Category Archives: Uncategorized

24-0414 Makao Ya Baadaye Ya Bwana Arusi Wa Mbinguni Na Bibi-Arusi Wa Duniani

UJUMBE: 64-0802 Makao Ya Baadaye Ya Bwana Arusi Wa Mbinguni Na Bibi-Arusi Wa Duniani

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Chumvi ya dunia,

Ee Bibi-arusi mpendwa, tunakuwa na wakati ulioje, tumeketi pamoja katika ulimwengu wa roho, katika uwepo wa Neno, tukikomaa, tukijitambua sisi ni nani, tunatoka wapi, na wapi tunakoenda.

Kujua, kutoka katika vilindi vya mioyo YETU, hivi SASA sisi ni wana na binti za Mungu. Si ati tutakuwa, tupo SASA HIVI. Sisi ni sifa za mawazo ya Mungu.

Shetani anapotushambulia, na kujaribu kutuonyesha makosa yetu, maisha yetu ya nyuma, na kushindwa kwetu kwa kila siku; anapojaribu kutuvunja akilini mwetu na rohoni kwa uwongo wake, tunamkumbusha tu na kumwambia, “Mungu, tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, aliniona mimi; hiyo ni kweli ewe Shetani, MIMI, naye akamtuma Yesu kunikomboa MIMI.” PIGA!

“Sasa Shetani, niache, kwa maana Damu ya Mwanawe yanena kwa ajili YANGU. Siwezi kutenda dhambi. Kukosea kwangu, ndio, makosa yangu mengi, hayo hata hayawezi kuonekana na Mungu. Kitu pekee Anachosikia ni sauti YANGU ikimuabudu na kumsifu Yeye, na kitu pekee Anachokiona ni uwakilisho WANGU.”

Uwakilisho wetu unatukusanya kutoka mashariki na magharibi, kaskazini na kusini, na kutuunganisha chini ya Neno aliloliandaa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake kwenye kanda. Ndilo jambo pekee atakaloliheshimu; kwa maana ndio Njia yake Yeye aliyoiandaa.

Anaenda kutuambia nini na kutufunulia kitu gani baadaye? Tumemsikia Yeye akinena kupitia nabii Wake mara nyingi sana akituambia kuhusu jinsi gani Makao yetu mapya yatakavyokuwa, lakini wakati huu itakuwa kana kwamba hatukuwahi kusikia lolote kulihusu wakati wowote ule.

Mjenzi wa Kiungu ameubuni huu kwa ajili ya mpendwa Wake. Mnaona? Loo! ni mahali pa jinsi gani, wakati, Tabia ya Mungu, Mjenzi Hodari wa Kiungu ameubuni kwa ajili ya sifa za Kiungu ambazo zimechaguliwa Kiungu tangu zamani na Mungu Mtakatifu Ambaye—Ambaye ndiye Mwanzilishi wa Uzima wa Mungu! Huo Mji utakuwaje! Wazia jambo hilo.

Hatuwezi kujizuia. Kuchangamshwa kwetu na matarajio yetu yapo kileleni. Mioyo yetu inaenda mbio kumsikia Mungu akinena nasi moja kwa moja na kutuambia kuwa hivi sasa anaandaa na kuyabuni Makao yetu mapya ili tuweze kuishi Milele yote pamoja Naye.

Tutasikia kipi kingine, na kitu gani kitakachofunuliwa kwetu Jumapili, Wakati anapotuambia kila kitu kuhusu Kuchaguliwa tangu zamani, Uwakilisho, Kipindi cha wakati, Siku ya Nane, Mlima Mtakatifu, Piramidi, na Kusanyiko Takatifu?

Je, tunaweza kuyafunga mawazo yetu kote kwa yale yanayotokea hivi sasa? Mungu anamkusanya Bibi-arusi Wake kutoka ulimwenguni kote ili aweze kutuambia jinsi gani Makao yetu mapya yatakavyokuwa. Yeye atatuambia kwa undani kila taarifa ndogo. Tutakuwa na wakati uliotukuka jinsi gani.

Kwa upande mwingine, vita vyetu havijawahi kupungua makali. Shetani anatushambulia kuliko wakati mwingine wowote. Mashambulizi yake hayaonekani kuwa mepesi ama kuondoka.

Lakini UTUKUFU kwa Mungu, IMANI yetu katika Neno lake haijawahi kuinuliwa kama hivi. IMANI yetu ya kujijua sisi ni nani imetia nanga ndani kabisa ya Nafsi yetu, hata hatuwezi kutetereka.

Sisi HATUNA cha kuogopa; HAKUNA cha kuhofia. Baba Yeye ndiye anayehusika kwa ajili yetu kikamilifu. Anatuongoza na kutuelekeza KILA HATUA ZETU. Ametushika katika kiganja cha Mkono Wake. Shetani ni mwongo tu ambaye mwisho wake uko karibu, naye anajua hilo. Yeye ndiye anayeogopa, anajua anashughulika na Bibi-arusi-Neno Lililonenwa wa Mungu naye hushindwa kila wakati.

