All posts by admin5

22-1009 Maswali na Majibu #2

UJUMBE: 64-0823E Maswali na Majibu #2

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bikira Safi aliyeposwa,

Mungu anatupenda sana hata akamfanya nabii wake ajibu maswali yetu YOTE, na akaweka majibu kwenye kanda. Wakati Tunapoyahitaji, yote tunayopaswa kufanya ni KUAMINI NA KUBONYEZA PLAY.

Je, ninaye Roho Mtakatifu?

Ishara ya Roho Mtakatifu, Mungu anapokufunulia na unaliona, BWANA ASEMA HIVI na kulikubali.

Basi ninaye Bwana, ulivyonifunulia Ujumbe huu na nimeukubali kama Bwana Asema Hivi !

Lakini, inaonekana kama ninakosea sana…na vipi kuhusu maisha yangu ya nyuma?

Si vile ulivyo, vile ulivyokuwa, au lo lote lile, ni yale Mungu amekufanyia wewe sasa. Hiyo ndiyo ishara.

Bwana, huyaoni maisha yangu ya nyuma na hata huyaoni makosa yangu mengi, mengi sasa, Unasikia sauti yangu tu; Utukufu Bwana, NINAYE ROHO MTAKATIFU.

Ndugu Branham, najua ulisema wewe siye changarawe pekee pwani, lakini ni nani atakayekuwa akimuongoza Bibi-arusi wa Kristo katika wakati wa mwisho?

Kwa msaada wa Mungu, naamini kuwa ninamuongoza Bibi-arusi wa Yesu Kristo.

Nina mambo mengi moyoni mwangu, nifanye nini?

Hakuna kilicho muhimu sasa ila kuwakusanya watoto wote wa Mungu pamoja na kusema, “Haya twendeni.”

Asante Bwana, tunafanya hivyo tu. Hakuna kitu kingine kilicho muhimu kwetu ila Neno Lako. Roho Wako Mtakatifu anatuongoza kupitia nabii Wako na tunakusanyika kulizunguka Neno Lako kutoka ulimwenguni kote, nasi tuko tayari Kwenda.

Nina maswali mengi, ninahitaji mwongozo, msaada, na majibu. Nitayapata wapi hayo?

Niko hapa kujaribu kuwasaidia, kwa sababu nawapenda. Ninyi ni watoto wangu niliomzalia Kristo. Nadai kila mmoja wenu. Nadai ninyi usiku huu; nadai ninyi wakati wote; mimi kila mara huwadai ninyi kisha—kama ndugu yangu na dada.

Tunakupenda pia Ndugu Branham. Tunajua Mungu alikutuma utuongoze na kutuelekeza. Tumelichunguza kwa Neno nalo linajipanga kikamilifu.

Ni nani Aliye Baba yangu katika Injili?

Ninyi ni watoto wangu; mi—mimi ni baba yenu katika Injili, si baba kama vile kasisi angalikuwa, mimi—mimi ni baba yenu katika Injili kama Paulo alivyosema pale.

Tunajua ni Roho Mtakatifu akuongozaye wewe kutuongoza, Ndugu Branham. Unasema kama vile tu Paulo alivyosema katika Biblia, kufuata hasa kabisa yale uliyosema, kwa kuwa ni Kweli, nasi hatupaswi kubadili yodi moja au nukta moja.

Utafanya nini Ndugu Branham?

Nimewazaa ninyi kwa Kristo, na sasa na—nawaposea ninyi Kristo; hilo ni kufanya ninyi muweke nadhiri ya ndoa kwa Kristo kama bikira wasafi. Msiniaibishe! Msiniaibishe! Ninyi iweni bikira safi.

Umetuposa sisi kwa Kristo kama mabikira kwa Neno Lake. Hatuwezi, na hata hatutavutiwa na mwingine. Tunakagua kila kitu tunachosikia na tunachofanya kwa Neno Lako lililohifadhiwa.

Je, ni jambo gani muhimu zaidi ninaloweza kufanya ili kuwa Bibi-arusi Wake, Ndugu Branham?

Kaa moja kwa moja na Neno.

Majibu yote kwa maswali yetu yanaweza kufupishwa kwa maneno haya:

KAA MOJA KWA MOJA NA NENO.

Ujumbe huu NI Neno la wakati wetu. Ndugu Branham ndiye Sauti ya Mungu kwa Wakati wetu. Kila kitu lazima kiendane na Neno. Neno halihitaji Kufasiriwa kwokwote. TUNAPOBONYEZA PLAY, YOTE TUNAYOHITAJI YANATOLEWA HAPO, KWENYE HIZO KANDA.

Je, Una jambo fulani moyoni mwako unalohitaji jibu? Njoo uungane nasi Jumapili
saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania) tunapopata majibu yetu yote tunaposikia : 64-0823E – Maswali Na Majibu #2.

Ndugu. Joseph Branham

22-1002 Maswali na Majibu #1

UJUMBE: 64-0823M Maswali na Majibu #1

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Maskani ya Branham,

Kama hamwezi kuja hapa maskanini, tafuteni kanisa fulani mahali fulani; enendeni kwalo. Ikiwa huwezi kuzisikiliza kanda pamoja nasi, Zisikiliza kanda mahali fulani. Kucheza na kuzisikiliza Kanda ndilo jambo muhimu zaidi ambalo mhubiri, mwalimu, mtume, nabii, mwinjilisti au wewe unaloweza kufanya.

