Sasa hivi tunakula vile vitu vigumu vya Mungu na kuwa na ufahamu pevu wa Neno Lake. Mungu ametupa Ufunuo wa kweli wa Neno Lake. Ufahamu wetu wa kiroho haujavurugika.
Sisi TUNAJUA Yeye ni Nani hasa. TUNAJUA hasa kile Yeye alicho. TUNAJUA hasa wapi tunakoelekea. TUNAJUA hasa sisi ni nani. TUNAMJUA Yeye tunayemwamini na kusadiki kuwa Yeye aweza kukilinda kile tulichoweka amana kwake hata siku ile.
Yeye amenena na kutufunulia sisi siri zote zilizokuwa zimefichwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu. Alituambia jinsi ambavyo wengine daima wao wameikataa njia Yake iliyoandaliwa na kutamani uongozi tofauti, lakini Yeye angekuwa na kundi dogo ambalo litadumu waaminifu kwa Neno Lake.
Kote ulimwenguni, hawatakusanyika mahali pamoja na kuwa na vitu shirika. Lakini makundi madogo yatakuwa yametawanyika kote duniani.
Utukufu, tumetawanyika duniani kote, lakini Tumeungana kama Mmoja kwa Kubonyeza Play na kuisikiliza Sauti ya Mungu ikizungumza nasi.
Hebu na tuchunguze na tutangulie kuonja yale Yeye atakayokuwa akitueleza kupitia malaika Wake mwenye nguvu siku ya Jumapili.
Wapendwa Wangu waliochaguliwa, sasa mmeketi pamoja katika Mahali pa Mbinguni. Si popote pale, bali katika mahali pa “Mbinguni”; ndipo mahali pako kama mwaminio. Mmeomba vya kutosha nanyi mko tayari kwa Ujumbe. Mmekusanyika pamoja kama watakatifu, mliobatizwa na Roho Mtakatifu, mliojazwa na baraka za Mungu. Mmeitwa, mmeteuliwa, nazo roho zenu zimewaleta katika hali ya Kimbinguni.
Nini kingetokea. Roho Wangu Mtakatifu atakuwa akitembea katika kila moyo. Mmezaliwa upya na mmekuwa kiumbe kipya katika Kristo Yesu. Dhambi zenu zote ziko chini ya Damu. Mko katika ibada kamilifu, huku mikono na mioyo yenu imeinuliwa Kwangu Mimi, mkiniabudu MIMI pamoja katika mahali pa Mbinguni.
Ninyi mlichaguliwa kimbele, Mkateuliwa, katika kutangulia Kwangu Kujua. Mkachaguliwa, Mkatakaswa, mkahesabiwa Haki kwa Kukusudiwa Kimbele. Haiwezekani kwenu ninyi kudanganywa. Nimewakusudia kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Ninyi ni mungu mdogo, mliotiwa muhuri kwa Roho Mtakatifu wa ahadi; sio tu waliozaliwa katika familia, Wana na Binti Zangu wenye mamlaka.
Nitawabariki kwa uponyaji wa kiungu, kutangulia kujua, ufunuo, maono, nguvu, lugha, fasiri, hekima, maarifa, na baraka zote za Kimbinguni, kwa furaha isiyoneneka na iliyojawa na Utukufu.
Kila moyo utajazwa na Roho Wangu. Mtakuwa mkitembea pamoja, mkiketi pamoja, katika mahali pa mbinguni. Hakuna wazo moja baya kati yenu, hakuna hata sigara moja inayovutwa, hakuna nguo moja fupi, hakuna jambo hili, lile au lingine, hakuna wazo moja baya, hakuna aliye na neno dhidi ya mwingine, kila mtu akinena kwa upendo na upatanifu, kila mmoja katika moyo mmoja na mahali pamoja.
Ndipo kutakuja ghafla toka Mbinguni sauti kama upepo wa nguvu ukienda kasi Nami nitawabariki kwa baraka zote za rohoni. Ndipo mtakuwa kama vile Daudi, mkicheza mbele ya Sanduku, mkiuambia ulimwengu hamuonei haya, NINYI NI BIBI-ARUSI WANGU WA KANDA! Mnabonyeza play na mnaamini KILA NENO ninalosema. Ninyi hamta, na hamwezi kuondoshwa!
Wengine wanaweza kulikataa, au wasilielewe, lakini kwenu ninyi, Ni Beji yenu ya Heshima. Kama vile Daudi alivyomwambia mkewe; “Hivi Mnadhani hili lilikuwa ni kitu, ngojeni tu hadi kesho, tutakuwa tukisikiliza kanda hata na zaidi, tukimsifu Bwana, tukiwa tumejazwa na Roho Wake; kwa maana tunaishi Kanaani, tukielekea nchi ya ahadi.”
Kisha nitaangalia chini kutoka Mbinguni na kukuambia:
“Wewe ni Bibi-arusi aupendezaye moyo Wangu.”
Baraka hizi zinaweza kuwa zako pia. Njoo, uungane nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) na ujionee uwepo wa Bwana zaidi ya hapo awali tunapoisikiliza Sauti ya Mungu ya siku hii ikinena nasi na kutuletea Ujumbe: Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #1 60-0515E.
Kumbukeni, hili ni kwa ajili ya kanisa, si kwa mtu aliyeko nje. Kwake ni siri katika mafumbo kwake, hawezi kulielewa kamwe, linamshinda akili, hajui kitu hata kidogo juu yake. Bali, kwa kanisa, ni asali mwambani, ni furaha isiyotamkika, ni dhamana iliyobarikiwa, ni nanga ya nafsini, ni tumaini na tegemeo letu, ni Mwamba wenye Imara, loo, ni kila kilicho chema. Kwa kuwa mbingu na nchi zitapita, bali Neno la Mungu halitapita kamwe.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko ya kusoma kabla ya Ujumbe:
Yoeli 2:28 Waefeso 1:1-5 I Wakorintho 12:13 1 Petro 1:20 Ufunuo 17:8 Ufunuo 13
Rafiki zangu wapendwa, wapendwa wangu, wapenzi wangu wa Injili, watoto wangu niliomzalia Mungu.
Ni wikendi ya ajabu vipi tuliokuwa nayo pamoja na Bwana wetu. Haikuwa kama kitu kingine chochote, kutumia tu wakati pamoja Naye, kuzungumza Naye, kuisikia Sauti Yake, kumwabudu Yeye, kumshukuru, na kumwambia jinsi gani tunavyompenda.
