All posts by admin5

23-0407 Ukamilifu

Ujume: 57-0419 Ukamilifu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Molingami Mwasi na Libala, tika ete biso nyoso elongo toyangana lelo mpe toyoka Liteya Bobongi be 57-0419. Ekozala koleka na Voice Radio na 12:30 nsima ya nzángá, ntango ya Jeffersonville, kasi mpo baoyo na ngambo na nivale minene, bómiyoka ba nsómi koyoka na ntango nyoso ekoki na manáka ya libota na bino

Ndeko Joseph Branham

23-0406 IBADA MAALUM YA USHIRIKA

Ujume: 57-0418 IBADA MAALUM YA USHIRIKA

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Mti wa Bibi-arusi Uliyorudishwa,

Kwa muda wa mwaka mzima, nimetazamia kwa hamu wikendi ninayoweza kufungia nje ulimwengu kabisa, kuzima vifaa vyangu vyote, kuomba siku nzima, kusikia Sauti Yake ikizungumza na moyo wangu, kushiriki Ushirika Naye, na kuweka wakfu upya maisha yangu kwa ukamilifu Kwa ajili ya Huduma yake. KILA SIKU inapaswa kuwa siku ya Pasaka kwetu, lakini wikendi hii ni tukio la kipekee sana, fursa takatifu; wakati uliotengwa kwa Bibi-arusi kukusanyika pamoja na Kuabudu. NIMESISIMKWA SANA kuhusu jambo hilo Enyi marafiki. Siwezi kungoja zaidi ili kujifungia na Mungu mahali pa siri, hapo katika Roho, nikiutazama Uso Wake; nikiungana na Bibi-arusi wa Kristo ulimwenguni kote, tukiketi katika mahali pa mbinguni. Lihimidiwe Jina la Bwana! Kwa kweli inapaswa kuwa wikendi inayotarajiwa sana na takatifu katika maisha yetu.

Loo, hebu tusimame dakika moja tu zaidi hapa. “Mahali pa Mbinguni.” Sasa, si popote pale, bali mahali pa Mbinguni. Tumekusanyika katika “Mbingu,” ina maana kwamba hapo ndipo mahali pa mwaminio. Basi, kama nimeomba vya kutosha, nawe umeomba vya kutosha, au kanisa limeomba vya kutosha, na tuko tayari kwa Ujumbe, nasi tumekusanyika pamoja kama watakatifu, walioitwa wakatoka, waliobatizwa na Roho Mtakatifu, wamejazwa na baraka za Mungu, wameitwa, wakateuliwa, wameketi pamoja mahali pa Mbinguni sasa, sisi ni wa Kimbinguni katika nafsi zetu. Roho zetu zimetuleta katika hali ya Kimbinguni. Loo, ndugu! Haya basi, hali ya Kimbinguni! Loo, nini kingetokea usiku wa leo, kungetokea nini usiku wa leo kama tungekuwa tumeketi hapa katika hali ya Kimbinguni, huku Roho Mtakatifu anatembea katika kila moyo ambao umezaliwa upya na ukawa kiumbe kipya katika Kristo Yesu? Dhambi zote zikiwa chini ya Damu, katika ibada kamilifu, huku tumemwinulia Mungu mikono yetu na mioyo yetu imeinuliwa, tumeketi katika mahali pa Mbinguni katika Kristo Yesu, tukiabudu pamoja katika mahali pa Mbinguni.

Je, umewahi kuketi mahali kama hapo? Loo, mimi nimeketi hata ningelia kwa furaha na kusema, “Mungu, kamwe usiniache nikaondoka hapa.” Mahali pa Mbinguni tu katika Kristo Yesu!

Akitubariki na Nini? Uponyaji wa Kiungu, kutangulia kujua, ufunuo, maono, nguvu, lugha, tafsiri, hekima, maarifa, baraka zote za Kimbinguni, na furaha isiyoneneka na iliyojawa na Utukufu, kila moyo umejazwa na Roho, tukitembea pamoja, tukiketi pamoja katika mahali pa Mbinguni, hakuna wazo moja baya kati yetu, hakuna hata sigara moja inayovutwa, hakuna nguo moja fupi, hakuna jambo hili, lile au lingine, hakuna wazo moja baya, hakuna aliye na neno dhidi ya mwingine, kila mtu akizungumza katika upendo na upatanifu, kila mtu katika moyo mmoja na mahali pamoja, “ndipo kukaja ghafla toka Mbinguni uvumi kama wa upepo wa nguvu ukienda kasi.” Haya basi, “Ametubariki kwa baraka zote za rohoni.”

Bwana Yesu pokea ibada zetu kwako wikendi hii ya Pasaka. Hebu na tuingie katika mahali pa mbinguni katika Kristo Yesu; na tupasue kuingia katika Patakatifu pa Patakatifu. Hakuna wazo moja baya, hakuna kizubaishi chochote, bali kwa nia moja, katika Mahali pamoja; basi kuwe na sauti kutoka Mbinguni ikija kama uvumi wa upepo wa nguvu uendao kasi katika kila moja ya nyumba zetu. “Njoo Bwana Yesu”, tuko tayari kukuona uso kwa uso.

Kwa maana Bibi-arusi amerudishwa kupitia Ujumbe wa Nuru ya jioni ya siku yetu; kupitia Ujumbe wa Malaki 4. Tunakushukuru Bwana kwa dhihirisho kamili la Kristo katika Kanisa Lake, si kanisa lililojengwa kwa mikono, bali dhihirisho kamili la Kristo aliyedhihirishwa ndani ya mtu, nabii wako, kwa ishara kuu na maajabu, naye amefunua Neno lote la Mungu tena. Na sasa linaishi ndani ya Bibi-arusi Wako ulimwenguni kote. Asante kwa kutuwezesha kuishi ili kuona Nuru hii kuu ya jioni, kulingana na unabii.

Basi Nuru ya jioni imetokea kwa ajili gani? Nuru ya jioni ni ya nini? Kurudisha. Whiu! Mnalipata? [Kusanyiko linasema, “Amina.”—Mh.] Nuru ya jioni ni kwa ajili ya kusudi lile lile la Nuru ya asubuhi, kurudisha kile kilichokatiliwa mbali na Nyakati za Giza, kupitia Roma. Mungu anaenda kurudisha, kwa kuangaza Nuru ya jioni (ya nini?), kulirudisha Neno lote la Mungu tena, dhihirisho kamili la Kristo katika Kanisa Lake. Kila kitu alichofanya Yeye, vile vile hasa alivyofanya, itakuwa hivyo tena katika Nuru ya jioni. Mnaona ninayomaanisha? Loo, hilo si ni zuri sana? [“Amina.”] Na kujua ya kwamba tunaishi papa hapa kuiona sasa, Nuru ya jioni, kulingana kabisa na unabii.

