All posts by admin5

22-0306 Muhuri Wa Sita

Ujume: 63-0323 Muhuri Wa Sita

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Kondoo wa Mungu,

Ni jambo gani kubwa zaidi liwezalo kuwa, tunaweza kuwa watu waliyotunukiwa zaidi vipi , kuliko kuwa na Mfalme wa wafalme , Bwana wa mabwana miongoni mwetu ?

Hebu fikiria jambo hilo. Uwepo wa Mfalme wa wafalme, Bwana wa mabwana uko pamoja nasi. Ametufunulia kuwa TUMEWASILI. Tumefika! Ufunuo aliotupa unatoka kwa Mungu. Ni kweli. Sisi ni Bibi-arusi Wake na Kondoo waliochaguliwa.

Tunasikia barua Zake za upendo kila wiki zikituambia: “Wana-Kondoo wangu wapendwa, nimefanya mwito Wangu wa kondoo. Mbuzi hawaujui, bali ninyi mmeutambua. Mmedumu waaminifu, kwa maana kondoo Wangu wananijua mimi na mgeni hawatamfuata. Haina budi kuwa ni ishara Yangu ya kiroho Sauti iliyothibitishwa PEKE YAKE .”

Hamkuchezeana kimahaba huko au hata kumtazama mwingine; mmedumu waaminifu kwa Sauti Yangu. Ninyi Ndio wale Nimekuwa nikingojea. Najua mmefanyiwa mzaha na kutoeleweka, lakini niliwaambia Mimi nitarudi kwa ajili yenu kama MTADUMU NA NENO LANGU, nanyi mmedumu nalo. SASA NAKUJA KWA AJILI YENU kama nilivyowahidi ningefanya. Neno ambalo mmekuwa mkilimwagilia maji linakuja kuwapeleka kwenye Makao Yetu Mapya.

Wengine wanaweza kutokuwa na ufunuo sisi tulio nao na kusema kuwa tunaonyesha heshima ya kibinadamu ; au kumwabudu mwanadamu na sio Bwana wetu. Wao ni vipofu jinsi gani . Ikiwa hiyo ni kweli, basi Bibi-arusi wa Kristo ng’ambo ya pazia la wakati pia walikuwa wamekosea.

Wakati Nabii alipomwona Bibi-arusi wakimkimbilia na kusema, “ndugu yetu mpendwa,” walimtwaa juu na kumketisha Mahali pa Juu . Nini…je BIBI-ARUSI wa Kristo alikuwa akionyesha heshima ya kibinadamu kwa nabii kwa kumweka Mahali pa Juu? Je Unasema hawakupaswa kufanya hivyo?

Kisha baada ya hayo, Bibi-arusi wote walikuwa wamesimama pale wakiwa wamevaa nguo zao ndefu nyeupe na kuanza kupaza Sauti, “Kama usingalijitokeza na Injili, tusingalikuwa hapa.” Kama yeye asingalijitokeza wasingalikuwa kule?

Ndipo Sauti kutoka juu ikasema tutahukumiwa kulingana na NENO alilotuhubiria, kisha atatukabidhi kwake.
Sauti haikusema kwamba tutahukumiwa kwa yale mtu fulani aliyosema au yale mtu fulani aliyofafanua kuwa alisema , bali yale Yeye aliyosema . Ndipo yeye atatukabidhi Kwake.

Naweza kuchukua nafasi hii kuzungumza kwa niaba ya sehemu ya Bibi-arusi walio na Ufunuo ule ule nilio nao, na niseme jinsi tunavyohisi. Kama tutahukumiwa kwa Neno hilo , na KIKOMO CHETU CHA MILELE kinategemea Neno ambalo Mungu alilonena kupitia nabii Wake, basi hatuna budi kulisikia PEKE YAKE Neno hilo kutoka kwenye Sauti ya Mungu kwa ajili ya wakati wetu. Hatuwezi, na hatutaweka kikomo chetu cha Milele juu ya yale mtu Fulani anafafanua, au kusema, bali yale ALIYOSEMA. TUNAWEZA KUSIKIA TU SAUTI YA MUNGU PEKE YAKE , na William Marrion Branham ndiye SAUTI PEKEE YA MUNGU…MUNGU ALISEMA HIVYO.

Niliwaudhi kwa kusema hivyo, samahani , lakini, nilihisi huenda nilakuchukiza, lakini, mimi ni Sauti ya Mungu kwenu .

Kwa hiyo tuna furaha na tunamshukuru Bwana kwamba tunafanya kama vile wale Bibi-arusi walivyokuwa wakifanya upande wa pili. Utukufu, Heshima na Sifa zote zinamwendea BWANA wetu MMOJA NA WA PEKEE YESU KRISTO. Kama vile nabii wa Ufunuo 22:9 alivyotuambia, mwabudu Mungu … TUNAFANYA HIVYO na kumpenda sana.

Muda umechelewa . Maandiko yanatimizwa haraka kuliko tunavyoweza kusoma yote yanayotendeka. Anakuja kwa ajili ya Bibi-arusi Wake upesi. Ulimwengu unaungana. Bibi-arusi anaungana. Jukwaa linaandaliwa kwa ajili ya Unyakuo.

Tunamsifu Bwana kwa ajili ya watu walioitwa na Mungu wanaohubiri Neno, Lakini wahudumu, wekeni Sauti hiyo nafasi ya Kwanza ambayo ninyi na watu wenu mtahukumiwa kwayo. Kusanyikeni katika makanisa yenu na msikie Sauti pekee ya Mungu iliyothibitishwa ikinena. Bonyeza Play.

Tunawaalika wote ambao wangetaka kuja ndani ya Safina na kuokolewa pamoja nasi tunapoungana na kusikia Sauti ya Mungu ikinena Maneno tutakayohukumiwa kwayo, saa 6:00 sita mchana , saa za Jeffersonville, ( ni saa 2:00 Mbili Usiku ya Tanzania) na kusikia Muhuri wa Sita 63-0323 .

Ni Chakula cha Kondoo kwa Kondoo wa Mungu. Hakuna kilichoongezwa, hakuna kilichoondolewa na hakuna kilichofafanuliwa, ni CHAKULA safi cha KONDOO kisichoghoshiwa.

Ndugu. Joseph Branham.

Kutoka 10:21-23
Isaya 13:6-11
Danieli 12:1-3
Mathayo 24:1-30
Mathayo 27:45
Yohana 10:27
Ufunuo sura ya 6 yote
Ufunuo 11:3-6

22-0227 Muhuri Wa Tano

Ujume: 63-0322 Muhuri Wa Tano

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Mwili Mmoja Mkuu wa Kristo,

Ni nini kinachotukia leo? Neno la Mungu linatimizwa. Siku ambazo Bibi-arusi alizongojea kwa muda mrefu sasa zinadhihirishwa mbele ya macho yetu. Siku ambazo nabii wa Mungu alituonya zinakuja, sasa zimefika.

Muhuri unafunguliwa. Ni kitu gani hicho? Siri inafunguliwa. Mnaona? Na wakati siri inapofunuliwa, basi baragumu inalia. Inatangaza vita. Pigo linashuka, na wakati wa kanisa ukaanza .

. Urusi
. Vita
. Ukomunisti
. Mafuta
. Mapigo

Wakati Urusi inapoenda huko kupata mafuta hayo, jihadhari .

Urusi, ukomunisti hauteki cho chote! Neno la Mungu haliwezi kushindwa. Urumi utauteka ulimwengu .

Malaika wa maangamizi anaushikilia mkono wa Urusi, ulioshika mabomu ya atomiki ; mpaka Kanisa la Mungu litakapoungana pamoja, na Mwili mmoja mkuu wa Kristo . “ Siwezi kufanya neno lo lote hadi utakapoingia huku.” Loo, kama hilo si dhamana iliyobarikiwa !

Kanisa, Bibi-arusi Wake, anaungana pamoja kutoka ulimwenguni kote kama Mwili Mmoja Mkuu wa Kristo, wakimsikiliza Mungu akinena na kufunua Neno Lake. Tunaona Neno likitimizwa katika ulimwengu unaotuzunguka, lakini pia tunaona Neno likitimizwa na kudhihirishwa ndani yetu.

