Category Archives: Uncategorized

25-0810 Matukio Ya Sasa Yanadhihirishwa Na Unabii

UJUMBE: 65-1206 Matukio Ya Sasa Yanadhihirishwa Na Unabii

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Kweli na Aliye Hai,

Wakati Yesu, Neno Mwenyewe, alipokuja duniani miaka 2000 iliyopita, Yeye alikuja kama vile alivyosema angekuja, kama Nabii. Neno Lake linatangaza, ya kwamba kabla Yeye hajaja tena, kule kudhihirishwa kukamilifu kwa Utu wa Yesu Kristo kutadhihirishwa tena katika mwili, katika nabii. Nabii huyo amekuja, jina lake ni William Marrion Branham.

Mtu yeyote anawezaje kutotambua kwamba kuisikiliza Sauti ya Mungu ikizungumza nao moja kwa moja kwenye kanda ndiyo Mapenzi makamilifu ya Mungu? Tunajua Neno daima humjia nabii Wake; Haliwezi kuja kwa njia nyingine yoyote. Halina budi kuja kupitia njia ya Mungu ambayo Yeye alitutabiria. Hiyo ndiyo njia pekee litakavyopata kuja. Mungu anasonga mbele moja kwa moja jinsi Yeye alivyoahidi angefanya. Yeye kamwe hakosi kufanya kwa njia ile ile Yeye aliyofanya daima.

Kila mmoja wao alikula kitu kile kile, wote walicheza katika Roho, wote walikuwa na kila kitu shirika; bali ilipofikia wakati wa utengano, Neno lilitenganisha. Ndivyo ilivyo siku hizi! Neno lilitenganisha! Wakati utakapowadia…

Tunauona wakati huo unatukia sasa hivi, Neno linatenganisha. Bibi-arusi anashutumiwa kwa kumwinua sana nabii wakati wao wanaposema, “Kuna wengine walioitwa na Mungu, watu waliojazwa na Roho Mtakatifu wa kumwongoza Bibi-arusi leo. Mnahitaji zaidi ya hizo kanda tu. Mungu amewaweka watu leo kuliongoza kanisa.”

“Unajaribu kuwazia wewe ndiwe uliye peke yako kwenye kundi lile. Kusanyiko lote ni takatifu!” Mungu kamwe hajawahi kushughulika jinsi hiyo. Alipaswa kuwa amejua vyema kuliko hivyo. Naye akasema, “Vema, kusanyiko lote ni takatifu. Unajaribu kujifanya…” Kama tungalilisema siku hizi, maneno ya mtaani, “Changarawe pekee ufukoni.”

Naye Musa alijua ya kwamba Mungu alikuwa amemtuma huko chini kwa ajili ya jambo hilo.

Mungu anao watu waliojazwa na Roho Mtakatifu wa kumwongoza Bibi-arusi Wake; kuwaongoza KWENYE BWANA ASEMA HIVI, NABII-MJUMBE. Kwani Ujumbe na mjumbe ni kitu kimoja. Hiyo ndiyo njia ya Mungu isiyobadilika kamwe kwa ajili ya siku hii, na daima.

Kwa sababu walisikiliza kosa fulani. Wakati Musa, aliyethibitishwa na Mungu, na kiongozi wa kuwaonyesha njia ya kwenda kwenye nchi ya ahadi, nao walikuwa wamekuja umbali huo vema, lakini basi wasingeendelea pamoja naye… Sasa, waaminio wanaweza kuona jambo hilo, bali wasioamini hawawezi kuliona Hilo limethibitishwa.

Sio tu kwamba wewe ulichaguliwa kuupokea Ufunuo huu mkuu wa wakati wa mwisho wa siku hii, bali Mungu, kwa njia ya Chakula Chake kilichohifadhiwa cha kanda, hunena katikati ya mistari na Bibi-arusi Wake kipenzi.

Ndipo endapo wewe ni mwana wa Mungu ama binti ya Mungu, ulikuwa ndani ya Mungu wakati wote. Lakini Yeye alijua utapandwa kwenye tuta gani na katika wakati gani. Kwa hiyo sasa umefanywa kiumbe, mwana wa Mungu, mwana ama binti ya Mungu aliyedhihirishwa upate kukabiliana na changamoto ya wakati huu kumthibitisha Mungu wa kweli na aliye hai wa wakati huu, Ujumbe unaotokea katika wakati huu. Hiyo ni kweli! Ulikuwapo pale kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Ni barua ya mahaba ilioje ya katikati ya mistari kwa Bibi-arusi Wake, UTUKUFU!!! Sio tu kwamba Yeye alitujua na kutuchagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, bali hapa Yeye anatuambia kwamba alituchagua sisi tuwe wana na binti zake waliodhihirishwa wa SIKU HII. Alituweka hapa duniani leo, juu ya watakatifu wengine wote tangu mwanzo, kwa maana Alijua sisi tungekabiliana na changamoto ya wakati huu kumthibitisha Mungu wa kweli na aliye hai wa wakati huu, Ujumbe unaotokea katika wakati huu.

Sisi tulikuwa ndani ya Mungu, jeni, neno, sifa tangu mwanzo, lakini SASA tunaketi PAMOJA katika ulimwengu wa roho katika Kristo Yesu, tukishiriki pamoja Naye kwa Neno Lake, kupitia Neno Lake; kwa kuwa sisi ni NENO LAKE, nalo linazilisha nafsi zetu.

Hatuwezi, na hatutaingiza Kitu chochote maishani mwetu ila Neno la Mungu lisiloghoshiwa. Tunatambua na kuamini kuwa Ndio njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku hii.

Tungependa muungane nasi Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapoisikia SAUTI PEKEE, Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda, unayoweza kusema AMINA kwayo, kwa kila Neno unalosikia.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: Matukio Ya Sasa Yanadhihirishwa Na Unabii 65-1206

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Mwanzo 22
Kumbukumbu la Torati 18:15
Zaburi 16:10 / 22:1 / 22:18 / 22:7-8 / 35:11
Isaya 7:14 / 9:6 / 35:7 / 50:6 / 53:9 / 53:12 / 40:3
Amosi 3:7
Zekaria 11:12 / 13:7 / 14:7
Malaki 3:1 / 4:5-6
Mathayo 4:4 / 24:24 / 11:1-19
Luka 17:22-30 / 24:13–27
Waebrania 13:8 / 1:1
Yohana 1:1
Ufunuo 3:14-21 / 10:7

25-0803 Mambo Yatakayokuwapo

UJUMBE: 65-1205 Mambo Yatakayokuwapo

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Sifa za Mungu,

Kila Neno lililonenwa katika Ujumbe huu ni barua ya mahaba kwa Bibi-arusi Wake. Kuwazia kwamba Baba yetu wa Mbinguni Yeye anatupenda sana, si tu kwamba Yeye alitaka tulisome Neno Lake, bali Alitaka tuisikie Sauti Yake ikizungumza na mioyo yetu ili aweze kutuambia: “Wewe ndiye usia Wangu ulio hai, sifa Yangu iliyo hai, ambayo ninaweza kuionyesha kwa ulimwengu.”

