Category Archives: Uncategorized

24-0512 Maswali na Majibu #3

UJUMBE: 64-0830M Maswali na Majibu #3

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Bikira Safi,

Jinsi gani ninavyopenda kuwahimiza kila wiki Kubonyeza Play na kuisikia Sauti ya Mungu ya siku yetu. Kwa maana najua ndio Mpango mkamilifu wa Mungu kwa ajili ya siku yetu.

Si yale Joseph Branham anayosema au kuamini. Ni yale Sauti ya Mungu iliyothibitishwa ilichotuambia:

Mimi ni Sauti ya Mungu kwenu.

Ikiwa mna ufunuo wowote wa Ujumbe huu hata kidogo, nukuu hiyo ndogo inapaswa kutosha sana kwenu kumwambia kila mtu mnayekutana naye; kila mwaminio, kuyaambia makanisa yenu, Sauti hiyo ndiyo Sauti iliyo muhimu sana MNAYOPASWA KUISIKIA.

Kuwazia, Maneno yale tunayosikia tunapobonyeza Play ni Sauti ya Mungu inayozungumza nasi moja kwa moja. Baba aliamuru irekodiwe na kuhifadhiwa ili tuweze Bonyeza Play kila sekunde ya kila siku; ili tuweze kumsikia akitutia moyo, kutubariki, kututia mafuta, na kutupilia mbali hofu na mashaka yetu yote, yote kwa Kubonyeza Play tu.

Lolote tunalohitaji papo hapo, Bonyeza Play, na hilo hapo. Yupo kwa ajili ya kutukumbusha SISI NI NENO. Yuko pamoja nasi, karibu nasi, NDANI YETU. Shetani ni mwongo. Ameshindwa. Hakuna kinachoweza kuliondoa Neno hilo kutoka kwetu. Mungu alitupa Hilo kwa kujua kwake tangu zamani, akijua sisi ni Bibi-arusi Wake. Tulikuwa pamoja Naye tangu mwanzo.

Ni Sauti gani tuwezayo kuisikia ambayo ingekuwa kuu kuliko ile Sauti pekee ambayo imethibitishwa na Nguzo ya Moto kuwa ndio Sauti ya Mungu?

Hakuna Sauti nyingine.

Hiyo Sauti ilituambia nini wiki iliyopita?

Mimi kila mara huwadai ninyi kisha—kama ndugu yangu na dada. Ninyi ni watoto wangu; mi—mimi ni baba yenu katika Injili, si baba kama vile kasisi angalikuwa, mimi—mimi ni baba yenu katika Injili kama Paulo alivyosema pale. Nimewazaa ninyi kwa Kristo, na sasa na—nawaposea ninyi Kristo; hilo ni kufanya ninyi muweke nadhiri ya ndoa kwa Kristo kama bikira wasafi. Msiniaibishe! Msiniaibishe! Ninyi iweni bikira safi.

Hatuna budi kukaa bikira safi kwa Neno, hiyo Sauti. Kwetu sisi, kuna NJIA MOJA TU ya kuwa na hakika kuwa tunafanya hivyo: KUBONYEZA PLAY.

Kama mnaniamini mimi kuwa yale mnayosema, mtumishi wa Mungu, nabii, sikizeni yale ninayowaambia. Ona? Huenda msifahamu, na msipoweza, basi fanyeni tu yale ninayowaambia mfanye.

Ndiyo, kuna watu wengine waliotiwa mafuta na Roho Mtakatifu, na kwa neema na rehema za Mungu, Naomba kuwa mimi ni mmoja wa watu hao. Ninaamini kuwa nimeitwa na Yeye kulidumisha Neno Lake mbele zenu na kuwaelekeza ninyi kwenye Ujumbe huu, Neno la Mungu, ile Sauti.

Kama vile Petro alivyosema, sitazembea kuwakumbusha daima kwamba KUNA SAUTI MOJA TU ambayo Mungu aliyoiita kulifunua Neno Lake. Sauti Moja ambayo Mungu aliyoithibitisha. Sauti moja ile ambayo Mungu aliyosema, “Msikieni Yeye.” Sauti moja ile ambayo Mungu aliyosema, “Mimi ni Sauti ya Mungu kwenu.”

Kumbukeni hili kwa mioyo yenu yote: dumuni kwa Neno hilo! Msiache Neno hilo! Cho chote ambacho ni kinyume cha Hilo, kiachilie, haidhuru ni nini. Ndipo unajua ni sahihi.

Hakika ninaelewa kwa nini ninaeleweka vibaya na kwamba wengine wanahisi kuwa niko kinyume na wahudumu wote; kwamba naamini hakuna mtu anayepaswa kuhubiri. “Ukimsikiliza mhudumu mwingine isipokuwa Ndugu Branham, wewe si Bibi-arusi.” Kama nilivyosema mara nyingi, sijawahi kusema hivyo au kuamini hivyo.

Nabii alilieleza hilo kikamilifu wiki iliyopita jinsi gani kabisa Ninavyojisikia na kile Ninachoamini.

Kulikuwa na angalau makanisa mengine matatu ya Ujumbe katika eneo la Jeffersonville wakati Ndugu Branham alipokuwa hapa. Katika ibada ya Jumapili iliyopita, alisema kwamba wachungaji wa mahali hawakuwepo pale katika ibada ya jioni. Walikuwa na ibada zao wenyewe za jioni. Hivyo, hawakujisikia kuja kumsikiliza Ndugu Branham katika ibada ya jioni, bali wawe na ibada makanisani mwao. Huo ndio ulikuwa uamuzi wao na kile walichojisikia wanaongozwa kufanya, na Ndugu Branham alikubali.

Leo hii bado kuna makanisa kadhaa katika eneo la Jeffersonville. Wao pia yawapasa wafanye kama jinsi wanavyojisikia wanaongozwa na Bwana kufanya. Kama hawajisikii kuzicheza kanda, Bwana asifiwe, wanafanya kile wanachojisikia wanaongozwa kufanya, na hivyo ndivyo wanavyopaswa kufanya. Wao bado ni ndugu na dada zetu na wanaupenda Ujumbe huu. Lakini lazima sisi tufanye kile tunachojisikia tunaongozwa kufanya: Kubonyeza Play. Tunataka kumsikia nabii.

Kama tu vile Ndugu Branham alivyofanya mnamo tarehe 30 Agosti, 1964, ninawaalika mje mkaungane nasi saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) kwa mara nyingine tena tunapomsikia nabii akituletea Ujumbe:  64-0830M Maswali Na Majibu #3.