Ni heshima iliyoje kuishi katika siku hii na kuwa sehemu ya Maandiko yanayotimia. Maneno ya kibinadamu yanawezaje kueleza yote yaliyo moyoni mwetu? Kama vile nabii alivyosema, Si mimi, kuna Kitu Fulani ndani kilindini, kikisukuma na kububujika ndani yangu; kisima kinachofoka maji ya Roho Mtakatifu. Ni Bibi-arusi akijifanya Mwenyewe tayari kwa ajili ya Bwana-arusi.
Jinsi gani bibi-arusi huchangamka kabla ya harusi yake. Moyo wake huanza kudunda kwa kasi sana wakati sekunde chache za mwisho zinapopita….anajua kuwa hatimaye wakati umefika. “Nimejiweka tayari. Anakuja kunichukua. Sasa tutakuwa MMOJA.”
Kwa kweli tunaishi katika nyakati za mwisho za kumalizia za wakati. Bibi-arusi hivi karibuni atanyakuliwa na kuitwa kwenye Karamu yetu ya fungate. Yeye anatupeleka kwenye viwango vipya. Hakuna swali tena; hakuna tena kushangaa; SISI NDIO BIBI-ARUSI.
Na bado Yeye hajamaliza. Bado Yeye anataka kumbariki na kumtia moyo Bibi-arusi Wake kipenzi aliyechaguliwa. Jinsi gani Yeye anavyopenda kumtia moyo na kumwambia jinsi gani Yeye anavyompenda. Jinsi anavyojivunia Yeye.
Yeye bado anao Ufunuo mwingine wa kipekee sana wa kumpa Bibi-arusi. Wakati kuna sauti nyingi sana ulimwenguni zinazokataa kucheza kanda, Yeye anataka tena kumhakikishia Bibi-arusi kwamba wako katika Mapenzi Yake makamilifu na Njia Yake iliyoandaliwa.
Mpango Wake daima umekataliwa. Bibi-arusi Wake daima ameteswa. Watu daima wanataka njia yao wenyewe, mawazo yao. Wanataka kiongozi tofauti awaongoze. Lakini Mungu alimtuma kiongozi MMOJA kumwongoza Bibi-arusi Wake, Yeye Mwenyewe, Roho Mtakatifu, na Roho Mtakatifu wa siku hii, kama ilivyo katika SIKU ZINGINE ZOTE, NI NABII WA MUNGU.
Siku zote wao wametaka watu wawaongoze. Katika siku za Samweli, Mungu alisema walikuwa wakimkataa Yeye kwa kutotaka Samweli awaongoze. Ilionekana kuwa jambo la ajabu kwa vile Samweli yeye pia alikuwa mtu, lakini tofauti ilikuwa Samweli alikuwa ndiye mtu ambaye Mungu alimchagua kuwaongoza. Haikuwa Samweli, Ilikuwa ni Mungu akimtumia Samweli. Yeye alikuwa ndiye SAUTI na MTU ambaye Mungu alimchagua KUWAONGOZA, lakini wao walitaka sauti zingine.
Sauli alijua watu walimcha Samweli, hivyo ilimbidi atangaze, “Sauli NA Samweli”. Ilibidi awaogopeshe watu ili wamfuate yeye. Kweli, alikuwa ameitwa. Kweli, alikuwa ametiwa mafuta na Samweli kuwa mfalme wao, lakini Mungu ANGALI alikuwa anayo Njia iliyoandaliwa, na nabii aliyemchagua Yeye kuwaongoza, hata kumwongoza na Sauli. Mungu alinena na nabii Wake na kumwambia Sauli la kufanya. Wakati Sauli alipoamua kuwa amepakwa mafuta yeye pia, na hakutaka kumsikia nabii tu, Mungu aliuondoa ufalme wake.
Kwa hiyo basi walipofanya jambo hilo, wakati kule kushindwa kukuu kulipokuja, ndipo Sauli alichinja maksai wawili wakubwa na kuwapeleka kwa watu wote. Na laiti mngaliona hapa. Wakati Sauli alipopeleka vipande vya yule maksai kwa Israeli wote na kusema, “Na iwe kwamba mtu ye yote ambaye hatamfuata Samweli na Sauli, na awe (huyu maksai) kama huyu.” Mnaona jinsi alivyojaribu kujiwakilisha kwa hila pamoja na mtu wa Mungu? Jinsi lilivyokuwa si la Kikristo. Uchaji wa watu ulikuwa kwa ajili ya Samweli. Bali Sauli akawafanya wote wamfuate kwa maana watu walimcha Samweli. “Na wamfuate Samweli na Sauli.”
Siku moja Sauli alifadhaika sana. Hakuweza kupata jibu kutoka kwa Mungu. Hakuweza kupata faraja. Alitaka majibu. Alijua ni wapi alipaswa kwenda ili kupata jibu alilotaka; palikuwa na mahali pa moja tu, NABII WA MUNGU, SAMWELI. Alikuwa amekwisha vuka ng’ambo, lakini bado yeye alikuwa angali ni SAUTI YA MUNGU, HATA KATIKA PARADISO.
Baba alitaka Bibi-arusi Wake ajue Yeye Alimchagua nani kumwongoza Bibi-arusi Wake katika siku hii ya mwisho, kwa hivyo Yeye Akamchukua malaika Wake mwenye nguvu kule ng’ambo ya pazia la wakati ili kwa mara nyingine tena atuambie, atufariji, na kututia moyo kwamba tuko katika Mapenzi Yake makamilifu na yaliyoandaliwa.
Yasikilize kwa makini sana YOTE anayosema nabii.
Sasa, nisingewataka ninyi mrudie jambo hili. Hili ni mbele ya kanisa langu, ama kondoo wangu ninaowachunga.
Kabla yeye hajatuambia lo lote, kwanza anatutaka tujue hili ni kwa ajili YETU PEKE YAKE, KANISA LAKE, KONDOO WAKE, WALE ANAOWACHUNGA. Kwa hivyo, kama huwezi kusema, “Ndugu Branham ni mchungaji WANGU,” nimesema jambo hilo hapo awali, lakini hakuna tu haja ya kulisoma zaidi, hili si kwa ajili yako, pamoja na kwamba yeye hakututaka hata tulirudie kwa ye yote yule ila kwa wale wanaoamini na kusema, “Ndugu Branham ni mchungaji wangu”.
