All posts by admin5

23-0219 Kristo Amefunuliwa Katika Neno Lake Mwenyewe

Ujume: 65-0822M Kristo Amefunuliwa Katika Neno Lake Mwenyewe

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 13MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Kundi langu Dogo,

Nawasalimu na ninyi mliyo kwenye mfumo huu wa simu, ambao ni mzuri sana, sana. Ninamshukuru sana Bwana mnaweza kuketi moja kwa moja majumbani mwenu, mkusanyike makwenu, makanisani mwenu, na kusikiliza ibada. Kila mahali sauti yangu inapokuja, jalia kundi hilo dogo libarikiwe.

Leo, nataka kuwaandikia barua ndogo ya mapenzi kutoka moyoni mwangu ili kuwatia moyo. Ninyi ndiyo wale ambao Mungu aliyowachagua kuwa Bibi-arusi Wake kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu; ninyi mnaosikiliza kanda hizi. Nimewaambia mara nyingi sana, kanda hizi ni kwa ajili yenu tu, ninyi ndiyo kusanyiko langu. Mimi Siwajibiki na wale ambao Mungu aliowapa wahudumu wengine kuwachunga; Mimi Ninawajibika tu na aina ya Chakula ninachowalisha ninyi. Kanda hizi ni kwa ajili yenu, maskani yangu pekee , wale ambao Mungu amenipa mimi kuwa mchungaji wenu. Ni Mana iliyofichwa, hao wengine hawawezi kuila.

Sasa, kama watu wanataka kutengeneza chakula cha kisasa na kadhalika huko nje, waache wapate ufunuo kutoka kwa Mungu na wafanye yale ambayo Mungu anawaambia wafanye, wale cho chote wanachotaka. Nitafanya jambo lilo hilo. Bali Jumbe hizi ni kwa ajili yenu ninyi tu.

Ninajaribu sana niwezavyo kudumu kwa unyofu na Neno, kwa ajili yenu ninyi ambao mmewekwa mikononi mwangu kutoka kwa Mungu, maana kondoo huhitaji chakula cha kondoo. “Kondoo Wangu huisikia Sauti Yangu.” Na hilo ndilo tunaloishi kwalo, kila Neno litokalo. Si Neno moja mara hii na mara nyingine, bali kila Neno litokalo kinywani mwa Mungu. Hilo ndilo ambalo ninyi watakatifu mnaishi kwalo.

Kila mtu hana budi kuwa na kitu fulani ambacho wanashikilia. Kitu fulani kinapaswa kuwa nguzo ya kushikilia, kwa maneno mengine, Mkataa. Na kila mtu hana budi kuwa na mkataa ama Yakini. Kwangu mimi, na kwa wale ambao ninatumaini ninawaongoza kwa Kristo, na kwa njia ya Kristo, Biblia ndiyo mkataa wetu.

Basi, tunatambua ya kwamba Mungu alitutumia manabii Wake. Hiyo ndiyo njia aliyokuwa nayo yakulileta Neno Lake kwa watu, kwa kinywa cha nabii Wake. Sasa katika siku hizi za mwisho, Yeye ameahidi kujidhihirisha Mwenyewe katika utimilifu tena, wa mwili Wake, katika Roho. Ni Mungu Mwenyewe katika maumbile ya herufi, sura ya nabii, akidhihirishwa katika mwili.

Sina budi kuishi daima katika uwepo wa yule Mwandishi nikiwa na kalamu yangu tayari wakati wo wote kuandika lo lote yeye Analosema. Nimeelekeza nia yangu daima kwenye mawazo Yake; si vile mwanadamu anavyofikiri, vile wakati huu unavyofikiri, vile kanisa linavyofikiri, vile ufalme unavyofikiri. Mawazo ya Mungu tu! Ninatamka tu mawazo ya Mungu kwa Neno.

Wakati Mungu anapoyafunua mawazo Yake Kwangu , mimi ninayatamka katika Neno kwenye kanda, “BWANA ASEMA HIVI.” Si, “ Mimi Nasema Hivi .” Ni, “BWANA ASEMA HIVI!” Ninaweza tu kulifasiri jinsi vile Mwandishi anavyotaka niwafasirie ninyi ; maana ni Neno la Mungu lisilokosea.

Kuna wengine wengi wanaojaribu kuniiga, kama makuhani, ama kadhalika. Nao wanafanya nini? Wanachafua tu, hivyo tu. Wasingeweza kufanya jambo hilo. Mungu alinituma mimi, nabii Wake, kumwongoza Bibi-arusi Wake; si mtu mwingine, wala si kundi la watu.

Maneno ninayonena, na vile ninavyotenda, itawapofusha wengine, lakini itayafungua macho ya wengine. Alinivalisha kwa namna ya mavazi ambayo ningevaa, tabia yangu, shauku yangu, kila kitu jinsi tu ilivyonipasa kuwa. Alinichagua kikamilifu kwa ajili yenu. Wengine wangesimama na kuangalia waseme, “Vema, siwezi. Kuna…Si—siwezi kuona.” Wao wamepofushwa.

Yeye atajifunua kwa yule yeye atakayemfunulia Hilo . Amelifanya hivi kwamba anaweza kujificha mwenyewe katika Maandiko, kwa mwanatheolojia mwenye akili sana aliyeko. Yeye Anaweza tu kujificha mwenyewe , akae papo hapo katika Maandiko, nao wanaweza kuyatazama siku nzima na wasiweze kuyaona; wayatazame maishani mwote, na wasiyaone kamwe. Anaweza tu Mwenyewe kujificha, akiketi pale.

Jambo lililopo sasa ni wale wanaoupokea Ujumbe mioyoni mwao, hawana budi kukaa katika Uwepo wa Mwana, wapate kuivishwa. Bonyeza Play halafu umwache Mwana aukaushe ubichi wote ukutoke, awafanye Wakristo waliokomaa.

Wakati yeye alipokuja mara ya kwanza, alikuwa mwanadamu. Alipokuja mara ya pili, akiwa na sehemu maradufu, alikuwa mwanadamu. Alipokuja kama Yohana Mbatizaji, alikuwa mwanadamu. Aliahidi kuja katika siku hii na kuishi na kujidhihirisha kwa mara nyingine tena ndani ya mwanadamu; Mwana wa Adamu akiishi katika mwili wa mwanadamu.

Sasa tuko katika wakati wa jicho, kinabii, ya Malaki 4. Hakuna kitu kingine kilichosalia kuja ila Yeye Mwenyewe kuingia ndani ya kitu hicho, ’ maana hilo ndilo jambo la mwisho lililopo.

Sikilizeni enyi wana-kondoo wangu wadogo, ninyi ambao Mungu amenipa kuwa mchungaji wenu. Wakati umeenda sana . Anakuja upesi kuwachukua ninyi , Bibi-arusi Wake. Kaeni na hizo kanda, hazihitaji kufasiriwa.

Ninawaalika ninyi Tai wadogo mje kuungana nami kwenye jambo pekee litakalomleta Bibi-arusi Wake pamoja Jumapili hii, saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville.( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Tanzania na Kenya pia ) Mtasikia Bwana Asema Hivi wakati Mungu anaponena kupitia mimi na kufunua: Kristo Amefunuliwa Katika Neno Lake Mwenyewe 65-0822M.

Kumbuka, KAENI NA HUDUMA YA KANDA . BONYEZA PLAY KILA SIKU.