Bibi-arusi wa kweli haishii katika Kuhesabiwa haki, ingawa anajua dhambi zake ni kana kwamba hakuwahi kuzitenda kamwe; Yeye haishii katika Utakaso, ingawa Ametakaswa na kutengwa kwa ajili ya utumishi; Haishii katika Pentekoste, ingawa amepokea ubatizo wa Roho Mtakatifu; bali anaendelea hadi kwenye NENO LA SIKU YETU: Malaki 4, Neno Lenyewe lililofanyika mwili tena katika mwanadamu. Ile, “Nitarudisha asema Bwana,” ambayo italeta Imani ya Kunyakuliwa kwa Bibi-arusi. Na Neno hilo lililodhihirishwa linaweza TU kuja kwa kuzisikia Kanda, Jina Lake la ajabu na lisifiwe.

Mmoja wao, Martin Luther, yeye alianza kuiangaza Nuru. Kulikuwako na Nuru ndogo, nguvu kidogo sana, ya kuhesabiwa haki.

Ndipo akaja Wesley, nguvu zaidi, utakaso.

Baada ya Wesley, akaja aliye na nguvu zaidi kuliko yeye, Pentekoste, ule ubatizo wa Roho Mtakatifu, katika nabii mwingine mkuu. Unaona?

Lakini katika siku za mwisho, za Malaki 4, Eliya atakuja pamoja na Neno lile lile. “Neno la Bwana lilimjia nabii.” Katika Nuru za jioni, atatokea, apate kurudisha na kurejesha. Kitu gani? “Kuirudisha mioyo ya watoto iirudie Imani ya Mungu.” Nuru ya nne!

Njooni mkusanyike kulizunguka Neno, majumbani mwenu, wakati wa wikendi ya Pasaka na hebu tumwabudu Bwana. Zimeni simu zenu isipokuwa kupiga picha, kusikiliza Nukuu ya Leo, na kuzicheza kanda kwenye programu ya The Table , programu ya Lifeline, au anuani ya kupakulia.

Ningependa sote tuungane kwenye ratiba ifuatayo:

ALHAMISI

Ilikuwa ni Alhamisi usiku ambapo Bwana Yesu alikuwa na Karamu ya Mwisho pamoja na wanafunzi wake, katika ukumbusho wa Pasaka kabla ya kule kutoka kwa wana wa Israeli. Ni fursa iliyoje tuliyo nayo ya kufanya ushirika na Bwana katika nyumba zetu, kabla ya wikendi yetu takatifu, na kumwomba yeye atusamehe dhambi zetu, na kutupa sisi sote kile tunachohitaji katika safari yetu.

Mungu, chunguza mioyo yetu sasa. Je, ile Damu iko humo Bwana? Kama haimo, twaomba kuwa—kuwa utaiweka sasa hivi, ukiondoa dhambi zetu na kuzifunika, nazo zitatengwa nasi, Bwana, dhambi za ulimwengu huu, ili tuwe watakatifu na wa kupendeza mbele za Baba yetu sasa tunapokuja kula ule—ule mwili wa Damu iliyomwagwa ya Mwana-Kondoo wetu, Mwana wa Mungu, Mwokozi wetu.

Asante kwa kuturuhusu kuishi katika kuona Nuru hii kuu ya jioni, kulingana na Unabii.

Kwa ndugu na dada zangu wa nchi za ng’ambo,

Hebu sote tuanze saa 12:00 KUMI NA MBILI jioni . kwa masaa ya nchi na eneo unaloishi, kusikia Ushirika 57-0418. na kisha tuende katika Ibada yetu maalumu ya Ushirika itakayokuwa ikicheza kwenye programu ya Lifeline ama unaweza kupakua Ujumbe kwa Kiingereza ama lugha zingine kwa kubofya kwenye anuani hapa chini.

Kufuatilia Ujumbe, tutakusanyika na familia zetu majumbani mwetu na kushiriki Meza ya Bwana.

Hivi karibuni tutakuwa na anuani ya kupakua vyote kanda na ibada ya Ushirika, au, itapatikana kwenye Voice Radio .

IJUMAA

Hebu tuende katika maombi pamoja na familia zetu saa  3:00 TATU asubuhi ( ni saa 10:00 KUMI jioni ya Tanzania)., na kisha tena saa   6:00 SITA mchana( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Tanzania ), tukimualika Bwana kuwa pamoja nasi na kujaza nyumba zetu na Roho Mtakatifu tunapojiweka wakfu Kwake.

Mawazo yetu na yarudi huko nyuma hadi siku ile pale Kalvari, zaidi ya miaka 2000 iliyopita, na kumwona Mwokozi wetu akining’inia msalabani, na kisha tujitoe vivyo hivyo kufanya daima yale yanayompendeza Baba:

Sasa tunaona ya kwamba ilimwakisi kikamilifu. Yule Mchongaji sasa alikuwa amelifanya Neno kuakisi kwenye kile Kipeo tena, kilichoitwa Mwanawe, Mungu, Imanueli. Wazia tu, ya kwamba, mtu ambaye amejidhili sana mpaka Mungu akajitambulisha Mwenyewe mle ndani, katika mwili huo, Naye akawa…Yeye na Mungu wakawa mmoja. “Mimi na Baba Yangu ni Mmoja. Baba Yangu anaishi ndani Yangu. Mimi daima hufanya lile linalomfurahisha Baba.”

Vipi kama Mkristo siku hizi angeweza kuwa na ushuhuda kama huo? Ungekuwa ni kipeo papa hapa Yuma, mtaani. Kama wewe ni dobi mwanamke huko nje nyuma beseni la kufulia, ungali utakuwa ni kipeo kwa Mungu, wakati unapoweza kusema, “Daima nafanya kile kinachompendeza Mungu,” na ulimwengu mzima unaweza kuona ka—kazi ya Yesu Kristo ikiakisi ndani yako.

Kisha saa  6:30 Sita na Nusu Mchana.,(  ni saa 1:30 MOJA na NUSU jioni ya Tanzania ), tuungane pamoja katika nyumba zetu ili kusikia, Ukamilifu 57-0419.

Kisha Hebu na tuungane tena pamoja katika maombi saa 9:00 TISA alasiri.( ni saa 4:00 Nne Usiku ya Tanzania). katika ukumbusho wa kusulubiwa kwa Bwana wetu.

JUMAMOSI

Hebu sote kwa mara nyingine tena tuungane katika maombi saa 3:00 TATU Asubuhi ( ni saa 10:00 kumi jioni ya Tanzania )., na  saa 06:00 SITA Mchana( ni saa 1:00 Moja jioni ya Tanzania)., na tutayarishe mioyo yetu kwa ajili ya mambo makuu atakayotutendea miongoni mwetu.

Bwana! Tafadhali, Bwana! Loo, naweza nikaimba kupita kiasi. Huenda nikahubiri kupita kiasi. Huenda nikapaza sauti kupita kiasi. Huenda nikalia kupita kiasi. Lakini kamwe sitaomba kupita kiasi. Ee Mungu, nichunguze na unijaribu.