Hiki ndicho kituo changu cha nyumbani; haya ndiyo makao yangu makuu; hapa ndipo tumeimarika. Sasa, shikilia hilo mawazoni haijalishi itakuwaje. Sasa, kama mna busara, mtashika jambo fulani. Haijalishi itakuwaje, haya ndiyo makao yetu makuu, papa hapa! Na wekeni hilo mawazoni na mrejee kwenye kanda hii siku fulani, ambamo mlinisikia nikifanya unabii. Vema, kumbukeni hayo.

Nabii alikuwa akifanya nini? Akihifadhi Chakula. Akihifadhi Chakula ili kwamba tupate Kitu cha kula, ili kwamba tupate Kitu cha kufanyia karamu. Tumekiweka hicho kwenye kanda zetu tumeziweka katika chumba chetu chenye Baridi.

Alisema kulikuwa na ghala moja tu ndogo katika nchi hii yote , ghala moja ndogo. Aliweka tu Akiba nyingi ; Ile Ishara, Yakini, Mihuri, Nyakati Saba za Kanisa, Makao ya Baadaye ,kuthibitisha Neno Lake, yote kwa ajili yetu, kwa hiyo tungekaa hapa tu na kusikiliza Atakapokuwa ameondoka.

Yaonekana yuko mbali sana, lakini bado tunakumbuka, mambo haya ni kweli. Haya ni maisha ambayo yatubidi kutembea peke yetu.

Ghala ZIMEJAA . Hakuna Chakula kingine ambacho kimethibitishwa na Mungu mwenyewe kuwa ni NENO SAFI ambalo halijavunda.

Ikiwa ungependa kufanya karamu pamoja nasi, tunakukaribisha uungane nasi, Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA . Saa za Jeffersonville (Ni saa 1:00 jioni ya Tanzania) tunapokuja Mezani na kula kama wageni Wake.

Maswali na Majibu 64-0823M

Ndugu. Joseph Branham

22-0925 Kuthibitisha Neno Lake

UJUMBE: 64-0816 Kuthibitisha Neno Lake

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Chumvi ya Dunia ,

Wakati tu inaonekana kana kwamba haiwezi kuwa bora zaidi, Yeye anatupa Mzigo mwingine wa Kanda wa mafunuo. Tuna uwakilisho kwa kuchaguliwa tangu awali. Hiyo ndiyo sababu tunatoka mashariki na magharibi, kaskazini na kusini, ili kusikia Neno lililo hai likidhihirishwa.

Mungu alipoumba ulimwengu, tulikuwa katika mawazo yake. Wakati mshitaki wetu anapoendelea kutunyooshea kidole na kumwambia Baba, “walifanya hivi, walifanya hivi, walifanya hivi,” Damu ya Bwana wetu Yesu inatufunika. Tunapoomba, Mungu hatuoni, Yeye husikia tu sauti zetu kupitia Damu ya Yesu.

Shetani hawezi kusumbua; ama, anaweza kukujaribu, bali hawezi kumpata Mkristo aliyezaliwa mara ya pili. Kwa maana, Mungu, tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, alitangulia kumwona, na akamtuma Yesu kumkomboa, nayo ile Damu inanena kwa niaba yake. Anawezaje kufanya dhambi wakati, hata, haiwezi kuonekana na Mungu? Yeye hata haninii…Kitu pekee anachosikia ni sauti yako. Yeye huona uwakilisho wako. Amina! Hiyo ni kweli. Mnaona?

Nabii wa Mungu alituambia mambo haya. Hakuwa yeye aliyekuwa Akinena ; alionyesha tu mawazo ya Mungu, sifa Zake za mambo ambayo hayana budi kutendeka . Anatumia mdomo wake kuyaeleza. Na baada ya yeye kuyaeleza ,  lazima yatimie . “Mbingu na nchi zitapita, bali Neno Langu halitashindwa kamwe.”

Amethibitisha Neno Lake kwetu tena na tena. Je, hajatuthibitishia kuwa: Mwana wa Adamu aliyefanyika mwili kati yetu? Je! hajatuthibitishia: Nabii wetu anatimiza kila andiko linalomuhusu ? Je, hajatuthibitishia: Sisi ni Bibi-arusi Wake? Je, hajatuthibitishia: Tunao ushahidi wa kweli wa Roho Mtakatifu?

Tuna wasiwasi wa nini basi? Ametuthibitishia, ikiwa tutamshindania Naye, Atatushindania . Neno Lake haliwezi kushindwa kamwe.

Wote wanaoamini Ujumbe huu na mjumbe wa wakati huu wataokolewa. Wote wasiouamini Ujumbe na Mjumbe, wataangamia pamoja na ulimwengu .

Sikilizeni kwa makini enyi kanisa. Wengi sana hawaelewi, ama hawana Ufunuo wa Neno. Wanahisi tunamtukuza sana mtu huyu. Ikiwa kweli unaamini Ndugu Branham ni nabii wa Mungu, basi fungua moyo wako na nafsi yako na usikilize kile isemacho Bwana Asema Hivi .

Ni kitu gani kitakachomleta Bibi-arusi pamoja? Ni nini kitakachomuunganisha Bibi-arusi kuwa Mmoja na Mungu?

“ Katika siku hiyo Mwana wa Adamu atafunuliwa.” Nini? Kuliunganisha Kanisa kwa kile Kichwa, kuliunganisha, arusi ya Bibi-arusi. Wito wa Bwana Arusi utakuja hapa , wakati Mwana wa Adamu atakaposhuka aje katika mwili wa mwanadamu kuunganisha hivyo viwili pamoja. Kanisa halina budi kuwa Neno, Yeye ni Neno, na hivyo viwili vitaungana pamoja, na kufanya hivyo, itachukua dhihirisho la kufunuliwa kwa Mwana wa Adamu.