Ndugu. Joseph Branham

24-0505 Maswali na Majibu #2

UJUMBE: 64-0823E Maswali na Majibu #2

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Neno-kamilifu,

Tunangojea tu kule Kuja kwa Bwana. Tukizitengeneza taa zetu, huku zikiwa zimejaa Mafuta, tukilisikiliza Neno lililofunuliwa mchana na usiku. Tukiomba vya kutosha, kila saa; si kila siku, kila saa. Tunajiweka tu wenyewe tayari kwa kukaa ndani, na kuamini, KILA NENO.

Tunatazamia, kila dakika, kwa wale waliolala katika mavumbi ya nchi waamshwe kwanza. Mara moja, tutawaona; baba, mama, waume, wake, kaka na dada. Hao hapo, wakisimama mbele zetu. Tutajua mara moja, tumewasili, wakati umefika. Imani ya kunyakuliwa itazijaza Roho zetu, akili na miili yetu. Ndipo miili hii iharibikayo itavaa ile isiyoharibika katika Neema ya kunyakuliwa ya Bwana.

Na kisha tutaanza kukusanyika pamoja. Sisi tulio hai na tuliosalia tutabadilishwa. Miili hii ipatikanayo na mauti haitaonja mauti. Kwa Ghafula, itakuwa kama upepo uvumao juu yetu … tutabadilishwa. Toka kwa mzee kuwa kijana, toka kwa mkongwe kuwa msichana.

Baada ya muda, tutasafiri kama wazo na wale waliokwisha fufuliwa tayari. KISHA…UTUKUFU…tutanyakuliwa pamoja nao ili kumlaki Bwana hewani.

Ni wakati ulioje ambao unaokuja kwa ajili yetu. Adui ANAJARIBU kutuweka chini, kutuhuzunisha, na kutuvunja moyo, lakini Mungu atukuzwe, hawezi. Tunao Ufunuo wa Yeye ni Nani; Ni yupi ambaye Yeye aliyemtuma kutuita sisi tutoke; sisi ni nani, si tutakuwa nani, SISI NI NANI. SASA limetia nanga katika NAFSI zetu, AKILI NA ROHO zetu, na hakuna kitu kinachoweza kuliondoa hilo kutoka kwetu. Tunajuaje? Mungu alisema hivyo!

Haya sio makao yetu, yote ni yako, Shetani, unaweza kuyachukua. Hatutaki sehemu yake na hatuyahitaji tena. Tunayo Makao ya Baadaye ambayo yamejengwa kwa ajili yetu. Na hata hivyo, shetani, tumepata taarifa, YAKO TAYARI. Ujenzi umekamilika. Nakshi zote za kumalizia zimekwisha kuwekwa mali pake. Nami ninayo habari fulani zaidi kwa ajili yenu, HIVI KARIBUNI SANA, Anakuja kutuchukua sisi ili tuweze kuwa na Fungate lisiloingiliwa kwa miaka 1000 pamoja Naye, nanyi hamjaalikwa, na hamtakuwepo.

Ni mambo tukufu jinsi gani ambayo Ujumbe huu unayotufunulia kila mara tunapo bonyeza Play. Mungu Mwenyewe alishuka, na kunena kupitia midomo ya mwanadamu ili aweze kutuambia mambo haya yote. Alituchagua na kutupa Ufunuo wa kweli na MZIMA wa Yeye Mwenyewe.

Yeye alikuwa Neno lililofanyika mwili, si lile Neno la siku za Musa, Musa alikuwa siku hiyo—Neno; si lile Neno la siku za Nuhu, Nuhu alikuwa Neno kwa siku hiyo; si siku ile—Neno lile la siku za Eliya, Eliya alikuwa Neno la siku hiyo; lakini Yeye alikuwa Neno la wakati uliopo, nao walikuwa wakiishi katika yaliyopita.

Je! Mko tayari?….Hili hapa linakuja. Ni pipa mara dufu na mzigo mzito, nasi tunalipenda Hilo sana!!

Jambo lile lile lajirudia! Hiyo ndiyo ishara ya Roho Mtakatifu, Mungu anapokufunulia na unaliona, BWANA ASEMA HIVI na kulikubali. Si vile ulivyo, vile ulivyokuwa, au lo lote lile, ni yale Mungu amekufanyia wewe sasa. Hiyo ndiyo ishara.

Haleluya, alipigilia msumari ndani. SASA hebu na tumsikie Yeye akiukaza.

Yeye alitupea ishara ya Roho Mtakatifu, Yohana 14. Yeye alisema, “Ninayo mengi ya kuwaambia. Sina wakati wa kuwaambia, lakini Roho Mtakatifu atakapokuja, Yeye atawaambia, atawakumbusha yote niliyowaambia, na mambo yajayo atawapasha habari zake.” Hamwoni? Hiyo ndiyo ishara. Huko ni kutabiri na kuwa— kuwa na fasiri ya Kiungu ya Neno lililoandikwa. Sasa, si hiyo ndiyo ishara ya nabii?

Roho Mtakatifu ndiye nabii wa kila kizazi. Yeye ni nabii wa kizazi chetu. Neno linakuja kwa nabii huyo TU. Ni Mungu akizungumza na kujidhihirisha Mwenyewe kupitia nabii Wake. Yeye ndiye Neno la siku hii. Ujumbe huu, KWENYE KANDA, ndio fasiri kamilifu ya Neno, lenye thibitisho la Kiungu.

“Ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika.” Kwa hivyo mambo haya yote madogo madogo ya kuruka juu na chini kama mtoto, kujaribu kunena kwa lugha, na mambo haya yote, ijapo ile iliyo kamili… Nasi tunayo siku hizi, kwa msaada wa Mungu, ile fasiri kamilifu ya Neno na thibitisho la Kiungu! Basi ile iliyo kwa sehemu imebatilishwa. “Nilipokuwa mtoto mchanga, nilisema kama mtoto mchanga, nilifahamu kama mtoto mchanga;tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto.” Amina!

Ile iliyo kamili imekuja; ile fasiri kamilifu ya Neno. BONYEZA PLAY. Hayo tu ndiyo yote Bibi-arusi Wake anayohitaji, na yote Anayotaka.

