Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukusanyike pamoja Jumapili saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) ili kusikia 65-1128E Juu Ya Mbawa Za Hua Mweupe Kama Theluji.
Jambo fulani linatendeka zaidi ya hapo nyuma kwa Bibi-arusi wa Kristo kote ulimwenguni. Mambo ambayo tumeyasikia na kutamani kuyaona sasa yanadhihirika mbele ya macho yetu.
Roho Mtakatifu anamuunganisha Bibi-arusi Wake kama alivyosema angefanya, kwa njia Yake PEKEE aliyoiandaa kwa ajili ya siku hii, Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.
Yeye analifunua na kulithibitisha Neno Lake zaidi ya hapo awali. Kama Kisima kinachofoka maji, Ufunuo unabubujika ndani yetu.
Huo muungano wa kiroho wa Kristo na Kanisa Lake sasa, wakati mwili unapofanyika Neno, nalo Neno linafanyika mwili, linadhihirishwa, linathibitishwa. Vile vile hasa Biblia ilivyosema ingetendeka katika siku hii, inatendeka, siku baada ya siku. Mbona, inalundikana upesi sana huko nje, katika yale majangwa, na mambo yanayotendeka, hata nisingeweza kufuatilia jambo hilo.
Kila siku Ufunuo zaidi na zaidi unafunuliwa na kudhihirishwa kwetu. Kama vile nabii, mambo yanatokea na yanatendeka haraka sana, hatuwezi hata kuyafuatilia…UTUKUFU!!!
Wakati wetu umefika. Maandiko yanatimia. Mwili unafanyika Neno, nalo Neno linafanyika mwili. Vile vile nabii alivyosema yangetukia sasa yanatendeka.
Kwa nini sisi?
Hakuna chachu, hakuna sauti isiyojulikana, hakuna fasiri ya mwanadamu inayohitajika miongoni mwetu. Tunalisikiliza tu Neno Safi Kamilifu kutoka kwenye kinywa cha Mungu kwa anavyozungumza nasi mdomo kwa sikio.
Sasa tunaona Neno lile lile lililoahidiwa, la Luka, la Malaki, ahadi hizi nyingine zote za siku ya leo, zikifanyika mwili, zikikaa kati yetu, ambazo tulisikia kwa masikio yetu; sasa tunamwona Yeye (kwa macho yetu) akifasiri Neno Lake Mwenyewe, hatuhitaji fasiri yo yote ya mwanadamu.
Ewe Bibi-arusi, hilo haliwezi kuwa wazi zaidi ya hapo. Ni Mungu, akisimama mbele ya Bibi-arusi Wake katika mwili wa mwanadamu, ambaye tunaweza kumwona kwa macho yetu wenyewe, akizungumza na kulifasiri Neno Lake Mwenyewe, na kuliweka kwenye kanda. Neno Kamilifu lililonenwa na kurekodiwa na Mungu Mwenyewe, hivyo halihitaji fasiri yoyote ya mwanadamu.
• Mungu anazungumza moja kwa moja na Bibi-arusi Wake, kwenye kanda.
• Mungu hulifasiri Neno Lake Mwenyewe, kwenye kanda.
• Mungu anajifunua Mwenyewe, kwenye kanda.
• Mungu akimwambia Bibi-arusi Wake, huhitaji fasiri yoyote ya mwanadamu, Neno Langu lililo kwenye kanda ndiyo yote BIBI-ARUSI WANGU ANALOHITAJI.
Kumbukeni, mtakapoondoka hapa, anzeni kutoka kwenye kapi sasa; mnaingia kwenye punje, bali kaeni katika Uwepo wa Mwana. Msiongeze, yale nimesema; msiondoe, yale nimesema. Kwa sababu, ninazungumza Ukweli kadiri niujuavyo, kama vile Baba alivyonipa. Mnaona?
Mungu ameitengeneza NJIA KAMILIFU PEKEE kwa Bibi-arusi kufanya vile hasa Yeye alivyotuamuru kufanya. Hilo halikuwezekana, hadi leo hii. Hakuna kubahatisha, hakuna kushangaa, hakuna swali ikiwa humo kuna kitu chochote kilichoongezwa, kuondolewa, au kufasiriwa. Bibi-arusi amepewa ule Ufunuo wa kweli: KUZICHEZA KANDA NDIYO NJIA KAMILIFU YA MUNGU.
Ikiwezekana, hebu niliseme hilo tena. Ufunuo wangu ni kwamba Bibi-arusi wa Yesu Kristo, si wengine, BIBI-ARUSI, hahitaji KITU KINGINE ila Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.
Lakini mara huyo Roho Mtakatifu kweli…Neno halisi linapoingia ndani yako (Neno, Yesu), basi, ndugu, Ujumbe si siri kwako basi; unaujua, ndugu, wote umeangaziwa mbele yako.
Ujumbe si siri kwangu. Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. Mbingu na nchi zote zinaitwa Yesu. Yesu ni Neno.
Nalo hilo Jina limo katika Neno kwa kuwa Yeye ni Neno. Amina! Yeye ni nini basi? Neno lililofasiriwa ni dhihirisho la Jina la Mungu.
Mungu anamuunganisha Bibi-arusi Wake na Sauti Yake, ambayo alikuwa ameirekodi na kuihifadhi kwa ajili ya siku hii, ili kwamba aweze kumkusanya Bibi-arusi Wake pamoja kama Jamii Moja. Bibi-arusi yeye ataliona na kulitambua Hilo kuwa NJIA PEKEE Yeye anayoweza kumkusanya Bibi-arusi Wake pamoja.
Yeye alilifanya hilo zaidi ya miaka 60 iliyopita ili kutuonyesha sisi jinsi gani ambavyo Yeye angelifanya hilo leo. Sisi ni “moja ya makanisa yake kwenye muunganisho wa simu”
Kama mimi siamini kwenda kanisani, basi kwa nini niwe na makanisa? Tulikuwa nayo kila mahali nchini, yameunganishwa hivi majuzi usiku, kila maili mia mbili mraba kulikuwapo na kanisa langu.
Wahudumu wengi huyaambia makanisa yao kuwa kwenye “muunganisho wa simu” au “kusikiliza hewani”, “kuusikiliza Ujumbe mmoja kwa wakati mmoja”, ati sio kwenda kanisani. YEYE AMETOKA KUSEMA HUKO NI KWENDA! Wao ni kwamba tu aidha hawalijui Neno ama hawawezi kuisoma barua ya mahaba kama vile Bibi-arusi awezavyo.
