All posts by admin5

22-0529 Imani Kamilifu

UJUMBE: 63-0825E Imani Kamilifu

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi mwenye Imani Kamilifu,

Kwa mara nyingine tena, naona haiwezekani kuweka kwa maneno kile ambacho Ujumbe huu, barua za Upendo wa Mungu wa kibinafsi, zilizoandikwa kwa Damu Yake, zilizonenwa kwa Sauti Yake, zinamaanisha kwetu. Kila kitu kingine hakimaanishi chochote. Tunampenda kutoka ndani kabisa ya mioyo yetu na Ametupa Upendo Mkamilifu Kwa ajili yake . Hakuna kinachoweza kutuondoa kwenye Neno hilo. Hakuna uradhi mwingine katika maisha yetu zaidi ya kumsikia yeye akiwasiliana nasi kama Rafiki kwa rafiki.

Hata sio sisi, ni Yeye anayeishi ndani yetu, akijiita Mwenyewe. Ni kilindi kikiita kilindi. Furaha kamili ya Kubonyeza play na kumsikia Mungu akitumia sauti ya mwanadamu kutuambia, sisi ni wateule wake. Kutuambia alitupenda kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu; kwa maana alijua tungempenda kwa yote yaliyokuwa ndani yetu, na tungedumu kuwa waaminifu Kwake na Neno Lake.

Yote tunayohitaji, Ametupa. Hakuna kinachokosekana. Neno Lake aliliandika kwa namna ya barua na kulihifadhi kwa maelfu ya miaka ili aweze kutuambia Upendo wote uliokuwa moyoni Mwake kwa ajili yetu.

Ndipo upendo wake unakuwa mkuu zaidi kwetu alivyotuambia: “Nitakuja katika mwili mara nyingine tena na kunena nanyi mdomo kwa sikio ili kusiwe na kutokuelewa, kusiwe na Mkanganyiko , kusiwe na haja ya fasiri. Nitachukua muda Wangu na kuwaeleza Upendo Wangu kwenu , nanyi mtaweza kuusikia tena na tena na tena. Nataka mjue, Baba yu ndani Yangu, Mimi niko ndani yenu, ninyi mko ndani Yangu, sisi ni MMOJA. Mwili wenu ni Mwili wangu, mfupa wenu ni Mfupa wangu, roho yenu ni Roho yangu.

Nitawaambieni yote yaliyo ndani ya Moyo Wangu kwa undani sana. Nitaliweka wazi hivi kwamba mtajua bila shaka, Maneno niliyoandika na kunena ni kwa ajili yenu, na hayatashindwa kamwe.

Nitawapa Imani Kamilifu, na Itakuwa ni Mtawala wa kila hali. Haidhuru adui anasema nini, italitawala mkiwa na Imani Kamilifu katika kile Neno Langu linasema mlicho. Haidhuru adui anajaribu kuwaambia nini, hata Msimsikilize. Masikio yenu ni bubu kwa kitu kingine chochote isipokuwa kile ambacho Roho Wangu amekwisha waambieni. Kimetia nanga mioyoni mwenu, na hakuna kitu kitakachowafanya mtoke Kwake.”

Imani hiyo Kamilifu tuliyo nayo katika kuujua Ujumbe huu kuwa ni Bwana Asema hivi, tunaitumia IMANI hiyohiyo KAMILIFU kwa kila ahadi aliyotuambia ni yetu katika Neno Lake. Ikiwa sisi ni wagonjwa na tunahitaji uponyaji, ni wetu. Ikiwa tunahitaji chochote, tunaweza kukipata, kwa kuwa tumetiwa mafuta na Roho Wake. Sisi ni masihi Wake watiwa mafuta wa siku za mwisho, tukionyesha ufufuo wa Yesu Kristo.

Ni tendo la Mapenzi anapojimwaga Yeye mwenyewe ndani yetu. Tunakuwa mmoja Naye kwa ajili ya Karamu hiyo kuu ya Arusi. Roho wake yuko hapa pamoja nasi na ndani yetu. Tuna jambo moja tu la kufanya, nalo ni kuliamini, kulikubali.

Sisi sio Malaika-Mjumbe wa 7 wa Mungu, lakini sisi ni wana na binti zake. Mikono yetu ni Mikono yake. Tunaamini kile kinachonenwa kwenye kanda kuwa ni Bwana Asema hivi. Ni Neno lililo hai.

Nabii wake ndiye mchungaji wetu. Tunaposikiliza Neno lililorekodiwa, tunaamini ni Mungu anayezungumza nasi moja kwa moja. Tuna Imani Kamilifu tukiamini hivyo.

Tunapokusanyika pamoja ulimwenguni kote kumsikiliza Mungu akizungumza nasi kwa njia ya nabii Wake, imani yetu inainuliwa juu zaidi na zaidi Mungu anapomkusanya Bibi-arusi Wake pamoja kwenye Neno Lake lililothibitishwa.