Njooni na Mbonyeze Play pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) na kusikia NENO KAMILIFU, LENYE ILE FASIRI KAMILIFU, LENYE THIBITISHO LA KIUNGU wakati tunaposikia:

Maswali na Majibu #2 – 64-0823E

Ndugu. Joseph Branham

24-0428 Maswali na Majibu #1

UJUMBE: 64-0823M Maswali na Majibu #1

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wasikilizaji Wa Kanda,

Siwezi tu kulisema vya kutosha, HAKUNA kitu kilicho kikubwa kuliko kuisikia Sauti ya Mungu ikisema nasi kupitia malaika-mjumbe Wake aliyethibitishwa kwa ajili ya siku yetu. Ufunuo baada ya Ufunuo Bwana anatufunulia. Hakuna mwisho Wake. Kila Ujumbe ni kama hatujawahi kuusikia hapo awali. Ni Neno la Uzima, Mana Safi, Chakula cha Mungu Kilichohifadhiwa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake, na yote tunayopaswa kufanya ni KUBONYEZA PLAY.

Tunasikia kila kitu kuhusu Unyakuo WETU unaokuja hivi karibuni. Tunaenda…UTUKUFU, TUNAKWENDA kwenye Karamu ya Arusi. Yeye alituchagua SISI tangu zamani kuwa Huko kwa kujua Kwake tangu zamani, na hakuna kitakachozuia jambo hilo. Neno hapa linaungana na mtu, na hao wawili wanakuwa Mmoja. Linamdhihirisha Mwana wa Adamu. Neno na Kanisa wanakuwa Mmoja. Lolote Mwana wa Adamu afanyalo, Yeye alikuwa Neno, Kanisa linafanya jambo lile lile.

Kabla sijaendelea mbele, mnaweza kutaka kulisoma hilo tena!! Tunawezaje kumwacha shetani atushushe? Sikilizeni kile sisi tunachotarajia. Sikilizeni sisi ni nani. Sikilizeni kile kinachoendelea SASA HIVI.

Tunaenda wapi? Kwenye Karamu YETU ya Arusi ambayo sisi tumechaguliwa tangu zamani kwenda huko kwa kujua Kwake tangu zamani, ambapo SISI, Neno Lake na Kanisa Lake, tunakuwa MMOJA NAYE, na lo lote afanyalo Mwana wa Adamu, TUNAFANYA JAMBO LILE LILE!!

Kisha tukasikia kila kitu kuhusu Makao YETU ya Baadaye. Mjenzi wa Kiungu ameubuni Mji WETU Mpya, ambamo Yeye ataishi pamoja NASI, Bibi-arusi Wake. Ameujenga na ameweka kila kitu kidogo kulingana na sisi TUNAVYOPENDA hasa; jinsi tu SISI tungetaka. Ambamo hapatakuwa na haja ya nuru, kwa kuwa Mwana-Kondoo atakuwa ndiye Nuru yetu. Ambamo nabii ataishi jirani karibu nasi; atakuwa jirani yetu. tutakula hiyo miti, na tutatembea kwenye barabara hizo za dhahabu kwenda kwenye chemchemi na kunywa. Tutatembea katika paradiso za Mungu, huku Malaika wanarukaruka kuizunguka dunia, wakiimba nyimbo za sifa. Utukufu! Haleluya!

Akithibitisha Neno Lake kwetu; Yeye, ile Nguzo ya Moto, alipiga picha Yake pamoja na malaika-mjumbe Wake ili kuthibitisha na kuuambia ulimwengu, “Msikieni Yeye.” Hatupaswi kutilia shaka Neno moja, kwa maana Si neno la nabii, ni Neno la Mungu lililonenwa kwa Bibi-arusi Wake. Kisha akatuambia, tuna uwakilisho kwa kuchaguliwa tangu awali, kutuhakikishia. Yeye hatuoni sisi, anasikia tu sauti yetu kupitia Damu ya Yesu. Sisi ni wakamilifu machoni pake.

Kilindi kinaita kilindi kuliko wakati wowote ule. naye Baba anatujaza kwa Neno Lake lililofunuliwa. Kila kitu tunachohitaji kujua kimerekodiwa na tumepewa SISI. Ni kwamba tu hakuna mwisho kwa Ujumbe huu wa Neno la Uzima. Hakuna kitu kikubwa kuliko kujua SISI ni Bibi-arusi Wake. Hakikisho la kujua kwamba kusikiliza Sauti hiyo, Kubonyeza Play, ndio Mapenzi makamilifu ya Bwana; Mpango Wake aliyouandaa.

Kuna mengi zaidi yajayo! Ni Neno lisiloisha la Maji ya Uzima kwa ajili ya Bibi-arusi Wake. Hatujawahi kuwa na kiu zaidi katika maisha yetu yote, lakini hatujawahi kuburudika sana tunapokunywa na kunywa yote tunayotaka.

Kila Jumapili, Bibi-arusi anasisimka sana kukusanyika pamoja na sehemu ya Bibi-arusi kutoka ulimwenguni kote, ili kusikia kile kinachofuata ambacho Yeye anaenda kukifunua. Alituambia kama hatuwezi kuja hapa Maskanini, tutafute kanisa fulani mahali fulani; twende kwalo.

Hatuwezi sote kukusanyika pamoja kwenye kituo cha nyumbani cha nabii; makao yake makuu ambako yeye ameimarika, bali tunaweza kuyageuza makanisa yetu, ama Nyumba zetu kuwa makanisa, ambapo tunamweka yeye mimbarani. Ambapo tunaweza kulishwa NENO KAMILIFU JINSI TU VILE LILIVYOFUNULIWA.

Hakuna kukusanyika kukuu, hakuna upako mkuu, hakuna mahali pazuri zaidi pa kuwa kuliko kuketi pamoja katika ulimwengu wa roho, tukiisikiliza Sauti ya Mungu.

Ninawaalika mje kuisikia Sauti ya Mungu iliyothibitishwa pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) anapozungumza nasi kwa mara nyingine tena kupitia malaika-mjumbe Wake, na kuyajibu maswali yote tuliyo nayo mioyoni mwetu, na kutuhakikishia kwamba sisi ni Bibi-arusi Wake.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe wa Jumapili:

Maswali na Majibu #1 64-0823M

24-0421 Kuthibitisha Neno Lake

UJUMBE: 64-0816 Kuthibitisha Neno Lake

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Kanisa-Bibi-arusi,

Mwana wa Adamu amekuja na kujifunua Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu kwa Bibi-arusi Wake. Amelisema, tunaliamini, na Yeye amelithibitisha. ni Bibi-arusi Wake. Sisi ndio Kanisa-Bibi-arusi Wake tuliojiweka tayari kwa kusikiliza na kuamini kila Neno lililotoka katika kinywa Chake.