Ndugu Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Kutoka 4:10-12
Isaya 53:1-5
Yeremia 1:4-9
Malaki 4:5
Luka Mtakatifu 17:30
Yohana Mtakatifu 1:1 / 1:14 / 7:1-3 / 14:12 / 15:24 / 16:13
Wagalatia 1:8
2 Timotheo 3:16-17
Waebrania 1:1-3 / 4:12 / 13:8
2 Petro 1:20-21
Ufunuo 1:1-3 / 10:1-7 / 22:18-19

23-0212 Nawe Hujui

UJUMBE: 65-0815 Nawe Hujui

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 11MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Anayengoja,

Nami najua ya kwamba, baada ya kuondoka kwangu kutoka dunia hii, hizo kanda na vitabu vitaendelea kuwepo, na wengi wenu ninyi watoto wadogo mtaona, katika siku zijazo, ya kwamba jambo hili ni Kweli kabisa, kwa maana nanena katika Jina la Bwana.

Njoo ukusanyike pamoja na sisi, Tai, Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA Saa Za Jeffersonville,( Ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Tanzania na Kenya pia ) . tunaposikia 65-0815 – Nawe Hujui.

Ndugu. Joseph Branham

23-0205 Matukio Yakidhihirishwa Na Unabii

Ujume: 65-0801e Matukio Yakidhihirishwa Na Unabii

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 11MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Watu wa Wakati huu,

Baba, tunakupenda sana. tunawezaje kuanza kueleza jinsi tunavyojisikia? Ulituchagua, ukatukusudia tangu zamani, nawe ukafanyika Mwanadamu aliye hai ili kutoa Maisha Yako kwa ajili yetu.

Ulituandikia mawazo Yako yenyewe kwetu kupitia manabii Wako, ili tupate Neno Lako. Ndipo, kama ulivyoahidi, ulikuja tena , ukijifunua Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu kwa matukio yanayodhihirishwa na unabii, kufasiri na kufunua Neno Lako.

Kwa kujichagulia wewe mwenyewe, ulimchagua William Marrion Branham kuwa mtu wa wakati huu. Ulimchagua ili kuvutia usikivu wetu. Uliongoza mikono yake. Uliongoza macho yake katika maono. Hakuweza kusema kitu cho chote ila kile ulichokuwa unamwonyesha.

Hakuweza kusema kitu cho chote ila kile ulichoweka kinywani mwake. Ulitawala kabisa ulimi wake, vidole vyake, na kila kiungo cha mwili wake. Yeye Alikuwa katika utawala wako mkamilifu .

Kisha, kwa kuchagua Kwako kwa mara nyingine tena, ulituchagua tuwe watu wa wakati huu. Kundi lako dogo la walio wachache limekusanyika kwa upako wa Neno Lako, likidhihirisha tena maisha ya Yesu Kristo. Sisi ni Neno Lako tukiungana na Neno. Hatuwezi kufanya kitu kingine .

Baba, tunataka kuwa katika Mapenzi yako makamilifu; hakuna kitu kingine muhimu kwetu. Hatutaki mawazo yetu, fikra zetu, au kile mtu mwingine ye yote asemacho, mapenzi Yako tu.

Tumeliendea Neno Lako ili kuona kile ulichosema tunapaswa kufanya ili kuwa Bibi-arusi Wako. Ulisema utauhukumu ulimwengu siku moja kwa Neno Lako. Ulituambia Neno Lako huwajilia manabii Wako PEKE YAO , ambao walichaguliwa tangu awali na kuamriwa tangu zamani na Wewe.

Ulituambia halimjii kamwe mwanatheolojia wala kundi la watu, bali kwa nabii Wako. Yeye Atakuwa mfasiri wako pekee wa kiungu wa Neno. Si mawazo yake, fikra zake, fasiri yake, bali Wewe ukinena kupitia kwake, ukilifasiri Neno Lako Mwenyewe.

Katika kila wakati, watu wanawaachilia watu waweke fasiri yao wenyewe kwenye Neno Lako, na inawafanya kuwa vipofu . Inafanya jambo lile lile lililofanyika kwa Mafarisayo na Masadukayo. Hiyo ndiyo sababu watu wanashindwa kulipata leo hii. Wao Wanasikiliza kile mtu mwingine anachosema juu Yake, badala ya kusikiliza Neno kama vile nabii Wako alivyowaambia wafanye.

Ulisema, kwanza Ninatuma Neno Langu, halafu kama watu hawataamini Neno Langu, basi Ninawapelekea wahudumu. Pia ulisema katika kila wakati wahudumu hupotoka ; si wote, bali wengi wao, na kuwaongoza watu kwao. Sisi tunataka kuwa katika Mpango Wako wa asili.

Inachanganya sana, wahudumu hawawezi kukubaliana wao kwa wao. Ndugu X hawezi kukubaliana na Ndugu Y; Ndugu Y hawezi kukubaliani na ndugu Z. Hawawezi kukubaliana  wao kwa wao. Wanaonekana kukubaliana juu ya jambo moja tu, hatupaswi kucheza kanda kanisani.
Ni Babeli tena, inachanganya sana. Tunaamini kuna Mchoro mmoja tu na ni lazima tujichonge wenyewe ili kueneana na Mchoro huo, sio kujaribu kukata Mchoro huo ili utuenee.

Kumekuwa na huduma nyingi sana ambazo zimeibuka na mawazo yao wenyewe, fasiri zao wenyewe na mafundisho. Wote wamekuwa si kitu. Kumekuwa na wahudumu wakubwa waliowekwa wakfu waliyoinuka wanaosema wanahubiri na kunukuu Ujumbe wa wakati huu, na huduma yao ndio Njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya wakati huu, na sio kanda.

Wana watu waaminifu wanaoenda kwenye makanisa yao, wakiwasikiliza kwa miaka mingi. Wana wahudumu wengi wanaowatembelea, mikutano, miamsho, mahubiri, wakisema wanachosema wao ndio Njia Yako iliyoandaliwa, na sio kanda. Ndipo siku moja wanasema, Ujumbe huu si kweli.

Je, hawakuwa wanachunguza alichokuwa anasema kwa kutumia kanda hizo? Je! walikuwa wakichukua tu kile alichosema kuwa ni Neno, Njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya wakati huu? Kama angalizicheza kanda, Sauti Yako iliyothibitishwa kwa watu, badala yake wao wenyewe wakijiweka kama sauti iliyo muhimu sana, wangejua waliyekuwa wakimsikiliza ni mpakwa mafuta wa uongo katika mafundisho ya wakati wa mwisho.

Hiyo haimaanishi kuwa huhitaji mchungaji. Haimaanishi wote ni wachungaji watiwa mafuta wa uongo. Hilo Halimaanishi kuna wengi wanaohubiri kile hasa Ndugu Branham alichosema. Bali inamaanisha jambo lililo muhimu sana unalopaswa kusikia ni Ujumbe uliyo kwenye kanda; Ndio BWANA ASEMA HIVI PEKEE.

Ni Mwongozo. Ni Yakini. Ni Neno la mwisho. Ndilo Neno Kamilifu pekee. Isipokuwa mchungaji, kiongozi wako wa kiroho, anasikiliza Neno hilo safi pamoja na watu wake, kuna kitu kitaenda kombo.