Sisi NI NENO. Tulikuwa ndani yake tangu mwanzo. Si kwamba tutakuwa hivyo siku moja, TUKO HIVYO SASA HIVI. Ikiwa sisi ni Neno, basi tunaweza KUNENA NENO, IKIWA TU TUTAAMINI… NASI TUNAAMINI.

Wewe ni aidha mwamini (NENO) ama wewe ni mwenye mashaka (SI NENO). Hakuna hata kiungo kimoja katika miili yetu kisichoamini Neno moja. Haya basi! Tumemthibitishia Shetani hivi punde: sisi ni Neno. Twaweza kuwa ngozi iliyo chini ya unyayo, LAKINI BADO TU SEHEMU YA ULE MWILI!!!

Kwa hiyo wakati huyo mwongo anapomjia mmoja wetu, Bibi-arusi anakusanyika kutoka ulimwenguni kote nasi TUNAMPIGA na KUMPIGA kwa Neno.

Ugonjwa unapomjia mmoja wetu, sisi huungana pamoja na KUMPIGA! Wakati mmoja wetu apatapo kujisikia kudhoofu na kushushwa moyo, sisi sote hufanya kitu gani? HUMPIGA!

Tunaenda Nyumbani, Ewe Bibi-arusi. Wakati umefika. Bibi-arusi amejiweka mwenyewe tayari. Tuko ndani ya Safina. Yeye Amefunga mlango nasi tuko ndani salama. Tunaweza kusikia muziki wa Bibi-arusi ashuke akitembea kwenye safu kuungana na Bwana-arusi.

Tutakuwa kwenye fungate yetu kwa miaka 1000, kisha tutaenda pamoja na kila mmoja na Yeye kwenye Makao yetu ya Baadaye.

Msilikose, Enyi marafiki. Kuna njia moja tu iliyoandaliwa na kuthibitishwa na Mungu: KANDA. Ni Nguzo ya Moto ikinena na kumwongoza Bibi-arusi Wake.

Lolote ufanyalo, iweke Sauti hiyo mbele yako na familia yako Jumapili hii. Imani chanzo chake ni kusikia, kulisikia Neno, na Neno huja kwa nabii. Roho Mtakatifu ni Nabii wa siku yetu akinena na Bibi-arusi Wake kwa Kanda.

Mnakaribishwa kuungana nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) wakati sehemu ya Bibi-arusi watakapoungana pamoja kumsikiliza Mungu, wote kwa wakati mmoja, akinena kupitia malaika Wake mwenye nguvu akituambia yote kuhusu: Makao Ya Baadaye Ya Bwana Arusi wa Mbinguni na Bibi-arusi wa Duniani 64-0802.

Ndugu. Joseph Branham

24-0407 Mabirika Yavujayo

UJUMBE: 64-0726E Mabirika Yavujayo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wanywaji Wa Kisima Kinachofoka Maji,

Bibi-arusi kamwe hatakuwa yeye yule tena baada ya wikendi ya Pasaka iliyo kuu ambayo Bwana aliyotupa. Tulikuwa tumefungiwa ndani pamoja Naye, tukishirikiana na kumwabudu Yeye wikendi yote. Uwepo wake ulizijaza nyumba zetu na makanisa yetu.

Tulikuwa chini ya matarajio makubwa kweli. Tulijua haya yalikuwa Mapenzi ya Bwana kwetu. Mungu alikuwa anajitayarisha kufanya jambo fulani. Tukafunga ulimwengu na vizubaishi vyake vyote. Tuliungana kutoka kote ulimwenguni kwa nia moja. Tulikuwa tumeketi pamoja katika mahali pa mbinguni, Tukijitayarisha vile ANGEZUNGUMZA NASI njiani.

Mioyo yetu ilikuwa ikilia, “Bwana, nifanye nifanane na Wewe zaidi. Nitayarishe kwa ajili ya huku kuja Kwako hivi karibuni. Nipe Ufunuo zaidi. Roho Wako Mtakatifu akijaze kila kiungo cha utu wangu.”

Wakati kila ibada ilipoanza, tulijiambia wenyewe, “Inawezekanaje? Nimezisikia Jumbe hizi maisha yangu yote, lakini sasa hivi zote zinaonekana kuwa mpya, kana kwamba sijawahi kuzisikia hapo awali. Yeye alikuwa akilifunua Neno Lake mioyoni na nafsini mwetu zaidi ya hapo awali”.

Ufunuo ufurikao ukaja tena ndani ya mioyo yetu… Ni Yeye… YEYE. Ni Roho Mtakatifu Mwenyewe AKIONGEA NASI MOJA KWA MOJA.

Sio mimi! Yeye! Yeye Ndiye! Ndio kwanza niwaambie, Yeye aliuchukua tu mwili wangu. Yeye huuchukua tu ulimi wangu, anayachukua macho yangu, kwa sababu Yeye alijua ningeyasalimisha Kwake, kwa hiyo Yeye alikuja tu na kunifanya nifanye hivyo. Kwa hiyo si mimi! Ni Yeye! Wala si mimi huko nje pamoja nanyi, ni Yeye huko nje pamoja nanyi. Yeye ndiye Ufufuo na Uzima. Loo, Mungu, Mungu; liamini. Loo, enyi watu: Mwaminini. Mwaminini. Yeye yupo hapa.