Kisha kuwazia kwamba baada ya dhabihu zake zote alizotoa hapa duniani, maisha aliyoishi, njia aliyofuata. Aliomba jambo moja:

“Ili nilipo Mimi, nao wawepo.” Yeye aliomba ushirika wetu. Hicho ndicho kitu pekee alichomwomba Baba katika maombi, ushirika wenu milele.

Nilipo Mimi, “Neno Lake,” hatuna budi kuwapo pia, kupokea ushirika Wake, ushirika Wake, milele. Kwa hiyo, ni lazima tuishi kwa kila Neno Yeye alilonena nasi kwenye kanda ili tuwe Bibi-arusi Neno Bikira Wake, ambalo linatufanya kuwa sehemu ya Bwana-arusi.

Huo ndio UFUNUO wa Yesu Kristo katika wakati huu. Si vile Yeye alivyokuwa katika wakati mwingine, Yeye ni nani SASA HIVI. Neno la siku hii. Mungu yuko wapi leo. Huo ndio Ufunuo wa siku hii. Sasa unakua katika Bibi-arusi, ukitufanya kufikia kimo kikamilifu cha wana na binti.

Tunajiona wenyewe katika Neno Lake. Tunajua sisi ni nani. Tunajua tuko katika mpango Wake. Hii ndiyo Njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku hii. Tunajua Unyakuo umekaribia. Hivi karibuni wapendwa wetu wataonekana. Kisha tutajua: Tumewasili. Sote tunaenda Mbinguni…ndiyo, Mbinguni, mahali halisi tu kama hapa.

Tunaenda mahali halisi ambapo tutafanya mambo, ambapo tutaenda kuishi. Tutafanya kazi. Tutapafurahia. Tutaishi. Tunaenda kwenye Maisha, kwenye Maisha halisi ya Milele. Tunaenda Mbinguni, paradiso. Kama tu vile Adamu na Hawa walivyoshughulika, na kuishi, na kula, na kufurahia, katika bustani ya Edeni kabla dhambi haijaingia, tuko njiani tukirudi moja kwa moja kule tena, moja kwa moja, kurudi moja kwa moja. Adamu wa kwanza, kwa njia ya dhambi, alitutoa. Adamu wa Pili, kwa njia ya haki, anaturudisha kutuingiza ndani tena; anatuhesabia haki na kuturudisha ndani.

Mtu yeyote anawezaje kuliweka katika maneno Kile jambo hili linachomaanisha kwetu sisi? Uhalisia kwamba tunakwenda kwenye paradiso ambapo tunaishi katika umilele wote pamoja. Hakuna huzuni tena, maumivu au kilio, ni ukamilifu tu juu ya ukamilifu.

Mioyo yetu inafurahi, roho zetu zinawaka moto ndani yetu. Shetani anazidi kutupa presha kila siku, lakini bado tunafurahi. Kwa nini:

• TUNAJUA, SISI NI NANI.
• TUNAJUA, HATUJA, NA HATUTA, MWANGUSHA YEYE.
• TUNAJUA, TUKO KATIKA MAPENZI YAKE MAKAMILIFU.
• TUNAJUA, YEYE AMETUPA UFUNUO WA KWELI WA NENO LAKE.

Ndugu Joseph, unaandika jambo lile lile kila wiki. UTUKUFU, nitaliandika kila wiki kwa sababu Yeye anakutaka ujue jinsi gani anavyokupenda. Wewe ni nani. Ni wapi unakokwenda. Hasi inakuwa chanya. Wewe ni Neno ukifanyika Neno.

Mpendwa ulimwengu, njooni muungane nasi Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville, (ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) kwenye mawasiliano ya simu, si kwa sababu “Mimi” ninawaalika, bali kwa sababu “YEYE” anawaalika. Si kwa sababu “Mimi” niliichagua kanda, bali kulisikia Neno pamoja na sehemu ya Bibi-arusi ulimwenguni kote kwa wakati mmoja.

Je! tunaweza kutambua kwamba inawezekana kwa Bibi-arusi kuisikia Sauti ya Mungu ulimwenguni kote, wote kwa wakati ule ule hasa? Huyo hana budi kuwa ni Mungu. Mungu alimfanya nabii afanye hivyo wakati ule malaika Wake alipokuwa hapa duniani. Yeye alimuhimiza Bibi-arusi kuungana katika maombi, WOTE KWA WAKATI ULE ULE WA JEFFERSONVILLE, saa 3:00, 6;00, 9:00; hilo ni kuu jinsi gani sasa hivi, kwamba Bibi-arusi anaweza kuungana kama KITU KIMOJA kuisikia Sauti ya Mungu ikinena nao wote kwa wakati mmoja?

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: Mambo Yatakayokuwapo 65-1205

Maandiko:

Mathayo 22:1-14
Yohana 14:1-7
Waebrania 7:1-10

25-0727 Unyakuo

UJUMBE: 65-1204 Unyakuo

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Bila Masharti,

Bwana alitupa wakati mzuri sana kambini wiki iliyopita alipotufunulia Neno Lake. Alithibitisha, kwa Neno Lake, ya kwamba Yakini yetu ni: Neno Lake, Ujumbe Huu, Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda; wote ni mmoja, Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. 

Tulisikia jinsi ambavyo shetani anavyojaribu kuutenganisha Ujumbe kutoka kwa mjumbe, lakini Bwana Yesu asifiwe, Mungu Mwenyewe alinena kupitia malaika Wake Mwenye nguvu na kutuambia:

Tunaona ya kwamba mtu anapokuja, ametumwa kutoka kwa Mungu, amechaguliwa na Mungu, akiwa na BWANA ASEMA HIVI ya kweli, ujumbe huo na mjumbe huyo ni mmoja na kitu kimoja. Kwa sababu yeye ametumwa kuwakilisha BWANA ASEMA HIVI, Neno kwa Neno, kwa hiyo yeye pamoja na ujumbe wake ni mmoja.

Huwezi kuutenganisha Ujumbe na mjumbe, wao ni kitu kimoja, BWANA ASEMA HIVI. Haijalishi kile mpakwa mafuta yeyote wa uongo anachosema, Mungu alisema wao ni mmoja na hawawezi kutenganishwa.

Kisha akatuambia hatuhitaji tambara la chujio ili kuwashika wadudu wowote wakati tunapozisikiliza kanda, kwa maana hakuna wadudu ama utomvu wa mdudu katika Ujumbe Huu. Ni kisima Chake kinachofoka maji ambacho daima kinatiririka kisafi na cheupe. Hububujika daima, hakikauki kamwe, kinaendelea tu kusukuma na kusukuma, kikitupa Ufunuo zaidi na zaidi wa Neno Lake.

Yeye alitukumbusha KAMWE TUSISAHAU kwamba agano Lake na sisi ni lisilopingika, halibadiliki, lakini zaidi ya yote, halina Masharti.

Iwe ni upendo, usaidizi au kujisalimisha, ikiwa jambo lisilo na masharti ni YAKINI nalo halijatii sheria na masharti yoyote maalum: litatendeka bila kujali ni nini kingine kitakachotokea.

Kisha akataka kuushindilia msumari, kwa hivyo akatuambia kwamba leo hii Maandiko Yake yanatimizwa mbele ya macho yetu.