Kwa nini wahudumu hawataki kucheza Sauti Yako iliyothibitishwa katika makanisa yao? Wanawezaje kusema ni makosa huku wanadai wanaamini kuwa ni Neno? Kwa nini wanatoa kila aina ya visingizio na kusema huduma yao ndiyo Njia Yako iliyoandaliwa kwa ajili ya Wakati huu, na sio Sauti Yako iliyothibitishwa kwenye kanda?

Kwa nini wanawatisha watu kwa kusema kwa sababu tunasema “BONYEZA PLAY” ili kuisikia Sauti yako, tunamwabudu mtu na sio Wewe unenaye kupitia mtu huyo?

Sisi tunakuabudu WEWE TU BABA. Tunalikagua kwa Neno lako tena na tena. Unatuambia kupitia nabii Wako kwa kila Ujumbe tunaosikia kwenye kanda: Ndiyo Njia Yako pekee iliyoandaliwa kwa ajili ya Wakati huu.

Wapi pengine ambapo Bibi-arusi Wako angeweza kwenda isipokuwa kuongoza moja kwa moja kwenye Neno Lako. Sisi ni Bibi-arusi- Neno Bikira wako. lazima tudumu na Nguzo Yako ya Moto. Ndipo mahali pekee tunapoweza kuridhika na kusema amina kwa kila Neno tunalosikia.

Baba, tunakuona Wewe ukiwa nje ya kanisa lako ukijaribu kuingia ndani, na hilo linaivunja mioyo yetu. Komeo liko kwa ndani nasi tumekufungulia mlango uingie. Hatujui kitu kingine . Hatutaki kitu kingine. Hatuwezi kuchukua kitu kingine. Tumetiwa mimba na Neno lako.

Asante Baba kwa Ufunuo wa Neno Lako. Hatumpingi yeyote, tuko kwa ajili ya Neno lako tu lililodhihirishwa na unabii. Tutasimama mbele zako siku moja kwenye hukumu. Kwa mioyo yetu yote tunataka kusema, “Baba, tumedumu na Neno Lako.”

Mtie moyo mchungaji wako, kiongozi wako wa kiroho, Kubonyeza Play Jumapili hii kusikia Sauti ya Mungu. Utahukumiwa siku moja kwa yale Neno la Mungu lisemayo kwenye kanda. Unawezaje kukipa nafasi kitu kingine cho chote?

Umealikwa kuja kuuungana nasi Jumapili hii saa 06 :00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, ( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Tanzania na Kenya pia ), kusikia: Matukio Yakidhihirishwa Na Unabii 65-0801e , Mungu anapozungumza kupitia midomo ya mtu aliyejichagulia. Yule ambaye alimpa tabaka yake, karama zake. Alimpa tabia yake, mwenendo wake, na cho chote kile, jinsi anavyojieleza, cho chote afanyacho. Yeye Alimfanya William Marrion Branham mtu wa wakati huu ili kuwashika watu wa wakati huu, nasi ndio WATU WA WAKATI HUU.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko Ya Kusoma Kabla Ya Kusikiliza Ujumbe :

Mwanzo 22:17-18
Zaburi 16:10 / Sura ya 22 yote / 35:11 / 41:9
Zekaria 11:12 / 13:7
Isaya 9:6 / 40: 3-5 / 50:6 / 53:7-12
Malaki 3:1 / sura ya 4 yote
Yohana Mtakatifu 15:26
Luka Mtakatifu 17:30 / 24:12-35
Warumi 8:5-13
Waebrania: 1:1 / 13:8
Ufunuo: 1:1-3 / Sura ya 10 yote

23-0129 Mungu Wa Wakati Huu Mwovu

UJUMBE: 65-0801m Mungu Wa Wakati Huu Mwovu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 13MB (use Firefox to download)

Mpendwa kundi dogo Neno-Bikira wa Kristo,

Hatuwezi kuwa kitu kingine. Hatuwezi kusikia kitu kingine. Hatujui kitu kingine. Hatutaki kitu kingine. Palipo na Nyama mbichi, KUBONYEZA PLAY, ambalo ni Neno la majira haya, Hapo ndipo Tai watakapokusanyika. Neno linakuwa hai ndani yetu.

Sisi hatuko sawa na mtu mwingine yeyote ! Ninyi ni watu waliotengwa, watakatifu kwa Bwana, waliowekwa wakfu kwa Neno na Roho wa Mungu, kuzaa matunda ya ahadi Yake ya siku hii. Tunazidi kukomaa na kuivishwa kwa kusikia Sauti ya Mungu.

Nabii alituambia turejee kwenye kanda hizi. Kama una kinasasauti, kusanya kundi la watu pamoja na ukaicheze, na msikilize kwa makini. Kusikiliza Sauti Yake, kile anachotuambia. Neno la Mungu halihitaji kufasiriwa; Yeye hujifasiria Mwenyewe. “Mimi ni Sauti ya Mungu kwenu.”

Nalo ndilo Hili, Biblia, neno moja lisiongezwe Kwake au kuondolewa Kwake. Dumuni waaminifu tu kwa Sauti hiyo. “Mgeni hawatamfuata,”

Anawezaje mtu yeyote kutoona Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii? Lakini utukufu kwa Mungu, tunaweza kuiona, kwa sababu tumechaguliwa kuiona . Hatuta, na hatuwezi kudanganywa, kwa sababu sisi ni Neno Lake lililodhihirishwa.

Ndugu na dada, hebu hilo nalizame ndani kwa dakika moja, SISI NI NENO LILILODHIHIRISHWA!! Mungu Mwenyewe, akinena kupitia midomo ya mwanadamu, anatuambia SISI NI NENO. Hatuna chochote cha kuogopa. Kila kitu tunachohitaji ni chetu.

Kila wiki tuko chini ya matarajio makubwa ya Bwana kutuzuru. Hatuna nafasi hapa ya kuketi kila mmoja, wala kila mmoja hawezi kuja Jeffersonville, kwa hiyo inatubidi tu kuwatumia Neno kupitia njia ya mtandao.

Tuko majumbani mwetu, makanisani mwetu, kwenye magari yetu, tumekusanyika kuzunguka vipaza sauti vyetu vidogo kutoka ulimwenguni kote, tukingojea Kuja kwa Bwana.

Wamekusanyika pamoja nasi huko katika Afrika, wakingojea Kuja kwa Bwana. Wamekusanyika pamoja nasi huko Mexico, wakingojea Kuja kwa Bwana. Huko Ulaya, Skandinavia, Australia, Mashariki ya kati, Amerika ya Kusini, kutoka pembe nne za dunia, wakingojea Kuja kwa Bwana.

Nasi tumekusanyika hapa kwenye kanisa la nyumbani, maskani, tukingojea Kuja kwa Bwana. Tuko umbali wa masaa mengi, Bali tuko pamoja kama JAMII MOJA, waamini, tukisikiliza Sauti ya Mungu, tukingojea Kuja kwa Masihi.

SISI NDIO watu walioitwa na waliochaguliwa na Mungu kutoka katika wakati huu mwovu kwa ajili ya Jina Lake. Tunajaribiwa na kuthibitishwa kwa Shetani kwamba sisi ni Neno. Sisi ni sehemu ya ule Mti wa Bibi-arusi wa Asili. Tunatazama maisha yetu yakidhihirishwa na Neno hilo.