Kutakuweko na ufufuo wa wafu. Yeye atathibitisha hilo. Kutakuweko na Kunyakuliwa kwa Kanisa. Atathibitisha hilo. Kutakuweko na ule Utawala wa Miaka Elfu. Atathibitisha hilo. Kutakuweko na Mbingu mpya na nchi mpya. Atathibitisha hilo, kwa sababu Neno Lake lilisema hivyo.

Sisi ndio tutakaokuweko huko. Atathibitisha hilo. Sisi ndio wale ambao tumekwisha kufanywa sehemu ya Neno hili. Alituchagua SISI tangu zamani kuwa Huko. Kutakuweko na Unyakuo kwa kujua kwake tangu zamani na hakuna kitakachozuia jambo hilo, tutakuweko huko!

Shetani amejaribu kwa muda mrefu kuwafanya watu watilie shaka Neno moja tu lililonenwa. Usifanye hivyo. Amini tu kila Neno. Huna budi kuamini kila Neno ili kuweko huko. Si neno la nabii, ni Neno la Mungu ambalo limerekodiwa na kuhifadhiwa kwenye Kanda.

Kuhani mkuu, askofu, kardinali, mchungaji?” Mungu! Kila Neno litokalo kinywani mwa Mungu. Tunajuaje ni Neno la Mungu? Yeye husema hivyo, kisha akalithibitisha. Yeye hulithibitisha Neno Lake.

Ni LAZIMA uamini kila Neno litokalo katika kinywa cha Mungu. Amethibitisha ni Neno Lake lililo kwenye Kanda. Amethibitisha kwamba William Marrion Branham ndiye malaika-mjumbe Wake wa saba; ndiye Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku yetu. Wote wasiouamini Ujumbe na mjumbe wataangamia.

Sasa, siongei hasa na wasikizi hawa. Haya yananaswa, mnaona, na yanaenda ulimwenguni kote. Je, mnafahamu, watu wa ulimwengu, ya kwamba Neno moja, Neno moja, si fungu moja la maneno, si aya moja, Neno moja, hilo tu ndilo Hawa alikosa kuamini.

Yeye ni Neno, nasi tulikuwa sehemu ya Neno Lake. Na hiyo ndiyo sababu tuko hapa, kuhakikisha mahali petu maishani. Kuamini kila Neno. Kukaa na Neno. Kumwelekeza Bibi-arusi kwa kila Neno lililo kwenye Kanda.

Katika siku yetu, yule Mwana wa Adamu amefunuliwa. AME liunganisha Kanisa kwa kile Kichwa; ameunganisha arusi ya Bibi-arusi. Ule Wito wa Bwana Arusi umekuja. Mwana wa Adamu amekuja katika mwili wa mwanadamu kuwaunganisha hao wawili pamoja. Yeye ni Neno. Sisi ni Neno Lake, na hao wawili wanaungana pamoja.

itachukua dhihirisho la kufunuliwa kwa Mwana wa Adamu… Si kasisi… Yesu Kristo, atashuka katika mwili wa mwanadamu kati yetu, naye atafanya Neno Lake dhahiri sana hata litaunganisha Kanisa pamoja Naye kama mmoja, Bibi-arusi, kisha ataenda Nyumbani kwenye Karamu ya Arusi. Amina.

Dhihirisho la Neno litamuunganisha Bibi-arusi. Linamdhihirisha Mwana wa Adamu tena, si wanathelogia wa kanisa. Mwana wa Adamu! Neno na Kanisa wanakuwa mmoja. Lo lote afanyalo Mwana wa Adamu, Yeye alikuwa Neno, Kanisa litafanya jambo lile lile.

Tumeunganishwa na Roho Mtakatifu, Neno Lake, Sauti Yake, nasi tunajitayarisha kwenda kwenye Karamu ya Arusi. Neno limetuunganisha, na hao wawili wanakuwa MMOJA.

Tunasema KANDA, KANDA, KANDA. Mnapaswa kuzicheza Kanda majumbani mwenu, makanisani mwenu. Tunashutumiwa kwa sisi kutilia mkazo sana kuhusu kuzicheza Kanda. Kwa nini tunasema hivyo? Ni nani anayenena NASI kwenye Kanda?

Sasa, kumbuka, huyo hakuwa Yesu akinena na Ibrahimu pale, ambaye angeyatambua mawazo rohoni mwa Sara nyuma yake. Huyo hakuwa Yesu, hakuwa amezaliwa bado. Bali alikuwa mtu katika mwili; ambaye Ibrahimu alimwita “Elohim, yule Mkuu Mwenyezi.”

Ikiwa mnaamini kwamba Mwana wa Adamu amefunuliwa katika siku yetu; Mungu akinena kupitia midomo ya mwanadamu, Anawezaje basi mtu ye yote kutokuona umuhimu wa kuiweka Sauti hiyo kuwa ndio SAUTI ILIYO MUHIMU KULIKO ZOTE MNAYOPASWA KUISIKIA?

Siwashutumu wengine ambao hawaoni na kuamini kile tunachoamini; wao ni ndugu na dada zetu, lakini Mimi NIMERIDHIKA VYA KUTOSHA, NIMEJAA TELE, NINA HAKIKISHO LA KUTOSHA hii ndiyo njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya Bibi-arusi Wake. Siwezi kufanya vinginevyo. Mimi na nyumba yangu, Kubonyeza Play ndiyo NJIA PEKEE.

Kwa mara nyingine tena ninaualika ulimwengu wote kuja kuungana nasi Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) tunaposikia:  Kuthibitisha Neno Lake 64-0816.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Mathayo Mt 24:24
Marko Mt 5:21-43 / 16:15
Luka Mt 17:30 / 24:49
Yohana Mt 1:1 / 5:19 / 14:12
Warumi 4:20-22
I Wathesalonike 5:21
Waebrania 4:12-16 / 6:4-6 /13:8
1 Wafalme 10:1-3
Yoeli 2:28
Isaya 9:6
Malaki 4

24-0414 Makao Ya Baadaye Ya Bwana Arusi Wa Mbinguni Na Bibi-Arusi Wa Duniani

UJUMBE: 64-0802 Makao Ya Baadaye Ya Bwana Arusi Wa Mbinguni Na Bibi-Arusi Wa Duniani

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Chumvi ya dunia,

Ee Bibi-arusi mpendwa, tunakuwa na wakati ulioje, tumeketi pamoja katika ulimwengu wa roho, katika uwepo wa Neno, tukikomaa, tukijitambua sisi ni nani, tunatoka wapi, na wapi tunakoenda.