Yeye ametupa Ufunuo wa kujua HIZI KANDA ndiyo Sauti ya Mungu inayonena nasi leo hii. Hizo Kanda ndio Maneno Yake, Sauti Yake…SAUTI YAKE, iliyorekodiwa na KUHIFADHIWA ili tuweze KUMSIKIA YEYE akinena nasi Maneno ya uzima wa Milele. Hizo ndiyo njia Yake iliyoandaliwa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake.

Ni matamu, masafi, Maji ya kisima yakibubujika na kububujika. Kadiri tulivyokunywa, ndivyo tulivyozidi kupaza sauti, “Zaidi Bwana, ZAIDI. Kijaze kikombe changu Bwana, kijaze Bwana”. Naye akakijaza! Kadiri tunavyozidi kunywa, ndivyo ANAVYOZIDI KUTUPA.

Kisha shetani akatamkwa ameshindwa kwa nguvu za Injili. Kwa Mungu wa Mbinguni Yule Aliyemchagua na Kumtuma Malaika Wake Atuhubirie Injili. Kwa Mungu Yule Aliyeliandika Neno na Kumtuma Malaika Wake ambaye Aliyekuwepo Kulithibitisha Neno Lake. “Toka ndani ya hawa watu, katika Jina la Yesu Kristo”.

ILIMBIDI ibilisi kumwacha kila mgonjwa, kila mtu anayeteseka. Sasa nguvu za Mungu zimetufufua tumepata afya njema na nguvu tena.

Kisha, kutoka ndani ya kilindi cha mioyo yetu tulisema:

“Mimi sasa nakubali ya kwamba Yesu Kristo, kama Mwana wa Mungu aliyefufuka, Yeye ni Mwokozi wangu, Yeye ni Mfalme wangu, Yeye ni Mponya wangu. Sasa nimepona. Nimeokoka. Nitamwishia Yeye aliyenifia. Nitasimama kutoka hapa katika upya wa maisha, nipate kusonga mbele nikafanye vizuri niwezavyo Kwake…kwa ajili Yake Yeye aliyefufuka kwa ajili yangu. Haleluya!”

Hiki ni Kisima Kinachofoka Maji tunachokinywea kila siku. Ndicho kisima pekee kinachotoka moja kwa moja kutoka Mbinguni kinachotiririka daima. Kinajitegemea chenyewe. Daima ni matamu na masafi. Hayajakufa na kuoza. Ni Maji ya uzima yanayobadilika kila wakati, yakifunua jambo jipya kwa Bibi-arusi kila wakati.

Daima kinabubujika. Haitubidi kuyavuta kwa mashine, kuyavuta kwa winchi, kuyapindisha, ama kujiunga nayo. Ni chemchemi ya Mungu ya Maji ya uzima, nasi hatuwezi kufikiri kunywa kitu kingine chochote.

Tunasikia leo, “Maji yetu ndio maji bora unayopaswa kunywa. Tumeyaweka kwenye mchakato wetu wa uchujaji wa hatua ya 7. Kisha tumeongeza madini yote TULIYOYACHUJA tumeyarudishamo tena katika maji tunayodhani mnahitaji kuongeza maji mwilini.

Utukufu kwa Mungu, haitupasi kubahatisha au kuhoji ikiwa kile tunachokunywa ama kile kilichoongezwa ama kuchujwa. KILA KITU tunachohitaji kiko katika Maji yetu.Tunachotakiwa tu kufanya ni KUBONYEZA PLAY na kunywa kama kibubujikavyo.

Ni faraja iliyoje kuyanywa Maji haya. Tungetoka kwenda maili nyingi ili tu kunywa kwenye hilo, lakini haitupasi kufanya hivyo. Tunalibeba kila mahali tuendapo. Majumbani mwetu, makanisani mwetu, kazini, tuendeshapo katika magari yetu, tuendapo matembezini… TUNAKUNYWA, NA KUNYWA, NA KUNYWA.

Ee ulimwengu, njooni mnywe kutoka kwenye Chemchemi iliyotolewa na Mungu. Ndio mahali PEKEE huhutaji kuwa na wasiwasi na kusema, “Naomba Roho Mtakatifu atanilinda ili nisije nikanywa kitu chochote nisichotakiwa kunywa.” LOTE NI NENO SAFI LILILOTHIBITISHWA LIKITIRIRIKA KUTOKA KWENYE CHEMCHEMI ZA MBINGUNI.

Hakuna mahali pengine Panapofaa Bibi-arusi Wake kunywa!

Njoo Unywe pamoja nasi kwenye Kisima chetu Kinachofoka maji Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) tunaposikia: Mabirika Yavujayo 64-0726E.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Zaburi 36:9
Yeremia 2:12-13
Yohana Mtakatifu 3:16
Ufunuo Sura ya 13

Pasaka 2024

Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo,

Kalvari inapaswa kukumbukwa kila siku. Tumesikia mengi sana kuihusu. Tumesoma mengi sana juu yake. Wahubiri wameihubiri tangu mwanzo wa wakati. Waimbaji wameimba juu yake katika nyakati zote. Manabii walitabiri miaka elfu nne kabla haijatukia, na manabii wa siku hizi wanatuonyesha kule nyuma ilipotendeka. Ni siku muhimu sana.