Kesho haitakuwa kama siku nyingine. Tutachukua Imani yetu Kamilifu Aliyotupa na tutaitumia kwa chochote tunachohitaji, nasi tutakipokea wakati Nguzo ya Moto inaponena kupitia mjumbe Wake mteule na kutuambia:

Je, mumeelewa na hayo niliyowatendea? Ninyi mumeniita “mchungaji wenu”; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo. Ikiwa mimi, niliye mchungaji wenu, nimekwisha tambulishwa na Yesu Kristo, ya kwamba mimi ninatenda kazi Yake, basi aminini Neno langu. Kwa kutenda hili tendo la imani, kwa kuweka mikono yangu juu yenu , nimekwisha kuhukumu magonjwa na mateso yanayowasumbua. Aminini hayo, ndipo mtatimiziwa haja zenu, hata ziwe ni nini, kwa maana mambo yote yanawezekana kwa hao waaminio . Na mnapoomba, aminini ya kwamba mmepokea mlichoomba . Nami naamini kabisa ya kwamba napokea, na moyoni mwangu napokea uponyaji wa kila mmoja wenu, naupokea, ya kwamba umetendeka. Naamini, naamini hayo kwa yote yaliyo ndani yangu .

Tunaamini kwa yote yaliyo ndani yetu, Ujumbe huu kuwa ni Sauti ya Mungu, iliyonenwa, iliyorekodiwa, iliyothibitishwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya siku hii. Tunaamini lo lote tuombalo, tutapokea, kwa kuwa ni BWANA ASEMA HIVI NI LETU.

Njoo uungane nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania),ili kupokea chochote unachohitaji tunapomsikiliza nabii wa Mungu akituambia jinsi ya kupokea: Imani Kamilifu 63-0825E .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma Kabla Ya Ibada :

Marko Mtakatifu 11:22-26 / 16:15-18
Yohana Mtakatifu 14:12 / 15:7
Waebrania 11:1 / 4:14
Yakobo 5:14
1 Yohana 3:21

22-0522 Ninawezaje Kushinda?

UJUMBE: 63-0825M Ninawezaje Kushinda?

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Waliyoungana,

Wakati na Umilele vitaungana pamoja wakati Mungu na watu Wake watakapoungana pamoja .

Ninakualika uje uungane pamoja na Bibi-arusi wa Mungu na kusikia Ujumbe 63-0825M Ninawezaje Kushinda? Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville.( Ni saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania).

Ndugu Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Ufunuo 3:21-22

22-0515 Wakati Wa Kuungana Na Ishara Yake

UJUMBE: 63-0818 Wakati Wa Kuungana Na Ishara Yake

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Mwili wa Mwili Wake, Neno la Neno Lake, Uhai wa Uhai Wake, Roho wa Roho Wake,

Mpendwa Bibi-arusi Mtangulizi ,

Tulipoketi pamoja katika ulimwengu wa roho kutoka duniani kote Jumapili iliyopita , tulikuwa tukisikiliza Sauti pekee ya Mungu iliyothibitishwa ikizungumza nasi. Kama kawaida, tulikuwa chini ya matarajio makubwa kusikia kile alichokuwa anaenda kutuambia. Roho Mtakatifu anaenda kutufunulia nini leo?

Huenda tumesikia maneno yake mara nyingi hapo kabla, lakini tulijua siku hiyo ingekuwa tofauti. Tungesikia jambo fulani ambalo hatukuwahi kusikia hapo kabla. Tungepokea Ufunuo zaidi hata ya tunavyoweza kufikiria. Angefungua mioyo yetu, akili zetu na nafsi zetu, na kufunua jambo ambalo lilikuwa SASA HIVI, katika Majira yake Halisi, kufunuliwa.

Kisha linatokea. Maneno makuu sana bwana arusi awezayo kusema na kufunua kwa Bibi-arusi wake, “Wewe ni utimilifu kamili wa Uungu kwa jinsi ya mwili, mtangulizi. Yote niliyokuwa, niliyamimina katika Kristo; yote Kristo aliyokuwa, niliyamimina ndani YAKO . WEWE NI Bibi-arusi-Neno wangu Mkamilifu niliyemchagua . “

Utu wetu wote uliruka kwa furaha. Baba ndo kwanza atuambie, sisi ni Bibi-arusi wake. Sisi ndio wale awapendao. Sisi tumetiwa mimba na Neno lake, na Neno lake PEKE YAKE . Tumbo letu limefungwa kwa kitu kingine chochote. Yeye amekuwa akitungojea sisi, na kutamani kutupata Sisi … SISI !!

Na wajua nini ? Yeye kamwe hakumtuma mtu mwingine kutuambia Maneno haya, Yeye amekuja na kuishi katika mwili wa kibinadamu kwa mara nyingine tena, ili apate kuzungumza moja kwa moja, mdomo kwa sikio, na KUTUAMBIA : “Nakupenda, Bibi-arusi wangu kipenzi .”

Tunapenda kuimba, tunapenda ushirika, tunapenda kukusanyika pamoja na waaminio, Lakini tunachopenda zaidi ya yote ni kusikia Sauti ya Mungu; Hivi asema Bwana, ikinena Nasi moja kwa moja . Kila ujumbe ni Kitu kikuu cha binafsi KWETU . Yeye aliweka kila neno Alilotaka kutuambia kwenye kanda ya sumaku hivi kwamba tuyasikie sisi wenyewe.