Kujua, kutoka katika vilindi vya mioyo YETU, hivi SASA sisi ni wana na binti za Mungu. Si ati tutakuwa, tupo SASA HIVI. Sisi ni sifa za mawazo ya Mungu.

Shetani anapotushambulia, na kujaribu kutuonyesha makosa yetu, maisha yetu ya nyuma, na kushindwa kwetu kwa kila siku; anapojaribu kutuvunja akilini mwetu na rohoni kwa uwongo wake, tunamkumbusha tu na kumwambia, “Mungu, tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, aliniona mimi; hiyo ni kweli ewe Shetani, MIMI, naye akamtuma Yesu kunikomboa MIMI.” PIGA!

“Sasa Shetani, niache, kwa maana Damu ya Mwanawe yanena kwa ajili YANGU. Siwezi kutenda dhambi. Kukosea kwangu, ndio, makosa yangu mengi, hayo hata hayawezi kuonekana na Mungu. Kitu pekee Anachosikia ni sauti YANGU ikimuabudu na kumsifu Yeye, na kitu pekee Anachokiona ni uwakilisho WANGU.”

Uwakilisho wetu unatukusanya kutoka mashariki na magharibi, kaskazini na kusini, na kutuunganisha chini ya Neno aliloliandaa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake kwenye kanda. Ndilo jambo pekee atakaloliheshimu; kwa maana ndio Njia yake Yeye aliyoiandaa.

Anaenda kutuambia nini na kutufunulia kitu gani baadaye? Tumemsikia Yeye akinena kupitia nabii Wake mara nyingi sana akituambia kuhusu jinsi gani Makao yetu mapya yatakavyokuwa, lakini wakati huu itakuwa kana kwamba hatukuwahi kusikia lolote kulihusu wakati wowote ule.

Mjenzi wa Kiungu ameubuni huu kwa ajili ya mpendwa Wake. Mnaona? Loo! ni mahali pa jinsi gani, wakati, Tabia ya Mungu, Mjenzi Hodari wa Kiungu ameubuni kwa ajili ya sifa za Kiungu ambazo zimechaguliwa Kiungu tangu zamani na Mungu Mtakatifu Ambaye—Ambaye ndiye Mwanzilishi wa Uzima wa Mungu! Huo Mji utakuwaje! Wazia jambo hilo.

Hatuwezi kujizuia. Kuchangamshwa kwetu na matarajio yetu yapo kileleni. Mioyo yetu inaenda mbio kumsikia Mungu akinena nasi moja kwa moja na kutuambia kuwa hivi sasa anaandaa na kuyabuni Makao yetu mapya ili tuweze kuishi Milele yote pamoja Naye.

Tutasikia kipi kingine, na kitu gani kitakachofunuliwa kwetu Jumapili, Wakati anapotuambia kila kitu kuhusu Kuchaguliwa tangu zamani, Uwakilisho, Kipindi cha wakati, Siku ya Nane, Mlima Mtakatifu, Piramidi, na Kusanyiko Takatifu?

Je, tunaweza kuyafunga mawazo yetu kote kwa yale yanayotokea hivi sasa? Mungu anamkusanya Bibi-arusi Wake kutoka ulimwenguni kote ili aweze kutuambia jinsi gani Makao yetu mapya yatakavyokuwa. Yeye atatuambia kwa undani kila taarifa ndogo. Tutakuwa na wakati uliotukuka jinsi gani.

Kwa upande mwingine, vita vyetu havijawahi kupungua makali. Shetani anatushambulia kuliko wakati mwingine wowote. Mashambulizi yake hayaonekani kuwa mepesi ama kuondoka.

Lakini UTUKUFU kwa Mungu, IMANI yetu katika Neno lake haijawahi kuinuliwa kama hivi. IMANI yetu ya kujijua sisi ni nani imetia nanga ndani kabisa ya Nafsi yetu, hata hatuwezi kutetereka.

Sisi HATUNA cha kuogopa; HAKUNA cha kuhofia. Baba Yeye ndiye anayehusika kwa ajili yetu kikamilifu. Anatuongoza na kutuelekeza KILA HATUA ZETU. Ametushika katika kiganja cha Mkono Wake. Shetani ni mwongo tu ambaye mwisho wake uko karibu, naye anajua hilo. Yeye ndiye anayeogopa, anajua anashughulika na Bibi-arusi-Neno Lililonenwa wa Mungu naye hushindwa kila wakati.

Sisi NI NENO. Tulikuwa ndani yake tangu mwanzo. Si kwamba tutakuwa hivyo siku moja, TUKO HIVYO SASA HIVI. Ikiwa sisi ni Neno, basi tunaweza KUNENA NENO, IKIWA TU TUTAAMINI… NASI TUNAAMINI.

Wewe ni aidha mwamini (NENO) ama wewe ni mwenye mashaka (SI NENO). Hakuna hata kiungo kimoja katika miili yetu kisichoamini Neno moja. Haya basi! Tumemthibitishia Shetani hivi punde: sisi ni Neno. Twaweza kuwa ngozi iliyo chini ya unyayo, LAKINI BADO TU SEHEMU YA ULE MWILI!!!

Kwa hiyo wakati huyo mwongo anapomjia mmoja wetu, Bibi-arusi anakusanyika kutoka ulimwenguni kote nasi TUNAMPIGA na KUMPIGA kwa Neno.

Ugonjwa unapomjia mmoja wetu, sisi huungana pamoja na KUMPIGA! Wakati mmoja wetu apatapo kujisikia kudhoofu na kushushwa moyo, sisi sote hufanya kitu gani? HUMPIGA!

Tunaenda Nyumbani, Ewe Bibi-arusi. Wakati umefika. Bibi-arusi amejiweka mwenyewe tayari. Tuko ndani ya Safina. Yeye Amefunga mlango nasi tuko ndani salama. Tunaweza kusikia muziki wa Bibi-arusi ashuke akitembea kwenye safu kuungana na Bwana-arusi.

Tutakuwa kwenye fungate yetu kwa miaka 1000, kisha tutaenda pamoja na kila mmoja na Yeye kwenye Makao yetu ya Baadaye.