Hilo papo hapo jibu letu kwa swali tunalopata shutuma nyingi sana kwa sisi kusema: “Ndugu Bramham ndiye mchungaji wetu.” (Hao ni wale watu wa kanda.) Wako sahihi, yeye yuko hivyo, nasi tuko hivyo.
Tafadhali msinikasirikie, mimi sisemi mambo haya ili kumkasirisha mtu ye yote, hilo lingekuwa kosa, bali ni yale Yeye anayomwambia Bibi-arusi. Mimi siweki fasiri yangu kwake, Yeye analisema wazi…Neno la Mungu halihitaji fasiri yo yote.
Ama ilikuwa kwamba nilikuwa katika mwili ama nje yake, ama ilikuwa kuhamishwa, Haikuwa kama ono lo lote nililopata kuona.
Sasa yeye anatuambia hili halikuwa kama ono lo lote alilopata kuona. Alikwenda mahali ambapo hajawahi kufika. Lilikuwa KUBWA kuliko ono lolote alilowahi kuona. Hakuwa akiota, aliuona mwili wake kitandani; ALIKUWEPO KULE.
Bibi-arusi wa Yesu Kristo, hebu hilo na lizame vizuri sana. Walikuwa ni Bibi-arusi wa Yesu Kristo kule ng’ambo ya pili, wa wakati uliopo, waliyokuja wakimkimbilia, wakipiga kelele na kumshika, wakimkumbatia na kusema, “Loo, ndugu yetu wathamani!”
Yeye alikuwa kule; aliweza kulihisi; aliweza kuwasikia. Walikuwa wakizungumza naye. Alisimama, na kutazama, alikuwa kijana. Akaangalia nyuma kwenye mwili wake mzee uliokuwa umelala pale mikono yake ikiwa nyuma ya kichwa chake.
Sasa tumethibitisha YEYE ALIKUWEPO KULE, na Ilikuwa ni Bibi-arusi wa Yesu Kristo aliyekuwa akimwona. Sasa hebu na tusikie kile ile sauti kutoka juu ilichokuwa ikimwambia.
Ndipo sauti hiyo iliyokuwa ikinena nami kutoka juu yangu, ikasema, “Unajua imeandikwa katika Biblia ya kwamba manabii walikusanywa pamoja na watu wao.”
Mungu hakuwa tu akimwonyesha na kumtia moyo nabii Wake, bali kulikuwa na mengi zaidi Kwenye jambo Hilo. Yeye angerudi na kutuambia sio tu wapi tunakoelekea na jinsi gani kungekuwa, bali kutuambia sisi tuko katika Mapenzi Yake makamilifu kwa Kubonyeza Play na hivyo ndivyo unavyofika mahali alipo Bibi-arusi.
Ndugu Branham alisema yeye alitaka kumwona Yesu vibaya sana. Lakini wakamwambia:
“Naam, Yuko juu kidogo tu, moja kwa moja upande ule.” Kasema, “Siku moja Yeye atakuja kwako.”
Wakaendelea kumwambia yeye ALIKUWA NANI.
“Wewe ulitumwa kuwa kiongozi na Mungu atakuja, na atakapokuja, Yeye atakuhukumu kulingana na yale uliyowafundisha, kwanza; kama wataingia ama hawataingia. Tutaingia kulingana na mafundisho yako.”
Ni nani aliyetumwa kama kiongozi? Tunaenda kuhukumiwa kulingana na yale nani aliyotufundisha? Tutaingia Mbinguni kulingana na mafundisho ya nani?
Mtu mmoja anaweza kusema, ninawafundisha watu wangu yale tu Ndugu Branham aliyosema…amina, unapaswa nami naamini baadhi wanafanya hivyo, lakini usilifanye “Ndugu Branham na Mimi”
Hebu tuendelee kusoma kwani Yeye anataka KUHAKIKISHA kwamba tunaelewa kwa uwazi zaidi.
Ndipo hao watu wakapiga kelele wakasema, “Tunajua jambo hilo, nasi tunajua tunarudi pamoja nawe siku moja duniani.” Kasema, “Yesu atakuja, nawe utahukumiwa kulingana na Neno ulilotuhubiria sisi.
Tutahukumiwa kwa Neno YEYE alilotuhubiria. Hivyo, hukumu inakuja kutokana na kile Sauti ya Mungu ilichosema kwenye kanda. Mtu yeyote anawezaje kusema ati hiyo Sauti iliyo kwenye kanda sio SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI mnayopaswa kuisikia?
“Halafu, kama ukikubalika wakati huo, ambapo utakubalika”
Je! Mko tayari. Hili litapigilia msumari kuhusu Mapenzi makamilifu ya Bwana ni yapi kwa Bibi-arusi wa Yesu Kristo. Bibi-arusi anamwambia nabii kile YEYE ATAKACHOFANYA. Si mtu mwingine. Sio kundi. Si mchungaji mwingine, nabii wa Mungu, WILLIAM MARRION BRANHAM.
“basi wewe utatukabidhi Kwake kama tunu yako ya huduma yako.”
Je! Ni nani atakayetukabidhi kwa Bwana Yesu? Je! Siku za kumsikiliza tu nabii zimekwisha? Je! Ndugu Branham hakuwahi kamwe kusema tucheze kanda?
Bibi-arusi anapiga kelele na kusema kama unataka kuwa Bibi-arusi ni bora Ubonyeze Play.
Bado haujashawishika? Vema, kuna hata na zaidi.
Kasema, “Utatuongoza Kwake na sote pamoja tutarudi duniani tukaishi milele.”
Ni nani wa kutuongoza Kwake? Ni nani anayemwongoza Bibi-arusi? Bibi-arusi anamwambia yeye kwamba YEYE ATAWAONGOZA BIBI-ARUSI KWAKE, kisha tutarudi duniani tukaishi milele.
Ikiwa kuna Ufunuo WOWOTE ndani yako hata kidogo. Ikiwa unadai unauamini Ujumbe Huu, ninaomba ya kwamba Mungu akufunulie ya kwamba ni LAZIMA uiweke Sauti Yake, kanda, kuwa ya KWANZA. Enyi Wachungaji, mrudisheni nabii kwenye mimbara zenu. Kanda ndio Sauti iliyo muhimu sana mnayopaswa kuisikia kwani mtaenda kuhukumiwa kwa SAUTI HIYO.