Ni rahisi kwa kila mtu kuamini kwamba Yesu alikuwa jawabu la moja kwa moja kwa kila unabii uliokuwa utimie ndani Yake, kwa sababu wanatazama nyuma kuona hayo yakitukia. Lakini katika wakati huu mwovu uliopo sasa, wanafanya jambo lile lile walilofanya wakati huo, kwa kulifasiri kwa njia nyingine, na wamewafanya watu waingie katika nguvu za upotevu wauamini uongo. Laiti wangetambua ni Neno lile lile la wakati huu likidhihirishwa.

Kuna jambo moja tu linaloweza kumleta Bibi-arusi pamoja, Ujumbe huu. Kuna jambo moja tu ambalo sote tunaweza kukubaliana kwalo, Ujumbe huu. Kuna Sauti moja tu ambayo imethibitishwa kuwa Bwana Asema hivi, Sauti ya Mungu kwenye kanda.

Sasa, makanisa tu baridi, ya kawaida, magumu, na kadhalika, ya theolojia za kujitengenezea, hayo hayangeweza; walio Wateule wasingewajali. Lakini ni kule juu karibu sana na jambo lililo halisi. Kuacha tu Neno moja ndivyo tu unavyopaswa kufanya. Lililoahidiwa kwa wakati huu; wakati mkuu sana!Enyi Wakristo, kila mahali, jihadharini na saa tunayoishi! Andikeni, na someni, na msikilize kwa makini.

Mungu wa wakati huu mwovu anafanya yote awezayo kuwadanganya watu kwa kuizuia Sauti Yake iliyothibitishwa isiwafikie. Anajaribu kuwafanya wasiamini Neno moja tu, kama alivyomfanyia Hawa hapo mwanzo.

Lakini Bibi-arusi-Neno wa Kristo anakuja kilipo Kichwa. Tunaungana tena kwa Mwenzi wetu pale tulipoanzia. Wakati wa kutoka umefika. Mungu anakuja kwa ajili Bibi-arusi Wake yule anayedumu na Neno Lake.

Roho Mtakatifu yuko hapa akimwita Bibi-arusi wa Kristo atoke. Yeye anafanya hivyo kwa kumthibitishia Neno Lake la ahadi Kwake, kwa ajili ya wakati huu, akionyesha ya kwamba Hilo ni Kristo.

Hakuna jambo lililo kuu kuliko kuungana na Bibi-arusi ulimwenguni kote, Kusikiliza Sauti ya Mungu ikinena nawe moja kwa moja. Hakuna haja ya kutumaini, kushangaa au hata kuomba ikiwa kile unachosikia ni kweli. Kwa maana Ndiyo SAUTI PEKEE ILIYOTHIBITISHWA YA BWANA ASEMA HIVI.

Njoo uungane nasi ukasikilize:

Baada ya hayo naliona malaika mwingine, akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka kuu; na nchi ikaangazwa kwa utukufu wake.

Saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville,( ni Saa 2:00 MBILI USIKU YA Tanzania na Kenya pia) tunaposikia: Mungu wa Wakati Huu Mwovu 65-0801M.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Mathayo Mtakatifu sura ya 24 yote /27:15-23
Luka Mtakatifu 17:30
Yohana Mtakatifu 1:1 / 14:12
Matendo 10:47-48
1 Wakorintho 4:1-5 / sura ya 14 yote
2 Wakorintho 4:1-6
Wagalatia 1:1-4
Waefeso 2:1-2 / 4:30
2 Wathesalonike 2:2-4 / 2:11
Waebrania sura ya 7 yote
1 Yohana Sura ya 1 yote / 3:10 / 4:4-5
Ufunuo 3:14 / 13:4 / Sura ya 6-8 na 11-12 zote / 18:1-5
Mithali 3:5
Isaya 14:12-14

23-0115 Watiwa Mafuta Katika Wakati Wa Mwisho

Ujume: 65-0725M Watiwa Mafuta Katika Wakati Wa Mwisho

PDF

Server S
Server G

pakua – m4a

pakua – amr 18MB (use Firefox to download)

Wapendwa Wakusanyikao Katika Zizi La Kondoo,

Nimeridhishwa na kumshukuru sana Bwana kwa kukusanyika pamoja na kila mmoja wenu katika zizi la Kondoo wa Mungu kila wiki, ambapo tumefichwa mahali petu pa siri, tukijilisha na kuishi kwa Chakula hicho Kilichofichwa. Ni Ufunuo wa Yesu Kristo, akijithibitisha na kujidhihirisha Mwenyewe kwetu.

Amejificha ili kwamba wengine waliangalie moja kwa moja na bado wasilione, bali kwetu sisi, Bibi-arusi Wake mteule, tunaliona waziwazi na kuamini kila Neno. Tumekaa na Neno Lake na nabii Wake kwani wao ni Mmoja na kitu kile kile .

Na iwapo wewe ni mwana wa Mungu, utakaa pamoja na nabii wa Biblia hii. Ni Neno.

Manabii wengi waliotiwa mafuta siku hizi wanasema “Ni Roho Mtakatifu ndiye unayepaswa kukaa naye, si nabii.” Kama manabii wa kale, kama tuna swali, inabidi kuwe na jibu sahihi. Ni lazima twende KWENYE NENO kuona kile nabii aliyetutangulia alichosema.

Lakini kuna Kristo mmoja aliye halisi, Roho, na huyo ni Neno lililofanyika mwili kama alivyoahidi kufanya.

Kristo MMOJA aliye halisi, Roho, ambaye Yeye aliahidi, Malaki 4, Luka 17, Mwana wa Adamu akijifunua Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu.

Ndiyo, kuna watu waliotiwa mafuta. Ndiyo, wana wito. Ndiyo, wana Roho Mtakatifu halisi. Ndiyo, wana nia na makusudi sahihi.

Basi tutajuaje wa kweli na wa uongo?

Angalia, wanafanana. Wametiwa mafuta namna ile ile. Lakini angalia, “Kwa matunda yao…”

Sipendi kusema mambo haya lakini saa imechelewa sana na wakati unaenda. Hili ndilo linalosemwa na kuhubiriwa leo na wale mbwa-mwitu wakali Paulo alilionya kanisa kuwahusu, na wale wapakwa mafuta wa uongo ambao Ndugu Branham aliyosema wangekuja. Wako hapa kati yetu, kama tu walivyosema.

Hapa kuna kipande kidogo cha barua iliyoandikwa kutoka kwa mhudumu . Matunda yao yanajaribu kutilia shaka juu ya nabii wa Mungu. Wanawaonya watu wao kuwa sisi ni miungu watu kwa sisi kumfuata nabii na Kubonyeza Play.

Sikiliza jinsi hili lilivyodanganyifu.

Nimekerwa kwamba pepo huyu amepenya tabaka zetu za ujumbe hivi kwamba sasa tunaita vitabu vya mahubiri ya William Branham SAUTI YA MUNGU. William Branham hakuwa sauti halisi ya Mungu , bali ni sauti ya mwanadamu ambayo Mungu aliyotumia. Biblia haisemi kamwe kwamba Yeye alikuwa ni sauti ya Mungu, bali Biblia inamtambulisha kama sauti ya malaika wa 7. ( Ufu 3:14; 10:7 ).

Hebu twende kwenye NENO na tumwache nabii wa Mungu ayaanike wazi mafundisho haya ya uongo.

Ikiwa kwa kusema hivyo niliwakera, mnisamehe, lakini, nilihisi kwamba hilo laweza kuchukiwa, lakini, MIMI NI SAUTI YA MUNGU KWENU .