Msilikose, Enyi marafiki. Kuna njia moja tu iliyoandaliwa na kuthibitishwa na Mungu: KANDA. Ni Nguzo ya Moto ikinena na kumwongoza Bibi-arusi Wake.

Lolote ufanyalo, iweke Sauti hiyo mbele yako na familia yako Jumapili hii. Imani chanzo chake ni kusikia, kulisikia Neno, na Neno huja kwa nabii. Roho Mtakatifu ni Nabii wa siku yetu akinena na Bibi-arusi Wake kwa Kanda.

Mnakaribishwa kuungana nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) wakati sehemu ya Bibi-arusi watakapoungana pamoja kumsikiliza Mungu, wote kwa wakati mmoja, akinena kupitia malaika Wake mwenye nguvu akituambia yote kuhusu: Makao Ya Baadaye Ya Bwana Arusi wa Mbinguni na Bibi-arusi wa Duniani 64-0802.

Ndugu. Joseph Branham

24-0407 Mabirika Yavujayo

UJUMBE: 64-0726E Mabirika Yavujayo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wanywaji Wa Kisima Kinachofoka Maji,

Bibi-arusi kamwe hatakuwa yeye yule tena baada ya wikendi ya Pasaka iliyo kuu ambayo Bwana aliyotupa. Tulikuwa tumefungiwa ndani pamoja Naye, tukishirikiana na kumwabudu Yeye wikendi yote. Uwepo wake ulizijaza nyumba zetu na makanisa yetu.

Tulikuwa chini ya matarajio makubwa kweli. Tulijua haya yalikuwa Mapenzi ya Bwana kwetu. Mungu alikuwa anajitayarisha kufanya jambo fulani. Tukafunga ulimwengu na vizubaishi vyake vyote. Tuliungana kutoka kote ulimwenguni kwa nia moja. Tulikuwa tumeketi pamoja katika mahali pa mbinguni, Tukijitayarisha vile ANGEZUNGUMZA NASI njiani.

Mioyo yetu ilikuwa ikilia, “Bwana, nifanye nifanane na Wewe zaidi. Nitayarishe kwa ajili ya huku kuja Kwako hivi karibuni. Nipe Ufunuo zaidi. Roho Wako Mtakatifu akijaze kila kiungo cha utu wangu.”

Wakati kila ibada ilipoanza, tulijiambia wenyewe, “Inawezekanaje? Nimezisikia Jumbe hizi maisha yangu yote, lakini sasa hivi zote zinaonekana kuwa mpya, kana kwamba sijawahi kuzisikia hapo awali. Yeye alikuwa akilifunua Neno Lake mioyoni na nafsini mwetu zaidi ya hapo awali”.

Ufunuo ufurikao ukaja tena ndani ya mioyo yetu… Ni Yeye… YEYE. Ni Roho Mtakatifu Mwenyewe AKIONGEA NASI MOJA KWA MOJA.

Sio mimi! Yeye! Yeye Ndiye! Ndio kwanza niwaambie, Yeye aliuchukua tu mwili wangu. Yeye huuchukua tu ulimi wangu, anayachukua macho yangu, kwa sababu Yeye alijua ningeyasalimisha Kwake, kwa hiyo Yeye alikuja tu na kunifanya nifanye hivyo. Kwa hiyo si mimi! Ni Yeye! Wala si mimi huko nje pamoja nanyi, ni Yeye huko nje pamoja nanyi. Yeye ndiye Ufufuo na Uzima. Loo, Mungu, Mungu; liamini. Loo, enyi watu: Mwaminini. Mwaminini. Yeye yupo hapa.

Yeye ametupa Ufunuo wa kujua HIZI KANDA ndiyo Sauti ya Mungu inayonena nasi leo hii. Hizo Kanda ndio Maneno Yake, Sauti Yake…SAUTI YAKE, iliyorekodiwa na KUHIFADHIWA ili tuweze KUMSIKIA YEYE akinena nasi Maneno ya uzima wa Milele. Hizo ndiyo njia Yake iliyoandaliwa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake.

Ni matamu, masafi, Maji ya kisima yakibubujika na kububujika. Kadiri tulivyokunywa, ndivyo tulivyozidi kupaza sauti, “Zaidi Bwana, ZAIDI. Kijaze kikombe changu Bwana, kijaze Bwana”. Naye akakijaza! Kadiri tunavyozidi kunywa, ndivyo ANAVYOZIDI KUTUPA.

Kisha shetani akatamkwa ameshindwa kwa nguvu za Injili. Kwa Mungu wa Mbinguni Yule Aliyemchagua na Kumtuma Malaika Wake Atuhubirie Injili. Kwa Mungu Yule Aliyeliandika Neno na Kumtuma Malaika Wake ambaye Aliyekuwepo Kulithibitisha Neno Lake. “Toka ndani ya hawa watu, katika Jina la Yesu Kristo”.

ILIMBIDI ibilisi kumwacha kila mgonjwa, kila mtu anayeteseka. Sasa nguvu za Mungu zimetufufua tumepata afya njema na nguvu tena.

Kisha, kutoka ndani ya kilindi cha mioyo yetu tulisema:

“Mimi sasa nakubali ya kwamba Yesu Kristo, kama Mwana wa Mungu aliyefufuka, Yeye ni Mwokozi wangu, Yeye ni Mfalme wangu, Yeye ni Mponya wangu. Sasa nimepona. Nimeokoka. Nitamwishia Yeye aliyenifia. Nitasimama kutoka hapa katika upya wa maisha, nipate kusonga mbele nikafanye vizuri niwezavyo Kwake…kwa ajili Yake Yeye aliyefufuka kwa ajili yangu. Haleluya!”

Hiki ni Kisima Kinachofoka Maji tunachokinywea kila siku. Ndicho kisima pekee kinachotoka moja kwa moja kutoka Mbinguni kinachotiririka daima. Kinajitegemea chenyewe. Daima ni matamu na masafi. Hayajakufa na kuoza. Ni Maji ya uzima yanayobadilika kila wakati, yakifunua jambo jipya kwa Bibi-arusi kila wakati.

Daima kinabubujika. Haitubidi kuyavuta kwa mashine, kuyavuta kwa winchi, kuyapindisha, ama kujiunga nayo. Ni chemchemi ya Mungu ya Maji ya uzima, nasi hatuwezi kufikiri kunywa kitu kingine chochote.

