Sauti tunayosikia kwenye kanda ndio Sauti ile ile iliyolitangaza Neno Lake katika Bustani ya Edeni, juu ya Mlima Sinai, na kwenye Mlima wa Kugeuzwa Sura. Inasikika leo kwa Ufunuo kamili na wa mwisho wa Yesu Kristo. Inamwita Bibi-arusi Wake atoke, ikimtayarisha kwa ajili ya Kunyakuliwa. Bibi-arusi analisikia, analikubali, analiishi, naye amejiweka mwenyewe tayari kwa kuliamini.
Hakuna mtu anayeweza kuliondoa Hilo kutoka kwetu. Maisha yetu hayawezi kuchezewa. Roho wake anawaka na kuangaza ndani yetu. Yeye ametupa Uzima Wake, Roho Wake, naye Anaudhihirisha Uzima Wake ndani yetu. Tumefichwa ndani ya Mungu nasi Tunalishwa kwa Neno lake. Shetani hawezi kutugusa. Sisi hatuwezi kuondoshwa. Hakuna kinachoweza kutubadilisha. Kwa Ufunuo, sisi tumekuwa BIBI-ARUSI NENO.
Wakati Shetani anapojaribu kutuangusha, tunamkumbusha tu jinsi Mungu anavyotuona. Anapotutazama, anachokiona tu ni dhahabu SAFI. Haki yetu ni haki YAKE. Sifa zetu ni sifa ZAKE mwenyewe zenye utukufu. Utambulisho wetu unapatikana katika Yeye. Kile alicho Yeye, sasa tunakionyesha. Kile alicho nacho Yeye, TUNAKIDHIHIRISHA SASA.
Jinsi gani Yeye anavyopenda kumwambia Shetani, “Sioni dosari yoyote ndani Yake; Yeye ni MKAMILIFU. Kwangu mimi, Yeye ni Bibi-arusi Wangu, amejaa utukufu ndani na nje. Tangu mwanzo hata mwisho, Yeye ni Kazi Yangu, na Kazi Zangu zote ni kamilifu. Kwa kweli, ndani Yake kumejumlishwa na kudhihirishwa hekima na kusudi Langu la milele”.
“Nimemwona Bibi-arusi Wangu anayependeza anastahili. Kama vile dhahabu inavyofulika, Yeye amestahimili mateso kwa ajili Yangu. Yeye hajapatana, kukunjwa, au kuvunjwa, bali amefanywa kitu chenye uzuri. Majaribu na majaribio yake ya maisha haya yamemfanya Yeye kuwa Bibi-arusi wangu kipenzi”.
Je! hivyo si kama tu Bwana? Anajua jinsi ya kututia moyo. Anatuambia, “Msivunjike moyo kamwe, bali jipeni moyo”. Anaona kazi zetu za upendo Kwake. Anaona kile kinachotulazimu kupitia. Anaona vita vya kila siku tunavyovivumilia. Kwa vile anavyotupenda sisi kupitia kila moja ya hayo.
Machoni pake sisi ni wakamilifu. Ametungojea sisi tangu mwanzo wa wakati. Hataruhusu lolote litutokee isipokuwa ni kwa manufaa yetu. Anajua tutashinda kila kizuizi ambacho Shetani anachoweka mbele yetu. Anapenda kumthibitishia kwamba sisi ni Bibi-arusi Wake. Hatuwezi kuondoshwa. Sisi ndio Wale ambao amekuwa akingojea tangu mwanzo. Hakuna kinachoweza kututenganisha Naye na Neno Lake.
Alitutumia malaika-mjumbe wake mwenye nguvu ili aweze kusema nasi mdomo kwa sikio. Aliirekodi ili kusiwe na maswali yale aliyosema. Alikuwa ameihifadhi ili Bibi-arusi Wake awe na kitu cha kula mpaka Yeye ajapo kumchukua.
Haijalishi ikiwa wengine wanatuelewa vibaya na wanatutesa kwa kusema sisi ni “Watu wa Kanda”, tunafurahi, kwa kuwa hili ndilo Yeye alilotufunulia sisi tufanye. Wengine hawana budi kufanya kama wanavyohisi kuongozwa kufanya, lakini kwetu sisi, hatuna budi kuungana pamoja chini ya Sauti moja, Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kwenye kanda.
Hatuwezi kufahamu kitu kingine chochote. Hatuwezi kuelewa kitu kingine chochote. Hatuwezi kufanya kitu kingine chochote. Hatuwezi KUKUBALI kitu kingine chochote. Sisi hatupingani na kile waamini wengine wanachohisi wanaongozwa na Bwana kufanya, lakini hiki ndicho Mungu AMETUONGOZA SISI KUFANYA, nasi ni lazima TUDUMU hapa.
Tumeridhika. Tunalishwa na Sauti ya Mungu. Tunaweza kusema “amina” kwa KILA NENO tunalosikia. Hii ndiyo Njia Mungu aliyotuandalia. Hatuwezi kufanya kitu kingine chochote.
Ninapenda tu kuwaalika kila mmoja kuja kuungana nasi. Tunazifanya ibada jinsi vile tu Ndugu Branham alivyozifanya wakati yeye alipokuwa hapa duniani. Ingawa yeye hayuko hapa katika mwili, jambo kuu ni kile Mungu alichomwambia Bibi-arusi Wake kwenye kanda.
Yeye aliualika ulimwengu kuwa sehemu ya MAWASILIANO ya simu, lakini tu ikiwa wao WALITAKA KUFANYA HIVYO. Aliwafanya wakusanyike popote walipoweza kuisikia Sauti ya Mungu ikizungumza nao wote kwa wakati mmoja. Hivyo ndivyo nabii wa Mungu alivyofanya wakati huo, kwa hiyo mimi ninajaribu tu kufanya yale yeye aliyofanya kama mfano wangu.
Hivyo, unaalikwa kuja kuungana nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunapomsikiliza mjumbe wa Mungu akituletea Ujumbe: Mungu Wa Wakati Huu Mwovu 65-0801M.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:
Mathayo Mt. sura ya 24/27:15-23 Mtakatifu Luka 17:30 Yohana Mtakatifu 1:1 / 14:12 Matendo 10:47-48 1 Wakorintho 4:1-5 / sura ya 14 2 Wakorintho 4:1-6 Wagalatia 1:1-4 Waefeso 2:1-2 / 4:30 2 Wathesalonike 2:2-4 / 2:11 Waebrania sura ya 7 1 Yohana Sura ya 1 / 3:10 / 4:4-5 Ufunuo 3:14 / 13:4 / Sura ya 6-8 na 11-12 / 18:1-5 Mithali 3:5 Isaya 14:12-14
Tuko chini ya matarajio na matazamio makubwa. Twaweza kulihisi jambo hilo, jambo fulani linaenda kutukia. Tunataka kuungana pamoja ili kuisikia Sauti Yako; kupata cho chote na kila kitu unachosema. Tunalitaka. Tunataka kuwa sehemu Yake. Tunaamini kila Neno.