Nilikuwa tu nikizungumza, muda mfupi uliopita, kuhusu madimbwi ya kina kirefu, jinsi yanavyoziakisi nyota; tia kina cha Roho wako ndani yetu, Bwana, kama nabii Daudi alivyosema, “Uniongoze kando ya maji matulivu,” sio maji yanayotiririka. Maji matulivu, niongoze huko, Bwana. Ninyamazishe.

Kisha saa  6:30 SITA na NUSU Mchana ( ni Saa 1:30 moja na Nusu jioni ya Tanzania )., Sote tutakusanyika pamoja kusikia NENO:
Kuzikwa 57-0420.

Hii itakuwa SIKUKUU ILIYO MUHIMU ilioje kwa Bibi-arusi Wake ulimwenguni kote.

Kisha tuungane tena pamoja katika maombi saa 9:00 TISA alasiri . ( ni Saa 4:00 Nne Usiku ya Tanzania )

JUMAPILI

Ni Siku kamilifu jinsi gani kusikia na kushiriki Kurejeshwa Kwa Mti wa Bibi-arusi. Kwanza Hebu na tuamke mapema kama vile Ndugu Branham alivyofanya asubuhi ile wakati rafiki yake mdogo, yule robin, alipomwamsha
saa 11:00 KUMI na MOJA asubuhi .. Hebu na tumshukuru Bwana kwa kumfufua Yesu kutoka kwa wafu:

Saa kumi na moja asubuhi ya leo, rafiki yangu mdogo mwenye kifua chekundu aliruka dirishani akaniamsha. Ilionekana kana kwamba moyo wake mdogo ungepasuka, akisema, “Amefufuka.”

Saa  3:00 TATU asubuhi .( ni saa 10:00 kumi jioni ya Tanzania)  hebu na tuungane kwa mara nyingine tena katika mnyororo wetu wa maombi, tukiombeana sisi kwa sisi na kujitayarisha kuisikia Sauti ya Mungu.

Saa  6:30 Sita na Nusu mchana .(ni Saa 1:30 Moja na Nusu jioni ya Tanzania )tutakusanyika pamoja kusikia Ujumbe wetu wa Pasaka:  Kurudishwa Kwa Mti wa Bibi-arusi 62-0422.

Baada ya Ibada hii, Hebu na tuungane tena katika maombi, tumshukuru kwa WIKENDI YA AJABU ALIOTUPATA KUWA PAMOJA NAYE NA PAMOJA NA BIBI-ARUSI WAKE ULIMWENGUNI KOTE.

Kwa ndugu na dada zangu walio nchi za ng’ambo, kama mwaka jana,

Ningependa kuwaalika kuungana nasi kwa matukio haya kwa saa za Jeffersonville, kwa vipindi vyote vya maombi kwenye ratiba hii na kwa kanda itakayochezwa   Jumapili Alasiri . Ninatambua, hata hivyo, kwamba kucheza Kanda Alhamisi, Ijumaa, na Jumamosi alasiri katika wakati wa Jeffersonville kungekuwa vigumu sana kwa wengi wenu, kwa hivyo tafadhali jisikie huru kucheza Jumbe hizo wakati wowote wa mchana unaokufaa. Ningependa, hata hivyo, tuungane wote pamoja Jumapili saa 6:30 Sita na Nusu mchana., saa za Jeffersonville, ( Ni saa 1:30 moja na Nusu jioni ya Tanzania )ili kusikia Ujumbe wetu wa Jumapili kwa pamoja.

Ningependa pia kukualika wewe na watoto wako kuwa sehemu ya karatasi za vipindi vya Creations na video za Maelekezo, na majaribio ya YF, ambayo familia yako yote inaweza kufurahia pamoja. Tunaamini mtayapenda kwa kuwa yote yanahusu NENO tutakalosikia wikendi hii.

Kwa ratiba ya wikendi, taarifa kuhusu kujiandaa kwa ajili ya ibada ya Ushirika, nyenzo zitakazohitajika kwa ajili ya vipindi vya Creations, majaribio ya Pasaka, na taarifa nyinginezo, tazama anuani zilizopo hapa chini.

Ni heshima kubwa kwangu kukualika wewe na familia yako kukusanyika pamoja na Bibi-arusi duniani kote kwa wikendi iliyojaa KUABUDU, SIFA NA UPONYAJI. Ninaamini kweli ni wikendi ambayo itabadilisha maisha yako milele.

Ndugu Joseph Branham

23-0402 Unyakuo

Ujume: 65-1204 Unyakuo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Neno Juu ya Neno,

Makanisa mengi yametatizika, yana mshangao , yameduwazwa, yamepigwa na butwaa, yamefadhaika, yamechanganyikiwa na hata kushangazwa na kile kinachoendelea kwa hawa “ Watu wa Kanda ” kutoka ulimwenguni kote kila Jumapili.

Ni Muungano Usioonekana wa Bibi-arusi wa Kristo, tukiketi katika uwepo wa Mwana, kuivishwa, tukijiweka wenyewe tayari. Bwana Arusi Wetu wa Mbinguni amekuwa akituambia yote kuhusu Makao yetu ya Baadaye Pamoja Naye.

Majuma machache tu yaliyopita Alituambia: “Dunia hii si Makao yako, ni Edeni ya Shetani, nami nitaiteketeza kwa moto. Wewe ni kipenzi changu, ambaye Nimekuchagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu kuwa Bibi-arusi wangu. Sasa, Jumapili hii nitakuambia yote kuhusu Unyakuo Wangu unaokuja hivi karibuni.”

Tuko chini ya matarajio makubwa sana. Tunaweza kulihisi jambo hilo hewani. Mambo yanatukia haraka sana.

Vile vile hasa Biblia ilivyosema ingetendeka katika siku hii, inatendeka, siku baada ya siku. Mbona, inalundikana upesi sana huko nje, katika yale majangwa, na mambo yanayotendeka, hata nisingeweza kufuatilia jambo hilo. Tuko karibu na kule Kuja kwa Yesu, kuunganishwa na Kanisa Lake, ambapo Neno linafanyika Neno.

Haya yote yanatendeka kwa ajili yetu, Bibi Mteule wake, Bibi-arusi wa siku hii. Sisi ndio pekee tunaoona mambo haya yakijifunua.

Ametuchagua tangu zamani kwa ajili ya wakati huu na hakuna mtu yeyote anayeweza kupachukua mahali petu. Sasa Sisi ni wana na binti waliodhihirishwa ili tuweze kushirikiana Naye; hicho ndicho yeye Anachotaka.

SISI ni Neno juu ya Neno, chembe hai juu ya chembe hai, Uhai juu ya Uhai, na kimo kikamilifu cha Bibi-arusi wa Bwana Yesu Kristo.

Kama unalo hitaji, litamke . Wewe ni Neno juu ya Neno. Usiangalie utusitusi huu katika ulimwengu unaotuzunguka; magonjwa, maradhi, mauaji, kukata tamaa, ukichaa wa watu ambao hawajui ikiwa wao ni mwanamume au mwanamke. SISI NI BIBI-ARUSI , tuliochaguliwa tangu zamani , tumehesabiwa haki, Bibi-arusi aliyedhihirishwa wa Bwana Yesu Kristo.