Tunasikia leo, “Maji yetu ndio maji bora unayopaswa kunywa. Tumeyaweka kwenye mchakato wetu wa uchujaji wa hatua ya 7. Kisha tumeongeza madini yote TULIYOYACHUJA tumeyarudishamo tena katika maji tunayodhani mnahitaji kuongeza maji mwilini.

Utukufu kwa Mungu, haitupasi kubahatisha au kuhoji ikiwa kile tunachokunywa ama kile kilichoongezwa ama kuchujwa. KILA KITU tunachohitaji kiko katika Maji yetu.Tunachotakiwa tu kufanya ni KUBONYEZA PLAY na kunywa kama kibubujikavyo.

Ni faraja iliyoje kuyanywa Maji haya. Tungetoka kwenda maili nyingi ili tu kunywa kwenye hilo, lakini haitupasi kufanya hivyo. Tunalibeba kila mahali tuendapo. Majumbani mwetu, makanisani mwetu, kazini, tuendeshapo katika magari yetu, tuendapo matembezini… TUNAKUNYWA, NA KUNYWA, NA KUNYWA.

Ee ulimwengu, njooni mnywe kutoka kwenye Chemchemi iliyotolewa na Mungu. Ndio mahali PEKEE huhutaji kuwa na wasiwasi na kusema, “Naomba Roho Mtakatifu atanilinda ili nisije nikanywa kitu chochote nisichotakiwa kunywa.” LOTE NI NENO SAFI LILILOTHIBITISHWA LIKITIRIRIKA KUTOKA KWENYE CHEMCHEMI ZA MBINGUNI.

Hakuna mahali pengine Panapofaa Bibi-arusi Wake kunywa!

Njoo Unywe pamoja nasi kwenye Kisima chetu Kinachofoka maji Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) tunaposikia: Mabirika Yavujayo 64-0726E.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Zaburi 36:9
Yeremia 2:12-13
Yohana Mtakatifu 3:16
Ufunuo Sura ya 13

Pasaka 2024

Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo,

Kalvari inapaswa kukumbukwa kila siku. Tumesikia mengi sana kuihusu. Tumesoma mengi sana juu yake. Wahubiri wameihubiri tangu mwanzo wa wakati. Waimbaji wameimba juu yake katika nyakati zote. Manabii walitabiri miaka elfu nne kabla haijatukia, na manabii wa siku hizi wanatuonyesha kule nyuma ilipotendeka. Ni siku muhimu sana.

Ni moja ya siku zilizo muhimu sana ambazo Mungu amepata kuzishusha duniani.

Ni kukusanyika kwa kipekee kulikoje kutoka ulimwenguni kote ambako Bibi-arusi atakuwanako wikendi hii ya Pasaka. Tutafunga milango yetu na kuuzima ulimwengu wa nje. Tutazima vifaa vyetu vyote ili tusizubaishwe, na tuongee Naye kabisa kabisa kila siku. Tutainua sauti zetu kwake kwa upatano, kwa nia moja na moyo mmoja, kumsifu, kumwabudu, kumwambia jinsi gani tunavyompenda.

Tutasikia Sauti Yake ikizungumza na mioyo yetu tunapoyaweka upya maisha yetu Kwake. Hakuna kitakachokuwa muhimu zaidi kwetu wakati tunapojitayarisha kwa ajili ya Ujio Wake wa hivi karibuni. Bibi-arusi anajiweka mwenyewe tayari zaidi ya hapo awali.

Ningependa sote tuungane kwenye ratiba ifuatayo:

ALHAMISI

Ilikuwa ni Alhamisi usiku ambapo Bwana Yesu alikula Karamu ya Mwisho na wanafunzi wake, katika ukumbusho wa Pasaka kabla ya kule kutoka kwa wana wa Israeli. Ni fursa iliyoje tuliyo nayo ya kuzungumza na Bwana katika nyumba zetu, kabla ya wikendi yetu takatifu, na kumwomba atusamehe dhambi zetu, na kutupa sisi sote yale tunayohitaji katika safari yetu.

Lijalie, Bwana. Waponye walio wagonjwa. Wafariji walio wachovu. Wape furaha wanaodhulumiwa. Wape amani walio wachovu, Chakula kwa wenye njaa, Maji kwa wenye kiu, furaha kwa wenye huzuni, uwezo kwa kanisa. Bwana, mlete Yesu miongoni mwetu usiku wa leo, tukiwa tunajitayarisha kushiriki ushirika unaowakilisha mwili Wake uliovunjwa-vunjwa. Tunaomba, Bwana, kwamba Yeye atatuzuru kwa njia ya ajabu sana…

Wabariki wengine, Bwana, kila mahali ulimwenguni, ambao wanangojea kwa furaha kuja kwa Bwana, taa zimetengenezwa, na dohani zimesuguliwa kabisa, na Nuru ya Injili ikiangaza katika sehemu zenye giza.

Hebu sote tuanze saa 12:00 KUMI NA MBILI JIONI. Masaa ya maeneo mnayoishi ili kusikia  Ushirika 62-0204, na kisha nabii atatupeleka katika Ibada yetu maalum ya Ushirika na Kutawadhana Miguu, ambayo itakuwa ikicheza kwenye app ya Lifeline (kwa Kiingereza), au unaweza kupakua ibada hii kwa Kiingereza ama lugha nyinginezo kwa kubofya anuani iliyo hapa chini.

Kufuatana na Ujumbe, tutakusanyika pamoja na familia zetu katika nyumba zetu na kula Meza ya Bwana.

IJUMAA

Hebu tuende katika maombi pamoja na familia zetu saa 3:00 TATU ASUBUHI,( ni saa 10:00 Kumi jioni ya Afrika Mashariki ) na kisha tena saa 6:00 SITA MCHANA,( ni saa 1:00 Moja jioni ya Afrika Mashariki ) tukimualika Bwana awe pamoja nasi na azijaze nyumba zetu na Roho Mtakatifu wakati tujiweka wakfu Kwake.