Kanisa ni nini? Hebu na tuone kile Ndugu Branham alichosema kanisa lilicho.
Makusanyiko mengi, mengi yamepata makao haya kama mlivyokuwa nayo hapa kutoka maskani. Pia imeunganishwa huko Phoenix, ya kwamba kila mahali ibada zilipo, inaingia moja kwa moja kwenye…Na wanakusanyika makanisani na majumbani, na mambo kama hayo, kupitia wimbi zuri sana.
Ndugu Branham anasema waziwazi kwamba watu wakiwa “majumbani” mwao na “mambo kama hayo” walikuwa ni moja ya makanisa yake kwenye muunganisho wa Simu. Kwa hivyo majumba, vituo vya mafuta, majengo, familia zilizokusanyika pamoja kwenye muunganisho wake wa simu hilo liliwafanya kuwa kanisa.
Hebu na tuisome kidogo zaidi BARUA YA MAHABA.
Tunayaombea makanisa yote na makusanyiko ambayo yamekusanyika kuzunguka vile—vile—vile vipaza sauti vidogo nchini kote, kutoka kwenye taifa, kote kote hata kwenye Pwani ya Magharibi, kule juu kwenye milima ya Arizona, chini kwenye mabonde ya Texas, mbali sana hata Pwani ya Mashariki, nchini kote, Bwana, ambako wao wamekutanika. Tuko umbali wa masaa mengi, bali, Bwana, sisi tuko pamoja usiku wa leo kama jamii moja, waamini, tukingojea kuja kwa Masihi.
Kwa hivyo wakiwa kwenye Muunganisho wa Simu, wakimsikiliza Ndugu Branham WOTE KWA WAKATI MMOJA; walikuwa pamoja kama jamii moja, waamini, wakingojea Kuja kwa Masihi.
Lakini ninyi mnasema ukifanya hivyo leo, huko sio kwenda kanisani, ati ni makosa, sio kukusanyika pamoja na zaidi sana tunapoona ile siku ikikaribia, huko sio kwenda kanisani?
Hebu niwaulizeni swali nanyi myajibu makusanyiko yenu. Kama Ndugu Branham angekuwa hapa leo, katika mwili, nanyi mngeweza kusikiliza hewani au kujiunganisha kwa simu ili kumsikiliza yeye kila Jumapili asubuhi, wote kwa wakati mmoja pamoja na Bibi-arusi kote ulimwenguni, enyi wachungaji, Je! mngeweza KUJIUNGANISHA KWA SIMU na kumsikia Ndugu Branham au mngehubiri?
Ndugu Branham anasema waziwazi wajibu wako ni kanisa lako. Kama ungekuwa hapa miaka 60 iliyopita naye Ndugu Branham alikuwa na ibada, lakini kanisa lako halingehudhuria bali lilikuwa na ibada yao wenyewe (jambo ambalo wahudumu wengi walilifanya wakati huo), Je, wewe ungeweza kwenda kwenye “kanisa lako”, au ungeenda kwenye “Maskani ya Branham” kumsikiliza Ndugu Branham?
Nitawapa jibu langu. Mimi ningekuwa nikisimama mlangoni kwenye mvua, theluji au tufani ya theluji ili niingie Maskanini kumsikiliza nabii wa Mungu. Kama NINGEKUWA nikienda kwenye lile kanisa lingine, ningeyabadilisha makanisa usiku huo.
Lakini mwanamke yule, hakujua kama nguvu zilikuwa katika ile fimbo ama la, bali yeye alijua Mungu alikuwa ndani ya Eliya. Hapo ndipo yule Mungu alipokuwa: ndani ya nabii Wake. Akasema, Kama Bwana aishivyo, na nafsi yako iishivyo, sitakuacha.
Ninawaalika kuungana nasi na kuwa moja ya makanisa ya Ndugu Branham kwenye muunganisho wa simu siku ya Jumapili saa 6:00 MCHANA, masaa ya Jeffersonville,(Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapoisikia Sauti ya Mungu ikituletea Ujumbe: Mahali Pekee Palipowekwa Na Mungu Pa Kuabudia 65-1128M.
Leo, Maneno haya Mungu aliyoyanena kupitia Malaika-Mjumbe Wake wa Saba yangali yanatimia kupitia SISI, BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.
Kama mimi siamini kwenda kanisani, basi kwa nini niwe na makanisa? Tulikuwa nayo kila mahali nchini, yameunganishwa kwa simu hivi majuzi usiku, kila maili mia mbili mraba kulikuwapo na kanisa langu.
Walikuwa katika makanisa, majumbani, majengo madogo, na hata kituo cha mafuta; wakiwa wametawanyika kote Marekani, wakisikiliza, wote kwa wakati mmoja Neno lilikuwa likitoka.
Na leo hii, sisi tungali ni MOJA YA MAKANISA YAKE. Yeye ANGALI NI MCHUNGAJI WETU. Neno Lake LINGALI HALIHITAJI FASIRI YOYOTE, nasi TUNGALI tumekusanyika ulimwenguni kote, TUMEUNGANISHWA KWA SIMU, tukiisikiliza SAUTI ya Mungu ikimkamilisha Bibi-arusi wa Yesu Kristo.
Leo, Neno hili lingali linatimia.
Kwa nini wao walifanya hivyo wakati huo? Kwa nini wachungaji waliyafunga makanisa yao ili kuusikia Ujumbe moja kwa moja? Wao wangeweza kusubiri tu wazipate kanda, kisha wakahubiri Ujumbe wao wenyewe kwa watu wao baadaye; nami nina hakika wengi wasio na Ufunuo walifanya hivyo.
Au labda wengine waliyaambia makusanyiko yao, “Sasa sikilizeni, sisi tunaamini Ndugu Branham ni nabii wa Mungu, lakini yeye hakusema tunatakiwa kumsikiliza yeye katika makanisa yetu. Mimi ninahubiri Jumapili hii, na kila Jumapili; ninyi zichukueni tu kanda na mzisikilize huko majumbani mwenu.”
Bibi-arusi wakati ule, ni kama tu Bibi-arusi sasa hivi, walikuwa na Ufunuo, nao walitaka kuisikia Sauti ya Mungu moja kwa moja wao wenyewe. Walitaka kuungana na Bibi-arusi kote nchini waisikie Sauti ya Mungu ilipokuwa ikitoka. Wao walitaka kutambulishwa kama moja ya makanisa yake, majumba, ama po pote walipokuwa, na Ujumbe, Sauti, na sasa, kanda.