Usiogope LOLOTE. Kuwa mwenye furaha na kushangilia. Muda umekaribia. Tunajiandaa kuondoka kwenye nyumba hii ya wadudu, UTUKUFU !!!

Njoo ujiweke tayari pamoja nasi kwa ajili ya Unyakuo , Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville ( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Tanzania). Kamwe Hutabaki kama ulivyokuwa.

Ndugu. Joseph Branham.

Maandiko ya kusoma Kabla ya Kusikiliza Ujumbe :

Zaburi 27:1-5

23-0326 Muungano Usioonekana Wa Bibi-Arusi Wa Kristo

Ujume: 65-1125 Muungano Usioonekana Wa Bibi-Arusi Wa Kristo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi Mteule,

Ungetoa nini ili Bwana Yesu aje kuingia nyumbani mwako Jumapili hii, aketi kwenye kochi lako, akuangalie machoni na anene nawe moja kwa moja?

Husingeweza kuzungumza. Usingependa kuzungumza. Yote ungalitaka kufanya ni kumwangalia yeye tu na kulia. Ungeogopa hata kufungua mdomo wako. Ungeweza kusema nini? Katika mawazo yako ungekuwa unawazia, Bwana, sistahili kabisa kwako Wewe kuwa hapa nyumbani mwangu. Mimi ni wa chini kabisa kuliko walio chini. Nimekukosea mara nyingi sana Bwana, lakini Bwana, nakupenda sana.

Ndipo ungetambua moyoni mwako, Anajua kabisa yale ninayowazia, hakuna kitu kilichofichwa Kwake. Anazijua kabisa siri za moyo wangu.

Unapotazama katika Macho Yake ya thamani, ungeona huo upendo na huruma. Angeweza kuzungumza nawe bila hata kufungua kinywa chake. Ungekuwa ukiwazia, Yeye yuko hapa, nyumbani mwangu, pamoja nami.

Moyo wako ungeanza kwenda mbio hata zaidi, ulipoona Akiwa karibu kutamka kitu fulani kwako. Mara moja, ile Sauti tamu sana ambayo hujawahi kuisikia ingesema, “ mpendwa, kipenzi changu ,usihofu, jina lako limo kwenye Kitabu changu cha Uzima cha Mwana-Kondoo. Si kitabu cha zamani cha ndoa yako ya kawaida, bali Kitabu Changu kipya cha Bibi-arusi. Ni cheti chako cha ndoa na Mimi.

Kipenzi, si kwamba tu umesamehewa dhambi zako zote na kushindwa kwako, Bali kwangu mimi , UMEHESABIWA HAKI. Machoni mwangu, hujawahi kufanya lolote baya.

Wewe ni mwana na binti yangu wa thamani, mwadilifu, asiye na dhambi. Unasimama bila doa; Bibi-arusi Wangu asiyeghoshiwa ambaye ameoshwa kwa Maji ya Damu Yangu Mwenyewe.

Kabla hata hakujakuwa na mwezi, nyota, au molekuli, ulikuwa mwana na binti yangu. Wewe ni onyesho la kimwili la sifa zilizokuwa ndani Yangu hapo mwanzo.

Jeni yako ya kiroho ilikuwa ndani Yangu kwa sababu wewe ni dhihirisho la sifa Zangu, mawazo Yangu. Ulikuwa ndani Yangu hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Wewe ni Bibi-arusi Wangu wa kiroho ambaye umekuwa ukikaa katika Uwepo wa Mwana, kuivishwa, kwa kusikiliza Neno Langu. Sasa umeanza kuwa na uamsho, kurudi na kujiweka sawa na Neno Langu. Wewe ni Bibi-arusi wangu, bibi-Mteule.

Sasa mnao muungano wa kiroho pamoja nami. Mwili wako unakuwa Neno, na Neno linafanyika mwili; likidhihirishwa na kuthibitishwa. Vile vile hasa nilivyowaambia ingetendeka katika siku hii, inatendeka, siku baada ya siku. Neno likifanyika Neno.

Mnao Ufunuo wa kweli wa siku hii ya mwisho: kukusanyika pamoja kwa Bibi-arusi Wangu kwa Ujumbe Huu. Hakuna wakati mwingine niliouahidi hilo. Niliwaahidi ninyi jambo Hilo, katika wakati huu: Malaki 4, Luka 17:30, Yohana Mtakatifu 14:12, Yoeli 2:38.

Tutakuwa na Sikukuu ya Kutoa shukrani Jumapili hii nitakapowaeleza hata na zaidi. Nitatumia muda mwingi, nikishiriki na kusherehekea Neno Langu pamoja nanyi. Nitawahakikishieni tena kwamba kwa kukaa na Neno Langu, nabii Wangu, Sauti Yangu, Kubonyeza Play, mko katika Mapenzi Yangu makamilifu .

Niliwaambia wao katika Neno Langu, Nasimama mlangoni, nabisha. Mtu yeyote akiisikia SAUTI yangu, na akaufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. Wengi hawatasikiliza na kufungua mlango wao, lakini kwa Ufunuo, ninyi mmefungua mlango wenu na kunikaribisha ndani.

Hawakubaliani na kuicheza Sauti Yangu katika makanisa yao. Iwapo wangemwacha tu Roho Mtakatifu achunguze nia zao kwa Neno, wangekubali. Mwache Kristo, Neno lililotiwa mafuta, achunguze dhamiri yako mwenyewe. Mwache yeye aingie ndani yako, uone kama Hiyo ni kweli ama sivyo.

Niliwaambia halitakuwa dhehebu litakalowakusanya pamoja, wao hawawezi kukubaliana kwenye Neno moja au mawili katika Biblia. Je! Niliwahi kamwe kuwaambia litakuwa kundi la watu? Hapana! Niliwaambia ulikuwa ni Ujumbe wa Mtu MMOJA; na mkasikiliza na kutii.

Kwa sababu hawakusikiliza na kukubali mpango wangu wa asili tangu mwanzo, Nikawatumia wahubiri, waalimu, mitume, wachungaji na manabii. Lakini walitumwa kuwaelekeza watu KURUDI kwenye Mpango wangu wa asili na mkamilifu, Malaika Wangu mwenye nguvu. Kwa maana ni Sauti ya Mungu kwenu.

Wametiwa mafuta, lakini MIMI nina NABII-MJUMBE MMOJA WA KUWAONGOZA NINYI. ROHO MTAKATIFU ​​NDIYE NABII. Je, sijawaambia mara nyingi, NENO LANGU LILILONENWA KUPITIA KWAKE HILO HALIHITAJI KUFASIRIWA, USIONGEZE KWALO AU KUONDOA CHOCHOTE ALICHOSEMA, SEMA TU YALE ALIYOSEMA KWENYE HIZO KANDA ? Huyo ndiye nabii, Roho Mtakatifu anayewaongoza.