Hebu mawazo yetu na yarudi nyuma hadi siku ile pale Kalvari, zaidi ya miaka 2000 iliyopita, na kumwona Mwokozi wetu akining’inia msalabani, na kisha tujitoe vivyo hivyo kufanya daima yale yanayompendeza Baba:

Iwapo siku hii ni muhimu sana, moja ya siku zilizo kuu sana, hebu na tuangalie mambo matatu ambayo siku hiyo ilimaanisha kwetu. Tungechukua mamia. Bali asubuhi ya leo nimechagua tu mambo matatu tofauti yaliyo muhimu sana ambayo tunataka kuyachunguza katika muda mfupi ujao; ambayo Kalvari ilimaanisha kwetu. Nami naomba ya kwamba itamhukumu kila mwenye dhambi aliyeko, ya kwamba itamfanya kila mtakatifu kupiga magoti yake, ya kwamba itamfanya kila mgonjwa ainue imani yake kwa Mungu na aondoke ameponywa, kila mwenye dhambi aokolewe, kila aliyerudi nyuma arudi na ajionee aibu, na kila mtakatifu afurahi na apate tumaini jipya na tumaini jipya.

Kisha saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA,( Ni saa 1:30 Moja na Nusu jioni ya Afrika Mashariki ) tuungane pamoja katika nyumba zetu ili kusikia,  Siku Hiyo Pale Kalvari 60-0925.

Kisha tuungane tena pamoja katika maombi saa 9:00 TISA ALASIRI.( ni saa 4:00 Nne Usiku ya Afrika Mashariki ) katika ukumbusho wa kusulubishwa kwa Bwana wetu.

JUMAMOSI

Hebu sote kwa mara nyingine tena tuungane katika maombi saa 3:00 TATU ASUBUHI.( ni saa 10:00 Kumi jioni ya Afrika Mashariki ) na  saa 6:00 SITA MCHANA,( ni saa 1:00 Moja Jioni ya Afrika Mashariki ) na kuitayarisha mioyo yetu kwa ajili ya mambo makuu Atakayotutendea sisi katikati yetu.

Ninaweza kumsikia akisema, “Shetani, njoo hapa!” Yeye ni Bosi sasa. Ananyosha mkono, anaunyakua ule ufunguo wa mauti na kuzimu kutoka ubavuni mwake, akauning’iniza ubavuni Mwake Mwenyewe. “Ninataka kukupa notisi. Umekuwa laghai muda mrefu kutosha. Mimi ni Mwana wa Mungu aliye hai niliyezaliwa na bikira. Damu Yangu ingali imelowa msalabani, na deni kamili limelipwa! Huna haki tena. Umenyang’anywa zote. Nipe funguo hizo!”

Kisha saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, ( ni 1:30 moja na Nusu jioni ya Afrika Mashariki ) sote tutakusanyika ili kusikia NENO:  Kuzikwa 57-0420.

Hii itakuwa SIKU-KUU iliyoje kwa Bibi-arusi Wake ulimwenguni kote.

Kisha tuungane tena pamoja katika maombi saa 9:00 TISA ALASIRI ( Ni saa 4:00 Nne Usiku ya Afrika Mashariki ).

JUMAPILI

Hebu kwanza tuamke mapema kama Ndugu Branham alivyofanya asubuhi ile wakati rafiki yake mdogo, robin, alipomwamsha saa 11:00 KUMI NA MOJA ASUBUHI. Hebu tumshukuru tu Bwana kwa kumfufua Yesu kutoka kwa wafu:

Saa kumi na moja asubuhi ya leo, rafiki yangu mdogo mwenye kifua chekundu aliruka dirishani akaniamsha. Ilionekana kana kwamba moyo wake mdogo ungepasuka, akisema, “Amefufuka.”

Saa 3:00 TATU ASUBUHI. ( Ni saa 10:00 Kumi jioni ya Afrika Mashariki ) na saa 6:00 SITA MCHANA,( ni saa 1:00 Moja jioni ya Afrika Mashariki ) hebu tuungane kwa mara nyingine tena katika mnyororo wetu wa maombi, kuombeana mmoja kwa mwingine na kujitayarisha wenyewe kuisikia Sauti ya Mungu.

Saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, ( Ni saa 1:30 Moja na Nusu jioni ya Afrika Mashariki ) tutakusanyika pamoja ili kuusikia Ujumbe wetu wa Pasaka:  Muhuri wa Kweli wa Pasaka 61-0402.

Saa 9:00 TISA ALASIRI, ( ni saa 4:00 Nne usiku ya Afrika Mashariki ) tuungane tena katika maombi, tukimshukuru Yeye kwa WIKENDI YA AJABU ALIYOTUPA PAMOJA NAYE NA PAMOJA NA BIBI-ARUSI WAKE ULIMWENGUNI KOTE.

Kwa ndugu na dada zangu walio nchi za ng’ambo, kama mwaka jana, ningependa kuwaalika kuungana nasi kwa masaa ya Jeffersonville, kwa masaa yote ya maombi yaliyo kwenye ratiba hii. Ninatambua, hata hivyo, kwamba kuzicheza Kanda ya Alhamisi, Ijumaa, na Jumamosi alasiri kwa masaa ya Jeffersonville kungekuwa vigumu sana kwa wengi wenu, kwa hivyo tafadhali jisikieni huru kucheza Jumbe hizo kwa masaa yafaayo kwenu. Ningependa, hata hivyo, tuungane pamoja Jumapili saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 1:30 MOJA NA NUSU Jioni masaa ya Afrika Mashariki ) ili kuusikia Ujumbe wetu wa Jumapili pamoja.

Ningependa pia kuwaalika ninyi na watoto wenu kuwa sehemu ya vipindi vya Ubunifu, Journaling, na maswali ya majaribio ya YF, ambayo familia yako yote yaweza kufurahia pamoja. Twaamini utayapenda kwa kuwa yote yanahusiana na NENO tutakalosikia wikendi hii.

Kwa ratiba ya wikendi, taarifa ya jinsi ya kujiandaa kwa ajili ya ibada ya Ushirika, nyenzo zitakazohitajika kwa ajili ya vipindi vya ubunifu, Maswali ya jaribio la Pasaka, na taarifa nyinginezo, tazama anuani zilizo hapa chini.

Hebu na tuzifunge simu zetu kwa ajili ya wikendi ya Pasaka isipokuwa kupiga picha, kusikia Nukuu ya Siku, na kucheza kanda kwenye app ya the Table, app ya Lifeline, au anuani za kupakua.

Ni heshima kubwa kwangu kukualika wewe na familia yako kukusanyika pamoja na Bibi-arusi ulimwenguni kote katika wikendi iliyojaa KUABUDU, SIFA NA UPONYAJI. Ninaamini kweli hakika ni wikendi ambayo itayabadilisha maisha yako milele.

Ndugu Joseph Branham