Category Archives: Uncategorized

23-0101 Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake

Ujume: 65-0718M Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 12MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi anayeelekea kwenye nchi ya Ahadi,

Je, ni kitu gani kinachoenda kutukia Mwaka huu Mpya?

Bibi-arusi amejiweka mwenyewe tayari kwa kukaa na Neno. Tumefanya Ushirika, tumeweka ile Ishara kwenye nyumba zetu, na kujitia muhuri wenyewe kwa Neno la kweli, lililothibitishwa. Hatujapatana, bali tumejiweka wenyewe mabikira kwa Sauti ya kweli ya Mungu.

Ni wakati wenye fahari vipi tunaoishi. Ni wakati ambao manabii wote walitamani kuuona; saa hii. Twajua kwa mambo ya asili kwamba Kanisa linajiweka tayari kuondoka. Saa za mwisho za kufunga zinawadia nasi tunafifia katika Umilele. Ni lazima tukae kwenye mstari na kuyaweka macho yetu kwenye Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya wakati wetu: Neno Lake, nabii Wake, ambaye ndiye Neno la wakati wetu.

Alimletaje Kristo hapa? Kwa Neno la manabii. Sivyo? Angeleta Bibi-arusi Wake hapa jinsi gani? Kwa Neno la manabii.

Ifanyweje? Tutafanya nini? Alitueleza jambo litupasalo kufanya: tumtake shauri nabii, Biblia, ambapo hatuwezi kuongeza au kupunguza. Kama tukifanya hivyo, Mungu atatuondoa katika Kitabu cha Uzima.

Muda umeenda sana, ili sisi kuwa Bibi-arusi wake lnatubidi tuwe katika Mapenzi yake makamilifu . Hatutaki kamwe Kumtendea Mungu Kazi bila Mapenzi yake, haijalishi inasikika nzuri vipi. Mungu alifanya ahadi jinsi angetenda leo. Mungu amelinena papa hapa katika Neno Lake jinsi angelitenda.

Atachukuaje Bibi-arusi Wake? Kwa Neno, sio kwa gari jipya, si kwa wazo la mwanatheologia, lakini kulingana na Neno Lake atamtambulisha. Usiweke kitu kimoja katika hilo au kuondoa kitu kimoja toka hilo sasa. Liache jinsi lilivyo. Unaona?

Kwa watu wengine, inaweza kuwachanganya sana kwani kuna manabii wengi wapakwa mafuta wasemao kuwa Mapenzi ya Bwana ya wakati huu ni yapi. Wanasema: “Ni makosa kucheza kanda kanisani, Ndugu Branham hakuwahi kamwe kusema jambo hilo. Wahudumu ndilo jambo lililo muhimu zaidi kwa sasa , na ndio njia iliyoandaliwa na Mungu kwa wakati huu. Kaa na mchungaji wako.”

Kwa hiyo, je, ni sawa kusikiliza kanda, lakini si kanisani? Je, Hatupaswi kuamini kila Neno lililo kwenye kanda, ila yale tu Roho Mtakatifu atuambiayo kipi ni Neno na kipi si Neno? Je, Kuwasikiliza wahudumu ndiko kutamkamilisha Bibi-arusi? Nisipokaa na mchungaji wangu siwezi kuwa Bibi-arusi? Je, Kama nikicheza tu kanda, niko nje ya Mapenzi makamilifu ya Mungu?

Kila mwamini anataka kufanya yaliyo sahihi na kuwa katika Mapenzi makamilifu ya Mungu. Hakuna anayetaka kuwa makosani au kuwa katika Mapenzi Yake yakuruhusia. Lazima kuwe na njia iliyo sahihi na ya kweli.

Ni wahudumu gani tunaopaswa kuwasikiliza…je, ni wote? Je! yatubidi kuchunguza yale wanayosema ikiwa ni Neno tunaporudi nyumbani kwa kusikiliza kanda, au tunapaswa tu kuchukua neno lao kwa jambo hilo? Yakini ni nini basi, je, ni neno la mchungaji wetu, ama ni yale Ndugu Branham aliyosema kwenye kanda?

Wanapaswa kuhubiri Neno, amina. Wanapaswa kuweka Neno mbele ya watu, amina. Lakini hawapaswi kuchukua mahali pa nabii wa Mungu. Wao si muhimu zaidi kuliko Sauti ya Mungu iliyothibitishwa. Wanaweza TU KUSEMA YALIYO KWENYE KANDA. Hiyo ndiyo Yakini ya Bibi-arusi.

Lazima zako tano ndizo hizo. Lazima iwe hivyo; wakati Wake; majira Yake wakati aliposema itakuwa; na mtu yule aliyemchagua, na lazima ije kwa nabii; na nabii yule lazima awe nabii aliyethibitishwa.

Mimi Sijaribu kushutumu Wahudumu ama kusema hawana mahali, Mungu apishe mbali. Ninasema tu, kuwachezea watu Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda ndilo jambo lililo muhimu sana ambalo wahudumu wanalopaswa kufanya. Chochote ninachosema, au mhudumu anachosema, au hata mshirika wakanisa anachosema, lazima yawe neno kwa neno yale nabii wa Mungu aliyosema.

Ninachukia kwamba unanikasirikia na unafikiri ninapingana na mchungaji wako, hilo silo lililo moyoni mwangu. Mimi Ninataka tu Bibi-arusi aungane pamoja kwa kitu KIMOJA PEKEE tunachoweza kuungana kwacho, UJUMBE HUU.

Katika wakati wa migawanyiko kama huu, mkanganyiko, tofauti kati ya watu, ninaamini Ujumbe huu tunaokwenda kuusikia Jumapili ni mojawapo ya Jumbe zilizo muhimu sana kwa wakati wetu.

Hebu na tufungue mioyo yetu na tuone kile Mungu analosema kwa kanisa, kwa watu wanaosikiliza kanda, na watu waliounganishwa kwa redio wanaosikiliza katika mataifa yote.

Kabla hatujaingia katika Nchi ya ahadi, kuna jambo tunalopaswa kufanya. Sauti ya Mungu inatutaka tusikilize kwa makini sana na tusikose kuelewa anachosema.

Alisema kama vile tu wakati Musa alipokuwa akizungumza na Israeli, baada ya yeye kuthibitishwa na Mungu na ile Nguzo ya Moto, na kujua alithibitishwa kuwa mtumishi wa Mungu kuwaongoza watoke . Lakini kabla hawajaenda katika nchi ile, aliwaambia: “ Naita mbingu na nchi kushuhudia dhidi yenu. Msiongeze kitu moja kwa yale niliyosema au kuondoa neno moja toka kwake.”

Nasema vivyo hivyo katika Jina la Yesu Kristo. Usiongeze kitu. Usiondoe—kuliwekea mawazo yako. Wewe sema tu yaliyosemwa katika kanda hizo. Tenda sawasawa kabisa na vile Bwana Mungu amekuamuru kutenda. Usiongezee Kwake.

Huyo ni BWANA MUNGU wetu akituamuru kwamba tunaweza KUSEMA TU YALIYOSEMWA KATIKA KANDA. Hatuwezi kuongezea kwake, kuondoa, kuweka mawazo yetu, fikira zetu, au fasiri yetu kwake. Sema tu yaliyosemwa katika kanda.

Ikiwa unaamini maneno haya yaliyonenwa na nabii wa Mungu aliyethibitishwa kuwa ni kweli, basi kwa nini KUBONYEZA PLAY kusiwe ndilo jambo lililo muhimu zaidi ambalo Bibi-arusi analoweza kufanya?

Alimtambulishaje alipokuja? Kwa mtu aliyekuwa na roho ya Eliya juu yake akitokea jangwani. Atamtambulishaje Bibi-arusi Wake? Aliahidi katika Malaki 4 kitu kile kile kabla ya kuiharibu dunia kama ilivyokuwa katika siku za Sodoma.