Itachukua dhihirisho la kufunuliwa kwa Mwana wa Adamu. Si wazo lako, si uelewa wako, si mawazo yako wala mahubiri yako. Mwana wa Adamu atamuunganisha Bibi-arusi pamoja na Bwana-arusi, nalo linatendeka HIVI SASA .

Hivi sasa tuko kwenye Karamu ya Harusi na Bwana Harusi na hivi karibuni tutaondoka kwenda kwenye Karamu yetu ya Arusi na Fungate.

Neno na Kanisa wanakuwa mmoja. Lo lote afanyalo Mwana wa Adamu, Yeye alikuwa Neno, Kanisa linafanya jambo lile lile .

Tunaweza tu kuishi kwa kila Neno litokalo katika Kinywa cha Mungu! Mungu amethibitisha kwamba nabii wetu ndiye Mnenaji wa Mungu kwa ajili ya wakati huu. Tunajuaje kuwa ni Neno la Mungu? Yeye amesema hivyo, ndipo akalithibitisha kwa Neno Lake.

Sisi ndio Kanisa-Bibi-arusi Aliye tayari katika siku za mwisho. Aliyeitwa kutoka katika mengine yote; yule ndege mwenye madoadoa kwa Damu Yake.

Baba, mioyo yetu inarukaruka, na moyo wangu unapigapiga, ninapowazia hayo na kujua ya kwamba maneno yako ni kweli, hamna hata moja linaloweza kushindwa .

Hii ndiyo njia pekee iliyoandaliwa na Mungu kwa siku hii. Ndiyo njia PEKEE ya kutobadilisha Neno moja. Kumbuka, Roho Mtakatifu anaweza kuja na kumtia mtu mafuta, na bado ni nje ya Mapenzi ya Mungu. NI LAZIMA TUDUMU NA NENO LA ASALI LILILOLITHIBITISHWA.

Ikiwa ungependa kudumu na Neno hilo na kusikia Sauti ya Mungu pamoja nasi, ninakualika uungane nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville,(ni Saa 1 :00 MOJA JIONI Ya Tanzania),tunaposikia: Kuthibitisha Neno Lake  64-0816 .

Si lazima uungane nasi au hata kusikia kanda ile ile kwa wakati mmoja pamoja nasi, lakini ninakusihi, msikie nabii wa Mungu.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Mathayo Mt 24:24

Marko Mt 5:21-43 / 16:15

Luka Mt 17:30 / 24:49

Yohana Mt 1:1 / 5:19 / 14:12

Warumi 4:20-22

I Wathesalonike 5:21

Waebrania 4:12-16 / 6:4-6 /13:8

1 Wafalme 10:1-3

Yoeli 2:28

Isaya 9:6

Malaki 4

22-0918 Makao Ya Baadaye Ya Bwana Arusi Wa Mbinguni Na Bibi-Arusi Wa Duniani

UJUMBE: 64-0802 Makao Ya Baadaye Ya Bwana Arusi Wa Mbinguni Na Bibi-Arusi Wa Duniani

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Rafiki wapendwa kwa Nabii ,

Moyo wangu unabubujika kwa furaha ninapowazia kuhusu sisi kukusanyika pamoja Jumapili hii ili kusikia Sauti ya Mungu ikisema nasi. Hakuna furaha kubwa maishani mwangu kuliko kuwa katika uwepo wa Roho Mtakatifu na kumsikia akisema na Bibi-arusi Wake, mdomo kwa sikio.

Hakuna kitu kingine katika ulimwengu huu kinachonipa furaha na amani, ila Neno Lake. Ninaposikia tu, “Habari za Asubuhi Marafiki,” mimi huketi tu, nikastarehe, na kunywa kutoka kwenye Kisima hicho kinachofoka maji kikiniambia Maneno ya Uzima wa Milele. Kuwazia, Mungu alimtuma kwangu MIMI NA WEWE, nasi ni MARAFIKI wa nabii wa Mungu na mjumbe.

Anatupenda sana hivi kwamba Alimtuma nabii Wake atuambie yote yahusuyo Makao yetu ya Baadaye. Alifurahishwa sana kutuambia yote yahusuyo hilo, hata kwa undani zaidi kuliko alivyoambiwa Yohana. Ametufunulia, Si mji wenye umbo la mraba, bali ni mji wenye umbo la piramidi, ambako Mwana-Kondoo atakuwa juu yake na Nuru ya ulimwengu.

Anatujulisha barabara zitajengwa kwa dhahabu na nyumba tutakazoishi zitakuwa za dhahabu safi sana. Yeye anaweka kila kitu kidogo jinsi tunavyopenda hasa, jinsi tungetaka tu. Hajaacha kitu chochote. Mjenzi wa Kiungu ameubuni kwa ajili yetu SISI, Mpendwa wake.

Miti ya Uzima itakuwako kule, nayo itazaa aina kumi na mbili za matunda. Na hayo Malango ya mji hayatafungwa usiku, kwa maana hakuna usiku kule, Yeye atakuwa ndiye Nuru yetu.

Ni nani atakayekuwa kule?

Ni akina nani waliokuja kwenye nchi mpya pamoja na nabii Nuhu? Hao walioingia pamoja naye safinani. Hiyo ni kweli? Hao ndio wanaotoka na kutembea mle. Mnaona? Hao walioingia pamoja na Nuhu, kwa ujumbe wake, hao ndio waliotoka wakatembea juu ya nchi mpya baada ya ubatizo wake wa maji .