Nini kinatendeka? Mungu anafanya historia. Mungu anatimiza unabii. Hiyo Daima husababisha kuvutia macho. Huwakusanya wapinzani wote, wale nderi wa Ujumbe tuliousikia Jumapili iliyopita, lakini pia linawakusanya Tai Wake pamoja. Kwa maana palipo Mzoga, hapo Tai watakusanyika.
Ni jibu la unabii wa nabii, angalieni, nitawapelekea Eliya nabii. Mungu anamthibitisha nabii Wake. Ni Mungu akitimiza unabii. Mungu akifanya historia, akilitimiza Neno Lake. Ni ule Mvuto wa Tatu ukitimia.
Najua yaonekana kama yote Nifanyayo tu ni kutokukubaliana na viongozi wote wa makanisa, naonekana kulaumu chochote wanachofanya, lakini ninaamini sisi ndio lile kundi fulani la watu ambao wamechaguliwa tangu asili Kubonyeza Play na kuusikia Ujumbe huo, Sauti hiyo, na kuufuata.
Sisi hatujali umati wa watu. Hatujali lawama za asiyeamini. Hatubishani nao. Tuna wajibu mmoja, huo ni kuamini na kupata kila sehemu Yake tuwezayo; tuiingize ndani kama Mariamu aliyeketi miguuni pa Yesu.
Hatuvutiwi na kitu kingine chochote. Hatuhitaji kitu kingine chochote. Tunaamini kwamba kila kitu tunachohitaji kusikia kiko kwenye kanda. Neno la Mungu halihitaji fasiri yoyote.
Ile ahadi imetimizwa. Ni wakati gani, bwana, na mvuto huu ni wa nini? Mungu akitimiza Neno Lake! Ni yeye yule jana, leo, na hata milele.
Ni mvuto gani? Mungu, kwa mara nyingine tena, akilitimiza Neno Lake, akiwakusanya watu Wake pamoja makanisani, vituo vya mafuta, majumbani, wamekusanyika kuzunguka vipaza sauti vidogo kutoka kote nchini, kote kote hata kwenye Pwani ya Magharibi, kule juu kwenye milima ya Arizona, chini kwenye mabonde ya Texas, mbali sana hata Pwani ya Mashariki; kote nchini na ulimwenguni kote.
Tuko umbali wa masaa mengi katika wakati, lakini Bwana, tuko pamoja kama jamii moja, waamini, tukingojea Kuja kwa Masihi. Ninajaribu kufuata na kufanya vile tu nabii Wako alivyofanya ili kumuunganisha Bibi-arusi Wako wakati yeye alipokuwa hapa. Kile yeye alichokifanya ndio mfano wangu.
Hatuna nafasi ya kumketisha kila mmoja hapa kwenye Maskani ya Branham, kwa hivyo inatulazimu tu kuwatumia Neno kwa njia ya simu, kama vile yeye alivyofanya wakati huo. Tumekusanyika hapa, Jeffersonville, katika makanisa yetu ya nyumbani, tukingojea Kuja kwa Bwana.
Umetoka kutuambia kutakuwa na wengi katika siku hizi za mwisho ambao watajaribu kukufanyia wewe kazi bila ya kuwa mapenzi Yako makamilifu. Kutakuwa na wengi ambao watatiwa mafuta na Roho Mtakatifu wa kweli, lakini watakuwa waalimu wa uongo. Bwana, njia pekee tunayojua KUWA NA HAKIKA ni kudumu na Neno, kudumu na mafundisho ya kanda, kudumu na Sauti Yako iliyothibitishwa.
Tunaamini sisi ndio Uzao Wako uliochaguliwa tangu asili ambao hatuwezi kutenda chochote bali kulifuata; ni zaidi ya maisha kwetu. Twaa maisha yetu, bali usichukue Hilo.
Nini kitatendeka Jumapili hii? Mungu atakuwa akitimiza Neno lake. Kote nchini, kwa njia ya simu, mamia ya watu watawekeleana mikono wao kwa wao kote taifani, pwani kwa pwani, kutoka Kaskazini hata Kusini, Mashariki hata Magharibi.
Hata kutoka nchi za ng’ambo ulimwenguni kote, sote tutawekeana mikono . Ulituambia, “hatuhitaji kadi ya maombi, si lazima kupitia kwenye mstari, tunahitaji tu IMANI.”
Tutainua mikono yetu na kusema, “Mimi ni mwamini.” Yapi yatatendeka?
Shetani, umeshindwa. Wewe u muongo. Na, kama mtumishi wa Mungu, na kama watumishi, tunakuamuru ya kwamba katika Jina la Yesu Kristo, ya kwamba utii Neno la Mungu na utoke ndani ya watu, kwa maana imeandikwa, “Katika Jina Langu watatoa pepo.”
Mungu mpendwa. Wewe ndiye Mungu wa Mbinguni uliyeshinda, siku hiyo kwa mvuto juu ya Mlima Kalvari, magonjwa yote na maradhi na kazi zote za Ibilisi. Wewe ni Mungu! Na watu wameponywa kwa mapigo Yako. Wao ni huru. Katika Jina la Yesu Kristo. Amina.
Mungu ATATIMIZA Neno Lake!
Ningependa kukualika uje kusikiliza pamoja nasi, sehemu ya Bibi-arusi Wake, tunapousikia Ujumbe: 65-0725E Nini Kinachovutia Kule Mlimani? Tutakusanyika Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville.(Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki).
Wengine wanaweza kuhisi sisi tu madhehebu kwa kukusanyika pamoja, kusikiliza Ujumbe uleule kwa wakati mmoja, lakini naamini kama Ndugu Branham angekuwepo hapa, angekuwa anafanya kile hasa tutakachokifanya, kumkusanya Bibi-arusi pamoja, kutoka ulimwenguni kote, kusikiliza kwa wakati mmoja KUMSIKIA YEYE.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko:
Mathayo 21:1-4 Zekaria 9:9 / 14:4-9 Isaya 29:6 Ufunuo 16:9 Malaki 3:1 / Sura ya 4 Yohana Mt 14:12 / 15:1-8 Luka Mt 17:22-30
Mungu alimtuma malaika-mjumbe wake wa saba amwongoze Bibi-arusi Wake; si mtu mwingine, si kundi la watu, bali MTU MMOJA, kwa maana Ujumbe na mjumbe Wake ni kitu kile kile. Neno la Mungu halihitaji kufasiriwa. Alilinena kwa Bibi-arusi Wake kupitia midomo ya mwanadamu nasi tunaliamini Hilo jinsi vile tu Yeye alivyolisema.