Kulingana na Neno, tuko katika Mapenzi Yake makamilifu na yaliyoandaliwa kwa ajili ya siku yetu kwa kusikiliza Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.
Ikiwa Mungu ameyafungua macho yako kwenye Ufunuo wa kweli wa Neno Lake, ninakualika uungane nasi Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tusikiapo 60-0515M Mfalme Aliyekataliwa.
Ni wakati mzuri sana jinsi gani ambao Bibi-arusi atakaokuwa nao Wikendi hii ya Pasaka. Naamini itakuwa moja ya mambo muhimu katika maisha yetu; wakati ambao hatutausahau kamwe. Wikendi kuu maalum.
Kila Pasaka imekuwa wakati ulio maalum kwa Bibi-arusi, tunapoufungia milango yetu ulimwengu wa nje kwa kuvizima vifaa vyetu vyote na vikengeusha-fikira vya kilimwengu, na kuyaweka tu wakfu upya maisha yetu Kwake. Ni wikendi nzima iliyowekwa wakfu kwa ajili Yake katika ibada, tunapozungumza Naye siku nzima kila siku, na kisha kulisikia Neno Lake.
Adui ameyafanya maisha yetu kukengeuka sana na kujaa shughuli za mambo mengi sana ya maisha hadi imekuwa vigumu sana kuufungia ulimwengu nje na kuongea Naye. Hata vifaa vile vile tunavyovitumia kusikia Neno, Shetani hutumia kuhatarisha wakati wetu.
Lakini wikendi hii itakuwa tofauti, na si kama wikendi nyingine ya Pasaka ambayo tumewahi kuwa nayo.
Wakati Bwana alipoweka moyoni mwangu kusikiliza ile Mihuri, sikujua jinsi gani tarehe zingeangukia. Lakini kama kawaida, wakati Wake ni mkamilifu. Jumapili mbili zilizopita, tulikuwa na majaliwa ya kuusikia Muhuri wa 4, Wakati wa Tai, tarehe 6 Aprili, siku ya kuzaliwa ya nabii; jinsi inavyofaa.
Lakini sasa, Bwana anayo hata na zaidi mengi aliyotuwekea sisi. Kama nilivyosema, nilipojisikia Bwana ameweka moyoni mwangu kuicheza Mihuri, nilijua ingechukua wiki kadhaa kumaliza kuicheza kwani kuna Jumbe 10 katika mfululizo huo.
Nilipoitazama kalenda, niliona kwamba Pasaka iliiangia kabla hatujamaliza kuusikia huu mfululizo mzima. Nikawaza mwenyewe, nadhani inatubidi tuache kuisikiliza ile Mihuri na Yeye atanipa Jumbe kwa ajili ya Pasaka.
Mara moja niliona… itakuwa KAMILIFU. Tunaweza kuendelea kuicheza Mihuri huku Muhuri wa Saba ukichezwa Asubuhi ya Jumapili ya Pasaka. Sikuweza kuamini, hilo liliendana kabisa na ratiba. Nilijua papo hapo, HUYU NI WEWE, BWANA.
Nimekuwa nimechangamshwa na nikiwa chini ya matarajio makubwa kwa ajili ya wakati wetu wa Pasaka pamoja na kila mmoja wetu, na pamoja Naye. Nilijua Yeye ametutengenezea ratiba.
Hivyo, ikiwa Bwana akipenda, tutaendelea kuisikiliza Mihuri katika kipindi chote cha Wikendi yetu ya kipekee ya Pasaka.
ALHAMISI
Ilikuwa ni Alhamisi usiku ambapo Bwana Yesu alishiriki Karamu ya Mwisho na wanafunzi Wake, katika ukumbusho wa Pasaka kabla ya kule kutoka kwa wana wa Israeli. Ni fursa iliyoje tuliyo nayo ya kufanya ushirika na Bwana majumbani mwetu, kabla ya wikendi yetu takatifu, na kumwomba atusamehe dhambi zetu, na atupe sisi sote kile tunachohitaji katika safari yetu.
Lijalie, Bwana. Waponye walio wagonjwa. Wafariji walio wachovu. Wape furaha wanaodhulumiwa. Wape amani walio wachovu, Chakula kwa wenye njaa, Maji kwa wenye kiu, furaha kwa wenye huzuni, uwezo kwa kanisa. Bwana, mlete Yesu miongoni mwetu usiku wa leo, tukiwa tunajitayarisha kushiriki ushirika unaowakilisha mwili Wake uliovunjwa-vunjwa. Tunaomba, Bwana, kwamba Yeye atatuzuru kwa njia ya ajabu sana…
Wabariki wengine, Bwana, kila mahali ulimwenguni, ambao wanangojea kwa furaha kuja kwa Bwana, taa zimetengenezwa, na dohani zimesuguliwa kabisa, na Nuru ya Injili ikiangaza katika sehemu zenye giza.
Hebu na tuanze sote saa 12:00 KUMI NA MBILI JIONI. kwa masaa ya nchi unayoishi ili kusikia Ushirika 62-0204, na kisha nabii atatupeleka katika ibada yetu maalum ya Ushirika na Kutawadhana Miguu, ambayo itakuwa ikicheza kwenye app ya Lifeline (kwa Kiingereza), au unaweza kuipakua ibada hiyo kwa Kiingereza au lugha nyinginezo kwa kubofya anuani iliyo hapa chini.
Tukiufuata Ujumbe, tutakusanyika pamoja na familia zetu majumbani mwetu na kuishiriki Meza ya Bwana.
IJUMAA
Hebu na twende kwenye maombi na familia zetu saa 3:00 TATU ASUBUHI(Ni saa 10:00 KUMI JIONI ya Afrika Mashariki)., na kisha tena saa 06:00 SITA MCHANA, (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tukimkaribisha Bwana awe pamoja nasi na azijaze nyumba zetu kwa Roho Mtakatifu tunapojiweka wakfu Kwake.