Ni kitu gani Yeye atatuambia na kutufunulia Jumapili hii tutakapokusanyika? ni majira gani?

Isaya alinena na kusema, “Bikira atachukua mimba na kuzaa mtoto”, lakini ilikuwa ni miaka 700 kabla ya majira yake ya kutimia. Mfalme Daudi alisema, “Walizua mikono yangu na miguu yangu.” Alizungumza kana kwamba ilikuwa mikono yake na miguu yake, lakini Hayakuwa majira yake yakutimia bado miaka 1,000.

Mungu alinena kupitia nabii wetu katika wakati wetu na kusema mambo mengi yasingewezekana kutimia mpaka leo hii. Tunaona mataifa na ulimwengu wakiungana zaidi ya wakati mwingine wowote. Tulidhani Ukomunisti ulikuwa kitu cha zamani na ulikuwa umesambaratishwa, lakini sasa tunaona ni hai sana na ni chombo mikononi mwa Mungu, kama vile alivyotabiri na kutuambia ulikuwa hivyo.

Ulimwengu ulidhani vita baridi vilikwisha, na hakuna tena tishio la vita ya nyuklia. Lakini leo, tishio la vita ya nyuklia limekuwa ni Halisi. Kila kitu kimewekwa mahali pake kama tu vile alivyotuambia kwamba itakuwa. Haya ndio majira yenyewe .

Jumapili Hii, Yeye kwa mara nyingine tena ATANENA NASI MOJA KWA MOJA , mdomo kwa sikio, nasi tutasikia Jambo kuu lingine ambalo lilinenwa na kuhifadhiwa kwa ajili yetu tu tusikie. Ni kitu gani yeye Atasema na kutufunulia? ni majira gani? Ni Kitu gani kinachotendeka ?

Mungu anamuunganisha Bibi-arusi Wake. Anakusanyika pamoja, kutoka Mashariki na Magharibi, na Kaskazini na Kusini. Kuna wakati wa kuungana, na huo unaendelea sasa hivi. Anaungana kwa sababu gani? Unyakuo.

Basi Ujumbe huu unatenda nini wakati tunaposikiliza Sauti ya Mungu kutoka kote ulimwenguni ? Kumuunganisha Bibi-arusi na Neno. Neno ni Mungu. Bwana arusi ni Neno. Bibi-arusi ni msikiaji wa hilo Neno, nasi Tunakuja pamoja katika muungano. Tunajiandaa kufanya arusi ambapo tunakuwa mmoja na Neno.

Yote aliyo Baba, ndivyo nilivyo Mimi; na yote niliyo Mimi, ndivyo mlivyo ninyi; na yote mliyo ninyi, ndivyo nilivyo Mimi. Katika siku hiyo mtajua ya kwamba Mimi niko ndani ya Baba Yangu, Baba ndani Yangu, Mimi ndani yenu, nanyi ndani Yangu.” Unaona? Katika “siku hiyo.” Siku gani ? Leo hii ! Tunaona zile siri kuu zilizofichwa za Mungu zikifunuliwa. Loo, jinsi ninavyopenda jambo hilo!

Huu ndio wakati wenyewe Hasa . Haya ndio majira yake hivi sasa . Bibi-arusi yuko tayari kwa ajili ya Bwana arusi. Tunasikiliza Tunaposikia kile kilio cha Usiku wa manane “Tazama, Bwana Arusi yuaja!” Tuko kabisa kwenye wakati wa mwisho.

Njoo uungane nasi Tunapoungana kwenye Neno, Jumapili Saa 6:00 SITA MCHANA ya Jeffersonville , ( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Tanzania) Tunaposikia sauti ya Mungu ikituambia ni : Wakati Wa Kuungana na Ishara Yake 63-0818 .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma Kabla ya ibada :

Zaburi 86: 1-11

Mathayo Mtakatifu 16: 1-3

22-0508 Kristo Ni Siri ya Mungu iliyofunuliwa

UJUMBE: 63-0728 Kristo Ni Siri Ya Mungu Iliyofunuliwa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Wapenzi wa Moyo Wake,

Ninayo heshima kubwa zaidi duniani. Bwana ameniruhusu nimtambulishe yeye mwenyewe kwenu, ili aweze kusema nanyi moja kwa moja kupitia chombo alichochagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu ili kunena na kuwafunulia Neno lake lote.

Si mtu wa Mungu tu, Ni Mungu Mwenyewe, Nguzo ya Moto, Roho Mtakatifu akizungumza nawe moja kwa moja, mdomo kwa sikio, nasi tunayo heshima na majaliwa kumwita nabii Wake mteule, MCHUNGAJI WETU.

Kamwe hatujiulizi kama kile tunachosikiliza ni mwanadamu, fikira zake, wazo lake, au fasiri yake ya Neno. Ni Mungu Mwenyewe Akinena nasi BWANA ASEMA HIVI.