Tunapokea changamko kwa Ufunuo kuliko hapo awali wakati nabii hizi zinapotimizwa.

Dunia iko katika hofu na wasiwasi . Wanangojea, wanatazama na kushangaa, nini kitatokea baadaye? Kesho ina kitu gani?
Je, haya yote yanamaanisha nini? Je, Urusi itateka? Vipi kuhusu uchumi?

Wakati huohuo, Bibi-arusi yuko kwenye AMANI. TUNAPUMZIKA, tukiwa tumejazwa na Roho wake Mtakatifu, tukimsikiliza akinena kupitia malaika wake mkuu mwenye nguvu akituambia: Msiogope kitu chochote Enyi kundi langu dogo, ninyi ni Kipenzi wangu Waliochaguliwa . Ninyi ni:

Waliochaguliwa kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Amina! Nao ni waaminifu kwa Neno. Amina! Whiu! Ninapenda jambo hilo. “Wanaitwa, waliochaguliwa, kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.” Na halafu, ni waaminifu kwa Neno, kwa uchaguzi wao, wote wamechangamshwa na divai mpya na Mafuta, wamepanda farasi tu moja kwa moja, wakishuka kuja kukabiliana na yeye. Wao wanajua zile Ngurumo zitatoa jambo hilo kwa ajili yetu, karibuni sana .

Anatambua kwamba sisi ni waaminifu kwa Neno lake. Tumefanya hivyo kwa uchaguzi wetu. Sasa tumepanda farasi tu moja kwa moja , tukijua zile Ngurumo zitatoa jambo hilo kwa ajili yetu karibuni sana, Naye atakuja na kutupeleka kwenye Makao yetu Mapya.

Kuna mengi zaidi anayotaka sisi tujue. Kitu fulani kinawaka tu moyoni mwake anataka kutuambia. Hawezi kusubiri zaidi kwani anajua itatupa Changamko. Kwa neema ya Mungu, alimruhusu nabii Wake atuone sisi, watu wake, kule ng’ambo ya pili pamoja naye. Akasema, “Nilipowaona ninyi nyote mlikuwa na NGUO NDEFU NYEUPE .”

Tulikuwa  tumekusanywa pamoja naye. Tulimchukua na kumketisha mahali pa juu kwenye kitu kikubwa na kirefu. Tulimwambia, “duniani, ulikuwa kiongozi wetu”.

Kulikuwa na mamilioni yetu sisi tukimkimbilia na kumkumbatia tukimwita “Ndugu”. Mara moja Sauti kutoka juu ilinena na kusema, “Watu hawa ni waongofu wako ambao umewaongoza. Utahukumiwa kwa yale uliyowaambia”.

Nabii alinena na kusema, “Kama kundi la Paulo likiingia, na langu pia , maana nimehubiri Neno lile lile kabisa.” Na sisi sote tukapaza Sauti WOTE MARA MOJA, KWA SAUTI MOJA:

” Tunategemea Jambo Hilo !”

Jina la Bwana lihimidiwe, tunategemea kila Neno alilonena kupitia nabii Wake. Tutahukumiwa kwa Neno hilo. Tulikuwa watu wa nabii. Alikuwa kiongozi wetu aliyetuongoza kwa Kristo. Sisi Sote tulikuwa na Nguo ndefu Nyeupe. Hatukutegemea kile mtu fulani alichosema ati Alisema , au kile mtu fulani alichosema inamaanisha , tulitegemea kila Neno Yeye alilosema.

Ni siku na wakati wa jinsi gani wa kuishi, Bibi-arusi. Ukisikia taarifa ya habari leo hii, utajua kilichotokea jana. Bonyeza Play, nawe utasikia kile kitakachotokea kesho, na siku inayofuata, na siku inayofuata, na siku inayofuata.

Njoo ukusanyike pamoja na Mwili Mmoja Mkuu Wa Kristo saa 6:00 Sita Mchana , saa za Jeffersonville, ( Ni saa 2:00 mbili Usiku ya Tanzania) Kusikia: Muhuri wa Tano 63-0322. Hakuna Kushangaa, hakuna kudhania , Bali ni KUJUA unasikia BWANA ASEMA HIVI kutoka kwenye Sauti ya Mungu kwa ajili ya wakati wetu.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Danieli 9:20-27

Matendo 15:13-14

Warumi 11:25-26

Ufunuo 6:9-11 / 11:7-8 / 22:8-9

22-0220 Muhuri Wa Nne

Ujume: 63-0321 Muhuri Wa Nne

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliyechangamshwa,

Siku ya Ujumbe ilipowadia, tulikuwa sote mahali pamoja, kutoka duniani kote, kukaja ghafla toka Mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi. “ Habari za jioni wapendwa. Hebu na tusimame sasa kwa muda kidogo tu kwa maombi ”. Roho Mtakatifu akajaza nyumba zetu zote na makanisa tulimokuwa tumeketi, kwa uwepo wake.

Ndipo nguvu ya Ufunuo wa Neno ikaanza kutupa changamko la furaha, changamko la utoshelevu; changamko ya kwamba imethibitishwa, imehakikishwa, ya kwamba sisi ni Bibi-arusi Kipenzi na Mteule wa Yesu Kristo.

Tunazingojea kwa hamu kubwa hizo Ngurumo Saba zitoe sauti Zao kwetu, kwa maana tunajua sasa, bila kivuli cha shaka, ya kwamba sisi ndiyo kundi lile ambalo limechukua Neno la Mungu. Tutakata vipande vipande na kukata kwalo. Tunaweza kufunga mbingu, tunaweza kufunga hiki, ama kufanya vile, lo lote tunalotaka kufanya. Adui atauawa kwa Neno litokalo katika kinywa chetu, kwa maana ni kali kuliko upanga ukatao kuwili. Tunaweza hata kuagiza tani bilioni mia moja za inzi ikiwa tukizitaka. Lo lote TUTAKALOSEMA, Litatukia, kwa maana ni Neno la Mungu likitoka katika kinywa cha Mungu.

Tutakuwa na mamlaka makamilifu, juu ya dunia, kwa kuwa sisi ni mungu mdogo. Mungu ni Mungu wa ulimwengu wote, kila mahali, lakini tutakuwa na dunia chini ya udhibiti wetu wenyewe. Tunaweza kunena , tunaweza kutoa majina, tunaweza kusema, tunaweza kuzuia maumbile, tunaweza kufanya lolote tunalotaka; ni urithi wetu uliyorejeshwa.

Shetani anasema, “Lakini wana hatia!” Bali yeye Anapaza sauti na kusema, “HAWANA HATIA. Wameungama dhambi zao na kusimama mbele zangu wakiwa wamehesabiwa haki kabisa. Siwezi hata kulikumbuka tena. Wao ni mwanangu kabisa.”

Hilo si wazo letu, wala si neno letu, bali ni NENO LAKE, AHADI YAKE, kwa maana Mungu habadilishi kamwe mpango Wake au njia Yake ya kufanya mambo. Yeye daima anamtumia mwanadamu, Naye anatuambia sisi ni Bibi-arusi Wake aliyerejeshwa na kudhihirishwa kikamilifu ambaye amedumu na Neno Lake.

Hatujawa na kitu kingine ila Neno Lake la Asili. Hatujachezeana kimahaba, ama hata kutazama kitu kingine cho chote, bali tumedumu na Sauti ya Mungu, Neno lililofanyika Mwili, Nguzo ya Moto iliyothibitishwa, Mwana wa Adamu, Bwana Asema hivi. Sisi ni Bibi-arusi-Neno Bikira Wake.