J-u-a lile lile lipambazukalo mashariki ndilo j-u-a lile lile litualo magharibi. Na M-w-a-n-a yule yule wa Mungu aliyetokea mashariki na kujithibitisha Mwenyewe kama Mungu aliyefanyika mwili ndiye M-w-a-n-a yule yule wa Mungu aliyeko katika kizio cha magharibi cha dunia ambaye anajitambulisha Mwenyewe kati ya kanisa usiku huu, Yeye yule jana, leo, na hata milele. Ile Nuru ya jioni ya Mwana imekuja. Leo Maandiko haya yametimia mbele yetu.

Yule Mwana wa Adamu amekuja tena katika mwili wa mwanadamu katika siku yetu, kama vile tu Yeye alivyoahidi angefanya, kumwita Bibi-arusi atoke. Ni Yesu Kristo akizungumza nasi moja kwa moja, na haihitaji fasiri yoyote ya mwandamu. Kitu pekee tunachohitaji, kitu pekee tunachotaka, ni Sauti ya Mungu inayonena kwenye kanda kutoka kwa Mungu Mwenyewe.

Ni ufunuo wa dhihirisho la Neno likifanywa halisi. Nasi tunaishi katika siku hiyo; Mungu asifiwe; Ufunuo wa siri ya Yeye Mwenyewe.

Ni wakati mtukufu jinsi gani Bibi-arusi aliyonao, akiwa amekaa kwenye uwepo wa Mwana, akiivishwa. Ngano imeirudia ngano tena, na hakuna chachu miongoni mwetu. Ni Sauti ya Mungu safi tu ikinena nasi, ikitufinyanga na kutufanya kuwa sura ya Kristo, aliye Neno.

Sisi ni wana na binti za Mungu, sifa Yake ile aliyoichagua tangu zamani ije katika wakati huu, wakati ulio mkuu sana katika historia ya ulimwengu.  Yeye alijua sisi hatungeshindwa, hatungepatana, bali tungekuwa Bibi-arusi Neno Wake mkweli na mwaminifu, Uzao Wake Mkuu wa Kifalme wa Ibrahimu ulioahidiwa ambao ungekuja.

Unyakuo umekaribia. Wakati umefika mwisho. Yeye anakuja kumchukua Bibi-arusi Wake ambaye amejiweka mwenyewe tayari bali amekaa kwenye Uwepo wa Mwana, akiisikia Sauti Yake ikimvika Bibi-arusi Wake. Hivi karibuni tutaanza kuwaona wapendwa wetu walioko ng’ambo ya pazia la wakati, ambao wanatungojea na kutamani sana kuwa pamoja nasi.

Kanda ndiyo njia iliyoandaliwa na Mungu ya kumkamilisha Bibi-arusi Wake. Kanda hizi ndicho kitu pekee kitakachomuunganisha Bibi-arusi Wake. Kanda hizi ndiyo Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi Wake.

Ninawalika mje muungane nasi, sehemu ya Bibi-arusi Wake, Jumapili hii saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia kila kitu kuhusu kile kinachokaribia kutukia hivi karibuni: Unyakuo 65-1204. 

 
Ndugu. Joseph Branham

25-0720 Juu Ya Mbawa Za Hua Mweupe Kama Theluji

UJUMBE: 65-1128E Juu Ya Mbawa Za Hua Mweupe Kama Theluji

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukusanyike pamoja Jumapili saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) ili kusikia  65-1128E Juu Ya Mbawa Za Hua Mweupe Kama Theluji.

Ndugu. Joseph Branham

25-0713 Mahali Pekee Palipowekwa Na Mungu Pa Kuabudia

UJUMBE: 65-1128M Mahali Pekee Palipowekwa Na Mungu Pa Kuabudia

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Familia ya Yesu Kristo,

Jambo fulani linatendeka zaidi ya hapo nyuma kwa Bibi-arusi wa Kristo kote ulimwenguni. Mambo ambayo tumeyasikia na kutamani kuyaona sasa yanadhihirika mbele ya macho yetu.

Roho Mtakatifu anamuunganisha Bibi-arusi Wake kama alivyosema angefanya, kwa njia Yake PEKEE aliyoiandaa kwa ajili ya siku hii, Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.

Yeye analifunua na kulithibitisha Neno Lake zaidi ya hapo awali. Kama Kisima kinachofoka maji, Ufunuo unabubujika ndani yetu.

Huo muungano wa kiroho wa Kristo na Kanisa Lake sasa, wakati mwili unapofanyika Neno, nalo Neno linafanyika mwili, linadhihirishwa, linathibitishwa. Vile vile hasa Biblia ilivyosema ingetendeka katika siku hii, inatendeka, siku baada ya siku. Mbona, inalundikana upesi sana huko nje, katika yale majangwa, na mambo yanayotendeka, hata nisingeweza kufuatilia jambo hilo.

Kila siku Ufunuo zaidi na zaidi unafunuliwa na kudhihirishwa kwetu. Kama vile nabii, mambo yanatokea na yanatendeka haraka sana, hatuwezi hata kuyafuatilia…UTUKUFU!!!

Wakati wetu umefika. Maandiko yanatimia. Mwili unafanyika Neno, nalo Neno linafanyika mwili. Vile vile nabii alivyosema yangetukia sasa yanatendeka.

Kwa nini sisi?

Hakuna chachu, hakuna sauti isiyojulikana, hakuna fasiri ya mwanadamu inayohitajika miongoni mwetu. Tunalisikiliza tu Neno Safi Kamilifu kutoka kwenye kinywa cha Mungu kwa anavyozungumza nasi mdomo kwa sikio.

Sasa tunaona Neno lile lile lililoahidiwa, la Luka, la Malaki, ahadi hizi nyingine zote za siku ya leo, zikifanyika mwili, zikikaa kati yetu, ambazo tulisikia kwa masikio yetu; sasa tunamwona Yeye (kwa macho yetu) akifasiri Neno Lake Mwenyewe, hatuhitaji fasiri yo yote ya mwanadamu.

Ewe Bibi-arusi, hilo haliwezi kuwa wazi zaidi ya hapo. Ni Mungu, akisimama mbele ya Bibi-arusi Wake katika mwili wa mwanadamu, ambaye tunaweza kumwona kwa macho yetu wenyewe, akizungumza na kulifasiri Neno Lake Mwenyewe, na kuliweka kwenye kanda. Neno Kamilifu lililonenwa na kurekodiwa na Mungu Mwenyewe, hivyo halihitaji fasiri yoyote ya mwanadamu.

  • • Mungu anazungumza moja kwa moja na Bibi-arusi Wake, kwenye kanda.
  • • Mungu hulifasiri Neno Lake Mwenyewe, kwenye kanda.
  • • Mungu anajifunua Mwenyewe, kwenye kanda.
  • • Mungu akimwambia Bibi-arusi Wake, huhitaji fasiri yoyote ya mwanadamu, Neno Langu lililo kwenye kanda ndiyo yote BIBI-ARUSI WANGU ANALOHITAJI.