Leo, Neno hili lingali linatimia.
Kwa nini wao/sisi Tunaliona na wengine hawalioni? Kwa kujua tangu zamani, sisi tulichaguliwa kuliona Hili. Lakini ninyi ambao hamkuchaguliwa, kamwe hamtaliona. Ngano inaliona nayo imeanza kuondoka.
Haimaanishi kwamba unapaswa kuacha kwenda kwenye kanisa lako. Wala haimaanishi mchungaji wako aache kuhudumu. Inamaanisha tu kwamba wahudumu wengi na wachungaji wengi wamesahau JAMBO KUU, nao hawawaambii watu wao SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI mnayopaswa kuisikia ni SAUTI ya Mungu iliyo kwenye kanda.
Kwenda kanisani kila siku ya kila wiki hakukufanyi wewe kuwa Bibi-arusi; hayo si matakwa ya Mungu. Mafarisayo na Masadukayo walikuwa na mafundisho hayo. Walijua kila herufi ya kila Neno, bali Neno lililo Hai lilikuwa limesimama PAPO HAPO katika mwili wa mwanadamu, lakini wao walifanya nini? Jambo lile lile wafanyalo wengi leo.
Wao watasema, “hayo yalikuwa ni madhehebu aliyokuwa akizungumzia. Ambao hawangemruhusu Ndugu Branham kuhubiri makanisani mwao, bali sisi tunalihubiri Neno na tunasema vile tu yeye alivyosema.”
Hilo ni zuri. Bwana asifiwe. Hivyo ndivyo unavyopaswa kufanya. Lakini kisha useme, leo ni tofauti, ni makosa kuzicheza kanda za Ndugu Branham katika kanisa lako. Wewe hauna tofauti na Mafarisayo na Masadukayo, au madhehebu.
Wewe ni mnafiki.
Kama ilivyokuwa wakati huo, ni Yesu, akisimama mlangoni akibisha, akijaribu kuingia ndani anene moja kwa moja na Kanisa Lake, nao hawataifungua milango yao, nao hawatazicheza kanda katika makanisa yao. “Yeye haji katika kanisa letu ahubiri”.
Adui atageuza hilo na kulizungusha katika pande nyingi sana kwani ANACHUKIA kufichuliwa, lakini hata hivyo, linadhihirishwa mbele ya macho yetu na wengi wanajiondokea.
“Hapo mwanzo kulikuwako” [kusanyiko linasema, “Neno!”—Mh.] “Naye Neno alikuwako kwa” [Kusanyiko linasema “Mungu!”—Mh.] “Naye Neno alikuwa” [Kusanyiko linasema “Mungu!”—Mh.]. “Naye Neno alifanyika mwili akakaa kwetu.” Hiyo ni kweli? Sasa tunaona Neno lile lile lililoahidiwa, la Luka, la Malaki, ahadi hizi nyingine zote za siku ya leo, zikifanyika mwili, zikikaa kati yetu, ambazo tulisikia kwa masikio yetu; sasa tunamwona Yeye (kwa macho yetu) akifasiri Neno Lake Mwenyewe, hatuhitaji fasiri yo yote ya mwanadamu. Ee kanisa la Mungu Aliye Hai! mlio hapa na kwenye simu! amkeni upesi, kabla hamjachelewa sana!
Ifungueni mioyo yenu na msikie yale ambayo Mungu ametoka kuwaambieni, makanisa yake yote. Sasa tunamwona YEYE, kwa macho yetu, AKILIFASIRI NENO LAKE MWENYEWE. Hatuhitaji fasiri yoyote ya mwanadamu!! AMKENI KABLA HAMJACHELEWA!!
Tumeyasikia mambo haya maisha yetu yote yale yaliyokuwa yanaenda kutukia katika wakati wa mwisho. Sasa tunaliona kwa macho yetu hilo likitukia.
Yeye Alituambia, KUNA NJIA MOJA PEKE YAKE, AMBAYO NDIYO NJIA YA MUNGU ILIYOANDALIWA ALIYOIFANYA KWA AJILI YA BIBI-ARUSI WAKE. LAZIMA UKAE NA SAUTI YA MUNGU ILIYO KWENYE KANDA.
Ninaualika ulimwengu mzima uje kuungana nasi Jumapili saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) na kuisikia Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii. Kisha wewe pia unaweza kusema, “Nimesikia habari Zako, bali sasa Ninakuona”.
Ndugu. Joseph Branham
Ujumbe: 65-1127E Nimesikia Bali Sasa Ninaona
Maandiko
Mwanzo 17 Kutoka 14:13-16 Ayubu sura ya 14 na 42:1-5 Amosi 3:7 Marko 11:22-26 na 14:3-9 Luka 17:28-30
Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukusanyike pamoja Jumapili saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni Saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) kusikia 65-1127B – Kujaribu Kumtumikia Mungu Bila Ya Kuwa Ni Mapenzi ya Mungu.
Haleluya! Udongo wa kuzalia wa mioyo yetu umetayarishwa kwa kulisikia Neno na imefunuliwa kwetu, SISI NDIYE Bibi-arusi mwadilifu wa Kristo; mwana wa Mungu wa thamani, mwadilifu, asiye na dhambi, akisimama pamoja na Bibi-arusi Neno msafi, asiyeghoshiwa, aliyeoshwa kwa Maji ya Damu Yake Mwenyewe.
Sisi tumekuwa Neno lililodhihirishwa lililofanyika mwili, ili Yesu apate kutuchukua sisi, ambao Yeye alitangulia kuwachagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, katika kifua cha Baba.
Ulimwengu unaweza kuona kule kudhihirishwa kwa Imani yetu kulingana na jinsi tulivyokuwa tukitenda, na kudhihirisha ya kwamba tunao Ufunuo wa kweli kutoka kwa Mungu wa Neno Lake lililothibitishwa, nasi hatuogopi. Hatujali kile ulimwengu mzima unachosema ama unachoamini…SISI HATUOGOPI. Kubonyeza Play ndiyo njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya Bibi-arusi wa Yesu Kristo.
Kuna wengi wanaosema wanauamini Ujumbe huu wa wakati wa mwisho, wanaamini kwamba Mungu alimtuma nabii, wanaamini William Marrion Branham alikuwa malaika-mjumbe wa saba, wanaamini kwamba alinena Bwana Asema Hivi, lakini wao HAWAAMINI kwamba Sauti ndiyo sauti iliyo muhimu zaidi unayopaswa kuisikia. Wao hawaamini kuwa yeye alinena Maneno ya kutokosea. Hawaamini kuzicheza kanda katika makanisa yao.