Ni moja ya siku zilizo muhimu sana ambazo Mungu amepata kuzishusha duniani.

Ni kukusanyika kwa kipekee kulikoje kutoka ulimwenguni kote ambako Bibi-arusi atakuwanako wikendi hii ya Pasaka. Tutafunga milango yetu na kuuzima ulimwengu wa nje. Tutazima vifaa vyetu vyote ili tusizubaishwe, na tuongee Naye kabisa kabisa kila siku. Tutainua sauti zetu kwake kwa upatano, kwa nia moja na moyo mmoja, kumsifu, kumwabudu, kumwambia jinsi gani tunavyompenda.

Tutasikia Sauti Yake ikizungumza na mioyo yetu tunapoyaweka upya maisha yetu Kwake. Hakuna kitakachokuwa muhimu zaidi kwetu wakati tunapojitayarisha kwa ajili ya Ujio Wake wa hivi karibuni. Bibi-arusi anajiweka mwenyewe tayari zaidi ya hapo awali.

Ningependa sote tuungane kwenye ratiba ifuatayo:

ALHAMISI

Ilikuwa ni Alhamisi usiku ambapo Bwana Yesu alikula Karamu ya Mwisho na wanafunzi wake, katika ukumbusho wa Pasaka kabla ya kule kutoka kwa wana wa Israeli. Ni fursa iliyoje tuliyo nayo ya kuzungumza na Bwana katika nyumba zetu, kabla ya wikendi yetu takatifu, na kumwomba atusamehe dhambi zetu, na kutupa sisi sote yale tunayohitaji katika safari yetu.

Lijalie, Bwana. Waponye walio wagonjwa. Wafariji walio wachovu. Wape furaha wanaodhulumiwa. Wape amani walio wachovu, Chakula kwa wenye njaa, Maji kwa wenye kiu, furaha kwa wenye huzuni, uwezo kwa kanisa. Bwana, mlete Yesu miongoni mwetu usiku wa leo, tukiwa tunajitayarisha kushiriki ushirika unaowakilisha mwili Wake uliovunjwa-vunjwa. Tunaomba, Bwana, kwamba Yeye atatuzuru kwa njia ya ajabu sana…

Wabariki wengine, Bwana, kila mahali ulimwenguni, ambao wanangojea kwa furaha kuja kwa Bwana, taa zimetengenezwa, na dohani zimesuguliwa kabisa, na Nuru ya Injili ikiangaza katika sehemu zenye giza.

Hebu sote tuanze saa 12:00 KUMI NA MBILI JIONI. Masaa ya maeneo mnayoishi ili kusikia  Ushirika 62-0204, na kisha nabii atatupeleka katika Ibada yetu maalum ya Ushirika na Kutawadhana Miguu, ambayo itakuwa ikicheza kwenye app ya Lifeline (kwa Kiingereza), au unaweza kupakua ibada hii kwa Kiingereza ama lugha nyinginezo kwa kubofya anuani iliyo hapa chini.

Kufuatana na Ujumbe, tutakusanyika pamoja na familia zetu katika nyumba zetu na kula Meza ya Bwana.

IJUMAA

Hebu tuende katika maombi pamoja na familia zetu saa 3:00 TATU ASUBUHI,( ni saa 10:00 Kumi jioni ya Afrika Mashariki ) na kisha tena saa 6:00 SITA MCHANA,( ni saa 1:00 Moja jioni ya Afrika Mashariki ) tukimualika Bwana awe pamoja nasi na azijaze nyumba zetu na Roho Mtakatifu wakati tujiweka wakfu Kwake.

Hebu mawazo yetu na yarudi nyuma hadi siku ile pale Kalvari, zaidi ya miaka 2000 iliyopita, na kumwona Mwokozi wetu akining’inia msalabani, na kisha tujitoe vivyo hivyo kufanya daima yale yanayompendeza Baba:

Iwapo siku hii ni muhimu sana, moja ya siku zilizo kuu sana, hebu na tuangalie mambo matatu ambayo siku hiyo ilimaanisha kwetu. Tungechukua mamia. Bali asubuhi ya leo nimechagua tu mambo matatu tofauti yaliyo muhimu sana ambayo tunataka kuyachunguza katika muda mfupi ujao; ambayo Kalvari ilimaanisha kwetu. Nami naomba ya kwamba itamhukumu kila mwenye dhambi aliyeko, ya kwamba itamfanya kila mtakatifu kupiga magoti yake, ya kwamba itamfanya kila mgonjwa ainue imani yake kwa Mungu na aondoke ameponywa, kila mwenye dhambi aokolewe, kila aliyerudi nyuma arudi na ajionee aibu, na kila mtakatifu afurahi na apate tumaini jipya na tumaini jipya.