Ni lazima tuwe waangalifu sana leo ni sauti gani inayotuongoza, na inatuambia nini. Kikomo chetu cha milele kinategemea uamuzi huo hasa; kwa hiyo ni lazima tuamue ni sauti gani ndio sauti iliyo muhimu zaidi ambayo tunayopaswa kuisikia. Ni Sauti gani ambayo imethibitishwa na Mungu? Ni Sauti gani iliyo na Bwana Asema Hivi? Haiwezi kuwa sauti yangu, maneno yangu, fundisho langu, lakini lazima liwe Neno, kwa hiyo ni lazima tuende kwenye Neno kuona kile Linachotuambia.
Je! linatuambia kwamba Yeye atainua huduma tano ituongoze mwishoni? Tunaweza kuona waziwazi katika Neno wao wana mahali pao; mahali muhimu sana, lakini Je, Neno linasema MAHALI POPOTE kuwa wao ndio watakaokuwa na sauti zilizo muhimu zaidi TUNAZOPASWA kuzisikia ili kuwa Bibi-arusi?
Nabii alituambia kutainuka watu wengi katika siku za mwisho watakaojaribu kumtendea Mungu kazi bila ya kuwa Mapenzi Yake. Ataibariki huduma yao, lakini sio njia Yake kamilifu ya kumwongoza Bibi-arusi Wake. Alisema Mapenzi yake makamilifu ni, na daima yamekuwa, ni kuisikia na kuiamini Sauti ya nabii wake aliyethibitishwa; kwa maana ni Hiyo, na hiyo peke yake ndio iliyo na Bwana Asema Hivi. Ndioamana alimtuma malaika Wake. Ndiomaana alimchagua yeye. ndiomaana Yeye aliirekodi. Ni Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake, Mana Iliyofichwa, kwa Bibi-arusi Wake.
Kwa kuwa saba kati ya nyakati saba, sijaona kitu ila watu wakiliheshimu neno lao wenyewe kuliko Langu. Kwa hiyo mwishoni mwa wakati huu ninawatapika mtoke katika kinywa Changu. Yote yamekwisha. Nitazungumza basi. Naam, niko hapa katikati ya Kanisa. Amina wa Mungu, aliye mwaminifu na wa kweli atajifunua Mwenyewe na itakuwa KWA NJIA YA NABII WANGU.” Loo! ndiyo, hivyo ndivyo ilivyo.
Saba kati ya nyakati saba watu wanaliheshimu neno lao wenyewe kuliko Langu. Unatakiwa kujiuliza mwenyewe, Je, jambo hili halifanyiki kati yetu hivi sasa? “Usicheze kanda kanisani, bali lazima umsikie mchungaji wako, zicheze tu kanda nyumbani kwako”. Wao hawaiweki Sauti Yake iliyo kwenye kanda kuwa ndio Sauti iliyo muhimu zaidi, bali sauti yao.
Wanawaelekeza watu kwao wenyewe, na umuhimu wa huduma YAO; Wito WAO kulileta Neno, kumwongoza Bibi-arusi; Lakini Bibi-arusi hawezi kulivumilia hilo. Hawatalikubali. Hawatalifanya jambo hilo. Hawatapatana kuhusu Hilo; ni Sauti ya Mungu na si kitu kingine. Hivyo ndivyo Neno linavyosema.
Swali lililo niani mwa watu siku hizi ni: Ni nani ambaye Mungu alimchagua kumuongoza Bibi-arusi Wake, Je, ni kanda au ni huduma tano? Je, wahudumu watamkamilisha Bibi-arusi? Je, wahudumu watamwongoza Bibi-arusi? Kulingana na Neno la Mungu, hiyo haijawahi kamwe kuwa Njia Yake.
Kuna watu wengi sana leo wanaosema wameufuata na kuuamini Ujumbe huu kwa miaka na miaka, lakini sasa wanaiweka huduma YAO kuwa ndio sauti iliyo muhimu zaidi unayopaswa kuisikia.
Utaifuata huduma ipi basi? Utaweka kikomo chako cha Milele kwenye huduma ipi? Wote wanasema wameitwa na Mungu kuhubiri Ujumbe. Sikatai ama kulihoji hilo, lakini baadhi ya wahudumu wenye ushawishi mkubwa katika vyeo vya huduma tano wanasema, “Hiyo siyo Sauti ya Mungu, ni sauti ya William Branham tu”. Wengine wanasema, “siku za Ujumbe wa mtu mmoja zimepita”. “Ujumbe huu sio Yakini”. Je, Huyo ndiye anayekuongoza?
Wanaume ambao wamehubiri katika mamia ya makusanyiko yao, viongozi wakubwa wa huduma tano, SASA wanaukana Ujumbe na KUSEMA “Ujumbe huu ni wa uongo”.
Nyingi kati ya huduma zote husema, “Hampaswi kusikiliza Sauti ya malaika wa Mungu kanisani, isipokuwa tu majumbani mwenu.” “Ndugu Branham hakusema kamwe kuzicheza kanda kanisani.”
Hilo halisadikiki. Siamini ndugu ama dada wanaosema wanaamini Ujumbe huu; kwamba Ndugu Branham ndiye malaika-mjumbe wa saba wa Mungu, ni Mwana wa Adamu anayezungumza, angeangukia kwenye kauli ya udanganyifu kama hiyo. Hilo lingepaswa kukuchefua tumbo. Ikiwa wewe ni Bibi-arusi, LITAKUCHEFUA.
Mungu hajawahi kamwe kubadilisha Nia Yake kuhusu Neno Lake. Daima Yeye amemchagua mtu mmoja kuwaongoza watu wake. Wengine wana mahali pao, lakini wao wanapaswa kuwaongoza watu kwa yule mmoja ambaye YEYE amemchagua kuwaongoza watu. Amkeni, enyi watu. Hebu jaribuni kusikiliza kile hawa wahudumu wanachowaambia, Nukuu hizo wanazotumia kuiweka huduma yao mbele ya ile ya nabii. Inawezaje huduma ya mtu ye yote kuwa ndio muhimu zaidi kuisikia kuliko Sauti ya Mungu iliyothibitishwa ambayo Yeye ameihakikisha na kuithibitisha kuwa Bwana Asema Hivi?