Yeye ndiye niliyemtuma kuwaita muwe Bibi-arusi Wangu. Yeye ndiye wa kuwatambulisha ninyi Kwangu. Yeye ndiye niliyesimama naye nilipomwonyesha kukaguliwa kwenu kimbele, Bibi-arusi Wangu. Niliwaambia yote kumhusu yeye katika Ufunuo niliposema, MIMI Yesu nimemtuma MALAIKA WANGU kuwashuhudia ninyi mambo haya KATIKA MAKANISA. Ni MIMI, natumia tu mwili wake na sauti yake kuzungumza nanyi.”

Ni siku ya ajabu jinsi gani tunayo kuwa nayo pamoja Naye. Hatujawahi kuwa wenye furaha au kuridhika zaidi hivi maishaini mwetu. Hii ndio YENYEWE . Hili ndilo tumekuwa tukingojea maisha yetu yote.

Hakuna kivuli cha shaka katika mioyo yetu ama akili zetu. Kwa maana kwa kila Ujumbe tunaosikia, anatuambia tuko katika Mapenzi yake makamilifu. Kuna Sauti moja tu itakayowaunganisha ninyi, kuwakamilisha, na kuwaleta pamoja…Mimi, MIMI NIKINENA KUPITIA NABII WANGU. SI MANENO YAKE, NI MANENO YANGU. NI NJIA YANGU ILIYOANDALIWA.

Meza imeandaliwa. Imejaa Makabeji, na matanipu, na mafigili…NENO JUU YA NENO, JUU YA NENO. Tutakuwa na Sikukuu ya Kutoa shukrani ambayo Haijawahi kutokea. Kutakuwa na yubile duniani kote wakati Bibi-arusi watakapokusanyika kandokando ya Meza zao ili kusikiliza Sauti ya Mungu ikinena nao. Nyumba zetu na makanisa yetu yatajazwa na uwepo wake. Tutaduwaa isipokuwa Utukufu, Haleluya zetu, jina la Bwana lihimidiwe.

Njoo uwe sehemu ya Kukusanyika huku kwa Familia ya Bibi-arusi kutoa Shukrani, anapotulisha. Usichelewe, kwani tutaanza kusherehekea Jumapili, saa 06:00 SITA kamili MCHANA , saa za Jeffersonville. ( ni Saa 1:00 MOJA kamili JIONI ya Tanzania na Kenya pia ) Kwa maana aliniambia angekuwepo.

NAKUJA na nitakuwa nikiwaambia yote kuhusu Muungano wenu Usioonekana wa Bibi-arusi wa Kristo 65-1125.

Nitawaoneni Pale Mezani.

Ndugu. Joseph Branham

AKA: Bibi Mteule Wake

23-0319 Kuchagua Bibi-Arusi

Ujumbe: 65-0429e Kuchagua Bibi-Arusi

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa, Mmoja Katika Milioni Moja,

Nimekuwa nikikusubiri kwa muda mrefu sana. Wewe ni Kipenzi changu wa moyo, na ninakupenda sana. Kama nilivyokuahidi, nimekuwa nikikutengenezea Makao mapya ambapo tutaishi pamoja katika Milele yote. Nimeweka kila kitu jinsi kabisa unavyovipenda.

Sasa Ninaweza kukutazama na kuona, wewe ni picha halisi yangu mimi . Una tabia Yangu hasa, Mwili Wangu, Mifupa Yangu, Roho Wangu yeye yule, kila kitu Changu jinsi ile ile , sawa kabisa. Umekuwa mmoja na Mimi.

Nilimtuma malaika Wangu mwenye nguvu duniani kukuita wewe kutoka katika Edeni ya Shetani. Nilimtuma ili aweze kueleza mawazo Yangu, sifa Zangu, na kuwaambia kuhusu mambo yajayo. Nilitumia kinywa chake na sauti yake kujieleza. Baada ya yeye kuyasema, naliyatimiza, kwa maana Mbingu na nchi zitapita, bali Neno Langu kwenu halitashindwa kamwe.

Nilijua uliponisikia nikizungumza, kwa kutumia sauti ya malaika Wangu, ungejua ndani kabisa ya moyo wako, huyo hakuwa yeye, ilikuwa ni Mimi nikizungumza nawe. Ilikuwa ni Mimi nikikutumia barua ya mapenzi, nikikuambia, Nimekuchagua kuwa Bibi-arusi Wangu kipenzi.

Machoni Mwangu, hakuna aliye kama wewe. Hakuna anayeweza kupachukua mahali pako. Umebaki mkweli na mwaminifu Kwangu. Ninapokutazama, Moyo Wangu unachangamka kwa furaha.

Wakati Nilipokuambia, kuwa mwangalifu sana kipenzi , kile unachosikiliza, kutakuwa na wapakwa mafuta wengi wanaotumia Maneno Yangu, lakini ni wa uwongo. Nawe ulielewa onyo Langu kwa Ufunuo na ukakaa mkweli na mwaminifu kwa Sauti Yangu.

Nilijisikia vizuri sana mlipoomba kwa bidii kuhusu ni kanisa la aina gani mnaloshiriki. Niliwaambia mfanye chaguo sahihi, na nikawapa mifano ya jinsi kanisa kamilifu lilivyo. Mlikumbuka niliposema hayo huwa yana roho, na mchague kanisa kamilifu.

Hata niliwaambia kuwa wangalifu sana ni nani aliye mchungaji wako. Kwa hiyo mnaweza kufikiria jinsi moyo Wangu ulivyoruka kwa furaha nilipowaona mmekaa na mchungaji Niliyemtuma kuwaleta ninyi Kwangu. Mlijua ni Roho Wangu Mtakatifu akiishi ndani ya nabii Wangu kuwaongoza ninyi Kwangu.

Nakumbuka siku mliyokuwa na furaha sana, na kuchangamshwa kweli, wakati nilipomwita malaika Wangu mahali pa juu ili niweze kumwonyesha ninyi mkikaguliwa Kimbele . Tulikuwa tumesimama hapo tukiwatazama mkipiga hatua taratibu ya Twendeni Askari wa Kristo mbele Yetu.

Alipenda jinsi nyote mlivyokuwa mmevalia vazi lenu la taifa mlikotoka ; kama Uswisi , Ujerumani, na kutoka kote ulimwenguni. Kila mmoja mkiwa na nywele zenu ndefu zilizotengenezwa vizuri. Sketi zenu zilikuwa ndefu nadhifu. Nilijisikia vizuri na kufurahi sana kuwaonyesha ninyi nyote kwake, ili aweze kurudi na kuwatia moyo na kuwaambia aliwaona Kule.

Kila jicho lilitutazama Sisi. Wakati wasichana wachache, nyuma ya mstari, walianza kuangalia huku na huko mahali pengine, yeye alipiga kelele , “Msifanye hivyo! Msiache hatua hizo!”

Wakati Nilipowaambia Ninawahifadhia chakula ninyi mpate kula, mlijua kabisa nilichokuwa nazungumzia. Mlitaka kuwa Bibi-arusi-Neno Bikira Wangu . Sijawahi kuwapata mkitaniana na mtu mwingine yeyote. Daima imekuwa ni Mimi, Neno Langu. Hilo lilinifurahisha sana Mimi.