Mpendwa Bibi-arusi wa nchi ya Ahadi, unao UFUNUO wa kweli. Uko katika Mapenzi Makamilifu ya Mungu. Umejitambua wewe ni nani. Uko katika Mpango wa Mungu kwa Kubonyeza Play. Wewe ni Neno. Wewe ni sehemu ya Bwana arusi. UTUKUFU!!!

Ni njia gani ya kuanza Mwaka Mpya. Bibi-arusi waliungana pamoja, wakifuata amri ya Mungu kwa, Kubonyeza Play .

Njoo ujiweke Mwenyewe tayari kwa Unyakuo pamoja nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville,( ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Tanzania na Kenya pia ) tunaposikia: 65-0718M ” Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake .”

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma kabla ya Kusikiliza Ujumbe :

Kumbukumbu la Torati 4:1-4 / 4:25-26
1 Mambo ya Nyakati 13
1 Mambo ya Nyakati 15:15
Zaburi 22
Marko 7:7
Yoeli 2:28
Amosi 3:7
Malaki 3
Mathayo 11:1-15
1 Wakorintho 13:1

22-1231 Lile Shindano & Ushirika

Ujume: 62-1231 Lile Shindano

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 13MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Wapendwa kundi wenyeji,

Ningependa tuwe na Ushirika kwa mara nyingine tena katika nyumba zetu katika Mkesha wa Mwaka Mpya, tarehe 31 Desemba. Maelekezo ya jinsi ya kupata divai, na jinsi ya kuoka mkate wa ushirika yanaweza kupatikana katika anuani zilizo hapa chini. Anuani yakupakua Sauti ya Ibada itapatikana hivi karibuni kwenye tovuti yetu. Au, unaweza kucheza sauti ya ibada kutoka kwenye programu ya Lifeline.

Kwa wenyeji katika eneo la Jeffersonville, mnaweza kutwaa divai ya Ushirika Ijumaa, tarehe 30 Desemba, kati ya saa 7:00 saba mchana – saa 10:00 kumi jioni, chini ya dari la VGR.

Tutasikiliza 62-1231 Lile Shindano , kuanzia Saa 11:00 Kumi na moja jioni, Majira ya Mashariki ya Kati ( ambayo ni saa Saba Usiku ya Tanzania) siku ya Jumamosi, tarehe 31 Desemba . Baada ya Ndugu Branham kuleta Ujumbe wa Mkesha wa Mwaka Mpya, tutasimamisha kanda na kuwa na takriban dakika 10 za Nyimbo za Kuabudu tunapojiandaa kwa ajili ya Meza ya Bwana. Kisha tutabonyeza kuendeleza tena kanda hiyo mahali ambapo Ndugu Branham anaanzisha ibada ya Ushirika. Kwenye kanda hii, anaacha sehemu ya ibada ya kutawadhana miguu, ambayo nasi tutazingatia hilo pia ( Hatutatawadhana miguu pia) .

Tunapogeukia mwaka mwingine katika Huduma Yake, hebu na tuyaweke wakfu maisha yetu upya Kwake kwa kulisikiliza Neno kwanza, na kisha kushiriki Meza Yake. Ni nafasi nzuri jinsi gani tuliyo nayo kwa mara nyingine tena ya kufanya nyumba zetu kuwa mahali Patakatifu ili kumkaribisha Mfalme wa Wafalme aje kujumuika nasi.

Mungu awabariki,

Ndugu Joseph

22-1225 Kuonea Haya

UJUMBE: 65-0711 Kuonea Haya

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Rebeka Bibi-arusi,

Baba amemtuma mtumishi Wake mwaminifu, Eliezeri, kumwinda Bibi-arusi Rebeka Wake . Tumemtambua, malaika-mjumbe Wake wa saba, William Marrion Branham, ambaye Yeye amemwagiza: Kumwita, Kumkusanya, Kumwongoza na hatimaye Kututambulisha sisi , Kwake.

Ametumiminia Nguvu Zake za Kuhuisha nyingi na ametuleta katika utambuzi wa mahali petu, nafasi yetu, na wajibu wetu, tukiwa watu walioitwa, waliotengwa na ulimwengu, waliowekwa wakfu kwa Mungu. Anatuongoza na kutuelekeza katika mambo tunayofanya na kuyanena, na kuleta heshima na utukufu kwa Jina Lake.

Hakuna kitu, popote, kinachoweza kututenganisha na Hicho, HAKUNA CHOCHOTE. Tumelindwa Milele katika Ufalme wa Mungu. Baba amepiga Muhuri Wake juu yetu hadi mwisho wa safari yetu.

Shetani anatupiga konde mchana na usiku. Yeye anatusema kila kitu, na kutushtaki, na kujaribu kutufanya tufikiri ya kwamba sisi si Bibi-arusi huyo. Anatupa kila kitu njiani mwetu kujaribu kutuvuruga, kama ugonjwa na huzuni, lakini hatumsikilizi. Hiyo Nguvu ya Kuhuisha imo SASA HIVI ndani yetu nasi tumetiwa muhuri na moyo wetu upo kwenye Neno hilo. Tunaruka juu ya ngamia wetu, tukimkimbilia Yeye tukielekea kwenye Karamu yetu kuu ya Harusi.

Hatuonei haya kile tunachoamini; kinyume chake, tunataka ulimwengu ujue, SISI NI WATU WA KANDA TUNAOAMINI KILA NENO LILILOSEMWA NA NABII WAKE MWAMINIFU ELIEZERI aliyemtuma kumwita BIBI-ARUSI REBEKA WAKE atoke na kumwongoza. Hatuongezi kwake au kuondoa hata Neno MOJA. Ujumbe huu ni Yakini yetu.

Yawezekanaje Mtu ambaye amejazwa na Roho Mtakatifu, amejaa Nguvu za Mungu, na upendo wa Mungu moyoni mwake, anawezaje kuongea na mtu kwa dakika chache tu na asitaje jambo fulani kuhusu Ujumbe ambao ametoka kuusikia kwenye Kanda?

Unapokutana na watu wanaodai kuwa waamini katika Ujumbe huu wa wakati wa mwisho, unaweza kuzungumza nao kwa dakika chache tu na unaweza kujua pale wanaposimama kuhusu kucheza kanda. Wao ni aidha Watu wa Kanda ama sio.

Haliwaziki kwamba wanaona kuwa ni aibu, au hata ni kosa, ikiwa unasema unacheza kanda kanisani mwako au nyumbani mwako. Wanahisi ni kinyume cha Neno na si Njia ya Mungu iliyoandaliwa . Unadharauliwa kwa sababu unasema wewe ni “Mtu wa Kanda”.

Wahudumu wanaocheza kanda katika makanisa yao wanadhiakiwa, na hata kuitwa wavivu. Na iwapo unasikiliza kanda ile ile kwa wakati mmoja , vema, wewe hata si mhudumu, wewe ni dhehebu, ama mwabudu mtu.

Nadhani wale watu wote kabla yetu ambao waliyokuwa kwenye mawasiliano ya simu katika makanisa yao na majumbani mwao, wakimsikiliza Ndugu Branham wote kwa wakati mmoja, yawezekana walikuwa ni madhehebu pia. Huenda walikuwa nje ya Mpango wa Mungu. Hawakuonea haya NA WALA SISI PIA HATUONEI HAYA.

Ndani ya dakika chache tu unapozungumza na watu, watakujulisha mara moja papo hapo ni upi msimamo wao: Ndiyo, Tunabonyeza Play. Ndiyo, tunasikiliza kanda Jumapili Kanisani mwetu ama majumbani mwetu. Ndiyo, kanda ile ile, kwa wakati mmoja.