Kumbukeni, mtakapoondoka hapa, anzeni kutoka kwenye kapi sasa; mnaingia kwenye punje, bali kaeni katika Uwepo wa Mwana. Msiongeze, yale nimesema; msiondoe, yale nimesema. Kwa sababu, ninazungumza Ukweli kadiri niujuavyo, kama vile Baba alivyonipa. Mnaona?

Mungu ameitengeneza NJIA KAMILIFU PEKEE kwa Bibi-arusi kufanya vile hasa Yeye alivyotuamuru kufanya. Hilo halikuwezekana, hadi leo hii. Hakuna kubahatisha, hakuna kushangaa, hakuna swali ikiwa humo kuna kitu chochote kilichoongezwa, kuondolewa, au kufasiriwa. Bibi-arusi amepewa ule Ufunuo wa kweli: KUZICHEZA KANDA NDIYO NJIA KAMILIFU YA MUNGU.

Ikiwezekana, hebu niliseme hilo tena. Ufunuo wangu ni kwamba Bibi-arusi wa Yesu Kristo, si wengine, BIBI-ARUSI, hahitaji KITU KINGINE ila Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.

Lakini mara huyo Roho Mtakatifu kweli…Neno halisi linapoingia ndani yako (Neno, Yesu), basi, ndugu, Ujumbe si siri kwako basi; unaujua, ndugu, wote umeangaziwa mbele yako.

Ujumbe si siri kwangu. Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. Mbingu na nchi zote zinaitwa Yesu. Yesu ni Neno.

Nalo hilo Jina limo katika Neno kwa kuwa Yeye ni Neno. Amina! Yeye ni nini basi? Neno lililofasiriwa ni dhihirisho la Jina la Mungu.

Mungu anamuunganisha Bibi-arusi Wake na Sauti Yake, ambayo alikuwa ameirekodi na kuihifadhi kwa ajili ya siku hii, ili kwamba aweze kumkusanya Bibi-arusi Wake pamoja kama Jamii Moja. Bibi-arusi yeye ataliona na kulitambua Hilo kuwa NJIA PEKEE Yeye anayoweza kumkusanya Bibi-arusi Wake pamoja.

Yeye alilifanya hilo zaidi ya miaka 60 iliyopita ili kutuonyesha sisi jinsi gani ambavyo Yeye angelifanya hilo leo. Sisi ni “moja ya makanisa yake kwenye muunganisho wa simu”

Kama mimi siamini kwenda kanisani, basi kwa nini niwe na makanisa? Tulikuwa nayo kila mahali nchini, yameunganishwa hivi majuzi usiku, kila maili mia mbili mraba kulikuwapo na kanisa langu.

Wahudumu wengi huyaambia makanisa yao kuwa kwenye “muunganisho wa simu” au “kusikiliza hewani”, “kuusikiliza Ujumbe mmoja kwa wakati mmoja”, ati sio kwenda kanisani. YEYE AMETOKA KUSEMA HUKO NI KWENDA! Wao ni kwamba tu aidha hawalijui Neno ama hawawezi kuisoma barua ya mahaba kama vile Bibi-arusi awezavyo.

Kanisa ni nini? Hebu na tuone kile Ndugu Branham alichosema kanisa lilicho.

Makusanyiko mengi, mengi yamepata makao haya kama mlivyokuwa nayo hapa kutoka maskani. Pia imeunganishwa huko Phoenix, ya kwamba kila mahali ibada zilipo, inaingia moja kwa moja kwenye…Na wanakusanyika makanisani na majumbani, na mambo kama hayo, kupitia wimbi zuri sana.

Ndugu Branham anasema waziwazi kwamba watu wakiwa “majumbani” mwao na “mambo kama hayo” walikuwa ni moja ya makanisa yake kwenye muunganisho wa Simu. Kwa hivyo majumba, vituo vya mafuta, majengo, familia zilizokusanyika pamoja kwenye muunganisho wake wa simu hilo liliwafanya kuwa kanisa.

Hebu na tuisome kidogo zaidi BARUA YA MAHABA.

Tunayaombea makanisa yote na makusanyiko ambayo yamekusanyika kuzunguka vile—vile—vile vipaza sauti vidogo nchini kote, kutoka kwenye taifa, kote kote hata kwenye Pwani ya Magharibi, kule juu kwenye milima ya Arizona, chini kwenye mabonde ya Texas, mbali sana hata Pwani ya Mashariki, nchini kote, Bwana, ambako wao wamekutanika. Tuko umbali wa masaa mengi, bali, Bwana, sisi tuko pamoja usiku wa leo kama jamii moja, waamini, tukingojea kuja kwa Masihi.

Kwa hivyo wakiwa kwenye Muunganisho wa Simu, wakimsikiliza Ndugu Branham WOTE KWA WAKATI MMOJA; walikuwa pamoja kama jamii moja, waamini, wakingojea Kuja kwa Masihi.

Lakini ninyi mnasema ukifanya hivyo leo, huko sio kwenda kanisani, ati ni makosa, sio kukusanyika pamoja na zaidi sana tunapoona ile siku ikikaribia, huko sio kwenda kanisani?

Hebu niwaulizeni swali nanyi myajibu makusanyiko yenu. Kama Ndugu Branham angekuwa hapa leo, katika mwili, nanyi mngeweza kusikiliza hewani au kujiunganisha kwa simu ili kumsikiliza yeye kila Jumapili asubuhi, wote kwa wakati mmoja pamoja na Bibi-arusi kote ulimwenguni, enyi wachungaji, Je! mngeweza KUJIUNGANISHA KWA SIMU na kumsikia Ndugu Branham au mngehubiri?

Ndugu Branham anasema waziwazi wajibu wako ni kanisa lako. Kama ungekuwa hapa miaka 60 iliyopita naye Ndugu Branham alikuwa na ibada, lakini kanisa lako halingehudhuria bali lilikuwa na ibada yao wenyewe (jambo ambalo wahudumu wengi walilifanya wakati huo), Je, wewe ungeweza kwenda kwenye “kanisa lako”, au ungeenda kwenye “Maskani ya Branham” kumsikiliza Ndugu Branham?

Nitawapa jibu langu. Mimi ningekuwa nikisimama mlangoni kwenye mvua, theluji au tufani ya theluji ili niingie Maskanini kumsikiliza nabii wa Mungu. Kama NINGEKUWA nikienda kwenye lile kanisa lingine, ningeyabadilisha makanisa usiku huo.

Lakini mwanamke yule, hakujua kama nguvu zilikuwa katika ile fimbo ama la, bali yeye alijua Mungu alikuwa ndani ya Eliya. Hapo ndipo yule Mungu alipokuwa: ndani ya nabii Wake. Akasema, Kama Bwana aishivyo, na nafsi yako iishivyo, sitakuacha.

Ninawaalika kuungana nasi na kuwa moja ya makanisa ya Ndugu Branham kwenye muunganisho wa simu siku ya Jumapili saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapoisikia Sauti ya Mungu ikituletea Ujumbe: Mahali Pekee Palipowekwa Na Mungu Pa Kuabudia 65-1128M.