Hiyo inamaanisha nini? INAMAANISHA HILO HALIJAFUNULIWA KWAO!
Ni ufunuo. Yeye amekufunulia jambo fulani kwa neema Yake. Hakuna kitu ulichofanya. Hukujitahidi upate imani. Kama ukiwahi kuwa na imani, umepewa hiyo kwa neema ya Mungu. Na Mungu anakufunulia, kwa hiyo imani ni ufunuo. Na Kanisa lote la Mungu limejengwa juu ya ufunuo.
Kwa IMANI imefunuliwa kwetu ya kwamba Ujumbe huu ndiyo Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda ambayo imerekodiwa, na kuhifadhiwa, ili kumlisha na kumkamilisha Bibi-arusi wa Yesu Kristo.
Ni IMANI ya kweli, isiyoghoshiwa katika yale Mungu aliyosema kwamba ni Kweli. Nayo imetia nanga ndani ya moyo na nafsi yetu na hakuna kitu kitakachoitikisa. Itakaa papo hapo mpaka nabii Wake atakapotutambulisha kwa Bwana wetu.
Hatuwezi kufanya vinginevyo. Yeye alitutayarisha sisi kulipokea na kuliamini Hilo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Yeye alijua sisi tungeipokea Sauti Yake katika wakati huu. Alitangulia kutujua tangu zamani na akatuchagua tangu asili kuipokea.
Basi, kazi ambazo Roho Mtakatifu anazifanya siku hizi, kwa maono haya yasiyoshindwa, ahadi zisizoshindwa, ishara zote za kimitume zilizoahidiwa katika Biblia, za Malaki 4, na, loo, Ufunuo 10:7, yote hayo yanatimia; na kuthibitishwa kisayansi, kwa njia yoyote ile. Na kama sijawaambia Kweli, mambo haya hayangetendeka. Lakini kama nimewaambia Kweli, yanashuhudia ya kwamba nimewaambia Kweli. Angali ni yeye yule jana, leo, na hata milele, na madhihirisho ya Roho Wake yanamnyakua Bibi-arusi. Hebu imani hiyo (ufunuo) iangukie ndani ya moyo wako, ya kwamba “Hii ndiyo ile saa.”
Hii ndiyo ile saa yenyewe. Huu ndio Ujumbe wenyewe. Hii ndiyo Sauti ya Mungu inayomwita Bibi-arusi wa Yesu Kristo. Loo, Ewe Kanisa, Bwana na auandae udongo wa kuzalia wa moyo wako upate kuwa na Imani na akufunulie ya kwamba kuisikiliza Sauti hii, kwenye kanda, ndiko kutamkamilisha na kumuunganisha Bibi-arusi wa Yesu Kristo.
Ninawaalika kwa mara nyingine tena mje kuungana nasi Jumapili saa 06:00 MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) kuipeleka IMANI yako ifike mahali pa juu, na kuketi pamoja nasi katika ulimwengu wa roho tunapoisikia Sauti ya Mungu ikitutayarisha kwa ajili ya ujio Wake wa hivi karibuni.
Ndugu. Joseph Branham
Tafadhali iweni katika maombi kwa ajili yetu wiki ijayo tunapoianza Kambi yetu ya kwanza ya Still Waters.
Ujumbe: Kazi Ni Imani Katika Matendo 65-1126 (Matendo Ni Imani Iliyodhihirishwa)
Hakuna njia ya kulikwepa, wewe ni Jeni ya Kiroho ya Mungu, dhihirisho la sifa za mawazo Yake, nawe ulikuwa ndani Yake kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
Hatuwezi kwenda zaidi, tunafanana kabisa na punje ile ile iliyoingia ardhini. Sisi ni Yesu yeye yule, katika mfano wa Bibi-arusi, tukiwa na nguvu zile zile, Kanisa lile lile, Neno lile lile linaloishi na kukaa ndani yetu, linafikia kilele chake, TAYARI KWA UNYAKUO.
Yeye alituambia tulivunja ndoa yetu ya kwanza, kwa mauti ya kiroho, na sasa tumezaliwa mara ya pili, ama tumeolewa tena, kwenye ndoa yetu mpya ya Kiroho. Si ya maisha yetu ya kimaumbile ya kale na mambo ya ulimwengu, bali ni ya Uzima wa Milele. Ile chembe hai iliyokuwa ndani yetu hapo mwanzo, imetupata!
Hilo linamaanisha nini? Linamaanisha kitabu chetu cha zamani kimetoweka pamoja na ndoa yetu ya zamani, kimehamishwa. SASA kiko katika “Kitabu Kipya” cha Mungu; si kitabu cha uzima… la, la, la… bali katika Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo. Kile Mwanakondoo alichokomboa. Ndicho cheti chetu cha ndoa ambapo Chembechembe yetu ya kweli ya uhai ya Milele inakaa.
Je! uko tayari? Hili hapa laja. Afadhali ujifinye na kujitayarisha kupaza sauti na kupiga kelele utukufu, haleluya, Bwana asifiwe, lina mitutu miwili na risasi za mbinguni.
“Unataka kuniambia ya kwamba kitabu changu cha zamani pamoja na makosa yangu yote na kushindwa kwangu kote…”
Mungu alikiweka kwenye Bahari ya Usahaulifu Wake, nawe si tu kwamba umesamehewa, bali umehesabiwa haki…Utukufu! “Umehesabiwa haki.”
Na hilo linamaanisha nini? Linamaanisha wewe hata hukuwahi kulitenda jambo hilo Machoni pa Mungu. Unasimama mkamilifu mbele za Mungu. UTUKUFU! Yesu, Neno, alipachukua mahali pako. Yeye alifanyika wewe, ili wewe, mwenye dhambi mchafu, upate kufanyika Yeye, NENO. Sisi ni NENO.
Hilo linatufanya sisi ile Chembechembe Yake ndogo ya uhai iliyokusudiwa tangu mwanzo. Sisi ni Neno likija juu ya Neno, juu ya Neno, juu ya Neno, juu ya Neno, nasi tunafikia kimo kikamilifu cha Kristo kusudi Yeye apate kuja kutuchukua tuwe Bibi-arusi Wake.
Nini kinachotendeka SASA HIVI?
Ni Muungano Usioonekana wa Bibi-arusi wa Kristo wakikusanyika kulizunguka Neno, kutoka ulimwenguni kote.