Kwa nini wengine husema, “Tunaenda kanisani Jumapili asubuhi, Jumapili usiku, na Jumatano usiku. Tunaye mchungaji mzuri sana; analiweka wazi sana na kwa dhairi sana kwetu sisi kuelewa. Anaufafanua Ujumbe ili niweze kuuelewa. Unahitaji kuwa na mhudumu ili uwe Bibi-arusi. Ndugu Branham hakusema kamwe kucheza kanda kanisani.”

Ni kipi basi unachosema ndilo jambo lililo muhimu zaidi? je, ni kile Wahubiri wasemacho, ni kile Ndugu Joseph asemacho, ama ni kile isemacho Sauti hasa ya Mungu mwenyewe kwenye Kanda? Yakini yako ni nini? ni kile kilicho kwenye Kanda , au ni kile mtu fulani asemacho?

Wahudumu ni wazuri, na katika Neno. Tunawahitaji. Lakini ni kipi MUHIMU ZAIDI , kuhubiri au Kanda?

Ikiwa Kanda hizi si jambo lililo muhimu zaidi katika maisha yako ya kibinafsi, katika maisha yako ya kanisa, basi kuna kasoro fulani . Umetoka kwenye Mpango wa Mapenzi makamilifu ya Mungu. RUDI KWENYE MSTARI.

Mtu anapokutana na Mungu; si katika kuuchochea mhemko, shauku fulani, ama fundisho fulani la kidini, katekismo fulani ama kanuni ya imani, ama fundisho la sharti ambalo amelikubali kwa ajili ya kuji—kujifariji, lakini wakati kweli anapofikia mahali kama vile Musa alivyopafikia, upande wa nyuma ya jangwa, akutane uso kwa uso na Mwenyezi Mungu, nawe unaiona hiyo Sauti ikisema nawe, imeambatana kabisa na Neno na ahadi ya wakati huo , kuna kitu inachokufanyia! Unaona, huionei haya, inakufanyia kitu fulani.

Katika siku yetu hii, utaji huo wa mapokeo umepasuliwa. Na hii hapa Nguzo ya Moto imesimama, ikidhihirisha Neno la siku hii. Uungu uliofunikwa katika mwili wa mwanadamu. Utukufu wa Shekinah kwa siku yetu ya leo. Mungu akisimama na kunena mbele zetu, amefunikwa katika mwili wa mwanadamu.

Musa alikuwa na Neno. Sasa kumbukeni, baada ya Neno kudhihirishwa, Musa alikuwa ni Musa tena. Mnaona? Lakini wakati Neno hilo lilipokuwa ndani Yake lipate kutolewa, yeye alikuwa ni Mungu; vema, yeye hakuwa ni Musa tena. Yeye alikuwa na Neno la Bwana kwa ajili ya wakati huo.

Ni sherehe ya KRISTO iliyoje ambayo sisi akina Rebeka tutakayokuwa nayo Jumapili hii. Siku nzima, kwa masaa tofauti siku nzima. Tutakuwa tukimsikia Eliezeri wetu akimwita Bibi-arusi wake atoke nasi tutakuwa tukimwambia hatuonei haya.

Bwana na awape sherehe ya KRISTO ya kupendeza, iliyojaa “UWEPO WAKE.”

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: 65-0711 Kuonea Haya

Maandiko ya kusoma Kabla kusikiliza ujumbe :

Marko Mtakatifu  8:34-38

RATIBA YA KRISMASI!

Ndugu na Dada Wapendwa,

Kwa sababu ya Krismasi kuwa kwenye siku ya Jumapili mwaka huu, nimejisikia moyoni mwangu kutokuwa na wakati maalum wa sisi kusikiliza Ujumbe siku hiyo. Familia nyingi zina watoto wadogo ambao huchangamka sana kufungua zawadi zao asubuhi ya Krismasi, na itakuwa vigumu sana kwao kutulia kusikiliza Ujumbe au kuwafanya wangoje hadi wakati fulani baadaye.

Na, hata hivyo, kwenye Krismasi, mwajua, watoto wadogo, huwezi kuwaambia vinginevyo. Wao, ninii tu, ni wakati wa Krismasi kwao. Nao wasingetaka maskini soksi zao zitundikwe, kungekuwa na kitu fulani. Ni desturi, hata katika taifa letu, kwamba wanatundika soksi, na kitu kingine. Mbona, nilifanya hivyo, nilipokuwa mtoto, na—na ingawa liko mba—mbali sana na Maandiko, njia iliyowekwa kama lilivyo. Hata hivyo, watoto ni ninii, wanasikia watoto wengine wakisema, “Vema, nilipata hiki kwa ajili ya Krismasi. Nilipata hiki.” Jamaa hao wadogo wanasimama huku, wanaangalia, mwajua. Huwezi, huwezi kuwafanya waelewe. Unaona? Kwa hiyo, kwamba tu, Krismasi itadumu. Naam.

Pia kunaweza kuwe na wengine ambao wangependelea kuamka mapema na kusikiliza Ujumbe, kama walivyopanga na washiriki wengine wa familia zao baadaye siku hiyo. Kwa hiyo nimeamua kwa kila familia kuchagua wakati ambao ungelingana vyema na ratiba yao ya kusikiliza Ujumbe. Tutatangaza Ujumbe huo kwenye Lifeline mara tatu tofauti Siku ya Krismasi:  Saa 3:00 Tatu Asubuhi . – Saa 06:00 Sita Mchana. – Saa 11:00 Kumi na moja Jioni. Tafadhali usijisikie kuwa ni lazima usikilize wakati mmojawapo wa nyakati hizi, lakini chagua wakati unaofaa zaidi kwako au kwa familia yako. Jambo muhimu zaidi ni, KUBONYEZA PLAY.

Inaweza ionekane kwa namna fulani inachekesha, asubuhi hii, kuvaa kabuti langu jukwaani, bali nilifurahia sana ku—kuonyesha hilo kabuti zuri nililopewa na kanisa hili. Nilimuona Ndugu Neville hapa juzijuzi, amevaa ile suti ya kupendeza, jinsi ilivyomkaa vizuri mno, na nikawaza, vema, ni…Ilionekana nzuri mno, na kusanyiko langu linazungumzia habari zake, nikafikiri, “Nitavaa tu kabuti jukwaani.”

Unajua, ninaamini kamwe hatukui. Sikuzote tu…Nami sitaki kukua. Unalionaje hilo, Ndugu Luther? La, kamwe hatutaki kukua, tunapenda siku zote tu kudumu tukali watoto.

Bwana na awape Sikukuu yakupendeza iliyojaa Uwepo Wake.

Ndugu. Joseph Branham

22-1218 Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake?

UJUMBE: 65-0418E Je! Mungu Habadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake?

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Masihi Wadogo,

Sisi ni watiwa-mafuta wa Mungu; waliotiwa mafuta na Roho Wake yule yule, kwa kazi zile zile, kwa Nguvu zile zile, kwa ishara zile zile. Imetoka tai hadi tai, kutoka Neno hadi Neno mpaka utimilifu wa Yesu Kristo udhihirishwe katika kila mmoja wa miili yetu kwa hitaji la kimwili , kiroho, au hitaji lolote tunalohitaji. Hizo Nguvu za kuhuisha zinaishi na kukaa ndani yetu. Sisi ni Masihi wadogo wa Mungu.

Kila wiki Ufunuo wa Ujumbe huu; sisi ni nani, wapi tunatoka, na wapi tunakoenda, unakuwa mkubwa zaidi na zaidi. Twajiuliza kwa matarajio makuu, lawezaje kuwa tukufu zaidi? Laweza kuwa wazi zaidi kiasi gani? Lakini kwa kila kanda mpya tunayosikia, Mungu ananena nasi mdomo kwa sikio na kutufunulia zaidi Neno Lake, na kutuhakikishia, SISI NI NANI.