Ninajua watu wanakariri tu jambo hilo, lakini sisi tunakunywa ndani . Kwa maana ndicho kitu pekee ambacho hukata kiu yetu na kutosheleza nafsi zetu. Ni Maneno ya Uzima wa Milele. Kwetu sisi, Ni Sauti ya Mungu. Ni Ujumbe wa wakati huu. Kwa hiyo, ni Neno, Sauti, Kanda, SIO KINGINECHO!

Tumeungana pamoja chini ya Kiongozi mmoja kama Israeli wa kale. Mungu Mmoja, aliyethibitishwa kwa Nguzo ya Moto, na kujifunua Mwenyewe kupitia nabii Wake kuwa Neno. Mungu yeye yule, Nguzo ile ile ya Moto, vivyo hivyo leo. Mungu hawezi kamwe kubadilisha asili yake. Mpango Wake hauwezi kamwe kubadilika kutoka kwa kile Alichoanza nacho, kwa sababu Yeye hana kikomo na mpango Wake na mawazo Yake yote ni kamilifu.

Ndiyo maana tuna matazamio makubwa kusikia kile ambacho anaenda kutufunulia siku ya Jumapili. Alisema ya kwamba Yeye amepiga pande zote za ncha zake, ndani na nje yake, na hata alionyesha kwa Maandiko na mpangilio wake wa matukio, mpaka tunajua ya kwamba Ujumbe huu ni Kweli kabisa. Hakuna makosa .

Lakini Jumapili, Roho Mtakatifu ataushika Ujumbe na kuuweka mahali ulipo sasa. Yeye ataujenga tangu pale ulipoanzia, na kuujenga moja kwa moja hadi wakati huu wa sasa.
Hebu tunywe machache tu ya yale Mungu atakayotuambia na kutufunulia kupitia mchungaji wetu siku ya Jumapili:

Ninyi ni mboni ya moyo wangu, wale ambao mmezaliwa kwa Bwana kwa Roho na kwa Neno la Kweli. Ninaomba tu na kumwomba Bwana awabariki na kuwaweka nyinyi kuunganishwa pamoja kwa vifungo vya upendo wa Kristo.

Bwana aliniweka Ni hifadhi Chakula ghalani kwa ajili yenu; mboga zenye afya nzuri, hapa katika maskani hii. Na leo hii, utapokea mzigo mzima wa Kanda . Itakufunulia Yesu Kristo katika saa tunayoishi. Ujumbe huu utawahifadhi na kuwatia nguvu. Utawapa nguvu za kiroho kwa kazi iliyo mbele yenu.

Hebu niwaambieni tena ninajua mnapenda kulisikia jambo hili: Ninyi ndiyo nambari iliyoteuliwa na iliyochaguliwa tangu zamani, ndio watu pekee watakaolisikiliza. Ninyi ndiye Bibi-arusi mteule ambaye hataanguka bali atashikilia Neno hilo bila kujali wengine wote ulimwenguni kote wanasema nini kuhusu hilo. Wewe ni Bibi-arusi Neno!

Mungu amekufunulia siri hii kuu, na huko ndiko Kuzaliwa upya. Sasa anakuleta pamoja ambapo ufunuo ulipo katika upatano mkamilifu. Mungu akilidhihirisha kupitia Neno Lake kwa matendo yale yale, mambo yale yale aliyofanya, akilidhihirisha Neno ndani yako.

Usisahau kamwe, Roho Mtakatifu, peke yake, ndiye Mfunuzi wa ufunuo wa Kiungu wa Kristo, na amekuwako katika nyakati zote. Kumbuka, Nyakati zote ! Neno la Bwana lilikuja kwa nani? Nabii, peke yake.

Ninatambua kuwa ninazungumza na maelfu kwenye kanda, tuna huduma ya kanda kote ulimwenguni. Na inaonekana kuwa tunaweza kutengeneza kanda kutoka hapa ambayo ni bora mara kumi kuliko mahali popote pengine . Ninatumai tu kila mwanamume anayesikia kanda hii, na kila mwanamke, ataelewa.

Sasa ni juu yao ikiwa wanataka kusikiliza kanda yoyote , lakini sitaki mlikose hili. Enyi watu wa kanda; huko msituni na popote mnapoisikia, sasa sikilizeni.

Tunazo kanda  kuhusu kile tunachoamini. Tunazo kanda zinazohusu nidhamu kanisani, jinsi tunavyoenenda sisi wenyewe katika kanisa la Mungu, jinsi tunavyopaswa kuja hapa pamoja na kuketi pamoja katika ulimwengu wa roho.

Natumai kila mtu kwenye kanda analipata jambo hilo. Ukishindwa, rudi kwenye kanda  hii tena . Sijui nitakuwa nanyi kwa muda gani zaidi. Kumbukeni, Hii ​​ndiyo Kweli, ya BWANA ASEMA HIVI. Ni kweli. Ni Maandiko .

Uongozi na Mwili umekuwa kitu kimoja. Ni Mungu akidhihirishwa ndani yenu , watu Wake. Hiyo ndiyo sababu mume na mke si wawili tena; wao ni mmoja. Mungu na Kanisa Lake ni mmoja, “Kristo ndani yenu,” ufunuo mkuu wa Mungu.