Ndugu. Joseph Branham

25-0706 Nimesikia Bali Sasa Ninaona

UJUMBE: 65-1127E Nimesikia, Bali Sasa Ninaona

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi aliyeunganishwa kwa simu,

Leo, Maneno haya Mungu aliyoyanena kupitia Malaika-Mjumbe Wake wa Saba yangali yanatimia kupitia SISI, BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO. 

Kama mimi siamini kwenda kanisani, basi kwa nini niwe na makanisa? Tulikuwa nayo kila mahali nchini, yameunganishwa kwa simu hivi majuzi usiku, kila maili mia mbili mraba kulikuwapo na kanisa langu.

Walikuwa katika makanisa, majumbani, majengo madogo, na hata kituo cha mafuta; wakiwa wametawanyika kote Marekani, wakisikiliza, wote kwa wakati mmoja Neno lilikuwa likitoka. 

Na leo hii, sisi tungali ni MOJA YA MAKANISA YAKE.  Yeye ANGALI NI MCHUNGAJI WETU. Neno Lake LINGALI HALIHITAJI FASIRI YOYOTE, nasi TUNGALI tumekusanyika ulimwenguni kote, TUMEUNGANISHWA KWA SIMU, tukiisikiliza SAUTI ya Mungu ikimkamilisha Bibi-arusi wa Yesu Kristo.

Leo, Neno hili lingali linatimia.

Kwa nini wao walifanya hivyo wakati huo? Kwa nini wachungaji waliyafunga makanisa yao ili kuusikia Ujumbe moja kwa moja? Wao wangeweza kusubiri tu wazipate kanda, kisha wakahubiri Ujumbe wao wenyewe kwa watu wao baadaye; nami nina hakika wengi wasio na Ufunuo walifanya hivyo. 

Au labda wengine waliyaambia makusanyiko yao, “Sasa sikilizeni, sisi tunaamini Ndugu Branham ni nabii wa Mungu, lakini yeye hakusema tunatakiwa kumsikiliza yeye katika makanisa yetu. Mimi ninahubiri Jumapili hii, na kila Jumapili; ninyi zichukueni tu kanda na mzisikilize huko majumbani mwenu.”

Bibi-arusi wakati ule, ni kama tu Bibi-arusi sasa hivi, walikuwa na Ufunuo, nao walitaka kuisikia Sauti ya Mungu moja kwa moja wao wenyewe. Walitaka kuungana na Bibi-arusi kote nchini waisikie Sauti ya Mungu ilipokuwa ikitoka. Wao walitaka kutambulishwa kama moja ya makanisa yake, majumba, ama po pote walipokuwa, na Ujumbe, Sauti, na sasa, kanda. 

Leo, Neno hili lingali linatimia.

Kwa nini wao/sisi Tunaliona na wengine hawalioni? Kwa kujua tangu zamani, sisi tulichaguliwa kuliona Hili. Lakini ninyi ambao hamkuchaguliwa, kamwe hamtaliona. Ngano inaliona nayo imeanza kuondoka.

Haimaanishi kwamba unapaswa kuacha kwenda kwenye kanisa lako. Wala haimaanishi mchungaji wako aache kuhudumu.  Inamaanisha tu kwamba wahudumu wengi na wachungaji wengi wamesahau JAMBO KUU, nao hawawaambii watu wao SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI mnayopaswa kuisikia ni SAUTI ya Mungu iliyo kwenye kanda. 

Kwenda kanisani kila siku ya kila wiki hakukufanyi wewe kuwa Bibi-arusi; hayo si matakwa ya Mungu.  Mafarisayo na Masadukayo walikuwa na mafundisho hayo. Walijua kila herufi ya kila Neno, bali Neno lililo Hai lilikuwa limesimama PAPO HAPO katika mwili wa mwanadamu, lakini wao walifanya nini? Jambo lile lile wafanyalo wengi leo. 

Wao watasema, “hayo yalikuwa ni madhehebu aliyokuwa akizungumzia. Ambao hawangemruhusu Ndugu Branham kuhubiri makanisani mwao, bali sisi tunalihubiri Neno na tunasema vile tu yeye alivyosema.”

Hilo ni zuri. Bwana asifiwe. Hivyo ndivyo unavyopaswa kufanya. Lakini kisha useme, leo ni tofauti, ni makosa kuzicheza kanda za Ndugu Branham katika kanisa lako. Wewe hauna tofauti na Mafarisayo na Masadukayo, au madhehebu. 

Wewe ni mnafiki. 

Kama ilivyokuwa wakati huo, ni Yesu, akisimama mlangoni akibisha, akijaribu kuingia ndani anene moja kwa moja na Kanisa Lake, nao hawataifungua milango yao, nao hawatazicheza kanda katika makanisa yao. “Yeye haji katika kanisa letu ahubiri”.

Adui atageuza hilo na kulizungusha katika pande nyingi sana kwani ANACHUKIA kufichuliwa, lakini hata hivyo, linadhihirishwa mbele ya macho yetu na wengi wanajiondokea.  

“Hapo mwanzo kulikuwako” [kusanyiko linasema, “Neno!”—Mh.] “Naye Neno alikuwako kwa” [Kusanyiko linasema “Mungu!”—Mh.] “Naye Neno alikuwa” [Kusanyiko linasema “Mungu!”—Mh.]. “Naye Neno alifanyika mwili akakaa kwetu.” Hiyo ni kweli? Sasa tunaona Neno lile lile lililoahidiwa, la Luka, la Malaki, ahadi hizi nyingine zote za siku ya leo, zikifanyika mwili, zikikaa kati yetu, ambazo tulisikia kwa masikio yetu; sasa tunamwona Yeye (kwa macho yetu) akifasiri Neno Lake Mwenyewe, hatuhitaji fasiri yo yote ya mwanadamu. Ee kanisa la Mungu Aliye Hai! mlio hapa na kwenye simu! amkeni upesi, kabla hamjachelewa sana!

Ifungueni mioyo yenu na msikie yale ambayo Mungu ametoka kuwaambieni, makanisa yake yote. Sasa tunamwona YEYE, kwa macho yetu, AKILIFASIRI NENO LAKE MWENYEWE. Hatuhitaji fasiri yoyote ya mwanadamu!!  AMKENI KABLA HAMJACHELEWA!!

Tumeyasikia mambo haya maisha yetu yote yale yaliyokuwa yanaenda kutukia katika wakati wa mwisho. Sasa tunaliona kwa macho yetu hilo likitukia. 

Yeye Alituambia, KUNA NJIA MOJA PEKE YAKE, AMBAYO NDIYO NJIA YA MUNGU ILIYOANDALIWA ALIYOIFANYA KWA AJILI YA BIBI-ARUSI WAKE. LAZIMA UKAE NA SAUTI YA MUNGU ILIYO KWENYE KANDA.

Ninaualika ulimwengu mzima uje kuungana nasi Jumapili saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) na kuisikia Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii. Kisha wewe pia unaweza kusema, “Nimesikia habari Zako, bali sasa Ninakuona”.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: 65-1127E   Nimesikia Bali Sasa Ninaona

Maandiko

Mwanzo 17
Kutoka 14:13-16
Ayubu sura ya 14 na 42:1-5
Amosi 3:7
Marko 11:22-26 na 14:3-9
Luka 17:28-30

25-0629 Kujaribu Kumtumikia Mungu Bila ya Kuwa Ni Mapenzi ya Mungu

UJUMBE: 65-1127B Kujaribu Kumtumikia Mungu Bila ya Kuwa Ni Mapenzi ya Mungu

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukusanyike pamoja Jumapili saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni Saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) kusikia  
65-1127B – Kujaribu Kumtumikia Mungu Bila Ya Kuwa Ni Mapenzi ya Mungu.