Anazungumza kuhusu SISI marafiki zangu! Tuko ndani ya Safina yetu ya siku hii; Neno Lake, Ujumbe Huu, pamoja na Nuhu wetu Nabii . Na huko ng’ambo katika Nchi hiyo, Mji ule ambako Mwana-Kondoo ndiye Nuru, yeye atatujua SISI. Sisi ni watu wake, vito katika taji yake. Tumetoka Mashariki na Magharibi, kuja kwenye mji uliojengwa mraba. Mji ule ambao Ibrahimu alikuwa anautafuta.

Huku nikiona Neno likijidhihirisha Lenyewe , ninajua, bila shaka hata kidogo, vito vya taji yangu vitang’aa kuliko kitu cho chote kile ulimwenguni, katika Siku ile.

Je! twaweza hata kuanza kuwazia… Nabii wa Mungu alisema, ALIJUA, bila shaka hata kidogo , ya kwamba SISI ni vito vya taji yake, na tutang’aa kuliko kitu chochote kile ulimwenguni katika siku ile . Haleluya… Utukufu…Jina la Bwana lisifiwe.

Marafiki, kama tunafikiri ni la ajabu, tukiketi pamoja kutoka kote ulimwenguni, tukisikiliza na kula Neno Lake katika kanda hizi, itakuwaje tutakapoishi katika mji ule pamoja Naye!

Nabii wa Mungu atakuwa jirani yetu wa karibu, na tutakapokula hiyo miti, na tutakapotembea kwenye barabara hizo, tutakapotembea kwenye barabara hizo za dhahabu kwenye chemchemi, kunywa kutoka kwenye chemchemi, kutembea katika paradiso za Mungu, huku Malaika wanarukaruka kuizunguka dunia, wakiimba nyimbo za sifa.

Loo, itakuwa ni Siku ya namna gani! Inastahili kwa vyote. Njia inaonekana inaparuza, wakati mwingine inakuwa ngumu, lakini, loo! itakuwa kitu kidogo sana nitakapomwona Yeye, kidogo sana. Vipi yale majina mabaya na mambo ambayo wao wamesema, hayo yatakuwa nini nitakapomwona Yeye katika Mji ule mzuri, mzuri sana wa Mungu?

Marafiki, siwezi kusubiri kuona, na kuwa katika mji ule. Ninatamani kuwa kule pamoja na Bwana na Mwokozi wetu, nabii Wake, na pamoja na kila mmoja wenu.

Ninaelekea kwenye Mji ule mzuri
Bwana wangu ameuandaa kwa walio Wake ;
Wakati wote Waliokombolewa wa nyakati zote Wataimba “Utukufu!”
Wakikizunguka Kiti Cheupe cha Enzi
Wakati mwingine ninatamani Mbinguni sana, Na utukufu nitakaouona kule
Itakuwa ni furaha jinsi gani nitakapomwona Mwokozi wangu ,
Katika Mji ule mzuri wa dhahabu!

Ninaualika ulimwengu uje kuungana na sisi, marafiki wa nabii, tunapokusanyika kukizunguka Kiti Chake cha Enzi ili kusikia Sauti ya Mungu ikisema nasi saa 6:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville,( ni Saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania) tunapomsikia Yeye akituambia yote kuhusu : Makao Ya Baadaye ya Bwana Arusi wa Mbinguni na Bibi-arusi wa Duniani 64-0802 . Naweza kukuahidi, itakuwa Sikukuu katika maisha yako.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe :

Mathayo Mt. 19:28

Yohana Mt. 14:1-3

Waefeso 1:10

2 Petro 2:5-6 / Sura ya 3 yote

Ufunuo 2:7 / 6:14 / 21: 1-14

Mambo ya Walawi 23:36

Isaya Sura ya 4 yote / 28:10 / 65:17-25

Malaki 3:6

22-0911 Mabirika Yavujayo

UJUMBE: 64-0726E Mabirika Yavujayo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wanywaji wa Maji ya Kisima Kinachofoka Maji.

Hatukupandikizwa, sisi ni sehemu ya uzao asili wa Neno. Roho Mtakatifu Mwenyewe, ameivisha, amethibitisha, na kujidhihirisha Mwenyewe kwetu. Tumelikubali kwa utimilifu Wake, kwa uwezo wa thibitisho lake na Ufunuo wa kile lilicho, nasi tumekuwa sehemu Yake. Ni zaidi ya uhai kwetu.

Roho Mtakatifu Mwenyewe alinena kupitia chombo kinyenyekevu, kisichostahili na kusema, “Hii hapa Fimbo Yangu ya kifalme , Neno Langu, lichukue, uende zako, na uupeleke Ujumbe.” Alichukua Neno Lake na kutubangua, kutufanya kuwa Bibi-arusi Wake.

Imewasumbua makasisi kuona watu wakitoka makanisani na kwenda kucheza kanda. Walisema, “Ikiwa yeyote wenu atahudhuria hiyo mikutano, utatupwa nje , tutakuweka nje ya shirika letu”.

Jibu lao ni: Mnaweza pia kutuachilia, tutaendelea hata hivyo! Tuko safarini pamoja na Bwana Yesu, Mwamba wetu uliopigwa, tukila Chakula cha malaika, mana iliyohifadhiwa ghalani kutoka juu, na kunywa kutoka kwenye Mwamba huo. Hatupaswi kamwe kuhangaikia kile tunachokunywa, Si chochote ila NENO SAFI.