Sio wazo langu; ni Nguvu Zake, ni Neno Lake. Aliliahidi ; ndilo hili hapa. Alisema lingekuwa hapa, ndilo hili hapa. Ninyi ni wana wa Mungu. Si kwamba mtakuwa ; MKO SASA HIVI!

Jaza kikombe chetu Bwana, tunakiinua juu, Bwana, njoo ukate kiu ya roho zetu. Mkate wa Mbinguni, utulishe, hadi tusihitaji zaidi. Jaza kikombe chetu, kijaze mpaka pomoni na utufanye tuwe wazima.

Ni wakati wa jinsi gani wa uamsho tutakaokuwa nao ulimwenguni kote tutakapokusanyika Jumapili ili kusikia: Kristo Ni Siri ya Mungu iliyofunuliwa 63-0728 saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville.( ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Tanzania ).

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma kwa maandalizi ya kusikiliza Ujumbe :

Mathayo Mtakatifu 16:15-17

Luka Mtakatifu Sura ya 24 yote

Yohana Mtakatifu 5:24 / 14:12

1 Wakorintho Sura ya 2 yote

Waefeso Sura ya 1 yote

Wakolosai Sura ya 1 yote

Ufunuo 7:9-10

22-0501 Mungu Hamwiti Mtu Hukumuni Bila Ya Kumwonya Kwanza

UJUMBE: 63-0724 Mungu Hamwiti Mtu Hukumuni Bila Ya Kumwonya Kwanza

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa kamani ndogo , springi kuu, ama chochote ulicho :

Sote ni Mwili wa Kristo, katika mahali petu, katika upatano, tukijaribu kufanya kazi vizuri sana tuwezavyo kwa ajili Yake. Hakuna kitu kingine muhimu kwetu, ila Neno Lake, Ujumbe huu.

Tunapenda tu kusikia nabii wa Mungu akituambia : “Kuna jambo fulani juu yenu watu fulani. Ninyi ni watu maalum katika maisha yangu. Kuna kitu kingine ambacho napenda tu kukutana nanyi na kuzungumza tu nanyi ”.

“Naangalia huku kwenye huduma yangu ndogo nyenyekevu; Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele, nami naona kile inachofanya; inaita na kuunganisha kundi la Bibi-arusi pamoja. Nikutoa Gurudumu kutoka kwenye gurudumu.”

Tunajua si mwanadamu, ni Neno la Mungu linalomkusanya Bibi-arusi Wake pamoja. Mambo ambayo tunaona yakitekelezwa si kitu mbali na Mungu. Hakuna tena huenda ikawa ndivyo, ingewezekana , inaonekana kana kwamba huenda ikawa, NI MUNGU!!

Tumefika mahali hapo kwamba Ndio Lulu ya thamani kubwa kwetu. Tumeachana na chochote mtu yeyote anachotuambia kinyume Chake. Hatuangalii kile mwanadamu ametimiza. Tunaangalia kile Mungu amesema na kile Yeye ameahidi angefanya katika Siku yetu, nasi tunamwona Yeye akikifanya.

Huo ndio Mkataa wetu. Kila kitu tulicho sisi, kila kitu tulichokuwa, kila kitu tunachotumaini kuwa, kimewekwa juu ya Ujumbe huu. Ni zaidi ya uhai kwetu.

Ni kama Haijawahi hapo kabla katika historia ya ulimwengu, tunamwona Mungu akitoa onyo, Jiandaeni kwa ajili ya hukumu. Bomu za atomiki ziko kwenye mabanda yake, kila kitu kiko tayari.

Wakati huu, si kwa kikundi kidogo tu cha watu, kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu, au katika siku za Ibrahimu; ni Mungu akiwaonya watu wa ulimwengu mzima, akinena kupitia nabii Wake, hili ndilo onyo lenu la mwisho.

Yeye Anatuambia, “Kabla sijaruhusu jambo hili litukie, ninatoa wito wa mwisho, kama tu nilivyofanya Sodoma, Tokeni kwake. Iweni tayari. Jambo fulani litatukia ”.

Ulimwengu unategemea ufanisi wao mkuu wa sayansi; uzalishaji wa kisayansi umeleta mauti kwa vizazi. Walio werevu na wenye elimu wanaingia upande wa kiakili : UMOJA WA MATAIFA , NATO, Shirikisho la Mataifa. Kila siku tunaona hukumu ikikaribia zaidi na zaidi. Kile nabii alichoona tokea mbali na kutuambia kingekuja kutokea, kinatendeka: Urusi, Vita, Mafuta, Vatikani, Wayahudi, Mabomu ya Nyuklia.

Hakuna tena kujiuliza nini kitatokea. Tunaliona likitendeka kila siku, na hofu duniani ni Hakika na inazidi kuwa kubwa zaidi na zaidi kila siku.

Lakini ni kama tu alivyofanya katika siku za Hezekia, wakati Mungu aliponena kupitia nabii wake na kuwaonya watu, “ Tengenezeni Mambo , kwa kuwa hukumu iko tayari kuanguka”. Nabii wake alikuwa akiwatayarisha watu kwa ajili ya wakati ule uliokuwa unakuja.