Nena kuhusu changamko kwa Ufunuo. Kama vile dada yetu pale Kisimani, haikutulazimu kukaa usiku kucha wala kukaa hadi usiku uliofuata, tumeipata sasa hivi. Sisi ni uzao Wake. Nuru hiyo ilitujia na kitu fulani ndani kikabubujika kwa Maisha mapya. Sasa tuko njiani kuwaambia kila mtu, “Tumefaulu. Kushangaa kote kumekwisha, Mungu Mwenyewe anazungumza nasi kwa kila Ujumbe tunaosikia, akituambia: ‘Ninyi ndio wale nimekuwa nikiwangojea. Sasa nitawapeleka kwenye Fungate letu. Nimewaandalia Makao Mazuri Kila kitu jinsi tu mnavyopendelea . Tutaishi milele pamoja.”

Kwetu sisi, Kweli ya Neno la Mungu lililoahidiwa imethibitishwa na kufunuliwa. Yohana 14:12, Yoeli 2:28, Timotheo wa Pili 3, Malaki 4, Ufunuo 10. Sasa tumejazwa Mafuta nasi tumechangamshwa.

Je, ungependa kuwa na Changamko lili Hili? Unaweza, lakini kuna mahali pamoja tu pa kuipata. Kama vile Yesu alipokuwa kwenye arusi nao wakaishiwa na divai. Kwa kweli walikuwa wakinywa divai na ilikuwa ikiwapa changamko, lakini DIVAI BORA ilitoka kwa Yesu mwenyewe moja kwa moja.

Njoo unywe Divai Bora Zaidi na upokee Changamko kwa Ufunuo bora kabisa pamoja nasi Jumapili hii saa 6:00 Sita Mchana , saa za Jeffersonville, (Ni saa 2:00 Mbili Usiku ya Tanzania), tunaposikia: Muhuri wa Nne 63-0321 .

Uwe tayari kulewa kwa Divai ya Roho Mtakatifu.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma ili kujitayarisha kusikia mahubiri “ Muhuri wa Nne” 63-0321 .

Mathayo Mtakatifu Sura ya 4 yote

Luka Mtakatifu 24:49

Yohana Mtakatifu 6:63

Matendo 2:38

Ufunuo 2:18-23, 6:7-8, 10:1-7, 12:13, 13:1-14, 16:12-16, 19:15-17

Mwanzo 1:1

Zaburi 16:8-11

2 Samweli 6:14

Yeremia Sura ya 32 yote

Yoeli 2:28

Amosi 3:7

Malaki Sura ya 4 yote

22-0213 Muhuri Wa Tatu

Ujume:: 63-0320 Muhuri Wa Tatu

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Bikira,

 Nimekuwa nikiomba na kumuuliza Bwana kile ambacho angenitaka niandike na kusema ambacho kingeweza kuwa baraka na faraja kwako, Bibi-arusi Wake.  Sina maneno, na sijui niseme nini.  Ninajiona sistahili hata kuandika maneno machache niandikayo, lakini ni heshima kuu sana  ya maishani mwangu kufanya chochote kwa ajili Yake.

 Ninaamini wakati wa kusikia Mihuri hii Saba ni mkamilifu sana.  Tunaweza kuona mpango mkuu wa Mungu ukifunuliwa na kuwekwa wazi mbele zetu.  Ujumbe baada ya Ujumbe unakuwa Ufunuo mkuu zaidi baada ya Ufunuo.  Tunamwona yeye akijifunua mwenyewe kwetu na kutuongoza.  Tunajua tunafanya yale hasa yeye aliyotuambia tufanye, “kudumu na Neno.”  Hakuna njia kuu zaidi ya kufanya hivyo kuliko Kubonyeza Play .

 Ninahisi wito alioweka moyoni mwangu ni kudumisha Ujumbe huu, sauti Yake, kanda hizi mbele yenu daima;  ili kukueleza umuhimu wa kuzisikiliza kanda.  Najua siwezi kulifikisha ipasavyo, lakini NAJUA niko sahihi kuwaambia “Bonyeza Play,” kwani si fikira zangu, wazo langu, wala maneno yangu, bali ni Maneno ya Mungu Mwenyewe anenayo kupitia malaika-mjumbe Wake wa 7, akituambia :

  Wakati mwingine wakati tunaposoma tu, na, sasa, iweni waangalifu sana. Na wakati unaposoma, chukueni kanda, zisikilizeni kwa makini sana. Kwa sababu, utalipata kwenye kanda, kwa sababu wamekuwa wakizicheza kanda hizo, na ni nzuri zinasikika vizuri . Kwa hiyo, mtalisikia vizuri zaidi humo .

 Kama nilivyosema mara nyingi sana hapo awali, sipingi huduma au chochote ambacho Mungu ameweka katika kanisa Lake.  Hiyo ingekuwa ni kwenda kinyume na Neno la Mungu.  Ninaamini wametiwa mafuta na wameitwa na Mungu.  Lakini ninaamini ya kwamba kusikiliza na kuweka Sauti yenyewe hasa ya Mungu mbele ya watu halina budi kuwa jambo la muhimu sana mtu yeyote aliyeitwa na Mungu angeweza kufanya.

 Haitoshi kusema tu, “Ninawaambia kusanyiko langu kuzicheza kanda.”  Ikiwa unaamini:

 . Hakuna upako mkuu kuliko kusikia Sauti ya Mungu kwenye kanda.

 . Ufunuo wote lazima utoke kwenye Sauti hiyo.

 . Imani ya Kunyakuliwa tunayohitaji itakuja kutoka kwenye kile isemacho Sauti hiyo.

 Mhudumu yeyote anawezaje kutotaka kuisikiliza Sauti hiyo, pamoja na kanisa lao, na kusema AMINA KWA KILA NENO?

 Kila mmoja lazima wawe na Kitu fulani wanachohisi na kuamini kuwa ni jambo la MUHIMU ZAIDI wanaloweza kufanya ili kuwa Bibi-arusi wa Kristo.  Kitu fulani lazima Kiwe cha MUHIMU SANA  cha Mungu na  Mapenzi yake Makamilifu.  Je, hiyo ni huduma ya mchungaji wako?  Ni Kusikiliza  wahudumu wengine?  Si kusema hilo ni kosa, la hasha, na hilo ni sawa kabisa kulingana na Neno, Lakini je! unaamini jambo la MUHIMU ZAIDI ni kusikiliza Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kwenye kanda?

 Ikiwa hilo ndilo unaloamini kuwa ndilo jambo MUHIMU SANA ungeweza kufanya, basi kwa nini huduma haitaki kucheza na kusikiliza huo UJUMBE  MUHIMU SANA NA MKAMILIFU pamoja na makusanyiko yao?

 Jiulize mwenyewe , au muulize mchungaji wako swali hili: Je, unaamini kuwa nukuu hii ni ya kweli, au je, hili ni kosa na ni kutokuelewa kwa Ndugu Branham, au kujaribu kujisifu mwenyewe?

 Unaona, ni vile vile ambavyo ingetukia sasa! Na, kwa kanisa, ni Kitu gani ? Neno lililofanyika mwili likifanywa mwili miongoni mwa watu Wake tena ! Unaona? Nao hawaliamini Hilo kamwe .

 Ikiwa unaamini kuwa nukuu hii ni ya kweli, na kwako wewe ni SAUTI YA MUNGU, Neno lililofanyika mwili, basi ni jinsi gani mtu ye yote asingeweza kuona kwamba HAKUNA KITU CHA MUHIMU zaidi Ya Kuisikia Sauti hiyo .

 Amka ewe bikira aliyelala, je nawe una Ufunuo huu au uko kama alivyosema: ”  Huliamini hilo kamwe . ”

 Kama vile nabii alivyotuambia, sisi ni Kitabu kipya cha Matendo, lile Tawi jipya, Wateule Wake.  Hivyo, wengi wanahisi kwamba Roho Mtakatifu sasa hivi anatuongoza kama watu binafsi au anatuongoza kwa huduma, wala si kwa nabii Wake.

 Kuna ukweli mwingi katika hili, LAKINI nabii alilisahihisha hili pia, na akatufunulia ukweli.