Shauku kubwa ya moyo wa kila mwamini ni kuwa katika MAPENZI MAKAMILIFU ya Mungu. Kamwe hatutaki kuwa katika mapenzi Yake ya kuruhusia. Mioyo yetu huvunjika na kupondeka ikiwa tunahisi tumefanya jambo lolote ambalo litamchukiza. Tunajua Mungu anayo Mapenzi makamilifu, nasi tunataka tu kuwa katika MPANGO WA MAPENZI YAKE MAKAMILIFU.

Katika maisha yangu, nimekuwa na msimamo mkali kwa kusema ninaamini jambo lililo muhimu zaidi ambalo kila mshiriki wa Bibi-arusi analoweza kufanya, washirika na wahudumu vilevile , ni KUBONYEZA PLAY . Ninaamini ndiyo Sauti ya Mungu PEKEE iliyothibitishwa kwa ajili ya Siku yetu ambayo lazima usikie na kutii kila Neno.

Nimesema ninaamini wahudumu wanahitajika kumrudisha Ndugu Branham kwenye mimbara zao na kucheza kanda katika makanisa yao, kwa kuwa Ndiyo Sauti moja muhimu sana iliyopo ambayo watu hawana budi kuisikia.

Nimepokea shutuma nyingi maishani mwangu kwa kuchukua msimamo huu kwa kile ninachoamini kuwa Mpango Wake na Mapenzi yake Makamilifu. Imeeleweka vibaya na kusemwa kwamba siamini katika huduma tano ya Waefeso 4.

Nimeeleza mara nyingi, nyingi sana huo ni uongo. Sijawahi kamwe kusema, wala sijawahi kuamini jinsi hiyo. Kuna wengi ambao wamepindisha maneno yangu na kuwaambia watu mambo ambayo sijawahi kusema ama kuamini, lakini hilo ni jambo la kutarajiwa.

Lazima kuwe na Kweli ya Neno la Biblia. Ikiwa unadai unaamini Ujumbe huu, basi hatuna budi kuchukua yale nabii aliyosema, kwani ndiyo fasiri halisi hasa ya Neno la Mungu. Kwa maana yeye ndiye mfasiri PEKEE wa Neno hilo.

Ikiwa ningewauliza kila mmoja wenu, “Ni nani anayetaka kuwa katika mapenzi makamilifu ya Mungu?”
Kila mmoja wenu angesema, “NDIYO, hiyo ndiyo haja ya moyo wangu.” Hivyo ni lazima tuangalie kwenye kile nabii alichosema ni Mapenzi Makamilifu ya Mungu.

KUMBUKA: Ikiwa Ujumbe huu ulio kwenye kanda si Yakini yako, na huamini kila Neno, ACHA KUSOMA BARUA HII. Kwangu mimi, wewe si mwamini, kwa hivyo sio kwa ajili yako. Mimi Ninaweza tu kukaa na yale Mungu aliyosema kwenye kanda.

Tunataka alichosema Yeye; si kile kanisa lilisema, kile alichosema Daktari Jones, kile alichosema mtu mwingine. Tunataka kile BWANA ASEMA HIVI ilichosema, kile Neno lilichosema.

Inatupasa kujikabidhi wenyewe kwenye mapenzi Yake na kwenye Neno Lake. Hatupaswi Kulitilia swali. Yatubidi Kuliamini tu. Usijaribu kutafuta njia ya kuliepa. Lichukue tu jinsi lilivyo.

Watu wengi wanajaribu kuepa, kupitia njia nyingine. Nawe unapofanya jambo hilo, Mungu atakuwa akikubariki, bali unafanya kazi katika mapenzi Yake ya kuruhusia wala si mapenzi Yake makamilifu, ya Kiungu. Mungu atakuruhusu kufanya jambo fulani, na hata akubariki katika kulifanya, bali hata hivyo si mapenzi Yake makamilifu.

Mungu alimtuma malaika-mjumbe wake wa saba duniani kumwita Bibi-arusi Wake atoke . Tunaamini ilikuwa ni Mwana wa Adamu akijifunua Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu. Ni Sauti yenyewe hasa ya Mungu ambayo imerekodiwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake.

Mungu mwenyewe alimwambia nabii wake, ukiwafanya watu WAKUAMINI , hakuna kitakachosimama mbele zako. Alikuwa ndiye aliyechaguliwa na Mungu kumwongoza Bibi-arusi Wake. Hakuna anayeweza kupachukua mahali pake. Haidhuru ni akina Kora wangapi walioinuka, ama Dathani wangapi, ilikuwa ni William Marrion Branham ambaye Mungu alimwita kumwongoza Bibi-arusi Wake. Huu ndio Mpango wa Mungu na MAPENZI YAKE MAKAMILIFU.

Iwapo watu hawatatembea katika mapenzi Yake makamilifu, Yeye ana mapenzi ya kuruhusia atakayokufanya uende kwayo.

Sasa, Mungu ni mwema…Yeye hutuma Neno Lake . Kama hutaamini Neno Lake, Basi ndipo anaweka katika Kanisa ofisi tano tofauti : Kwanza, mitume, manabii, walimu, wachungaji, wainjilisti. Ni kwa ajili ya kulikamilisha Kanisa.

Kwa hivyo, wahudumu waliinuliwa tu kwa sababu watu katika nyakati zote hawakukubali MPANGO WA MAPENZI MAKAMILIFU ya Mungu; Neno Lake lililonenwa na nabii Wake. Tunapaswa kuamini tu Neno ambalo nabii wa Mungu alilonena. Hatuhitaji mtu mwingine yeyote au kitu kingine chochote.

Basi kazi ya wahudumu ni KUWARUDISHA watu kwenye Mpango wa Mapenzi Yake Makamilifu, ambao ni: KAENI NA HIZO KANDA, KWA MAANA NI MAPENZI MAKAMILIFU YA MUNGU. Kisha weka MPANGO HUO WA MAPENZI MAKAMILIFU mbele zao kila wakati kwa: KUBONYEZA PLAY.

Huna budi kurudi na kuanzia mahali ulipoanzia, ama mahali ulipoachia, na kuchukua kila Neno la Mungu.

Kwa hivyo unapaswa kufanya nini ili uwe katika MAPENZI YAKE MAKAMILIFU : Kubonyeza Play .

Wachungaji wanapaswa kufanya nini ili wawe katika MAPENZI YAKE MAKAMILIFU: Kubonyeza Play.

Nabii wa Mungu alikuwa anafanyaje akienda kwenye mikutano? Kuombea tu wagonjwa, na kila kitu namna hiyo? Angesema mambo kwa njia isiyo dhahiri ambayo kondoo wangesikia, kwa sababu tunajua kile anachozungumzia. Ama kweli, ilikuwa tu ni chambo kwenye ndoano. Aliwaonyesha ishara kama utambuzi, na alijua siri za mioyo yao, ili tu kuwachochea watu. Lakini kisha akasema jambo muhimu zaidi lilikuwa ni :

Muda si muda, kanda inaangukia nyumbani mwao. Imelenga penyewe, basi. Kama yeye ni kondoo, anakuja moja kwa moja Nalo. Kama yeye ni mbuzi, anapiga hiyo kanda teke.

Je, Wewe ni kondoo au ni mbuzi? Kundi dogo la Mungu moyo wake uko kwenye Neno hilo. Tuko katika Mapenzi Yake Makamilifu kwa Kubonyeza Play kwa kuwa huo ulikuwa, na ndio, Mpango wake wa asili.

Kaa moja kwa moja na Neno Lake, maana hilo ndilo litakalotokea mwishoni, lile Neno, Neno kwa Neno. “Ye yote atakayeondoa Neno moja Kwake, ama kuongeza neno moja Kwake!” Halina budi kudumu, Neno hilo.