Nuhu aliwatayarisha watu kwa wakati wake. Ulikuwa ni wito wa rehema kabla ya hukumu. Mungu alikuwa na njia iliyoandaliwa, nabii wa kuwaongoza.

Aliwatumia Neno Lake. Naye daima hulituma Neno Lake kwa nabii Wake, kama alivyofanya katika wakati wa Nuhu. Alifanya jambo lile lile katika siku za Nuhu. Katika siku za Eli-…za Musa, tunaona Yeye alifanya jambo lile lile. Aliwatumia nabii Wake, nao wakajitenga na kutokuamini. Sasa, watu wa jinsi hiyo ndio waliotoka. Hao ndio walioliamini.

Tumejitenga na kutokuamini kote. Mungu anayo njia iliyoandaliwa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake leo. Alituahidi katika Neno Lake, “Kabla ya hukumu, nitawapelekea nabii kulikusanya Kundi langu dogo nyenyekevu, nami nitawaketisha upande mmoja, nao watakuwa na amani, wakiingojea hukumu ijayo na kuiepuka. ”.

Sisi ndio kundi lile dogo. Sisi ndio wale ambao Baba anaowapenda nasi tunangojea kwa hamu kubwa Ujio wake wa hivi karibuni . Ulimwengu unaporomoka pande zote kutuzunguka, lakini sisi tuko katika pumziko na amani.

Tunajua tuko katika mapenzi yake makamilifu. Haijalishi tuko wapi ulimwenguni, Mungu ana njia iliyoandaliwa kwamba sisi sote tunaweza kuungana pamoja kwenye Neno Lake, kwenye Sauti Yake. Ni njia iliyoandaliwa na Mungu.

Naye huyu nabii akawaongoza kwenye njia iliyoandaliwa na Mungu. Sasa, hiyo ndiyo njia ya Mungu ya kufanya mambo. Unaona?

Njoo uepuke hukumu ijayo pamoja nasi na usikilize:  63-0724 Mungu Hamwiti Mtu Hukumuni Bila ya Kumwonya Kwanza , Jumapili hii saa 6:00 Sita MCHANA , saa za Jeffersonville (Ni Saa 1:00 Moja JIONI ya Tanzania). Ni Sauti ya Mungu ikinena na kutuambia: Hii ndiyo njia Yangu iliyoandaliwa kwa ajili ya Siku hii.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kwa maandalizi ya kusikiliza Ujumbe :

Isaya 38:1-5

Amosi Sura ya 1 yote.

Pasaka 2022

Mpendwa BIBI-ARUSI ALIYEUNGANA Ambaye Anayenena NENO,

Huu ni wakati mzuri zaidi wa maisha yangu marafiki zangu! Tunaona Neno likitimizwa mbele ya macho yetu kuliko wakati mwingine wowote. Inasisimua jinsi gani kutambua Yeye ni Nani, mjumbe Aliyemtuma ni nani, na kisha KUJUA SISI NI NANI! Asante Baba. Hatukufikiri kamwe matukio haya yangetukia namna hii, lakini haya hapa yanatukia papa hapa mbele ya macho yetu, jinsi kabisa nabii Wako alivyosema kwenye kanda.

Niko chini ya matarajio makubwa kuona Roho wake Mtakatifu akituleta karibu Naye kuliko hapo awali kabla ya wikendi hii ya Pasaka. Ningependa kuwaalika kila mmoja wenu kushiriki nasi kwenye Ujumbe huu, pamoja na Bibi-arusi Wake ulimwenguni kote.

” Basi wakati jambo lo lote ndogo linapozuka, mbona unatenda kama mtoto? Inakupasa kuwa mtu mzima. Nena na watu! Amina. “Kisha mwendelee mbele.” Amina. Ndivyo hivyo “Usilie, nena!” Amina. Jamani, napenda hilo. “Mbona unanililia? Nena tu na watu, kisha songeni mbele kwa shabaha yenu.” Cho chote kile, kama ni magonjwa, cho chote kile, kama ni kufufua wafu ama cho chote kile, nena! Nilithibitisha hayo. Nena na watu! ”

Ni fursa iliyoje tuliyo nayo ya kuchangamsha imani yetu, hivyo sisi pia tunaweza Kunena NENO. Njoo ukusanyike pamoja na Bibi-arusi katika wikendi ya Pasaka, tunapojitayarisha kwa ajili ya Kutoka kwa mwisho. Maisha yetu lazima yaistahili Injili, kwa maana kizazi hiki kiko chini ya Shtaka. LAKINI SASA hakuna sababu ya Bibi-arusi wake kulialia, BALI KUNENA! Songeni mbele kwa shabaha yenu. Jina la Bwana lihimidiwe!