 Mtu fulani alikuwa akizungumza nami hapa si muda mrefu uliopita.  Kasema, “Lakini Ndugu Branham…” [Ndugu Branham anasafisha koo lake—Mh.] Samahani.  Kasema, “baada ya Roho Mtakatifu kuja, hakuna Malaika wanaoliongoza kanisa, ama kuelekeza watu binafsi.  La, bwana.”  Kasema, “Ni Roho Mtakatifu anayetuongoza.”

 Huko ni kutokuelewa kati ya Malaika na Roho Mtakatifu .  HILO NI KOSA, Malaika waliliongoza Kanisa kote kote, na wangali wanaliongoza Kanisa. Sahihi kabisa .

 Malaika wake analiongoza na kulielekeza Kanisa Lake.  Sote tuna nafasi zetu na wito wetu, lakini malaika peke yake ndiye anapaswa kumwongoza Bibi-arusi.

 Sikiliza kile nabii wa Mungu alichosema kuhusu huduma zingine zote ukilinganisha na kile ambacho Mungu ALICHOMWITIA YEYE KUFANYA,

 Ni kama tu mtu ambaye anafanya kazi ya—ya opareta wa simu, yeye si fundi umeme kabisa. Yeye huenda akafanya kazi ndogo ya umeme. Na kama vile, kama mtu ni mlinda nyaya za umeme, vema, bila shaka yeye…Mtu akiwa ni mchimba mashimo ya nguzo za umeme, naye hajafanya kazi yo yote ya ulinzi wa nyaya za umeme, afadhali asizikaribie; lakini huenda akafanya kazi ndogo ya kurekebisha ama jambo fulani lile .

 Lakini wakati lile Jambo halisi litakapofunuliwa katika siku ya mwisho, ya sehemu ya mwisho ya Kanisa, ni wakati Mungu amesema ya kwamba Yeye angetutumia, kulingana na Maandiko. Nasi tumeyachunguza kindani kabisa, ya kwamba Yeye alibashiri ya kwamba Roho ya Eliya ingerudi juu ya mtu fulani .

 Wakati Mtu fulani anapojaribu kubishana nawe na kukuambia, “inahitaji zaidi ya kusikiliza kanda tu.  Ndugu Branham kamwe hakusema kuzicheza kanda kanisani.  Itahitaji huduma kumkamilisha Bibi-arusi;”  ama chochote kile ambacho mtu ye yote anaweza kukuambia, ili kujaribu na kukufanya utilie shaka na ya kwamba kusikiliza Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kwenye kanda kanisani mwenu ni makosa…

 Kama tu vile jamaa fulani anavyoanza, kujaribu kubishana nawe ;  ikiwa unajua pa kusimama, Tambua kile anachoamini .

 Kama wanadai kuamini  kuwa , “Ujumbe Huu ni Neno.  William Marrion Branham ni malaika-mjumbe wa Saba wa Mungu.  Ujumbe huu ndio Yakini Yao.  Ujumbe huu ni Mwana wa Adamu akijifunua mwenyewe katika mwili kama alivyoahidi angefanya…”

 Ni kama tu kumchukua sungura na kumwachilia awe huru kwenye zizi, na umeziba kila tundu. Wewe simama tu langoni; lazima arudi. Imekwisha. Unaona? Hana budi kurudi langoni tena, maana hiyo ndiyo njia pekee anayoweza kutokea. Atatokeza kichwa chake apenyeze hapa, na karibu avunje shingo yake; halafu aende kule, mahali kule. Wewe simama tu na umwangalie, naye atarudi moja kwa moja. Unaona? Imekwisha .

 Shikilieni Mafundisho hayo ya Kanda.  Semeni tu kile kanda zinachosema.  Msibadili Neno moja.  Msiongeze kwake, wala kuondoa Neno moja.  Ni Sauti ya Mungu kwenu.  Ni Neno Lililofanyika Mwili.  Ni Maneno yasiyoweza kukosea.  Yeye ni mchungaji wenu.  Malaika wake anawaongoza.  Ni  Bwana Asema Hivi .

 Maadamu uko katika Neno hilo, uko salama .

 Njoo Utengeneze taa yako na kuijaza Mafuta Jumapili hii saa 6:00 Sita Mchana , saa za Jeffersonville, ( ni saa 2:00 mbili Usiku ya Tanzania), wakati malaika mteule wa Mungu anaponguruma na kuuvunja  Muhuri wa Tatu 63-0320 , na kuufunua kwa Bibi-arusi Wake.

 Ndugu.  Joseph Branham.

 Maandiko ya kusoma ili kujitayarisha kusikia mahubiri, “ Muhuri wa Tatu .”

 Maandiko:

 Mathayo Mtakatifu 25:3-4

 Yohana Mtakatifu 1:1, 1:14, 14:12, 17:17

 Matendo Sura ya 2 yote

 I Timotheo 3:16

 Waebrania 4:12, 13:8

 1 Yohana 5:7

 Mambo ya Walawi 8:12

 Yeremia  Sura ya 32 yote

 Yoeli 2:28

 Zekaria 4:12

22-0206 Muhuri Wa Pili

Ujume: 63-0319 Muhuri Wa Pili

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Tawi Jipya,

Kimetendeka; kile ambacho watakatifu wote walio tutangulia wamekuwa wakingojea. Ule Mti wa Asili sasa umetoa tawi jipya. Tumewasili. Sisi ndilo hilo Tawi Jipya. Roho Mtakatifu ameshuka, na Roho wa Mungu yuko juu yetu. Ile Imani ya Asili, ya Kipentekoste, ya kimitume imerejeshwa na malaika Wake wa 7. Sasa, nabii Wake anaenda nyumba kwa nyumba, akimega mkate pamoja nasi. Kuna ishara kuu, maajabu, na Ufunuo juu ya Ufunuo unaomwagwa juu yetu.

Tunaziweka taa zetu zikiwa zimetengenezwa na zimejaa Mafuta. Tunadumu na Neno la Asili, kama alivyotuambia tufanye. Wengine wanaweza kutaka Kanisa, lakini sisi HATUTAKI LOLOTE ILA SAUTI YA MUNGU YA ASILI.

Sasa, hebu wazia tu jambo hilo sasa. Hebu tuninii tu—tujaribu kuyaingiza yale tunayoamini kwamba Roho Mtakatifu angetutaka tujue .
Sasa kumbukeni , “ Hakuna lo lote linaloweza kufunuliwa; Mungu hatafanya neno lo lote, hata kidogo, mpaka kwanza alifunue kwa watumishi Wake, manabii.” Na kabla ya Yeye hajafanya neno lo lote, hulifunua .

Hakuna kinachoweza kufunuliwa kwa Bibi-arusi; ikiwa si na nabii Wake kwanza. Kama kuna siri zozote zitakazofunuliwa, ufunuo wowote mpya, cho chote tunachohitaji ili kuwa Bibi-arusi Wake na kunyakuliwa, Ni lazima kwanza umjie nabii ndipo YEYE atatufunulia jambo Hilo, Bibi-arusi Wake.

Kufunua nini? Siri ya Ngurumo Saba. Hilo lina maanisha nini? Inamaanisha moja ya mambo mawili. Labda tayari ipo kwenye kanda na itafunuliwa ufikapo wakati wake kufunuliwa kwetu.

Lakini nawazia, wakati siri hizo zinapoanza kufunuliwa, Mungu alisema, “Zifiche sasa. Ngoja kidogo. Nitazifunua katika siku hiyo. Usiziandike, hata kidogo, Yohana, maana zitawakwaza. Zi—ziache tu, unaona. Lakini nitazifunua katika siku ile ambayo kuna haja ya kuzijua .”

Ama, atamtuma nabii Wake kurudi duniani ili kututambulisha Kwake, ndipo nabii Wake atatufunulia siri ya zile Ngurumo Saba.

Na ndipo kunakuja Ngurumo saba za siri ambazo hata hazijaandikwa kamwe. Hiyo ni kweli. Nami naamini ya kwamba, kupitia Ngurumo hizo Saba, zitafunuliwa katika siku za mwisho ili kumkusanya Bibi-arusi pamoja kwa ajili ya kupata imani ya kunyakuliwa. Kwa sababu, ile tuliyo nayo sasa hivi, ha—hatungeweza kufanya jambo hilo. Kuna jambo fulani. Hatuna budi kupiga hatua mbele zaidi.