Daima tumekuwa na uamsho unaoendelea. Chemchemi yetu daima inabubujika tena na tena, na tena na tena. Hakuna mwisho wake.
Tunapata kinywaji safi na baridi cha maji kila tunapobonyeza Play. Tunakitegemea na tunaishi kwacho. Jambo likupasalo kufanya tu ni kwenda kule na Unywe.

Tunaishi kwa chemchemi hiyo kila siku! Haitubidi kuvuta, kuchimba, kuvuta kwa mashine, au chochote kile; tunashiriki tu katika njia aliyoiandaa yeye , bure . Unaweza kuchukua taratibu zako zote zakujitengenezea unazotaka, visima vyako vyote vya kale vya maji yanayooza; kwetu sisi, tumekuja kwenye Chemchemi yake safi. Ni Furaha yetu. Ni Nuru na Nguvu zetu.

Yeye ndiye furaha yangu. Yeye ndiye Nuru yangu. Yeye ni—Yeye ni nguvu zangu. Yeye ni Maji yangu. Yeye ni Uzima wangu. Yeye ni Mponya wangu. Yeye ni Mwokozi wangu. Yeye ni Mfalme wangu. Kila ninachohitaji kinapatikana Kwake. Kwa nini niwe na hamu ya kukiendea kitu kingine?

Kwetu sisi hakuna mahali pengine pa kwenda ila moja kwa moja kwenye Chemchemi iliyotolewa na Mungu. Hatuna hofu kamwe tutakunywa nini. Haitulazimu kuweka kitambaa cha kale cha kuchujia ambacho kinaweza kutoa vitu vikubwa, lakini huacha juisi mbaya. TUNAPATA TU MAJI SAFI YA KISIMA KINACHOFOKA MAJI YENYE MADINI NA VIRUTUBISHO VYOTE TUNAVYOHITAJI.

Ametuhakikishia: Watoto wangu wachanga , msiwe na wasiwasi tena, mnao ushahidi wa kweli wa Roho Mtakatifu. Mmenithibitishia Mimi ya kwamba mnaamini kila Neno. Mmelipokea, NINYI NI WANGU. SISI NI KITU KIMOJA. MUME NA MKE.

Ninakuja kwa ajili yenu katika muda mfupi, katika kufumba na kufumbua jicho. Ninawaandalia Makao mapya. Mtapenda jinsi nilivyoyafanya.
Najua ni ngumu sana kwenu sasa, na mna mitihani mingi na majaribu na mizigo yenu ni mizito. Lakini msisahau, hamna chochote cha kuhofia , Nimewapa Neno Langu. Ninyi ni Neno Langu . Tayari nimefanya kila kitu kwa ajili yenu. Nena Neno na msiwe na shaka. Mnayo Imani yenu, pamoja na nabii Wangu aliwapa Imani yake.

Ningependa uungane nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, ( Ni saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania) kusikia 64-0726E Mabirika Yavujayo , na kunywa kutoka kwenye Chemchemi hii inayofoka maji inapobubujisha Neno Safi ambalo halihitaji chujio.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza ibada

Zaburi 36:9
Yeremia 2:12-13
Yohana Mtakatifu 3:16
Ufunuo Sura ya 13 yote.

22-0904 Kutambua Siku Yako Na Ujumbe Wake

UJUMBE: 64-0726M Kutambua Siku Yako Na Ujumbe Wake

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Waliokatwa Watoke,

Nataka kila mtu ajue kwanini tunafuraha sana jinsi hii!!

Tumelikubali Neno la Bwana. Neno lililofunuliwa lililonenwa, na nabii wa Mungu wa Malaki 4. Sisi ni Bibi-arusi wa Yesu Kristo. Sisi Ndio ambao tumedumu waaminifu kwa Sauti Yake iliyothibitishwa. Sisi ndio ambao Aliyowapa Lulu ya thamani kuu, Ufunuo wa kweli wa Ujumbe Wake na mjumbe Wake.

Mungu amechukua Neno la nabii Wake na kumbangua Bibi-arusi anayeamini kila nukta na kila yodi. Ametukata, kama alivyoahidi atafanya. Sisi ni kondoo wa Mungu, na tunaisikia tu Sauti ya Mungu! “Kondoo Wangu huisikia Sauti Yangu,” tunapobonyeza Play.

Tuna Washiriki kutoka kote nchini; kutoka New York, kutoka Massachusetts, hadi Boston, Maine, Tennessee, Georgia, Alabama, na kote nchini. Kutoka Afrika hadi Mexico, Ulaya hadi Australia, tunakusanyika pamoja, chini ya Ujumbe Mmoja, Sauti Moja, nayo inamuunganisha Bibi-arusi kwa ajili ya Kunyakuliwa.

Nabii wetu, mjumbe wa Mungu, Mwana wa Adamu akijifunua Mwenyewe katika mwili, anapaza sauti, “Shetani, ondoka njiani, nina Ujumbe wa Mfalme. Mimi ni Mjumbe wa Mfalme. Nina Neno lililothibitishwa la siku hii. Nimekusudiwa kumwita Bibi-arusi Wake atoke na Kumwongoza.”

“Ninajaribu kuwavuta watu fulani, kuwakata niwaondoe kwenye mambo haya. kuwavuta watoke; kuwaonyesha, kwa Maandiko, ya kwamba Mungu amesimama hapa; pamoja na thibitisho la Nguzo ya Moto”

Mungu ametambua ya kwamba kuna watu fulani ulimwenguni ambao aliwakusudia Uzima. Alitambua ulikuwa ni wakati wa kumtuma mjumbe Wake kumwita Bibi-arusi Wake atoke, Hivyo Yeye Akamtuma . Sisi Ndio wale Waliotambua jambo hilo. Sisi ndio wale Aliojua tungeamini kila Neno.