Kama kawaida yetu tufanyavyo kwa wikendi ya Pasaka, Hebu tujifungie mbali na ulimwengu kadri tuwezavyo kwa kuzima simu zetu isipokuwa kupiga picha, kusikia Nukuu ya Siku, na kucheza kanda kwenye programu ya Lifeline au kutoka kwenye anuani ya kupakua. Hebu na tumtolee Bwana wikendi hii takatifu kikamilifu, na tusiifanye Pasaka hii kuwa jambo la kijamii, bali kujiweka wakfu kwenye Neno, katika nyumba zetu. Ningependa sisi sote tuungane pamoja wikendi hii kwa ratiba ifuatayo, kwa Saa za kutwa za Mashariki (EDT) isipokuwa kama ifahamike vinginevyo.

ALHAMISI

Ilikuwa ni Alhamisi usiku ambapo Bwana Yesu alikula Karamu ya Mwisho na wanafunzi wake katika ukumbusho wa Pasaka kabla ya kutoka kwa wana wa Israeli. Ni fursa iliyoje ya kufanya ushirika na Bwana katika nyumba zetu, kabla ya wikendi yetu takatifu, na kumwomba atubariki sisi na familia zetu, na kutupa sisi sote kile tunachohitaji katika safari yetu.

Baba wa Mbinguni, tunashukuru kwa ajili ya jambo hili, wakati mwingine wa kukusanyika pamoja, upande huu wa Umilele. Na tunatarajia asubuhi ya leo kuhuishwa upya kwa nguvu kuja kutoka Kwako, zipate kututia moyo kwa ajili ya safari iliyoko mbele. Tumekusanyika kama wana wa Kiebrania walivyofanya asubuhi na mapema, kuokota mana iliyokuwa imetolewa kwa ajili yao usiku kucha, kuwapa nguvu kwa ajili ya siku ijayo. Tunakusanyika kwa ajili ya Mana ya kiroho, asubuhi ya leo, ipate kutupa nguvu kwa ajili ya safari.

Hebu na tuanze wote saa 12:00 kumi na mbili JIONI . kwa masaa ya nchi zetu, na tumsikie Yeye akituambia kwamba tuko katika Kutoka kwa mwisho, tunapokusanyika kukizunguka Kiti Chake cha Enzi ili kusikia Ujumbe: Kutoka kwa Tatu 63-0630M .

Sambamba Tunaposikiliza Ujumbe, tutakusanyika na familia zetu katika nyumba zetu na kushiriki Meza ya Bwana.

Hivi punde tutakuwa na Anuani ya kupakua kanda na ibada ya Ushirika, au, itapatikana kwa muda ulioratibiwa wa ibada kwenye Voice Radio, kwenye app ya Lifeline.

IJUMAA
Hebu na twende kwenye maombi na familia zetu saa 3 :00 Tatu ASUBUHI ( Ni saa 10:00 Kumi jioni ya Tanzania) ., na kisha tena saa 6:00 Sita MCHANA, ( Ni Saa 1:00 Moja Jioni ya Tanzania) Kumualika Bwana awe pamoja nasi na Bibi-arusi wake kutoka ulimwenguni kote katika wikendi hii ya kipekee sana; na ajaze nyumba zetu kwa Roho wake Mtakatifu tunapojitolea kumwabudu.

Hebu Fahamu zetu na zirudi nyuma hadi siku ile pale Kalvari, zaidi ya miaka 2000 iliyopita, na kumwona Mwokozi wetu akining’inia msalabani, kisha tujitoe vivyo hivyo kufanya daima yale yanayompendeza Baba.

Sasa angalieni. Wakati alipokuja ulimwenguni, wakati kulikuwapo na zaidi, kutokuamini kwingi duniani wakati huo kadiri kulivyowahi kuwa, hata hakukumpunguzia mwendo. Aliendelea moja kwa moja kuhubiri vivyo hivyo, na kuponya vivyo hivyo. Hakukumsumbua. Kulikuwako na wakosoaji. Mtu huyo alikosolewa tangu alipokuwa mtoto mchanga mpaka alipokufa msalabani. Je! hilo lilimzuia? La, bwana. Lengo Lake lilikuwa ni nini? “Kufanya sikuzote yale Baba ameandika. Kufanya daima yale yanayompendeza .”
.

Kisha saa 6:30 Sita na Nusu MCHANA . (Ni saa 1:30 Moja na Nusu jioni ya Tanzania) hebu na tufikirie kwa dhati juu ya swali muhimu sana katika maisha yetu, tunapokusanyika kukizunguka Kiti Chake cha Enzi ili kusikia Ujumbe: Je, Maisha Yako Yanaistahili Injili? 63-0630E .

Kisha Hebu na tuungane pamoja Tena katika maombi saa 9:00 Tisa ALASIRI (Ni saa 4:00 Nne Usiku ya Tanzania) . katika ukumbusho wa kusulubiwa kwa Bwana wetu.