Yeye ametuambia, na kutuambia, kunaweza kuwa na watu waliotiwa mafuta kweli, na Roho Mtakatifu wa kweli juu yao, ambao ni wa uongo. Kuna NJIA MOJA tu ya kuwa na hakika, KUKAA NA NENO LA ASILI, kwa maana Ujumbe huu na mjumbe ni kitu kile kile. Kuna Sauti moja tu ambayo Mungu aliichagua kuwa Bwana Asema Hivi…MOJA.
Huduma ya kweli itakuambia kwamba HAKUNA KITU kilicho muhimu zaidi kuliko kulisikia Neno la Mungu kutoka kwenye Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. Wao wanaweza kuhubiri, kufundisha, au chochote walichoitiwa kufanya, LAKINI LAZIMA WAIWEKE SAUTI YA MUNGU KUWA NAFASI YA KWANZA; LAKINI WAO HAWAFANYI HIVYO, BALI WANAIWEKA HUDUMA YAO KUWA NDIO NAFASI YA KWANZA. Matendo yao yenyewe yanathibitisha kile wanachoamini.
Wanakwepa kujibu swali kuhusu kuiweka Sauti ya Mungu kwenye mimbara zao kwa kusema, “Ndugu Joseph haamini katika wahudumu. Haamini katika kwenda kanisani. Wao wanamwabudu mtu. Wanafuata fundisho hilo la Joseph. Yeye anatengeneza dhehebu kwa kucheza na kusikiliza wote kanda ileile.” Wakiwakengeusha tu watu kutoka kwenye swali kuu hasa, lakini matendo yao yanathibitisha kile wanachoamini kwa kile wanachowafundisha watu wao: HUDUMA YAO NDIO NAFASI YA KWANZA.
Wanasema, kuwafanya watu wasikilize wote kanda ile ile kwa wakati mmoja ni dhehebu. Je! Hivyo sivyo hasa alivyofanya Ndugu Branham Wakati yeye alipokuwa hapa; kuwaunganisha watu kwa simu ili wasikie Ujumbe wote kwa wakati mmoja?
Wewe jiulize, kama Ndugu Branham angekuwepo hapa leo katika mwili, Je! hangewafanya Bibi-arusi wote KUJIUNGANISHA KWA SIMU ili wamsikie yeye wote kwa wakati mmoja? Je! asingejaribu kuwakusanya Bibi-arusi pamoja katika HUDUMA YAKE kama vile yeye alivyofanya kabla Mungu hajampeleka nyumbani?
Hebu niingize kitu fulani hapa. Wakosoaji watasema, unaona, anafanya yale yale, kumsifia huyo mtu sana; wao wanamfuata mtu, William Marrion Branham!! Hebu tu tuone kile Neno linachosema kuhusu hilo pia:
Katika siku za mjumbe wa saba, katika siku za wakati wa Laodikia, mjumbe wake atafunua siri za Mungu kama zilivyofunuliwa kwa Paulo. Yeye atanena, na hao watakaompokea nabii huyo katika jina lake mwenyewe watapokea matokeo mema ya huduma ya nabii huyo.
Hili litamkasirisha shetani zaidi ya chochote kile naye atanishambulia hata na zaidi, lakini enyi watu, afadhali mlichunguze hili kwa Neno. Si kwa sababu mimi nimelisema, hapana, basi ningekuwa kama mtu yeyote yule; bali ifungueni mioyo yenu na nia zenu na mlichunguze hilo kwa Neno. Si kile mtu mwingine ye yote anachosema au anachowafasiria, bali kile nabii wa Mungu alichosema.
Baada ya barua hii wao watawapa nukuu baada ya nukuu baada ya nukuu, nami nasema AMINA kwa kila nukuu, LAKINI VIPI KUHUSU JAMBO LILILO KUU? Je! wanazitumia nukuu kuwaambia kuwa kumsikia nabii ndilo jambo mnalopaswa kufanya, au HUDUMA YAO? Wakisema Ujumbe, nabii, basi waambieni waiweke hiyo Sauti KUWA NAFASI YA KWANZA katika kanisa lenu.
Juu ya msingi wa tabia za wanadamu peke yake, mtu ye yote anajua ya kwamba palipo na watu wengi kuna hata na maoni yasiyopatana juu ya mambo madogo-madogo ya fundisho muhimu ambalo wote wanashikilia pamoja.
Hilo hapo. Hii nukuu moja tu inawaambia haiwezi na HAITAKUWA kundi la watu. Si wahudumu watakaowaunganisha watu kwa sababu ya tabia za wanadamu peke yake; wamegawanyika juu ya maoni ya mambo madogo-madogo ya mafundisho muhimu. Wote hawawezi kukubaliana, kwa hivyo mnapaswa kurudi kwenye NENO LA ASILI.
Ni nani basi atakayekuwa na mamlaka ya kutokosea ambayo itarudishwa katika wakati huu wa mwisho, kwa kuwa wakati huu wa mwisho utarudi kwenye kumdhihirisha Bibi-arusi wa Neno Halisi?
NI NANI atakayetuongoza? SAUTI MOJA, iliyo na mamlaka ya kutokosea ndio itamwongoza Bibi-arusi.
Hiyo inamaanisha tutakuwa na Neno tena kama lilivyotolewa kikamilifu, na kueleweka kikamilifu katika siku za Paulo.
Utukufu… Limetolewa kikamilifu na kueleweka kikamilifu. Halihitaji fasiri, kwa vile lilivyotolewa kikamilifu, na sisi, Bibi-arusi, tunalielewa kikamilifu na kuamini kila Neno.
Hilo hapo. Yeye anamtuma nabii aliyethibitishwa.
Anatuma nabii baada ya karibu miaka elfu mbili.
Yeye anamtuma mtu fulani aliye mbali sana na madhehebu, elimu, na ulimwengu wa dini hivi kwamba kama vile Yohana Mbatizaji na Eliya wa kale,
Yeye ata-sikia tu kutoka kwa Mungu
Ata-kuwa na “Bwana asema hivi” na kunena kwa niaba ya Mungu.
Yeye atakuwa kinywa cha Mungu
NAYE, KAMA INAVYOTANGAZWA KATIKA MAL. 4:6, ATAIGEUZA MIOYO WA WATOTO IWAELEKEE BABA ZAO.