Nimewachagua , NINYI , kuwa Bibi-arusi Wangu. Ninawapenda sana, kama vile ninyi mnavyonipenda Mimi. Msivunjike moyo, jipeni ​​moyo, iweni wenye furaha , Shangilieni, siku ile inakaribia upesi nitakapokuja kuwachukua. Ni Wakati mzuri vipi Tutakaokuwa nao .

Ninyi Wengine, TUBUNI, dunia inanguruma. Siku moja Los Angeles itazama chini ya bahari, Kama vile nilivyowaambia ingekuwa. Ghadhabu yangu inakokomoa papa hapa chini yake. Sitazuia ufuko huo muda zaidi tena. Utatiririka ndani ya bahari kina cha maili moja, kote kote mpaka kwenye Bahari ya Salton. Itakuwa mbaya zaidi kuliko siku ya mwisho wa Pompeii.

Naenda kuisafisha dunia hii kwa moto hivi karibuni. Nitaua kila kitu Kilicho juu yake na chini yake. Mnayaona yale yanayoendelea ulimwenguni kote, kama nilivyowaambia. Mnamwona Bibi-arusi Wangu akiungana pamoja kulizunguka Neno Langu, kama vile nilivyowaambia.

Sasa huu ndiyo wakati Wenyewe . Sasa haya ndiyo majira yenyewe. Jiandaeni!

Ile saa ya ghadhabu Yake iko juu ya nchi. Kimbieni wakati kungali na wakati wa kukimbia, na mwingie ndani ya Kristo.


Mmealikwa kuja kuungana nasi, sehemu ya Bibi-arusi Wake, tunapojiweka wenyewe tayari kwa ajili ya Kuja Kwake, kwa kusikia Sauti ya Mungu ikisema nasi na kutuletea Ujumbe: Kuchagua Bibi-arusi 65-0429E Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA saa za Jeffersonville.( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Tanzania na Kenya pia )

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma Kabla ya Kusikiliza Ujumbe :

Mwanzo 24:12-14
Isaya 53:2
Ufunuo 21:9

23-0312 Makao Ya Baadaye Ya Bwana Arusi Wa Mbinguni Na Bibi-Arusi Wa Duniani

UJUMBE: 64-0802 Makao Ya Baadaye Ya Bwana Arusi Wa Mbinguni Na Bibi-Arusi Wa Duniani

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Duniani,

Malaki 4 ni Neno la Mungu, nayo imezaa kwa jinsi yake, SISI, Bibi-arusi Wake. Ni Roho Mtakatifu, Utu wa Yesu Kristo, katika matendo , aliyewekwa ndani ya mioyo yetu. Tumehuishwa kwa KILA Neno alilonena, kwa kuwa “Kondoo Wangu huisikia Sauti Yangu; mgeni hawatamfuata.”

Imekuwa ya ajabu jinsi gani miezi hii iliyopita , kumfuata nabii huko Jeffersonville. Mungu amekuwa akizungumza kupitia malaika wake mwenye nguvu na kutulisha kwa Chakula chake kilichohifadhiwa Ghalani kutoka kwenye GHALA LAKE MOJA DOGO katika nchi yote. Ni Mana Iliyofichwa, ni kwa ajili ya Bibi-arusi Wake tu.

Kwa kila Ujumbe tunaousikia, tunashiriki na kufurahi pamoja; “Najua nimezisikia Jumbe hizi mara nyingi sana hapo awali, lakini KAMWE sijawahi kuzisikia kama hivi sasa”. Hakika ni chemchemi ya Maji yaliyo Hai yanayobubujika ndani yetu. Hatuwezi kujizuia. Ndiyo yote tunayotaka kuzungumzia. Hatukuwahi kuwa na uhakika katika maisha yetu, wakujua sisi ni nani na wapi tunaelekea.

Hakuna kujiuliza tena:
“ Mimi Sijui tu. Nimefanya mambo mengi ya kutisha maishani mwangu. Nimemkosea Bwana mara nyingi sana. Inaonekana DAIMA mimi hujichafua.”

Hakuna kutumai tena :
“Natumai kweli kuwa mimi ni mtoto wa Mungu. NINATAKA kuwa. Naomba niwe.”

Siku hizo ZIMEKWISHA . Sasa TUNAJUA . Utukufu kwa Mungu!!

Tunajuaje? Mungu amekuwa akizungumza nasi moja kwa moja kwa Sauti Yake iliyo kwenye kanda, akituambia tena na tena, “Mimi niko ndani yenu, ninyi mko ndani Yangu. Sisi ni MMOJA. Niliwachagua NINYI kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Ninyi ni nyama ya Nyama Yangu , mfupa wa Mfupa Wangu”.

Ni Ujumbe mkamilifu jinsi gani Mungu aliyotuzungumzia siku ya Jumapili kutuambia yote kuhusu jinsi ulimwengu huu tunaoishi si wetu, ni Edeni ya Shetani. Jinsi alivyomdanganya Hawa hapo mwanzo kuhoji na kutilia shaka NENO MOJA tu. Alivua utaji mtakatifu wa Mungu, na kujivika utaji wa maarifa, ndipo macho yake yakafumbuliwa naye akajua alikuwa yu uchi.

Shetani alipotosha Neno la asili, na sasa amempofusha kwamba bado yu uchi wala hajui. Amekuwa malkia wa Shetani na dunia hii ndiyo Edeni ya ufalme wake.

Jumapili, Bwana-arusi wetu wa Mbinguni anataka kumkumbusha Bibi-arusi Wake wa duniani mahali Makao yetu ya baadaye yalipo na vile yatakavyokuwa. “Mpendwa Kipenzi , kwa kuwa sasa nimekwisha kuambia yote kuhusu ulimwengu huu na jinsi Edeni ya Shetani ilivyo, ninataka kukuambia KWA MARA NYINGINE TENA kuhusu Makao YAKO ya Baadaye na mimi .

Nataka kuwaambieni kinaganaga. Najua mmenisikia nikiwaambia juu Yake mara nyingi, lakini ngojeni tu, wakati huu itakuwa kana kwamba hamjawahi kunisikia nikiwaambieni hapo kabla.

Nataka kuingia kwa undani sana. Ninataka kuwafunulia Ninyi mko katika Mapenzi yangu Makamilifu kwa kukaa na Neno langu na nabii Wangu. Ninataka kuwapa mfano wa kile mnachofanya leo hii kama mfano mkamilifu wa ule mji mpya mtakaoishi ndani yake.

Tutaingilia jambo fulani hakika. Nitawadondoshea kitu fulani kidogo; Naamini mtalikamata. Mtaishi katika Mji huo pamoja Nami. Nabii wangu ataishi karibu nanyi . Atakuwa jirani yako. Mtatembea kwenye barabara hizo za dhahabu na kunywa kutoka kwenye Chemchemi Yangu. Mtatembea katika paradiso za Mungu, huku Malaika wakirukaruka na kuimba nyimbo za sifa.