Kisha saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA,( Ni saa 1:30 Moja na Nusu jioni ya Afrika Mashariki ) tuungane pamoja katika nyumba zetu ili kusikia,  Siku Hiyo Pale Kalvari 60-0925.

Kisha tuungane tena pamoja katika maombi saa 9:00 TISA ALASIRI.( ni saa 4:00 Nne Usiku ya Afrika Mashariki ) katika ukumbusho wa kusulubishwa kwa Bwana wetu.

JUMAMOSI

Hebu sote kwa mara nyingine tena tuungane katika maombi saa 3:00 TATU ASUBUHI.( ni saa 10:00 Kumi jioni ya Afrika Mashariki ) na  saa 6:00 SITA MCHANA,( ni saa 1:00 Moja Jioni ya Afrika Mashariki ) na kuitayarisha mioyo yetu kwa ajili ya mambo makuu Atakayotutendea sisi katikati yetu.

Ninaweza kumsikia akisema, “Shetani, njoo hapa!” Yeye ni Bosi sasa. Ananyosha mkono, anaunyakua ule ufunguo wa mauti na kuzimu kutoka ubavuni mwake, akauning’iniza ubavuni Mwake Mwenyewe. “Ninataka kukupa notisi. Umekuwa laghai muda mrefu kutosha. Mimi ni Mwana wa Mungu aliye hai niliyezaliwa na bikira. Damu Yangu ingali imelowa msalabani, na deni kamili limelipwa! Huna haki tena. Umenyang’anywa zote. Nipe funguo hizo!”

Kisha saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, ( ni 1:30 moja na Nusu jioni ya Afrika Mashariki ) sote tutakusanyika ili kusikia NENO:  Kuzikwa 57-0420.

Hii itakuwa SIKU-KUU iliyoje kwa Bibi-arusi Wake ulimwenguni kote.

Kisha tuungane tena pamoja katika maombi saa 9:00 TISA ALASIRI ( Ni saa 4:00 Nne Usiku ya Afrika Mashariki ).

JUMAPILI

Hebu kwanza tuamke mapema kama Ndugu Branham alivyofanya asubuhi ile wakati rafiki yake mdogo, robin, alipomwamsha saa 11:00 KUMI NA MOJA ASUBUHI. Hebu tumshukuru tu Bwana kwa kumfufua Yesu kutoka kwa wafu:

Saa kumi na moja asubuhi ya leo, rafiki yangu mdogo mwenye kifua chekundu aliruka dirishani akaniamsha. Ilionekana kana kwamba moyo wake mdogo ungepasuka, akisema, “Amefufuka.”

Saa 3:00 TATU ASUBUHI. ( Ni saa 10:00 Kumi jioni ya Afrika Mashariki ) na saa 6:00 SITA MCHANA,( ni saa 1:00 Moja jioni ya Afrika Mashariki ) hebu tuungane kwa mara nyingine tena katika mnyororo wetu wa maombi, kuombeana mmoja kwa mwingine na kujitayarisha wenyewe kuisikia Sauti ya Mungu.

Saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, ( Ni saa 1:30 Moja na Nusu jioni ya Afrika Mashariki ) tutakusanyika pamoja ili kuusikia Ujumbe wetu wa Pasaka:  Muhuri wa Kweli wa Pasaka 61-0402.

Saa 9:00 TISA ALASIRI, ( ni saa 4:00 Nne usiku ya Afrika Mashariki ) tuungane tena katika maombi, tukimshukuru Yeye kwa WIKENDI YA AJABU ALIYOTUPA PAMOJA NAYE NA PAMOJA NA BIBI-ARUSI WAKE ULIMWENGUNI KOTE.

Kwa ndugu na dada zangu walio nchi za ng’ambo, kama mwaka jana, ningependa kuwaalika kuungana nasi kwa masaa ya Jeffersonville, kwa masaa yote ya maombi yaliyo kwenye ratiba hii. Ninatambua, hata hivyo, kwamba kuzicheza Kanda ya Alhamisi, Ijumaa, na Jumamosi alasiri kwa masaa ya Jeffersonville kungekuwa vigumu sana kwa wengi wenu, kwa hivyo tafadhali jisikieni huru kucheza Jumbe hizo kwa masaa yafaayo kwenu. Ningependa, hata hivyo, tuungane pamoja Jumapili saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 1:30 MOJA NA NUSU Jioni masaa ya Afrika Mashariki ) ili kuusikia Ujumbe wetu wa Jumapili pamoja.

Ningependa pia kuwaalika ninyi na watoto wenu kuwa sehemu ya vipindi vya Ubunifu, Journaling, na maswali ya majaribio ya YF, ambayo familia yako yote yaweza kufurahia pamoja. Twaamini utayapenda kwa kuwa yote yanahusiana na NENO tutakalosikia wikendi hii.

Kwa ratiba ya wikendi, taarifa ya jinsi ya kujiandaa kwa ajili ya ibada ya Ushirika, nyenzo zitakazohitajika kwa ajili ya vipindi vya ubunifu, Maswali ya jaribio la Pasaka, na taarifa nyinginezo, tazama anuani zilizo hapa chini.