Hili linaenda kote nchini. Huko New York, sasa ni saa tano na dakika ishirini na tano. Juu kule Philadelphia na karibu kote kule, hao watakatifu wapendwa wanaoketi kule wakisikiliza, sasa hivi, katika makanisa kila mahali. Huko juu kabisa, huko chini kabisa karibu na Mexico, huko juu kabisa karibu na Canada na kila mahali, kotekote. Maili mia mbili, popote pale katika bara la Marekani ya Kaskazini hapa, karibu yote, watu wako chonjo, wakisikiliza hivi sasa. Maelfu mara maelfu, wakisikiliza.
Na huo ndio Ujumbe wangu kwenu, enyi Kanisa, ninyi ambao ni muungano, muungano wa kiroho kwa Neno.
Yeye alisema ulikuwa ni muungano wa kiroho wa Kristo na Kanisa Lake, Nao UNATENDEKA SASA HIVI. Mwili unafanyika Neno, nalo Neno linafanyika mwili. Tumedhihirishwa, na kuthibitishwa; vile vile hasa Biblia ilivyosema ingetendeka katika siku hii, Nalo linatendeka sasa, siku baada ya siku katika kila mmoja wetu.
Mungu anaenda kuwa na Kanisa adilifu. Bibi-arusi Neno Wake mkweli na mwaminifu. SISI NDIO BIBI MTEULE wa Bwana wetu Yesu Kristo.
Ni Saa Ngapi, Bwana?
Tuna ufunuo katika siku hizi za mwisho, kwa ajili ya Ujumbe wa Bwana Mungu kumkusanya Bibi-arusi Wake pamoja. Hakuna wakati mwingine ambao umeahidiwa hilo. Imeahidiwa katika wakati huu: Malaki 4, Luka 17:30, Yohana Mtakatifu 14:12. Yoeli 2:38. Ahadi hizo ni kama tu vile Yohana Mbatizaji alivyojitambulisha katika Maandiko.
Ni nani aliyeyatimiza maandiko haya?
Malaika Wake wa saba mwenye nguvu, William Marrion Branham. Daima alifanya jambo hilo kwa mpangilio. Alilifanya kila wakati kwa mpangilio. Yeye analifanya tena katika siku yetu, akimwita atoke na kumkusanya Bibi-arusi Wake mwadilifu katika siku ya mwisho kwa nabii Wake.
Ni wakati mtukufu jinsi gani ambao Bibi-arusi alionao. Kila kukusanyika kunakuwa kukuu zaidi na zaidi na kutamu zaidi na zaidi. Hakujawahi kuwa na wakati kama huu. Mashaka yote yametoweka.
Njoo uungane nasi tunapomsikia Neno lililoahidiwa la siku yetu akinena, na kutuambia sisi ni nani na kipi kinachotukia katika siku yetu. Muungano Usioonekana wa Bibi-arusi wa Kristo 65-1125.
Sasa Mungu daima amewatuma viongozi Wake, Yeye daima hajakosa kuwa na kiongozi, katika nyakati zote. Mungu daima amekuwa na mtu fulani aliyemwakilisha katika dunia hii, katika nyakati zote.
Mungu hataki sisi tutegemee akili zetu au mawazo yoyote yaliyobuniwa na mwanadamu. Ndiyo maana Yeye humtumia Bibi-arusi Wake Kiongozi; kwa kuwa yeye ana fahamu, jinsi ya kwenda na nini cha kufanya. Mungu HAJAWAHI KAMWE KUBADILI mpango Wake. Yeye hajashindwa kamwe kuwatumia watu Wake Kiongozi, bali huna budi kumkubali Kiongozi huyo.
Huna budi kuamini kila Neno Yeye analosema kupitia Kiongozi Wake. Huna budi kwenda njia Kiongozi Wake anayosema uende. Ukipata kusikiliza na kuamini sauti zingine kama kiongozi wako, mwishowe utapotea tu.
Yohana Mtakatifu 16 inasema Yeye alikuwa na mambo mengi ya kutuambia na kutufunulia, hivyo Yeye angemtuma Roho Wake Mtakatifu Kutuongoza na kutuambia. Alisema Roho Mtakatifu ndiye nabii-kiongozi wa kila kizazi. Hivyo, manabii Wake walitumwa kumwakilisha Roho Mtakatifu ili kumwongoza Bibi-arusi Wake.
Roho Mtakatifu anatumwa kuliongoza kanisa, si kundi fulani la watu. Roho Mtakatifu ndiye hekima yote. Mwanadamu huwa mgumu, asiyejali.
Si huyo mtu, bali ni Roho Mtakatifu NDANI ya mtu huyo. Mtu Aliyemchagua kujiwakilisha Mwenyewe na kuwa kiongozi wetu wa duniani ambaye anaongozwa na Kiongozi wetu wa Mbinguni. Neno linatuambia hatuna budi kumfuata Kiongozi huyo. Haidhuru tunafikiri nini, yale yanayoonekana ni ya maana, au kile mtu mwingine asemacho, sisi hatuwezi kupambanua jambo hilo, kiongozi ndiye tu anayeweza.
Mungu hutuma Kiongozi, naye Mungu anataka mkumbuke ya kwamba huyo ni Kiongozi Wake aliyemchagua.
Nabii-kiongozi wetu amechaguliwa na Mungu kulinena Neno Lake. Neno lake ni NENO LA MUNGU. Nabii- kiongozi, na yeye peke yake, ndiye aliye na fasiri ya kiungu ya Neno. Mungu alilinena Neno Lake kwake mdomo kwa sikio. Kwa hivyo, huwezi kupinga, kubadilisha, au kulihoji Neno la Kiongozi wako.
Lazima umfuate Yeye, na Yeye peke yake. Usipofanya hivyo, mwishowe utapotea. Kumbuka, unapomwacha, Kiongozi aliyechaguliwa na Mungu, unakuwa peke yako, kwa hiyo sisi tunataka kuwa karibu na kiongozi Aliyemchagua, na kusikia na kutii kila Neno Yeye analolisema kupitia yeye.
Kiongozi wetu ametufundisha kwamba agano la kale lilikuwa kivuli cha agano jipya.