Ninamshukuru sana Bwana kujua, kwa Ufunuo wa kiroho, ya kwamba niko katika Mapenzi Yake Makamilifu kulingana na Neno Lake. Siongezi fasiri yangu Kwake, ama ufahamu wangu Kwake, bali ninasikia kwa masikio yangu BWANA ASEMA HIVI na Mapenzi Yake Makamilifu ni kitu gani .

Ninakualika uje Ukatafute madini pamoja nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville,(Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Tanzania ) tunaposikia: Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake? 65-0418E . Kuna vito vingi vya thamani sana katika Ujumbe huu, utakuwa TAJIRI katika Roho wake Mtakatifu tukimaliza.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma Kabla ya Kusikiliza Ujumbe :

Kutoka sura ya 19 Yote
Hesabu 22:31
Mathayo Mtakatifu 28:19
Luka 17:30
Ufunuo sura ya 17 yote

22-1211 Ni Kuchomoza Kwa Jua

Ujume: 65-0418M Ni Kuchomoza Kwa Jua

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 14MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Hekalu la Nguvu za Utendaji ,

Mwanadamu daima ametamani moyoni mwake kuwa kama Ibrahimu alipokuwa ameketi nyumbani kwake karibu saa 11:00. Aliiinua macho na kuwaona wanaume watatu wakija kwake wakiwa na vumbi kwenye mavazi yao. Akawakimbilia upesi, na kusema, “Bwana Wangu.” Aliyesimama pale mbele zake, katika mwili wa mwanadamu akinena, alikuwa ni Melkizedeki Mkuu.

Jumapili hii, shauku hiyo katika mioyo yetu itatimia kwa kila mmoja wetu. Sisi sote tutakusanyika pamoja kutoka ulimwenguni kote, tukimsikiliza Melkizedeki yule yule mkuu akizungumza NASI. Mtu ambaye hakuwa na baba, wala mama, hana mwanzo wa siku zake au mwisho wa uhai, Mungu,  en morphe , akizungumza nasi kupitia midomo ya mwanadamu, kama jinsi Alivyofanya siku hiyo kwa Ibrahimu.

Hakuna njia nyingine ya kusikia Sauti hiyo isipokuwa UBONYEZE PLAY. Hakujawahi kuwa na wakati katika historia ambapo Bibi-arusi ameungana kutoka kote ulimwenguni kuisikia Sauti ya Melkizedeki ikinena kwa wakati huohuo mmoja . Mungu anamuunganisha Bibi-arusi Wake kwa Sauti hiyo.

Tumekuwa, kwa miaka, na Neno la Mungu. Sasa tunaye Mungu wa Neno, mnaona, na papa hapa akiliishi Neno Lake. Kwa hiyo ni kweli, moja ya ishara kuu za mwisho zilizoahidiwa Kanisa kabla ya Kuja kwa Bwana.

Jumapili hii, Bibi-arusi atakuwa na Ujumbe wa Pasaka Desemba hii; na ni Ujumbe ulioje tutakaosikia.

Mitambo. Nguvu za utendaji. Nguvu za kuhuisha. Kristo aliyefufuka. Wana wa Mungu Waliodhihirishwa. Roho yule yule aliyekaa ndani ya Kristo anakaa ndani yetu. Uhai ule ule, nguvu zile zile, baraka zile zile, alizokuwa nazo, tunazo. Hati ya kumiliki. Ile Mbegu ya kwanza iliyopevuka inatikiswa mbele ya watu. Sisi sasa tu nyama ya nyama yake, mfupa wa mfupa Wake; uhai wa uhai wake, Nguvu za Nguvu Zake! Sisi ni Yeye!

Yesu Kristo aliyefufuka; Melkizedeki Mwenyewe, atatoa mlio na kutuambia, “Nilirekodi Sauti yangu na kuiweka kwenye kanda ya sumaku ili niweze kuwavuta ninyi kwangu, nami ningeweza kusema nanyi kama vile nilivyomfanyia Ibrahimu. Ninawataka msikie moja kwa moja kutoka Kwangu .”

Ninyi ndilo Kanisa langu lililochaguliwa na kukusudiwa tangu zamani! Miili yenu ni hekalu la Nguvu za Utendaji , kwa sababu tangu mwanzo mlikuwa sehemu ya ile Mitambo.

Huo ni ule ufunuo wa Kiungu wa Neno lililofanyika mwili. Kama lilikuwa mwili katika siku hiyo kwa njia ya Mwana, Bwana Arusi, ni mwili leo kwa Bibi-arusi. Mnaona?

Hizo Nguvu za Kuhuisha zinaishi ndani yetu. Hatupaswi kuogopa KITU. Roho yule yule aliyekuwa ndani Yake, sasa yu ndani yetu na anaihuisha miili yetu ipatikanayo na mauti. Hatutumaini hivyo, TUNAJUA HIVYO. Tayari tumefaulu, yeye alifaulu kwa ajili yetu.

Kisha, ili kuhitimisha alasiri, Melkizedeki atazungumza kwa mara nyingine tena na kusema;

Watu hawa, ambao ni raia wenzangu wa Ufalme, wenye kumiliki Nguvu za kuhuisha, lihuishe kwao, Bwana, sasa hivi . Naomba Roho aende kutoka tai hadi tai, kutoka kwenye Neno hadi Neno, mpaka utimilifu wa Yesu Kristo udhihirishwe katika kila mmoja wa hiyo miili, kwa ajili ya haja za kimwili, za kiroho, ama haja zo zote walizo nazo, tunapowekeana mikono. Katika Jina la Yesu Kristo.

Kutoka tai hadi tai, Neno hadi Neno, utimilifu wa Yesu Kristo utadhihirishwa katika kila mmoja wa miili yetu. UTUKUFU!!

Hili linaweza tu kutukia kwa KUBONYEZA PLAY, kwa hivyo njoo uungane nasi na ushiriki katika Yubile ya mlo bora wa Chakula kilichohifadhiwa , tunaposikia Sauti Hiyo, Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, ( ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Tanzania ) ikituletea Ujumbe, Ni Kuchomoza Kwa Jua 65-0418M .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma Kabla ya Kusikiliza Ujumbe :

Mambo ya Walawi 23:9-11
Mathayo 27:51 / 28:18
Marko 16:1-2
Luka Mtakatifu 17:30 / 24:49
Yohana Mtakatifu 5:24 / 14:12
Matendo 10:49 / 19:2
Warumi 8:11
1Wathesalonike 4:16
Waebrania 13:8
Ufunuo 1:17-18

22-1204 Huyu Melkizedeki Ni Nani?

UJUMBE: 65-0221E Huyu Melkizedeki Ni Nani?

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Mawazo ya Mungu,

Natumai uko tayari kwa Jumapili hii. Nena kuhusu jinsi mioyo yetu itakavyowaka ndani yetu anaponena nasi njiani katika nyumba zetu na makanisa yetu…SUBIRI TU!

Katika mwezi huu uliopita Ametuambia tuhakikishe tunaingia katika Merikebu sahihi…na tuko. Alituambia ya kwamba Uzao halisi wa Mungu hautarithi pamoja na kapi…ndipo akasema, SISI NDIYO UZAO HUO. Kisha, tukasikia kwa masikio yetu, Mungu akinena kupitia mwanadamu na kututangazia, Leo, Maandiko haya yametimia mbele ya yaya haya macho yetu.

Alituambia Jumapili iliyofuata kwamba tuko katika Mahali palipoandaliwa na Mungu pa Kuabudia, na kwa sababu tuko, HATUJAFANYA uzinzi na Neno Lake. Kwa hiyo, sisi ni Bibi-arusi Neno Bikira Safi wake.