Atawarudisha wateule wa siku za mwisho nao watamsikiliza nabii aliyethibitishwa akitoa kweli halisi kama vile ilivyokuwa kwa Paulo.
Atairudisha kweli kama walivyokuwa nayo.
Na hao wateule walio pamoja naye katika siku hiyo watakuwa ndio wanaomdhihirisha Bwana kwa kweli na watakuwa ndio Mwili Wake na kuwa sauti Yake na kutenda kazi Zake. Haleluya! Unaliona hilo?
Umealikwa kuja kuungana nasi wakati tunapokisikia kinywa cha Mungu, Sauti ile itakayo muunganisha Bibi-arusi wa Yesu Kristo, Nabii wake aliyethibitishwa, anapotupa ukweli halisi, saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)
Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukusanyike pamoja Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni Saa 1 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) ili kusikia 65-0718E Chakula cha Kiroho Kwa Wakati Wake.
Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu tukusanyike pamoja Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA saa za Jeffersonville,(Ni Saa 1 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki), kusikia 65-0718M – Kujaribu Kumtendea Mungu Kazi Bila ya Kuwa Mapenzi ya Mungu.
Hakujawahi kuwa na wakati au watu kama leo hii. Sisi tumo ndani yake, warithi wa yote aliyotununulia. Anashiriki utakatifu wake pamoja nasi, mpaka ndani yake, tumekuwa haki halisi ya Mungu.
Yeye alitujua tangu zamani kwa amri ya Kiungu, ya kwamba tungekuwa Bibi-arusi Wake. Alituchagua sisi, hatukumchagua Yeye kamwe. Hatukuja wenyewe, ilikuwa ni chaguo Lake. Sasa ameweka ndani ya mioyo yetu na nafsi zetu Ufunuo mkamilifu wa Neno Lake.
Siku baada ya siku, Yeye anatufunulia Neno Lake, akimimina Roho Wake juu yetu, akiyadhihirisha maisha Yake mwenyewe ndani yetu. Kamwe Bibi-arusi Wake hakuwahi kutia nanga zaidi mioyoni mwao wakijua wako katika mapenzi Yake makamilifu, na katika mpango Wake, kwa kukaa na Neno Lake, kuisikia Sauti Yake.
Upendo wa Mungu na Ujumbe huu umejaa mioyoni mwetu mpaka unabubujika tu. Hakuna kitu kingine sisi tunachotaka kusikia, kuzungumzia, kufanyia ushirika, au kushiriki tu nukuu ambayo tumesikia na kumsifu Bwana.
Sisi ni kama vile Musa upande wa nyuma ya jangwa. Tumetembea uso kwa uso na Mwenyezi Mungu, nasi tunaiona hiyo Sauti ikisema nasi; imeambatana kabisa na Neno na ahadi ya wakati huu. Imetufanyia kitu fulani. Hatuionei haya. Tunapenda kuitangaza kwa ulimwengu. Tunaamini Bwana Yesu ndiye Ujumbe wa saa hii na sisi NDIO BIBI-ARUSI WAKE.
Ametuimarisha kwa Neno Lake. Hakuna shaka hata kidogo, hii ndiyo njia iliyoandaliwa na Mungu. Mungu kamwe habadilishi nia Yake kuhusu Neno Lake. Yeye alimchagua malaika Wake wa saba kumwita Bibi-arusi Wake atoke, na kisha kumweka Yeye kwenye mstari sawa na Neno Lake.
Hakuna kitu katika maisha haya ila Yeye na Neno Lake. Hatuwezi kupata ya kutosha ya jambo hilo. Ni zaidi ya uhai kwetu sisi. Injili na Nguvu za Mwenyezi Mungu zimeenea ulimwenguni kote kuliko hapo awali. Neno sasa liko mikononi na masikioni mwa Bibi-arusi. Wakati wa kutengana unatukia sasa, wakati Mungu anamwita Bibi-arusi, naye shetani analiita kanisa.
Tunakupenda Wewe na Neno Lako, Bwana. Hatuwezi kupata ya kutosha. Tumeketi katika uwepo wa Neno lako kila siku, tukiivishwa, tukijitayarisha kwa ajili ya Kuja Kwako hivi karibuni. Baba, litakuwa limekaribia sana. Tunaweza kulihisi, Bwana. Tunasubiri kwa hamu kubwa.
Baba, jalia tuwe waaminifu vya kutosha na tuzifanye upya nadhiri zetu tena. Tunajua Imani yetu katika Neno lako inawaka mioyoni mwetu. Umeondoa mashaka yote. Hakuna kitu hapo ila Neno Lako. Tuna hakika, nasi hatuoni haya kuuambia ulimwengu, sisi ni Bibi-arusi Wako wa Kanda.
Ninataka kuualika ulimwengu kuja kusikiliza pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia Ujumbe: Kuonea Haya 65-0711.
Siku imeenda sana na Kuja kwa Bwana kumekaribia. Mlango unajifunga na wakati unaisha, ikiwa bado haujaisha. Muda umeenda sana kushangaa-shangaa; wa kuwa kama unyasi unaotikiswa na upepo; wa kuwa na masikio ya utafiti. Ni wakati wa kufanya maamuzi dhahiri. Yanilazimu nifanye nini ili kuwa Bibi-arusi Wake?
Je! Mungu hubadilisha Nia Yake kuhusu Neno Lake? KAMWE. Basi tunapaswa kujitahidi kila siku, kwa moyo na roho zetu zote kuwa katika MAPENZI YAKE MAKAMILIFU. Inatupasa kujikabidhi wenyewe kwenye mapenzi Yake na Neno Lake. Usilihoji kamwe, liamini tu na ulikubali. Usijaribu kutafuta njia ya kuliepa. Lichukue tu jinsi lilivyo.
Nabii anatuambia katika Ujumbe huu ya kwamba kusudi lake lote ni kutuonyesha ya kwamba Mungu hana budi kutimiza Neno Lake kusudi adumu kuwa Mungu, lakini watu wengi wanataka kuliepa, na kupitia njia nyingine. Wanapofanya jambo hilo, wanajikuta wakipiga hatua, na Mungu akiwabariki, bali wanafanya kazi katika mapenzi Yake ya kuruhusia na wala si katika mapenzi Yake makamilifu, ya Kiungu.
Nabii anaturudisha kwenye Neno na kutupa mifano ya kutazama, kujifunza, na kutukumbusha, Mungu HABADILISHI Nia Yake wala njia Yake, Yeye ni Mungu wala HABADILIKI.