Israeli walipotoka Misri wakienda kwenye ile nchi ya ahadi, katika Kutoka 13:21, Mungu alijua ya kwamba wao hawajapita njia hiyo hapo kabla. Ilikuwa tu maili arobaini, bali hata hivyo walihitaji kitu fulani cha kwenda pamoja nao. Wangepotea njia. Kwa hiyo Yeye, Mungu, akawatumia Kiongozi. Kutoka 13:21, kitu kama hiki, “Ninamtuma Malaika Wangu aende mbele zenu, ile Nguzo ya Moto, ili awalinde njiani,” kuwongoza kwenye nchi hii ya ahadi. Nao wana wa Israeli wakamfuata Kiongozi yule, ile Nguzo ya Moto (usiku), Wingu mchana. Wakati iliposimama, wao wakasimama. Wakati iliposafiri, wao wakasafiri. Basi Yeye alipowafikisha karibu na ile nchi, nao hawakuwa wanastahili kuvuka, Yeye aliwaongoza akawarudisha jangwani tena.
Alisema hilo ni kanisa leo hii. Tungekuwa tayari tumekwishaondoka kama tu tungejisahihisha wenyewe na kujiweka sawa, bali Yeye hana budi kuzidi kutuongoza kuzunguka na kuzunguka na kuzunguka.
Wao walipaswa tu kumfuata kiongozi wao kama vile YEYE ALIVYOIFUATA na kusikia kutoka kwenye ile Nguzo ya Moto. Yeye aliwaambia yale Mungu aliyosema nao walipaswa kutii kila Neno yeye alilosema. Yeye alikuwa ndiye Sauti ya yule Kiongozi. Lakini wao walihoji na kubishana na yule kiongozi aliyechaguliwa na Mungu, hivyo wakatangatanga nyikani kwa miaka 40.
Kulikuwa na wahudumu wengi katika siku za Musa. Mungu alikuwa amewachagua kuwasaidia hao watu, kwa vile Musa asingeweza kufanya yote. Lakini wajibu wao ulikuwa ni kuwaelekeza watu kwenye yale Musa aliyosema. Biblia haisemi chochote kile hao watu walichosema, inasema tu yale Musa aliyosema kuwa ndilo Neno la kuwaongoza hao watu.
Wakati Mungu alipomwondoa Musa jukwaani, Yoshua alitawazwa kuwaongoza hao watu, ambalo inamwakilisha Roho Mtakatifu leo. Yoshua hakuhubiri jambo lolote jipya, wala yeye hakujaribu kupachukua mahali pa Musa, wala hakujaribu kufasiri kile kiongozi alichosema; yeye aliyasoma tu yale Musa aliyosema na kuwaambia watu, “Kaeni na Neno. Kaeni na yale Musa aliyosema”. Yeye aliyasoma tu yale Musa aliyosema.
Ni mfano mkamilifu jinsi gani wa leo hii. Mungu alimthibitisha Musa kwa Nguzo ya Moto. Nabii wetu alithibitishwa kwa Nguzo ile ile ya Moto. Maneno ambayo Musa aliyoyanena yalikuwa ni Neno la Mungu na yakawekwa ndani ya lile Sanduku. Nabii wa Mungu alinena katika siku yetu na Hilo liliwekwa kwenye kanda.
Wakati Musa alipoondolewa jukwaani, Yoshua alitawazwa kuwaongoza hao watu kwa kuyadumisha Maneno aliyoyanena Musa mbele yao. Aliwaambia waamini na wadumu na kila Neno lililonenwa na kiongozi wa Mungu.
Yoshua aliyasoma kila mara yale Musa aliyoyaandika Neno kwa Neno kutoka kwenye magombo. Yeye aliliweka Neno mbele yao daima. Neno la siku yetu halikuandikwa, bali lilirekodiwa ili Roho Mtakatifu aweze kumfanya Bibi-arusi Wake asikie Neno kwa Neno kile Yeye alichosema, kwa Kubonyeza Play.
Mungu kamwe habadilishi mpango Wake. Yeye ndiye Kiongozi wetu. Sauti Yake ndiyo inayomwongoza na kumuunganisha Bibi-arusi Wake leo. Sisi tunataka tu kuisikia Sauti ya Kiongozi wetu vile Inavyotuongoza kwa Nguzo ya Moto. Ni muungano usioonekana wa Bibi-arusi wa Kristo. Tunaijua Sauti Yake.
Wakati kiongozi wetu anapokuja mimbarani, Roho Mtakatifu anamshika na Si yeye tena, bali ni yule Kiongozi wetu. Anakiinua kichwa chake hewani na kupaza sauti, “Bwana Asema Hivi, Bwana Asema Hivi, Bwana Asema Hivi! Na kila mshiriki wa Bibi-arusi wa Kristo kote ulimwenguni huja moja kwa moja kwake. Kwa nini? TUNAMJUA KIONGOZI WETU KWA JINSI TU YEYE ANAVYOONGEA.
Kiongozi wetu = Neno Neno = Humjia nabii Nabii = Mfasiri pekee wa kiungu wa Mungu; kiongozi Wake wa duniani.
Kaeni nyuma ya Neno! Loo, naam, bwana! Kaeni na Kiongozi huyo. Kaeni vema sawasawa nyuma Yake. Msiende mbele Yake, kaeni nyuma Yake. Hebu Hilo na liwaongoze, msiliongoze. Liachilieni liende.
Ndugu. Joseph Branham
Ujumbe:
62-1014E – Kiongozi
Maandiko:
Marko 16:15-18 Yohana Mtakatifu 1:1 / 16:7-15 Matendo 2:38 Waefeso 4:11-13 / 4:30 Waebrania 4:12 2 Petro 1:21 Kutoka 13:21
Sauti tunayoisikia kwenye kanda ndio Urimu na Thumimu ya Mungu kwa Bibi-arusi Wake. Hiyo sasa imemuunganisha sawasawa pamoja Bibi-arusi Wake katika moyo mmoja na nia moja kuwa kanisa halisi lililojazwa na Roho, lililojaa nguvu za Mungu, linaloketi pamoja katika katika mahali pa kimbinguni, likitoa dhabihu za kiroho, sifa za Mungu, huku Roho Mtakatifu akitembea kati yetu.
Kristo alitutumia sisi Roho Wake Mtakatifu anene kupitia malaika Wake wa saba ili atujenge sisi kama watu binafsi tufikie kiwango cha Yesu Kristo, kusudi tupate kuwa kituo cha nguvu na makao ya Roho Mtakatifu, kwa Neno Lake.
Sisi ni warithi wa kila kitu. Ni mali yetu binafsi, hiyo ni MALI YETU sisi. Ni zawadi ya Mungu kwetu, na hakuna mtu anayeweza kuichukua kutoka kwetu. NI YETU.