Jumapili hii, Yeye atatuunganisha sisi sote kwa mara nyingine tena na kunena kupitia Malaika-Nabii Wake mkuu na kutuambia, MIMI NDIMI HUYU MELKIZEDEKI, nami ninajidhihirisha kwenu katika mwili wa kibinadamu, kama vile nilivyosema nitafanya katika Neno Langu.

UTUKUFU! Je, umefuraishwa? Je, umebarikiwa Kusikotamkika? Vema, KUNAYO MENGI ZAIDI YAJAYO. Anaenda kukamilisha hadithi hii kuu.

Wazia Hilo, TULIKUWA katika mawazo hasa ya Mungu tangu mwanzo. Miaka elfu nne kabla ya Yesu hajaja duniani, na miaka elfu kadhaa kabla hujaja duniani, Yesu, katika Mawazo ya Mungu, alikufa kwa ajili ya dhambi zetu. NA KISHA , MAJINA YETU yakawekwa kwenye Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo.

Je, hilo linazama niani mwako? Majina yetu yaliteuliwa na Mungu na kuwekwa kwenye Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo kabla kabisa ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Alijua macho yetu, kimo chetu, chochote tulicho. Tulikuwa katika mawazo Yake hapo mwanzo….katika mawazo ya Mungu! Basi, kitu pekee tulicho ni Neno la Mungu lililodhihirishwa. Baada ya Yeye kuliwaza, akalinena, nasi hawa hapa.

Ni vigumu kuelewa. Mungu akituambia mambo haya yote. Alitupenda sana hivi kwamba alitaka kuhakikisha kwamba tutalisikia moja kwa moja kutoka Kwake Mwenyewe , hivyo akafanya irekodiwe ili kwamba Jumapili, Desemba 4, 2022, Angeweza tena kumleta Bibi-arusi Wake pamoja na kutuambia: “Nilifanya haya yote kwa ajili yako wewe. Nilitaka ulisikie moja kwa moja kutoka Kwangu. NAKUPENDA. WEWE NI BIBI-ARUSI WANGU. NAKUJA KUKUCHUKUA HIVI KARIBUNI .”

Ndiyo maana tunajua tunapoingia katika Uwepo wa Mungu, kitu fulani ndani yetu kinatuambia ya kwamba tunatoka mahali fulani, nasi tunarudi tena kwa Nguvu hizo zinazotuvuta.

Mungu ameondoa kinyago kwenye kitu hicho chote na tunaweza kukiona. Mungu, en morphe, aliyetiwa kinyago katika Nguzo ya Moto. Mungu, en morphe, katika Mtu aliyeitwa Yesu. Mungu, en morphe, katika Kanisa Lake. Mungu juu yetu, Mungu pamoja nasi, Mungu ndani yetu; Mungu Anayejidhili.

Hatuna chochote cha kuogopa. Hakuna cha kuhofia, hata kifo. Tunapoondoka hapa, hata hatujafa. Nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii  ikiaribiwa, tuna nyingine TAYARI inayotungoja, En morphe.

Ni Vigumu Kwangu kungojea kumsikia akizungumza nasi na kufunua mambo haya yote Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville. (Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Tanzania) Njoo uungane nasi Katika mahali pekee unapoweza kusikia SAUTI YA MUNGU iliyothibitishwa ikikuambia mdomo kwa sikio Yeye NI NANI , sisi ni NANI na tunaelekea wapi. BONYEZA PLAY.

Huyu Melkizedeki Ni Nani? 65-0221E

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma Kabla ya Kusikiliza Ujumbe :

Mwanzo Sura ya 18 yote
Kutoka 33:12-23
Yohana Mtakatifu 1:1
Warumi 8:1
2 Wakorintho 5:1
2 Wathesalonike 4:13-18
1Timotheo 3:16 / 6:15
Waebrania 7:1-3 /13:8
Ufunuo 10:1-7 / 21:16

22-1127 Ndoa Na Talaka

UJUMBE: 65-0221M Ndoa Na Talaka

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa kundi la Nabii,

Kumbuka, ninasema jambo hili kwa kundi langu tu. Na huko nje hewani, ninasema hili kwa wafuasi wangu mwenyewe. Ujumbe huu ni kwa ajili yao tu, na yale nitakayosema hapa.

Mhudumu ye yote, yeye, hao ni wake, ndiyo, yeye ni mchungaji wa kundi, acha atende cho chote anachotaka. Hilo ni juu yake na Mungu. Kasisi ye yote, mhubiri ye yote, hiyo ni juu yako, ndugu yangu.

Ninazungumza tu hapa Jeffersonville, mahali pekee ambapo ningezungumzia jambo hili , ni kwa sababu ni kundi langu mwenyewe . Ndilo kundi ambalo Roho Mtakatifu amenipa kulifahamu na kuwa msimamizi wake , ataniwajibisha kwa ajili yake . Na watu hawa wangu wamekuwa waongofu hapa kutoka nchini kote, ambao nimewaongoza kwa Kristo .

Ni jiwe la kifuniko kwa wikendi ya Shukrani jinsi gani . Ninashukuru sana kuwa sehemu ya kundi hilo dogo ambalo bado analisimamia pamoja na kila mmoja wenu. Hakuna mahali pengine ambapo tunaweza kwenda.

Baba ametutumia tai mkuu arukaye ili kumwongoza Bibi-arusi Wake. Kuna sauti nyingi zinazowatia moyo watu na kunena Maneno ambayo yaliyonenwa na nabii wake, lakini kuna SAUTI MOJA tu iliyotumwa kumuongoza na kumuunganisha Bibi-arusi Wake.

Maneno ambayo nabii wa Mungu aliyonena kwenye Kanda ni Yakini yetu. Tunaeleweka vibaya kwa sababu tunasema tunaamini KILA NENO, lakini tuliamriwa na nabii wa Mungu kufanya hivyo hasa.

Nasema vivyo hivyo katika Jina la Yesu Kristo. Usiongeze kitu. Usiondoe—kuliwekea mawazo yako. Wewe sema tu yaliyosemwa katika kanda hizo. Tenda sawasawa kabisa na vile Bwana Mungu amekuamuru kutenda. Usiongezee Kwake.!

Amka ulimwengu. Muda umekaribia. Maneno aliyosema nabii wa Mungu, MUNGU AMETUAMURU ; Kuamini, kusema na kutenda, HASA yale aliyosema kwenye kanda. Si kile ninachosema, si kile kuhani ama wahubiri wenu wanayosema, bali yale nabii wa Mungu aliyosema KWENYE KANDA .

Hakuna kitu muhimu zaidi kuliko kusikia Sauti Hiyo kwenye kanda, HAKUNA. Tutaenda kuhukumiwa kwa yale yaliyonenwa KWENYE KANDA . Sio kwa niliyosema, bali yale ALIYOSEMA YEYE .

Nakutakia YALIYO BORA SANA. Maneno yangu machache ni ya kuwatia moyo, kama vile mchungaji yeyote apaswavyo, kuamini kila Neno. Siwafundishi : kutilia shaka jambo lolote mnalosikia kwenye kanda, kuna makosa kwenye kanda, hamna budi kunisikia mimi kadiri mpaswavyo kumsikia nabii. Nawaandikia maneno machache ya kuwatia moyo DUMUNI NA NENO LA ASILI, BONYEZA PLAY. Ninawataka muwe Bibi-arusi Neno safi, asiyeghoshiwa.

Mungu aliruhusu Maneno Yake yarekodiwe katika siku hii ili kila kiumbe hai kiweze kusikia Sauti Yake. Katika siku za Paulo, walikuwa na waandishi wa kuandika yale aliyokuwa akihubiri, ambayo ni Biblia. Lakini LEO, Mungu alitaka iwe KUU zaidi. Tunaweza Kubonyeza Play na kumsikia kwa masikio yetu wenyewe Yesu Kristo aliyefufuka akizungumza nasi, mdomo kwa sikio.