Ninyi mtakuwa vito kwenye taji ya nabii Wangu. Mtang’aa kuliko kitu chochote kile ulimwenguni, katika Siku ile. Kuna mengi nataka kuwafunulieni Jumapili. Ni siku ya ajabu iliyoje tutakayokuwa nayo pamoja”.

Anayo mengi sana ambayo ametuwekea akiba katika wiki chache zijazo, kama hatakuja na kutuchukua kabla ya wakati huo. Wiki baada ya wiki, akituambia, sisi ni akina nani, tunakoelekea, jinsi kutakavyokuwa kule. Atakuwa akituongoza hadi kwenye wiki iliyo tukufu sana ya Pasaka ambayo hatujawahi kamwe kuwa nayo, iliyojawa na si kingine ila kumsifu na kumwabudu yeye.

Ni wakati wa kusisimua jinsi gani . Tunaona unabii ukitimia mbele ya macho yetu. Tunaona Neno likidhihirishwa NDANI YETU. Kuja Kwake kunaweza kutokea wakati wowote. Tunasimama mlangoni tukiwa na shada la maua mikononi mwetu. Tunaweza kusikia farasi wakienda shoti na mchanga ukivingirishwa chini ya magurudumu.

Lile gari la Kale la Farasi litasimama hivi karibuni. Tutaruka kutoka kwenye mlango wa mwili huu mzee na kurukia mikononi Mwake. Atatutazama na kusema, “Yote yamekwisha sasa, mpenzi, nitakupeleka sasa kwenye Makao yako ya Baadaye.”

Unaalikwa kuwa sehemu ya siku zilizo kuu ambazo ulimwengu haujawahi kuona. Wana tai watakusanyika kutoka ulimwenguni kote ili kusikia Sauti ya Mungu ikizungumza na Bibi-arusi Wake na kumwambia yote kuhusu: Makao Ya Baadaye ya Bwana-arusi Wa Mbinguni na Bibi-arusi wa Duniani 64-0802 , saa 06:00 SITA Mchana , saa za Jeffersonville. ( Ni saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania na Kenya pia ).

Ndugu. Joseph Branham

Ukumbusho: Msisahau kuhusu badiliko la saa ya Akiba ya mchana.

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikia Ujumbe:

Mathayo 19:28
Yohana 14:1-3
Waefeso 1:10
2 Petro 2:5-6 /Sura ya 3 yote.
Ufunuo 2:7 / 6:14 /21:1-14
Walawi 23:36
Isaya Sura ya 4 yote / 28:10 / 65:17-25
Malaki 3:6

23-0305 Edeni ya Shetani

UJUMBE: 65-0829 Edeni ya Shetani

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Watoto Wangu Wapendwa,

Ninyi ni sifa Yangu, Baba yenu wa Mbinguni. Mlikuwa ndani yangu tangu mwanzo. Hamkumbuki hilo sasa, lakini mlikuwemo humo pamoja Nami . Nilitamani sana kuwajua kwa sababu nilitaka kuwasiliana nanyi, nizungumze nanyi, niwapende, na kuwapa mkono.

Kama mtoto wangu, wewe ni sehemu Yangu, uliyefanyika mwili, kama vile nilivyofanyika mwili, ili tushirikiane mmoja na mwengine kama familia ya Mungu duniani. Hilo ndilo lilikuwa kusudi Langu na ndilo nililotaka tangu mwanzo.

Niliwatengenezea Bustani ya Edeni ili tuweze kuwa na ushirika , lakini adui Yangu akaingia kimya kimya kwa udanganyifu , na kuutawala ulimwengu huu kwa kufasiri vibaya mpango wangu kwenu.

Ni saa danganyifu mnayoishi ndani yake, lakini pia ni wakati mzuri zaidi ya nyakati zote, kwa sababu sasa mnaelekea ule Utawala mkuu wa Miaka Elfu tena; mnaelekea Edeni tena.

Roho wangu si kitu ambacho mmeelimishwa. Ni kitu ambacho Mimi nilikiweka ndani yenu kwa kujua kwangu tangu awali kwa mkono Wangu wenye nguvu. Sasa mwito Wangu wa mwisho unatoka kumshika Bibi-arusi Wangu; “Tokeni kati yao, mkatengwe nao”.

Leo wao hawajaribu kuliimarisha Neno Langu katika mioyo ya watu, wanajaribu kujiimarisha wao wenyewe . Makanisa yanajaribu kuimarisha fundisho la kanisa ndani ya moyo wa mtu. Kila mtu akisema, “Nilitenda hili. Mimi, mie, langu, dhehebu langu, mimi, hili.” Wanajiimarisha wao wenyewe na si Neno Langu lililonenwa kupitia nabii wangu.

Haiwabidi kuelewa yote Nisemayo, inawabidi kuliamini tu kwa sababu nilisema hivyo, na hilo latosha milele.

Roho wangu Mtakatifu anatenda kazi ndani yenu. Ni Uzima uliyo ndani yenu, si msisimko wa mwili ; sio namna fulani ya uhakika wa matendo ya kimwili, Bali ni Mtu, MIMI, Yesu Kristo, Neno la Mungu, lililowekwa mioyoni mwenu, nalo linahuisha kila Neno la wakati huu. Ni Roho Wangu Mtakatifu akitenda kazi ndani yenu kulingana na Neno.

Bibi-arusi wangu wa kwanza alianguka kwa kusikiliza hoja za Shetani, lakini Nimewakomboa ninyi kwa nafsi Yangu, ambalo ni Neno lililofanyika mwili. NINYI HAMTANIANGUSHA. Ninyi ni Bibi-arusi-Neno Bikira Wangu ambao hamtasikiliza hoja za Shetani. Mtakaa na Neno Langu.

Baada ya ule Utawala wa Miaka Elfu kumalizika, basi kutakuweko na Edeni iliyowekwa tena; Ufalme wangu mkuu utarudishwa tena. Niliupigania dhidi ya Shetani katika bustani ya Gethesemane, nami nikainyakua Edeni Yangu. Sasa nimeenda kuiandaa Edeni yenu Mpya huko Mbinguni. Nitarudi tena kuwachukueni hivi karibuni, kwa hivyo msifadhaike mioyoni mwenu.

Hakutakuwa na Bahari tena, kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zitapita. Nitaifanya upya kwa ubatizo wa Moto ambao utaua kila mdudu mbaya , kila maradhi, kila ugonjwa, na kila uchafu uliowahi kuwa duniani.

Dunia itapasuka, kutatokea Dunia Mpya . Mbingu hii ya kwanza na nchi ya kwanza zitapita. Kutakuwa na Yerusalemu Mpya ikishuka kutoka Kwangu Mimi kutoka Mbinguni. Hapo nitakuwa pamoja nanyi, sifa Zangu za kweli, Wanangu wa kiume na wakike. Tutakuwa na ushirika katika utakatifu, macho yenu yakiwa yametiwa upofu yasione dhambi yo yote.