Mawazo yetu na yarudi huko nyuma hadi kwenye siku ile pale Kalvari, yapata miaka 2000 iliyopita, na kumwona Mwokozi wetu akining’inia msalabani, na kisha tujitoe vivyo hivyo kufanya daima yale yanayompendeza Baba:
Iwapo siku hii ni muhimu sana, moja ya siku zilizo kuu sana, hebu na tuangalie mambo matatu ambayo siku hiyo ilimaanisha kwetu. Tungechukua mamia. Bali asubuhi ya leo nimechagua tu mambo matatu tofauti yaliyo muhimu sana ambayo tunataka kuyachunguza katika muda mfupi ujao; ambayo Kalvari ilimaanisha kwetu. Nami naomba ya kwamba itamhukumu kila mwenye dhambi aliyeko, ya kwamba itamfanya kila mtakatifu kupiga magoti yake, ya kwamba itamfanya kila mgonjwa ainue imani yake kwa Mungu na aondoke ameponywa, kila mwenye dhambi aokolewe, kila aliyerudi nyuma arudi na ajionee aibu, na kila mtakatifu afurahi na apate tumaini jipya na tumaini jipya.
Kisha saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA,(Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) Hebu na tuungane pamoja majumbani mwetu kusikia: 63-0323 Muhuri wa Sita.
Kisha tuungane pamoja katika maombi mara baada ya ibada, katika ukumbusho wa kusulubiwa kwa Bwana wetu.
JUMAMOSI
Tuungane tena sote katika maombi Saa 3:00 TATU ASUBUHI (Ni saa 10:00 KUMI JIONI ya Afrika Mashariki) na saa 6:00 Saa SITA MCHANA,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) na kuitayarisha mioyo yetu kwa ajili ya mambo makuu Yeye atakayotufanyia miongoni mwetu.
Ninaweza kumsikia akisema, “Shetani, njoo hapa!” Yeye ni Bosi sasa. Ananyosha mkono, anaunyakua ule ufunguo wa mauti na kuzimu kutoka ubavuni mwake, akauning’iniza ubavuni Mwake Mwenyewe. “Ninataka kukupa notisi. Umekuwa laghai muda mrefu kutosha. Mimi ni Mwana wa Mungu aliye hai niliyezaliwa na bikira. Damu Yangu ingali imelowa msalabani, na deni kamili limelipwa! Huna haki tena. Umenyang’anywa zote. Nipe funguo hizo!”
Kisha saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, sote tutakusanyika pamoja kulisikia NENO: 63-0324m Maswali na Majibu Juu ya Mihuri.
Hii itakuwa SIKU ILIYO MAALUM jinsi gani kwa Bibi-arusi Wake ulimwenguni kote.
Kisha tuungane pamoja katika maombi mara baada ya ibada.
JUMAPILI
Hebu kwanza na tuamke mapema kama vile Ndugu Branham alivyofanya asubuhi wakati rafiki yake mdogo, robin, alipomwamsha saa 11:00 ASUBUHI.. Hebu na tumshukuru tu Bwana kwa kumfufua Yesu kutoka kwa wafu:
Saa kumi na moja asubuhi ya leo, maskini rafiki yangu mwenye kifua chekundu aliruka dirishani akaniamsha. Ilionekana kana kwamba moyo wake mdogo ungepasuka, akisema, “Amefufuka.”
Saa 3:00 TATU ASUBUHI (Ni saa 10:00 KUMI JIONI ya Afrika Mashariki) na saa 6:00 Saa SITA MCHANA,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tuungane kwa mara nyingine tena katika mnyororo wetu wa maombi, tuombeane na kujitayarisha kuisikia Sauti ya Mungu.
Saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, (Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) tutakusanyika pamoja kuusikia Ujumbe wetu wa Pasaka: 63-0324e Muhuri wa Saba.
Saa 9:00 TISA ALASIRI, Hebu na tuungane tena katika maombi, tumshukuru Yeye kwa Ajili ya WIKENDI YA AJABU ALIOTUPATIA KUWA PAMOJA NAYE NA PAMOJA NA BIBI-ARUSI WAKE ULIMWENGUNI KOTE.
Kwa ndugu na dada zangu walio nchi za ng’ambo, kama vile mwaka jana, ningependa kuwaalika kuungana nasi kwa masaa ya Jeffersonville, katika nyakati zote za maombi kwenye ratiba hii. Ninatambua, hata hivyo, kwamba kuzicheza Kanda Alhamisi, Ijumaa, na Jumamosi alasiri kwa masaa ya Jeffersonville ingekuwa vigumu sana kwa wengi wenu, kwa hivyo tafadhali jisikieni huru kuzicheza Jumbe hizo katika masaa yanayowafaa. Ningependa, hata hivyo, tuungane pamoja sote Jumapili saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) ili kuusikia Ujumbe wetu wa Jumapili pamoja.
Ningependa pia kukualika wewe na watoto wako kushiriki vipindi vya Creations, Journaling, na maswali ya YF, ambayo familia yako yote inaweza kufurahia pamoja. Tunafikiri mtayapenda kwa kuwa yote yanalenga NENO tutakalosikiliza wikendi hii.
Kwa ratiba ya wikendi, taarifa ya kuhusu jinsi ya kujiandaa na ibada ya Ushirika, nyenzo zitakazohitajika kwa ajili ya vipindi vya Creations, Maswali ya Pasaka, na taarifa nyinginezo, tazama anuani zilizopo hapa chini.
Hebu na tuzifunge simu zetu kwa ajili ya wikendi ya Pasaka isipokuwa kupiga picha, kusikia Nukuu ya Siku, na kucheza kanda kwenye app ya the Table, app ya Lifeline, au anuani inayoweza kupakuliwa.
Ni heshima kubwa kwangu kukualika wewe na familia yako kukusanyika pamoja na Bibi-arusi kote ulimwenguni kwa ajili ya wikendi iliyosheheni IBADA, SIFA NA UPONYAJI. Ninaamini kweli ni wikendi ambayo itayabadilisha maisha yako milele.
Tumewasili. Tumefika. Kule Kuthibitishwa kwa Neno kumethibitisha ya kwamba Ufunuo wetu wa Ujumbe Huu unatoka kwa Mungu. Tuko katika MAPENZI Yake MAKAMILIFU kwa kudumu na Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.
Kubonyeza Play ni muhimu jinsi gani? Maneno tunayosikia kwenye kanda ni muhimu sana, matakatifu sana, hivi Mungu Mwenyewe hata asingeweza kumwamini kumpa hayo Malaika…hata kwa mmoja wa Malaika Wake wa Mbinguni. Ilibidi yafunuliwe na kuletwa kwa Bibi-arusi Wake na nabii Wake, kwa maana huyo ndiye Neno la Mungu humjia, nabii Wake, PEKE YAKE.