Ndugu. Joseph Branham

25-0622 Kazi Ni Imani Katika Matendo

UJUMBE: 65-1126 Kazi Ni Imani Katika Matendo

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Neno Lililofanyika Mwili,

Haleluya! Udongo wa kuzalia wa mioyo yetu umetayarishwa kwa kulisikia Neno na imefunuliwa kwetu, SISI NDIYE Bibi-arusi mwadilifu wa Kristo; mwana wa Mungu wa thamani, mwadilifu, asiye na dhambi, akisimama pamoja na Bibi-arusi Neno msafi, asiyeghoshiwa, aliyeoshwa kwa Maji ya Damu Yake Mwenyewe.

Sisi tumekuwa Neno lililodhihirishwa lililofanyika mwili, ili Yesu apate kutuchukua sisi, ambao Yeye alitangulia kuwachagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, katika kifua cha Baba.

Ulimwengu unaweza kuona kule kudhihirishwa kwa Imani yetu kulingana na jinsi tulivyokuwa tukitenda, na kudhihirisha ya kwamba tunao Ufunuo wa kweli kutoka kwa Mungu wa Neno Lake lililothibitishwa, nasi hatuogopi. Hatujali kile ulimwengu mzima unachosema ama unachoamini…SISI HATUOGOPI. Kubonyeza Play ndiyo njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya Bibi-arusi wa Yesu Kristo.

Kuna wengi wanaosema wanauamini Ujumbe huu wa wakati wa mwisho, wanaamini kwamba Mungu alimtuma nabii, wanaamini William Marrion Branham alikuwa malaika-mjumbe wa saba, wanaamini kwamba alinena Bwana Asema Hivi, lakini wao HAWAAMINI kwamba Sauti ndiyo sauti iliyo muhimu zaidi unayopaswa kuisikia. Wao hawaamini kuwa yeye alinena Maneno ya kutokosea. Hawaamini kuzicheza kanda katika makanisa yao.

Hiyo inamaanisha nini? INAMAANISHA HILO HALIJAFUNULIWA KWAO!

Ni ufunuo. Yeye amekufunulia jambo fulani kwa neema Yake. Hakuna kitu ulichofanya. Hukujitahidi upate imani. Kama ukiwahi kuwa na imani, umepewa hiyo kwa neema ya Mungu. Na Mungu anakufunulia, kwa hiyo imani ni ufunuo. Na Kanisa lote la Mungu limejengwa juu ya ufunuo.

Kwa IMANI imefunuliwa kwetu ya kwamba Ujumbe huu ndiyo Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda ambayo imerekodiwa, na kuhifadhiwa, ili kumlisha na kumkamilisha Bibi-arusi wa Yesu Kristo.

Ni IMANI ya kweli, isiyoghoshiwa katika yale Mungu aliyosema kwamba ni Kweli. Nayo imetia nanga ndani ya moyo na nafsi yetu na hakuna kitu kitakachoitikisa. Itakaa papo hapo mpaka nabii Wake atakapotutambulisha kwa Bwana wetu.

Hatuwezi kufanya vinginevyo. Yeye alitutayarisha sisi kulipokea na kuliamini Hilo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Yeye alijua sisi tungeipokea Sauti Yake katika wakati huu. Alitangulia kutujua tangu zamani na akatuchagua tangu asili kuipokea.

Basi, kazi ambazo Roho Mtakatifu anazifanya siku hizi, kwa maono haya yasiyoshindwa, ahadi zisizoshindwa, ishara zote za kimitume zilizoahidiwa katika Biblia, za Malaki 4, na, loo, Ufunuo 10:7, yote hayo yanatimia; na kuthibitishwa kisayansi, kwa njia yoyote ile. Na kama sijawaambia Kweli, mambo haya hayangetendeka. Lakini kama nimewaambia Kweli, yanashuhudia ya kwamba nimewaambia Kweli. Angali ni yeye yule jana, leo, na hata milele, na madhihirisho ya Roho Wake yanamnyakua Bibi-arusi. Hebu imani hiyo (ufunuo) iangukie ndani ya moyo wako, ya kwamba “Hii ndiyo ile saa.”

Hii ndiyo ile saa yenyewe. Huu ndio Ujumbe wenyewe. Hii ndiyo Sauti ya Mungu inayomwita Bibi-arusi wa Yesu Kristo. Loo, Ewe Kanisa, Bwana na auandae udongo wa kuzalia wa moyo wako upate kuwa na Imani na akufunulie ya kwamba kuisikiliza Sauti hii, kwenye kanda, ndiko kutamkamilisha na kumuunganisha Bibi-arusi wa Yesu Kristo.

Ninawaalika kwa mara nyingine tena mje kuungana nasi Jumapili saa 06:00 MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) kuipeleka IMANI yako ifike mahali pa juu, na kuketi pamoja nasi katika ulimwengu wa roho tunapoisikia Sauti ya Mungu ikitutayarisha kwa ajili ya ujio Wake wa hivi karibuni.

Ndugu. Joseph Branham

Tafadhali iweni katika maombi kwa ajili yetu wiki ijayo tunapoianza Kambi yetu ya kwanza ya Still Waters.

Ujumbe: Kazi Ni Imani Katika Matendo 65-1126 (Matendo Ni Imani Iliyodhihirishwa)

Maandiko ya kusoma:

Mwanzo 15:5-6, 22:1-12
Matendo 2:17
Warumi 4:1-8, 8:28-34
Waefeso 1:1-5
Yakobo 2:21-23
Yohana Mtakatifu 1:26, 6:44-46

25-0615 Muungano Usioonekana Wa Bibi-Arusi Wa Kristo

UJUMBE: 65-1125 Muungano Usioonekana Wa Bibi-Arusi Wa Kristo

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi Mteule wa Mungu,

Hakuna njia ya kulikwepa, wewe ni Jeni ya Kiroho ya Mungu, dhihirisho la sifa za mawazo Yake, nawe ulikuwa ndani Yake kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Hatuwezi kwenda zaidi, tunafanana kabisa na punje ile ile iliyoingia ardhini. Sisi ni Yesu yeye yule, katika mfano wa Bibi-arusi, tukiwa na nguvu zile zile, Kanisa lile lile, Neno lile lile linaloishi na kukaa ndani yetu, linafikia kilele chake, TAYARI KWA UNYAKUO.

Yeye alituambia tulivunja ndoa yetu ya kwanza, kwa mauti ya kiroho, na sasa tumezaliwa mara ya pili, ama tumeolewa tena, kwenye ndoa yetu mpya ya Kiroho. Si ya maisha yetu ya kimaumbile ya kale na mambo ya ulimwengu, bali ni ya Uzima wa Milele. Ile chembe hai iliyokuwa ndani yetu hapo mwanzo, imetupata!