Ibrahimu alitambua ya kwamba Mungu alikuwa akisema naye katika mwili wa Kibinadamu. Alitambua ishara Yake na kumwita B-W-A-N-A, Elohim, na akabarikiwa na Bwana. Tumetambua ya kwamba kama ilivyokuwa katika siku hiyo, ndivyo itakavyokuwa wakati Mwana wa Adamu atakapodhihirishwa, Elohim, akinena katika mwili wa kibinadamu.

Sisi ni sehemu yake, na Mwanawe, na tutadumu naye milele. Si kwa wito wetu au uchaguzi wetu, bali kwa uchaguzi wake. Hatukuwa na uhusiano wowote nalo. Yeye ndiye aliyetuchagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Haidhuru utahubiri namna gani, hata ufanye nini, haliwezi kuivishwa, haliwezi kudhihirishwa, haliwezi kuthibitishwa; ila tu na Yeye aliyesema, “Mimi Ndimi Nuru ya ulimwengu,” lile Neno. Kwa hiyo hakuna budi kutokee Nguvu fu—fu—fulani, Roho Mtakatifu Mwenyewe, kuivisha, ama kuthibitisha, ama kuhakikisha, ama kudhihirisha ya kwamba yale ambayo Yeye amebashiri yangetukia katika siku hii. Nuru ya jioni inaleta hilo. Ni wakati wa jinsi gani!

Alituona katika lile ono tulipokuwa tukipita mbele yake. Tulipitia mahali pale pale alipopitia Bibi-arusi wakati alipopitia hapo mwanzo, Alfa na Omega. Alikuwa akiangalia wengine wakitoka mstarini, na alikuwa akijaribu kumvuta , lakini sisi ndio Wale tuliopaza Sauti, “Tunategemea jambo Hilo.”

Angalia, “Kama vile Yane na Yambre pia walivyompinga Musa,” yeye atakuja moja kwa moja, baadhi yao . Si , sasa, yeye hazungumzi kuhusu Mmethodisti, Mbaptisti, hapa; wao wako nje ya picha . Unaona? “Lakini kama vile Yane na Yambre walivyoshindana na Musa na Haruni, vivyo hivyo hao nao; watu walioharibikiwa na akili zao kuhusu ile Kweli.” wamepotoka wakaingia katika mafundisho ya sharti na mafundisho ya kanisa, badala ya Biblia.

Jinsi inavyotupasa kuwa waangalifu sana kudumu na Neno la kweli, lililothibitishwa la siku yetu. Ni lazima kila wakati tukumbuke na kutambua Neno humjia nani. Ni nani aliye mfasiri pekee wa kiungu wa Neno? Ni nani Aliye Neno la siku yetu ?

Roho wa Mungu, ambaye ni Neno la Mungu, “Neno Langu ni Roho na Uzima,” litamweka Bibi-arusi mahali Pake. Kwa maana, Yeye Atatambua nafasi yake katika Neno, ndipo anakuwa ndani ya Kristo, litamweka kwenye nafasi yake .

Umealikwa kuja kusikiliza Sauti pekee ya Mungu iliyothibitishwa ya siku yetu, na kutambua nafasi yako katika Neno na kuwekwa mahali pako tunapomsikia Elohim akisema kupitia nabii Wake na kutuletea Ujumbe: Kutambua Siku Yako na Ujumbe Wake 64-0726M , saa 06:00 MCHANA , saa za Jeffersonville (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania.)

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikia Ujumbe:

Hosea: Sura ya 6 yote

Ezekieli: Sura ya 37 yote

Malaki: 3:1 / 4:5-6

2 Timotheo: 3:1-9

Ufunuo: Sura ya 11 yote

Mungu, umba ufufuo ndani yangu! Jalia niwe huo ufufuo. Jalia kila mmoja wetu awe huo ufufuo, ufufuo ndani yangu. Nifanye mimi, Bwana, nipate njaa, nifanye nione kiu. Umba ndani yangu, Bwana, kile ambacho kinahitajika ndani yangu. Nijalie, tangu saa hii na kuendelea, niwe wako; mtumishi aliyewekwa wakfu zaidi, mtumishi bora, aliyebarikiwa zaidi na Wewe; mwenye uwezo zaidi, mnyenyekevu zaidi, mwema zaidi, mwenye kupenda kufanya kazi zaidi; mwenye kuangalia zaidi mambo ambayo ni ya kweli, na kusahau mambo yaliyo nyuma, na mambo yasiyo ya kujenga. Jalia nikaze mwendo kuelekea kwenye mede ya wito mkuu wa Kristo. Amina.

Rev. William Marrion Branham

22-0828 Kuenda Nje Ya Kambi

UJUMBE: 64-0719E Kuenda Nje Ya Kambi

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wana Tai ,

Hebu na tukusanyike pamoja Sote na kusikia Ujumbe 64-0719E Kwenda Nje ya Kambi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville. ( Ni saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania)

Ndugu Joseph Branham

22-0821 Sikukuu Ya Baragumu

UJUMBE: 64-0719M Sikukuu Ya Baragumu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Kubonyeza Play,

Kila Jumapili tunakusanyika na kusikiliza Huduma kuu iliyo hai katika historia ya ulimwengu. Tunapata wakati mtukufu zaidi tunapokutana pamoja ili kusikia Sauti ya Mungu! Ni Yesu, Mwana wa Mungu, akijifunua Mwenyewe kwa Maandiko, akilifanya andiko hilo ambalo limechaguliwa tangu zamani kwa ajili ya Siku siku hii, kama ilivyokuwa katika siku Yake, na siku Zingine zote, LIISHI. Na Kuamini Hilo, ndio Dhihirisho la kuwa una Roho Mtakatifu .

