Hebu na tukitumie sasa.

 Ndugu.  Joseph Branham