Sasa utamwamini nani, nabii huyu wa uongo aliyetiwa mafuta, au MALAIKA-MJUMBE WA SABA WA MUNGU ALIYETHIBITISHWA ? Unawezaje kukaa chini ya mhudumu yeyote ambaye anayeamini au anayekufundisha mambo kama hayo? Afadhali uingie katika Neno wakati ungalipo.

Kosa la kutisha limefanywa na jumuia ya ujumbe katika kumfanya William Branham kuwa mungu kwa kumfanya kuwa yakini. William Branham hakuwa kamwe yakini! Neno la Mungu ndilo Yakini.

Amina, Neno la Mungu NDIYO Yakini yetu. Neno lilikuja kwa nani, kwako wewe au kwake YEYE? Ni nani aliye mfasiri wa kiungu wa NENO LA MUNGU, wewe au YEYE? Ni nani ambaye Nguzo ya Moto ilimthibitisha kuwa Bwana Asema hivi, wewe au YEYE?

Kwa sababu ukiwa na watu wawili, una maoni mawili.

Hatuhitaji watu wawili wala maoni yao, tunahitaji tu kile nabii wa Mungu alichosema kwenye kanda.

Yapasa kuwe na Yakini moja thabiti , na Yakini yangu ni Neno, Biblia .

Hilo hapo, kama vile ulivyosema, Biblia ni Yakini yake na yetu, lakini kisha anasema:

Najua ninyi ni Ndugu , mnanichukua mimi kama Yakini Yenu .

Kwa hivyo subiri kidogo, hilo linasikika kinyume na ULICHOSEMA. Alisema kwamba tunamchukua yeye kama Yakini Yetu.

Mradi ninamfuata Mungu kama Paulo alivyosema katika Maandiko , “ Mnifuate mimi kama ninavyomfuata Kristo .”

Je, huyo si aliyetiwa mafuta? Je, hakujua alichokuwa anazungumzia?

Hivi Nabii wa Mungu alituambia nini wiki iliyopita?

Tunaona ya kwamba mtu anapokuja, ametumwa kutoka kwa Mungu, amechaguliwa na Mungu, akiwa na BWANA ASEMA HIVI ya kweli, ujumbe huo na mjumbe huyo ni mmoja na kitu kimoja .

Alisema huwezi kuwatenganisha, ni kitu kimoja, lakini unasema tunapaswa kuwatenganisha?

William Branham hana tofauti na mwanadamu ye yote apatikanaye na mauti, kwa maana alikuwa mtu wa tabia moja na Eliya alivyokuwa .

Amina, alikuwa mwanadamu tu hakika, lakini alikuwa NDIYE MTU ambaye Mungu alimchagua kufunua Neno Lake lote kwake , na kutuongoza kwenda kwenye Nchi ya Ahadi. Yeye ndiye ambaye Mungu alisema, wafanye watu WAKUAMINI.

Kitu kile kile, wametiwa mafuta, wakihubiri Injili ya Pentekoste, bali wakiikana ahadi ya siku hii ya Neno kuthibitishwa , “ Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele .”

Tutajuaje tofauti ikiwa wao ni wapakwa mafuta wa kweli wa Roho Mtakatifu? Anatupa mifano ili tujue kati ya manabii wa uongo na nabii wa kweli.

Balaamu na Musa. Mikaya na Zedekia. Yeremia na
Hanania. Katika kila kisa wote wawili walikuwa manabii waliotiwa mafuta wa Mungu, lakini alituambia tufanye nini, TUDUMU NA NABII WA MUNGU ALIYETHIBITISHWA. Hiyo ndiyo njia PEKEE ya kuwa na uhakika kwamba unafuata Njia ya Mungu iliyoandaliwa, na uko katika mapenzi Yake makamilifu.

Mimi ndiye tu ninayekuwa karibu wakati anapoyafanya. Mimi nilikuwa tu sauti aliyoitumia Yeye, kusema jambo Hilo. Haikuwa yale niliyojua; ni yale niliyojitolea kwake tu , aliyozungumza kupitia .

Hayo ndiyo yote Bibi-arusi anayotaka na anayohitaji. Sauti Moja. Nabii mmoja. Ujumbe Mmoja. Mjumbe mmoja.

Ee Baba, jinsi tunavyoshukuru kwa neema na rehema zako kwetu. Ulituambia hakuna lisilowezekana kwako. Hakuna lisilowezekana kwetu sisi. Kwa maana yote yanawezekana kwao waaminio, nasi TUNAAMINI.

Njoo uungane nasi Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, (ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Tanzania na Kenya pia.) tukiwa na Sauti iliyochaguliwa ya Mungu ikituambia yote kuhusu  Watiwa-Mafuta katika Wakati wa Mwisho 65-0725M.

Ndugu.  Joseph Branham

23-0108 Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake

UJUMBE: 65-0718e Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Watafuta Madini ,

Kuna kisima kinachofoka maji cha Ufunuo ambacho kinabubujika ndani yetu zaidi ya hapo awali. Tumesikia Ujumbe huu maisha yetu yote, na daima tumeamini kila Neno, lakini SASA imedhihirishwa ndani yetu zaidi kabisa ya hapo awali.

Sasa huu ndio wakati wake , sasa ni majira yake tunakula mambo ya siri ya Mungu ambayo ulimwengu umefichwa. Kitu kile watu wanachokicheka, ndicho kitu tunachokiomba. Kile kitu ambacho watu wanaita “wenda wazimu,” tunakiita “Kikuu!”
Mungu ametufunulia kuna njia moja tu iliyoandaliwa ya kuwa Bibi-arusi Wake, KUBONYEZA PLAY.

Lakini Mungu ashukuriwe, tuna Chakula kilichofichwa, Chakula cha kiroho, hata tunaishi kwa fadhili na rehema za ufunuo wa Yesu Kristo katika siku hizi za mwisho, akijithibitisha Mwenyewe miongoni mwa watu Wake.

Kwa kila Ujumbe anaousikia Bibi-arusi, Yeye hututhibitishia hayo ni Mapenzi yake makamilifu. Sio kile TUNACHODHANI Anasema, wala si kile TUNACHODHANI Inamaanisha , NI HASA KABISA Yale yeye Asemayo na bado wengine hata hawawezi kuliona; wamepofushwa. Mungu amelificha. Wanalitazama moja kwa moja, lakini hawalioni. Kwetu sisi, NDIYO YOTE TUYAONAYO.

Tunapokusanyika kila wiki, ni vigumu kungoja kusikia kile Atakachoenda kutuambia na kutufunulia. Jumapili hii, yeye hatatupa vijisehemu fulani vidogo vya vito vya thamani vilivyofichwa, Yeye atatupa jiwe kubwa la madini na KULlLIPUA tena na tena ili kuhakikisha tunalipata.

. Huyo nabii alikuwa amekaa kwa muda mrefu sana katika Uwepo wa Mungu, Manabii wa Agano la Kale, ama wa wakati wo wote, walipoishi katika Uwepo wa Mungu mpaka wakawa Neno, Ujumbe wao ni Neno Lenyewe . Pia, kumbukeni, yeye alisema, “BWANA ASEMA HIVI.”

. Tunaona ya kwamba mtu anapokuja, ametumwa kutoka kwa Mungu, amechaguliwa na Mungu, akiwa na BWANA ASEMA HIVI ya kweli, ujumbe huo na mjumbe huyo ni mmoja na kitu kimoja.

. Basi wakati mtu anapokuja na BWANA ASEMA HIVI , yeye na Ujumbe huo ni mmoja .

