22-0130 Muhuri Wa Kwanza

Ujume: 63-0318 Muhuri Wa Kwanza

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Malkia wa Mbinguni,

MIMI , Mfalme wenu, nitanguruma kwenu NINYI siku ya Jumapili na kuwaambia NINYI , NINYI ndiyo Bibi-arusi Wangu. Nimewachagua NINYI kimbele. nimewakomboa NINYI. Nimewahesabia haki NINYI na Niliyaweka majina yenu kwenye Kitabu changu cha Uzima cha Mwana-Kondoo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. WEWE ni Malkia Wangu Kipenzi.

Nimewangojea na kuwangojea NINYI ili niweze kurejesha yote ambayo Adamu wangu wa kwanza alipoteza. Urithi wake wote ambao alipoteza. Ushirika wake wote na haki ya Uzima. Nilikuwa nimempa mamlaka makuu kamili juu ya dunia. Yeye Alikuwa mungu wa dunia nikiwa mimi ndiye Mungu wa ulimwengu wote.

Yeye alikuwa na mamlaka juu ya dunia hii. Angeweza kunena, aliweza kutoa majina, aliweza kusimamisha maumbile, aliweza kufanya lo lote alilotaka kufanya. Lakini alipoteza hayo Yote.

Sasa, kama nilivyokuahidi WEWE katika Neno Langu, Nimerudisha yote aliyopoteza na nimekurudishia WEWE. Yamekombolewa. Umilikaji halali wa yote yaliyopotezwa na Adamu sasa ni YAKO. Umilikaji wa halali wa hiyo hati-miliki ya kuwazika ya Uzima wa Milele, ambayo inamaanisha ya kwamba WEWE una kila kitu ambacho Adamu alikipoteza.

Nimekuwa aliye jamaa yako wa karibu. Nilidai kilicho Changu. Nilikitwaa kitabu cha ukombozi kutoka kwenye Mkono wa Baba Yangu, nikachana ile mihuri kutoka katika kitabu hicho na nikakituma kwa malaika-mjumbe wangu wa saba ili akufunulie WEWE. Atakurudishia WEWE Imani ya asili ya Biblia na atakufunulia WEWE siri Zangu zote.

Nimekuhakikishia na kukuthibitishia mambo haya kupitia Adamu Wangu wa kwanza aliyerejeshwa kikamilifu; Malaika wangu wa saba nabii-mjumbe. Angeweza kunena na kuwaumba kindi, kumrudishia samaki uhai , kudhibiti hali ya hewa na kuirudisha Tufani kule ilikotoka. Angeweza kunena na kuwafufua wafu. Hata nilipigwa picha YANGU pamoja naye ili kuonyesha ulimwengu, huyu ndiye Adamu Wangu wa kwanza aliyerejeshwa, msikieni yeye. Sasa WEWE, Malkia Wangu, una kila kitu ambacho Adamu alikipoteza.

Kumbuka, malaika-mjumbe wangu wa saba atakuwa duniani wakati wa Kuja Kwangu. Atakutambulisha KWANGU. Parapanda hiyo ya mwisho italia na waliokufa katika Kristo watafufuka. Wale walio hai na waliosalia watanyakuliwa pamoja nao, ili kunilaki hewani wakati ule ule malaika Wangu wa saba anapotoa Ujumbe wake. Muhuri wa mwisho unafunguliwa. Ile Parapanda ya mwisho italia; Nitakuja kudai mali yangu, WEWE, na ndipo nitakupeleka WEWE kwenye Karamu YETU ya Harusi.

Malkia wangu mpendwa, njoo unisikie Nikizungumza NAWE na kukufunulia kila kitu unachohitaji. Nimekuhifadhia WEWE Chakula hiki ili WEWE uwe Malkia Wangu. Nitazungumza na WEWE saa 6:00 Sita mchana, saa za Jeffersonville, ( ni Saa 2:00 Mbili Usiku Ya Tanzania), ambapo nitanguruma KWAKO Muhuri wa Kwanza 63-0318 .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma ili kujitayarisha kwa ajili ya kusikiliza Ujumbe:

Mathayo Mtakatifu10:1 / 11:1-14 / 24:6 / 28:19

Yohana Mtakatifu12:23-28

Matendo 2:38

2 Wathesalonike 2:3-12

Waebrania 4:12

Ufunuo 6:1-2 / 10:1-7 / 12: 7-9/ 13:16 / 19:11-16

Malaki Sura ya 3 yote na sura ya 4 yote

Danieli 8:23-25 ​​/ 11:21 / 9:25-27