Hilo linamaanisha nini? Linamaanisha kitabu chetu cha zamani kimetoweka pamoja na ndoa yetu ya zamani, kimehamishwa. SASA kiko katika “Kitabu Kipya” cha Mungu; si kitabu cha uzima… la, la, la… bali katika Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo. Kile Mwanakondoo alichokomboa. Ndicho cheti chetu cha ndoa ambapo Chembechembe yetu ya kweli ya uhai ya Milele inakaa.

Je! uko tayari? Hili hapa laja. Afadhali ujifinye na kujitayarisha kupaza sauti na kupiga kelele utukufu, haleluya, Bwana asifiwe, lina mitutu miwili na risasi za mbinguni.

“Unataka kuniambia ya kwamba kitabu changu cha zamani pamoja na makosa yangu yote na kushindwa kwangu kote…”

Mungu alikiweka kwenye Bahari ya Usahaulifu Wake, nawe si tu kwamba umesamehewa, bali umehesabiwa haki…Utukufu! “Umehesabiwa haki.”

Na hilo linamaanisha nini? Linamaanisha wewe hata hukuwahi kulitenda jambo hilo Machoni pa Mungu.
Unasimama mkamilifu mbele za Mungu. UTUKUFU! Yesu, Neno, alipachukua mahali pako. Yeye alifanyika wewe, ili wewe, mwenye dhambi mchafu, upate kufanyika Yeye, NENO. Sisi ni NENO.

Hilo linatufanya sisi ile Chembechembe Yake ndogo ya uhai iliyokusudiwa tangu mwanzo. Sisi ni Neno likija juu ya Neno, juu ya Neno, juu ya Neno, juu ya Neno, nasi tunafikia kimo kikamilifu cha Kristo kusudi Yeye apate kuja kutuchukua tuwe Bibi-arusi Wake.

Nini kinachotendeka SASA HIVI?

Ni Muungano Usioonekana wa Bibi-arusi wa Kristo wakikusanyika kulizunguka Neno, kutoka ulimwenguni kote.

Hili linaenda kote nchini. Huko New York, sasa ni saa tano na dakika ishirini na tano. Juu kule Philadelphia na karibu kote kule, hao watakatifu wapendwa wanaoketi kule wakisikiliza, sasa hivi, katika makanisa kila mahali. Huko juu kabisa, huko chini kabisa karibu na Mexico, huko juu kabisa karibu na Canada na kila mahali, kotekote. Maili mia mbili, popote pale katika bara la Marekani ya Kaskazini hapa, karibu yote, watu wako chonjo, wakisikiliza hivi sasa. Maelfu mara maelfu, wakisikiliza.

Na huo ndio Ujumbe wangu kwenu, enyi Kanisa, ninyi ambao ni muungano, muungano wa kiroho kwa Neno.

Yeye alisema ulikuwa ni muungano wa kiroho wa Kristo na Kanisa Lake, Nao UNATENDEKA SASA HIVI. Mwili unafanyika Neno, nalo Neno linafanyika mwili. Tumedhihirishwa, na kuthibitishwa; vile vile hasa Biblia ilivyosema ingetendeka katika siku hii, Nalo linatendeka sasa, siku baada ya siku katika kila mmoja wetu.

Mungu anaenda kuwa na Kanisa adilifu. Bibi-arusi Neno Wake mkweli na mwaminifu. SISI NDIO BIBI MTEULE wa Bwana wetu Yesu Kristo.

Ni Saa Ngapi, Bwana?

Tuna ufunuo katika siku hizi za mwisho, kwa ajili ya Ujumbe wa Bwana Mungu kumkusanya Bibi-arusi Wake pamoja. Hakuna wakati mwingine ambao umeahidiwa hilo. Imeahidiwa katika wakati huu: Malaki 4, Luka 17:30, Yohana Mtakatifu 14:12. Yoeli 2:38. Ahadi hizo ni kama tu vile Yohana Mbatizaji alivyojitambulisha katika Maandiko.

Ni nani aliyeyatimiza maandiko haya?

Malaika Wake wa saba mwenye nguvu, William Marrion Branham. Daima alifanya jambo hilo kwa mpangilio. Alilifanya kila wakati kwa mpangilio. Yeye analifanya tena katika siku yetu, akimwita atoke na kumkusanya Bibi-arusi Wake mwadilifu katika siku ya mwisho kwa nabii Wake.

Ni wakati mtukufu jinsi gani ambao Bibi-arusi alionao. Kila kukusanyika kunakuwa kukuu zaidi na zaidi na kutamu zaidi na zaidi. Hakujawahi kuwa na wakati kama huu. Mashaka yote yametoweka.

Njoo uungane nasi tunapomsikia Neno lililoahidiwa la siku yetu akinena, na kutuambia sisi ni nani na kipi kinachotukia katika siku yetu. Muungano Usioonekana wa Bibi-arusi wa Kristo 65-1125.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko:

Mathayo 24:24
Luka mt. 17:30 / 23:27-31
Yohana 14:12
Matendo 2:38
Warumi 5:1 / 7:1-6
2 Timotheo 2:14
1 Yohana 2:15
Mwanzo 4:16-17 / 25-26
Danieli 5:12
Yoeli 2:28
Malaki 4

25-0608 Kiongozi

UJUMBE: 62-1014E Kiongozi

PDF

BranhamTabernacle.org

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Anayejikusanya Pamoja,

Sasa Mungu daima amewatuma viongozi Wake, Yeye daima hajakosa kuwa na kiongozi, katika nyakati zote. Mungu daima amekuwa na mtu fulani aliyemwakilisha katika dunia hii, katika nyakati zote.

Mungu hataki sisi tutegemee akili zetu au mawazo yoyote yaliyobuniwa na mwanadamu. Ndiyo maana Yeye humtumia Bibi-arusi Wake Kiongozi; kwa kuwa yeye ana fahamu, jinsi ya kwenda na nini cha kufanya. Mungu HAJAWAHI KAMWE KUBADILI mpango Wake. Yeye hajashindwa kamwe kuwatumia watu Wake Kiongozi, bali huna budi kumkubali Kiongozi huyo.

Huna budi kuamini kila Neno Yeye analosema kupitia Kiongozi Wake. Huna budi kwenda njia Kiongozi Wake anayosema uende. Ukipata kusikiliza na kuamini sauti zingine kama kiongozi wako, mwishowe utapotea tu.

Yohana Mtakatifu 16 inasema Yeye alikuwa na mambo mengi ya kutuambia na kutufunulia, hivyo Yeye angemtuma Roho Wake Mtakatifu Kutuongoza na kutuambia. Alisema Roho Mtakatifu ndiye nabii-kiongozi wa kila kizazi. Hivyo, manabii Wake walitumwa kumwakilisha Roho Mtakatifu ili kumwongoza Bibi-arusi Wake.

Roho Mtakatifu anatumwa kuliongoza kanisa, si kundi fulani la watu. Roho Mtakatifu ndiye hekima yote. Mwanadamu huwa mgumu, asiyejali.