. Mbingu zinatangaza jambo hilo, Biblia inalitangaza, Ujumbe unalitangaza. Yote ni jambo lile lile.

. Nabii, Neno, Ujumbe; mjumbe, Ujumbe, na Ujumbe, walikuwa mmoja.

. Mtu ye yote na ujumbe wake ni mmoja .

Nena kuhusu Mgodi wa Dhahabu.

Ikiwa una hata chembe ya Ufunuo , nadhani yeye analiweka wazi kweli hilo; Ujumbe na mjumbe ni MMOJA . Je, unasikia alichosema… MMOJA !! Basi Enyi Wahudumu, hamwezi kumtenganisha mjumbe na Ujumbe.

Unatakiwa kumweka MJUMBE kanisani mwako pamoja na UJUMBE aliouleta vinginevyo wewe haukubali UJUMBE WOTE. WEWE SI BIBI-ARUSI.

Loo! Tena, jambo hilo linaufanya Ujumbe na mjumbe kuwa ni kitu kimoja. Chakula cha kiroho kiko tayari, na kiko katika wakati wake sasa.

Kwetu sisi, tunaoamini saa ya Mungu tunayoishi, mjumbe Aliyemtuma, kila Neno alilonena; mambo haya ni Chakula kilichofichwa.

Jinsi tunavyoupenda Ujumbe huu, na unapowazia tu, “Kunawezaje kuwa mengine zaidi?” Yeye Anaweka jiwe la kifuniko juu Yake kwa kutuambia sisi ni nani sasa.

Hivi hamwoni mamlaka ya Mungu aliye hai katika Kanisa lililo hai, Bibi-arusi ? Wagonjwa wanaponywa, wafu wanafufuliwa, viwete wanatembea, vipofu wanaona, Injili inatangazwa katika nguvu Zake, kwa maana Ujumbe na mjumbe ni kitu kimoja. Neno liko ndani ya Kanisa, katika mtu.

Neno Hilo NDANI YETU . Sisi ni Ujumbe. Tunayo mamlaka. Ujumbe huu na sisi NI MMOJA!! Nena kuhusu kububujika tena na tena na tena.

Bibi-arusi ni sehemu ya Mume, Kanisa ni sawa na Kristo. “Kazi nizifanyazo Mimi ninyi nanyi mtazifanya.”

Sisi ni sehemu ya Mume!!

SISI NI SAWA NA KRISTO!!

Unafikiri inasikika sasa vizuri , na kuubariki moyo wako kwa kusoma tu nukuu hizi, subiri tu mpaka uisikie Sauti ya Mungu ikikuelezea hizo mdomo kwa sikio Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville,( ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya tanzania na Kenya pia) tunaposikia: 65-0718E. Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake.

Umealikwa kuja kuungana nasi. Kama huwezi, BONYEZA PLAY wakati wowote, Ujumbe wowote, mahali popote, na umsikie mjumbe wa Mungu akikuletea Ujumbe wa Mungu.

Ndugu. Joseph Branham.

Ndivyo ilivyo leo, ya kwamba Chakula cha Uzima ambacho watoto wanakula, kinafuata Ujumbe wa Mungu, kuwahifadhi katika wakati wa ukame.

Maandiko ya kusoma kabla ya Kusikiliza Ujumbe :

1 Wafalme 17:1-7
Amosi 3:7
Yoeli 2:28
Malaki 4:4
Luka 17:30
Yohana 14:12

23-0101 Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake

Ujume: 65-0718M Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 12MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi anayeelekea kwenye nchi ya Ahadi,

Je, ni kitu gani kinachoenda kutukia Mwaka huu Mpya?

Bibi-arusi amejiweka mwenyewe tayari kwa kukaa na Neno. Tumefanya Ushirika, tumeweka ile Ishara kwenye nyumba zetu, na kujitia muhuri wenyewe kwa Neno la kweli, lililothibitishwa. Hatujapatana, bali tumejiweka wenyewe mabikira kwa Sauti ya kweli ya Mungu.

Ni wakati wenye fahari vipi tunaoishi. Ni wakati ambao manabii wote walitamani kuuona; saa hii. Twajua kwa mambo ya asili kwamba Kanisa linajiweka tayari kuondoka. Saa za mwisho za kufunga zinawadia nasi tunafifia katika Umilele. Ni lazima tukae kwenye mstari na kuyaweka macho yetu kwenye Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya wakati wetu: Neno Lake, nabii Wake, ambaye ndiye Neno la wakati wetu.

Alimletaje Kristo hapa? Kwa Neno la manabii. Sivyo? Angeleta Bibi-arusi Wake hapa jinsi gani? Kwa Neno la manabii.

Ifanyweje? Tutafanya nini? Alitueleza jambo litupasalo kufanya: tumtake shauri nabii, Biblia, ambapo hatuwezi kuongeza au kupunguza. Kama tukifanya hivyo, Mungu atatuondoa katika Kitabu cha Uzima.

Muda umeenda sana, ili sisi kuwa Bibi-arusi wake lnatubidi tuwe katika Mapenzi yake makamilifu . Hatutaki kamwe Kumtendea Mungu Kazi bila Mapenzi yake, haijalishi inasikika nzuri vipi. Mungu alifanya ahadi jinsi angetenda leo. Mungu amelinena papa hapa katika Neno Lake jinsi angelitenda.

Atachukuaje Bibi-arusi Wake? Kwa Neno, sio kwa gari jipya, si kwa wazo la mwanatheologia, lakini kulingana na Neno Lake atamtambulisha. Usiweke kitu kimoja katika hilo au kuondoa kitu kimoja toka hilo sasa. Liache jinsi lilivyo. Unaona?

Kwa watu wengine, inaweza kuwachanganya sana kwani kuna manabii wengi wapakwa mafuta wasemao kuwa Mapenzi ya Bwana ya wakati huu ni yapi. Wanasema: “Ni makosa kucheza kanda kanisani, Ndugu Branham hakuwahi kamwe kusema jambo hilo. Wahudumu ndilo jambo lililo muhimu zaidi kwa sasa , na ndio njia iliyoandaliwa na Mungu kwa wakati huu. Kaa na mchungaji wako.”

Kwa hiyo, je, ni sawa kusikiliza kanda, lakini si kanisani? Je, Hatupaswi kuamini kila Neno lililo kwenye kanda, ila yale tu Roho Mtakatifu atuambiayo kipi ni Neno na kipi si Neno? Je, Kuwasikiliza wahudumu ndiko kutamkamilisha Bibi-arusi? Nisipokaa na mchungaji wangu siwezi kuwa Bibi-arusi? Je, Kama nikicheza tu kanda, niko nje ya Mapenzi makamilifu ya Mungu?

Kila mwamini anataka kufanya yaliyo sahihi na kuwa katika Mapenzi makamilifu ya Mungu. Hakuna anayetaka kuwa makosani au kuwa katika Mapenzi Yake yakuruhusia. Lazima kuwe na njia iliyo sahihi na ya kweli.

Ni wahudumu gani tunaopaswa kuwasikiliza…je, ni wote? Je! yatubidi kuchunguza yale wanayosema ikiwa ni Neno tunaporudi nyumbani kwa kusikiliza kanda, au tunapaswa tu kuchukua neno lao kwa jambo hilo? Yakini ni nini basi, je, ni neno la mchungaji wetu, ama ni yale Ndugu Branham aliyosema kwenye kanda?