Haitakuwa ni kundi la watu ambao watakaofunua siri hiyo, Itakuwa ni Malaika-mjumbe Wake wa 7, William Marrion Branham. Hiyo si kwa sababu “MIMI ” nilisema hivyo; ni kwa sababu NENO LINASEMA HIVYO!!

“ Anachukua kile Kitabu na, cha Mihuri, na kuzivunja,” na kumwonyesha malaika wa saba ; kwa kuwa hii pekee, siri za Mungu, ndiyo huduma ya yule malaika wa saba .

Inasema yote hapo. Huduma ya Siri za Mungu si ya mwingine ila malaika wa saba. Zile Ngurumo Saba zitamkusanya Bibi-arusi pamoja na kutupa imani ya kunyakuliwa.
Ikiwa Ngurumo ndizo zitamkusanya Bibi-arusi pamoja, na siri ya Ngurumo haina budi kutoka kwa malaika wa 7, basi hakuna jambo la muhimu zaidi kwa Bibi-arusi kufanya kuliko KUBONYEZA PLAY . Hilo ndilo litakalomkusanya Bibi-arusi pamoja kwa ajili ya Unyakuo.

Dumu na Neno la Asili kwenye kanda. BONYEZA PLAY .

Na kanda zitafunua mengi Yake, wakati unajifunza .

Jina la Bwana libarikiwe! Utukufu kwa Mungu! Tunaipenda hisi hiyo tamu tunayopata kutokana na kusikia Sauti ya Mungu ikizungumza nasi kwenye kanda. Tunamsikia tu Roho Mtakatifu akifurika pande zote kutuzunguka tunapotembea Nayo. Tunaenda nayo nyumbani. Tunaishikilia kwenye mto wetu.

Njoo usikilize pamoja nasi Jumapili saa 6:00 Sita Mchana , saa za Jeffersonville, ( ni Saa 2:00 mbili Usiku ya Tanzania), Roho Mtakatifu anapokuja kwa uvumi majumbani mwetu na kutufunulia yote tunayohitaji, tunaposikia: Muhuri wa Pili 63-0319.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Mathayo Mtakatifu 4:8 / 11:25-26 / 24:6

Marko Mtakatifu 16:16

Yohana Mtakatifu 14:12

2 Wathesalonike 2:3

Waebrania 4:12

Ufunuo 2:6 / 6:3-4 / Sura ya 17 yote nzima / 19:11-16

Yoeli 2:25

Amosi 3:6-7

22-0130 Muhuri Wa Kwanza

Ujume: 63-0318 Muhuri Wa Kwanza

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Malkia wa Mbinguni,

MIMI , Mfalme wenu, nitanguruma kwenu NINYI siku ya Jumapili na kuwaambia NINYI , NINYI ndiyo Bibi-arusi Wangu. Nimewachagua NINYI kimbele. nimewakomboa NINYI. Nimewahesabia haki NINYI na Niliyaweka majina yenu kwenye Kitabu changu cha Uzima cha Mwana-Kondoo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. WEWE ni Malkia Wangu Kipenzi.

Nimewangojea na kuwangojea NINYI ili niweze kurejesha yote ambayo Adamu wangu wa kwanza alipoteza. Urithi wake wote ambao alipoteza. Ushirika wake wote na haki ya Uzima. Nilikuwa nimempa mamlaka makuu kamili juu ya dunia. Yeye Alikuwa mungu wa dunia nikiwa mimi ndiye Mungu wa ulimwengu wote.

Yeye alikuwa na mamlaka juu ya dunia hii. Angeweza kunena, aliweza kutoa majina, aliweza kusimamisha maumbile, aliweza kufanya lo lote alilotaka kufanya. Lakini alipoteza hayo Yote.

Sasa, kama nilivyokuahidi WEWE katika Neno Langu, Nimerudisha yote aliyopoteza na nimekurudishia WEWE. Yamekombolewa. Umilikaji halali wa yote yaliyopotezwa na Adamu sasa ni YAKO. Umilikaji wa halali wa hiyo hati-miliki ya kuwazika ya Uzima wa Milele, ambayo inamaanisha ya kwamba WEWE una kila kitu ambacho Adamu alikipoteza.

Nimekuwa aliye jamaa yako wa karibu. Nilidai kilicho Changu. Nilikitwaa kitabu cha ukombozi kutoka kwenye Mkono wa Baba Yangu, nikachana ile mihuri kutoka katika kitabu hicho na nikakituma kwa malaika-mjumbe wangu wa saba ili akufunulie WEWE. Atakurudishia WEWE Imani ya asili ya Biblia na atakufunulia WEWE siri Zangu zote.

Nimekuhakikishia na kukuthibitishia mambo haya kupitia Adamu Wangu wa kwanza aliyerejeshwa kikamilifu; Malaika wangu wa saba nabii-mjumbe. Angeweza kunena na kuwaumba kindi, kumrudishia samaki uhai , kudhibiti hali ya hewa na kuirudisha Tufani kule ilikotoka. Angeweza kunena na kuwafufua wafu. Hata nilipigwa picha YANGU pamoja naye ili kuonyesha ulimwengu, huyu ndiye Adamu Wangu wa kwanza aliyerejeshwa, msikieni yeye. Sasa WEWE, Malkia Wangu, una kila kitu ambacho Adamu alikipoteza.

Kumbuka, malaika-mjumbe wangu wa saba atakuwa duniani wakati wa Kuja Kwangu. Atakutambulisha KWANGU. Parapanda hiyo ya mwisho italia na waliokufa katika Kristo watafufuka. Wale walio hai na waliosalia watanyakuliwa pamoja nao, ili kunilaki hewani wakati ule ule malaika Wangu wa saba anapotoa Ujumbe wake. Muhuri wa mwisho unafunguliwa. Ile Parapanda ya mwisho italia; Nitakuja kudai mali yangu, WEWE, na ndipo nitakupeleka WEWE kwenye Karamu YETU ya Harusi.

Malkia wangu mpendwa, njoo unisikie Nikizungumza NAWE na kukufunulia kila kitu unachohitaji. Nimekuhifadhia WEWE Chakula hiki ili WEWE uwe Malkia Wangu. Nitazungumza na WEWE saa 6:00 Sita mchana, saa za Jeffersonville, ( ni Saa 2:00 Mbili Usiku Ya Tanzania), ambapo nitanguruma KWAKO Muhuri wa Kwanza 63-0318 .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma ili kujitayarisha kwa ajili ya kusikiliza Ujumbe:

Mathayo Mtakatifu10:1 / 11:1-14 / 24:6 / 28:19

Yohana Mtakatifu12:23-28

Matendo 2:38

2 Wathesalonike 2:3-12

Waebrania 4:12

Ufunuo 6:1-2 / 10:1-7 / 12: 7-9/ 13:16 / 19:11-16

Malaki Sura ya 3 yote na sura ya 4 yote

Danieli 8:23-25 ​​/ 11:21 / 9:25-27

22-0123 Pengo Kati Ya Nyakati Saba Za Kanisa Na Ile Mihuri Saba

Ujume: 63-0317e Pengo Kati Ya Nyakati Saba Za Kanisa Na Ile Mihuri Saba

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi anayepiga vifijo na kufurahi,

Tuko katika Neno na tuna wakati mkuu zaidi katika maisha yetu yote. Kufundisha, kujiweka wakfu, na ufunuo. Hakuna kitu muhimu zaidi kuliko kusikia Sauti ya Mungu kwenye kanda.

Ujumbe huu ni kila kitu kwetu sisi. Unatupa kuridhika kukamilifu. Kitu pekee kinachoweza kuzima kiu ya nafsi zetu ni kumsikia Mungu akisema nasi kupitia nabii wake.