Dhihirisho la kweli la kuwa na Roho Mtakatifu sio ati kwenda kanisani kila Jumapili; Ni kwamba unaamini ya kwamba “Mimi Ndiye ,” Neno la Siku yako. Neno la Siku hii ni nini? Nabii wa Mungu ndiye Neno la Siku hii naye anapaswa kuwarudisha watu kwenye Neno, ili kwamba Bibi-arusi amjue Mumewe, amjue Mwenziwe, Neno lililofunuliwa.

Maisha yake mwenyewe, kazi zake mwenyewe, hufunua na kulithibitisha Neno la Siku hii.

Ni Roho Mtakatifu aliyerudi tena Kanisani; Kristo, Mwenyewe, aliyefunuliwa katika mwili wa mwanadamu, wakati wa jioni, kama tu alivyoahidi angefanya. Ninajua kwa namna fulani hilo linawakaba wao kidogo, lakini lazima usome katikati ya mistari na kuona, hiyo inafanya ile picha ije.

Sisi ni Uzao wa Kifalme wa Ibrahimu, Bibi-arusi. Ishara ya mwisho ambayo Ibrahimu aliwahi kuona kabla ya mwana aliyeahidiwa kuja ilikuwa ni nani? Mungu, katika umbo la mwanadamu, ambaye aliweza kuyatambua mawazo ya watu. Mtu mmoja, sio dazani, mtu mmoja.

Najua watu wengi hawakubaliani na jambo hilo, bali najua ndilo hili. Najua jambo hilo. Si kwa sababu ninasema mnalisema; kwa sababu, sikulitoa kwangu mimi. Ma—mawazo yangu si yangu mwenyewe . Cho chote kile kilichoniambia jambo hilo, kama kimekosea, basi kimekosea. Bali sisemi jambo hili kwa nafsi yangu, ninasema yale Mtu mwingine amesema. Mtu huyo mwingine ni Mungu aliyenena nasi na kufanya mambo haya yote ambayo amefanya, na akajitokeza, mnaona, kwa hiyo mimi najua ya kwamba ni kweli.

Tunasikiliza wazo lenyewe la Mungu; si mawazo ya mwanadamu, bali ya Mungu. Nabii wetu ndiye mfunuzi wa Neno lililoandikwa.

Tunaelewa kwamba kuzicheza kanda majumbani mwenu ama makanisani mwenu si kwa kila mtu, bali ni kwa ajili Yetu , Ndiyo NJIA PEKEE. Tunapenda kusikia Sauti ya Mungu ikizungumza nasi moja kwa moja. Hatuhitaji fasiri au ufafanuzi wowote; ni Mungu akisema Nasi mdomo kwa sikio .

Jumapili hii tutakuwa tukimsikia Mungu akisema na kutuambia jinsi alivyomwonyesha nabii wake sisi katika onyesho la awali ng’ambo ya pili. Jinsi Bibi-arusi huyo alivyokuwa akimtazama yeye moja kwa moja, akizungumza naye, nasi tulikuwa tumesimama pamoja naye. Tulikuwa tukitembea kikamilifu mbele za Bwana.

Kisha Mungu anazungumza kupitia nabii wake na kutabiri kwa mara nyingine tena na kusema:

Yawezekana kuwe na baadhi huko nje katika mataifa, ulimwenguni kote, ambao hata kanda hii ingewakuta manyumbani mwao au makanisani mwao. Tungeomba, Bwana, kwamba wakati ibada inaendelea, pale—pale…au kanda inachezwa, au nafasi yo yote tunayoweza kuwamo, au—au hali, yule Mungu mkuu wa Mbinguni na aheshimu huu unyofu wa mioyo yetu asubuhi hii, na kuponya wahitaji, kuwapa wao yale wanayohitaji.

Kama unazisikiliza hizo Kanda, na kuamini kwamba ndizo
Sauti ya Mungu kwa ajili ya wakati wetu, basi chochote unachoweza kuwa unakihitaji, Mungu atakuwa akizungumza kupitia mjumbe Wake na kusema, “ Wape chochote tunachohitaji .

Hilo linaweza kutukia tu kwa KUBONYEZA PLAY rafiki yangu.
Ikiwa ungependa kumsikia Mungu akinema na kufasiri Neno Lake Mwenyewe, akijifunua Mwenyewe kupitia mwili wa mwanadamu, na upokee chochote unachohitaji, njoo uungane nasi Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA , saa Jeffersonville,( Ni Saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania) tunapomsikia Mungu akisema nasi tunaposikia: Sikukuu ya Baragumu 64-0719M .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Mambo ya Walawi Sura ya16 yote

Mambo ya Walawi 23:23-27

Isaya 18:1-3

Isaya 27:12-13

Ufunuo 10:1-7

Ufunuo 9:13-14

Ufunuo 17:8

22-0814 Kile Kipeo

UJUMBE: 64-0705 Kile Kipeo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Kipeo,

Nawezaje kuwaandikia leo bila kuwakumbusha kile ambacho mchungaji wetu alichosema kuhusu kila mmoja wetu Jumapili iliyopita?