“Lolote mtakalomwomba Baba katika Jina Langu, hilo nitalifanya.” Nani awezaye kukana lolote hapo? “Amin, amin, nakuambia, ukiuambia mlima huu, Ng’oka, wala usitie shaka moyoni mwako, bali waamini kwamba hayo uliyosema yatatukia, lolote ulilosema litakuwa lako.” Ni ahadi zilizoje! Haziishii tu kwenye uponyaji, lakini kwa lo lote.
Utukufu kwa Mungu…LOLOTE TUOMBALO!
Tangu mwanzo wa wakati, viumbe vyote vya Mungu vimekuwa vikiugua na kuingojea siku ambayo wana wakamilifu wa Mungu watakapodhihirishwa. Siku hiyo imefika. Hii ndiyo siku hiyo. Huu ndio huo wakati. Sisi ndio hao wana na binti za Mungu waliodhihirishwa.
Sisi ni chombo kilicho hai cha Mungu anachotembelea, anachoona nacho, anachotumia kuzungumza, anachofanyia kazi. Ni Mungu akitembea kwa miguu miwili NDANI YETU.
Sisi tu nyaraka Zake zilizoandikwa zinazosomwa na watu wote. Wana na binti Zake wenye mamlaka waliochaguliwa, waliochaguliwa tangu zamani, anaowafanya kuwa mtu aliye hai, sanamu hai, kimo cha mtu mkamilifu.
Tunaanguka kifudifudi mbele ya Mungu aliye hai, nguvu zilizo hai, maarifa hai, saburi hai, utauwa hai, Nguvu hai zitokazo kwa Mungu aliye hai, zinamfanya mtu aliye hai kuwa sanamu hai katika kimo cha Mungu.
Ni Kristo, katika utu wa Roho Mtakatifu juu yetu, pamoja na ubatizo wa kweli wa Roho Wake Mtakatifu, na Wema Wake wote ukiwa umetiwa muhuri ndani yetu. Mungu, akiishi ndani yetu katika Maskani iitwayo Jengo. Maskani iliyo hai, ya mahali pa kukaa Mungu aliye hai; Kanisa kamilifu, kwa ajili ya Jiwe Kamilifu la Kifuniko la kutufunika.
Mungu alimtuma nabii kumwita Bibi-arusi Wake atoke na kumwongoza. Ilikuwa ni Adamu Wake wa kwanza aliyerejeshwa kikamilifu, kimo cha mtu mkamilifu katika siku yetu, kulifunua Neno Lake kwa Bibi-arusi Wake. Siwezi kuondoshwa kwenye hilo. Hakuna kinachoweza kuniondosha. Sijali mtu ye yote anasema nini; halinisogezi hata kidogo. Nitashikilia papo hapo.
Nitangoja, nitangoja, nitangoja. Haileti tofauti yo yote. Inashikilia pale pale. Kisha, siku moja, nitapiga kelele pamoja na watakatifu wengine wote kwa moyo mmoja: “Tunapumzika kwa uhakika juu ya kila Neno!
Ninaahidi, asubuhi ya leo, Kwake, kwa moyo wangu wote, ya kwamba, kwa masaada Wake na kwa neema Yake, ninaomba ya kwamba nitaomba kila siku, bila kukoma, mpaka nitakaposikia kila moja ya mahitaji haya yakitiririka katika maskini mwili wangu huu, mpaka niweze kuwa dhihirisho la Kristo aliye hai.
KWANGU MIMI, kuisikiliza Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda ndio mpango wa Mungu kwa ajili ya siku hii. Ndilo Neno lililo hai la Yesu Kristo. Ndio Yakini yangu kulingana na Neno la Mungu. Ndio njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii.
Hivyo, ningependa kuwaalika kuungana nami Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) ninapomsikiliza William Marrion Branham, ambaye ninaamini kuwa ndiye Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku yetu, akimfundisha Bibi-arusi wa Kristo jinsi ya kuwa: Kimo Cha Mtu Mkamilifu 62-1014M.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko ya kusoma kabla ya Ujumbe:
Mathayo 5:48 Luka Mtakatifu 6:19 Yohana Mtakatifu 1:1 / 3:3 / 3:16 / 5:14 / 14:12 Matendo 2:38 / 7:44–49 / Sura ya 10 / 19:11 / 28:19 Waefeso 4:11-13 Wakolosai Sura ya 3 Waebrania 10:5 / 11:1 / 11:32-40 Yakobo 5:14 2 Petro 1-7 Isaya 28:19
Kwa Kubonyeza Play, tunalisikiliza Neno la Mungu lisilokosea. Ni kila Neno Kweli, kila kifungu Chake. Tumeitwa na kuhifadhiwa, tumejazwa na kutengwa; tumejazwa na Roho Mtakatifu, na sasa tayari tuko katika Nchi ya Kanaani. Hatuogopi cho chote…LO LOTE LILE, tunajua sisi ni nani.
Kwa sababu tumedumu na Neno Lake, kama alivyotuamuru kufanya, Anaenda kutuambia kwamba alituachia sisi urithi. Ulilifanya jambo hilo lini, Baba? Nilipowachagua ninyi na kuyaweka majina yenu kwenye Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
Wakati utimilifu wa wakati ulipowadia, nilimtuma Yesu Mwana-Kondoo, Aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili muupate urithi wenu wa kuwa wana na binti Zangu, miungu wadogo.
Ilinibidi niwakague mitikisiko na sehemu zilizolegea kabla sijawaweka mahali penu.
● “Je! Unaamini kuicheza Sauti Yangu iliyo kwenye kanda kanisani ni makosa?”
● “Ndiyo, hupaswi kuzicheza kanda kanisani.”
● “Analikataa. Unatikisika.”
● “Je! Unaamini Neno Langu lililo kwenye kanda linahitaji kufasiriwa?”
● “Ndiyo, Linahitaji mtu fulani kulifafanua.”
● “Unatikisika. Lipige teke nje. Bado hauko tayari.”
Ukiwa tayari, utasema, “Amina” kwa kila Neno.
● “Je! Mnaamini kwamba Mimi ni yeye yule jana, leo na hata milele?”
● “Amina.”
● “Je! Mnaamini kuwa Sauti Yangu iliyo kwenye kanda ndio SAUTI ILIYO MUHIMU KULIKO ZOTE mnayopaswa kuisikia?”
● “Amina.”
● “Je! Mnaamini Sauti Yangu iliyo kwenye kanda ndio itakayomuunganisha Bibi-arusi?”