Kila siku anatupa ufunuo zaidi wa Yeye Mwenyewe na sisi wenyewe. Uhakikisho wa kina zaidi kwamba, kwa “Kubonyeza Play,” tunasikia Neno Lake na tunafanya kama vile Yeye alivyotuamuru kufanya. Sisi ni kondoo wake, na kondoo hawezi kujiongoza mwenyewe; inabidi awe na kiongozi. Na Roho Mtakatifu anatuongoza Kwake, Sauti Yake inenayo Maneno ya kutoweza kukosea kwenye kanda.

Si kwa bahati kwa sisi kusikiliza Jumbe hizi pamoja, Yeye alituchagua sisi kufanya hivyo. “hatua za wenye haki huongozwa na Bwana.” Kuna sababu fulani. Hatuwezi kusaidia. Ujumbe kwenye kanda ndio tu Bibi-arusi anaotaka. Kwa kuusikia, inatupa mkono wenye nguvu wa Imani kushikilia na kuamini kila Neno.

Kwa nini tunaamini ni muhimu sana kwa wote wanaojiita “Bibi-arusi wa Mungu” kuzisikiliza kanda ?

Neno linatuambia wazi kwamba Biblia yenyewe iliandikwa na manabii. Hayakuwa mawazo yao, wala fikra zao, bali Roho Mtakatifu akiwasukuma kuandika Biblia. Biblia pia inatuambia kwamba Bwana Mungu hatafanya neno LOLOTE mpaka atakapolifunua Neno Lake kwa nabii Wake. Wengine wanaweza kunena Hilo na kulitangaza, lakini wanaweza kusema TU yale ambayo nabii wa Mungu amekwisha kusema.

Kama unaamini ya kwamba William Marrion Branham ni Malaika-mjumbe wa 7 aliyethibitishwa na Mungu, basi kile alichosema KWENYE KANDA si maneno yake, bali ni mawazo yenyewe hasa ya Mungu Mwenyewe yaliyotambulishwa. Unaweka Kikomo chako cha Milele kwenye kila Neno alilonena kwenye hizo kanda, kama unavyoamini hiyo kuwa ni BWANA ASEMA HIVI. Haiwezi kuongezwa kwake wala kuondolewa kutoka kwake, wala halihitaji kufasiriwa; Ni Mwana wa Adamu akizungumza kupitia kwa mtu aliyemchagua ili kutimiza Neno Lake.

Bibi-arusi wa kweli anajua umuhimu wa kuzisikiliza kanda. Kwetu sisi, kanda hizi ni kuu na huduma nyingine zote ni ndogo. Kila mtu lazima wajiulize kama kikomo chao cha Milele kinategemea kuamini kila Neno ambalo nabii wa Mungu alilonena. Kama ninaamini ni Sauti ya Mungu inayonena na kumwita Bibi-arusi Wake, basi hakuna kitu cha maana zaidi kuliko KUBONYEZA PLAY, kwani nitahukumiwa kwa kila Neno ambalo NABII WA MUNGU ALILOSEMA…si kwa lile mtu fulani alilosema kwamba nabii wa Mungu alisema.

Kama unaamini unahitaji zaidi ya hizi kanda , basi kwako huoni umuhimu kuweka msisitizo wa kuzisikiliza kanda, bali unaweka umuhimu zaidi kwenye huduma. Unaweza kuwa na mkuu mmoja tu.

Tutakaposikiliza kanda Jumapili hii, Mungu Mwenyewe atazungumza nasi na kutuambia tuna umiliki wa halali wa hati-miliki ya kuwazika ya Uzima wa Milele. Tuna kila kitu ambacho Adamu na Hawa walikipoteza. Kitaletwa kwetu katika ufunuo, na kutoka katika Mkono wa Mungu kwa kuthibitishwa.

Kisha atatuambia nini kiliendelea Mbinguni. Jinsi Yesu Mwenyewe alivyokitwaa kile Kitabu, akaichana muhuri, kisha akakipeleka kwa nabii aliyemchagua na akamwambia ampe Bibi-arusi Wake….Nena kuhusu vifijo !!!! Kila kitu duniani na Mbinguni kitatusikia tukipiga vifijo na kupiga vigelegele tunapoona majina yetu yameandikwa kwenye Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo.

Naye akakitwaa kile Kitabu, (utukufu!) akakifungua kile Kitabu, na kuichana ile Mihuri; na kukituma duniani, kwa malaika Wake wa saba, kukifunua kwa watu Wake! Haya basi. Loo! jamani! Ni kitu gani kilichotukia? Vigelegele, vifijo, zile haleluya, watiwa mafuta, nguvu, utukufu, dhihirisho!

Na maskini Yohana, aliyekuwa amesimama pale, ndugu yetu, akilia! “Mbona,” yeye akasema, “kila kitu Mbinguni, kila kitu duniani, na kila kitu chini ya bahari, vilinisikia nikisema kwa sauti kuu, ‘Amina! Amina! Baraka, heshima, na uweza, na nguvu, ziwe Kwake Yeye aishiye milele na milele.’”

Unaweza kuusikia wapi ufunuo huu mkuu? KWENYE KANDA TU. Kuna jambo la Kipekee kwa Bibi-arusi wanapomsikia Mungu Mwenyewe akisema kupitia midomo ya mwanadamu na kuwaambia, “WEWE NDIWE BIBI-ARUSI WANGU KIPENZI.”

Njoo uketi katika uwepo wa Roho Mtakatifu kwa Kubonyeza Play , Jumapili saa 6:00 sita Mchana, saa za Jeffersonville,( ni saa 2:00 Mbili Usiku ya Tanzania) tunaposikia Malaika-mjumbe Wake wa saba akileta: Pengo Kati ya Nyakati Saba za Kanisa Na Ile Mihuri Saba 63-0317E .
Tutakuwa tukipiga vifijo na kushangilia na kusema haleluya.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kwa maandalizi ya kusikiliza Ujumbe:

Mambo ya Walawi: 25:47-55

Yeremia: 32:1-15

Zekaria: 3:8-9 / 4:10

Warumi: 8:22-23

Waefeso: 1:13-14 / 4:30

Ufunuo: 1:12-18 / Sura ya 5 yote / 10:1-7 / 11:18

22-0116 Mungu Akijificha Kwa Urahisi, Halafu Akijifunua Kwa Jinsi Hiyo

Ujume: 63-0317M Mungu Akijificha Kwa Urahisi, Halafu Akijifunua Kwa Jinsi Hiyo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Kundi dogo la Eliya ,

 Sisi ni watu wateule, wakipekee na wasio wa kawaida  kwa ulimwengu, na kwa waaminio wengi, lakini hata hivyo, sisi ni ukuhani wa kiroho, taifa la kifalme, tukimtolea Mungu dhabihu za kiroho, pamoja na matunda ya midomo yetu tukilisifu Jina Lake.  Tunataka kuuambia ulimwengu kwamba tuna furaha sana, tunashukuru sana, na kuheshimika sana kuwa Wamoja Wao.

 Tumeuza lulu zetu nyingine zote, Yeye alipotupa Lulu ya thamani kuu, Ufunuo Wa Yeye Mwenyewe.  Tunaona Neno lenyewe la Mungu likidhihirishwa.  Ahadi ile ile ya siku za mwisho, Nuru za jioni zile zile ambazo zingeangaza.

 Imefunuliwa kilindi kabisa mioyoni mwetu kwamba Sauti tunayoisikia kwenye kanda ni Mwana wa Adamu akijifunua Mwenyewe.  Sauti hiyo ilituambia: Kaeni hapa, Angalieni Chakula Hiki kilichohifadhiwa ambacho nimewawekea kwenye hizo kanda.  Ikiwa una maswali yoyote, Rudi kwenye kanda hizi.  Inaweza hata kukushangaza kidogo, lakini cheza tena kanda na usikilize kwa makini.  Kama wewe ni Bibi-arusi, Roho Mtakatifu atakufunulia jambo Hilo.  Kumbuka, kanda hazihitaji kufasiriwa kokote, sema tu kile kilicho kwenye hizo kanda.  Mimi ni mchungaji wenu na ninyi ni kundi langu dogo, Dumuni na mafundisho ya kanda.