Mungu aliichana ile Mihuri, akaikabidhi kwa malaika-mjumbe Wake wa saba wa duniani, na kumfunulia Kitabu chote cha Ufunuo. Kisha, Mungu akanena kupitia malaika Wake wa duniani na kufunua KILA KITU kwa Bibi-arusi Wake.
Kila maelezo madogo yamenenwa na kufunuliwa kwetu. Mungu ametujali sana hivi kwamba Yeye hakutuambia tu mambo ambayo yametukia hapa duniani tangu mwanzo wa wakati, bali alinena kupitia malaika Wake na kutuambia mambo yanayoendelea katika mahali kama paradiso sasa hivi.
Yeye hakutaka tuhangaike, ama tusiwe na hakika juu ya kile wakati ujao unachoshikilia kwa ajili yetu wakati tuiachapo maskani hii ya kidunia. Kwa hiyo, Mungu Mwenyewe alimchukua malaika Wake wa saba mwenye nguvu ng’ambo ya pazia la wakati, kusudi aweze kuliona, kulihisi, hata azungumze nao kule ng’ambo. Haikuwa ono, alikuwepo KULE.
Mungu alimpeleka huko ili yeye aweze kurudi na kutuambia: “Nilikuwa huko, nililiona. Linatukia SASA HIVI… Mama zetu, baba zetu, kaka zetu, dada zetu, wanetu, mabinti zetu, wake, waume, babu, Musa, Eliya, WATAKATIFU WOTE ambao waliotangulia huko wamevalia mavazi meupe, wakipumzika na wakitungojea SISI”.
Hatutalia tena, maana Itakuwa ni furaha tupu. Hatutakuwa na huzuni tena, maana itakuwa furaha tupu. Hatutakufa kamwe, maana yote ni Uzima mtupu. Hatuwezi kuzeeka, maana sote tutakuwa vijana milele.
Ni ukamilifu…kuongeza ukamilifu…kuongeza ukamilifu, nasi tunakwenda huko!! Na kama vile Musa, hatutaacha hata ukwato, SOTE TUNAKWENDA…FAMILIA YETU YOTE.
Ni muhimu jinsi gani KUMPENDA huyo malaika wa saba mwenye nguvu?
Nayo ikalia, ikasema, “Vyote ulivyowahi kupenda…” thawabu ya huduma yangu. Sihitaji thawabu yo yote. Akasema,“Vyote ulivyowahi kupenda, na wote waliowahi kukupenda,Mungu amekupa.”
Hebu tulisome hilo tena tafadhali: Amesema nini?….Mungu amekupa WEWE!!
Nasi tutaungana nao na kupaza sauti, “Tunategemea Jambo Hilo”
Tumekitegemeza kikomo chetu cha milele juu ya nini? KILA NENO LILILONENWA KWENYE KANDA. Ninamshukuru sana Bwana kuwa ametupa Ufunuo wa Kweli kwamba Kubonyeza Play ndilo jambo lililo MUHIMU SANA ambalo Bibi-arusi analopaswa kufanya.
Je! ungependa kupumzika pamoja nasi? Njoo uungane nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia yote yahusuyo wakati ujao unachoshikilia, wapi tunakoenda, na jinsi ya kufika huko, tunaposikia Sauti ya Mungu ikinena na kuufungua: Muhuri Wa Tano 63-0322.
Baba anatukusanya pamoja kwa Neno Lake, na kule kuthibitishwa kwa Ufunuo huo kunatupa changamko. Yeye alituchagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, kwa maana Yeye alijua tungekuwa waaminifu kwa Neno Lake kwa uchaguzi wetu wenyewe.
Hebu niliseme hilo tena ili liweze kuzama ndani kabisa. Yeye Alitazama kote katika wakati, hadi mwisho kabisa wa nyakati zote, na KUTUONA SISI… hivi unalisikia hilo? ALIKUONA WEWE, ALINIONA MIMI, na akatupenda, kwa sababu kwa uchaguzi wetu wenyewe, sisi tungedumu NA NENO LAKE.
Wakati huohuo, huenda aliwaita pamoja malaika Zake wote na makerubi na kutuelekezea sisi kidole na kusema: “HUYO NDIYE MWANAMKE MWENYEWE,” “HUYO NDIYE BIBI-ARUSI WANGU,” “HAO NDIO AMBAO NIMEKUWA NIKIWASUBIRI!”
Kama vile Yohana, hiyo ndiyo sababu tunapiga makelele haya yote na kupaza sauti, na kumsifu Bwana, tumechangamshwa na Divai Mpya na tunajua, BILA SHAKA HATA CHEMBE, SISI NI Bibi-arusi Wake.
Ni kama mvua na mvua za ngurumo zote ambazo tumekuwa nazo hapa Jeffersonville wiki hii…Sisi pia tunatuma ONYO kwa ulimwengu.
Bibi-arusi anapokea MVUA YA NGURUMO YA UFUNUO, NAYO INATOA MAFURIKO YA UFUNUO. BIBI-ARUSI AMEJIWEKA TAYARI NAO WAMEJITAMBUA WAO NI NANI. NENDA MAHALI SALAMA UPESI. BONYEZA PLAY AMA UANGAMIE.
Hatuishi katika wakati wa Simba, au wakati wa Ndama, wala Wakati wa Mwanadamu; tunaishi katika WAKATI WA TAI, Naye Mungu ametutumia tai mwenye nguvu, Malaki 4, kumwita Bibi-arusi Wake atoke na kumwongoza.
Litakuwa jambo lenye manufaa jinsi gani Jumapili hii, tutakapokuwa tumeungana pamoja tukiusikiliza Muhuri wa Nne. Itakuwa ni Siku ya Kuzaliwa ya nabii-tai mwenye nguvu wa Mungu.
Hebu na tuisherehekee siku hii ya ajabu na tumshukuru Bwana kwa kututumia mjumbe-tai Wake, ambaye aliyemtuma kutuita tutoke na kilifunua Neno Lake.
Ndugu. Joseph Branham
Ujumbe: Muhuri wa Nne 63-0321
Muda: saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)
Hebu niianze barua yangu leo na bomu la atomiki la Mungu; si bunduki aina ya 22, BOMU LA ATOMIKI kwa Bibi-arusi wa Yesu Kristo.