Ni siku ya jinsi gani tunayoishi. Huku ulimwengu wa kawaida ukiporomoka karibu nasi, tuna mahali palipoandaliwa ambapo tunaweza kwenda na kupumzika tu. Tunapapata kwenye KANDA. Tumeziweka katika vyumba vyetu baridi na kufanyia karamu Chakula Kilichohifadhiwa ambacho kimehifadhiwa katika ghala. Nabii wetu anaweza kuwa ameondoka muda mrefu, lakini bado tunangali tunakumbuka mambo haya ni kweli, na tunafanya kama vile Mungu alivyotuamuru kufanya, DUMUNI NA HIZO KANDA.

Njoo uwe na karamu iliyo bora ya Shukrani ambayo hujawahi kamwe kula Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, ( Ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya tanzania) Wakati Sauti ya Mungu inapozungumza nasi Ujumbe: Ndoa Na Talaka 65-0221M .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma Kabla ya Kusikiliza Ujumbe :

Mathayo Mtakatifu 5: 31-32 / 16: 18 / 19: 1-8 / 28:19
Matendo 2:38
Warumi 9:14-23
1Timotheo 2:9-15
1Wakorintho 7:10-15 / 14:34
Waebrania 11:4
Ufunuo 10:7
Mwanzo sura ya 3 yote
Mambo ya Walawi 21:7
Ayubu 14:1-2
Isaya 53 yote
Ezekieli 44:22

22-1120 Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia

Ujume: 65-0220 Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 8 MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bi Yesu Kristo,

Jinsi tunavyopenda kusikia majina yetu yakiitwa. Kufikiri tu, sisi ndio wale Anaowajia. Bibi-arusi wa Kifalme kwa Mwana aliyeahidiwa wa Kifalme. Uzao wake maalumu wa Kifalme wa Ibrahimu ambao umekuwa mkweli na mwaminifu kwa kila Neno.

Hatujafanya uzinzi, wala hata kukonyezana, na neno lingine lo lote; tumejiweka tu wasafi na tumekaa na kila Neno.

Kuna wanawake Wakristo wengi wazuri ulimwenguni leo, wanawake waaminifu; Bali kuna Bi Yesu Kristo mmoja tu. Sisi ndio tunaenda Nyumbani pamoja Naye. Sisi ndio Mke wake Aliyeteuliwa .

Alituambia katika Neno Lake kwamba angekuja mara nyingine tena, kama jinsi tu alivyokuja hapo awali. hapo yeye alisimama, akijifunua katika mwili wa mwanadamu, akisoma Neno na kutuambia, “Leo Maandiko haya yametimia machoni penu,” nasi tukamtambua, na tukawa Bi Yesu Kristo wake.

Imefunuliwa kwetu ya kwamba M-w-a-n-a yule yule wa Mungu aliyetokea mashariki na kujithibitisha Mwenyewe kama Mungu aliyefanyika mwili ndiye M-w-a-n-a yule yule wa Mungu aliyeko katika kizio cha magharibi cha dunia ambaye anajitambulisha Mwenyewe kati ya Bibi-arusi wake. Ile nuru ya jioni ya Mwana imekuja.

Na kama ningeuliza swali kuhusu cho chote, yapaswa kuwe na jibu la kweli. Kwaweza kuwe na lililo la karibu nalo; lakini yapaswa kuwe na jibu la kweli, la moja kwa moja kwa kila swali. Kwa hiyo, basi, kila swali linalozuka maishani mwetu, yabidi kuwe na jibu la kweli na sahihi.

Katika wakati wetu kuna maswali mengi na mabishano miongoni mwa watu.

. Je, ni muhimu jinsi gani kusikiliza kanda za nabii wa Mungu?

. Je, ni muhimu jinsi gani kusikia na kuamini kila Neno?

. Yakini yetu ni nini? Je! Ni yale aliyosema kwenye kanda, ama Roho Mtakatifu humwongoza kila mtu kuamua lipi ni Neno na lipi si Neno.

. Je, ni lazima tuwe na mtu, au kundi la watu, kutuvunjia-vunjia ?

. Je! Neno linasema baada ya Yeye kumtuma Eliya nabii, Yeye atatuma kundi la watu ambalo halina budi kuwafafanulia Hilo?

. Je, tunahitaji mtu fulani wa kutufasiria Neno au kulivunja-vunja ?

. Je, tunapaswa kuzisikiliza tu kanda katika nyumba zetu, magari, na vituo vya mafuta, na kisha kumsikia mhudumu tunapoenda kanisani?

. Je, tucheze kanda katika makanisa yetu?

. Je, ni Sauti ya Mungu kwa ajili ya wakati wetu au la?

Sasa, kama ni swali la Biblia, basi lapaswa liwe na jibu la Biblia. Halingepaswa kuweza kuja kutoka kundi la watu, kutoka kwenye ushirika wo wote ule, au kutoka kwa mwalimu fulani, au kutoka kwa madhehebu fulani. Lapaswa litoke moja kwa moja katika Maandiko…

Kwa hiyo, ikiwa tunataka kupata jibu sahihi kwa maswali yetu, ni lazima twende kwenye Maandiko. Kisha, ni lazima tuamue, ni nani aliye mfasiri wa Kiungu wa Maandiko. Je, kila mtu anajiamulia kivyake?

Nabii haimaanishi kunena Neno tu, bali pia ni kutabiri, na ni mfasiri wa Kiungu wa Neno, Neno la Kiungu lililoandikwa.

Kwa hiyo kama nabii ndiye mfasiri wa Kiungu wa Maandiko, basi kile nabii huyo alichosema ni Neno la Mungu kwa Bibi-arusi Wake ambalo limekwisha kufasiriwa, NI HAYO TU.

Hilo haliondoi wahudumu, au nafasi ambayo Mungu amewaitia. Wameitwa na Mungu kudumisha Neno hilo lililonenwa na nabii wa Mungu mbele ya kundi lao. Wawaelekeze watu wao kwa huyo mjumbe na Ujumbe wa Saa hii.

Kila neno wanalohubiri lazima lipimwe kwa Maneno ambayo nabii wa Mungu aliyosema kwenye kanda. Hawapaswi kubadilisha, wala hata kuweza kufasiri hata NENO MOJA. Maandiko ya Mungu yanafasiriwa TU na nabii Wake.

Sasa, kila moja yao, bila shaka, ungeweza kuona wazo lao, nami siwezi kuyalaumu. Kila moja hudai kwamba wao ndio ile kweli, wana ile kweli. Na watu ambao ni washiriki wa makanisa hayo wanapaswa kuiamini hiyo, kwa sababu wamesalimisha kikomo cha—chao, kikomo chao cha Milele, juu ya mafundisho ya kanisa lile. Nayo yanatofautiana sana, moja kwa lingine, mpaka inazusha maswali mbalimbali mia tisa na kitu.

Ikiwa Ujumbe huu ulionenwa na nabii wa Mungu si Yakini yako, bali ni kile ambacho mtu ama watu fulani wasemayo ndio Neno, Basi kikomo chako cha Milele kinategemea yale WANAYOSEMA.

Maneno yangu yanaonekana kupingana kabisa na ye yote na wahudumu wote. Siwapingi. Ninaamini Mungu ameweka watu halisi katika Kanisa Lake na kuyaangalia makundi Yake kuweka Ujumbe huu mbele yao. Ninaamini wanahubiri na kuamini Ujumbe huu. Lakini kwa nini hawataki kumweka Ndugu Branham nyuma ya mimbara zao Kama Sauti iliyo muhimu sana yakusikia? Kwa nini wanaweka huduma yao kuwa sawa na, pia muhimu kama ile Sauti?