 Najua wengi sana hawaelewi tunachofanya kwa kusikiliza Ujumbe uleule wote kwa wakati mmoja, lakini ni sawa, bado ni ndugu na dada zetu nasi tunawapenda na hatupaswi kamwe kusema dhidi yao.  Kila Mtu lazima afanye kama wanavyohisi wanaongozwa Na Bwana kufanya.  Mungu hufanya kazi na kutuongoza kama watu binafsi.

 Nabii alituambia lazima tuchunguze kila kitu kwa Neno, na kukithibitisha kwa Neno, kama tu alivyofanya.  Neno la wakati huu, Ni na daima imekuwa, Biblia.  Biblia inatuambia katika siku za mwisho angefunua kikamilifu siri na mafumbo yote katika Biblia yake kwa nabii ambaye atamtuma.  Yeye Mwenyewe angenena kupitia nabii huyu na kujidhihirisha Mwenyewe katika mwili kama alivyofanya kwa Ibrahimu.  Neno Lake lisingekuwa maneno ya mwanadamu, bali  Maneno yenyewe ya Mungu Mwenyewe.  Ingekuwa BWANA ASEMA HIVI, kwa hiyo Biblia na Sauti hiyo zingekuwa kitu kimoja na sawa.

 Kuna Kilindi  kikiita kilindi  ndani ya mioyo yetu kusikia hiyo Sauti iliyothibitishwa.  Tunataka kusikia Sauti ya Mungu moja kwa moja kutoka kwa nabii Wake Aliyechaguliwa.  Kuna upendo kama huu mioyoni mwetu kusikia Sauti hiyo na kustarehe tu tukijua hatuhitaji kuhoji chochote tunachosikia, inabidi tu kuamini KILA NENO.

 Hakuna mahali pengine ambapo tunaweza kufanya hivyo.  Sio kwamba mtu fulani angetuambia jambo lisilo  sahihi au kutupotosha, kwa vile wao pia wana Roho Mtakatifu, Lakini tunajua kwamba wanaweza kutuambia jambo Lisilo Sahihi bila kupenda.  Lakini tunaposikia Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kwenye kanda, hata kama hatuelewi kinachosemwa, Baba Mungu alisema inatupasa tu kusema AMINA, TUNAAMINI KILA NENO.  Hatuwezi kufanya hivyo kwa sauti nyingine yoyote.

 Tuliamriwa na Sauti hiyo pia:

 Msinisikilize mimi , bali sikilizeni kile nilichosema. Nilichosema ni ujumbe . Msimjali mjumbe kamwe; angalieni ujumbe. Kazeni macho yenu, si juu ya mjumbe, lakini juu ya ujumbe—kile ulichosema . Hilo ndilo jambo la kuangalia `“ .

 Alichosema NI Ujumbe wa wakati huu.  Tunapaswa kukaza macho yetu juu ya Ujumbe;  Ndilo jambo la kuangalia .

 Anatufunulia mambo kuliko hapo awali.  Kila Ujumbe tunaosikia unasikika kama Ujumbe mpya ambao hatujawahi kamwe kuusikia.  Ingawa tumezisikia mara mamia hapo awali, hatuwezi kueleza, ni kama tunausikia kwa mara ya kwanza naye anatupa Ufunuo zaidi na zaidi.

 Hatuwezi tu kuwazia mtu yeyote Asitake kusikia Jumbe hizi pamoja nasi.  Kuna muungano kama huo na Umoja pamoja na Bibi-arusi na Neno Lake.  Tumeridhika kabisa zaidi ya wakati mwingine maishani mwetu.

 Kwa mara nyingine tena tuko chini ya matarajio makubwa.  Ni kana kwamba Mihuri inafunguliwa sasa hivi.  Anaenda kutuonyesha mambo ambayo hatujawahi kamwe kuyaona hapo awali na kuleta Nuru kwa mambo ambayo tumesikia mara nyingi ,nyingi sana hapo awali;  lakini sasa, tutaliona waziwazi.

 Tunajua ya kwamba kila kitu tunachohitaji kwa ajili ya Unyakuo Wake ujao hivi karibuni, ni ile Sauti kwenye hizo kanda.

 Mungu alimtuma nabii Wake kwa ono upande wa nyuma wa jangwa huko Arizona ambako alitwaliwa juu na malaika saba, kisha akarudishwa Jeffersonville kufunua siri zilizofichwa za ile Mihuri Saba kwa Bibi-arusi.

 Njoo usikilize pamoja nasi Mungu anapozungumza nasi mdomo kwa sikio Jumapili hii saa 4:00 nne Asubuhi., saa za Jeffersonville,( ni saa 12:00 kumi na mbili jioni ya Tanzania),  nasi tutasikia: Mungu Akijificha  Kwa Urahisi, Halafu Akijifunua Kwa Jinsi  Hiyo 63-0317M .

 Tutauanza Ujumbe huu kwenye aya ya #94, baada ya ibada ya kuweka wakfu.

 Ndugu.  Joseph Branham

 1 Mambo ya Nyakati 17:1-8

 Isaya 35:8 / 40:1-5 / 53:1

 Malaki Sura ya 3 yote

 Mathayo Mtakatifu 11:10, 11:25-26

 Yohana Mtakatifu 14:1-6

 1 Wakorintho Sura ya 13 yote

 Ufunuo Sura ya 21 yote

22-0109 Hii Ndiyo Ishara Ya Mwisho, Bwana?

Ujume: 62-1230E Hii Ndiyo Ishara Ya Mwisho, Bwana?

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Hekalu la Mungu,

 Ujumbe huu hauna kikomo katika nguvu. Wenyewe Ni Mkamilifu ndani yake.  Ni Neno la mwisho juu ya mambo yote.  Hakuna kitu kingine kwa Bibi-arusi ila ile Sauti ambayo imerekodiwa kwenye kanda.  Ni Ujumbe wa Mungu uliothibitishwa wa wakati huu.  Ni Yakini yetu.

 Tuko safarini mwetu kuelekea Nchi ya Ahadi, tukiongozwa na Roho Mtakatifu, Nguzo ya Moto.  Chakula chetu cha Kiroho kimehifadhiwa ili kutuhifadhi  katika safari yetu.  Yote tunayohitaji yametolewa.

 Daudi alitayarisha kwa wingi kabla ya kifo chake vitu vyote vilivyohitajika ili kujenga nyumba ya Bwana .  Aliamuru kwamba lazima iwe ya ukuu kupindukia, ya umaarufu, na ya utukufu, katika nchi zote.

 Kisha akazungumza na Sulemani, na kumpa yote ambayo alikuwa ametayarisha kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu la Bwana.  Akampa mfano wa ukumbi, na nyumba zake, wa hazina, na vyumba vya juu, na vyumba vya ndani, na mahali pa kiti cha rehema.

 Akampa kielelezo cha vyote alivyokuwa navyo kwa roho, vya nyua za nyumba ya Bwana.  Vyumba vyote vilivyozunguka pande zote, hazina za nyumba ya Mungu, na hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.

 zamu za makuhani na Walawi, na kwa ajili ya kazi yote ya utumishi wa nyumba ya Bwana.  Pia akampa vyombo vyote vya utumishi katika nyumba ya Bwana .  Dhahabu na fedha kwa vyombo vyote vya huduma za kila namna.  Uzani wa dhahabu na fedha kwa kila kinara.  dhahabu na fedha kwa kila meza ya mikate ya wonyesho, ndoana, mabakuli, vikombe na mabakuli.

 kwa ajili ya madhabahu ya uvumba, dhahabu safi kwa uzani;  na dhahabu kwa mfano wa gari la makerubi, walionyosha mabawa yao, na kulifunika sanduku la agano la BWANA.

 Yote yalikuwa yametayarishwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya jengo hilo.  Hakukuwa na chochote kilichopungua.  Ni lazima afuate Ramani kwa usahihi  kulijenga Hekalu la Bwana.

 Lakini katika wakati wetu, Mungu anajenga Hekalu lingine, Bibi-arusi Wake.  Hekalu hili halitaharibiwa, bali litaishi Milele pamoja Naye.  Ametayarisha na kuhifadhi kwa wingi kwa kila kitu kinachohitajika ili kujenga Hekalu Lake jipya.