Sasa, tunaona ya kwamba wote hawa wawili walikuwa watu wa kiroho, wote wawili walikuwa manabii, wote wawili walikuwa wameitwa. Naye Musa, akiwa moja kwa moja kazini, akiwa na Nguzo ya Moto mpya mbele yake kila siku, Roho wa Mungu akiwa juu yake, akiwa kazini. Huyu hapa mtumishi mwingine wa Mungu anakuja, aliyeitwa na Mungu, aliyechaguliwa na Mungu, nabii ambaye anajiliwa na Neno la Mungu. Hapa ndipo penye hatari. Hakuna mtu angaliweza kukataa mtu huyo kuwa ni wa Mungu—wa Mungu, kwa maana Biblia ilisema Roho wa Mungu alinena naye, naye alikuwa nabii.
Bwana, jinsi gani hilo linavyofanana sana? Ninawezaje kujua, wakati WOTE wawili walikuwa manabii? Wote wawili ni watu waliojazwa na Roho walioitwa na Mungu, waliochaguliwa na Mungu; manabii wa Mungu ambao Neno la Mungu huwajia. Wote wawili wakisema Roho Mtakatifu anawaongoza.
Hebu tusome na tujifunze nukuu chache kwa makini sana kuhusu kile ambacho malaika-mjumbe wa saba wa Mungu asemacho. Tunataka kile yeye anachosema; si kile kanisa linachosema, kile ambacho Daktari Jones asemacho, ama kile mtu mwingine yeyote asemacho. Sisi Tunataka kile BWANA ASEMA HIVI asemacho kupitia nabii Wake.
Musa, akiwa nabii aliyechaguliwa na Neno la Bwana, alithibitishwa ya kwamba alikuwa amechaguliwa kuwa kiongozi wao kwa ajili ya majira hayo, na ya kwamba Ibrahimu alikuwa ameahidi mambo haya yote,…
Hakuna mtu angaliweza kupachukua mahali pa Musa. Haidhuru ni Kora wangapi walioinuka, na ni Dathani wangapi; ilikuwa ni Musa, Mungu alikuwa amemwita, kwa vyo vyote.
Musa ndiye ambaye Mungu alikuwa amemchagua kuwaongoza watu. Wanaume wengine waliinuka na kusema wamepakwa mafuta, watu waliojazwa na Roho Mtakatifu pia. Mungu alikuwa amewaita waongoze pia. Lakini Musa alikuwa ndiye kiongozi wa Mapenzi Makamilifu ya ya Mungu ya asili wa kuwaongoza.
Lakini, na iwapo watu hawatatembea katika mapenzi Yake makamilifu, Yeye ana mapenzi ya kuruhusia atakayokufanya uende kwayo. Angalia, Yeye hurusu jambo hilo, kweli, bali atalifanya litende kazi kwa utukufu Wake, katika mapenzi Yake makamilifu. Sasa kama mngetaka…
Hakuna anayetaka kuwa katika mapenzi ya Mungu yakuruhusia. Bibi-arusi wa kweli anataka kuwa katika mapenzi Yake makamilifu, wakati wote, haijalishi gharama.
Kuna kutokubaliana kwingi, mawazo mengi, mkanganyiko mwingi, maoni mengi, juu ya umuhimu wa kucheza kanda.
Sote tunajua hili ndilo suala lenyewe ambalo limewatenganisha waaminio wa Ujumbe leo. Tunajua Bibi-arusi LAZIMA, NA ATA-ungana pamoja; hilo ni Neno.
Kuna watu waliojazwa na Roho, walioitwa na Mungu katika Kanisa leo. Wao ni watu waliotiwa mafuta na Mungu walioitwa kuhubiri Ujumbe huu. Lakini hakuna hata mmoja wao ambaye tunaweza sote kukubaliana kwake.
Wanawezaje wao kuwa ndio wa kumuunganisha Bibi-arusi? Je, twaweza kuungana kwenye huduma yao? Kwa kweli wao wameitwa kuliongoza kundi lao, lakini kuwarudisha hao kwenye MPANGO WA ASILI wa Mungu. kwa KIONGOZI WAKE. Kwa NABII WAKE. Sio kwenye huduma yao.
Kama wao hawakufundishi kwamba ile Sauti iliyo kwenye kanda hiyo ndio UNAPASWA uifuate, na lazima uamini kuwa ndiyo Sauti iliyo muhimu zaidi unayopaswa kuisikia, wako tu katika mapenzi Yake ya kuruhusia.
Iwapo wanakuambia kuwa Ndio Sauti iliyo muhimu zaidi, nao wanaamini kweli hivyo, basi inakuwaje hawabonyezi play kila wakati mnapokutana?
Ikiwa unataka kuwa na hakika, NA HAKIKA, kwamba uko katika mapenzi Yake makamilifu, kuna NJIA moja tu ya HAKIKA. Ni kusikia Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kwenye kanda.
Muda si muda, kanda inaangukia nyumbani mwao. Imelenga penyewe, basi. Kama yeye ni kondoo, anakuja moja kwa moja Nalo. Kama yeye ni mbuzi, anapiga hiyo kanda teke.
Lazima niwe na HAKIKA. Siwezi, na sita-bahatisha hata kidogo kwa kikomo changu cha Milele. NAJUA Sauti iliyo kwenye kanda ni Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi. NAJUA Hiyo haikosei. NAJUA Ilithibitishwa na Nguzo ya Moto. NAJUA Ndiye ambaye Mungu alimchagua kumwongoza Bibi-arusi Wake. NAJUA ya kwamba Sauti hiyo ndiyo Sauti pekee inayoweza na itakayo muunganisha Bibi-arusi. NAJUA itakuwa ni Sauti hiyo nitakayoisikia ikisema “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu”.
LAZIMA NIBONYEZE PLAY niisikie hiyo Sauti. Unaalikwa kuja kuungana nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia: 65-0418E Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake?
Ndugu. Joseph Branham
Tutauanza Ujumbe huu kwenye aya ya 61.
Maandiko ya kusoma kabla ya Kusikiliza Ujumbe:
Kutoka sura ya 19 Hesabu 22:31 Mathayo Mt. 28:19 Luka 17:30 Ufunuo sura ya 17
Mpendwa Bibi-arusi Wa Kristo, Hebu sote tukusanyike pamoja Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA saa za Jeffersonville (ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) kusikia 65-0221E – “Huyu Melkizedeki Ni Nani?”