Wanapaswa kuhubiri Neno, amina. Wanapaswa kuweka Neno mbele ya watu, amina. Lakini hawapaswi kuchukua mahali pa nabii wa Mungu. Wao si muhimu zaidi kuliko Sauti ya Mungu iliyothibitishwa. Wanaweza TU KUSEMA YALIYO KWENYE KANDA. Hiyo ndiyo Yakini ya Bibi-arusi.

Lazima zako tano ndizo hizo. Lazima iwe hivyo; wakati Wake; majira Yake wakati aliposema itakuwa; na mtu yule aliyemchagua, na lazima ije kwa nabii; na nabii yule lazima awe nabii aliyethibitishwa.

Mimi Sijaribu kushutumu Wahudumu ama kusema hawana mahali, Mungu apishe mbali. Ninasema tu, kuwachezea watu Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda ndilo jambo lililo muhimu sana ambalo wahudumu wanalopaswa kufanya. Chochote ninachosema, au mhudumu anachosema, au hata mshirika wakanisa anachosema, lazima yawe neno kwa neno yale nabii wa Mungu aliyosema.

Ninachukia kwamba unanikasirikia na unafikiri ninapingana na mchungaji wako, hilo silo lililo moyoni mwangu. Mimi Ninataka tu Bibi-arusi aungane pamoja kwa kitu KIMOJA PEKEE tunachoweza kuungana kwacho, UJUMBE HUU.

Katika wakati wa migawanyiko kama huu, mkanganyiko, tofauti kati ya watu, ninaamini Ujumbe huu tunaokwenda kuusikia Jumapili ni mojawapo ya Jumbe zilizo muhimu sana kwa wakati wetu.

Hebu na tufungue mioyo yetu na tuone kile Mungu analosema kwa kanisa, kwa watu wanaosikiliza kanda, na watu waliounganishwa kwa redio wanaosikiliza katika mataifa yote.

Kabla hatujaingia katika Nchi ya ahadi, kuna jambo tunalopaswa kufanya. Sauti ya Mungu inatutaka tusikilize kwa makini sana na tusikose kuelewa anachosema.

Alisema kama vile tu wakati Musa alipokuwa akizungumza na Israeli, baada ya yeye kuthibitishwa na Mungu na ile Nguzo ya Moto, na kujua alithibitishwa kuwa mtumishi wa Mungu kuwaongoza watoke . Lakini kabla hawajaenda katika nchi ile, aliwaambia: “ Naita mbingu na nchi kushuhudia dhidi yenu. Msiongeze kitu moja kwa yale niliyosema au kuondoa neno moja toka kwake.”

Nasema vivyo hivyo katika Jina la Yesu Kristo. Usiongeze kitu. Usiondoe—kuliwekea mawazo yako. Wewe sema tu yaliyosemwa katika kanda hizo. Tenda sawasawa kabisa na vile Bwana Mungu amekuamuru kutenda. Usiongezee Kwake.

Huyo ni BWANA MUNGU wetu akituamuru kwamba tunaweza KUSEMA TU YALIYOSEMWA KATIKA KANDA. Hatuwezi kuongezea kwake, kuondoa, kuweka mawazo yetu, fikira zetu, au fasiri yetu kwake. Sema tu yaliyosemwa katika kanda.

Ikiwa unaamini maneno haya yaliyonenwa na nabii wa Mungu aliyethibitishwa kuwa ni kweli, basi kwa nini KUBONYEZA PLAY kusiwe ndilo jambo lililo muhimu zaidi ambalo Bibi-arusi analoweza kufanya?

Alimtambulishaje alipokuja? Kwa mtu aliyekuwa na roho ya Eliya juu yake akitokea jangwani. Atamtambulishaje Bibi-arusi Wake? Aliahidi katika Malaki 4 kitu kile kile kabla ya kuiharibu dunia kama ilivyokuwa katika siku za Sodoma.

Mpendwa Bibi-arusi wa nchi ya Ahadi, unao UFUNUO wa kweli. Uko katika Mapenzi Makamilifu ya Mungu. Umejitambua wewe ni nani. Uko katika Mpango wa Mungu kwa Kubonyeza Play. Wewe ni Neno. Wewe ni sehemu ya Bwana arusi. UTUKUFU!!!

Ni njia gani ya kuanza Mwaka Mpya. Bibi-arusi waliungana pamoja, wakifuata amri ya Mungu kwa, Kubonyeza Play .

Njoo ujiweke Mwenyewe tayari kwa Unyakuo pamoja nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville,( ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Tanzania na Kenya pia ) tunaposikia: 65-0718M ” Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake .”

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma kabla ya Kusikiliza Ujumbe :

Kumbukumbu la Torati 4:1-4 / 4:25-26
1 Mambo ya Nyakati 13
1 Mambo ya Nyakati 15:15
Zaburi 22
Marko 7:7
Yoeli 2:28
Amosi 3:7
Malaki 3
Mathayo 11:1-15
1 Wakorintho 13:1

22-1231 Lile Shindano & Ushirika

Ujume: 62-1231 Lile Shindano

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 13MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Wapendwa kundi wenyeji,

Ningependa tuwe na Ushirika kwa mara nyingine tena katika nyumba zetu katika Mkesha wa Mwaka Mpya, tarehe 31 Desemba. Maelekezo ya jinsi ya kupata divai, na jinsi ya kuoka mkate wa ushirika yanaweza kupatikana katika anuani zilizo hapa chini. Anuani yakupakua Sauti ya Ibada itapatikana hivi karibuni kwenye tovuti yetu. Au, unaweza kucheza sauti ya ibada kutoka kwenye programu ya Lifeline.

Kwa wenyeji katika eneo la Jeffersonville, mnaweza kutwaa divai ya Ushirika Ijumaa, tarehe 30 Desemba, kati ya saa 7:00 saba mchana – saa 10:00 kumi jioni, chini ya dari la VGR.

Tutasikiliza 62-1231 Lile Shindano , kuanzia Saa 11:00 Kumi na moja jioni, Majira ya Mashariki ya Kati ( ambayo ni saa Saba Usiku ya Tanzania) siku ya Jumamosi, tarehe 31 Desemba . Baada ya Ndugu Branham kuleta Ujumbe wa Mkesha wa Mwaka Mpya, tutasimamisha kanda na kuwa na takriban dakika 10 za Nyimbo za Kuabudu tunapojiandaa kwa ajili ya Meza ya Bwana. Kisha tutabonyeza kuendeleza tena kanda hiyo mahali ambapo Ndugu Branham anaanzisha ibada ya Ushirika. Kwenye kanda hii, anaacha sehemu ya ibada ya kutawadhana miguu, ambayo nasi tutazingatia hilo pia ( Hatutatawadhana miguu pia) .

Tunapogeukia mwaka mwingine katika Huduma Yake, hebu na tuyaweke wakfu maisha yetu upya Kwake kwa kulisikiliza Neno kwanza, na kisha kushiriki Meza Yake. Ni nafasi nzuri jinsi gani tuliyo nayo kwa mara nyingine tena ya kufanya nyumba zetu kuwa mahali Patakatifu ili kumkaribisha Mfalme wa Wafalme aje kujumuika nasi.