Hebu na tuzifunge simu zetu kwa ajili ya wikendi ya Pasaka isipokuwa kupiga picha, kusikia Nukuu ya Siku, na kucheza kanda kwenye app ya the Table, app ya Lifeline, au anuani za kupakua.

Ni heshima kubwa kwangu kukualika wewe na familia yako kukusanyika pamoja na Bibi-arusi ulimwenguni kote katika wikendi iliyojaa KUABUDU, SIFA NA UPONYAJI. Ninaamini kweli hakika ni wikendi ambayo itayabadilisha maisha yako milele.

Ndugu Joseph Branham

24-0324 Kutambua Siku Yako Na Ujumbe Wake

UJUMBE: 64-0726M Kutambua Siku Yako Na Ujumbe Wake

PDF

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapenzi Watu Wathamani na Wapendwa,

Inapendeza sana jinsi gani kujua sisi ndio Bibi-arusi Wake mpendwa na Wathamani. Tumefanyizwa kutoka ulimwenguni kote, tukikusanyika pamoja kulizunguka Neno Lake, tukisikiliza Sauti ya Mungu ikizilisha nafsi zetu.

Tumelikubali katika ukamilifu wake, na katika nguvu ya kuthibitishwa kwake na ufunuo wake. Tumekuwa sehemu Yake. Ni kitu ambacho kiko ndani yetu. Ni zaidi ya uhai kwetu.

Tumetambua: Malaika-Mjumbe Wake wa Saba.
Tumetambua: Ujumbe wa Nuru ya Jioni.
Tumetambua: Sisi ni Nani.

Mungu amechukua Neno la nabii Wake na kutubangua. Ametukata kwa Malaki 4, kama alivyoahidi angefanya. Tunaamini kila Neno kwa mioyo yetu yote.

Kuna uamsho mkubwa unaoendelea miongoni mwa watu. Wao pia wanatambua umuhimu wa kuisikia Sauti hiyo. Wanataka kurudi na kuzicheza kanda katika makanisa yao.

Wamejulishwa na Roho Mtakatifu, kwamba hii ndiyo Njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku hii. Wanatambua kuwa hii ndio Sauti wanayohitaji kuisikia. Ndicho Chakula cha Mungu kilichohifadhiwa kwa ajili ya kumkamilisha Bibi-arusi Wake.

Neno liliahidi jambo Hilo. Kanda zinalitangaza. Wao wanaliamini.

Ilifanyaje? Iliwasumbua makuhani, kuona hao watu wakiondoka makanisani na kwenda zao. Akasema, “Kama yeyote wenu akihudhuria mikutano Yake, mtatengwa na ushirika. Tutawafukuza moja kwa moja kutoka katika dhehebu.”

Haliaminiki, lakini hilo limekuwa ni jambo lile lile leo hii. Watakufukuza katika makanisa yao ukisema, “Tafadhali, chezeni kanda.” Je! Hivi tumewahi kamwe kuwazia huenda hiki ndicho kinachowatenganisha watu? Kuicheza Sauti ya Mungu katika makanisa yetu?

Kanisa limesahau manabii wao. Wao “hawawahitaji tena,” ndivyo wanavyodai. Bali Mungu anajua hana budi kuwa nao; Yeye huwakata watu Wake kwa Neno Lake. Lakini kwao Hilo limepitwa na wakati sana katika siku hii.

Tutakaa na nabii wetu. Tunaamini kuwa ndio Sauti inayomwita Bibi-arusi Wake. Kwetu sisi, hakuna kitu chochote kilicho muhimu zaidi ya KUBONYEZA PLAY.

Loo, enyi kondoo za Mungu, sikilizeni Sauti ya Mungu! “Kondoo Wangu huisikia Sauti Yangu.”

Njoo uisikie na uitambue Sauti hiyo pamoja nasi, Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) tunaposikia,  Kutambua Siku Yako na Ujumbe Wake 64-0726M.

Ndugu. Joseph Branham

24-0317 Kuenda Nje Ya Kambi

UJUMBE: 64-0719E Kuenda Nje Ya Kambi

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Askari Wakristo,

Wazieni jambo hilo! Ni mwisho wa wakati, Haleluya! Tumewasili. Ile Siku kuu ya Kuja kwa Bwana kumchukua Bibi-arusi Wake imekaribia. Tunakusanyika wenyewe pamoja kutoka ulimwenguni kote, tukikamilishwa kwa kusikiliza Sauti ya Mungu. Tunatazamia na kungojea wapendwa wetu watokee… ni siku yoyote sasa.

Kitu pekee ambacho tumeagizwa kufanya ni “Dumuni na Neno”. Yote tuyaonayo ni Yesu, na Yeye ni Neno lililofanyika mwili. Huo ndio Ufunuo wa siku yetu. Hiyo ndio Kambi ya Mungu kwa ajili ya Bibi-arusi Wake.