Malaki 3 ilisema, “Namtuma mjumbe Wangu mbele ya uso Wangu kuitengeneza njia.” Na yule ambaye alipelekwa kuitengeneza ile njia, alimtambua Yeye pale. “Huyo Ndiye! Hakuna kosa. Huyo Ndiye! Ninaona ishara ikimfuata Yeye. Najua kwamba huyo Ndiye; Nuru ikishuka kutoka Mbinguni na kukaa juu Yake.” Ilikuwa dhahiri, huyo alikuwa Ndiye.

Basi, ndugu yangu, nataka kukuuliza wewe jambo fulani, katika kufunga. Tungeweza kusema hivi. Hivi katika Malaki 4, hatukuahidiwa tai mwingine, Nguzo ya Nuru itafuata , kuonyesha kanisa lililokosea siku hii kwamba Yeye ni Waebrania 13:8, “yeye yule jana, leo, na hata milele”? Hivi hatukuahidiwa mwingine atakayeruka aje kutoka nyikani?

Je, tunapaswa kufuata nini? Nguzo hiyo ya Nuru. Hiyo Nguzo ya Nuru ni nani? Yule tai, Malaki 4. Ni nani aliyekuwa na Nguzo ya Moto juu ya kichwa chake kumthibitisha yeye alikuwa nani? William Marrion Branham.

Kila wakati tunapokusanyika, hatuna budi kuiweka Sauti hiyo mbele ya watu. Ni lazima tuipe Sauti ya Mungu NAFASI YA KWANZA. Si kumwabudu mtu huyo, bali kumwabudu yule Mungu Aliye Katika mtu huyo.

Huyo ndiye mtu ambaye Mungu amechagua kumwongoza Bibi-arusi Wake. Mtu huyo ndiye mtu ambaye Mungu amechagua kufasiri Neno Lake. Mtu huyo ndiye mtu ambaye Mungu amechagua kufunua kwake siri zake zote. Mtu huyo ndiye ambaye Mungu alisema, “Wafanye watu WAKUAMINI ”, SI MTU MWINGINE YE YOTE AU ASEMAYO MTU AWAYE YOTE YULE, WEWE, WILLIAM MARRION BRANHAM . Mtu huyo ndiye atakayetutambulisha kwa Yesu Kristo.

Mwanamume au mwanamke anayeongeza lo lote kwa yale ninayosema, haamini yale nisemayo.

Njoo na uwe Bi Yesu Kristo pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, ( Ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Tanzania) tunaposikia kinywa cha Mungu kilichochaguliwa kikinena na kutuambia:  Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia 65-0220 .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe :

Kumbukumbu la Torati 16:1-3
Kutoka 12:3-6
Malaki Sura ya 3 & 4
Luka 17:30
Warumi 8:1
Ufunuo 4:7

22-1113 Leo Maandiko Haya Yametimia

UJUMBE: 65-0219 Leo Maandiko Haya Yametimia

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Uzao wa Kifalme wa kiroho wa Ibrahimu,

Ni kanisa gani unaloweza kwenda na kujua, bila shaka yo yote, ya kwamba kila Neno unalosikia ni Bwana Asema Hivi? Hakuna mahali popote, isipokuwa tu usikilize Sauti ya Mungu ikisema nawe kwenye kanda.

Sisi ni tai wa Mungu na hatutapatana hata kwa Neno moja. Tunataka tu Mana mpya kila ibada na Haiji tena mpya kuliko kuisikia moja kwa moja kutoka kwa Mungu Mwenyewe. Tunaruka juu zaidi na zaidi tunaposikia kila Ujumbe. Kadiri tunavyoenda juu zaidi , ndivyo tunavyoweza kuona zaidi . Kama hakuna Mana katika kanisa hili, tai wa Mungu wanapaa juu kidogo mpaka waipate.

Jinsi gani mioyo yetu inavyoruka kwa furaha tunapomsikia Mungu akizungumza nasi na kutuambia ya kwamba sisi ndio Kanisa Lake halisi, Kanisa la Mungu, lililozaliwa mara ya pili, ambalo linaloamini kila Neno la Mungu mbele ya kitu chochote kile, bila kujali ni kitu gani, kwa sababu sisi ni Bibi-arusi-Neno Bikira Wake Asiyeghoshiwa.

Kuna msukosuko mwingi miongoni mwa watu leo. Kama ilivyokuwa katika siku za Yesu, wale waliojiita waamini walikuwa wakichukua mafafanuzi ya yale makuhani walikuwa Wamesema kuhusu Maandiko. Walikuwa wakiamini mafafanuzi ya Neno ya Watu. Hiyo ndiyo ilisababisha wakose kuiona ile Kweli ya Mungu, kwa sababu kulikuwa na mafafanuzi mengi sana yaliyotengenezwa na Wanadamu ya Neno la Mungu. Mungu hahitaji mtu yeyote afafanue Neno Lake. Yeye ni Mfafanuzi Wake Mwenyewe.

Je, unaamini kama ungeishi wakati wa Yesu, ungeamini kila Neno alilosema, bila kujali kuhani wako alisema nini? Je, ungemwambia kuhani wako kwamba kumsikiliza Yesu ndilo jambo muhimu zaidi unaloweza kufanya? Je, ungemwambia Maneno ya Yesu hayahitaji kufasiriwa? Kama wangekuwa na kanda za Mahubiri ya Yesu, je! ungalimwambia kuhani wako unataka abonyeze play ili uweze kusikia yale hasa Yesu aliyosema na jinsi alivyoyasema?

Vema, hilo halikuwa kwa ajili ya wakati wako; huu ni wakati wako, huu ndio wakati wako. Biblia yasema, ni Yeye yule jana, leo, na hata milele. Kile Unachofanya na kusema hivi sasa ndivyo hasa ungefanya wakati huo.

Tunaamini kwamba M-w-a-n-a wa Mungu yule yule aliyetokea mashariki na kujithibitisha Mwenyewe kama Mungu aliyefanyika mwili, ndiye M-w-a-n-a yule yule wa Mungu Aliyeko katika kizio cha magharibi cha dunia ambaye anajitambulisha Mwenyewe miongoni mwetu. Tunaamini Leo Maandiko haya yametimia mbele yetu.

Hakika ninaamini huu ndio mwaka uliokubaliwa, mwaka wa yubile. (ama mwaka wa Sikukuu). Ikiwa Unatamani kubaki mtumwa na kutoamini Ujumbe huu kuwa ni Bwana Asema Hivi ; Ikiwa Ujumbe huu sio Yakini yako; ikiwa unaamini inahitaji mtu kuufafanua Ujumbe huu; Ikiwa unaamini ni makosa kuzicheza kanda kanisani mwako; Basi itakubidi upelekwe na shimo litatobolewa masikioni mwako kwa msharasi, Na ndipo itakupasa kumtumikia huyo mwenye watumwa siku zako zote.

Lakini Kanisa la kweli la Bibi-arusi linaamini Neno lote la Mungu katika utimilifu Wake na katika nguvu Zake. Sisi ndio lile Kanisa Teule ambalo linajiondoa na kuwekwa kando kutoka kwenye mambo hayo, nalo dhihirisho la Mungu limeuvutia usikivu wetu. Sisi ndio ule Uzao wa Kifalme wa kiroho wa Ibrahimu.

Kwa hivyo tuna shukrani kwenu kuwa hapa mkafurahie ushirika huu pamoja nasi, ambao tunatarajia Mungu atatupa katika mkutano huu.

Kwa hivyo tunakualika uungane nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, ( Ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya tanzania) tunaposikia 65-0219 Leo Maandiko Haya Yametimia . Tunatarajia Kile Mungu anachofanya wakati wa mikutano hii. Ile Nuru ya jioni ya Mwana imekuja.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma :

Yohana Mtakatifu Sura ya 16 yote
Isaya 61:1-2
Luka Mtakatifu 4:16