Sisi ndio Bibi Wake mdogo anayependeza; asiyeghoshiwa, asiyeguswa na dhehebu la mtu ye yote, nadharia yo yote iliyobuniwa na mwanadamu. Sisi ni Bibi-arusi wa Neno asiyeghoshiwa kabisa! Sisi ndio yule binti wa Mungu aliyetiwa mimba.
Sisi ni watoto wa Neno Lake lililonenwa, ambalo ni Neno Lake la asili! Hakuna dhambi katika Mungu, kwa hivyo hakuna dhambi ndani yetu, kwa vile tulivyo mfano Wake Mwenyewe. Twawezaje kuanguka? Hilo Haliwezekani….HAIWEZEKANI! Sisi ni sehemu Yake, NENO Lake LA ASILI.
Tunawezaje kujua hili bila shaka yoyote? UFUNUO. Biblia nzima, Ujumbe huu, Neno la Mungu, yote ni Ufunuo. Hivyo ndivyo tunavyojua ukweli kati ya Sauti hii na sauti zingine zote, kwa sababu ni Ufunuo. Na Ufunuo wetu unaambatana kabisa na Neno, sio kinyume cha Neno.
Na juu ya mwamba huu” (ufunuo wa kiroho wa Neno ni nini) “Nitajenga Kanisa Langu; wala milango ya kuzimu haitaliangamiza.” Mke Wake hatashawishiwa na mwanamume mwingine. “Nitalijenga Kanisa Langu, na milango ya kuzimu haiwezi kulitikisa kamwe.”
Tutakuwa wakweli na waaminifu kwa Neno Lake na Sauti Yake, peke yake. Kamwe hatutatiwa unajisi na mwanamume mwingine na kufanya uzinzi. Tutabaki kuwa Bibi-arusi Neno Bikira Wake. Hatutaangalia, kusikiliza au kuvutiwa na neno lingine lolote.
Liko ndani ya mioyo yetu. Hatungaliweza kamwe kuwa na mume mwingine, ila MUME wetu MMOJA, Yesu Kristo, Mtu mmoja, Mungu, Imanueli. Mkewe atakuwa maelfu mara maelfu ya maelfu. Hilo linaonyesha ya kwamba Bibi-arusi hana budi kutoka katika Neno. “Bwana Yesu Mmoja, na Bibi-arusi Wake wengi, umoja.”
Lazima tukumbuke na kuelewa hili si la kila mtu, ni kundi la nabii PEKE YAKE. Wafuasi wake mwenyewe. Ujumbe huu ni kwa ajili yao tu, lile kundi dogo ambalo Roho Mtakatifu alimpa kulisimamia.
Mungu atamwajibisha yeye kwa yale anayotuambia, na Mungu atatuwajibisha sisi, waongofu wake kutoka nchini kote, wale ambao amewaongoza kwa Kristo, kuamini kila Neno Lake na kutokupatana kamwe.
Ni jambo lakupendeza sana jinsi gani kwetu kuketi na kumsikiliza Yeye akitueleza jinsi sisi tulivyo wateule wake. Jinsi Bibi-arusi Wake wa kwanza, na Bibi-arusi wa pili, walivyomwangusha; Bali sisi, Bibi-arusi Wake mkuu wa wakati wa mwisho HATUTAMWANGUSHA. Tutabaki kuwa Bibi-arusi Neno Bikira Wake wa kweli, na mwaminifu hadi mwisho.
Imani yetu katika Neno lake inakua zaidi kila siku. Tunajiweka wenyewe tayari kwa kusikiliza na kutii kila Neno Lake, kuisikia Sauti yake ikinena nasi, kuzisoma Biblia zetu, kuomba na kumwabudu Yeye siku nzima.
Tunajua Yeye anakuja upesi sana. Dakika yoyote sasa. Kama vile Nuhu, tulikuwa tukitumaini Yeye alikuwa yuaja jana; labda kesho asubuhi, adhuhuri, jioni, lakini tunajua Yeye anakuja. Nabii wa Mungu na Neno Lake hawakosei, ANAKUJA. Tunahisi ni siku ya 7, nasi tunaweza kuona mawingu yakijikusanya na matone makubwa ya mvua yakianguka; wakati umefika.
Tuko salama salimini ndani ya Safina, tukingojea kwa hamu kubwa. Njoo uungane nasi wakati tunaposikia Sauti ya Mungu ikitufariji Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, tunaposikia: Ndoa Na Talaka 65-0221M.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:
Mathayo Mt 5:31-32 / 16:18 / 19:1-8 / 28:19 Matendo 2:38 Warumi 9:14-23 Timotheo wa Kwanza 2:9-15 Wakorintho wa Kwanza 7:10-15 / 14:34 Waebrania 11:4 Ufunuo 10:7 Mwanzo sura ya 3 Mambo ya Walawi 21:7 Ayubu 14:1-2 Isaya 53 Ezekieli 44:22
Kama tungeuliza swali kuhusu cho chote maishani mwetu, yapaswa kuwe na jibu la kweli. Kwaweza kuwe na lililo la karibu nalo, lakini kunapaswa kuwa na jibu la kweli, la moja kwa moja kwa kila swali. Kwa hiyo, basi kila swali linalozuka maishani mwetu, yabidi kuwe na jibu la kweli na sahihi.
Kama tuna swali la Biblia, lazima kuwe na jibu la Biblia. Hatutaki lije kutoka kwenye kundi la watu, kutoka kwenye ushirika wo wote ule, au kutoka kwa mwalimu fulani, au kutoka kwa madhehebu fulani. Tunataka litoke moja kwa moja katika Maandiko. Ni lazima tujue: ni mahali gani pa kweli na sahihi pa Mungu pa kumwabudia?
Mungu alichagua kukutana na binadamu; siyo kanisani, siyo katika madhehebu, siyo katika kanuni ya imani, lakini katika Kristo. Hapo ndipo mahali pekee ambapo Mungu atakutana na mtu, na anapoweza kumwabudia Mungu, ni katika Kristo. Ni mahali hapo pekee. Haidhuru kama wewe ni Mmethodisti, Mbatisti, Mkatoliki, Mprotestanti, hata uwe nani, kuna mahali pamoja tu ambapo unaweza kwa usahihi kumwabudu Mungu, hapo ni katika Kristo.
Mahali pekee sahihi, na alipopachagua Mungu pa kumwabudia Yeye ni katika Yesu Kristo; hiyo ni Njia Yake pekee iliyoandaliwa.