Sasa, kama unataka kuandika mambo hayo; bila shaka, nyote mnayajua: Yesu, Yohana 14:12; na Yoeli, Yoeli 2:38; Paulo, Timotheo wa Pili 3; Malaki, mlango wa 4; na Yohana mfunuzi, Ufunuo 10, kumi na saba, moja hadi kumi na saba. Unaona, ni vile vile ambavyo ingetukia sasa!
Notisi na onyo: Nukuu ifuatayo si kwa ajili yako ikiwa wewe unaamini.
“Tunamwelezea sana nabii wa Mungu.” “Huwezi kuwa Bibi-arusi ikiwa tu unamsikiliza nabii.” “Kuzicheza kanda kanisani ni kosa.” “Mwenge umepitishwa; jambo lililo muhimu zaidi leo ni kuwasikiliza wahudumu.” “Kubonyeza play wote kwa wakati mmoja ni dhehebu.”
Kwa kanisa, ni Kitu gani? Neno lililofanyika mwili likifanywa mwili miongoni mwa watu Wake tena! Unaona?
KABUUM…Kwa hivyo kwa kubonyeza play, tunaweza kulisikia Neno lililofanyika mwili, likinena nasi mdomo kwa sikio anapolifunua Neno Lake.
Na mtu fulani anaweza kusema ati Sio SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI UNAYOPASWA KUISIKIA? Sehemu hii ya nukuu ni kwa ajili yako.
Nao hawaliamini Hilo kamwe.
Kadiri Bwana anavyozidi kutupa sisi Ufunuo zaidi wa Neno Lake, na sisi ni nani, ndivyo kila mtu aliye nje ya Ufunuo huo anavyozidi kuwa mbali zaidi.
Hebu niseme jambo hilo, vizuri hasa, ili mninii… litadidimia ndani sana. Ninataka hili lilipatie hasa. Hiyo ndiyo shida yenu leo, mnaona, hamlijui Neno! Mnaona?
Mungu anao watu waliotiwa mafuta kuhubiri Ujumbe Huu, lakini kuna Yakini moja tu: Neno. Unapomsikia mhudumu, au mtu ye yote akinena, ni lazima uwe na imani ya kuamini kuwa anachokisema ndicho HASA ambacho nabii wa Mungu alichokwisha sema. Neno lao, ufunuo wao, fasiri yao inaweza kushindwa; Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda HAIWEZI KUSHINDWA KAMWE.
Nena kuhusu Mungu katika urahisi kwa kubonyeza play…Yeye analisema TENA.
Wanapitwa Naye, Neno lililo hai lililodhihirishwa katika mwili, kwa Neno lililoahidiwa. Neno liliahidi kufanya mambo haya. Ahadi ilifanywa, ya kwamba itakuwa hivi katika siku za mwisho.
Sikiliza Ngurumo Yake. Ngurumo ni Sauti ya Mungu. William Marrion Branham ndiye Sauti ya Mungu kwa kizazi hiki.
Bi-Bibi arusi hajawa na uamsho bado. Mnaona? Hakujakuwako na uamsho humo, hakujakuwako na madhihirisho ya Mungu kumwamsha Bibi-arusi bado. Mnaona? Tunautarajia huo sasa. Itahitaji hizo Ngurumo Saba zisizojulikana kule nyuma, kumwamsha Yeye tena, unaona. Naam. Yeye atazituma. Aliliahidi. Sasa angalia.
Unaweza kulipindisha hilo ukipenda, lakini zile Ngurumo Saba zitampa Bibi-arusi changamko kwa Ufunuo na imani ya kunyakuliwa, ambayo huja tu kwa Roho Mtakatifu akizungumza kupitia nabii wa Mungu. Hilo linatendeka SASA HIVI ulimwenguni kote. Mungu amemchangamsha Bibi-arusi Wake na Neno Lake.
Si hivyo tu, bali tayari Yeye amekwisha mwambia adui yetu la kufanya.
Usiwaguse. Wao wanajua wanakoenda, kwa maana wametiwa Mafuta Yangu. Na kwa kutiwa kwa Mafuta Yangu, wao wana divai ya furaha, maana wanajua Neno Langu la ahadi, ‘Nitawafufua tena.’ Usidhuru Hao! Usiende ukajaribu kuwachafua.
Yeye amemwambia adui yetu aiondoe mikono yake michafu mbali nasi. Lakini je! ugonjwa bado ungali unaweza kutushambulia? Ndiyo. Je! bado tungali tunayo matatizo? Ndiyo. Lakini Yeye pia alituambia la kufanya.
Ni la kilindi. Lisome polepole na mara tena na tena.
Kabla ya kuwa Neno, ni wazo. Nalo wazo halina budi kuumbwa. Vema. Kwa hiyo, mawazo ya Mungu yakawa uumbaji wakati yaliponenwa, kwa Neno. Hapo ndipo wakati anapoyaleta kwa—kwako kama wazo, wazo Lake, nalo linafunuliwa kwako. Halafu, lingali ni wazo mpaka wewe utakapolinena.
Mawazo Yake yakawa uumbaji wakati yaliponenwa. Kisha, mawazo Yake yaliletwa na kufunuliwa kwetu kama Neno. Sasa lingali ni wazo kwetu mpaka tutakapolinena. KWA HIYO TUNAYANENA… NA KUYAAMINI.
Mimi ni Uzao wa Kifalme wa Ibrahimu. Mimi ni Bibi-arusi wa Kristo. Niliteuliwa na kuchaguliwa tangu zamani kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu kuwa Bibi-arusi Wake, na hakuna kitu kinachoweza kulibadili hilo. Kila ahadi katika Biblia ni yangu. Ni Neno Lake kwangu. Mimi ni mrithi wa Ahadi yenyewe. Yeye ndiye Bwana Mungu aniponyaye magonjwa yangu yote. Chochote ninachokihitaji ni changu, Mungu alisema hivyo.
Mungu katika Urahisi: Imani huja kwa kusikia, kulisikia Neno. Neno huja kwa nabii.
Kila mtu anataka kuzitumia “NUKUU” kuthibitisha mawazo yao, mafikara yao, ujumbe wao. Nao wako sahihi, nafanya vivyo hivyo na mimi, ndio maana yote niwapayo ni nukuu za kuwaambia: Dumuni na Kanda. Isikilizeni hiyo Sauti. Sauti hiyo ni Sauti ya Mungu. Hamna budi kuamini kila Neno lililo kwenye Kanda, si yale mtu mwingine yeyote asemayo. Hiyo Sauti NDIO SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI MNAYOPASWA KUISIKIA.