Si huyo mtu, bali ni Roho Mtakatifu NDANI ya mtu huyo. Mtu Aliyemchagua kujiwakilisha Mwenyewe na kuwa kiongozi wetu wa duniani ambaye anaongozwa na Kiongozi wetu wa Mbinguni. Neno linatuambia hatuna budi kumfuata Kiongozi huyo. Haidhuru tunafikiri nini, yale yanayoonekana ni ya maana, au kile mtu mwingine asemacho, sisi hatuwezi kupambanua jambo hilo, kiongozi ndiye tu anayeweza.

Mungu hutuma Kiongozi, naye Mungu anataka mkumbuke ya kwamba huyo ni Kiongozi Wake aliyemchagua.

Nabii-kiongozi wetu amechaguliwa na Mungu kulinena Neno Lake. Neno lake ni NENO LA MUNGU. Nabii- kiongozi, na yeye peke yake, ndiye aliye na fasiri ya kiungu ya Neno. Mungu alilinena Neno Lake kwake mdomo kwa sikio. Kwa hivyo, huwezi kupinga, kubadilisha, au kulihoji Neno la Kiongozi wako.

Lazima umfuate Yeye, na Yeye peke yake. Usipofanya hivyo, mwishowe utapotea. Kumbuka, unapomwacha, Kiongozi aliyechaguliwa na Mungu, unakuwa peke yako, kwa hiyo sisi tunataka kuwa karibu na kiongozi Aliyemchagua, na kusikia na kutii kila Neno Yeye analolisema kupitia yeye.

Kiongozi wetu ametufundisha kwamba agano la kale lilikuwa kivuli cha agano jipya.

Israeli walipotoka Misri wakienda kwenye ile nchi ya ahadi, katika Kutoka 13:21, Mungu alijua ya kwamba wao hawajapita njia hiyo hapo kabla. Ilikuwa tu maili arobaini, bali hata hivyo walihitaji kitu fulani cha kwenda pamoja nao. Wangepotea njia. Kwa hiyo Yeye, Mungu, akawatumia Kiongozi. Kutoka 13:21, kitu kama hiki, “Ninamtuma Malaika Wangu aende mbele zenu, ile Nguzo ya Moto, ili awalinde njiani,” kuwongoza kwenye nchi hii ya ahadi. Nao wana wa Israeli wakamfuata Kiongozi yule, ile Nguzo ya Moto (usiku), Wingu mchana. Wakati iliposimama, wao wakasimama. Wakati iliposafiri, wao wakasafiri. Basi Yeye alipowafikisha karibu na ile nchi, nao hawakuwa wanastahili kuvuka, Yeye aliwaongoza akawarudisha jangwani tena.

Alisema hilo ni kanisa leo hii. Tungekuwa tayari tumekwishaondoka kama tu tungejisahihisha wenyewe na kujiweka sawa, bali Yeye hana budi kuzidi kutuongoza kuzunguka na kuzunguka na kuzunguka.

Wao walipaswa tu kumfuata kiongozi wao kama vile YEYE ALIVYOIFUATA na kusikia kutoka kwenye ile Nguzo ya Moto. Yeye aliwaambia yale Mungu aliyosema nao walipaswa kutii kila Neno yeye alilosema. Yeye alikuwa ndiye Sauti ya yule Kiongozi. Lakini wao walihoji na kubishana na yule kiongozi aliyechaguliwa na Mungu, hivyo wakatangatanga nyikani kwa miaka 40.

Kulikuwa na wahudumu wengi katika siku za Musa. Mungu alikuwa amewachagua kuwasaidia hao watu, kwa vile Musa asingeweza kufanya yote. Lakini wajibu wao ulikuwa ni kuwaelekeza watu kwenye yale Musa aliyosema. Biblia haisemi chochote kile hao watu walichosema, inasema tu yale Musa aliyosema kuwa ndilo Neno la kuwaongoza hao watu.

Wakati Mungu alipomwondoa Musa jukwaani, Yoshua alitawazwa kuwaongoza hao watu, ambalo inamwakilisha Roho Mtakatifu leo. Yoshua hakuhubiri jambo lolote jipya, wala yeye hakujaribu kupachukua mahali pa Musa, wala hakujaribu kufasiri kile kiongozi alichosema; yeye aliyasoma tu yale Musa aliyosema na kuwaambia watu, “Kaeni na Neno. Kaeni na yale Musa aliyosema”. Yeye aliyasoma tu yale Musa aliyosema.

Ni mfano mkamilifu jinsi gani wa leo hii. Mungu alimthibitisha Musa kwa Nguzo ya Moto. Nabii wetu alithibitishwa kwa Nguzo ile ile ya Moto. Maneno ambayo Musa aliyoyanena yalikuwa ni Neno la Mungu na yakawekwa ndani ya lile Sanduku. Nabii wa Mungu alinena katika siku yetu na Hilo liliwekwa kwenye kanda.

Wakati Musa alipoondolewa jukwaani, Yoshua alitawazwa kuwaongoza hao watu kwa kuyadumisha Maneno aliyoyanena Musa mbele yao. Aliwaambia waamini na wadumu na kila Neno lililonenwa na kiongozi wa Mungu.

Yoshua aliyasoma kila mara yale Musa aliyoyaandika Neno kwa Neno kutoka kwenye magombo. Yeye aliliweka Neno mbele yao daima. Neno la siku yetu halikuandikwa, bali lilirekodiwa ili Roho Mtakatifu aweze kumfanya Bibi-arusi Wake asikie Neno kwa Neno kile Yeye alichosema, kwa Kubonyeza Play.

Mungu kamwe habadilishi mpango Wake. Yeye ndiye Kiongozi wetu. Sauti Yake ndiyo inayomwongoza na kumuunganisha Bibi-arusi Wake leo. Sisi tunataka tu kuisikia Sauti ya Kiongozi wetu vile Inavyotuongoza kwa Nguzo ya Moto. Ni muungano usioonekana wa Bibi-arusi wa Kristo. Tunaijua Sauti Yake.

Wakati kiongozi wetu anapokuja mimbarani, Roho Mtakatifu anamshika na Si yeye tena, bali ni yule Kiongozi wetu. Anakiinua kichwa chake hewani na kupaza sauti, “Bwana Asema Hivi, Bwana Asema Hivi, Bwana Asema Hivi! Na kila mshiriki wa Bibi-arusi wa Kristo kote ulimwenguni huja moja kwa moja kwake. Kwa nini? TUNAMJUA KIONGOZI WETU KWA JINSI TU YEYE ANAVYOONGEA.

Kiongozi wetu = Neno
Neno = Humjia nabii
Nabii = Mfasiri pekee wa kiungu wa Mungu; kiongozi Wake wa duniani.

Kaeni nyuma ya Neno! Loo, naam, bwana! Kaeni na Kiongozi huyo. Kaeni vema sawasawa nyuma Yake. Msiende mbele Yake, kaeni nyuma Yake. Hebu Hilo na liwaongoze, msiliongoze. Liachilieni liende.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe:

62-1014E – Kiongozi

Maandiko:

Marko 16:15-18
Yohana Mtakatifu 1:1 / 16:7-15
Matendo 2:38
Waefeso 4:11-13 / 4:30
Waebrania 4:12
2 Petro 1:21
Kutoka 13:21