Mungu awabariki,

Ndugu Joseph

22-1225 Kuonea Haya

UJUMBE: 65-0711 Kuonea Haya

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Rebeka Bibi-arusi,

Baba amemtuma mtumishi Wake mwaminifu, Eliezeri, kumwinda Bibi-arusi Rebeka Wake . Tumemtambua, malaika-mjumbe Wake wa saba, William Marrion Branham, ambaye Yeye amemwagiza: Kumwita, Kumkusanya, Kumwongoza na hatimaye Kututambulisha sisi , Kwake.

Ametumiminia Nguvu Zake za Kuhuisha nyingi na ametuleta katika utambuzi wa mahali petu, nafasi yetu, na wajibu wetu, tukiwa watu walioitwa, waliotengwa na ulimwengu, waliowekwa wakfu kwa Mungu. Anatuongoza na kutuelekeza katika mambo tunayofanya na kuyanena, na kuleta heshima na utukufu kwa Jina Lake.

Hakuna kitu, popote, kinachoweza kututenganisha na Hicho, HAKUNA CHOCHOTE. Tumelindwa Milele katika Ufalme wa Mungu. Baba amepiga Muhuri Wake juu yetu hadi mwisho wa safari yetu.

Shetani anatupiga konde mchana na usiku. Yeye anatusema kila kitu, na kutushtaki, na kujaribu kutufanya tufikiri ya kwamba sisi si Bibi-arusi huyo. Anatupa kila kitu njiani mwetu kujaribu kutuvuruga, kama ugonjwa na huzuni, lakini hatumsikilizi. Hiyo Nguvu ya Kuhuisha imo SASA HIVI ndani yetu nasi tumetiwa muhuri na moyo wetu upo kwenye Neno hilo. Tunaruka juu ya ngamia wetu, tukimkimbilia Yeye tukielekea kwenye Karamu yetu kuu ya Harusi.

Hatuonei haya kile tunachoamini; kinyume chake, tunataka ulimwengu ujue, SISI NI WATU WA KANDA TUNAOAMINI KILA NENO LILILOSEMWA NA NABII WAKE MWAMINIFU ELIEZERI aliyemtuma kumwita BIBI-ARUSI REBEKA WAKE atoke na kumwongoza. Hatuongezi kwake au kuondoa hata Neno MOJA. Ujumbe huu ni Yakini yetu.

Yawezekanaje Mtu ambaye amejazwa na Roho Mtakatifu, amejaa Nguvu za Mungu, na upendo wa Mungu moyoni mwake, anawezaje kuongea na mtu kwa dakika chache tu na asitaje jambo fulani kuhusu Ujumbe ambao ametoka kuusikia kwenye Kanda?

Unapokutana na watu wanaodai kuwa waamini katika Ujumbe huu wa wakati wa mwisho, unaweza kuzungumza nao kwa dakika chache tu na unaweza kujua pale wanaposimama kuhusu kucheza kanda. Wao ni aidha Watu wa Kanda ama sio.

Haliwaziki kwamba wanaona kuwa ni aibu, au hata ni kosa, ikiwa unasema unacheza kanda kanisani mwako au nyumbani mwako. Wanahisi ni kinyume cha Neno na si Njia ya Mungu iliyoandaliwa . Unadharauliwa kwa sababu unasema wewe ni “Mtu wa Kanda”.

Wahudumu wanaocheza kanda katika makanisa yao wanadhiakiwa, na hata kuitwa wavivu. Na iwapo unasikiliza kanda ile ile kwa wakati mmoja , vema, wewe hata si mhudumu, wewe ni dhehebu, ama mwabudu mtu.

Nadhani wale watu wote kabla yetu ambao waliyokuwa kwenye mawasiliano ya simu katika makanisa yao na majumbani mwao, wakimsikiliza Ndugu Branham wote kwa wakati mmoja, yawezekana walikuwa ni madhehebu pia. Huenda walikuwa nje ya Mpango wa Mungu. Hawakuonea haya NA WALA SISI PIA HATUONEI HAYA.

Ndani ya dakika chache tu unapozungumza na watu, watakujulisha mara moja papo hapo ni upi msimamo wao: Ndiyo, Tunabonyeza Play. Ndiyo, tunasikiliza kanda Jumapili Kanisani mwetu ama majumbani mwetu. Ndiyo, kanda ile ile, kwa wakati mmoja.

Kwa nini wengine husema, “Tunaenda kanisani Jumapili asubuhi, Jumapili usiku, na Jumatano usiku. Tunaye mchungaji mzuri sana; analiweka wazi sana na kwa dhairi sana kwetu sisi kuelewa. Anaufafanua Ujumbe ili niweze kuuelewa. Unahitaji kuwa na mhudumu ili uwe Bibi-arusi. Ndugu Branham hakusema kamwe kucheza kanda kanisani.”

Ni kipi basi unachosema ndilo jambo lililo muhimu zaidi? je, ni kile Wahubiri wasemacho, ni kile Ndugu Joseph asemacho, ama ni kile isemacho Sauti hasa ya Mungu mwenyewe kwenye Kanda? Yakini yako ni nini? ni kile kilicho kwenye Kanda , au ni kile mtu fulani asemacho?

Wahudumu ni wazuri, na katika Neno. Tunawahitaji. Lakini ni kipi MUHIMU ZAIDI , kuhubiri au Kanda?

Ikiwa Kanda hizi si jambo lililo muhimu zaidi katika maisha yako ya kibinafsi, katika maisha yako ya kanisa, basi kuna kasoro fulani . Umetoka kwenye Mpango wa Mapenzi makamilifu ya Mungu. RUDI KWENYE MSTARI.

Mtu anapokutana na Mungu; si katika kuuchochea mhemko, shauku fulani, ama fundisho fulani la kidini, katekismo fulani ama kanuni ya imani, ama fundisho la sharti ambalo amelikubali kwa ajili ya kuji—kujifariji, lakini wakati kweli anapofikia mahali kama vile Musa alivyopafikia, upande wa nyuma ya jangwa, akutane uso kwa uso na Mwenyezi Mungu, nawe unaiona hiyo Sauti ikisema nawe, imeambatana kabisa na Neno na ahadi ya wakati huo , kuna kitu inachokufanyia! Unaona, huionei haya, inakufanyia kitu fulani.

Katika siku yetu hii, utaji huo wa mapokeo umepasuliwa. Na hii hapa Nguzo ya Moto imesimama, ikidhihirisha Neno la siku hii. Uungu uliofunikwa katika mwili wa mwanadamu. Utukufu wa Shekinah kwa siku yetu ya leo. Mungu akisimama na kunena mbele zetu, amefunikwa katika mwili wa mwanadamu.

Musa alikuwa na Neno. Sasa kumbukeni, baada ya Neno kudhihirishwa, Musa alikuwa ni Musa tena. Mnaona? Lakini wakati Neno hilo lilipokuwa ndani Yake lipate kutolewa, yeye alikuwa ni Mungu; vema, yeye hakuwa ni Musa tena. Yeye alikuwa na Neno la Bwana kwa ajili ya wakati huo.

Ni sherehe ya KRISTO iliyoje ambayo sisi akina Rebeka tutakayokuwa nayo Jumapili hii. Siku nzima, kwa masaa tofauti siku nzima. Tutakuwa tukimsikia Eliezeri wetu akimwita Bibi-arusi wake atoke nasi tutakuwa tukimwambia hatuonei haya.

Bwana na awape sherehe ya KRISTO ya kupendeza, iliyojaa “UWEPO WAKE.”

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: 65-0711 Kuonea Haya

Maandiko ya kusoma Kabla kusikiliza ujumbe :

Marko Mtakatifu  8:34-38