Biblia ilituahidi Tai katika Malaki 4; Nguzo ya Nuru tunayopaswa kuifuata. Atalionyesha kanisa lililokosea Yeye ni Waebrania 13:8, Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele. Pia tumeahidiwa katika Luka 17:30 kwamba Mwana wa Adamu (Tai) atakuwa akijifunua Mwenyewe kwa Bibi-arusi Wake.
Katika Ufunuo 4:7, inatuambia kwamba kulikuwa na Wenye Uhai wanne, na wa kwanza akiwa simba. Mwenye Uhai aliyefuata alikuwa ndama. Kisha, aliyefuata alikuwa ni mwanadamu; Na mwanadamu huyo alikuwa wale watengenezaji, elimu ya mwanadamu, theolojia, na kadhalika.
Lakini Biblia ilisema, wakati wa jioni, yule Mwenye Uhai wa mwisho ambaye alikuwa aje alikuwa Tai arukaye. Mungu angempa Bibi-arusi Wake wa wakati wa mwisho Tai; Mwana wa Adamu Mwenyewe, akijifunua Mwenyewe katika mwili kumwongoza Bibi-arusi Wake.
Biblia pia inasema mambo yote ya kale, katika Agano la Kale, yalikuwa ni vivuli vya mambo yajayo. Kivuli hicho kinapokaribia, negativu humezwa na picha yenyewe. Kile Kilichotokea wakati huo ni kivuli cha kile ambacho kingetokea leo.
Katika I Samweli 8, Agano la Kale linatuambia Mungu alikuwa amemtoa Samweli nabii kuwaongoza watu. Watu walimwendea na kumwambia wanataka mfalme. Samweli alifadhaika sana hata moyo wake nusura ukome.
Mungu alikuwa anawaongoza watu Wake kupitia kwa nabii huyu aliyewekwa wakfu, aliyethibitishwa kwa Maandiko naye akaona kwamba alikuwa amekataliwa. Akawakusanya watu akawasihi wasimwache Mungu Ambaye alikuwa amewabeba kama watoto, na kuwafanikisha na kuwabariki. Lakini wao wakakaidi.
Wakamwambia Samweli. “Hujakosea katika uongozi wako. Hujakuwa mdanganyifu katika mambo yako ya fedha. Umejaribu uwezavyo kutuweka sawa na Neno la Bwana. Tunaifurahia miujiza, hekima, chakula na ulinzi wa Mungu.Tunauamini. Tunaupenda. Na isitoshe hatutaki kuukosa. Ni kwamba tu tanataka mfalme wa kutuongoza vitani.
Sasa bila shaka tunapotoka kwenda vitani yangali ni makusudio yetu kuacha makuhani watutangulie huku Yuda wakifuata, nasi tutapiga matarubeta na kupiga makelele na kuimba. Hatutarajii kuacha yo yote ya mambo hayo. LAKINI TUNATAKA MFALME AMBAYE NI MMOJA WETU APATE KUTUONGOZA.”
Hawa hawakuwa watu wa kimadhehebu wa siku hizo. Kwa kweli hawa walikuwa ni watu waliodai kwamba YEYE ALIKUWA nabii wa Mungu ambaye alichaguliwa na Mungu kuwaongoza.
“Ndiyo, wewe ni nabii. Tunaamini Ujumbe. Mungu anakufunulia wewe Neno Lake, nasi tunalipenda, na isitoshe hatutaki kuukosa, lakini sisi tunamtaka mtu mwingine zaidi YAKO atuongoze; mmoja wetu sisi. Bado tunakusudia kusema tunauamini Ujumbe uliotuletea. Ni Neno. Wewe ni nabii, lakini si wewe tu pekee ama Sauti iliyo muhimu zaidi.”
Wapo watu wazuri ulimwenguni siku hizi, makanisa mazuri. Lakini kuna Bi Yesu Kristo mmoja, na Huyo ni sisi, ndio Wale Yeye anakuja kuwachukua; Bibi-arusi Neno Wake aliye safi ambaye atakayekaa na SAUTI PEKEE YA MUNGU ILIYOTHIBITISHWA NA KUHAKIKISHWA KUWA BWANA ASEMA HIVI.
Ikiwa ungependa kuungana nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) bado tutakuwa kwenye mawasiliano ya simu ulimwenguni kote tukisikiliza. Hiki ndicho kitakachotendeka.
Njoo juu ya ndugu zangu, dada, rafiki zangu, hapa katika sehemu hii usiku wa leo na huko nje kwenye simu. Majimbo mengi mbalimbali yanasikiliza, mahali pote tokea Pwani ya Mashariki hadi ya Magharibi. Naomba, Mungu Mpenzi, huko chini kuvuka majangwa kule Tucson, huko mbali California, juu huko Nevada na Idaho, kwenda hadi Mashariki na kila mahali, chini huko Texas; wakati mwaliko huu unatolewa, watu wameketi katika—katika makanisa madogo, vituo vya mafuta, majumbani, wakisikiliza. Ee Mungu, jalia mwanamume yule aliyepotea au mwanamke, mvulana au msichana, saa hii, aje Kwako. Lijalie hilo sasa hivi. Tunaomba katika Jina la Yesu, kwamba wataona mahali hapa pa usalama wakati muda ungalipo.
Sasa, Bwana, pambano hili limekwisha kabiliwa, kwamba Shetani, yule laghai mkuu, yeye hana haki ya kumshikilia mtoto wa Mungu. Yeye ni kiumbe kilichoshindwa. Yesu Kristo, mahali pekee pa kuabudia, Jina pekee la kweli, alilomshindia hapo Kalvari. Nasi tunadai Damu Yake sasa hivi, kwamba Yeye alishinda kila maradhi, kila ugonjwa.
Nami namwagiza Shetani kuwaacha wasikizi hawa. Katika Jina la Yesu Kristo, toka katika watu hawa, na wafanywe huru
Kila mtu ambaye anakubali kuponywa kwake juu ya msingi wa Neno lililoandikwa, toa ushuhuda wako kwa kusimama kwa miguu yako na kusema, “Ninakubali sasa kuponywa kwangu katika Jina la Yesu Kristo.” Simama kwa miguu yako.
Mungu asifiwe! Basi. Angalia huku, viwete na kadhalika wakiinuka. Mungu asifiwe. Naam. Aminini tu. Yeye yupo hapa.
Ndugu. Joseph Branham
Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia 65-0220
Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:
Kumbukumbu la Torati 16:1-3 Kutoka 12:3-6 Malaki Sura ya 3 & 4 Luka 17:30 Warumi 8:1 Ufunuo 4:7