Ujumbe huu, Sauti hii, kanda hizi, ndicho kila kitu tunachohitaji kwa ajili ya Unyakuo. Hatuhitaji kitu kingine chochote. Tumeitwa tutoke, tumetengwa na kila kitu kingine isipokuwa ile Sauti. Tumeshawishika kuwa Sauti hiyo ndiyo Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii.

Wazieni jambo hilo, Yeye ametupatia nabii mkuu wa nyakati zote. Yule ambaye Nguzo ya Moto Mwenyewe alipiga picha naye ili aweze kuuambia ulimwengu, “Huyu ni malaika wangu mwenye nguvu. Yeye ni Sauti Yangu kwenu. Yale Anenayo duniani Mimi nitarudisha mwangwi mbinguni. Hakuna aliye kama yeye”.

“Nimemkabidhi yeye, na yeye peke yake, siri Zangu zote nilizozificha tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu. Yeye ndiye niliyemchagua tangu awali kuwaita NINYI mtoke katika ulimwengu huu mje Kwangu. Yeye ndiye niliyemchagua kuwatangulia, kuwaongoza, na kuwaelekeza. Nawatangazieni, msikieni Yeye, kwa maana si yeye anenaye, NI MIMI, YULE MIMI NIKO ALIYE MKUU.

Nimewaweka wakfu watu wakuu na kuwaita kuutangazia ulimwengu na kuuambia , “Leo maandiko ya Malaki 4, Ufunuo 10:7 na Luka 17:30 yametimia mbele ya macho yenu. Yule Malaika wake mwenye nguvu amewasili, kama jinsi Maandiko yalivyotangaza. Mungu yuko hapa miongoni mwetu, akijifunua Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu kama alivyosema angefanya.”

Ni Yesu Kristo yeye yule jana, leo na hata milele. Tumeitwa kuwaelekeza ninyi kwake yeye, malaika wa Mungu. Yeye ndiye ambaye Roho Mtakatifu alimchagua kuongoza na kumwita Bibi-arusi Wake atoke. Msihojiane, msibishane, msigombane na kushindana ni nani atakayekuwa kuhani mkuu; nani anayetakiwa kuwa hili, lile, ama linginelo. DUMUNI NA SAUTI HIYO. Kwa maana kuna SAUTI YA MUNGU moja tu iliyothibitishwa na jina lake ni William Marrion Branham.

Yatupasa kuwa waangalifu sana kudumu na hiyo Sauti, kwa kuwa kuna wengi wanaotaka kuwaongoza kwingineko. Mapokeo yao yanaiweka Sauti hiyo ya kweli mbali na watu. Yeye amekuwa mgeni kwa wengi wao. Sauti yao imepachukua mahali pa Sauti hiyo, hata wakati Mungu, kwa njia ya kanda, anapowazuru, Yeye ni mgeni.

Ule uwepo mkuu wa Agosti u pamoja nasi. Mtu yeyote mwepesi wa kuhisi Roho anaweza kujua Sauti hiyo ni Sauti ya Mungu. Ndio ile Kambi ya Mungu kwa ajili ya siku hii.

Kila mtu anayedai kuwa Bibi-arusi wa Kristo lazima aamue ni Kambi gani aliyomo. Ni lazima wajiulize swali hili rahisi: Hivi ni Sauti gani ambayo Bibi-arusi wote wanaweza kusema “AMINA” kwayo?

Kama kweli wewe ni Bibi-arusi wa Kristo, mwenye Ufunuo wa kweli wa Neno la siku hii, kuna jibu moja tu: Sauti ya Mungu iliyo kwenye Kanda. Bila shaka Shetani anajaribu kuliendesha hilo kwa njia nyingi tofauti, lakini hakuna jibu lingine kwa Bibi-arusi. Ni rahisi jinsi hiyo.

Sote tunajua kwamba Shetani anatumia jibu hilo ili kutugawanya. Lakini Neno linatuambia Bibi-arusi hana budi KUUNGANA… TUMEUNGANA, kwa SAUTI PEKEE INAYOTUUNGANISHA.

Njoo uungane nasi, kwa maana ile saa imechelewa sana.

“Nataka kwenda nje ya kambi. Haidhuru itanigharimu nini, nitautwaa msalaba wangu na kuubeba kila siku. Nitatoka nje ya kambi. Hata watu waseme nini juu yangu, nataka kumfuata nje ya kambi. Niko tayari kwenda.”

Ikiwa unataka kuwa katika ile Kambi ya Mungu ya siku hii, LAZIMA UAMINI Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda ndio Sauti iliyo muhimu sana unayopaswa kuisikia.

Njoo uungane na sehemu ya Bibi-arusi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) tunapoisikia ile Sauti ambayo Mungu aliyoichagua kumwongoza Bibi-arusi Wake, anapotuletea Ujumbe, Kuenda Nje ya Kambi 64-0719E.

Sio “kambi fulani”; ni “ILE KAMBI”.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Ibada :

Waebrania 13:10-14
Mathayo 17:4-8

24-0310 Sikukuu Ya Baragumu

UJUMBE: 64-0719M Sikukuu Ya Baragumu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Watoto wa Nuru,

Tunayo shukurani jinsi gani kuwa tunatembea katika Nuru Yake. Kuwa sehemu ya Nuru hiyo, kutambulishwa na Nuru Yake. Kuitwa na kuchaguliwa Na Yeye. Sisi ni Bibi-arusi wa Kristo, tumetambulishwa pamoja Naye. Hao wawili sasa ni Mmoja.