JUMAMOSI

Hebu na Tuungane pamoja kwa mara nyingine tena katika maombi saa 3:00 Tatu ASUBUHI ( Ni Saa 10:00 Kumi jioni ya Tanzania) ., na saa 6:00 Sita MCHANA .,( Ni Saa 1:00 Moja Jioni ya Tanzania) na tuitayarishe mioyo yetu kwa ajili ya mambo makuu atakayotutendea kati yetu,

“ Baada ya kulileta shtaka hili dhidi ya marafiki wa—wangu wahubiri huko, na yanibidi niseme mambo haya magumu; lakini Bwana, niliyatenda kwa punzi Yako. Najisikia kuwa Wewe uliniambia nitende hili. Sasa, haumo mabegani mwangu, Bwana. Ni—ninafuraha umeniondokea. Na wao watende nao lo lote wapendalo, Baba. Naomba kuwa wataupokea. Naomba kuwa Wewe utamwokoa kila mmoja, Bwana. Na humo kutokee ufufuo wa wenye haki na Uweza mkuu uje kati ya Kanisa kabla tu ya kuondoka Kwake. Si vigumu kuomba hayo, kwa maana Wewe uliyaahidi. Nasi twatazamia, Bwana, huo mvuto wa tatu tunaojua kuwa utatenda mambo kati yetu .”

Kisha saa 6:30 Sita na Nusu MCHANA.( Ni Saa 10:30 Kumi na Nusu jioni ya Tanzania). sote tutakusanyika pamoja ili kusikia NENO: Lile shtaka 63-0707M . Hii itakuwa SIKU ILIYO KUU jinsi gani kwa Bibi-arusi Wake ulimwenguni kote.

Kisha Hebu na tuungane pamoja tena katika maombi saa 9:00 Tisa ALASIRI. ( Ni Saa 4:00 Nne Usiku ya Tanzania) katika ukumbusho wa kusulubiwa kwa Bwana wetu.

JUMAPILI

Ni siku nzuri jinsi gani ya kutolialia tena, Bali KUNENA! Ni asubuhi iliyoje ya ufufuo! Hebu na tuamke mapema kama vile Ndugu Branham alivyofanya asubuhi ile wakati rafiki yake mdogo, robin, alipomwamsha Saa 11:00 Kumi na moja ALFAJIRI ( ni Saa 6:00 Sita Mchana ya Tanzania) .. Hebu na tumshukuru tu Bwana kwa kumfufua Yesu kutoka kwa wafu:

“ Saa kumi na moja asubuhi ya leo, rafiki yangu mdogo mwenye kifua chekundu aliruka dirishani akaniamsha. Ilionekana kana kwamba moyo wake mdogo ungepasuka, akisema, “Amefufuka.”

Saa 3:00 Tatu ASUBUHI Saa za Jeffersonville ( ni Saa 10:00 Kumi jioni ya Tanzania) Hebu na tuungane kwa dhati kwa mara nyingine tena katika Maombi yetu ya mnyororo , kuombeana mmoja kwa mwingine na tukijitayarisha wenyewe kuisikia Sauti ya Mungu.

Saa 6:30 Sita na Nusu MCHANA saa za Jeffersonville ( Ni saa 1:30 Moja na Nusu Jioni ya Tanzania) tutakusanyika pamoja ili kusikia Ujumbe wetu wa Pasaka: Mbona unalialia? Nena! 63-0714M .

Baada ya Ibada hii, Hebu na tuungane tena katika maombi, Kumshukuru kwa WIKENDI YA AJABU ALIOTUPATIA PAMOJA NAYE NA PAMOJA NA BIBI-ARUSI WAKE ULIMWENGUNI KOTE.

Kwa ndugu na dada zangu walio nchi za ng’ambo, ningependa kuwaalika kuungana nasi kwa matukio haya kwa masaa ya Jeffersonville, kwa masaa yote ya maombi kwenye ratiba hii na kwa kanda itakayochezwa Jumapili asubuhi. Ninatambua, hata hivyo, kwamba kucheza Kanda hizi za Alhamisi, Ijumaa, na Jumamosi alasiri kwa masaa ya Jeffersonville ingekuwa vigumu sana kwa wengi wenu, kwa hivyo tafadhali jisikie huru kucheza Jumbe hizo wakati wowote wa siku husika unaokufaa. Ningependa, hata hivyo, sote tuungane pamoja Jumapili saa 6:30 Sita na Nusu MCHANA za Jeffersonville, ( Ni Saa 1:30 Moja na Nusu Jioni ya Tanzania) ili kusikia Ujumbe wetu wa Jumapili kwa pamoja.

Ningependa pia kukualika wewe na watoto wako kuwa sehemu ya karatasi za creations, mafunzo , na maswali ya YF, ambayo familia yako yote inaweza kufurahia pamoja. Tunafikiri mtayapenda kwa kuwa yote yanahusu NENO ambalo tutakalosikia wikendi hii.

Kwa ratiba ya wikendi, Taarifa kuhusu kujiandaa kwa ajili ya ibada ya Ushirika, nyenzo zitakazohitajika kwa ajili ya kazi za creations , Maswali ya Pasaka, na taarifa nyinginezo, tazama anuani zilizo hapa chini.

Ni heshima kubwa kwangu kukualika wewe na familia yako kuungana pamoja na Bibi-arusi duniani kote kwa wikendi iliyojaa KUABUDU , SIFA NA UPONYAJI. Ninaamini kweli ni wikendi ambayo itabadilisha maisha yako milele.

Ndugu Joseph Branham