Wengine huzitumia nukuu kuwaleta ninyi kwenye huduma yao, kwenye kanisa lao, kwenye fasiri zao, ufunuo wao. “Dumuni na mchungaji wenu.” (Vema, ninaipenda hiyo pia, kwa sababu sisi tunadumu naye, ila tu mchungaji tofauti.) “Yeye siye changarawe pekee ufukoni.” “Yeye hakusema kamwe kuzicheza kanda kanisani.”
Usiweke fasiri yo yote ya kibinafsi Kwake. Yeye anataka Neno lililo safi, lisiloghoshiwa, hata ubembe wo wote usiwepo. Singetaka mke wangu afanye ubembe na mwanamume mwingine. Na unapoanza kusikiliza hoja za namna yo yote, zaidi ya Hilo, unasikiliza, unafanya ubembe na Shetani. Amina! Hilo halikufanyi ujisikie kubarikiwa? Mungu anakutaka ubakie msafi kabisa. Udumu daima hapo na Neno hilo. Dumu Nalo. Vema.
Mimi na nyumba yangu, tutabonyeza play na kulifuata Neno la Mungu lililofanyika Mwili linenalo kupitia malaika-mjumbe Wake wa saba. Hatutaongeza fasiri yetu ya kibinafsi Kwake; hatutabembana au kusikiliza hoja yoyote. TUTADUMU NA NENO HILO KAMA LILIVYONENWA KWENYE KANDA. Ni Mungu katika Urahisi.
Ni wakati mtukufu jinsi gani tutakaokuwa nao Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) Tusikiapo: Muhuri Wa Tatu 63-0320. Ningependa kuwaalika mje mkaungane nasi tunapoungana katika Neno la leo.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:
Mathayo mt. 25:3-4 Yohana Mt. 1:1, 1:14, 14:12, 17:17 Matendo Sura ya 2 I Timotheo 3:16 Waebrania 4:12, 13:8 1 Yohana 5:7 Mambo ya Walawi 8:12 Yeremia Sura ya 32 Yoeli 2:28 Zekaria 4:12
Hebu nichukue fursa hii kuliweka wazi kwa mara nyingine tena. Mimi sipingani na huduma tano. Ninaamini katika huduma tano. Sioni ni vibaya kumsikiliza mhudumu. Naamini unapaswa kumsikiliza mchungaji wako pale ambapo Mungu amekuweka. Nisemalo ni kwamba, Ninaamini Mungu alimtuma nabii katika siku yetu. Mungu alilifunua Neno Lake kwa nabii Wake. Mimi naweza kukosea, mchungaji wako anaweza kukosea, lakini LAZIMA tukubaliane (tukisema tunauamini UJUMBE HUU ni kweli na Ndugu Branham ni nabii wa Mungu) yale yaliyosemwa kwenye kanda ni Bwana Asema Hivi. Kama huamini hilo, basi wewe huamini Ujumbe huu. Hivyo, Mimi ninaamini ndio SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI UNAYOPASWA KUISIKIA. Huhitaji kunisikia mimi, huhitaji kumsikia mtu mwingine yeyote, lakini LAZIMA UISIKIE SAUTI HIYO ILIYO KWENYE KANDA.
Swali: Je! tuko katika Mapenzi Yake makamilifu kwa kuzicheza Kanda? Jibu: NDIYO.
Swali: Je! Bibi-arusi anahitaji zaidi ya yale yaliyosemwa kwenye Kanda? Jibu: HAPANA.
Swali: Je! tunakosa kitu kwa sisi kusikiliza Kanda TU? Jibu: HAPANA.
Swali: Je! tunaweza kuwa Bibi-arusi kwa kusikiliza Kanda TU? Jibu: NDIYO, KWA MSISITIZO ZAIDI!
Sasa kumbukeni, “Hakuna lo lote linaloweza kufunuliwa; Mungu hatafanya neno lo lote, hata kidogo, mpaka kwanza alifunue kwa watumishi Wake, manabii.”
Hivyo, YOTE tunayohitaji yamekwisha nenwa na yako kwenye kanda; au, wakati malaika Wake wa saba atakaporudi duniani, YEYE atatuambia basi.
Loo! Bibi-arusi, hebu na tuwazie kile kinachotendeka miongoni mwa Bibi-arusi wa Kristo ulimwenguni kote. Baba anamkusanya Bibi-arusi Wake pamoja kwa Sauti Yake Naye Ananguruma, “Bwana Asema Hivi.”
Kumbukeni, alituambia zile Ngurumo zilikuwa kitu gani: “sauti kuu ya kishindo cha Ngurumo ni Sauti ya Mungu”. Nayo Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi ni nini? Malaika-mjumbe wa saba wa Mungu, William Marrion Branham.
Yeye alisema kunakuja Ngurumo saba za siri ambazo hata hazijaandikwa kamwe. Na ya kwamba kupitia Ngurumo hizo Saba, zitamkusanya Bibi-arusi pamoja kwa ajili ya kupata imani ya kunyakuliwa.
Neno la Bwana huwajia manabii Wake. Kama angekuwa na utaratibu bora zaidi, angeliutumia. Yeye alichagua utaratibu bora zaidi ya wote hapo mwanzo Naye hawezi, na hatabadilika.
Kwa hiyo, Sauti ya Mungu, inayonena kupitia malaika Wake wa saba, inamkusanya Bibi-arusi Wake pamoja na kutupa Imani ya Kunyakuliwa.
Kanisa halijashangaa tangu mwaka wa 1933, kule chini mtoni siku ile, ya kwamba William Marrion Branham ndiye Sauti ya Mungu, Inayonguruma, “Bwana Asema Hivi,” naye alitumwa kumwita, kumkusanya, na kumwongoza Bibi-arusi.
Ningependa kuwaalika mje msikilize pamoja nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) wakati Bwana wetu Yesu anapokifungua kile Kitabu, kuuvunja huo Muhuri, na kuutuma duniani, kwa malaika Wake wa saba, atufunulie huo SISI!
Ndugu. Joseph Branham
Tarehe: Jumapili, 23 Machi, 2025
Ujumbe: Muhuri wa Pili 63-0319
Muda: Saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)