Nisingeweza kuliandika mara nyingi sana. Hatuwezi kulisema vya kutosha. Ujumbe huu unamaanisha KILA KITU kwetu. Kujua kuwa tunao Ufunuo wa kweli wa Neno Lake ni zaidi ya chochote tungeweza kuweka kwa maneno.

Kuishi katika siku hii na kuwa sehemu ya kile kinachotendeka, ndio heshima iliyo kuu ambayo Mungu angeweza kutupa. Jinsi lilivyokuwa jambo kuu kuketi katika mikutano katika Maskani ya Branham, kuona na kumsikia malaika wa Mungu akizileta Jumbe hizi, ni KUU hata na zaidi kule kuishi katika siku hii, na wakati huu, na kuwa ule utimilifu wa Neno hilo.

Mungu, katika Mpango Wake mkuu, ameandaa Njia ambayo tungeweza kukusanyika kutoka ulimwenguni kote, kuisikiliza Sauti ya Mungu sote kwa wakati mmoja, ili kukamilishwa na Neno Lake. Kusubiri kusikia katika sekunde yoyote malaika-mjumbe wetu wa saba aseme;

“Tazama Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!”

Hakujawahi kuwa na kitu chochote kama Hicho tangu mwanzo wa wakati. Kule Kumalizika kwa Mpango mkuu wa Mungu kunatukia, SASA HIVI, na sisi tu sehemu Yake. Ile Siku kuu ya Bwana imekaribia.

Siri zote zimefunuliwa kwa Bibi-arusi na malaika-mjumbe wa Mungu. Ile Mihuri, zile Nyakati, Ngurumo, Imani ya Kunyakuliwa, Mvuto wa Tatu…KILA KITU kimekwishanenwa na kiko kwenye kanda ili Bibi-arusi aweze kuzisikia tena na tena, nayo INATUKAMILISHA.

Roho Mtakatifu amerudi Kanisani tena; Kristo, Mwenyewe, akifunuliwa katika mwili wakibinadamu, wakati wa jioni kama alivyoahidi.

Sikiliza kwa makini sasa ewe Bibi-arusi, likamate.

Tumeitwa na Neno; Kristo mwenyewe ametuita. Amejiweka mwenyewe dhahiri kwetu; Waebrania 13:8, Luka 17:30, Malaki 4, Waebrania 4:12, Maandiko haya yote aliyoahidi.

Ni Yesu, Mwana wa Mungu, ambaye amejifunua kwetu kwa Maandiko haya ambayo yaliyochaguliwa tangu zamani kwa ajili ya siku hii, YAISHI TENA.

Na, kuamini Hilo, ndio dhihirisho la Roho Mtakatifu.

Mungu alimtuma nabii Wake kumwita Bibi-arusi Wake atoke. Neno linatuambia nabii ni Neno lililo hai la Mungu, lililodhihirishwa. Ndio ishara ya mwisho ambayo ulimwengu utakayopata; Yehova akinena katika umbo la mwanadamu.

Mtu katika mwili wa kibinadamu, kama nabii, hata hivyo ilikuwa ni Elohimu akilitambua wazo lililokuwa katika moyo wa Sara, nyuma Yake. Naye Yesu alisema, “Kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, ndivyo itakavyokuwa katika ukamilifu wa dahari, wakati Mwana wa Adamu,” si Mwana wa Mungu, “wakati Mwana wa Adamu atakapokuwa akifunua.”

Bibi-arusi anajua isipokuwa uwe daima katika Neno, hutajua Yeye ni nani. Wao wanajua umuhimu wa kuiweka Sauti hiyo mbele zao kila siku kwa Kubonyeza Play.

Sasa Bibi-arusi hana budi kuondoka jukwaani, na kwenda juu, ili wale manabii wawili wa Mungu katika Ufunuo waweze kutokea jukwaani ili kupiga Baragumu ya Saba. Kuwajulisha Kristo.

Njoo uwe sehemu ya unabii uliotimia Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) wakati nabii wa Mungu anapoleta Ujumbe, Sikukuu ya Baragumu 64-0719M, na kuzungumza na Baba na kusema,

Yawezekana kuwe na baadhi huko nje katika mataifa, ulimwenguni kote, ambao hata kanda hii ingewakuta manyumbani mwao au makanisani mwao. Tungeomba, Bwana, kwamba wakati ibada inaendelea, pale—pale…au kanda inachezwa, au nafasi yo yote tunayoweza kuwamo, au—au hali, yule Mungu mkuu wa Mbinguni na aheshimu huu unyofu wa mioyo yetu asubuhi hii, na kuponya wahitaji.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Walawi 16 yote
Walawi 23:23-27
Isaya 18:1-3
Isaya 27:12-13
Ufunuo 10:1-7
Ufunuo 9:13-14
Ufunuo 17:8