Nimewajieni tena kama nilivyowaahidi ningefanya. Nimelitimiza Neno langu kwenu. Nililirekodi Neno Langu kwenye kanda ya sumaku ili kusiwe na mkanganyiko, hakuna swali, Neno langu safi tu kwa ajili yenu; kwa kuwa ni Bwana Asema Hivi.

Wekeni dhamiri zenu ziwe safi. Ifunikeni mioyo yenu. macho yenu
yafunikwe yasione mambo ya ulimwengu ya kufanywa mtu mkubwa fulani .

Msisahau kamwe, nitageuka huko magharibi na kurudi tena, mojawapo ya siku hizi. Mpaka wakati huo, peleka Jina Langu ; Litafurahisha moyo, peleka, uendako, kwa Kubonyeza Play.

Msipatane hata kwa Neno moja. Neno Langu kwenye kanda halihitaji kufasiriwa. Ninyi ni sehemu Yangu, sifa Yangu. Ulimwengu huu ni Edeni ya Shetani, lakini nimewafanyia Edeni Mpya ambamo tutaishi milele pamoja. Hadi wakati huo, unganeni kwenye Neno Langu. Pendaneni.

Njoo uungane nao katika Maskani ya Branham Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA saa za Jeffersonville, ( ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Tanzania na Kenya pia ) , na mnisikie mimi Nikinena kupitia nabii Wangu niliyemchagua na kufunua Neno Langu mnaposikia; Edeni ya Shetani 65-0829.

Kwa Niaba Yake,
Ndugu Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Kusikiliza Ujumbe :

2 Timotheo 3:1-9
Ufunuo 3:14
2 Wathesalonike 2:1-4
Isaya 14:12-14
Mathayo 24:24

23-0226 Chujio La Mtu Mwenye Busara

Ujume: 65-0822e Chujio La Mtu Mwenye Busara

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Kusanyiko la Ndugu Branham,

Ningependa kualika ulimwengu kuungana nasi kwa njia ya mawasiliano ya simu Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, (ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Tanzania) Wakati sisi Tai tunapokusanyika pamoja kila maili mia mbili mraba katika mojawapo ya makanisa ya nabii. Tutamsikia Mungu akinena kupitia malaika-mjumbe wake wa saba na kutuambia:

Ujumbe huu, na Jumbe zote zingine ambazo ninazungumzia, zinaelekezwa kwenye kusanyiko langu. Si kwa ajili ya kusanyiko lako isipokuwa wawe wanataka kulipokea. Bali limeelekezwa kwa watu hawa hapa.

Yeye anazungumza nasi, UTUKUFU, kusanyiko lake. Si ninyi mnaosema, “Ndugu Branham ni nabii, bali yeye si mchungaji wetu. Mchungaji wetu anasema kuzicheza kanda kanisani hakulingani na Neno la Wakati huu.” “Mchungaji wetu anatuambia yatupasa tumsikilize Yeye. Kulingana na Neno, anatuongoza sasa hivi kwa Roho Mtakatifu .”

Nabii aliwaeleza ninyi na mchungaji wenu.

kwa ajili ya wahudumu wo wote mahali po pote, wakati wo wote, hili halielekezwi kwa madhumuni ya kudharau mafundisho yenu, hili hata halielekezwi kwa kondoo wenu.

Hatutaki kubishana nanyi ndugu na dada. Tunaelewa, halielekezwi kwenu, bali kwetu sisi, tunaoamini kwamba Roho Mtakatifu amemweka malaika-mjumbe Wake wa saba kuwa mchungaji wetu na kutuongoza sisi, kanisa Lake. Tunaamini kuzicheza kanda ndiyo NJIA PEKEE YA KWELI. Mko sahihi na mnafanya kile nabii alichowaambia NINYI mfanye:

Na sikuzote mimi huwarejesha, kama wao ni washiriki wa kanisa fulani, “Mwoneni mchungaji wenu.”

Yawabidi mfanye jinsi mchungaji wenu anavyosema.

Kisha nabii anamwambia mchungaji wenu kwa mara nyingine tena, ili tu kuhakikisha ameelewa.

Sasa, ewe mchungaji, nataka ujue jambo hilo, ya kwamba, ninazungumza haya kwa ajili ya kusanyiko langu peke yake. Nami nina haki ya kutenda jambo hilo, kwa maana nimewekwa na Roho Mtakatifu kuwachunga kondoo hawa.

Yeye Ametumwa kutuchunga sisi, kondoo wake; wale ambao Mungu amempa KUWATUNZA. Roho Mtakatifu ndiye mchungaji wetu anapotuzungumzia na kutuongoza kila siku kwa Sauti yake iliyothibitishwa.

Hivi ndivyo Bwana atuongozavyo kufanya. Hatuko dhidi yenu ama mchungaji wenu, au jinsi mnavyohisi kuongozwa na Bwana kufanya. Kila mmoja yampasa kufanya jinsi anavyohisi Bwana anamwongoza kufanya kulingana na Neno.

Tuna chujio moja, UJUMBE HUU. Kila kitu tunachokisikia lazima kipitie kwenye chujio hilo. Sauti tunayoisikia kwenye kanda hizi ndiyo Sauti pekee tunayoamini kwa 100% kuwa Bwana Asema Hivi.

Hivi unaamini ya kwamba huko kutiwa mafuta juu ya watu hao kunamaanisha ya kwamba ni upako wa Roho Mtakatifu?” Naam, bwana, Roho Mtakatifu halisi wa Mungu juu ya mtu, na hata hivyo wao ni wa uongo.

Kikomo chetu cha milele kinategemea kile YEYE ALICHOSEMA KWENYE KANDA, si kile mtu mwingine yeyote ama kundi la watu wanachosema. Kwa hiyo, hatuwezi, na hatutamsikiliza mtu mwingine . anawezaje Mtu yeyote kubahatisha ?

Njooni mkusanyike pamoja nasi zaidi sana kama mwonavyo ile siku ikikaribia.

Watu wanaweza kuketi moja kwa moja nyumbani mwao ama nini hii mwao…wakusanyike makwao, makanisani mwao, na kadhalika, na kusikiliza ibada.

Hilo, marafiki , kulingana na nabii wa Mungu, si kulingana na fasiri ya mtu fulani ya kile Biblia inachosema, ni kukusanyika pamoja kulizunguka Neno zaidi sana kama tunavyoona ile siku ikikaribia.

Sanduku lina faida gani bila Mungu? Ni sanduku tu la mbao, meza mbili za mawe.

Njoo ukusanyike pamoja nasi tunaposikiliza chujio lililoandaliwa na Mungu, anapotuletea Ujumbe: Chujio La Mtu Mwenye Busara 65-0822E.

Ndugu. Joseph Branham

Chunguzeni kile mnachopigania. Chunguzeni kilichowaleta hapa. Chunguza kwa nini unaenda kanisani. Nini kinachowafanya… Ni vyema kwenda kanisani, bali usiende kanisani tu; jambo hilo halitawaokoa.