 Uungu, Uzao wa Nyoka, Majuma Sabini ya Danieli, Nyakati Saba za Kanisa, Mihuri Saba, Kutambua Siku Yako, Ndoa na Talaka, Kufunuliwa Kwa Mungu, Ile Ishara, Yakini, Watiwa-Mafuta, Chakula cha Kiroho, Kristo ni Siri, na mamia na mamia zaidi .  ambazo lazima zifuatwe kwa usahihi .

 Amehifadhi kila kitu tunachohitaji, lakini ni lazima tufuate Ramani kwa usahihi, bila kubadilisha yodi moja au nukta moja.

 Sasa, huku ni, jambo ninalonena asubuhi hii, ni kuhifadhi Chakula, kuhifadhi Chakula, ili kwamba mpate kitu cha kula, ili kwamba mpate kitu cha kufanyia karamu. Kiwekeni Hicho kwenye kanda zenu; mkaziweke katika chumba chenye baridi. Pengine wakati mrefu baada ya kuondoka kwangu, mngali mtakumbuka mambo haya ni kweli. Ketini chumbani mwenu mkazisikize. Mnaona? Na hiki ni Chakula, kihifadhini Hicho katika ghala.

 Alisema katika maskani huhisi kama nyumbani kwake kuliko mahali pengine popote.  Palikuwa ni Mahali ambapo Chakula kilihifadhiwa.

 Kule nje kwenye mikutano ninakoenda, hamnisikii nikihubiri Jumbe hizi. La, niliwaahidi, kuja kwenye Maskani hii. Papa hapa ndipo mimi huhubiria jumbe zangu. Nina tatu ama nne zaidi hapa, ambazo Bwana amenipa mimi, nina Maandiko juu yake, ambayo nisingethubutu kuhubiri mahali pengine po pote ila papa hapa. Hapa ndipo Neno la Mungu lilipoanzia. Na, hata Mungu atakapolibadili, ninakaa papa hapa na kuutoa papa hapa. Hiyo ni kweli.

 Nabii wa Bwana alinena na kusema kulikuwa na kundi la watu wanaomwamini, na walio na njaa na kushikilia kila neno alilosema. Ninyi ndilo kundi hilo la watu. Ninyi ndilo kusanyiko lake.  Ninyi ndilo hilo kundi lake dogo.

 Nimekuwa katika maombi na kuhisi Bwana anatuongoza kufuata Jumbe alizoziweka kwa wingi nabii Wake katika ghala Lake ili kumjenga Bibi-arusi Wake.

 Tutaendelea kumfuata nabii Wake tunaposikiliza:  Hii ​​Ndiyo Ishara ya Mwisho, Bwana?  62-1230E .  Ningependa kukualika uungane nasi Jumapili saa 4:00 nne Asubuhi ., saa za Jeffersonville,( ni saa 12:00 kumi na mbili jioni ya Tanzania), kusikia Chakula hiki kilichotayarishwa na kuhifadhiwa maalum ambacho kitakujenga ndani ya Hekalu la Bwana.

  “ Wakati umekwisha .” Kama ndivyo ilivyo, hebu na tujiandae, marafiki, kumlaki Mungu wetu. Kumekwisha wekwa chakula kingi sana sasa; hebu na tukitumie. Hebu na tukitumie sasa.

 Ndugu.  Joseph Branham

22-0102 Yakini

Ujume: 62-1230m Yakini

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi arusi wa Ujumbe wa Mtu Mmoja,

 Huu Umekuwa mwaka Mkuu jinsi gani kwa Bibi-arusi.  Ametuunganisha kutoka ulimwenguni kote kwa kitu pekee kinachoweza kuleta Bibi-arusi Wake pamoja, Ujumbe wa wakati huu, Sauti yenyewe ya Mungu ikimwita Bibi-arusi Wake atoke .

 Na sasa, naamini uko tayari kugonga kilele kile cha mwisho kule kuleta imani ambayo italinyakua Kanisa hata Utukufuni; na lipo katika hizo Jumbe!

 Ufunuo wa Ujumbe huu sasa umetia nanga ndani kabisa ya mioyo yetu.  Matendo yetu yanaambatana kabisa na Neno.  Tunajua fundisho letu ni kamilifu na Neno, haliongezi chochote Kwake wala kuondoa lolote Kwake.  Kwetu sisi, si kingine ila Neno kwenye kanda.

 Amekuwa akitutayarisha kwa ajili ya kilele cha mwisho kwa kutupa Imani tunayohitaji kwa ajili ya Unyakuo.  Imani hiyo, iko ndani yetu SASA.  Uhai wa Kristo umezalishwa karibu katika njia ya kufanyika mwili, kupitia sisi, kama ilivyokuwa ndani ya Kristo.

 Tunaweza kuona maisha yake.  “Kazi nizifanyazo mimi nanyi mtazifanya, yeye aaminiye.”  Si yeye ajifanyaye anaamini, si yeye ajidhaniaye kuwa anaamini, bali, “Yeye aaminiye.”  “Yeye aniaminiye Mimi, kazi nizifanyazo Mimi yeye naye atazifanya.”  Kwa nini?  Ametiwa nanga kwenye Mwamba uleule.  Mwamba ulikuwa nini?  Neno, daima.  Umetiwa nanga hapo.  Ni Nyota yako ya kaskazini unapopotea baharini .

 Tumetia nanga sana kwenye Mwamba huo.  Tuna hakika nalo.  Tumeyakinika nalo.  Hatuchukui Neno la mtu mwingine, tunadumu na Bwana Asema hivi.  Tumekuja kwenye Yakini Yetu.

 Tumeridhika kabisa na tumetosheka. Hakuna kushangaa tena kama ilivyokuwa katika siku za Waamuzi, na kwa walio wengi sana leo, ambapo kila mtu alifanya lililo sawa machoni pake mwenyewe, ambapo kila mtu alikuwa na yakini yake mwenyewe na kufanya yale tu aliyotaka kufanya.  Mungu habadilishi kanuni zake, hawezi na awe Mungu.  Ikiwa Mungu atawahi kusema lolote au kufanya jambo lolote, ni lazima afanye vivyo hivyo kila wakati.

 Mungu daima hutuma nabii kuwaongoza watu wake.  Alitutumia Nabii Wake malaika wa 7 ;  Mwana wa Adamu akijifunua Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu, kumwita Bibi-arusi Wake atoke na kumwongoza .  Kanda ni Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi Wake.  HIYO NDIO YAKINI YETU.

 Akapanda akaenda kule…Alijua…Nami napenda hilo, jinsi alivyokuja; alifikia kwenye yakini yake, nguzo yake ya kujishikilia.

 Mungu anamwita Bibi-arusi Wake pamoja. Yeye Hatabadilisha mpango Wake. Yeye Hatatuma kundi la watu kumkusanya Bibi-arusi Wake.  Bibi-arusi Wake ataungana tu kwenye Neno safi, hiyo ni Sauti ya Mungu kwenye hizo Kanda.  Ni huduma ya kweli ya Mungu kwa ajili  ya siku hii .

Hakuna njia bora ya kuanza Mwaka Mpya kuliko kukusanyika pamoja na kusikia nguzo yetu yakushikilia , Yakini yetu, ikizungumza nasi. Ningependa kuwaalika kila mmoja kuja kusikiliza pamoja nasi Jumapili saa 4:00 nne Asubuhi ., saa za Jeffersonville,( ni Saa kumi na mbili jioni ya Tanzania), ili kusikia Ujumbe: Yakini 62-1230M.

 Kama hamwezi kuungana nasi, ninawatia moyo kuchagua Ujumbe wa kucheza katika nyumba zenu, au mtie moyo mchungaji wenu kuchagua Ujumbe ambao ninyi pia mnaweza kuketi  pamoja, chini ya upako huu mkuu uliopo, na kusikia yakini ya Bibi-arusi iliyothibitishwa.

 Ndugu.  Joseph Branham