● “Amina.”
● “Je! Mnaamini kwamba malaika Wangu mwenye nguvu ndiye atakayewatambulisha ninyi Kwangu Mimi?”
● “Amina.”
Mmeanza kukazika sasa. Nimewakagua mtikisiko na maeneo yaliyolegea. Niko tayari kuufunga mlango. Nitauweka Muhuri Wangu juu yenu. Mmefuzu ukaguzi Wangu.
Sasa hebu niwaambieni jambo fulani, Enyi Watu Wangu wapendwa na wa thamani mlio katika nchi za kanda; huko nchi za ng’ambo na popote mlipo, msiogope. Kila kitu ni sawa. Niliwajua ninyi kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Nilijua mambo yote yatakayotukia.
Ninakuja kuwachukua ninyi hivi karibuni na kuwapeleka Mahali ambapo Hakuna mauti, hakuna huzuni, hakuna wivu, hakuna kitu cho chote; Ni ukamilifu tu, upendo mkamilifu.
Hadi wakati huo, msisahau kamwe, Ninawapa Neno Langu, NINYI NI NENO LANGU lililofanyika mwili. Kama mnahitaji JAMBO LOLOTE, Linene, kisha Liaminini; Ni urithi wenu.
Nitawatumia ninyi Sauti Yangu tena Jumapili hii na kuwafafanulia jambo Hilo Lote. Nitawaambia kwa mara nyingine tena ninyi ni nani, wapi mnakoelekea, na jinsi gani kulivyo kule ng’ambo, sasa hivi.
Njooni muungane na Bibi-arusi Wangu ninapowafanya wao waketi pamoja katika mahali pa Mbinguni Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) na mnisikie Mimi nikiwaweka ninyi mahali penu kwa Neno Langu. 60-0522E Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #4
Tunapobonyeza Play, ni asali mwambani, ni furaha isiyotamkika, ni dhamana iliyobarikiwa, ni nanga ya nafsi zetu, ndio tumaini na tegemeo letu, ni Mwamba wenye Imara, ni kila kitu kilicho chema, ndio Njia ya Mungu iliyoandaliwa ya siku hii.
Kwa sababu Tunabonyeza Play, Sauti ya Mungu imetuposea; imetuposa kwa Kristo, kama Bikira Safi kwa Neno Lake. Tunaye ila Mwalimu Mmoja tu, Sauti Moja, Nabii Mmoja, anayetuongoza kwa Roho Mtakatifu.
Bali hili ni kanisa, ninawafundisha. Haya yananaswa kwenye kanda. Nawataka watu wanaosikiliza kanda, wakumbuke, hili ni kwa ajili ya kanisa langu.
Ni thibitisho lililoje kwetu sisi ya kwamba tuko katika Mapenzi Yake makamilifu. Kanda hizo ni kwa ajili ya kanisa Lake. Yeye anatufundisha. Anatuambia, sikilizeni kanda.
Yeye aliuanza mfululizo huu wa Kufanywa Wana Wenye Mamlaka kwa kutueleza kile kilichotokea siku chache zilizopita. Ndipo, kwenye kila Ujumbe, yeye hunena habari za wakati alipokuwa amebadilishwa. Jinsi gani Hilo litakuwa ni muhimu kwa Bibi-arusi kusikia kile kilichotukia na kile Bibi-arusi alichomwambia yeye.
Nabii wetu atahukumiwa kwa Neno alilohubiri na kuliacha kwenye kanda. Wale Bibi-arusi kule ng’ambo ya pili walimwambia atakubaliwa na Bwana wetu. Kisha yeye atatukabidhi Kwake kama tunu za huduma yake, kisha tutarudi duniani tena tukaishi milele.
Kila Neno tunalolisikia ni kito cha thamani. Tunaendelea tu kuliweka wazi na kuliweka wazi Yeye anapozidi kufunua zaidi tunaposoma katikati ya mistari.
Jinsi gani tupendavyo kulishiriki Hilo na ndugu na dada zetu, “Je, umelisikia hili?”
“Yeye alituchagua katika Yeye kabla ulimwengu hata haujakuweko”? Huo ndio urithi wetu. Mungu alituchagua, kisha akamwacha Yesu aje alipe ile deni. Hiyo ni nini? Kumwaga Kwake kwa Damu Yake, kusudi tusihesabiwe dhambi. Hufanyi lo lote.
Kisha, mara tu baada ya hilo, Je, umelipata hili?
“Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, kwa Bwana.” Umeelekeza macho yako Kalvari, na hakuna kitu kitachokuzuia! Mwenendo wa maisha yako, unatembea katika Barabara Kuu ya Mfalme, umepakwa na Mafuta ya thamani, ukielekea kwenye Patakatifu pa patakatifu. Whiu! Amina.
Sisi tulikuwa kama ile fimbo ya Haruni, fimbo ya kale iliyokauka ambayo alikuwa ameibeba kwa miaka arobaini kule jangwani. Lakini sasa, kwa sababu tumewekwa katika Mahali pale Patakatifu kwa kuisikia Sauti ya Mungu ikinena nasi kwenye kanda, tumechipuka na kuchanua, tukiwa tumejaa Roho Wake Mtakatifu, nasi Bibi-arusi Wake tukipaza sauti kwa mapafu yetu yote.
⚪ Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, kwa Bwana, kanda ndizo nafasi ya kwanza mioyoni mwetu.
⚪ Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu kwa Bwana, Yeye alituchagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
⚪ Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, kwa Bwana, sisi ni Bibi-arusi wa Yesu Kristo.
⚪ Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, kwa Bwana, haileti tofauti yo yote yale mtu ye yote asemayo, hatuzirudishi kanda, tunazicheza nyingi zaidi.
⚪ Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, kwa Bwana, tumeyaelekeza macho yetu Kalvari, na hakuna kitu kitakachotuzuia.
Nina furaha sana kuungana moyoni na watu wengi hapa ambao wanajua kwamba Hili ni Neno la Mungu lisilokosea. Basi Hilo, Hilo ni Kweli kwa kila Neno, kila Neno Lake, kila fungu Lake. Na kwa neema ya Mungu, kama nilivyotunukiwa kuiangalia ile Nchi ambayo siku moja tutaizuru.
Njoo uungane nasi Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika) Nabii anapolichukua kila Neno na kulifafanua tu kindani. Atalipeleka hadi Mwanzo na kulifafanua kindani, na atalipeleka hadi Kutoka na kulifafanua tena, na hata hadi Ufunuo; na Ni Yesu kwa kila kipengee!