Bali kujua ya kwamba mahali po pote niwezapo kwenda…sina ku—kundi fulani ulimwenguni , nilijualo, linaloshikamana nami kama kundi hili. Mungu na—na ajalie tuwe wasioweza kutengana sana, hata, katika Ufalme ujao, naomba kwamba tuwe huko pamoja; ombi langu.

Hakuna kundi duniani linaloshikamana na nabii wa Mungu, na Ujumbe ambao Mungu alionena kwenye kanda, kama sisi. Na kwa sababu tunafanya hivyo, tutakuwa tusioweza kutengana katika Ufalme ule mpya pamoja naye na Bwana wetu Yesu Kristo. Haiwi bora zaidi ya hapo!

Hizi ni siku kuu sana za maisha yetu. Tumeridhika kabisa kuwa mpumbavu wa Kristo na Ujumbe Wake wa wakati wa mwisho. Kuitwa nati kwa sababu tunaamini kila Neno kwenye kanda hizo na kusema, BONYEZA PLAY.

Sisi ni Washiriki wa Lile Kanisa Moja la Pekee. Hatukujiunga Nalo, tulizaliwa ndani Yake. Kila wiki tunakusanyika pamoja kutoka ulimwenguni kote na kuendeleza mapenzi na Kristo na kusema, “Loo, jinsi ninavyokupenda ‘Jesu!’”

Tunaweza kuwa nati kwa ulimwengu, lakini Baba ametupa Ufunuo Wa yeye Mwenyewe katika wakati wetu, Mungu mwenye ngozi, na imetuvuta, Bibi-arusi Wake, Kwake.

Tunapenda tu jinsi lilivyo rahisi, lakini wakati huo huo, jinsi tu lilivyo la Kilindi. Lakini yakupasa uwe na Ufunuo upate kuliona, Nasi TUNAO.

Alijificha Mwenyewe katika utaji wa binadamu, katika Kanisa Lake, akijifunua Mwenyewe kwa imani yako na imani yangu, pamoja, kutuunganisha pamoja, tukifanya umoja wa Mungu. Mimi siwezi kufanya kitu bila ninyi; ninyi hamwezi kufanya kitu bila mimi; hakuna anayeweza kufanya kitu bila Mungu. Kwa hiyo, sote pamoja linafanya kitu kimoja, ule muungano. Mungu alinituma kwa kusudi hilo; mnaamini jambo hilo; na hapa linatendeka. Ndilo hilo hasa, mnaona, limehakikishwa kikamilifu.

Sisi ni Kama wale watu wakitembea barabarani kutoka Emau siku ile. Tunamsikiliza Yeye akizungumza nasi sote wakati wa mchana. Kisha tunamwalika ndani ya nyumba zetu ili tuweze kujifungia pamoja Naye peke yake. Ndipo anafanya jambo fulani awezalo yeye tu kulifanya, kuumega Mkate wa Uzima wa Milele. Tunamtambua papo hapo. Kisha tunasema, je mioyo yetu haikuwaka ndani yetu alipokuwa akisema nasi njiani.

Kila Wiki tunakusanyika kwa matarajio makubwa, tukijiuliza, “Atatuambia na kutufunulia nini wiki hii”. Tutatumiana nukuu mmoja kwa mwingine na kuzungumzia hilo wiki nzima. “Je, ulimsikia aliposema”:

“Ilinichukua miaka elfu nne kukitengeneza Kipeo Changu; lakini sasa imenichukua karibu miaka elfu mbili kutengeneza Kipeo kingine, Wewe, Bibi-arusi Wangu. Ninakitengeneza kwa njia Yake isiyobadilika , namna ile ile nilivyokitengeneza Kipeo Changu cha kwanza, Neno Langu. Hivyo ndivyo ninavyojitengenezea Vipeo Vyangu , kwa kuwa unaweza tu kuwa Kipeo kikamilifu wakati linapokuwa ni Neno kamilifu.”

Ndugu yangu, usione hili kuwa baya, lakini waza kwa dakika moja. Kama Yeye alitoa Kwake, kile kiumbe cha asili, ili amtengenezee Bibi-arusi, Yeye hakuumba kiumbe kingine; Yeye alichukua sehemu ya ule uumbaji asili. Basi kama Yeye alikuwa Neno, Bibi-arusi anapaswa kuwa nini? Hana budi kuwa Neno la asili, Mungu Aliye Hai katika Neno.

Nena kuhusu yubile ya mlo bora. Sisi ni sehemu ya uumbaji wa asili. Sisi ni sehemu ya Neno la asili. Mungu anaishi ndani yetu. Sisi ni Kipeo Chake. Sisi ndio kundi lile linaloshikamana na nabii Wake. Sisi ni wasioweza kutengana na nabii Wake na Bwana Yesu Kristo. Sisi ni MMOJA Na Yeye.

Kama nawe pia ungependa moyo wako uwake ndani yako kama unavyowaka ndani yetu, njoo uungane nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville,( ni Saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania), Wakati sehemu ya Bibi-arusi inapokusanyika Pamoja na kumwalika Yeye Majumbani mwetu, na katika makanisa yetu, tunapomsikia Mungu akisema Nasi na kutufunulia Maneno ya Uzima wa Milele, anapotuletea Ujumbe: Kile Kipeo 64-0705 .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Isaya 53:1-12
Malaki 3:6
Mathayo Mt 24:24
Marko Mt 9:7
Yohana Mt 12:24 / 14:19